'Ruksa' kwa watumishi wa umma kushiriki siasa

Wakuu,

nijuavyo mimi, Murunya yuko mamlaka ya Ngorongoro.... sasa alijiuzulu nafasi yake ya ukurugenzi kabla ya kugombea EALA?? na kama hapana je ni sawa kisheria na taratibu ilhali bado ni mtumishi wa umma

Hii ina maana gani kwa watumishi wa serikali, na je angegombea kupitia chama cha upinzani bado hili lisingehojiwa??

MSAADA TAFADHALI
 
Hata akirudi selikarini aminini kwamba hana chama wala hatatumika kwa minajiri ya chama. hahahahahaaaaaaaa
 
Asilimia kubwa hawana utashi wala maarifa ya kuongoza watu. Ila ndo hivyo tena...siasa na mifumo inawabeba na kuwapendelea
 
Huyu freemason alikuwa anaishi usa kufanyakazi ngorongoro, jamani ingekuwa ndio uamuzi wangu huyu mngemkuta segerea maana amefanya ufisadi wa kutisha ngorongoro, mungu okoa taifa hili, hata mrunya' jamani waoneeni hurumz watz, wamechoka eti, yaani fisadi kama huyu eti mbunge ee yehova tusaidie
 
Asilimia kubwa hawana utashi wala maarifa ya kuongoza watu. Ila ndo hivyo tena...siasa na mifumo inawabeba na kuwapendelea
Mrunya amesha staff NCAA. Huyu jamaa ni kiazi kwa kwenda mbele. Vipi amefanikiwa ubunge wa EA ? Nilisikia anagombea.
 
Kuwa Mbunge na kuwa mtumishi wa umma.

7th August 2012
Leo wakati anachangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira Mbunge wa Viti maalumu Mtoto wa kike wa Mzee Kawawa alianza kuchangia kwa kudeclare interest kwamba yeye bado ni mfanyakazi wa mfuko wa hifadhi ya jamii ambao hakuutaja jina na kwa sasa tokea ameteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu (ccm) yupo kwenye likizo ndefu ya bila malipo.

kwa uelewa wangu mimi Serikali ilitoa waraka wa kuwataka watumishi wote wa umma ikiwemo watumishi wa mifuko ya hifadhi ya jamii watakaogombea ubunge na majina yao yakishapitishwa na NEC anatakiwa astaafu utumishi wa umma.

Inakuaje huyu mheshimiwa binti wa mzee kawawa bado ni muajiriwa wa mfuko huo aliodeclare interest na kwamba eti yupo likizo bila malipo.

Mi nadhani kwa uelewa wangu si sahihi anapaswa kwa maelekezo ya serikali alitakiwa awe amestaafu na sio kuwa likizo bila malipo au labda yeye ni wa viti maalumu au anaupendeleo maalumu kwa kuwa binti wa Mzee kawawa?

Naomba kujuzwa zaidi kuhusiana na hili suala labda uelewa wangu sio sahihi
 
Tatizo lenu ni kutumia hili neno UBUNGE wakati nchi za wenzenu hutumia neno "Representative", kitu ambacho hata Zanzibar wamekifanya.

Nani alikuambia kwamba uwakilishi ni ajira? Kama ni ajira ni taasisi gani imemuajiri? Ingekuwa hivyo basi uwakilishi wowote ukiwamo uwakilishi wa kijiji au hata udiwani basi ungekuwa ni ajira.

Kuna sheria ya ajira. Sasa wawakilishi wanakuwa coverede vipi na hii. Muda wa kazi unajulikana ni masaa mangapi kwa wiki. Je, muwakilishi muda wake kwa wiki ni kiasi gani kwa kulingana na ajira?

Sheria ya ajira inaweka likizo siku 28 kama sikosei. Je huyo mwakilishi {mbunge} likizo yake ni muda gani kama ulishawahi kusikia mbunge ameenda likizo?

Hivyo, huyo dada yuko sahihi kabisa. Kama nitahitajika kufafanua zaidi basi nasubiri michango yenu.
 
CCM na Utawala wa kifalme! watoto wa viongozi hao, hawaguswi na sheria wakiwa ccm
 
Tatizo lenu ni kutumia hili neno UBUNGE wakati nchi za wenzenu hutumia neno "Representative", kitu ambacho hata Zanzibar wamekifanya.

Nani alikuambia kwamba uwakilishi ni ajira? Kama ni ajira ni taasisi gani imemuajiri? Ingekuwa hivyo basi uwakilishi wowote ukiwamo uwakilishi wa kijiji au hata udiwani basi ungekuwa ni ajira.

Kuna sheria ya ajira. Sasa wawakilishi wanakuwa coverede vipi na hii. Muda wa kazi unajulikana ni masaa mangapi kwa wiki. Je, muwakilishi muda wake kwa wiki ni kiasi gani kwa kulingana na ajira?

Sheria ya ajira inaweka likizo siku 28 kama sikosei. Je huyo mwakilishi {mbunge} likizo yake ni muda gani kama ulishawahi kusikia mbunge ameenda likizo?

Hivyo, huyo dada yuko sahihi kabisa. Kama nitahitajika kufafanua zaidi basi nasubiri michango yenu.

Oh kumbe ubunge sio ajira! Ni nini basi mbona umepaacha wazi? Mama lishe ambaye anafanya kazi zaidi mara utakavyo ya isemavyo hiyo sheria yako ya ajira, hana ajira....au kwa vile hana likizo ya siku 28! Tafsiri yako ya ajira ni so narrow kama ndio hivi. Basi the unemployed ni wengi kuliko data zitolewazo!
 
Oh kumbe ubunge sio ajira! Ni nini basi mbona umepaacha wazi? Mama lishe ambaye anafanya kazi zaidi mara utakavyo ya isemavyo hiyo sheria yako ya ajira, hana ajira....au kwa vile hana likizo ya siku 28! Tafsiri yako ya ajira ni so narrow kama ndio hivi. Basi the unemployed ni wengi kuliko data zitolewazo!

Kabla ya kuuliza maswali zaidi jibu swali langu kwamba iwapo unadhani ubunge ni ajira basi ni taasisi gani imemuajiri?
 
Kabla ya kuuliza maswali zaidi jibu swali langu kwamba iwapo unadhani ubunge ni ajira basi ni taasisi gani imemuajiri?

Kwa Tanzania mbunge/ubunge ni AJIRA ndiyo maana wanalipwa MISHAHARA, PENSHENI baada ya kumaliza kipindi chao cha miaka mitano.

Taasisi iliyowaajiri ni OFISI YA BUNGE, Jana tumesambaziwa waraka unaonesha mishahara ya WAFANYAKAZI WA OFISI YA BUNGE japo ya WABUNGE ILIFICHWA.

Kama Ubunge usingekuwa kazi ya ajira basi ofisi ya bunge isingehangaika kuwalipa mishahara na kiinua mgongo
 
Kabla ya kuuliza maswali zaidi jibu swali langu kwamba iwapo unadhani ubunge ni ajira basi ni taasisi gani imemuajiri?

Nilisikia siku hizi mshahara wao ni milioni kumi na moja! Nani anawalipa huo mshahara kama sio mwajiri!
 
Kuna jamaa zangu walikuwa ni waajiriwa wa mifuko hiyo hiyo ya hifadhi ya jamii kabla ya uchaguzi mkuu. Ilibidi waachie kazi kwanza ili kwenda kugombea kwa tiketi ya CCM. Bahati mbaya kwao wakapigwa chini na CDM. Hadi leo hii hawajafanikiwa kurejea kazini, wanasema kibali hicho kinatolewa na Katibu Mkuu Kiongozi. Bado hajatoa sasa. Walidanganyika wakaingia chaka. Sasa mnaponiambia kuna Mbunge kabisa and still bado ni mwajiriwa, naukumbuka usemi kuwa binadamu wote ni sawa lakini sio sawasawa! Au ubunge wa upendeleo hauhusiki na kanuni hizi za utumishi wa umma? Anyway, ni upepo tu!
 
Leo wakati anachangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira Mbunge wa Viti maalumu Mtoto wa kike wa
Mzee Kawawa alianza kuchangia kwa kudeclare interest kwamba yeye bado ni mfanyakazi wa mfuko wa hifadhi ya jamii ambao hakuutaja jina na kwa sasa tokea ameteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu (ccm) yupo kwenye likizo ndefu ya bila malipo.
kwa uelewa wangu mimi Serikali ilitoa waraka wa kuwataka watumishi wote wa umma ikiwemo watumishi wa mifuko ya hifadhi ya jamii watakaogombea ubunge na majina yao yakishapitishwa na NEC anatakiwa astaafu utumishi wa umma.
Inakuaje huyu mheshimiwa binti wa mzee kawawa bado ni muajiriwa wa mfuko huo aliodeclare interest na kwamba eti yupo likizo bila malipo.
Mi nadhani kwa uelewa wangu si sahihi anapaswa kwa maelekezo ya serikali alitakiwa awe amestaafu na sio kuwa likizo bila malipo au labda yeye ni wa viti maalumu au anaupendeleo maalumu kwa kuwa binti wa Mzee kawawa?
Naomba kujuzwa zaidi kuhusiana na hili suala labda uelewa wangu sio sahihi

Serikali inatambua likizo isiyokua na malipokwa wafanyakazi wote. Mtumishi wa Umma anaweza kupata kazi UN au ofisi yoyote isiyo ya serikali bila kupoteza kazi yake ya utumishi wa umma, anachotakiwa kufanya ni kuomba likizo isiyokua na malipo. Pindi akimaliza mkataba wake anarudi katika utumishi wa umma. Siyo jambo geni katika utumishi wa umma hilo.

Mh D. Kamala alikua mbunge wa Nkenge baada ya kushindwa ubunge alirudi kwenye ajira yake ya mwanzo. mwininge ni
Dk Sengongo Mvungi mwaka 2005 aligombea Uraisi kupitia NCCR baada ya uchaguzi akarudi kwenye ajira yake ya mwanzo. Wapo wengi wenye kesi kama hizo siyo huyo tu.
 
Kwa Tanzania mbunge/ubunge ni AJIRA ndiyo maana wanalipwa MISHAHARA, PENSHENI baada ya kumaliza kipindi chao cha miaka mitano.

Taasisi iliyowaajiri ni OFISI YA BUNGE, Jana tumesambaziwa waraka unaonesha mishahara ya WAFANYAKAZI WA OFISI YA BUNGE japo ya WABUNGE ILIFICHWA.

Kama Ubunge usingekuwa kazi ya ajira basi ofisi ya bunge isingehangaika kuwalipa mishahara na kiinua mgongo

Mheshimiwa,

Mnatakiwa ku-research mambo na si kufuata mkumbo kwa sababu wengi wanasema. Nimesema ubunge ni uwakilishi na hakuna mwakilishi anayelipwa mshahara. Mwakilishi hulipwa allowance na si mshahara.

Wala hunifundishi kutamka au kusikia neno mshahara wa mbunge. Ninajua Tanzania wengi mnajua kwamba mbunge analipwa mshahara kwa sababu vyombo vya habari vinaandika hivyo.

Lakini hayo ni makosa ya kiswahili kukosa neno sahihi ya kile anacholipwa mwakilishi. Kama anacholipwa mfanyakazi ni mshahara {salary} basi anacholipwa mwakilishi huwezi kukiita salary kwa sababu nilizoeleza hapo juu na hutaki kuziamini kwamba mbunge si mwajiriwa wa taasisi yoyote.

Mkutano wa Bajeti ndiyoo mrefu kupita yote kwani mingine ina siku zisizozidi 10. Sasa utasemaje kuwa huyo ni mfanyakazi na hivyo kinachoingia mfukoni mwake kwa uwakilishi wa ain hiyo kiitwe mshahara.

Hivyo, ninajua kuna hela inaingia mfukoni mwa mbunge lakini kwa muelewa ataona aibu kuiita salary au mshahara. Tutafute neno lolote tu la kiswahili lakini si mshahara kama unaopokea wewe.

Nimeuliza maswali yanayosaidia kuelewa lakini hamtaki kujibu. Nimeuliza ni lini mbunge anachukua likizo ya siku 28 au hata ya uzazi. Sasa ni ajira hgani haina likizo.

Hapo juu umeeleza mishahara ya watumishi au staff wa ofisi ya Bunge. Kuanzia Spika, Katibu wa Bunge na staff wote pale ofisini ni tofauti kabisa na wabunge unaowafananisha. BUnge likiisha wabunge wanarudi majimboni kwao. Hawa staff wa pale wanaendelea kuchapa kazi zao tena wengine wako Dodoma na wengine wako D'Salaam. Ofisi ya BUnge inayowalipa iko chini ya Waziri Mkuu na kama sikosei ni ile portfolio anayoshughulikia Lukuvi.

Kitendo cha katibu wa bunge na staff wenzake kubaki ofisini na kufanya kazi kila siku, kingetosha kukupa picha kwamba hawa ni staff yaani watumishi wa umma na wabunge si staff.

Kingine ni kwamba angalia kiapo cha mbunge na kiapo cha mtumishi wa umma. Hapa mtumishi wa umma ni kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Waziri na Spika.

Watumishi wa umma hawa wanaapa viapo viwili yaani kiapo cha uaminifu kwa Jamhuri. Lakini vilevile wakimaliza kuapa cha Uaminifu wanaapa kingine kiitwcho kiapo cha Ofisi yaani kuzitumikia ofisi zao.

Ndiyo sababu unakuta Rais, huapa mara mbili. Vivyo hivyo Spika huapa mara mbili mle Bungeni wakati mbunge huapa mara moja tu. Mbunge hana kiapo cha Ofisi kwa sababu hana ofisi katika Jamhuri hii inayotambua kazi yake kwamba akabidhiwe hiyo ofisi na ndani ya hiyo ofisi atapata mshahara.

Hata ukiangalia Job description kwenye Katiba imetaja majukumu ya viongozi watano kama ifuatavyo: {Rais (Ib. 33-37), Makamu wa Rais (Ib. 47-48), Waziri Mkuu (Ib. 52), Waziri (Ib. 58), Jaji Mkuu (Ib. 119)}.

Sura ya tatu ya Katiba imetengwa kuelezea utekelezaji wa Bunge na ipo kwenye ibara ya 62 hadi 101. Katika ibara zote hizo 40, hakuna hata moja inayotaja majukumu au madaraka ya binadamu tunayemuita Mbunge. Badala yake, ibara ya 63 na 64 imetaja na kufafanua majukumu ya mkusanyiko mzima unaoitwa Bunge.

Hivyo, hakuna sentensi hata moja kweny ekatiba inayotaja jukumu la binadamu tunayemuita mbunge na kwamba kwa jukumu hilo anastahili kuitwa mwajiriwa au kupewa hicho mnachoita mshahara.

Hivyo, hakuna kitu kiitwcho mshahara wa mbunge ambao ungekuwepo ungeenda kwenye pension organisations. Lakini haiko hivyo na ndiyo maana wewe unachokiita kiinua mgogo cha mbunge kiuhalisia kinaitwa GRATUITY. Sasa hili nalo kwangu ni tatizo maana sijui neno GRATUITY kwa kiswahili.

Kama sijaeleweka niko tayari kurudi.
 
Mh D. Kamala alikua mbunge wa Nkenge baada ya kushindwa ubunge alirudi kwenye ajira yake ya mwanzo. mwininge ni Dk Sengongo Mvungi mwaka 2005 aligombea Uraisi kupitia NCCR baada ya uchaguzi akarudi kwenye ajira yake ya mwanzo. Wapo wengi wenye kesi kama hizo siyo huyo tu.

Acha uongo wewe Dr.(?) Kamala aliposhindwa ubunge wa Nkenge hakurudi MZUMBE IDM kufundisha.

Dr. Mvungi alikuwa mgombea, hakuchagulia, wapo aspirants wengi tu kutoka CCM walioshindwa kwenye preferential votes na wengine kwenye general election lakini wakarudi makazini. Tatizo hapa ni kwamba tayari umechaguliwa wether VITI MAALUM au kupitia JIMBO automatically unapoteza ajira ya utumishi wa umma.

BTW, serikali siku nyingi ilishasitisha LIKIZO BILA MALIPO, unless for special jobs kama wale wanaokwenda kufanya kazi kwenye International organization. Sijui kama viti maalumu ni SPECIAL JOBS.

But one thing I'm SURE for, and I bet my neck. First Kama huyo binti asingekuwa mtoto wa Kawawa and Second Kama binti huyo angeupata huo ubunge wa viti maalumu kupitia vyama vya UPINZANI. Believe asingerudi tena NSSF.

BTW, sikapendi haka ka-binti kwani eti ndiyo kawa wakilishi ka wafanyakazi kupitia viti maalumu, lakini sijakasikia hata siku moja kakitetea wafanyakazi kuhusu sheria kandamizi ya SSRA ya kuzuia mafao ya kujitoa. UZURI WA MKAKASI NDANI NI KIPANDE CHA MTI!
 
Oh kumbe ubunge sio ajira! Ni nini basi mbona umepaacha wazi? Mama lishe ambaye anafanya kazi zaidi mara utakavyo ya isemavyo hiyo sheria yako ya ajira, hana ajira....au kwa vile hana likizo ya siku 28! Tafsiri yako ya ajira ni so narrow kama ndio hivi. Basi the unemployed ni wengi kuliko data zitolewazo!

Mama Lishe si muajiriwa wala muwakilish bali ni mfanyabiashara yaani muuza chakula.
 
Back
Top Bottom