Riwaya: UCHU

Riwaya: UCHU

Wewe ndo boya uliyechukulia siriaz jambo la utani. Huku sio siasani wewe yan akitajwa profesa unamfikiria tu yule prof wenu wa nanihii....pole sana

moonoooooooooooooooooooooooooooomimi napita tu
 
Daaah TECHMAN vipi nmekuja mbio nikijua kitu kimewekwa
 
Last edited by a moderator:
[h=3]KAZI IMEANZA[/h]

Baada ya kuzungumza na Phillipe JKS alimpigia simu ofisa mmoja wa usalama aliyekuwa anashughulikia maswala ya uchukuzi wa abiria. JKS ndiye aliyemsaidia sana ofisa huyu kupanda hadi kufikia ofisa usalama mwandamizi.


"Mulamba", JKS aliita baada ya simu kupokelewa.


"Ndiyo, nani mwenzangu?".


"Pole kwa kukuamsha, naona ulikuwa bado umelala, huyu ni JKS".


Mulamba mara moja usingizi ulimtoka na kuinuka kabisa kitandani na kuketi kwenye ncha ya kitanda.


"Ndiyo mzee, hapana nilikuwa nimeamka ila bado nilikuwa najinyooshanyoosha tu kwani jana nilichelewa kulala", alimjibu kwa woga. Ile sauti ya woga ilimfurahisha JKS maana alipenda na kufurahia kutetemekewa.


"Hamna neno, sasa sikiliza, hii ni amri toka juu kuliko hata mimi. Si unamjuwa Willy Gamba?".


"Ndiyo mzee, nani asiyemjua katika fani yetu hii", Mulamba alijibu.


"Amepewa kazi toka ngazi za juu, na jana alienda Arusha na ndege za Shirika la Ndege Tanzania. Kwa vile sasa hayuko tena kwenye ajira ya serikali, hii kazi amepewa nje ya mipango ya kiserikali maana ni kazi nyeti na serikali haitaki itambulike kuwa inahusika. Ila alitakiwa ajulikane yuko wapi kila wakati, lakini toka jana jioni hajulikani aliko. Sasa imeamriwa tutumie ofisi yako tujuwe yuko wapi na ripoti hiyo isiende kwa mtu yeyote ila mimi", JKS alimaliza.


"Hilo nitalifanya sasa hivi mzee, ila nataka kujua alikuwa anatarajia kwenda wapi baada ya kutoka Arusha?", Mulamba aliuliza.


"Baada ya kutoka Arusha alitakiwa kurudi hapa Dar es Salaam, halafu anende Kigali. Kuna ndege ya asubuhi sana ya ATC toka Kilimanjaro ambayo itaondoka saa moja, kama yumo nipe habari, kama hayumo tafiti ujuwe anakuja Dar es Salaam na usafiri gani, nipate habari haraka. Angalia usafiri wote mabasi, malori na kadhalika.


"Usiwe na wasiwasi mzee, nitakujulisha baada ya saa chache, tutampata tu. Tukimpata tumfanyeje?".


"Usifanye chochote, wewe eleza tu yuko wapi".


"Haya, asante".


"Kwa heri", JKS alikata simu.


Baada ya kukata simu ya Mulamba, JKS alipiga simu Paris kwa Jean na kumweleza mambo yaliyotokea Arusha na hadhari aliyokuwa amechukuwa tayari. Jean, akiwa bado na usingizi kwani Paris ilikuwa yapata saa kumi na nusu za asubuhi, tulikuwa tunapishana saa mbili.


"Nataka utakaponipigia tena simu unieleze kuwa tayari keshauawa, vinginevyo usinipigie simu mpaka utakapofanikiwa kazi hiyo. Natuma pesa leo asubuhi kupitia kwa yule rafiki yangu mwenye kampuni ya kitalii ya Concord Tours zikusaidie kukamilisha kazi. Vilevile nitawapigia simu na marafiki zangu wengine huko Afrika Mashariki wakupe msaada wowote utakaohitaji", Jean alimalizia na kukata simu bila bila kumsubiri JKS ajibu.


Kwa mara ya kwanza katika maisha yake JKS alisikia woga. Alizijua nguvu za Jean na akajuwa itabidi atimize hii kazi, vinginevyo mambo yangeweza kumgeukia. Alifikiria jinsi Jean alivyokuwa amemwahidi kumsaidia kuunyakuwa urais wa Tanzania na alikuwa anaujuwa uwezo wa Jean kuifanikisha azma yake hiyo. Na dhamira ya JKS kuwa Rais ilizidi vitu vingine vyote, lakini leo huyu Willy Gamba angeweza kumfanya akose nafasi hii. Asubuhi hii alisikia jasho la baridi likimtiririka mgongoni na kujisemea kwa sauti. "Kwa kila hali lazima aondoke".


Bila kujua amesema kwa sauti kubwa mke wake aliyekuwa amelala bado alishtuka na kuuliza. "Unasemaje?".


"Hapana, sijasema kitu", JKS alijibu.


Mke wake alimjua sana. Hivyo, akanyamaza lakini alijuwa mzee alikuwa anasumbuliwa na kitu fulani.
 
KAZI IMEANZA


II


Willy alitua kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza mnamo saa mbili na nusu za asubuhi. Asubuhi kabla hajaondoka nyumbani alimpigia simu rafiki yake mmoja ambaye alikuwa na wadhifa wa juu ndani ya Chama cha Msalaba Mwekundu na kumwomba msaada kati ya ndege zao zilizokuwa Mwanza moja impeleke Kigali. Willy aliwahi kukisaidia sana Chama hiki, na huyu rafiki yake aliona bahati sana kupata fursa kama hii ili nae alipe angalau fadhila kidogo za Willy kwa yote aliyowahi kuwatendea.


"Bila shaka Willy, sasa hivi nitapiga simu Mwanza na hiyo saa mbili na nusu unayotegemea kufika Mwanza utakuta ndege ndogo ya injini mbili aina ya Cessina yenye namba MMT 3 ikikusubiri. Sisi tunaruhusiwa bila matatizo kutua Kigali kutokana na hali ilivyo Wilayani Ngara. Hivyo, huna haja ya kuhangaika kupata kibali cha kutua, hicho sisi tunacho na utakuta maofisa wetu pale Mwanza wameshawasiliana na Kigali", yule rafiki yake Willy alieleza.


"Nitafurahi sana, na kama vilevile mtawaeleza kuwa mimi ni afisa wenu", Willy aliongezea.


"Bila shaka", rafiki yake alijibu huku akicheka maana alijua Willy haendi Kigali bure.


Kwa hiyo, Willy alipotelemka ndani ya ndege ya kukodi ya Tanzanair alikuta ndege ya Chama cha Msalana Mwekundu iko tayari.


"Ina maana mimi sasa nitarudia hapa?", rubani wa Tanzanair alimuulizia alipomwona anashuka na mfuko wake.


"Ngoja kidogo", Willy alimjibu.


Willy alikwenda mpaka kwenye ile ndege na kumkuta rubani na ofisa mmoja wa Msalaba Mwekundu wakimsubiri Willy.


"Karibu mzee", wote wawili walitamka kwa pamoja Willy akawapa mikono kuwasalimia.


"Asanteni sana", alijibu.


"Sisi tuko tayari, ila tu tunaomba uende na ndugu yetu mmoja ambaye anaenda huko vilevile kikazi", yule afisa alimwambia willy.


Willy alimwangalia yule jamaa, na kumwona ni wa makamu yake na wa umbo lake.


"Sawa, lakini ningeomba aje na ile ndege ndogo ambayo nimekuja nayo ili rubani awe na mtu wa kuzungumza nae, maana hiyo nayo inakuja Kigali, ila kwa sababu lazima ijaze mafuta na kukaguliwa kidogo ndio sababu imebidi mimi nikifika tu hapa nipate ndege nyingine kwa vile nina miadi maalumu ya kiserikali pale uwanja wa Kigali na mtu ambaye ataondoka saa moja kuanzia sasa", Willy alieleza.


"Basi, vizuri sana. Je, ndege yako ina vibali vyote vya kutua?", yule ofisa aliuliza maana alijua jinsi hali ilivyokuwa uwanjani pale Kigali.


"Hamna taabu, kila kitu kipo", Willy alijibu, kisha akaenda kwa rubani wa ndege yake.


"Sasa ukishajaza mafuta utakuja na yule bwana pale, naye anakuja Kigali. Ukishamshusha tu basi wewe urudi", Willy alimweleza.


Yule rubani alishangaa kwanini wasitumie ndege moja badala ya ndege mbili. Lakini kwa vile haikuwa shughuli yake na kwa vile alikuwa ameagizwa kwenda mpaka Kigali aliamua kubaki ameshangaa lakini atekeleze wajibu wake.


"Sawa mzee", yule rubani alimjibu huku sauti ikionyesha mshangao. Willy alitoa dola mia za kimarekani, akampa.


Tabasamu safi likaonekana usoni mwa rubani.


"Asante sana mzee", alijibu tena na kupeana mikono ya kuagana. Willy alikwenda kwenye ndege, na rubani wa Chama cha Msalaba Mwekundu akaiondoa ndege kuelekea Kigali ikiwa yapata saa tatu kasoro robo. saa za asubuhi.
 
KAZI IMEANZA


III


Ilikuwa saa tatu na dakika kama tano hivi, Mulamba alipompigia simu JKS. JKS alikuwa tayari amefika ofisini.


Simu ya moja kwa moja kwa JKS ililia na haraka akainua. "Nani", aliuliza kwa shauku.


"Mulamba, mzee".


"Haya vipi mmempata?".


"Mzee huyu mtu tumeweza kupata nyendo zake zote, ila hatukuweza kumpata yeye kabisa maana alikuwa hatua moja mbele kila tulipokuwa karibu kumpata".


"Una maana gani, hebu sema mambo ya kueleweka", JKS aliuliza kwa ukali.


"Ndio nilitaka nikupe ripoti kamili mzee. Kutokana na taarifa za uchunguzi wetu, aliondoka Arusha jana kwa ndege ya kukodi ya Tanzanair, hivyo hakulala Arusha ila alilala hapa Dar es Salaam. Leo asubuhi ameondoka Dar es Salaam kwa ndege hiyo hiyo ya kukodi ya Tanzaniair na anaelekea Kigali. Habari za watu wangu nilizozipata hivi punde ni kwamba ameondoka Mwanza mnamo saa tatu kamili kuelekea Kigali. Hali ndivyo ilivyo mzee. Sijui tukusaidie nini tena?", Mulamba aliuliza.


"Ndege hiyo ya Tanzaniar ni namba ngapi?", JKS aliuliza.


"Namba zake ni MHZT 12".


"Sawa basi asante, nikikuhitaji nitakutafuta".


"Haya, asante mzee", Mulamba alijibu huku akipumua kwani alikuwa amejawa na wasiwasi angetakiwa kufanya nini tena kwani hakutaka kazi yoyote ya kuhusiana na Willy Gamba, maana mtu huyu alikuwa ni moto wa kuotea mbali. Alibaki anashangaa tu hasa ni nini kilikuwa kinatokea kati ya serikali na Willy Gamba.


JKS alijishika kichwa na kujua kazi imekuwa ngumu na yeye peke yake asingeiweza. Huyu Willy Gamba alikuwa kweli kabisa mtu wa hatari na hakika kuwapo kwake Rwanda kungezua balaa, lazima kila njia ifanyike kabla hajaleta madhara. Hakukuwa na njia nyingine ila kurudi kwa Jean maana yeye alikuwa na uwezo mkubwa kufanya mambo Rwanda kuliko yeye. Uwezo wa JKS uliishia ndani ya mipaka ya Tanzania, isipokuwa tu propagada ya kisiasa ndio angeweza kusaidia kokote ulimwenguni kwani alikubalika sana duniani kote kisiasa. Ingawaje Jean alikuwa amemwamru ampigie simu ikiwa Willy ameshauawa, lakini JKS alionelea afadhali atukanwe kuliko kunyamaza. Aliinua simu akampigia Jean kwenye simu yake ya kutembea nayo (Mobile).


"Hallo", Jean alijibu baada ya kupokea.


"JKS hapa".


"Ehe, mambo mazuri?", Jean aliuliza kwa shauku.


"Hapana, mambo yanazidi kuwa magumu", JKS alijibu na akamweleza jinsi sasa Willy Gamba alivyokuwa anaelekea Kigali.


"Mbona mtu huyu nitampenda", Jean alijibu kwa kejeli.


JKS alinyamaza. Hakuwa na la kusema.


"Hapa kweli tunashughulika na mtu mjuzi, huyo anatakiwa apambane na watu wenye ujuzi kama yeye. Basi niachie huyo mtu kwa sasa. Nitarudi kwako baadae, nipe hiyo namba ya ndege na maelezo mengine yote kuhusu hiyo ndege na huyo mtu wako", Jean alimalizia.


JKS alimpa maelezo yote huku akifurahi kuwa Jean ameelewa na hakuweza kumkasirikia. Baada ya kumpa maelezo JKS alikata simu na kuinuka kitini na kwenda kusimama dirishani mwa ofisi yake na kuwaangalia ndege aina ya tausi waliokuwa wakicheza nje tu ya dirisha lake.


Mara mawazo yake yakarudi kwa Willy Gamba. Kuuawa kwa Willy ndio kupata kwake Urais, maana huyu mtu asipouawa anaweza kuchokonoa ukweli wa mambo na kuleta kashifa ambayo ingeweza kumgusa hata yeye kwani JKS alikuwa mmoja wa watu waliokuwa wanahusika na swala zima la Rwanda, tokea maswala ya kisiasa mpaka kufikia mauaji. Na serikali ya Tanzania ilikuwa imeweka mambo yote yahusuyo Rwanda chini yake na ofisi yake kwa vile aliaminika kuwa ni kiongozi mwadilifu.


Baada ya kukata simu ya JKS, Jean alipiga simu Rwanda kwa rafiki yake alikuwa ndani ya Jeshi la RPF. Baada ya RPF kushika madaraka Rwanda, Col. Gatabazi alikuwa wa kwanza kupata simu iliyofanya kazi. Hii yote ilikuwa kwa hisani ya Jean ambaye alikuwa na uhusiano wa karibu na mkuu wa jeshi la Ufaransa lililokuwa Rwanda pamoja na mkuu wa Idara ya Usalama wa Nje wa Ufaransa (DGSE). Inasemekana kuwa Jean ndiye aliyewasaidia hata kupata vyeo hivi kutokana na kuwa kwake karibu na uongozi wa juu wa serikali ya Ufaransa.


Jean alikuwa kama ndiye mshauri mkuu wa serikali ya Ufaransa kuhusu maswala ya Rwanda. Kutokana na kuwa kwake karibu na Rais pamoja na watu wote muhimu ndani na nje ya serikali ya Rwanda. Kwa hiyo baada ya Kigali kuangukia mikononi mwa RPF tu na maofisa wa jeshi hilo kujinyakulia nyumba za kukaa zilizokimbiwa na maofisa wa serikali ya MNRD. Col. Gatabazi ambaye siku zote alijulikana kama mkereketwa mkubwa wa RPF, hakuwa mkereketwa ila msaliti na ndiye aliyekuwa akitoa siri zote za RPF kwa Jean, na Jean akazitoa kwa rafiki zake wa serikali ya MNRD. Kwa hiyo, baada ya kupata nyumba tu Jean alihakikisha kuwa Col. Gatabazi anapata simu ili kila kilichokuwa kinaendelea ndani ya RPF kimfikie.


Kutokana na huo uhaini wake Col. Gatabazi alijipenyeza na kujiweka karibu kabisa na kiongozi wa RPF na akaaminika sana. Inasemekana alikuwa Mhutu, lakini mama yake alikuwa Mtutsi. Baba yake alifariki akiwa na umri wa miaka miwili na akakulia kwa mjomba wake na kwa vile alikuwa amechukuwa umbo la mama yake alitambuliwa kama Mtutsi tu. Ila yeye alijuwa ni Mhutu na inasemekana aliwahi kuambiwa kuwa baba yake aliuawa na wajomba zake kwa vile hawakutaka dada yao aolewe na Mhutu. Hivi kinyongo alikuwa nacho moyoni na ndio sababu alipopata nafasi ya kuwasaliti Watutsi alifanya hivyo kwa moyo mmoja.


Baada ya serikali ya MNRD kuanguka na RPF kuingia, Jean alimhakikishia Col. Gatabazi kuwa serikali hiyo isingeweza kukaa madarakani kwa muda mrefu kwani ingepinduliwa na yeye angeiongoza serikali inayofuata. Jean alimhakikishia kuwa serikali ya Ufaransa isingeiruhusu serikali ya RPF ikae madarakani kwani viongozi wake walikuwa na mwelekeo wa Kiingereza kwa kukaa kwao Uganda na hivyo wangeathiri nguvu (influence) ya Ufaransa ndani ya Rwanda kitu ambacho Ufaransa isingekiruhusu kabisa. Kwa hiyo kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya MNRD waliokimbia na watu wengine walio ndani kama Col. Gatabazi kwa msaada wa serikali ya Ufaransa. Jean alikuwa anatayarisha jeshi la kuivamia tena Rwanda na kuchukua madaraka toka kwa RPF. Kwa hiyo, Col. Gatabazi alikuwa anajitayarisha kuwaggeuka wenzake mara wakati wa kufanya hivyo utakapofika.


Col. Gatabazi alikuwa anataka kutoka nyumbani kwenda ofisini kwake, Merridian Hotel, ambako ndiko ofisi zake zilikuwa kwani ndiye aliyekuwa anashughulikia uratibu wa shughuli zote za vikosi mbalimbali vya jeshi la RPF na kuripoti kwa mkuu wa majeshi.


Simu ililia. Hallo Col. Gatabazi?".


"Jean".


"Mbona leo unanipigia simu saa hizi? Saa zetu unazijuwa", Col. Gatabazi aliuliza.


"Kuna dharura", Jean alijibu na kumweleza juu ya Willy Gamba na athari za kuwa kwake Kigali.


"Hivyo ni vizuri hiyo ndege yake ingetunguliwa ikiwa hewani iwe mwisho wa tatizo la huyu mtu maana toka jana anatusumbua, nafikiri hiyo ndio njia rahisi", Jean alimalizia.


"Si Tanzania italalamika sana na kwa sasa hivi serikali ya RPF inataka sana kueleweka vizuri, hasa kwa serikali kama ya Tanzania", Col. Gatabazi alijibu kwa njia ya kuuliza swali.


"Usijali, Tanzania inaunga mkono kwa kusema hiyo ndege iliruka anga zetu bila ruhusa hata haikutoa habari huko Tanzania kama ilikuwa inakuja Kigali. Hilo niachie mimi na wewe utasikia itakavyokuwa maana utacheka", Jean alijibu.


"Basi ngoja niwahi kwani watatua kwenye dakika thelathini zijazo kutokana na maelezo yako ya saa walizoondoka mjini Mwanza".


"Asante, kwa heri, ila nipigie simu baada ya tukio".


"Sawa", Col. Gatabazi alijibu.
 
KAZI IMEANZA


IV


Ndege ya Chama Cha Msalaba Mwekundu ilitua kwenye uwanja wa ndege wa Kayibanda mjini Kigali yapata saa nne kamili. Willy Gamba alichukua mkoba wake na kutelemka.


"Asante", Willy alimshukuru rubani na kumpa dola mia za kimarekani.


"Asante sana mzee", yule rubani alishukuru na kufunga mlango tayari kwa kuruka tena.


Willy alikwenda moja kwa moja kwenye jengo la uwanja wa ndege na kuelekea Uhamiaji. Ulinzi uwanjani ulikuwa bado mkali lakini kwa sababu alikuja kwa ndege ya Chama Cha Msalaba Mwekundu na alikuwa amefanyiwa mpango na rafiki yake Dar es Salaam aje apokelewe na mmoja wa maafisa wa Msalaba Mwekundu walioko Kigali, yeye akiwa kama Afisa wa habari wa Msalaba Mwekundu kimataifa na ndivyo Chifu alivyomtayarishia pasipoti aliyoikuta nyumbani, taratibu zake pale uwanja wa ndege zilikwenda haraka bila kipingamizi chochote.


Katika pasipoti yake hii jina lake lilikuwa George Mambo.


Alipojitokeza tu nje, alimkuta mwenyeji wake aliyekuwa amevaa beji ya Msalaba Mwekundu na kwa vile na yeye toka alipotua tu aliweka beji aliyokuwa amepewa na Msalaba Mwekundu wakatambuana mara moja.


"Bwana George Mambo natumai", yule mwenyeji wake alisema huku akitoa mkono wa salamu.


"Ndio mimi. Habari zako", Willy alijibu na kusalimu.


"Nzuri, mimi naitwa Vicent Nyemazi, ni afisa wa habari hapa, na mimi ni Mhutu ila mimi siyo Mhutu mwenye siasa kali", Vicent alijibu huku akitabasamu.


"Vizuri sana na pole kwa yote yaliyotokea hapa nchini kwenu".


"Asante sana, ndio hali ya dunia. Gari nimeegesha hapo mbele", Vicent alieleza.


"Mkahawa wa hapa umefunguliwa?", Willy aliuliza.


"Ndio, uko wazi".


"Unajuwa nimeondoka asubuhi sana, sijanywa hata chai na ndege zetu kama unavyojuwa si kama ndege za abiria, hamna chochote hata kikombe cha chai", Willy alijibu huku akiangalia saa yake.


"Sawa, twende hapa kuna mkahawa mzuri, na hali imeanza kurudi kama zamani, hivyo vitu vingi vinaendelea kama kawaida.


Walipanda juu kwenye mkahawa na willy aliagiza kahawa na kipande cha mkate na Vicent akaagiza kahawa peke yake. Willy aliangalia saa yake kwa chati kabisa, akajuwa ile ndege ya Tanzanair ilikuwa karibu kutua, na alitaka tu kuona kama kungeweza kuwa na fununu za kuja kwake. Hii ilikuwa hadhari tu kwani aliamini hakuna mtu ambaye angeweza kujua kuwa anakuja kwa jinsi alivyokuwa ameondoka Dar es Salaam kisirisiri.


"Ah, vipi hali ya huko Ngara, nasikia hali ya wakimbizi ni mbaya sana, yaani chakula, maji na madawa ni taabu", Vicent aliuliza.


"Ni kweli hali ni mbaya, jumuiya ya kimataifa inajaribu kusaidia lakini wakimbizi ni wengi mno. Fikiria watu kama wa mji huu mnamo wiki moja watengeneze mji mwingine ambao haukuwepo kabisa, ambako ni porini tu hakuna huduma za kijamii za aina...". Kabla Willy hajamaliza kueleza mlio mkubwa ulitokea na mara ukatokea mlipuko. Willy na Vicent walikimbilia dirishani kuangalia kwenye uwanja wa ndege ambako ndiko mlipuko ulikotokea. Kwenye barabara zinakoondokea na kutua ndege wakaona vipande vya ndege vimesambaa na kuwaka moto.


"Kazi imeanza", Willy alisema na kumvuta Vicent mkono. Wakakimbilia chini kuangalia kwani vishindo vya kukimbia uwanjani vilisikika kutoka kila pahala.


Walipofika chini na kuelekea uwanjani walikuta magari ya jeshi aina ya Landrover yakiwa yamejaa askari yakielekea pale mabaki ya ndege yalipoangukia na wengine wakija huku kwenye jengo la uwanja ili kuzuia watu wasiende kule uwanjani.


Vicent na Willy walionyesha beji zao za Msalaba Mwekundu wakiomba wafike kwenye tukio lakini walikataliwa na askari ambao kwa sasa walikuwa wamechachamaa. Willy aligundua kuwa kumbe walishajua atafika na maskini yule rubani na afisa wa Msalaba Mwekundu waliuawa kwa kufikiri ni yeye. Willy alimshukuru Mungu kwa kumfanya afikiri na kufanya kama alivyofanya.


Kweli kama Msoke alivyosema, kazi hii tayari ilionyesha kuwa ni ya hatari. Ila kilichomshangaza Willy ni jinsi yule mtu aliyeshambulia ndege ya Tanzanair alivyojuwa kuwa yeye angekuwemo mle ndani ya ile ndege. Hii ilionyesha kuwa kati ya wale maafisa wa PAM miongoni mwao kulikuwa na msaliti, lakini kwa sasa hakukuwa na haja ya kufikiria hicho ila kufanya kilichomleta Kigali. Huyu msaliti angetafutwa baadaye. Jinsi ile ndege ilivyokuwa imepigwa na kombora. Willy alijua kabisa kuwa hakuna mabaki ya binadamu ambayo yangeweza kutambuliwa, kwani kombora lililotumika lilikuwa kubwa wakati ndege yenyewe ilikuwa ndogo.


"Twende zetu, nipeleke hotelini, acha wanajeshi wafanye kazi yao", Willy alimvuta Vicent wakaondoka huku wakisesera kuelekea kwenye gari la Vicent.


"Kwanini wameipiga ile ndege?", Vicent aliuliza huku akifungua mlango wa gari.


"Huenda ilikuwa na hatari, bado unajuwa mambo hayajatengamaa hapa", Willy alijibu.


"Unafikia hoteli gani?".


"Nafikiri jaribu Meridian Hotel kama kuna nafasi", Willy alijibu na kuikacha Hotel Des Mille Collines aliyokuwa amepangiwa na rafiki za Musoke, kwani sasa hakukuwa tena na kumwamini mtu yeyote kwa vile hakujuwa nani alikuwa ametoa amri ya kupigwa kombora ndege aliyopaswa kuwemo na huyo mtu alikuwa anajuwa habari kiasi gani kumhusu yeye Willy.


"Sawa, pale hotelini wanatua na watu wetu kutoka mataifa ya nje wako pale. Na vilevile pana usalama maana ofisi zingine za jeshi ziko pale, na maafisa wengine wa jeshi wanakaa pale", Vicent alimweleza Willy. Wakati wakielekea Meridian Hotel walikutana na magari madogo ya jeshi, kama matatu, yakielekea uwanja wa ndege. Willy aliona wengi walikuwa maofisa wa vyeo vya juu na akahisi walikuwa wanakwenda kutathimini tukio lililotokea.


Walipofika Meridian walikuwa watu wako vikundi vikundi wakizungumza, bila saka walikuwa wamepata habari za tukio la uwanja wa ndege. Vicent likwenda mapokezi na kuzungumza na mmoja wa wafanyakazi wa pale ambaye alionekana kumfahamu sana, na baada ya muda kidogo Willy aliitwa kujaza fomu za kupatiwa chumba. Baada ya kupewa funguo alichukua mkoba wake na vicent akamweleza kuwa atamsubiri kwenye mkahawa wa hoteli.


"Si utataka twende ofisini?", Vicent aliuliza.


"Bila shaka", Willy alijibu.


"Basi utanikuta hapo kwenye mkahawa".


"Asante", Willy alijibu na kuelekea kwenye ngazi kwani alikuwa ameelezwa lifti zilikuwa hazifanyi kazi. Alikuwa amepewa chumba namba 412, ghorofa ya nne.


V
Baada ya Col. Gatabazi kuhakikisha kuwa hakuna kitu kilichobaki ndani ya ndege na ndege yenyewe, alielekea nyumbani kwake ili akampashe habari Jean. Alipompata Jean alimweleza. "Kazi tayari, mtu wako hata mfupa haukuonekana, kawa hewa".


"Safi sana, hakika mimi hupenda mtu wa vitendo na siyo maneno", Jean alijibu.


"Lililobaki ni la kujieleza kwanini tumeipiga hiyo ndege, lakini tayari mkuu nimemwandikia taarifa safi ambayo hawezi kuwa na mashaka nayo. Wasiwasi wangu Tanzania tu", Col. Gatabazi alieleza.


"Nilikwambia Tanzania niachie mimi. Tuongee jioni. Kama kawaida mzigo mwingine unatua leo, na ni shehena kubwa", Jean alijibu na kabla Col. Gatabazi hajajibu alikata simu.


Baada ya kukata simu ya Col. Gatabazi. Jean alimpigia simu JKS, Dar es Salaam. JKS, aliyekuwa na wasiwasi mkubwa aliipokea simu haraka ilipolia. "Nani".


"Jean hapa. Kigali Bingo!!, mambo safi".
 
Kazi nzuri TECHMAN
Pale tunapokwama kuleta muendelezo ndani ya wakati ni jambo jema kuona wapo wapo waliotayari kuendeleza! Big up tena mkuu. Tupo pamoja utakapokwama tutalisongesha
 
Last edited by a moderator:

MIGUU YA NYOKA

Willy alipowasili kwa Col. Thomas Rwivanga, alimkuta anamsubiri. willy alikuwa amemweleza kuwa angekuwa anaendesha gari la Msalaba Mwekundu na angekuja peke yake bila Vicent. Col. Rwivanga alikuwa amemweleza njia ya kupita mpaka huko nyumbani kwake, Kimihurura.

Col. Rwivanga aliposikia mwungurumo wa gari alitoka nje na kwenda kumpokea Willy.

"Habari yako?", Col. Rwivanga alimsalimia Willy huku akimpa mkono.

"Safi, na wewe?", Willy alimjibu.

"Safi kabisa, nafurahi sana kuonana na wewe, Mzee Musoke amenieleza habari zako, nami nilikuwa na shauku kubwa ya kukutana nawe. Karibu ndani", Col. Rwivanga alimkaribisha Willy.

"Asante sana, nimekaribia", Willy alijibu huku akiingia ndani na kuketi.

"Nikupe kinywaji gani?"

"Klabu soda inatosha", Willy alijibu.

Col. Rwivanga alileta Klabu soda mbili na kuzifungua, wakaanza kunywa.

"Ehee, habari ya maisha?", Col. Rwivanga aliuliza.

"Safi, naamini Mzee Musoke amekueleza kwanini niko hapa".

"Ndio amenieleza".

"Imebidi nikuone mapema maana kuna jambo lililotokea ambalo linaonyesha kuwa katika uongozi wenu kuna mtu aliyejuwa kuwa mimi nimo ndeani ya ile ndege iliyotunguliwa leo asubuhi, akiwa na nia ya kuniua, bahati nzuri sikuwemo ila nilitakiwa kuwemo kwenye ndege hiyo. Na ninafikiri yeyote yule aliyeagiza hiyo ndege itunguliwe anaamini kuwa mimi sasa ni marehemu", Willy alimweleza Col. Rwivanga ambaye wakati huo alikuwa akimwangalia kwa mshangao mkubwa.

"Hivi swala unaloijia hapa ni nyeti kiasi hicho, mpaka wanataka kukuua! Mimi Mzee Musoke aliponieleza, sikutegemea kama kunaweza kuwa na hatari yoyote, maana wewe unakuja kutathimini tu hali ya mambo yalivyotokea mpaka kufikia watu wengi namna ile kuuawa. Lakini sasa inaonekana kuja kwako kumetia watu wasiwasi na wameamua kukumaliza kabisa hata hujaanza huo uchunguzi. Ndugu Gamba hii inaonekana kuna jambo kubwa ambalo hata sisi hatulifahamu. Hii ni hatari na ni hatari kubwa", Col. Rwivanga alijibu.

"Je, unaweza kujuwa ni nani au ni vipi ile ndege ilitunguliwa?, Huenda tukaanzia hapo ndipo tutajuwa hasa ni nani anahusika na kwa sababu gani?", willy aliuliza.

"Taarifa niliyopata kuhusu tukio hilo kwenye kikao cha makamanda wa jeshi, ambayo imetolewa na Col. Gatabazi, ambaye ndiye mkuu wa utawala jeshini, inasema ndege hiyo ilipoitwa kwenye rada ijitambulishe haikufanya hivyo. Kwa hiyo Luteni Silasi Biniga, ambaye ndiye anaongoza wanajeshi wanaolinda uwanja alimtaarifu Meja Juvenal Mukama, Mkuu wa Kikosi cha Mizinga kinacholinda mji huu, ambaye alitoa amri kuwa kama inakaribia kutua na bado haitoi taarifa yoyote itunguliwe. Na ndivyo ilivyofanyika. Baada ya kujuwa kuwa ilikuwa ndege ya kukodi ya kampuni ya kukodisha ndege ya Kitanzania, habari zilipelekwa Dar es Salaam, na habari tulizopata toka Wizara ya mambo ya Nje ya Tanzania ni kwamba ndege hiyo ilikuwa imekodiwa na mtu mmoja kwa jina la Juma Omari aliyejitambulisha kama mwandishi wa habari na masuala yote ya kupata vibali vya kutua alifanya mwenyewe. Hivyo, serikali ya Tanzania inaunga mkono kutunguliwa kwa ndege hiyo ambayo imeingia anga ya watu bila kibali wala kujitambulisha na huku rubani na kampuni hiyo ikijuwa hali ya hatari iliyomo nchini Rwanda. Taarifa hiyo tumeipata jioni hii na serikali ya Tanzania imezidi kusema itaichukulia hatua kampuni hiyo ya ndege kwani inaweza kuwa inatumiwa na maadui wa Rwanda na kuweza kuleta uhusiano mbaya kati ya nchi zetu rafiki", Col. Rwivanga alieleza na ukawa ni wakati wa Willy kushangazwa na maelezo hayo.

"Rafiki yangu, hapa kuna jambo kubwa maana sababu ya kutunguliwa ndege hii ni moja tu, ambayo ni kutaka kuniua mimi. Lakini sasa maelezo ya makamanda wenu. Col. Gatabazi na maelezo kutoka Dar es Salaam, yamenichanganya kabisa na nahisi kuna kitu kikubwa tusichokijua", Willy alijibu.

"Sasa tufanye nini?", Col. Rwivanga alimwuliza.

"Kwanza, nataka aliyetaka kuniua aendelee kufikiri kwamba ameniua. Pili, huenda huyu Lt. Silasi Biniga anaweza akawa na habari zinazoweza kutusaidia kufumbua hiki kitendawili hivyo anafaa kuonwa na kuulizwa", Willy alijibu.

"Basi niache huyu mimi nitamwuliza", Col. Rwivanga alijibu.

"Hapana, niachie mimi, swala hili linaweza kuwa vilevile linaugusa uongozi wenu. Mimi nikiwa mtu baki naweza kupata ukweli bila kuleta kasheshe sasa hivi. Ni lazima tujitahidi tujue undani wa jambo hili maana ni zito. Naomba tu unieleze huyu Luteni Biniga anakaa wapi nami nitaenda kumwona", Willy alijibu.

"Inaweza kuwa hatari kwako, unajuwa hawa watu ni wanajeshi safi", Col. Rwivanga alimwasa Willy.

"Usijali, hatari ndio jina la kazi yangu", Willy alijibu.

Wote wakacheka, maana Musoke alikwishampa Col. Rwivanga maelezo kamilifu kuhusu Willy na uwezo wake.

"Sawa, huyu Luteni Biniga anakaa barabara ya tatu tu kutoka hapa kwangu, sehemu hiihii ya Kamihurura". Kisha akamweleza mtaa na nyumba ilipo.

"Sasa hivi naanza kushangaa, wakati wanajeshi wa cheo chake wengi bado wako kambini na wengine wako huko Ndera ambako ndiko kuna nyumba za maofisa wa ngazi ya chini yeye anakaa sehemu ambayo wanakaa maofisa wa ngazi za juu. Sijui huenda ikawa tu bahati yake", Col. Rwivanga alisema kama vile anajisemea mwenyewe.

"Nafikiri nikionana naye nitajua. Naona niende kama saa tatu hivi. Nitaacha gari hapa na kwenda kwa miguu", Willy alisema.

"Uamzi wako. Kwa vile bado kuna muda mpaka saa tatu ngoja nitengeneze chakula kidogo", Col. Rwivanga alieleza.


"Na mimi nitakusaidia kupika, kupika ni moja ya starehe zangu", Willy alieleza huku wakiinuka kuelekea jikoni.
 
Back
Top Bottom