kidi kudi
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 2,419
- 1,981
- Thread starter
- #21
UCHU
SURA YA KWANZA
ARUSHA II
Musoke aliangalia ndani ya kitabu chake cha
simu, akaipata namba ya Chifu ya nyumbani na
kumpigia simu.
Alipoangalia saa ilikuwa yapata saa tano usiku.
"Hallo", alisikia sauti ya Chifu, ikiwa na nguvu
kama ya kijana wa miaka thelathini.
"Mzee, shikamoo, Musoke hapa".
"Marahaba Musoke, habari za siku nyingi, nini
kinakufaya unipigie simu saa hizi?".
"Umekasirika Mzee?".
"Hapana, shauku".
"Bado tu uko vilevile, utafikiri hujastaafu?".
"Mwili ndio unastaafu lakini nafsi huwa haistaafu
maana nafsi haizeeki isipokuwa mwili".
"Ahsante nitazingatia, huo ushauri, maana nami
naitwa mzee sasa na nafsi yangu imeanza
kukubali".
"Hapana usiruhusu kabisa. Haya, lete habari
zinazokufanya umpigie simu mzee kama mimi
saa hizi kwanza uko wapi?".
"Niko Arusha".
"Aha, nilifikiri uko Kampala".
"Niko Arusha, Chifu". Ilikuwa ukimwita Chifu
mara moja anajuwa kazi imeanza.
"Haya lete hizo habari".
Musoke alimweleza habari zote toka mwanzo
mpaka mwisho. Pia alimweleza jinsi idara za
upelelezi za serikali zilivyokataa kumsaidia kwa
kitu nyeti kama hiki.
"Pole sana", Chifu alimjibu baada ya kuyasikia
yote.
"Tatizo lako ni kubwa, la kuangaliwa kwa makini
sana. Mimi mwenyewe nimekuwa nikishangazwa
sana na mambo yalivyo Rwanda. Enzi zetu sisi
tusingeruhusu hali kama hiyo itokee, wewe
mwenyewe unajuwa msimamo wetu ulivyokuwa".
"Ndio Chifu, lakini serikali zetu za sasa kila mtu
eti na nchi yake, eti hiyo ndio wanaiita
demokrasia", Musoke alijibu.
Wakati wanazungumza kwenye simu mawazo ya
Chifu yalikuwa yanakwenda kama Kompyuta
kutafuta nani angeweza kumsaidia Musoke na
Chama chake cha PAM katika azma yao ya
kutafuta kiini cha matatizo ya Rwanda. Chifu
mwenyewe alikuwa mwana PAM, na aliamini
Umoja katika Afrika.
"Jack", Musoke alishituka kusikia Chifu akimuita
kwa jina lake la kwanza. Hii ilikuwa na maana
amekwisha pata jawabu. "Nafikiri nitakupatia
ufumbuzi wa tatizo lako. Mtu mmoja tu katika
Afrika hii ambaye anaweza kuifanya kazi yako.
Hivi sasa ameacha kazi za kiserikali maana
ameowa na anafanya shughuli zake. Lakini
kutokana na imani yake katika Umoja wa Afrika
anaweza akaifanya kazi hii, huna haja ya kuwa
na kikosi, maana yeye pekee ni kikosi.
Nitazungumza naye, nipe namba yako ya simu
na chumba chako; nitakupigia simu kesho
asubuhi".
"Ahsante Chifu, nilijuwa wewe ndiye
utakayenimalizia matatizo yangu", Musoke
alijibu kisha akampa namba ya simu ya pale
hotelini na namba ya chumba. Alipomaliza tu
akasikia simu ikikatwa. Akajuwa tayari Mzee
yuko kazini.
Chifu alipokata simu ya Musoke, alipiga simu
nyingine.
"Hallo".
"Chifu".
"Aha shikamoo".
"Marahaba, tuonane kusho asubuhi,
tutastafutahi pamoja pale Kili, kama kawaida.
"Sawa Mzee, kesho", Chifu alijibiwa.
"Kesho, ahsante", Chifu alijibu na kukata simu.
ITAENDELEA...
SURA YA KWANZA
ARUSHA II
Musoke aliangalia ndani ya kitabu chake cha
simu, akaipata namba ya Chifu ya nyumbani na
kumpigia simu.
Alipoangalia saa ilikuwa yapata saa tano usiku.
"Hallo", alisikia sauti ya Chifu, ikiwa na nguvu
kama ya kijana wa miaka thelathini.
"Mzee, shikamoo, Musoke hapa".
"Marahaba Musoke, habari za siku nyingi, nini
kinakufaya unipigie simu saa hizi?".
"Umekasirika Mzee?".
"Hapana, shauku".
"Bado tu uko vilevile, utafikiri hujastaafu?".
"Mwili ndio unastaafu lakini nafsi huwa haistaafu
maana nafsi haizeeki isipokuwa mwili".
"Ahsante nitazingatia, huo ushauri, maana nami
naitwa mzee sasa na nafsi yangu imeanza
kukubali".
"Hapana usiruhusu kabisa. Haya, lete habari
zinazokufanya umpigie simu mzee kama mimi
saa hizi kwanza uko wapi?".
"Niko Arusha".
"Aha, nilifikiri uko Kampala".
"Niko Arusha, Chifu". Ilikuwa ukimwita Chifu
mara moja anajuwa kazi imeanza.
"Haya lete hizo habari".
Musoke alimweleza habari zote toka mwanzo
mpaka mwisho. Pia alimweleza jinsi idara za
upelelezi za serikali zilivyokataa kumsaidia kwa
kitu nyeti kama hiki.
"Pole sana", Chifu alimjibu baada ya kuyasikia
yote.
"Tatizo lako ni kubwa, la kuangaliwa kwa makini
sana. Mimi mwenyewe nimekuwa nikishangazwa
sana na mambo yalivyo Rwanda. Enzi zetu sisi
tusingeruhusu hali kama hiyo itokee, wewe
mwenyewe unajuwa msimamo wetu ulivyokuwa".
"Ndio Chifu, lakini serikali zetu za sasa kila mtu
eti na nchi yake, eti hiyo ndio wanaiita
demokrasia", Musoke alijibu.
Wakati wanazungumza kwenye simu mawazo ya
Chifu yalikuwa yanakwenda kama Kompyuta
kutafuta nani angeweza kumsaidia Musoke na
Chama chake cha PAM katika azma yao ya
kutafuta kiini cha matatizo ya Rwanda. Chifu
mwenyewe alikuwa mwana PAM, na aliamini
Umoja katika Afrika.
"Jack", Musoke alishituka kusikia Chifu akimuita
kwa jina lake la kwanza. Hii ilikuwa na maana
amekwisha pata jawabu. "Nafikiri nitakupatia
ufumbuzi wa tatizo lako. Mtu mmoja tu katika
Afrika hii ambaye anaweza kuifanya kazi yako.
Hivi sasa ameacha kazi za kiserikali maana
ameowa na anafanya shughuli zake. Lakini
kutokana na imani yake katika Umoja wa Afrika
anaweza akaifanya kazi hii, huna haja ya kuwa
na kikosi, maana yeye pekee ni kikosi.
Nitazungumza naye, nipe namba yako ya simu
na chumba chako; nitakupigia simu kesho
asubuhi".
"Ahsante Chifu, nilijuwa wewe ndiye
utakayenimalizia matatizo yangu", Musoke
alijibu kisha akampa namba ya simu ya pale
hotelini na namba ya chumba. Alipomaliza tu
akasikia simu ikikatwa. Akajuwa tayari Mzee
yuko kazini.
Chifu alipokata simu ya Musoke, alipiga simu
nyingine.
"Hallo".
"Chifu".
"Aha shikamoo".
"Marahaba, tuonane kusho asubuhi,
tutastafutahi pamoja pale Kili, kama kawaida.
"Sawa Mzee, kesho", Chifu alijibiwa.
"Kesho, ahsante", Chifu alijibu na kukata simu.
ITAENDELEA...