Nimekuwa nikifuatilia matokeo ya rufaa zinazoombwa na watahiniwa wanapohisi kuonewa katika usahihishaji wa Mitihani mara baada ya Matokeo kutolewa na Baraza la Mitihani. Haya ni pamoja na matokeo ya Form IV,VI,Vyeti na Diploma za Ualimu.
Mara nyingi rufaa zote(angalia matokeo ya sasa website ya NECTA), matokeo yake huwa hayabadiliki. Wao wanaandika "Hayajabadilika"
Huko nyuma wakati niko shule ilikuwa ni kawaida walimu kama binadamu, kupitiwa na kukosesha mwanafunzi swali alilofanyavizuri. Na ni kote, Chekechea hadi vyuo. Inakuwaje NECTA kusiwe na binadamu wa namna hiyo wakati tunaambiwa wasahihishaji hukusanywa kutoka taasisi zilezle ambako tumekuwa tukishuudia kasoro hizo za kibinadamu? yahani warufaa woote hakuna aliyeshinda!!! Wote hakuna aliyekuwa na busara na kupima alichofanya kuwa hakistahili kukatiwa rufaa!!
Hivi ni sahihi na kuwatendea haki watahiniwa, rufaa zao kurejewa(kupitiwa upya) na taasisi ileile inayotuhumiwa kusahihisha vibaya? Nahisi Necta hawawezi tenda haki kwa sababu:
1) Wao ni watuhumiwa wa kutokutenda haki katika usahihishaji wa mwanzo
2) Wataacha matokeo yawe yaleyale ili kuficha udhaifu uliofanyika mwanzo
3) Wastahiki wa kushinda rufaa hawatapewa ushindi kwa kuofia hata wale wasiositahiki watakuwa wamepoteza imani kwa wasahihishaji.
Maoni yangu: Kuwepo na chombo au Kamati maalumu baada ya matokeo ambayo itafanya kazi hiyo badala ya kufanywa na Baraza. Kamati hiyo isiwe na mafungamano yoyote na NECTA. Ikibidi warufani wenyewe walipie gharama za kurejea usahihishaji. Baraza linaweza kuwekewa utaratibu kupitia kile kilichofanywa na kamati hiyo itakayojitegemea. Hapa Warufaa watakuwa wametendewa haki. Mnasemaje?
Mara nyingi rufaa zote(angalia matokeo ya sasa website ya NECTA), matokeo yake huwa hayabadiliki. Wao wanaandika "Hayajabadilika"
Huko nyuma wakati niko shule ilikuwa ni kawaida walimu kama binadamu, kupitiwa na kukosesha mwanafunzi swali alilofanyavizuri. Na ni kote, Chekechea hadi vyuo. Inakuwaje NECTA kusiwe na binadamu wa namna hiyo wakati tunaambiwa wasahihishaji hukusanywa kutoka taasisi zilezle ambako tumekuwa tukishuudia kasoro hizo za kibinadamu? yahani warufaa woote hakuna aliyeshinda!!! Wote hakuna aliyekuwa na busara na kupima alichofanya kuwa hakistahili kukatiwa rufaa!!
Hivi ni sahihi na kuwatendea haki watahiniwa, rufaa zao kurejewa(kupitiwa upya) na taasisi ileile inayotuhumiwa kusahihisha vibaya? Nahisi Necta hawawezi tenda haki kwa sababu:
1) Wao ni watuhumiwa wa kutokutenda haki katika usahihishaji wa mwanzo
2) Wataacha matokeo yawe yaleyale ili kuficha udhaifu uliofanyika mwanzo
3) Wastahiki wa kushinda rufaa hawatapewa ushindi kwa kuofia hata wale wasiositahiki watakuwa wamepoteza imani kwa wasahihishaji.
Maoni yangu: Kuwepo na chombo au Kamati maalumu baada ya matokeo ambayo itafanya kazi hiyo badala ya kufanywa na Baraza. Kamati hiyo isiwe na mafungamano yoyote na NECTA. Ikibidi warufani wenyewe walipie gharama za kurejea usahihishaji. Baraza linaweza kuwekewa utaratibu kupitia kile kilichofanywa na kamati hiyo itakayojitegemea. Hapa Warufaa watakuwa wametendewa haki. Mnasemaje?