Ngoja niwaache Wahaya, niwaongelee Wanyakyusa. Wanyakyusa ni watu wa kusaidiana ila si watu wa kunyanyuana. Wanyakyusa (wanaoishi nje ya kwao) husaidiana kwa tahadhari sana, anayekusaidia huwa makini kuhakikisha hauji kumzidi hapo baadaye na ikitokea ukaonyesha mwekekeo wa kumzidi basi anaweza akakuanzishia tifu from no where, mara upo Pol8si mara Mahakamani. Hao ndiyo Wanyakyusa wa ugenini.
Na wanaposaidiana huwa wanahakikisha anakufahamu na kawaida kuna ubaguzi miongoni mwao.
Wanapokuwa na vikao vyao usitarajie utamkuta wa Keko Magurumbasi amechanganyikana na wa Upanga.
Kuhusu kunyanyuana huwa hawajadili mipango ya maendeleo ya kwao bali huibua mijadala ya majungu tu na kupingana kusiko na tija. Hawawezi kufikiria kwenda kusaidia shule, barabara au hospital, hawajadili mazingira ya elimu, afya n.k wanayopitia watu wa kwao sababu tu watoto au familia zao haziishi huko. Walio kwenye nafasi hawawezi kujenga ushawishi wa mipango kadhaa ya kimaendeleo ikafanyike kwao sababu hawai fikirii jamii ya kwao na watu wao, bali huwaza na kuishia katika level ya familia au ndugu tu.
Wanapenda sana sifa kwa kujisifia maendeleo ya kwao yaliyoletwa wakati wa mkoloni wakati wao hawajachangia hata moja. Akina Mwandosya ndiyo hao wanazeeka na sasa wanahitaji kupumzika. Lakini kwa bahati mbaya sana hakuna aliyeiga na kufuata mfano wake, mbaya zaidi walikua busy kujifanya wapo karibu na Mwandosya na wanamfahamu sana. Moyo wake na intelligence yake anazeeka nayo.
Kuna wakati Wanyakyusa likikua ni kabila la kujivunia, lakini siyo hawa Wanyakyusa wa hivi sasa, sijui wametengenezwa maabara!! Wamepausha na kuupoteza kabisa unyakyusa asilia.