Malafyale
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 13,813
- 11,126
MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ameeleza kusikitishwa na kushtushwa na hatua ya kundi la wabunge kupinga hatua yake ya kutaka tume huru au majaji kufanya uchunguzi upya kuhusu sakata la Richmond.
Hatua hiyo ya Rostam imekuja ikiwa ni siku moja tu baada ya wabunge watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupinga hoja yake inayoonekana kutaka kuingilia maamuzi ya Bunge.
Hawa ni wapuuzi, wanasukumwa na chuki, alisema Rostam alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli za wabunge hao; Aloyce Kimaro (Vunjo), Lucas Selelii (Nzega) na James Lembeli (Kahama).
Mbali ya hilo, mbunge huyo wa Igunga ambaye jina lake lilitajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata wa mkataba kati ya Shirika la Umeme (TANESCO) na Kampuni ya Richmond Development Company LCC alisema hoja zinazomhusisha yeye na umiliki wa mitambo ya Dowans ndizo zilizoliingiza taifa katika tatizo la giza leo hii.
Kwa hali ya kawaida miye si wa kujibizana na watu wa aina ya Kimaro... ni kudhani kwao Dowans ni yangu ndo kumepeleka nchi kuingia gizani. Aibu, alisema Rostam ambaye alilieleza Tanzania Daima kuwa alikuwa yuko nje ya nchi.
Rostam ambaye kwa mara ya kwanza aliwasilisha hoja ya kutaka kuundwa kwa tume huru au ya majaji ndani ya kikao cha maridhiano kati ya wabunge wa CCM na kamati inayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, alisema baadhi ya wabunge wanaomshambulia wanafanya hivyo si kwa matakwa yao bali kwa kutumwa na mtu ambaye hata hivyo hakumtaja.
Katika hatua nyingine, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alieleza kushangazwa na hatua ya wabunge hao kuonekana wakihofia kuundwa kwa tume huru wakati huo huo wakitamba kuwa ripoti ya kamati ya Bunge ya Richmond ilikuwa ni sahihi.
Alisema iwapo ni kweli wanakiamini wanachokipigania, basi ilikuwa ni vyema waruhusu tume ya majaji ifanye uchunguzi upya na wa haki, na ambao iwapo ungebaini wao kuhusika katika kadhia hii, wafikishwe mbele ya vyombo vya kisheria.
Kama wanaona kweli ripoti ni sahihi si ndo watapata kutuona tunachukuliwa hatua na azma yao dhidi yetu kukamilika? Haiingii akilini kuogopa, alisema.
Akimzungumzia Kimaro, mbunge huyo wa Igunga alieleza kushangazwa na hatua yake ya kuwa mstari wa mbele kushutumu wenzake ilhali ukweli ukionyesha kwamba alikuwa ameshindwa kuliongoza jimbo lake la Vunjo, ambalo lilikaribia kuchukuliwa na chama cha upinzani cha TLP.
Jimbo alilopewa na wananchi limemshinda na kidogo tupokonywe na TLP kwa sababu ya kushindwa kuliongoza, alisema Rostam.
Katika mahojiano ya simu ya jana, Rostam alirejea kauli yake aliyopata kuisema siku zilizopita kwamba, iwapo angekuwa ndiye mmiliki wa Dowans, asingeona aibu kulisema hilo kwani, huo ni mradi mkubwa ambao hauwezi kumilikiwa na Mtanzania yeyote binafsi.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti juzi, Selelii, Lembeli na Kimaro, walipinga hatua ya Rostam kutaka kuundwa kwa tume huru wakisema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni na wajibu wa Bunge.
Wabunge hao ambao siku zote wamekuwa na msimamo mkali kuhusu sakata la Richmond na masuala mengine yanayohusu tuhuma za ufisadi, walimtaka Rostam kuzisoma kanuni za Bunge na wakasisitiza mbunge mwenzao huyo hakuonewa katika maamuzi yaliyofikiwa.
Hatua hiyo ya Rostam imekuja ikiwa ni siku moja tu baada ya wabunge watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupinga hoja yake inayoonekana kutaka kuingilia maamuzi ya Bunge.
Hawa ni wapuuzi, wanasukumwa na chuki, alisema Rostam alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli za wabunge hao; Aloyce Kimaro (Vunjo), Lucas Selelii (Nzega) na James Lembeli (Kahama).
Mbali ya hilo, mbunge huyo wa Igunga ambaye jina lake lilitajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata wa mkataba kati ya Shirika la Umeme (TANESCO) na Kampuni ya Richmond Development Company LCC alisema hoja zinazomhusisha yeye na umiliki wa mitambo ya Dowans ndizo zilizoliingiza taifa katika tatizo la giza leo hii.
Kwa hali ya kawaida miye si wa kujibizana na watu wa aina ya Kimaro... ni kudhani kwao Dowans ni yangu ndo kumepeleka nchi kuingia gizani. Aibu, alisema Rostam ambaye alilieleza Tanzania Daima kuwa alikuwa yuko nje ya nchi.
Rostam ambaye kwa mara ya kwanza aliwasilisha hoja ya kutaka kuundwa kwa tume huru au ya majaji ndani ya kikao cha maridhiano kati ya wabunge wa CCM na kamati inayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, alisema baadhi ya wabunge wanaomshambulia wanafanya hivyo si kwa matakwa yao bali kwa kutumwa na mtu ambaye hata hivyo hakumtaja.
Katika hatua nyingine, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alieleza kushangazwa na hatua ya wabunge hao kuonekana wakihofia kuundwa kwa tume huru wakati huo huo wakitamba kuwa ripoti ya kamati ya Bunge ya Richmond ilikuwa ni sahihi.
Alisema iwapo ni kweli wanakiamini wanachokipigania, basi ilikuwa ni vyema waruhusu tume ya majaji ifanye uchunguzi upya na wa haki, na ambao iwapo ungebaini wao kuhusika katika kadhia hii, wafikishwe mbele ya vyombo vya kisheria.
Kama wanaona kweli ripoti ni sahihi si ndo watapata kutuona tunachukuliwa hatua na azma yao dhidi yetu kukamilika? Haiingii akilini kuogopa, alisema.
Akimzungumzia Kimaro, mbunge huyo wa Igunga alieleza kushangazwa na hatua yake ya kuwa mstari wa mbele kushutumu wenzake ilhali ukweli ukionyesha kwamba alikuwa ameshindwa kuliongoza jimbo lake la Vunjo, ambalo lilikaribia kuchukuliwa na chama cha upinzani cha TLP.
Jimbo alilopewa na wananchi limemshinda na kidogo tupokonywe na TLP kwa sababu ya kushindwa kuliongoza, alisema Rostam.
Katika mahojiano ya simu ya jana, Rostam alirejea kauli yake aliyopata kuisema siku zilizopita kwamba, iwapo angekuwa ndiye mmiliki wa Dowans, asingeona aibu kulisema hilo kwani, huo ni mradi mkubwa ambao hauwezi kumilikiwa na Mtanzania yeyote binafsi.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti juzi, Selelii, Lembeli na Kimaro, walipinga hatua ya Rostam kutaka kuundwa kwa tume huru wakisema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni na wajibu wa Bunge.
Wabunge hao ambao siku zote wamekuwa na msimamo mkali kuhusu sakata la Richmond na masuala mengine yanayohusu tuhuma za ufisadi, walimtaka Rostam kuzisoma kanuni za Bunge na wakasisitiza mbunge mwenzao huyo hakuonewa katika maamuzi yaliyofikiwa.