gilbert35
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 253
- 476
- Thread starter
- #21
Halfani Sudy anasimulia HATARI
Mawasiliano 0629 360357
Mahali Getho
“Hatupendi kuwafanyia hiki tunachoenda kuwafanyia, lakini hatuna namna nyingine sahihi ya kufanya zaidi ya kufanya hivi, mmejifanya wakaidi, na siku zote hivi ndivyo tuwafanyavyo wakaidi” Daniel alisema kwa sauti ndogo wakati akimfuata yule aliyejiita mwenyekiti.
Hii ni Sehemu ya Tano
Mwenyekiti alimwangalia usoni Daniel, aliiona dhamira halisi ya kufanyiwa jambo baya katika sura ya Daniel Mwaseba.
“Msituue, msituue, msituue….” Mwenyekiti alisema kwa sauti ndogo huku akimwangalia Daniel kwa macho ya huruma.
“Hatuwaui, ila tutakachowafanya ni bora tungewaua” Daniel alisema wakati akiwasha jiko la umeme lilikuwa pembeni ya kiti alichofungiwa Mwenyekiti. Jiko lilipotengeneza miale ya moto, akakiweka kile chuma alichokitoa kabatini, kikaanza kupata moto. Kulingana na moto ulivyokuwa mkali ilichukua dakika zipatazo tano kile chuma kubadilika rangi na kuwa chekundu.
“Ninawapa nafasi ya mwisho ya kuwasikiliza, hamtaipata nafasi hii tena katika maisha yenu endapo nikianza kuwatesa. Nitazipasha korodani zenu kwa kile chuma cha moto! Hamtaweza kupata watoto tena. Niwaahidi tu, sitakuwa na huruma nanyi tena!” Daniel alisema akimsogelea Mwenyekiti.
“Sisi tumetumwa, tumetumwa tu, tumetumwa tu sisi…” Mwenyekiti alisema kwa sauti ya uwoga huku akimwangalia Daniel Mwaseba.
“Mmetumwa na nani?” Martin aliuliza swali akimtazama Mwenyekiti.
“Jamani, kwa kifupi sisi ni vibaka tu wa mtaani, mimi ninaitwa Babu Ogutu, yule mwenzangu anaitwa Okello. Kazi zinayotuweka hapa mjini ni kazi haramu. Mara kadhaa tunakodiwa na watu mbalimbali kwa ajili ya kuwafanyia kazi zao haramu. Wiki moja iliyopita tukiwa kijiweni kwetu alikuja kijana mmoja wa makamo. Alijitambulisha kuwa anaitwa John Masalu, alituita pembeni na kutuambia kwamba kuna kazi ya kufanya ambayo ingetuingizia pesa nyingi sana, tulikubali bila kujiuliza kwakuwa ndio kazi zetu. Alitupakia kwenye gari yake na kutupeleka katika jumba moja maeneo ya Oysterbay. Ndani ya hilo jumba ndimo tulipokutana na Mrombo”
“Mrombo ni nani?” Daniel Mwaseba alimkatisha Babu Ogutu na kuuliza swali. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kulisikia hilo jina.
“Mrombo, Mrombo ni jambazi anayeogopeka sana hapa jijini Dar es salaam. Wizi mwingi mkubwa unaofanyika hapa jijini kunakuwa na mkono wwa Mrombo. Kwa mfano uvamizi wa benki ya LDB pale Mlimani city uliofanyika wiki moja iliyopiata ilikuwa ni kazi ya genge la Mrombo. Uvamizi wa Juso Supermarket uliofanyika juzi kule Mikocheni pia ulifanywa na genge la Mrombo. Pia uvamizi wa vituo mbalimbali vya mafuta vinakuwa na mkono wa Mrombo”
“Eeeh endelea, milivyokutana na Mrombo?” Daniel alimkatisha Babu Ogutu.
“Mrombo ndiye aliyetupa majukumu ya kazi ile, mimi nijifanye kuwa mwenyekiti wa mtaa na Okello ajifanye kuwa mjumbe. Ilikuwa ni kazi ndogo sana lakini ingetuingizia shilingi milioni mbili. Mimi na mwenzangu tulikubali bila kujifikiria mara mbili. Jana, John Masalu alitufuata kijiweni kwetu na kutuambia kuwa leo ndio ilikuwa siku ya kazi. Na ilipofika leo asubuhi, John Masalu alitupitia na gari yake, ndani ya gari tuliwakuta wale askari na moja kwa moja tukaja ofisini kwako” Babu Ogutu alielezea kwa kirefu.
“Huyo John Masalu yeye yupo wapi?” Daniel aliuliza swali.
“John Masalu ndio yule askari aliyejitambulisha kwako kama Inspeta Hayman. Yule sio askari, ila ana urafiki na maaskari wengi hapa jijini, ambao anawatumia katika madili yake mbalimbali” Babu Ogutu alisema.
“Unaweza kutupeleka katika nyumba anayoishi Huyo Mrombo?” Daniel Mwaseba alimuuliza tena Babu Ogutu, aliamini kila alichosema.
“Atatuua, Mrombo atatuua…” Okello alisema huku sauti yake ikimaanisha alichokuwa anakisema. Walikuwa wanamuogopa Mrombo.
“Kwani mnajua sisi tutawafanya nini endapo msipotupeleka?” Daniel aliuliza swali huku akimwangalia Okello.
Okello alikaa kimya.
“Babu Ogutu, mtatupeleka nyumbani kwa Mrombo, kwa njia yoyote ile lazima tumpate Mrombo ili tujue malengo ya watu hawa” Daniel alisema akimwangalia Babu Ogutu.
Babu Ogutu aliitikia kwa kutikisa kichwa.
“Tutakuja hapa baada ya nusu saa, tukija moja kwa moja tutaelekea nyumbani kwa Mrombo. Nawaonya, msijaribu kufanya ujanja wa aina yoyote ile wa kutuhadaa, utagharimu maisha yenu!” Daniel alisema wakati akitoka nje, Martin Hisia naye alifata kwa nyuma.
Walipofika sebuleni walimkuta Hannan akiwa amekaa sofani, ameipakata tarakilishi yake akiwasubiri kwa hamu. Daniel Mwaseba alichukua nafasi ya kumueleza Hannan kila kitu kilichotokea katika chumba cha mateso. Mara kadhaa Hannan alikuwa anaitikia kwa kutikisa kichwa wakati Daniel akimsimulia na kuuliza sehemu asipoelewa vizuri.
“Hayo ndio yetu Hannan kutoka katika chumba cha mateso. Kikubwa tumeondoka na jina moja tu, Mrombo, eeeh tuambie wewe umepata nini juu ya zile kazi mbili tulizokupa za kufatilia namba ya Msamaria mwema na yule mtu aliyenipigia kunipa vitisho tukiwa hapa?” Daniel alisema huku akimwangalia Hannan.
Hannan alikohoa kidogo kuitengeneza sauti yake sawa, macho yake yakaelekea kwenye tarakilishi yake huku akiongea, “Msamaria mwema, imenifanya nitumie program maalum kuweza kuingia katika kanzidata ya mawasiliano ya jeshi la Polisi, sio kazi ndogo hata kidogo, sio tu yahitaji uwe na program maalum ambayo sio rahisi kwa mtu wa kawaida kuwa nayo lakini pia inabidi uwe mtaalam wa hadhi ya juu sana kuweza kucheza na kompyuta. Nimeyasikiliza mawasiliano yote ya Polisi ya leo asubuhi katika kanzidata yao, hakuna simu iliyopigwa kutoka kwa mtu anayejiita Msamaria mwema, na hiyo inamaanisha kwamba yote aliyoyasema Babu Ogutu ni kweli, Inspekta Hayman alikuwa Polisi feki, yeye alikuwa mwenyekiti feki, na wenzie wote hawakuwa halisi kwa maana ya neno halisi linavyomaanisha. Baada ya kutopata lolote kutoka katika kanzidata ya mawasiliano ya jeshi la Polisi nikahamia kwa huyu mtu aliyekupigia simu ya vitisho hivi punde. Baada ya kuichunguza namba ile, nimegundua kwamba namba imesajiliwa kwa jina la Witness Msombe. Nilianza kumchunguza huyo Witness Msombe ni nani, majibu niliyoyapata ni kwamba Witness Msombe ni mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Dar es salaam, Witness yupo mwaka wa pili akisomea hiyo shahada ya sheria. Hayo ndio niliyoyagundua juu ya zile namba mbili ulizonipa” Hannan alisema huku akiinyanyua sura yake iliyokuwa imeiinamia tarakilishi yake iliyokuwa juu ya mapaja yake.
“Safi sana Hannan, umefanya kazi kubwa sana, sasa tumepapata pa kuanzia ili kujua hawa watu wana mpango ndani ya nchi hii. Kwanza lazima tukamchukue Mrombo nyumbani kwake na kumleta hapa, ni yeye ndiye atakayetuambia anashirikiana na kina nani? Na wana mpango gani? Pili lazima tuende chuo kikuu cha Dar es salaam kuonana na huyo Witness Msombe. Lazima atuambie iweje namba yake itumike kunitishia, na bila shaka yeye atakuwa anajua mahali alipowekwa Dokta Tawakal” Daniel Mwaseba alisema kwa kirefu.
“Upo sahihi Daniel, lazima tuyafanye hayo uliyosema, lakini tutaweza kweli peke yetu kufanya mambo yote hayo, ninashauri tuongeze nguvukazi ya kutusaidia ili tufanikishe uchunguzi wetu” Martin alitoa ushauri wake.
“Upo sahihi Martin, tunahitaji nguvukazi ili kukamilisha uchunguzi wetu kwa wakati, pengine kabla ya mimi na Hannan hatujamaliza likizo zetu. Lakini niseme tu uchunguzi huu utafanywa na watu watano tuliomo humu ndani. Nitamwambia Chifu juu ya mpango wa watu hawa tukikamilisha au itakapobidi. Safari hii nataka niwaoneshe mimi ni nani hawa wapuuzi walionikatisha safari yangu ya kwenda Dubai kula starehe” Daniel alisema akimwangalia Martin Hisia.
“Daniel, unasemaje tupo watano wakati tupo watatu tu, mimi, wewe na Hannan, hao watu wawili wengine wapo wapi?” Martin aliuliza huku akimwangalia Daniel kwa mshangao.
“Sijakosea Martin, tupo watano humu ndani, Tutawatumia Babu Ogutu na Okello katika uchunguzi wetu, wale ndio watakamilisha idadi ya hao watu watano” Daniel alisema kwa kujiamini.
“Khhaaaa Daniel, umeshawaamini wale majambazi?” Martin na Hannan walijikuta wakiuliza kwa pamoja.
“Ninawaamini, ni shida tu ndizo zilizowafanya wachague upande ule haramu, tutawapa nafasi ya kubadilika na kusahihisha makosa waliyoyafanya hapa duniani. Babu Ogutu jinsi anavyoongea anaonesha kabisa hafurahii alichokuwa anakifanya, bila shaka ugumu wa maisha umemfanya aichague njia ile. Nitaenda kuongea nao, na bila shaka watakubali kuungana na sisi katika uchunguzi wetu” Daniel alisema kwa kirefu.
“Daniel, wewe ni kiongozi wangu katika operesheni nyingi sana, operesheni zilizoisha kwa mafanikio makubwa na kuiokoa nchi yetu katika hatari kutokana na uongozi wako madhubuti, lakini kwa mara ya kwanza leo napingana na wewe, sikubaliani na mpango wako wa kuwatumia wahalifu katika uchunguzi wa suala hili. Wale ni nyoka wenye sumu kali na sisi ni binadamu wa kawaida, Daniel, hakujawahi kutokea urafiki wa dhati kati ya nyoka wenye sumu kali na binadamu wa kawaida hata siku moja” Martin alionesha msimamo wake kwa kukataa mpango wa Daniel Mwaseba.
“Martin najua hisia zako zinapokupeleka, lakini naomba ukubali mpango wangu huu, hata hao wakina David unaoweza kushauri tuwatumie walikuwa katika upande sawa na kina Babu Ogutu. Hata wewe mwenyewe ulikuwa upande ule kabla hujahamia upande huu. Ni imani yangu kwako ndio iliyotuleta pamoja leo hii. Naomba unikubalie tufanye kazi na wale watu, kuna faida kubwa sana tukiwaonesha kuwa tumewaamini” Daniel Mwaseba naye alisimamia msimamo wake.
“Moja…..” Hannan alianza kuhesabu huku akinyoosha kiganja chake kwa mbele.
“Mbili…..” Martin akadakia, akanyoosha kiganja chake na kugusanisha juu ya kiganja cha Hannan.
“Tatu……” Daniel Mwaseba alimalizia huku naye akikigusisha kiganja chake juu ya mikono ya Hannan na Martin.
“Mojaaaa, mbiliiiiii, tatuuuuuu…………” Wote watatu, walihesabu kwa pamoja kwa sauti kubwa huku viganja vyao vikiwa vimeshikana.
“Tunaishi pamoja…”Daniel Mwaseba alisema….
“…na tutakufa pamoja!” Hannan Halfani na Martin Hisia waliitikia.
Walikuwa wameelewana, na walikuwa tayari kuanza kazi.
*****
Je nini kitatokea?
LAKO JICHO.
Mawasiliano 0629 360357
Mahali Getho
“Hatupendi kuwafanyia hiki tunachoenda kuwafanyia, lakini hatuna namna nyingine sahihi ya kufanya zaidi ya kufanya hivi, mmejifanya wakaidi, na siku zote hivi ndivyo tuwafanyavyo wakaidi” Daniel alisema kwa sauti ndogo wakati akimfuata yule aliyejiita mwenyekiti.
Hii ni Sehemu ya Tano
Mwenyekiti alimwangalia usoni Daniel, aliiona dhamira halisi ya kufanyiwa jambo baya katika sura ya Daniel Mwaseba.
“Msituue, msituue, msituue….” Mwenyekiti alisema kwa sauti ndogo huku akimwangalia Daniel kwa macho ya huruma.
“Hatuwaui, ila tutakachowafanya ni bora tungewaua” Daniel alisema wakati akiwasha jiko la umeme lilikuwa pembeni ya kiti alichofungiwa Mwenyekiti. Jiko lilipotengeneza miale ya moto, akakiweka kile chuma alichokitoa kabatini, kikaanza kupata moto. Kulingana na moto ulivyokuwa mkali ilichukua dakika zipatazo tano kile chuma kubadilika rangi na kuwa chekundu.
“Ninawapa nafasi ya mwisho ya kuwasikiliza, hamtaipata nafasi hii tena katika maisha yenu endapo nikianza kuwatesa. Nitazipasha korodani zenu kwa kile chuma cha moto! Hamtaweza kupata watoto tena. Niwaahidi tu, sitakuwa na huruma nanyi tena!” Daniel alisema akimsogelea Mwenyekiti.
“Sisi tumetumwa, tumetumwa tu, tumetumwa tu sisi…” Mwenyekiti alisema kwa sauti ya uwoga huku akimwangalia Daniel Mwaseba.
“Mmetumwa na nani?” Martin aliuliza swali akimtazama Mwenyekiti.
“Jamani, kwa kifupi sisi ni vibaka tu wa mtaani, mimi ninaitwa Babu Ogutu, yule mwenzangu anaitwa Okello. Kazi zinayotuweka hapa mjini ni kazi haramu. Mara kadhaa tunakodiwa na watu mbalimbali kwa ajili ya kuwafanyia kazi zao haramu. Wiki moja iliyopita tukiwa kijiweni kwetu alikuja kijana mmoja wa makamo. Alijitambulisha kuwa anaitwa John Masalu, alituita pembeni na kutuambia kwamba kuna kazi ya kufanya ambayo ingetuingizia pesa nyingi sana, tulikubali bila kujiuliza kwakuwa ndio kazi zetu. Alitupakia kwenye gari yake na kutupeleka katika jumba moja maeneo ya Oysterbay. Ndani ya hilo jumba ndimo tulipokutana na Mrombo”
“Mrombo ni nani?” Daniel Mwaseba alimkatisha Babu Ogutu na kuuliza swali. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kulisikia hilo jina.
“Mrombo, Mrombo ni jambazi anayeogopeka sana hapa jijini Dar es salaam. Wizi mwingi mkubwa unaofanyika hapa jijini kunakuwa na mkono wwa Mrombo. Kwa mfano uvamizi wa benki ya LDB pale Mlimani city uliofanyika wiki moja iliyopiata ilikuwa ni kazi ya genge la Mrombo. Uvamizi wa Juso Supermarket uliofanyika juzi kule Mikocheni pia ulifanywa na genge la Mrombo. Pia uvamizi wa vituo mbalimbali vya mafuta vinakuwa na mkono wa Mrombo”
“Eeeh endelea, milivyokutana na Mrombo?” Daniel alimkatisha Babu Ogutu.
“Mrombo ndiye aliyetupa majukumu ya kazi ile, mimi nijifanye kuwa mwenyekiti wa mtaa na Okello ajifanye kuwa mjumbe. Ilikuwa ni kazi ndogo sana lakini ingetuingizia shilingi milioni mbili. Mimi na mwenzangu tulikubali bila kujifikiria mara mbili. Jana, John Masalu alitufuata kijiweni kwetu na kutuambia kuwa leo ndio ilikuwa siku ya kazi. Na ilipofika leo asubuhi, John Masalu alitupitia na gari yake, ndani ya gari tuliwakuta wale askari na moja kwa moja tukaja ofisini kwako” Babu Ogutu alielezea kwa kirefu.
“Huyo John Masalu yeye yupo wapi?” Daniel aliuliza swali.
“John Masalu ndio yule askari aliyejitambulisha kwako kama Inspeta Hayman. Yule sio askari, ila ana urafiki na maaskari wengi hapa jijini, ambao anawatumia katika madili yake mbalimbali” Babu Ogutu alisema.
“Unaweza kutupeleka katika nyumba anayoishi Huyo Mrombo?” Daniel Mwaseba alimuuliza tena Babu Ogutu, aliamini kila alichosema.
“Atatuua, Mrombo atatuua…” Okello alisema huku sauti yake ikimaanisha alichokuwa anakisema. Walikuwa wanamuogopa Mrombo.
“Kwani mnajua sisi tutawafanya nini endapo msipotupeleka?” Daniel aliuliza swali huku akimwangalia Okello.
Okello alikaa kimya.
“Babu Ogutu, mtatupeleka nyumbani kwa Mrombo, kwa njia yoyote ile lazima tumpate Mrombo ili tujue malengo ya watu hawa” Daniel alisema akimwangalia Babu Ogutu.
Babu Ogutu aliitikia kwa kutikisa kichwa.
“Tutakuja hapa baada ya nusu saa, tukija moja kwa moja tutaelekea nyumbani kwa Mrombo. Nawaonya, msijaribu kufanya ujanja wa aina yoyote ile wa kutuhadaa, utagharimu maisha yenu!” Daniel alisema wakati akitoka nje, Martin Hisia naye alifata kwa nyuma.
Walipofika sebuleni walimkuta Hannan akiwa amekaa sofani, ameipakata tarakilishi yake akiwasubiri kwa hamu. Daniel Mwaseba alichukua nafasi ya kumueleza Hannan kila kitu kilichotokea katika chumba cha mateso. Mara kadhaa Hannan alikuwa anaitikia kwa kutikisa kichwa wakati Daniel akimsimulia na kuuliza sehemu asipoelewa vizuri.
“Hayo ndio yetu Hannan kutoka katika chumba cha mateso. Kikubwa tumeondoka na jina moja tu, Mrombo, eeeh tuambie wewe umepata nini juu ya zile kazi mbili tulizokupa za kufatilia namba ya Msamaria mwema na yule mtu aliyenipigia kunipa vitisho tukiwa hapa?” Daniel alisema huku akimwangalia Hannan.
Hannan alikohoa kidogo kuitengeneza sauti yake sawa, macho yake yakaelekea kwenye tarakilishi yake huku akiongea, “Msamaria mwema, imenifanya nitumie program maalum kuweza kuingia katika kanzidata ya mawasiliano ya jeshi la Polisi, sio kazi ndogo hata kidogo, sio tu yahitaji uwe na program maalum ambayo sio rahisi kwa mtu wa kawaida kuwa nayo lakini pia inabidi uwe mtaalam wa hadhi ya juu sana kuweza kucheza na kompyuta. Nimeyasikiliza mawasiliano yote ya Polisi ya leo asubuhi katika kanzidata yao, hakuna simu iliyopigwa kutoka kwa mtu anayejiita Msamaria mwema, na hiyo inamaanisha kwamba yote aliyoyasema Babu Ogutu ni kweli, Inspekta Hayman alikuwa Polisi feki, yeye alikuwa mwenyekiti feki, na wenzie wote hawakuwa halisi kwa maana ya neno halisi linavyomaanisha. Baada ya kutopata lolote kutoka katika kanzidata ya mawasiliano ya jeshi la Polisi nikahamia kwa huyu mtu aliyekupigia simu ya vitisho hivi punde. Baada ya kuichunguza namba ile, nimegundua kwamba namba imesajiliwa kwa jina la Witness Msombe. Nilianza kumchunguza huyo Witness Msombe ni nani, majibu niliyoyapata ni kwamba Witness Msombe ni mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Dar es salaam, Witness yupo mwaka wa pili akisomea hiyo shahada ya sheria. Hayo ndio niliyoyagundua juu ya zile namba mbili ulizonipa” Hannan alisema huku akiinyanyua sura yake iliyokuwa imeiinamia tarakilishi yake iliyokuwa juu ya mapaja yake.
“Safi sana Hannan, umefanya kazi kubwa sana, sasa tumepapata pa kuanzia ili kujua hawa watu wana mpango ndani ya nchi hii. Kwanza lazima tukamchukue Mrombo nyumbani kwake na kumleta hapa, ni yeye ndiye atakayetuambia anashirikiana na kina nani? Na wana mpango gani? Pili lazima tuende chuo kikuu cha Dar es salaam kuonana na huyo Witness Msombe. Lazima atuambie iweje namba yake itumike kunitishia, na bila shaka yeye atakuwa anajua mahali alipowekwa Dokta Tawakal” Daniel Mwaseba alisema kwa kirefu.
“Upo sahihi Daniel, lazima tuyafanye hayo uliyosema, lakini tutaweza kweli peke yetu kufanya mambo yote hayo, ninashauri tuongeze nguvukazi ya kutusaidia ili tufanikishe uchunguzi wetu” Martin alitoa ushauri wake.
“Upo sahihi Martin, tunahitaji nguvukazi ili kukamilisha uchunguzi wetu kwa wakati, pengine kabla ya mimi na Hannan hatujamaliza likizo zetu. Lakini niseme tu uchunguzi huu utafanywa na watu watano tuliomo humu ndani. Nitamwambia Chifu juu ya mpango wa watu hawa tukikamilisha au itakapobidi. Safari hii nataka niwaoneshe mimi ni nani hawa wapuuzi walionikatisha safari yangu ya kwenda Dubai kula starehe” Daniel alisema akimwangalia Martin Hisia.
“Daniel, unasemaje tupo watano wakati tupo watatu tu, mimi, wewe na Hannan, hao watu wawili wengine wapo wapi?” Martin aliuliza huku akimwangalia Daniel kwa mshangao.
“Sijakosea Martin, tupo watano humu ndani, Tutawatumia Babu Ogutu na Okello katika uchunguzi wetu, wale ndio watakamilisha idadi ya hao watu watano” Daniel alisema kwa kujiamini.
“Khhaaaa Daniel, umeshawaamini wale majambazi?” Martin na Hannan walijikuta wakiuliza kwa pamoja.
“Ninawaamini, ni shida tu ndizo zilizowafanya wachague upande ule haramu, tutawapa nafasi ya kubadilika na kusahihisha makosa waliyoyafanya hapa duniani. Babu Ogutu jinsi anavyoongea anaonesha kabisa hafurahii alichokuwa anakifanya, bila shaka ugumu wa maisha umemfanya aichague njia ile. Nitaenda kuongea nao, na bila shaka watakubali kuungana na sisi katika uchunguzi wetu” Daniel alisema kwa kirefu.
“Daniel, wewe ni kiongozi wangu katika operesheni nyingi sana, operesheni zilizoisha kwa mafanikio makubwa na kuiokoa nchi yetu katika hatari kutokana na uongozi wako madhubuti, lakini kwa mara ya kwanza leo napingana na wewe, sikubaliani na mpango wako wa kuwatumia wahalifu katika uchunguzi wa suala hili. Wale ni nyoka wenye sumu kali na sisi ni binadamu wa kawaida, Daniel, hakujawahi kutokea urafiki wa dhati kati ya nyoka wenye sumu kali na binadamu wa kawaida hata siku moja” Martin alionesha msimamo wake kwa kukataa mpango wa Daniel Mwaseba.
“Martin najua hisia zako zinapokupeleka, lakini naomba ukubali mpango wangu huu, hata hao wakina David unaoweza kushauri tuwatumie walikuwa katika upande sawa na kina Babu Ogutu. Hata wewe mwenyewe ulikuwa upande ule kabla hujahamia upande huu. Ni imani yangu kwako ndio iliyotuleta pamoja leo hii. Naomba unikubalie tufanye kazi na wale watu, kuna faida kubwa sana tukiwaonesha kuwa tumewaamini” Daniel Mwaseba naye alisimamia msimamo wake.
“Moja…..” Hannan alianza kuhesabu huku akinyoosha kiganja chake kwa mbele.
“Mbili…..” Martin akadakia, akanyoosha kiganja chake na kugusanisha juu ya kiganja cha Hannan.
“Tatu……” Daniel Mwaseba alimalizia huku naye akikigusisha kiganja chake juu ya mikono ya Hannan na Martin.
“Mojaaaa, mbiliiiiii, tatuuuuuu…………” Wote watatu, walihesabu kwa pamoja kwa sauti kubwa huku viganja vyao vikiwa vimeshikana.
“Tunaishi pamoja…”Daniel Mwaseba alisema….
“…na tutakufa pamoja!” Hannan Halfani na Martin Hisia waliitikia.
Walikuwa wameelewana, na walikuwa tayari kuanza kazi.
*****
Je nini kitatokea?
LAKO JICHO.
