Rukwa: Polisi Waua tena Mwananchi!

Rukwa: Polisi Waua tena Mwananchi!

Nyahende Thomas

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
211
Reaction score
104
Kwa mujibu wa taarifa ya habari ITV saa 2 usiku huu, mfanyabiashara mmoja mjini Sumbawanga ameuwawa baada ya kuvamiwa na kushambuliwa kwa risasi na askari polisi, akiwa nyumbani kwake mjini Sumbawanga kwa kutuhumiwa kwa wizi.


MYTAKE.
Chondechonde polisi mnawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi.
 
Kwa mujibu wa taarifa ya habari ITV saa 2 usiku huu, mfanyabiashara mmoja mjini Sumbawanga ameuwawa baada ya kuvamiwa na kushambuliwa kwa risasi na askari polisi, akiwa nyumbani kwake mjini Sumbawanga kwa kutuhumiwa kwa wizi.


MYTAKE.
Chondechonde polisi mnawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi.

Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?
 
we acha bwana tabia polisi inatia hasira ukijaribu kuangalia wengine ni MAMULUGO KWA KUFOJI VYETI NA KUTUMIA VYETI VYA WATU IVI ile moto uliowashwa kukagua vyeti vya maaskari ulifikia wapi?
 
Yale yale!!!!! Tukisema kazi imewashinda wanakataa...Vifo vya kutuhumiwa mpaka lini? Kuna agenda gani iliyofichika? It's too much jamani
 
Polisi wenyewe ndio MAJAMBAZI, kwani mtu akiwa mtuhumiwa ndio apigwe kwa risasi? Hapo ni kwamba walisikia anapesa nyingi na wanataka kuzichukua na kupotezea ushahidi kiaina huku wakimbambikia tuhuma za wizi.

toka lini na wapi hiyo hutoke polisi akauwe mtu home kwake?
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

we USITUTAFUTIE BAN ZISIZO NA MSINGI KWANI HAJUI KUA WANANCHI HAWANA IMANI NA POLISI KAMA WE NDIO MSEMAJI HAPA JAMVINI UMEBUGI TENA SANA raia hawana imani na jeshi la polisi kamwambie MAKENGEZA IVYO
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?
Kwani sheria inaruhusu kuua wahalifu?
 
we USITUTAFUTIE BAN ZISIZO NA MSINGI KWANI HAJUI KUA WANANCHI HAWANA IMANI NA POLISI KAMA WE NDIO MSEMAJI HAPA JAMVINI UMEBUGI TENA SANA raia hawana imani na jeshi la polisi kamwambie MAKENGEZA IVYO

Siwezi kukulaumu kwasababu inawezekana mimba yako ilitungwa kwenye nyumba ya wageni.
 
Kwani lazima wakimtuhumu mtu wamuue?? inamaana hamna namna nyingine ya kufanya, nazani Jeshi letu linatakiwa kuwa trained ku deal na vitu vya namna hii bila mauaji
 
Ile kidhibiti ya madawa ya kulevya ilopelekqa kwa mkemia mkuu ili hali ikiwa ni mchanganyiko wa sukari na chumvi; vipi ilikuwa inatufikishia ujumbe gani sisi wananchi?

Anyway, wengine wanasema mjini shule huenda kuna watu wamejifunza kitu ktk hili na mengine yajayo.
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Kwa hiyo ndo auliwe? Mbona watu mnakuwa vilaza kiasi hicho? Kweli watu mkishalaaniwa uwezo wa kutambua mema na mabaya hupotea!
 
mimi nadhani hili jeshi la polisi linatakiwa lisafishwe kabisa
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?


Wewe pia una makosa katika hoja yako. Taarifa inaonesha polisi wametoa hukumu ya kosa nje ya mahakama. Hakuna uhalali wa kutoa adhabu kwa tuhuma tu kwa mtu. Adhabu inatakiwa kutoka baada ta tuhuma husika kuthibitishwa kama ni kweli. Kwa hiyo bado hao polisi wako unaowatetea wana makosa. Pili, unapozungumzia jambo la kujenga chuki dhidi ya polisi unamaanisha chuki ilikuwa hakuna. Hapa pia mtizamo wako una makosa kwa sababu chuku dhidi ya polisi ipo muda mrefu. Kwa hiyo kama kuna kitu kinafanyika sasa ni kuiongeza hiyo chuki dhidi ya polisi kwa sababu hiyo chuki iliishajengwa siku nyingi. Makadirio yangu ni kwamba katika kila watanzania 10 utaozungumza nao, 9 wanalichukia jeshi la polisi kwa kuendesha jeshi hilo kwa rushwa, kupandikizia wananchi kesi za kutunga, kupora kazi za mahakama, na kuajiri vilaza huko.
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Katika mfumo wa sheria ni mahakama pekee inaweza kuthibitisha uhatia wa mtu na si vingenevyo,polisi wanaruhusa ya kutumia silaha kwa armed bandit aliyekataa kusurrender.....
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Kwa hiyo kama alikuwa mwizi uhalali wa polisi kumuua upo wapi?.Watanzania mmekuwaje mnashabikia mauaji.
 
Hilo linaloshabikia litakuwa polisi lenzao
 
Kwa hiyo kama alikuwa mwizi uhalali wa polisi kumuua upo wapi?.Watanzania mmekuwaje mnashabikia mauaji.
Hiyo ni kawaida ya viwavi wa CCM,kazi yao kubwa ni kuitetea serikali kwa nguvu zao zote,wengine ndio ajira yao hiyo mwisho wa siku wanapanga foleni Lumumba kama wakoma.
 
Taarifa imesema alituhumiwa kwa wizi, hiyo ya kudai polisi wanawamaliza wananchi wasio na hatia huku wahalifu wakijivinjari bila wasiwasi inatoka wapi tena? Au unataka kujenga chuki kati ya polisi na wananchi? Wananchi wakilichukia jeshi la polisi wewe utafaidika na nini?

Kwa hiyo mtu akituhumiwa kwa wizi adhabu yake ni kupigwa risasi hadi kufa? Au ni sheria mpya ya MAGAMBA walio waambia Polisi kule kwenye mkutano wao Dom???!!! Mbona wapo watu walio kwisha hukumiwa kunyongwa huko Magerezani na hawajanyongwa? Iweje hawa watuhumiwa huku uraiani wauawe kisa ni kutuhumiwa tu??
 
Back
Top Bottom