Rostam sasa awaita akina Selelii "wapuuzi"

Malafyale

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
13,813
11,126
MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ameeleza kusikitishwa na kushtushwa na hatua ya kundi la wabunge kupinga hatua yake ya kutaka tume huru au majaji kufanya uchunguzi upya kuhusu sakata la Richmond.

Hatua hiyo ya Rostam imekuja ikiwa ni siku moja tu baada ya wabunge watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupinga hoja yake inayoonekana kutaka kuingilia maamuzi ya Bunge.

‘‘Hawa ni wapuuzi, wanasukumwa na chuki,” alisema Rostam alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli za wabunge hao; Aloyce Kimaro (Vunjo), Lucas Selelii (Nzega) na James Lembeli (Kahama).

Mbali ya hilo, mbunge huyo wa Igunga ambaye jina lake lilitajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata wa mkataba kati ya Shirika la Umeme (TANESCO) na Kampuni ya Richmond Development Company LCC alisema hoja zinazomhusisha yeye na umiliki wa mitambo ya Dowans ndizo zilizoliingiza taifa katika tatizo la giza leo hii.

“Kwa hali ya kawaida miye si wa kujibizana na watu wa aina ya Kimaro... ni kudhani kwao Dowans ni yangu ndo kumepeleka nchi kuingia gizani. Aibu,” alisema Rostam ambaye alilieleza Tanzania Daima kuwa alikuwa yuko nje ya nchi.

Rostam ambaye kwa mara ya kwanza aliwasilisha hoja ya kutaka kuundwa kwa tume huru au ya majaji ndani ya kikao cha maridhiano kati ya wabunge wa CCM na kamati inayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, alisema baadhi ya wabunge wanaomshambulia wanafanya hivyo si kwa matakwa yao bali kwa kutumwa na mtu ambaye hata hivyo hakumtaja.

Katika hatua nyingine, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alieleza kushangazwa na hatua ya wabunge hao kuonekana wakihofia kuundwa kwa tume huru wakati huo huo wakitamba kuwa ripoti ya kamati ya Bunge ya Richmond ilikuwa ni sahihi.

Alisema iwapo ni kweli wanakiamini wanachokipigania, basi ilikuwa ni vyema waruhusu tume ya majaji ifanye uchunguzi upya na wa haki, na ambao iwapo ungebaini wao kuhusika katika kadhia hii, wafikishwe mbele ya vyombo vya kisheria.

‘‘Kama wanaona kweli ripoti ni sahihi si ndo watapata kutuona tunachukuliwa hatua na azma yao dhidi yetu kukamilika? Haiingii akilini kuogopa,” alisema.

Akimzungumzia Kimaro, mbunge huyo wa Igunga alieleza kushangazwa na hatua yake ya kuwa mstari wa mbele kushutumu wenzake ilhali ukweli ukionyesha kwamba alikuwa ameshindwa kuliongoza jimbo lake la Vunjo, ambalo lilikaribia kuchukuliwa na chama cha upinzani cha TLP.

‘‘Jimbo alilopewa na wananchi limemshinda na kidogo tupokonywe na TLP kwa sababu ya kushindwa kuliongoza,” alisema Rostam.

Katika mahojiano ya simu ya jana, Rostam alirejea kauli yake aliyopata kuisema siku zilizopita kwamba, iwapo angekuwa ndiye mmiliki wa Dowans, asingeona aibu kulisema hilo kwani, huo ni mradi mkubwa ambao hauwezi kumilikiwa na Mtanzania yeyote binafsi.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti juzi, Selelii, Lembeli na Kimaro, walipinga hatua ya Rostam kutaka kuundwa kwa tume huru wakisema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni na wajibu wa Bunge.

Wabunge hao ambao siku zote wamekuwa na msimamo mkali kuhusu sakata la Richmond na masuala mengine yanayohusu tuhuma za ufisadi, walimtaka Rostam kuzisoma kanuni za Bunge na wakasisitiza mbunge mwenzao huyo hakuonewa katika maamuzi yaliyofikiwa.
 
Kama unahisi kutotendewa haki mahali popote, unatinga mbele ya sheria, hakuna aliye juu ya sheria, kama rais mwenyewe ndiye mwenye kinga ya kushitakiwa na bado anashitakiwa litakuwa Bunge.

Jamani RA kama anawashauri zaidi ya wale wapambe wake, mshaurini mwenzenu ajifunze kukaa kimya ...oh haya heri mimi sijasema kitakachomkuta... msije kusema hakushauriwa and by then it might be too late...
 
"Kwa hali ya kawaida miye si wa kujibizana na watu wa aina ya Kimaro... ni kudhani kwao Dowans ni yangu ndo kumepeleka nchi kuingia gizani. Aibu,"

hapa kuna namna .... kwahiyo hili giza ni kutukomoa kwa kumshtukia kwamba ni yake ama?
 
'‘Jimbo alilopewa na wananchi limemshinda na kidogo tupokonywe na TLP kwa sababu ya kushindwa kuliongoza," alisema Rostam.

Katika mahojiano ya simu ya jana, Rostam alirejea kauli yake aliyopata kuisema siku zilizopita kwamba, iwapo angekuwa ndiye mmiliki wa Dowans, asingeona aibu kulisema hilo kwani, huo ni mradi mkubwa ambao hauwezi kumilikiwa na Mtanzania yeyote binafsi.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti juzi, Selelii, Lembeli na Kimaro, walipinga hatua ya Rostam kutaka kuundwa kwa tume huru wakisema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni na wajibu wa Bunge.
Wabunge hao ambao siku zote wamekuwa na msimamo mkali kuhusu sakata la Richmond na masuala mengine yanayohusu tuhuma za ufisadi, walimtaka Rostam kuzisoma kanuni za Bunge na wakasisitiza mbunge mwenzao huyo hakuonewa katika maamuzi yaliyofikiwa.

Some unintended revelations..!
 
Anachotukumbusha RA ni KINGA NZITO kupita kiasi ililonalo BUNGE letu ambayo maamuzi yake hayahojiwi na MAMLAKA nyingine yoyote. Tulijadili hili kwa kina badala ya kupoteza muda mwingi kumjadili yeye ambaye hata hivyo amekwisha jadiliwa sana humu.
 
Anachotukumbusha RA ni KINGA NZITO kupita kiasi ililonalo BUNGE letu ambayo maamuzi yake hayahojiwi na MAMLAKA nyingine yoyote. Tulijadili hili kwa kina badala ya kupoteza muda mwingi kumjadili yeye ambaye hata hivyo amekwisha jadiliwa sana humu.

Wewe una mashaka au kutopendezwa na hilo?

For my case, kwa vile bunge halikurupuki kupitisha maamuzi, na linakaa ki`wapiga-kura zaidi kuliko kiserikali na chama(japo wanapenyeza vidole huko) naona ni sawa kwake kuwa na supremacy hiyo.
 
Wewe una mashaka au kutopendezwa na hilo?

For my case, kwa vile bunge halikurupuki kupitisha maamuzi, na linakaa ki`wapiga-kura zaidi kuliko kiserikali na chama(japo wanapenyeza vidole huko) naona ni sawa kwake kuwa na supremacy hiyo.
Checks and balances lazima ziwepo hata kama ni maamuzi ya kitaasisi kama BUNGE. Bunge letu limewahi kupitisha maamuzi ya ajabu kabisa yakiwemo takrima, hoja ya mgombea binafsi, juzi Zitto alijaribu kutoa hoja Wabunge waondoke kwenye bodi za taasisi za umma wakakataa,....
Bunge kama hili la kwetu halipaswi kuwa na kinga hii. Bado ni la CHAMA kimoja.
 
kimzungumzia Kimaro, mbunge huyo wa Igunga alieleza kushangazwa na hatua yake ya kuwa mstari wa mbele kushutumu wenzake ilhali ukweli ukionyesha kwamba alikuwa ameshindwa kuliongoza jimbo lake la Vunjo, ambalo lilikaribia kuchukuliwa na chama cha upinzani cha TLP.

'‘Jimbo alilopewa na wananchi limemshinda na kidogo tupokonywe na TLP kwa sababu ya kushindwa kuliongoza," alisema Rostam.

Jimbo la Vunjo lazima litachukuliwa na TLP si kwasababu Mheshimiwa Kimaro ameshindwa kufanyakazi bali wakaazi wengi wa Vunjo bado wanamkubali Bwana L A Mrema.
 
Hao akina Selelii si wampeleke mahakamani, kama kweli ni viongozi wazuri?
 
Rostam kama anataka majaji kuchunguza tuhuma zake ni jambo linalowezekana ila sii kwa namna anavyotaka yeye. Anachotakiwa kufanya ni kuiomba ofisi ya DPP imfungulie kesi ya kuikana kampuni yake ya kitapeli na huko mahakami atakutana na jopo la majaji watatu anaowataka na watamhukumu kwa uhuru na kwa haki kabisa!!
 
Bottom line Tanzania hakuna kiongozi msafi. Ni sawa na kauli aliyowahi kutoa Bob Mugabe kwamba kiongozi yoyote wa Afrika anayehisi kwamba yeye amechukua madaraka kimabavu na awe wa kwanza kumnyooshea kidole. Twende mbele turudi nyuma ili tuweze kuwa wasafi inabidi watanzania wenyewe waseme sasa INATOSHA.
 
Bottom line Tanzania hakuna kiongozi msafi. Ni sawa na kauli aliyowahi kutoa Bob Mugabe kwamba kiongozi yoyote wa Afrika anayehisi kwamba yeye amechukua madaraka kimabavu na awe wa kwanza kumnyooshea kidole. Twende mbele turudi nyuma ili tuweze kuwa wasafi inabidi watanzania wenyewe waseme sasa INATOSHA.

Hii ya Mugabe nasikia wapambe wote mkutanoni walishikwa na ganzi! na haikuwahi kutolewa magazetini sijui wewe nawe ulikuwamo?
 
Mie ningekuwa wewe rostamu nisingeendelea kukaa katika nchi ambayo wabunge wake ni waapuuzi! wakati nina kwetu kwa wenye akili.
Kama unadhani chuki tu ndio zinasababisha haya yote si urudi tu kwenu ....unanga'nga'nia nini hapa! ulikotoka umeua? mcheza kwao hutunzwa hapa hautunziki tena!!!! rudi kwenu tuachie nchi yetu bwana

Unajua nakumbuka wakati nakimbia mchaka mchaka kuna wimbo tuliimba " tanzania tanzani nchi yenye mali nyingi watu wengi wa ulaya wanaililia sana" kashamba ka bibi
ooooh mie ponjoro mwenye asili ya tanzania! mmmh mnatufanya sisi wajinga ndio waliwao....kizazi kipya kinakuja na hata sasa kipo haturuhusu kukaa jamvi moja na watu wa aina hiiii! nimesema mwisho wenu haupo mbali,....tumechoka.
 
Wenzake wakati wakipinga uchunguzi mpya walinukuu kanuni za bunge kuwa, kinachopitishwa bunge hakiwezi kuundiwa tume na mhimili mwingine wa dola.
Yeye mbona hasemi kanuni za bunge zinasemaje mtu akihisi hatatendewa haki?
Chaajabu maazimio 18 kati ya 20 yametekelezwa sasa hiyo tume itaundwa kuchunguza hayo yaliyosalia au itabatlisha ripoti yote ya awali? Kwanini linalo mhusu R.A ndo liwe la uongo mengine sawa? HANA JIPYA
 
Wenzake wakati wakipinga uchunguzi mpya walinukuu kanuni za bunge kuwa:- kinachopitishwa na bunge hakiwezi kuundiwa tume na mhimili mwingine wa dola.
Yeye mbona hasemi kanuni za bunge zinasemaje mtu akihisi hajatendewa haki?

Chaajabu maazimio 18 kati ya 23 yametekelezwa sasa hiyo tume itaundwa kuchunguza hayo yaliyosalia au itabatlisha ripoti yote ya awali? Kwanini linalo mhusu R.A ndo liwe la uongo mengine sawa? HANA JIPYA
 
Kanuni haziruhusu ajenda iliyokwisha fungwa na bunge kuhojiwa na mhimili mwingine wa dola. Kama anataka tume mbona hatwambii kanuni zinasemaje?

Maazimio 18 kati ya 23 yamekwisha tekelezwa sasa hiyo tume ya majaji itachunguza hayo matano yaliyobaki? Au hata hayo mengine ni ya uongo?
R.A huna jipya umechemsha
 
Watu wengine wana raha sana duniani mfano rostam, yaani anatuchezea tu vichwa vyetu.kutuibia katuibia sana huyu huyu anasababisha tunashindwa kujadili mambo ya muhimu tunamjadili yeye tumemchoka nae huyu muasia arudi tu uarabuni tujue moja.............anatupotezea tu muda wetu...
 
RA ishakula kwake akae atulie, Dili lao la kuleta Richmond na kutaka kuuza mitambo mibovu ya dowans wenzao wamewazidi akili.
 
Back
Top Bottom