Riwaya ya Kijasusi: Mlio wa Risasi Harusini

1647345626190.png



Kitabu Tsh 10,000/=
Softcopy Tsh 3,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel

Mzigo upo wa kutosha.
 
MLIO WA RISASI HARUSINI ( Episode 05)
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

>>>>>>>>>>>>>>> Episode 05 <<<<<<<<<<<<<<<

ILIPOISHIA

Akashusha pumzi nzito mithili ya kobe mzee. Ni kama alikuwa amebeba mzigo mzito. Punde alisikia maji yakimwagwa kwenye pipa lililokuwa sebuleni alipokuwa yule mwanamke. Hapo akajua kuwa yule Mama alikuwa ametoka kuchota maji. Akahisi kichwa kikimzunguka. Macho yakaingiwa na giza zito. Hatimaye alipoteza fahamu.

ENDELEA
Ni kutokana na kuvuja kwa damu nyingi ndiko kuliko sababisha apoteze fahamu. Kwa kawaida mtu hupoteza fahamu ikiwa ataishiwa na damu, au kama ataishiwa na maji mwilini. Au kupata maumivu makali au mshtuko. Robert alizinduka baada ya masaa matano kupita yapata mida ya saa tisa alasiri. Palikuwa kimya katika chumba kile. Akageuza macho yake upande wa uvungu alipoingilia. Akashtuka! Aliona miguu ya mtu iliyokanyaga sakafun; hii ilimaanisha kitandani kulikuwa kuna mtu amekaa. Ilikuwa ni miguu ya kike kutokana na kucha zilizokuwa zimepakwa rangi nyekundu. “ huenda ni yule Mama niliyekuwa namsikia nje akiwajibu wale watu wabaya waliokuwa wakimkimbiza”Akawaza. Akataka atoke lakini akili yake ilimuonya kuwa asifanye jambo la kijinga kama lile. Siku zote subira yavuta heri, hivyo ndivyo alivyoamini. Basi akaamua kutulia mulemule uvunguni. Njaa ilianza kumuuma. Akatamani atoke amuombe yule Mama chakula. Lakini angethubutuje. Hilo kamwe asingejaribu. Mbu wa uvunguni waliendelea kusherehekea mwili wake kwa kumng'ata hali iliyofanya ahisi maumivu makali. Alijitahidi kuwafukuza lakini mbu wale walikuwa wakimzomea kwa sauti zao zilizokuwa zikivuma kama kivumvuu! Yule Mama aliamka kitandani akatembea kidogo mpaka lilipokabati. Yule Mama alikuwa anavaa nguo. Alimaliza kuvaa kisha akavaa viatu vyake. Yote haya Robert aliyaona akiwa chini ya uvungu. Yule Mama bado hakujua kuwa mule chumbani kwake kulikuwa na mtu aliyekuwa akimtazama kuanzia alipokuwa akivaa mpaka anamaliza. Yule Mama alimaliza kujiremba usoni huku kichwani kukiwa na lemba. Akatoka akafunga mlango wa chumba kwa nje. Kisha Robert akamsikia yule Mama akirudishia mapazia ya sebuleni na hatimaye akamsikia akitoka nje na kufunga mlango wa sebuleni. Kimya ndicho kikatawala mule ndani. Robert akaona ule ndio muda wa yeye kutoka uvunguni. Alitoka akitambaa kama nyoka. Akakimbilia ndoo ya maji iliyokuwa mule chumbani. Akachota maji na kikombe kilichokuwa juu ya mfuniko wa ile ndoo. Kidogo alisikia ahueni. Nguvu zikamrudia kidogo tofauti na awali. Akaangaza kukikagua kile chumba. Aligundua kilikuwa ni chumba cha mtu mwenye kipato cha chini. Kitanda kilikuwa ni kikubwa cha tano kwa sita kilichokuwa kimetandikwa kwa umaridadi. Juu ilifungwa chandarua nyeupe. Kulikuwa pia na kiti cha mbao cha kuegemea. Pia kulikuwa na kabati kuukuu la nguo ambalo juu yake kulikuwa na mkoba mweusi wa kisasa na boksi kubwa kiasi. Akasogea lilipo lile kabati kisha akalishusha lile boksi. Alikuta limefungwa. Akalifungua Ambapo alikuta midoli mingi ndani yake. “ Hii midoli niya nini? Kwa nini ipo humu ndani? Huyu Mama anakazi gani nayo? Je ni mfanyabiashara wa midoli? Kama ni mfanyabiashara wa midoli mbona iwepo pale na siyo dukani au sokoni?” Alijiuliza maswali mengi lakini hakuwa na majibu. Akarudishia lile boksi kama alivyolikuta kisha akalirudisha juu ya kabati vilevile alivyolikuta. Akachukua ule mkoba mweusi wa kisasa uliokuwa pale juu ya kabati. Akafungua zipu ambapo ndani alikuta passport mbili. Passport moja iliandikwa jina la Angelika Efraimu. Wakati passport ya pili ikiwa na jina la Husna Koloa. Kitendo cha Robert kukuta passport mbili mule ndani kiliibua hisia mpya kwenye akili yake. Awali aliona wakazi wa chumba kile kama watu masikini lakini sasa hisia zake zikabadilika. Robert aliamini kuwa mtu masikini siyo rahisi kumiliki passport ya kusafiria nchi za nje.

Akaona funguo mbili na bahasha. Akaifungua ile bahasha lakini hakuona la maana. Akarudishia vizuri ule mkoba. Lakini hakurudisha funguo alizoziona. Alienda mlangoni kuzijaribu kuona kama zitafungua ule mlango. Funguo ya kwanza ilikataa lakini funguo ya pili ikakubali. Akatokea upande wa sebuleni ambapo ndipo alipopitia alipokuwa akikimbizwa na wale watu waliotaka kumuua asubuhi. Akaona sufuria ikiwa imefunikwa akaenda kuifunua. Akakuta ndizi zilizorostiwa na nyama. Akachukua sahani akachota ndizi zikajaa. Kisha akakaa kwenye moja ya makochi yaliyokuwa pale sebuleni. Kwa kweli alifurahia mlo ule. Kilikuwa chakula kilichopikwa kikapikika. Kilichorostiwa kikarostika. Akala kwa hamu na nidhamu. Kwa udenda tena kwa kupenda. Akatosheka si haba. Alikuwa mstaarabu; aliosha kile chombo kisha akakirudisha mahali pake. Akafunika ile sufuria kama alivyoikuta. Tayari ilikuwa imetimia saa kumi na mbili za jioni. Punde akasikia watu wakigusa kitasa cha mlango wa sebule. Akakimbia haraka chumbani akafunga na funguo ule mlango wa chumbani. Wale watu waliingia sebuleni. Akawasikia wakiongea huku wanacheka. Alisikia sauti ya yule Mama akiongea. Alikuwa akiwakaribisha chakula. Yule Mama alienda kupakua chakula. Alishangaa kuona chakula kimepungua kwa kiwango kile. Kama ni mlango mbona alifunga iweje chakula kipungue kwa kiwango kile. Nani kala chakula chake. Yule Mama alijiuliza. Hakutaka kuamini kuwa ati alipika kidogo wakati alipika kingi na akakiacha kingi. Akawapakulia kidogo kidogo wakawa wanakula huku wanapiga stori za kawaida. Robert alijitahidi kusikiliza hakuambulia jambo lolote la hatari. Walimaliza kula. Punde ule mlango wa chumbani ukafunguliwa. Kisha aliyeingia akawasha taa ya chumbani ambapo giza lilikimbia na kufanya chumba kiwe na nuru. Alikuwa ni yule Mama. Akaenda lilipo lile boksi akalishusha chini. Robert alikuwa kajichimbia uvunguni. Baadaye aliwaita wale watu waliokuwa kule sebuleni. Robert akiwa uvunguni aliona mabuti makubwa ya watu wawili wakiingia mule chumbani. Yalikuwa ni mabuti makubwa meusi kama ya wanajeshi.. Aliishikilia pumzi yake ili isijetoka kwa nguvu wale watu wakamshtukia mule uvunguni. Yule Mama akalifungua lile boksi. Akatoa mdoli mmoja baada ya mwingine. Wale watu kila mmoja alishika mdoli wake wakiwa wamechuchumaa. Robert akajisogeza ndani zaidi ya uvungu ili asijekuonekana. Akaliacha jicho lake moja likining'inia ili awaone wale watu walichokuwa wanakifanya. Akaona sura ya moja ya wale watu. Aliogopa sana. Alimuona mtu mwenye sura ya kutisha inayokaribiana na ushenzi. Yule mtu alikuwa amefuga ndevu chini ya pua yake kama askari wa kikoloni. Ndevu hizo zilikuwa ishara ya ubedui wake. Mtu wa pili hakuona uso wake. Wale watu na yule Mama walikuwa kimya bila kuongea. Akaona yule mtu akichana ule mdoli aliokuwa ameushika. Aliuchana tumboni ambapo unga ulimwagika kutoka katika tumbo la ule mdoli. Kisha yule mtu akapeleka kile kisu puani mwae, akanusa. “OOH! Hawa watu ni wauza sembe.”Akawaza. Alihisi hatari inaweza kumkuta endapo watu wale wangemuona. Yule mtu aligeuka kama anaangalia uvunguni hali iliyomfanya Robert ajisogeze kwa haraka uvunguni na kufikia ukuta ambapo alipogusa ukuta umeme ukazima. Robert alishtuka. Hata wale watu walishangaa kuona taa imezima. Chumba kilijawa na giza. Yule Mama alichungulia dirishani akaona umeme sehemu zingine upo. Hata taa ya sebuleni pia ilikuwa ikiwaka.

"Itakuwa swichi ya chini ya kitanda imejifyatua" yule Mama aliongea huku akienda kilipokuwa kitanda. Robert akajua kuwa yeye ndiye aliyezima switchi iliyokuwa ukutani alipokuwa akijisogeza ili asiyonekane. Yule Mama akamuomba mmoja wa wale watu wamsaidie kusogeza kitanda ili apate mahali pakupitisha mkono wake iliposwichi ili awashe taa. Ama kweli siku ya kufa nyani mti yote inateleza. Bora ingekuwa nyani sasa. Yeye alijiona kama tumbili tuu. Akili yake ilimzunguka na kumfunika kama shuka. Akapeleka haraka mkono ukutani kabla kitanda hakijasogezwa na wale watu. Kisha akabonyeza ile swichi. Taa!. Umeme ukawaka. Wale watu walishangaa taa kuwaka. Walibaki wamesimama wakiwa wanashangaa jambo lile. Huku Robert Wasiwasi ulitanda moyoni mwake kama ukungu kwa mafungu. Wale watu wawili na yule Mama walirudi kwenye ile midoli iliyokuwa na madawa ya kulevya. Walipomaliza kuihakikisha. Yule mtu mmoja ambaye Robert hakuona sura yake alitoa begi alilokuwa amelivaa mgongoni na kuanza kuiweka ile midoli. Robert alishangaa kumuona yule Mama akiwasha sigara ngumu na kuiweka mdomoni. Akasikia harufu kali ya bangi kutoka katika moshi wa ile sigara. Moyoni akajisema, “Mama mzuri kama huyu kumbe mla ndumu bhana”. Yule Mama alivuta mpaka ikafika katikati kisha akampa yule mtu mwenye sura ya kikatili iliyohifadhi ushenzi. Looh! Yule mtu kiboko. Alikuwa akivuta mpaka mashavu yanaingia ndani na kuunda mashimo kwenye mashavu yake. Kisha anaondoa sigara mdomoni na kufutua mashavu yake. Alafu Alitoa moshi mwingi puani kisha akapanua mdomo ambapo moshi ulitoka mafungu mafungu kama mawingu.

Ilikuwa tayari imetimia majira ya saa nne usiku. Wale watu walitoka kwenye ile nyumba ya yule Mama. Hiyo ilikuwa nafasi ya pekee na kamwe isitokee kwa Robert kuweza kuepa katika nyumba ile yenye watu hatari. Akajiburuta mule uvunguni akatoka. Akafika sebuleni akakutana na panya waliokuwa wakikimbia kimbia baada ya yeye kutokea. Hakutaka kuchelewa asijekukutwa mule ndani. Akaenda kwenye mlango wa sebule akakitekenya kitasa cha mlango! Mlango ulikuwa haujafungwa zaidi ya kurudishiwa. Hii ilimuambia kuwa yule Mama asingekuwa ameenda mbali na kitambo kidogo angerejea. Alifanikiwa kutoka; Akapokelewa na giza jepesi na ubaridi uliompuliza. Kwake ilikuwa kama muujiza kuiona tena dunia. Akatembea huku akilitazama anga lililokuwa limenakshiwa kwa makundi ya nyota. Alikumbuka alivyokuwa shule alivyofundishwa na mwalimu wake wa jiographia. Mwalimu wake alimuambia kuwa; nyota ni magimba makubwa yaliyopo angani yanayotoa nuru. Kutokana na umbali huonekana kama nukta tuu imulikayo. Nyota zipo zaidi ya mabilioni na kila moja ipo mahali pake. Mafungu ya nyota ambayo huitwa fungunyota ambayo huwa kuanzia milioni mpaka bilioni huitwa galaxy. Jua ni moja ya nyota zilizopo katika galaxy yaani fungunyota. Galaxy yetu inafahamika kama milk way ambapo mfumo wetu wa jua ndio ulipo. Dunia ni moja ya sayari katika mfumo wa jua. Zipo sayari nyingine kama zebaki, yuranus, venus na zuhura miongoni mwa nyingine. Robert alitamani ahamie zilipo sayari nyingine. Dunia ilikuwa tayari imemchosha kwa kiwango kikubwa. Ni hiihii dunia iliyomnyang'anya Ismaiya wake. Ni hiihii dunia iliyomuua Ramla mwanamke asiye na hatia, dunia ambayo ilimfanya alazwe kwa zaidi ya miezi sita na sasa amegeuka mkimbizi apigaye mbizi kwenye ardhi. Iweje aipende dunia. Kwa kweli hata ingekuwa ni wewe usingeipenda hii dunia. Alikuwa akihisi maumivu makali kwenye kichwa chake. Alichukua bodaboda na kuomba apelekwe makumbusho mahali alipokuwa akiishi.



*************************************************​


Adele alipelekwa hospitali akiwa yupo hoi kutokana na kipigo cha mbwa koko alichopewa na Robert . Hakuamini kama Robert angempiga kipigo kikali kiasi kile. “Yaani Robert ndio wakunipiga mimi kama mwizi. Haiwezekani. Nasema haiwezekani'” Adele alikuwa akifikiri akiwa kalala juu ya kitanda akiwa na bandeji juu ya jicho la kushoto. Chuki na husuda ziliujaza moyo wake.

"Ama zangu ama zake. Nasema yule mshenzi atanijua mimi ndiye Adele" bado Adele alikuwa akichochewa na roho yake mbaya kama mchawi. Roho ya kisasi ya kumwaga damu ilimvaa kama koti la muuza bucha. Sasa alichohitaji ni panga kwa ajili ya kumkatakata Robert kama nyama. Punde aliingia daktari akiwa kavaa koti jeupe. Akamsalimia Adele kisha akamuambia apanue mdomo. Adele alipanua mdomo kisha daktari akaweka ndani ya mdomo kifaa kiitwacho oral thermometer akamuambia afunge mdomo wake. Oral thermometer ni kifaa cha kisasa kinachotumika kupima joto la mwili wa binadamu ambapo huwekwa mdomoni kwenye ulimi. Baada ya muda aliitoa ile oral themometer mdomoni mwa Adele. Kisha akachukua kifaa kilichozunguka shingo yake kiitwacho stethoscope ambacho kazi yake ni kusikikiliza milio na mitetemo ndani ya mwili wa mwanadamu kama vile mapafu, na moyo. Daktari akaivaa ile stethoscope masikioni kisha akaanza kupima mapigo ya moyo wa Adele. Kisha akapima na maeneo ya mapafu. Alipomaliza alimuomba radhi Adele aliyekuwa ametulia tuli.
"Unaendelea vizuri Adele. Nafikiri kama hali itaendelea hivi. Jioni utaruhusiwa" daktari alimuambia Adele huku akimtazama kwa macho ya kidaktari yaliyojawa faraja na pole. Adele akaruhusiwa jioni akaingia ndani ya gari yake ambayo ndio ileile waliyoenda nayo kule makaburini alipokuwa na Robert. Tofauti na ilivyotarajiwa. Badala Adele aende nyumbani kwake akapumzike lakini yeye hakufanya hivyo. Moja kwa moja alienda kituo cha Polisi. Alipofika aliongea na mkuu wa kituo cha Polisi. Ni kama walikuwa wanafahamiana. Mkuu wa Polisi baada ya kuongea na Adele aliwaagiza Polisi waanze msako wa kumtafuta Robert. Adele akatoa picha mbili zilizoonyesha taswira ya Robert. Wale Polisi walipeana wakaanza kuzitazama zile picha kutaka kumjua huyo Robert anafananaje. Sasa kila mmoja alikuwa ameshamjua Robert anafananaje.

Ilikuwa mida ya saa kumi na mbili kuelekea saa moja usiku zoezi la kumtafuta Robert lilipoanza. Walianzia mitaa ya kinondoni yalipozunguka yale makaburi. Wengine waliingia katika kila nyumba ya kulala wageni kuona kama wangempata Robert . Lakini Robert hakuonekana. Walimtafuta kwenye kumbi za starehe lakini Robert hakuonekana. Waliingia mpaka ubungo kwenye makampuni ya mabasi kuona kama Robert alikata tiketi akaondoka. Walitumia picha yake kumuulizia Robert kwa watu lakini watu wengi hawakuwa wanamfahamu wala hawajawahi kumuona mtu kama huyo kwenye hii dunia. Ulikuwa msako mkali mithili ya anayetafutwa gaidi aliyetishia kupindua serikali. Lakini kumbe ni Robert kijana wa watu asiye na hatia. Kijana aliyedhulumiwa mchumba wake na sasa anakimbiza roho yake isije naswa na shetani Adele. Tayari ilikuwa imetimia saa tatu usiku mambo yakiwa bilabila. Robert hakuonekana. Polisi wakakata tamaa ya kumpata Robert. Kisha wakaamua kurejea kituoni; ghafla wakiwa wanarejea wakaona bodaboda mbele yao ikija kwa kasi. Nyuma ya ile bodaboda alikuwepo amepakizwa mtu ambaye taa ya gari ilipommulika walimfananisha na Robert. Walipishana kwa kasi na ile bodaboda. Wakamuona yule mtu kwa nyuma akiwa anajeraha kichwani huku shati alilokuwa amelivaa likiwa limelowa damu. Wakageuza gari haraka wakaanza kuifukuzia ile bodaboda.

Punde wakaifikia ile bodaboda na kuiwaisha mwanga full light. Jambo hili lilimshtua sana Robert. Akageuka nyuma akaliona gari la Polisi likiwa karibu yao. Mapigo ya moyo yalimkimbia. Hisia za hofu zikamkumbatia. Akawasikia wale Polisi wakimshinikiza dereva bodaboda asimame. Kizaazaa kikaanza. Bodaboda akakaidi amri yao kwa hofu. Uoga wake ulitokana na kutokuwa na bima ya ile pikipiki, hakuwa amelipia sumatra. Kubwa zaidi hakuwa na kadi ya ile pikipiki kutokana na kuwa aliinunua kimagendo. Alijua kuwa kama angesimama basi pikipiki yake ingechukuliwa na yeye angefunguliwa mashtaka ya kumiliki chombo cha moto kwa njia ya udanganyifu. Hakuwa tayari kuona jambo hilo linatokea. Kwa upande wa Robert yeye hakutaka kuingia muda ule mikononi mwa Polisi. Hakuwaamini kabisa Polisi kutokana na tukio alilolifanya Ismaiya siku ile ya harusi ambapo aliwapanga Polisi bandia. Hivyo alihisi huenda wale siyo Polisi bali ni watu wa Adele waliotumwa wamkamate. Waliongeza kasi kuliko kawaida. Wakakimbia mpaka wakaupita upepo. Walipita eneo la makumbusho na kukatisha lilipojengo la sayansi na chuo cha ustawi wa jamii. Polisi nao hawakuwa lelemama. Ilikuwa kama mbio za paka na panya. wakikata Polisi nao walikata. Walipopinda Polisi nao walipinda bila kuwaachia nafasi. Wakafika sinza afrikana kwenye mataa; hawakuwa na bahati. Gari aina ya Nissan patrol nyeupe iliyokuwa inatokea barabara ya Mwenge TRA iliwavaa na kuwarusha huko. Ile Nissan haikusimame iliendelea kuchanja upepo kwa kasi na kuacha ajali mbaya eneo lile.

*************************************************​

Fahamu zilimrejea Sajenti Warioba. Macho hayakuona lolote kutokana na giza la kile chumba. Kulikuwa na giza nene hii ilimuambia kuwa ule ulikuwa ni usiku. Chumba kile hakikuwa na dirisha hali iliyofanya kiwe na joto kali na hewa nzito. Jambo hilo lilimfanya Sajenti Warioba ashindwe kupumua vizuri. Mwili wake uliojawa na makovu ulikuwa unatoka jasho kutokana na joto la mule ndani. Uso wake haukuwa na siafu. “ Wale siafu wanaroho mbaya sana, sijui yule mshenzi kawatolea wapi, khaa!” Akawaza. Punde akasikia kitasa cha mlango kikicheza. Kisha mlango ukafunguliwa lakini kutokana na giza hakuona mtu yeyote akiingia. Alisikia sauti ya hatua za mtu anayetembea mule chumbani lakini hakuwa akimuona. Giza lilikuwa zito mno kiasi kwamba hata mtu angesimama mita moja asingeweza kumuona.

Hii ilimpa hofu. Akahisi ni yule mtu mweusi kama lami. Mtu katili asiye na huruma amerudi kuendelea kumpa mateso. Mapigo yake yalipiga sana. Alijua muda wa kupokea kipigo ulikuwa umefika. Wakati huu alijua kuwa hakitakuwa kipigo tena bali ikiwezekana kifo. Punde akasikia mtu akimshika mikono yake iliyokuwa imefungwa nyuma ya nguzo aliyokuwa ameigemea kwa mgongo.

"Usinipige tafadhali! Nakusihi usinipige" Sajenti Warioba aliongea kwa sauti akimuomba yule mtu asiyemuona. Akashangaa kuona kamba iliyofunga mikono yake zikifunguliwa. Kisha yule mtu asiyemuona akazifungua kamba za miguu yake. Hofu ya Sajenti ikaongezeka mara dufu. Akili yake ikamuambia kuwa anaenda kubadilishiwa adhabu na huenda ikawa kali zaidi. Tayari alikuwa amefunguliwa mikono na miguu. Akahisi mikono na miguu yake kuwa na ganzi kutokana na kamba alizokuwa amefungwa kukazwa sana. Akasimama akisubiri maelekezo ya mtu yule. Alitamani akimbie lakini giza lilimzuia. Kimya kitambo kikapita bila kumsikia yule mtu aliyemfungua akiongea. Akaamua kutembea polepole akipapasa papasa asije akajigonga.

"shika hii" akashtuka na kusimama aliposikia sauti ikiongea huku akikabidhiwa nguo. Ilikuwa ni sauti ambayo moja kwa moja aliitambua kama sauti ya Joseph.

Joseph ndiye aliyekuja kumfungua mikono na miguu kisha akamletea na nguo ambapo Sajenti alipoikunjua aligundua ilikuwa ni kanzu. Ingawaje hakujua ni kanzu ya rangi gani kutokana na giza. Unajua muda wote Sajenti Warioba aliokuwa akipigwa na yule mtu mweusi alikuwa yupo uchi wa mnyama. Hata Joseph na yule Mama walivyokuja walimkuta Sajenti Warioba akiwa uchi. Ndio maana Joseph alikuja na kanzu itakayomsitiri.

"Joseph! kumbe ni wewe" Sajenti akasema huku akiivaa ile kanzu.

"Tuondoke kabla hawajashtuka. Nimemuacha yule Mama akiwa amelala" Joseph akasema huku akimshika mkono akimvuta Sajenti waondoke. Walitoka kwenye kile chumba na kuingia katika korido ambapo kidogo kulikuwa na mwanga hafifu uliomfanya Sajenti Warioba aone. Wakatembea kwa kunyata kwa haraka bila ya kusikiwa. lilikuwa ni jumba kubwa lenye vyumba sita vikubwa sana. Waliendelea kutembea kwa tahadhari Joseph akiwa ndiye kiongozi. Sajenti Warioba pamoja na cheo chake lakini kwa muda ule alimuona Joseph kama boss wake licha ya umri wake kuwa mdogo. Alijifunza kuwa katika maisha siyo kila wakati unaweza kuwa kiongozi. Kuna wakati unaweza hata ongozwa na mtoto mdogo. Kama hiyo haitoshi kuna wakati hata mnyama anaweza geuka msaada na kukuongoza. Hii ilimfunza kuwa kila mtu anapaswa kuheshimiwa bila kujali umri au hadhi yake. Punde wakasikia mtu akija kwa kuburuta miguu.

"BLM huyo anakuja" Joseph aliongea huku akimvuta Sajenti kwenye ua la bandia lililokuwa pembeni. Sajenti Warioba akataka kumuona huyo BLM ndio nani. Pia alijiuliza kuwa Joseph alijuaje kama anayekuja ni BLM. Punde jimama likajitokeza likiwa limefunga kanga yake kifuani. Lilikuwa likitembea kivivu kutokana na uzito wa makalio yake.

Yule Mama alikuwa anakaribia lile ua ambalo wakina Sajenti walikuwa wamejificha. Waliogopa sana. Walijua kama wataonekana ule ndio ungekuwa mwisho wao. Yule Mama alikuwa ameshafika usawa wa lile ua. Akasimama karibu kabisa na mahali alipojificha Sajenti.



Sajenti alihisi moyo wake unataka kupasua kifua baada ya kumuona vizuri Yule Mama, alikuwa ni Yule Mama wa Makamo aliyemuona ile siku akiwa anamlazimisha Joseph kufanya mapenzi. Ile kanga ya yule Mama ilikuwa ikipepeswa na upepo na kuupiga piga uso wa Sajenti.



Yule Mama alibonyeza simu yake kisha akaweka sikioni. Ikaita kwa muda mrefu lakini haikupokelewa. Huenda aliyekuwa akipigiwa alikuwa amelala. Jambo lilimfanya Sajenti ahisi kuwa huenda yule Mama amewaona na alikuwa anampigia yule mtu mweusi asiye na huruma aje awakamate. Sajenti alifikiri kidogo. Akataka kujitokeza lakini akili yake ilimuonya. Akili yake ilimuambia kuwa anahitaji utulivu na subira katika jambo analotaka kulifanya. Pia aliwaza kama atajitokeza na kumteka yule Mama alafu akatokea yule mtu mweusi ambaye itabidi wapambane inaweza mletea madhara Joseph ambaye ni mtoto mdogo. Yule Mama akapita kuelekea kwenye kile chumba walichotoka Sajenti.

"Humu ndani mpo watu wangapi?"Sajenti akamuuliza Joseph.

"Inategemea. Lakini leo tupo watatu pamoja na wewe ni wanne" Joseph akajibu akiwa anataka kuinuka lakini Sajenti alimzuia.

"Subiri kidogo. Kwa hiyo yupo huyu Mama, wewe na yule mtu mweusi anayetisha?"

"Hapana. Yule mtu aliondoka jana. Yule hakai humu. Anakujaga tuu kuchukua mzigo"
Joseph alijibu akiongea lafudhi ya Arusha.

"Mzigo gani?" Sajenti Warioba aliuliza huku akivutiwa na habari apewazo na Joseph.

"Viungo vya binadamu"

"Viungo vya binadamu?"
Sajenti Warioba akajikuta akitoa sauti kwa mshangao.

"Unashangaa nini? Hata watoto wachanga huwachukua"

"Hao watoto wanawatoa wapi? Na hivyo viungo vya binadamu wanapata wapi?"

"Hee! Huu ni mtandao mkubwa jombaa! Mmiliki wa hili jengo ni daktari mkubwa katika nchi hii"
Joseph akaongea kama mtu anayejua mambo mengi katika jumba lile. Alikuwa ni mtoto mdogo lakini alikuwa anajua maovu mengi yanayofanywa na watu wale wabaya.
"Wewe umejuaje mambo yote haya?" Sajenti akauliza swali lililoonekana la kipuuzi mbele ya Joseph.

"Tuondoke kwanza haya yote nitakuhadithia. Kuendelea kukaa humu ni hatari" Joseph alikasema huku akinyanyuka.

Walitembea kwa tahadhari wakafika sebuleni. Sajenti aliikagua ile sebule iliyosheheni vitu vya thamani. Ukutani aliona picha kubwa iliyowaonyesha watu wa tatu. Mmoja alikuwa ni yule Mama aliyemuona kwa mara ya kwanza akiwa anataka kulala na Joseph. Yule Mama aliyewapita pale walipokuwa wamejificha kwenye ua la bandia. Mtu wa pili alikuwa ni mwanaume mmoja wa makamu mwenye umri wa kuanzia miaka hamsini hivi. Mtu wa tatu alikuwa mtoto wa kike mwenye umri kati ya miaka kumi na nane hivi. Huyu binti alikuwa mbele kidogo ya wazazi wake ambao ni huyo Mama na mwanaume wa makamu mwenye nywele zenye mvi. Joseph alikuwa akifungua mlango wa sebuleni wakati Sajenti akiendelea kukagua ile sebule. Sajenti akaiona flash juu ya sofa. Akili yake ikamtuma aichukue. Alipoichukua tuu alishtuka kusikia milio ya alarm ikilia nyumba nzima. Ilikuwa milio iliyokuwa ikiashiria hatari na kutoa taarifa kuwa kuna hatari. Tayari Joseph alikuwa amefungua mlango na wote wakatoka kwa upesi. Jumba zima lilikuwa likilia ile sauti ya alamu. Wakakimbilia eneo yalipokuwepo magari na kuingia ndani ya gari aina ya land rover. Joseph aliwahi kufungua geti wakati Sajenti akihangaika kuwasha gari. Jumba bado lilikuwa likilia. Na punde milio ya risasi kutoka katika jumba lile ilisikika. Kutokana na gari kutokuwa na funguo Sajenti Warioba alitumia ujuzi wa ziada. Muda huo geti lilikuwa lipo wazi Joseph alikuwa ametoka nje akikimbia.



Risasi ziliendelea kulipiga gari alilopanda Sajenti Warioba. Sajenti akachungulia kwenye dirisha la gari kuona risasi zilikuwa zinatokea wapi. Alimuona mtu kwenye ghorofa ya pili ya lile jumba akimrushia risasi. Gari lilikuwa limeshawaka. Sajenti akaingiza gia na kulitoa gari kwa kasi. Akatoka getini wakati yule Mama mwenye makalio akiwa ametoka nje ya sebule akimsindikiza na risasi lakini hakuambulia kitu. Yule mtu juu ya ghorofa aliendelea kurusha risasi akiwa na bunduki aina ya smg. Katika hali ya kusikitisha Sajenti alishushudia Joseph akilambwa risasi ya mgongo akiwa anakimbia kumfuta kwenye dari huku yeye akimmulika na taa za gari. Joseph akadondoka chini. Sajenti akashika breki akashuka kwa haraka. Alimkuta Joseph akiwa anapumua kwa tabu huku damu zikitoka puani na mdomoni. Joseph alikuwa na hali mbaya sana.



Akamlaza Joseph mapajani mwake.

"Joseph usife tafadhali" Akambembeleza Joseph aliyekuwa akimtazama kwa macho ya buriani, wakati huo taa ya gari ikiwamulika. Joseph aliingiza mkono mfukuni akatoa kikaratasi akamkabidhi Sajenti bila kusema lolote kisha macho yake yakafumba.

"hapana! Joseph! Joseph! Joseph amka!" Joseph ndio alikuwa ameaga duniani.

Kifo cha Joseph kilimuumiza sana Sajenti Warioba. Aliumia ungedhani ni mtu aliyemfahamu muda mrefu lakini kumbe ni mtu aliyefahamiana kwa muda mchache usiyozidi siku tatu. Kilichomuumiza zaidi ni kitendo cha yeye kushindwa kuokoa maisha yake, kijana ambaye aliweza kumuokoa kutoka katika jumba lile la watu wabaya. Alijilaumu sana. Joseph kamuokoa lakini yeye ameshindwa kuokoa maisha yake. Akakumbuka siku ya kwanza aliyomuona Joseph na yule Mama mwenye matako makubwa wakiwa chumbani wakati yeye akiwachungulia kwenye dirisha. Alikumbuka pia siku Joseph alipoingia mule chumbani alipokuwa akiteswa na yule mtu mweusi kama msudani mwenye roho mbaya. Alikumbuka jinsi macho ya upole ya Joseph yalivyomtazama siku ile alivyokuwa akishambuliwa na siafu wakali wa lile jitu katili. Yalikuwa ni macho ya mtu mwenye huruma. Macho ya mkombozi. Ghafla sauti za risasi ambayo ilikuwa umbali wa mita kama ishirini ikasikika hali iliyofukuza mawazo yote ya Sajenti aliyekuwa amemkumbatia Joseph. Akamuachia Joseph pale chini akakimbilia lilipo gari. Aliingia ndani ya gari huku milio ya risasi ikizidi kumsakama. Akatia gia na kuondoka kwa kasi kama mwenda wazimu. Huyo akaikamata barabara iendayo kigamboni na ndani ya dakika ishirini alipokelewa na mataa ya Daraja la kigamboni. Daraja la kigamboni ni Daraja linalounganisha kata ya kurasini na kigamboni. Linaurefu usipungua mita mia sita na upana usiyopungua mita thelasini. Ni moja ya madaraja marefu katika ukanda wa nchi za afrika mashariki. Daraja hili lilizinduliwa tarehe 19/04/2016 ambapo lilizinduliwa na Rais John Pombe Magufuli na kupewa jina, Daraja la Nyerere kama heshima na kumbukumbu kwa rais wa kwanza wa Tanzania hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Akiwa katikati ya Daraja hilo lenye njia sita za kupitisha magari. Punde akaona magari matatu yakija kwa kasi mbele yake yakiwa yamewasha taa yenye mwanga mkali. Moyo wake ukapasuka. Akili yake ikakosa utulivu. Akapunguza mwendo kwa kukanyaga breki huku akiligeuza gari lake kwa ufundi wa hali ya juu. Sekunde tuu gari yake iligeuka ilipotoka lakini akashikwa na butwaa kuona kwa mbali magari mengine matatu yakiwa na watu walioshika bunduki yakiwa yanakuja kwa mwendo wa tufani. Akatoka ndani ya ile landrover akipokelewa na milio ya risasi huku akimulikwa na tochi za wale watu waliokuwa wakija na yale magari. Akakimbia kwa kasi akajirusha kutoka Darajani mpaka baharini. Lilikuwa tukio la kijasiri lisilohitaji mtu muoga kulifanya. Wale watu wakalifikia gari aina ya land rover ambalo Sajenti alikuwa amelitelekeza. Wakasimama pale alipojirushia wakiumia kurunzi zao kumulikamulika chini ilipobahari ambapo waliiona bahari ikiwa imetulia kana kwamba Sajenti Warioba hakuwa amejirusha humo. Walimulika na tochi zao huku wakipiga risasi kuelekea baharini. Walipiga risasi kama mvua baharini kusudi kama Sajenti angekuwa karibu zimpate. Wakakaa kwa dakika kumi lakini hawakuona dalili ya Sajenti Warioba kutokea juu.


ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 06)
Mrunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

>>>>>>>>>>>>>>> Episode 06 <<<<<<<<<<<<<<<<<<<<

ILIPOISHIA
Lilikuwa tukio la kijasiri lisilohitaji mtu muoga kulifanya. Wale watu wakalifikia gari aina ya land rover ambalo Sajenti alikuwa amelitelekeza. Wakasimama pale alipojirushia wakiumia kurunzi zao kumulikamulika chini ilipobahari ambapo waliiona bahari ikiwa imetulia kana kwamba Sajenti Wariob
a hakuwa amejirusha humo. Walimulika na tochi zao huku wakipiga risasi kuelekea baharini. Walipiga risasi kama mvua baharini kusudi kama Sajenti angekuwa karibu zimpate. Wakakaa kwa dakika kumi lakini hawakuona dalili ya Sajenti Warioba kutokea juu.

ENDELEA.....


SURA YA TATU

Gari la kontena lilionekana likiingia katika hospitali ya Ambagon iliyopo jijini Dar es salaam. Liliingia katika geti la nyuma la hospitali hiyo. Likapaki na punde mlango wa nyuma wa lile kontena ukafunguliwa. Kisha akatoka mtu mmoja aliyevalia nguo kama daktari wa ebola. Yule mtu alitembea kidogo akitazama huku na huko kama mtu aliyekuwa akiangalia usalama, alipoona hali ni shwari. Punde mlango wa dereva ulifunguliwa na mtu akashuka. Huyu alikuwa ndiye dereva wa hili gari la kontena. Yule dereva akamsogelea yule mtu aliyetokea kwa nyuma. Wakawa wanajadiliana jambo fulani kwa sauti ya chini. Kisha dereva akarudi ndani ya gari na yule mtu aliyevalia kama daktari wa ebola akapiga hatua kuufuata mlango uliokuwa ukimtazama. Kabla hajaufikia ule mlango ulifunguliwa na mtu mmoja akajitokeza. Walishikana mikono kwa kusalimiana na wote wakaingia ndani ya lile jengo la hospitali. Mara wakatoka watu waliobeba mabegi makubwa meupe yanayotumika kuwekea maiti. Lile jengo lilikuwa ni Mortuary ambapo maiti huhifadhiwa. Watu hawa walikuwa wakiichukua miili ile na kuipakiza ndani ya lile gari. Wanaipeleka wapi hakuna aliyekuwa anajua isipokuwa wao wenyewe. Walitoa miili ishirini wakaipakiza ndani ya lile gari. Ndani ya gari pia ilikuwepo miili mingine. Dooh! Hii ilikuwa hatari sana. Yule mtu aliyevalia kama daktari wa ebola akachukua kibegi akamkabidhi yule mtu aliyetoka mortuary. Yule mtu akafungua kile kibegi akakuta mabulungutu ya pesa yaliyopangwa vizuri. Akatabasamu kisha akafunga. Wale vijana waliosaidia kubeba ile miili ya maiti waliokuwa wanne walisimama mbele ya yule mtu aliyepewa kibegi cha pesa kusubiri malipo yao. Yule mtu alitoa notinoti kisha akampa kila mmoja elfu kumi.

"Boss lakini tulipatana laki mbili mbili. Mbona unatupa kumi tuu?’’ Kijana mmoja aliongea. Bila shaka ndiye alikuwa kiongozi wa wenzake katika kazi hiyo haramu. Yule mtu akamtazama kwa dharau kisha akachomoa bastola na kumpiga risasi ya kichwa. Risasi haikutoa sauti kutokana na kuwa bastola ilikuwa imewekewa kiwambo cha kuzuia sauti kutoka. "Mwingine anayehitaji laki mbili?" Yule mtu aliongea kwa sauti ya kikatili akiwatazama wale vijana watatu waliotekewa na kujawa na hofu ya tukio walilolishuhudia . Wale vijana watatu waliobaki hawakujibu kitu, walikaa kimya kwa hofu. Waliogopa kuuawa kama mwenzao aliyekuwa amechapwa risasi.

"Wewe pandisha huo mzoga juu ya gari" Yule mtu akamuambia kijana mmoja aupandishe mwili wa mwenzake aliyepigwa risasi ya kichwa.

Yule kijana hakuwa na pingamizi zaidi ya kufanya kama alivyoagizwa. Angewezaje kuleta ubishi ikiwa aliuona ubongo wa mwezake ukiwa umelala pale ardhini. Kwani yeye hapendi kuishi. Thubutu! Hata angekuwa kichaa wa namna gani bado angependa kuishi.

"Haya futikeni. Sheria za kazi mnazijua. Mkitoa siri kifo halali yenu". Yule mtu aliyewapiga risasi akasema wakati wale vijana watatu wakiondoka kwa kukimbia. Gari liliondoka katika hospitali ya Ambagon. Lilitembea kwa zaidi ya masaa mawili likiliacha jiji la Dar es salaam kwa mbali sana. Lilikuwa linakaribia Chalinze yapata majira ya saa tisa usiku. Robert alizinduka akajikuta yupo ndani ya begi. Alishangaa inawezekana vipi awe mule ndani. Alivuta kumbukumbu kujua alifikaje pale. Lakini alichokumbuka ni kuwa mara ya mwisho alikuwa akikimbizwa na gari ya Polisi. Alikumbuka pia alipata ajali baada ya bodaboda aliyoipanda kugongwa na gari aina ya Nissan patrol nyeupe. Iweje awe mule ndani ya begi. Kitambo kidogo Akagundua yupo ndani ya gari kutokana na mitikisiko ya mule ndani. Harufu ya mule ndani ilikuwa ikimuumiza pua. Ilikuwa harufu kali ya marashi ya maiti. Alijikurupua mpaka akatoka kwenye lile begi. Macho yake yalipokelewa na giza nene, lakaini kitambo kidogo mboni ya macho yake ziliweza kuzoea giza lile na kuanza kuona. Akashangaa kuona mabegi mengi kama alilokuwamo yeye. ilikuwa ni miili ya watu. Alifungua begi moja. Akashtuka! Kutoka kwenye lile begi alikutana na maiti ya kutisha sana. Maiti ile ilikuwa imetobolewa macho huku jicho moja likining’inia. Robert aliogopa sana. Hapo akajua yupo sehemu hatari sana. “Itakuwa walidhani nimekufa” Robert aliwaza moyoni. Njaa kali tumboni ilimtekenya. Alikuwa hajala tokea siku ile aliyokula ndizi rosti na nyama kwenye ile nyumba ya yule Mama alipokuta midoli yenye madawa ya kulevya.

Ilikuwa ni siku ya pili tokea apate ajali ya bodaboda alipokuwa akiwakimbia Polisi. Akanyanyuka akaanza kutembea mule ndani ya lile gari huku akikanyaga yale mabegi yenye maiti. Akafika nyuma kabisa ambapo alishtuka kuona maiti isiyokuwa ndani ya begi. Ulikuwa ni mwili wa yule mtu aliyepigwa risasi ya kichwa kwa kukataa malipo ya elfu kumi. Aliifikia ile maiti kisha akaanza kuikagua kwenye mifuko yake ya suruali. Alikuta noti ya shilingi elfu kumi na simu ya smartphone. Akaichukua ile noti ya elfu kumi na ile simu. Kisha akamvua suruali yule mtu aliyepigwa risasi alafu akaivaa, kwani yeye alikuwa yu uchi. Hivyo akaona achukue suruali ya yule kijana aliyepigwa risasi. Pia akachukua ile simu ya smartphone akaanza kuikagua kagua. Akaingia sehemu ya picha akaona picha za yule kijana akiwa na familia yake. Aligundua yule mtu alikufa kifo kibaya cha kupigwa risasi ya kichwa, alikuwa baba wa mtoto mmoja. Akaona video moja ikimuonyesha marehemu akicheza na mtoto wake na mke wake. Alimtazama mke wa marehemu akagundua ni mwanamke asiyefikisha miaka ishirini na tano. Alijikuta akimuonea huruma sana. Aliwalaani waliofanya unyama ule kwa yule kijana. Hata hivyo hakujua kwa nini kijana yule aliuawa. Akaingia upande wa meseji akakuta meseji tano ambazo hazikuwa zimesomwa. Alizifungua akakuta meseji kutoka kwa mke wa yule mtu aliyeuawa isemayo;
“Mume wangu nakupenda. Usisahau kesho natakiwa kwenda zahanati kuangalia maendeleo ya ujauzito"

Dooh! Robert pumzi zilimkaba. Hapo akagundua kuwa mke wa yule kijana aliyekuwa amekufa alikuwa ni mjamzito. Dunia ndivyo ilivyo Mama Susan, unaweza ukatamani kucheka lakini yenyewe ikakufanya kulia. Unaweza ukataka kula lakini yenyewe ikakufanya uliwe. Hii ndio dunia Mama Susan. Robert aliongea akiiambia ile simu kana kwamba anamuambia Mama Susan kweli. Aligundua mke wa yule aliyeuawa alikuwa anaitwa Mama Susan baada ya kusoma namba ilivyohifadhiwa. Baada ya masafa marefu lile gari lilisimama. Robert alishtuka akiwa amepitiwa na usingizi wa njaa. Usingizi wa mang'amu ng'amu. Punde akasikia mlango wa nyuma wa lile kontena alilokuwapo ukiguswaguswa. Akajua punde utafunguliwa. Akili yake ilifanya kazi kwa upesi. Akajifunika chini ya moja ya zile maiti. Mlango ulifunguliwa kisha wakaingia watu wawili mule ndani ambao walikuwa kana kwamba wanatafuta kitu fulani. Wale watu walienda kule alipokuwa mara ya kwanza. Robert aliingiwa na hofu. Aliogopa wale watu wasijeona lile begi alilokuwepo yeye kuwa halina maiti ndani. Hii ingewafanya washtuke kuwa kuna maiti imefufuka na kutoroka. Hata hivyo hawakufika. Walirudia njiani. Waliutoa ule mwili wa yule aliyepigwa risasi ya kichwa kisha wakarudishia ule mlango. Robert akashusha pumzi kama mtu aliyemaliza mbio ndefu. Njaa ilizidi kumtafuna. Alitamani muujiza utokee wa kupata chakula. Lakini zilikuwa ndoto za mchana. Ama kweli adui yako muombee njaa wahenga walisema. Leo msemo huu Robert aliuthibitisha siyo kwa kuhadithiwa. Aliona makali ya njaa. Cheza na mambo yote lakini siyo njaa. Ni njaa hiyo hiyo ndio inayofanya watu wauane. Ni njaa hiyo hiyo inayofanya watu wawekeane husda na visasi. Njaa ni mbaya hakuna asiyejua. Ule mwili wa maiti aliojifunika nao ulikuwa ukitoa majimaji yenye harufu mbaya. Akashindwa kuvumilia harufu na uzito wa ile maiti. Alihisi ile ilikuwa maiti ya mwanamke kutokana na kuwa na manyonyo. Aliitoa kisha akatoka. Alikuwa hoi bin taabani. Ndani ya gari bado hewa iliendelea kuwa nzito kutokana na kutokuwa na sehemu za kuingizia hewa.

"Siwezi kufa kama mpuuzi. Lazima nifanye kitu. Mimi ni mwanaume bhana" Robert aliongea mwenyewe huku giza lililokuwa mule ndani ya gari likimtazama. Akanyanyuka na kuanza kukanyaga zile maiti mpaka ulipo mlango wa nyuma wa gari lile. Akajaribu kuusukuma. Kama utani mlango ukafunguka. Robert hakuamini kabisa. Alihisi kama anaota ndoto ya mchana lakini haikuwa ndoto. Ilikuwa ni kweli. Alipokelewa na upepo wa nje na kigiza cha saa moja moja kikiwa kimetanda. Aliangaza macho yake huku na huko lakini hakuona nyumba yoyote zaidi ya vichaka vifupi vifupi na miti michache mirefu. Lile gari lilikuwa likienda kwa kasi sana kiasi kwamba unahitaji umakini unapotaka kuruka. Kama ni mtu mwoga huwezi kuruka. Robert aliona ni afadhali kuruka na kuvunjika mguu au kufa kabisa kuliko kuendelea kubakia mule ndani akinukiwa na harufu mbaya za maiti. Kama hiyo haitoshi angeweza kuvumulia harufu ya maiti lakini hakuwa tayari kuingia katika mikono ya wale watu asiojua wanapeleka wapi zile maiti. Akili yake ilimuambia kuwa watakuwa ni watu wabaya wasio na huruma. Hivyo kama wakimkamata wataweza kumdhuru. Alikumbuka mwili wa yule mtu aliyepigwa risasi kichwani. Kwa kweli hakuwa tayari kuona akipatwa na madhila kama aliyokutana nayo yule kijana.. Ingawaje hakujua alipigwa na kina nani lakini aliamini ni kuwa watu waliompiga yule mtu risasi watakuwa ni watu wabaya sana.

Punde gari lilipunguza mwendo kidogo jambo lililomfanya Robert achungulie kwa pembeni kuona nini kinaendelea. Akawaona kwa mbali askari wa barabarani, wawili wakipunga mkono kulisimamisha gari lao. “Muda wa kujikomboa umewadia” Akawaza. Aliiona ile ni nafasi ya mwisho ya kutetea maisha yake. Kitendo cha gari kupunguza mwendo alikihesabu kama msaada uliokuja kwa wakati muafaka. Angewezaje kukaa na maiti mule ndani ilhali yeye siyo maiti. Hata kama walidhani amekufa lakini siyo sasa ambapo yu hai. Hata hivyo hakujua maiti zile zilikuwa zinapelekwa wapi, wala hakutaka kujua zinapopelekwa. Akaruka; kwa nyuma ya gari kisha akajiviringisha kama jongoo mpaka nje ya barabara. Akajificha kwenye vichaka. Alichubuka magotini na mgongoni lakini ilikuwa afadhali kuliko kukutwa mule ndani na wale watu wabeba maiti. Akiwa kichakani aliona lile gari likisimama. Wale askari walilisogelea wakitaka kulikagua. Akamuona mtu mmoja akishuka kwenye lile gari la kontena. Yule mtu alivalia mavazi kama daktari wa ebola.

Askari wa barabara aliyevalia shati jeupe yenye mikanda mabegani. Akiwa amelichomekea vyema kwenye suruali yake nyeupe ambapo kiunoni kulikuwepo na mkanda wenye bendera ya Tanzania. Chini alivalia viatu vyeusi. Kiukweli alikuwa nadhifu sana. Yule askari akaelekea mpaka alipofika nyuma kabisa ya lile gari. Hapo aliona mlango wa nyuma wa lile gari ukiwa wazi. Akamuita yule mtu aliyevalia mavazi kama daktari wa ebola. Yule mtu alishtuka kuona mlango wa gari lao upo wazi wakati wao walikuwa wameufunga. Alijitahidi kuficha mshtuko wake lakini trafiki aliweza kuiona hofu aliyokuwa nayo.

Trafiki akiwa na kurunzi akapanda kuchungulia ndani ya lile gari akimulika kwa kutumia kurunzi, alishtuka kuona miili ya maiti ikiwa ndani ya mabegi. Masikini! haikuwa bahati yake, daktari wa ebola akampiga risasi na kabla hajaanguka alimkamata na kumrushia ndani ya gari. Yote hayo Robert alikuwa akiyaona akiwa kajificha kwenye kichaka. Alihisi kama anatazama filamu ya kutisha lakini haikuwa filamu. Lile lilikuwa tukio la kweli kabisa. Yule mtu alitoka kule nyuma akaenda alipoyule trafiki mwingine ambaye alikuwa akiongea na dereva wa lile gari. Trafiki alishangaa kumuona yule mtu mwenye mavazi kama daktari wa ebola ameshika bastola.

"Weka mikono kichwani" Yule mtu aliyevalia kama daktari alimuarisha trafiki. Bila kubisha akiwa na simu ya upepo aliweka mikono yake kichwani. Bila kupoteza muda yule mtu alimfyatulia risasi trafiki iliyoharibu vibaya kifua chake; akadondoka chini kama mti uliopigwa shoka la mwisho. Robert alitaka kupiga kelele lakini alijishika mdomo wake. Alitetemeka kwa hofu. Aliamini kuwa wale watu walikuwa watu wakatili wasiyo na huruma hata chembe. Aliwaona ni watu waliobobea katika kuua watu. Wao kuua mtu ilikuwa jambo rahisi kama kuua mbu. Iweje wawaue askari wa watu waliokuwa kwenye majukumu yao ya kulinda na kusimamia usalama wa barabarani. Hakika watu wale waliuvuruga moyo wa wake. Akamuona dereva wa lile gari akishuka. Kisha wakambeba yule trafiki aliyekuwa ameshajifia kwa kupigwa risasi na yule daktari muuaji. Walimburuta mpaka nyuma ya gari na kumrusha juu ndani ya gari.

Kisha yule dereva akapanda kufunga ule mlango wa nyuma wa lile gari. Akiwa anafunga punde walisikia sauti ya simu ikiita kichakani. Ilikuwa ni simu aliyokuwa nayo Robert . Ile simu aliyoichukua kwa yule kijana aliyepigwa risasi ya kichwa aliyemkuta ndani ya gari. Mume wa Mama Susan. Kama kuna mambo ambayo yalimrostisha na kumchomea Robert ilikuwa ni ile simu. Kitendo cha ile simu kulia kilikuwa kitendo kibaya zaidi katika maisha yake. Akajitahidi kuizima lakini akashindwa. Dereva na daktari muuaji waliangalia kule sauti ya simu ilipokuwa inatokea. Waliona mwanga wa simu lakini hawakuona mtu. Ni kutokana na umbali ndio maana hawakuweza kumuona Robert. Wakaanza kurusha risasi kuelekea kule alipokuwa Robert . Dereva akakimbia ndani ya gari akatoka na bunduki aina ya AK47. Robert alianza kukimbia akifukuzwa na risasi zilizokuwa zikija nyuma yake kama nyuki. Akakimbia huku wale watu wakimfutia kwa kasi sana. Walikuwa wakimkimbiza Robert kama wawindaji wanaokimbiza swala kwa mishale. Robert alikuwa akikimbia huku akijibanza kwenye miti ili risasi zisimpate. Wale watu walidhamiria bhana. Dereva akarudi tena kwenye gari kuliondoa gari barabarani na kuliingiza vichakani kumfuata Robert aliyekuwa akikimbizwa na yule daktari muuaji. Kama ni shabaha hawa watu walibobea. Kama siyo ile miti mingi aliyokuwa akijificha Robert basi muda mrefu Robert angekuwa kashapasuliwa ubongo. Kwa maana ilikuwa kila alipokuwa anajibanza risasi iliparuza sekunde ileile pembeni ya ule mti aliojificha. Ni kusema kama angechelewa kidogo ubongo wake ungechanwa na risasi. Lakini jambo la kushangaza ni kuwa Robert alikuwa anajua kukimbia hujapata kuona. Alikimbia kama duma wa brazili. Embu fikiria kama aliweza kuwakimbia wale watu kule makaburini waliokuwa mamia sembuse hawa watu wawili.

Lakini pamoja na kukimbia kwake asije akaleta masihara na watu wale. Walikuwa wawili lakini hatari ambao kuua ndio kazi iliyokuwa inawapa kipato. Wao hujisikia raha kuona mtu akitoa macho anapokata roho. Hupenda kumuona mtu akitapatapa wakati roho ikiacha mwili. Hivyo Robert anapaswa kuwa makini kuliko anavyoweza kufikiri. Akakimbia kwa muda wa dakika kumi huku nyuma daktari muuaji akija adoado kama zombi. Na yule dereva akija na gari lake. Wakiwa wanakimbia punde aliingia kwenye msitu ambao ulikuwa na giza zaidi. Alikimbia akiikumbakumba miti na kuanguka anguka kutokana na hofu na giza. Akahisi pumzi imekuwa ndogo lakini aliona ni bora afe akiwa anakimbia kuliko kukamatwa na wale watu. Alikuwa akikimbia huku kumbukumbu zake zikimrudisha siku alipokuwa akifanya mapenzi na mpenzi wake, Ismaiya. Alikumbuka tabasamu la Ismaiya huku akiendelea kukumbuka Alihisi kuchoka. Akaona ajifiche kwenye kichaka kilichokuwa mbele yake. Alitulia kwenye kichaka akisikiliza kama atasikia sauti za wale watu. Palikuwa kimya. msitu ulikuwa kimya sauti ya pumzi itokayo katika pua yake ndio iliondoa utulivu wa msitu ule. Akashusha pumzi, kifua kikipanda na kushuka. Roho ilitokota kama uji wa mzazi. Alihofia wale watu wa baya waliokuwa wakimfutia kwa lengo la kutoa uhai wake. Kitambo kidogo akiwa amepata unafuu macho yake yalipumbazika na kuchanganyikiwa kuona kwa mbali mwanga wa tochi ukiwa unakuja kule alipokuwa. Ule mwanga ulikuwa ukihama hama ukimulika huku na huku kama mtu anayetafuta jambo fulani. Alijua kuwa hakuna mwingine anayeweza kuwa ndani ya msitu kwa usiku ule zaidi ya wale mashetani wawili wenye kiu na roho yake. Wale watu walikuwa wapo radhi wakose kila kitu kwenye hii dunia lakini siyo kumkosa Robert . Kitendo cha Robert kuepa walikihesabu kama fedheha kubwa. Hawakuwa tayari kukimbiwa na Robert . Kwa uzoefu wao walishakimbizana na majangili na watu hatari kuliko Robert . Leo mtu asiyejua hata wapi ilipokambi ya jeshi awakimbie. Thubutu! Robert hakutaka waendelee kumsogelea akajinyanyua kama ng'ombe aliyechoka kisha akaanza kukimbia akiwa kifua wazi na suruali aliyoichukua kwa yule mtu aliyepigwa risasi aliyemkuta ndani ya gari. Alikimbia kama duma anayekimbiza windo lake. Bahati haikuwa yake. Mbele yake palikuwa mto mkubwa wenye maji ambayo yalikuwa yakinguruma mithili ya simba mwenye njaa. Kunguruma kwa maji ya mto ule ni kama kulikuwa kunamuambia ukiingia tuu nakumeza. Aliyatazama mawimbi ya ule mto ambayo yalikuwa ni kana kwamba yakimbembeleza aingie ndani ili yajipatie chakula kwa usiku ule. Yale mawimbi yalilalama kuwa tangu mchana hayajapata kitoweo. Hivyo Robert aingie tuu ili mto ule ujipatie chakula. Robert akayaambia yale mawimbi ya ule mto kimoyo moyo; ninyi mawimbi nioneeni huruma. Ninasiku nne sijala. Kama ninyi ni tokea mchana hamjapata kitoweo basi mwenzenu ni siku ya nne leo. Masikini Robert ni kama alikuwa amechanganyikiwa. Punde nyuma yake akamulikwa na tochi kisha mlio wa risasi ulifuatia. Hali iliyofanya msitu mzima uteteme. Ilikuwa ni AK47 silaha hatari ambayo ni sekunde tuu inaweza ondoa uhai wa kiumbe yoyote chini ya juu. Usiku ule silaha hiyo ilitaka roho yake,. Robert akavuta pumzi kisha akapiga hatua moja, mbili, tatu huyo akajirusha mithili ya kipa arukiavyo mpira wa penati. Huyoo! Huyoo chwaaa! Alitoma ndani ya mto. Huku risasi za wale watu zikimfukuzia mithili ya mwizi wa kuku. Wale watu walifika kando ya ule mtu ambapo Robert alijirusha mtoni. Wakamulika huku na huku lakini mto uliwazomea huku mawimbi yakiwadhihaki. Kwa hasira za mkizi walipiga hovyo hovyo risasi kwenye ule mto lakini hiyo haikufanya mto umtoe Robert ndani ya maji. Waliondoka wakiwa hawaamini kama wamemkosa. Roho iliwauma sana. Walijua lile lilikuwa kosa kubwa kwa biashara yao. Walijua kuwa huenda mtu aliyewakimbia ataenda kutoa siri ya biashara yao haramu waifanyayo. Walijua kuwa huenda mtu aliyewakimbia atatoa siri kuwa wao ndio waliowaua wale matrafiki. Wakaanza kuufuata ule mto ulipokuwa unaelekea huku wakimulika mulika ndani ya mto. Robert alichukuliwa na mto akigongeshwa gongeshwa kwenye kingo za mto na sakafu ya ule mto. Alijitahidi kuogelea lakini hakuwa na ujuzi wowote wa kupiga mbizi. Hata kama angejua kuogelea bado asingefurukuta kutokana na maji ya mto ule kuwa na nguvu. Ulikuwa ni mto Ruaha moja ya mito mikubwa katika nchi ya Tanzania. Mto Ruaha mkuu ni mto wenye urefu wa kilometa mia nne sabini na tano. Unapita katika mbuga kubwa iitwayo mbuga ya taifa ya Ruaha ambayo ni miongoni mwa mbuga zenye wanyama wengi ambao ni kivutio kikubwa cha utalii. Mto Ruaha pia ni chanzo kikuu cha bwawa la mtera na kidatu ambapo umeme wa maji unazalishwa. Pia mto Ruaha hupita katikati ya pori la akiba Selous kabla haujaingia mto Rufiji.

Kitendo cha Robert kubebwa na mto Ruaha kilikuwa ni kitendo cha hatari sana. Ndani ya mto Ruaha kulikuwa na viboko na mamba ambao wangeweza kumdhuru. Punde Robert alikwama kwenye jiwe kubwa lililokuwa kwenye ule mto. Hiyo ilikuwa nafuu kwake. Akapanda juu ya lile jiwe huku akitetemeka kwa baridi kali. Iringa ni moja ya mikoa iliyopo nyanda za juu kusini katika nchi ya Tanzania yenye hali ya hewa ya baridi kali. Robert alitetemeka kutokana kwa baridi iliyokuwa ikiyapiga mapafu yake akiwa kifua wazi. Bado alikuwa kwenye lile jiwe akifikiria ni namna gani atatoka pale mtoni. Aliliona tawi la mti uliokuwa pembeni ya mto. Akapata wazo la kulipanda lile tawi litalomfikisha nje ya mto. Alilishika huku akichukua tahadhari asiteleze. Akafanikiwa kulipanda lile tawi na kufika juu ya ule mti. Hapo akaona ni bora akae juu ya mti kama ngedere kuliko kushuka chini na giza lile. Akiwa juu ya mti alikumbuka yale yote yaliyokuwa yamempata. Alikumbuka siku ya harusi ya yeye na Adele ambapo msafara mkubwa wa magari yaliyokuwa yakiongozana kwenda ukumbini. Alimkumbuka Ramla alivyopigwa risasi siku ile ya harusi. Hapa huzuni ilimuingia machozi yakimlenga lenga.

Usingizi ulimpitia. Akalala akiwa amekumbatia tawi la mti kama nyani. Mungu siyo Athumani jua likachomoza. Ndege waliokuwa wameweka makazi katika mti ule walipiga makelele wakiwaita ndege wengine waje kumuona kiumbe aliyevamia makazi yao. Kundi kubwa la ndege lilikuwa likiuzunguka ule mti na kupiga kelele kumuasha Robert ili aamke. Ni mpaka ndege mmoja alipofika na kumdonoa Robert sikioni hapo ndipo Robert akaamka, alishtuka kuona kundi kubwa la ndege likiwa juu ya ule mti likimpigia kelele kuwa aondoke katika makazi yao. Aliwafukuza wale ndege wakaruka lakini hawakwenda mbali walirudi tena. Akasimama juu ya ule mti akaangaza macho yake huku na huko kuangalia mandhari ya eneo lile. Alishuhudia makundi makubwa ya tembo kwa mbali yakila majani na watoto wao. Akageuza macho upande wa pili akaona swala na pundamilia wenye rangi ya kuvutia. Kwa mbali aliwaona kiboko wakichezea maji kwenye mto Ruaha ambapo usiku wake ulikuwa umembeba. Alijua yupo hifadhi ya Ruaha. Kwa mbali aliona bwawa kubwa lenye maji. Hilo lilikuwa bwawa la mtera. Akawaona ndege weupe makundi makundi.

Akashuka chini ya ule mti akiwa kifua wazi huku ngozi yake ikiwa imeota vipele vya baridi kama fenesi. Alitembea kwa tahadhari kwani alijua kuwa yupo katika mbuga ambapo wanyama wakali ni lazima wangekuwepo. Akayaona matunda pori akachuma, akala. Angalau akajisikia ahueni. Aliyala mpaka akashiba. Hakujua ni matunda gani lakini kwa vile aliwaona ndege wakila akajua siyo sumu. Sasa alikuwa mtu mpya mwenye nguvu. Akatembea kwa masaa matatu jua likiwa limepanda juu kabisa. Kwa mbali akasikia watu wakiongea huku wakija kule alipokuwepo. Akatembea haraka kuzifuata zile sauti. Lakini akili yake ilimuonya kuwa huenda wale hawakuwa watu wazuri. Aidha alikumbuka wale watu hatari waliomkimbiza usiku. Akili yake ikamuambia ajifiche. Akajificha kwenye mti. Aliwaona watu watatu wenye magobori wakiwa wamebeba pembe za ndovu. Akashtuka. Alibaini walikuwa majangili wanaoua wanyama pori bila kibali. Akatamani ajitokeze awakamate. Lakini angethubutuje ikiwa hakuwa na silaha yoyote zaidi ya suruali yake iliyokaukia mwilini huku akiwa kifua wazi. Aliwafuata nyuma nyuma bila ya wao kujua. Punde walitokea kwenye sehemu walipoficha gari lao. Waliingia ndani ya gari kisha Robert akakimbia haraka mpaka chini ya ile gari aina pickup yenye rangi ya kijani mpauko. Gari ilianza kutembea kwa kasi sana. Walitembea kwa muda mrefu kwenye barabara ya vumbi. Robert alishikilia chini ya gari mpaka akachoka. Kama asingekula yale matunda pori ni wazi asingeweza kushikilia pale chini ya gari kwa muda mrefu kiasi kile. Lile gari la wale watu lilitimua vumbi jambo ambalo lilimpa tabu sana Robert . Muda wote alikuwa amefumba macho ili vumbi lisiingie machoni. Punde gari lilivuka kwenye mfereji wenye maji machafu. Yale maji yenye matope yalimlowesha Robert aliyekuwa chini ya gari.

Punde gari likaingia kwenye barabara ya lami. Hapa Robert aliona ni afadhali. Aliona jinsi lami ilivyokuwa ikirudi nyuma kwa kasi kutokana na kasi ya gari. Kama angeigusa hata kidogo ni wazi ngozi yake ingechubuka. Hatimaye gari lilisimama. Walikuwa wamefika kwenye mji wa Mafinga. Walikuwa wamesimamishwa na trafiki wa pale Mafinga yapata mishale ya saa tisa mchana. Trafiki walilikagua lile gari kwa bahati mbaya wale watu walikutwa na pembe za ndovu. Trafiki wakawawaweka wale majangili chini ya ulinzi, wakawavisha pingu kisha wakaelekea na lile gari kituo cha Polisi cha Mafinga. Robert alijua kama atatoka muda ule naye angejumuishwa kwenye kundi la wale majangili. Akiwa chini ya gari pale kituo cha Polisi aliona jambo baya lililomchefua roho. Aliwaona mbwa wa Polisi wakija kule alipokuwa yeye. Japokuwa hawakumuona lakini alijua fika kuwa mbwa wanauwezo mkubwa wa kunusa. Hivyo kama wale mbwa wawili wangekuja eneo lile basi wangemuona jambo ambalo hakutaka litokee. Bahati haikuwa upande wake. Robert alimuona moja ya wale mbwa akija kule alipokuwepo. Alifika mpaka karibu na lile gari na ana kwa ana waligongana macho na lile jibwa linoko lenye kihere here. Mbwa alipofikia lile gari alilokuwepo Robert, chini yake likaanza kubweka. Huhu! Huhu! Huhu! Huhu! Mbwa alibweka kwa sauti ya juu sana. Huhu! Huhu! Huhu! Lile jibwa lilibweka likiingiza kichwa chake kwenye uvungu wa lile gari ambapo Robert alikuwepo. Mkojo ulikuwa ukimtoka kwa hofu. Lile jibwa lilikuwa na sura mbaya kuliko mbwa wowote hapa duniani. Jibwa lile liliizidi kwa ubaya hata sura ya mbwa aitwaye bulldog ambaye inasemekana ndiye mbwa mwenye sura mbaya duniani. Yule mbwa alipoona Robert amekojoa alafu ule mkojo unatiririka aliposimamia likanyamaza kisha likakung'uta miguu yake likaondoka. Kumbe hata wanyama wanajua kuwa kujikojolea ni dalili ya woga. Huenda pia lilimuonea huruma. Lile jibwa liliondoka na kumuacha Robert akiwa anatweta kwa hofu. Alikuwa haamini kama lile jibwa lingemuacha. Tayari ilikuwa imehitimu saa moja jioni kigiza kikiwa kimetawala eneo lote la mji wa Mafinga.baridi kali ilimpiga Robert pale chini ya gari lakini aliona ni bora baridi kuliko akamatwe na Polisi. Akashuka chini ya lile gari alipokuwa amepakumbatia. Kisha akalala kwa kujinyoosha ardhini. Walau alijisikia ahueni. Alibilingilita kama mwanajeshi akatoka kwa nje. Hapakuwa na watu wengi zaidi ya Polisi mmoja mmoja. Hii ni kutokana na baridi kali. Aliangaza huku na huku akaona geti la kutokea ambapo kulikuwepo na mlinzi. Alitembea kwa kasi kama kichaa akafika pale getini na bila kusalimia akatoka. Yule mlinzi alibaki akimtazama kwa mshangao. Alimuona ni kichaa kutokana na jinsi alivyokuwa kifua wazi huku mwili mzima ukiwa umejaa matope.

Robert alifanikiwa kuliacha eneo la kituo cha Polisi cha Mafinga. Akaingia mtaani akiwa kajikumbatia kifuani kutokana na baridi. Watu wote aliopishana nao walikuwa wamevaa makoti na masweta mazito ya baridi. Yeye peke yake ndio alikuwa hana sweta kama hiyo haitoshi yeye alikuwa kifua wazi kabisa. Giza lilikuwa limeshaingia. Alipitia sokoni akakuta wauza mitumba ndio walikuwa wakifungasha mizigo yao. Akatoa ile noti ya shilingi elfu kumi akanunua tisheti ya elfu moja mia tano akaivaa. Muuza nguo alimshangaa lakini Robert hakujali. Akanunua na kanda mbili za yeboyebo za elfu moja akavaa. Sasa alikuwa mtu kamili. Akaondoka kwenda kutafuta nyumba ya wageni apate kupumzika. Mwili wake ulihitaji kupumzika baada ya shurba aliyoipata kwa siku nne mfululizo bila kupata usingizi wa kueleweka. Akapata gesti bubu ya shilingi elfu tano. Alilipia kisha akazama ndani. Kilikuwa ni chumba kidogo chenye kitanda cha nne kwa sita. Mashuka yake yalikuwa ya rangi ya samawati na mito miwili. Hapakuwa na chandarua kutokana na kuwa na baridi mji wa Mafinga hakukuwa na mbu wengi. Dirisha la kile chumba lilikuwa la wastani kwa ukubwa likiwa na vioo ili baridi isipenye ndani. Kwa pembeni kulikuwa na kijimeza kidogo ambacho juu yake kulikuwa na televisheni ya chogo. Pembeni ya ile Tv kulikuwa na pakti mbili za salama kondomu.

Robert aliporidhika na mandhari ya chumba kile alijibwaga kitandani kwa uchovu. Kisha akatoa ile simu ambayo muda huo ilikuwa imezima kutokana na kuingia maji kwa muda mrefu. Ni maji ya mto Ruaha ndio yaliyoifanya simu ile iharibike. Akaiwekea kwenye meza. Kisha akatoka nje ambapo aliagiza aletewe chipsi kavu za elfu moja. Alimuagiza mhudumu wa ile guest kuwa mtu wa chipsi akileta ampelekee chumbani kwake. Yeye atakuwa ameenda kuoga. Robert alienda kuoga. Akiwa bafuni yule mtu wa chipsi alileta lakini hakumkuta Robert chumbani hivyo akamuachia dada mhudumu wa guest. Baada ya dakika kumi Robert alitoka akiwa safi mwenye nguvu mpya. Akarejea chumbani akawa anajifutafuta. Punde alisikia mlango wake ukigongwa. Alichukua shuka la akajifunika kimasai. Alienda kufungua mlango akamkuta ni yule mhudumu akiwa kabeba sahani iliyojaa chips. Akamkaribisha ndani na bila hiyana yule mhudumu akaingia.

"Karibu dada. Naona unataka kurudia nje" Robert akasema huku akiweka ile sahani ya chips kwenye meza.

"Mimi na wewe nani wakumkaribisha mwenzake?" Yule dada mhudumu akasema akijifaraguza

"Haya basi yaishe. Niite Robert "

" Naitwa Savilatangu, wengi huniita Savila"

"Ooh! Savilatangu jina zuri. Wewe ni mhehe?"

"Huoni hata jina langu. Bado uulize"

"Jina lako lina nini?"

"Halina kitu. Huoni ni jina lakihehe kabisa"

"Sawa! Usije ukajinyonga bure"
Robert alimtania na wote wakacheka.

Robert alishangaa kuona chipsi zilivyokuwa nyingi. Kama angekuwa Dar es salaam zile chips angeuziwa elfu tatu. Lakini Mafinga ziliuzwa elfu moja tuu. Hii ni kutokana na mkoa wa Iringa ulikuwa unaongoza kwa kulima viazi mviringo kuliko mkoa wowote hapa Tanzania. Robert alikula huku akipiga stori na Savila mtoto wa kihehe. Savila alikuwa ni mwanamke mzuri mwenye uso mpana kidogo. Macho ya mviringo yaliyotoka nje kidogo. Midomo mikubwa ambayo wanawake wengi hutamani kuwa nayo. Alikuwa mfupi kiasi lakini mwenye mapaja manene yaliyoshiba yaliyofanya sketi aliyoivaa kumbana na kuchora nguo yake ya ndani mapajani na kwenye makalio. Robert akajikuta akiingia tamaa ya ngono alipoona mapaja ya Savilatangu aliyejilaza kitandani huku akijiongelesha stori za hapa na pale za mji wa Mafinga. Alikuwa akimhadithia Robert baada ya kujua alikuwa mgeni katika mji ule. Wakati Savila akihadithia alijua kuwa Robert anamsikiliza lakini kumbe haikuwa hivyo. Robert alizama kwenye hisia nzito za mapenzi. Macho yake yalikuwa yakiangalia mapaja ya Savila kwa uchu huku udenda ukimtoka kama fisi aliyeona mzoga. Savila aligundua kuwa Robert hamsikilizi. Akamuona Robert akiwa anayaangalia mapaja yake yenye rangi ya kahawia yaliyonona haswa. Aibu ya kike ikamshika. Akaona mahali pale siyo salama tena. Savila aliwajua wanaume kuwa ni watu wenye tamaa ya haraka ya ngono. Alijua kuwa ni wanaume wachache tena waliowagonjwa na waliokufa ndio hawataweza kutamani mapaja kama yake yaliyonona. Akanyanyuka pale kitandani ili aondoke lakini Robert akamzuia. Akamlaza kitandani kwa nguvu kisha akampandia juu kama dume la bata huku akitweta. "Unataka kufanya nini?" Savila aliongea huku akijitahidi kujinasua. Robert akamtazama bila kumjibu. Walitazamana kama wanamasumbwi waliopigana makonde mfululizo wakachoka. Robert akaupitisha mkono wake kilipokifua cha Savila. Savila hisia za mapenzi zilimzunguka, akili yake ikamkimbia. Chezea vyote lakini usicheze na ashki ya mapenzi. Ashki ya mapenzi ikipanda unaweza kujikuta unabaka hata kuku. Ndicho kilichomkuta Savila. Kitendo cha kuguswa maziwa yake na Robert kilikuwa ni kama imeminywa swichi ya kuwasha hisia zake za mapenzi. Robert aliendelea kugusa sehemu nyeti ambapo ndani ya dakika tano Savila alikuwa hoi akipumua kama mgonjwa wa kifafa. Robert hakutaka kulaza damu. Alimchojoa nguo zake haraka haraka na ndani ya sekunde Savila alikuwa yupo kama alivyozaliwa.


Robert akavua lile shuka alilolivaa kimasai na wote walikuwa wapo uchi kama walivyozaliwa.
"Tumia kondomu" Savila aliongea huku akigugumia kwa utamu wa kupapaswa. Maneno ya Savila yalivuruga mkondo mzima wa Robert . Hisia zilikatika kama umeme. Alikumbuka kuwa mkoa wa Iringa na njombe ndio mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya UKIMWI. Ugonjwa aliouogopa kuliko kitu chochote. Alianza kujilaumu kwa kuendekeza tamaa bila kutumia akili. Hata hivyo wataalamu wa mambo walisema; kichwa cha chini kikisimama basi kichwa cha juu hugeuka kopo tupu. Robert alimshukuru Mungu kwa kumuokoa na dhambi ile ya uzinzi. Hata hivyo maneno ya Savila yalimfanya amuone kama naye ana UKIMWI. Alivaa shuka lake kisha akamuomba Savila aondoke pale chumbani. Savila aliondoka akiwa amefura kwa hasira. Iweje Robert ampandishe midadi alafu ashindwe kuishusha. Akaondoka kwa hasira kama dubu aliyeibiwa mtoto wake.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 07)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300


>>>>>>> Episode 07 <<<<<<<<<<<<

ILIPOIISHIA
kichwa cha chini kikisimama basi kichwa cha juu hugeuka kopo tupu. Robert alimshukuru Mungu kwa kumuokoa na dhambi ile ya uzinzi. Hata hivyo maneno ya Savila yalimfanya amuone kama naye ana UKIMWI. Alivaa shuka lake kisha akamuomba Savila aondoke pale chumbani. Savila aliondoka akiwa amefura kwa hasira. Iweje Robert ampandishe midadi alafu ashindwe kuishusha. Akaondoka kwa hasira kama dubu aliyeibiwa mtoto wake.

ENDELEA


Robert akabaki mwenyewe chumbani. Usingizi ulimpitia akalala fofofo kama mtu aliyekufa. Uchovu wa maswahibu ya karibia wiki nzima ulimfanya alale kama mfu. Hatimaye kulikucha. Akiwa katika mji wa Mafinga. Alijihisi nguvu mpya baada ya kupumzika kwa usiku mzima. Akaenda mpaka kwa mafundi simu akiwa na ile simu janja aliyoichukua kwenye lile gari la kifo. Alitaka akaiuze kwa bei ya kutupa ili walau apate pesa kidogo za kujikimu na nauli ya kurudi Dar es salaam. Akashtuka kuona kundi kubwa la Polisi likiwa na mwanamke aliyekuwa anamfanaanisha. Hakuwa mwanamke mwingine isipokuwa Mama Susan aliyemuona kwenye simu aliyokuwa ameibeba. Mapigo yake ya moyo yalianza kucheza sebene. Mbilinge mbilinge punde zitaanza. Moyoni alinung'unika na kulalama. Maisha ya kukimbizwa kimbizwa yalishamchosha. Alitaka kuishi kama binadamu wengine kwa amani. Adele alimfanya awe mkimbizi katika nchi yake. Mtu anayetafutwa kwa udi na uvumba kama gaidi. Akatembea kwa haraka akaingia kwenye kibanda cha fundi simu.

"Karibu ndugu yangu" fundi alimkaribisha Robert kwa lafudhi ya kihehe. "Ahsante sana. Vipi hapa mnanunua simu mbovu?"

"Simu ya aina gani ndugu"
Fundi aliongea huku akiendelea kutengeneza simu nyingine.

"Tecno camon c9 ndugu"Robert akajibu huku akiangalia nje kwa wasiwasi wa wale Polisi. Akaitoa ile simu janja aina tecno akampa fundi. Fundi aliiwasha lakini haikuwaka.
"Nafikiri imeisha chaji. Labda uibusti kwanza" Robert aliongea akimuangalia fundi aliyekuwa anaiwasha ile simu. Akaichomeka chaji simu ikatoa mwanga kwenye kioo kuonyesha inaingiza chaji. Robert alishukuru sana kuona simu ile imewaka. Sasa alijua wanaweza kufanya biashara akajipatia pesa kidogo zitakazomsaidia pale Mafinga.

"Nambie unanipa bei gani hapo fundi" Robert aliongea sauti ikiwa inatoka vizuri tofauti na awali. "Nina elfu sabini ndugu yangu" fundi akasema akiendelea kukagua mafaili ya ile simu. "Sabini! Embu acha utani fundi. Leta laki moja hapo nikuachie mzigo" Robert akasmea akijichekesha kibiashara. Punde ile simu ikaita. Moyo wa Robert ulipasuka. Aliona dili lake linaweza kufeli jambo ambalo hakuwa tayari kuona linatokea. Fundi akampa Robert ile simu ili aipokee. Robert alishtuka alipoona jina kwenye kioo cha simu. Alikuwa ni Mama Susani. Alihisi misuli ya haja kubwa ikilegea na kinyesi kikitaka kutoka. Akajikaza!. Aliikata kisha akatoa laini ya simu. Akashusha pumzi. Hakika alikuwa amechoka presha ikiwa ipo juu. Alimrudishia Fundi simu kisha akamuambia ampe hela.

"Punguza ndugu yangu. Si unajua vyuma vimekaza" fundi akasema akitoa noti za elfu kumi zilizokuwa saba mkononi mwake.

"Ongeza ishirini tumalize kazi" Robert aliongea kamawauza mitumba.

"Acha hizo ndugu. Haya chukua na hii" Fundi alimuongezea Robert noti ya elfu kumi. Jumla ikawa elfu themanini. Robert akaona isiwe tabu akaziweka mfukoni zile pesa akamuaga. Akiwa anatoka mlangoni alipishana na Polisi aliyevalia nguo za kaki na kofia. Alishtuka lakini akaficha mshtuko wake. Alimsalimia kwa tabasamu la kirafiki kisha akaondoka kwa upesi. Alijua kuwa yule Polisi alikuwa miongoni mwa wale Polisi walioongozana na Mama Susan aliyekuwa mke wa yule mtu mwenye simu aliyepigwa risasi ya kichwa. Robert alijua kabisa kuwa wale Polisi na Mama Susan walikuwa wakifuatilia mawasiliano ya ile simu. Kwa kuangalia mnara unaposoma. Kutokana na teknolojia kukua siku hizi. Simu ikiibiwa inaweza kufuatiliwa hata ikiwa imezimwa kutokana na kuwa simu nyingi siku hizi zimewekwa chipu maalumu ya kunasa eneo simu hiyo ilipo hata kama imezimwa. Hiyo ilimfanya Robert akimbilie kituo cha mabasi ya Mafinga kwa safari ya kurudi Dar es salaam.



*************************************************​


Sajenti Warioba alipiga mbizi akisaidiwa na mawimbi makubwa ya bahari mpaka ufukweni karibu na afya resort ambapo ni sehemu ya nzuri ya mapumziko. Sajenti alikuwa hoi kutokana na kupiga maji. Hata hivyo suala la kuogelea halikuwa kikwazo kwake. Sajenti Warioba alibobea katika mafunzo ya jeshi la majini. Aliweza kuyachezea maji kama papa wa baharini. Kilichomfanya awe hoi ni njaa iliyokuwa ikitafuna utumbo wake. Bado giza lilikuwa juu ya nchi yapata saa kumi usiku. Aliondoka akiwa chapachapa na kanzu aliyopewa na Joseph. Ilikuwa ni kanzu ya kijivu iliyomkaa vyema ungedhani ni ostadhi aliyefuzu visomo vyote vya juzuu. Akapita afya resort kwa tahadhari ambapo eneo lote lilikuwa kimya huku taa za maeneo yale zikimtazama. akageuka nyuma akaliona Daraja la kigamboni ambapo muda mfupi uliopita alikuwa ametoka kujirusha akiwakimbia wale watu wabaya waliotoka asikokujua. Alitembea kwa kitambo barabara zikiwa nyeupe bila ya kuwa na watumiaji isipokuwa gari mojamoja ambapo kila alipoona mwanga wa gari alijificha kwa kuogopa wale watu wabaya. Punde aliifikia barabara ya Nelson Mandela ambapo aliyaona malori yenye makontena yakitoka bandarini.

Akadandia lori moja kwa nyuma kama komando kisha akapanda juu kabisa ya kontena. Akajilaza chali uso wake ukatazama anga lililofunikwa na mawingu mepesimepesi yaliyokuwa yakipelekwa na upepo. Lile lori lenye kontena lilifika kilwa road maeneo ya uhasibu. Likakata kulia kufuata uelekeo wa kariakoo gerezani. Walikafika kariakoo Sajenti akashuka. Yapata majira ya saa kumi na moja tayari ambapo sauti za adhana zikiita waumini wa kiislamu waende kuswali. Daladala chache zilikuwa zimeanza kupiga kazi. Sajenti alishuka juu ya lile kontena la lori bila kuonekana. Sajenti akapanda daladala za makumbusho. Haikumchukua muda alikuwa kwenye stendi ya makumbusho kutokana na kutokuwa na foleni. Akatembea kwa miguu mpaka nyumbani kwake kijitonyama. Alipofika alibadilisha kwanza ile kanzu ya kijivu. Akailoweka kwenye beseni na sabuni ya unga. Akaelekea kwenye friji na kuchukua kipande cha papai ambacho tayari kilikuwa kimekatwa na kumenywa maganda. Alikirusha mdomoni kama karanga. Kisha akachukua mkate wa boflo na maziwa ya unga ya Nedo. Akakoroga chai ya maziwa kisha akaenda nayo sebuleni. Akiwa kavaa taulo tuu aliichukua laptop yake aina ya apple macbook pro with touch bar. Akaiwasha na kuchomeka ile flash aliyoichukua kule kwenye lile jumba hatari lililotaka kuinyofoa roho yake. Flash ilihitaji neno la siri ili ifunguke. Sajenti Warioba akajaribu kuingiza password mbili tatu lakini ikakataa kufunguka. Alikata tamaa. Moyoni alihisi kuwa flash ile itakuwa na mambo mazito ya siri ya wale watu. Akakumbuka maneno ya Joseph kuwa watu wale walikuwa wakifanya biashara ya viungo vya binadamu na watoto wachanga. Sasa aliona yakuwa yeye alikuwa mzembe. Kama angemuokoa Joseph huenda asingepata shida kwa kiwango kile. Aliona umuhimu wa Joseph kama angekuwa hai. Akajilaumu huku akiegemea kwenye sofa kama mtu aliyechoka. Punde aliamka kama mtu aliyekumbuka jambo muhimu. Alienda mpaka bafuni alipoiloweka ile kanzu. Aliipapasa mfukoni akakuta kile kikaratasi alichopewa na Joseph kabla ya kukata roho. Akaichukua ile karatasi ambayo tayari ilikuwa imelowana kwa maji ya sabuni ya unga. Aliikunjua taratibu ile karatasi ili isichanike kutokana na kulowana. Alikuta maandishi meusi yaliyosomeka Ambagon. Alishangaa kuona maneno; hakujua yanamaana gani.

"Huenda hii ni password ya kufungulia ile flash" Sajenti alijisemea. Akatoka akiwa na kile kikaratasi kilichoandikwa Ambagon. Akayaingiza maneno hayo kwenye sehemu ya password. flash ikafunguka. Sajenti hakuamini kama maneno yale yangefungua ile flash. Akaachia tabasamu huku akimshukuru marehemu Joseph. Alimuona Joseph ni kijana mdogo lakini aliyejaliwa akili ya kipekee sana. Lakini ndio hivyo tena aliuawa mbele ya macho yake. Akaona picha za miili ya watu waliokufa wakiwa uchi wamekatwa katwa baadhi ya miili yao. Aliwaona waliokatwa sehemu zao za siri. Akawaona waliokatwa mikono na miguu. Zilikuwa ni picha za kutisha mno. Wale watu walifanyiwa ukatili mkubwa. Alifungua faili jingine hapo aliona vitoto vichanga vikiwa uchi huku vitovu vyao vikining’inia vikiwa havijakatwa. Hapa mapigo ya moyo wa Sajenti Warioba yalianza kudunda kwa kasi. Alishikwa na wasiwasi. Akaona faili lililoandikwa POP. Akabonyeza! Ikafunguka. Aliona video moja akaibonyeza. Video ikafunguka. Macho yake hayakuamini. Aliduwaa! Aliona kwenye ile video watu waliovalia makoti meupe yaliyoandikwa Ambagon kwa nyuma yenye rangi ya bluu. Chini walivalia mabuti kama yale ya mvua yenye rangi nyeupe. Yale makoti yalikuwa na makofia waliokuwa wameyavaa kichwani. Mikononi mwao walikuwa wamevaa maglove yenye rangi nyeupe. Wote walivaa miwani meupe mithili ya daktari wa upasuaji wa neva za ufahamu. Aligundua wale walikuwa ni madaktari. Kwa idadi walikuwa wanafika kumi na mbili wakiendelea na pirikapirika katika lile jengo lilionekana linavitengo mbalimbali.

Video ilionyesha upande mwingine ambapo aliona unyama ambao hajawahi kuuona tangu azaliwe. Aliona watu wakiwa wamelazwa kwenye vitanda vyenye mashuka meupe wakiwa wamefungwa mikono yao upande huu na upande huu. Pia miguu yao ilifungwa mguu huu na mguu huu kila mmoja upande wake. Midomo ya wale watu ilikuwa imefungwa na kamba ya kitambaa chekundu. Huku wakiwa wamefunikwa kuanzia kwenye kifua mpaka mapajani kwa kitambaa cheupe. Sajenti alianza kukagua uso wa mtu mmoja baada ya mwingine. Aliziona sura zao zilivyochoka kwa mateso. Alimuona mtu mmoja akiwa amechanika chanika uso kama aliyechanwa na viwembe. Huyu alitisha sana, mtu mwenye roho ndogo asingeweze kumtazama. Lakini Sajenti Warioba roho yake ilikuwa ngumu kama ya paka hivyo alimkodolea macho kama anayezungumza naye. Punde akaona mlango ukifunguliwa. Kisha wakaingia madaktari wawili waliovalia nguo za kijani na kofia ya kijani huku pua zao zikiwa zimezibwa na kitambaa cha rangi ya kijani. Mikononi mwao wote walikuwa na magloves. Mmoja alikuwa kabeba sinia lenye mikasi, visu na vitu kama bisibisi. Pia kulikuwa na kichupa chenye rangi ya zambarau kama spirit. Walitembea miguu ikienda sawa mtihili ya wanajeshi wanaopiga gwaride. Sajenti yote hayo aliyaona kupitia laptop yake aliyoichomeka flash. Alizichunguza sura za wale watu waliofungwa kamba kitandani akagundua kuwa walikuwa na hofu sana. Kamera ilimsogeza mmoja wa watu wale. Masikini alikuwa anatoa jasho huku mapigo ya moyo wake yakidunda kwa kasi sana. “Iweje awaogope madaktari” Sajenti alijiuliza lakini aligundua lilikuwa ni swali la kijinga sana. Wale madaktari walisimama kwenye kitanda cha tatu ambapo alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa akitoa machozi huku kwikwi ikimtingisha. Wale madaktari waliovalia nguo za kijani kama madaktari wa upasuaji walipofika wala hawakuongea naye chochote yule kijana. Walikitoa kile kitambaa cheupe kilichomfunika kifuani mpaka mapajani.

"Msinikate tafadhali!. Nihurumieni…! Kaka nihurumie mdogo wako" Yule kijana alipiga kelele akiomba ahurumiwe na wale madaktari. Hata hivyo wale madaktari hawakujali ombi lake. Daktari mmoja alichukua sindano kisha akachukua kile kichupa chenye dawa ya rangi ya zambarau akainyonya kwenye sindano. Kisha akanyanyua juu na kuipiga piga na kidole cha shahada kuichanganya vizuri ile dawa. Yule kijana aliendelea kuomboleza huku akijivuta vuta kujaribu kukata zile kamba alizofungwa mkononi na miguuni. Uso wake ulitiririka jasho la kifo. Alijua dakika zijazo atakuwa marehemu. Tena marehemu aliyekufa kifo cha kinyama. Sajenti alibaki ametoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango alipomuona yule daktari akimchoma yule kijana sindano kwenye shingo. Walimgeuza shingo kwa nguvu kisha wakatafuta mshipa wa damu wa shingoni. Walipouona wakaingiza ile sindano kwenye shingo. Chwaaa! Kisha yule daktari akasukuma ile dawa yenye rangi ya zambarau.

"Uwiiiiiiiiii! Nakufa MamaMamama! Nakufa...!. Nyie ni mashetani" Yule kijana alipiga mayowe ya uchungu wa ile dawa.

Ile dawa ilikuwa ni kali sana. Ilifanya mpaka macho yake yakawa mekundu. Aliwatukana wale madaktari matusi mazito huku akiwalaani. Lakini hiyo haikumsaidia lolote. Sekunde chache kabla ya dakika. Ngozi iliacha mwili ikaanza kufutuka kama puto. Yote hayo yakifanyika yule kijana alikuwa akilia sana. Sajenti Warioba bila kujijua machozi yalitoka huku hisia zake zikimtesa moyoni. Alimuonea huruma kijana wa watu aliyekuwa akipata mateso makali dhidi ya wale madaktari wakatili wasiyo na huruma. Mwili mzima ngozi ilikuwa imefutuka. Alikufa.

Sajenti akashusha pumzi baada ya tukio la kinyama aliloliona kwenye ile video. Lilikuwa ni tukio lililomaliza kabisa nguvu zake. Akaondoka kwenye lile faili lenye ile video akaona faili jingine lililoandikwa “A”. Alitaka kulifungua lakini lilihitaji password. Akajiuliza kwa nini faili lile lihitaji password. Lilikuwa na jambo gani la siri. Na kama ni siri ilikuwa ni siri gani. Yalikuwa ni maswali yasiyo na majibu. Alijaribu kuingiza password lakini zote ziligoma. Alikata tamaa akaacha nayo. Alijipumzisha kwenye kochi akifikiria mambo yote aliyokutana nayo kwa siku tatu. Zilikuwa ni siku tatu lakini zilizobeba mambo mazito, mabaya na yakikatili. Mambo yaliyohatarisha uhai wake. Alikumbuka siku alipoenda kwenye ukumbi wa double x ilipofanyika harusi ya Adele na Robert . Harusi iliyogeuka mkosi. Alikumbuka alivyoingia kwenye ile hotel ambapo alionyeshwa video za cctv ambapo alimuona yule mtu mrefu mweusi kama msudani aliyevalia kofia. Usingizi ulimpitia tayari pakiwa pamekucha kabisa.

*************************************************​


Robert akapanda basi linalotoka mbeya kuelekea Dar es salaam. Lilikuwa ni basi zuri sana kutoka China. Basi lile lilikuwa ni double siti. Lilikuwa na televisheni kila baada ya siti tatu. Lilikuwa na sehemu ya kuchajia simu. Pia lilikuwa na kiyoyozi. Alikaa kwenye siti ya dirishani kutokana na kuwa gari lilikuwa halijajaa kwani haikuwa kipindi cha likizo au sikukuu ambapo magari hufurika mpaka abiria hupewa vigoda vya kukalia kama siyo kusimama kabisa. Akaona maandishi yaliyoandikwa kwa rangi nyekundu mwendo kasi unaua. Kisha akaona chini yake mawasiliano ikiwa dereva ataendesha kwa kasi kupitiliza watu wapige kwa namba hizo.
Akajisemea moyoni; Sasa ajali zitapungua. Maana moja ya sababu za ajali nyingi hapa nchini ni pamoja na mwendo mkali bila kufuata sheria za barabarani. Tayari walikuwa wameshapita Iringa sasa waliisogelea ilula. Luninga mule ndani ya basi zilikuwa zikionyesha filamu ya devil kingdom iliyoigizwa na nguli wa filamu Tanzania steveni Kanumba. Devil kingdom ni filamu iliyochezwa na marehemu Steven Kanumba, Pacho Mwamba, Kajala Masanja, Fatuma Makongoro na Ramsey Nouah huyu akiwa ni raia kutoka nchi ya Ghana. Baadaye waliingia Morogoro. Wakapewa dakika kumi za kuchimba dawa pale stendi ya Mabasi, Msamvu. Abiria wa morogoro wanaoenda Dar es salaam waliingia na kujaza siti zote zilizokuwa zipo wazi. Robert alirejea ndani ya gari akamkuta mgeni amekaa kwenye kiti ambacho kilikuwa wazi. Akamsalimia kisha akapita kukaa ilipositi yake ya dirishani. Wakaondoka morogoro giza likiwa limeshatanda. Magari yaliwasha taa ili dereva waweze kuona. Punde mziki ulilisikika ukiimba huku luninga ikimuonyesha msanii mmoja akiimba huku akitingisha rasta zake kichwani. Alikuwa lucky dube moja ya wasanii mashuhuri wa muziki wa regge. Robert aliutazama na kuusikiliza muziki wa lucky dube. Ulikuwa ni muziki wenye ujumbe mkubwa sana. Ujumbe ambao kama utazingatiwa dunia itakuwa salama na watu wataishi kwa amani na furaha.

Ulikuwa ni wimbo uitwao "Different colours, one people" Ulikuwa ni wimbo mzuri sana ambao ulimfanya Robert atingishe kichwa chake kama lucky dube akifuata mapigo ya regge. Kuna kipande alijikuta akikiimba akifuatana na lucky dube kwenye luninga.

" they were created in the image of god, and who are you to separate them bible says, he made man in his image, but it didn' t say black or white, look at me you see black, i look at you i see white, now is the time to kick that away and join me in my song

Saa tatu unusu Basi lilikuwa linaingia ubungo. Robert alifurahi kuliona jiji la Dar kwa mara nyingine akiwa mzima. Ilikuwa ni bahati sana kwake kurejea akiwa mzima wa afya kutokana na maswahibu yaliyomkuta. Akachukua bodaboda mpaka makumbusho alipokuwa akiishi. Alifika na kukuta geti la nyumba aliyokuwa amepanga likiwa limefungwa kwa ndani. Ilikuwa ni desturi ya wakazi wa nyumba hiyo kufunga geti ifikapo mida ya saa tatu usiku. Robert aliona asibishe kwanza hodi mpaka aende kula. Akazunguka kwa nyuma karibu na stendi ya daladala za makumbusho ambapo alikuta wachoma chipsi na mishikaki wakiendelea na shughuli zao. "Nipatie chipsi zege na mishikaki mitano" Robert akaagiza huku akitoa noti ya elfu tano mfukoni. Wale vijana walikuwa wepesi sana. Walimuandalia fastafasta kama vijana wa mjini waliobobea kwenye kazi hiyo.

"Boss unafunga au unalia hapahapa?" moja wa wale vijana alimuuliza Robert akiwa kavaa kofia nyeupe na kikoti cheupe cha upishi.

"Usifunge, nakula hapahapa" Robert akajibu akiwa anaingalia chips yake ilivyokuwa imeandaliwa kwa ufundi wa hali ya juu.

"Boss kuna vinywaji " yule kijana muuza chips aliongea huku akimuwekea Robert sahani ya chips kwenye meza.

"Leta seven up ya baridi" Robert alijibu akijivuta vizuri kwenye meza. Robert alizisifu zile chips. Ni miezi karibia nane sasa mdomo wake haukuingia chips mayai.

"Sasa hizi ndio chips" Robert alijisema kwa sauti ya chini. Huku akizikandia zile chips kavu alizokula kule Mafinga. Alimsifu mpishi wa chips zile. Alikuwa ni mpishi haswa aliyefanya mdomo wa Robert udondoze udenda kwa utamu. Akamaliza kula akalipa pesa kisha akaondoka kurudi nyumbani kwake. Bado geti lilikuwa limefungwa kama ilivyoawali. Aligonga geti mara tatu kisha sauti ya kike kutoka ndani ilisikika. "Nakuja" Robert alitulia akifikiri mawili matatu. Punde alisikia sauti ya mtu anayepiga hatua anayekuja kufungua geti. Alijiweka sawa ungedhani ni mwanafunzi anayeingia katika ofisi ya mwalimu mkuu.

"Nani?" ile sauti ya kike kutoka ndani ya geti iliongea ikiuliza.

"Ni mimi Robert Mama Rukia" Robert alijibu kwa sauti kavu. Kitendo cha Mama Rukia kusikia sauti ya Robert kilimchanganya sana. Robert huyu huyu mpangaji wake aliyegongwa na gari aina ya nisan patrol nyeupe maeneo ya sinza africana akafariki. Au ni Robert yupi huyo. Lakini sauti ilikuwa ni ileile ya Robert aliyekuwa mpangaji wake.

"Robert yupi?" Mama Rukia aliuliza kwa sauti ya kitetemeshi kutokana na woga ulioshika misuli ya midomo yake kulegea. " Robert mpangaji wako" Robert alijibu huku akigusa gusa geti kuona kama limefunguliwa.

"Mama Rukia, nakuomba ufungue"Robert alimsisitiza Mama Rukia mpaka akafungua geti. Mama Rukia alishtuka sana. Akahisi miguu ikilegea na kabla hajaanguka Robert alimuwahi. Presha ilikuwa juu sana, akapoteza fahamu. Ohoo! Robert alipagawa. Alifikiri kuwa Mama Rukia amekufa. Alianza kuhaha kama kichaa. Alijua ule mzimu wa mkosi bado unamuandama. Alimuita Mama Rukia lakini Mama Rukia alikuwa kimya akiwa kafumba macho. Alipeleka sikio lake kwenye kifua cha Mama Rukia. Huuuh! Alishusha pumzi baada ya kusikia mapigo ya moyo wa Mama Rukia. Robert alimuita mfanyakazi lakini nyumba ilikuwa kimya sana. Hii ilimuambia kuwa Mama Rukia alikuwa mwenyewe ndani ya nyumba. Akajikakamua mpaka akambeba na kumpeleka hadi sebuleni akamlaza kwenye zulia. Aliikuta sebule ni ileile aliyoiacha. Haikuwa na mabadiliko yoyote isipokuwa hakuona picha kubwa iliyokuwa ukutani ya baba Rukia. Hata hivyo hakujishughulisha na mambo yasiyomhusu. Alichukua kitambaa cha meza kubwa iliyokuwa mule ndani kisha akaanza kumpepea. Alimpepea kwa dakika tano Mama Rukia akafumbua macho. Robert akafurahi sana. Aliona ni afadhali Mama Rukia ameamka. Mama Rukia alikuwa muoga lakini Robert alimsihi asimuogope. Mama Rukia alikaa kwenye sofa akijifunga kanga zake vizuri.

"Najua wewe ni mzimu wa Robert . Tafadhali usiniue" Mama Rukia akasema hofu ikiwa dhahiri usoni.

"Hapana Mama. Mimi ni Robert halisi na wala siyo mzimu"

"Nakusihi Usinidhuru . Nitakupa kila kitu ila tuu usinidhuru
" Mama Rukia akapiga magoti akimuomba Robert .

"Mama..! Ni stori ndefu sana" Robert akasema, akimshika mkono Mama Rukia aamke.

"Wewe tumekuzika. Nami nilihudhuria kwenye mazishi yako" Mama Rukia aliongea kisha akameza fumba kubwa la mate. Maneno hayo yalimshtua sana Robert . Moyoni alijisemea inamaana mimi ni marehemu. Nimekufa na kuzikwa. Alihisi kama hajamsikia vizuri Mama Rukia.

Kufa siyo tatizo lakini kitendo cha Mama Rukia kusema hata kwenye mazishi yake alikuwepo ndicho kilimchanganya zaidi. "Mama Rukia. Mimi nipo hai. Sijafa wala sijazikwa. Mumemzika mtu mwingine nyie" Robert alisema uso wake ukiwa umekosa utulivu. Habari ile ilikuwa imemchanganya sana. "Nisubiri hapa nakuja" Mama Rukia aliongea huku akiamka akaelekea chumbani. Alimuacha Robert akiwa anatafakari habari zile za kutisha. Punde Mama Rukia alirudi akiwa ameshika bahasha ya kaki. Alimsogelea Robert akaingiza mkono ndani ya ile bahasha akatoa picha tatu.

"Tazama picha hii" Mama Rukia alimpa Robert picha moja aingalie. Robert alishtuka sana. Ile picha ilikuwa ikimuonyesha akiwa ndani ya jeneza zuri puani akiwa na pamba. Pembeni alikuwa amesimama Mama yake akiwa amevaa nguo nyeupe. Alimuona Mama yake akiwa analia sana huku akiwa ameshika mkononi kitambaa kama mtandio akipeleka mkono usoni kama mtu aliyekuwa anataka kujifuta machozi. Jeneza lake lilikuwa chini ya turubai likiwa limezungukwa na watu kadhaa waliokuwa kwenye foleni kwa ajili ya kumuaga marehemu ambaye ni yeye. Robert alikuwa mtu wa kwanza kuona watu waliohudhuria kwenye msiba wake. Yeye ndiye mtu wa kwanza aliowaona watu waliomzika. Kwa kawaida mwanadamu hajui ni nani atakayemzika na kamwe hawezi kuwaona siku atakapokuwa amekufa. Lakini Robert alivunja rekodi kwa kuona watu waliohudhuria kwenye msiba wake. Akawatazama wale watu kwenye foleni waliokuwa nyuma ya Mama yake kwenda kumuaga marehemu. Akashtuka kumuona mwanamke mmoja aliyevalia baibui jeusi akiwa amejifunika gubigubi kutoka kichwani mpaka kwenye unyayo. Alivalia kininja usoni akiwa ameachia tuu macho yake yaliyotenganishwa katikati na kitambaa cheusi kwenye mstari wa pua. Alijiuliza Yule atakuwa ni nani. Lakini hakuna aliyeweza kumjibu. Mama Rukia alipoona Robert amerizika kuiangalia ile picha ya kwanza alimpa picha ya pili. Hii ilionyesha wakati jeneza lake likiingizwa kaburini. Alimuona Mama yake alivyokuwa analia kwa uchungu mwingi. Aliwaona ndugu zake wakilia kwa uchungu sana. Alijikuta akitoa machozi kama mtoto mdogo. Nini kilimliza. Aliwaonea huruma sana Mama yake na ndugu zake. Kumbe nilikuwa napendwa hivi. Robert aliwaza kimoyo moyo huku akivuta makamasi mepesi yaliyoanza kumtoka kutokana na kulia. Picha hii pia alimuona yule dada aliyevalia baibui jeusi kama mujahidina wa kiarabu. Huyu ni nani. Au ni yule shetani Adele. Robert alijiuliza lakini kabla hajapata majibu. Mama Rukia alimpa picha ya tatu. Robert alishtuka kumuona yule dada aliyevalia hijabu akiweka ua lenye alama ya kopa kuashiria upendo kwa marehemu. Huyu atakuwa ni Adele huyu. Lakini kwa nini avae hijabu. Robert alijiuliza. Akili yake ikamuambia huenda ni kwasababu yeye ndiye chanzo cha kifo chake ndio maana aliona avae baibui ili asitambulike. Wazo hilo lilipata nguvu sana kwenye akili yake.

"Bado wewe siyo mzimu?" Mama Rukia alimuuliza Robert aliyekuwa akizitazama kwa pamoja zile picha. Kwa kweli hapo Robert alikosa majibu. Ni kweli kabisa yule aliyemuona ndani ya jeneza ni yeye mwenyewe. Alimuona pia Mama yake. Hapa alikosa cha kuongea lakini alikumbuka jambo kisha akamtazama Mama Rukia.

"Wewe ndiye uliyepiga hizi picha" Robert alimuuliza Mama Rukia huku akimtazama. Jambo hili lilimtisha Mama Rukia. Akajibu kwa wasiwasi.

"Hapana! Siyo mimi. Kuna mdada alizileta hapa" Mama Rukia aliongea huku akichukua moja ya zile picha.

"Huyu hapa ndio alileta hizi picha siku tatu baada ya mazishi yako" Mama Rukia alimuonyesha Robert yule dada aliyevaa hijabu aliyekuwa kwenye picha. Robert akaishika tena ile picha. Mara hii aliitazama kwa kitambo akijaribu kumtambua yule dada aliyevaa hijabu. Hakumtambua kabisa. Hakujua ni nani. Lakini alihisi kuwa yule dada alikuwa ni Adele. Alijua Adele ndio mtu pekee anayeweza kucheza michezo kama hiyo.

"Alisema yeye ni nani..?"

"Hakujitambulisha jina lake. Alinipa akanitishia" Mama Rukia alidakia maneno ya Robert . "Alikutishia?"

"Yaani! Wewe acha tuu! Alinambia nikae na hii bahasha"


"Alafu" Robert aliongea huku akiongeza umakini kumsikiliza Mama Rukia. "Akanambia siku ukija wewe nikupe" Mama Rukia aliongea akiwa anamtazama Robert . Kimya kidogo kilitokea kisha Mama Rukia akaendelea.

"Akanambia nisipofanya kazi hii atanifanya jambo baya"

"Hukumuambia nimekufa?" Robert aliuliza kama swali la nyongeza.

"Nilimuambia ila akasema nikae na hiyo bahasha siku ukija nikupe, pia akasema hata yeye alijua umekufa kama mimi nijuavyo, lakini akasisitiza nikupe siku utakayokuja. "

Mama Rukia alimaliza kuongea akijifunga kanga yake iliyokuwa inaachia achia kutokana na mwili wake ulifungashia huko nyuma. Robert alichanganyikiwa sana. Picha alizoziona na maneno ya Mama Rukia vilivuruga medula oblungata yake. Alikuwa na maswali mengi kuliko majibu. Ikiwa yeye alikufa akazikwa iweje alijikuta ndani ya kontena la gari lenye maiti. Je kaburi lilifukuliwa. Alijiuliza lakini hakupata majibu. Ikabidi amuulize Mama Rukia.

"Kaburi langu halikufukuliwa"

"Mimi sijui. Lakini lingefukuliwa ningesikia kwenye vyombo vya habari" Mama Rukia akasema akiwa anapiga miayo ya usingizi. Kama hiyo haitoshi. Kilichomvuruga zaidi ni habari za yule mwanamke mvaa hijabu aliyemuona kwenye picha alizopewa na Mama Rukia.

alinambia ukija nikupe" maneno ya Mama Rukia yalipita katika kichwa cha Robert . Yalikuwa maneno machache lakini yalikuwa mazito.

"Ndugu zako walikuja kuchukua vitu vyako kwenye nyumba yako "

Mama Rukia aliongea hali iliyomfanya Robert aache kufikiri na amuangalie.

"Unasema nini Mama Rukia?"

"Vitu vyako vimechukuliwa na ndugu zako"

"Uliwapa kwa nini?" Robert akasema..

"Niliwapa kwa nini! Sasa vingebaki hapa kufanya nini wakati wewe ulikufa"
Mama Rukia alijibu akionyesha kukerwa na swali la Robert . Kitambo kidogo kilipita hakuna aliyeongea kitu. Robert alianza kuwaza tena.

"Ila usijali utapata pa kupumzika tuu" Mama Rukia aliongea huku akiondoka kwenda kumuandalia Robert chumba cha kulala.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel


 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 08)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300


>>>>>>> Episode 08 <<<<<<<<<<<<

ILIPOISHIA

Vitu vyako vimechukuliwa na ndugu zako"
"Uliwapa kwa nini?" Robert akasema..
"Niliwapa kwa nini! Sasa vingebaki hapa kufanya nini wakati wewe ulikufa"
Mama Rukia alijibu akionyesha kukerwa na swali la Robert . Kitambo kidogo kilipita hakuna aliyeongea kitu. Robert alianza kuwaza tena.
"Ila usijali utapata pa kupumzika tuu" Mama Rukia aliongea huku akiondoka kwenda kumuandalia Robert chumba cha kulala.

ENDELEA

Mwanamke mmoja aliyevalia hijabu gubigubi aliingia ndani ya gari aina ya Rav4 ya kijivu. Aliwasha gari kisha akaendesha polepole geti likifunguliwa na mlinzi. Alimpungia mlinzi mkono kupitia dirisha la gari akatoka. Alikuwa akiishi maeneo ya msasani macho. Alichukua muekeleo wa ubalozi wa marekani, akatokea makutano ya morocco karibu na jengo la airtel. Akiwa ndani ya gari alikuwa mwingi wa mawazo. Aliendesha kama mtu asiyeona. Punde akachukua kawawa road ambapo alitembea kwa dakika tano akakata kinondoni road kuelekea yalipo makaburi ya kinondoni. Akafika eneo la makaburi akashuka ndani ya gari. Moja kwa moja alitembea akiwa kashika baibui lake lilisiburuzike chini kwenye vumbi. Akasimama mbele ya kaburi lililoandikwa Robert Gabriel. Machozi yalianza kububujika yakilowesha kitambaa kichofunika uso wake. Aliliangalia lile ua aliloliweka siku ya msiba. Uchungu ulimkaba kooni akaanza kulia kwa kwikwi huku sauti ndogo ikitoka. Akainama chini akashika mchanga wa lile kaburi akasimama akiwa mkononi kabeba mchanga wa lile kaburi. Kisha akaongea kama mtu anayeomba dua.

"Umepeperushwa na upepo wa hila. Umepeperushwa kama vumbi lipeperukavyo" Hapa alisema huku akiwa akiachia kidogo kidogo mchanga aliokuwa ameubeba mkononi. Ule mchanga ukawa unapeperushwa na upepo kuelekea upande wa msalaba wa lile kaburi. Punde akiwa amebakiza mchanga kidogo alihisi kichefuchefu. Alishika tumbo lake kisha akainama na kuanza kutapika. Alitapika kama mgonjwa wa malaria. Looh! Alitapikia kaburi la Robert karibu na ua aliloliweka siku ya msiba. Alikuwa ameinama chini bado. Kichefu chefu kilimchefua akachefuka mpaka akatapika alichokula jana na juzi. Alikuwa hoi taabani. Unapotapika unapoteza maji mengi mwilini hivyo nguvu za mwili huisha ndivyo ilivyokuwa kwake. Punde Mama Rukia na Robert wakiwa wameongozana kuja kumuonyesha Robert kaburi lake. Wakiwa umbali kama wa mita thelasini na tano Mama Rukia alisimama ghafla. Na Robert naye akasimama akiwa mbele kwa hatua tatu. Alimtazama Mama Rukia alimkuta akiwa kaduwaa kama mtu aliyeona kitu cha kushtusha. Akaangalia mbele kule alipokuwa akitazama Mama Rukia. Akaona mwanamke aliyevaa hijabu jeusi gubigubi akiwa kainamia kaburi. Akili ya Robert ilimuambia kuwa yule ni mchawi. Kama siyo mchawi basi ni jini. Sasa alijua ni kwa nini Mama Rukia alikuwa ameshikwa na butwaa lile. Alihisi mwili ukipanda joto la wasiwasi. Robert tokea azaliwe hakuwahi kumuona mchawi wala hakuwahi kuona jini. Lakini leo kwa macho yake amekutana na kile alichokuwa anaamini ni mchawi kama siyo jini. Mama Rukia akili yake ilikosa utulivu. Iliteleza katika mishipa yake ya ubongo. Akili yake ilimuambia kuwa kuna mchezo anachezewa. Ilimuambia asipokuwa makini leo inaweza kuwa ndio mwisho wa uhai wake. Aligeuka nyuma akaanza kukimbia kurudi walipotoka. Heee! Robert alishangaa kuona Mama Rukia anakimbia. “Anakimbia nini”. Hakuwa na muda wa kujibu swali hilo. Alihisi kuna hatari inakuja. Tena siyo hatari ndogo bali hatari inayohatarisha maisha. Ukizingatia ameona mtu aliyeinamia kaburi akiwa kavaa nguo nyeusi kama hijabu. Naye akanza kukimbia akimkimbilia Mama Rukia. Mama Rukia kuona Robert anamfuata akiwa anamkimbilia. Aliongeza mwendo. Pamoja na ubonge wa Mama Rukia lakini haikumzuia asikimbie kwa kasi. Ungedhani ni kiboko anayekimbia. Hiyo yote ni kutokana na kuhisi jambo la hatari. Wataalamu wanasema, mtu anapoona jambo la ghafla na la hatari tezi ya adrenali huzalisha homoni zinazomfanya mtu afanye mambo nje ya uwezo wa kawaida ili akabiliane na hatari inayomkabili. Ndivyo ilivyokuwa kwa Mama Rukia. Alikimbia kwa kasi tofauti na mwili wake.

Robert kuona Mama Rukia akiongeza kasi alihisi hatari imewakaribia zaidi na ipo mgongoni mwake. Hakuna mwingine aliyekuwa nyuma isipokuwa yeye. Alijiuliza kama mtu wa mbele anakimbia kwa kasi ile. Yeye wa nyuma aliyekuwa karibu na hatari anapaswa akimbieje. Akaongeza kasi kama siku alipokuwa akikimbizwa na wale watu waliotaka kumuua kwa kumpiga mawe alipokuwa akimpiga Adele maeneo ya hapohapo kwenye makaburi ya kinondoni. Akaongeza kasi zaidi akafikia ile kasi aliyokuwa akiwakimbia wale watu wawili dereva na daktari wa ebola waliokuwa wamebeba maiti kule porini.. Alimfikia lakini kabla hajampita Mama Rukia akaanguka chini baada ya kujikwaa. Alianguka kama mti uliopigwa shoka la mwisho. Robert alifunga breki kama magari ya mashindano hali iliyofanya atimue vumbi. Aliangalia nyuma lakini hakuona mtu anayewafuatia. Alimsogelea Mama Rukia aliyekuwa ameanguka pale chini.
"Tafadhali! msiniue Robert mwanangu msiniue" Mama Rukia akasema kwa tabu akitweta tweta hovyo kutokana na kukimbia sana.

"Nani wanakuua, mimi sikuui Mama Rukia" Robert aliongea akishika bega la Mama Rukia “Mnataka nini? Au mmetumwa na baba Rukia" Mama Rukia alitweta akiwa anaongea uso wake akiwa kauficha chini ya ardhi ili asimuone Robert . Alikuwa akimuogopa Robert muda ule. Alimuona kama mzuka.

"Ninyi ni mizimu! Semeni mnataka nini!" Mama Rukia aliongeza.

"Mzimu hauna mwili kama huu Mama Rukia"

"Bali unamwili kama wa yule mwanamke?"

"mwanamke?"

"Usinifanye mimi mtoto mdogo Robert" Mama Rukia alisema kama mtu aliyekata tamaa na yupo tayari kwa lolote.

Robert alikuwa haelewi Mama Rukia alikuwa anaongelea nini. Hata hivyo Mama Rukia naye alikuwa anaamini kuna njama Robert anaifanya ili wamuue. Mama Rukia aliamini Robert alikuwa mzimu kwa kile alichokiona kwenye lile kaburi.

"Unajua sikuelewi Mama Rukia"

"Utaelewaje wakati mmepanga kuniua"


"Tukuue!"

"Niueni! Niueni tuu!"

Mama Rukia sasa hakuwa anaongea tena bali alikuwa anapayuka kama mtu aliyepagawa. Aliongea akiwa kainuka akakaa kumtazama Robert aliyekuwa kainama.

"Tukuue? mimi na nani?"

"Nakuambia niueni. Yaani ulitaka nikulete kaburini asubuhi asubuhi ili mje mniue na yule mwanamke"

Mama Rukia aliongea kama Mama wa kiswahili muda huu. Aliongea akinyoshea kule kaburini walikomuona yule mtu aliyeinamia lile kaburi. Robert alianza kuelewa kile alichokuwa anakizungumza Mama Rukia. Akasimama akaangalia kule alipomuona yule mwanamke aliyevalia nguo nyeusi akiwa kainama kwenye kaburi. Alimuona yule mwanamke aliyevalia hijabu jeusi akiwa amesimama. Robert alishtuka alipomuona vizuri. Alikuwa ndiye yuleyule mwanamke aliyemuona kwenye picha alizoonyeshwa na Mama Rukia. Mapigo ya moyo wake yalibadili mwelekeo kama bendera inayofuata upepo wa kipindi cha kipupwe. Alitaka kujua yule alikuwa ni nani. Anafanya nini pale makaburini. Na lile ni kaburi la nani. Yule mwanamke aliyekuwa kavaa hijabu jeusi akiwa amejifunika gubigubi usoni aliondoka kaburini kuelekea alipopaki gari lake aina ya rav4. Robert kuona hivyo alianza kumfuata kwa hatua ndogo ndogo kama mtu aliyepumbazika. Mama Rukia alibaki kumshangaa Robert aliyekuwa akimuacha pale chini. Robert aliongeza kasi alipomuona yule mwanamke akiwa amelifikia gari lililopaki na kuingia ndani. Alianza kulikimbilia kwa kasi kumuwahi yule mwanamke kabla hajaondoka. Mama Rukia aligeuka mtazamaji wa filamu hiyo isiyokuwa na muongozaji ingawaje ilivutia. Yule mwanamke aliyevalia hijabu jeusi akiwa gubigubi tokea utosini mpaka unyayoni alitia gia. Gari likiwa linaondoka punde kioo cha dirisha kiligongwa kwa pupa. Yule mwanamke aligeuka upande wa dirisha palipogongwa. Alishtuka sana. Alimuona Robert . Hakuamini macho yake.

Walibaki wametumbuliana macho bila kusemeshana. Yule mwanamke alimtambua aliyekuwa kwenye kioo cha dirisha la gari ni Robert lakini Robert hakuwa amemtambua mwanamke aliyekuwa akimtazama aliyevaa hijabu.

"Naomba ufungue mlango" Robert aliongea akijaribu kufungua mlango wa gari. Yule mwanamke hakumjibu kitu zaidi ya kumtazama. Alitamani hata aisikie sauti ya yule mwanamke lakini ni kama alikuwa akiongea na bubu. Yule mwanamke alinyamaza kama bubu wa kuzaliwa.

Punde yule mwanamke alitia gia lile gari na kuliondoa taratibu taratibu. Robert alilifukuzia gari dirishani huku akigonga kioo cha gari. Gari liliongeza mwendo na kumuacha Robert akipepesuka kwa kutaka kuanguka. akabaki akilitazama gari likiyoyoma mithili ya kuku atazamaye mwewe aliyebeba kifaranga chake. Alilisindikiza kwa macho huku gari nalo likimuaga kwa vumbi. Robert alishtuka bega lake likishikwa kwa nyuma. Kabla hajavuta pumzi sauti kutoka nyuma ilifuatia.

"Mbona kakukimbia Robert?". Sauti ya Mama Rukia kutoka nyuma iliyapapasa masikio ya Robert aliyekuwa akidhihakiwa na vumbi la lile gari la yule mwanamke mvaa hijabu. Akamgeukia Mama Rukia. Akalakiwa na uso wa umbeya uliokuwa na kiu ya kujua ni kwa nini yule mwanamke aondoke bila kumsikiliza. Waliondoka pale kurudi nyumbani. Wakiwa ndani ya gari hakuna aliyetaka kuzungumza. Aliyekuwa akiendesha gari alikuwa Mama Rukia. Mama Rukia alikuwa akimchungulia mara kwa mara Robert kupitia kioo cha dereva cha ndani. Alimuona Robert akiwa kwenye lindi la mawazo. Aliuona uso wa Robert ukiwa na simanzi kubwa. Alitaka kumuuliza lakini kabla hajafanya hivyo ghafla kwa mbele umbali wa mita kama mia wakiwa maeneo ya magomeni kanisani waliona kundi kubwa la vijana waliofunga barabara wakiandamana. Mama Rukia alisimamisha gari nyuma ya gari nyingine iliyokuwa mbele. Wasingeweza kupita kutokana na barabara kufungwa kwa mbele. Waandamanaji waliwafikia wakiwa wamebeba mabango yao juujuu huku wakiimba nyimbo za kudai haki zao. Robert alichungulia kwenye dirisha kusoma mabango ya wale waandamanaji. Aliona bango moja lenye picha ya kiongozi mmoja aliyevalia suti juu yake kukiwa na maandishi yaliyosomeka. "Huyu ndiye kiongozi wetu aliyeshinda" inaonekana kulikuwa na uchaguzi hivyo ndiyo Robert aliwaza. Mara akaona watu wakipasua vioo vya magari yaliyombele ya gari lao. Akili yake ilikosa utulivu. Alifikiri afanye nini ili ajinasue na hatari ile. Akamtazama Mama Rukia aliyekuwa naye akishangaa ujio mpya wa tukio lile la unyang'anyi. Robert alishuka kisha akasimama pale mlangoni akiangaza macho yake kuangalia wapi usalama ulipo. Eneo lote la magomeni kanisani liliukuwa limechafuka. Wale waandamanaji kumbe ndani yao lilikuwepo kundi la wezi ambao walikuwa wanafanya wizi na kuumiza watu. Wale watu walikuwa wanawachoma watu visu kama hutakuwa na kitu cha kuwapa. Akili yake ilimuambia warudi walipotoka.

"Shuka tukimbie huoni watu wanaumizwa" Robert aliongea huku akimuangalia Mama Rukia kwa macho ya kusisitiza kuwa watoke. Wakatoka na kuanza kukimbia. Walikimbia wakaingia njia iendayo sinza kupitia tandale iliyopo pale magomeni kanisani.

*************************************************​


Giza lilifunika mji wa Dar es salaan. Sauti za viumbe wa usiku na sauti za magari ya watu wanaorudi makwao kutoka ofisini zilikuwa sikikisika. Adele alikuwa ameketi kwenye nyumba yake iliyokuwepo mbezi beach akitazama luninga. Alikuwa yupo na mwanaume mmoja aliyekuwa yupo bize na laptop. Punde luninga ilitoa sauti ya muziki ulioashiria kuwa ni muda wa taarifa ya habari. Jambo hilo lilifanya Adele awe makini kusikia habari zilizojiri mchana wa siku ile. Pia yule mwanaume aliacha shughuli zake na ile laptop akaja karibu na Adele kusikiliza taarifa ya habari.

"Wafuasi wa chama cha upinzani wafanya maandamano kupinga matokeo ya Ubunge. Wawili wauawa kumi wakiambulia majeraha. Rashid juma ripota wetu anayotaarifa kamili" Alikuwa ni mtangazaji wa taarifa ya habari aliyekuwa akiongea. Macho ya Adele na yule mwanaume yalikuwa makini bila ya kupepesa pepesa macho. Adele alishtuka alipoona sura ya Robert kwenye taarifa ya habari. Alimuona akikimbia akiwa amemshika mwanamke mmoja ambaye Adele hakuwa akimfahamu. Alishtuka kumuona Robert aliyeamini kuwa amekufa. Alijuliza inawezekana vipi mtu aliyekufa amuone tena akiwa hai. Alihisi kuota lakini haikuwa ndoto. Lilikuwa ni jambo la kweli kabisa. Yule aliyemuona kwenye habari hakuwa ni katuni bali alikuwa ni Robert kabisa. Adele akamtazama yule mwanaume ambaye naye alikuwa akitazama taarifa ya habari. Adele alitamani atoke muda uleule mbezi beach akamtafute Robert lakini hiyo haikuwezekana. Akili yake ilimwambia kuwa atawezaje kwenda muda ule ilhali lile tukio limetokea mchana. Akakumbuka ile siku aliyopigwa na Robert kipigo cha paka shume. Roho ya kisasi ikamvaa kwa nguvu. Kitendo cha Robert kugongwa na nisan patrol pale Africana kilivuruga mipango ya Adele.

Adele alitaka kumkamata Robert akiwa mzima mzima ili amtese kwa mikono yake mwenyewe.

SURA YA NNE


Sajenti Warioba alichoka roho na akili. Mambo aliyoyaona yalikuwa mambo yakutisha sana. Hakuwahi kuona mtu akichunwa ngozi tokea azaliwe. Leo hii kwa macho yake kupitia flash aliyoiiba kwenye lile jumba la watu wabaya. Amejionea mtu akichunwa kama mbuzi. Tena aheri mbuzi yeye huchunwa ngozi akiwa ameshachinjwa akafa lakini yule mtu alichunwa ngozi akiwa hai na nguvu zake. Looh! Usingizi ulimtongoza Sajenti Warioba lakini alisimama akajinyoosha mithili ya paka afukuzavyo usingizi kwa kujinyoosha. Angewezaje kulala ilhali uchunguzi wake haujakamilika. Mpaka muda ule hakupata la maana katika uchunguzi wa aliyeharibu harusi ya Robert na Adele. Hakupata muelekeo wowote wa aliyemuua Ramla siku ile ya harusi. Matokeo yake alikumbana na mambo yakutisha yaliyohatarisha uhai wake. Sajenti aliupapasa uso wake uliokuwa na majeraha ya wale siafu wabaya wa yule mtu mweusi mwenye roho ya mamba. Aliushika mdomo wake uliopasuka kutokana na kupigwa ngumi na lile jitu jeusi. Kisha akaingia chumbani kubadili nguo. Akavaa suruali ya kadeti ya rangi ya kaki na tisheti nyeusi aliyoichomekea vyema. Kichwani alivalia kapero nyeusi. Alichukua koti lake kama la makoti ya mvua akalivaa. Alijitazama kwenye kioo huku akiiweka kofia yake vizuri. Juu ya kabati aliichukua bastola yake. Aliikagua bastola kama ina risasi akaona zipo za kutosha. Aliitia bastola kwenye mkoba wake uliopo kiunoni. Sasa alirizika akatoka nje. Alizunguka mpaka ilipo pikipiki yake aina ya boxer. Akaikagua kama inamafuta ya kutosha. Yalikuwepo. Akatoka nyumbani yapata majira ya saa tatu asubuhi. Akiwa anapita njiani aliona watu wakiwa wamezunguka sehemu ya kusomea magazeti. Kuna nini pale. Mbona watu wengi. Sajenti alikuwa akifikiria akiwa anaendesha pikipiki yake huku koti lake likipepea kama bendera. Akili yake ikamtuma asimame naye aone ni jambo gani lililokusanya watu wote wale. Alisimamisha pikipiki hatua kumi kutokea wale watu waliposimamia. Akatembea mpaka lilipo lile kundi akasimama nyuma ya watu wale. Alipeleka macho yake mpaka kwenye meza ya magazeti. Macho yake yalikutana na habari ya kushangaza. Ni habari hii ndiyo iliyowafanya watu wengine wakusanyike pale. Aliona picha ya gari lake likiwa kwenye Daraja la kigamboni. Ni lile gari aliloliacha jana usiku kwenye Daraja la kigamboni alipojirusha baharini.

Chini ya lile gazeti kuliandikwa maneno yaliyosomeka "jambazi laua mtoto lajitosa baharini"
moyo wa Sajenti ulilipuka kama moto wa gesi. Alihisi akili yake ikimkimbia huku nguvu zake zikijificha kwenye pembe za viungio vya magoti. Akanunua lile gazeti akasogea pembeni karibu na pikipiki yake. Kisha akatafuta ile habari akaiona ukurasa wa nne wa lile gazeti.

"jambazi hilo ambalo bado jina lake halijafahamika . Pia limesababisha mauaji ya kijana aliyejulikana kwa jina moja, Joseph. Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kufuatia tukio hilo la kinyama." Yalikuwa ni maneno yaliyoandikwa ndani ya lile gazeti. Sajenti hakuamini, aliuona mwili kama gunia la chumvi. Mwili wake ulitokwa jasho jingi kama mgonjwa wa homa kali.

"Haiwezekani! Mimi sijamuua Joseph. Alalalaaa!" Sajenti aliongea kwa sauti ya chini. Kiasi kwamba mtu aliyekuwa anapita karibu yake akasikia. Yule mtu alishangaa kumsikia Sajenti akiongea mambo ya mauaji akiwa pekee yake na gazeti. Sajenti alimuona yule mtu akimtazama huku akitembea taratibu kwenda mbele.

"Unashangaa nini mwanaume mzima. Angalia mbele utagongwa" Sajenti alimkoromea yule mtu aliyekuwa akimtazama. Yule mtu kwa aibu aliondoka akiwa na donge la uhondo wa kutaka kujua kuwa kwa nini Sajenti Warioba aliongea maneno yale. Sajenti aliondoka na lile gazeti akifuata uelekeo wa ubungo. Alifika ubungo akasimamisha pikipiki mbele ya kituo cha bodaboda. Akamuita bodaboda mmoja.

"Habari kaka" Sajenti alisalimia huku pikipiki yake ikinguruma tukutukutuku!.

"Salama tuu kaka" Dereva bodaboda alimjibu akimtazama Sajenti kwa udadisi.

"Samahani! Unaifahamu hospitali ya Ambagon" Sajenti Warioba aliuliza.

"Ahaa! Ile ya wareno?"

Bodaboda aliongea kama mtu anayeifahamu. Jambo ambalo lilimfanya Sajenti Warioba ajibu bila kufikiri.

"Yeah hiyohiyo" Sajenti akajibu kama mtu anayeifahamu hiyo hospitali,wakati ndio mara ya kwanza anasikia inamilikiwa na wareno.

"Ipo pale Riverside. Ukifika tuu utaona jengo la ghorofa lenye rangi ya kahawia. Juu kuna bango kubwa limeandikwa Hospitali ya Ambagon" yule bodaboda alitoa maelezo yaliyomridhisha Sajenti Warioba. Sajenti akaaga akaondoka kuelekea riverside. Alipofika aliliona jengo la kahawia lenye ghorofa sita kwenda juu. Juu kabisa kulikuwa na bango kubwa lenye maandishi yaliyosomeka hospitali ya Ambagon alafu chini yake kulikuwa na maneno ya kireno 'hospital em Ambagon'. Akapunguza mwendo akakatisha kulia kufuata barabara inayoelekea kwenye lile jengo la hospitali. Punde akaliona geti la ile hospitali. Moyo wake ulipoteza utulivu kama mtu aliyeona jambo la hatari. Aliona mlinzi kwenye kijumba chake. Ndani ya geti aliona watu waliovalia nguo za kijani, nyeupe na makoti meupe wakiwa katika pirika pirika zao. Aligundua kuwa wale watakuwa Wauguzi na madaktari wa ile hospitali. Aliwaona pia madaktari wakizungu wakiingia na kutoka. Huku wengine wakipita kwenye korido ndefu za ile hospitali. Mbele kabisa mule ndani kulikuwa na sehemu ya kuegesha magari ambapo aliyaona magari yakiwa yamepaki pamoja na gari nne za kubebea wagonjwa zenye msalaba mwekundu. Aliendelea kuchunguza akiwa nje kabisa ya geti ng'ambo ya pili ya barabara akijifanya anaongea na simu. Punde aliona prado nyeusi ikiingia mule hospitalini. Aliifuatilia kwa macho mpaka iliposimama eneo la kuegeshea magari. Macho yake yalikuwa tayari kumuona atakayeshuka mule ndani ya gari. Akiwa katika kushangaa sauti ya mlinzi ilivuruga muono wake.

"Habari boss. Umesimama muda mrefu hapa. Hujasoma lile tangazo, haturuhusu mtu kusimama hapa"
Yule mlinzi alizungumza akimuonyesha Sajenti kibao chenye tangazo. Sajenti aliyapeleka macho yake kwenye lile tangazo. Ambalo lilikuwa linamaneno.

"Você não tem permissão para ficar aqui" Alafu chini yake yaliandikwa maneno ya kiswahili yaliyosomeka.
"Huruhusiwi kusimama hapa" Maneno ya juu ni lugha ya kireno.

Sajenti akababaika baada ya kusoma ujumbe wa kile kibao. Kabla hajajibu kitu macho yake yalipumbaa alipomuona aliyekuwa ameshuka kwenye lile gari. Alimuona yule Mama bonge aliyemuona kule kwenye lile jumba alilokuwa ametekwa na kupewa kipigo kibaya na yule mtu mweusi kama mkaa. Yule Mama aliyekuwa akimrubuni marehemu Joseph. Kitendo cha Sajenti kuduwaa kwa kumuona Mama bonge kilimfanya yule mlinzi amshtukie. Mlinzi aligeuza shingo yake kutazama kule alipokuwa anaangalia Sajenti Warioba. Naye alimuona yule Mama.

"Mbona unamuangalia BLM, unashida naye" yule mlinzi alimuuliza Sajenti Warioba. Sajenti alimtazama mlinzi. Jina BLM siyo mara yake ya kwanza kulisikia. Alimsikia Joseph akilitaja siku ile alipokuwa amejificha kwenye ua wakati wakiwa wanatoroka. Leo mlinzi naye amelitaja jina lilelile. Alizidi kushangaa ila wakati huu akajifanya kama mtu aliyekuwa amepumbazwa tuu na maumbile ya BLM.

"Kuna wanawake jamani. Mzigo wote ule" Sajenti aliongea huku akimsifia BLM aliyekuwa akiingia katika jengo moja hospitalini.

"Huyo ndiye BLM boss. Mke wa daktari mkuu wa hospitali hii" mlinzi aliongea akimsifia Mama bonge kana kwamba wanauhusiano wa karibu.. Punde BLM alitoka kwenye lile jengo alilokuwa ameingia. Bila kutarajiwa waligongana macho na Sajenti Warioba. Wote walibabaika kama watu waliokuwa wakitafutana kwa muda mrefu na leo wamekutana bila kutarajia. Kama maadui waliohasimiana kwa miaka mingi na leo wapo kwenye ulingo wa vita. Sajenti alizuga akamuaga yule mlinzi. Akawasha pikipiki yake akaondoka. Mlinzi alibaki ameduwaa.

Ghafla BLM alimuita. "Ulikuwa unaongea nini na yule mtu?" BLM akamuuliza mlinzi ambaye sura yake ilikuwa imezingirwa na hofu ya mtumishi kwa boss wake.

"Alikuwa kasimama pale nje. Ndio nikaenda kumuuliza kwa nini kasimama muda mrefu eneo hili"
"Akakujibuje?"
"Kabla hajanijibu wewe ndio ukatokea"

“Wewe usinitanie! Hakuna lolote mliloongea?"
BLM aliongea akiwa ameyatoa macho yake kwa ukali. Jambo ambalo lilimfanya mlinzi awe kama mbwa koko aliyekutana na fisi pori.

"Kweli boss. Hakuongea lolote" Mlinzi alisema kwa sauti ya unyonge huku kirungu alichokishika kikimdharau kikaanguka. Iweje mlinzi aliyehitimu mafunzo ya kijeshi anywee kiasi kile. Ndio maana kirungu kikadondoka. Sajenti Warioba aliingia mtaa wa pili ambapo aliona hotel nzuri ya kifahari. Alimuomba mhudumu wa ile hotel ampe chumba kilichopo ghorofa ya juu kabisa. Akalipa pesa za chumba kisha akapanda juu kwa kutumia lifti. Alifika kwenye chumba namba 66 akaingia. Kilikuwa chumba kikubwa kilichobeba choo na bafu. Kulikuwa na kitanda kikubwa cha nane kwa nane. Juu ilikuwepo feni ya rangi nyeupe pamoja na sofa la watu wawili karibu na dirisha. Aliridhika na mazingira ya chumba kile. Alivua koti lake akaliweka kitandani kisha akaenda dirishani akachungulia. Aliiona hospitali ya Ambagon ikiwa imepakana na hotel aliyochukua. Hapa sasa alijihakikishia kwamba uchunguzi wake utaenda vizuri. Alianza kupepeleza hospitali ya Ambagon akiwa pale dirishani juu ya ghorofa ya 12 chumba namba 66. Aliona eneo lote la hospitali. Lilikuwa ni eneo kubwa.

Hakuona upande wa mbele wa hospitali kule alipomuona BLM kutokana na kuzuiwa na jengo la ghorofa la ile hospitali. Akarudi kitandani akajilaza akitafakari namna atakavyofanya kazi yake. Aliamini kuwa hospitali ile itakuwa imejaa mambo mazito. Usingizi ulimpitia kutokana na kuwa hakulala usingizi mzuri kwa siku nne. Usingizi ulimchukua mpaka saa kumi na mbili jioni ambapo alizinduka. Alishangaa kuona muda ulikuwa umeenda. Akaitazama saa yake ya mkononi ambayo ilimuambia kuwa ni saa kumi na mbili unusu. Akamka haraka akakimbilia dirishani. Bado giza lilikuwa halijaingia. Njaa ilianza kulichokoza tumbo lake. Alihisi kutaka kula. Akaenda karibu na kisanduku cha simu ya mezani ambacho kilikuwa mule ndani. Akapiga simu akaagiza samaki wawili wakubwa na chapati. Dakika kumi hazikuisha mlango wa chumba chake uligongwa. Aliuendea akaufungua ambapo alipokelewa na uso wa mwanamke aliyevalia sare zilizonyooshwa vizuri kwa pasi. Mwanamke yule alikuwa amebeba sinia kubwa juu yake kukiwa na sahani ya samaki na chapati.

"Samahani kaka. Nimekuletea chakula ulichoagiza" Yule mhudumu wa kike aliongea kwa sauti ya adabu yenye taaluma ya ukaribu kwa wateja. Sajenti Warioba alilipokea lile sinia akimkaribisha mhudumu aje ili wale wote. Mhudumu hakukubaliana na ombi la Sajenti. Alimshukuru kwa adabu ya kibiashara na akamuaga. Sajenti alirudishia mlango na moja kwa moja alienda lilipo sofa lililokuwa karibu na dirisha mule ndani akakaa. Alianza kufakamia msosi alioletewa. Kilikuwa chakula kitamu sana. Samaki alikuwa amekaangwa vyema sana. Chapati nazo zilikuwa tamu na laini. Sajenti aliridhika na mlo wa hoteli ile. Akamaliza kula sasa alikuwa na nguvu. Muda wa kazi ulikuwa umefika yapata majira ya saa moja na nusu giza likiwa limeingia kabisa. Alichungulia dirishani ilipo hospitali ya Ambagon. Mzunguko wa watu ulikuwa umepungua. Walikuwepo watu wachache waliokuwa wakitembea katika viunga vya hospitali ile. Akachungulia nje upande wa chini akiwa juu ya gorofa ya kumi na mbili kuelekea kwenye ile hospitali. Aliona mti wa mkuyu mule ndani. Alifungua dirisha la kioo kisha akatoa kiwili wili chake nje. Alikuwa akipiga mahesabu ya kuruka kule chini kwenye ule mti wa mkuyu uliokuwa mule hospitalini. Kulikuwa ni mbali asikuambie mtu. Kutoka ghorofa ya kumi na mbili kuruka mpaka chini ilihitaji uwe na moyo mgumu kama chuma. Lakini Sajenti aliona hiyo ndio njia pekee anaweza kuitumia kuliko kushuka chini kabisa na kupitia getini ambapo angeulizwa maswali mengi. Njia pekee aliyoiona itafaa kwa wakati ule ni kujirusha kwenye ule mti wa mkuyu. Hapa ni lazima achunge sana. Asije akadhani ni vile alivyojirusha baharini. Hapa akikosea kidogo kudaka tawi atajikuta chini matumbo yake yakiwa yamepasuka. Sajenti alihesabu moja, mbili tatu huyo akaruka kuelekea kwenye ule mti. Kama nyani, alivunja vunja matawi akiwa anadondoka mpaka alipolidaka tawi la mkuyu na kulala juu yake. Alipata michubuko kidogo tumboni na mkononi. Kunguru waliokuwa kwenye ule mti wa mkuyu waliruka na kuanza kupiga makelele. Jambo ambalo lilimshtua mlinzi. Mlinzi aliyekuwa mbele kabisa aliamua kuzunguka nyuma kabisa ya jengo la hospitali ambapo wale kunguru walikuwa wakizunguka ule mti. Sajenti alishtuka kuona mwanga wa tochi ukija kule alipokuwepo. Alimuona mlinzi akimulika juu walipo wale kunguru waliokuwa wakiruka ruka huku wakipiga kelele. Yule mlinzi alifika chini ya ule mti wa mkuyu ambapo alishangazwa kuona majani na matawi madogo madogo yakiwa yameanguka chini. Muda wote Sajenti alikuwa amejificha juu ya mkuyu akiwa kabana pumzi kama yupo kwenye maji ya kina kirefu. Mlinzi aliinua tochi yake akamulika juu ya mkuyu. Mwanga ulimkosa kosa Sajenti Warioba akaukwepa. Kama siyo wepesi wake basi angekuwa ameonekana. Lakini siyo kwa Sajenti Warioba. Alikuwa ni mwepesi kama paka. Mlinzi baada ya kutokuona kitu aliondoka. Sajenti alishusha pumzi aliyoizuia kwa muda mrefu. Akashuka mpaka chini kwa tahadhari. Asingejiongopea kuwa atakaposhikwa angegeuzwa supu ya kongoro. Hivyo umakini ulikuwa ni muhimu muda ule.

Akatembea upande ambao yule mlinzi alielekea. Akaona mlango ukiwa wazi pakiwa na korido ndefu huku taa ikiwaka. Akatulia kwa kitambo mpaka alipojiridhisha kuwa hakuna mtu karibu na eneo lile. Alikimbia akiwa kainama chapuchapu akaingia kwenye ule mlango. Akatembea kwenye korido ndefu yenye milango mingi iliyokuwa imefungwa. Alitembea mpaka alipofika mwisho wa ile korido ambapo kulikuwa na njia mbili. Moja inaenda kushoto nyingine inaenda kulia. Alikatisha kulia ambapo mbele kulikuwa na bango kubwa lililoandikwa " a sala especial" ambapo ilimaanisha chumba maalumu. Akatembea tena lakini punde alisikika mtu akija kule alipokuwa anaenda. Akili ilifanyakazi haraka. Aligeuka nyuma akafikrii arudi nyuma lakini aliona ni mbali na ataonekana hata kabla hajamalizika. Ikabidi ajikaze atembee kwa kujiamini kama mzoefu wa mule ndani. Punde alitokea mtu mmoja aliyevalia koti jeupe lililoandikwa “A”. Yule mtu alishtuka kumuona Sajenti mahali pale. Ni kawaida kwa wafanyakazi wa hospitali ya Ambagon wakiwa kazini kuvaa koti na kofia. Sajenti hakuwa amevaa koti lakini alikuwa amevaa kapero isiyo ya hospitali.

Walikuwa wameshakaribiana kama hatua tatu kila mmoja akimtazama mwenzake. " viver em sangue" Yule mtu aliyevalia koti jeupe aliongea akimsalimia Sajenti. Salamu hiyo ilimaanisha "kuishi katika damu" Sajenti hakujua ajibu nini. Yule mtu kuona hivyo moja kwa moja akajua aliyesimama mbele yake ni adui. Akachomoa bastola fasta kama umeme. Sajenti akabaki ameduwaa asiamini kasi aliyokuwa nayo yule mtu katika kuichukua bastola kiunoni mwake. Sajenti Warioba alinyanyua mikono juu kama ishara ya kujisalimisha. Yule mtu aliyevalia koti jeupe na kofia ya kidaktari akamsogelea taratibu Sajenti huku akiwa ameishika vyema bastola yake tayari kwa kumshambuliaendapo angeleta hila yoyote.

"Weka mikono kichwani. Ukijaribu kuleta ujanja nitakupasua hicho kichwa" yule mtu aliongea kwa vitisho akitazamana na Sajenti kwa macho ya ndondi.

" Wewe ni nani na umekuja kufuata nini?" Yule mtu akamuuliza Sajenti Warioba kwa sauti ya kibabe. Sajenti alikuwa akifikiri afanye jambo gani ili aweze kujiokoa. Maneno ya yue mtu hayakuwa na mzaha hata kidogo. Alijua kuwa endapo atafanya kosa moja anaweza kupata matatizo. "Wewe kibwengo si nakuuliza! Sina muda wa kupoteza kukuangalia hapa, Umekuja kutupeleleza?" Daktari alikoroma akiwa anatembea kwa kumzunguka Sajenti Warioba. Kidogo Sajenti alikumbuka jambo. Akakumbuka alikuwa amevaa mkufu shingoni wenye vigololi vyenye marashi maalumu ya kijasusi yanayotumiwa kwa ajili ya kumfanya mtu apige chafya. Marashi hayo yakipulizwa hupaswi kuyavuta. Ukiyavuta utapiga chafya wewe kama umenusa ugoro. Sajenti Warioba alishusha kidevu chake chini mpaka cheni ilipokuwa imening'inia juu kidogo ya kifua. Alifanya hivyo huku macho yake yakimtazama yule daktari uchwara. Bado mikono yake ilikuwa imeshika kichwa. Kidevu chake kiliminya moja ya vile vigololi kwenye cheni kikapasuka. Kikatoa harufu. Sajenti alibana pumzi ili asiivute ili harufu. Punde ile korido yote ikajawa na harufu ya kile kigololi. Yule daktari alianza kupiga chafya kwa mkupuo mpaka akapoteza umakini na bastola yake. Ulikuwa wakati wa Sajenti Warioba kujitetea. Kwa upesi alirusha teke nyuzi arobaini na tano likaipiga ile bastola ya yule daktari. Ile bastola ikaanguka. Sasa wakawa wanaangaliana kila mmoja akiwa mikono mitupu. Inaitwa kavukavu. Yule mtu alipiga tena chafya mpaka pua ikatoa kamasi. Sajenti alimchapa ngumi kali ikatua kwenye kidevu. Yule daktari aligugumia maumivu ya ngumi ya Sajenti. Sasa akawa kama amepagawa. Alirusha mateke mfululizo ya double kicks. Chini ya sekunde alirusha mateke matano. Mawili yakampata Sajenti kwenye kifua na mbavu. Sajenti alipepesuka kabla hajakaa sawa yule daktari alimrukia na mateke mawili ya tikitaka ambayo Sajenti aliyaona. Akayapangua lakini yalimzidi nguvu akaanguka chini. Moyoni Sajenti alijiuliza huyu ni daktari au Bedui. Mateke yake ungedhani ni bill bilansi wa kwenye filamu. Sajenti alipoona kuwa adui yake amebobea kwenye mateke akaona abadili mbinu ya mapambano. Alijua kuwa mtu anayejua kurusha mateke hupendelea ngumi za mbali kwa mbali. Hivyo yeye anatakiwa apigane naye akiwa zero distance.

Akiwa pale chini alijivirisha upesi kama umeme akamfikia yule daktari akataka kumpiga ngwala lakini hila yake iligundulika. Yule daktari alikuwa makini sana. Alimkwepa kwa kuruka kisha akamsindikiza na teke la nguvu la mgongoni lililomrusha ukutani. Sajenti aligugumia maumivu baada ya kujigonga ukutani. Aliamka kwa tabu daktari akiwa nyuma yake anamsubiri ili ampe dozi ya mwisho. Alikuwa ameandaa ngumi jiwe ambayo aliamini kuwa ndiyo itakayomaliza ugomvi ule. Sajenti aligeuka kama mzaha vile aliiona ngumi yenye uzani wa kilo tano ikija huku kivuli chake kikifunika uso wake. Alipeleka uso wake pembeni. Ile ngumi jiwe ikapita ikiparuza sikio lake la kulia. Yule mtu hakuamini kama Sajenti angeweza kuiona ngumi yake. Sajenti akamsukuma kwa mikono yake akisimsindikiza na ngumi ya moto iliyopiga katika kingo za mdomo wa juu wa daktari. Mdomo wa daktari ukapasuka kutokana na kujing'ata baada ya kupigwa ngumi. Sajenti hakutaka daktari avute pumzi. Alimchapa kichwa kikali kilichotua katika mwamba wa juu wa pua yake. Alipiga yowe dogo la maumivu akishika pua yake. Sajenti akaanza kujirusha rusha kama mwana kick box kana kwamba anamwambia na kumtambia kuwa mimi ni Sajenti na wewe ni daktari. Huwezi nipiga ilhali kupiga ni fani yangu. Daktari alikuwa ameshika pua yake iliyokuwa imepasuka ikivuja damu. Sajenti alimrushia ngumi lakini daktari hakukubali alikuwa ameshaiona. Aliipangua kama mzaha. Kisha akamdokoa kwenye makwapa Sajenti Warioba ili kulemaza mkono wake. Sajenti akarusha ngumi nyingine. Hii nayo daktari akaikwepa kwa kuinama hali iliyomfanya Sajenti apoteze mhimili wake. Yule daktari aliinama na kumvamia Sajenti kama anampiga kichwa cha tumbo. Wakakokotana mpaka ukutani huku Sajenti Warioba akimpiga ngumi za mgongo daktari. Walibwagana chini. Wakaanza kugarazana. Looh! Daktari alikuwa na nguvu sana. Alimkamata vyema Sajenti na kumuweka chini kisha akamkalia tumboni akimpiga ngumi za uso. Sajenti alizuia uso wake usipatwe na ngumi za daktari lakini mikono yake ilishindwa kuhimili mvua ya ngumi za daktari. Sajenti akaona hapa akileta mchezo anaweza kupoteza maisha. Akakusanya nguvu zake zote na kumsukuma kwa nguvu daktari lakini ilikuwa kazi bure. Daktari alimng'ang'ania kama ruba.

Sajenti uso ulikuwa umelegezwa na ngumi za daktari. Alikunja vidole viwili kama herufi v kisha akavikaza na kuvirusha kwenye macho ya yule daktari. Hapa alifanikiwa. Lilikuwa ni pigo baya sana lililoyaadhibu macho ya daktari. Daktari akapiga kelele akiyalilia macho yake hiyo ilikuwa nafasi ya mwisho kwa Sajenti kulipa kisasi chake. Kipigo alichopewa kilikuwa ni kikali kilichomdhoofisha. Akampiga teke la mdomo na ngumi mfululizo za haraka haraka. Yule daktari alikuwa kama mlevi wa gongo kwa mapigo machache ya Sajenti. Aliangalia kama anasinzia huku akiyumba yumba kama mlevi. Sajenti alimpiga ngumi nyingine kama ya mwisho lakini siyo ya mwisho kabisa. Punde alisikia watu wakija upande wa pili. Walikuwa wakiongea huku wakitembea kwa kasi.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 09)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300


>>>> Episode 09 <<<<<<<<<<

ILIPOISHIA
Lilikuwa ni pigo baya sana lililoyaadhibu macho ya daktari. Daktari akapiga kelele akiyalilia macho yake hiyo ilikuwa nafasi ya mwisho kwa Sajenti kulipa kisasi chake. Kipigo alichopewa kilikuwa ni kikali kilichomdhoofisha. Akampiga teke la mdomo na ngumi mfululizo za haraka haraka. Yule daktari alikuwa kama mlevi wa gongo kwa mapigo machache ya Sajenti. Aliangalia kama anasinzia huku akiyumba yumba kama mlevi. Sajenti alimpiga ngumi nyingine kama ya mwisho lakini siyo ya mwisho kabisa. Punde alisikia watu wakija upande wa pili. Walikuwa wakiongea huku wakitembea kwa kasi.

ENDELEA
Walikuwa wakiongea huku wakitembea kwa kasi. Akaiwahi ile bastola ya yule daktari aliyempa kipigo ambaye muda huo alikuwa akiyumba kama tawi la mti linalopepeswa na upepo. Sajenti baada ya kukamata ile bastola akamdaka yule daktari na kumuweka kama ngao yake. Alikaa kwa nyuma akamkaba huku bastola akiwa amemuwekea chini ya kidevu. Wale watu walitokea wakiwa wawili. Walishtuka kuona daktari mwenzao akiwa kapigwa pini. Kabla hawajamaliza kushangaa Sajenti akawatupia risasi zilizowapata kwenye vifua vyao. Wakadondoka kama midebwedo mpaka sakafuni wakilakiwa na damu zao. Akampiga risasi na yule daktari aliyemtumia kama kinga. Sasa alikuwa amemaliza kazi. Alijishika shika uso wake uliokuwa umevimba kutokana na ngumi za yule daktari uchwara. Akamburuza yule daktari aliyekuwa akipigana naye mpaka walipokuwa wenzake. Akambwaga hapo. Akawapapasa mifukoni akakuta kwenye mfuko wa daktari mmoja funguo nyingi akazichukua na kuzitia mfukoni. Akaondoka akiwa kajiweka vizuri kuelekeo walipokuwa wanatokea wale madaktari wawili. Kwa mbele korido ilikuwa inakatisha kulia huku juu yake kukiwa na kibao kimeandikwa " os quartos escuros" ikiwa na maana ya vyumba vya giza. Taa ya hii korido ilikuwa ya rangi ya bluu. Sajenti akatoa bastola akaishika vizuri huku kidole kimoja akikiingiza kwenye kilimi cha ile bastola. Alihisi eneo lile halikuwa salama. Akatembea kwenye ile korido ndefu pembeni yake kukiwa na milango upande na upande. Ghafla akasimam kutokana na kuona kwa mbele kivuli cha watu wawili waliokuwa upande wa pili wa korido inapokatishia. Aliwasikia wakinong'ona kama watu wanaoteta jambo fulani. Akasogea kwa utulivu bila kupoteza utulivu wa korido zile. Aliwasikia wakiongea. "Mzigo wetu thamani yake ni milioni mia sita. Iweje watupe milioni mia mbili. Hawa watu wanatulalia" Alisikia sauti ya mmoja wa wale watu wakiongea yeye akitazama vivuli vyao.
"Kwanza wao wanapata hela nyingi sana. Kilo moja ya ngozi ya mtu wanaiuza milioni hamsini brazili. Alafu sisi tunawapa mzigo wa kutosha"

Mtu wa pili aliongea wakati Sajenti akiwasikiliza. Ilikuwa habari iliyomfanya Sajenti ahisi mwili joto. Kijasho chepesi kilimtoka makwapani. Zilikuwa habari za kutisha sana. Punde akasikia watu wengine wakija nyuma yake wakiwa wanaongea. Bado walikuwa hawajatokeza kwenye korido aliyokuwepo. Hapa alichanganyikiwa. Akili yake ilipoteza utulivu.. Akisema aende mbele kulikuwa na watu. Tena watu aliowasikia wakijadili mambo mazito ya kutisha. Hawa hakutaka kabisa wamuone. Alihisi kuonekana kwake na watu wale ngozi yake ingekuwa halali yao. Alijiona ni kama panya aliyejipeleka mtegoni. Akisema arudi nyuma hakujua waliokuwa wanakuja ni watu wa aina gani. Alibabaika kama mtu aliyeibiwa maeneo ya stendi. Punde watu wale walitokea wakiwa wanakuja kwa kasi wakiongea. Sajenti Warioba aliuwahi mlango mmoja uliokuwa umefungwa akajibanza. Akajitahidi kuufungua lakini haukufunguka. Hamadi! Wale watu wakamuona akiwa anahangaika kufungua mlango. Walichomoa bastola zao zilizokuwa kiunoni wakaanza kumrushia risasi. Sajenti naye akaanza kujibu mashambulizi huku akijibanza kwenye ule mlango. Sehemu ya kujibanza kwenye ule mlango ilikuwa ni ndogo isiyomtosha. Korido yote ilitawaliwa na milio ya risasi. Utulivu wote ulipotea. Punde wale watu wawili ambao Sajenti Warioba aliona vivuli vyao nao waliingia katika ulingo wa mapambano. Hii ikafanya idadi yao kufika watano waliokuwa wakipambana na Sajenti Warioba. Looh! Salale. Sajenti akapigwa risasi ya bega la kushoto. Jambo ambalo lilimfanya aangushe bastola yake. Kwa bahati alikuwa na bastola nyingine kiunoni ambayo ilikuwa ndio yake. Ile iliyodondoka aliichukua kwa yule daktari aliyempa kichapo akamuua na madaktari wenzake wawili. Wale watu wabaya walikuwa wakishambulia huku wakiwa wamejificha kila mmoja kwenye mlango wake. Walikuwa wakipiga risasi huku wakikimbilia mlango unaofuata kuelekea alipo Sajenti Warioba.

"Ninapaswa nikimbie"
Sajenti akawaza. Kwa upesi akaugeukia mlango na kuupiga risasi kwenye kitasa mlango ukafunguka. Akangia humo na kuanza kukimbia huku bega lake likiwa linavuja damu. Nyuma yake wale watu walikuwa wakimfukuzia kwa uchu wa kumuua.

*************************************************​



"Robert .... Roo..baa.t.iii! Siwezi tena. Nimechoka sana" Mama Rukia alisema kwa tabu huku akikaa chini. Robert ilibidi asimame na kumfuata pale alipokuwa amekaa. Hata hivyo walikuwa wamekimbia umbali mrefu kidogo. Walikuwa wamefika tandale kwa bibi nyau.

"Simama! Simamisha tunaenda" Robert aliikimbilia bajaji iliyokuwa inapita barabarani. Bajaji ilisimama.
"Tupeleke makumbusho" Robert akasema huku akimnyooshea mkono Mama Rukia kuwa aamke waondoke.
"Hamna shida boss"

Dereva bajaji alijibu huku akiachia tabasamu la ukarimu. Wakaingia ndani ya bajaji na kuondoka. Mama Rukia hakuamini kama kweli amepona katika sekeseke lile. Alimshukuru sana Robert kwa kumsaidia. Moyoni alikiri kuwa kama siyo Robert siku ile angejeruhiwa na wale vijana wabaya wenye njaa ya pesa. Hawakuchukua muda mrefu walifika nyumbani kwa Mama Rukia. Hiyo ilikuwa mida ya saa saba mchana. Wote walikuwa hoi.
"Nenda kaoge mimi acha niandae chakula cha mchana" Mama Rukia alimwambia Robert aliyekuwa kajilaza kivivu kwenye sofa. Robert aliamka akaenda kuoga. Akiwa bafuni, uso ukiwa na mapovu ya sabuni alimkumbuka yule mwanamke aliyevaa baibui na kujifunika gubugubi kule makaburini. Alikumbuka alivyomuona akiwa kainama kwenye kaburi ambalo watu waliamini wamemzika yeye. Taswira ya yule mwanamke mvaa baibui akiwa ndani ya gari wakitazamana ilimpitia tena. Alijaribu kumkumbuka ni nani lakini akashindwa. Kama ni Adele mbona hana urefu ule wala umbo kama la Adele. Alipotaka kuamini kuwa huenda ni Ismaiya wazo hilo alilipinga hapohapo. Hawezi kuwa Ismaiya hata kidogo. Kwanza Ismaiya amekufa miezi tisa iliyopita. Kama angekuwa hai muda wote huo angejitokeza. Sasa kama siyo Adele wala siyo Ismaiya, atakuwa ni nani yule mwanamke. Robert alibaki njia panda bila majibu.

Akarudi sebuleni ambapo alikuta tayari Mama Rukia alikuwa ameshapika chakula na kukiandaa mezani. Alikuwa amepika ugali wa sembe, matembele na samaki za kukaangwa. Kilikuwa chakula kizuri sana. Walikula huku wakipiga stori ambapo stori ya yule mwanamke mvaa baibui ikiwa ndio mada kuu. Mama Rukia alimshauri Robert aende kwa waganga wa kienyeji. Mama Rukia aliamini kuwa kuna nguvu za giza zinazomfuata Robert . Na kama hatokuwa makini akapuuza anaweza kujikuta akikumbwa na majanga makubwa zaidi. Kama kuna maneno yaliyomchefua Robert ni maneno ya Mama Rukia. Robert katika maisha yake hakupenda mambo ya kichawi na kishirikina. Hakuwahi kujiingiza na aliapa kuwa kamwe hataweza kujiingiza katika nguvu za giza. Leo Mama Rukia bila haya wala soni. Tena kirahisi rahisi tuu anamshauri aende kwa sangoma. Hilo Robert hakuwa tayari kuliona linatokea. "Umekosa cha kuongea umeona hilo ndio useme?" Robert akasema.

"Nimekushauri tuu. Wewe ndio muamuzi..."Kabla Mama Rukia hajamalizia kujibu alipaliwa kutokana na mwiba kumkaba kooni. Alikohoa mfululizo mpaka machozi yakatoka. Alijitahidi kukohoa kusudi ule mwiba uondoke kooni lakini haikiwezekana. Robert akaamka haraka kwenda kumpiga ngumi za mgongoni Mama Rukia lakini haikufua safu. Sekunde chache Mama Rukia alikuwa mwekundu akiwa hajiwezi kwa kukohoa. Hali ya Mama Rukia ilizidi kuwa mbaya kuliko kawaida. Alikohoa mpaka nguvu zikamuisha. Robert alimsha tonge ili angalau ule mwiba utoke lakini ndio aliharibu kabisa. Mama Rukia alitapika chakula chote alichokuwa amekila. Sasa hapa Robert alihisi kuchanganyikiwa. Alitoka nje akaagiza bajaji. Alimuacha Mama Rukia akiwa hajitambui sebuleni. Punde alirejea akiwa na bajaji. Walimchukua moja kwa moja hospitalini kwa ajili ya matibabu. Ilichukua kama dakika thelasini mpaka walipofika hospitali ya Ambagon. Walipokelewa na vigari vya kusukuma vya kulazia wagonjwa. Mama Rukia akalazwa kwenya moja ya vile vitoroli vya kubebea wagonjwa. Wauguzi waliompokea walikuwa wamevali rangi ya kijani na viatu vyeusi. Walikisukuma kwa kasi kile kigari kilichombeba Mama Rukia kumuwahisha mgonjwa ili apate matibabu. Robert alikuwa naye akija nyuma yao kwa mwendo wa haraka. Walikatisha kulia ambapo kulikuwa na korido ndefu yenye milango pembeni pembeni. Mbele yake walikuwepo wagonjwa wengine wakisubiri zamu zao ya kumuona daktari. Wale Wauguzi walisimama walipofika kwenye mlango ulioandikwa kwa juu " a sala do médico" ikimaanisha chumba cha daktari. Muuguzi mmoja alifungua mlango akaingia wakati Muuguzi mwingine akiwa kasimama na Robert huku wagonjwa wengine waliokuwa wamekaa kwenye mabenchi wakitazama.

Punde mlango ulifunguliwa akatoka yule Muuguzi aliyeingia akatoa ishara ya kuingia ndani.
"Kaka Samahani, tunaomba usubiri pale kwenye benchi. Tutakuita" Muuguzi alisema kwa sauti ya kiuguzi yenye ukarimu ndani yake. Robert hakusema chochote akabaki amesimama akiwaangalia wale Wauguzi wakisukuma kile kigari mpaka walipoufunga mlango wa chumba kile. Akaenda kukaa kwenye benchi walipokaa wagonjwa wengine waliokuwa wanasubiria huduma. Akiwa kwenye benchi alifikiri mambo mengi sana. Alikumbuka tokea siku ya harusi mikosi ilipoanza. Alijiuliza kwa nini yote yale yanampata. Tokea siku ya harusi yake na Adele maisha yake yalibadilika sana. Alikuwa akiishi kama panya. Maisha ya wasiwasi kila siku. Mikosi na majanga vilimuandama bila kuchoka. Maisha kwake akaanza kuyaona hayana maana tena. Alikumbuka alipokuwa mdogo alikuwa na ndoto nyingi sana. Lakini ndoto kubwa ilikuwa aje kuwa mtangazaji wa habari. Aliipenda kazi ya utangazaji kutoka moyoni. Ili kutimiza ndoto yake alisoma mpaka akafaulu shule ya msingi kuelekea shule ya vipaji ya kibaha. Hapo alimaliza kidato cha nne na kufaulu kwa ufaulu mkubwa uliompeleka shule nyingine ya vipaji ya Tabora boys. Hatimaye alienda chuo kikuu cha Dar es salaam school of journalism and mass communication (sjmc - udsm). Huko ndiko alikokutana na Ismaiya na Adele katika harakati za masomo ya chuo.

Hayo yote Robert aliyakumbuka akiwa ameketi katika benchi akisubiri majibu kutoka kwa madaktari kuhusu hali ya Mama Rukia. Punde akaona jambo ambalo hakulitegemea. Roho yake ilichafuka kama bahari. Mwili uliingia ganzi. Alihisi kama anaota ndoto akiwa ndotoni. Mapigo yake ya moyo ni kama yalisimama hali iliyomfanya abaki ameduwaa kama kapigwa shoti ya umeme. Nini aliona. Hata macho yake yalimuuliza. Hata akili yake ilishindwa kutafsiri kwa haraka alichokuwa amekiona.

Alimuona mwanamke aliyefanana na Ismaiya kwa asilimia kubwa. Kama siyo Ismaiya atakuwa ni nani. Akajiuliza. Yule mwanamke alitembea kuelekea alipokaa Robert. Yule mwanamke hakuwa amemuona Robert kwani alikuwa anatembea polepole akichechemea huku akiwa kashika kiuno chake. Tumbo lake lilikuwa kubwa hali iliyomfanya asione vidole vyake vya miguuni. Alikuwa ni mjamzito. Hiyo ndio ilimfanya Robert amuone mwanamke yule kuwa hajafanana na Ismaiya kwa asilimia mia moja. Pembeni yake yule mwanamke alikuwa na mwanaume mrefu na mweusi sana aliyejaa vizuri. Uso wa mwanaume yule ulikuwa uso usio wa mzaha. Mara kwa mara alikuwa akimsaidia kumkokota yule mwanamke aliyefanana na Ismaiya. -Bado Robert moyo wake ulikosa utulivu kabisa. Punde yule mwanamke alinyanyua uso wake kuangalia mbele. Lahaula! Walijikuta wamegongana macho na Robert. Yule mwanamke alionyesha kuhamaki. Ni kama alishtushwa kumuona Robert eneo lile. Bila kutarajia miguu yake ililegea akataka kuanguka sakafuni lakini lile jibaba jeusi refu alilokuwa nalo likamdaka kabla hajaanguka. Hali hiyo ikazua taharuki miongoni mwa waliokuwa eneo lile Robert akiwa mmoja wapo. Wauguzi walikuwa wameshafika hata kabla ya Robert kufika pale. Walimbeba na kumpakiza kwenye kigari cha wagonjwa. Robert alikuwa ameshafika pale kilipokuwa kile kigari alicholazwa yule mwanamke mwenye ujauzito. Wauguzi walikisukuma kile kigari huku Robert akiwafuata nyuma nyuma akimchungulia yule mwanamke aliyefanana na Ismaiya. Walikuwa wamefanana haswa. Robert aliuona uso wa yule mwanamke ukiwa umefumba macho yake ambayo kutokana na muinuko wake yalionekana yalikuwa macho makubwa. Aliyakumbuka macho ya Ismaiya yaliyokuwa makubwa yenye kurembua.

Akili yake iliingia wasiwasi. Alihisi yule alikuwa ni Ismaiya. Alijiuliza maswali kuwa kama yule mwanamke siyo Ismaiya ni kitu gani kimemfanya aanguke na kupoteza fahamu. Mbona alivyogongana naye macho alionyesha kushtuka. Nini kilimfanya ashtuke kama siyo Ismaiya. Akafikiri kuwa huenda Ismaiya alishtushwa kukutana naye maeneo kama yale. Walifika kwenye mlango wa wodi ya wazazi ambapo ilibidi Wauguzi ndio waingie lakini Robert na yule mbaba mweusi mrefu mwenye mwili wa kibondia wao walibaki nje.

"Pole sana brother! Yaani kama usingemuwahi angeanguka chini. Sijui ingekuwaje"

Robert akasema akimpa pole yule baba mweusi aliyekuwa amechanganyikiwa.

"Hata mimi sijui ingekuwaje. Daah!. Ahsante sana ndugu" yule mtu akasema kwa sauti ya upole sana tofauti na umbo lake lililoashiria ubabe na kila dalili za fujo.

"Naitwa Gabriel, nami nimemleta mke wangu hapa. Amekuja kujifungua" Robert alisema akidanganya jina ingawaje ametumia jina la baba yake. "Nashukuru kukufahamu ndugu. Niite Jacob. Yule ni mke wangu" yule mtu alikasema akiuangalia mlango wa wodi uliokuwa unafunguliwa kisha akatoka Muuguzi mmoja aliyevalia sare ya kijani mpauko.

"Dokta! Dokta! Mke wangu anaendeleaje"Jacob alimshika yule Muuguzi kwa papara.

"Samahani kaka, kuwa mvumilivu. Mke wako atajifungua salama. Msubiri dokta yeye ndiye atakupa maelezo ya mke wako. Sawa kakaangu. Ni vizuri mkienda kukaa pale kuliko kusimama hapa, mkeo atakuwa salama" Muuguzi aliongea kwa sauti ya ukarimu kama inavyotakiwa katika kazi hiyo.

"Ahsante sana dada" Jacob kasema, akimshukuru yule Muuguzi kisha akashusha pumzi nzito "Mke wangu anaitwa akwilina kigoda. Uchungu umempata leo hii asubuhi mida ya saa nne" Robert aliendelea kudanganya lengo lake alitaka kujua jina la yule mwanamke aliyeamini kuwa ni Ismaiya.

"Kwa hiyo kajifungua mtoto gani?" Jacob aliuliza kwa udadisi akimtazama Robert ambaye muda huo alijitambulisha kama Gabriel.

"Bado hajajifungua. Mpaka wasiwasi unaniingia. Kama amekufa si waniambie...."

"Aaah! Gabriel maneno gani hayo unasema. Mkeo atajifungua tuu salama. Maneno huumba,
mwombe Mungu amsamaha" Jacob alimkatisha Robert . Aliongea kama mhubiri mwenye kuwahubiri watu waache dhambi na kufanya toba. Kumbe mtu huyu anajua habari za Mungu. Robert aliwaza kimoyo moyo akichekelea namna alivyocheza na akili ya jitu lile jeusi lenye sura inayoakisi ubabe lakini sauti yake yenye mwangwi wa upole.

"Basi samahani, tuachane na hayo. Mke wako anaitwa nani?" Robert aliuliza muda huu akiwa na hofu kidogo usoni mwake. Alihisi swali lake linaweza kushtukiwa. Hata hivyo swali lake lilimfanya Jacob amtazame vizuri usoni mwake kana kwamba ameongea matusi. Jacob alimwangalia Robert usoni kuona kama ataona hila yoyote lakini Robert aliificha hofu yake. Jacob hakuona tashwishi yoyote katika uso wa Robert .

"Anaitwa philomena zahoro. Nampenda sana mke wangu" Jacob alitamka kwa hisia za ndani kabisa. Robert alijikuta akisikia wivu moyoni mwake. Japokuwa maneno hayo yalipunguza imani aliyokuwa nayo kuwa mwanamke yule alikuwa ni Ismaiya. Lakini kitendo cha Jacob kumuambia yule alikuwa ni philomena kilimvunja moyo sana. Alitamani angesikia yule mtu mweusi akimjibu kuwa mke wake alikuwa anaitwa Ismaiya. Lakini haikuwa hivyo. Donge kavu lilimpita kooni huku hasira kiasi zikiutingisha moyo wake. Jacob alishangaa kumuona Robert akiwa amebadilika usoni. Aliuona uso wa Robert ukiwa umejikunja huku macho yake yakiwa hayajatulia. Jacob aliingia wasiwasi. Alijiuliza iweje Gabriel abadilike baada ya majibu yake. Nini alikuwa anataka akisikie kutoka kwake. Hata hivyo Jacob hakuwa ameongea uongo wowote. Ni kweli yule mwanamke alikuwa akiitwa philomena zahoro na wala hakuwa akiitwa jina jingine isipokuwa hilo.

"Kwani ndugu, kuna shida? Mbona kama umebadilika. Embu niambie ukweli" Jacob alimsogelea Robert karibu kama mtu anayemshawishi mtu anunue bidhaa haramu.

“Wala hakuna tatizo mr. Jacob. Hilo jina limenikumbusha mbali sana"

"Wapi huko mr. Gabriel? Je unamfahamu mke wangu?"
Jacob aliuliza kwa kisebu sebu. "Hapana! Simjui. Ni stori ndefu sana Jacob. Wala haitaisha ikiwa nitaisimulia muda huu" Robert alimkatisha Jacob akaongea kama mtu anayekumbuka historia ya zamani sana.

Punde mlango ulifunguliwa akatoka daktari wa kike aliyevalia koti jeupe nyuma yake alikuwepo Muuguzi aliyevalia sare ya kijani mpauko.

"Mume wa philomena zahoro ni nani?" Daktari wa kike aliuliza akizikagua sura za Robert na Jacob.

"Mimi hapa dokta"

Jacob alijibu akiinua mkono juu kama mwanafunzi anayejibu swali Darasani.

"Mkeo alipata mshtuko ndio maana akapoteza fahamu.."

"Dokta kwa hiyo anaendeleaje mke wangu?"


Jacob alimkatisha dokta aliyekuwa anaongea

"Mr. Jacob, taratibu. Kuwa na subira. Sawa!"

"Sawa dokta. Nakusikiliza. Amejifungua salama?"

"Mke wako alizinduka baada ya dakika kumi. Hongera mke wako kajifungua mtoto wa kiume"
dokta akasema huku uso ukiwa umechanua tabasamu la pongezi kwa Jacob.

"Woooooh! Thanks lord. Thanks father. Ooooyoyo! Now i will be called father" Jacob alimvaa dokta na kumkumbatia kwa shangwe na furaha. Watu waliokuwa eneo lile walibaki kuduwaa huku nyuso zao zikitabasamu. Dokta alimuomba Jacob amuachie. Jacob akamuachia.

Uso wa Jacob ulibadilika sana. Alikuwa akicheka cheka kama mwendawazimu. Sasa yeye ni baba. Furaha ya kuwa baba hailingani na jambo lolote kwa mwanaume. Kila mwanaume hufurahia hatua hii. Akili yake ilifikiri mambo mengi kwa wakati mmoja. Kuna wakati alifikiri jina atakalompa mtoto. Kuna wakati alifikiri mtoto atakuwa anafananaje. Basi tuu ilimradi tuu furaha itakavyomtuma. Dokta aliingia ndani akiwaacha Jacob, Robert na Muuguzi aliyekuwa akimtazama Robert muda wote tokea wamekuja pale na daktari.

"Samahani Robert naomba tusogee pembeni tuongee" Muuguzi aliongea huku akimshika mkono. Robert alishtuka sana kusikia jina lake likitajwa na yule Muuguzi. Tena jina halisi siyo lile la baba yake aitwaye Gabriel aliyemdanganya Jacob.

"Mimi siitwi Robert , naitwa Gabriel". Robert akasema akificha aibu ya kuumbuliwa mbele ya Jacob aliyemdanganya jina lake. Hakutaka Jacob ahisi amemdanganya.

"Okey! Samahani! Naomba tuzungumze" Muuguzi aliongea akiwa amemsogeza pembeni Robert. Robert alikuwa na wasiwasi sana. Alijiuliza kuwa Muuguzi anataka kumuambia nini. Alijiuliza kuwa Muuguzi alijuaje jina lake ilhali mule hospitalini hakuna aliyekuwa anamfahamu. “Ooh! Mama Rukia, ndio atakuwa ni yeye aliyewaambia jina langu” Robert alikuwa akifikiri.

"Samahani Robert , naitwa Camila ni muuguzi hapa. Naomba uchukue namba yangu ninamazungumzo yamoto na wewe" Camila alisema akimtekenya Robert chini ya kiganja. Robert alimtazama Camila asijue amjibu ndio au hapana. Camila alitoa karatasi iliyoandikwa namba ya simu kisha akamkabidhi Robert mkononi. "Utanicheki jioni. Sawa Robert !"

"Nimekuambia siitwi Robert mbona umekazania"


Robert akasema hasira zikimkaba kooni.

"Sorry! Usisahau kunitafuta". Camila alisema huku akiwa anaondoka. Robert akabaki akimsindikiza na macho huku akiyaangalia makalio yaliyojichonga kwenye ile sare aliyokuwa ameivaa Camila.

*************************************************​

Mama Rukia na Robert walirudi nyumbani baada ya kuruhusiwa. Usiku huo Robert alikuwa amejilaza kitandani akiwa katika lindi la mawazo. Alimkumbuka yule mwanamke aliyefanana na Ismaiya ambaye ni mke wa Jacob. Alikumbuka maneno ya Jacob kuwa mwanamke yule alikuwa anaitwa philomena zahoro. Hakika duniani wawili wawili. Robert alijisemea mwenyewe. Kama ni kufanana walikuwa wamefanana haswa. Hata mapacha hawawezi kufanana vile. Punde alikumbuka habari ya Camila Muuguzi aliyempa namba kule hospitalini. Akaichukua ile karatasi kisha akatoka chumbani kwenda kwa Mama Rukia kuomba simu. Alitoka chumbani kwake na moja kwa moja akaelekea kilipochumba cha Mama Rukia ambapo alikuta kimefungwa taa ikiwa inawaka kwa ndani kuashiria kuwa Mama Rukia bado alikuwa macho. Akagonga mara mbili na kabla hajagonga mara ya tatu alisikia sauti ya Mama Rukia ikiongea kuwa anakuja.

Mlango ulifunguliwa na Mama Rukia alitokea akiwa kavaa kanga moja tuu akiwa kaibania kwenye maziwa yake. Uso wake ulikuwa na majimaji; alikuwa ametoka kuoga.

"Vipi Robert leo unataka tulale wote?"

Mama Rukia alisema akicheka huku akiufanya uso wake uwe kama shangingi la mjini lililobobea kuiba waume za watu.

" Hapana Mama Rukia. Nilikuwa naomba simu" Robert alijibu.

"Huna kingine kweli! Sema usiogope" Mama Rukia alisema akiingia ndani kuchukua simu.

"Haya hiyo hapo. Ningeshangaa usipate mchumba kule hospitalini" Mama Rukia akasema kwa madaha huku akijichekesha kama muimba taarabu.

Robert hakujibu kitu zaidi ya kumuaga.

"Nitakurudishia baada ya dakika kumi na tano" Robert alisema kisha akaondoka.

"Wala hamna shida. We tumia tuu hata usiku mzima. Sawa mume" Mama Rukia alichomekea utani. Robert alibaki kucheka huku akimuona Mama Rukia kama Mama anayependa sana utani wa mapenzi. Alifika chumbani kisha akaichukua ile karatasi aliyopewa na Camila. Aliiandika kwenye simu kisha akaipigia. Looh! Simu haikuwa na salio. Alisonya. Akatuma tafadhali nipigie kwa namba aliyopewa na Camila. Bahati nzuri simu ikarudisha ujumbe wake umepokelewa kwa namba ile ya Camila.. Alisubiri kuona kama atapigiwa lakini hakupigiwa. Dakika ilikatika lakini hakupigiwa. Alituma tafadhali nipigie nyingine. Kisha akasubiri kwa dakika mbili lakini hakupigiwa. Alijikuta aakikasirika. Fumba la hasira lilimkaba kooni. Alituma tafadhali mpaka zikaisha bila ya kupigiwa. Mwishowe alikata tamaa. Akaona huenda muda ule Camila alikuwa amelala. Au yupo na mume wake. Alijikuta wivu ukimkaba kama tai shingoni. Taswira ya Camila ilipita kichwani mwake. Camila alikuwa msichana mfupi mfupi mwenye kaumbo potabo kanakoelekea kuwa bonge. Kutokana na umbo lake hilo ndio maana sare za uuguzi alizokuwa amezivaa zilikuwa zinamkaa na kuchora umbo lake la kichokozi.

Robert alikumbuka kidoti cha Camila kilichokiwa karibu na jicho lake hali iliyoongeza urembo wake. Kumbukumbu hizo hazikumsaidia kitu ikiwa mtu mwenyewe anayemkumbuka hampigii simu. Alijkuta akijitukana kwa kusubiri simu ya mtu ambaye huenda muda huyo kalala na mwanaume mwingine. Au huenda yupo bar anakunywa na mwanaume wake. Yote hayo alikuwa akiyawaza Robert akiwa kitandani. Robert alishtuka alipokumbuka sauti nyororo ya Camila iliyolitaja jina lake. Alijuaje jina langu. Nani alimuambia naitwa Robert . Au Mama Rukia ndiye alimuambia jina langu. Maswali mfululizo yalikipiga kichwa cha Robert . Alitamani atoke akamuulize Mama Rukia lakini akili yake ilimuambia kama atafanya jambo ilo basi tangu siku hiyo ingemdharau na kumuona yeye ni zumbukuku. Punde roho ya udadisi ilimuingia. Alitaka kuikagua simu ya Mama Rukia. Akafungua upande wa galeri ambapo kulikuwa na picha na video. Aliona picha za Mama Rukia akiwa katika mapozi mbalimbali. Hakika Mama Rukia alijaliwa uzuri usiosemeka. Licha ya utu uzima wake lakini bado uzuri wake ulitikisa mioyo ya wanaume waliopata nafasi ya kumuona. Umbo lake nene lililojazia vyema ndilo lililomfanya Robert azidi kutafuta picha zingine akiamini picha ambazo hajaziona zitakuwa nzuri zaidi ya zile alizoziona. Akaendelea kupangusa lakini punde alivutiwa na picha moja ikimuonyesha Mama Rukia na mwanaye Rukia. Robert alikiri kuwa Mama Rukia alizaa mtoto mrembo sana. Walifanana sana. Akapangusa zaidi na zaidi mpaka akafika kwenye video. Tobaaa! Alishtuka sana. Macho yake yaliona video za uchi za kizungu. Alishangaa sana. Kwa alivyokuwa anamheshimu Mama Rukia hakutegemea kama angekuta video zile za x kwenye simu ya Mama Rukia.

Aliitoa haraka lakini kumbe video karibia zote zilikuwa ni za uchi. Robert alichoka roho na mwili. Lakini aliona Mama Rukia alikuwa na haki ya kutizama video hizo angalau kwa kujiliwaza kutokana na upweke.

Punde simu ikaita. Alishtuka huku uso wake ukijawa na shauku za kupagawa alipoiona namba ya Camila kwenye kioo cha simu ya Mama Rukia.

"Hello Camila kidoti" Robert akasema kwa sauti iliyotulia mithili ya kijana barubaru.

"Hello. Sorry who is this"

Camila aliongea kwa madoido huki akidondosha umombo.

"Hahaha! Can you guess?"

"I can't guess. Please tell me who are you. Otherwise I will hang up "


Camila akasema huku akiwa mbali na utani.

"Okey don't panic dear. Its me Gabriel"

"Hahaha! Nilijua tuu ni wewe. Alafu wewe siyo Gabriel. Wewe ni Robert "
Camila akasema kwa uchangamfu ungedhani anaongea na shoga yake.

"Camila! Ulijuaje mimi naitwa Robert ?"

"Siyo tuu jina lako. Mimi nakufahamu kuliko ujijuavyo. Najua ulimdanganya yule kaka pale hospitalini"
Camila alisema kwa majigambo huku sauti yake akiilainisha na kuifanya izidi kuwa laini. Robert akashangaa kusikia Camila akimuambia kuwa alimdanganya yule mtu kule hospitalini aitwaye Jacob. Moyoni alihisi kuwa Camila atakuwa ni mtu mwenye taarifa zake nyingi sana. Alizitoa wapi taarifa zake hilo hakuwa analijua.

"Nani alikuambia ninaitwa Robert ?"

"Hahahah! Nani asiyekujua Robert . Wewe ulidhani haufahamiki"

“Haya sema shida yako. Ulitaka nikupigie ili iweje? Hiyo habari ya moto ni ipi?"
Robert akasema akiwa kama mtu aliyepaniki.

"Tulia Robert . Leo ni lini?"

"Jumatano"
" tukutane jumapili. Tutaongea jambo la moto"
Camila akasema

"kwani usiseme leoleo?”

“ Mambo mengine kuyazungumza haipaswi kwenye simu, tukutane uso wa uso”

“ Basi sawa! Lini sasa?:” Robert akasema.

"Hahah! Mr. Robert ..! Jambo la moto halihitaji haraka. Mbona pupa sasa"
Robert alikaa kimya bila kujibu kitu chochote. Alijikuta akiwa na hasira. Alitaka amtukane lakini nafsi yake ilimuonya asithubutu kufanya jambo baya kama lile. Alijua kuwa anahitaji awe na subira ili apate kujua hilo jambo la moto alilo nalo Camila.

"Jumapili nitakupigia simu wapi tutakutana. Sawa Robert !" Camila aliendelea kuongea kupisha ukimya uliosababishwa na Robert kutokuongea.

" Vyovyote utakavyoamua. Hata tusipokutana ni sawa"Robert alisima.

"Hahaha! Umepaniki broo! Usiku mwema Robert naona umechoka kuongea"

Camila aliongea akimdhihaki Robert. Kisha akakata simu.

*************************************************​


Jumapili ilikuwa imefika. Siku ambayo Robert alikuwa ameisubiri kwa hamu zote. Zilikuwa ni siku nne tokea aambiwe na Camila kuwa watakutana lakini yeye aliziona kama mwaka mzima. Alifika mileniam tower kama alivyoelekezwa na Camila. Punde ilisimama gari aina ya nissan patrol nyeupe kama ile iliyomgonga siku ile alipokuwa akikimbizwa na Polisi wa Adele. Kioo cha ile gari kilishuka na punde uso uliovalishwa miwani nyeusi ulionekana ndani ya gari. Robert alimuangalia yule dada lakini hakumfahamu mpaka alipovua miwani yake. Loooh! Alikuwa ni Camila. Camila alikuwa amebadilika jumla. Alikuwa amependeza sana. Kitendo cha yeye kuvaa miwani nyeusi kilipotezea sura yake. Camila akamuashiria Robert aingie ndani ya gari na safari ikaanza. Mule ndani kulikuwa kimya. Camila alikuwa kavaa hereni kubwa za mduara kama msanii aitwaye nakaya. Muda wote macho yake yalikuwa mbele mithili wa dereva wa msafara wa raisi.

"Tunaelekea wapi?"

Robert alivunja ukimya uliokuwa mule ndani ya gari.

" Tunaenda kwangu. Huko ndipo lilipo jambo la moto".

"Kwako? Nishushe! Nishushe. Jambo gani hilo usiloweza kunambia hapa?"


Robert akasema sauti ikiwa inakwama kwama. Ni kama alikuwa ameingiwa na kigugumizi cha ukubwani. Camila hakujibu kitu chochote. Punde gari ilisimama mbele ya geti kubwa na kupiga honi mara mbili. Sekunde haikuisha lile geti lilifunguliwa likiwa linateleza. Robert alikaa kimya huku akitazama ndani ya geti ambapo kulikuwepo na jumba kubwa la kisasa ambapo kwa nje kulikuwa na bustani ya maua mbalimbali. Camila akaliingiza gari ndani huku geti likijifunga. Bado Robert alikuwa akichungulia nje kupitia dirisha la gari wakati Camila akilipaki gari mahali pake.

"Tumefika Robert . Jisikie huru. Si unaona wala siyo mbali" Camila aliongea huku akimtazama Robert kwa tabasamu la kirafiki. Walishuka na moja kwa moja walielekea ndani ambapo Robert alishuhudia samani za kisasa katika sebule iliyopambwa kwa mapambo ya gharama. Hii iliashiria kuwa mmiliki wa ile nyumba alikuwa ni mtu mwenye kipato kikubwa. Na kama mmiliki ni Camila basi Robert alianza kuamini kuwa hospitali ya Ambagon inalipa wafanyakazi wake mishahara mikubwa sana.Camila alimkaribisha Robert kwa juisi ya machungwa na pasheni ambayo aliitoa kwenye jokofu kubwa kutoka ujerumani.

"Haya nambie hilo jambo la moto"

Robert aliongea huku akimtazama Camila. Lakini katika hali isiyotarajiwa. Robert alisikia sauti ya mtoto akilia kutoka nyuma yake. Akageuka. Alishtuka kumuona yule mwanamke aliyemuona hospitalini aliyekuwa na mimba. Ambaye alikuwa amefanana na Ismaiya kwa kiasi kikubwa.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 10)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

>>>>>>>>>> Episode 10 <<<<<<<<<<<<<<<

ILIPOISHIA
Robert aliongea huku akimtazama Camila. Lakini katika hali isiyotarajiwa. Robert alisikia sauti ya mtoto akilia kutoka nyuma yake. Akageuka. LAlishtuka kumuona yule mwanamke aliyemuona hospitalini aliyekuwa na mimba. Ambaye alikuwa amefanana na Ismaiya kwa kiasi kikubwa.

ENDELEA
Sajenti Warioba aliingia katika chumba kile ambacho kilikuwa na giza totoro. Bega lake liliendelea kuvuja damu nyingi huku maumivu makali akiyasikia. Nyuma yake alisindikizwa na milio ya risasi iliyokuwa inamfuata kwa uchu wa roho yake. Akiwa mule ndani macho yake yalipata tabu kuona. Alitembea kwa fujo akivikumba vitanda vya mule chumbani. Hapo alibaini kuwa kile chumba kilikuwa wodi ingawaje macho yake yalikuwa hayaoni chochote kutokana na giza. Wale watu waliokuwa wakimfukuza kwa risasi nao wakaingia kwenye kile kile chumba alichokuwa ameingia. Kulikuwa na giza zito sana. Waliwasha tochi zao wakamulika huku na huku kwenye kile chumba kumtafuta Sajenti. Hawakumuona mule ndani. Wakaenda mpaka mwisho wa wodi hatimaye waliona kijimlango kidogo kikiwa kimefunguliwa. Wakajua kuwa Sajenti Warioba alikuwa amepitia mlango huo kuwakimbia. Wakaingia. Walimalizika wakakiacha kile chumba kikiwa kimya. Kumbe Sajenti Warioba alikuwa kajificha juu ya Dari. Sajenti alifungua kale kamlango kusudi wale wauaji wakija wajue kuwa alipitia mlango ule ili kuwahadaa. Akafanikiwa kuwachenga.

Akiwa juu ya Dari alihisi maumivu makali upande wa bega lake lililokuwa limejeruhiwa na risasi. Damu ilikuwa ikitoka nyingi jambo ambalo Sajenti alilihofia. Akashuka kutoka Darini. Akarudi kule alipokuwa ametoka kukimbizwa. Alifika kwenye ile korido alipokuta vile vivuli viwili vya watu waliokuwa wakizungumzia habari za biashara ya ngozi ya binadamu. Akatembea kwa tahadhari na kwa umakini mkubwa huku mkono wake wa kulia akiwa ameishika vyema bastola yake kwa ajili ya kukabiliana na hatari yoyote. Alitembea kwenye zile korido mpaka alipofika sehemu ambayo mbele yake hapakuwa na njia isipokuwa mlango mkubwa wa geti la aluminiam. Aliukaribia ule mlango akinyata kwa umakini bila ya kuyabughuzi mazingira ya eneo lile. Akakishika kitasa cha ule mlango wa aluminian polepole akakitekenya kukifungua lakini ulikuwa umefungwa. Alijaribu kuchungulia mule ndani lakini hakuona jambo lolote. Kulikuwa na giza. Macho yake yalishindwa kuona yaliyokuwepo mule ndani ya ule mlango wa aluminium. Aliikumbuka ile funguo aliyoichukua kwa yule daktari uchwara. Akaichukua na kujaribu kufungua. Ilikuwa kama bahati tuu mlango ukafunguka. Aliingia mule ndani akarudishia mlango na kuufunga na funguo. Sajenti Warioba bhana. Yaani anajifungia kabisa. Kwa kweli mimi nisingeweza.

Akaanza kukikagua kile chumba ambacho kilikuwa ni kikubwa sana kama wodi. Kutokana na giza macho yake yalipata tabu kuona vizuri alitamani pangekuwa na nuru hata ya mwanga wa mshumaa ili aone chochote lakini haikuwa hivyo. Kulikuwa na giza sana. Hapakuwa na dirisha lakini kulikuwa na baridi kali ya kiyoyozi. Sajenti alitembea tembea bila kuona chochote. Kidogo alifika sehemu akapokelewa na na harufu kali ya manukato kama marashi ya maiti. "Haya marashi yanatokea wapi?" Sajenti Warioba alikuwa anajiuliza kimoyo moyo. Akili yake ilimuambia kuwa huenda pale ni mortuary. Sehemu ya kuhifadhia maiti. Akafika ukutani ambapo aliona swichi ya kuwashia taa. Akili yake ilimuambia awashe taa. Alisita lakini alikuwa ameshachoshwa na lile giza. Aliwasha taa.Moyo wake ulilipuka kama bomu. Ilibaki kidogo aanguke. Macho yake yalishtuka kuona masanduku mengi ya kuwekea maiti. Alizima taa tachaaa! Akashusha pumzi huku giza likimkumbatia tena. Kweli kile kilikuwa chumba cha giza. Majeneza yote yale. Sajenti alikuwa anawaza huku akiwa kasimama kama mlingoti katikati ya giza

Akawasha tena swichi ya taa. Tachaaa! Mwanga ukatawala tena ile wodi. Yale majeneza yalikuwa yamepangwa kwenye vitanda maalumu vya kuwekea majeneza vyenye matairi. Pia yaliwekwa kwa mpangilio yakiwa katika mistari iliyonyooka. Sajenti aliyazungusha macho yake akikagua jeneza moja baada ya jingine. Alishtuka. Haaaa!. Alihamaki. Hakuamini kile macho yake yalichokiona. Ni kama alikuwa anaota. Na kama ni ndoto ilikuwa ndoto mbaya ya majinamizi na mazimwi. Sajenti aliona sanduku moja la kioo la kuwekea maiti ambalo ndani yake kulikuwa na mtu. Mtu yule alikuwa anamfahamu fika kabisa. Alipiga hatua kulisogelea lile jeneza la kioo huku akimtazama yule mtu. Uso wake ulijawa na simanzi iliyochanganyika na kutoamini kile alichokuwa anakiona. Alikuwa ameshalifikia. Alipiga magoti mpaka kwenye usawa wa uso wa yule mtu aliyekuwa ndani ya jeneza. Yule mtu ndani ya jeneza alikuwa amefumba macho yake ungedhani yupo usingizini na kama ukimuamsha angeamka. Lakini tangu lini mtu akifa anaamka.

Pua na masikio yake yalikuwa na pamba akiwa yupo uchi wa mnyama. Sajenti alitoa machozi yakitiririka katika mashavu yake. Kwa sauti dhaifu Sajenti Warioba aliita; "Joseph! Joseph.... Joseph laizaer" alikuwa ni Joseph kijana aliyeuawa kule Twangoma alipokuwa kwenye lile jumba la watu hatari. Joseph kijana mwenye roho nzuri aliyemuokoa. Kijana aliyekufa akiwa hana hatia yoyote. Sajenti alijikuta akilia sana. Alilishika jeneza alilokuwamo Joseph.

"Sajenti Warioba. Usilie! Usilie Sajenti Warioba. Wafuatilie hawa watu. Uwakamate uwafikishe katika mikono ya sheria" Joseph alifumbua macho yake na kuanza kuongea huku puani kukiwa na pamba. Macho yake yalikuwa mekundu kutokana na kufumba macho muda mrefu.

Sajenti alishtuka kuona Joseph anaongea. Walitazamana.

"Joseph! Joseph! Ngoja nikutoe humu ndani". Sajenti aliongea huku akitafuta mahali pa kulifungua lile jeneza la kioo. Aliona vitufe viwili. Kitufe kimoja kilikuwa cha kijani wakati kitufe kingine kikiwa chekundu. Alisogelea kile kitufe cha kijani kwenye lile jeneza la kioo alilokuwemo Joseph. Joseph bado alikuwa anamtazama tuu Sajenti Warioba. Sajenti alimtazama Joseph kwa macho yanayosema nabonyeza. Wakati Joseph akimtazama kwa macho yasemayo bonyeza. Sajenti alibonyeza kile kitufe cha kijani cha lile jeneza la kioo. Punde mfuniko wa juu wa lile jeneza ukafunguka. Ghafla bin vuu sauti ya hatari ilianza kulia huku taa ya ile wodi ikibadilika badilika rangi kufuatana na mlio wa ile alamu. Sajenti alioogopa sana. Kumbe Joseph wala hakuwa ameongea wala hakuwa amemka. Yale yalikuwa ni mawazo yake tuu. Joseph alikuwa amelala huku macho yake akiwa ameyafumba. Mdomo wake alikuwa ameufunga wala hakuongea lolote. Mawazo ya Sajenti ndio yalifanya mdomo wa Joseph uongee ilhali haukuongea. Mawazo ya Sajenti ndio yaliyofanya macho ya Joseph yatazame ilhali hayakuwa yanatazama. Ile sauti ya alamu ilikuwa kama ni ishara ya hatari. Ilikuwa inaita walinzi kuwa kulikuwa na tatizo. Sajenti alilijua hili. Hivyo alianza kutafuta namna ya kuondoka mule ndani. Aliondoka pale akiufuata mlango wa kutokea ambao ndio aliojia. Kabla hajafika kwenye ule mlango alisikia sauti za watu wakija kwenye ule mlango. Akasimama Kisha akaanza kurudi kinyume nyume polepole huku akifikiria kipi afanye.

Hofu ilikuwa imeujaza moyo wake. Tayari alijiingiza akatika shimo la hatari. Na endapo ataleta mchezo basi ule ndio utakuwa mwisho wa maisha yake. Alikimbia mpaka alipofika kwenye jeneza moja la kioo lililokuwa tupu. Akavua nguo zote. Akajifuta ile damu iliyokuwa kwenye bega mpaka pakawa safi. Akazificha nguo zake chni ya moja ya jeneza la mbao. Kisha akaingia ndani ya lile jeneza la kioo lililokuwa tupu. Akajinyoosha kisha akarudishia mfuniko. Akafumba macho kama mtu aliyekufa lakini alikumbuka kuwa hakuwa na pamba za kuweka masikioni wala puani. Hata hivyo hakuwa na jinsi kwa kuwa kwa muda ule angepata wapi pamba. Punde wale watu waliingia wakiwa watatu. Wawili walikuwa na bunduki za kivita. Mmoja alikuwa na AK47 wakati mwingine akiwa na smg. Walivalia mavazi ya rangi ya Dark bluu huku nyuso zao zikiwa zimezibwa kama wanamgambo wa alkaida. Nyuma ya zile nguo zao yaliandikwa maneno Ambagon. Yule mmoja hakuwa na bunduki wala hakuwa amevaa kama hawa wawili. Yeye alikuwa kavaa koti jeupe la kidaktari. Wale watu walianza kusaka kilichofanya alamu ilie. Wakaembea huku na huku. Wakikagua majeneza. Sajenti aliwachungulia kwa kijicho upembe wakati taa ikiendelea kumulikamulika rangi tofautitofauti huku mlio wa alamu ya hatari ukiendelea kulia.

Sajenti akahisi kijasho alipowaona wale watu wakiwa wamelifikia jeneza la kioo la Joseph ambalo lilikuwa lipo wazi. Alijilaumu ni kwa nini alisahau kulifunga. Aliwaona wale watu wakijadili mambo mawili matatu. Kisha alimuona yule mtu aliyevalia koti jeupe kama daktari akitoa kifaa na kuanza kupitisha juu ya lile jeneza ulipomwili wa Joseph. Moja kwa moja Sajenti Warioba alijua maana yake. Leo ndio ilikuwa mwisho wake. Alijua kuwa yule daktari alikuwa anachunguza kama lile jeneza lilikuwa limeshikwa na mtu au laa. Hivyo alikuwa anatumia kile kifaa kuangalia kama ataona alama za vidole. Kama alivyowaza Sajenti Warioba ndivyo ilivyokuwa. Yule daktari aliona alama za vidole kwenye lile jeneza la kioo. Aliona alama za vidole kwenye kioo na kwenye kile kitufe cha kijani ambacho sajanti Warioba alikuwa amekibonyeza mpaka mfuniko wa jeneza ukafunguka.

"Kuna mtu ameingia humu ndani akashika hili sanduku" Yule daktari aliongea akiwaambia wale watu waliovalia makombati ya Dark bluu huku nyuso zao wakiwa wamezifunika. Sajenti Warioba alisikia kila kitu. Alijua kinachofuata hapo ni msako. Na kama watafanya msako basi angekamatwa kirahisi kama kuku wa kisasa. Jambo hilo hakutaka litokee na hakuwa tayari kuliruhusu. Yeye hakuogopa kukamatwa wala hakuogopa kufa. Alijua kuwa alizaliwa siku moja na atakufa siku moja. Lakini hakuwa tayari kufa kienyeji. Alitaka afe kwa heshima na afe kiume. Sasa alifikiria atatumia mbinu gani ili aweze kuporochoka mule wodini. Akataka kutoka mule ndani ya jeneza lakini akili yake ikamuonya. Akili yake ilimuambia aache ujinga. Ilimuuliza kwani hajaona wale watu wenye silaha za kivita ambao nyuso zao hawakutaka zionekane. Alibaki ametulia akisubiri maelekezo ya akili yake. Yule daktari na wale makomando wawili walianza msako wa nguvu. Wakaanza kufunua jeneza moja baada ya jeneza jingine. Kila walipofika kwenye kila jeneza yule daktari alichukua alama ya vidole vya kila maiti. Bila shaka walitafuta maiti ambayo ingefanana alama ya vidole na vidole vilivyoonekana kwenye jeneza la Joseph.

Sajenti akahisi koo lake kukauka. Alihisi kiu lakini haikuwa kiu. Ilikuwa ni hofu ya kifo. Wale watu walikuwa wamekaribia jeneza la kioo alilokuwemo Sajenti. Jasho jepesi lilitoka makwapani likatiririka mpaka kwenye sponji la lile jeneza la kioo. Punde yule daktari na wale watu wawili walifika kwenye lile jeneza la kioo alilokuwamo Sajenti. Wakalifungua huku wote wakiwa kimya. Sajenti moyo wake ulizidi kupoteza muelekeo wa kupiga. Presha ilikuwa juu sana.

"Huyu mbona hawakumnyoa nywele za huku?" mmoja wa wale makomando aliuliza baada ya kuona mavuzi ya Sajenti. Looh! Kauli hiyo ilimvuraga sana Sajenti. Alihisi sasa anaenda kushtukiwa kama wameshaanza kuona dalili ndogo ndogo hizi wakiona alama za vidole itakuwaje.

Utaratibu wa kile chumba ni kuwa huwezi ingizwa kwenye jeneza ukiwa una nywele mahali popote pale. Iwe nywele za kichwa, nyusi, ndevu, nywele za kwapani au mavuzi. Sasa Sajenti Warioba alikuwa na kipara kichwani, hakuwa na nywela kwapani wala ndevu zote alizinyoa. Lakini nyusi alikuwa nazo na mavuzi hakunyoa. Hii ilikuwa hatari kwake. Daktari aliingiza mkono kuuchukua mkono wa Sajenti Warioba huku wale makomando wakijiweka sawa kutokana na kushikwa na machale. Ili kama kutatokea la kutokea washambulie. Kama umeme Sajenti Warioba aliunyongolota mkono wa daktari na kumvuta ndani ya jeneza huku akiitoa bastola yake aliyokuwa ameficha chini ya mgongo na kumpiga komando mmoja kichwani. Muda huo yule daktari tayari alikuwa kamlalia Sajenti juu kama kinga yake huku jeneza likipasuka vioo. Yule komando mwingine alijiviringa kama mpira akajibaza nyuma ya majeneza. Lilikuwa ni tukio la sekunde chache sana lakini lililobeba ufundi na ujuzi usiosemeka. Yule daktari hakuamini kama jambo lile lingetokea kwa namna ile. Kwake alilichukulia kama muujiza usiowezekana. Wepesi wa Sajenti Warioba uliupita kasi ya mwanga. Daktari alipumua kama panya aliyekoswa koswa na mtego. Nyuma ya shingo yake aliwekewa mdomo wa bastola ambapo aliambiwa hata akikohoa tuu au kupiga chafya ingetosha kupasua ubongo wake.

Sajenti akajinasua pale kwenye jeneza akiwa amemuweka chini ya ulinzi yule daktari. Palikuwa kimya yule komando ni kana kwamba alikuwa akipiga hesabu za Matrix. Punde yule komando alianza kurusha risasi hovyo hovyo bila mpangilio kuelekea alipokuwa Sajenti na daktari.
"Komando! Komando utaniua. Acha!" Daktari aliongea kumnyamazisha yule komando asije akamlenga na risasi kwani yeye ndio ngao ya Sajenti. Kitambo kidogo kukawa kimya huku yule komando akiwa kajificha nyuma ya kabati kubwa la kuhifadhia madawa ya maiti. Mara ghafla yule komando alijitokeza na kuanza kumshambulia Sajenti na risasi. Alimpiga daktari risasi nyingi za kifua. Alidhamiria kuwa amuue daktari na Sajenti kwa pamoja. Jambo hilo Sajenti alilishtukia. Akamsukuma daktari kwa mbele kwa kumpiga teke la mgongo kuelekea kwa yule komando kisha akampiga yule komando risasi ya kichwa. Yule komando alidondoka chini na daktari.

Sajenti alikuwa ameshamaliza kazi. Akabaki amesimama akiwa uchi wa mnyama huku ameishika bastola yake mkononi. Alivaa nguo zake alizokuwa amezificha chini ya jeneza. Kisha akaenda kuwapekua daktari na wale makomando wawili aliowaua mule wodini. Kwa daktari hakukuta jambo lolote la maana isipokuwa kile kifaa cha kupimia alama za vidole. Akamsogelea komando mmoja akamvua ile kofia lililofunika uso wake. Alikutana na sura ngumu. Dooh! Alitisha kama nini. Hakumuangalia yule wa pili. Akatoka mule wodini akaondoka akaifuata korido ambayo aliijia. Akakata kulia kisha akakata kushoto tena ambapo alikuta korido ndefu yenye milango mingi sana. Akasimama baada ya kuvutiwa na mlango wa chumba kimoja kilichoandikwa " quarto para os mortos" ikimaanisha; chumba cha wafu.

Akafungua mlango akakuta upo wazi. Macho yake yalikutana na mabegi makubwa meupe ambayo ndani yake yalikuwa na maiti. Yale mabegi ya maiti yalikuwa yameandikwa na maandishi ya bluu yaliyosomeka Ambagon. Aliikagua ile wodi ya maiti ambapo aligundu mule ndani kulikuwa na maiti zisizopungua mia moja.

"Jesus christ! Hawa watu ni mashetani. Lazima wawajibike" Sajenti Warioba alisema wakati akiendelea kustaajabu mambo yale ya kutisha. Punde alisikia mbele kabisa sauti. Akaangalia. Kumbe kwa mbele lilikuwepo geti la chuma. Alisikia mtu akilishika kwa nje kana kwamba analifungua. Alijiongeza harakaharaka akaenda kwenye kabati moja kubwa akachukua begi akajiingiza naye ndani ya begi. Geti lilifunguka na punde watu wanne waliingia. Hawakuwa na muda wa kujadili. Walianza kuzisomba zile maiti na kuzipeleka nje ambapo kulikuwa na lori lililokuwa limepaki.. Wale watu walikuwa chapu chapu bhana. Dakika kumi hazikufika maiti zote zilikuwa zimepakiwa ndani ya kontena akiwepo na Sajenti Warioba.
*************************************************​
MELI YA AMBAGON
Meli ilianza safari kutoka bandari bubu ya mtwara yapata majira ya saa kumi usiku. Bahari ilikuwa imetulia. Mawimbi yalikuwa ya kawaida huku hali ya upepo ikiwa shwari kabisa. Hii ilikuwa ni bahari ya hindi ambayo ni miongoni mwa bahari kubwa katika sayari hii ya dunia. Sajenti Warioba alikuwa miongoni mwa waliokuwa ndani ya meli hiyo. Alichoka kukaa ndani ya begi la maiti kutokana na kushindwa kupumua vizuri na harufu kali ya marashi ya maiti. Akatoka ndani ya begi akapokelewa na mwale wa mwanga uliotoka kwenye kadirisha ka lile kontana ambako kaliachwa wazi ili hewa iingie kusudi zile maiti zisije haribika kwa haraka ijapokuwa zilikuwa zimewekwa madawa.
Akaenda mpaka kalipo kale dirisha akapanda akachungulia. Alishangaa kuona makontena mengine kwa nje. Akatoka ndani ya lile kontena. Alikuta makontena mengi sana kama ishirini lakini yakiwa kwenye ukumbi. Hakujua ule ukumbi ulikuwa ni ukumbi wa meli. Yeye alidhani labda ni ukumbi tuu wa kawaida ambapo ni sehemu ya kuhifadhia makontena. Akatembea tembea mule ukumbini akikaguakagua. Kila kontena liliandikwa Ambagon. Aliona geti kubwa. Moja kwa moja akajua ule ndio mlango wa kutokea ambapo hayo makontena ndipo yalipoingiziwa. Akaenda kuufungua akaukuta upo wazi. Alifungua taratibu bila kutoa sauti. Alichungulia upande wa pili akaona kuna masofa mawili ya kukalia, meza ambayo juu yake kuna chupa kubwa ya wine na luninga iliyokuwa inaonyesha muziki wa kimarekani.
Alipohakikisha hakuna mtu. Akatembea tembea akiangaza macho yake. Aliona simu ya smartphone kwenye moja ya yale masofa. Aliichukua ile simu kisha akaibonyeza bonyeza. Haikuwa na pattern wala passward. Akagundua kuwa simu ile ilikuwa imeunganishwa na huduma ya roaming ambapo mtu huruhusiwa kupiga simu nchi nyingine bila shida. Aliitia mfukoni kisha akaendelea kukikagua kile chumba. Akagundua kulikuwa na milango mingine miwili. Akili yake ikamuagiza afuate mlango wa kushoto. Alichungulia kupitia sehemu ya kuingizia funguo upande wa chumbani. Aliona watu wawili mwanamke na mwanaume wakifanya mapenzi. Mwanaume alikuwa anaasili ya kizungu wakati mwanamke alikuwa ni Mtanzania. Hakujishuhulisha nao aliwaacha wajilie utamu kwa raha zao. Punde simu iliita aliyokuwa ameiweka mfukoni. Sauti ya simu iliwashtua na kuwafanya watazame mlangoni alipokuwa anachungulia Sajenti Warioba. Sajenti alijibanza huku hofu ikiwa imeupiga kofi moyo wake. Yule mwanamke aliamka kwenda kuchukua simu. Sajenti alikimbia mbio akairudisha ile simu kwenye sofa kisha akafungua ule mlango wa kushoto kama umeme. Kwa kweli Sajenti alikuwa amefuzu mafunzo ya kijeshi. Wepesi wake ulikuwa mfano wa kipanga anavyonyakua kifaranga cha kuku.

Akaurudishia mlango wakati huo yule mwanamke akiufungua mlango ule aliokuwa anachungulia Sajenti Warioba mwanzo. Sajenti alijibanza upande wa pili ambapo macho yake yalikutana na korido ndefu yenye mapipa mapipa.

"Kwenye line ya simu, hello! Ndio tumeondoka Tanzania.(upande wa pili unaongea bila Sajenti kusikia). Sawa mkuu" Yule mwanamke aliongea na simu kwa sauti ya mtu anayeongea na boss wake. Sajenti alishtuka kusikia kuwa wanaondoka Tanzania. Wanaondoka Tanzania kwenda wapi. Alitamani kujua kuwa wanaelekea wapi lakini nani wakumuambia. Je ajitokeze amuulize yule mwanamke. Thubutu yake! Labda kama hajipendi. Kwani alikuwa amesahau habari za zile maiti alizokuwa nazo ndani ya kontena. Au labda alikuwa amesahau kuhusu wale watu alioona vivuli vyao kule hospitali ya Ambagon waliokuwa wakijadili habari za ngozi za binadamu. Kama angekuwa amesahau hayo huenda angejitokeza na kumuuliza yule mwanamke.

Lakini Sajenti Warioba alikuwa anakumbuka vyema mambo hayo. Alikumbuka pia zile video alizoziona kwenye laptop yake zilizokuwa kwenye flash aliyoiiba kule kwenye lile jumba la watu wabaya kigamboni. Punde akiwa kajibanza pembeni ya mlango akasikia hatua za watu zikitokea koridoni zikija kule alipokuwa. Sajenti alichanganyikiwa. Alikuwa njia panda kuwa arudi kwenye kile chumba akakutane na yule mwanamke aliyekuwa anaongea na simu. Au awafuate wale watu anaowasikia wakija.

Akili yake ilicheza kama calculator. Akajificha kwenye pipa moja lenye rangi nyeusi lililokuwa karibu yake kama hatua tano. Sekunde hazikuisha wale watu walijitokeza wakija kuufuata ule mlango aliokuwa ametoka Sajenti. Hatua zao zilitoa mlio ulioutesa moyo wa Sajenti. Walitembea polepole lakini kwa vishindo. Yaani walikuwa wakipiga hatua tatu kisha wanasimama sekunde kumi. Hiyo iliuvuruga moyo wa Sajenti Warioba aliyekuwa amejibanza kwa kujikunyata mithili ya kinda la ndege lililonyeshewa na mvua. Walifika karibu na lile pipa alilokuwa amejificha wakasimama tena. Mara hii wakasimama kama dakika mbili hivi. Jasho jepesi lilianza kumtoka Sajenti. Alijua kuwa muda wa kuonekana umefika. Video za wale watu wanaochunwa ngozi alizoziona zilipita kichwani mwake. Alijua naye sasa muda mfupi ujao anaweza kuchunwa ngozi yake.

Akiwa katika kuwaza punde ilidondoka anjivu(kitambaa cha kujifutia usoni) karibu yake. Hapo akajua kwisha habari yake. Akaona mkono mweupe wenye kucha nzuri ndefu zilizopakwa rangi nyekundu na saa ya mkononi ukipapasa papasa chini kuchukua kile kitambaa. Ule mkono moja kwa moja Sajenti Warioba alijua kuwa ni mkono wa mwanamke mrembo na aliyezoea kuitumia vitu vya kifahari na anasa ya pesa. Alitamani akisogeze kile kitambaa kwenye ule mkono ili yule mwanamke ambaye hajamuona akichukue lakini atakisogezaje sasa maana alijua kama angepeleka mkono huenda mkono wake ungegongana na ule mkono mweupe. Mara ule mkono ulimfuata karibu na kiatu chake akawa anasogeza mguu wake ili usije ukaguswa. Bahati njema ule mkono ulikishika kile kitambaa na kukichukua. Moyo wa Sajenti ulikuwa umechakaa vibaya mno kwa tukio hilo. Ulikuwa mkono mweupe mzuri lakini uliacha majeraha makali ya hofu katika moyo wake. Sajenti akawaona wale watu wakiwa wanaelekea kwenye ule mlango aliotoka kisha wakashikamana tena. Alikuwa ni mwanamke na mwanaume. Mwanamke alikuwa mweupe mwenye umbo matata kama la kuchora. Alikuwa kavaa chupi tuu na sidiria zenye rangi ya kahawia. Nyuma ya mgongo wake kulikuwa na tattoo ya nyoka mwenye mabawa. Yule mwanamke na yule mwanaume walinyonyana ndimi zao kwa raha zao bila ya kujua kulikuwa na mtu nyuma yao aliyejificha kwenye pipa akiwatazama. Kama wangegeuka nyuma basi muda huohuo wangemuona Sajenti. Lakini mapenzi yaliwazidi nguvu. Yaliwapeleka mputa mputa hata muda wa kugeuka nyuma waliukosa. Waliingia ndani na kurudisha mlango hali iliyomfanya Sajenti Warioba ashushe pumzi nzito kama mtu aliyemaliza mbio ndefu. Akatoka hapo moja kwa moja akaelekea kule walipotoka yule mwanamke mweupe na yule mwanaume. Akaingia katika chumba kimoja ambacho kilikuwa na dirisha dogo. Akaenda kuchungulia kwenye kile kidirisha. Alishangaa kuona mawimbi ya bahari yakinesa nesa kwa madaha. Hakuamini macho yake. Inamaana nipo ndani ya meli. Alijiuliza lakini lilikuwa swali lenye jibu hapohapo. Alimkumbuka yule mwanamke aliyekuwa anaongea na simu kuwa ndio wanaondoka Tanzania. Hapa ndipo akaelewa kuwa kumbe walitumia usafiri wa majini kwa kutumia meli.

'Sasa tunaelekea wapi' Sajenti akajiuliza akiwa amekata tamaa. Hakuwahi fikiri kwamba kazi ile ingempeleka mpaka melini. Yeye alijua ni kazi ndogo tuu kwa uzoefu wake. Lakini kumbe alijiingiza katika shimo la watu hatari ambao kuua kwao ndio kazi. Masikini Sajenti!

Sajenti akaanza kukikagua kile chumba. Aliona meza kubwa ambayo juu yake kulikuwa na kete tatu za heroine. Chini ya ile meza kulikuwa na chupa kubwa ya vodka. Upande wa kushoto kulikuwa na kabati kubwa lililofungwa lakini funguo zake zilikuwa zinaning'inia. Akili ya udadisi ikamuambia Sajenti aende kulifungua aone kuna nini. Alilifungua lile kabati akashtuka kuona silaha tofauti tofauti za kivita. Aliona bunduki sita za aina tofauti tofauti. Aliona bastola nane na jambia moja lililokuwa linaning'inia. Yote haya aliyaona huku moyo wake ukicheza shere kwa hofu. Akashika lile jambia ambalo lilikuwa lina makali kama kiwembe. Kwenye mpini wa lile jambia aliona nembo ya A, akajua ilikuwa inamaanisha Ambagon. Akiwa anakagua lile jambia punde aliona taswira ya mtu kwenye lile jambia akiwa nyuma yake ameshika bastola. Kabla hajaamua kufanya lolote alisikia kichwa chake kikiguswa na kitu kama bastola. Alijua tayari ameshawekwa chini ya ulinzi. Asingeweza kujiongopea kuwa yupo katika ukingo wa mauti. Mate yalikauka mdomoni huku koo lake likiwa kavu kama mvuta sonyo. AKAmeza fumba kubwa la mate kwa tabu kupitia koo lake.

" quem você é?"

Sauti kavu ya kibabe kutoka nyuma iliongea. Ikimaanisha 'wewe ni nani". Sajenti hakuwa anajua lugha ya kireno hivyo hakuelewa anaulizwa nini.

" eu pergunto a você quem você é chamado. E o que voce quer?"

Yule mtu alimuuliza tena Sajenti Warioba huku akimpiga kitako cha bastola kwenye shingo. "nakuuliza unaitwa nani na unataka nini?". Maumivu makali yalipenya katika shingo ya Sajenti kutokana na kipigo alichopigwa na yule mtu aliyekuwa nyuma yake. Sajenti muda huo alikuwa ameweka mikono yake juu kama mateka. Pengine ungemshauri angempiga na lile jambia lakini angempigaje ikiwa jambia lenyewe lilikuwa limefungwa na mnyororo kwenye kabati. Hakuwa na mbinu ya maajabu zaidi ya kunyosha mikono yake juu. Aligeuka taratibu lakini kabla hajafanya hivyo akapigwa teke moja kali la mgongo akaangukia ndani ya lile kabati zilipokuwa zile silaha. Kwa haraka akainuka akiwa ameshika bastola yake akamgeukia yule mtu na kumnyooshea bastola. Alipojaribu kutekenya ulimi wa ile bastola aligundua kuwa bastola haikuwa na risasi.

"Hahahahaha! Wewe kichaa kumbe"

yule mtu alicheka akaongea kiswahili chenye lafudhi mbovu ya kireno. Sajenti aliishiwa pozi. Alibaki ameduwaa akiwa ameishika bastola isiyo na kitu. Akamtazama yule mtu ambaye alikuwa mbrazili mwenye umbo nene na midevu mingi kama wanafalsafa wa kigiriki. Kichwani alikuwa amevaa boshori huku mikono yake ikiwa imechorwa tattoo. Punde mlango ulifunguliwa akatokea kijana akiwa anaongea hata kabla hajaufungua mlango jambo lililofanya yule mbrazili bonge kugeuka ulipomlango. Hiyo ndio ilikuwa fursa ya Sajenti kujiokoa. Kabla mlangoni hajatokea mtu Sajenti akamrukia yule mbrazili kwa kumpiga kiwiko kwenye utosi. Lilikuwa pigo moja mujarabu lililompeleka chini yule mbrazili. Kijana alitokea mlango akapokelewa na bastola kidevuni. Ilikuwa kama filamu lakini lilikuwa tukio halisi. Kijana alibaki ameduwaa asijue afanye nini.

"Usiniue braza! Mimi siyo mtu mbaya. Tafadhali usiniue" yule kijana akasema akiwa anahofu kubwa usoni mwake. Maneno hayo yakamfanya Sajenti amkumbuke Joseph. Kijana aliyemuokoa kwenye lile jumba lakini yeye akashindwa kumuokoa. Sajenti alitazama uso wa yule kijana hakuona tashwishwi yoyote isipokuwa hofu.

"Walinichukua Dar es salaam. Sikujua mteja wangu kuwa ni jambazi. Tafadhali usiniue" yule kijana alizidi kumsihi Sajenti Warioba. Muda huu alikuwa amepiga magoti huku uso wake ukiwa unaangaliana na mdomo wa bastola aliyoishika Sajenti Warioba.

"Wewe unafanya biashara gani?" Sajenti aliuliza akijipa utulivu.

"Mm..mmh! Mimi ni shoga kakaangu"

yule kijana aliongea kwa kigugumizi huku akiona aibu kwa maneno aliyokuwa ameyatamka. Sajenti Warioba hakushtuka sana kutokana na maelezo ya yule kijana. Uzoefu katika kazi yake aliwahi shuhudia mambo kama hayo. Hivyo hilo halikumshangaza.

"Unamuda gani kwenye hii meli?"

"Nina kama miezi mitatu humu. Sijawahi kurudi nyumbani tokea niingie humu. Nirudishe nyumbani kaka yangu"

" Polepole"
Sajenti alimkatisha baada ya kuona yule kijana akizidisha sauti yake.

"Samahani kaka yangu. Nimechoka! Nimechoka kuwa mtumwa"

Kijana alisema akiwa amekunja mikono kama mtu anayesali. Aliongea kwa huruma sana mpaka machozi yakawa yanatoka. Sajenti aliingiwa na roho ya huruma. Katika maisha yake hakutaka kuona watu wanateseka. Aliapa kuwa atasaidia yeyote atakayehitaji msaada wake ikiwa anaouwezo wa kumsaidia. Leo hii kijana huyu anahitaji msaada wake.

"Acha kulia! Haya amka hapo chini" Sajenti alisema akimnyanyua yule kijana pale chini na mkono wake wa kushoto huku mkono wa kulia ukiwa umeshika bastola.
"Jina lako nani kijana?" Sajenti aliuliza akimtazama yule kijana.

"Nani? Mimi?"

"Ndio, kwa tupo wangapi humu?"

" Aaah! Sorry. Naitwa Omary"

"Sema majina yote. Omary nani?"


Sajenti akasema kwa ukali kidogo huku macho yake akiyakaza na kuyafanya yaogopeshe.

"Omary matatizo"

"Matatizo..! Okey sawa!”


Sajenti aliongea kwa mshangao huku akitabasamu.

"Unajua njia ya kutoroka humu ndani?" Sajenti Warioba aliuliza.

"Ndio naijua lakini kwa sasa tupo mbali sana kwenye bahari. Unataka kutoroka?"

Omary alisema hofu ikiwa imepungua. Omary kimaumbile alikuwa kijana mweupe kiasi aliyetoboa masikio na kuvaa hereni. Nywele zake aliziweka bleach ya rangi ya ugoro akiwa amenyoa kiduku. Macho yake yalikuwa yamelegea kiasi. Kama mtu asipomuangalia mara mbili basi anaweza kusema ni mwanamke. Sauti yake ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na sauti ya kike. Huyo ndiye Omary shoga katika meli kubwa ya Ambagon.

Sajenti alitafakari kidogo kidogo kisha akamjibu Omary.

"Ndio nataka kutoroka humu?"

"Kwani uliingiaje huku kaka?
" Omary aliongea huku akimrembulia Sajenti Warioba.

Hii ilimfanya Sajenti aone aibu kumtazama Omary kutokana na macho yake na namna anavyolamba lamba midomo yake. Omary aliligundua jambo hili. Hata hivyo hakujali.
"nitakuambia siku nyingine mdogo wangu. Tuondoke hapa kabla huyu hajaamka" Sajenti akasema huku akitaka kuondoka lakini Omary akamzuia.

"Hatuwezi ondoka tukamuacha huyu hapa. Akiamka atatoa taarifa alafu tutatafutwa. Wewe hilo hujalitafakari?" Omary akasema kama mtu mwenye akili sasa tofauti na muda ule alipokuwa akirembua na kulambalamba midomo yake. Sajenti aliitikia kwa kichwa kama ishara ya kumuunga mkono Omary kuwa kaongea kitu cha maana.

"Sasa tumfanyeje?" Sajenti aliuliza akimtazama yule mbrazil bonge aliyekuwa amezimia pale chini. Omary.hakujibu chochote. Alitembea moja kwa moja mpaka kwenye dirisha akabonyeza moja ya vitufe vilivyokuwepo pale. Dirisha likafunguka.

"Tumtupe baharini".

Omary alizungumza huku akiwa amegeuka alipokuwa amesimama Sajenti. Walimburuta. Looh! Lile librazil lilikuwa zito kama gunia la chumvi. Walijitahidi kumburuta mpaka dirishani. Hapo wakamnyanyua na kumtupa bahari. Sajenti na Omary walisimama dirishani wakiungalia mwili wa yule mbrazil ukidondoka mpaka ukatua baharini na kuyafanya maji ya bahari kutawanyika kuupisha mwili wa yule mbrazil. Bado ilikuwa usiku lakini karibia kulikiwa kuna kucha kutokana na uwepo wa mawingu ya njano yaliyosharabu mwanga wa jua. Sajenti na Omary walitoka kwenye kile chumba wakaanza kutembea kwenye zile korido. Aliyekuwa mbele ni Omary kutokana na kuwa alikuwa ndiye mwenyeji katika meli ile. Walifika sehemu wakakuta ngazi zakushuka chini. Hapa Sajenti akaingia wasiwasi. Alianza kujiuliza mbona amemuamini kwa haraka sana Omary. Je kama anampeleka kwa wale watu wabaya. Alikumbuka alipokuwa jeshini ambapo mwalimu wake wa jeshi aliwahi kumuambia asimuamini mtu yeyote. Iweje leo amuamini kijana huyu tena aliyemkuta katika mazingira hatari kama yale. Sajenti akasimama. Omary naye alipoona Sajenti kasimama naye akasimama kwenye ngazi ya nne kwenda chini kisha akatazama juu alipo Sajenti.

"Vipi mbona umesimama braza?"

Omary alimuuliza Sajenti akimtazama usoni.

"Huko ni wapi tunaenda?"

"Nakupeleka mafichoni. Sehemu ambayo watu hawafiki kwa urahisi"
Omary alisema akijaribu kumtoa hofu Sajenti Warioba. Omary alimhakikishia kuwa hawezi kumuuza wala kumsaliti. Sajenti Warioba aliuangalia uso wa Omary kuona kama ataona tashwishi yoyote lakini hakuona shaka yoyote. Walienda mpaka walipofika sehemu iliyokuwa kama karakana ya kuhifadhia vifaa chakavu. Omary akaufata mlango mmoja wa bati uliokuwa umeshika kutu. Alifungua ndani yake kulikuwa na giza. Sajenti alisimama mlangoni wakati Omary akiwa ameingia ndani.

"Braza ingia ndani" Omary alisema huku akiwasha taa ya chemli iliyokuwa mule ndani. Sajenti aliingia mule ndani. Chumba kilikuwa kinamakorokoro mengi ambayo mengi yao yalikuwa ni vipuri chakavu vya meli. Aliona godoro kuukuu likiwa limekunjwa na kufungwa kamba katikati. Omary akalifungua lile godoro akajilaza juu yake. Sajenti aliendelea kukikagua kile chumba. Akagundua kulikuwa na mlango mwingine mfupi kama futi nne. Alitaka kuuliza ule mlango ulikuwa ni njia ya kwenda wapi lakini akili yake ikamuonya asiulize maswali mengi. Sajenti alienda akakaa kwenye lile godoro. Alikuwa yupo hoi kwa kuchoka. Usiku mzima alikuwa hajalala. Pia alihisi njaa kali ikiutafuna utumbo wake, pia maumivu kwenye bega lake la kushoto yalizidi kumdhoofisha. Lakini asingeweza kumuambia kijana mdogo kama Omary. Alijilaza kwenye lile godoro na bila kujielewa usingizi ulimpitia. Alilala fofofo kama mtu aliyekufa. Hili lilikuwa kosa kubwa sana. Unawezaje kulala sehemu hatari kama ile. Sehemu yenye watu wabaya wasiyo na huruma. Watu ambao kuua kwao ni jambo la mzaha tuu. Alafu Sajenti ati analala. Kwa kweli hapa alifanya kosa kubwa mno. Akiwa amelala takriban lisaa limoja. Alihisi mtu akimpapasa kifuani mwake. Bado alikuwa katikati ya usingizi na akili ya kawaida. Alihisi mkono wa mtu ukimshika kifuani ukateremka mpaka kwenye sehemu zake za siri. Alijisikia raha sana. Akili yake iliingia katika ulimwengu mwingine kabisa. Sehemu zake za siri zilitomaswa zikibinywa binywa kwa ufundi mkubwa. Sajenti aligugumia kwa utamu aliokuwa akiupata. Punde suruali yake ikavuliwa na akashangaa mtu akimkalia juu yake. Alifumbua macho yake yake akakuta giza totoro. Alimsukuma yule mtu; alikuwa Omary. Sajenti alighadhibika sana. Aliwasha taa ya chemli.
"Hivi wewe unaakili kweli. Eeh! Unaniletea ushetani wako. Nani afanye huo usodoma wako. Nitakuua unajua wewe pusi"

Sajenti Warioba alifoka akimtingisha tingisha Omary ambaye muda huo alikuwa yupo uchi wa mbuzi mee.

"Umeniona mimi mchafu si ndio?"

Hapa Sajenti aliongea akimning'iniza Omary juu kwa kumkaba shingoni. Omary alipiga ukelele kwa maumivu aliyokuwa anayapata.

"Samahani braa..zaa! Mimi napenda sana mchezo huu. Nimeathirika kisaikolojia. Nisamehe! Utaniua kaka"

Omary aliongea huku sauti yake ikitoka kwa tabu kutokana na kukabwa na Sajenti Warioba.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 11)
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300


>>>>>>>>>> Episode 11 <<<<<<<<<<<<<<<<<

ILIPOISHIA
Sajenti Warioba alifoka akimtingisha tingisha Omary ambaye muda huo alikuwa yupo uchi wa mbuzi mee.
"Umeniona mimi mchafu si ndio?"
Hapa Sajenti aliongea akimning'iniza Omary juu kwa kumkaba shingoni. Omary alipiga ukelele kwa maumivu aliyokuwa anayapata.
"Samahani braa..zaa! Mimi napenda sana mchezo huu. Nimeathirika kisaikolojia. Nisamehe! Utaniua kaka"
Omary aliongea huku sauti yake ikitoka kwa tabu kutokana na kukabwa na Sajenti Warioba.


ENDELEA

*************************************************​
Tayari ilikuwa imefika saa tatu na nusu asubuhi. Njaa ilipamba moto katika matumbo yao. "Braza ngoja mimi nikakuletee chakula. Tukikaa humu tutakufa njaa. Tutafika bandari ya Durban, afrika kusini baada ya siku saba na nusu"

Omary aliongea huku akipiga piga miayo ya njaa. Sajenti hakuwa na ubishi wowote licha ya kuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa kuwa huenda Omary anaweza akaenda alafu akarudi na wale watu wabaya. Hilo lilimfanya akose amani. Lakini angefanya nini. Achague njaa au afe na wasiwasi wake. Omary akamuacha Sajenti mule ndani akaenda kuleta chakula. Sajenti alibaki mule ndani akitafakari mwenendo wa uchunguzi wake. Mpaka muda ule aliona yupo nje kabisa ya malengo ya uchunguzi wake. Yeye alikuwa anafanya uchunguzi wa uhalifu uliotokea siku ya harusi ya Adele na Robert. Alitakiwa arudishe majibu ya ni akina nani waliovuruga harusi ile. Ni kina nani waliomuua Ramla aliyekuwa mshenga wa Adele. Sasa yote hayo ameyaacha anachunguza mambo ambayo hakuyapanga wala hakutumwa. Hii ilitosha kumuambia kwamba ameshafeli. Ikapita nusu saa hivi. Hii ikampa kidogo mashaka. Mbona Omary harudi. Nini kimetokea huko alipoenda. Au kakamatwa. Au wanapanga namna ya kunikamata, machale yakaanza kumcheza. Akaamka akaenda kufungua ule mlango wa bati wenye kutu waliojia na aliotokea Omary kwenda kuleta chakula. Akajaribu kuufungua lakini ulikuwa umefungwa kwa nje. Ubaridi wa woga ulimpitia kwenye mishipa yake ya damu. Akajua tayari kakamatika kirahisi kama kuku wa kisasa. Akaenda kwenye ule mlango mwingine mfupi. Nao ulikuwa umefungwa na kufuli lakini kwa ndani. Punde akasikia mlango wa bati ukiguswa na mtu anayetaka kuufungua. Hakujua ni nani. Akaenda mpaka mlangoni akaweka sikio kwenye mlango kusikiliza mienendo ya upande wa pili. Aligundua kuwa aliyekuwa akiufungua ule mlango alikuwa yupo pekee yake.

"Omary!" Sajenti akaita kwa sauti ya chini kama mtu anayenong'ona.

“Braza ni Mimi" Omary aliitikia huku akiwa anaufungua mlango. Omary Aliingia akiwa kabeba mfuko wa karatasi. Wakarudishia mlango wakarudi kwenye godoro kukaa. Omary alimkabidhi Sajenti Warioba ule mfuko wa karatasi wa kaki ambao ndani yake kulikuwa na nyama choma na ndizi zilizokaangwa pamoja na chupa moja ya vodka.

"Mimi nimeshakula huko. Kula tuu braza" Omary aliongea akiwa ameanza mchezo wake mbaya wa kulegeza macho na kujilamba lamba. Mchezo huo ulikuwa unamkera sana Sajenti. Alitamani amwambie aache lakini alikumba msemo usemao mtumikie kafiri upate mradi.
"basi kula walau nyama" Sajenti aliongea akimbembeleza Omary ambaye muda huo alikuwa amelala kwa mapozi ya kike.

"Wewe kaka embu kuwa muelewa basi. Nimekuambia nimekula"

Omary aliongea kwa sauti ya kike kabisa. Huku akibetua betua midomo yake. Kitendo cha Omary kukataa kula chakula kilimfanya Sajenti aingiwe na wasiwasi. Alihisi huenda kile chakula kimewekewa madawa ya kulevya ambayo akila atasinzia. hivyo itawarahisisha kazi ya kumkamata. Akakumbuka zile kete mbili za heroine alizozikuta kule kwenye kile chumba cha mbrazili.

"Kama huli hata kipande kimoja cha nyama nami sitakula chakula chako" Sajenti akasema huku akikifunga kile chakula kwenye ule mfuko wa kaki. Alifanya hivyo kumjaribu Omary ingawaje alikuwa na njaa na alikitamani sana. Omary kuona Sajenti amesusa kula. Ilibidi aamke akaenda kuchukua kipande kimoja cha nyama na ndizi.

"Haya mume nawe amka ule. Najua huwezi kula wakati mkeo sili. Haya amka sasa" Omary alisema akiwa ameilegeza sauti yake. Sajenti alikasirika sana. Maneno ya Omary yalimkera kupita kiasi."Wewe ni fala nini. Usiniletee upuuzi hapa" Sajenti aligomba kwa sauti hali iliyomfanya Omary amuonyeshee ishara kuwa anapiga kelele.

"Shiiii! Acha kupiga kelele sasa. Mdomo uliponza kichwa shauri yako. Unadhani upo kwako humu" Sajenti alinyamaza hasira zikitingisha mashavu na midomo yake. Alitamani ampige hata makofi mawili lakini akakumbuka alipokuwa jeshini alivyofundishwa na mwalimu wake kuwa mwanajeshi mzuri ni yule anayeweza kuzuia mihemko yake. Akameza fumba la mate kisha akaanza kula. Ilikuwa ni nyama ya mbuzi iliyorostiwa kwa ufundi wa hali ya juu. Sajenti alikula haraka haraka mate yakimtoka mdomoni kwa utamu. Kwa kweli alifurahia mlo ule. Alimaliza kula wakawa wanapiga stori mbili tatu na Omary. Omary alianza kusimulia sababu iliyomfanya mpaka akajiingiza kwenye ushoga.

"Stori ndefu sana braza. Yaani sitaki hata kukumbuka" Omary alisema akiwa ametulia. Muda huu alionyesha uhalisia zaidi. Huzuni na simanzi ziliufunika uso wake. Machozi yalianza kumlengalenga. Nani ambaye asingeelewa kile ambacho anataka kuhadithia kuwa ni hadithi ya kusikitisha. Hadithi iliyojawa na visa vyenye simanzi na vilio. Sajenti Warioba kwa utulivu na ushawishi akazungumza.

"Omary! Kila hadithi inamsomaji. Kila ngoma inawachezaji. Tafadhali naomba unisimulie kwa ufupi" Omari alimtazama Sajenti Warioba kwa uso wa uchovu wa huzuni. Kisha akayakunja macho yake kama mtu anayekumbuka mbali.

"Nilimaliza shule ya msingi kwa msisi handeni. Nilikuwa naishi na bibi yangu mzaa Mama. Mama yangu alikuwa akiishi Dar es salaam maeneo ya mtoni mtongani ya temeke. Hakuwa akiishi na baba yangu kwani baba alikataa mimba yangu. Hivyo Mama akaamua kunilea yeye kama yeye" Omary aliweka kituo kwa kumeza fumba la mate. Alihadithia kwa utulivu sana. Sauti yake haikuwa ile yakishoga kama awali. Hata yale macho ya kurembua sasa yalikuwa hayarembui. Zaidi ya kuzingirwa na machozi. Omary akaendelea kusimulia.

"Mimba aliipatia huko huko Dar es salaam. Kama unavyojua mimba inahitaji uangalizi na malezi. Na Mama hakuwa na kazi ya maana zaidi ya uMama ntilie. Pesa zote alizopata ziliishia kwenye kodi. Hivyo mimba ilivyokuwa maisha ya Dar yakamshinda. Akaamua kurudi kwa bibi mpaka akajifungua mtoto wa kiume. Akamuita Omary matatizo" Uso wa Omary ulibadilika. Mdomo wake ulianza kutetemeka. Machozi yalitiririka kama mifereji katika mashavu yake. Alianza kulia.

"Sijawahi kumuona baba yangu tokea kuzaliwa. Sijui yupo wapi. Mama aliamua kumuita baba yangu matatizo. Matatizo! Matatizo! Ati matatizo ndio baba yangu. Omary matatizo. Hiiiiihiii" Omary alizidisha kulia kama yupo msibani. Hali iliyomfanya Sajenti ambembeleze. "Jikaze Omary. Wewe ni mwanaume. Usilie Omary"

" Ati mimi ni mwanaume. Omary mwanaume. Nilitoka handeni kama mwanaume nikiwa
Darasa la saba. Nilikuwa na miaka kumi na mbili. Nikafika Dar es salaam alipokuwa akiishi Mama na mume wake mpya ambaye ni baba wa kambo" Omary aliweka kituo kisha akavuta makamasi mepesi yaliyokuwa yananing'inia puani. Alijipangusa machozi machoni kisha akaendelea.

"Mama alikuwa muuza bar moja pale mjini. Alikuwa akiondoka saa tisa jioni na kurudi saa tano za usiku. Hapo alikuwa amepika chakula cha usiku. Baba yangu wa kambo akirudi tulikuwa tunakula naye. Baba alikuwa ni konda wa daladala zilizokuwa zinatoka Mbagala rangitatu kwenda makumbusho" Alimeza fumba la mate kisha akamtazama Sajenti Warioba aliyeonekana kunogewa na stori hiyo ya kusisimua.

"Eehe ikawaje sasa?" Sajenti aliuliza.

"Maisha ya pale mtongani nilianza kuyazoea. Pale nyumbani nilipaona kama nyumbani. Japokuwa sikupendezwa na tabia ya Mama kurudi akiwa amelewa lakini sikuwa na lakufanya. Mama alikuwa akilewa sana. Kila mara akirudi nyumbani alikuwa akimtukana baba" machozi yalianza kutiririka tena katika uso wa Omary. Na kila alipokuwa akifanya hivi Sajenti alijua kuna jambo baya anaenda kulisimulia. Hii ilimfanya azidishe utulivu.

" Mama alikuwa akimfukuza baba chumbani ati akalale sebuleni. Siku moja baba alikuja chumbani kwangu akagonga mlango. Nilimfungulia. Akanambia amekuja kulala na mimi. Nilijua tuu kafukuzwa na Mama. Alafu pale sebuleni kuna mbu. Hivyo alichoka kung'atwa na mbu" akameza fumba la mate na kuvuta makamasi puani. Kisha akaanza kulia kwa sauti ya kutetema. "Huruma zangu zikaniponza braza. Huruma! Huruma ni mbaya jamani!
Akapanda kitandani tukalala wote. Mara usiku nikiwa nimelala nikasikia mtu akinikumbatia mwili wangu. Nilitaka kujinasua lakini sauti nzito ikaniambia nisihofu. Ni baba. Nikabaki nimetulia tuu. Alinishika sehemu zangu za siri. Kisha akaniingilia. Nilisikia maumivu makali sana. Sitakaa nisahau siku ile".


Kufikia hapa Omary alilia mfululizo akiwa anatingishwa kichwa chake kama mtu anayekataa kuamini historia yake. Sajenti Warioba alibaki amemtizama Omary kwa huruma. Alimuona ni kijana mdogo asiyestahili madhila yote yale.

"Baba wa kambo akanipa elfu ishirini na kuniambia nisiseme. Niliiona ni pesa nyingi. Tokea hapo ikawa ndio tabia yangu kuingiliwa na baba. Wewe ulisema mimi ni mwanaume lakini mume wa Mama yangu alinigeuza mwanamke wake kwa miaka mitatu" Omary aliendelea kulia ikafikia hawezi kusimulia tena. Sajenti Warioba alimkumbatia akawa anambembeleza mpaka usingizi ulipompitia Omary.

Sajenti aliitafakari historia mbaya ya Omary aliyohadithiwa. Ilikuwa ni historia ya kikatili sana. Alitamani amjue huyo baba yake Omary wa kambo. Ili amfungulie mashtaka. Ona sasa kijana wa watu anapata tabu. Ona sasa amegeuzwa mwanamke huku katika meli za maharamia watu wenye roho za kuua. Sajenti aliwaza mambo yote hayo. Sajenti alipitiwa na usingizi bila kujua wote wakawa wamelala. Wakwanza kuamka alikuwa ni Omary. Omary aliamka na moja kwa moja alitoka kwenye kile chumba. Punde alirejea akiwa na mwanamke na mwanaume mmoja wa kireno. Omary alishangaa kutokumkuta Sajenti Warioba kwenye kile chumba.

"Nilimuacha amelala hapa" Omary aliongea akimtazama yule mwanamke.

" Wewe usituchezee akili. Yupo wapi huyo mtu" yule mwanamke alisema kwa hasira huku akimtazama.

"Alikuwa hapa kweli. Alikaa hapa akiwa anakula kile chakula mlichonipa" Omary akasema akiwa anaangaza macho yake huku na huko. Ni kweli Omary alimuacha Sajenti pale akiwa amelala. Sasa kaenda wapi. Hilo ndilo lililomchanganya. Omary alijua kuwa yule mwanamke siyo mtu wa mchezo. Kitendo cha kutokumkuta Sajenti Warioba pale chumbani kinaweza kuhatarisha uhai wake.

"Wee mbwa naona umeanza kunizoea. Sasa leo utambua mimi ni nani" yule mwanamke alionsema kwa sauti ya kibabe yenye dalili zote za shari.

"Ommy huenda yupo sahihi. Si unaona ule mlango umefunguliwa" yule mreno akasema kwa kiswahili kibovu kama kanjibai. Wote walitazama kwenye ule mlango mfupi wa futi nne. Walishangaa kutokuona kufuli pale. Waliusogelea ule mlango mfupi ambao haukua na kufuli. Waliamini aliyeiondoa kufuli ile ni Sajenti. Kama paka anavyonyata kunyemelea panya ndivyo walivyokuwa wakinyata kuusogelea ule mlango. Waliufikia. Yule mreno akaushika ili kuufungua. Aliushika akamtazama yule mwanamke aliyekuja naye. Yule mwanamke akamtingishia kichwa kama ishara ya kumruhusu aufungue ule mlango. Wakati huo yule mwanamke alijiweka tayari kufanya shambulio kwa hatari itakayo jitokeza. Waliufungua ghafla yule mreno alipigwa usoni hali iliyomfanya yule mwanamke apige risasi hovyo. Looh! Kumbe ilikuwa ni kipepeo kikubwa cheusi ndicho kilichompiga usoni.

"Hoiii!" yule mreno alishusha pumzi nzito akiwa kaanguka chini kwa hofu. Wote walikitukana kipepeo cha watu kilichokuwa kinaendelea kuruka ruka mule ndani. Wakaingia upande wa pili ambapo kulikuwa na mabomba na vipuri vikuukuu vya meli. Walidhani kuwa ndipo alipokuwa amekimbilia Sajenti. Hata hivyo walikuwa sahihi. Sajenti hakuwa na njia nyingine ya kutokea zaidi ya ule mlango mfupi wa futi nne. Kulikuwa na giza sana. Kilichowasaidia ni tochi ya simu aliyokuwa ameishika yule mwanamke. Walimulika kila sehemu lakini hawakuweza kumuona Sajenti. Mule ndani kulikuwa na tando nyingi za buibui. Hii iliwafanya kila mara kupangusa nyuso zao pindi ziliposhikwa na utando wa buibui. Wakatembea mule ndani kumsaka Sajenti lakini hapakuwa na dalili ya mtu . Omary yeye alikuwa amebeba taa yake ya chemli. Alihisi huenda Sajenti Warioba ni mzimu kama siyo jini. Inawezekanaje amuache akiwa amelala kwa dakika zisizozidi mbili alafu arudi amkose. Haya hata kama kakimbia basi amekimbilia wapi maana kama ni msako wameufanya mpaka wamechoka. Ile meli wanaijua ndani nje. Wanajua njia zote za kutorokea na kujifichia. Iweje mgeni awatoroke kienyeji kiasi kile.

Moja kwa moja Omary alijua kuwa ataonekana ni muongo. Na uongo ni kosa kubwa katika kundi la Ambagon. Kosa ambalo hukumu yake ni kifo. Omary akajuta. Aliona ni bora asingeenda kumshtaki Sajenti kwa wale watu wabaya. Punde walisikia kwa mbele kitu kikichakura chakura. Hima walinyoshea bastola zao upande ule waliosikia sauti hiyo. Yule mwanamke akamulika tochi kuelekea upande waliosikia sauti. Aliishia kusonya baada ya kumuona panya akiwa anakula fupa la nyama. Kwa hasira alimpiga panya yule risasi aliyekuwa akisheherekea msosi wake. Walishusha pumzi kupunguza hofu iliyosababishwa na panya ambaye walidhani ni Sajenti. Baada ya kutafuta kwa muda mrefu kama lisaa limoja na nusu. Wakachoka.

"Leo utatutambua. Huwezi kutudanganya kama watoto wadogo" yule mwanamke aliongea kwa ukali kama mtu aliyeaibishwa.

"Dadaangu! Nilikuwa naye. Kwa nini nidanganye..."

" Wee koma! Mimi siyo dadaako. Mbwa wewe leo utanijua mimi ni nani"
Yule mwanamke alimkatiza Omary akamkunja tai shingoni na kumsogelea usoni. Nyuso zao zikiwa zimekaribiana zero distance.

"Nisamehe dadaangu"

"Nimekuambia mimi siyo dadaako. Kaa kimya nguruwe wee!"


alimkemea na kumchapa kofi kali la shavuni. Waliondoka kule chini wakafunga kile kimlango kwa nje ili kama kweli Sajenti aliingia mule ndani asiweze kutoka. Muda wote huo Sajenti Warioba alikuwa amejificha ndani ya bomba moja kubwa ambalo alilifungua kwa kulisogeza. Maneno yote waliyoyaongea aliyasikia. Alimlaumu sana Omary kwa kitendo cha kumsaliti. Sajenti alikuwa tayari kumsaidia Omary kutoka mule ndani ya meli. Alipanga kuwa kama angefanikiwa kumtorosha kutoka mule melini angeenda kumsomesha ili naye awe na maisha yake. Lakini kumbe Omary alikuwa ni mtu mbaya asiyefaa hata kwa mkopo. Sajenti aliona hata ile hadithi aliyosimuliwa na Omary huenda ilikuwa ni danganya toto. Hakuiamini tena. Zaidi ya yote alishukuru kwa kuwa salama mpaka muda ule. Akatoka kwenye lile bomba akiwa hoi kwa kujikunja mule bombani. Akajinyoosha kuviweka sawa viungo vyake huku akivuta pumzi kufidia pumzi aliyoikosa alipokuwa ndani ya lile bomba. Kutokana na kukaa muda mrefu kwenye bomba macho yake yalikuwa yameshazoea giza. Aliona kiasi cha kumfanya atembee bila kujikwaa. Alikaa kule chini siku mbili mfululizo bila kula. Njaa ilimuuma sana. Akafanya mbinu zote alizozijua na alizofunzwa ili atoke kule chini lakini ilishindikana. Alikiona kifo kwa mbali kikimkonyeza kwa dhihaka. Alibaki anakitazama tuu asijue afanye nini wala akiambie nini. Akatembea tembea kule chini kuona kama atapata upenyo wowote wa kutoka lakini hakuona dalili yoyote ya kuwepo kwa upenyo. Punde akafika sehemu ambayo alisikia harufu kali ya kitu kilichooza. Itakuwa ni harufu ya nini hii. Sajenti alijiuliza huku akiifuata harufu inapotokea. "fuuuh! Mmmh!" alishika pua yake. Aliona mzoga wa panya ukiwa unafunza. Ni yule panya aliyeuawa kwa risasi na yule mwanamke mwenye roho mbaya. Sajenti Warioba awali aliwahi kusikia kuwa hakuna kifo kibaya kama kifo cha moto. Pia aliwahi kusikia kuwa hakuna kifo cha kikatili kama kifo cha maji. Kama kuna vifo alivyowahi kuviona ni vya kikatili basi ni kifo cha kuchinjwa na kisu au panga. Lakini leo mawazo yake yalibadilika. Alibadilisha mtazamo kuhusu kifo kibaya na cha kikatili kama siyo mateso. Leo hii kama angeulizwa ataje kifo kibaya basi angesema bila hata kufikiri kuwa kifo cha njaa ndio kifo cha kikatili chenye maumivu makali yasiyosemeka. Usicheze na njaa. Hata wahenga walikwisha sema kuwa adui yako mwombee njaa. Njaa ni habari nyingine kabisa. Sajenti nguvu zilimuisha kabisa. Aliona akitembea anapepesuka. Aliishika bastola yake. Akaitazama.

" Leo nataka uniue rafiki yangu. Umenisaidia sana rafiki yangu. Leo nami nataka uniue" Sajenti aliiambia bastola yake iliyokuwa ikimtazama bila kujibu chochote. Akaibusu kama ishara ya mapendo. Sajenti alikuwa katika hatua ya mwisho ya kufanya maamuzi ya kujiua. Aliona ni bora ajiue kuliko mateso aliyokuwa anayapata. Aliona ni heri mateso ya risasi yatakayodumu kwa sekunde chache kuliko mateso ya njaa yanayomtesa kwa muda wote ule.

Akaingiza kidole kwenye kilimi cha bastola yake. Kijasho chepesi cha njaa na hofu kikamtoka. Alipumua kwa nguvu. Hofu ya kifo ilimshika. Akaanza kuhesabu. Moja, mbili... Kabla hajafika tatu alishtuka kusikia kitu kinatembea tembea upande wake wakulia. Akageuka upesi kutazama. Huuh! Kumbe alikuwa panya. Alimpiga yule panya risasi ambayo ilimchakaza kichwani. Akamchukua yule panya. Mate yalimtoka mdomoni ungedhani aliona nyama choma. Lakini haikuwa nyama choma bali panya buku jike aliyenona. Alijua kabisa kuwa panya haliwi lakini atafanya nini ikiwa hakukuwa na kitu kingine cha yeye kula. Alianzia iliposhingo yake iliyokuwa inavuja damu. Hakika alijisikia kinyaa lakini kinyaa hakikuzidi njaa yake. Alimaliza kula panya wote kasoro mkia wake. Hahaha! Alijicheka kwa kula panya. Sajenti alipata nguvu mpya. Akahisi ahueni kidogo. Sasa hakutaka azidiwe tena na njaa mpaka ashindwe kufikiri vizuri namna ya kutoroka. Aliwahi kuambiwa na mwalimu wake jeshini kuwa njaa humfanya mtu asifikiri vizuri. Pia njaa humfanya mtu akubali jambo lolote lile bila kujali kuwa jambo hilo ni zuri au baya. Ndio maana adui ukimkamata unamnyima kwanza chakula. Hapo lazima utapata unachokihitaji. Alienda kwenye ule mlango mfupi ambao ulifungwa kwa upande wa pili. Alijaribu tena kuufungua lakini haukufunguka. Alipata wazo kuwa aitumie bastola yake kufungua mlango ule. Wazo hili aliliona ni jema na linafaa kabisa. Aliichukua bastola yake akaiweka usawa wa ilipokufuli iliyopo upande wa pili. Akafyatua risasi paa! Akapiga ingine paa! Akasikia kufuli likidondoka chini upande wa pili. Hapo akajua kazi imekwisha. Alifungua mlango. Akakuta lile godoro likiwa vilevile alivyoliacha. Akaondoka kwenda kwenye mlango wa bati wenye kutu. Nao ulikuwa umefungwa kwa nje. Aliichukua bastola yake akapiga sehemu aliyohisi inakomeo lililofunga mlango ule. Nao ukafunguka.



*************************************************​

Siku saba zilipita meli ikatia nanga katiba bandari ya Durban iliyopo afrika ya kusini. Safari ya kueleke brazil ilianza. Kutoka bandari ya Durban mpaka bandari ya santos nchini brazil ni siku zaidi ya ishirini ukiwa baharini. Umbali kutoka Durban mpaka bandari ya santos ni
4838 nautical miles. Nautical mile ni kipimo kinachotumika kupima umbali katika safari za angani na majini. Sajenti Warioba bado aliendelea kuishi kwa ujanja ujanja mule ndani kama mjusi wa ukutani. Alikuwa akiiba makombo ya wale mabaharia pindi walipokuwa wanayatupa kwenye vyombo vya takataka. Siku kumi na tano zilimfanya aizoee ile meli. Tayari alikuwa naye ni miongoni mwa mabaharia katika meli ile. Ingawaje yeye alikuwa baharia wakujificha.

Siku ya ishirini na tisa meli ya Ambagon ilitia nanga katika kisiwa cha ilhal montao de trigo ambacho kipo karibu kabisa na bandari kubwa ya santos iliyopo Brazil. Walifika usiku wa saa sita. Kulikuwa na giza anga lote likiwa limetawaliwa na nyota. Sajenti alianza kufanya harakati za kutoroka. Alipanda mpaka vyumba vya juu bila ya kuonekana. Akafika kwenye korido moja ndefu kiasi ambapo kulikuwa na milango miwili upande na upande. Akaufuata mlango mmoja akachungulia. Alishangaa kuona Hall kubwa lenye watu wa rangi tofauti tofauti wakifanya starehe. Lilikuwa ni kasino la ile meli. Moyoni alijisemea kumbe hii meli inawatu wengi kiasi hiki. Wale watu katika lile kasino walikaa kwa mzunguko kufuatana na mpangilio wa viti na meza. Juu ya meza zao kulikuwa na vinywaji mbalimbali vya gharama. Vinywaji vingi vilikuwa ni pombe kali. Sajenti aliendelea kuchungulia akichunguza mule ndani. Lakini ghafla alihisi kitu kigumu kikigusa kichogo chake. Bila kupoteza muda Sajenti Warioba akageuka na pigo moja takatifu la kiwiko cha mkono kilichompata yule mtu aliyemuwekea bastola kwa nyuma. Yule mtu aligugumia bastola ikiwa imeanguka sakafuni. Sajenti aligeuka. Hamadi! Alikutana na jitu kubwa kama licheza mieleka. Bila shaka lilikuwa mlinzi wa lile kasino. Lilikuwa jitu kubwa la miraba minne. Jeusi tii lililonyoa kipara kichwani. Kifuani lilikuwa na maziwa liliyokuwa likiyachezesha chezesha kibabe kumtisha Sajenti Warioba. Sajenti hakuwahi kuona mtu wa namna ile tokea kuzaliwa. Watu wa namna hii aliwahi kuwaona tuu kwenye video hasa mchezo wa mieleka.

Sajenti akalisogelea lile jitu ambalo aliliita Umaga. Wakawa wanazunguka zunguka kila mmoja akimtafutia mwenzake nafasi ya kumshambulia. Umaga akarusha ngumi. ikapita pembeni ya sikio la Sajenti. Upepo aliousikia Sajenti uliingia sikio hili ukatokea sikio la pili. Ilikuwa ngumi ambayo kama ingempata Sajenti basi ingemsababishia madhara ikiwezekana kifo. Sajenti alijua kuwa ili alipige lile jitu alihitajika atumie mbinu ya kupigana akiwa mbali kidogo. Kwa kuhofia kukamatwa na jitu lile jeusi ambalo uso wake ulihifadhi ukatili wa kila namna. Sajenti akarusha ngumi ikalipiga kwenye tumbo. Lile jitu likacheka. Likamuamuru apige zaidi na zaidi. Sajenti akaona sasa hii dharau. Akaifunga ngumi yake kisha akaitupa tena kwa nguvu zake zote. Lakini ilitua kama mzaha katika tumbo la lile jitu na kudunda kama kitenesi. Lile jitu lilicheka kwa dharau. Likajitutumua likikaza kifua chake. Sajenti aliingiwa na woga. Akarudi nyuma polepole lile jitu likimfuata huku likinguruma kama simba. Likarusha ngumi nzito Sajenti akaikwepa. Likarusha ngumi ya pili Sajenti akainama ikapita kama panga boya lkikata upepo. Sajenti akamrukia na kumpiga kichwa cha kidevu. Lile jitu uso wake ukainuka juu huku jino moja likiruka juu. Lilikuwa pigo takatifu ambalo kama angepigwa mtu mwenye afya mgogoro angekufa papohapo lakini lile jitu lilipandisha maruhani. Likamfata Sajenti Warioba kama mbogo aliyejeruhiwa huku mdomoni likivuja damu. Sajenti alirudi nyumanyuma mpaka akafikia ukutani. Lilirusha ngumi ikapiga bega la Sajenti, akagugumia kwa maumivu makali. Ni bega lile lile aliloshambuliwa na risasi kipindi kile akiwa kwenye hospitali ya Ambagon.

Lile jitu likampiga teke la tumbo Sajenti akadondoka chini karibu na ile bastola ya lile jitu. Kwa kweli Sajenti hakuwa tayari kupokea pigo jingine. Aliichukua ile bastola na kumpiga risasi ya kichwa lile dubwana likamuangukia kwa juu. Dooh! Lilikuwa zito kama gunia la kahawa. Akalisukuma kwa pembeni kisha akaliburuza mpaka mafichoni. Alilipekua katika mifuko ya suruali yake akakuta kadi iliyowekwa nembo ya Ambagon ambayo ni herufi A. Akarudi kwenye ule mlango akaufungua kisha akatoma ndani ya kasino. Hakuna aliyekuwa na habari na mtu. Kila mtu alikuwa yupo bize kujipa raha za dunia. Kwa mbele aliona jukwaa kubwa ambapo aliwaona malaya wakiwa uchi wa mnyama wakicheza kwa madoido na ushankupe. Aliwaona wazungu, waafrika na waarabu. Karibu mataifa yote aliwaona wawakilishi wao kwenye lile jukwaa. Alitembea akijifanya mwenyeji ili asije akashtukiwa. Alipigana vikumbo na wanawake malaya waliokuwa wamesimama kwa kukosa wanaume wa kukaa nao. Kila meza alikuwa amekaa mwanaume na mwanamke. Wanaume wengine walikuwa wanavuta sigara wakiwa vifua wazi. Wengine walikuwa wamevaa suti kali za gharama. Wengi wao umri wao ulikuwa kati ya miaka thelasini na nane mpaka sabini.

Sajenti alikaa meza moja iliyokuwa na mzee mmoja mwenye asili ya kihindi aliyevaa miwani nyeusi na kofia kama la cowboy wa kimexico. Hakumsalimia akakaa tuu na kujifanya yupo bize kuangalia lilipojukwaa walipokuwa wanacheza wale Malaya wakifuata mdundo wa muziki uliokuwa ukipiga. Sekunde haikuisha alikuja mwanamke mweupe mwenye asili ya kibrazil.

"suas notícias bom irmão" mwanamke aliyekuja alimsalimia Sajenti. Sajenti aligeuka kumtazama na kumjibu.

"ola'" Sajenti alijibu kwa kifupi. Akimaanisha sijambo. Kwani alisalimiwa 'habari yako kaka'. "Wewe ni mswahili. Mbona unaongea kama Mtanzania" yule mwanamke aliongea kiswahili kibovu sana. Sajenti alishangaa kusikia yule mwanamke akiongea kiswahili. Kwa haraka akajibu.

"Hapana mimi ni mkenya. "

"Ahaa! Ulipandia mombasa?"

"Ndio! Nawe ulipandia wapi?"
Sajenti alijibu haraka alafu naye akamtupia swali.

" Mimi mwenyeji wa mji wa Juquei. Ilipofukwe nzuri za Juquei. Huwa nakuja kwenye hii meli kwa kazi hii" yule mwanamke alisema akitingisha tingisha nywele zake ndefu zisiingie machoni. Akapeleka glass mdomoni aliyokuwa ameishika mkononi.

"Ahaa! Sawasawa!" Sajenti aliitikia akihitaji maelezo ya ziada.

"Nipo hapa kwa ajili ya kuwapa wanaume raha. Wafikapo katika kisiwa hiki cha montao de trigo kila mrembo humu hujichukulia mteja wake" yule mwanamke alisema.. Sajenti aligundua kuwa yule mwanamke alikuwa anaitwa Fernanda da silva kutokana na kitambulisho kilichokuwa kinaning'inia shingoni mwake.

"Utanilipa bei gani. Ninasehemu nzuri ya kulala tukitoka humu" Fernanda akasema akiyashika mabega ya Sajenti Warioba akiwa kamzunguka mgongoni. Hapa Sajenti akili yake ikamuambia kuwa hii ndio ilikuwa nafasi yake ya mwisho kutoka mule ndani. Aligundua kuwa kumbe ile meli licha ya kuwa inasafirisha miili na viungo vya watu lakini pia kulikuwa na matajiri waliokuwa wakizunguka dunia nzima wakiponda raha na wanawake malaya huku wakinywa na kula. Bila shaka wengi wa wasafiri mule ndani ya ile meli hawakujua kuwa meli ile pia ilikuwa inasafirisha bidhaa za magendo. Kama wangelijua huenda hata wasingethubu kuingia humo.

Muda wa kutoka melini ukawadia. Ilikuwa ni asubuhi tulivu kabisa katika kisiwa cha montao de trigo. Sajenti na Fernanda walikuwa kwenye msururu mrefu wa watu wanaotoka nje ya meli. Walipofika mlango wa kutokea walitakiwa wakabidhi vile vitambulisho. Fernanda alitoa kitambulisho chake wakati Sajenti Warioba akihaha kwa wasiwasi. Sajenti naye alitoa kile kitambulisho cha lile jitu alilopigana nalo kule ndani. Yule mkaguzi alikikagua kile kitambulisho kwa muda kidogo tofauti na alivyofanya kwa Fernanda. Moyo wa Sajenti alipwita pwita kama ringi la gari. Aliomba kimoyo moyo wasije wakamshtukia. Yule mkaguzi alimtazama usoni Sajenti Warioba kama ataona tashwishi yoyote lakini Sajenti alitabasamu kirafiki kumuondoa hofu. Yule mkaguzi naye alitabasamu na kumruhusu. Sajenti alishusha pumzi akiwa haamini. Chezea Ambagon wewe. Moto wa Ambagon siyo wa kitoto. Wakatoka; Fernanda akiwa amemshika kiuno chake. Punde alimuona yule mwanamke aliyemuona akifanya mapenzi kule katika meli, aliyetoka kupokea simu wakati Sajenti akiwa kajificha upande wa pili wa mlango. Ndio huyohuyo mwanamke aliyekuja na mwanaume wakireno aliyekuwa akimfokea Omary. Sajenti akamtazama kwa jicho la kuiba iba. Punde yule mwanamke aligeukia kule alipokuwepo Sajenti Warioba. Wakagongana macho lakini Sajenti akayaondoa macho yake na kumtazama Fernanda. Yule mwanamke aliingiwa wasiwasi kwa kitendo cha kumuona Sajenti Warioba. Hata hivyo alimpuuzia. Walitembea mpaka zilipo teksi za uber. Wakapanda na moja kwa moja wakaelekea upande wa pili wa ufukwe. Hapo Fernanda akamuambia Sajenti Warioba kuwa watapanda boat ya kuelekea ilipo beach ya Juquei ambapo ndio nyumbani kwake, Fernanda. Wakapakia boat na ndani ya nusu saa walikuwa wamefika fukwe ya Juquei.

Fukwe ya Juquei ilikuwa na mchanga mzuri mweupe. Maji yake yalikuwa meupe ambayo ukiyatazama unaweza kuona samaki anayepita chini kabisa. Pia ni fukwe ambayo ilikuwa na milima yenye kijani cha kupendeza. Ilikuwa ni saa mbili asubuhi lakini watu walikuwa wengi. Hasa watalii waliokuja kufanya utalii. Sajenti alivutiwa na mandhari ya fukwe ile. Walitembea kwa miguu mwendo wa dakika kumi wakiiacha fukwe ya Juquei wakikatiza mitaa na kona ya mji mdogo wa Juquei. Punde walisimama mbele ya geti jeusi ambapo Fernanda alienda kulifungua kisha wakaingia ndani. Sajenti alistaajabu mandhari ya mule ndani. Akaona bustani zenye maua ya kupendeza ya kila rangi. Aliona pia swimming pool la kuogelea ambapo pembeni yake kulikuwa na viti na vitanda maalumu vya kulalia. Mbele yake alitazamana na jumba kubwa la kifahari lenye madirisha ya aluminium na vioo vya gharama. Juu ya jumba lile kulikuwa na vigae vya rangi ya damu ya mzee ambavyo ndio vilikuwa paa la jumba lile. Fernanda alimkaribisha ndani Sajenti Warioba ambaye macho yake yalikuwa yakistaajabu kila alichokuwa anakiona.

"Hapa ni wapi Fernanda?" swali lilimponyoka Sajenti huku wakiwa wameshaingia sebuleni.

"Hapa ni kwangu mume wangu” Fernanda alijibu akijitahidi kuongea kiswahili kilichonyooka.

Mpaka muda huo Fernanda hakujua Sajenti alikuwa anaitwa nani. Wala Sajenti hakumuuliza Fernanda jina lake. Kama unakumbuka Sajenti alijua jina la huyu mwanamke wa kibrazil baada ya kusoma kitambulisho alichokuwa amekivaa kule kwenye kasino wakiwa melini.

Ni kawaida kwa malaya kutokuuliza majina ya wateja wao. Unajua kwa nini. Labda na wewe unaweza kujua ni kwasababu gani. Ila sababu kubwa ni kuwa watauliza majina ya wateja wangapi, kwa maana wao hulala na watu wengi. Hicho ndicho kinawafanya wasiulize majina ya wateja wao labda wawe wateja wa kudumu. Sajenti Warioba alipitisha macho yake kukagua sebule ya nyumba ile. Aliona picha kubwa ikiwa ukutani ikimuonyesha Fernanda akiwa amevaa gauni jeupe la harusi. Pembeni yake kulikuwa na picha nyingine ndogo ikimuonyesha Fernanda akiwa na Mama wa makamo ambaye moja kwa moja Sajenti alijua atakuwa ni Mama yake na Fernanda kutokana na kufanana.

Fernanda alikuwa kaingia ndani akiwa kamuacha Sajenti pale sebuleni. Sajenti aligundua sebule ile ilikuwa na kamera za siri za cctv zilizotegwa kwenye feni iliyokuwa juu ikizunguka upande huu na upande huu waliyoikuta ikiwa hivyohivyo inazunguka. Kamera nyingine ilikuwa imetegwa kwenye kinyago cha dragon kilichokuwa juu kabisa ya kabati la vyombo lililokuwa kwenye sebule ya kulia chakula. Ni elimu na mbinu za kijeshi ndizo zilizomsaidia Sajenti Warioba kujua kuwa mule ndani kulikuwa na kamera. Mtu wa kawaida wala asingeweza kujua jambo hili.

Hofu na mashaka vilibisha hodi katika moyo wake. Iweje Fernanda aweke kamera humu ndani. Fernanda ni nani hasa. Je ni kazi hiihii ya umalaya ndio mpaka nyumba hii ifungwe kamera. Au kuna kazi ingine anayoifanya Fernanda. Hata hivyo Sajenti hakutaka kumuamini sana Fernanda. Atawezaje kumuamini ikiwa walikutana kwenye meli hatari ya Ambagon. Sajenti aliamini kuwa mtu yeyote aliyekuwa kwenye ile meli hakupaswa kuaminiwa. Aliwaona watu wote mule ndani ni watu hatari na wauaji. Punde Fernanda alitoka chumbani akiwa kavaa taulo la kuogea. Alitembea kwa madaha kama mlimbwende anayetumbuiza jukwaani. Alilegeza macho yake ya kijivu na kuzirusha rusha nywele zake mbele na nyuma kumchanganya zaidi Sajenti. Sajenti alipagawa akajisemea kuwa leo amekamatika. Leo napewa mapenzi ya kimataifa. Yeye si alizoea mapenzi ya kibongo bongo leo kakutana na Fernanda malaya aliyebobea katika tasnia ya ukahaba. Fernanda akatembea kimanjonjo mpaka ilipo home thietre kubwa ya muziki. Kisha akawasha muziki wa kibrazili. Kisha akabenjuka na kumtazama Sajenti na macho ya uchu. Fernanda ndio kaanza hivyo. Sijui kama Sajenti atasalimika na mahaba ya kibrazil.

Akapeleka kidole mdomoni akaking'ata kisha akafumba macho yake kwa madaha na kuyafumbua polepole yakiwa yanarembua. Muda wote alikuwa akifanya hivi huku akimtazama Sajenti aliyekuwa kasimama kama sanamu la michelin. Muziki ulianza kuchanganya. Fernanda alihakikisha mapigo ya muziki hayamuachi. Alikata mauno muziki ulipohitaji akate mauno. Alitingisha matako muziki ulivyomuamrisha kufanya hivyo. Akainama chini na kuanza kutambaa kama mtoto kumfuata Sajenti ambaye muda huo alikuwa hajielewi. Kisha akasimama upesi akiwa amemkaribia Sajenti kama hatua moja. Wakiwa wanatazamana huku muziki ukiimba kama filamu ya kihindi. Fernanda akashika lile taulo lake akalirusha juu likanata kwenye feni. Feni ikawa inazunguka na lile taulo. Fernanda akabaki uchi kama alivyozaliwa huku cheni ya dhahabu ikiwa kiunoni na pete ikiwa kitovuni. Kitendo cha Fernanda kulirusha taulo juu ya feni Sajenti alikielewa. Alijua kuwa Fernanda kafanya vile makusudi kuziba kamera ili isiwachukue video wala kuwapiga picha. Sajenti akanyanyua uso wake juu kulitazama lile taulo. Alishangaa kuliona likiwa limeiziba kwa ufasaha ile kamera. Moyoni alimuona Fernanda kama mwanamke mwenye shabaha sana. Mtu mwingine asingeweza kurusha vile tena bila ya kuangalia juu.

Muda huo Fernanda hakujua kuwa Sajenti kaelewa mchezo mzima. Fernanda akamshika Sajenti shingoni na kumnyonya mdomo wake. Walinyonyana ndimi kwa dakika tano mfululizo huku Fernanda akimchojoa Sajenti nguo zake. Dakika kumi wote walikuwa wapo uchi wakipumua kama bata dume. Walifanya mapenzi palepale sebuleni kila mmoja akionyesha utundu wake. Hii ilikuwa kama finali ya kombe la dunia la mapenzi. Timu ya brazil ikiwakilishwa na Fernanda na timu ya Tanzania ikiwakilishwa na Sajenti. Mechi ilikuwa ni kali kila mmoja akijaribu kushambulia. Mpaka dakika ya tisini walikuwa wamefungana mbili mbili. Mechi ilienda matuta ambapo kwa mara ya kwanza kombe la dunia likaenda Tanzania. Walienda kuoga wakarudi kitandani kupumzika. Fernanda hakuamini kwamba kuna mwanaume anaweza kufanya mapenzi kwa kiwango kile mpaka aridhike. Amefanya mapenzi na wanaume wengi lakini wote hakuna aliyewahi kumfikisha katika pepo ya mahaba. Leo hii kwa mara ya kwanza alionja pepo pasipokifo akiwa na Sajenti Warioba.

"Wewe hata usiponilipa. Kiukweli umenifurahisha. Tutapumzika alafu jioni tutafanya tena" Fernanda alisema akiwa kalala kifuani mwa Sajenti akisikiliza mapigo ya moyo wa Sajenti yakikimbia.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 11)
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300



ILIPOISHIA

Sajenti Warioba alifoka akimtingisha tingisha Omary ambaye muda huo alikuwa yupo uchi wa mbuzi mee.
"Umeniona mimi mchafu si ndio?"
Hapa Sajenti aliongea akimning'iniza Omary juu kwa kumkaba shingoni. Omary alipiga ukelele kwa maumivu aliyokuwa anayapata.
"Samahani braa..zaa! Mimi napenda sana mchezo huu. Nimeathirika kisaikolojia. Nisamehe! Utaniua kaka"
Omary aliongea huku sauti yake ikitoka kwa tabu kutokana na kukabwa na Sajenti Warioba.


ENDELEA

*************************************************​
Tayari ilikuwa imefika saa tatu na nusu asubuhi. Njaa ilipamba moto katika matumbo yao. "Braza ngoja mimi nikakuletee chakula. Tukikaa humu tutakufa njaa. Tutafika bandari ya Durban, afrika kusini baada ya siku saba na nusu"

Omary aliongea huku akipiga piga miayo ya njaa. Sajenti hakuwa na ubishi wowote licha ya kuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa kuwa huenda Omary anaweza akaenda alafu akarudi na wale watu wabaya. Hilo lilimfanya akose amani. Lakini angefanya nini. Achague njaa au afe na wasiwasi wake. Omary akamuacha Sajenti mule ndani akaenda kuleta chakula. Sajenti alibaki mule ndani akitafakari mwenendo wa uchunguzi wake. Mpaka muda ule aliona yupo nje kabisa ya malengo ya uchunguzi wake. Yeye alikuwa anafanya uchunguzi wa uhalifu uliotokea siku ya harusi ya Adele na Robert. Alitakiwa arudishe majibu ya ni akina nani waliovuruga harusi ile. Ni kina nani waliomuua Ramla aliyekuwa mshenga wa Adele. Sasa yote hayo ameyaacha anachunguza mambo ambayo hakuyapanga wala hakutumwa. Hii ilitosha kumuambia kwamba ameshafeli. Ikapita nusu saa hivi. Hii ikampa kidogo mashaka. Mbona Omary harudi. Nini kimetokea huko alipoenda. Au kakamatwa. Au wanapanga namna ya kunikamata, machale yakaanza kumcheza. Akaamka akaenda kufungua ule mlango wa bati wenye kutu waliojia na aliotokea Omary kwenda kuleta chakula. Akajaribu kuufungua lakini ulikuwa umefungwa kwa nje. Ubaridi wa woga ulimpitia kwenye mishipa yake ya damu. Akajua tayari kakamatika kirahisi kama kuku wa kisasa. Akaenda kwenye ule mlango mwingine mfupi. Nao ulikuwa umefungwa na kufuli lakini kwa ndani. Punde akasikia mlango wa bati ukiguswa na mtu anayetaka kuufungua. Hakujua ni nani. Akaenda mpaka mlangoni akaweka sikio kwenye mlango kusikiliza mienendo ya upande wa pili. Aligundua kuwa aliyekuwa akiufungua ule mlango alikuwa yupo pekee yake.

"Omary!" Sajenti akaita kwa sauti ya chini kama mtu anayenong'ona.

“Braza ni Mimi" Omary aliitikia huku akiwa anaufungua mlango. Omary Aliingia akiwa kabeba mfuko wa karatasi. Wakarudishia mlango wakarudi kwenye godoro kukaa. Omary alimkabidhi Sajenti Warioba ule mfuko wa karatasi wa kaki ambao ndani yake kulikuwa na nyama choma na ndizi zilizokaangwa pamoja na chupa moja ya vodka.

"Mimi nimeshakula huko. Kula tuu braza" Omary aliongea akiwa ameanza mchezo wake mbaya wa kulegeza macho na kujilamba lamba. Mchezo huo ulikuwa unamkera sana Sajenti. Alitamani amwambie aache lakini alikumba msemo usemao mtumikie kafiri upate mradi.
"basi kula walau nyama" Sajenti aliongea akimbembeleza Omary ambaye muda huo alikuwa amelala kwa mapozi ya kike.

"Wewe kaka embu kuwa muelewa basi. Nimekuambia nimekula"

Omary aliongea kwa sauti ya kike kabisa. Huku akibetua betua midomo yake. Kitendo cha Omary kukataa kula chakula kilimfanya Sajenti aingiwe na wasiwasi. Alihisi huenda kile chakula kimewekewa madawa ya kulevya ambayo akila atasinzia. hivyo itawarahisisha kazi ya kumkamata. Akakumbuka zile kete mbili za heroine alizozikuta kule kwenye kile chumba cha mbrazili.

"Kama huli hata kipande kimoja cha nyama nami sitakula chakula chako" Sajenti akasema huku akikifunga kile chakula kwenye ule mfuko wa kaki. Alifanya hivyo kumjaribu Omary ingawaje alikuwa na njaa na alikitamani sana. Omary kuona Sajenti amesusa kula. Ilibidi aamke akaenda kuchukua kipande kimoja cha nyama na ndizi.

"Haya mume nawe amka ule. Najua huwezi kula wakati mkeo sili. Haya amka sasa" Omary alisema akiwa ameilegeza sauti yake. Sajenti alikasirika sana. Maneno ya Omary yalimkera kupita kiasi."Wewe ni fala nini. Usiniletee upuuzi hapa" Sajenti aligomba kwa sauti hali iliyomfanya Omary amuonyeshee ishara kuwa anapiga kelele.

"Shiiii! Acha kupiga kelele sasa. Mdomo uliponza kichwa shauri yako. Unadhani upo kwako humu" Sajenti alinyamaza hasira zikitingisha mashavu na midomo yake. Alitamani ampige hata makofi mawili lakini akakumbuka alipokuwa jeshini alivyofundishwa na mwalimu wake kuwa mwanajeshi mzuri ni yule anayeweza kuzuia mihemko yake. Akameza fumba la mate kisha akaanza kula. Ilikuwa ni nyama ya mbuzi iliyorostiwa kwa ufundi wa hali ya juu. Sajenti alikula haraka haraka mate yakimtoka mdomoni kwa utamu. Kwa kweli alifurahia mlo ule. Alimaliza kula wakawa wanapiga stori mbili tatu na Omary. Omary alianza kusimulia sababu iliyomfanya mpaka akajiingiza kwenye ushoga.

"Stori ndefu sana braza. Yaani sitaki hata kukumbuka" Omary alisema akiwa ametulia. Muda huu alionyesha uhalisia zaidi. Huzuni na simanzi ziliufunika uso wake. Machozi yalianza kumlengalenga. Nani ambaye asingeelewa kile ambacho anataka kuhadithia kuwa ni hadithi ya kusikitisha. Hadithi iliyojawa na visa vyenye simanzi na vilio. Sajenti Warioba kwa utulivu na ushawishi akazungumza.

"Omary! Kila hadithi inamsomaji. Kila ngoma inawachezaji. Tafadhali naomba unisimulie kwa ufupi" Omari alimtazama Sajenti Warioba kwa uso wa uchovu wa huzuni. Kisha akayakunja macho yake kama mtu anayekumbuka mbali.

"Nilimaliza shule ya msingi kwa msisi handeni. Nilikuwa naishi na bibi yangu mzaa Mama. Mama yangu alikuwa akiishi Dar es salaam maeneo ya mtoni mtongani ya temeke. Hakuwa akiishi na baba yangu kwani baba alikataa mimba yangu. Hivyo Mama akaamua kunilea yeye kama yeye" Omary aliweka kituo kwa kumeza fumba la mate. Alihadithia kwa utulivu sana. Sauti yake haikuwa ile yakishoga kama awali. Hata yale macho ya kurembua sasa yalikuwa hayarembui. Zaidi ya kuzingirwa na machozi. Omary akaendelea kusimulia.

"Mimba aliipatia huko huko Dar es salaam. Kama unavyojua mimba inahitaji uangalizi na malezi. Na Mama hakuwa na kazi ya maana zaidi ya uMama ntilie. Pesa zote alizopata ziliishia kwenye kodi. Hivyo mimba ilivyokuwa maisha ya Dar yakamshinda. Akaamua kurudi kwa bibi mpaka akajifungua mtoto wa kiume. Akamuita Omary matatizo" Uso wa Omary ulibadilika. Mdomo wake ulianza kutetemeka. Machozi yalitiririka kama mifereji katika mashavu yake. Alianza kulia.

"Sijawahi kumuona baba yangu tokea kuzaliwa. Sijui yupo wapi. Mama aliamua kumuita baba yangu matatizo. Matatizo! Matatizo! Ati matatizo ndio baba yangu. Omary matatizo. Hiiiiihiii" Omary alizidisha kulia kama yupo msibani. Hali iliyomfanya Sajenti ambembeleze. "Jikaze Omary. Wewe ni mwanaume. Usilie Omary"

" Ati mimi ni mwanaume. Omary mwanaume. Nilitoka handeni kama mwanaume nikiwa
Darasa la saba. Nilikuwa na miaka kumi na mbili. Nikafika Dar es salaam alipokuwa akiishi Mama na mume wake mpya ambaye ni baba wa kambo" Omary aliweka kituo kisha akavuta makamasi mepesi yaliyokuwa yananing'inia puani. Alijipangusa machozi machoni kisha akaendelea.

"Mama alikuwa muuza bar moja pale mjini. Alikuwa akiondoka saa tisa jioni na kurudi saa tano za usiku. Hapo alikuwa amepika chakula cha usiku. Baba yangu wa kambo akirudi tulikuwa tunakula naye. Baba alikuwa ni konda wa daladala zilizokuwa zinatoka Mbagala rangitatu kwenda makumbusho" Alimeza fumba la mate kisha akamtazama Sajenti Warioba aliyeonekana kunogewa na stori hiyo ya kusisimua.

"Eehe ikawaje sasa?" Sajenti aliuliza.

"Maisha ya pale mtongani nilianza kuyazoea. Pale nyumbani nilipaona kama nyumbani. Japokuwa sikupendezwa na tabia ya Mama kurudi akiwa amelewa lakini sikuwa na lakufanya. Mama alikuwa akilewa sana. Kila mara akirudi nyumbani alikuwa akimtukana baba" machozi yalianza kutiririka tena katika uso wa Omary. Na kila alipokuwa akifanya hivi Sajenti alijua kuna jambo baya anaenda kulisimulia. Hii ilimfanya azidishe utulivu.

" Mama alikuwa akimfukuza baba chumbani ati akalale sebuleni. Siku moja baba alikuja chumbani kwangu akagonga mlango. Nilimfungulia. Akanambia amekuja kulala na mimi. Nilijua tuu kafukuzwa na Mama. Alafu pale sebuleni kuna mbu. Hivyo alichoka kung'atwa na mbu" akameza fumba la mate na kuvuta makamasi puani. Kisha akaanza kulia kwa sauti ya kutetema. "Huruma zangu zikaniponza braza. Huruma! Huruma ni mbaya jamani!
Akapanda kitandani tukalala wote. Mara usiku nikiwa nimelala nikasikia mtu akinikumbatia mwili wangu. Nilitaka kujinasua lakini sauti nzito ikaniambia nisihofu. Ni baba. Nikabaki nimetulia tuu. Alinishika sehemu zangu za siri. Kisha akaniingilia. Nilisikia maumivu makali sana. Sitakaa nisahau siku ile".


Kufikia hapa Omary alilia mfululizo akiwa anatingishwa kichwa chake kama mtu anayekataa kuamini historia yake. Sajenti Warioba alibaki amemtizama Omary kwa huruma. Alimuona ni kijana mdogo asiyestahili madhila yote yale.

"Baba wa kambo akanipa elfu ishirini na kuniambia nisiseme. Niliiona ni pesa nyingi. Tokea hapo ikawa ndio tabia yangu kuingiliwa na baba. Wewe ulisema mimi ni mwanaume lakini mume wa Mama yangu alinigeuza mwanamke wake kwa miaka mitatu" Omary aliendelea kulia ikafikia hawezi kusimulia tena. Sajenti Warioba alimkumbatia akawa anambembeleza mpaka usingizi ulipompitia Omary.

Sajenti aliitafakari historia mbaya ya Omary aliyohadithiwa. Ilikuwa ni historia ya kikatili sana. Alitamani amjue huyo baba yake Omary wa kambo. Ili amfungulie mashtaka. Ona sasa kijana wa watu anapata tabu. Ona sasa amegeuzwa mwanamke huku katika meli za maharamia watu wenye roho za kuua. Sajenti aliwaza mambo yote hayo. Sajenti alipitiwa na usingizi bila kujua wote wakawa wamelala. Wakwanza kuamka alikuwa ni Omary. Omary aliamka na moja kwa moja alitoka kwenye kile chumba. Punde alirejea akiwa na mwanamke na mwanaume mmoja wa kireno. Omary alishangaa kutokumkuta Sajenti Warioba kwenye kile chumba.

"Nilimuacha amelala hapa" Omary aliongea akimtazama yule mwanamke.

" Wewe usituchezee akili. Yupo wapi huyo mtu" yule mwanamke alisema kwa hasira huku akimtazama.

"Alikuwa hapa kweli. Alikaa hapa akiwa anakula kile chakula mlichonipa" Omary akasema akiwa anaangaza macho yake huku na huko. Ni kweli Omary alimuacha Sajenti pale akiwa amelala. Sasa kaenda wapi. Hilo ndilo lililomchanganya. Omary alijua kuwa yule mwanamke siyo mtu wa mchezo. Kitendo cha kutokumkuta Sajenti Warioba pale chumbani kinaweza kuhatarisha uhai wake.

"Wee mbwa naona umeanza kunizoea. Sasa leo utambua mimi ni nani" yule mwanamke alionsema kwa sauti ya kibabe yenye dalili zote za shari.

"Ommy huenda yupo sahihi. Si unaona ule mlango umefunguliwa" yule mreno akasema kwa kiswahili kibovu kama kanjibai. Wote walitazama kwenye ule mlango mfupi wa futi nne. Walishangaa kutokuona kufuli pale. Waliusogelea ule mlango mfupi ambao haukua na kufuli. Waliamini aliyeiondoa kufuli ile ni Sajenti. Kama paka anavyonyata kunyemelea panya ndivyo walivyokuwa wakinyata kuusogelea ule mlango. Waliufikia. Yule mreno akaushika ili kuufungua. Aliushika akamtazama yule mwanamke aliyekuja naye. Yule mwanamke akamtingishia kichwa kama ishara ya kumruhusu aufungue ule mlango. Wakati huo yule mwanamke alijiweka tayari kufanya shambulio kwa hatari itakayo jitokeza. Waliufungua ghafla yule mreno alipigwa usoni hali iliyomfanya yule mwanamke apige risasi hovyo. Looh! Kumbe ilikuwa ni kipepeo kikubwa cheusi ndicho kilichompiga usoni.

"Hoiii!" yule mreno alishusha pumzi nzito akiwa kaanguka chini kwa hofu. Wote walikitukana kipepeo cha watu kilichokuwa kinaendelea kuruka ruka mule ndani. Wakaingia upande wa pili ambapo kulikuwa na mabomba na vipuri vikuukuu vya meli. Walidhani kuwa ndipo alipokuwa amekimbilia Sajenti. Hata hivyo walikuwa sahihi. Sajenti hakuwa na njia nyingine ya kutokea zaidi ya ule mlango mfupi wa futi nne. Kulikuwa na giza sana. Kilichowasaidia ni tochi ya simu aliyokuwa ameishika yule mwanamke. Walimulika kila sehemu lakini hawakuweza kumuona Sajenti. Mule ndani kulikuwa na tando nyingi za buibui. Hii iliwafanya kila mara kupangusa nyuso zao pindi ziliposhikwa na utando wa buibui. Wakatembea mule ndani kumsaka Sajenti lakini hapakuwa na dalili ya mtu . Omary yeye alikuwa amebeba taa yake ya chemli. Alihisi huenda Sajenti Warioba ni mzimu kama siyo jini. Inawezekanaje amuache akiwa amelala kwa dakika zisizozidi mbili alafu arudi amkose. Haya hata kama kakimbia basi amekimbilia wapi maana kama ni msako wameufanya mpaka wamechoka. Ile meli wanaijua ndani nje. Wanajua njia zote za kutorokea na kujifichia. Iweje mgeni awatoroke kienyeji kiasi kile.

Moja kwa moja Omary alijua kuwa ataonekana ni muongo. Na uongo ni kosa kubwa katika kundi la Ambagon. Kosa ambalo hukumu yake ni kifo. Omary akajuta. Aliona ni bora asingeenda kumshtaki Sajenti kwa wale watu wabaya. Punde walisikia kwa mbele kitu kikichakura chakura. Hima walinyoshea bastola zao upande ule waliosikia sauti hiyo. Yule mwanamke akamulika tochi kuelekea upande waliosikia sauti. Aliishia kusonya baada ya kumuona panya akiwa anakula fupa la nyama. Kwa hasira alimpiga panya yule risasi aliyekuwa akisheherekea msosi wake. Walishusha pumzi kupunguza hofu iliyosababishwa na panya ambaye walidhani ni Sajenti. Baada ya kutafuta kwa muda mrefu kama lisaa limoja na nusu. Wakachoka.

"Leo utatutambua. Huwezi kutudanganya kama watoto wadogo" yule mwanamke aliongea kwa ukali kama mtu aliyeaibishwa.

"Dadaangu! Nilikuwa naye. Kwa nini nidanganye..."

" Wee koma! Mimi siyo dadaako. Mbwa wewe leo utanijua mimi ni nani"
Yule mwanamke alimkatiza Omary akamkunja tai shingoni na kumsogelea usoni. Nyuso zao zikiwa zimekaribiana zero distance.

"Nisamehe dadaangu"

"Nimekuambia mimi siyo dadaako. Kaa kimya nguruwe wee!"


alimkemea na kumchapa kofi kali la shavuni. Waliondoka kule chini wakafunga kile kimlango kwa nje ili kama kweli Sajenti aliingia mule ndani asiweze kutoka. Muda wote huo Sajenti Warioba alikuwa amejificha ndani ya bomba moja kubwa ambalo alilifungua kwa kulisogeza. Maneno yote waliyoyaongea aliyasikia. Alimlaumu sana Omary kwa kitendo cha kumsaliti. Sajenti alikuwa tayari kumsaidia Omary kutoka mule ndani ya meli. Alipanga kuwa kama angefanikiwa kumtorosha kutoka mule melini angeenda kumsomesha ili naye awe na maisha yake. Lakini kumbe Omary alikuwa ni mtu mbaya asiyefaa hata kwa mkopo. Sajenti aliona hata ile hadithi aliyosimuliwa na Omary huenda ilikuwa ni danganya toto. Hakuiamini tena. Zaidi ya yote alishukuru kwa kuwa salama mpaka muda ule. Akatoka kwenye lile bomba akiwa hoi kwa kujikunja mule bombani. Akajinyoosha kuviweka sawa viungo vyake huku akivuta pumzi kufidia pumzi aliyoikosa alipokuwa ndani ya lile bomba. Kutokana na kukaa muda mrefu kwenye bomba macho yake yalikuwa yameshazoea giza. Aliona kiasi cha kumfanya atembee bila kujikwaa. Alikaa kule chini siku mbili mfululizo bila kula. Njaa ilimuuma sana. Akafanya mbinu zote alizozijua na alizofunzwa ili atoke kule chini lakini ilishindikana. Alikiona kifo kwa mbali kikimkonyeza kwa dhihaka. Alibaki anakitazama tuu asijue afanye nini wala akiambie nini. Akatembea tembea kule chini kuona kama atapata upenyo wowote wa kutoka lakini hakuona dalili yoyote ya kuwepo kwa upenyo. Punde akafika sehemu ambayo alisikia harufu kali ya kitu kilichooza. Itakuwa ni harufu ya nini hii. Sajenti alijiuliza huku akiifuata harufu inapotokea. "fuuuh! Mmmh!" alishika pua yake. Aliona mzoga wa panya ukiwa unafunza. Ni yule panya aliyeuawa kwa risasi na yule mwanamke mwenye roho mbaya. Sajenti Warioba awali aliwahi kusikia kuwa hakuna kifo kibaya kama kifo cha moto. Pia aliwahi kusikia kuwa hakuna kifo cha kikatili kama kifo cha maji. Kama kuna vifo alivyowahi kuviona ni vya kikatili basi ni kifo cha kuchinjwa na kisu au panga. Lakini leo mawazo yake yalibadilika. Alibadilisha mtazamo kuhusu kifo kibaya na cha kikatili kama siyo mateso. Leo hii kama angeulizwa ataje kifo kibaya basi angesema bila hata kufikiri kuwa kifo cha njaa ndio kifo cha kikatili chenye maumivu makali yasiyosemeka. Usicheze na njaa. Hata wahenga walikwisha sema kuwa adui yako mwombee njaa. Njaa ni habari nyingine kabisa. Sajenti nguvu zilimuisha kabisa. Aliona akitembea anapepesuka. Aliishika bastola yake. Akaitazama.

" Leo nataka uniue rafiki yangu. Umenisaidia sana rafiki yangu. Leo nami nataka uniue" Sajenti aliiambia bastola yake iliyokuwa ikimtazama bila kujibu chochote. Akaibusu kama ishara ya mapendo. Sajenti alikuwa katika hatua ya mwisho ya kufanya maamuzi ya kujiua. Aliona ni bora ajiue kuliko mateso aliyokuwa anayapata. Aliona ni heri mateso ya risasi yatakayodumu kwa sekunde chache kuliko mateso ya njaa yanayomtesa kwa muda wote ule.

Akaingiza kidole kwenye kilimi cha bastola yake. Kijasho chepesi cha njaa na hofu kikamtoka. Alipumua kwa nguvu. Hofu ya kifo ilimshika. Akaanza kuhesabu. Moja, mbili... Kabla hajafika tatu alishtuka kusikia kitu kinatembea tembea upande wake wakulia. Akageuka upesi kutazama. Huuh! Kumbe alikuwa panya. Alimpiga yule panya risasi ambayo ilimchakaza kichwani. Akamchukua yule panya. Mate yalimtoka mdomoni ungedhani aliona nyama choma. Lakini haikuwa nyama choma bali panya buku jike aliyenona. Alijua kabisa kuwa panya haliwi lakini atafanya nini ikiwa hakukuwa na kitu kingine cha yeye kula. Alianzia iliposhingo yake iliyokuwa inavuja damu. Hakika alijisikia kinyaa lakini kinyaa hakikuzidi njaa yake. Alimaliza kula panya wote kasoro mkia wake. Hahaha! Alijicheka kwa kula panya. Sajenti alipata nguvu mpya. Akahisi ahueni kidogo. Sasa hakutaka azidiwe tena na njaa mpaka ashindwe kufikiri vizuri namna ya kutoroka. Aliwahi kuambiwa na mwalimu wake jeshini kuwa njaa humfanya mtu asifikiri vizuri. Pia njaa humfanya mtu akubali jambo lolote lile bila kujali kuwa jambo hilo ni zuri au baya. Ndio maana adui ukimkamata unamnyima kwanza chakula. Hapo lazima utapata unachokihitaji. Alienda kwenye ule mlango mfupi ambao ulifungwa kwa upande wa pili. Alijaribu tena kuufungua lakini haukufunguka. Alipata wazo kuwa aitumie bastola yake kufungua mlango ule. Wazo hili aliliona ni jema na linafaa kabisa. Aliichukua bastola yake akaiweka usawa wa ilipokufuli iliyopo upande wa pili. Akafyatua risasi paa! Akapiga ingine paa! Akasikia kufuli likidondoka chini upande wa pili. Hapo akajua kazi imekwisha. Alifungua mlango. Akakuta lile godoro likiwa vilevile alivyoliacha. Akaondoka kwenda kwenye mlango wa bati wenye kutu. Nao ulikuwa umefungwa kwa nje. Aliichukua bastola yake akapiga sehemu aliyohisi inakomeo lililofunga mlango ule. Nao ukafunguka.



*************************************************​

Siku saba zilipita meli ikatia nanga katiba bandari ya Durban iliyopo afrika ya kusini. Safari ya kueleke brazil ilianza. Kutoka bandari ya Durban mpaka bandari ya santos nchini brazil ni siku zaidi ya ishirini ukiwa baharini. Umbali kutoka Durban mpaka bandari ya santos ni
4838 nautical miles. Nautical mile ni kipimo kinachotumika kupima umbali katika safari za angani na majini. Sajenti Warioba bado aliendelea kuishi kwa ujanja ujanja mule ndani kama mjusi wa ukutani. Alikuwa akiiba makombo ya wale mabaharia pindi walipokuwa wanayatupa kwenye vyombo vya takataka. Siku kumi na tano zilimfanya aizoee ile meli. Tayari alikuwa naye ni miongoni mwa mabaharia katika meli ile. Ingawaje yeye alikuwa baharia wakujificha.

Siku ya ishirini na tisa meli ya Ambagon ilitia nanga katika kisiwa cha ilhal montao de trigo ambacho kipo karibu kabisa na bandari kubwa ya santos iliyopo Brazil. Walifika usiku wa saa sita. Kulikuwa na giza anga lote likiwa limetawaliwa na nyota. Sajenti alianza kufanya harakati za kutoroka. Alipanda mpaka vyumba vya juu bila ya kuonekana. Akafika kwenye korido moja ndefu kiasi ambapo kulikuwa na milango miwili upande na upande. Akaufuata mlango mmoja akachungulia. Alishangaa kuona Hall kubwa lenye watu wa rangi tofauti tofauti wakifanya starehe. Lilikuwa ni kasino la ile meli. Moyoni alijisemea kumbe hii meli inawatu wengi kiasi hiki. Wale watu katika lile kasino walikaa kwa mzunguko kufuatana na mpangilio wa viti na meza. Juu ya meza zao kulikuwa na vinywaji mbalimbali vya gharama. Vinywaji vingi vilikuwa ni pombe kali. Sajenti aliendelea kuchungulia akichunguza mule ndani. Lakini ghafla alihisi kitu kigumu kikigusa kichogo chake. Bila kupoteza muda Sajenti Warioba akageuka na pigo moja takatifu la kiwiko cha mkono kilichompata yule mtu aliyemuwekea bastola kwa nyuma. Yule mtu aligugumia bastola ikiwa imeanguka sakafuni. Sajenti aligeuka. Hamadi! Alikutana na jitu kubwa kama licheza mieleka. Bila shaka lilikuwa mlinzi wa lile kasino. Lilikuwa jitu kubwa la miraba minne. Jeusi tii lililonyoa kipara kichwani. Kifuani lilikuwa na maziwa liliyokuwa likiyachezesha chezesha kibabe kumtisha Sajenti Warioba. Sajenti hakuwahi kuona mtu wa namna ile tokea kuzaliwa. Watu wa namna hii aliwahi kuwaona tuu kwenye video hasa mchezo wa mieleka.

Sajenti akalisogelea lile jitu ambalo aliliita Umaga. Wakawa wanazunguka zunguka kila mmoja akimtafutia mwenzake nafasi ya kumshambulia. Umaga akarusha ngumi. ikapita pembeni ya sikio la Sajenti. Upepo aliousikia Sajenti uliingia sikio hili ukatokea sikio la pili. Ilikuwa ngumi ambayo kama ingempata Sajenti basi ingemsababishia madhara ikiwezekana kifo. Sajenti alijua kuwa ili alipige lile jitu alihitajika atumie mbinu ya kupigana akiwa mbali kidogo. Kwa kuhofia kukamatwa na jitu lile jeusi ambalo uso wake ulihifadhi ukatili wa kila namna. Sajenti akarusha ngumi ikalipiga kwenye tumbo. Lile jitu likacheka. Likamuamuru apige zaidi na zaidi. Sajenti akaona sasa hii dharau. Akaifunga ngumi yake kisha akaitupa tena kwa nguvu zake zote. Lakini ilitua kama mzaha katika tumbo la lile jitu na kudunda kama kitenesi. Lile jitu lilicheka kwa dharau. Likajitutumua likikaza kifua chake. Sajenti aliingiwa na woga. Akarudi nyuma polepole lile jitu likimfuata huku likinguruma kama simba. Likarusha ngumi nzito Sajenti akaikwepa. Likarusha ngumi ya pili Sajenti akainama ikapita kama panga boya lkikata upepo. Sajenti akamrukia na kumpiga kichwa cha kidevu. Lile jitu uso wake ukainuka juu huku jino moja likiruka juu. Lilikuwa pigo takatifu ambalo kama angepigwa mtu mwenye afya mgogoro angekufa papohapo lakini lile jitu lilipandisha maruhani. Likamfata Sajenti Warioba kama mbogo aliyejeruhiwa huku mdomoni likivuja damu. Sajenti alirudi nyumanyuma mpaka akafikia ukutani. Lilirusha ngumi ikapiga bega la Sajenti, akagugumia kwa maumivu makali. Ni bega lile lile aliloshambuliwa na risasi kipindi kile akiwa kwenye hospitali ya Ambagon.

Lile jitu likampiga teke la tumbo Sajenti akadondoka chini karibu na ile bastola ya lile jitu. Kwa kweli Sajenti hakuwa tayari kupokea pigo jingine. Aliichukua ile bastola na kumpiga risasi ya kichwa lile dubwana likamuangukia kwa juu. Dooh! Lilikuwa zito kama gunia la kahawa. Akalisukuma kwa pembeni kisha akaliburuza mpaka mafichoni. Alilipekua katika mifuko ya suruali yake akakuta kadi iliyowekwa nembo ya Ambagon ambayo ni herufi A. Akarudi kwenye ule mlango akaufungua kisha akatoma ndani ya kasino. Hakuna aliyekuwa na habari na mtu. Kila mtu alikuwa yupo bize kujipa raha za dunia. Kwa mbele aliona jukwaa kubwa ambapo aliwaona malaya wakiwa uchi wa mnyama wakicheza kwa madoido na ushankupe. Aliwaona wazungu, waafrika na waarabu. Karibu mataifa yote aliwaona wawakilishi wao kwenye lile jukwaa. Alitembea akijifanya mwenyeji ili asije akashtukiwa. Alipigana vikumbo na wanawake malaya waliokuwa wamesimama kwa kukosa wanaume wa kukaa nao. Kila meza alikuwa amekaa mwanaume na mwanamke. Wanaume wengine walikuwa wanavuta sigara wakiwa vifua wazi. Wengine walikuwa wamevaa suti kali za gharama. Wengi wao umri wao ulikuwa kati ya miaka thelasini na nane mpaka sabini.

Sajenti alikaa meza moja iliyokuwa na mzee mmoja mwenye asili ya kihindi aliyevaa miwani nyeusi na kofia kama la cowboy wa kimexico. Hakumsalimia akakaa tuu na kujifanya yupo bize kuangalia lilipojukwaa walipokuwa wanacheza wale Malaya wakifuata mdundo wa muziki uliokuwa ukipiga. Sekunde haikuisha alikuja mwanamke mweupe mwenye asili ya kibrazil.

"suas notícias bom irmão" mwanamke aliyekuja alimsalimia Sajenti. Sajenti aligeuka kumtazama na kumjibu.

"ola'" Sajenti alijibu kwa kifupi. Akimaanisha sijambo. Kwani alisalimiwa 'habari yako kaka'. "Wewe ni mswahili. Mbona unaongea kama Mtanzania" yule mwanamke aliongea kiswahili kibovu sana. Sajenti alishangaa kusikia yule mwanamke akiongea kiswahili. Kwa haraka akajibu.

"Hapana mimi ni mkenya. "

"Ahaa! Ulipandia mombasa?"

"Ndio! Nawe ulipandia wapi?"
Sajenti alijibu haraka alafu naye akamtupia swali.

" Mimi mwenyeji wa mji wa Juquei. Ilipofukwe nzuri za Juquei. Huwa nakuja kwenye hii meli kwa kazi hii" yule mwanamke alisema akitingisha tingisha nywele zake ndefu zisiingie machoni. Akapeleka glass mdomoni aliyokuwa ameishika mkononi.

"Ahaa! Sawasawa!" Sajenti aliitikia akihitaji maelezo ya ziada.

"Nipo hapa kwa ajili ya kuwapa wanaume raha. Wafikapo katika kisiwa hiki cha montao de trigo kila mrembo humu hujichukulia mteja wake" yule mwanamke alisema.. Sajenti aligundua kuwa yule mwanamke alikuwa anaitwa Fernanda da silva kutokana na kitambulisho kilichokuwa kinaning'inia shingoni mwake.

"Utanilipa bei gani. Ninasehemu nzuri ya kulala tukitoka humu" Fernanda akasema akiyashika mabega ya Sajenti Warioba akiwa kamzunguka mgongoni. Hapa Sajenti akili yake ikamuambia kuwa hii ndio ilikuwa nafasi yake ya mwisho kutoka mule ndani. Aligundua kuwa kumbe ile meli licha ya kuwa inasafirisha miili na viungo vya watu lakini pia kulikuwa na matajiri waliokuwa wakizunguka dunia nzima wakiponda raha na wanawake malaya huku wakinywa na kula. Bila shaka wengi wa wasafiri mule ndani ya ile meli hawakujua kuwa meli ile pia ilikuwa inasafirisha bidhaa za magendo. Kama wangelijua huenda hata wasingethubu kuingia humo.

Muda wa kutoka melini ukawadia. Ilikuwa ni asubuhi tulivu kabisa katika kisiwa cha montao de trigo. Sajenti na Fernanda walikuwa kwenye msururu mrefu wa watu wanaotoka nje ya meli. Walipofika mlango wa kutokea walitakiwa wakabidhi vile vitambulisho. Fernanda alitoa kitambulisho chake wakati Sajenti Warioba akihaha kwa wasiwasi. Sajenti naye alitoa kile kitambulisho cha lile jitu alilopigana nalo kule ndani. Yule mkaguzi alikikagua kile kitambulisho kwa muda kidogo tofauti na alivyofanya kwa Fernanda. Moyo wa Sajenti alipwita pwita kama ringi la gari. Aliomba kimoyo moyo wasije wakamshtukia. Yule mkaguzi alimtazama usoni Sajenti Warioba kama ataona tashwishi yoyote lakini Sajenti alitabasamu kirafiki kumuondoa hofu. Yule mkaguzi naye alitabasamu na kumruhusu. Sajenti alishusha pumzi akiwa haamini. Chezea Ambagon wewe. Moto wa Ambagon siyo wa kitoto. Wakatoka; Fernanda akiwa amemshika kiuno chake. Punde alimuona yule mwanamke aliyemuona akifanya mapenzi kule katika meli, aliyetoka kupokea simu wakati Sajenti akiwa kajificha upande wa pili wa mlango. Ndio huyohuyo mwanamke aliyekuja na mwanaume wakireno aliyekuwa akimfokea Omary. Sajenti akamtazama kwa jicho la kuiba iba. Punde yule mwanamke aligeukia kule alipokuwepo Sajenti Warioba. Wakagongana macho lakini Sajenti akayaondoa macho yake na kumtazama Fernanda. Yule mwanamke aliingiwa wasiwasi kwa kitendo cha kumuona Sajenti Warioba. Hata hivyo alimpuuzia. Walitembea mpaka zilipo teksi za uber. Wakapanda na moja kwa moja wakaelekea upande wa pili wa ufukwe. Hapo Fernanda akamuambia Sajenti Warioba kuwa watapanda boat ya kuelekea ilipo beach ya Juquei ambapo ndio nyumbani kwake, Fernanda. Wakapakia boat na ndani ya nusu saa walikuwa wamefika fukwe ya Juquei.

Fukwe ya Juquei ilikuwa na mchanga mzuri mweupe. Maji yake yalikuwa meupe ambayo ukiyatazama unaweza kuona samaki anayepita chini kabisa. Pia ni fukwe ambayo ilikuwa na milima yenye kijani cha kupendeza. Ilikuwa ni saa mbili asubuhi lakini watu walikuwa wengi. Hasa watalii waliokuja kufanya utalii. Sajenti alivutiwa na mandhari ya fukwe ile. Walitembea kwa miguu mwendo wa dakika kumi wakiiacha fukwe ya Juquei wakikatiza mitaa na kona ya mji mdogo wa Juquei. Punde walisimama mbele ya geti jeusi ambapo Fernanda alienda kulifungua kisha wakaingia ndani. Sajenti alistaajabu mandhari ya mule ndani. Akaona bustani zenye maua ya kupendeza ya kila rangi. Aliona pia swimming pool la kuogelea ambapo pembeni yake kulikuwa na viti na vitanda maalumu vya kulalia. Mbele yake alitazamana na jumba kubwa la kifahari lenye madirisha ya aluminium na vioo vya gharama. Juu ya jumba lile kulikuwa na vigae vya rangi ya damu ya mzee ambavyo ndio vilikuwa paa la jumba lile. Fernanda alimkaribisha ndani Sajenti Warioba ambaye macho yake yalikuwa yakistaajabu kila alichokuwa anakiona.

"Hapa ni wapi Fernanda?" swali lilimponyoka Sajenti huku wakiwa wameshaingia sebuleni.

"Hapa ni kwangu mume wangu” Fernanda alijibu akijitahidi kuongea kiswahili kilichonyooka.

Mpaka muda huo Fernanda hakujua Sajenti alikuwa anaitwa nani. Wala Sajenti hakumuuliza Fernanda jina lake. Kama unakumbuka Sajenti alijua jina la huyu mwanamke wa kibrazil baada ya kusoma kitambulisho alichokuwa amekivaa kule kwenye kasino wakiwa melini.

Ni kawaida kwa malaya kutokuuliza majina ya wateja wao. Unajua kwa nini. Labda na wewe unaweza kujua ni kwasababu gani. Ila sababu kubwa ni kuwa watauliza majina ya wateja wangapi, kwa maana wao hulala na watu wengi. Hicho ndicho kinawafanya wasiulize majina ya wateja wao labda wawe wateja wa kudumu. Sajenti Warioba alipitisha macho yake kukagua sebule ya nyumba ile. Aliona picha kubwa ikiwa ukutani ikimuonyesha Fernanda akiwa amevaa gauni jeupe la harusi. Pembeni yake kulikuwa na picha nyingine ndogo ikimuonyesha Fernanda akiwa na Mama wa makamo ambaye moja kwa moja Sajenti alijua atakuwa ni Mama yake na Fernanda kutokana na kufanana.

Fernanda alikuwa kaingia ndani akiwa kamuacha Sajenti pale sebuleni. Sajenti aligundua sebule ile ilikuwa na kamera za siri za cctv zilizotegwa kwenye feni iliyokuwa juu ikizunguka upande huu na upande huu waliyoikuta ikiwa hivyohivyo inazunguka. Kamera nyingine ilikuwa imetegwa kwenye kinyago cha dragon kilichokuwa juu kabisa ya kabati la vyombo lililokuwa kwenye sebule ya kulia chakula. Ni elimu na mbinu za kijeshi ndizo zilizomsaidia Sajenti Warioba kujua kuwa mule ndani kulikuwa na kamera. Mtu wa kawaida wala asingeweza kujua jambo hili.

Hofu na mashaka vilibisha hodi katika moyo wake. Iweje Fernanda aweke kamera humu ndani. Fernanda ni nani hasa. Je ni kazi hiihii ya umalaya ndio mpaka nyumba hii ifungwe kamera. Au kuna kazi ingine anayoifanya Fernanda. Hata hivyo Sajenti hakutaka kumuamini sana Fernanda. Atawezaje kumuamini ikiwa walikutana kwenye meli hatari ya Ambagon. Sajenti aliamini kuwa mtu yeyote aliyekuwa kwenye ile meli hakupaswa kuaminiwa. Aliwaona watu wote mule ndani ni watu hatari na wauaji. Punde Fernanda alitoka chumbani akiwa kavaa taulo la kuogea. Alitembea kwa madaha kama mlimbwende anayetumbuiza jukwaani. Alilegeza macho yake ya kijivu na kuzirusha rusha nywele zake mbele na nyuma kumchanganya zaidi Sajenti. Sajenti alipagawa akajisemea kuwa leo amekamatika. Leo napewa mapenzi ya kimataifa. Yeye si alizoea mapenzi ya kibongo bongo leo kakutana na Fernanda malaya aliyebobea katika tasnia ya ukahaba. Fernanda akatembea kimanjonjo mpaka ilipo home thietre kubwa ya muziki. Kisha akawasha muziki wa kibrazili. Kisha akabenjuka na kumtazama Sajenti na macho ya uchu. Fernanda ndio kaanza hivyo. Sijui kama Sajenti atasalimika na mahaba ya kibrazil.

Akapeleka kidole mdomoni akaking'ata kisha akafumba macho yake kwa madaha na kuyafumbua polepole yakiwa yanarembua. Muda wote alikuwa akifanya hivi huku akimtazama Sajenti aliyekuwa kasimama kama sanamu la michelin. Muziki ulianza kuchanganya. Fernanda alihakikisha mapigo ya muziki hayamuachi. Alikata mauno muziki ulipohitaji akate mauno. Alitingisha matako muziki ulivyomuamrisha kufanya hivyo. Akainama chini na kuanza kutambaa kama mtoto kumfuata Sajenti ambaye muda huo alikuwa hajielewi. Kisha akasimama upesi akiwa amemkaribia Sajenti kama hatua moja. Wakiwa wanatazamana huku muziki ukiimba kama filamu ya kihindi. Fernanda akashika lile taulo lake akalirusha juu likanata kwenye feni. Feni ikawa inazunguka na lile taulo. Fernanda akabaki uchi kama alivyozaliwa huku cheni ya dhahabu ikiwa kiunoni na pete ikiwa kitovuni. Kitendo cha Fernanda kulirusha taulo juu ya feni Sajenti alikielewa. Alijua kuwa Fernanda kafanya vile makusudi kuziba kamera ili isiwachukue video wala kuwapiga picha. Sajenti akanyanyua uso wake juu kulitazama lile taulo. Alishangaa kuliona likiwa limeiziba kwa ufasaha ile kamera. Moyoni alimuona Fernanda kama mwanamke mwenye shabaha sana. Mtu mwingine asingeweza kurusha vile tena bila ya kuangalia juu.

Muda huo Fernanda hakujua kuwa Sajenti kaelewa mchezo mzima. Fernanda akamshika Sajenti shingoni na kumnyonya mdomo wake. Walinyonyana ndimi kwa dakika tano mfululizo huku Fernanda akimchojoa Sajenti nguo zake. Dakika kumi wote walikuwa wapo uchi wakipumua kama bata dume. Walifanya mapenzi palepale sebuleni kila mmoja akionyesha utundu wake. Hii ilikuwa kama finali ya kombe la dunia la mapenzi. Timu ya brazil ikiwakilishwa na Fernanda na timu ya Tanzania ikiwakilishwa na Sajenti. Mechi ilikuwa ni kali kila mmoja akijaribu kushambulia. Mpaka dakika ya tisini walikuwa wamefungana mbili mbili. Mechi ilienda matuta ambapo kwa mara ya kwanza kombe la dunia likaenda Tanzania. Walienda kuoga wakarudi kitandani kupumzika. Fernanda hakuamini kwamba kuna mwanaume anaweza kufanya mapenzi kwa kiwango kile mpaka aridhike. Amefanya mapenzi na wanaume wengi lakini wote hakuna aliyewahi kumfikisha katika pepo ya mahaba. Leo hii kwa mara ya kwanza alionja pepo pasipokifo akiwa na Sajenti Warioba.

"Wewe hata usiponilipa. Kiukweli umenifurahisha. Tutapumzika alafu jioni tutafanya tena" Fernanda alisema akiwa kalala kifuani mwa Sajenti akisikiliza mapigo ya moyo wa Sajenti yakikimbia.

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel

Safi sana Mkuu…Kazi nzur
 
MLIO WA RISASI HARUSINI (Episode 12)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300


>>>>>>>>>>>>> Episode 12 <<<<<<<<<<<<
ILIPOISHIA
Fernanda hakuamini kwamba kuna mwanaume anaweza kufanya mapenzi kwa kiwango kile mpaka aridhike. Amefanya mapenzi na wanaume wengi lakini wote hakuna aliyewahi kumfikisha katika pepo ya mahaba. Leo hii kwa mara ya kwanza alionja pepo pasipokifo akiwa na Sajenti Warioba.
"Wewe hata usiponilipa. Kiukweli umenifurahisha. Tutapumzika alafu jioni tutafanya tena" Fernanda alisema akiwa kalala kifuani mwa Sajenti akisikiliza mapigo ya moyo wa Sajenti yakikimbia.

ENDELEA

Jioni ilifika Fernanda akamuambia Sajenti kuwa watoke waende kutembea tembea. Sajenti hakuwa na pingamizi. Walijiandaa na Fernanda akamtafutia Sajenti nguo za kuvaa zilizokuwa mule ndani. Walitoka wakiwa wamekumbatiana. Walipendezea kwa kweli. Watu walikuwa wakiwashangaa walipokuwa wakipita. Wanaume wakware na wenye roho mbaya wa kibrazil walimuonea wivu Sajenti Warioba kutembea na Fernanda. Waliona ni matusi muafrika mweusi kama Sajenti kutembea na mbrazil mwenzao. Wakafika katika club moja ya usiku ambapo juu yake kulikuwa na kibao kilichosomeka "boate são paulo" ikimaanisha club ya usiku ya san paulo. Huko walicheza na kuburudika. Sajenti hakutaka kunywa pombe. Alijua hatari ya pombe. kulewa kwa wakati ule siyo uamuzi mzuri kwa usalama wake. Kwanza yupo ugenini. Pili yupo na mtoto wa watu ambaye aliamini wenyeji hawakumuangalia kwa macho mazuri. Sasa atalewa vipi. Labda awe mwendawazimu.

Punde Sajenti akashtuka kumuona mwanamke mmoja akiingia. Alikuwa ni yule mwanamke aliyemuona kule kwenye meli. Mwanamke yule alikuwa ameongozana na Omary. Omary na yule mwanamke wakapita moja kwa moja bila ya kumuona Sajenti mpaka eneo la mbele. Walikuwa ni kama wanamtafuta mtu fulani ambaye Sajenti aliingia wasiwasi kuwa huenda walikuwa wanamtafuta yeye. Muziki ulikuwa ukipiga. Watu walikuwa wakifurahia. Fernanda alikuwa amesimama akiwa anacheza muziki. Wakati Sajenti akiwa katika msitu mzito wa hofu. Punde waliingia wanaume wa miraba minne wakiwa wawili waliovalia suti nyeusi na miwani nyeusi. Walimpiga kikumbo Fernanda aliyekuwa akicheza na glass yake mkononi. Hali iliyomfanya Fernanda apepesuke na kuangusha ile glass. Fernanda aliwatukana wale watu wenye miraba minne wenye asili ya kibrazil. Wale watu walimfuata na kumzaba kofi kali lililompelekea Fernanda kuangukia meza iliyokuwa na vinywaji vya Sajenti. Sajenti akaamka kwa kasi akiwa ameshika chupa akampiga mmoja wa zile njemba usoni. Kisha akampiga kisukusuku cha mdomo yule mwingine. Yalikuwa ni mapigo yalioachana kwa nusu sekunde jambo lililofanya wale watu wasiweze kukwepa. Hali ilibadilika katika club ile. Haikuwa tena ukumbi wa starehe bali uligeuka ukumbi wa vurugu. Watu wengine walianza kukimbia kimbia huku na huko baada ya kuona vurugu zinaongezeka. Sajenti akisaidiana na Fernanda walijitahidi kupigana na wale watu wabaya. Sajenti alitaka amalize ule mchezo mapema ili aondoke na Fernanda kabla hajaonwa na Omary na yule mwanamke. Hakuwahofia wale mabaunsa waliomletea fujo Fernanda bali alimuogopa yule mwanamke ambaye alijua kuwa ni mwanachama wa kundi la Ambagon. Alijua kama yule mwanamke angemuona basi angekuwa na kibarua kizito cha kujiokoa. Kukamatwa na kundi la Ambagon lilikuwa ni jambo ambalo Sajenti hakutaka litokee. Hakuwa tayari kuchunwa ngozi yake kama mbuzi. Hakuwa tayari viungo vyake vichukuliwe na wale wahuni wa Ambagon. Kama ni kufa alijua atakufa lakini siyo mikononi mwa wale mashetani wasiyo na huruma. Alitaka azikwe kwa heshima kama watu wengine. Tena apigiwe mizinga ishirini na moja kama heshima ya kuwa mwanajeshi.

Akatumia ujuzi wake wa karate kumpiga moja ya wale mabaunsi kwenye koo lake. Yule mtu akapiga yowe dogo kwa tabu na kudondoka chini. Fernanda naye alihangaika na lile jitu jingine. Lilikuwa limemzidi mbinu likamkaba shingoni na kumuwekea kisu cha tumboni.

Sajenti akanyosha mikono juu ili lile jitu lisimchome kisu Fernanda. Lile jitu likamtazama Sajenti kisha kwa dharau likatabasamu. Lile jitu liliyapeleka macho yake mpaka alipokuwa mwenzake ambaye alikuwa anaugulia maumivu ya shingo. Likayakunja macho yake kwa hasira lakini kabla halijafanya jambo lolote. Fernanda akalikanyaga chini na kiatu chake cha kwakwakwa chenye kisigino chenye ncha kali. Likapiga yowe kubwa kama mbwa. likamuachia Fernanda. Lilikuwa ni pigo makini lililomuacha na maumivu makali. Omary alikuwa wa kwanza kumuona Sajenti baada ya kutazama upande aliosikia yowe. Akamuona Sajenti akimpiga teke la tumbo yule mtu aliyekuwa amemuwekea kisu cha tumbo Fernanda. Omary akamuonyesha yule mwanamke upande alipokuwa Sajenti. Yule mwanamke alishtuka kumuona Sajenti akiwa anapigana. Kilichomfanya ashangae ni kutokana na kumkumbuka Sajenti Warioba. Alikumbuka alimuona kule kwenye kisiwa cha montao de trigio waliposhuka kwenye meli ya Ambagon. Akakumbuka walivyogongana macho na Sajenti alafu Sajenti akayakwepesha. Yule mwanamke alimuona pia Fernanda. Alikumbuka kuwa wote aliwaona wakiwa kule kisiwani. Omary alitaka aende kule alipo Sajenti lakini yule mwanamke alimzuia na mkono kifuani. Akamwambia atulie. Walitazama jinsi Sajenti na yule mtu walivyokuwa wakipigana. Akagundua kuwa kwa mapigo aliyokuwa anayapiga Sajenti ni wazi alikuwa na ujuzi wa ngumi. Alihisi huenda Sajenti alikuwa mwanajeshi kutokana na mapigo yake. Uzoefu wa yule mwanamke ulimuambia kuwa mtu wa kawaida hawezi kupigana kwa mtindo ule. Hii ilimfanya aanze kujihadhari na Sajenti kutokana na kugundua kuwa hakuwa mtu wa mchezo.

Yule mwanamke alichukua simu yake akabonyeza bonyeza kisha akairudisha mfukoni mwa suruali aliyokuwa ameivaa. Akashtuka kumuona Fernanda akiokota kisu na kumrukia nacho yule mtu aliyekuwa anapigana na Sajenti. Fernanda alilichoma lile jitu kisu cha mgongoni. Lile jitu likasimama kwa sekunde kumi likipiga hatua kama zombi kugeuka upande wa nyuma alipokuwa Fernanda. Likamtazama kwa macho ya buriani huku mdomoni damu zikitoka. Hatimaye lilianguka chini kama mti uliopigwa shoka la mwisho. Sajenti na Fernanda hawakutaka kupoteza muda. Wakaondoka haraka. Walijua tayari wameshaharibu. Wameshaua mtu jambo ambalo ni kosa kisheria kwa nchi yoyote ile. Waliondoka bila ya kujua nyuma yao walikuwa wanafuatiliwa na mwanamke hatari asiye na huruma ambaye alikuwa na Omary. Walirudi nyumbani kwa Fernanda wakiwa wanashindana na muda kama watu wanaokimbizwa. Fernanda akabadili nguo harakaharaka kisha akachukua mkoba wake mweusi akatoka nao mpaka sebuleni ambapo alimuacha Sajenti. "Where are we going now my dear?"

Sajenti aliuliza kwa lugha ya kingereza sauti yake ikiwa na dalili zote za wasiwasi. "Tunaelekea Rio je deneiro mume wangu" Fernanda akasema huku akiizima ile feni iliyokuwa inazunguka zunguka pale sebuleni.

"Naomba unitolee hilo taulo hapo juu ya feni mpenzi" Fernanda alisema huku akitazama juu ilipofeni na lile taulo. Sajenti naye alitazama juu kuiangalia ile feni na taulo. Alipanda juu ya stuli ya sponji akalitoa lile taulo. Baada ya taulo kutolewa kwenye feni. Fernanda alienda kwenye swichi kuiwasha tena ile feni. Hapo Sajenti akaelewa maana ya Fernanda kufanya hivyo. Alimuona Fernanda ni mwanamke mwenye akili sana. Hata hivyo akili yake ilimuambia kuwa anapaswa awe makini naye. Wakatoka mule ndani kuelekea nje. Fernanda alitembea hatua kumi na tano mpaka ulipoukuta wa lile jumba. Akaingiza mkono kwenye mkoba wake kisha akatoa kitu kama rimoti. Akabonyeza. Kumbe haukuwa ukuta bali lilikuwa ni siling board lililopakwa rangi inayofanana na ukuta. Lilikuwa ni geti ambalo ndani yake kulikuwa chumba cha kuhifadhia magari. Lile geti la ceiling board ambalo mwanzo Sajenti alidhani ni ukuta likapanda juu kama mfano wa maduka ya siku hizi yenye milango ya kupanda juu. Ndani kulikuwa na magari mawili. Moja lilikuwa jekundu na jingine jeusi. Fernanda aliingia mule ndani akapanda kwenye gari jekundu aina bmw x6. Lilikuwa gari la kifahari sana. Fernanda akalitoa mule ndani mpaka nje alipokuwa amesimama Sajenti. Akamugiza Sajenti apande ndani ya gari. Sajenti akapanda kisha Fernanda akashusha kioo cha dirisha la gari lililo upande wake akatoa mkono nje ulioshika ile rimoti. Akabonyeza lile geti la ceiling board la ile nyumba likarudi kama lilivyokuwa awali. Kisha akaondoa gari mpaka kwenye geti ambapo alitoa tena mkono dirishani akabonyeza rimoti, geti likafunguka. Wakatoka na gari mpaka nje kabisa. Akabonyeza rimoti geti likajifunga.

Safari ya Rio de jeneiro ikaanza kutoka katika mji wa Juquei ilipofukwe nzuri ya Juquei. Ilikuwa yapata saa nne na nusu usiku walipoanza safari yao kuelekea Rio de jeneiro. Ndani ya gari kulikuwa kimya. Hakuna aliyekuwa akiongea isipokuwa sauti ya mngurumo wa gari. Kila mmoja alitafakari alichokuwa anakijua. Walitembea kwa mwendo wa lisaa limoja bila ya kuongea chochote. Sajenti aliamua kuvunja ukimya.

" Inaonyesha wewe ni mzoefu barabara hii!"

"Hahaha! Kwa nini?"
Fernanda alisema huku akicheka. Fernanda ni mtu apendaye kucheka. Mara nyingi tokea afahamiane na Sajenti amekuwa ni mtu wa kufurahi. Sajenti naye akacheka kisha akamjibu. "Hahaha! Uendeshaji wako tuu unaonekana barabara hii wewe siyo mgeni"
"Hahaha! Ni kweli hii barabara mara kwa mara naitumia. Huu ni mwaka wa saba tokea nianze kuitumia".
"Mwaka wa saba? Aisee! Basi ndio maana. Maana mwendo huu ni lazima uwe mzoefu ndio uendeshe gari kwa kasi hii"
Sajenti alisema huku akichungulia kwenye vioo vya pembeni kuona kama kuna gari yoyote inawafuata kwa nyuma. Hakuna gari yoyote. Akajua bado wako salama. "Kwani naendesha kwa kasi sana?" Fernanda aliuliza huku akigeuka kumtazama Sajenti.
"Hahaha! Unachekesha sana Fernanda".

"Mbona huu ni mwendo wa kawaida mume. Au unaogopa? Hahaha!"
Fernanda akacheka. Kikweli ile gari ilikuwa inaendeshwa kwa mwendo mkali sana. Jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa usalama wao. Lakini kilichomshangaza Sajenti Warioba ni ule ujasiri wa Fernanda. Alikuwa hata haogopi. Aligundua kuwa Fernanda alikuwa ni dereva mzuri wa gari. Walifika sehemu yenye mlima kidogo wenye konakona nyingi na msitu. Sajenti alitegemea kutokana na kona nyingi ambazo zilikuwa kali na zilizokuwa kwenye mlima. Alitegemea Fernanda atapunguza mwendo lakini haikuwa hivyo. Fernanda alilala na kona za ule mlima kama mchezo. Roho ya Sajenti ilikuwa juujuu kama kamba ya kunyongea. Ghafla mvua kubwa ilianza kunyesha. Hapa Fernanda akapunguza mwendo kutokana na matairi ya gari kuteleza barabarani. Walikuwa wapo msituni juu ya mlima wakati mvua kubwa ikinyesha. Hapakuwa na dalili ya makazi ya watu. Wala hawakupishana na gari lolote. Kulikuwa kimya. Mngurumo wa mvua na radi ndio zilisikika. Vimuli muli vilimulika hali iliyomfanya Warioba kuona msitu mnene kupitia dirishani. Wote walikuwa kimya hakuna aliyekuwa akiongea. Fernanda aliendesha gari kwa umakini huku macho yake yakionyesha utulivu. Ni kwamba alikuwa na uzoefu wa safari za namna hiyo. Taa za gari zilijitahidi kupambana kufukuza giza na matone ya mvua ili kumuwezesha Fernanda kuona.

Walimaliza kupanda ule mlima sasa wakaanza kushuka kwenye mteremko mkali wenye kona kona nyingi wakiwa bado wapo kwenye msitu mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Msitu wote ulizingirwa na wingu zito jeusi ambalo lilikuwa likimulika mulika kwa radi. Sajenti hakuwahi kuona mvua kubwa kwa kiwango kile tangu kuzaliwa. Yeye alizoea mvua za Tanzania ambazo siyo kubwa sana. Lakini mvua za brazil aliziona ni mvua zenye vitisho kutokana na ukubwa wake na radi. Ni kutokana na kuwa nchi ya brazil ni moja ya nchi zilizopo katika tabia ya nchi ya kiikweta ambapo mvua zake siyo lelemama. Nchi nyingine kwa afrika ni kama jamhuri ya kidemokrasia ya kongo. Mvua za maeneo haya ni mvua kubwa haswa zisizohitaji mchezo. Punde Sajenti kupitia vioo vya gari aliona kwa nyuma gari ikija kwa kasi ikiwa imewasha full light. Moyo ulimpasuka pwaa! Aliogopa sana. Akamgeukia Fernanda ambaye naye alikuwa ameona jambo hilo. Fernanda alikanyaga mafuta na kuongeza kasi ya gari bila kujali mvua inanyesha wala kujali kuwa gari linateleza. Sajenti aligeuka nyuma kuangalia gari lile lililokuwa linawafukuza kwa nyuma. Hakuona mtu yeyote isipokuwa mwanga mkali kutoka katika lile gari. Fernanda alilala na kona za mteremko wa ule mlima kama kichaa. Sajenti awali alidhani kuwa Fernanda anajua gari lakini kumbe alikuwa anajidanganya. Hakuwahi ona udereva wa Fernanda. Muda huu sasa ndio alijua kuwa Fernanda alikuwa ni dereva hatari wa viwango vya kimataifa. Aliendesha gari kama ndege. Yaani ilikuwa inapaa juujuu kama haigusi barabara vile. Sajenti alikumbuka mashindano ya magari yakiwa yanachanja mbuga. Akajiona naye sasa yupo kwenye mashindano hayo. Dereva alikuwa ni Fernanda alafu yeye ni msoma ramani. Mara mlio wa risasi ulisikika kutoka upande wa nyuma. Zilikuwa ni risasi mfululizo zikiikosa kosa gari lao.. Fernanda alizidisha kasi akijaribu kuliweka gari katikati ya barabara lisiteleze. Ilikuwa kila baada ya mita mia moja kulikuwa na kona jambo ambalo lilihitaji umakini mkubwa. Hata hivyo Fernanda aliijua fika njia hiyo. Njia hiyo hata angefumba macho angeweza kuendesha gari. Lile gari kutoka nyuma lililokuwa linawafukuza liliwagonga kwa nyuma hali iliyowafanya wakose utulivu na kupoteza mhimili. Ilibaki kidogo watoke nje ya barabara lakini Fernanda alikata kona kali hali iliyolifanya gari lao ligeukia lilipokuwa linatoka huku likienda kinyume nyume likitazamana na gari la maadui. Lilienda kinyume nyume kwa kasi huku wakitazamana na lile gari lililokuwa linawafukuzia. Wale watu walirusha risasi kuwapiga wakina Sajenti. Risasi zilipasua kioo cha mbele cha gari la kina Sajenti. Sajenti na Fernanda walikuwa katika wakati mgumu. Walikuwa wakiinama kukwepa risasi zilizokuwa tayari zimepasua kioo chote cha mbele.

Fernanda akaligeuza gari kwa kasi kama lilivyokuwa mwanzo kutazama mbele walipokuwa wanaelekea. Lahaula! Mbele yao kulikuwa na Daraja refu ambalo chini yake kulikuwa na mto mkubwa unaopitisha maji yaliyofurika. Kama wangeendelea kwenda kinyume nyume wangezama mtoni. Fernanda akajitahidi kuliweka gari sawa kwa kuzungusha usukani kwa haraka ambapo alikwangua kidogo kingo za Daraja ambazo kama zisingekuwepo wangeingia mtoni. Wakati huo wale watu wabaya waliendelea kuwafukuza huku wakiwatupia risasi kwa mfululizo bila kukoma. Wakapita kwenye lile Daraja salama salimini gari ikiwa haina vioo vya mbele hali iliyosababisha maji ya mvua kubwa kuingia ndani ya gari na kuwalowanisha. Mvua ilikuwa ikiwapiga usoni kwa nguvu sana. Hii ilikuwa ni hatari kwani ilimfanya Fernanda apoteze utulivu na umakini wa kuendesha gari jambo ambalo ilikuwa ni hatari. Pia usukani ulikuwa unateleza kutokana na kulowa maji. Gari lililokuwa linawafukuza kwa nyuma liliwakaribia na kuwa usawa wao. Magari yao yalikuwa yanalandana kwa kasi huku yakikatisha kona za ule mshuko wa mlima. Fernanda kwa haraka alikanyaga breki baada ya kuona mdomo wa bunduki ukielekezwa upande wake. Lile gari likawapita kwa kasi likiacha gari lao nyuma kama mita kumi. Kama Fernanda asingekanyaga breki basi ule ndio ulikuwa mwisho wao. Kwani baada ya kukanyaga breki walisikia mlio wa risasi nzito ukilia.

"Ruka nyuma, nyanyua hiyo siti utaona bunduki. Ichukue tuwakabili hawa nguruwe" Fernanda akasema huku mdomo wake ukipigwa na matone makubwa ya mvua. Sajenti akiwa chapachapa kwa kulowa aliruka nyuma. Akanyanyua siti na kukuta bunduki aina ya AK47 ambayo ni bunduki ya kivita.

Aliichukua akarudi nayo mbele tayari kwa mapambano. Wakati huo ile gari ya maadui ilikuwa imeenda kuziba barabara kwa mbele ili wasipite. Sajenti alianza kulenga shabaha kama mdunguaji mahiri. Kama kuna somo ambalo Sajenti Warioba alifaulu akiwa jeshini ni somo la ulengaji wa shabaha. Sajenti alikuwa anashabaha kuliko mtu yeyote yule. Hata ungekuwa umbali gani angekudungua tuu. Kwake ilikuwa ni dhambi ya kutokwenda mbinguni kupoteza risasi moja. Akapiga risasi nne na zote ziliwapata maadui. Walikuwa ni maadui wanne waliokuwa wakiwafukuza. Kimya kikafuatia mvua ikienelea kunyesha. Wakalisogelea lile gari wakakuta kuko kimya. Hii iliashiria kuwa hakuna mtu aliyekuwa hai. Wakasimamisha gari wakashuka kwa tahadhari, wakakuta miili minne ikiwa imelala roho zao zikiwa mbali nayo. Yote ilikuwa imepigwa risasi kichwani. Fernanda alishangaa kuona watu wale wakiwa wamelengwa wote kichwani sehemu ileile. Wote walipigwa kwenye paji la uso.
"Unashabaha mume wangu ndio maana hata kule hukosi" Fernanda alisema akimkumbatia Sajenti wote wakiwa wamelowa chapachapa. Akampelekea mdomo wake kisha wakanyonyana ndimi zao huku mvua ikiwanyeshea na vimulimuli vikiwamulika. Fernanda alipata hisia kali za mapenzi. Akamvuta Sajenti mpaka lilipopaki lile gari la wale maaduli. Wakashikana wakashikamana. Wakavua wakavuana nguo. Mwisho wakapeana mahaba mazito huku matone makubwa ya mvua yakimwagika katika miili yao. Hiyo ilikuwa ni baada ya dhiki ni faraja. Dhiki ya maadui waliokuwa wakiwarushia risasi. Sasa waliona wajifariji na kujipongeza kwa kula raha ya mapenzi. Walimaliza, Sajenti aliifuata ile miili kuipekua. Walikuwa wote ni wabrazili. Alikuta simu kwenye mfuko wa suruali ya moja wa wale watu waliokuwa wamekufa. Akaikagua. Akashtuka kuona namba yenye code ya kitanzania. Aliikariri kichwani harakaharaka. Kisha akaendelea kuikagua ile simu. Akataka kuingia kwenye upande wa meseji lakini alizuiwa kutokana na simu kudai password. Aliingia upande wa picha. Aliona picha nyingi lakini hakuona hata moja ambayo ingemsaidia. Punde alishtuka kuona picha ya BLM akiwa na yule mwanamke aliyemuona kwenye meli. Bila shaka unakumbuka BLM ni yule Mama bonge ambaye Sajenti kwa mara ya kwanza alimuona kwenye lile jumba kule kigamboni mwembe mtengu akiwa anataka kulala na Joseph. Pia Sajenti Warioba alimuona BLM kwenye ile hospitali ya Ambagon. Leo tena anamuona kwenye simu ya moja ya wale watu wabaya.

Akakumbuka maneno ya Joseph siku ile wakiwa wamejificha kwenye ua katika lile jumba kule kigamboni. Moyoni alianza kuamini maneno ya Joseph kuwa huenda ni kweli yule Mama na mume wake wanahusika na biashara haramu ya viungo vya watu. Hakuona picha nyingine ya maana itakayomsaidia kwenye uchunguzi wake. Akaitupa ile simu kisha wakaondoka na Fernanda kurudi kwenye gari lao. Walipoingia ndani ya gari ambalo lilikuwa limejaa maji ya mvua na bado mvua ilikuwa ikipiga. Fernanda alibonyeza kitufe kimoja kwenye gari. Mara kioo cha mbele kikatokea kikaziba ule uwazi wa mbele. Sajenti alibaki mdomo wazi kwa kushangaa. Angeachaje kushangaa ikiwa hajawahi kuona gari kama ile. Ilikuwa ni haki yake. Wakaondoka pale wakilikwepa lile gari la wale maadui lililokuwa katikati ya barabara. Safari ikaendelea mvua bado ilikuwa ikinyesha huku giza nene likiwafunika katikati ya msitu kwenye ule mlima. Fernanda aliweka nyimbo za kibrazili kufukuza ukimya uliokuwa mule ndani. Gari ilitembea kwa kasi kubwa baada ya kumaliza ule mlima. Bado mvua ilikuwa inanyesha. Muziki mlaini wa kibrazili uliendelea kupiga huku gari likichanja mbuga yenye vichaka vifupi na virefu. Kwa mbali kabisa waliona mataa yakiwapokea. Sajenti akatambua kuwa wanakaribia mji mwingine baada ya purukushani nzito waliyoipata katika kale kamlima. Walipita miji kadhaaa mpaka walipoingia katika mji wa agra dos reis.hapo ilikuwa imeshafika saa kumi na mbili asubuhi. Waliingia sehemu ya kuwekea mafuta wakaongeza mafuta. Hawakutaka kupumzika. Wao walichotaka ni kufika jiji la Rio de janeiro. Fernanda aliendesha gari kwa umakini na kwa tahadhari. Hakuendesha kama alivyokuwa anaendesha usiku. Aliendesha kawaida kuepuka kusimamishwa na askari wa barabarani. Masaa matatu yaliwafikisha katika mji wa campo grande ambapo walisimamisha gari katika duka moja la nguo. Fernanda alishuka akamuacha Sajenti ndani ya gari. Hakukaa sana mule dukani alitoka akiwa kabeba mfuko ambao ndani yake kulikuwa na nguo. Walibadilisha nguo zilizonyeshewa na mvua ya usiku wakavaa nguo mpya kabisa. Sasa walikuwa watu wapya. Ile baridi iliyokuwa ikiwapiga iliisha. Waliondoka pale kwenye duka la nguo wakazunguka katika mji ule wa campo grande wakitafuta mgawaha mzuri kwa ajili ya kunywa kifungua kinywa. Mji wa campo grande ulikuwa ni mji uliopangika vizuri. Watu wake walikuwa bize na kazi zao. Kila mmoja alikuwa na hamsini zake. Sajenti aligundua kuwa mji ule wakazi wengi walikuwa ni wabrazil wenyewe. Punde walifika mbele ya mgawaha mmoja uliokuwa pembeni ya barabara inayoelekea Rio de janeiro. Walishuka wakaenda kupata kifungua kinywa. Walipomaliza walirudi ndani ya gari kuendelea na safari. Wote walikuwa wamechangamka matumbo yao yakiwa mazito kutokana na kupata chakula. Masaa mawili yakawafikisha katika mji wa meier ambao ni mji mdogo baada ya mji wa campo grande. Hapo wakaendelea kukata mwendo.

Ni majira ya saa kumi jioni ndio waliingia katika jiji la Rio de janeiro. Jiji ambalo lilisifika kwa utalii na utamaduni katika nchi ya brazil. Sajenti alichungulia nje kupitia dirishani ambapo kwa mbali aliona sanamu la Yesu likiwa juu mlima corcovado ambao ni mlima wenye mita 710.

Mlima corcovado ni mlima wenye mita 710 kutoka usawa wa bahari. Siyo mlima mrefu sana lakini ni mlima maarufu katika jiji la Rio de janeiro. Umaarufu wake unatokana na uwepo wa sanamu la yesu juu yake. Sajenti Warioba bado alikuwa akishangazwa na uzuri wa jiji la Rio de janeiro ambalo ni jiji la pili kwa ukubwa baada ya sao paulo. Rio de janeiro ni jiji maarufu zaidi duniani kuliko majiji mengine yaliyopo brazil.

Sajenti alishangazwa na jinsi maghorofa ya jiji hilo yakimtazama kwa shani ya ajabu. Alistaajabishwa na miundombinu ya aina yake yenye kuacha mdomo wazi wageni. Fernanda akafungua droo ya gari akatoa miwani nyeusi akaivaa usoni. Sajenti alimtazama Fernanda aliyekuwa bize akiendesha gari huku akijiweka vizuri nywele zake ndefu kama mhindi. Ndio alikuwa na haki ya kuwa na nywele ndefu kama muhindi kutokana na sababu kuwa wabrazili pia wanaasili ya wahindi wekundu licha ya kutawaliwa na mataifa mengine kama wareno. Fernanda aliendesha gari akipita kwenye flyover kwa namna ambayo ilimfanya Sajenti azidi kumuona kuwa yeye ni dereva wa kimataifa. Sajenti siyo kwamba yeye hajui kuendesha gari. Anajua sana. Tena sana lakini tokea azaliwe hajawahi kuendesha gari katika barabara za flyover nyingi kama zile. Walitokea katika fukwe kubwa ya kupendeza ambapo kulikuwa na watu wengi kama kumbikumbi. Watu karibia wote walikuwa wamevaa nguo za fukweni. Ambazo ni nguo za kuogelea. Walipaki gari eneo la kuegesha magari kisha wakashuka. Sajenti alipokelewa na upepo mwanana mtamu ambao hajawahi kuuona maishani mwake. Tokea azaliwe hakuwahi kujua kama kuna upepo wenye ladha kama ule. Kushoto kwake kulikuwa na jengo kubwa ambalo juu yake kulikuwa na maandishi yaliyosomeka kwa lugha ya kireno " bem-vindo às praias de ipanema" ikimaanisha karibu kwenye fukwe za ipanema.

Ilikuwa ni beach ya ipanema. Moja ya fukwe maarufu katika jiji la Rio de janeiro. Ilikuwa ni beach ambayo mtu yeyote aliyefika nchini brazil lazima afike katika fukwe hiyo. Watalii na watu kutoka mataifa mbalimbali walikuwepo wakifurahia maisha. Sajenti aliona watu wakiogelea kwa namna ya kustaajabisha. Aliona pia watu wakicheza michezo ya majini wakiwa wanafanya mashindano ya boat na parachuti baharini. Roho yake ililipuka kwa furaha kufika katika beach hiyo ambayo ilifananishwa na paradiso. Akawaona baadhi ya wafrika weusi wakiwa na wapenzi wao wakizungu. Hakuona muafrika akiwa na muafrika. Bali aliona kama siyo mwanamke wa kiafrika akiwa na mzee wa kizungu basi aliona kijana wa kiafrika akiwa na bibi wa kizungu. Yeye peke yake ndio alikuwa na msichana wa kibrazil wanaolingana umri. Jambo hilo lilifanya baadhi wa waafrika wenzake kumshangaa na kumuonea wivu. Hata hivyo hakujali. Alichojali ni usalama wake.

Wakatafuta sehemu nzuri ya kupumzika wakakaa. Ilikuwa tayari ni saa kumi na mbili za jioni jua likipunga miale yake ya mwisho mwisho kuiaga siku hiyo. Lakini fukwe ya ipanema ndio kwanza kulikuwa kumekucha. Watu walikuwa wanaongezeka maradufu. Fernanda alivua nguo akabakiwa na kichupi na brazia kwenye maziwa. Kisha akamlalia Sajenti kwenye kile kitanda maalumu cha fukweni.

"Punguza nguo tukaoge"

Fernanda aliongea akijibebisha na kiswahili chake kama cha kanjibai. Sajenti akatabasamu kisha akavua tishet aliyonunuliwa kule kwenye mji wa campo grande. Akabakiwa na bukta nyepesi ya ndani. Sajenti hakutaka kuonekana mshamba. Alimbeba Fernanda mpaka baharini wakaingia wote majini. Fernanda alikuwa akicheka cheka kwa furaha. Aliyaona yale ndio maisha aliyostahili kuishi mrembo kama yeye. Moyoni mwake aliahidi kumpenda Sajenti siku zote za maisha yake licha ya utofauti wa kitaifa na kirangi. Yeye ni mbrazil na Sajenti ni mkenya. Alijua ni mkenya kwa sababu Sajenti alimdanganya. Waliogelea mpaka saa moja unusu usiku. Beach ya ipanema haikuwa na giza kutokana na mataa makubwa yaliyokuwa yanawaka. Ilikuwa ni kama mchana. Ili mtu ajue ni usiku kitu pekee ambacho kingemjulisha kilikuwa ni uwepo wa nyota za angani. Walienda wakapanda kwenye boat za kuogelea. Yule mtu aliyewapa ile boat alimpa maelekezo Sajenti namna ya kuiendesha boat ile. Sajenti alielewa semina ile ya muda mfupi. Hao wakaingia majini. Fernanda akamshikilia Sajenti kwa nyuma wakati Sajenti akiwa anaendesha akiyakata mawimbi ya bahari kwa kasi. Kila walipoyakata mawimbi maji yaliwarukia jambo ambalo liliwafanya washangilie kwa kupiga makelele kama watoto. Nywele za Fernanda zilikuwa zikipepeswa na upepo kama bendera hali iliyozidisha uanamke wake. Kama ingekuwa ni filamu basi ingekuwa filamu ya kihindi au kifilipino. Lakini haikuwa filamu bali lilikuwa tukio la kweli kabisa. Walitosheka na mchezo huo wakiwa hoi bin taabani. Wakatoka majini yapata saa tatu usiku. Wakaenda kwenye mgahawa wakiwa tepetepe wamelowa maji. Hakuna aliyewashangaa kwani ilikuwa ni kawaida hata kwa watu wengine. Wakachukua juisi za kopo zenye mirija na nyama choma. Wakakaa sehemu nzuri iliyokuwa na watu wachache ambao nao walikuwa na wapenzi wao. "Hivi unaitwa nani mume wangu. Maana mpaka sasa hujanambia jina lako"

Fernanda alianza mjadala akiwa ameweka mrija mdomoni.

" Kumbe sikukwambia jina langu. Haha! Ajabu hii"

"Ajabu kidogo. Yaani nipo na mtu hata simjui jina lake. Mtu anayenipa raha moyoni"

" Naitwa Otieno, ukipenda niite otiti"


Sajenti akasema kwa majivuno ungedhani ni jina lake kumbe ni jina la uongo.

"Hahah! Otiti! Jina zuri sana"

Fernanda alisema akijifaraguza na macho yake ya kijivu.

"Hivi kenya na Tanzania wapi mko wanaume wenye kupenda?" Fernanda aliuliza swali la uchokozi.

"Kenya ndio top mpenzi" Sajenti alijibu.

"Aah! Wapi. Unatetea upande wako. Mimi nimeishi kenya na Tanzania. Kenya nimeishi mombasa na nairobi. Tanzania nimeishi zanzibar,. Dar es salaam na Arusha"
Fernanda alisema kisha akameza fumba la juisi kupitia mrija kisha akaendelea.

" Watanzania wanajua kupenda kuliko ninyi wakenya"

"Ahaa! Wapi. Kwa hiyo mimi sikupendi?"
Sajenti aliingilia mazungumzo ya Fernanda kwa swali.

"Hata mimi najiuliza mapenzi haya umeyatolea wapi. Kenya hakuna wanaume kama wewe"

"Embu acha utani mpenzi" Sajenti akatabasamu huku moyoni mwake akitamani amwambie ukweli kuwa yeye ni Mtanzania. Lakini alikumbuka kuwa bado hajamaliza kazi yake ya uchunguzi. Hivyo kumwambia ukweli Fernanda huenda kungemletea madhara. Hata hivyo bado hakuwa anamuamini Fernanda. Walizungumza mengi mpaka ilipohitimu saa nne unusu usiku ambapo walienda kupakia kwenye gari wakaondoka mpaka ilipo hotel ya copacabana iliyopokaribu na beach ya copacabana. Siku hiyo hawakufanya lolote kutokana na uchovu wa tangu jana usiku walipokuwa kwenye ule msitu kwenye kile kilima. Sajenti akiwa kitandani alikumbuka matukio yote yaliyomtokea. Tokea akiwa kigamboni kwenye lile jumba la watu wabaya. Alikumbuka alivyojirusha baharini kwenye Daraja la kigamboni.. Akakumbuka siku alipokutana na Fernanda kwenye lile kasino kwenye ile meli ya Ambagon. Mawazo yake yalimpeleka mpaka tukio la usiku wa jana yake alipokuwa kwenye ule msitu wenye kilima ambapo mvua kubwa ilikuwa ikinyesha huku wale watu wabaya wakiwafuata. Sajenti alivuta pumzi zito alipokumbuka gari lao lilivyopasuliwa kioo cha mbele na wale mabedui waliotaka kuwaua. Moja kwa moja alitambua kuwa wale walikuwa ni watu kutoka kundi baya la Ambagon. Kundi ambalo aliliona ni kundi la mashetani. Hatimaye mawazo yake yalimrejesha chumbani akiwa na Fernanda ambapo muda huo alikuwa kawasha laptop yake. Sajenti akamsogelea Fernanda akatazama kile alichokuwa anakiangalia Fernanda kwenye laptop. Alishtuka kumuona yule mwanamke akiwa na Omary kwenye ile nyumba ya Fernanda walioiacha kule Juquei. Sajenti alishangaa iweje yule mwanamke na Omary wawe kwenye ile nyumba ya Fernanda.

"Hawa watu walikuwa wanatufuatilia. Nadhani ndio waliotuma wale watu jana usiku" Fernanda alisema akiwatazama watu wale kwenye laptop. Sajenti alikaa kimya akitazama laptop iliyokuwa inamuonyesha yule mwanamke akikagua nyumba ya Fernanda kule Juquei.
"Unawajua watu hawa?"Fernanda alisema akimtazama Sajenti Warioba usoni.

" Hapana" Sajenti alijibu akibabaika.

"Mbona umejibu kwa wasiwasi. Huyu mwanamke si tulimuona kule kwenye kisiwa cha montao de trigo" Fernanda akasema akimdadisi Sajenti.

"Mimi sikumuona. Ulimuona akifanyaje?"

"Tuachane na haya mume. Tupumzike"


Fernanda alisema akamkumbatia Sajenti kwa mahaba. Kitendo cha Sajenti kumuona Omary na yule mwanamke kwenye nyumba ya Fernanda kilimnyima amani sana. Alihisi hata mule hotelini hayuko salama. Usingizi uliokuwa unamnyemelea ulipotea. Angelalaje kwa mfano wakati alijua kuwa kuna watu wa wabaya walikuwa wanamtafuta kwa udi na uvumba. Fernanda alipitiwa na usingizi akamuacha Sajenti akiwa macho. Sajenti alipoona Fernanda amelala akampekua kwenye mkoba wake. Aliona passport tatu zenye picha ya Fernanda lakini majina tofautitofauti. Akaona pia mabunda ya pesa yenye dola za kutosha. Aliona pia kadi tatu za benki. Sajenti alijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Kwa nini Fernanda alikuwa na passport zote zile tena zenye majina tofauti tofauti. Alichoshangaa ni kuwa katika passport zote hakuona jina la Fernanda jina ambalo alijua ndilo jina lake. Akaendelea kupekua ule mkoba wa Fernanda akakuta simu janja ambayo ilikuwa imezimwa. Akajaribu kuiwasha kwa bahati nzuri ikawaka. Aliona picha ya Fernanda kwenye kioo cha simu. Alianza kubonyeza bonyeza kuona kama ataona jambo lolote la maana lakini hakuona kitu. Zilikuwa ni picha za kawaida za Fernanda. Upande wa meseji hakuona jambo lolote la maana. Meseji zote zilikuwa kwa lugha ya kireno. Sajenti alitoka kwenye kile chumba akatokea kwenye korido ndefu. Alipanda kwenye lift ambayo alibonyeza kitufe kilichoandikwa alama G kumaanisha ground yaani chini. Dakika tano alikuwa yupo chini kabisa ya ile hoteli ya copacabana.

Alipofika chini alikutana na jambo la kushtusha. Pale mapokezi alimuona Omary na yule mwanamke wakiwa wanaongea na mtu wa mapokezi. Aliwaona wakitoa karatasi na kumpa yule mtu wa mapokezi. Yule mtu wa mapokezi aliitazama ile karatasi. Kisha alimsikia yule mwanamke asiye na jina aliyekuwa na Omary akimuuliza yule mtu wa mapokezi kuwa aliwaona watu waliokuwa kwenye ile picha. Swali hilo liliufanya moyo wa Sajenti upasuke. Yule mhudumu aliwatazama. Kisha akawauliza.

" Quem é você?" akimaanisha wewe ni nani.

" Somos soldados ilimitados" Yule mwanamke aliyekuwa na Omary alijibu huku akitoa kitambulisho.

Alimaanisha kuwa wao ni askari wa kimataifa wasiyo na mipaka wa interpol kutoka umoja wa mataifa. Yule mtu kwenye mapokezi kusikia hivyo aliingiwa na wasiwasi. Wala hakuchukua kile kitambulisho alichokuwa akipewa na yule mwanamke. Alikiri kuwa ni kweli anawajua watu wale waliokuwa kwenye picha. Kisha akawaelekeza ghorofa na chumba walichochukua. Sajenti alirudi mbio kwenye lift akaiamrisha imrudishe kule alipomuacha Fernanda. Alirudi mpaka chumbani akamkuta Fernanda bado amelala fofofo kama maiti. "Fernanda! Fernanda wake up!" Sajenti alimuita Fernanda huku akimtingisha aamke

ITAENDELEA

Jipatie simulizi yote ya MLIO WA RISASI HARUSINI Softcopy kwa Tsh 3,000/= Kitabu Tsh 10,000/=

0693322300
Airtelmoney
Robert Her
iel
 
Achia mkwaju mkuu nipo kwa watu huku burudani zako zinanifanya kuwa happy na kuona nipo home land
 
Back
Top Bottom