Tumosa
JF-Expert Member
- Jul 21, 2016
- 16,527
- 52,623
[emoji23] [emoji23] [emoji23] sikujua kuwa mambo yashanoga huku
[emoji23] [emoji23] [emoji23] sikujua kuwa mambo yashanoga huku
Shikamooo
[emoji23] [emoji23]Tivu santee
Inatisha jamani nitalalaje
Na kukutag juuu! Tumosa Tumosa[emoji23] [emoji23] [emoji23] sikujua kuwa mambo yashanoga huku
Sijashinda jf jamani,jioni hii ndo nmeingia [emoji4] [emoji4]
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] barikiwa Steve*UNA NINI LAKINI MELISSA? --- 06*
*Simulizi za series*
ILIPOSHIA
Alipomaliza, akakata simu na kumpatia Darren. Alafu ghafla akadondoka na kuzirai tena. Kabla Darren hajahangaika naye, akaita kwa sauti ya chini, “Mama.” kisha na kusema, “Wewe ni nani? … Melissa …” akatazama simu yake na kuuliza tena, “wewe ni nani?”
ENDELEA
Alishinwa kupata majibu. Alijikuta kwenye maswali ya mkanganyiko juu ya mama yake na Melissa. Wana nini kati yao? Wana nini ambacho hakijui? Wana nini ambacho wanamficha?
Akaketi kitandani akiwaza na kuwazua. Hata alipompigia Melissa hakupokea bali tu akituma ujumbe kuwa wataongea punde atakapokuwa peke yake. Mwishowe akaamua kuzima simu akidhamiria kutomtafuta tena Melissa.
Akambeba mama yake na kumweka kitandani. Alafu akafungua madirisha apate hewa wakati akiangalia kuandaa mengine. Alipomaliza kila kitu, akajilaza kitandani akiwaza sana. Mwishowe usingizi ukambeba.
Kidogo akiwa usingizini, akasikia hodi mlangoni. Akafumbua macho yake kwa uvivu akitazama mlango. Kidogo akajikusanya kitandani na kusogea karibu akiuliza ni nani anayegonga. Hakujibiwa. Alipoufungua akamwona mwanaume fulani mwenye mwili mpana akiwa amevalia koti la sufi na shati jepesi kwa ndani. Mwanaume huyo shingoni alikuwa amechora ‘tattoo’. Na uso wake mpana ulikuwa na kovu kwenye fuvu la shavu la kushoto. Macho yake yalikuwa madogo yaliyozama ndani, ila aliyakodoa.
Akauliza kwa sauti kavu, “Wewe ni Darren?” Darren akatikisa kichwa. “Naweza kukusaidia?”
Bwana yule hakujibu, badala yake akatazama ndani na kisha akarudisha macho yake kwenye uso wa Darren. Mara akamsukumia kando na kuzama ndani pasi na ruhusa.
“Hey!” Darren akapaza, “Unataka nini?” lakini bwana yule hakumjali, akiwa anasonga kwa hatua nzito, akawa anamuelekea Sarah, mama yake Darren.
Basi Darren upesi akaamka na kumkimbilia. Akamrukia mgongoni na kumkaba lakini hakuwa na nguvu ya kushindana na mtu huyo. Kwa kutumia mkono mmoja akanyofolewa mgongoni na kutupiwa ukutani. Alijibamiza sana kichwani kiasi cha kupoteza uwezo wa kujimudu kusimama tena, basi kwa mbali akawa anatazama kinachoendelea akiwa hana msaada wowote.
Bwana yule akamfuata mama yake na kwa kutumia mikono yake mipana akamkaba koo na kumminya kwanguvu. Akamminya sana. Darren akanyoosha mkono wake wa kuume akitaka kumsaidia mama yake. Akaita kwa kunong’ona. Lakini hayo yote hayakuwa na msaada. Hakuwa anajiweza.
Mbele ya macho yake bwana yule akammaliza mama yake na kisha akaondoka zake. Darren akatiririsha chozi akinong’ona, “Mama … mama … mama.”
Mara akasikia sauti ya kunong’ona, “Nipo hapa mwanangu.”
Alipotazama kushoto kwake ndipo akagundua kuwa mama yake alikuwa ameketi hapo. Alikuwa ameshaamka toka kwenye usingizi wa kukosa fahamu na kumbe yeye alikuwako usingizi akiona hayo yote!
Akamkumbatia mama yake kwanguvu akisema, “Mama, upo hai!” mama yake akamdaka kichwa na kumpapasa. “Nipo hai mwanangu. Nani alikuambia nimekufa?” akasema kwa tabasamu.
Darren akamtazama mama yake, na kabla hajasema jambo, wakasikia hodi mlangoni. Darren akashtuka sana. Akamtazama mama yake kwa kukodoa na kumwambia, “Jifiche!”
“Kwanini?” Mama akashangaa. Darren hakumpa maelezo zaidi badala yake akamsisitizia ajifiche wakati yeye akiwa anatafuta silaha. Alipopata kipande cha nondo akauendea mlango. Na kabla hajaufungua, akamsisitizia tena mama yake ajifiche. Mama hakuwa anajua kinachoendelea, akabaki akiduwaa.
“Nani?” Darren akauliza mlangoni. Kimya. Akauliza tena, “Nani?” mara hii sauti yake ikiwa na amri ndani. Mara akajibiwa na sauti ya kike, “Ni mimi!” basi akadhani ni Melissa. Akafungua mlango, uso kwa uso akakutana na jirani yake; mdada mrefu mwembamba aliyening’iniza headphone shingoni, kichwa chake amekifunika na kofia ya soksi nzito.
“Hey, Darren!”
“Hey, Rosetta. Mambo?” Darren akasalimu akificha mkono wake wenye nondo nyuma.
“Safi. Samahani kwa usumbufu, Darren. Nina ujumbe wako.” Rosetta aliposema hayo akachomeka mkono wake mfukoni na kutoa kikaratasi cheupe alichomkabidhi Darren na kumwambia, “Ni kutoka kwa Melissa!”
“Yuko wapi?” Darren akawahi kuuliza.
“Ameshaondoka,” Rosetta akajibu na kuongezea, “Nilimkuta chini. Aliponiona akanipatia na kisha yeye akaondoka zake mara moja.”
“Sawa, ahsante,” Darren akafunga mlango na kufungua ujumbe ule aliokabidhiwa. Ulikuwa ni wa ishara na hakuelewa jambo. Ni alama mbalimbali ambazo alihisi anaumwa na kichwa kuzichambua.
Akampatia ujumbe huo mama yake na kumuuliza kama kuna chochote anaweza kuambulia. “Umetoka kwa Melissa.”
Mama akatazama lakini naye hakupata kitu, ila alihisi kuna jambo. Na jambo hilo si zuri! Akamwambia Darren, “Mtafute Melissa!” naye Darren akatumia simu yake kupiga, hakuwa anapatikana. Ndipo akamshauri mama yake, “Acha niende kwake mwenyewe. Pengine ntaonana naye kuliko tunavyoongozana kila muda.”
Kwa kishingo upande, mama akaridhia. Basi Darren akashuka chini akimwacha mama yake ndani. Akakwea usafiri na kwenda moja kwa moja kwenye makazi ya Melissa.
Aliposhuka toka kwenye gari akaangaza mazingira alafu taratibu akiwa amedumbukiza mkono wake wa kuume mfukoni, akajongea. Kichwani akiwa anamuwazia Melissa. Akaapa kuwa akimkuta mwanamke huyo basi ni lazima amwambie kinachoendelea. Hatomwacha mpaka amweleze hayo. Amechoka kuzungushwa sasa.
Kama baada ya dakika tano akawa mlangoni mwa chumba cha Melissa. Akaukuta wazi. Akausogeza na kuzama ndani. Kila kitu kilikuwa sawa ila chumba kilikuwa kitupu. Hamna mtu!
Akaita akikagua lakini napo hakukuwa na jambo. Akaduwaa. Akampigia simu Melissa lakini napo haikuwa inapatikana, sasa akachoka kabisa, akajitupia kitandani.
Akangoja hapo kwa masaa lakini Melissa asionekane. Akajigeuza huku na kule, kule na huku. Akapiga simu na kutuma ujumbe, bado hamna kitu! Mpaka inafika saa nne usiku alikuwa kapa.
Basi akaona ni stara alale hapo, ili Melissa akirudi amkutie hapo. Lakini kabla hajafanya hivyo, akaona amtaarifu mama yake juu ya uamuzi huo. Akampigia simu. Nayo ikaita pasipo kupokelewa. Akapiga mara sita, majibu yakawa yaleyale. Akapata shaka.
Akaamua kurudi kwake kumkuta mamaye. Ndani ya dakika kadhaa akawa amefika mlangoni. Akabisha mlango usifunguliwe. Napo akausukuma pasipo mafanikio. Mlango ulikuwa umefungwa kwa komeo ndani.
Ikambidi afanye jitihada za makusudi kuzama ndani. Akauvunja mlango kwa teke zito kisha akajivuta kwenda kutazama kitandani. Kulikuwa kimya kana kwamba hamna kiumbe chochote humo. Ukimya huo ukamtisha zaidi Darren.
Akajongea, na alipofika kitandani, akamwona mama yake katika hali ya kushangaza. Hakuwa mama tena, bali mwili tu! Tena mwili uliokauka kaukau na kubabukababuka kama ngozi ya kenge!
Darren akahisi kupoteza nguvu. Aakamshika mamaye ambaye haikuwa inaeleweka nini kimemtokea kisha akalia kwanguvu sana. Akalia kwanguvu sana!
Hakuwa anaamini kama mama yake amefariki. Ilikuwa ni kama miujiza mbele ya macho yake. Na ni kweli ni muujiza. Imekuaje? Amekufaje kwa namna hiyo ingawa alimwacha akiwa salama salmini?
Hata wakati gari la wagonjwa na polisi wanawasili, bado Darren alikuwa anadhani yu ndotoni. Kwa mujibu wa taarifa ya kiuchunguzi wa mwili, ikabainika kuwa Mama yake Darren, Sara, alikuwa amechomwa moto mpaka kufa. Lakini hakuna aliyekuwa anajua huo moto ulitokea wapi? Na nani aliyemchoma? Ilikuwa ni kitendawili mtu kuungua ndani ya nyumba peke yake huku kila kitu kikibaki salama!
Majirani hawakuwa na habari yoyote juu ya tukio hilo.
Na hata Polisi walishindwa kutoa majibu ya kueleweka.
Darren na baba yake, bwana Gerald, wakafanya taratibu za mazishi wakiridhia kuwa siku inayofuata Sarah azikwe kwa maana hafai kukaa zaidi. Basi kama hivyo walivyokubaliana, kesho yake wakawa wapo makaburini.
Mbele yao akasimama kiongozi wa dini pamoja pia na jeneza lililomhifadhi Sarah lakini Darren akiwa yupo mbali sana kimawazo. Kitu pekee alichoambulia toka kwenye kinywa cha kiongozi wa dini aliyekuwa amesimama mbele yao ilikuwa ni swala la moto tu.
“... hamna anayejua moto ulianzia upande upi wa msitu,” kiongozi wa dini alinena kwa msisitizo. “Watu walikuja kufahamu ukiwa tayari umetafuna karibia nusu na robo yake. Ukiwa unawaka kwa fujo mno, na madhara yake yakiwa makubwa! …”
Kutoka kwenye maongezi hayo, Darren akajifunza kuwa kumbe siku ile ambayo mama yake alifariki, ilitokea ajali kubwa ya moto huko California.
Kidogo akashangazwa na jambo hilo, lakini hakuhangaika nalo sana. Alikuwa ana vitu vingi vya kujadili kichwani mwake. Wakamzika mama na kisha wakarudi nyumbani. Huko ndo’ baba yake akamwambia, “Kuna kitu nataka tuzungumze.”
***
Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja mkuu.*UNA NINI LAKINI MELISSA? -- 02*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mama akatoa macho kwa mshangao. “Hapana!” akakanusha akitikisa kichwa. “Hapana, mpenzi. Ni hatari!”
“Huoni ni hatari akiendelea kutokujua?” Baba akauliza. Mama akatazama chini akiwa na sura ilonywea. Alikuwa anahofia.
Alikuwa anatakiwa kuhofia.
ENDELEA
Hakusema jambo mpaka pale Baba alipomshika bega na kumwambia kwa upole, “nikamwambie? Niruhusu nifanye hivyo!”
Mama akatikisa kichwa. “Hapana, Gerald. Si muda sahihi hivi sasa. Ni mapema sana. Tungoje kidogo tafadhali.”
Baba akamtazama asiseme jambo bali kushusha pumzi ndefu puani na kisha akajiendea zake ajiandae kuoga. Muda si mrefu, Darren akaaga anakwenda. Mama akamwomba sana ile picha ya Bibi lakini Darren akagoma kumpatia. Kwa kumpoza akamwambia kuwa atamrudishia kesho kutwa yake.
“Nakuahidi mama,” Darren akaapa kabla hajaenda zake. Alinyookea nyumbani kwake kisha akampigia simu Melissa akimwomba aje nyumbani kwake kwani kuna dharura.
Kama baada ya lisaa, Melissa akawa amefika hapo. Alikuwa amevalia topu nyeupe na jeans nyeusi. Alipendeza. Tuseme hata akivalia gunia mwanamke huyu hupendeza kutokana na umbo na uzuri wake.
Akamkumbatia Darren na kisha akamjulia hali kwa tabasamu pana. Lakini akafanikiwa kuona jambo usoni mwa Darren. Mwanaume huyo hakuwa sawa.
“Kuna tatizo Darren?” akauliza kwa sauti yake ya chini.
Darren ndipo akatoa picha ile, picha ya Bibi yake na wale wenza, na kumwonyeshea Melissa. “Melissa huyu ni wewe?”
Kwa mwanzoni Melissa akapigwa na butwaa. Mtu alikuwa akifanana naye vilivyo. Ilikuwa ni ajabu. Akachukua kama dakika mbili akitazama picha ile kisha akamuuliza Darren, “umetoa wapi picha hii?”
“Kwa Bibi yangu,” Darren akajibu. “Yule niliyekuambia kumhusu.”
“Yule marehemu?” Melissa akauliza upesi. Brian akatikisa kichwa. “ Ndiye huyo huyo!”
“Na yeye ni yupi kati ya hawa?”
“Huyu hapa!” Darren akaonyeshea kwa kidole. “Hapa ni mnamo miaka ya alfu moja mia tisa na hamsini!”
Melissa akaendelea kuitazama ile picha kana kwamba mtu anayekumbuka jambo. Darren akamuuliza, “Vipi Melissa? Umemtambua huyo mtu?”
Melissa akatikisa kichwa akiendelea kutazama ile picha alafu nwishowe akairejesha mikononi mwa Darren na kusema, “Anafanana na mimi sana!”
“Ndio! Hata mimi nilishangazwa sana ndiyo maana nikaibeba nije nikwonyeshe!”
Melissa akawa amenyamaza kimya. Macho yake yalionyesha yu mbali kifikra. Darren akamtazama na kumwita mara mbili kabla mwanamke huyo hajashtuka na swali, “Unaweza ukanipeleka huko kwa Bibi yako?”
“Amefariki!” Darren akamjibu akimtolea macho. “Au wataka kuona kaburi?”
“Twende hivyo hivyo!” Melissa akasihi. “Sidhani kama kutakuwa na shida, Darren!”
Darren akafikiri kidogo kisha akamwambia wataenda huko mwisho wa wiki kwani atabanwa na kazi hapa siku za usoni.
“Darren,” Melissa akaita akijitengenezea kumtazama mwanaume huyo. “Naomba, nipo chini ya miguu yako, tafuta siku ya karibuni. Mpaka mwisho mwingine wa wiki ni mbali sana!”
Darren akashangazwa na hitaji hilo la ghafla. “Melissa, ni haraka mno! Vipi kuhusu rat—”
“Tafadhali, Darren!” Melissa akanong’ona kwa huruma. Macho yake yalipoa na uso wake ukiwa kama ule wa mtoto aombapo kitu. Darren akashindwa kukataa. “Sawa, basi tufanye keshokutwa.”
“Kwanini sio kesho?” Melissa akauliza kwa upole. Darren akamtazama kwanza mwanamke huyo, alafu punde uso wake ukawa mgumu, “Melissa kwani kuna nini huko kitakachopotea tukikawia?”
“Darren, ungalikuwa wewe umefanana na mtu pichani hivi usingelipata hamu ya kujua?”
“Sawa,” Darren akalegea. “Tutaenda huko hiyo kesho.”
Basi baada ya hapo wakafanya mpango wa chakula, wakawasha pia na runinga watazame baadhi ya filamu. Wakachoma hapo masaa mpaka kiza kilipoingia. Wakala na kuendelea kutazama runinga wakiwa wanapeana mabusu na maneno matamu.
Usiku ulipokuwa mkubwa zaidi wakaenda kitandani, na kabla ya kulala ‘wakanyooshana migongo’. Wakachoka sana na basi usingizi ukawakwapua kwa upesi sana wasidumu hata lisaa.
Wakiwa wamelala, ni saa tisa ya usiku, ghafla Melissa anaamka na kuketi kitako kitandani. Kuna jambo linamtatiza kichwani. Anamtazama Darren, yu hoi hajielewi. Basi anatoka kitandani na kwenda kuifuata ile picha ya Bibi pale mezani.
Akaiteka kwa mikono yake membamba kisha akairejea kuitazama kwa macho yake makavu pamoja na kiza. Baada ya sekunde mbili, akasema kwa kunong’ona, “Tabitha … Cassandra … Bessie.!”
Akisema majina hayo akawa anamtazama mmoja baada ya mwingine. Punde akasikia Darren akijigeuza kitandani, upesi akatazama. Mwanaume huyo hakuwa ameamka. Bado alikuwa kwenye lindi kubwa la usingizi. Melissa akaachana naye na kuendelea kutazama ile picha, mwishowe akaiweka kifuani mwake akiwa na uso wa mawazo.
“Tabitha, nangoja jua lichomoze,” akasema hivyo na basi akarejea kitandani mwake na kulala.
Masaa yakazidi kusonga mpaka kufikia majira ya saa kumi na moja. Hapo Darren akashtuka toka usingizini na kuangaza. Alidhani pengine amekawia. Akafungua dirisha na kutazama nje, bado kiza. Basi kabla hajajirudisha kitandani akaenda chooni kwa haja ndogo.
Alipotoka huko, kama bahati tu, akajikuta macho yake yakiangukia mezani pale alipoacha picha yake. Akasonga karibu na kuitazama tena picha ile akitumia msaada wa taa ndogo ya mezani.
Akajikuta anatabasamu kumwona mtu mithili ya Melissa. Ila alipoitazama picha hiyo zaidi akagundua yule Melissa wa pichani alikuwa ana kovu dogo chini ya goti lake la kushoto. Aliweza kuona hivyo maana gauni lilikuwa limeishia magotini.
Basi kwa hamu ya kutaka kujua akamsogelea Melissa kitandani kisha akamtazama mguu wake wa kushoto. Hapo akaona kovu lile lile la kwenye picha! Ni kovu dogo ambalo hakupata hata kulijua kwa muda wote huo ambao amekuwa na Melissa kwenye mahusiano.
“Inawezekanaje?” akajiuliza. Akairejesha picha ile mezani kisha akazima taa na kurejea kitandani. Akalala nyuma ya mgongo wa Melissa aliyekuwa amelala kiubavu na kidogo akapitiwa na usingizi.
Ila hapo Melissa akafungua macho. Macho yake yalikuwa makavu tofauti na mtu atokaye usingizini. Melissa hakuwa amelala. Melissa alisikia na kuona kila kitu ambacho Darren ametoka kukifanya.
Hakufanya kitu na badala yake akalala. Asubuhi ya saa moja kamili wakaamka na kujiandaa kwa ajili ya safari. Kufikia saa tatu tayari wapo kwenye basi wakienda kijijini, countryside.
Walipopoteza masaa matatu barabarani wakafika kituoni. Wakatembea kwa ufupi kabla ya kufika kwenye nyumba kubwa ya Bibi. Hapo Melissa akasimama kuitazama nyumba hiyo kwa umakini. Naye Darren aliyekuwa ametangulia mbele ikamlazimu amrejelee, akatabasamu akimwambia, “Ndiyo hapa! … ni pazuri, sio?”
“Ndio, ni pazuri!” Melissa akajibu pasipo kumaanisha kwa uso wake, wakazama ndani. Humo akang’aza sana macho, ndani ya nyumba nzima na pia huko nje kana kwamba mtu anayetaka kununua akitaka kubaini madhaifu.
Walipokuwa nje, akamwomba Darren amwonyeshe kaburi la Bibi yake. Naye Darren pasipo ajizi, akampeleka magharibi ya mbali ya nyumba hiyo na kumwonyeshea, “Ndiyo hapa!”
Melissa akasoma kibao cha kaburi. Kilisomeka kwa jina la Cecilia Goodwin. Akauliza, “hili ndilo jina la bibi yako?”
“Ndio,” Darren akamjibu.
“Ahsante. Tunaweza tukarudi ndani.”
Wakarudi huko na Darren akampatia Melissa picha za Bibi yake. Kwa taratibu akazitazama moja baada ya nyingine.
“Sikumwona mtu huyo tena,” alisema Darren. “Yupo kwenye picha moja tu.”
Melissa asiseme kitu akaendelea kukagua picha zile. Alipomaliza akamkabidhi Darren na kisha akalaza kichwa chake kochini. Darren akazirejesha picha hizo na kisha kujumuika na Melissa hapo sebuleni.
Usiku ulipowadia, Melissa akamnong’oneza Darren kwenye sikio lake la kulia, “Nakuhitaji mpenzi.”
Darren akamtazama mwanamke huyo kwa kukodoa, “Melissa, tumefanya jana tu!”
Melissa akang’ata lips zake na kulegeza macho. “Kwani kuna ubaya, mpenzi?” akauliza akiweka kiganja chake kifuani mwa Darren.
“Hamna ubaya ila si kawaida yako.”
Melissa akatabasamu. Akafungua kifungo kimoja cha shati la Darren. “Sasa nitafanya nini na ingali u karibu yangu, tena tukiwa wapweke wenye nafasi?” akateta kwa sauti ya puani.
Darren asijibu, mwanamke huyo akaanza kubusu kifua chake na hatimaye akatimiza adhma yake. Darren akawa hoi kana kwamba amelima ekari za mbaazi. Hata alipojilaza hapo kochini akawa kama mfu!
Basi Melissa akajivalia nguoze na kisha akaelekea stoo. Huko akateka chepe na kutoka ndani ya nyumba kisha akaelekea moja kwa moja kule mashariki ya mbali kukuta kaburi la Cecilia Goodwin, bibi yake Darren.
Hapo kabla hajafanya chochote akaita kwa kunong’oneza, “Tabitha!”
Kisha akaanza kuchimba kaburi.
**
Sent using Jamii Forums mobile app
Nawe pia Tumosa[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] barikiwa Steve
[emoji120] [emoji120] [emoji120]
Asante steve[emoji120][emoji120]
Ila chunga usisome mwenyewe. [emoji4] [emoji4]Asante steve[emoji120][emoji120]
Hapa natamani utupie nyingine[emoji23]