Riwaya: Una nini Melissa?

Riwaya: Una nini Melissa?

*UNA NINI LAKINI MELISSA? ---- 05*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

“Unadhani nani kaichukua?” Mama akauliza akitoa macho. Darren akajibu, “Melissa. Nadhani kaichukua Melissa!”

Basi upesi Mama akamdaka mkono na kumwambia, “twende huko upesi!”

ENDELEA

Darren hakuwahi kumwona mama yake kwenye hali hiyo na tangu alipowahi kumwambia juu ya Melissa, uzuri na uchangamfu wake, mama hakuwahi kuguswa kiasi cha kutaka kumwona Melissa. Lakini mbona hili la picha? Akapigwa na butwaa.

Mama yake alimkokota mpaka nje mbele ya gari la baba yake, akamweka ndani na kuwasha chombo kabla hajakanyagia mafuta pasipo kujali! Gari likapepea kama kishada kutafuta makazi ya Melissa!

Ndani ya muda mfupi wakaja jikuta wapo kwenye foleni ndefu. Mama akakasirika akipiga usukani kwanguvu. Darren akaendelea kutahamaki.

“Mama, una nini?”

“Darren, kwanini ulimpa Melissa ile picha?” Mama akafoka. Macho yake yalikuwa mekundu kana kwamba kitambaa.

“Sikumpatia,” Darren akajitetea, “Nilitahamaki haipo kwenye begi langu na si vinginevyo!” Lakini Mama bado akamwona ni mjinga. “Darren, nilikuambia nini kuhusu ile picha mara ya kwanza nilipokuona nayo?”

“Najua, nakumbuka. Sijafanya kwa kudhamiria. Tafadhali!”

Mama akalaza kichwa chake kwenye kiti akitema hewa ndefu.

“Mama,” Darren akaita. “Kwani picha ile ina nini? Naomba uniambie kwanini umekuchanganya namna hii?”

Mama hakumjibu, alikuwa anatazama magari meengi yaliyokuwa yamesimama mbele yake akitamani ayatafune au ayakanyage kwa juu aende zake. Akiwa anatazama, akajikuta chozi linamtoka kwenye jicho la kulia. Akalipangusa na kuvuta kamasi jepesi puani.

“Mama!” Darren akaita kwa sauti kuu. “Kwanini hutaki kunambia? Kwanini unaninyamazia? Hunisikii?”

Mama akamtazama kana kwamba mbogo aliyejeruhiwa na kisha hakusema kitu. Macho yake yangekufanya usikie njaa hata kama umetoka kula. Yangekufanya utafute mlango wa kutokea kama ni mgeni. Na kama basi ni mtoto angelia pasi na kifani. Hata Darren aliogopa. Hajawahi kumwona mama yake akiwa anatisha vile tangu amepata ufahamu kama mtu mzima!

Magari yakaruhusiwa kwenda, na mama akatia chombo moto. Akaendesha upesi kumchukua dakika nane tu kufika mbele ya makazi anayokaa Melissa. Hapo wakapanda ngazi upesi na punde wakawa wapo mlangoni wakigonga.

“Melissa!” mama aliita lakini kulikuwa kimya. Na akiwa hapo akahisi harufu ya yale majani ambayo Melissa aliyachoma kwenye kibakuli. Akachanganyikiwa. “Melissaaa!” akaita akibamiza mlango makofi, lakini bado kulikuwa kimya. Kimya baridi. Basi Mama akamwamuru Darren avunje mlango huo wapate kuingia ndani.

“Mama, upo sawa kweli?” Darren akatoa macho. Mama akarudia kumwambia, “Vunja mlango Darren!” kisha na kuongezea, “Au nivunje mimi?”

Lakini Darren bado alisita kufanya hivyo. “Mama, tutaitwa wezi. Tutavunjaje mlango wa mtu ambaye hayupo!”

“Vunja, Darreeen!” Mama akafoka akitoa macho kana kwamba simba. Basi Darren akaupiga mlango huo kumbo la nguvu, nao ukavunjika wakazama ndani! Mama akatazama kushoto na kulia, kulia na kushoto. Melissa hakuwapo! Wala nayo picha haikuwa mahali panapoonekana.

Walichoambulia kuona ilikuwa ni kile kibakuli cheupe cha udongo ambacho Melissa alichomea majani na marker pen nyekundu. Lakini Mama akawa amejua kilichotokea. Aliidaka marker pen ile na kuitazama vema kana kwamba anatafuta jambo kwenye ramani, kisha akasema kwa sauti ya chini, “Darren, tumekawia.”

“Tumekawia na nini?” Darren akawahi kuuliza.

Mama akamwambia kana kwamba bibi anayesimulia simulizi wajukuuze, “Wanaamshwa tena, Darren!” akasema akitazama dari. “Watakapoamka tena, wote hao, hatutakuwa na uwezo wa kuwazuia tena.”

Alafu ghafla akamtazama Darren na kumkwida shati lake. “Darren, si kwamba watachukua tu nyumba yetu, bali wataiteka dunia nzima. Darren inabidi tuwazuie. Tuwazuie haraka iwezekanavyo!”

Na alipomaliza kusema hayo akadondoka chini na kuzirai!

“Mama! Mamaa!” Darren akasumbuka naye. Akampepea na kumpepea lakini haikusaidia, mama hakuwa na fahamu hata lepe! Basi akambeba na kurupukurupu mpaka chini kwenye gari. Akampakia ndani na kisha akarejea tena kule juu kwa Melissa. Akaurudishia mlango baada ya kutazama kuwa kila kitu kii chema alafu akamrejea mama yake na kumwendesha kumpeleka nyumbani.

Akiwa njiani, akajaribu tena kumpigia Melissa. Hakuwa anapatikana! Akang’ata meno yake kwanguvu akinguruma. “Upo wapi Melissa? Upo wapii?”

Alimfikisha mama yake nyumbani. Akamlaza kitandani akijaribu kumpepea na kuhakikisha kuna hewa ya kutosha ndani. Baada ya muda kidogo, Mama akaamka kichwa kikiwa kinauma. Akamtazama Darren wake kwa macho ya upole na pasipo kusema kitu akatabasamu kwa mbali.

“Mama,” Darren akaita akiweka kiganja chake kwenye paji la uso la mama yake, kisha akawa anamtengenezea nywele. “Unajisikiaje hivi sasa?”

“Vizuri,” mama akasema kwa kunong’ona.

“Mama, unaweza ku--” kabla hajamalizia nayo simu yake ikaita. Alikuwa ni Melissa.

“Ni Melissa huyo?” Mama akauliza. Darren akamtazama na kumlaghai, “Hapana.” kisha akatoka kwenda kando aongee kwa uhuru.

“Melissa,” akaita kwa kunong’ona kisha akauliza, “Upo wapi?”

“Nipo kwako,” Melissa akamjibu.

“Unafanya nini huko na mimi sipo?”

“Nimekuja kukutazama wewe, Darren. Unaweza kuja hivi sasa?”

Darren kabla hajajibu, akageuka atazame ndani. Hamaki akakutana uso kwa uso na mama yake! Akashtuka kiasi cha moyo wake kutaka kutoka nje.

“Darren,” Mama akasema kwa sauti ya chini, lakini kwa namna alivyokuwa anamtazama Darren ni kana kwamba simba awindaye kwa kunyata. Akasema, “Tunaenda wote huko, Darren.”

“Wapi?” Darren akauliza kana kwamba hajui kinachoendelea. Mama akamjibu, “Huko aliko Melissa!”

“Sijaongea na Melissa mama,” Darren akadanganya na kuapa lakini mama akabaki akimtazama asiseme jambo la nyongeza.

“Kweli, sijaongea naye mama. Naomba tafadhali upumzike. Nakuja muda si mrefu.”

Kimya.

“Mama, mbona unanitazama hivyo?”

Kimya.

“Mama, una shida gani? Mbona upo hivyo?”

Kimya. Mama aliendelea kumtazama Darren kwa macho ya kwenye kona. Mwishowe Darren akaanza kuhisi moyo wake unapiga kwa kasi. Alianza kuogopa. Basi akaona ni kheri akaongozana na mamaye huko kwake.

Wakashuka na kujipaki kwenye gari alafu moja kwa moja wakaelekea huko. Walitumia kama dakika ishirini na nane barabarani. Walipofika na kufungua mlango, hawakumkuta yeyote. Chumba kilikuwa kitupu!

Darren akampigia simu Melissa, na kidogo simu ikapokelewa.

“Upo wapi, Melissa?”

“Darren …” Melissa akaita na kusema, “Nilikuita wewe, na si familia nzima.”

Darren akatazama nje ya dirisha lake kama atamwona Melissa. “Upo wapi?” akauliza akiangazaangaza.

“Utakapokuwa mwenyewe, nitakuambia,” Melissa akamjibu, na kabla hajatia neno, mama yake akampokonya simu na kuongea na Melissa.

“Binti wa shetani, popote utakapokuwa, nitakutafuta na kukumaliza. Kwa nguvu na akili yangu yote, kwa udi na uvumba, nitakutia mikononi na kukuangamiza.

Hauna nafasi tena kwenye dunia hii. Na kama walivyoenda wenzako na wewe utaenda vivyo hivyo. Sitabakiza hata unywele wako kwenye uso wa dunia. Mifupa yako nitaivunjavunja kutengenezea unga wa sigara na meno yako nitayatengenezea mkufu nikauvae shingoni mwangu.”

Alipomaliza, akakata simu na kumpatia Darren. Alafu ghafla akadondoka na kuzirai tena. Kabla Darren hajahangaika naye, akaita kwa sauti ya chini, “Mama.” kisha na kusema, “Wewe ni nani? … Melissa …” akatazama simu yake na kuuliza tena, “wewe ni nani?”


**

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*UNA NINI LAKINI MELISSA? --- 06*

*Simulizi za series*


ILIPOSHIA

Alipomaliza, akakata simu na kumpatia Darren. Alafu ghafla akadondoka na kuzirai tena. Kabla Darren hajahangaika naye, akaita kwa sauti ya chini, “Mama.” kisha na kusema, “Wewe ni nani? … Melissa …” akatazama simu yake na kuuliza tena, “wewe ni nani?”

ENDELEA

Alishinwa kupata majibu. Alijikuta kwenye maswali ya mkanganyiko juu ya mama yake na Melissa. Wana nini kati yao? Wana nini ambacho hakijui? Wana nini ambacho wanamficha?

Akaketi kitandani akiwaza na kuwazua. Hata alipompigia Melissa hakupokea bali tu akituma ujumbe kuwa wataongea punde atakapokuwa peke yake. Mwishowe akaamua kuzima simu akidhamiria kutomtafuta tena Melissa.

Akambeba mama yake na kumweka kitandani. Alafu akafungua madirisha apate hewa wakati akiangalia kuandaa mengine. Alipomaliza kila kitu, akajilaza kitandani akiwaza sana. Mwishowe usingizi ukambeba.

Kidogo akiwa usingizini, akasikia hodi mlangoni. Akafumbua macho yake kwa uvivu akitazama mlango. Kidogo akajikusanya kitandani na kusogea karibu akiuliza ni nani anayegonga. Hakujibiwa. Alipoufungua akamwona mwanaume fulani mwenye mwili mpana akiwa amevalia koti la sufi na shati jepesi kwa ndani. Mwanaume huyo shingoni alikuwa amechora ‘tattoo’. Na uso wake mpana ulikuwa na kovu kwenye fuvu la shavu la kushoto. Macho yake yalikuwa madogo yaliyozama ndani, ila aliyakodoa.

Akauliza kwa sauti kavu, “Wewe ni Darren?” Darren akatikisa kichwa. “Naweza kukusaidia?”

Bwana yule hakujibu, badala yake akatazama ndani na kisha akarudisha macho yake kwenye uso wa Darren. Mara akamsukumia kando na kuzama ndani pasi na ruhusa.

“Hey!” Darren akapaza, “Unataka nini?” lakini bwana yule hakumjali, akiwa anasonga kwa hatua nzito, akawa anamuelekea Sarah, mama yake Darren.

Basi Darren upesi akaamka na kumkimbilia. Akamrukia mgongoni na kumkaba lakini hakuwa na nguvu ya kushindana na mtu huyo. Kwa kutumia mkono mmoja akanyofolewa mgongoni na kutupiwa ukutani. Alijibamiza sana kichwani kiasi cha kupoteza uwezo wa kujimudu kusimama tena, basi kwa mbali akawa anatazama kinachoendelea akiwa hana msaada wowote.

Bwana yule akamfuata mama yake na kwa kutumia mikono yake mipana akamkaba koo na kumminya kwanguvu. Akamminya sana. Darren akanyoosha mkono wake wa kuume akitaka kumsaidia mama yake. Akaita kwa kunong’ona. Lakini hayo yote hayakuwa na msaada. Hakuwa anajiweza.

Mbele ya macho yake bwana yule akammaliza mama yake na kisha akaondoka zake. Darren akatiririsha chozi akinong’ona, “Mama … mama … mama.”

Mara akasikia sauti ya kunong’ona, “Nipo hapa mwanangu.”

Alipotazama kushoto kwake ndipo akagundua kuwa mama yake alikuwa ameketi hapo. Alikuwa ameshaamka toka kwenye usingizi wa kukosa fahamu na kumbe yeye alikuwako usingizi akiona hayo yote!

Akamkumbatia mama yake kwanguvu akisema, “Mama, upo hai!” mama yake akamdaka kichwa na kumpapasa. “Nipo hai mwanangu. Nani alikuambia nimekufa?” akasema kwa tabasamu.

Darren akamtazama mama yake, na kabla hajasema jambo, wakasikia hodi mlangoni. Darren akashtuka sana. Akamtazama mama yake kwa kukodoa na kumwambia, “Jifiche!”

“Kwanini?” Mama akashangaa. Darren hakumpa maelezo zaidi badala yake akamsisitizia ajifiche wakati yeye akiwa anatafuta silaha. Alipopata kipande cha nondo akauendea mlango. Na kabla hajaufungua, akamsisitizia tena mama yake ajifiche. Mama hakuwa anajua kinachoendelea, akabaki akiduwaa.

“Nani?” Darren akauliza mlangoni. Kimya. Akauliza tena, “Nani?” mara hii sauti yake ikiwa na amri ndani. Mara akajibiwa na sauti ya kike, “Ni mimi!” basi akadhani ni Melissa. Akafungua mlango, uso kwa uso akakutana na jirani yake; mdada mrefu mwembamba aliyening’iniza headphone shingoni, kichwa chake amekifunika na kofia ya soksi nzito.

“Hey, Darren!”

“Hey, Rosetta. Mambo?” Darren akasalimu akificha mkono wake wenye nondo nyuma.

“Safi. Samahani kwa usumbufu, Darren. Nina ujumbe wako.” Rosetta aliposema hayo akachomeka mkono wake mfukoni na kutoa kikaratasi cheupe alichomkabidhi Darren na kumwambia, “Ni kutoka kwa Melissa!”

“Yuko wapi?” Darren akawahi kuuliza.

“Ameshaondoka,” Rosetta akajibu na kuongezea, “Nilimkuta chini. Aliponiona akanipatia na kisha yeye akaondoka zake mara moja.”

“Sawa, ahsante,” Darren akafunga mlango na kufungua ujumbe ule aliokabidhiwa. Ulikuwa ni wa ishara na hakuelewa jambo. Ni alama mbalimbali ambazo alihisi anaumwa na kichwa kuzichambua.

Akampatia ujumbe huo mama yake na kumuuliza kama kuna chochote anaweza kuambulia. “Umetoka kwa Melissa.”

Mama akatazama lakini naye hakupata kitu, ila alihisi kuna jambo. Na jambo hilo si zuri! Akamwambia Darren, “Mtafute Melissa!” naye Darren akatumia simu yake kupiga, hakuwa anapatikana. Ndipo akamshauri mama yake, “Acha niende kwake mwenyewe. Pengine ntaonana naye kuliko tunavyoongozana kila muda.”

Kwa kishingo upande, mama akaridhia. Basi Darren akashuka chini akimwacha mama yake ndani. Akakwea usafiri na kwenda moja kwa moja kwenye makazi ya Melissa.

Aliposhuka toka kwenye gari akaangaza mazingira alafu taratibu akiwa amedumbukiza mkono wake wa kuume mfukoni, akajongea. Kichwani akiwa anamuwazia Melissa. Akaapa kuwa akimkuta mwanamke huyo basi ni lazima amwambie kinachoendelea. Hatomwacha mpaka amweleze hayo. Amechoka kuzungushwa sasa.

Kama baada ya dakika tano akawa mlangoni mwa chumba cha Melissa. Akaukuta wazi. Akausogeza na kuzama ndani. Kila kitu kilikuwa sawa ila chumba kilikuwa kitupu. Hamna mtu!

Akaita akikagua lakini napo hakukuwa na jambo. Akaduwaa. Akampigia simu Melissa lakini napo haikuwa inapatikana, sasa akachoka kabisa, akajitupia kitandani.

Akangoja hapo kwa masaa lakini Melissa asionekane. Akajigeuza huku na kule, kule na huku. Akapiga simu na kutuma ujumbe, bado hamna kitu! Mpaka inafika saa nne usiku alikuwa kapa.

Basi akaona ni stara alale hapo, ili Melissa akirudi amkutie hapo. Lakini kabla hajafanya hivyo, akaona amtaarifu mama yake juu ya uamuzi huo. Akampigia simu. Nayo ikaita pasipo kupokelewa. Akapiga mara sita, majibu yakawa yaleyale. Akapata shaka.

Akaamua kurudi kwake kumkuta mamaye. Ndani ya dakika kadhaa akawa amefika mlangoni. Akabisha mlango usifunguliwe. Napo akausukuma pasipo mafanikio. Mlango ulikuwa umefungwa kwa komeo ndani.

Ikambidi afanye jitihada za makusudi kuzama ndani. Akauvunja mlango kwa teke zito kisha akajivuta kwenda kutazama kitandani. Kulikuwa kimya kana kwamba hamna kiumbe chochote humo. Ukimya huo ukamtisha zaidi Darren.

Akajongea, na alipofika kitandani, akamwona mama yake katika hali ya kushangaza. Hakuwa mama tena, bali mwili tu! Tena mwili uliokauka kaukau na kubabukababuka kama ngozi ya kenge!

Darren akahisi kupoteza nguvu. Aakamshika mamaye ambaye haikuwa inaeleweka nini kimemtokea kisha akalia kwanguvu sana. Akalia kwanguvu sana!

Hakuwa anaamini kama mama yake amefariki. Ilikuwa ni kama miujiza mbele ya macho yake. Na ni kweli ni muujiza. Imekuaje? Amekufaje kwa namna hiyo ingawa alimwacha akiwa salama salmini?

Hata wakati gari la wagonjwa na polisi wanawasili, bado Darren alikuwa anadhani yu ndotoni. Kwa mujibu wa taarifa ya kiuchunguzi wa mwili, ikabainika kuwa Mama yake Darren, Sara, alikuwa amechomwa moto mpaka kufa. Lakini hakuna aliyekuwa anajua huo moto ulitokea wapi? Na nani aliyemchoma? Ilikuwa ni kitendawili mtu kuungua ndani ya nyumba peke yake huku kila kitu kikibaki salama!

Majirani hawakuwa na habari yoyote juu ya tukio hilo.
Na hata Polisi walishindwa kutoa majibu ya kueleweka.

Darren na baba yake, bwana Gerald, wakafanya taratibu za mazishi wakiridhia kuwa siku inayofuata Sarah azikwe kwa maana hafai kukaa zaidi. Basi kama hivyo walivyokubaliana, kesho yake wakawa wapo makaburini.

Mbele yao akasimama kiongozi wa dini pamoja pia na jeneza lililomhifadhi Sarah lakini Darren akiwa yupo mbali sana kimawazo. Kitu pekee alichoambulia toka kwenye kinywa cha kiongozi wa dini aliyekuwa amesimama mbele yao ilikuwa ni swala la moto tu.

“... hamna anayejua moto ulianzia upande upi wa msitu,” kiongozi wa dini alinena kwa msisitizo. “Watu walikuja kufahamu ukiwa tayari umetafuna karibia nusu na robo yake. Ukiwa unawaka kwa fujo mno, na madhara yake yakiwa makubwa! …”

Kutoka kwenye maongezi hayo, Darren akajifunza kuwa kumbe siku ile ambayo mama yake alifariki, ilitokea ajali kubwa ya moto huko California.

Kidogo akashangazwa na jambo hilo, lakini hakuhangaika nalo sana. Alikuwa ana vitu vingi vya kujadili kichwani mwake. Wakamzika mama na kisha wakarudi nyumbani. Huko ndo’ baba yake akamwambia, “Kuna kitu nataka tuzungumze.”


***

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*UNA NINI LAKINI MELISSA? --- 06*

*Simulizi za series*


ILIPOSHIA

Alipomaliza, akakata simu na kumpatia Darren. Alafu ghafla akadondoka na kuzirai tena. Kabla Darren hajahangaika naye, akaita kwa sauti ya chini, “Mama.” kisha na kusema, “Wewe ni nani? … Melissa …” akatazama simu yake na kuuliza tena, “wewe ni nani?”

ENDELEA

Alishinwa kupata majibu. Alijikuta kwenye maswali ya mkanganyiko juu ya mama yake na Melissa. Wana nini kati yao? Wana nini ambacho hakijui? Wana nini ambacho wanamficha?

Akaketi kitandani akiwaza na kuwazua. Hata alipompigia Melissa hakupokea bali tu akituma ujumbe kuwa wataongea punde atakapokuwa peke yake. Mwishowe akaamua kuzima simu akidhamiria kutomtafuta tena Melissa.

Akambeba mama yake na kumweka kitandani. Alafu akafungua madirisha apate hewa wakati akiangalia kuandaa mengine. Alipomaliza kila kitu, akajilaza kitandani akiwaza sana. Mwishowe usingizi ukambeba.

Kidogo akiwa usingizini, akasikia hodi mlangoni. Akafumbua macho yake kwa uvivu akitazama mlango. Kidogo akajikusanya kitandani na kusogea karibu akiuliza ni nani anayegonga. Hakujibiwa. Alipoufungua akamwona mwanaume fulani mwenye mwili mpana akiwa amevalia koti la sufi na shati jepesi kwa ndani. Mwanaume huyo shingoni alikuwa amechora ‘tattoo’. Na uso wake mpana ulikuwa na kovu kwenye fuvu la shavu la kushoto. Macho yake yalikuwa madogo yaliyozama ndani, ila aliyakodoa.

Akauliza kwa sauti kavu, “Wewe ni Darren?” Darren akatikisa kichwa. “Naweza kukusaidia?”

Bwana yule hakujibu, badala yake akatazama ndani na kisha akarudisha macho yake kwenye uso wa Darren. Mara akamsukumia kando na kuzama ndani pasi na ruhusa.

“Hey!” Darren akapaza, “Unataka nini?” lakini bwana yule hakumjali, akiwa anasonga kwa hatua nzito, akawa anamuelekea Sarah, mama yake Darren.

Basi Darren upesi akaamka na kumkimbilia. Akamrukia mgongoni na kumkaba lakini hakuwa na nguvu ya kushindana na mtu huyo. Kwa kutumia mkono mmoja akanyofolewa mgongoni na kutupiwa ukutani. Alijibamiza sana kichwani kiasi cha kupoteza uwezo wa kujimudu kusimama tena, basi kwa mbali akawa anatazama kinachoendelea akiwa hana msaada wowote.

Bwana yule akamfuata mama yake na kwa kutumia mikono yake mipana akamkaba koo na kumminya kwanguvu. Akamminya sana. Darren akanyoosha mkono wake wa kuume akitaka kumsaidia mama yake. Akaita kwa kunong’ona. Lakini hayo yote hayakuwa na msaada. Hakuwa anajiweza.

Mbele ya macho yake bwana yule akammaliza mama yake na kisha akaondoka zake. Darren akatiririsha chozi akinong’ona, “Mama … mama … mama.”

Mara akasikia sauti ya kunong’ona, “Nipo hapa mwanangu.”

Alipotazama kushoto kwake ndipo akagundua kuwa mama yake alikuwa ameketi hapo. Alikuwa ameshaamka toka kwenye usingizi wa kukosa fahamu na kumbe yeye alikuwako usingizi akiona hayo yote!

Akamkumbatia mama yake kwanguvu akisema, “Mama, upo hai!” mama yake akamdaka kichwa na kumpapasa. “Nipo hai mwanangu. Nani alikuambia nimekufa?” akasema kwa tabasamu.

Darren akamtazama mama yake, na kabla hajasema jambo, wakasikia hodi mlangoni. Darren akashtuka sana. Akamtazama mama yake kwa kukodoa na kumwambia, “Jifiche!”

“Kwanini?” Mama akashangaa. Darren hakumpa maelezo zaidi badala yake akamsisitizia ajifiche wakati yeye akiwa anatafuta silaha. Alipopata kipande cha nondo akauendea mlango. Na kabla hajaufungua, akamsisitizia tena mama yake ajifiche. Mama hakuwa anajua kinachoendelea, akabaki akiduwaa.

“Nani?” Darren akauliza mlangoni. Kimya. Akauliza tena, “Nani?” mara hii sauti yake ikiwa na amri ndani. Mara akajibiwa na sauti ya kike, “Ni mimi!” basi akadhani ni Melissa. Akafungua mlango, uso kwa uso akakutana na jirani yake; mdada mrefu mwembamba aliyening’iniza headphone shingoni, kichwa chake amekifunika na kofia ya soksi nzito.

“Hey, Darren!”

“Hey, Rosetta. Mambo?” Darren akasalimu akificha mkono wake wenye nondo nyuma.

“Safi. Samahani kwa usumbufu, Darren. Nina ujumbe wako.” Rosetta aliposema hayo akachomeka mkono wake mfukoni na kutoa kikaratasi cheupe alichomkabidhi Darren na kumwambia, “Ni kutoka kwa Melissa!”

“Yuko wapi?” Darren akawahi kuuliza.

“Ameshaondoka,” Rosetta akajibu na kuongezea, “Nilimkuta chini. Aliponiona akanipatia na kisha yeye akaondoka zake mara moja.”

“Sawa, ahsante,” Darren akafunga mlango na kufungua ujumbe ule aliokabidhiwa. Ulikuwa ni wa ishara na hakuelewa jambo. Ni alama mbalimbali ambazo alihisi anaumwa na kichwa kuzichambua.

Akampatia ujumbe huo mama yake na kumuuliza kama kuna chochote anaweza kuambulia. “Umetoka kwa Melissa.”

Mama akatazama lakini naye hakupata kitu, ila alihisi kuna jambo. Na jambo hilo si zuri! Akamwambia Darren, “Mtafute Melissa!” naye Darren akatumia simu yake kupiga, hakuwa anapatikana. Ndipo akamshauri mama yake, “Acha niende kwake mwenyewe. Pengine ntaonana naye kuliko tunavyoongozana kila muda.”

Kwa kishingo upande, mama akaridhia. Basi Darren akashuka chini akimwacha mama yake ndani. Akakwea usafiri na kwenda moja kwa moja kwenye makazi ya Melissa.

Aliposhuka toka kwenye gari akaangaza mazingira alafu taratibu akiwa amedumbukiza mkono wake wa kuume mfukoni, akajongea. Kichwani akiwa anamuwazia Melissa. Akaapa kuwa akimkuta mwanamke huyo basi ni lazima amwambie kinachoendelea. Hatomwacha mpaka amweleze hayo. Amechoka kuzungushwa sasa.

Kama baada ya dakika tano akawa mlangoni mwa chumba cha Melissa. Akaukuta wazi. Akausogeza na kuzama ndani. Kila kitu kilikuwa sawa ila chumba kilikuwa kitupu. Hamna mtu!

Akaita akikagua lakini napo hakukuwa na jambo. Akaduwaa. Akampigia simu Melissa lakini napo haikuwa inapatikana, sasa akachoka kabisa, akajitupia kitandani.

Akangoja hapo kwa masaa lakini Melissa asionekane. Akajigeuza huku na kule, kule na huku. Akapiga simu na kutuma ujumbe, bado hamna kitu! Mpaka inafika saa nne usiku alikuwa kapa.

Basi akaona ni stara alale hapo, ili Melissa akirudi amkutie hapo. Lakini kabla hajafanya hivyo, akaona amtaarifu mama yake juu ya uamuzi huo. Akampigia simu. Nayo ikaita pasipo kupokelewa. Akapiga mara sita, majibu yakawa yaleyale. Akapata shaka.

Akaamua kurudi kwake kumkuta mamaye. Ndani ya dakika kadhaa akawa amefika mlangoni. Akabisha mlango usifunguliwe. Napo akausukuma pasipo mafanikio. Mlango ulikuwa umefungwa kwa komeo ndani.

Ikambidi afanye jitihada za makusudi kuzama ndani. Akauvunja mlango kwa teke zito kisha akajivuta kwenda kutazama kitandani. Kulikuwa kimya kana kwamba hamna kiumbe chochote humo. Ukimya huo ukamtisha zaidi Darren.

Akajongea, na alipofika kitandani, akamwona mama yake katika hali ya kushangaza. Hakuwa mama tena, bali mwili tu! Tena mwili uliokauka kaukau na kubabukababuka kama ngozi ya kenge!

Darren akahisi kupoteza nguvu. Aakamshika mamaye ambaye haikuwa inaeleweka nini kimemtokea kisha akalia kwanguvu sana. Akalia kwanguvu sana!

Hakuwa anaamini kama mama yake amefariki. Ilikuwa ni kama miujiza mbele ya macho yake. Na ni kweli ni muujiza. Imekuaje? Amekufaje kwa namna hiyo ingawa alimwacha akiwa salama salmini?

Hata wakati gari la wagonjwa na polisi wanawasili, bado Darren alikuwa anadhani yu ndotoni. Kwa mujibu wa taarifa ya kiuchunguzi wa mwili, ikabainika kuwa Mama yake Darren, Sara, alikuwa amechomwa moto mpaka kufa. Lakini hakuna aliyekuwa anajua huo moto ulitokea wapi? Na nani aliyemchoma? Ilikuwa ni kitendawili mtu kuungua ndani ya nyumba peke yake huku kila kitu kikibaki salama!

Majirani hawakuwa na habari yoyote juu ya tukio hilo.
Na hata Polisi walishindwa kutoa majibu ya kueleweka.

Darren na baba yake, bwana Gerald, wakafanya taratibu za mazishi wakiridhia kuwa siku inayofuata Sarah azikwe kwa maana hafai kukaa zaidi. Basi kama hivyo walivyokubaliana, kesho yake wakawa wapo makaburini.

Mbele yao akasimama kiongozi wa dini pamoja pia na jeneza lililomhifadhi Sarah lakini Darren akiwa yupo mbali sana kimawazo. Kitu pekee alichoambulia toka kwenye kinywa cha kiongozi wa dini aliyekuwa amesimama mbele yao ilikuwa ni swala la moto tu.

“... hamna anayejua moto ulianzia upande upi wa msitu,” kiongozi wa dini alinena kwa msisitizo. “Watu walikuja kufahamu ukiwa tayari umetafuna karibia nusu na robo yake. Ukiwa unawaka kwa fujo mno, na madhara yake yakiwa makubwa! …”

Kutoka kwenye maongezi hayo, Darren akajifunza kuwa kumbe siku ile ambayo mama yake alifariki, ilitokea ajali kubwa ya moto huko California.

Kidogo akashangazwa na jambo hilo, lakini hakuhangaika nalo sana. Alikuwa ana vitu vingi vya kujadili kichwani mwake. Wakamzika mama na kisha wakarudi nyumbani. Huko ndo’ baba yake akamwambia, “Kuna kitu nataka tuzungumze.”


***

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] barikiwa Steve
 
*UNA NINI LAKINI MELISSA? -- 02*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Mama akatoa macho kwa mshangao. “Hapana!” akakanusha akitikisa kichwa. “Hapana, mpenzi. Ni hatari!”

“Huoni ni hatari akiendelea kutokujua?” Baba akauliza. Mama akatazama chini akiwa na sura ilonywea. Alikuwa anahofia.

Alikuwa anatakiwa kuhofia.

ENDELEA
Hakusema jambo mpaka pale Baba alipomshika bega na kumwambia kwa upole, “nikamwambie? Niruhusu nifanye hivyo!”
Mama akatikisa kichwa. “Hapana, Gerald. Si muda sahihi hivi sasa. Ni mapema sana. Tungoje kidogo tafadhali.”
Baba akamtazama asiseme jambo bali kushusha pumzi ndefu puani na kisha akajiendea zake ajiandae kuoga. Muda si mrefu, Darren akaaga anakwenda. Mama akamwomba sana ile picha ya Bibi lakini Darren akagoma kumpatia. Kwa kumpoza akamwambia kuwa atamrudishia kesho kutwa yake.
“Nakuahidi mama,” Darren akaapa kabla hajaenda zake. Alinyookea nyumbani kwake kisha akampigia simu Melissa akimwomba aje nyumbani kwake kwani kuna dharura.
Kama baada ya lisaa, Melissa akawa amefika hapo. Alikuwa amevalia topu nyeupe na jeans nyeusi. Alipendeza. Tuseme hata akivalia gunia mwanamke huyu hupendeza kutokana na umbo na uzuri wake.
Akamkumbatia Darren na kisha akamjulia hali kwa tabasamu pana. Lakini akafanikiwa kuona jambo usoni mwa Darren. Mwanaume huyo hakuwa sawa.
“Kuna tatizo Darren?” akauliza kwa sauti yake ya chini.
Darren ndipo akatoa picha ile, picha ya Bibi yake na wale wenza, na kumwonyeshea Melissa. “Melissa huyu ni wewe?”
Kwa mwanzoni Melissa akapigwa na butwaa. Mtu alikuwa akifanana naye vilivyo. Ilikuwa ni ajabu. Akachukua kama dakika mbili akitazama picha ile kisha akamuuliza Darren, “umetoa wapi picha hii?”
“Kwa Bibi yangu,” Darren akajibu. “Yule niliyekuambia kumhusu.”
“Yule marehemu?” Melissa akauliza upesi. Brian akatikisa kichwa. “ Ndiye huyo huyo!”
“Na yeye ni yupi kati ya hawa?”
“Huyu hapa!” Darren akaonyeshea kwa kidole. “Hapa ni mnamo miaka ya alfu moja mia tisa na hamsini!”
Melissa akaendelea kuitazama ile picha kana kwamba mtu anayekumbuka jambo. Darren akamuuliza, “Vipi Melissa? Umemtambua huyo mtu?”
Melissa akatikisa kichwa akiendelea kutazama ile picha alafu nwishowe akairejesha mikononi mwa Darren na kusema, “Anafanana na mimi sana!”
“Ndio! Hata mimi nilishangazwa sana ndiyo maana nikaibeba nije nikwonyeshe!”
Melissa akawa amenyamaza kimya. Macho yake yalionyesha yu mbali kifikra. Darren akamtazama na kumwita mara mbili kabla mwanamke huyo hajashtuka na swali, “Unaweza ukanipeleka huko kwa Bibi yako?”
“Amefariki!” Darren akamjibu akimtolea macho. “Au wataka kuona kaburi?”
“Twende hivyo hivyo!” Melissa akasihi. “Sidhani kama kutakuwa na shida, Darren!”
Darren akafikiri kidogo kisha akamwambia wataenda huko mwisho wa wiki kwani atabanwa na kazi hapa siku za usoni.
“Darren,” Melissa akaita akijitengenezea kumtazama mwanaume huyo. “Naomba, nipo chini ya miguu yako, tafuta siku ya karibuni. Mpaka mwisho mwingine wa wiki ni mbali sana!”
Darren akashangazwa na hitaji hilo la ghafla. “Melissa, ni haraka mno! Vipi kuhusu rat—”
“Tafadhali, Darren!” Melissa akanong’ona kwa huruma. Macho yake yalipoa na uso wake ukiwa kama ule wa mtoto aombapo kitu. Darren akashindwa kukataa. “Sawa, basi tufanye keshokutwa.”
“Kwanini sio kesho?” Melissa akauliza kwa upole. Darren akamtazama kwanza mwanamke huyo, alafu punde uso wake ukawa mgumu, “Melissa kwani kuna nini huko kitakachopotea tukikawia?”
“Darren, ungalikuwa wewe umefanana na mtu pichani hivi usingelipata hamu ya kujua?”
“Sawa,” Darren akalegea. “Tutaenda huko hiyo kesho.”
Basi baada ya hapo wakafanya mpango wa chakula, wakawasha pia na runinga watazame baadhi ya filamu. Wakachoma hapo masaa mpaka kiza kilipoingia. Wakala na kuendelea kutazama runinga wakiwa wanapeana mabusu na maneno matamu.
Usiku ulipokuwa mkubwa zaidi wakaenda kitandani, na kabla ya kulala ‘wakanyooshana migongo’. Wakachoka sana na basi usingizi ukawakwapua kwa upesi sana wasidumu hata lisaa.
Wakiwa wamelala, ni saa tisa ya usiku, ghafla Melissa anaamka na kuketi kitako kitandani. Kuna jambo linamtatiza kichwani. Anamtazama Darren, yu hoi hajielewi. Basi anatoka kitandani na kwenda kuifuata ile picha ya Bibi pale mezani.
Akaiteka kwa mikono yake membamba kisha akairejea kuitazama kwa macho yake makavu pamoja na kiza. Baada ya sekunde mbili, akasema kwa kunong’ona, “Tabitha … Cassandra … Bessie.!”
Akisema majina hayo akawa anamtazama mmoja baada ya mwingine. Punde akasikia Darren akijigeuza kitandani, upesi akatazama. Mwanaume huyo hakuwa ameamka. Bado alikuwa kwenye lindi kubwa la usingizi. Melissa akaachana naye na kuendelea kutazama ile picha, mwishowe akaiweka kifuani mwake akiwa na uso wa mawazo.
“Tabitha, nangoja jua lichomoze,” akasema hivyo na basi akarejea kitandani mwake na kulala.
Masaa yakazidi kusonga mpaka kufikia majira ya saa kumi na moja. Hapo Darren akashtuka toka usingizini na kuangaza. Alidhani pengine amekawia. Akafungua dirisha na kutazama nje, bado kiza. Basi kabla hajajirudisha kitandani akaenda chooni kwa haja ndogo.
Alipotoka huko, kama bahati tu, akajikuta macho yake yakiangukia mezani pale alipoacha picha yake. Akasonga karibu na kuitazama tena picha ile akitumia msaada wa taa ndogo ya mezani.
Akajikuta anatabasamu kumwona mtu mithili ya Melissa. Ila alipoitazama picha hiyo zaidi akagundua yule Melissa wa pichani alikuwa ana kovu dogo chini ya goti lake la kushoto. Aliweza kuona hivyo maana gauni lilikuwa limeishia magotini.
Basi kwa hamu ya kutaka kujua akamsogelea Melissa kitandani kisha akamtazama mguu wake wa kushoto. Hapo akaona kovu lile lile la kwenye picha! Ni kovu dogo ambalo hakupata hata kulijua kwa muda wote huo ambao amekuwa na Melissa kwenye mahusiano.
“Inawezekanaje?” akajiuliza. Akairejesha picha ile mezani kisha akazima taa na kurejea kitandani. Akalala nyuma ya mgongo wa Melissa aliyekuwa amelala kiubavu na kidogo akapitiwa na usingizi.
Ila hapo Melissa akafungua macho. Macho yake yalikuwa makavu tofauti na mtu atokaye usingizini. Melissa hakuwa amelala. Melissa alisikia na kuona kila kitu ambacho Darren ametoka kukifanya.
Hakufanya kitu na badala yake akalala. Asubuhi ya saa moja kamili wakaamka na kujiandaa kwa ajili ya safari. Kufikia saa tatu tayari wapo kwenye basi wakienda kijijini, countryside.
Walipopoteza masaa matatu barabarani wakafika kituoni. Wakatembea kwa ufupi kabla ya kufika kwenye nyumba kubwa ya Bibi. Hapo Melissa akasimama kuitazama nyumba hiyo kwa umakini. Naye Darren aliyekuwa ametangulia mbele ikamlazimu amrejelee, akatabasamu akimwambia, “Ndiyo hapa! … ni pazuri, sio?”
“Ndio, ni pazuri!” Melissa akajibu pasipo kumaanisha kwa uso wake, wakazama ndani. Humo akang’aza sana macho, ndani ya nyumba nzima na pia huko nje kana kwamba mtu anayetaka kununua akitaka kubaini madhaifu.
Walipokuwa nje, akamwomba Darren amwonyeshe kaburi la Bibi yake. Naye Darren pasipo ajizi, akampeleka magharibi ya mbali ya nyumba hiyo na kumwonyeshea, “Ndiyo hapa!”
Melissa akasoma kibao cha kaburi. Kilisomeka kwa jina la Cecilia Goodwin. Akauliza, “hili ndilo jina la bibi yako?”
“Ndio,” Darren akamjibu.
“Ahsante. Tunaweza tukarudi ndani.”
Wakarudi huko na Darren akampatia Melissa picha za Bibi yake. Kwa taratibu akazitazama moja baada ya nyingine.
“Sikumwona mtu huyo tena,” alisema Darren. “Yupo kwenye picha moja tu.”
Melissa asiseme kitu akaendelea kukagua picha zile. Alipomaliza akamkabidhi Darren na kisha akalaza kichwa chake kochini. Darren akazirejesha picha hizo na kisha kujumuika na Melissa hapo sebuleni.
Usiku ulipowadia, Melissa akamnong’oneza Darren kwenye sikio lake la kulia, “Nakuhitaji mpenzi.”
Darren akamtazama mwanamke huyo kwa kukodoa, “Melissa, tumefanya jana tu!”
Melissa akang’ata lips zake na kulegeza macho. “Kwani kuna ubaya, mpenzi?” akauliza akiweka kiganja chake kifuani mwa Darren.
“Hamna ubaya ila si kawaida yako.”
Melissa akatabasamu. Akafungua kifungo kimoja cha shati la Darren. “Sasa nitafanya nini na ingali u karibu yangu, tena tukiwa wapweke wenye nafasi?” akateta kwa sauti ya puani.
Darren asijibu, mwanamke huyo akaanza kubusu kifua chake na hatimaye akatimiza adhma yake. Darren akawa hoi kana kwamba amelima ekari za mbaazi. Hata alipojilaza hapo kochini akawa kama mfu!
Basi Melissa akajivalia nguoze na kisha akaelekea stoo. Huko akateka chepe na kutoka ndani ya nyumba kisha akaelekea moja kwa moja kule mashariki ya mbali kukuta kaburi la Cecilia Goodwin, bibi yake Darren.
Hapo kabla hajafanya chochote akaita kwa kunong’oneza, “Tabitha!”
Kisha akaanza kuchimba kaburi.


**

Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*UNA NINI LAKINI MELISSA? -- 07*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Kidogo akashangazwa na jambo hilo, lakini hakuhangaika nalo sana. Alikuwa ana vitu vingi vya kujadili kichwani mwake. Wakamzika mama na kisha wakarudi nyumbani. Huko ndo’ baba yake akamwambia, “Kuna kitu nataka tuzungumze.”

ENDELEA

Akamwambia kuna mengi anataka kuteta naye ila yote hayo yapasa yawe ya siri baina wao. Hategemei kumwona mtu yeyote anapata kuyafahamu, na basi kwa kufanya hivyo atakuwa amejiweka shidani.

Maneno hayo yakamfanya Darren awe mtulivu na msikivu sana maana yalimaanisha ni jambo kubwa lenye uzito. Baba yake, Mr Gerald, akanywa kwanza fundo la glasi ya whisky kisha akamtazama mwanaye machoni.

"Sikia, Darren," akasema kabla hajasafisha koo lake na kujipangusa kwa mgongo wa kiganja. "Kuna mambo ya ajabu ajabu hapa katikati. Najua hauyafahamu na nilipata kumsisitizia sana mama yako akwambie lakini hakuwa tayari. Mpaka kifo kinamkuta hajatekeleza ahadi yake hiyo..."

Akaweka kituo akitazama sakafuni kifikira. "Ulikuwa ni wakati mgumu sana, kwangu na kwake. Tangu yu kwenye usichana mpaka tulipokupata wewe. Nakumbuka, pindi alipokuwa msichana mdogo, alikuwa anapitia mambo ya ajabu sana. Ndoto za ajabu. Na mara kwa mara akinambia anaona watu wa ajabu wakimjia.

Kuna muda tulikuwa tunashindwa kulala. Angesema kuna mtu nyuma ya mlango. Mtu dirishani. Mtu koridoni. Mtu kila sehemu! Hatukuwa na amani, na, Mungu nisamehe, nilishawahi kufikiria kuachana naye maana hayakuwa yanavumilika."

Akanywa tena fundo la whisky. Kuyaongea hayo aliyokuwa anaongea, ilimpasa apashe kichwa na kujitoa ufahamu.

"... lakini kila nilipokuwa nataka kumwacha, ningalijiuliza, vipi ingekuwa mimi? Ningejisikiaje mtu angeniacha kwasababu ya matatizo yangu? Bila shaka ningehisi nimetupwa na kukomolewa, basi nikapiga moyo konde. Maisha ya taabu, taabu sana.

Tukahama pale tulipokuwa tunakaa kwa kudhani aidha hapafai, lakini bado matatizo yakawa yaleyale. Shida haikuwa nyumba. Shida ilikuwa damu. Damu ya mama yako. Na hata angeenda wapi, basi angelibadilisha jambo."

Aliposema hayo akanyamaza kana kwamba anapangilia sentensi kichwani. Na kabla hajateta lingine, akanywa tena whisky, tena saa hii mara mbili tofauti na hapo awali kisha akanguruma kama simba kwa kuwakwa na koo.

"Unakumbuka kwenye msiba wa bibi yako?" Akauliza.

"Ndio, nakumbuka," Darren akajibu.

"Uliona bibi yako alizikwaje?" Baba akauliza, naye Darren alipofikiria kidogo akasema, "Hatukumuaga kama wengine. Na hakukuwa na kiongozi wa dini kuendesha misa!"

"Unadhani kwanini?"

"Sijajua kwanini ... lakini ... mimi sikuwahi kuona ubaya wowote wa bibi alipokuwa hai!"

"Ni sawa. Na hamna shida yoyote katika hilo. Lakini utakuwa umejifunza kuwa mama yako hakuwa na mahusiano mazuri na bibi yako, japo alikuwa mama yake. Ni aghalabu angeenda kumtembelea na kumjulia hali. Sio?"

"Ndio."

"Darren, Bibi yako hakuwa mtu wa kawaida. Na alimweka kifungoni mama yako kwa takribani miaka tisa! Sijui nisemeje, sikuwa mtu wa kuamini hayo mambo hapo kabla, ila baada ya kukutana na mama yako ndipo nikaelewa juu ya uwepo wake.

Ni kama kheri, tukiwa tumehamia kwenye makazi mapya, baada ya kukaa hapo kwa miezi mitatu, tukapata jirani ambaye alitokea South Carolina. Jirani huyu baada ya kukaa siku tatu tu kando na sisi, akafahamu yale tuliyokuwa tunapitia.

Nakumbuka siku moja nikiwa natoka kazini, aliniita na kunambia angependa kuongea na mimi mambo kadhaa. Nilisita kidogo ila sikuona haja ya kumkatalia. Nikasonga akanipatia kiti nikae sebuleni mwake. Hapo akaniuliza akiwa amenikodolea macho yake ya kizee, 'una shida kubwa, sio?'

Mimi nikamkatalia, lakini aliweza kuona ndani yangu. Kwa upole akasema anataka kunisaidia na kama nikiwa tayari kukiri kuwa nina hiyo shida basi atakuwa radhi. Mimi nikakataa. Sikuwa namfahamu hata kidogo na nilihofia asije akaniongezea matatizo mengine zaidi ya yale niliyokuwa nayo.

Basi nikaondoka nikiwaza sana. Kesho yake nilipopita hapo kwake, nikamkuta kibarazani. Nikamsalimu na kwenda. Siku hiyo usiku nikapata tabu sana. Mama yako alinikaba mno na kwa macho yangu nikashuhudia nyayo za damu koridoni! Nikakoma ubishi.

Kesho nilipotoka kazini nikamwendea yule mama na kumwambia nina shida. Naomba anisaidie kwa namna yoyote ile. Na atakapoweza, basi nitajikunja kwa kadiri ya uwezo wangu nimpatie chochote cha thamani.

Kwa wakati huo nilikuwa nimekonda sana. Sitamaniki. Hata nguo zangu nazoendea kazini zikiwa zimefubaa, chafu na kukuu. Sikuwa na raha na maisha haya.

Yule mama akaniambia yu tayari kunisaidia, cha muhimu nimlete mke wangu kwake nikiwa na petali nne za maua zamaridi, mafuta ya ngamia na matumbawe toka baharini.

Japo masharti yalikuwa magumu, nikaridhia. Ugumu wake haukuwa sawa na ule nlokuwa napitia kila siku. Nikatafuta vitu hivyo na ndani ya siku mbili nikavipata vyote. Nikambeba mke wangu na kumpeleka huko.

Basi mama yule akafanya mambo yake. Sikuelewa anachofanya, alikuwa anaongea kwa lugha ya ajabu. Alitengeneza maji na kuchanganya na petali zile za zamaridi kisha akampaka Sarah mafuta yale ya ngamia kwenye paji la uso.

Na kama nakumbuka vema, alichukua unga nisiojua wa nini, akautia kwenye maji yenye zile petali alafu kama haitoshi, akamchanja Sarah kwenye mkono wake wa kushoto, akakinga damu na kuweka humo.

Mwishowe akatengeneza uji mzito ambao akawa anachovyea na kuandikia kwenye kitabu akiwa ananena kwa lugha ya ajabu. Alipomaliza kuandika, akakizungusha kile kitabu kichwani mwa Sarah na kumgusishia kwenye paji la uso kisha akamwambia naye aseme maneno alokuwa anayatamka.

Sarah alipofanya hivyo, akazirai. Mama yule akan'tazama na kunambia, kitabu kile kiende kuhifadhiwa mbali msituni kwani ndiyo roho pekee salama ya Sarah. Kadiri kitabu kitakapokuwa salama, naye atakuwa vivyo. Lakini kitakapoharibika, naye ataenda vivyo hivyo.

Na kwa kadiri ambavyo kitabu hicho kitakuwa hai, hamna mtu yeyote mbaya anaweza kumdhuru, akisisitizia zaidi juu ya majini. Watamwogopa kama ukoma na watamkimbia popote pale atakapokanyaga."

Basi hapa Darren akajikuta akimkumbuka Melissa. Mbona alikuwa akimkimbia mama yake? Lakini hakuwaza sana, akaendelea kumpatia masikio babaye aliyekuwa na mengi ya kumwambia.

"Na tokea hapo mama yako hakusumbuliwa tena. Na punde bibi yako alipofariki, ni yeye ndiye akashauri kuwa nyumba ile iuzwe. Na hata vile vilivyomo ndani visichukuliwe hata kimoja kwa kuhofia vyaweza kubeba na kusafirisha matatizo!"

Darren akakumbuka kuhusu ile picha ya bibi yake na namna ambavyo mama yake alivyokuwa ameghafirika kuitafuta. Akajikuta akitikisa kichwa kwa masikitiko. Sasa ndiyo alijiona mjinga.

"Mama yako," baba akaendelea kuteta kwa huzuni, "alikufa kwasababu ya moto uliochoma msitu wa kule California. Kitabu chake kitakuwa kimeungua na basi hivyo maisha yake. Hamna kitu ambacho kingeweza kumwokoa.

Lakini nahofia sana, Darren. Nahofia zaidi kuhusu maisha yako. Sidhani kama yatakuwa sawa na kuondoka kwa mama yako. Hata yangu pia. Naamini uwepo wake ulitufanya tukawa salama zaidi."

Akashusha pumzi ndefu kisha akahitimisha kwa kusema, "Na kwa usalama wetu Darren, inabidi tuachane kabisa na ile nyumba. Ile ya bibi yako. Usiende tena huko, wala kuhusiana nayo kwa njia yoyote ile. Sawa?"

Darren akatikisa kichwa. "Sawa." Macho yake yalikuwa mekundu yaliyochoka.

Basi tangu hapo, miaka ikaenda na kwenda. Baba yake Darren akasumbuliwa sana na ugonjwa wa saratani ya koo kwasababu ya uvutaji mkubwa wa sigara hivyo akajifia na kumwacha Darren peke yake.

Baada ya mwaka mmoja, Darren akamwoa mwanamke mrembo aitwaye Josephine, na kuwa na familia. Akaishi mbali kabisa na nyumbani, huko New York. Ndani ya mwaka mmoja wakajaaliwa mtoto wa kiume waliyemwita William.

Lakini ...

Darren atabaki vipi salama na ingali damu yake ndi' ile ile ya mama yake? Kama ametoka kwenye tumbo la aliyetoka kwenye tumbo la asiye binadamu, kivipi anasalimika kwa upesi?

***

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*UNA NINI LAKINI MELISSA? -- 08*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Lakini ...

Darren atabaki vipi salama na ingali damu yake ndi' ile ile ya mama yake? Kama ametoka kwenye tumbo la aliyetoka kwenye tumbo la asiye binadamu, kivipi anasalimika kwa upesi?

ENDELEA

"Nadhani leo nitakawia kutoka kazini," alisema Darren akiwa anakunywa chai. Pembeni yake alikuwapo mkewe akiwa amembebelea mtoto. Darren alikuwa ameshajiandaa kikazi, amevalia suti na tai yake nadhifu.

"Kwanini?" Josephine akauliza akimtazama kwa shaka. Hakuwa kuzoea mambo hayo ya mumewe kukawia hivyo alitarajia kutakuwa na sababu kubwa.

"Nina kazi kubwa sana," akasema Darren. "Na nisipozimaliza leo basi itaniwia ugumu sana hapo baadae."

Mkewe akaelewa lakini asisite kumwonyesha mumewe kuwa atamkumbuka. Na basi atakapopata namna, ajitahidi kuwahi.

"Usijali," Darren akamtoa shaka kisha akambusu kwenye paji la uso kabla hajasimama. "Nitajitahidi mpenzi wangu. Ila ukiona nimekawia zaidi basi usikasirike ... unajua namba yangu, utan'pigia nikikawia kufanya hivyo."

Basi akaenda zake baada pia ya kumwaga mwanaye ambaye sasa alikuwa na mwaka mmoja tangu azaliwe. Akajiweka kwenye gari na kisha akaanza safari ya kwenda kazini.

Akaendesha salama mpaka alipokuja kukuta foleni baada ya kama dakika arobaini na tano akiwa barabarani. Akiwa hapo, kwa kuepuka kuboreka kwa kungoja, akawasha redio na kuskiza habari za asubuhi.

Zikapita habari kadhaa, hakuzijali sana japo alizipa sikio. Kidogo akiwa anaskiza ndipo ikaja habari ya ghalfa juu ya ajali kubwa ilotokea huko kaskazini mwa Marekani, hapa akajikuta akiguswa na kujawa na umakini. Akategea sikio na akili yake yote kwa sauti aliyokuwa anaisikia redioni.

Basi akapata kupashwa kuwa moto mkubwa umetafuna msitu wa Orleans. Bahati hakuna taarifa ya mtu yeyote mpaka muda huo ambaye ameripotiwa kufa au kudhurika.

Habari hii japo ilipita na kuendelea na zingine, bado ikabakia kwenye kichwa cha Darren. Alipata kukumbuka juu ya moto ule uliokula msitu miaka ile ulivyommaliza mama yake katika namna ya ajabu. Alijikuta akimkumbuka mama yake, baba yake, bibi yake na hata Melissa!

Mawazo yake yote yalihama, na kwa muda akawa hana raha. Hata akajisahau kuwa yu barabarani na basi inabidi aweke msisitizo mkubwa asisababishe ajali kama si kuwakwaza wengine.

Alikuja kushtuliwa na honi kali nyuma yake maana foleni ilikuwa inaenda sasa. Naye akatia gari yake moto na kusonga mpaka kazini. Bado alikuwa ndani ya muda. Akajiweka kitini na kuanza kupangilia mambo yake atakayoanza kuyafanya moja baada ya jingine. Lakini kabla hajaanza, mawazo yale ya moto yakamteka tena!

Akabaki hapo kwenye kiti akiwaza sana. Alikuja kustaajabu amekula lisaa lizima na dakika zake tena akishtuka baada ya mhudumu akija kumuuliza kama angependelea chai au kahawa kwa siku hiyo.

"Mungu wangu!" Akalalama akitazama saa ya ukutani. "Nimechele .... Jack, niletee kahawa tu! ... sawa? Haraka basi!"

Akaanza fanya kazi zake moja baada ya nyingine. Alipomaliza za makaratasi, basi akaenda 'lab' huko nako akahangaika kwa masaa kabla hajaenda kupata chakula cha mchana. Ni ndani ya jengo hilo hilo. Akiwa hapo anakula, naye mfanyakazi mwenzake aitwaye Roby akaja na kujiunga naye.

Alikuwa ni mwanaume 'blonde', mwembamba na mwenye kuvalia nguo zilizomzidi. Macho yake yalikuwa yamefunikwa na miwani yenye fremu nyembamba ya chuma. Mdomoni amebana toothpick.

"Hey, Darren!"

"Hey!"

Akaweka sahani yake yenye chakula mezani kisha akavuta kiti na kuketi.

"Unaendeleaje leo?"

"Nimebanwa sana na kazi. Ni siku ngumu."

"Ooh! Pole, nami ilikuwa hivyo jana yake. Nadhani ni muda wa kufikiriwa kuongezewa mshahara sasa."

Darren akaendelea kula pasipo kusema kitu.

"Darren, hauniungi mkono kwenye hilo?"

"Hata nikikuunga, itasaidia nini Roby?" Akasema Darren akitafuna. "Hamna cha kufanya. Kama kingekuwepo basi kingeshafanyika kwa muda mrefu tu."

"Kwahiyo umeridhika na hali?"
"Roby, sina muda wa kuongea sana ndugu yangu. Natazamia nimalize chakula kisha nikamalize viporo vyangu."

"Sawa. Ila Darren nina wazo ..."

Darren akamtazama pasipo kunena kitu.

"Si jipya sana. Ni kuhusu lile wazo lako ulilowahi kunambia hapo kabla."

"Wazo gani?"

"La kufungua sehemu yetu kule uliponambia."

"Haiwezekani kwa sasa. Kwa muda ule kulikuwa kuna sponsorship. Haukuniunga mkono kwa woga wako. Sasa unadhani saa hii tutafanya nini? Una pesa hiyo?"

Kabla Roby hajajibu, Darren akanyanyuka na kugonga meza, "baadae, Roby!" Kisha akaenda zake. Akarudi 'lab' na kuendelea na kazi zake. Mpaka jioni akawa amemaliza huko. Sasa akawa amebakia na kazi ya kuandika ripoti tu.

Akiwa amejichokea, ila hana namna, akaandika ripoti hizo mpaka majira ya saa nne usiku. Watu waliondoka kazini na sehemu kubwa ya jengo ikawa ipo gizani kutokana na kutokuwa na watu.

Na zaidi kukawa kimya. Hata Darren akawa anasikia sauti ya keyboard ya tarakilishi kana kwamba honi ya gari. Kila alipokuwa anabofya ikawa inatoa mlio wa nguvu. Na ni kwasababu kulikuwa na ukimya tu eneoni.

Akiwa anaandika, mara akasikia jambo. Ilikuwa ni kama sauti ya watu wakiteta kwa umbali mdogo, basi akaacha kuchapa kazi yake na kusimamisha masikio. Punde sauti hiyo ikakoma. Basi naye akaachana nayo na kuendelea kuchapa kazi yake.

Akachapa kidogo, sauti ile ikajirudia tena. Alisikia watu wanateta japo hajui wanazungumzia nini. Na zaidi mmoja wao akaangua kicheko! Kicheko hicho kikavuma kana kwamba mtu huyo alikuwapo karibu kabisa. Na kwa namna kubwa kikamuogofya Darren!

Akatoka kwenye kiti chake na kuujongea mlango, akaufungua na kutazama nje. Hakuona kitu. Akapaza sauti, "helloooooow!" Napo hakusikia kitu isipokuwa mwangwi wa sauti yake kumrudia.

Akanyamaza akisimama hapo askize. Kidogo akasikia tena sauti za watu, zilikuwa zinatokea kulia kwake. Akapaza tena sauti, "Helloooow! Kuna mtu huko?"

Kimya. Mara akasikia kicheko na kilipokoma kukawa kimya kama shimoni. Akastaajabu. Akaanza kupiga hatua kwenda kule aliposikia sauti ile. Alipojongea mpaka mwisho, akaangaza kama ataona kitu. Hola!

Kidogo akasikia, 'tap!' Alipogeuza shingo yake kutazama nyuma, akaona taa ya ofisi yake imezimwa! Moyo ukamlipuka. Kabla hajafanya jambo, akasikia sauti kubwa ya kitu kama alarm! Mwili ukamtetemeka kwanguvu!

Alipoweka akili yake sawa ndipo akabaini huo ulikuwa ni mlio wa simu yake. Simu ilikuwa inaita. Basi haraka akaendea ofisi yake na kukamata simu, mkewe alikuwa anampigia. Alipopokea, akajongea 'switch' ya kuwashia taa na kuibofya. Hakukuwa na umeme!

"Bado upo kazini?" Mkewe aliuliza.

"Ndio, nipo kazini, ila ..." akajaribu tena kwa kubofyabofya switch. Bado matokeo yalikuwa yaleyale. " ... ningoje maana nakuja muda si mrefu!"

Akakata simu na kukusanya kilicho cha kwake. Umeme haukuwapo hivyo asingeweza kuendelea na kazi tena. Akafunga ofisi na kutoka ndani lakini akilaumu kwani alikuwa amebakiza kazi kidogo sana amalize kabisa.

Akatembea kama hatua nane, mara umeme ukarudi! Akasimama na kujiuliza arudi ofisini ama aendelee na safari yake ya kwenda nyumbani? Basi baada ya kujiuliza huko kwa muda mfupi, akaona kheri akamalizie kazi kabisa kesho awe huru.

Akarejea na kuketi kitini kisha akawasha tarakilishi. Akaanza kuchapa na kuchapa. Ila hakudumu sana, akasikia tena sauti ya watu ikiteta na kucheka! Na mara hii, umeme ukamkatikia ndani ya ofisi!

Kidogo, akasikia sasa watu wakiteta ndani ya ofisi. Tena si mbali kabisa na yeye. Kwa kando ya kushoto.

***

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom