Ruge Mutahaba kubali kuwa mlikosea

Ruge Mutahaba kubali kuwa mlikosea

HA ha ha nimemsikiliza zamalad mwenyewe ktk ayo tv naona katumia maneno makali sana dhid ya waliomkosoa kwamba et upeo wao wa kufikili ni mdogo, ikumbukwe kwamba ndan ya waliokosoa wakiwemo TCRA, MAKONDA na BAADHI YA WANANCHI hii kauli sikuipenda na inatafsiri pana ingawa yeye na upeo wake mkubwa kama anavyodai kashindwa kuliona hilo coz had rais naye upeo wake ni mdogo kwa mujibu wake kwan ndiye aliye mteua mh makonda
my take;
unapotaka kuzungumza jambo ebu kua na uwanja mpana wa kufikilia kabla kutenda na sio unaroporopo tu kisa una uhuru wa kuongea
Zamaradi upeo wake ni wa kuandaa vipindi na kina wema na wolper maana angalau anajua maovyovyo yao vipi kama hii awaachie kina Vicky Ntetema na nguli wengine wanaojua
 
Taifa la kinafiki hili...........si ajabu huyo Kaoge bado yupo mtaani bila kubugudhiwa wala kutafutwa..
 
Badala ya kuishambulia Clouds na Ruge, ebu atafutwe Kaoge na akamatwe ashtakiwe kwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.Hii ni jinai, hatuna sababu.Hv nikıjitoa hadharani kwenye TV kwamba mimi ndo nimemua Askari nitaachwa?
Itakuwa alihidiwa"kulindwa"kwanza
 
Wanaosema kile kipindi kimefundisha, kimefundisha nini? Nani hajui kuwa kuna mashoga na athari za uushoga zipoje? Kwa nini yule shoga hakuzungumzia madhara ya ushoga? Kama ni kufundisha kwa nini wasimlete daktari ili aweze kueleza madhara ya ushoga na huyo shoga ajue na ajibu maswali hapo kama anakubali kuendelea na hiyo kazi au vipi baada ya kujua madhara? Kuomba mtaalam wa kupachikwa mimba nalo ni jambo la kutetea? Vipi kwa vijana walio angalia kile kipindi na wao wakaona njia ya ushoga ni bora wanaweza pata watoto bila kuoa watakuwa wameisaidia jamii? Kile kipindi kilipaisha ushoga badala ya kuelea athari za ushoga.
 
Clouds tv sahiv inaonekana nchi yingi za EastAfrica na nyinginezo kupitia dstv, sasa kwa jambo kama lile linaonyesha jamii ya Africa kwamba sisi Tz ndo tulivo ukizingatia kiswahili ni maarufu zahiv
 
Hao jamaaa nasikia pale mjengone kuna vijana wake nao ni majerui
 
Kutokana na michango ya wadau nimejifunza kuwa,
-Hata humu JF kuna mashoga wengi tu.
-Vyombo vya dola haviwajibiki, kama kutomkamata huyo shoga alijipata promo ya bure.
-Regulatory Authority kama TCRA inatoa maamuzi kwa uoga. Adhabu gani ndogo namna hiyo! Tena hii sio mara ya kwanza kwa Clouds...ndio maana wanatuhumiwa pale kuna mashoga.
-Media zinatumika kama toilet paper hawa Clouds Media.
-Nashauri tukapate ushauri Gambia, Zimbabwe na Uganda ili tujitambue zaidi kuwa sisi ni wanaume wa kiafrika na sio vibaraka wa kupelekeshwa na tamaduni za kubomoa.
 
Ila huo msamaha waombe wa nini? Ni uoga tu wa kutumbuliwa, haya mambo yapo na ni vizuri watu wakayajua.

Nina uhakika kipindi hicho kimesaidia wengi kwa njia mbalimbali kwa mazuri.
watu wayajue ili iweje?
 
Hakuna asiyefahamu kuwa haya mambo yapo na yapo tangu enzi na enzi. Ukisoma vitabu vitakatifu vya dini ikiwemo Biblia utakuta haya mambo yanazungumziwa ambapo ni ishara kwamba yapo tangu miaka maelfu mia huko nyuma, lakini hoja hapa ni kwamba: hivi kitu kibaya katika jamii huwa kinaelezewa kwa kukemea au kwa kujaribu kukipamba!?

Ukitafsiri maudhui ya kile kipindi, je, kilikuwa kinaikanya jamii kuachana na hiyo kasumba au kilikuwa kinaishawishi jamii kuona ushoga ni jambo la kawaida!? Kwa namna walivyohojiana, ni mashoga wangapi wangejiona wako njia mbaya na wanatakiwa kuacha na ni mashoga wangapi walifurahi na kujiona wako njia sahihi (tena wengine walimpongeza eti amejieleza vizuri na kwa kujiamin)!? Ukijaribu kutafsiri yale mahojiano, unadhani asilimia ya watu waliovutiwa na kuhamasika na ushoga huenda hata kutamani kuendelea au kuingia kabisa inalingana na waliohamasika kuacha!? TAFAKARI
Vitabu vya dini ndo mdudu gani? Kwanza yakupasa ujue hakuna kitu kinaitwa mungu
 
Wabongo ukiwaonesha kitu kwa ku-point kwa kidole wanang'ang'ania kuangalia kidole chako badala ya kitu ulichoki-point.

Remmy Ongala naye alikumbana na kadhia hii pale alipoachia wimbo wake wa "Mambo kwa Soksi",ulifungiwa kwa hoja hii hii ya maadili lakini leo hii serikali yenyewe kupitia wizara ya afya kila saa wanatangaza CONDOM tena bila tafsida.

Hivi maadili ya nchi hii si yaandikiwe kitabu tuyajue wote kuliko ilivyo sasa au huwa yanabadilika?
 
Unakimbia kivuli chako mwenyewe ilihali umemulikwa na mwanga wa ukweli.... "Kaoge" kaongea vitu vingi sana kuhusu "wenzake" so kwanini wasichukue data hizo kukomesha hayo mambo.... Sitaki kuelemea upande wowote, ila tuzungumze ukweli hata kama hatutaki kuusikia, lasivyo itakuwa tunajidanganya as hayo mambo Kwenye jamii zetu yapo na yanaendelea..
 
Hivi wajibu wa chombo cha habari ni kutangaza yanayotokea (news) au yanayotakiwa na mamlaka za eneo husika!?
Mfano clouds wako kwenye satellite ambapo wanaonekana nje ya maeneo yanayotawaliwa na TCRA, sasa itakuwa ni haki kama mamlaka za hapa hazitaki lakini 'tcra'/mamlaka za nchi zingine ambako kuna watazamaji/wasikilizaji wa chombo husika hazizuii kinachotangazwa kuna ubaya gani!?
Sikubaliani na ushoga lakini kama kweli tunataka kuingia kwenye ushindani wa utandawazi na kuepuka kulishwa na kupokea kila kitu kuna haja ya kuzipa uhuru hizi taasisi za utangazaji. tuwachukulie kama watu wenye uelewa na competence sawa na walioajiriwa TCRA na wanaoipenda nchi yao badala ya vitisho uchwala!
 
Zamaladi na maneno yake haya inadhihirisha asivyo na busara wala hekima, kushupaza shingo eti kisa wewe ni fulani ni ulimbukeni sana.
 
Niliangalia na nilijifunza mambo mengi sana hususani watoto wa kiume. Siungani na mawazo yako
 
Mbona hata wewe ni shoga na wala sikuchukii!

Mkuu Nyani, kwa afya yako, ukiona mada zinazoanzishwa na "mashoga" jitahidi kupita kando au piga kimya kama wasemavyo watoto wa mjini. Ukijidai kushiriki basi watakushusha hadi kiwango chao na kukushinda kwa uzoefu! Hizi ni mada maalum kwa watu maalum kwa malengo maalum. Wanajuana wenyewe.
 
Back
Top Bottom