HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,399
- 6,077
Season 1 The Football
Mtunzi.Patrick Ck
Sehemu 1
Msafara wa rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania,uliwasili katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es
salaam.Dr Vivian Sebastian Matope
rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania akashuka garini akiwa
amevalia suti ya rangi nyeupe
iliyompendeza vilivyo.Kichwani
hakuwa amebadili mtindo wake
wa nywele.Dr Vivian hakupenda
kuweka madoido katika nywele
zake.Alipenda kuzipunguza na
kuzifanya fupi.Alikuwa na mwili
mwembamba wastani na
kumfanya awe ni mmoja kati ya
marais wanawake wazuri zaidi
duniani. Akiwa katika ulinzi mkali Dr
Vivian alianza kuelekea ndegeni
huku akisalimiana na kuagana na
baadhi ya viongozi waliofika pale
uwanjani kumuaga.Alipomaliza
kuagana na viongozi mbali mbali
akamuita pembeni mkurugenzi wa
idara ya idara ya usalama wa taifa
ndugu George Mzabwa
“George umefikia wapi
kuhusu lile suala ?Kuna chchote
kimepatikana mpaka leo? Akauliza
Dr Vivian
“Madam president lile suala
bado gumu lakini tunaendelea
kulifanyia kazi.Mpaka sasa bado
hatujafikia hatua ya kuridhisha na
ndiyo maana umeona nimekuwa
kimya sijafika kwako kukupa mrejesho wowote” Akasema
George.Dr Vivian akamtazama
akatabasamu na kusema
“Nitakaporejea nataka nikute
tayari kuna hatua imekwisha
pigwa ama sivyo nitakuondoa
katika nafasi hiyo na kuwapa
wengine wenye uwezo wa kufanya
kazi kwa kasi kama
ninavyotaka.Sioni sababu ya
kukukwamisha katika
kulishugulikia suala hili wakati
kila kitu unacho.Naomba ulifanyie
kazi hilo nililokwambia na
nitakaporejea nikute aidha ripoti
ya hili suala,au barua ya kuachia
ngazi au nikuondoe mwenyewe
katika nafasi hiyo.Tumeelewana
George? Akauliza Dr Vivian Nimekuelewa madam
president” akajibu George
“ Good” akasema Dr Vivian na
kupanda ngazi kuingia
ndegeni.Alipofika katika mlango
wa ndege akageuka na
kuwapungia mkono watu
waliokuja kumuaga halafu
akaingia ndegeni
Dr Vivian ni rais wa kwanza
mwanamke kuongoza jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Alizaliwa
22 Octoba 1970 akiwa mtoto wa
kwanza wa Kanali Sebastian
Matope na mke wake Getruda
Mazimbo.Alipata elimu yake ya
msingi katika shule ya msingi
Azimio mjini Dodoma ambako
baba yake alikuwa akifanya kazi wakati huo.Alijiunga na shule ya
sekondari ya St Bernadetha
inayomilikiwa na masista wa
shirika la mtakatifu Bernadetha
iliyoko mkoani Kilimanjaro.Lengo
kuu la kujiunga na shule hiyo iliyo
chini ya watawa ilikuwa ni
kujiunga na maishaya utawa.Toka
akiwa mtoto dogo Dr Vivian
aliyapernda maisha yale ya
kitawa.Alisoma katika shule hiyo
hadi kidato cha sita na matokeo
yalipotoka Vivian alifaulu kwa
kiwango cha juu kwa kupata
daraja la kwanza.Matokeo hayo
yalimfanya Vivian abadili lengo
lake la kuwa mtawa na akachagua
kuendelea na masomo ya udaktari
.Aliendelea na elimu ya juu katika fani ya udaktari katika vyuo vikuu
kwenye nchi mbali mbali kama vile
Israel,Cuba,Urusi,Marekani na
China.Mwaka 2007 aliamua
kurejea nchini Tanzania baada ya
familia yake yaani wazazi wake
wote na mdogo wake kuuawa na
watu wasiojulikana.
Baada ya kurejea nchini Dr
Vivian alifanya kazi kama daktari
wa watoto katika hospitali ya taifa
ya Muhimbili.Alianza kujiingiza
taratibu katika siasa na kutokana
na kipawa chake kikubwa cha
uongozi alichokuwa nacho,Dr
Vivian alijikuta akishika nafasi
kadhaa ndani ya chama na hapo
ndipo alipoanza
kujulikana.Daktari huyu mwenye haiba ya kipekee,mwenye urefu wa
5.8.ngozi nyororo na uso
usiokauka tabasamu alifahamika
sana kwa misimamo yake thabiti
isiyoyumba katika yale mambo
anayoyaamini na hasa katika
kusimamia haki za watu wa hali za
chini wanaokandamizwa.
Tabia yake hii ya msimamo
usiotetereka ilianza kuonekana
pale alipokuwa rais wa serikali ya
wanafunzi katika chuo kikuu
kimoja alichosoma nchini
Marekani.Katika chuo hicho kikuu
wanafunzi wenye asili ya Afrika
walikuwa wanabaguliwa na
kutopewa kipaumbele katika
mambo mengi.Haikuwa rahisi
kwake kuweza kushinda nafasi ya rais wa serikali ya wanafunzi na
aliposhinda kitu cha kwanza
alichoanza kukishughulikia ni
suala la ubaguzi uliokithiri hapo
chuoni.Jambo hili lilimletea
misukosuko mikubwa na hata
kuondolewa katika nafasi yake ya
rais wa wanafunzi baada ya
kuonekana anakiuka sheria za
chuo lakini hii haikumkatisha
tamaa kuendelea kuwapigania
wale waliokuwa
wanabaguliwa.Baada ya mvutano
mkali na chuo hicho hatimaye
ushindi ukapatikana na taratibu za
chuo zikabadilishwa,wanafunzo
wote wakawa na haki sawa.Kwa
wale wanaofuatilia mambo ya
nyota,hii ilikuwa ni ishara tosha kwamba nyota ya Dr Vivian ilianza
kung’aa na siku moja ingeweza
kung’aa na kutoa mwangaza
mkubwa
Wakati akiendelea na
masomo yake aliwahi kuchaguliwa
kuwa msemaji wa wanafunzi
wenye asili ya Afrika katika katika
vyuo vikuu vya Marekani na katika
mojawapo ya hotuba aliyowahi
kuitoa katika kongamano
lililofanyika siku ya kuikumbuka
hotuba aliyoitoa mwanaharakati
aliyepigania haki za watu weusi
nchini Marekani Martin Luther
aliyoitoa 28 August 1963,Vivian
aliweka wazi ndoto yake ya
kuliona siku moja bara la Afrika
linatoka gizani na kuwa bara lenye nuru na nguvu.Alieleza
kusikitishwa kwake na
ukandamizwaji na unyonyaji
unaofanywa na mataifa makubwa
yenye nguvu dhidi ya mataifa
masikini ya bara la Afrika.Hotuba
hii iliyojaa msisimko iliwavutia
watu wengi na kumfanya Vivian
ajulikane na kualikuwa katika
makongamano mbali mbali.Katika
mojawapo ya hotuba alizowahi
kutoa aliweka wazi nia yake ya
siku moja kuwa kiongozi na
kuziunganisha nchi zote za Afrika
na kuwa nchi nmoja yenye nguvu
kijeshi na kiuchumi. Alitamani
siku moja awe rais wa kwanza wa
Afrika na kuongoza bara hili lenye
kila aina ya utajiri. Alipofanikiwa kushinda nafasi
ya urais wa Tanzania,Dr Vivian
amefanya mambo makubwa kwa
muda wa miaka miwili ambayo
amekuwa madarakani.Ni rais
mdogo kwa umri ukilinganisha na
marais wengi wa mataifa mengine
lakini mambo makubwa
aliyoyafanya yamewashangaza
wengi.Ni rais asiyesita kuchukua
maamuzi magumu na
asiyetetereka katika maamuzi
yake.Huyu ndiye Dr Vivian rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye amepewa jina la utani la
Dr White kutokana na staili yake
ya kipekee ya kupenda rangi
nyeupe kuanzia mavazi yake hadi
magari yanayotumika katika msafara wake.Mara chache sana
huonekana katika mavazi ya rangi
nyingine lakini siku zote huwa
katika mavazi meupe.
Baada ya kuingia ndegeni Dr
Vivian akasalimiana na marubani
na wahudumu wa ndege yake na
kujiandaa kwa ajili ya kuelekea
jijini New York Marekani
kuhudhuria mkutano mkuu wa
umoja wa mataifa unaofanyika kila
mwaka na ambao huudhuriwa na
wakuu wote wa nchi wanachama
wa umoja wa mataifa.Huu ni
mkutano wake wa kwanza
kuhudhuria tangu achaguliwe
kuwa rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.Mkutano
uliopita aliwakilishwa na makamu wa rais na mwaka huu
anahudhuria yeye
mwenyewe.Katika safari hii
aliongozana na mawaziri
wanne,maafisa wengine kadhaa
pamoja na walinzi wake na jumla
msafara wake ulikuwa na watu
ishirini.
Ndege ilikaa katika njia yake
ya kurukia ikaanza kuondoka
taratibu na kuongeza kasi kisha
ikapaa huku viongozi waliofika
pale uwanjani kumuaga rais
wakipunga mikono kumtakia rais
na ujumbe wake safari
njema.Ndege ilipokaa sawa
angani,Dr Viviana akaitisha kikao
na watendaji alioambatana nao
katika safari ile.Walikutana katika chumba cha mikutano kilichomo
ndani ya ndege ile kubwa chenye
uwezo wa kuchukua watu zaidi ya
ishirini.Walijadiliana mambo
kadhaa kuhusiana na safari yao ile
na baada ya takribani saa moja na
nusu kikao kikamalizika wajumbe
wakatoka na rais akaenda katika
chumba chake kupumzika kwani
safari ile ilikuwa ndefu.Akiwa
chumbani akamuita mdogo wake
Theresa.
Theresa Sebastian Matope ni
msichana mwenye weusi wa
kung’aa na umbo la
kupendeza.Wazazi wa Dr Vivian
walimchukua Theresa toka katika
kituo cha kulelea watoto yatima
akiwa mtoto mdogo sana na kumlea kama mtoto wao wa
kumzaa.Kwa hivi sasa ndiye
mwandishi wa hotuba za rais
“Theresa naomba nione
hotuba uliyoiandaa ninayokwenda
kuitoa New York” Akasema Dr
Vivian baada ya Theresa kuingia
mle chumbani kwake.Theresa
akatoka na kwenda kuchukua
kompyuta yake akarejea na
kumuonyesha Dr Vivian hotuba ile
aliyokuwa anaiandaa
“Imebaki sehemu ndogo ya
kumalizia kuhusiana na
mabadiliko ya tabia nchi Afrika”
Akasema Theresa na Dr Vivian
akaipitia hotuba ile taratibu halafu
akasema Hii ni hotuba nzuri sana
lakini bado haijafikia kiwango
ninachokihitaji.Hii ni hotuba
yangu ya kwanza katika mkutano
huu mkubwa na ninataka iwe kali
na yenye msisimko.Nimezoeleka
hotuba zangu huwa zinakuwa kali
na zenye msisimko.Nataka
viongozi wa dunia waelewe
msimamo wangu na wa Tanzania
katika mambo mbali mbali hivyo
iongeze ukali hotuba hii” akasema
Dr Vivian
“Dada labda uniweke wazi
unataka nilenge maeneo yapi
hasa.Ulinipa mambo ya kuzingatia
wakati wa kuiandaa hotuba hii na
nimeyafuata ,nimelenga mambo ya
uchumi,misaada ya masharti na unyonyaji wa rasilimali
zetu,mabadiliko ya tabia nchi na
mengineyo” akasema Theresa.Dr
Vivian akaitazama tena hotuba ile
na kusema
“Hotuba hii si mbaya,imekaa
vizuri lakini kuna sehemu ambazo
zinahitaji lugha kali zaidi
kuonyesha msisitizo.Hotuba hii
imepoa sana.Lakini usijali endelea
nayo na utakapomaliza niletee
nitaisahihisha
mwenyewe,samahani kama
nimekukwaza” akasema Dr Vivian
“Usijali dada” akasema
Theresa na kuchukua kompyuta
yake ili atoke Vivian akamuomba
asubiri.Kaa nami kidogo
Theresa,bado tunayo safari
ndefu.Nyakati kama hizi ndipo
tunaweza kukaa na kuongea
mambo yanayotuhusu sisi.Tukifika
marekani kutakuwa na mikutano
mingi hivyo hatutaweza kupata
nafasi nzuri ya kuzungumza
mambo yetu” akasema Dr Vivian
“Ni kweli dada.Japokuwa tuko
pamoja muda mwingi lakini
hatupati nafasi ya kuzungumza
mambo yetu ya kifamilia” akasema
Theresa na kujimiminia juice
katika glasi
“Kabla sijaingia ndegeni
nilikuwa na mazungumzo na
George Mzabwa.Nilimuuliza
amefikia wapi kuhusiana na kazi niliyompa ya kuchunguza mauaji
ya familia yetu.Amekuwa
ananikimbia kimbia kila
ninapotaka kulizungumzia jambo
hili.Jibu alilonipa
halijaniridhisha.Amesema
kwamba mpaka sasa bado
hajafanikiwa kugundua lolote.Ni
miaka miwili imepita sasa toka
nimempa kazi hiyo na ameniudhi
sana.Nimemwambia nitakaporejea
aidha nikute taarifa kwamba watu
waliofanya kitendo kile kiovu
wamepatikana au nikute barua
yake ya kuachia ngazi mezani
kwangu ama sivyo nitamuondoa
na kumpeleka sehemu nyingine
kwani ameshindwa kazi.Sielewi
kuna nini katika jambo hili hadi lishindwe kupatiwa
majibu.Ninafikiria kutafuta mtu
mwingine wa kuongoza idara ya
usalama wa taifa kwa kasi
ninayoihitaji.George hawezi
kuendana na kasi yangu” akasema
Dr Vivian
“Hata mimi nashangaa na
kujiuliza kulikoni katika suala hili?
Inawezekajane mpaka leo hii
hakuna taarifa yoyote kuhusiana
na wauaji wa familia yetu?Jeshi la
polisi wamefanya
uchunguzi,usalama wa taifa pia
lakini mpaka leo hii hakuna
chombo chochote kilichotoa
majibu ni nani waliua familia yetu
na kwa nini.Vyombo hivi vyote
viwili wanazo rasilimali za kutosha kuwawezesha kufanikisha
uchunguzi wa jambo hili lakini
mpaka leo wameshindwa kubaini
watu waliofanya unyama ule.Hapa
kuna kitu kinatia shaka dada”
akasema Theresa
“Tuachane na hayo
nitayashughulikia nitakaporejea
kwani suala hili kwa sasa
linaonekana kama fumbo gumu
lisiloweza kufumbuka.Nitalivalia
njuga mimi mwenyewe na safari
hii lazima nitapata majibu,lazima
fumbo hili lifumbuke” akasema Dr
Vivian na kumuomba Theresa
amletee juice ya mchanganyiko wa
matunda kinywaji anachokipenda
sanaNathan kanipigia simu leo
asubuhi na kunitaarifu kwamba ile
kazi yake aliyokwenda kuifanya
Uswisi imemalizika na hivyo
atanifuata New York na baada ya
mkutano kumalizika tutarejea
wote Da es salaam kuendelea na
maandalizi ya ndoa yetu.Theresa
siwezi kueleza furaha niliyonayo
kwani imebaki miezi mwili tu na
mimi niingie katika ndoa na
mwanaume ninayempenda kwa
dhati.Hata hivyo kuna kitu nataka
kukisikia toka kwako.Watu
wanaongeaje huko mitaani
kuhusiana na ndoa yangu na
Nathan? Nilitaka jambo hili liwe la
kimya kimya lakini watu
wamefukunyua hadi wakagundua ninataka kufunga ndoa”Akauliza
Dr Vivian huku
akitabasamu.Theresa akanywa
funda la juice halafu akasema
“Japokuwa Nathan ulikuwa
naye katika kipindi chote cha
kampeni na kuzunguka naye nchi
nzima lakini bado watu
hawamfahamu vizuri ni
nani.Nimekuwa napitia baadhi ya
maoni ya watu mtandaoni na
nimeona watu wanahoji kwa nini
rais wao aolewe na mtu wa kutoka
nje ya nchi?Tanzania imejaa vijana
wa kila aina wasomi na wabobezi
wa mambo mbali
mbali,haujawaona hao wote hadi
moyo wako ufunguke kwa mtu wa
taifa lingine?Lakini haya yasikuogopeshe ni mawazo tu ya
watu yanayotokea katika mijadala
mbali mbali inayoendelea huko
mitandaoni” akasema Theresa .Dr
Vivian akatabasamu nba kuuliza
“Wewe je una maoni gani?
“Kuhusu nini dada Vivi?
“Kuhusu mimi na
Nathan.Nakufahamu wewe huna
tabia ya kuficha kitu bali husema
kweli toka moyoni.Sijawahi kupata
maoni yako kuhusiana na hili suala
langu na
Nathani.Unaliongeleaje?Nathani ni
mwanaume ambaye naweza
kusema kwamba ninampenda kwa
dhati ya moyo wangu lakini je
unadhani watu wangu
watampenda na kumkubali?Tafadhali kuwa
muwazi kwangu.You are my
sister” akasema Dr Vivian
“Dada ,mapenzi kama yalivyo
hayachagui rangi,umri hata
taifa.Moyo unaweza kufunguka
kwa mtu yeyote awe
mweusi,mweupe n.k.Wewe
umeufungua moyo wako kwa
Nathan na hakuna ubaya wowote
lakini….” Theresa akasita kidogo
akanywa maji ya matunda na
kuendelea
“Umeomba nikueleze ukweli
wangu na nitakueleza ukweli
wangu japo hautakuwa mzuri sana
lakini lazima niuseme kwa kuwa
umeomba.Hakuna mtu
atakayeweza kukuzuia usiolewe na Nathan mwanaume unayempenda
kwa dhati ya moyo wako lakini
ndoa hii ingekuwa na tija zaidi
kama Nathan angekuwa ni
mtanzania.Anaweza akabadili
uraia wake na kuwa mtanzania
lakini damu yake bado ni
Marekani.Kama akiwa mumeo
yeye ndiye atakayekuwa mshauri
wako mkuu kwa mambo mbali
mbali hivyo anapaswa awe ni mtu
anayeipenda Tanzania na
kuifahamu vyema,ayafahamu
matatizo ya waTanzania na
yamguse ili aweze kukushauri
vizuri namna ya kuzitatua
changamoto mbali mbali
unazokumbana nazo katika kazi
yako.Nathani yeye ni mmarekani na Tanzania ameifahamu kwa
sababu yako tu na sina hakika
kama anaweza kuwa mshauri
mzuri katika masuala yanayohusu
Tanzania.Ikitokea akashindwa
kukushauri au akakushauri vibaya
mzigo wote wa lawama utakuwa
juu yako.Lakini haya ni mawazo
yangu tu na usiyachukulie kama
ndiyo mtazamo wa
watanzania.Nathan ni kijana mzuri
na sioni kama ana tatizo lolote”
akasema Theresa
“Theresa ahsante sana.Ndiyo
maana huwa ninapenda kukuomba
ushauri.Una mtazamo wa
mbali.Unafaa sana kuwa mshauri
wa rais na nitalitazama hilo siku za
usoni.Umezungumza mambo ya msingi na ambayo sikuwa
nimeyafikiria kabla sijakubali
kuolewa na Nathan.Vipi kuhusu
wewe na yule mtu wako Damian?
Bado mnaendelea na ugomvi
wenu? Kwa nini masuala yenu
msiyatafutie ufumbuzi na
kuyamaliza ili msonge mbele kwa
amani?
“Dada Vivi kuna mambo
mengine hayafai
kuyalazimisha.Nimetafakari sana
na kugundua mimi ndiye
niliyekuwa nalazimisha penzi
wakati mwenzangu hana muda
nami.Kila wakati mimi ndiye
niliyekuwa nikipiga magoti
kuomba msamaha hata kama si
mimi niliyekosa.Lengo lilikuwa ni kunusuru penzi letu kwa kuwa
Damian nilimpenda zaidi ya
ninavyoweza kueleza.Lakini ulifika
wakati nikasema imetosha na
nikaamua kila mmoja aendelee na
maisha yake.Niliumia mwanzoni
but now I’m happy.Nina amani ya
moyo na ninasubiri yule ambaye
ameumbwa kwa ajili yangu
ajitokeze.Naamini yupo mahala
fulani na muda ukifika nitampata”
akasema Theresa
“Hongera kwa maamuzi
hayo.Mimi nilitamani sana
kukushauri hivyo toka awali lakini
sikutaka kuingilia masuala
yako.Unapoona uko katika
mahusiano halafu wewe ndiye
mwenye kuumia kila siku na mwenzako hajali basi chukua
hatua haraka,huo uhusiano
hautakufikisha mahala
kokote.Natumai tayari umepata
somo la kutosha na utakuwa
makini safari hii kutafuta
mwanaume yule ambaye atakufaa
katika maisha yako.Ukikosea
kuchagua utaumia sana.Mapenzi
yanaumiza mno.Kuna nyakati hata
mimi ninawaza kuhusu Nathan
kama hatutakuwa na migogoro
pindi tutakapofunga ndoa.Nataka
nielekeze akili yangu katika
kuwasadia watanzania
walionichagua na kuwatatulia kero
zao na nitakuwa na muda mdogo
sana wa kushughulikia masuala ya
mapenzi.Hiki hawezi kuwakikwazo kwa Nathan na kikaleta
mgogoro kati yetu?Laiti Mungu
angeweza kunionyesha maisha
nitakayoishi nikiwa na Nathan
ningeweza kufanya maamuzi lakini
Mungu ametuficha na hatuelewi
chochote kuhusu dakika ijayo”
akasema Dr Vivian
“Usiwe na wasi wasi
dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole
na hana matatizo.Lakini …”
Theresa akasita
“Lakini nini Theresa? Mbona
umesita? Sema unachotaka
kukisema” akasema Dr
Vivian.Theresa akafikiri kidogo na
kusema
“Nothing.Ngoja nikuache
upumzike,mimi naenda kuimalizia hotuba hii halafu na mimi
nipumzike” akasema Theresa na
kuchukua kompyuta yake akatoka
mle chumbani.
“Theresa alitaka kuniambia
nini halafu akasita? Akajiuliza Dr
Vivian baada ya Theresa kutoka
mle chumbani
“Theresa si mtu wa kuficha
jambo,au aliona halina maana
ndiyo maana akaamua kuachana
nalo.Hata hivyo kuna jambo
amelizungumza la maana sana
kwangu na sikuwa nimelitilia
maanani hapo kabla.Nikiolewa na
Nathan yeye ndiye atakayekuwa
mshauri wangu katika mambo
mengi lakini atanishauri kitu gani
kama haifahamu vyema Tanzania wala matatizo ya watanzania?
Akajiuliza
“Nimetoka mbali na Nathan na
ninamfahamu vyema.Hata kama
haifahamu vizuri Tanzania wala
matatizo yake lakini nina imani
atanishauri vizuri kwani ni kijana
mpole na mwenye busara ya hali
ya juu.Sina shaka hata kidogo na
upendo wake kwangu na hata
mimi ninampenda mno na ndiyo
maana hata aliponitamkia kwamba
anataka kunioa niliruka ruka kwa
furaha.Mengi yatasemwa lakini
sitakiwi kuyasikilza.Natakiwa
kuziba masikio na kuyapuuza
kwani huyu ndiye chaguo
langu.Nathan ameingia katika kila
mshipa wa mwili wangu” akawaza na kuinuka kitandani akachukua
kompyuta yake akafungua mahala
anakohifadhi picha na kuzitazama
picha za gauni lake zuri atakalovaa
siku ya harusi yake,akatabasamu
“Sipati picha namna
nitakavyopendeza ndani ya gauni
hili lililobuniwa na mbunifu
chipukizi wa mavazi wa
kitanzania.Naamini
nitakapoonekana nimelivaa gauni
hili jina lake litapaa ulimwenguni
kwani wengi watataka kufahamu
nani alibuni vazi zuri kama hili.”
Akatabasamu na kuanza kutazama
picha nyingine za wabunifu mbali
mbali wa mavazi ya harusi
Alipotoka chumbani kwa
rais,Theresa akaenda katika moja wapo ya ofisi zilizomo ndani ya
ndege hii kubwa akachomeka
spika za masikioni katika
kompyuta yake akaanza kusikiliza
muziki.Uso wake ulionyesha
mabadiliko
“Mambo tuliyozungumza na
dada Vivi yameniharibia kabisa
siku yangu.Kwanza ni kuhusu yule
mchumba wake Nathan.Moyo
wangu haumkubali kabisa na hata
mwenyewe analifahamu hilo na
sijui kwa nini simpendi.Kila
nimuonapo karibu na dada amani
hutoweka kabisa.Najua
wanapendana lakini moyoni
mwangu hana kibali.Si kwamba
ninamchukia ila ninaona hafai
kuwa na Vivian.Nilitaka nimueleze hivyo dada lakini nikasita kwani
asingefurahia maneno hayo.Hata
hivyo siwezi kuingilia mapenzi
yao.Kama wanapendana acha
waoane lakini ningefurahi sana
kama dada yangu angeolewa na
kijana mtanzania” akawaza
Theresa na kufumbua macho
baada ya mlango kufunguliwa na
mtu kuingia mle ofisini.Alikuwa ni
waziri wa mambo ya nje
“Theresa nimekufuata
wewe,kuna kitu nataka
unisaidie.Naomba uipitie hii
hotuba yangu na uirekebishe kama
kuna mapungufu” akasema waziri
huyo na kutoka .Theresa
akaendelea kusikiliza mziki huku
akiipitia hotuba ile ya yule waziri na mara kumbu kumbu fulani
ikamjia akaacha kazi aliyokuwa
anaifanya akajiegemeza kitini
“Ni miaka zaidi ya kumi sasa
imepita lakini bado picha ya
yaliyomkuta baba haijafutika
kichwani na inanitesa kila
uchao.Nilikuwepo na nilishuhudia
kila kilichotokea.Najiuliza kwa
nini mimi?Kwa nini Mungu
akanichagua mimi niyashuhudie
yale yote? Naamini Mungu ana
sababu zake na ndiyo maana
katika watu wote ambao
walimzunguka baba alinichagua
mimi na kunibebesha mzigo huu
mzito.Kila siku ninapolikumbuka
jambo hili mwili wote hupata
baridi.Bado ile milio ya risasi zilizochukua uhai wa baba,mama
na kaka Kelvin ninaisikia
masikioni kila nilalapo.Nimebaki
natembea na siri hii nzito ambayo
hakuna anayeifahamu hata dada
Vivian hafahamu chochote.Ni mimi
pekee ninayefahamu sababu ya
baba ,mama na kaka Kelvin
kuuawa.Ni kwa sababu ya
Football” Machozi yakamtoka
“Nimekuwa najilazimisha
kutaka kulisahau jambo hili lakini
nimeshindwa.Ninaogopa kuliweka
wazi suala hili kwa ajili ya usalama
wangu na dada.Ninaogopa hata
kumueleza dada Vivian kwani
yanaweza kumkuta kama
yaliyomkuta baba .Waliomuua
baba walikuwa wanaitafuta hiyo football ni vipi endapo mpaka sasa
wakawa bado wanaitafuta?
Nitayaweka hatarini sana maisha
ya dada nikimueleza kuhusiana na
hili suala.Ngoja niendelee kulibeba
na itakuwa ni siri yangu pekee na
Mungu wangu.Nimeibeba na
kutembea na siri hii kwa zaidi ya
miaka kumi na nitaendelea
kutembea nayo.Yawezekana wale
jamaa bado wanaendelea
kutuchunguza.Sina hakika kama
watakuwa wamekata
tamaa.Lazima watakuwa
wanachunguza kwa siri ili kujua
football iko wapi.Lakini hii football
ni kitu gani?Ina siri gani ndani
yake?Baba hakuwahi kunieleza
chochote kuhusiana nayo.Ninavyofahamu mimi mkoba
ule uliopewa jina la football asili
yake ni nchini Marekani ambako
kila asafiripo rais wa Marekani
huwa anasafiri nao na ndani yake
kuna mambo ya siri ya kiusalama
kuhusiana na mambo ya
nyuklia.Hapa Tanzania rais Anorld
alianzisha mtindo wa kutembea na
begi kila anakoenda na akalipa
jina la football na baba ndiye
aliyekuwa mbebaji wake mkuu,je
kulikuwa na siri gani humo ndani
yake? Akajiuliza Theresa na
kukumbuka zikamrejesha mbali
Mtunzi.Patrick Ck
Sehemu 1
Msafara wa rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania,uliwasili katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es
salaam.Dr Vivian Sebastian Matope
rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania akashuka garini akiwa
amevalia suti ya rangi nyeupe
iliyompendeza vilivyo.Kichwani
hakuwa amebadili mtindo wake
wa nywele.Dr Vivian hakupenda
kuweka madoido katika nywele
zake.Alipenda kuzipunguza na
kuzifanya fupi.Alikuwa na mwili
mwembamba wastani na
kumfanya awe ni mmoja kati ya
marais wanawake wazuri zaidi
duniani. Akiwa katika ulinzi mkali Dr
Vivian alianza kuelekea ndegeni
huku akisalimiana na kuagana na
baadhi ya viongozi waliofika pale
uwanjani kumuaga.Alipomaliza
kuagana na viongozi mbali mbali
akamuita pembeni mkurugenzi wa
idara ya idara ya usalama wa taifa
ndugu George Mzabwa
“George umefikia wapi
kuhusu lile suala ?Kuna chchote
kimepatikana mpaka leo? Akauliza
Dr Vivian
“Madam president lile suala
bado gumu lakini tunaendelea
kulifanyia kazi.Mpaka sasa bado
hatujafikia hatua ya kuridhisha na
ndiyo maana umeona nimekuwa
kimya sijafika kwako kukupa mrejesho wowote” Akasema
George.Dr Vivian akamtazama
akatabasamu na kusema
“Nitakaporejea nataka nikute
tayari kuna hatua imekwisha
pigwa ama sivyo nitakuondoa
katika nafasi hiyo na kuwapa
wengine wenye uwezo wa kufanya
kazi kwa kasi kama
ninavyotaka.Sioni sababu ya
kukukwamisha katika
kulishugulikia suala hili wakati
kila kitu unacho.Naomba ulifanyie
kazi hilo nililokwambia na
nitakaporejea nikute aidha ripoti
ya hili suala,au barua ya kuachia
ngazi au nikuondoe mwenyewe
katika nafasi hiyo.Tumeelewana
George? Akauliza Dr Vivian Nimekuelewa madam
president” akajibu George
“ Good” akasema Dr Vivian na
kupanda ngazi kuingia
ndegeni.Alipofika katika mlango
wa ndege akageuka na
kuwapungia mkono watu
waliokuja kumuaga halafu
akaingia ndegeni
Dr Vivian ni rais wa kwanza
mwanamke kuongoza jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Alizaliwa
22 Octoba 1970 akiwa mtoto wa
kwanza wa Kanali Sebastian
Matope na mke wake Getruda
Mazimbo.Alipata elimu yake ya
msingi katika shule ya msingi
Azimio mjini Dodoma ambako
baba yake alikuwa akifanya kazi wakati huo.Alijiunga na shule ya
sekondari ya St Bernadetha
inayomilikiwa na masista wa
shirika la mtakatifu Bernadetha
iliyoko mkoani Kilimanjaro.Lengo
kuu la kujiunga na shule hiyo iliyo
chini ya watawa ilikuwa ni
kujiunga na maishaya utawa.Toka
akiwa mtoto dogo Dr Vivian
aliyapernda maisha yale ya
kitawa.Alisoma katika shule hiyo
hadi kidato cha sita na matokeo
yalipotoka Vivian alifaulu kwa
kiwango cha juu kwa kupata
daraja la kwanza.Matokeo hayo
yalimfanya Vivian abadili lengo
lake la kuwa mtawa na akachagua
kuendelea na masomo ya udaktari
.Aliendelea na elimu ya juu katika fani ya udaktari katika vyuo vikuu
kwenye nchi mbali mbali kama vile
Israel,Cuba,Urusi,Marekani na
China.Mwaka 2007 aliamua
kurejea nchini Tanzania baada ya
familia yake yaani wazazi wake
wote na mdogo wake kuuawa na
watu wasiojulikana.
Baada ya kurejea nchini Dr
Vivian alifanya kazi kama daktari
wa watoto katika hospitali ya taifa
ya Muhimbili.Alianza kujiingiza
taratibu katika siasa na kutokana
na kipawa chake kikubwa cha
uongozi alichokuwa nacho,Dr
Vivian alijikuta akishika nafasi
kadhaa ndani ya chama na hapo
ndipo alipoanza
kujulikana.Daktari huyu mwenye haiba ya kipekee,mwenye urefu wa
5.8.ngozi nyororo na uso
usiokauka tabasamu alifahamika
sana kwa misimamo yake thabiti
isiyoyumba katika yale mambo
anayoyaamini na hasa katika
kusimamia haki za watu wa hali za
chini wanaokandamizwa.
Tabia yake hii ya msimamo
usiotetereka ilianza kuonekana
pale alipokuwa rais wa serikali ya
wanafunzi katika chuo kikuu
kimoja alichosoma nchini
Marekani.Katika chuo hicho kikuu
wanafunzi wenye asili ya Afrika
walikuwa wanabaguliwa na
kutopewa kipaumbele katika
mambo mengi.Haikuwa rahisi
kwake kuweza kushinda nafasi ya rais wa serikali ya wanafunzi na
aliposhinda kitu cha kwanza
alichoanza kukishughulikia ni
suala la ubaguzi uliokithiri hapo
chuoni.Jambo hili lilimletea
misukosuko mikubwa na hata
kuondolewa katika nafasi yake ya
rais wa wanafunzi baada ya
kuonekana anakiuka sheria za
chuo lakini hii haikumkatisha
tamaa kuendelea kuwapigania
wale waliokuwa
wanabaguliwa.Baada ya mvutano
mkali na chuo hicho hatimaye
ushindi ukapatikana na taratibu za
chuo zikabadilishwa,wanafunzo
wote wakawa na haki sawa.Kwa
wale wanaofuatilia mambo ya
nyota,hii ilikuwa ni ishara tosha kwamba nyota ya Dr Vivian ilianza
kung’aa na siku moja ingeweza
kung’aa na kutoa mwangaza
mkubwa
Wakati akiendelea na
masomo yake aliwahi kuchaguliwa
kuwa msemaji wa wanafunzi
wenye asili ya Afrika katika katika
vyuo vikuu vya Marekani na katika
mojawapo ya hotuba aliyowahi
kuitoa katika kongamano
lililofanyika siku ya kuikumbuka
hotuba aliyoitoa mwanaharakati
aliyepigania haki za watu weusi
nchini Marekani Martin Luther
aliyoitoa 28 August 1963,Vivian
aliweka wazi ndoto yake ya
kuliona siku moja bara la Afrika
linatoka gizani na kuwa bara lenye nuru na nguvu.Alieleza
kusikitishwa kwake na
ukandamizwaji na unyonyaji
unaofanywa na mataifa makubwa
yenye nguvu dhidi ya mataifa
masikini ya bara la Afrika.Hotuba
hii iliyojaa msisimko iliwavutia
watu wengi na kumfanya Vivian
ajulikane na kualikuwa katika
makongamano mbali mbali.Katika
mojawapo ya hotuba alizowahi
kutoa aliweka wazi nia yake ya
siku moja kuwa kiongozi na
kuziunganisha nchi zote za Afrika
na kuwa nchi nmoja yenye nguvu
kijeshi na kiuchumi. Alitamani
siku moja awe rais wa kwanza wa
Afrika na kuongoza bara hili lenye
kila aina ya utajiri. Alipofanikiwa kushinda nafasi
ya urais wa Tanzania,Dr Vivian
amefanya mambo makubwa kwa
muda wa miaka miwili ambayo
amekuwa madarakani.Ni rais
mdogo kwa umri ukilinganisha na
marais wengi wa mataifa mengine
lakini mambo makubwa
aliyoyafanya yamewashangaza
wengi.Ni rais asiyesita kuchukua
maamuzi magumu na
asiyetetereka katika maamuzi
yake.Huyu ndiye Dr Vivian rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye amepewa jina la utani la
Dr White kutokana na staili yake
ya kipekee ya kupenda rangi
nyeupe kuanzia mavazi yake hadi
magari yanayotumika katika msafara wake.Mara chache sana
huonekana katika mavazi ya rangi
nyingine lakini siku zote huwa
katika mavazi meupe.
Baada ya kuingia ndegeni Dr
Vivian akasalimiana na marubani
na wahudumu wa ndege yake na
kujiandaa kwa ajili ya kuelekea
jijini New York Marekani
kuhudhuria mkutano mkuu wa
umoja wa mataifa unaofanyika kila
mwaka na ambao huudhuriwa na
wakuu wote wa nchi wanachama
wa umoja wa mataifa.Huu ni
mkutano wake wa kwanza
kuhudhuria tangu achaguliwe
kuwa rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.Mkutano
uliopita aliwakilishwa na makamu wa rais na mwaka huu
anahudhuria yeye
mwenyewe.Katika safari hii
aliongozana na mawaziri
wanne,maafisa wengine kadhaa
pamoja na walinzi wake na jumla
msafara wake ulikuwa na watu
ishirini.
Ndege ilikaa katika njia yake
ya kurukia ikaanza kuondoka
taratibu na kuongeza kasi kisha
ikapaa huku viongozi waliofika
pale uwanjani kumuaga rais
wakipunga mikono kumtakia rais
na ujumbe wake safari
njema.Ndege ilipokaa sawa
angani,Dr Viviana akaitisha kikao
na watendaji alioambatana nao
katika safari ile.Walikutana katika chumba cha mikutano kilichomo
ndani ya ndege ile kubwa chenye
uwezo wa kuchukua watu zaidi ya
ishirini.Walijadiliana mambo
kadhaa kuhusiana na safari yao ile
na baada ya takribani saa moja na
nusu kikao kikamalizika wajumbe
wakatoka na rais akaenda katika
chumba chake kupumzika kwani
safari ile ilikuwa ndefu.Akiwa
chumbani akamuita mdogo wake
Theresa.
Theresa Sebastian Matope ni
msichana mwenye weusi wa
kung’aa na umbo la
kupendeza.Wazazi wa Dr Vivian
walimchukua Theresa toka katika
kituo cha kulelea watoto yatima
akiwa mtoto mdogo sana na kumlea kama mtoto wao wa
kumzaa.Kwa hivi sasa ndiye
mwandishi wa hotuba za rais
“Theresa naomba nione
hotuba uliyoiandaa ninayokwenda
kuitoa New York” Akasema Dr
Vivian baada ya Theresa kuingia
mle chumbani kwake.Theresa
akatoka na kwenda kuchukua
kompyuta yake akarejea na
kumuonyesha Dr Vivian hotuba ile
aliyokuwa anaiandaa
“Imebaki sehemu ndogo ya
kumalizia kuhusiana na
mabadiliko ya tabia nchi Afrika”
Akasema Theresa na Dr Vivian
akaipitia hotuba ile taratibu halafu
akasema Hii ni hotuba nzuri sana
lakini bado haijafikia kiwango
ninachokihitaji.Hii ni hotuba
yangu ya kwanza katika mkutano
huu mkubwa na ninataka iwe kali
na yenye msisimko.Nimezoeleka
hotuba zangu huwa zinakuwa kali
na zenye msisimko.Nataka
viongozi wa dunia waelewe
msimamo wangu na wa Tanzania
katika mambo mbali mbali hivyo
iongeze ukali hotuba hii” akasema
Dr Vivian
“Dada labda uniweke wazi
unataka nilenge maeneo yapi
hasa.Ulinipa mambo ya kuzingatia
wakati wa kuiandaa hotuba hii na
nimeyafuata ,nimelenga mambo ya
uchumi,misaada ya masharti na unyonyaji wa rasilimali
zetu,mabadiliko ya tabia nchi na
mengineyo” akasema Theresa.Dr
Vivian akaitazama tena hotuba ile
na kusema
“Hotuba hii si mbaya,imekaa
vizuri lakini kuna sehemu ambazo
zinahitaji lugha kali zaidi
kuonyesha msisitizo.Hotuba hii
imepoa sana.Lakini usijali endelea
nayo na utakapomaliza niletee
nitaisahihisha
mwenyewe,samahani kama
nimekukwaza” akasema Dr Vivian
“Usijali dada” akasema
Theresa na kuchukua kompyuta
yake ili atoke Vivian akamuomba
asubiri.Kaa nami kidogo
Theresa,bado tunayo safari
ndefu.Nyakati kama hizi ndipo
tunaweza kukaa na kuongea
mambo yanayotuhusu sisi.Tukifika
marekani kutakuwa na mikutano
mingi hivyo hatutaweza kupata
nafasi nzuri ya kuzungumza
mambo yetu” akasema Dr Vivian
“Ni kweli dada.Japokuwa tuko
pamoja muda mwingi lakini
hatupati nafasi ya kuzungumza
mambo yetu ya kifamilia” akasema
Theresa na kujimiminia juice
katika glasi
“Kabla sijaingia ndegeni
nilikuwa na mazungumzo na
George Mzabwa.Nilimuuliza
amefikia wapi kuhusiana na kazi niliyompa ya kuchunguza mauaji
ya familia yetu.Amekuwa
ananikimbia kimbia kila
ninapotaka kulizungumzia jambo
hili.Jibu alilonipa
halijaniridhisha.Amesema
kwamba mpaka sasa bado
hajafanikiwa kugundua lolote.Ni
miaka miwili imepita sasa toka
nimempa kazi hiyo na ameniudhi
sana.Nimemwambia nitakaporejea
aidha nikute taarifa kwamba watu
waliofanya kitendo kile kiovu
wamepatikana au nikute barua
yake ya kuachia ngazi mezani
kwangu ama sivyo nitamuondoa
na kumpeleka sehemu nyingine
kwani ameshindwa kazi.Sielewi
kuna nini katika jambo hili hadi lishindwe kupatiwa
majibu.Ninafikiria kutafuta mtu
mwingine wa kuongoza idara ya
usalama wa taifa kwa kasi
ninayoihitaji.George hawezi
kuendana na kasi yangu” akasema
Dr Vivian
“Hata mimi nashangaa na
kujiuliza kulikoni katika suala hili?
Inawezekajane mpaka leo hii
hakuna taarifa yoyote kuhusiana
na wauaji wa familia yetu?Jeshi la
polisi wamefanya
uchunguzi,usalama wa taifa pia
lakini mpaka leo hii hakuna
chombo chochote kilichotoa
majibu ni nani waliua familia yetu
na kwa nini.Vyombo hivi vyote
viwili wanazo rasilimali za kutosha kuwawezesha kufanikisha
uchunguzi wa jambo hili lakini
mpaka leo wameshindwa kubaini
watu waliofanya unyama ule.Hapa
kuna kitu kinatia shaka dada”
akasema Theresa
“Tuachane na hayo
nitayashughulikia nitakaporejea
kwani suala hili kwa sasa
linaonekana kama fumbo gumu
lisiloweza kufumbuka.Nitalivalia
njuga mimi mwenyewe na safari
hii lazima nitapata majibu,lazima
fumbo hili lifumbuke” akasema Dr
Vivian na kumuomba Theresa
amletee juice ya mchanganyiko wa
matunda kinywaji anachokipenda
sanaNathan kanipigia simu leo
asubuhi na kunitaarifu kwamba ile
kazi yake aliyokwenda kuifanya
Uswisi imemalizika na hivyo
atanifuata New York na baada ya
mkutano kumalizika tutarejea
wote Da es salaam kuendelea na
maandalizi ya ndoa yetu.Theresa
siwezi kueleza furaha niliyonayo
kwani imebaki miezi mwili tu na
mimi niingie katika ndoa na
mwanaume ninayempenda kwa
dhati.Hata hivyo kuna kitu nataka
kukisikia toka kwako.Watu
wanaongeaje huko mitaani
kuhusiana na ndoa yangu na
Nathan? Nilitaka jambo hili liwe la
kimya kimya lakini watu
wamefukunyua hadi wakagundua ninataka kufunga ndoa”Akauliza
Dr Vivian huku
akitabasamu.Theresa akanywa
funda la juice halafu akasema
“Japokuwa Nathan ulikuwa
naye katika kipindi chote cha
kampeni na kuzunguka naye nchi
nzima lakini bado watu
hawamfahamu vizuri ni
nani.Nimekuwa napitia baadhi ya
maoni ya watu mtandaoni na
nimeona watu wanahoji kwa nini
rais wao aolewe na mtu wa kutoka
nje ya nchi?Tanzania imejaa vijana
wa kila aina wasomi na wabobezi
wa mambo mbali
mbali,haujawaona hao wote hadi
moyo wako ufunguke kwa mtu wa
taifa lingine?Lakini haya yasikuogopeshe ni mawazo tu ya
watu yanayotokea katika mijadala
mbali mbali inayoendelea huko
mitandaoni” akasema Theresa .Dr
Vivian akatabasamu nba kuuliza
“Wewe je una maoni gani?
“Kuhusu nini dada Vivi?
“Kuhusu mimi na
Nathan.Nakufahamu wewe huna
tabia ya kuficha kitu bali husema
kweli toka moyoni.Sijawahi kupata
maoni yako kuhusiana na hili suala
langu na
Nathani.Unaliongeleaje?Nathani ni
mwanaume ambaye naweza
kusema kwamba ninampenda kwa
dhati ya moyo wangu lakini je
unadhani watu wangu
watampenda na kumkubali?Tafadhali kuwa
muwazi kwangu.You are my
sister” akasema Dr Vivian
“Dada ,mapenzi kama yalivyo
hayachagui rangi,umri hata
taifa.Moyo unaweza kufunguka
kwa mtu yeyote awe
mweusi,mweupe n.k.Wewe
umeufungua moyo wako kwa
Nathan na hakuna ubaya wowote
lakini….” Theresa akasita kidogo
akanywa maji ya matunda na
kuendelea
“Umeomba nikueleze ukweli
wangu na nitakueleza ukweli
wangu japo hautakuwa mzuri sana
lakini lazima niuseme kwa kuwa
umeomba.Hakuna mtu
atakayeweza kukuzuia usiolewe na Nathan mwanaume unayempenda
kwa dhati ya moyo wako lakini
ndoa hii ingekuwa na tija zaidi
kama Nathan angekuwa ni
mtanzania.Anaweza akabadili
uraia wake na kuwa mtanzania
lakini damu yake bado ni
Marekani.Kama akiwa mumeo
yeye ndiye atakayekuwa mshauri
wako mkuu kwa mambo mbali
mbali hivyo anapaswa awe ni mtu
anayeipenda Tanzania na
kuifahamu vyema,ayafahamu
matatizo ya waTanzania na
yamguse ili aweze kukushauri
vizuri namna ya kuzitatua
changamoto mbali mbali
unazokumbana nazo katika kazi
yako.Nathani yeye ni mmarekani na Tanzania ameifahamu kwa
sababu yako tu na sina hakika
kama anaweza kuwa mshauri
mzuri katika masuala yanayohusu
Tanzania.Ikitokea akashindwa
kukushauri au akakushauri vibaya
mzigo wote wa lawama utakuwa
juu yako.Lakini haya ni mawazo
yangu tu na usiyachukulie kama
ndiyo mtazamo wa
watanzania.Nathan ni kijana mzuri
na sioni kama ana tatizo lolote”
akasema Theresa
“Theresa ahsante sana.Ndiyo
maana huwa ninapenda kukuomba
ushauri.Una mtazamo wa
mbali.Unafaa sana kuwa mshauri
wa rais na nitalitazama hilo siku za
usoni.Umezungumza mambo ya msingi na ambayo sikuwa
nimeyafikiria kabla sijakubali
kuolewa na Nathan.Vipi kuhusu
wewe na yule mtu wako Damian?
Bado mnaendelea na ugomvi
wenu? Kwa nini masuala yenu
msiyatafutie ufumbuzi na
kuyamaliza ili msonge mbele kwa
amani?
“Dada Vivi kuna mambo
mengine hayafai
kuyalazimisha.Nimetafakari sana
na kugundua mimi ndiye
niliyekuwa nalazimisha penzi
wakati mwenzangu hana muda
nami.Kila wakati mimi ndiye
niliyekuwa nikipiga magoti
kuomba msamaha hata kama si
mimi niliyekosa.Lengo lilikuwa ni kunusuru penzi letu kwa kuwa
Damian nilimpenda zaidi ya
ninavyoweza kueleza.Lakini ulifika
wakati nikasema imetosha na
nikaamua kila mmoja aendelee na
maisha yake.Niliumia mwanzoni
but now I’m happy.Nina amani ya
moyo na ninasubiri yule ambaye
ameumbwa kwa ajili yangu
ajitokeze.Naamini yupo mahala
fulani na muda ukifika nitampata”
akasema Theresa
“Hongera kwa maamuzi
hayo.Mimi nilitamani sana
kukushauri hivyo toka awali lakini
sikutaka kuingilia masuala
yako.Unapoona uko katika
mahusiano halafu wewe ndiye
mwenye kuumia kila siku na mwenzako hajali basi chukua
hatua haraka,huo uhusiano
hautakufikisha mahala
kokote.Natumai tayari umepata
somo la kutosha na utakuwa
makini safari hii kutafuta
mwanaume yule ambaye atakufaa
katika maisha yako.Ukikosea
kuchagua utaumia sana.Mapenzi
yanaumiza mno.Kuna nyakati hata
mimi ninawaza kuhusu Nathan
kama hatutakuwa na migogoro
pindi tutakapofunga ndoa.Nataka
nielekeze akili yangu katika
kuwasadia watanzania
walionichagua na kuwatatulia kero
zao na nitakuwa na muda mdogo
sana wa kushughulikia masuala ya
mapenzi.Hiki hawezi kuwakikwazo kwa Nathan na kikaleta
mgogoro kati yetu?Laiti Mungu
angeweza kunionyesha maisha
nitakayoishi nikiwa na Nathan
ningeweza kufanya maamuzi lakini
Mungu ametuficha na hatuelewi
chochote kuhusu dakika ijayo”
akasema Dr Vivian
“Usiwe na wasi wasi
dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole
na hana matatizo.Lakini …”
Theresa akasita
“Lakini nini Theresa? Mbona
umesita? Sema unachotaka
kukisema” akasema Dr
Vivian.Theresa akafikiri kidogo na
kusema
“Nothing.Ngoja nikuache
upumzike,mimi naenda kuimalizia hotuba hii halafu na mimi
nipumzike” akasema Theresa na
kuchukua kompyuta yake akatoka
mle chumbani.
“Theresa alitaka kuniambia
nini halafu akasita? Akajiuliza Dr
Vivian baada ya Theresa kutoka
mle chumbani
“Theresa si mtu wa kuficha
jambo,au aliona halina maana
ndiyo maana akaamua kuachana
nalo.Hata hivyo kuna jambo
amelizungumza la maana sana
kwangu na sikuwa nimelitilia
maanani hapo kabla.Nikiolewa na
Nathan yeye ndiye atakayekuwa
mshauri wangu katika mambo
mengi lakini atanishauri kitu gani
kama haifahamu vyema Tanzania wala matatizo ya watanzania?
Akajiuliza
“Nimetoka mbali na Nathan na
ninamfahamu vyema.Hata kama
haifahamu vizuri Tanzania wala
matatizo yake lakini nina imani
atanishauri vizuri kwani ni kijana
mpole na mwenye busara ya hali
ya juu.Sina shaka hata kidogo na
upendo wake kwangu na hata
mimi ninampenda mno na ndiyo
maana hata aliponitamkia kwamba
anataka kunioa niliruka ruka kwa
furaha.Mengi yatasemwa lakini
sitakiwi kuyasikilza.Natakiwa
kuziba masikio na kuyapuuza
kwani huyu ndiye chaguo
langu.Nathan ameingia katika kila
mshipa wa mwili wangu” akawaza na kuinuka kitandani akachukua
kompyuta yake akafungua mahala
anakohifadhi picha na kuzitazama
picha za gauni lake zuri atakalovaa
siku ya harusi yake,akatabasamu
“Sipati picha namna
nitakavyopendeza ndani ya gauni
hili lililobuniwa na mbunifu
chipukizi wa mavazi wa
kitanzania.Naamini
nitakapoonekana nimelivaa gauni
hili jina lake litapaa ulimwenguni
kwani wengi watataka kufahamu
nani alibuni vazi zuri kama hili.”
Akatabasamu na kuanza kutazama
picha nyingine za wabunifu mbali
mbali wa mavazi ya harusi
Alipotoka chumbani kwa
rais,Theresa akaenda katika moja wapo ya ofisi zilizomo ndani ya
ndege hii kubwa akachomeka
spika za masikioni katika
kompyuta yake akaanza kusikiliza
muziki.Uso wake ulionyesha
mabadiliko
“Mambo tuliyozungumza na
dada Vivi yameniharibia kabisa
siku yangu.Kwanza ni kuhusu yule
mchumba wake Nathan.Moyo
wangu haumkubali kabisa na hata
mwenyewe analifahamu hilo na
sijui kwa nini simpendi.Kila
nimuonapo karibu na dada amani
hutoweka kabisa.Najua
wanapendana lakini moyoni
mwangu hana kibali.Si kwamba
ninamchukia ila ninaona hafai
kuwa na Vivian.Nilitaka nimueleze hivyo dada lakini nikasita kwani
asingefurahia maneno hayo.Hata
hivyo siwezi kuingilia mapenzi
yao.Kama wanapendana acha
waoane lakini ningefurahi sana
kama dada yangu angeolewa na
kijana mtanzania” akawaza
Theresa na kufumbua macho
baada ya mlango kufunguliwa na
mtu kuingia mle ofisini.Alikuwa ni
waziri wa mambo ya nje
“Theresa nimekufuata
wewe,kuna kitu nataka
unisaidie.Naomba uipitie hii
hotuba yangu na uirekebishe kama
kuna mapungufu” akasema waziri
huyo na kutoka .Theresa
akaendelea kusikiliza mziki huku
akiipitia hotuba ile ya yule waziri na mara kumbu kumbu fulani
ikamjia akaacha kazi aliyokuwa
anaifanya akajiegemeza kitini
“Ni miaka zaidi ya kumi sasa
imepita lakini bado picha ya
yaliyomkuta baba haijafutika
kichwani na inanitesa kila
uchao.Nilikuwepo na nilishuhudia
kila kilichotokea.Najiuliza kwa
nini mimi?Kwa nini Mungu
akanichagua mimi niyashuhudie
yale yote? Naamini Mungu ana
sababu zake na ndiyo maana
katika watu wote ambao
walimzunguka baba alinichagua
mimi na kunibebesha mzigo huu
mzito.Kila siku ninapolikumbuka
jambo hili mwili wote hupata
baridi.Bado ile milio ya risasi zilizochukua uhai wa baba,mama
na kaka Kelvin ninaisikia
masikioni kila nilalapo.Nimebaki
natembea na siri hii nzito ambayo
hakuna anayeifahamu hata dada
Vivian hafahamu chochote.Ni mimi
pekee ninayefahamu sababu ya
baba ,mama na kaka Kelvin
kuuawa.Ni kwa sababu ya
Football” Machozi yakamtoka
“Nimekuwa najilazimisha
kutaka kulisahau jambo hili lakini
nimeshindwa.Ninaogopa kuliweka
wazi suala hili kwa ajili ya usalama
wangu na dada.Ninaogopa hata
kumueleza dada Vivian kwani
yanaweza kumkuta kama
yaliyomkuta baba .Waliomuua
baba walikuwa wanaitafuta hiyo football ni vipi endapo mpaka sasa
wakawa bado wanaitafuta?
Nitayaweka hatarini sana maisha
ya dada nikimueleza kuhusiana na
hili suala.Ngoja niendelee kulibeba
na itakuwa ni siri yangu pekee na
Mungu wangu.Nimeibeba na
kutembea na siri hii kwa zaidi ya
miaka kumi na nitaendelea
kutembea nayo.Yawezekana wale
jamaa bado wanaendelea
kutuchunguza.Sina hakika kama
watakuwa wamekata
tamaa.Lazima watakuwa
wanachunguza kwa siri ili kujua
football iko wapi.Lakini hii football
ni kitu gani?Ina siri gani ndani
yake?Baba hakuwahi kunieleza
chochote kuhusiana nayo.Ninavyofahamu mimi mkoba
ule uliopewa jina la football asili
yake ni nchini Marekani ambako
kila asafiripo rais wa Marekani
huwa anasafiri nao na ndani yake
kuna mambo ya siri ya kiusalama
kuhusiana na mambo ya
nyuklia.Hapa Tanzania rais Anorld
alianzisha mtindo wa kutembea na
begi kila anakoenda na akalipa
jina la football na baba ndiye
aliyekuwa mbebaji wake mkuu,je
kulikuwa na siri gani humo ndani
yake? Akajiuliza Theresa na
kukumbuka zikamrejesha mbali