Rostam Aishtaki Mwanahalisi

Hii miCCM sijui haijui kama hawa mahindi na maarabu wanaurafiki wa mashaka?

Ubaguzi.... Ukabila, Udini, Umajimbo, Ukanda!! Tuwakome Mafisadi kwa ufisadi wao please! Hawa Chenge, Richmomd, Karamagi, Balali Makapa....wote ni wamatumbi kabisa, ni CCM na Wanatuua polepole kwa ufisadi wao!
 
Sasa huyu RA anashangaza kweli, Kaspian ni kampuni yake na hao Richmond wanatumia email adress ya Kaspian, hapo kweli hakuna mahusiano????
 
Sasa huyu RA anashangaza kweli, Kaspian ni kampuni yake na hao Richmond wanatumia email adress ya Kaspian, hapo kweli hakuna mahusiano????

Kama nilivyowaeleza tokea mwanzo na nauhakika hiyo ndiyo dira ya Mwanahalisi(Hakikisha unapata nakala ya Jtano) Mahakamani ndipo tutakapopata ukweli wa Mambo
 
Huku ndiko kunakopangwa na CCM ili kujaribu kuzima hoja na kuwafanya watu waogope kusema,rostam hana ubavu wa kushitaki kwani hilo ni wazo ambalo mafisadi walitakiwa wawahi mapema kuwashitaki wanaowaumbua na huku kuchelewa kupelekwa mahakamani wao mwanzo ni kuwapa nafasi ya kufanya hivyo na ndio wameanza subirini wengine ambao watafuata hifadhi ya mahakama.
 
Jamani Tusimbeze na kumdharau RA
Tusimbeze Rostam, hatikisi kiberiti
WIKI iliyopita nilikusanya magazeti yote ya wiki. Niliyasoma kijuu juu, ila nilipata fursa ya kuyapitia kwa ufasaha Jumapili nilipotoka kanisani.

Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza wanahabari kwa kazi nzuri wanayofanya kuelimisha, kuburudisha na kuhabarisha jamii. Kimsingi nimekuta magazeti mengi kwa asilimia kubwa yakilifahamisha Taifa letu nini kinaendelea katika jamii.

Hata hivyo, wakati napitia gazeti la Raia Mwema, toleo namba 025, nilikutana na makala ndefu iliyochapishwa ukurasa wa nne na kuendelea ukurasa wa 22. Mwandishi wa makala hii ni Lula wa Ndali Mwananzela.

Makala hii ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho: “Sipendi Rostam Aziz atikise kiberiti bungeni.” Alichambua na kuhoji Rostam alitaka kuzungumza nini bungeni hadi nchi nzima ikatetemeka.

Katika moja ya aya zake anasema: “Kitu gani hasa alitaka kusema kiasi kwamba kwa nyakati tofauti imeonekana kana kwamba ana ‘jambo’ kubwa ambalo lingeweza kuleta vurugu bungeni?”

Anafafanua kuwa Rostam alitaka kupeleka maelezo ya ufafanuzi kuhusiana na mkataba wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond.

Makala hiyo inasema Rostam angetumia muda huo kujisafisha, na si ajabu angefika na vielelezo vyake zikiwamo fomu za BRELA zenye kuonyesha wamiliki halisi wa Richmond, na hivyo kujisafisha yeye na washirika wake.

Ameandika mengi, anayojua aliyatoa wapi, lakini pengine ninukuu aya ifuatayo iliyonifanya kuandika makala hii: “Hivi ni lini mara ya mwisho kwa Rostam kutoa mchango bungeni na alichangia nini? Ni kitu gani ambacho Rostam Aziz alisema bungeni katika mijadala ya bajeti au mingineyo ambayo inaweza kukumbukwa? Kama huko kote hajasema jambo lolote la kukukumbukwa, iweje leo tugwaye kama Taifa eti Rostam anataka kusema? Huku ni kujifanya duni kusiko na sababu.”

Nimeamua kuijibu makala hii baada ya kuona tabia inayoibuka katika jamii yetu inastahili kukemewa vinginevyo itatupeleka pabaya. Namchukulia Rostam Aziz kama raia yeyote wa nchi hii mwenye haki ya msingi ya kujitetea anapokuwa ametuhumiwa.

Ni wiki iliyopita tu, tumeshuhudia Spika wa Bunge Samuel Sitta akijikanyaga juu ya uamuzi muhimu unaohusu kanuni za Bunge. Spika ni mhimili wa kanuni hizi, akijua kuwa jambo lililoamuliwa na Bunge haliwezi kujadiliwa katika muda wa miezi 12, katika mkutano wa 10, akasema Rostam angelazimika kuthibitisha tuhuma dhidi ya kamati ya Dk. Harrison Mwakyembe.

Rostam alikuwa akidai kutotendewa haki na kwamba kamati ilifanya kazi nje ya muda wake, hivyo aliamini kuwa ilifanya kazi kisiasa. Kama kweli wangekuwa na nia ya kumhoji wangeweza kumhoji, ila kumhoji kwao kungeweza kuvuruga mchezo wa kisiasa ulionuiwa.

Bunge la Mkutano wa 11 Sitta alikubali kumpa Rostam nafasi ya kutoa maelezo yake, lakini akatoa sharti kuwa shurti yaandikwe. Rostam alipoyaandika, Spika akabadili milingoti ya goli. Akasema kanuni za Bunge haziruhusu jambo lolote lililoamuliwa na Bunge kujadiliwa upya katika kipindi cha miezi 12!

Mwandishi wa makala ile anakiri nguvu na umuhimu wa Rostam Aziz katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akisema kuwa nguvu kubwa aliyonayo ndani ya chama hicho ilimwogofya Spika Sitta,, pale anaposema: “Sasa kama mmoja wa mashabiki wake (Rostam) naye ataanza kumtwanga mangumi, basi si tu inawezekana kupata ufa mkubwa, lakini yaweza kabisa kusarambatika”.

Mwandishi huyu huyu anayekiri nguvu ya Rostam, ndiye anadiriki kuhoji Rostam angesema nini na aliwahi kusema nini bungeni.

Kilichonisikitisha zaidi, mwandishi wa makala hiyo naye ameangukia katika mkumbo. Anamwagia matope Rostam, bila kuchunguza na wala sijui kilichomtuma afanye hivyo.

Sitaki pia kuamini kama kweli mwandishi huyu anaishi nchini na ni mfuatiliaji mzuri wa masuala ya kisiasa.

Sina sababu ya kutumia nguvu kuonyesha ukweli umelala wapi katika kueleza Rostam alipata kuchangia nini akiwa bungeni. Kwa uchache niorodheshe matukio haya aliyotenda kwa ufasaha wa hali ya juu na kutikisa nchi akiwa bungeni.

Mwaka 1994 Taifa lilikumbwa na mfumuko wa bidhaa kutoka Zanzibar. Bidhaa hizo zilikuwa zikipita kwa njia ya panya, maarufu kama ‘Zanzibar route.’ Zilikuwa azikiingia nchini bila kulipa kodi na kufurika madukani. Rostam alisimama bungeni, akajenga hoja na Serikali ikachukua hatua za haraka kudhibiti hali hiyo.

Alidiriki kuwatuhumu hata viongozi wa Zanzibar kuhusiana na biashara hiyo. Hapo alionyesha ujasiri wa kwanza akiwa mbunge kijana kuliko wote wakati huo.

Mwaka 1977 Rostam alikuwa mbunge pekee aliyekataa kuunga mkono muswada wa Sheria ya Madini. Alisema muswada huo ulikuwa na upungufu mkubwa wa msingi na akaonya kuwa iwapo ungepitishwa, vizazi vijavyo vingewahukumu wabunge kwa uamuzi huo. Leo kamati ya Madini ya Rais, chini ya Jaji Mark Bomani, imeipitia sheria hii. Si ajabu matokeo yatakuwa sawa na alivyokuwa amependekeza Rostam.

Mwaka 1999 Rostam huyu huyu ambaye mwandishi hakumbuki iwapo aliwahi kusema lolote bungeni, aliweka historia katika chama tawala. Akiwa mbunge wa chama tawala, aliongoza kundi la wabunge 50 kupinga iliyoitwa kesi ya uhaini dhidi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF).

Kumbuka CUF ni chama cha upinzani. Kesi hii ilikuwa imepandikizwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Nne wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour, akidai wabunge hao walikuwa na njama za kumpindua. Baada ya hoja ya Rostam, muda mfupi baadaye watuhumiwa wote waliachiwa.

Mwaka huo huo, kwa ujasiri mkubwa, Rostam aliongoza mapambano dhidi ya Dk. Salmin aliyetaka kubadili Katiba ya Zanzibar na kuongeza muda wake wa kuwa madarakani.

Yapo mengi, ila nikumbushe hata hili. Rostam huyo huyo anayebezwa, mwaka 2001, alisimama kidete kupinga mabadiliko ya Katiba yaliyokuwa yakimpa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mamlaka makubwa zaidi, ikiwa ni pamoja na kuteua wabunge 10.

Lakini si vibaya nikakumbusha kwamba pamoja na mengi yaliyozungumzwa na Rostam bungeni, na ambayo yamekuwa na manufaa kwa Taifa ni pamoja na lile la mwaka 2004 bungeni.

Katika mkutano wa Bunge la Bajeti, Rostam alimbana vilivyo aliyekuwa Waziri wa Uchumi na Mipango, Dk. Abdallah Kigoda juu ya kazi za wizara hiyo.

Nakumbuka vizuri sana suala hili. Hasa kutokana na ujasiri wake wa kuzuia shilingi, akitaka apewe majibu ya hoja kadhaa. Mosi, ilikuwa akitaka ahakikishiwe kuwa wizara hiyo inaachana na mpango wa kukusanya takwimu za uchumi, badala yake ibuni mipango thabiti ya uchumi na kuisimamia ipasavyo.

Akapendekeza Wizara ya Uchumi na Mipango iunganishwe na Wizara ya Fedha, kwani kazi zake zilikuwa pacha na zilizohitaji kuwa chini ya kiongozi mmoja. Leo suala hilo limetekelezwa na Seriakali iliyo madarakani.

Akataka uwepo udhibiti wa hali ya juu ili shilingi isiporomoke kila uchao, kwani athari za kushuka kwa thamani kulikuwa kunayumbisha uchumi.

Mjadala ulikuwa mkali mno, na wote walioshuhudia wanakumbuka vizuri hoja za Rostam ambazo baadaye zimetekelezwa.

Sipendi kuendelea zaidi ya hapo. Natumaini mwenye macho haambiwi tazama. Wapo wabunge wa kubezwa, lakini Rostam Aziz si mmoja wao, mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni.

Nimjuavyo Rostam Aziz, kwa ujasiri aliouonyesha ni kweli angetikisa nchi. Hata hivyo, hoja zinazopenyezwa kuwa angeweza kukiumbua chama chake, Chama Cha Mapinduzi, inaelekea wanaozitoa hawamfahamu vilivyo.

Kwa jinsi anavyojulikana, Rostam atakuwa mtu wa mwisho kukiumbua chama chake, hofu inayoonekana inatokana na ujasiri uliowekwa wazi na sehemu ya historia niliyoonyesha hapo juu.

Kwa vyovyote iwavyo, Mwananzela hakumtendea haki Rostam. Uandishi wa aina hii ni hatari kwa ustawi wa Taifa. Ninashauri bora kutoandika pale tusipokuwa na taarifa sahihi, vinginevyo tunaishia kujiumbua na kulipotosha Taifa.
Na Joseph Wambura-RAIA MWEMA Aprili 23, 2008
 
Haya yalioandikwa inawezekana ni sawa lakini je Mbona kila dili anakutwa yeye?

Kila kitu anaonewa?

Wanasheria wa mwana halisi nafikiri inabidi wachukue Mabox ya mafaili yote. Kila uchafu wote hili kuonyesha huyu mtu siyo msafi. Kuanzia EPA, Kagoda stailmpaka Richie
 
Mkoloni na mwizi mwenye uraia wa utata ROstam Azizi ni shemeji ya mkuu wa kaya. Kiburi chote hiki kinapata nguvu toka somewhere.

Rostam anaweza akashinda hii case na mwanahalisi wajiandae kupigana vizuri na wasipuuzie hii case. Wale wana JF wenye nia ya kuchangia kwa hali na mali kwenye case ya mwanahalisi wafanye hivyo lakini wasishangae kama akishinda hii case.

Ukiwa unalipwa mamilioni ya dola na serikali ya Tanzania kila mwezi, unakuwa na uwezo wa kununua kila jaji hapo Tanzania na kushawishi matokeo ya case dhidi yako.

Hili jambo ni zito na muhimu sana, ni kipimo pia cha uadilifu wa Kikwete.
 
Ni vizuri sana RA amekwenda mahakamani mimi kama Mtanzania ningependa kujua ukweli wa mambo.

Tunachojua RA ni Mtuhumiwa na Kampuni ya Richmond ni Kampuni ya Mfukoni. Na kingine ni kwamba yeye ana uhusiano na Dowans ambayo ndiyo iliyoinunua Richmond.

Karamagi, Msabaha, Ex-waziri Mkuu wote wameisha sema ni Kampuni hewa. Cha kushangaza RA kama ana share na Dowans alipata wapi contact za kampuni hewa hili imuuzie Mkataba wa Richmond?

Mahakamani tu ndipo EL, Karamagi, wafanyakazi wa Wizara nk watatwambia nani ni nani.

Kama ni ya Kinara wa nchi na hilo tulijue. Nafikiri hili kwa watanzania ni kama neema. Hila pia watanzania wakikomaa vizuri bila kumtelekeza mwanahalisi, ukweli tunaoutafuta tutaupata.

Jaji sijui kuongwa ataongwa tu kama wananchi hatutakuwa makini na jinsi kesi inavyokwenda. Siku hizi watu waliowengi wanajua sheria akitokea mslaliti ajue mbele ya safari tutaulizana. Kinachotakiwa haki itendeke kwa RA na pia kwa mwanahalisi.
 
Hili jambo ni zito na muhimu sana, ni kipimo pia cha uadilifu wa Kikwete.
Mwafrika wa kike naomba kukataa kuwa hiki ndicho kipimo cha kikwete,anaweza kumtosa kuwafurahisha nyie then RA akaendelea kupeta,ndiyo staili mpya nayotumika na kuna mtu ndiye aliwashauri,na wanamtumia sana kwa sasa.

1.Angalia suala la EPA,watu wameshajulikana ila wameachwa bila kushugulikiwa,sie tumefurahi ila hakuna cha ziada.

2.Suala la BOT,Ripoti imetoka naikafanywa siri,kuna nini ndani ya hiyo ripoti ambacho watanzania wengine hawatakiwi kukifahamu.

3.Kuanguka kwa mara ya pili kwa Lowassa,Tumeshangilia,ila nini kimefanyika baada ya watu hwao kujiuzuru.

4.Suala la Buzwagi,Je ni nani keshachukuliwa hatua,na ilikuwa sawa kwa watu hao kusaini mkataba huko nje?

Mie nitapima Uadilifu wa kikwete kama akiruhusu serikali ya Umoja wa kitaifa kule Zanzibar na kumng'oa Gray Mgonja,huyu ndiye source ya haya matatizo yote.He is their Head-teacher when you talks about all dirty deals,the king of spinning in the government.na hata ushauri wa kwenda kusajili TANGOLD huko Nje ni wake,

Mama,
siko tayari tena kufungwa bao la kisigino,Je uko tayari tena!!Mwache aende mahakamani ili aje atuambie who owns RDC?
 
He is not serious since he want to show tanzanian that he is above the law. Let him ggo to the court and the whole antion to see how corrupt he is.
 
Mfa maji haachi kutapatapa, yeye anadhani watanzania ni matahira ila iko siku hawa mafisadi watatamani dunia ipasuke, subiri.
 
Okay! now he is talking, sasa cha muhimu hapa ni kwa Mwanahalisi kwenda naye kwenye sheria, ili ukweli usemwe wazi ninasema haitakuja tena nafasi kama hii, kama ikibidi tuwasaidie wenzetu wa huko gazeti la Mwanahalisi kwa hali na mali, ili hii ishu ifike mahakamani ili nyani akomwe mchana,

Wakuu wa Mwanahalisi, hapa tuko ukurasa mmoja wakuu huyu Patel ni kukutana naye mahakamani tu na apewe ukweli wa uovu wake, upo mwingi sana, labda tuanze kuwasogezea ushahidi pole pole,

wananchi hatuwezi kutishiwa nyau na mafisadi...!
Kwa mara nyingine tena mnajaribu kumdanganya Kubenea kuwa unao ushahidi wa kumsaidia ktk kesi yake na mh RA.napenda kuwaambia kwanza kuwa jamaa hawezi kuwa amekurupuka kufungua kesi kwani ni wazi nae ana wanasheria wake kadhaa ambao wamemshauri vema.Najua mfuasi mwaminifu wa malecela unafuraha sana now
 
Ukisikia mimi nakuunga mkono na kukubali ukifanya vyema ES ni kwenye maswala kama haya .You have said it all .Nakupongeza kabisa na sasa huyu jamaa nadhani kalengeshwa na ndiyo mwisho wake sasa .
SASA HUKU NDIO KUMTISHIA NYAU,RA HAWEZI KULENGESHWA NA MTU,ANA AKILI YA KUTOSHA NA KWA HAKIKA ATASHINDA KESI HII.
 
kafungua kweli kesi ?Je washauri hana wa kumweleza kwamba aachane na haya ? Je ataweza mikiki ya mahakamani maana Mwana Halisi atapata mawakili kibao na kupambana na hapo unaweza kushanaa viongozi wa CCM sasa wanaitwa Mahakamani .Ni kweli kafungua ama waandishi tu jamani ?Maana tuliambiwa Masha kafungua ikawa hadithi hadi sasa .
Kaka acha kukaa na kuota ndoto kwanza kuwa na mawakili kibao sio ushindi katika kesi,nyie mnaishia kupiga kelele humu jf na wala hamtatoa pua zaenu mahakamani.Kennedy Fungamtama anawatosha kabisa.Na zamu ya Raiamwema imefika staytuned watoto wa walalahoi.
 
SASA HUKU NDIO KUMTISHIA NYAU,RA HAWEZI KULENGESHWA NA MTU,ANA AKILI YA KUTOSHA NA KWA HAKIKA ATASHINDA KESI HII.

Dikteta
Mie nimeona kwanza jina then nikasema kuna kazi .Kusoma comments zikatoa majibu ya mawazo yangu .Karibu kaka .Njoo slow hapa ni JF.Personalities attack hazina room hapa .Unamvaa Mzee ES kwa uhuru wake wa mawazo ? Mbona unasema Rostam ambaye unamwita Mh.Wakati sote tunamjua ni mwizi tu , atashinda na hupingwi ? Anaweza kupata wnasheria wakamwingiza mkenge ili aishe vile vile .The guy is iranian ndiyo maana hajali maisha ya Watanzania .
 
I still believe the man has every right kuwasue mwanahalisi after all hakuna chombo chochote cha sheria kilichomstaki kuwa ufisadi au rushwa

Yes i have my doubts about the man lakini i wont fall into playa hating eti nimchukie tuu kwa sababu kahusishwa na rushwa...nop, thats not how i operate. Na nikitazama media ya Tanzania, well i am not surpprised at all

Got for it Rostam huko mahakamani ndio tutajua PUMBA NI ZIPI NA MCHELE NI UPI
 
Ubaguzi.... Ukabila, Udini, Umajimbo, Ukanda!! Tuwakome Mafisadi kwa ufisadi wao please! Hawa Chenge, Richmomd, Karamagi, Balali Makapa....wote ni wamatumbi kabisa, ni CCM na Wanatuua polepole kwa ufisadi wao!

Bora useme wewe maana hapa hawana focus kabisa na wanajidai wana ushahidi kumbe ni ushabiki ambao mahakama kamwe haiwezi kudeal nao,rangi ya rostam sio ushahidi wa kesi mahakamani.
 
wacheni haki ya mungu iijiidhirishe
ni wakati wa kusali na kuomba....mama mchungaji rwakatare alipotangaza kuna watoto wa kishirikina wengi wal;ipinga na kulaani ananua watoto sasa mungu kajiidhirisha mtoto yuleyule kakutwa ankula fuvu la mtu....hivyo tuwaache hawa mafisadi wanapojaribu kucheza na nguvu za mungu wacheni mungu ajiidhirishe
hata yona alimezwa na samaki kwa manufaa ili akawaokoe watu ...so hata huyu kwenda mahakamani mapenzi ya mung kufukua mengi yaliyojifisha
mungu uinuliwe kwa hili
 
Sasa huyu RA anashangaza kweli, Kaspian ni kampuni yake na hao Richmond wanatumia email adress ya Kaspian, hapo kweli hakuna mahusiano????
Kaka acha kukurupuka richmond hawajapata kutumia email ya richmond bali ni dowans.RA ataprove kirahisi kabisa kuwa yeye hausiki a \richmond kama alivyoanza wakili Tenga wa Richmond kusema last month kuwa kampuni ipo na inawenyewe,sasa kama mwenyewe akijitokeza na KUBENEA atatoa ushahidi gani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom