Rukwa: Polisi Waua tena Mwananchi!

Rukwa: Polisi Waua tena Mwananchi!

Kwa mujibu wa
taarifa ya habari ITV saa 2 usiku huu, mfanyabiashara mmoja mjini
Sumbawanga ameuwawa baada ya kuvamiwa na kushambuliwa kwa risasi na
askari polisi, akiwa nyumbani kwake mjini Sumbawanga kwa kutuhumiwa kwa
wizi.


MYTAKE.
Chondechonde polisi mnawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu
wakijivinjari bila wasiwasi.

zungumzia pia na askari akiwa na silaha alivyokatwa panga na raia na raia huyo kabla ya kupigwa shaba nadhani furaha yako askari anguawa ndo ufurahi
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Mkuu inaonekana hata wewe ulicho kiandika hukifahamu; nahisi ndo matatizo ya kusoma shule za kata au na wewe ni miongoni mwa vijana wa kawa-mbwa 60% mliozungusha round about;

Huyo ni mtuhumiwa, PoliCCM hawana mamlaka ya kumhukumu mtuhumiwa kwa adhabu ya kifo. Kazi ya polisi ilikuwa ni kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha mahakamani, Hakimu atoe hukumu.

Wana JF msilete porojo kwenye sakata linalo husisha kutoa uhai wa binadamu mwenzetu; Suppose huyo aliye hukumiwa na poliCCM angekuwa ni Baba yako, Kaka yako, Mdogo wako, Mjomba wako, Binamu yako, Ndugu yako, rafiki yako, au jirani yako, ungethubutu kuandika huo upuuzi?

Narudia kusema kwamba siyo kila post lazima uchangie, wakati mwingine jifunze kusoma post za great thinkers waweza elimika.
 
Hawa polisi wa ccm wana nini jk anawatuma wakauewe wafanyabiashara wachukue pesa au tatizo nini ?
 
So mtu ukituhumiwa kwa wizi unauawa sasa apo polisi mnajitifautishaje na raia ambao hutia moto wezi?
 
taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

hawa ndio waliofoji vyeti hata sisi tumepita huko ccp. Hatujafundishwa kuua watu, kama waliweza kufika kwa mtuhumiwa walishindwa nn kumkamata, ripoti haionyeshi kama kulikuwa na resistance, hizi siraha tunazopewa tuzitumie vizuri, mnalipaka jeshi matope. Afande igp anatukanwa na watu bule. Kuna kukagua vyeti vyetu polisi wote.
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Mpaka hapo siyo mtuhumiwa tena bali Polisi walimhukumu kifo! Sheria namba ngapi hiyo Mkuu?
 
Back
Top Bottom