Rostam Aziz Kung'atuka!

Kung'atuka ili kuinusuru CCM ni jambo la busara ila kung'atuka kabla ya kufanya marejesho ya pesa zetu haiwezekani. Kwanza wana JF mnaona jinsi mpango wa kususia simu za Vodacom unavyoanza kufanya kazi. Kazeni buti hata na wengine tususie biashara zao mpaka kieleweke. Huyu jama ni mwepesi kusoma alama za nyakati maana hapo ameona kuwa huko mbele ataambulia patupu ndio maana anaanza kutapatapa.
 
Is this what asked by JF members previously? I also heard some wabunge asking for this. Waondoke bungeni na ktk chama chetu,is what they have been saying. Mashaka ya nini endapo huyu mkulu anataka kung'atuka ktk siasa za bongo? Let the news be it and not an agenda for serious people within JF
 
"When u r in light, everything will follow u. But when u enter dark, even
your own shadow" Adolph Hitler - Come on Adolfo!
 
kishashiba huyo ... loh! hajui kula na kipofu ... anafakamia kwa mikono yote miwili ... he is only good for the dead ... aanze mbele
 
Hakuwatendea haki wananchi wa jimbo lake ufisadi wote huo na kuwaacha igunga wako taabani inasikitisha sana. Sheria ichukue mkondo wake.
 
Hata akijiuzulu/kung'atuka yeye kutakuwa na tofauti gani. Nchi imeshashikwa na mafisadi, kila tunapogeukia wapo
 
Pesa za mtelezo za epa na richmond zimeisha hana tena pa kuchota kutokana na kimbelembele cha jf, sasa abaki kwenye ubunge kufanya nini?

mmesahau ya marehemu gulamali? yeye baada ya kuwa mbunge akaona ubunge haunufaishi biashara zake akaamua naye kulala mbele. mnafikiri rostam aziz ana uchungu gani na wanyamwezi wa igunga?
 
CHADEMA, CCM wamkatalia Rostam kung'atuka

Na Mwandishi Wetu, Tabora

VYAMA vya CHADEMA na CCM katika wilaya ya Igunga mkoani hapa, vimesema havitamruhusu Mbunge wa Jimbo la Igunga, Bw. Rostam Aziz, kuacha kugombea ubunge mwaka 2010.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti mjini Igunga juzi, kutokana na kauli ya Bw. Rostam ya kutogombea tena ubunge mwaka 2010, viongozi wa vyama hivyo walisema bado wanahitaji huduma yake.

Walisema Mbunge huyo amewafanyia mengi jimboni na kwamba mwaka 2010 ni mapema kuacha kugombea, kwa kuwa kuna mambo ambayo ameahidi kuyatekeleza, hivyo kuhitaji muda zaidi.

Katibu wa CHADEMA wa Wilaya, Bw. Moka Changarawe, alisema mbunge huyo amewasaidia kwa mambo mengi, yakiwamo ya kuwajengea mabwawa na huduma mbalimbali za maendeleo tena bila kujali itikadi za vyama.

"Mbunge huyu kuna ahadi ameanza kuzitekeleza, hivyo haitakuwa vema aachie ngazi huku akiwa katikati ya kuzikamilisha, sisi tutampa muda mwingine amalizie, lakini si sasa," alisema na kuongeza kuwa hata wanachama wa CHADEMA Igunga wana imani naye.

Alisema katika mkutano wa wazee wa Igunga Jumanne iliyopita, siku anasimikwa kuwa Chifu wa Wanyamwezi kijijini Mwisi, Igunga alikozaliwa, wana CHADEMA walisimama na kumwomba aendelee kugombea.

Naye Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Igunga, Bw. Felix Mkunde, alisema kauli ya Bw. Rostam, waliipokea kwa hisia tofauti na kwamba wataijadili ili wahakikishe anabadili msimamo wake kwa kuwa bado wanamhitaji.

"Hayo ni mawazo yake binafsi, hatuwezi kumlazimisha kubadili msimamo, lakini bila shaka ni mwelewa na ataelewa ni nini tunachokizungumza sisi na kwa nini tunahitaji bado mchango wake jimboni," alisema Bw. Mkunde.

Aliungwa mkono na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Bibi Evelyne Jordan, ambaye alisema Halmashauri ya Wilaya ya CCM kwa kauli moja ilishasema kuwa haitambui wazo hilo la Mbunge Rostam na bado inamhitaji.

Hata hivyo, Bw. Rostam alipoulizwa, alisema ni kweli huo kwa sasa ndio msimamo wake na si lazima awahudumie wananchi wa Igunga akiwa bungeni, kwani anaweza kutoa mchango wake akiwa nje ya Bunge.

"Kama mwana Igunga, nitaendelea kuwatumikia wananchi hata nikiwa nje ya Bunge," alisema.

Kuhusiana na hilo, Bibi Jordan alisema akiwa bungeni na nje ya Bunge ni tofauti, na ndiyo sababu wafanyabiashara na vijana wa wilaya ya Igunga wameshasema hawatakubali kumpoteza na wanamtaka aendelee kuwawakilisha bungeni.

Bw. Rostam aliingia bungeni mwaka 1994 baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa Igunga, marehemu Charles Kabeho na katika uchaguzi wa 1995 na 2000 alipita bila kupingwa.

Source: Majira


Jamani hata kama ni ku-spin kwa ajili ya kutetea maslahi ya mafisadi, basi hii imevuka mipaka no wonder hata mwandishi wa habari hiyo hajataja jina lake maana ni aibu kubwa sana.

Kweli kabisa kiongozi wa CHADEMA wa ngazi ya wilaya anaweza kutoa kauli kama hiyo? Bado anasubiri nini kwenda CCM ili akaungane na RA kwenye kampeni za kujijenga kisiasa baada ya kuona umaarufu wake unadondoka kwa kasi kubwa huku akiwa amezingirwa na tuhuma kila kona. Kama huyo kiongozi wa CHADEMA alitoa kauli basi ninashawishika kusema kwamba hapo Igunga CHADEMA haina kiongozi wala wanachama. Kama kuna ofisi za CHADEMA basi inabidi zifungwe na viongozi wake wahamie ofisi ya CCM wilaya ya Igunga.

Wana-CHADEMA hebu fuatilieni hii habari kama ni ya kweli!

Hivi ni kweli kwamba RA kazaliwa Mwisi? Wazazi wake wako wapi? Kuna mada nyingi sana huwa zinam-refer kama m-Iran, na wazazi wake wako Iran, je, waliondoka kwenda Iran mara baada ya kumzaa ama imekaaje maana mimi sielewi elewi haya mambo
 
ni kweli amekosea kwa kuwa ukweli si viongozi hao tu ndio wanamtaka RA bali nijuavyo mimi ni wananchi wenyewe wa jimbo la Igunga.jamaa anakubalika kule .
 
huyu mkuu wa chadema kachanganyikiwa au? vyama vya upinzani wakati mwengine vinakosa misimamo kiasi cha kusikitisha.
kiongozi huyo wa chadema inamaana ikiwa rostam atasimama kuomba ubunge jimboni hapo hawezi kumpigia kampeni mgombea wa chadema hata siku moja, kwa vile anataka rostam atimize ahadi zake!
total shame
 
Hii haishangazi hata kidogo maana tumeshindwa kueleza vizuri kazi za mbunge ni nini. Kwa wananchi wengi, kazi ya mbunge ni kutoa misaada kama hiyo ya kujenga mabwawa, kugawa mahindi wakati wa njaa, n.k. Sasa kwa wale wanaoijua Igunga, kazi hizi Rostam kazifanya vizuri sana pengine kuliko mbunge yeyote yule. Swali linakuja, je hizi ndio kazi kweli za mbunge? Kama wananchi hawaelewi kazi za mbunge, hilo sio kosa lao, ni la kwetu sisi tunaoelewa lakini hatuwajibiki kuwaelimisha.

Kwa hiyo pamoja na kwamba viongozi wangu wa wilaya wa CHADEMA wameungana na wa CCM kumtaka Rostam abaki siwashangai kabisa. Najishangaa mimi kwa kushindwa kuwaelimisha hawa viongozi wangu waelewe kazi za mbunge ili waweze kumtathimini mbunge wao vizuri.

Tusikimbilie kufikiri hili nalo Rostam kawahonga wananchi ili waongee vile. Kama ni hongo itakuwa ni hiyo ya kuwapelekea misaada ambayo ndiyo silaha kubwa sana ya wabunge wengi wengine.
 
Na hawa wazee wa vijijini nao hawajamfahamu mwenzao yaani jamaa mirija imeanza kukatwa na zile fedha anazosanya hazitatosha kuwalaghai na wao ,zaidi hawafahamu walilomchagulia sio litokane na nguvu binafsi za huyo fisadi,kama miradi aliyoanzisha ni kwa madai yae dhidi ya serikali kwa wanavijiji hao kwa wanaIgunga hao basi wanayo haki ya kumshauri aendelee lakini kama misaada ni kutoka mfukoni mwa uyo Muirani basi kama alikuwa na moyo wa kweli kuwasaidia basi ataendeleza yale aliyoyabakisha hata akiwa nje ya Ubunge si zaidi ya hapo tutabaki palepale alikuwa akiwapa vijihela kidogo na kujemga jenga kwa kusuasua huku akitumia kusuasua huko kuvuta muda wa kula wakati yeye akichota mabilioni ,kias wamwambie abaki maaa akiwanunua kwa milioni moja tu na wao wakiona kama vile ndie mfalme wao wakati kama majisenti yasingechotwa kwenye Serikali kuu basi Serikali ingeliweza kuwajengea hicho alichowajengea kila mtaa.
Waamsheni hao washamba ! ila kuna kitu kimoja siku hizi katika mambo ya kisiasa kuna jambo limezuka la kusingizia Wazee utasikia wazee wamenitaka niendelee tena ,sijui wazee wameona bado nina nguvu ,sijui wazee hawatokubali na hasa wenye mtindo huu ni hiki Chama Cha Mafisadi.
 
chedema itatuambia huyo mkuu wa chadema hapo kaongea kama mwananchi wa ingunga na sio kama kiongozi wa chama cha chadema wilayani hapo.
 
Hii haishangazi hata kidogo maana tumeshindwa kueleza vizuri kazi za mbunge ni nini. Kwa wananchi wengi, kazi ya mbunge ni kutoa misaada kama hiyo ya kujenga mabwawa, kugawa mahindi wakati wa njaa, n.k. Sasa kwa wale wanaoijua Igunga, kazi hizi Rostam kazifanya vizuri sana pengine kuliko mbunge yeyote yule. Swali linakuja, je hizi ndio kazi kweli za mbunge? Kama wananchi hawaelewi kazi za mbunge, hilo sio kosa lao, ni la kwetu sisi tunaoelewa lakini hatuwajibiki kuwaelimisha.

Kwa hiyo pamoja na kwamba viongozi wangu wa wilaya wa CHADEMA wameungana na wa CCM kumtaka Rostam abaki siwashangai kabisa. Najishangaa mimi kwa kushindwa kuwaelimisha hawa viongozi wangu waelewe kazi za mbunge ili waweze kumtathimini mbunge wao vizuri.

Tusikimbilie kufikiri hili nalo Rostam kawahonga wananchi ili waongee vile. Kama ni hongo itakuwa ni hiyo ya kuwapelekea misaada ambayo ndiyo silaha kubwa sana ya wabunge wengi wengine.
 
Kuna Umuhimu wa kuwaelimisha Wanyamwezi wa Igunga wajue ni kiasi gani cha fedha ambazo Rostam ameshawaibia kama wananchi wa Tanzania halafu tuone kama kweli watamhitaji tena: - Njaa na Ujinga vikikumbatina watu watakaangwa na mafuta yao bila kujijua
 
Kwa UMASIKINI wa FIKRA na KIPATO wa Watanzania walio wengi (hasa mikoani) akina RA wanakaribia "kuabudiwa" kwa "misaada" wanayotoa. Hatuna jinsi kwa sasa baada ya kuwafukarisha watu wetu kwa MAKUSUDI.
 
Hizo story zenu za ufisadi na nini sijui wananchi wa kawaida hata hawaelewi ni kitu gani! Wao mradi kawajengea bwawa moja la kunyweshea ng'ombe wao basi ni mbunge mzuri. Kama kawapa vijana wafanya biashara ndogo ndogo mtajiwa wa shs kama laki moja kila mmoja kwa vijana 100 (Total 10m) hizo wao wanaona ni pesa nyingi sana. Hawajui ameiba rasimali kiasi gani!

Hivi ni kweli Rostam kazaliwa Mwisi - Igunga?? Mbona anasemekana ni raia wa Irak aliyekuja nchini miaka ya karibuni?
 
Siwalaumu wananchi wa Igunga,Rostam kwetu ni fisadi lakini utamwambiaje Ngosha wa kule kijijini kuhusu rostam ambaye amempelekea maji na shule ...hata mimi ningemwomba aendelee,who cares about EPA wakati hata zisingeibiwa na Aziz zingeibiwa na mafisadi wengine wa Chadema au CCM,watu hawataki makubwa ni madogo madogo tuu kama maji tena ya visima tuu wala sio ndani ya nyumba....wapinzani wanze kuwa practical sasa ili washinde maana maneno matupu hayashindi kwa mazingira ya njaa kama TZ kwa sasa
 
Hizo story zenu za ufisadi na nini sijui wananchi wa kawaida hata hawaelewi ni kitu gani! Wao mradi kawajengea bwawa moja la kunyweshea ng'ombe wao basi ni mbunge mzuri. Kama kawapa vijana wafanya biashara ndogo ndogo mtajiwa wa shs kama laki moja kila mmoja kwa vijana 100 (Total 10m) hizo wao wanaona ni pesa nyingi sana. Hawajui ameiba rasimali kiasi gani!

Hivi ni kweli Rostam kazaliwa Mwisi - Igunga?? Mbona anasemekana ni raia wa Irak aliyekuja nchini miaka ya karibuni?

Huy ni Muirani na mwanzo alikuwa jamaa wa kawaida tu mchangamfu na mwingi wa maneno ,ila aliwatapeli wenzake ,na kisa na mikasa ni hayo mambo ya amdini,alikutana na waIrani wenzake na kuwa mwenyeji wao na jamaa walikuwa na noti ile mbaya na kumjulisha nia na madhumuni ya kuwepo hapa Tanganyika ni kutaka kuazzisha mradi wa uchimbaji dhahabu kwa bahati wakapata eneo na jamaa wakamwaga fedha nyingi mpaka inakaribia mitambo kuanza kazi ,na wakati ule vuguvugu la terosisti na alqaeda ,Rostam machale yakamcheza na kupanga na kupangua akawachomea utambi jamaa wale wa Kiirani wenzie kuwa wanahusika na mambo ya alkaeda ,na mipando kupangwa wakatiwa mkiki na kutakiwa waondoke haraka nchini bila ya kudai chochote la si hivyo watakamatwa na kupelekwa Guntanamo bay ,sifa za huko Guantanamo zilikuwa nazo zimepamba moto ,Wairani wakaacha anwani na adresi za kwao ,hadi hii leo jamaa kabinya na ndio imeshatoka na yeye amebaki na mtaji. Ni zulma tu na mali ya zulma haisaidii zaidi ya hasara ila hasara yake kama ugonjwa wa aids haikufanyii haraka haraka utaona unaanza kubadilika kidogo kidogo .
 
Mimi nadhani huyu Jamaa wa Chadema kaongelea kwa capacity ya uelewa wake tu kama alivyo sema Kitila .Sasa akisimama wa Chadema yeye atampigia nani hilo ni swala jingine lakini bado yeye ni Ngosha kama wengine kule kwao na kwa macho yao Rostam ndiye haswa.Kwa CCM Wilaya is obvious kwamba mapato na hata kukatiwa ili akauguze mtoto hayatakuwepo_One has to sweat to rectify the situation including kumwendea RA aje na second thought .

Umasikini mbaya wandugu .
 
Back
Top Bottom