Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Bado think tank ya CHADEMA inabaki kuwa bora kwa nyakati tulizoona. Bado CHADEMA inabaki kuwa akili kubwa kati ya vyama vyote vya siasa Tanzania kwasasa, kwanini nathubutu kusema haya?
Imeshatibitika wazi kwamba kuna kundi kubwa na lenye nguvu la wahafidhina kwenye mfumo ambao hawataki na hawako tayari kwa mabadiliko.
Imeshathibitika wazi ya kwamba kuna kundi kubwa la wafaidikaji, wakiwemo familia za wanasiasa wa CCM na marafiki zao, wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji katika sekta mbalimbali, imeshathibitika wazi ya kwamba kuna mataifa rafiki wa CCM, yanayofaidika kiuchumi na kijamii kwa CCM kuwepo madarakani, hivyo hayako tayari kuona CCM inaondoshwa.
Imeshathibitika wazi kwamba kupata Katiba Mpya kwasasa ni kipengele kigumu mno. Imeshathibitika wazi ya kwamba kupata Tume Huru ya Uchaguzi itakayokidhi mahitaji ya sasa kisiasa kwenye uchaguzi mkuu pia ni ngumu mno!
Sasa CHADEMA ifanyeje kuweza kutoboa?
~ CHADEMA inahitaji kufanya siasa kwa amani, usalama na utulivu.
~ CHADEMA inahitaji kuongeza wigo wa wanachama na kujiimarisha tangu chini kabisa bila mizengwe na kuleteana tafrani.
~ CHADEMA inahitaji kufanya siasa za kistaarabu na malumbano ya hoja, ili wananchi waweze kupambanua pumba na mchele.
~ CHADEMA inahitaji sana ulinzi na usalama wa viongozi wake wa ngazi zote, wanachama na wafuasi wake, mali, vitega uchumi na uwekezaji wake popote pale Tanzania
Sasa hili litawezekanaje?
Ilikuwa ni muhimu kupara mkakati wa maridhiano. Maridhiano ambayo kwa sehemu kubwa yanayomhitaji mkuu wa kaya kuliko timu zilizokuwa zimeundwa toka vyama mbalimbali kasoro CHADEMA.
Kwanini hili?
Katiba ya sasa inampa madaraka makubwa mkuu wa nchi, hata kama ana washauri nyuma ya pazia lakini anapojitokeza hadharani kauli yake ndio final!
~ Kwa kuliona hili maridhiano yalikuwa ni muhimu zaidi kati ya CHADEMA na CCM kupitia mkuu wa nchi, na ndio maana maridhiano husika yakabeba taswira ya mkuu wa nchi na CHADEMA na hakuna chawa wala kunguni aliyeleta fyoko zaidi ya kulalama mitandaoni.
Faida zake ni nini kwa pande hizi mbili?
Ndani ya CCM kuna makundi yaliyomsumbua sana mama, hasa yale makundi faidika na awamu iliyopita! Haya yamekuwa yakimpinga waziwazi hadharani mitandaoni na sirini pia, kuna haya makundi ya wataka Urais 2025 nayo yamekuwa yakiibuka mara kwa mara lakini yakakutana na nyundo ya mfumo na kusambaratishwa nayo haya ni masumbufu.
CHADEMA ni chama kikuu cha Upinzani Tanzania chenye wanachama milion kumi na wafuasi idadi sawa na hiyo ama kuzidi kidogo. Kwenye siasa watu ni mtaji mkubwa sana, kwa ubunifu wa maridhiano yaliyokuja mama ameweza kuwasambaratisha wakosoaji na wasumbufu wote hasa ndani ya chama chake! Kwahiyo sasa mama ana wasaa mzuri wa kupiga kazi huku wasiompenda wakimuogopa sasa kwa kudhani ana backup ya chama kikuu cha upinzani Tanzania.
Faida kwa upande wa CHADEMA sasa;
Kufanya siasa za ukosoaji wa hoja kwa makada na wanasiasa wa CCM bila kumhusisha sana mama.
Lengo ni nini?
Kupata Katiba ni lazima uwe na Bunge lenye wabunge wenye utayari na uwezo wa kulisimamia hilo kidete. Kwa mfumo wetu wa sasa wa tume ya uchaguzi, system huwa inamakinika zaidi na kura za Urais.
CHADEMA kwa kudili zaidi na wanasiasa wa CCM ni kutafuta uungwaji mkubwa wakati wa uchaguzi ili CHADEMA ipate majority ya wabunge. Ukishakuwa na majority ya Wabunge hata Rais akitoka upande mwingine una faida ya kufanya mengi kupitia Bunge kama mhimili huru.
Chawa wa mama na Samia gang wameonekana ni uchuro zaidi ya kumsadia mama kuliko faida na political mileage anayoipata kupitia maridhiano na CHADEMA.
Hizi tuhuma za kulamba asali na ukosoaji mwingine wa kijinga ni hasira, wivu husuda na kijicho kwa wale wote ambao hawakuridhishwa na hayo maridhiano yanayowaweka CHADEMA na mama kwenye nafasi bora zaidi kisiasa Tanganyika!
Ni alfajiri nyingine tena ya faraja kuu!
Imeshatibitika wazi kwamba kuna kundi kubwa na lenye nguvu la wahafidhina kwenye mfumo ambao hawataki na hawako tayari kwa mabadiliko.
Imeshathibitika wazi ya kwamba kuna kundi kubwa la wafaidikaji, wakiwemo familia za wanasiasa wa CCM na marafiki zao, wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji katika sekta mbalimbali, imeshathibitika wazi ya kwamba kuna mataifa rafiki wa CCM, yanayofaidika kiuchumi na kijamii kwa CCM kuwepo madarakani, hivyo hayako tayari kuona CCM inaondoshwa.
Imeshathibitika wazi kwamba kupata Katiba Mpya kwasasa ni kipengele kigumu mno. Imeshathibitika wazi ya kwamba kupata Tume Huru ya Uchaguzi itakayokidhi mahitaji ya sasa kisiasa kwenye uchaguzi mkuu pia ni ngumu mno!
Sasa CHADEMA ifanyeje kuweza kutoboa?
~ CHADEMA inahitaji kufanya siasa kwa amani, usalama na utulivu.
~ CHADEMA inahitaji kuongeza wigo wa wanachama na kujiimarisha tangu chini kabisa bila mizengwe na kuleteana tafrani.
~ CHADEMA inahitaji kufanya siasa za kistaarabu na malumbano ya hoja, ili wananchi waweze kupambanua pumba na mchele.
~ CHADEMA inahitaji sana ulinzi na usalama wa viongozi wake wa ngazi zote, wanachama na wafuasi wake, mali, vitega uchumi na uwekezaji wake popote pale Tanzania
Sasa hili litawezekanaje?
Ilikuwa ni muhimu kupara mkakati wa maridhiano. Maridhiano ambayo kwa sehemu kubwa yanayomhitaji mkuu wa kaya kuliko timu zilizokuwa zimeundwa toka vyama mbalimbali kasoro CHADEMA.
Kwanini hili?
Katiba ya sasa inampa madaraka makubwa mkuu wa nchi, hata kama ana washauri nyuma ya pazia lakini anapojitokeza hadharani kauli yake ndio final!
~ Kwa kuliona hili maridhiano yalikuwa ni muhimu zaidi kati ya CHADEMA na CCM kupitia mkuu wa nchi, na ndio maana maridhiano husika yakabeba taswira ya mkuu wa nchi na CHADEMA na hakuna chawa wala kunguni aliyeleta fyoko zaidi ya kulalama mitandaoni.
Faida zake ni nini kwa pande hizi mbili?
Ndani ya CCM kuna makundi yaliyomsumbua sana mama, hasa yale makundi faidika na awamu iliyopita! Haya yamekuwa yakimpinga waziwazi hadharani mitandaoni na sirini pia, kuna haya makundi ya wataka Urais 2025 nayo yamekuwa yakiibuka mara kwa mara lakini yakakutana na nyundo ya mfumo na kusambaratishwa nayo haya ni masumbufu.
CHADEMA ni chama kikuu cha Upinzani Tanzania chenye wanachama milion kumi na wafuasi idadi sawa na hiyo ama kuzidi kidogo. Kwenye siasa watu ni mtaji mkubwa sana, kwa ubunifu wa maridhiano yaliyokuja mama ameweza kuwasambaratisha wakosoaji na wasumbufu wote hasa ndani ya chama chake! Kwahiyo sasa mama ana wasaa mzuri wa kupiga kazi huku wasiompenda wakimuogopa sasa kwa kudhani ana backup ya chama kikuu cha upinzani Tanzania.
Faida kwa upande wa CHADEMA sasa;
Kufanya siasa za ukosoaji wa hoja kwa makada na wanasiasa wa CCM bila kumhusisha sana mama.
Lengo ni nini?
Kupata Katiba ni lazima uwe na Bunge lenye wabunge wenye utayari na uwezo wa kulisimamia hilo kidete. Kwa mfumo wetu wa sasa wa tume ya uchaguzi, system huwa inamakinika zaidi na kura za Urais.
CHADEMA kwa kudili zaidi na wanasiasa wa CCM ni kutafuta uungwaji mkubwa wakati wa uchaguzi ili CHADEMA ipate majority ya wabunge. Ukishakuwa na majority ya Wabunge hata Rais akitoka upande mwingine una faida ya kufanya mengi kupitia Bunge kama mhimili huru.
Chawa wa mama na Samia gang wameonekana ni uchuro zaidi ya kumsadia mama kuliko faida na political mileage anayoipata kupitia maridhiano na CHADEMA.
Hizi tuhuma za kulamba asali na ukosoaji mwingine wa kijinga ni hasira, wivu husuda na kijicho kwa wale wote ambao hawakuridhishwa na hayo maridhiano yanayowaweka CHADEMA na mama kwenye nafasi bora zaidi kisiasa Tanganyika!
Ni alfajiri nyingine tena ya faraja kuu!