newmzalendo
JF-Expert Member
- Mar 23, 2009
- 1,386
- 583
![]()
Mwaka Jana mwezi Juni, Mchg. Mtikila alitoa tuhuma ambazo hazikupewa uzito unaostahili. Hata hivyo habari za hivi karibuni na uchunguzi huru uliofanyika unatupa sababu ya kuamini kuwa kuna kitu kuhusu maisha na uraia wa Rostam Aziz (Igunga - CCM) kinafichwa kwa makusudi au kwa kutegemea kuwa hakitaulizwa. Maelezo ya Mtikila aliyoyatoa mwaka jana ni haya yafuatayo aliyoyapa kichwa cha "Hatima ya Mwajemi Sakarir". Soma kijarida chako pia na ufanye uamuzi wako mwenyewe ni nini kinafichwa na kwa nini?
HATIMA YA MWAJEMI SAKARIR (ROSTAM) AZIZ
Kiini cha ufisadi wa kutisha na uporaji wa Nchi yetu, unaofanywa kama vile Watanganyika wote ni mataahira, ni kutoweka kwa uraia wa kweli wa kuipenda nchi yetu na kuwa na uchungu nayo wa kiwango cha uhanga kwa ajili yake. Kwa sababu ya 'utaahira' wetu nchi yetu imekamatwa na mbunifu mkuu na nahodha wa mikakati iliyo mingi ya wizi wote uliuofanyika katika Benki Kuu na Hazina ya Nchi yetu, ambaye ni Mwajemi yaani raia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mwajemi huyu jina lake halisi alilopewa pamoja utambulisho wake alipozaliwa kule kwao Iran ni SAKARIR mwana wa AZIZ. Sakarir alipokuja Tanzania kuipora Nchi ya 'mataahira' kama anavyopenda kutudharau yeye mara nyingi, alijipa jina la 'Rostam'. Wazazi wa Sakarir hawajawahi kuishi hapa, wapo kwao Iran, wakiwa na biashara kubwa ya nyama na kufuga ng?ombe. Sakarir alipozaliwa alipata elimu yake ya msingi kwao Iran, na baadaye akapata elimu ya juu Uingereza ambako pia anao ndugu.
Nilipoanza kuzungumzia uraia wa 'Rostam' Aziz alibabaisha kuwa alizaliwa Ndala Mission, lakini ni mwongo, ingawa alisahau kwamba Premji wa Kigoma alizaliwa hapa lakini hakuwa raia kwa sababu wazazi wake hawakuwa wameukana uraia wa kwao, wala yeye Premji hakuwa ameomba uraia kwa mujibu wa Sheria, hata kama aliweza kujipatia Passport ya nchi hii kwa njia za ufisadi kama alivyofanya yeye. 'Rostam' amepata kudanganya kwamba alisoma shule ya msingi Mwisi, alipoona atagundulika upesi akasema alisoma Mwamala, Nzega, lakini siyo kweli.
Rostam Aziz anazo Passport mbili za kusafiria, yaani ya Nchi yetu ambayo aliipata kwa udanganyifu, anayoitumia kusafiria hadi Nairobi, na ya kwao Uajemi yaani Iran ambayo husafiria kutoka Nairobi kwenda kwao, Dubai na kwingine alikolimbikiza mapesa aliyaipora Nchi yetu.
Kwa ufupi Sakarir alipofika nchini mwetu baada ya masomo yake Uingereza, aliunganishwa na viongozi watatu wa CCM waliokuwa marafiki sana ambao ni pamoja na Rais Kikwete.
Rostam alipata nguvu ya kisiasa kwa kutumia mapesa mengi ya mfuko maalum wa nchi yao wa 'Iranians in Diaspora', aliyoyapata kama raia mwaminifu wa Iran, aliye na shughuli zenye maslahi kwa nchi yao katika nchi ya nje. Nguvu hii ndiyo iliyomtia Benjamin Mkapa mkononi mwake na kuwa msingi wa uhuni na jeuri yote aliyonayo leo.
Mafisadi walionufaika na mtaji huo wa Sakarir Aziz ndio waliofanya uhaini wa kumpa Ubunge wa Igunga alipofariki hayati Charles Kabeho. Wazee wa Kiajemi waliolowea hapa, Hussein Heidari na Hassan nduguye ndio waliompokea kijana Sakarir Aziz kule Igunga, kwa sababu wanao uhusiano na mkewe Aziz yaani mama yake Sakarir au Rostam.
Hawa wazee ndio waliomnadi huyu Mwajemi kwa wazee wa Igunga katika kuiba Ubunge wa Nchi ya watu ambao anawachukulia kuwa 'mataahira'. Sakarir Aziz anao nduguze wa kiume wawili yaani Jahangir Aziz ambaye alipigana kizalendo kabisa ile vita ya nchi yao dhidi ya Iraq, na wa pili ni Akram Aziz.
Kamati yetu imejitolea kuwasaidia wananchi wa Igunga wanaotaka kufungua kesi dhidi ya Sakarir Aziz na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwa kuwanyima uwakilishi Bungeni tangu Mbunge wao hayati Charles Kabeho alipofariki. Kwani Mwajemi wa Jamhuri ya Kiislamu, 'Rostam' Aziz hawajali kabisa wananchi wa Jimbo lile, hata katika maafa kama ya kukosa kabisa usafiri baada ya madaraja ya mto Mbutu kuzolewa na mafuriko, au machafuko yaliyotokana na masuala ya ushirikina.
'Rostam' Aziz anashirikiana katika kupora Nchi yetu na gabachol* mwingine aitwaye Yusuf Manji, ambaye pia si raia wa nchi hii na akibisha ushahidi utatolewa.
Bilashaka Wabunge safari hii watataka kujua ni nani hasa waliotoa Passports za Tanzania kwa 'Rostam' Aziz, Jahangir Aziz na Akram Aziz na kwa misingi gani.
Wezi hawa wanaipora nchi hii bila huruma, na ndio wanaowaambia watawala wa CCM cha kufanya ili wakombe mapesa yetu B.O.T na Hazina, na kutumia matrilioni yetu kuwatia viongozi wetu ndani ya mifuko ya makoti yao, ambamo wanalishwa masazo yao na kuchomoza vichwa kuchungulia nje kama vindege kuwasanifu wananchi, na kurudi mifukoni mwao wakidhani wanakula kumbe wanaliwa wao na Nchi yao! Hatutaki Rais wetu wala Wabunge wetu wawe vindege ndani ya mifuko ya makoti ya 'Rostam' Aziz na Yusuf Manji!
'Rostam' na yusuf Manji wapo Dodoma na shehena ya mapesa ya EPA, kwa kazi ya kuwanunua wabunge wanaowadharau kwamba eti ni mataahira, wawe karatasi ya msalani (toilet paper) ya kuwasafisha uchafu wao halafu na yenyewe itokomee pamoja na uchafu, kwani haiwi safi tena baada ya kutumiwa!
Tunaitaka Serikali iwakamate hawa wahalifu hatari wa Taifa letu huko Dodoma na kuwapokonya makaratasi yao yote ya kusafiria na kuwaleta kizimbani maramoja kwa uharamia wote walioifanyia Nchi yetu.
Saa ya ukombozi ni sasa!
Mchungaji C. Mtikila
MWENYEKITI WA KAMATI
26/6/2008
Swali:Kwanini Rostam hakufungua mashtaka dhidi ya Mtikila ya kumzushia kuwa si raia na kujaribu kumchafua jina lake ukizingatia kuwa tuhuma ya kuitwa "fisadi papa" na ya kuambiwa kuwa si "raia" hiyo ya "papa" ni mtoto tu? Kwanini serikali haikumkemea Mtikila na kumpiga mkwara wa kumchukulia hatua n.k )?
hivi hili swala liliishia wapi vile 🙂:coffee: