John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 712
- 1,240
Kati ya maswali na masuala ambayo watumishi wengi wa umma wamekuwa wakijiuliza ama kuyatakakari baada ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi ni haki, wajibu na mipaka yao katika kujihusisha na siasa zikiwemo za vyama.
Aidha majibu mepesi ya maswali hayo yamekuwa ni hisia finyu kuwa watumishi wote wa umma hawapaswi kujihusisha na vyama vya siasa. Ama kwa kwa upande mwingine yamekuwepo pia mawazo potofu kwamba watumishi wa umma wanapaswa kujihusisha na chama kinachotawala pekee na hawapaswi kabisa kujihusisha na vyama vya upinzani. Aidha wapo watumishi wa umma ambao wamekuwa wakitoa maneno ama kufanya vitendo ambavyo hawaruhusiwi kufanya katika ushiriki wao katika siasa.
Kabla ya chaguzi ndogo za Busanda na Biharamulo niliandika mfululizo wa makala nne kuchambua suala hili mintaarafu Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma kuhusu maadili ya watumishi wa umma katika mfumo wa vyama vingi kwa kurejea pia sheria na kanuni zinazohusika. Nawaletea makala hizi hapa, kama sehemu ya kuendeleza mjadala kuhusu suala husika.
Katika mfululizo huu, sijachambua hatua ambazo mtumishi wa umma anayetaka kugombea uongozi wa kisiasa anapaswa kuzifuata, sijachambua masuala mahususi kuhusu Ubunge wa Afrika Mashariki na sijazungumzia mambo ambayo si ruhusa kwa watumishi wa umma kuyafanya kuhusiana na ushiriki wao kwenye siasa. Uchambuzi wa masuala hayo na mengine utafuata katika hatua ya baadaye. Nawatakia mjadala mwema
JJ
Aidha majibu mepesi ya maswali hayo yamekuwa ni hisia finyu kuwa watumishi wote wa umma hawapaswi kujihusisha na vyama vya siasa. Ama kwa kwa upande mwingine yamekuwepo pia mawazo potofu kwamba watumishi wa umma wanapaswa kujihusisha na chama kinachotawala pekee na hawapaswi kabisa kujihusisha na vyama vya upinzani. Aidha wapo watumishi wa umma ambao wamekuwa wakitoa maneno ama kufanya vitendo ambavyo hawaruhusiwi kufanya katika ushiriki wao katika siasa.
Kabla ya chaguzi ndogo za Busanda na Biharamulo niliandika mfululizo wa makala nne kuchambua suala hili mintaarafu Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma kuhusu maadili ya watumishi wa umma katika mfumo wa vyama vingi kwa kurejea pia sheria na kanuni zinazohusika. Nawaletea makala hizi hapa, kama sehemu ya kuendeleza mjadala kuhusu suala husika.
Katika mfululizo huu, sijachambua hatua ambazo mtumishi wa umma anayetaka kugombea uongozi wa kisiasa anapaswa kuzifuata, sijachambua masuala mahususi kuhusu Ubunge wa Afrika Mashariki na sijazungumzia mambo ambayo si ruhusa kwa watumishi wa umma kuyafanya kuhusiana na ushiriki wao kwenye siasa. Uchambuzi wa masuala hayo na mengine utafuata katika hatua ya baadaye. Nawatakia mjadala mwema
JJ
IX Political Neutrality:
Political Participation
I. A Public Servant can participate in politics provided that when so doing he/she observes the following limitations:-
i) shall not conduct or engage oneself with political activities during official hours or at work premises;
ii) shall not take part in political activity which will compromise or be seen to compromise his/her loyalty to the Government;
iii) shall not provide services with bias due to his/her political affiliation;
iv) shall not pass information or documents availed through his/her position in the service to his/her political party.
Political Influence
II. Although public servants have a right to communicate with their political representatives they:-
i) shall not use such influence to intervene on matters affecting him/her which are in dispute between the government and him/her;
ii) shall not use such influence for furthering personal ends which are not part of the Government policy.
pakua na soma Tanzania Code of Ethics for Public Servants
Kuwa Mbunge na kuwa mtumishi wa umma.
7th August 2012
Leo wakati anachangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira Mbunge wa Viti maalumu Mtoto wa kike wa Mzee Kawawa alianza kuchangia kwa kudeclare interest kwamba yeye bado ni mfanyakazi wa mfuko wa hifadhi ya jamii ambao hakuutaja jina na kwa sasa tokea ameteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu (ccm) yupo kwenye likizo ndefu ya bila malipo.
kwa uelewa wangu mimi Serikali ilitoa waraka wa kuwataka watumishi wote wa umma ikiwemo watumishi wa mifuko ya hifadhi ya jamii watakaogombea ubunge na majina yao yakishapitishwa na NEC anatakiwa astaafu utumishi wa umma.
Inakuaje huyu mheshimiwa binti wa mzee kawawa bado ni muajiriwa wa mfuko huo aliodeclare interest na kwamba eti yupo likizo bila malipo.
Mi nadhani kwa uelewa wangu si sahihi anapaswa kwa maelekezo ya serikali alitakiwa awe amestaafu na sio kuwa likizo bila malipo au labda yeye ni wa viti maalumu au anaupendeleo maalumu kwa kuwa binti wa Mzee kawawa?
Naomba kujuzwa zaidi kuhusiana na hili suala labda uelewa wangu sio sahihi
WARAKA : Sheria Mpya Kwa Watumishi Wa Umma Kugombea Nafasi Za Kisiasa Uchaguzi 2015
IKULU imetoa waraka mpya kwa watumishi wa umma wenye nia ya kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa, ikiwamo urais, ubunge na udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Kwa mujibu wa waraka huo, mtumishi wa umma anayetaka kuwania moja ya nafasi hizo za kisiasa, atalazimika kuacha kazi na kulipwa mafao yake, endapo jina lake litateuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kama mgombea.
Waraka huo wenye Kumbukumbu CAB 157/547/01/47 ukiwa na kichwa cha habari ‘Kuhusu utaratibu kwa watumishi wa umma wanaogombea nyadhifa za kisiasa nchini', umetolewa Januari 2, mwaka huu na kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.
Pamoja na mambo mengine, utaratibu huo umelenga kuondoa upendeleo katika utoaji huduma kwa wananchi na matumizi mabaya ya ofisi kunakofanywa na baadhi ya watumishi wa umma wenye nafasi za kisiasa.
"Baadhi ya watumishi wa umma wenye nafasi za uongozi wa kisiasa wamekuwa wakitoa huduma kwa upendeleo, hususani pale anayehudumiwa akiwa mpigakura wake au anatoka katika chama chake cha siasa," unasema waraka huo..
Waraka huo uneongeza kuwa baadhi ya watumishi hao wa umma wenye nafasi za kisiasa, wamekuwa wakitumia nafasi walizanazo katika ofisi zao kushawishi watumishi wenzao kupigia kura chama fulani au mgombea fulani.
Aidha unasema upo uwezekano wa kuwapo mgongano wa kimasilahi baina ya siasa na utumishi wa umma, ambao unaweza kusababisha baadhi ya watumishi wasio waadilifu kutoa siri za Serikali kwa masilahi ya kisiasa.
"Katika baadhi ya kazi imekuwapo migongano baina ya watumishi ambao ni viongozi wa kisiasa na menejimenti, hasa katika masuala ya kinidhamu, hali ambayo inaathiri ufanisi wa kazi.
"Kutokana na kasoro hizo na ili kuhakikisha kazi za kiutendaji haziingiliani na kuathiriwa na shughuli za kisiasa, Serikali imeamua kutoa mwongozo mpya kwa lengo la kurekebisha kasoro zilizojitokeza.
"Kwa msingi huo, Serikali imetoa utaratibu utakaozingatiwa na watumishi wote wa umma watakaogombea nafasi za uongozi wa kisiasa katika ngazi mbalimbali," ilisema sehemu ya waraka huo.
Waraka huo unasema madhumuni yake ni kuweka mipaka ya nafasi ya mtumishi wa umma anapoamua kushiriki kwenye shughuli za kisiasa bila kuathiri utendaji wa shughuli za Serikali.
Maelekezo ya Serikali:
"Mtumishi wa umma atakayeamua kugombea ubunge wa viti maalumu aruhusiwe kufanya hivyo na baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kumtangaza kuwa mbunge, utumishi wake ukome na alipwe mafao yake," ilisema sehemu ya waraka huo.
Waraka huo unasema mtumishi atakayeamua kugombea ubunge katika Bunge la Afrika Mashariki, Bunge la Jamhuri ya Muunguno na udiwani watalazimika kuacha kazi na kulipwa mafao yao.
"Mtumishi wa umma anayeteuliwa na waziri mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuwa diwani, atakuwa na hiari ya kuchukua likizo bila malipo kwa kipindi chote cha wadhifa huo."
Pia waraka huo umesema endapo mtumishi atashindwa katika uchaguzi na anataka kurudi kwenye utumishi wa umma, hana budi kuomba upya ajira kwa mamlaka zinazohusika.
Aidha waraka huo umeonya kuwa mtumishi atakayekiuka maelekezo hayo atachukuliwa hatua za kinidhamu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu katika chombo anachokisimamia.
Waraka huo umetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 8 (1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Sura 298 na kuanza kutumika Desemba mosi, 2014.
Masharti hayo ni tofauti na utaratibu uliokuwapo awali ambao unaruhusu mtumishi wa umma kugombea nafasi za kisiasa kwa kuomba likizo bila malipo, huku akitambuliwa bado ni mtumishi aliyepo kazini.