THE FOOTBALL
Mtunzi .Patrick Ck
Sehemu 3
OFISI ZA USALAMA WA TAIFA
– DAR ES SALAAM
Shughuli ziliendelea kama
kawaida katika jengo hili la ofisi za
usalama wa taifa.Baada ya kurejea
toka uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Julius Nyerere
kumuaga rais,mkurugenzi wa
idara ya usalama wa taifa George
Mzabwa akahudhuria vikao viwili
vya kazi halafu akaenda kujifungia
ofisini kwake.Alijiegemeza kitini
na kuzama mawazoni.Aliwaza sana
na halafu akachukua karatasi
akaanza kuandika.Alipomaliza
akasoma kile alichokiandika
akaridhika na kuiweka karatasi ilekatika bahasha na juu ya bahasha
ile akaandika
TO MADAM PRESIDENT.Akaiweka
mezani barua ile halafu akafunga
mlango kwa funguo na kusimama
kati kati ya ofisi.Akaitazama ofisi
yake ,akatoa bastora na kuitazama
kwa uchungu
Wafanyakazi wa ofisi hii ya
usalama wa taifa wakiwa
wanaendelea na shughuli zao za
kawaida walistushwa na mlio wa
risasi.Shughuli zikasimama ghafla
na wote wakijiuliza nini
kimetokea.Tahadhari zikaanza
kuchukuliwa haraka kubaini risasi
ile imelia toka wapi ndani ya jengo
lile.Wakati wakijiuliza huku kila
mmoja akiwa katika tahadhari kubwa na ulinzi ukiwa
umeimarishwa katika sehemu zote
za kuingilia na kutokea,Stella
katibu muhtasi wa George Mzabwa
alishuka ngazi huku akikimbia na
kupiga kelele.Akatoa taarifa
kwamba amesikia mlio wa risasi
katika ofisi ya George.Haraka
haraka watu wakakimbilia ofisini
kwa George na kujaribu kugonga
mlango lakini hakukuwa na mtu
yeyote aliyeitikia toka
ndani,wakapiga simu ya George
ikaita bila kupokelewa hivyo
ikawalazimu kuuvunja mlango na
kuingia ndani wakamkuta George
Mzabwa amelala sakafuni damu
ikimvuja na pembeni yake
kulikuwa na bastora.Hakuwa na uhai na ubongo wake
ulisambaa.Alikuwa amejipiga
risasi kichwani.Uchunguzi
ukafanyika ili kuona kama
shambulio lile lilifanywa na mtu
kutokea nje lakini hakukuwa na
dalili zozote za kuonyesha kama
George alishambuliwa kutokea
nje.Hili lilikuwa ni tukio
lililomshangaza kila
mmoja.Hakuna aliyefahamu
sababu ya George kujiua kwani
muda mfupi uliopita alikuwa na
uso wenye furaha kabisa na
hakuonyesha kama ana tatizo
lolote.Juu ya meza yake kulikutwa
barua aliyomuandikia rais muda
mfupi kabla ya kifo chake. Polisi walitaarifiwa wakafika
kwa haraka na baada ya
kujiridhisha kwamba George
alijiua mwenyewe wakaondoka na
mwili wake kuupeleka hospitali
kwa ajili ya kuuhifadhi na taratibu
nyingine kabla ya kuukabidhi kwa
familia yake
************
Dr Vivian akiwa
amejipumzika katika chumba
chake huku dege likiendelea
kupasua anga kuelekea
Marekani,simu iliyomo mle
chumbani inayotumia mtandao wa
intanet ikaita.Akainua mkono wa
simu na kuipokea Hallow” akasema Dr Vivian
“Madam president pole na
safari ni mimi Dr Makame”
akasema makamu wa rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
“Ahsante Dr Makame.Sisi tuko
angani tunaendelea na
safari.Mnaendeleaje huko?
“Habari za huku si njema
sana.Kuna tukio limetokea ambalo
nimeona ni vyema nikikujulisha
mapema”
“Nini kimetokea Dr makame?
“George Mzabwa mkurugenzi
wa idara ya usalama wa taifa
amefariki dunia”
“George amefariki dunia?!! Dr
Vivian akastuka Ndiyo mheshimiwa
rais.Nimeletewa taarifa hizo na
nimezithibtisha kupitia inspekta
generali wa polisi” akasema Dr
makame na rais akavuta pumzi
ndefu
“Amefariki vipi?Amepata
ajali?
“Amejipiga risasi kichwani
mheshimiwa rais”
Uso wa Dr Vivian ulionyesha
mstuko mkubwa.Hakuwa
ametarajia kusikia habari kama ile
“Madam president” akaita
makamu wa rais baada ya kuona
kumekuwa kimya.
“Nimestushwa sana na taarifa
hizi.Imekuaje hadi George
akachukua maamuzi hayo magumu ya kujiua?akauliza Dr
Vivian
“Hilo ni jambo
linalomshangaza kila
mmoja.Hakuna aliyetegemea kama
angeweza kuchukua maamuzi
kama haya ya kujiua.Tulikuwa
wote uwanja wa ndege asubuhi
tukasalimiana na alikuwa vizuri
tu,hakuonyesha tatizo
lolote.Hatujui nini kilimsibu hadi
akachukua mamauzi haya,hata
hivyo kuna barua imekutwa
mezani kwake ambayo
amekuandikia wewe.Tunadhani
aliiandika muda mfupi kabla
hajajiua” Ameniandikia barua? Kuna
yeyote ameifungua na kuisoma?
Akauliza Dr Vivian
“Hapana madam president
hakuna aliyeifungua.Imefungwa
ndani ya bahasha”
“Good.Ihifadhi hadi
nitakaporejea”
“Sawa madam president”
“Jambo lingine,nataka
ufanyike uchunguzi kwa mara
nyingine wa kina kujiridhisha
kama kweli George Mzabwa
amejiua au kuna watu
waliomuua.Inashangaza sana kwa
mtu kama George kuchukua
maamuzi haya magumuSawa madam president
nitaelekeza hivyo.Nawatakieni
safari njema”
“Ahsante sana Dr Makame
kwa taarifa.Hakikisha uchunguzi
huo unafanyika haraka.Kuanzia
nyumbani kwake,ofisini kote
kupekuliwe ili sababu ya George
kujiua ijulikane” akasema Dr
Vivian na kukata simu
“George amejiua …” akasema
na kuzidi kushangaa
“Lakini kwa nini afanye hivi?
Kwa nini ajiue?Kwa nini iwe sasa?
Kuna kitu gani kimemkwaza
?akaendelea kujiuliza maswali
“Jambo hili linahitaji
uchunguzi wa kina kubaini sababu
ya kujiua.Nitaisoma hiyo barua aliyoniandikia kujua alichokisema
lakini nimestuka
sana,sikutegemea kama anaweza
akafanya jambo kama hili”
akawaza Dr Vivian
“Au yale maneno
niliyomwambia asubuhi pale
uwanja wa ndege yamemkwaza?
Nilimtaka nitakaporejea nikute
ripoti ya uchunguzi au nikute
barua yake ya kuachia nafasi
yake.Yawezekana amefikiria sana
na akaamua kujiua.Apumzike kwa
amani huko aliko kwani hata hivyo
alikuwa katika orodha ya viongozi
ambao utendaji wao wa kazi
haujaniridhisha.Nitatafuta mtu
mahiri na mchapakazi
atakayechukua nafasi yake na atakayekuwa tayari kufanya kazi
kwa kasi ninayoitaka.Kipimo cha
mtendaji ninayemtaka ni kutegua
kitendawili cha vifo vya wazazi
wangu.Haiwezekani mpaka leo hii
yapata miaka kumi suala hili
limeshindwa kupata
majibu.Limekuwa ni fumbo
lililoshindwa kufumbuliwa.Tuna
vyombo mahiri kabisa kwa
uchunguzi lakini kwa nini
wameshindwa kubaini nani
aliteketeza familia yangu?Halafu
kuna hili begi ambalo baba
alikuwa analibeba enzi za utawala
wa rais Anorld liko wapi? Lilipotea
rais Anorld alipofariki katika
ajali?Nahisi hivyo kwani hata rais
aliyefuata baada ya Anorld hakuwahi kuwa na lile begi ambalo
rais Anorld alikuwa anatembea
nalo kila aendako.Mfumo ule
uliigwa toka marekani ambao wao
ndani ya begi hilo wanaloliita
football kuna nuclea codes lakini
sisa hatuna nyuklia je kwa nini rais
Anold alikuwa anatembea na begi
lile kila aendako?Siri gani alikuwa
anatembea nayo?Swali lingine
ambalo bado mpaka leo sijapata
majibu yake ni je baba aliokoka
vipi toka katika ndege ile ya
rais?Maelezo aliyotoa baba
hayajawahi kuniingia akilini.Bado
naamini kuna vitu vinakosekana
katika maelezo yake aliyoyatoa
kwa vyombo vya uchunguzi baada
ya ajali.Kwa bahati mbaya nyumba yake iliungua moto muda mfupi
baada ya kufariki kwahiyo hakuna
mahala kokote tunakoweza kupata
taarifa zake zozote.Laiti
kungekuwa na nyaraka zake
zozote tungeweza kuzichambua na
kugundua kama kuna jambo
alikuwa analificha.Hili jambo kweli
ni fumbo gumu na ili kulifumbua
ninahitaji mtu jasiri na mahiri
ambaye anaweza kulishughulikia
jambo hili na kulipatia majibu.Kwa
miaka takribani miwili sasa tangu
nilipompa George alishughulikie
jambo hili hakuna majibu yoyote
na badala yake leo amejipiga risasi
na kufa.Ukiacha hii miaka miwili
niliyompa George,vyombo vya
uchunguzi vimelichunguza jambo hili kwa miaka zaidi ya kumi sasa
na mpaka leo hakuna majibu
yoyote.Kuna nini hapa?Hii
inanifanya nizidi kuamini kwamba
kuna kitu kimejificha katika jambo
hili na sintachoka hadi nihakikishe
nimeufahamu ukweli na wahusika
wanakamatwa na kufikishwa
mbele ya sheria” akawaza Dr
Vivian na kutoka mle chumbani
akamuita Edwin Swai mmoja kati
ya washauri watatu wa mambo ya
usalama wakaenda katika chumba
cha mazungumzo ya faragha
“Edwin kuna taarifa
nimeipokea muda mfupi uliopita
toka Dar es salaam ambayo si
nzuri.George Mzabwa amefariki
dunia” akasema Dr Vivian George amefariki dunia?Nini
kimemuua?Amepata ajali?Akauliza
Edwin naye akishangazwa na
taarifa zile
“Hajapata ajali amejiua kwa
kujipiga risasi”
“Amejipiga risasi?
“Ndiyo amejipiga risasi ofisini
kwake”
“Oh my God !! akasema Edwin
kwa masikitiko
“Inasikitisha lakini pia
inashangaza sana kwa maamuzi
haya aliyoamua kuyachukua
George.Mungu ampumzishe kwa
amani” akasema rais
“Amen” akajibu Edwin .
“Kufuatia tukio hilo nahitaji
kuiziba nafasi ya George hivyo nahitaji kumpata mtu mahiri sana
ambaye anaweza kuiongoza idara
ya usalama wa taifa kwa umahiri
mkubwa.Utendaji wa George
haukuwa umeniridhisha hata
kidogo na hata hivyo nilikuwa
katika mipango ya
kumuondoa.Wewe umekuwa
katika mambo haya ya usalama
kwa muda mrefu hivyo naamini
unawafahamu watu wengi wazuri
na wanafaa kuongoza idara ya
usalama wa taifa,ninakuomba
upendekeze watu watatu
unaowaamini na mimi nitachagua
mmoja” akasema Dr Vivian
Edwin akafikiri kwa muda
kisha akasema Sawa madam president
nitajitahidi kulifanyia kazi hilo
jambo kuanzia sasa na hadi
tutakaporejea Dar es salaam
nitakukabidhi mafaili ya watu
watatu nitakaowapendekeza kwa
ajili ya kuziba nafasi ya George
Mzabwa” akasema Edwin
“Nitashukuru sana.Zingatia
sihitaji tu mtu wa kuziba nafasi
bali nahitaji mtu ambaye
anafahamu nini anakifanya na
anayeweza kufanya kazi zake kwa
umahiri mkubwa sana.Idara ya
usalama wa taifa ni idara nyeti
kwa nchi hivyo hatuwezi kuiweka
kwa mtu kwa kuwa ni rafiki yetu
bali anatakiwa mtu mwenye uwezo wa kuiongoza kwa weledi
mkubwa” akasema Dr Vivian
“Nitalizingatia hilo
mheshimiwa rais katika
mapendekezo yangu
nitakayokupa” akasema Edwin
“Good.Jambo la pili nahitaji
kupata mpelelezi mahiri sana kuna
kazi nyeti nataka anisaidie
kuifanya.Naamini unaweza
ukamfahamu mpelelezi yoyote
mahiri sana hivyo nisaidie niweze
kumpata” akasema Dr Vivian
“Madam president tunao
wapelelezi wengi mahiri hapa
nchini.Wapo waliobobea katika
chunguzi za ndani,wapo wabobezi
katika chunguzi za kimataifa,tunao
wa kila aina.Sijui unahitaji mpelelezi mwenye sifa zipi?
Akauliza Edwin
“Edwin itakuwa vyema kama
nikikuweka wazi kuhusu jambo
ninalotaka kulichunguza.Nataka
kuchunguza na kuupata ukweli
kuhusiana na mauaji ya familia
yangu.Nadhani unafahamu kama
familia yangu iliuawa kwa siku
moja na na mpaka leo hii imepita
miaka zaidi ya kumi hakujawahi
kutolewa ripoti yoyote ya
uchunguzi na wala hakuna
aliyewahi kukamatwa kuhusiana
na mauaji yale.Jambo hili limebaki
kuwa kama fumbo gumu
kulifumbua.Jeshi la polisi,usalama
wa taifa wote wamelichunguza
jambo hili na mpaka leo hakuna ripoti yoyote.Nahitaji mtu wa
kuweza kulifumbua fumbo hili.Mtu
ambaye anaweza kutafuna mfupa
huu uliowashinda wengi.Hata
kama ni mtu wa kutoka nje niko
tayari kumlipa kiasi chochote cha
fedha ili mradi uwe na uhakika
kwamba ana uwezo wa kulifumbua
fumbo hili.Sitaki kuamini eti suala
hili limeshindwa kupatiwa
ufumbuzi hadi leo kama Marekani
walivyoshidwa hadi leo hii kupata
ufumbuzi kuhusiana na mauaji ya
wanamuziki Tupac na Christopher
Wallace.Bado nina matumaini
makubwa kwamba endapo
utafanyika uchunguzi wa kina
walioufanya mauaji haya lazima
watapatikana.Hayakuwa mauaji ya bahati mbaya waliotekeleza
mauaji yale walikuwa na sababu
zao na ninataka kufahamu hiyo
sababu ndiyo maana nahitaji mtu
mahiri sana ambaye nitampa kila
nyenzo atakayohitaji ili aweze
kufanikisha uchunguzi huu”
Akasema Dr Vivian.Edwin Swai
akakuna kichwa kidogo na kusema
“Mheshimiwa rais
nakubaliana nawe kwamba hili
suala la kifo cha kanali Sebastian
ni gumu na kama ulivyosema
uchunguzi wake umechukua zaidi
ya miaka kumi.Nadhani huu ni
uchunguzi uliokuwa mrefu zaidi
kuwahi kufanyika hapa nchini na
kama kwa muda huo wote
hawajapata wahusika basi ni wazi hawataweza kufanikiwa
kuwapata.Wazo la kumtafuta
mpelelezi ambaye ataweza
kulifumbua fumbo hili ni wazo zuri
na hata mimi nakubaliana nalo
lakini..” akasita kidogo
“Mbona umesita Edwin?
Akauliza akauliza Dr Vivian
“Kwa uchunguzi mkubwa
kama huu anahitaji mtu mwenye
umahiri wa pekee.Kwa wale
ninaowafahamu mimi sina uhakika
kama kuna mmoja wao anaweza
kuwa na sifa ya kulichunguza suala
hili.Kuna mtu mmoja ambaye yeye
anaweza kukusaidia katika jambo
hili.Anaitwa Meshack Jumbo.Huyu
mzee aliwahi kuiongoza idara ya
ujasusi wa kimataifa kwa miaka mingi na kwa ufanisi
mkubwa.Huyu nina imani anaweza
kukutafutia mtu sahihi
atakayekufaa” akasema Edwin
“Anapatikana wapi huyo
Meshack Jumbo?
“Anaishi Dr es
salaam.Amekwisha staafu kazi na
kwa sasa anapumzika
anajishughulisha na shughuli zake
ndogo ndogo.Ninaweza
kumuandaa ili mkutane muongee
tutakaporejea Dar es salaam”
Dr Vivian akafikiri kidogo na
kusema
“Sawa nahitaji kuonana
naye.Usimweleze chochote
kuhusiana na haya niliyokwambia.Nitamwambia mimi
mwenyewe”
“Sawa madam president”
akasema Edwin na kutoka mle
katika kile chumba.Rais
akazunguka zunguka ndegeni
kuzungumza na watu alioongozana
nao na mara akamuona Theresa
na kustuka kidogo
“Kuna tatizo Theresa,mbona
umejitenga huku peke
yako?akauliza
“Hapana dada Vivian.Sina
tatizo lolote ni uchovu tu” akajibu
Dr Vivian akaketi katika kiti cha
pembeni yake
“Nakufahamu vizuri
Theresa,kama kuna jambo
linakusumbua au limekukwaza huwa unapenda kujitenga na
kukaa peke yako.Niambie tafadhali
kama kuna tatizo lolote.Au
umekwazika na yale maneno
nilikwambia kuhusiana na ile
hotuba? Akauliza Dr Vivian
“Dada Vivi sina tatizo
lolote.Nimeamua nikae hapa
nitafakari mambo yangu .Kama
ningekuwa na tatizo ningekwisha
kueleza” akasema Theresa
“Bado tuna safari ya saa
kadhaa jitahidi basi upate nafasi ya
kutosha ya kupumzika.Tukifika
New York nitakuwa na mambo
mengi ya kufanya kwa hiyo nafasi
ya kupumzika ni finyu sana”
akasema Dr Vivian huku akiinuka na mara akakumbuka kitu na
kukaa
“Nimepewa taarifa na
makamu wa rais muda mfupi
uliopita George Mzabwa amefariki
dunia”
“George amefariki?! Theresa
akastuka
“Ndiyo kafariki.Amejipiga
risasi ofisini kwake”
Theresa akamtazama dada
yake kwa mshangao
“Kwa nini amefanya hivyo?
Kwa nini kachukua maamuzi hayo
ya kujitoa uhai? Akauliza
“Hakuna anayejua kwa nini
amechukua maamuzi
haya.Nimeagiza uchunguzi wa kina
ufanyike kubaini sababu ya yeye kujiua.Kwa upande mwingine
nahisi labda yale maneno
niliyomwambia pale uwanja wa
ndege wakati naondoka
yalimkwaza na akaamua kujiua
kwani nimeambiwa kuna barua
ameniandikia.Nahisi ndani ya
barua hiyo atakuwa ameeleza
sababu ya kuchukua maamuzi ya
kujiua” akasema Dr Vivian
akanyamaza kidogo na kusema
“Mkurugenzi wa idara ya
usalama wa taifa ni mtu mkubwa
na mpaka achukue maamuzi ya
kujiua lazima ipo sababu kubwa na
nzito.Hata hivyo tusubiri
uchunguzi ufanyike na tutafahamu
kwa nini alichukua maamuzi
yale.Jambo lingine nimeamua kumtafuta mpelelezi mwenye
uwezo mkubwa wa kulichunguza
suala la vifo vya familia
yetu.Lazima tuwapate wale
walioiteketeza familia yetu.Bado
sijakata tamaa na siwezi kuamini
eti jambo hili
limeshindikana.Nimeamua
kulivalia njuga mimi mwenyewe
hili jambo na nitahakikisha jambo
hili linafika mwisho.Nitakaporejea
Dar es salaam nitaonana na mtu
ambaye atanisaidia kumpata mtu
mpelelezi mahiri wa kuifanya kazi
hii” akasema Dr Vivian na kurejea
chumbani kwake
“Hili suala linazidi kuchukua
sura mpya na kuzidi
kuniogopesha.George Mzabwa kujitoa uhai si kwa bahati
mbaya.Kuna sababu kubwa.Hisia
za dada zinaweza kuwa kweli
kwamba yale maneno
aliyomueleza asubuhi wakati
anaondoka yamechangia kwa yeye
kujitoa uhai lakini kama suala la
kifo cha baba limesababisha ajitoe
uhai basi suala hili lina siri kubwa
ndani yake.Yawezekana labda
kuna kitu alikigundua na ambacho
hawezi kukiweka wazi na ndiyo
maana akachukua maamuzi ya
kujiua.Unapozungumzia kifo cha
baba unazungumzia pia football
lile begi alilokuwa analibeba na
ambalo mpaka leo hii hakuna
anayefahamu liko
wapi.Nilichonacho hapa ni huu msalaba pekee ambao alinitaka
nisiutoe shingoni mwangu hadi
nitakapomkabidhi rais wa wakati
huu na hakunipa maelezo yoyote
ya kina.Mwili
unanitetemeka,natamani
nimueleze dada Vivian ukweli
lakini naogopa” akawaza Theresa
“Ni mpelelezi gani huyo
anayeweza kulifumbua fumbo hili
lililowashidna hata idara ya
usalama wa taifa? Natamani
nimuone na nina imani hata yeye
mwenyewe hatafika popote
ataishia njiani.Mimi sintafumbua
mdomo wangu na nitaendela
kukaa na siri hii .Sitaki
kuhatarisha uhai wangu na wa
dada yangu Vivian.” Akaendelea kuwaza Theresa huku dege
likiendelea kupasua anga
NEW YORK - MAREKANI
Saa moja za jioni kwa saa za
Marekani ambayo ni saa tisa za
usiku kwa saa za Afrika
mashariki,dege la rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania liligusa
ardhi ya jiji la New york
Marekani.Dr Vivian na ujumbe
wake walipokewa kwa mujibu wa
itifaki na kupelekwa katika hoteli
waliyopangiwa kufikia ambako
rais na ujumbe wake wote
walifikia.Rais hakutaka hata
mmoja aliyeongozana naye
akafikie sehemu nyingine.Baada ya kuoga na kupumzika rais na
ujumbe wake wakapata chakula
cha usiku na kisha akawa na
mazungumzo na balozi wa
Tanzania nchini Marekani.Balozi
alimtaarifu rais kwamba wale
watu aliomtaarifu kwamba
walihitaji kuonana na kuzungumza
naye kuhusiana na mambo kadhaa
ya uwekezaji nchini Tanzania
watakuja usiku ule kuonana
naye.Rais hakuwa na kipingamizi
hivyo akakubali kuonana na hao
wawekezaji.
Wakati rais na balozi wa
Tanzania nchini marekani
wakiendelea na mazungumzo
wakafahamishwa kwamba kuna
watu wanne walikuwa wamefikakwa ajili ya kuuonana na
rais.Balozi akamtaarifu rais
kwamba watu aliokuwa
amemweleza wamefika na rais
akawakaribisha.Ulikuwa ni
ujumbe wa watu wanne.Kiongozi
wa ujumbe ule alijitambulisha
kama Jing wang halafu
akawatambulisha na wenzake
alioambatana nao ambao ni Ling
Huang,Peng Li na wote hawa
walitoka nchini China.Mwisho
akamtambulisha Kim Yung Su
mjumbe maalum wa rais wa Korea
Kaskazini .
Dr Vivian akatabasamu baada
ya Jing wang kufanya utambulisho
ule ingawa kwa ndani alistuka sana kusikia katika ujumbe ule
kuna mtu anatoka Korea kaskazini
“Karibu sana Jing wang na
ujumbe wako.Nafurahi kuonana
nanyi” akasema Dr Vivian
“Hata sisi tunafurahi kuonana
kuonana nawe mheshimiwa
rais.Kwa kuwa umechoka kwa
safari ndefu tutajitahidi
mazungumzo yetu yawe mafupi”
akasema Jing na kunyamaza baada
ya mlinzi kuingia mle ndani na
kumnong’oneza rais kitu
“Mr Nathan amewasili yuko
mapokezi” akasema yule mlinzi
kwa kunong’ona
“Apelekwe chumbani nina
mazungumzo na wageni wangu
sasa hivi” akasema rais na yule mlinzi akatoka na rais akamtaka
Jing aendelee
“mheshimiwa rais
,utatusamehe kwa kuingilia ratiba
yako kwa ujio huu usio rasmi
lakini kutokana na umuhimu wake
imetulazimu kumuomba balozi
wako atusaidie tuweze kuonana
nawe kwani tunafahamu utakuwa
na majukumu mengi hapa New
York na tusingeweza kupata nafasi
ya kuonana na
kuzungumza.Tunashukuru sana
kwa kukubali kuonana
nasi.Mheshimiwa rais sisi ni
wawakilishi wa wafanya biashara
wakubwa wenye makampuni
makubwa toka China.Nadhani
dunia nzima inafahamu juu ya urafiki wa China na Tanzania
lakini kwa usiku huu hatukuja
kuzungumzia juu ya China na
Tanzania bali tumemsindikiza
mwenzetu huyu ambaye ni mmoja
wa wajumbe wa kutoka Korea
Kaskazini wanaohudhuria
mkutano wa umoja wa mataifa
lakini yeye amekuja na salamu
maalum kutoka kwa rais wa Korea
Kaskazini.Tumeongozana naye
kwa sababu isingekuwa rahisi yeye
kuja kuonana nawe moja kwa moja
hata hivyo naomba niseme
machache .Nchi ya Korea Kaskazini
iko katika mageuzi makubwa ya
kiuchumi kwa sasa kwa hiyo
wanatafuta mashirikiano ya
kibiashara na mataifa mbali mbali na wanaelekeza nguvu kutafuta
masoko ya bidhaa zao,kununua
malighafi na kuwekeza barani
Afrika.Kutokana na Korea
kaskazini kufahamika sana katika
harakati zake za kijeshi nchi nyingi
zinasita au kutotaka kuwa na
mashirikiano yoyote na Korea
kaskazini hivyo kutulazimu China
kuwasaidia wenzetu
kuwaunganisha na marafiki zetu
mbali mbali duniani.Tanzania kwa
sasa inafanya mageuzi makubwa
ya kiuchumi na kwa kuwa ina sera
nzuri za kuvutia wawekezaji
,wafanya biashara kutoka Korea
kaskazini wamependa sana kuwa
na mashirikiano ya kibiashara na
Tanzania lakini nchi hizi hazina mashirikiano ya kibiashara kwa
sasa hivyo panahitajika sehemu ya
kuanzia na kikao hiki ni sehemu ya
kuanzia.Kwa hiyo mheshimiwa
rais naomba nisiwe msemaji mkuu
wa kikao hiki na nimuachie Kim
Yung Su ana mengi atakueleza
alichotumwa na kiongozi wake”
akasema Jing Wang
“Karibu sana Kim” akasema
Dr Vivian.
“Ahsante sana mheshimiwa
rais.Kama alivyosema Jing Wang
ninatokea Korea Kaskazini na
nimetumwa salamu maalum toka
kwa rais wetu.Kwanza anakupa
pongezi nyingi kwa mafanikio
makubwa ambayo Tanzania
imeyapata kwa muda mfupi uliokaa madarakani.Umeonyesha
dira na mfano kwa viongozi wengi
duniani.
Korea Kaskazini inajulikana
sana duniani kote kwa harakati
zake za kijeshi hasa msuguano kati
yake na Marekani unaotokana na
majaribio ya silaha kali.Msuguano
huu umesababisha lakini nchi
nyingi zisitake kuwa na
mashirikiano ya kibiashara kwa
kuogopa vikwazo toka nchi kubwa
zenye nguvu na tajiri
duniani.China imekuwa ni
mshirika mkubwa wa kibiashara
wa Korea Kaskazini.Zipo pia nchi
nyingine zinazofanya biashara na
sisi kama vile Russia.Kwa upande
wa Afrika kuna Burkina faso n.k.Kwa sasa nchi yetu iko katika
mageuzi makubwa ya
kiuchumi.Tunataka kuukuza
uchumi wetu uwe imara na ili
kufanikisha hilo imetulazimu
kubadili sera zetu za
uchumi.Tumeanza kukaribisha
wawekezaji toka nje jambo ambalo
halikuwepo hapo kabla.Kama
haitoshi wafanya biashara wetu
sasa wanaruhusiwa kutoka na
kwenda kufanya uwekezaji katika
nchi nyingine pia.Tumeona fursa
kubwa ya kuimarisha
mashirikiano zaidi na Tanzania
kwani tumegundua kuna fursa
nyingi za kuwekeza na nchi zote
mbili zikafaidika.Wafanya
biashara wa Korea Kaskazini wako tayari kuwekeza nchini Tanzania
katika viwanda vya nguo
vitakavyotumia pamba ya
wakulima wa Tanzania na hivyo
kuachana na kuagiza guo
zilizotumika toka Marekani na
mataifa ya ulaya.Hivi karibuni
Tanzania mmetangaza ugunduzi
mkubwa wa mafuta na gesi na
Korea kaskazini tunahitaji sana
mafuta safi ambayo kwa sasa
tunayapata kutoka China”
akanyamaza kidogo halafu
akasema
“Haya yote niliyoyaeleza ni
madogo lakini kubwa zaidi ni
kwamba Korea Kaskazini inataka
kufanya uwekezaji mkubwa katika
uchimbaji wa madini ya Uranium.Tanzania ina kiwango
kikubwa sana cha madini ya Urani
na mpaka sasa hakuna uwekezaji
wowote uliokwisha fanywa
kutokana vikwazo na masharti
yaliyowekwa na umoja wa mataifa
kuhusiana na uchumbaji wa
madini ya Urani.Tunahitaji sana
Urani kwa ajili ya kuzalisha nishati
ya umeme wa uhakika kwa
viwanda vyetu hivyo basi
tunahitaji madini haya kwa
kiwango kikubwa.Uwekezaji huu
mkubwa katika madini haya ya
Urani utaupaisha sana uchumi wa
Tanzania.Mheshimiwa rais kwa
kuwa muda wetu ni mfupi hizo
ndizo salamu nilizotumwa na
kiongozi wetu niziwasilishe kwako nina imani umezipokea na
kiongozi wetu angefurahi sana
kusikia jibu zuri toka kwako
kuhusiana na hizi salamu zake”
akasema Kim Yung Su.Dr Vivian
akawatazama wale watu mle ndani
kwa zamu halafu akasema
“Ahsanteni sana kwa kuja
kuniona.Ujumbe wenu umefika na
nimezipokea salamu.Tanzania na
china tuna urafiki mkubwa wa
tangu enzi za waasisi wa mataifa
yetu mawili.Biashara kati ya China
na Tanzani ni kubwa sana hivi sasa
na kiwango cha uwekezaji
kimeongezeka kwa nchi zote
mbili.Korea Kaskazini hatujawahi
kuwa ma mahusiano ya kibiashara
japokuwa tuna mahusiano ya kibalozi na balozi wa Korea
kaskazini yuko nchini Tanzania
japokuwa Tanzania hatuna balozi
wetu Korea kaskazini na hata
mahusiano ya Tanzania na Korea
kaskazini ni madogo sana siku
hizi.Ni mara ya kwanza kusikia
kwamba Korea kaskazini
wanataka kufanya biashara na
Tanzania.Hili si jambo rahisi
kulifanyia maamuzi kutokana na
sera na mwonekano wa nchi hii
machoni pa dunia.Japokuwa Korea
kaskazini wameamua kubadili
sera zao za kiuchumi lakini bado
inaendelea kuwekewa vikwazo
mbali mbali na umoja wa mataifa
kutokana na sera zake za
silaha.Sitaki kuingia katika mambo ya kisiasa ya nchi yako Kim bali
nataka nijielekeze katika hili suala
mlilolileta kwangu kutafuta
mashirikiano ya kibiashara na
uchumi.Hili ni wazo jema na mimi
binafsi nimelipokea.Tanzania vile
vile tuko katika mageuzi makubwa
ya kiuchumi kwa hiyo
tunakaribisha uwekezaji toka
sehemu mbali mbali ili mradi uwe
ni uwekezaji wenye kuleta faida
kwa nchi yangu na watu
wake.Tunalima pamba nyingi na
litakuwa jambo lenye manufaa
makubwa endapo tutapata
viwanda vingi vya nguo kutakuwa
na soko la uhakika kwa pamba ya
wakulima wetu na hivyo kuinua
kilimo cha pamba kwa hiyo wazo la kuwekeza katika viwanda vya
nguo ninalikaribisha kwani lina
tija kwa wakulima wangu na
ninataka Tanzania iwe kinara
katika uzalishaji wa nguo barani
Afrika.Kuhusu Tanzania kuiuzia
mafuta na gesi Korea Kaskazini
hilo halina tatizo kwani tuna
hazina kubwa sana ya mafuta na
gesi na bado tunaendelea
kugundua gesi zaidi katika maeneo
mbali mbali.Korea kaskazini
mmeonyesha nia ya kutaka
kuwekeza katika madini ya Urani.”
Akanyamaza kidogo na kuvuta
pumzi ndefu na kusema
“Ni kweli Tanzania tuna
karibu ratili milioni 70 za madini
ya Urani na bado utafiti unaendelea katika sehemu
nyingine mbali mbali na mwelekeo
unaonyesha kwamba kuna
uwezekano wa kupata kiasi
kingine kikubwa zaidi cha madini
ya Uranium.Pamoja na kuwa na
kiwango kikubwa cha madini ya
Urani lakini mpaka leo bado
hatujafanya uwekezaji wowote na
hatujanufaika chochote kwa
uwepo wa madini haya nchini
kwetu.Kumekuwa na shinikizo
kadhaa toka kwa umoja wa mataifa
na toka nchi tajiri kutishia
kutuwekea vikwazo vya kiuchumi
endapo tutaanza uchimbaji na
biashara ya Urani.Shinikizo
zinatoka sehemu mbali mbali ili
tusichimbe madini ya Urani.Nilipoingia madarakani
nimewaelekeza wataalamu wangu
wapitie upya sera yetu kuhusu
madini haya ya urani na kutoa
mapendekezo nini tufanye ili
tuanze uchimbaji na kunufaika na
rasilimali tuliopewa na
Mungu.Mmeonyesha nia ya
kujenga mgodi mkubwa wa madini
haya ya Urani ni wazo zuri.Nitakaa
na wataalamu wangu tutalijadili
hilo halafu tutawaelezeni nini
tumeamua”
“Ahsante sana mheshimiwa
rais kwa kutupokea na kuzipokea
salamu za mkuu wetu.Kama
nilivyosema awali kwamba ujio
huu umebisha hodi na rais
angependa sana kujua kama tulipobisha hodi tulifunguliwa
mlango na kukaribishwa ndani?
Akauliza Kim huku
akitabasamu.Dr Vivian naye
akatabasamu na kusema
“Tanzania ni rafiki wa kila
mmoja.Hatuna maadui.Maadui
zetu ni wale wanaopinga
maendeleo yetu na kukwamisha
kusonga mbele.Wale wote
wanaokuja kwetu kwa nia njema
ya kuwekeza tunawakaribisha kwa
mikono miwili.Tanzania
hatufungamani na upande wowote
na hiyo ndiyo sera yetu toka
wakati wa muasisi wa taifa
letu.Hatuchaguliwi marafiki wala
mtu wa kufanya naye biashara na
tunaweza kufanya biashara hata na Korea kaskazini japokuwa
hatukubaliani nao kuhusiana na
sera zake za silaha na majaribio ya
makombora inayoyafanya lakini
milango iko wazi kwa mtu yeyote
kuja kuwekeza Tanzania ili mradi
uwe ni uwekezaji wenye manufaa
kwetu na si wale wanaokuja
kuchukua rasilimali zetu na
kutuacha masikini” akasema Dr
Vivian.Waliendelea na maongezi
na baadae wakaagana na moja kwa
moja akaelekea chumbani
kwake.Alielekeza kutosumbuliwa
tena kwani alihitaji
kupumzika.Aliingia chumbani
kwake na kumkuta Nathan
amejilaza kitandani.Nyuso zao
wote zikachanua kwa tabasamu.Dr Vivian akamfuata Nathan pale
kitandani wakakumbatiana na
kuanza kubusiana.Kila mmoja
alionekana kuwa na hamu sana na
mwenzake
“Nath…” Dr Vivian akataka
kusema kitu Nathan akamzuia
“Tutaongea baadae lakini
kwanza tumalize shughuli
muhimu” akasema Nathan huku
mikono yake yenye nguvu
ikiendelea kukivinjari kifua cha
Vivian ambaye taratibu alianza
kuzidiwa kutokana na utundu wa
Nathan.Alishindwa kujizuia
ikamlazimu amuachie Nathan
afanye kile alichokikusudia Ulikuwa ni mtanange wa
dakika arobaini na Nathan
alimpeleka Dr Vivian vilivyo.
“Ninajivunia sana kuwa na
mwanaume kama wewe una nguvu
za ajabu .Unanifikisha pale
ninapotaka.Ahsante sana Nathan”
akasema Dr Vivian na kumbusu
Nathan
Waliongea mambo mengi
yanayowahusu kuhusiana na ndoa
yao na maisha yao ya usoni na
mara Nathan akauliza
“Nilipokuja niliambiwa
kwamba kuna wageni
unazungumza nao faragha.Ni
wageni gani hao?
“Nilikutana na ujumbe wa
wafanyabiashara wa China wakiwa wameambatana na mjumbe
maalum wa rais wa Korea
Kaskazini” akasema Dr Vivian na
kumstua Nathan
“Walikuwa wanataka nini?
Akauliza
“Korea kaskazini wanataka
kuanzisha mahusiano ya
kibiashara na Tanzania
.Tumezungumzia kuhusu
uanzishwaji wa viwanda vya nguo
na lingine kubwa wanataka
kuwekeza katika uchimbaji wa
Uranium”
“Umewapa jibu gani?
“Tanzania inakaribisha
wawekezaji toka sehemu mbali
mbali duniani na sioni tatizo kwa
wawekezaji toka Korea kaskazini kuwekeza Tanzania.Nitajadiliana
na wenzangu tuangalie suala hili
kwa mapana zaidi.Wewe una
maoni gani kuhusu jambo hili?
Unatarajia kuwa mume wa rais na
utakuwa ndiye mshauri wangu
mkubwa.Nipe maoni yako katika
jambo hili”
“kwa upande wangu sina
kipingamizi chochote katika
kukaribisha uwekezaji nchini
Tanzania ila lazima muwe makini
na watu wanaotaka kuja
kuwekeza.Uwekezaji wowote
kutoka Korea Kaskazini na hasa
katika madini ya Urani utaiweka
nchi ya Tanzania pabaya sana
kimataifa.Kwanza kuwa mshirika
tu na Korea kaskazini ambayo ina maadui wengi inaweza kuiletea
mtatizo Tanzania lakini kwenda
mbali zaidi na kuwaruhusu
wachimbe madini ya Urani
kutaongeza mgogoro.Korea
kaskazini wapo katika msuguano
mkubwa na mataifa makubwa
kutokana na sera zake za
utengenezaji wa makombora na
inadaiwa wana makombora
kadhaa ya nyuklia na wakipata
madini hayo ya urani wataongeza
nguvu katika kutengeneza silaha
za nyuklia na watazidi kuwa tishio
kwa dunia.Hilo ni jambo
mnalopaswa kulitazama kwa
macho sita.Si suala la kufanyia
mzaha” akasema Nathan
“Nini basi ushauri wako? “Tanzania bado ni nchi
masikini,bado inahitaji misaada
toka mataifa makubwa
yaliyoendelea.Sitaki kuona
ukiingiza nchi yako katika
matatizo au migongano na mataifa
wafadhili.Nashauri uachane kabisa
na hao wakorea.Watawawekeni
katika matatizo makubwa.
Tanzania itawekewa vikwazo vya
kiuchumi,mtafungiwa kuuza nje
bidhaa zenu na kunyimwa
misaada.Hili likitokea uchumi wa
Tanzania utayumba sana” akasema
Nathan
“Tanzania ni nchi huru na
haiwezi kupangiwa taifa la kufanya
nalo biashara .Tutafanya biashara
na yeyote yule ambaye tutaonana ana maslahi kwetu.Tumechoshwa
na huu ukandamizwaji
unaofanywa na haya mataifa
makubwa.Ni wakati wa Afrika
kusimama na kuungana kupinga
huu unyanyasaji mkubwa
unaofanywa na haya mataifa
yakiongozwa na nchi yako
marekani.Mungu katupa rasilimali
zitufaidishe kwa nini tunakatazwa
kuzitumia?Kwa nini tuendelee
kuwa masikini wakati utajiri
tunao?Utajiri wetu unaporwa na
sisi tunaachiwa mashimo na
hazina za hawa wakubwa
zinaendelea kunona kwa madini
wanayoyachuma toka
kwetu.Siwezi kuivumilia hali kama
hii iendelee.Afrika lazima tufaidike na rasilimali Mungu alizotupa
kuliko kuacha zichukuliwe na
hawa wakubwa na sisi kubaki
masikini” akasema Dr Vivian.
“Tuachane na hayo Vivian huo
ulikuwa ni ushauri wangu.Tujikite
katika mambo yanayotuhusu sisi
wawili.Tuna maisha yanatusubiri
baada ya kufunga ndoa kwa hiyo ni
muda muafaka wa kupanga
kuhusu maisha yatu ya
baadae.Halafu mpenzi wangu
kuna jambo ninataka kukuuliza”
“Uliza Nathan na samahani
kwa sauti ya juu niliyoitoa
kutokana na lile suala.Unajua
linapokua suala la maslahi ya
Tanzania huwa ninaweka uzito
mkubwa sana” “Usijali mpenzi.Wewe hivi
sasa ni rais wa nchi na
ikimpendeza Mungu baada ya
miezi miwili toka sasa tunaweza
kufunga ndoa.Ninajiuliza kuhusu
suala la familia,namaanisha
watoto.Umekwisha wahi kulifikiria
hilo kuhusu namna tutakavyoweza
kupata watoto wetu?
Swali lile likaonekana
kumstua Dr Vivian.Akafikiri
kidogo na kusema
“Nathan naomba tuliache hilo
suala tutalizungumza siku
nyingine huu si wakati wake”
akasema Dr Vivian
“Vivian huu ni wakati wetu
mzuri wa kulizungumza hili
jambo.Muda uliobaki ni mdogo na kutokana a kutingwa na mambo
mengi kuna uwezekano tusipate
nafasi ya kuliongelea.Kabla ya
kuingia katika ndoa tunapaswa
kulizungumza na kupata muafaka
ili lisituletee mgogoro huko
mbeleni”akasema Nathan
“Nimekuelewa Nathan lakini
sijui nikujibu nini” akasema Dr
Vivian na kuiamisha kichwa
akafikiri kidogo halafu akasema
“Kwani lazima kuwa na
watoto?
“Ulazima upo mpenzi tena
mkubwa.Watu wawili
mnapoungana na kuwa mwili
mmoja kwa kufunga ndoa,kikubwa
kinachotarajiwa ni kupata watoto
na kutengeneza familia yenye furaha.Kama hakuna tatizo lolote
la kimaumbile kwa mmoja kati ya
wanandoa basi watoto ni
lazima.Hilo ni agizo tumepewa na
Mungu kwamba nendeni
mkazaane muijaze
dunia.Mnapofunga pingu za
maisha Mungu anawatumia
kuendelea kazi yake ya uumbaji
kwa kuwajalia watoto” akasema
Nathan
“Bila watoto ndoa haiwezi
kuwa na furaha? Dr Vivian
akauliza
“Ndoa inaweza kuwa na
furaha bila watoto lakini endapo
hakuna tatizo lolote linaloweza
kutuzuia kupata watoto kwa ninitusizae?Mbona umeuliza maswali
hayo huna mpango wa kuzaa?
“Nathan naomba niwe mkweli
kwako kwamba sina wazo la kuwa
na mtoto hasa kwa wakati
huu.Kwa hivi sasa akili yangu
nimeielekeza katika kuwahudumia
waTanzania.Sitaki niingie katika
jambo lingine lolote
litakalonifanya nishindwe
kuwatumikia watu wangu
walionichagua kwa mapenzi
makubwa.Suala la mtoto itabidi
lisubiri labda hadi hapo
nitakapomaliza kipindi changu cha
uongozi” akasema Dr Vivian
“Hapana mpenzi hatuwezi
kusubiri hadi muda huo.Kwa sasa
una miaka 47,ukimaliza kipindi chako cha kwanza cha uongozi
utakuwa na miaka
50.Ukichaguliwa katika kipindi cha
pili utakuwa na miaka 55 unataka
upate mtoto wa kwanza ukiwa na
umri huo wa uzee?
“Nathan naomba unielewe
kwa sasa nina majukumu mazito
kwa nchi yangu na sintakuwa na
muda kulea mtoto.Utanisamehe
sana kwa hilo.Kama ni mtoto wapo
wengi tunaweza kuchukua wawili
au watatu katika vituo vya kulelea
watoto yatima tukawalea kama
watoto wetu kwa maopenzi
makubwa”
“Hapana Vivian.Sitaki mtoto
asiye wangu.Nataka kulea mtoto
wa damu yangu na si mtoto wa kuokota.Kama unaona kutakuwa
na ugumu kulea nizalie mtoto na
mimi nitalea mwenyewe wakati
ukiendelea na majukumu yako ya
urais” akasema Nathan.Dr Vivian
akamtazama na kusema
“Hilo haliwezeka ni
Nathan.Bado siko tayari kuwa
mama na pengine sitakuwa mama
katika maisha yangu yote”
Jibu lile la Dr Vivian
likaonekana kumkasirisha sana
Nathan.
“Vivian kwa nini
unanifanyia?Kwa nini hutaki kuzaa
mtoto na mimi? Kuna faida gani ya
kuingia katika ndoa ambayo
haitakuwa na uzao?Nakupenda
mno Vivian lakini kwa msimamo wako juu ya suala la mtoto
umenifanya nijifikirie mara mbili
kama kweli tuko tayari kuingia
katika ndoa.Umenishangaza sana
Vivian” akasema Nathan.Vivian
akasimama na kumtazama Nathan
kwa muda akasema
“Nathan nakupenda sana zaidi
ya unavyoweza kufikiri lakini siko
tayari kwa sasa kuwa na mtoto
hivyo basi una fursa mbili za
kuchagua.Aidha wewe na mimi
tuishi bila mtoto au tuachane
ukatafute mwanamke
atakayekuzalia mtoto.Chagua moja
mimi niko tayari kwa lolote”
akasema Dr Vivian.Nathan
akasimama na kutaka kumshika
mkono lakini Dr Vivian akamzuia Usinishike tafadhali.Naomba
ufahamu kwamba mimi ni
mwanamke nisiyependa
kuyumbishwa na mtu
yeyote.Katika maisha yangu
ninamuogopa Mungu pekee na si
mwanadamu yeyote.Nataka mtu
ambaye nitaolewa naye awe ni mtu
atakayeendana na mimi na
misimamo yangu.Ninaomba
uchague kati ya hayo mawili
niliyokwambia.Au nikuchagulie?
Akauliza Dr Vivian kwa ukali
“Vivian mpenzi nakuomba
haya mambo yasifike huko
tafadhali.Mimi na wewe hatupaswi
kufika hatua kama hiyo ya
kulumbana kiasi hiki.Haya mambo
yanazungumzika na tukae chini tuzungumze.Tumetoka mbali na
tusianze kukorofishana kwa
wakati huu ambao tuko karibu
sana kuifikia ile ndoto yetu ya
kufunga ndoa na kuwa kitu
kimoja.Siko tayari kutengana nawe
kwa sababu nakupenda lakini
suala la mtoto naomba ulifikirie
mpenzi wangu,ni la muhimu
sana.Hatuwezi kamwe kuwa na
furaha katika ndoa yetu bila kuwa
na watoto.” akasema Nathan
“Nathan unaonekana bado
hujanifahamu vyema.Nimekupa
fursa ya kuchagua lakini
umeshindwa kufanya hivyo na
badala yake bado unaendelea
kunichefua.Sasa nisikilize kwa
makini.Mimi ni rais na ninaongoza waTanzania zaidi ya milioni
hamsini kwa hiyo akili yangu yote
nimeielekeza huko.Walinichagua
kwa mapenzi makubwa na wana
imani kubwa na mimi kwamba
nitawasaidia kuboresha maisha
yao.Watoto wa watanzania ni
watoto wangu pia hivyo natakiwa
kuhakikisha kwamba wako salama
kila siku na wana afya
njema.Natakiwa kuhakikisha
wanapata elimu iliyo
bora,natakiwa kuhakikisha wazazi
wao wana maisha mazuri na yaliyo
bora kwa hiyo kila dakika ambayo
Mungu ananijalia kuishi
ninaielekeza katika kutatua kero
za watanzania na ndiyo maana
mara nyingi hata usiku silali ninakesha nikifanya kazi kwa
ajiliya watanzania masikini hivyo
sintakuwa na muda wa kulea
mtoto.Pamoja na kukuelewesha
huko lakini bado umeonyesha
kwamba hauko tayari kuishi bila
mtoto na mimi siko tayari kuwa na
mtoto hivyo katu hatutaweza kuwa
na amani katika hiyo ndoa
yetu.Kwa sababu hiyo ninaona kitu
cha msingi ni mapenzi yetu kuishia
hapa.Ile safari yetu na zile ndoto
zetu zote ziishie hapa.Inaniuma
lakini sina namna nyingine ya
kufanya kwani Tanzania ni
muhimu zaidi kwangu kuliko
mapenzi.Siku zote huwa ninasema
nchi yangu kwanza na mambo
mengine baadae”