Kuhamasisha maendeleo siyo kazi ya wabunge. Kama mnasubiri masihi ashuke awahamasishe basi mtasubiri sana sana. Rungwe na Tukuyu kwa nilivyoona haraka mbali na kilimo, mnaweza kuanzisha shughuli za viwanda vidogo vidogo kama alivyosema mkuu
kapalamsenga.
Jaribuni kuiga mfano wa Mufindi kule Iringa, ambako hali yake ya hewa inafanana kwa asilimia kubwa na Rungwe na Kyela. Wao pale wana viwanda vingi na hivyo bidhaa zinatoka mashambani na kuuzwa moja kwa moja viwandani hapo hapo. Bidhaa kama chai inaenda Chai Bora, magogo yanaenda kule Sao-Hill au kiwanda cha mgololo.
Hili limepelekea wakulima kupata sana nafuu, na Mafinga kuwa soko kubwa sana ambalo wafanyabiashara wa Afrika Mashariki wanafurika hasa kwenye biashara ya magogo. Rungwe kama mtaamua kutengeneza viwanda vya kusindika chakula mbona mtafika mbali sana na kutakuwa na soko kubwa sana maana badala ya kupata kadhia ya usafirishaji basi mtakuwa mnauza viwandani huko huko. Hili inabidi liende sambamba na kujitahidi kuanzisha mazao mapya ya chakula.
Pili, Rungwe na Kyela kuna vivutio vingi sana vya utalii, kule Arusha wazawa wengi wamejikita sana kwenye biashara ya utalii kwanini ninyi hamuangalii hizi fursa ?? Ukitoka lake Ngosi na useme ulale Tukuyu huwezi kupata hata hoteli na lodge nzuri. Nini tatizo ?? Mkuu
Consigliere kasema mindset inabidi zibadilike....