SURA YA TATU
III
Joram alifika chumbani kwake baada ya dakika
kadhaa. Akiwa mchovu, huku jicho lake moja
likiwa limevimba kutokana na pambano lake na
Chonde, alipita moja kwa moja hadi bafuni ili
ayaepuke maswali ya Nuru. Huko ndani alioga
vizuri, akaisafisha damu yote na kushevu
kikamilifu; kisha taratibu akarudi chumbani
ambako macho yake yalivutwa na hali ya vurugu
lililokuwa limetokea hapo.
Alitazama vitanda vyote na kutoiona dalili ya
kuwepo Nuru. Akaenda mezani ambako
hakushangaa kukuta ujumbe ule ukiwa juu ya
karatasi yenye damu damu. Aliusoma kwa makini,
akiuchunguza mwandiko huo ambao ulikorogwa
katika hali ya kupoteza uhalisi wake. Akatikisa
kichwa na kutokwa na tabasamu jembamba.
Usiku huo alilala huku akiwa amelisahau
tabasamu hilo katika uso wake.
ITAENDELEA