Kumeibuka wimbi la matapeli Dodoma ambao wanajifanya wenyewe ni wafanyakazi wa TAMISEMI wanaitaji sh. 700,000 mpaka 1,000,000 ili mwalimu alioomba nafasi aweze kupata kazi na kupangiwa mjini au hata kijijini na baadae watamtoa huko alipo lakini cha muhimu apate kwanza.
Inawezekana mtu au watu wanaofanya hivi wakawa na connection na wafanyakazi wasio waaminifu wa TAMISEMI. Nimewahi kushuhudia mwaka jana watu wakitoa milioni 2 mwaka jana katika kampuni moja ya kimataifa iitwayo SICPA ili wapate kazi na hayo yalifanywa na HR akishirikiana na ma-team leader wa kila kanda.
Sasa hayo mambo tena yanakuja katika serikali ni hatari kwa sababu najua wanafunzi wengi wa vyuo wanadaiwa na wamekomboa vyeti vyao kwa gharama hivyo kuwaongezea gharama nyingine za kutoa rushwa haina afya. Na wamedai hawatoi majina ili waendelee kuvuna pesa za sikuuu na mwaka mpya.
Kwa sheria ya JamiiForums inanizuia kuweka namba zao humu lakini ukija inbobo nakupatia namba. Nasikia wameanzisha kauli mbiu bila maji hulambia ajira na hivi ajira zenyewe hazina interview.
Inawezekana mtu au watu wanaofanya hivi wakawa na connection na wafanyakazi wasio waaminifu wa TAMISEMI. Nimewahi kushuhudia mwaka jana watu wakitoa milioni 2 mwaka jana katika kampuni moja ya kimataifa iitwayo SICPA ili wapate kazi na hayo yalifanywa na HR akishirikiana na ma-team leader wa kila kanda.
Sasa hayo mambo tena yanakuja katika serikali ni hatari kwa sababu najua wanafunzi wengi wa vyuo wanadaiwa na wamekomboa vyeti vyao kwa gharama hivyo kuwaongezea gharama nyingine za kutoa rushwa haina afya. Na wamedai hawatoi majina ili waendelee kuvuna pesa za sikuuu na mwaka mpya.
Kwa sheria ya JamiiForums inanizuia kuweka namba zao humu lakini ukija inbobo nakupatia namba. Nasikia wameanzisha kauli mbiu bila maji hulambia ajira na hivi ajira zenyewe hazina interview.