VIDEO: Msanii Roma na wenzake warejea rasmi uraiani. Kufunguka Jumatatu

Casuist

JF-Expert Member
Jul 23, 2014
1,179
2,940


Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Roma akiongea baada ya kutoka hospitali ya Mwananyamala. Amesema yeye na wenzake ni wazima wa afya, kimwili na kiakili na kuwashukuru watanzania wote waliowapigania kipindi cha sintofahamu yao.

Roma amesema kutokana na masuala ya makubaliano yao ya kuachiwa, wameomba kupumzika leo na kesho kisha Jumatatu wataongea kwa kina yote yaliyowapata.
 
Mhhhhhhhhhhhhh. Hayo makubaliano ya kuachiwa kama yanawabana sasa wasiongee kitu, ninashindwa kujua jumatatu kama wataongea kwa uhuru au wataongea kwa mujibu wa hayo makubaliano ya kuachiwa.

Tanzania my mamaland!. Tunatabasamu nyuso mioyo ikivuja damu. Nadhani amesahau kuishukuru serikali kati ya wale aliowashukuuru kwa kuwapigania.

Ninatamani na Saanane aachiwe kwa makubaliano ya kuachiwa.
 
Namshukuru Mungu kwa kuonekana kwao maaana huku mitaani maneno ya yalikuwa yamesha kuwa mengi kwa serikali. Mungu anaipenda serikali yetu. Hongera JPM kwa kuwa na wapelelezi walio bobea Mungu akubariki aminaa
Tumia akili, unadhan kusema amepewa masharti ya kuachiwa, ingekuwa ni upelelez c wangemchukua hao maaskar toka kwa watekaji bila masharti, yaan angeokolewa bila masharti.
 
Back
Top Bottom