Riwaya: The Football

HaMachiach

JF-Expert Member
Dec 15, 2015
3,399
6,077
Season 1 The Football
Mtunzi.Patrick Ck

Sehemu 1

Msafara wa rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania,uliwasili katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es
salaam.Dr Vivian Sebastian Matope
rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania akashuka garini akiwa
amevalia suti ya rangi nyeupe
iliyompendeza vilivyo.Kichwani
hakuwa amebadili mtindo wake
wa nywele.Dr Vivian hakupenda
kuweka madoido katika nywele
zake.Alipenda kuzipunguza na
kuzifanya fupi.Alikuwa na mwili
mwembamba wastani na
kumfanya awe ni mmoja kati ya
marais wanawake wazuri zaidi
duniani. Akiwa katika ulinzi mkali Dr
Vivian alianza kuelekea ndegeni
huku akisalimiana na kuagana na
baadhi ya viongozi waliofika pale
uwanjani kumuaga.Alipomaliza
kuagana na viongozi mbali mbali
akamuita pembeni mkurugenzi wa
idara ya idara ya usalama wa taifa
ndugu George Mzabwa
“George umefikia wapi
kuhusu lile suala ?Kuna chchote
kimepatikana mpaka leo? Akauliza
Dr Vivian
“Madam president lile suala
bado gumu lakini tunaendelea
kulifanyia kazi.Mpaka sasa bado
hatujafikia hatua ya kuridhisha na
ndiyo maana umeona nimekuwa
kimya sijafika kwako kukupa mrejesho wowote” Akasema
George.Dr Vivian akamtazama
akatabasamu na kusema
“Nitakaporejea nataka nikute
tayari kuna hatua imekwisha
pigwa ama sivyo nitakuondoa
katika nafasi hiyo na kuwapa
wengine wenye uwezo wa kufanya
kazi kwa kasi kama
ninavyotaka.Sioni sababu ya
kukukwamisha katika
kulishugulikia suala hili wakati
kila kitu unacho.Naomba ulifanyie
kazi hilo nililokwambia na
nitakaporejea nikute aidha ripoti
ya hili suala,au barua ya kuachia
ngazi au nikuondoe mwenyewe
katika nafasi hiyo.Tumeelewana
George? Akauliza Dr Vivian Nimekuelewa madam
president” akajibu George
“ Good” akasema Dr Vivian na
kupanda ngazi kuingia
ndegeni.Alipofika katika mlango
wa ndege akageuka na
kuwapungia mkono watu
waliokuja kumuaga halafu
akaingia ndegeni
Dr Vivian ni rais wa kwanza
mwanamke kuongoza jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Alizaliwa
22 Octoba 1970 akiwa mtoto wa
kwanza wa Kanali Sebastian
Matope na mke wake Getruda
Mazimbo.Alipata elimu yake ya
msingi katika shule ya msingi
Azimio mjini Dodoma ambako
baba yake alikuwa akifanya kazi wakati huo.Alijiunga na shule ya
sekondari ya St Bernadetha
inayomilikiwa na masista wa
shirika la mtakatifu Bernadetha
iliyoko mkoani Kilimanjaro.Lengo
kuu la kujiunga na shule hiyo iliyo
chini ya watawa ilikuwa ni
kujiunga na maishaya utawa.Toka
akiwa mtoto dogo Dr Vivian
aliyapernda maisha yale ya
kitawa.Alisoma katika shule hiyo
hadi kidato cha sita na matokeo
yalipotoka Vivian alifaulu kwa
kiwango cha juu kwa kupata
daraja la kwanza.Matokeo hayo
yalimfanya Vivian abadili lengo
lake la kuwa mtawa na akachagua
kuendelea na masomo ya udaktari
.Aliendelea na elimu ya juu katika fani ya udaktari katika vyuo vikuu
kwenye nchi mbali mbali kama vile
Israel,Cuba,Urusi,Marekani na
China.Mwaka 2007 aliamua
kurejea nchini Tanzania baada ya
familia yake yaani wazazi wake
wote na mdogo wake kuuawa na
watu wasiojulikana.
Baada ya kurejea nchini Dr
Vivian alifanya kazi kama daktari
wa watoto katika hospitali ya taifa
ya Muhimbili.Alianza kujiingiza
taratibu katika siasa na kutokana
na kipawa chake kikubwa cha
uongozi alichokuwa nacho,Dr
Vivian alijikuta akishika nafasi
kadhaa ndani ya chama na hapo
ndipo alipoanza
kujulikana.Daktari huyu mwenye haiba ya kipekee,mwenye urefu wa
5.8.ngozi nyororo na uso
usiokauka tabasamu alifahamika
sana kwa misimamo yake thabiti
isiyoyumba katika yale mambo
anayoyaamini na hasa katika
kusimamia haki za watu wa hali za
chini wanaokandamizwa.
Tabia yake hii ya msimamo
usiotetereka ilianza kuonekana
pale alipokuwa rais wa serikali ya
wanafunzi katika chuo kikuu
kimoja alichosoma nchini
Marekani.Katika chuo hicho kikuu
wanafunzi wenye asili ya Afrika
walikuwa wanabaguliwa na
kutopewa kipaumbele katika
mambo mengi.Haikuwa rahisi
kwake kuweza kushinda nafasi ya rais wa serikali ya wanafunzi na
aliposhinda kitu cha kwanza
alichoanza kukishughulikia ni
suala la ubaguzi uliokithiri hapo
chuoni.Jambo hili lilimletea
misukosuko mikubwa na hata
kuondolewa katika nafasi yake ya
rais wa wanafunzi baada ya
kuonekana anakiuka sheria za
chuo lakini hii haikumkatisha
tamaa kuendelea kuwapigania
wale waliokuwa
wanabaguliwa.Baada ya mvutano
mkali na chuo hicho hatimaye
ushindi ukapatikana na taratibu za
chuo zikabadilishwa,wanafunzo
wote wakawa na haki sawa.Kwa
wale wanaofuatilia mambo ya
nyota,hii ilikuwa ni ishara tosha kwamba nyota ya Dr Vivian ilianza
kung’aa na siku moja ingeweza
kung’aa na kutoa mwangaza
mkubwa
Wakati akiendelea na
masomo yake aliwahi kuchaguliwa
kuwa msemaji wa wanafunzi
wenye asili ya Afrika katika katika
vyuo vikuu vya Marekani na katika
mojawapo ya hotuba aliyowahi
kuitoa katika kongamano
lililofanyika siku ya kuikumbuka
hotuba aliyoitoa mwanaharakati
aliyepigania haki za watu weusi
nchini Marekani Martin Luther
aliyoitoa 28 August 1963,Vivian
aliweka wazi ndoto yake ya
kuliona siku moja bara la Afrika
linatoka gizani na kuwa bara lenye nuru na nguvu.Alieleza
kusikitishwa kwake na
ukandamizwaji na unyonyaji
unaofanywa na mataifa makubwa
yenye nguvu dhidi ya mataifa
masikini ya bara la Afrika.Hotuba
hii iliyojaa msisimko iliwavutia
watu wengi na kumfanya Vivian
ajulikane na kualikuwa katika
makongamano mbali mbali.Katika
mojawapo ya hotuba alizowahi
kutoa aliweka wazi nia yake ya
siku moja kuwa kiongozi na
kuziunganisha nchi zote za Afrika
na kuwa nchi nmoja yenye nguvu
kijeshi na kiuchumi. Alitamani
siku moja awe rais wa kwanza wa
Afrika na kuongoza bara hili lenye
kila aina ya utajiri. Alipofanikiwa kushinda nafasi
ya urais wa Tanzania,Dr Vivian
amefanya mambo makubwa kwa
muda wa miaka miwili ambayo
amekuwa madarakani.Ni rais
mdogo kwa umri ukilinganisha na
marais wengi wa mataifa mengine
lakini mambo makubwa
aliyoyafanya yamewashangaza
wengi.Ni rais asiyesita kuchukua
maamuzi magumu na
asiyetetereka katika maamuzi
yake.Huyu ndiye Dr Vivian rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye amepewa jina la utani la
Dr White kutokana na staili yake
ya kipekee ya kupenda rangi
nyeupe kuanzia mavazi yake hadi
magari yanayotumika katika msafara wake.Mara chache sana
huonekana katika mavazi ya rangi
nyingine lakini siku zote huwa
katika mavazi meupe.
Baada ya kuingia ndegeni Dr
Vivian akasalimiana na marubani
na wahudumu wa ndege yake na
kujiandaa kwa ajili ya kuelekea
jijini New York Marekani
kuhudhuria mkutano mkuu wa
umoja wa mataifa unaofanyika kila
mwaka na ambao huudhuriwa na
wakuu wote wa nchi wanachama
wa umoja wa mataifa.Huu ni
mkutano wake wa kwanza
kuhudhuria tangu achaguliwe
kuwa rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.Mkutano
uliopita aliwakilishwa na makamu wa rais na mwaka huu
anahudhuria yeye
mwenyewe.Katika safari hii
aliongozana na mawaziri
wanne,maafisa wengine kadhaa
pamoja na walinzi wake na jumla
msafara wake ulikuwa na watu
ishirini.
Ndege ilikaa katika njia yake
ya kurukia ikaanza kuondoka
taratibu na kuongeza kasi kisha
ikapaa huku viongozi waliofika
pale uwanjani kumuaga rais
wakipunga mikono kumtakia rais
na ujumbe wake safari
njema.Ndege ilipokaa sawa
angani,Dr Viviana akaitisha kikao
na watendaji alioambatana nao
katika safari ile.Walikutana katika chumba cha mikutano kilichomo
ndani ya ndege ile kubwa chenye
uwezo wa kuchukua watu zaidi ya
ishirini.Walijadiliana mambo
kadhaa kuhusiana na safari yao ile
na baada ya takribani saa moja na
nusu kikao kikamalizika wajumbe
wakatoka na rais akaenda katika
chumba chake kupumzika kwani
safari ile ilikuwa ndefu.Akiwa
chumbani akamuita mdogo wake
Theresa.
Theresa Sebastian Matope ni
msichana mwenye weusi wa
kung’aa na umbo la
kupendeza.Wazazi wa Dr Vivian
walimchukua Theresa toka katika
kituo cha kulelea watoto yatima
akiwa mtoto mdogo sana na kumlea kama mtoto wao wa
kumzaa.Kwa hivi sasa ndiye
mwandishi wa hotuba za rais
“Theresa naomba nione
hotuba uliyoiandaa ninayokwenda
kuitoa New York” Akasema Dr
Vivian baada ya Theresa kuingia
mle chumbani kwake.Theresa
akatoka na kwenda kuchukua
kompyuta yake akarejea na
kumuonyesha Dr Vivian hotuba ile
aliyokuwa anaiandaa
“Imebaki sehemu ndogo ya
kumalizia kuhusiana na
mabadiliko ya tabia nchi Afrika”
Akasema Theresa na Dr Vivian
akaipitia hotuba ile taratibu halafu
akasema Hii ni hotuba nzuri sana
lakini bado haijafikia kiwango
ninachokihitaji.Hii ni hotuba
yangu ya kwanza katika mkutano
huu mkubwa na ninataka iwe kali
na yenye msisimko.Nimezoeleka
hotuba zangu huwa zinakuwa kali
na zenye msisimko.Nataka
viongozi wa dunia waelewe
msimamo wangu na wa Tanzania
katika mambo mbali mbali hivyo
iongeze ukali hotuba hii” akasema
Dr Vivian
“Dada labda uniweke wazi
unataka nilenge maeneo yapi
hasa.Ulinipa mambo ya kuzingatia
wakati wa kuiandaa hotuba hii na
nimeyafuata ,nimelenga mambo ya
uchumi,misaada ya masharti na unyonyaji wa rasilimali
zetu,mabadiliko ya tabia nchi na
mengineyo” akasema Theresa.Dr
Vivian akaitazama tena hotuba ile
na kusema
“Hotuba hii si mbaya,imekaa
vizuri lakini kuna sehemu ambazo
zinahitaji lugha kali zaidi
kuonyesha msisitizo.Hotuba hii
imepoa sana.Lakini usijali endelea
nayo na utakapomaliza niletee
nitaisahihisha
mwenyewe,samahani kama
nimekukwaza” akasema Dr Vivian
“Usijali dada” akasema
Theresa na kuchukua kompyuta
yake ili atoke Vivian akamuomba
asubiri.Kaa nami kidogo
Theresa,bado tunayo safari
ndefu.Nyakati kama hizi ndipo
tunaweza kukaa na kuongea
mambo yanayotuhusu sisi.Tukifika
marekani kutakuwa na mikutano
mingi hivyo hatutaweza kupata
nafasi nzuri ya kuzungumza
mambo yetu” akasema Dr Vivian
“Ni kweli dada.Japokuwa tuko
pamoja muda mwingi lakini
hatupati nafasi ya kuzungumza
mambo yetu ya kifamilia” akasema
Theresa na kujimiminia juice
katika glasi
“Kabla sijaingia ndegeni
nilikuwa na mazungumzo na
George Mzabwa.Nilimuuliza
amefikia wapi kuhusiana na kazi niliyompa ya kuchunguza mauaji
ya familia yetu.Amekuwa
ananikimbia kimbia kila
ninapotaka kulizungumzia jambo
hili.Jibu alilonipa
halijaniridhisha.Amesema
kwamba mpaka sasa bado
hajafanikiwa kugundua lolote.Ni
miaka miwili imepita sasa toka
nimempa kazi hiyo na ameniudhi
sana.Nimemwambia nitakaporejea
aidha nikute taarifa kwamba watu
waliofanya kitendo kile kiovu
wamepatikana au nikute barua
yake ya kuachia ngazi mezani
kwangu ama sivyo nitamuondoa
na kumpeleka sehemu nyingine
kwani ameshindwa kazi.Sielewi
kuna nini katika jambo hili hadi lishindwe kupatiwa
majibu.Ninafikiria kutafuta mtu
mwingine wa kuongoza idara ya
usalama wa taifa kwa kasi
ninayoihitaji.George hawezi
kuendana na kasi yangu” akasema
Dr Vivian
“Hata mimi nashangaa na
kujiuliza kulikoni katika suala hili?
Inawezekajane mpaka leo hii
hakuna taarifa yoyote kuhusiana
na wauaji wa familia yetu?Jeshi la
polisi wamefanya
uchunguzi,usalama wa taifa pia
lakini mpaka leo hii hakuna
chombo chochote kilichotoa
majibu ni nani waliua familia yetu
na kwa nini.Vyombo hivi vyote
viwili wanazo rasilimali za kutosha kuwawezesha kufanikisha
uchunguzi wa jambo hili lakini
mpaka leo wameshindwa kubaini
watu waliofanya unyama ule.Hapa
kuna kitu kinatia shaka dada”
akasema Theresa
“Tuachane na hayo
nitayashughulikia nitakaporejea
kwani suala hili kwa sasa
linaonekana kama fumbo gumu
lisiloweza kufumbuka.Nitalivalia
njuga mimi mwenyewe na safari
hii lazima nitapata majibu,lazima
fumbo hili lifumbuke” akasema Dr
Vivian na kumuomba Theresa
amletee juice ya mchanganyiko wa
matunda kinywaji anachokipenda
sanaNathan kanipigia simu leo
asubuhi na kunitaarifu kwamba ile
kazi yake aliyokwenda kuifanya
Uswisi imemalizika na hivyo
atanifuata New York na baada ya
mkutano kumalizika tutarejea
wote Da es salaam kuendelea na
maandalizi ya ndoa yetu.Theresa
siwezi kueleza furaha niliyonayo
kwani imebaki miezi mwili tu na
mimi niingie katika ndoa na
mwanaume ninayempenda kwa
dhati.Hata hivyo kuna kitu nataka
kukisikia toka kwako.Watu
wanaongeaje huko mitaani
kuhusiana na ndoa yangu na
Nathan? Nilitaka jambo hili liwe la
kimya kimya lakini watu
wamefukunyua hadi wakagundua ninataka kufunga ndoa”Akauliza
Dr Vivian huku
akitabasamu.Theresa akanywa
funda la juice halafu akasema
“Japokuwa Nathan ulikuwa
naye katika kipindi chote cha
kampeni na kuzunguka naye nchi
nzima lakini bado watu
hawamfahamu vizuri ni
nani.Nimekuwa napitia baadhi ya
maoni ya watu mtandaoni na
nimeona watu wanahoji kwa nini
rais wao aolewe na mtu wa kutoka
nje ya nchi?Tanzania imejaa vijana
wa kila aina wasomi na wabobezi
wa mambo mbali
mbali,haujawaona hao wote hadi
moyo wako ufunguke kwa mtu wa
taifa lingine?Lakini haya yasikuogopeshe ni mawazo tu ya
watu yanayotokea katika mijadala
mbali mbali inayoendelea huko
mitandaoni” akasema Theresa .Dr
Vivian akatabasamu nba kuuliza
“Wewe je una maoni gani?
“Kuhusu nini dada Vivi?
“Kuhusu mimi na
Nathan.Nakufahamu wewe huna
tabia ya kuficha kitu bali husema
kweli toka moyoni.Sijawahi kupata
maoni yako kuhusiana na hili suala
langu na
Nathani.Unaliongeleaje?Nathani ni
mwanaume ambaye naweza
kusema kwamba ninampenda kwa
dhati ya moyo wangu lakini je
unadhani watu wangu
watampenda na kumkubali?Tafadhali kuwa
muwazi kwangu.You are my
sister” akasema Dr Vivian
“Dada ,mapenzi kama yalivyo
hayachagui rangi,umri hata
taifa.Moyo unaweza kufunguka
kwa mtu yeyote awe
mweusi,mweupe n.k.Wewe
umeufungua moyo wako kwa
Nathan na hakuna ubaya wowote
lakini….” Theresa akasita kidogo
akanywa maji ya matunda na
kuendelea
“Umeomba nikueleze ukweli
wangu na nitakueleza ukweli
wangu japo hautakuwa mzuri sana
lakini lazima niuseme kwa kuwa
umeomba.Hakuna mtu
atakayeweza kukuzuia usiolewe na Nathan mwanaume unayempenda
kwa dhati ya moyo wako lakini
ndoa hii ingekuwa na tija zaidi
kama Nathan angekuwa ni
mtanzania.Anaweza akabadili
uraia wake na kuwa mtanzania
lakini damu yake bado ni
Marekani.Kama akiwa mumeo
yeye ndiye atakayekuwa mshauri
wako mkuu kwa mambo mbali
mbali hivyo anapaswa awe ni mtu
anayeipenda Tanzania na
kuifahamu vyema,ayafahamu
matatizo ya waTanzania na
yamguse ili aweze kukushauri
vizuri namna ya kuzitatua
changamoto mbali mbali
unazokumbana nazo katika kazi
yako.Nathani yeye ni mmarekani na Tanzania ameifahamu kwa
sababu yako tu na sina hakika
kama anaweza kuwa mshauri
mzuri katika masuala yanayohusu
Tanzania.Ikitokea akashindwa
kukushauri au akakushauri vibaya
mzigo wote wa lawama utakuwa
juu yako.Lakini haya ni mawazo
yangu tu na usiyachukulie kama
ndiyo mtazamo wa
watanzania.Nathan ni kijana mzuri
na sioni kama ana tatizo lolote”
akasema Theresa
“Theresa ahsante sana.Ndiyo
maana huwa ninapenda kukuomba
ushauri.Una mtazamo wa
mbali.Unafaa sana kuwa mshauri
wa rais na nitalitazama hilo siku za
usoni.Umezungumza mambo ya msingi na ambayo sikuwa
nimeyafikiria kabla sijakubali
kuolewa na Nathan.Vipi kuhusu
wewe na yule mtu wako Damian?
Bado mnaendelea na ugomvi
wenu? Kwa nini masuala yenu
msiyatafutie ufumbuzi na
kuyamaliza ili msonge mbele kwa
amani?
“Dada Vivi kuna mambo
mengine hayafai
kuyalazimisha.Nimetafakari sana
na kugundua mimi ndiye
niliyekuwa nalazimisha penzi
wakati mwenzangu hana muda
nami.Kila wakati mimi ndiye
niliyekuwa nikipiga magoti
kuomba msamaha hata kama si
mimi niliyekosa.Lengo lilikuwa ni kunusuru penzi letu kwa kuwa
Damian nilimpenda zaidi ya
ninavyoweza kueleza.Lakini ulifika
wakati nikasema imetosha na
nikaamua kila mmoja aendelee na
maisha yake.Niliumia mwanzoni
but now I’m happy.Nina amani ya
moyo na ninasubiri yule ambaye
ameumbwa kwa ajili yangu
ajitokeze.Naamini yupo mahala
fulani na muda ukifika nitampata”
akasema Theresa
“Hongera kwa maamuzi
hayo.Mimi nilitamani sana
kukushauri hivyo toka awali lakini
sikutaka kuingilia masuala
yako.Unapoona uko katika
mahusiano halafu wewe ndiye
mwenye kuumia kila siku na mwenzako hajali basi chukua
hatua haraka,huo uhusiano
hautakufikisha mahala
kokote.Natumai tayari umepata
somo la kutosha na utakuwa
makini safari hii kutafuta
mwanaume yule ambaye atakufaa
katika maisha yako.Ukikosea
kuchagua utaumia sana.Mapenzi
yanaumiza mno.Kuna nyakati hata
mimi ninawaza kuhusu Nathan
kama hatutakuwa na migogoro
pindi tutakapofunga ndoa.Nataka
nielekeze akili yangu katika
kuwasadia watanzania
walionichagua na kuwatatulia kero
zao na nitakuwa na muda mdogo
sana wa kushughulikia masuala ya
mapenzi.Hiki hawezi kuwakikwazo kwa Nathan na kikaleta
mgogoro kati yetu?Laiti Mungu
angeweza kunionyesha maisha
nitakayoishi nikiwa na Nathan
ningeweza kufanya maamuzi lakini
Mungu ametuficha na hatuelewi
chochote kuhusu dakika ijayo”
akasema Dr Vivian
“Usiwe na wasi wasi
dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole
na hana matatizo.Lakini …”
Theresa akasita
“Lakini nini Theresa? Mbona
umesita? Sema unachotaka
kukisema” akasema Dr
Vivian.Theresa akafikiri kidogo na
kusema
“Nothing.Ngoja nikuache
upumzike,mimi naenda kuimalizia hotuba hii halafu na mimi
nipumzike” akasema Theresa na
kuchukua kompyuta yake akatoka
mle chumbani.
“Theresa alitaka kuniambia
nini halafu akasita? Akajiuliza Dr
Vivian baada ya Theresa kutoka
mle chumbani
“Theresa si mtu wa kuficha
jambo,au aliona halina maana
ndiyo maana akaamua kuachana
nalo.Hata hivyo kuna jambo
amelizungumza la maana sana
kwangu na sikuwa nimelitilia
maanani hapo kabla.Nikiolewa na
Nathan yeye ndiye atakayekuwa
mshauri wangu katika mambo
mengi lakini atanishauri kitu gani
kama haifahamu vyema Tanzania wala matatizo ya watanzania?
Akajiuliza
“Nimetoka mbali na Nathan na
ninamfahamu vyema.Hata kama
haifahamu vizuri Tanzania wala
matatizo yake lakini nina imani
atanishauri vizuri kwani ni kijana
mpole na mwenye busara ya hali
ya juu.Sina shaka hata kidogo na
upendo wake kwangu na hata
mimi ninampenda mno na ndiyo
maana hata aliponitamkia kwamba
anataka kunioa niliruka ruka kwa
furaha.Mengi yatasemwa lakini
sitakiwi kuyasikilza.Natakiwa
kuziba masikio na kuyapuuza
kwani huyu ndiye chaguo
langu.Nathan ameingia katika kila
mshipa wa mwili wangu” akawaza na kuinuka kitandani akachukua
kompyuta yake akafungua mahala
anakohifadhi picha na kuzitazama
picha za gauni lake zuri atakalovaa
siku ya harusi yake,akatabasamu
“Sipati picha namna
nitakavyopendeza ndani ya gauni
hili lililobuniwa na mbunifu
chipukizi wa mavazi wa
kitanzania.Naamini
nitakapoonekana nimelivaa gauni
hili jina lake litapaa ulimwenguni
kwani wengi watataka kufahamu
nani alibuni vazi zuri kama hili.”
Akatabasamu na kuanza kutazama
picha nyingine za wabunifu mbali
mbali wa mavazi ya harusi
Alipotoka chumbani kwa
rais,Theresa akaenda katika moja wapo ya ofisi zilizomo ndani ya
ndege hii kubwa akachomeka
spika za masikioni katika
kompyuta yake akaanza kusikiliza
muziki.Uso wake ulionyesha
mabadiliko
“Mambo tuliyozungumza na
dada Vivi yameniharibia kabisa
siku yangu.Kwanza ni kuhusu yule
mchumba wake Nathan.Moyo
wangu haumkubali kabisa na hata
mwenyewe analifahamu hilo na
sijui kwa nini simpendi.Kila
nimuonapo karibu na dada amani
hutoweka kabisa.Najua
wanapendana lakini moyoni
mwangu hana kibali.Si kwamba
ninamchukia ila ninaona hafai
kuwa na Vivian.Nilitaka nimueleze hivyo dada lakini nikasita kwani
asingefurahia maneno hayo.Hata
hivyo siwezi kuingilia mapenzi
yao.Kama wanapendana acha
waoane lakini ningefurahi sana
kama dada yangu angeolewa na
kijana mtanzania” akawaza
Theresa na kufumbua macho
baada ya mlango kufunguliwa na
mtu kuingia mle ofisini.Alikuwa ni
waziri wa mambo ya nje
“Theresa nimekufuata
wewe,kuna kitu nataka
unisaidie.Naomba uipitie hii
hotuba yangu na uirekebishe kama
kuna mapungufu” akasema waziri
huyo na kutoka .Theresa
akaendelea kusikiliza mziki huku
akiipitia hotuba ile ya yule waziri na mara kumbu kumbu fulani
ikamjia akaacha kazi aliyokuwa
anaifanya akajiegemeza kitini
“Ni miaka zaidi ya kumi sasa
imepita lakini bado picha ya
yaliyomkuta baba haijafutika
kichwani na inanitesa kila
uchao.Nilikuwepo na nilishuhudia
kila kilichotokea.Najiuliza kwa
nini mimi?Kwa nini Mungu
akanichagua mimi niyashuhudie
yale yote? Naamini Mungu ana
sababu zake na ndiyo maana
katika watu wote ambao
walimzunguka baba alinichagua
mimi na kunibebesha mzigo huu
mzito.Kila siku ninapolikumbuka
jambo hili mwili wote hupata
baridi.Bado ile milio ya risasi zilizochukua uhai wa baba,mama
na kaka Kelvin ninaisikia
masikioni kila nilalapo.Nimebaki
natembea na siri hii nzito ambayo
hakuna anayeifahamu hata dada
Vivian hafahamu chochote.Ni mimi
pekee ninayefahamu sababu ya
baba ,mama na kaka Kelvin
kuuawa.Ni kwa sababu ya
Football” Machozi yakamtoka
“Nimekuwa najilazimisha
kutaka kulisahau jambo hili lakini
nimeshindwa.Ninaogopa kuliweka
wazi suala hili kwa ajili ya usalama
wangu na dada.Ninaogopa hata
kumueleza dada Vivian kwani
yanaweza kumkuta kama
yaliyomkuta baba .Waliomuua
baba walikuwa wanaitafuta hiyo football ni vipi endapo mpaka sasa
wakawa bado wanaitafuta?
Nitayaweka hatarini sana maisha
ya dada nikimueleza kuhusiana na
hili suala.Ngoja niendelee kulibeba
na itakuwa ni siri yangu pekee na
Mungu wangu.Nimeibeba na
kutembea na siri hii kwa zaidi ya
miaka kumi na nitaendelea
kutembea nayo.Yawezekana wale
jamaa bado wanaendelea
kutuchunguza.Sina hakika kama
watakuwa wamekata
tamaa.Lazima watakuwa
wanachunguza kwa siri ili kujua
football iko wapi.Lakini hii football
ni kitu gani?Ina siri gani ndani
yake?Baba hakuwahi kunieleza
chochote kuhusiana nayo.Ninavyofahamu mimi mkoba
ule uliopewa jina la football asili
yake ni nchini Marekani ambako
kila asafiripo rais wa Marekani
huwa anasafiri nao na ndani yake
kuna mambo ya siri ya kiusalama
kuhusiana na mambo ya
nyuklia.Hapa Tanzania rais Anorld
alianzisha mtindo wa kutembea na
begi kila anakoenda na akalipa
jina la football na baba ndiye
aliyekuwa mbebaji wake mkuu,je
kulikuwa na siri gani humo ndani
yake? Akajiuliza Theresa na
kukumbuka zikamrejesha mbali
 
Nemesis,Tumosa,ADK,mbobo,Abuu Share,yusuphu lubuva,Madamu S,Shunie,ram,mbududa,Tater,chodo1990,Toyota escudo,indundidotcom,boy lanugo,Jackal,tembobrek,nipo2,muxa,naima4730
 
Season 1 The Football
Mtunzi.Patrick Ck

Sehemu 1

Msafara wa rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania,uliwasili katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es
salaam.Dr Vivian Sebastian Matope
rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania akashuka garini akiwa
amevalia suti ya rangi nyeupe
iliyompendeza vilivyo.Kichwani
hakuwa amebadili mtindo wake
wa nywele.Dr Vivian hakupenda
kuweka madoido katika nywele
zake.Alipenda kuzipunguza na
kuzifanya fupi.Alikuwa na mwili
mwembamba wastani na
kumfanya awe ni mmoja kati ya
marais wanawake wazuri zaidi
duniani. Akiwa katika ulinzi mkali Dr
Vivian alianza kuelekea ndegeni
huku akisalimiana na kuagana na
baadhi ya viongozi waliofika pale
uwanjani kumuaga.Alipomaliza
kuagana na viongozi mbali mbali
akamuita pembeni mkurugenzi wa
idara ya idara ya usalama wa taifa
ndugu George Mzabwa
“George umefikia wapi
kuhusu lile suala ?Kuna chchote
kimepatikana mpaka leo? Akauliza
Dr Vivian
“Madam president lile suala
bado gumu lakini tunaendelea
kulifanyia kazi.Mpaka sasa bado
hatujafikia hatua ya kuridhisha na
ndiyo maana umeona nimekuwa
kimya sijafika kwako kukupa mrejesho wowote” Akasema
George.Dr Vivian akamtazama
akatabasamu na kusema
“Nitakaporejea nataka nikute
tayari kuna hatua imekwisha
pigwa ama sivyo nitakuondoa
katika nafasi hiyo na kuwapa
wengine wenye uwezo wa kufanya
kazi kwa kasi kama
ninavyotaka.Sioni sababu ya
kukukwamisha katika
kulishugulikia suala hili wakati
kila kitu unacho.Naomba ulifanyie
kazi hilo nililokwambia na
nitakaporejea nikute aidha ripoti
ya hili suala,au barua ya kuachia
ngazi au nikuondoe mwenyewe
katika nafasi hiyo.Tumeelewana
George? Akauliza Dr Vivian Nimekuelewa madam
president” akajibu George
“ Good” akasema Dr Vivian na
kupanda ngazi kuingia
ndegeni.Alipofika katika mlango
wa ndege akageuka na
kuwapungia mkono watu
waliokuja kumuaga halafu
akaingia ndegeni
Dr Vivian ni rais wa kwanza
mwanamke kuongoza jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Alizaliwa
22 Octoba 1970 akiwa mtoto wa
kwanza wa Kanali Sebastian
Matope na mke wake Getruda
Mazimbo.Alipata elimu yake ya
msingi katika shule ya msingi
Azimio mjini Dodoma ambako
baba yake alikuwa akifanya kazi wakati huo.Alijiunga na shule ya
sekondari ya St Bernadetha
inayomilikiwa na masista wa
shirika la mtakatifu Bernadetha
iliyoko mkoani Kilimanjaro.Lengo
kuu la kujiunga na shule hiyo iliyo
chini ya watawa ilikuwa ni
kujiunga na maishaya utawa.Toka
akiwa mtoto dogo Dr Vivian
aliyapernda maisha yale ya
kitawa.Alisoma katika shule hiyo
hadi kidato cha sita na matokeo
yalipotoka Vivian alifaulu kwa
kiwango cha juu kwa kupata
daraja la kwanza.Matokeo hayo
yalimfanya Vivian abadili lengo
lake la kuwa mtawa na akachagua
kuendelea na masomo ya udaktari
.Aliendelea na elimu ya juu katika fani ya udaktari katika vyuo vikuu
kwenye nchi mbali mbali kama vile
Israel,Cuba,Urusi,Marekani na
China.Mwaka 2007 aliamua
kurejea nchini Tanzania baada ya
familia yake yaani wazazi wake
wote na mdogo wake kuuawa na
watu wasiojulikana.
Baada ya kurejea nchini Dr
Vivian alifanya kazi kama daktari
wa watoto katika hospitali ya taifa
ya Muhimbili.Alianza kujiingiza
taratibu katika siasa na kutokana
na kipawa chake kikubwa cha
uongozi alichokuwa nacho,Dr
Vivian alijikuta akishika nafasi
kadhaa ndani ya chama na hapo
ndipo alipoanza
kujulikana.Daktari huyu mwenye haiba ya kipekee,mwenye urefu wa
5.8.ngozi nyororo na uso
usiokauka tabasamu alifahamika
sana kwa misimamo yake thabiti
isiyoyumba katika yale mambo
anayoyaamini na hasa katika
kusimamia haki za watu wa hali za
chini wanaokandamizwa.
Tabia yake hii ya msimamo
usiotetereka ilianza kuonekana
pale alipokuwa rais wa serikali ya
wanafunzi katika chuo kikuu
kimoja alichosoma nchini
Marekani.Katika chuo hicho kikuu
wanafunzi wenye asili ya Afrika
walikuwa wanabaguliwa na
kutopewa kipaumbele katika
mambo mengi.Haikuwa rahisi
kwake kuweza kushinda nafasi ya rais wa serikali ya wanafunzi na
aliposhinda kitu cha kwanza
alichoanza kukishughulikia ni
suala la ubaguzi uliokithiri hapo
chuoni.Jambo hili lilimletea
misukosuko mikubwa na hata
kuondolewa katika nafasi yake ya
rais wa wanafunzi baada ya
kuonekana anakiuka sheria za
chuo lakini hii haikumkatisha
tamaa kuendelea kuwapigania
wale waliokuwa
wanabaguliwa.Baada ya mvutano
mkali na chuo hicho hatimaye
ushindi ukapatikana na taratibu za
chuo zikabadilishwa,wanafunzo
wote wakawa na haki sawa.Kwa
wale wanaofuatilia mambo ya
nyota,hii ilikuwa ni ishara tosha kwamba nyota ya Dr Vivian ilianza
kung’aa na siku moja ingeweza
kung’aa na kutoa mwangaza
mkubwa
Wakati akiendelea na
masomo yake aliwahi kuchaguliwa
kuwa msemaji wa wanafunzi
wenye asili ya Afrika katika katika
vyuo vikuu vya Marekani na katika
mojawapo ya hotuba aliyowahi
kuitoa katika kongamano
lililofanyika siku ya kuikumbuka
hotuba aliyoitoa mwanaharakati
aliyepigania haki za watu weusi
nchini Marekani Martin Luther
aliyoitoa 28 August 1963,Vivian
aliweka wazi ndoto yake ya
kuliona siku moja bara la Afrika
linatoka gizani na kuwa bara lenye nuru na nguvu.Alieleza
kusikitishwa kwake na
ukandamizwaji na unyonyaji
unaofanywa na mataifa makubwa
yenye nguvu dhidi ya mataifa
masikini ya bara la Afrika.Hotuba
hii iliyojaa msisimko iliwavutia
watu wengi na kumfanya Vivian
ajulikane na kualikuwa katika
makongamano mbali mbali.Katika
mojawapo ya hotuba alizowahi
kutoa aliweka wazi nia yake ya
siku moja kuwa kiongozi na
kuziunganisha nchi zote za Afrika
na kuwa nchi nmoja yenye nguvu
kijeshi na kiuchumi. Alitamani
siku moja awe rais wa kwanza wa
Afrika na kuongoza bara hili lenye
kila aina ya utajiri. Alipofanikiwa kushinda nafasi
ya urais wa Tanzania,Dr Vivian
amefanya mambo makubwa kwa
muda wa miaka miwili ambayo
amekuwa madarakani.Ni rais
mdogo kwa umri ukilinganisha na
marais wengi wa mataifa mengine
lakini mambo makubwa
aliyoyafanya yamewashangaza
wengi.Ni rais asiyesita kuchukua
maamuzi magumu na
asiyetetereka katika maamuzi
yake.Huyu ndiye Dr Vivian rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye amepewa jina la utani la
Dr White kutokana na staili yake
ya kipekee ya kupenda rangi
nyeupe kuanzia mavazi yake hadi
magari yanayotumika katika msafara wake.Mara chache sana
huonekana katika mavazi ya rangi
nyingine lakini siku zote huwa
katika mavazi meupe.
Baada ya kuingia ndegeni Dr
Vivian akasalimiana na marubani
na wahudumu wa ndege yake na
kujiandaa kwa ajili ya kuelekea
jijini New York Marekani
kuhudhuria mkutano mkuu wa
umoja wa mataifa unaofanyika kila
mwaka na ambao huudhuriwa na
wakuu wote wa nchi wanachama
wa umoja wa mataifa.Huu ni
mkutano wake wa kwanza
kuhudhuria tangu achaguliwe
kuwa rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.Mkutano
uliopita aliwakilishwa na makamu wa rais na mwaka huu
anahudhuria yeye
mwenyewe.Katika safari hii
aliongozana na mawaziri
wanne,maafisa wengine kadhaa
pamoja na walinzi wake na jumla
msafara wake ulikuwa na watu
ishirini.
Ndege ilikaa katika njia yake
ya kurukia ikaanza kuondoka
taratibu na kuongeza kasi kisha
ikapaa huku viongozi waliofika
pale uwanjani kumuaga rais
wakipunga mikono kumtakia rais
na ujumbe wake safari
njema.Ndege ilipokaa sawa
angani,Dr Viviana akaitisha kikao
na watendaji alioambatana nao
katika safari ile.Walikutana katika chumba cha mikutano kilichomo
ndani ya ndege ile kubwa chenye
uwezo wa kuchukua watu zaidi ya
ishirini.Walijadiliana mambo
kadhaa kuhusiana na safari yao ile
na baada ya takribani saa moja na
nusu kikao kikamalizika wajumbe
wakatoka na rais akaenda katika
chumba chake kupumzika kwani
safari ile ilikuwa ndefu.Akiwa
chumbani akamuita mdogo wake
Theresa.
Theresa Sebastian Matope ni
msichana mwenye weusi wa
kung’aa na umbo la
kupendeza.Wazazi wa Dr Vivian
walimchukua Theresa toka katika
kituo cha kulelea watoto yatima
akiwa mtoto mdogo sana na kumlea kama mtoto wao wa
kumzaa.Kwa hivi sasa ndiye
mwandishi wa hotuba za rais
“Theresa naomba nione
hotuba uliyoiandaa ninayokwenda
kuitoa New York” Akasema Dr
Vivian baada ya Theresa kuingia
mle chumbani kwake.Theresa
akatoka na kwenda kuchukua
kompyuta yake akarejea na
kumuonyesha Dr Vivian hotuba ile
aliyokuwa anaiandaa
“Imebaki sehemu ndogo ya
kumalizia kuhusiana na
mabadiliko ya tabia nchi Afrika”
Akasema Theresa na Dr Vivian
akaipitia hotuba ile taratibu halafu
akasema Hii ni hotuba nzuri sana
lakini bado haijafikia kiwango
ninachokihitaji.Hii ni hotuba
yangu ya kwanza katika mkutano
huu mkubwa na ninataka iwe kali
na yenye msisimko.Nimezoeleka
hotuba zangu huwa zinakuwa kali
na zenye msisimko.Nataka
viongozi wa dunia waelewe
msimamo wangu na wa Tanzania
katika mambo mbali mbali hivyo
iongeze ukali hotuba hii” akasema
Dr Vivian
“Dada labda uniweke wazi
unataka nilenge maeneo yapi
hasa.Ulinipa mambo ya kuzingatia
wakati wa kuiandaa hotuba hii na
nimeyafuata ,nimelenga mambo ya
uchumi,misaada ya masharti na unyonyaji wa rasilimali
zetu,mabadiliko ya tabia nchi na
mengineyo” akasema Theresa.Dr
Vivian akaitazama tena hotuba ile
na kusema
“Hotuba hii si mbaya,imekaa
vizuri lakini kuna sehemu ambazo
zinahitaji lugha kali zaidi
kuonyesha msisitizo.Hotuba hii
imepoa sana.Lakini usijali endelea
nayo na utakapomaliza niletee
nitaisahihisha
mwenyewe,samahani kama
nimekukwaza” akasema Dr Vivian
“Usijali dada” akasema
Theresa na kuchukua kompyuta
yake ili atoke Vivian akamuomba
asubiri.Kaa nami kidogo
Theresa,bado tunayo safari
ndefu.Nyakati kama hizi ndipo
tunaweza kukaa na kuongea
mambo yanayotuhusu sisi.Tukifika
marekani kutakuwa na mikutano
mingi hivyo hatutaweza kupata
nafasi nzuri ya kuzungumza
mambo yetu” akasema Dr Vivian
“Ni kweli dada.Japokuwa tuko
pamoja muda mwingi lakini
hatupati nafasi ya kuzungumza
mambo yetu ya kifamilia” akasema
Theresa na kujimiminia juice
katika glasi
“Kabla sijaingia ndegeni
nilikuwa na mazungumzo na
George Mzabwa.Nilimuuliza
amefikia wapi kuhusiana na kazi niliyompa ya kuchunguza mauaji
ya familia yetu.Amekuwa
ananikimbia kimbia kila
ninapotaka kulizungumzia jambo
hili.Jibu alilonipa
halijaniridhisha.Amesema
kwamba mpaka sasa bado
hajafanikiwa kugundua lolote.Ni
miaka miwili imepita sasa toka
nimempa kazi hiyo na ameniudhi
sana.Nimemwambia nitakaporejea
aidha nikute taarifa kwamba watu
waliofanya kitendo kile kiovu
wamepatikana au nikute barua
yake ya kuachia ngazi mezani
kwangu ama sivyo nitamuondoa
na kumpeleka sehemu nyingine
kwani ameshindwa kazi.Sielewi
kuna nini katika jambo hili hadi lishindwe kupatiwa
majibu.Ninafikiria kutafuta mtu
mwingine wa kuongoza idara ya
usalama wa taifa kwa kasi
ninayoihitaji.George hawezi
kuendana na kasi yangu” akasema
Dr Vivian
“Hata mimi nashangaa na
kujiuliza kulikoni katika suala hili?
Inawezekajane mpaka leo hii
hakuna taarifa yoyote kuhusiana
na wauaji wa familia yetu?Jeshi la
polisi wamefanya
uchunguzi,usalama wa taifa pia
lakini mpaka leo hii hakuna
chombo chochote kilichotoa
majibu ni nani waliua familia yetu
na kwa nini.Vyombo hivi vyote
viwili wanazo rasilimali za kutosha kuwawezesha kufanikisha
uchunguzi wa jambo hili lakini
mpaka leo wameshindwa kubaini
watu waliofanya unyama ule.Hapa
kuna kitu kinatia shaka dada”
akasema Theresa
“Tuachane na hayo
nitayashughulikia nitakaporejea
kwani suala hili kwa sasa
linaonekana kama fumbo gumu
lisiloweza kufumbuka.Nitalivalia
njuga mimi mwenyewe na safari
hii lazima nitapata majibu,lazima
fumbo hili lifumbuke” akasema Dr
Vivian na kumuomba Theresa
amletee juice ya mchanganyiko wa
matunda kinywaji anachokipenda
sanaNathan kanipigia simu leo
asubuhi na kunitaarifu kwamba ile
kazi yake aliyokwenda kuifanya
Uswisi imemalizika na hivyo
atanifuata New York na baada ya
mkutano kumalizika tutarejea
wote Da es salaam kuendelea na
maandalizi ya ndoa yetu.Theresa
siwezi kueleza furaha niliyonayo
kwani imebaki miezi mwili tu na
mimi niingie katika ndoa na
mwanaume ninayempenda kwa
dhati.Hata hivyo kuna kitu nataka
kukisikia toka kwako.Watu
wanaongeaje huko mitaani
kuhusiana na ndoa yangu na
Nathan? Nilitaka jambo hili liwe la
kimya kimya lakini watu
wamefukunyua hadi wakagundua ninataka kufunga ndoa”Akauliza
Dr Vivian huku
akitabasamu.Theresa akanywa
funda la juice halafu akasema
“Japokuwa Nathan ulikuwa
naye katika kipindi chote cha
kampeni na kuzunguka naye nchi
nzima lakini bado watu
hawamfahamu vizuri ni
nani.Nimekuwa napitia baadhi ya
maoni ya watu mtandaoni na
nimeona watu wanahoji kwa nini
rais wao aolewe na mtu wa kutoka
nje ya nchi?Tanzania imejaa vijana
wa kila aina wasomi na wabobezi
wa mambo mbali
mbali,haujawaona hao wote hadi
moyo wako ufunguke kwa mtu wa
taifa lingine?Lakini haya yasikuogopeshe ni mawazo tu ya
watu yanayotokea katika mijadala
mbali mbali inayoendelea huko
mitandaoni” akasema Theresa .Dr
Vivian akatabasamu nba kuuliza
“Wewe je una maoni gani?
“Kuhusu nini dada Vivi?
“Kuhusu mimi na
Nathan.Nakufahamu wewe huna
tabia ya kuficha kitu bali husema
kweli toka moyoni.Sijawahi kupata
maoni yako kuhusiana na hili suala
langu na
Nathani.Unaliongeleaje?Nathani ni
mwanaume ambaye naweza
kusema kwamba ninampenda kwa
dhati ya moyo wangu lakini je
unadhani watu wangu
watampenda na kumkubali?Tafadhali kuwa
muwazi kwangu.You are my
sister” akasema Dr Vivian
“Dada ,mapenzi kama yalivyo
hayachagui rangi,umri hata
taifa.Moyo unaweza kufunguka
kwa mtu yeyote awe
mweusi,mweupe n.k.Wewe
umeufungua moyo wako kwa
Nathan na hakuna ubaya wowote
lakini….” Theresa akasita kidogo
akanywa maji ya matunda na
kuendelea
“Umeomba nikueleze ukweli
wangu na nitakueleza ukweli
wangu japo hautakuwa mzuri sana
lakini lazima niuseme kwa kuwa
umeomba.Hakuna mtu
atakayeweza kukuzuia usiolewe na Nathan mwanaume unayempenda
kwa dhati ya moyo wako lakini
ndoa hii ingekuwa na tija zaidi
kama Nathan angekuwa ni
mtanzania.Anaweza akabadili
uraia wake na kuwa mtanzania
lakini damu yake bado ni
Marekani.Kama akiwa mumeo
yeye ndiye atakayekuwa mshauri
wako mkuu kwa mambo mbali
mbali hivyo anapaswa awe ni mtu
anayeipenda Tanzania na
kuifahamu vyema,ayafahamu
matatizo ya waTanzania na
yamguse ili aweze kukushauri
vizuri namna ya kuzitatua
changamoto mbali mbali
unazokumbana nazo katika kazi
yako.Nathani yeye ni mmarekani na Tanzania ameifahamu kwa
sababu yako tu na sina hakika
kama anaweza kuwa mshauri
mzuri katika masuala yanayohusu
Tanzania.Ikitokea akashindwa
kukushauri au akakushauri vibaya
mzigo wote wa lawama utakuwa
juu yako.Lakini haya ni mawazo
yangu tu na usiyachukulie kama
ndiyo mtazamo wa
watanzania.Nathan ni kijana mzuri
na sioni kama ana tatizo lolote”
akasema Theresa
“Theresa ahsante sana.Ndiyo
maana huwa ninapenda kukuomba
ushauri.Una mtazamo wa
mbali.Unafaa sana kuwa mshauri
wa rais na nitalitazama hilo siku za
usoni.Umezungumza mambo ya msingi na ambayo sikuwa
nimeyafikiria kabla sijakubali
kuolewa na Nathan.Vipi kuhusu
wewe na yule mtu wako Damian?
Bado mnaendelea na ugomvi
wenu? Kwa nini masuala yenu
msiyatafutie ufumbuzi na
kuyamaliza ili msonge mbele kwa
amani?
“Dada Vivi kuna mambo
mengine hayafai
kuyalazimisha.Nimetafakari sana
na kugundua mimi ndiye
niliyekuwa nalazimisha penzi
wakati mwenzangu hana muda
nami.Kila wakati mimi ndiye
niliyekuwa nikipiga magoti
kuomba msamaha hata kama si
mimi niliyekosa.Lengo lilikuwa ni kunusuru penzi letu kwa kuwa
Damian nilimpenda zaidi ya
ninavyoweza kueleza.Lakini ulifika
wakati nikasema imetosha na
nikaamua kila mmoja aendelee na
maisha yake.Niliumia mwanzoni
but now I’m happy.Nina amani ya
moyo na ninasubiri yule ambaye
ameumbwa kwa ajili yangu
ajitokeze.Naamini yupo mahala
fulani na muda ukifika nitampata”
akasema Theresa
“Hongera kwa maamuzi
hayo.Mimi nilitamani sana
kukushauri hivyo toka awali lakini
sikutaka kuingilia masuala
yako.Unapoona uko katika
mahusiano halafu wewe ndiye
mwenye kuumia kila siku na mwenzako hajali basi chukua
hatua haraka,huo uhusiano
hautakufikisha mahala
kokote.Natumai tayari umepata
somo la kutosha na utakuwa
makini safari hii kutafuta
mwanaume yule ambaye atakufaa
katika maisha yako.Ukikosea
kuchagua utaumia sana.Mapenzi
yanaumiza mno.Kuna nyakati hata
mimi ninawaza kuhusu Nathan
kama hatutakuwa na migogoro
pindi tutakapofunga ndoa.Nataka
nielekeze akili yangu katika
kuwasadia watanzania
walionichagua na kuwatatulia kero
zao na nitakuwa na muda mdogo
sana wa kushughulikia masuala ya
mapenzi.Hiki hawezi kuwakikwazo kwa Nathan na kikaleta
mgogoro kati yetu?Laiti Mungu
angeweza kunionyesha maisha
nitakayoishi nikiwa na Nathan
ningeweza kufanya maamuzi lakini
Mungu ametuficha na hatuelewi
chochote kuhusu dakika ijayo”
akasema Dr Vivian
“Usiwe na wasi wasi
dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole
na hana matatizo.Lakini …”
Theresa akasita
“Lakini nini Theresa? Mbona
umesita? Sema unachotaka
kukisema” akasema Dr
Vivian.Theresa akafikiri kidogo na
kusema
“Nothing.Ngoja nikuache
upumzike,mimi naenda kuimalizia hotuba hii halafu na mimi
nipumzike” akasema Theresa na
kuchukua kompyuta yake akatoka
mle chumbani.
“Theresa alitaka kuniambia
nini halafu akasita? Akajiuliza Dr
Vivian baada ya Theresa kutoka
mle chumbani
“Theresa si mtu wa kuficha
jambo,au aliona halina maana
ndiyo maana akaamua kuachana
nalo.Hata hivyo kuna jambo
amelizungumza la maana sana
kwangu na sikuwa nimelitilia
maanani hapo kabla.Nikiolewa na
Nathan yeye ndiye atakayekuwa
mshauri wangu katika mambo
mengi lakini atanishauri kitu gani
kama haifahamu vyema Tanzania wala matatizo ya watanzania?
Akajiuliza
“Nimetoka mbali na Nathan na
ninamfahamu vyema.Hata kama
haifahamu vizuri Tanzania wala
matatizo yake lakini nina imani
atanishauri vizuri kwani ni kijana
mpole na mwenye busara ya hali
ya juu.Sina shaka hata kidogo na
upendo wake kwangu na hata
mimi ninampenda mno na ndiyo
maana hata aliponitamkia kwamba
anataka kunioa niliruka ruka kwa
furaha.Mengi yatasemwa lakini
sitakiwi kuyasikilza.Natakiwa
kuziba masikio na kuyapuuza
kwani huyu ndiye chaguo
langu.Nathan ameingia katika kila
mshipa wa mwili wangu” akawaza na kuinuka kitandani akachukua
kompyuta yake akafungua mahala
anakohifadhi picha na kuzitazama
picha za gauni lake zuri atakalovaa
siku ya harusi yake,akatabasamu
“Sipati picha namna
nitakavyopendeza ndani ya gauni
hili lililobuniwa na mbunifu
chipukizi wa mavazi wa
kitanzania.Naamini
nitakapoonekana nimelivaa gauni
hili jina lake litapaa ulimwenguni
kwani wengi watataka kufahamu
nani alibuni vazi zuri kama hili.”
Akatabasamu na kuanza kutazama
picha nyingine za wabunifu mbali
mbali wa mavazi ya harusi
Alipotoka chumbani kwa
rais,Theresa akaenda katika moja wapo ya ofisi zilizomo ndani ya
ndege hii kubwa akachomeka
spika za masikioni katika
kompyuta yake akaanza kusikiliza
muziki.Uso wake ulionyesha
mabadiliko
“Mambo tuliyozungumza na
dada Vivi yameniharibia kabisa
siku yangu.Kwanza ni kuhusu yule
mchumba wake Nathan.Moyo
wangu haumkubali kabisa na hata
mwenyewe analifahamu hilo na
sijui kwa nini simpendi.Kila
nimuonapo karibu na dada amani
hutoweka kabisa.Najua
wanapendana lakini moyoni
mwangu hana kibali.Si kwamba
ninamchukia ila ninaona hafai
kuwa na Vivian.Nilitaka nimueleze hivyo dada lakini nikasita kwani
asingefurahia maneno hayo.Hata
hivyo siwezi kuingilia mapenzi
yao.Kama wanapendana acha
waoane lakini ningefurahi sana
kama dada yangu angeolewa na
kijana mtanzania” akawaza
Theresa na kufumbua macho
baada ya mlango kufunguliwa na
mtu kuingia mle ofisini.Alikuwa ni
waziri wa mambo ya nje
“Theresa nimekufuata
wewe,kuna kitu nataka
unisaidie.Naomba uipitie hii
hotuba yangu na uirekebishe kama
kuna mapungufu” akasema waziri
huyo na kutoka .Theresa
akaendelea kusikiliza mziki huku
akiipitia hotuba ile ya yule waziri na mara kumbu kumbu fulani
ikamjia akaacha kazi aliyokuwa
anaifanya akajiegemeza kitini
“Ni miaka zaidi ya kumi sasa
imepita lakini bado picha ya
yaliyomkuta baba haijafutika
kichwani na inanitesa kila
uchao.Nilikuwepo na nilishuhudia
kila kilichotokea.Najiuliza kwa
nini mimi?Kwa nini Mungu
akanichagua mimi niyashuhudie
yale yote? Naamini Mungu ana
sababu zake na ndiyo maana
katika watu wote ambao
walimzunguka baba alinichagua
mimi na kunibebesha mzigo huu
mzito.Kila siku ninapolikumbuka
jambo hili mwili wote hupata
baridi.Bado ile milio ya risasi zilizochukua uhai wa baba,mama
na kaka Kelvin ninaisikia
masikioni kila nilalapo.Nimebaki
natembea na siri hii nzito ambayo
hakuna anayeifahamu hata dada
Vivian hafahamu chochote.Ni mimi
pekee ninayefahamu sababu ya
baba ,mama na kaka Kelvin
kuuawa.Ni kwa sababu ya
Football” Machozi yakamtoka
“Nimekuwa najilazimisha
kutaka kulisahau jambo hili lakini
nimeshindwa.Ninaogopa kuliweka
wazi suala hili kwa ajili ya usalama
wangu na dada.Ninaogopa hata
kumueleza dada Vivian kwani
yanaweza kumkuta kama
yaliyomkuta baba .Waliomuua
baba walikuwa wanaitafuta hiyo football ni vipi endapo mpaka sasa
wakawa bado wanaitafuta?
Nitayaweka hatarini sana maisha
ya dada nikimueleza kuhusiana na
hili suala.Ngoja niendelee kulibeba
na itakuwa ni siri yangu pekee na
Mungu wangu.Nimeibeba na
kutembea na siri hii kwa zaidi ya
miaka kumi na nitaendelea
kutembea nayo.Yawezekana wale
jamaa bado wanaendelea
kutuchunguza.Sina hakika kama
watakuwa wamekata
tamaa.Lazima watakuwa
wanachunguza kwa siri ili kujua
football iko wapi.Lakini hii football
ni kitu gani?Ina siri gani ndani
yake?Baba hakuwahi kunieleza
chochote kuhusiana nayo.Ninavyofahamu mimi mkoba
ule uliopewa jina la football asili
yake ni nchini Marekani ambako
kila asafiripo rais wa Marekani
huwa anasafiri nao na ndani yake
kuna mambo ya siri ya kiusalama
kuhusiana na mambo ya
nyuklia.Hapa Tanzania rais Anorld
alianzisha mtindo wa kutembea na
begi kila anakoenda na akalipa
jina la football na baba ndiye
aliyekuwa mbebaji wake mkuu,je
kulikuwa na siri gani humo ndani
yake? Akajiuliza Theresa na
kukumbuka zikamrejesha mbali
Pamoja mkuu.
 
Mkuu Kulubule wewe ni moto tena wa kuotea mbali, hutaki kutuacha tupumue ni bandika bandua...Ahsante xana, tupo pamoja kwenye huu uwanja wa Football, ni kukaba mwanzo mwenga....
 
THE FOOTBALL

Sehemu 2

JUNE 2007 – DAR ES SALAAM
Saa tatu za usiku familia ya
Kanali Sebastian Matope wamekaa
sebuleni wakitazama filamu baada
ya kumaliza kupata mlo wa
usiku.Theresa akainuka akaenda
chumbani kwake na kurejea na
bahasha ya khaki akampatia baba
yake
“Nini hii,mchango? Akauliza
kanali Sebastian.Theresa hakujibu
kitu akatabasamu.Baba yake
akaifungua na kukuta ni ripoti ya
matokeo ya mtihani.Akaipitia na
kutabasamu
“Theresa hujawahi
kuniangusha hata mara
moja.Safari hii tena umeshikanamba mbili.Hongera
sana.Unastahili zawadi kubwa kwa
bidii kubwa unayoionyesha
shuleni” akasema Kanali Sebastian
na kumpa mkewe ripoti ile naye
aipitie
“Zawadi gani utanipatia safari
hii baba? Theresa akauliza.Kanali
Matope akafikiri kidogo na
kusema
“Kwa kuwa umenifurahisha
sana kwa matokeo haya mazuri
nitasafiri nawe kwenda nje ya
nchi”
“Kweli baba? Akauliza
Theresa kwa furaha
“Ndiyo.Kesho rais ana safari
ya kwenda Misri.Kuna kikao kifupi
cha marais wa nchi zinazopitiwa na mto Nile na kwa kuwa mto Nile
chanzo chake ni Tanzania basi rais
wetu naye atahudhuria kikao
hicho.Wakati kikao kinaendelea
wewe utapata nafasi ya kuzunguka
katika jiji la Cairo na kama muda
utaruhusu basi waweza pata nafasi
kufika katika mapiramidi na
utajifunza mambo mengi kwa
kuona kwa macho kuliko kusoma
tu vitabuni”
“Ahsante sana baba.Siwezi
kuelezea furaha yangu.Siamini
kama na mimi nitasafiri na rais
hapo kesho”
“Nitakutambulisha kwa rais
na kumueleza juhudi zako katika
masomo.Naamini hata yeye
mwenyewe atafurahi kwani anapenda sana vijana wanaojituma
katika kazi na masomo” Akasema
Kanali Matope na Theresa akaruka
ruka kwa furaha kubwa.
“Nitafutahi sana baba kama
nitapata nafasi ya kwenda
kujionea mapiramidi kwani
tumekuwa tunayasoma katika
historia.Itakuwa ni somo zuri sana
kwangu kuyashuhudia ana kwa
ana na nitakuja vile vile
kuwasimulia wenzangu maajabu
hayo makubwa ya
dunia.Tutakwenda sote huko
katika mapiramidi? Akauliza
Theresa
“Hautaongozana na mimi
Theresa ila nitakutafutia mtu
kutoka ubalozi wetu ambaye atakutembeza katika sehemu
mbali mbali za jiji la Cairo na kama
nafasi itapatikana basi
atakufikisha hadi katika
mapiramidi”
“Jamani baba kwa nini
usitafute nafasi tukaongozana
wote?Nitafurahi sana nikiwa nawe
mtu niliyemzoea ili iwe rahisi hata
kuuliza maswali”
“Hata mimi ningefurahi sana
kama ningepata nafasi ya
kukutembeza katika jiji la Cairo
lakini kazi yangu
hainiruhusu.Natakiwa kuwa
karibu na rais muda
wote.Usiogope mtu
nitakayekutafutia atakuwa
anaongea kiswahili na utamuuliza kitu chochote utakacho” akasema
Kanali Matope
“Kwani baba lile begi ambalo
huwa unalibeba kila unaposafiri
na rais lina nini ndani
yake?Hakuna mtu mwingine
anayeweza kukusaidia
kulibeba?Sijawahi kuona mtu
mwingine analibeba zaidi yako”
akasema Theresa na kumfanya
baba yake atabasamu
“Lile si begi kama mabegi
mengine.Lile ni begi maalum
linaitwa football”
“Football?? Theresa
akashangaa na kuangua kicheko
“Ndiyo linaitwa Football.Najua
umeshangaa kusikia jina hili
linalomaanisha mpira wa miguu lakini haimaanishi kama begi hili
linabeba mpira wa miguu.Mle kuna
mambo ya siri na hubebwa na mtu
ambaye amekula kiapo cha
kuhakikisha kwa vyovyote vile
hata kutokee nini football
linakuwa salama.Kulibeba begi lile
lazima upitie mafunzo maalum ya
komando na kufuzu kwa kiwango
cha juu.Lengo ni kuhakikisha
anayelibeba begi lile anakuwa ni
mtu mwenye mbinu na uwezo
mkubwa wa kujilinda na kuilinda
football.Asili ya jina hili ni
Marekani ambako rais wa
Marekani ana begi lake ambao
husafiri nalo kila aendako na
mataifa mengine yakaiga mtindo
huo japokuwa kila taifa lina jambo lake linalowekwa ndani yake
lakini mara nyingi huwa ni siri za
nchi zinazohusiana masuala ya
usalama.Hata hivyo muda wangu
wa kustaafu umekaribia na kuna
mtu mwingine anayeandaliwa
kushika nafasi yangu.Nadhani
nimejibu swali lao” akasema
kanali Matope
“Ndiyo nimekuelewa
baba.Kumbe jukumu ulilolibeba ni
kubwa na la hatari sana”
“Ni jukumu kubwa na la hatari
lakini ulinzi wake ni wa kutosha na
wa uhakika.Pamoja na uwezo
wangu mkubwa wa kujilinda na
kuilinda football lakini kuna
walinzi wanne ambao kazi yao ni kunilinda mimi na hilo begi”
akasema Kanali Matope
“Nini kitatokea endapo begi
hilo litapotea?akauliza Theresa na
kanali Sebastian akacheka
“Football haiwezi
kupotea.Tumekula kiapo cha
kuhakikisha tunailinda hadi tone
la mwisho la damu yetu kwa hiyo
unapolibeba begi kama lile basi
uhai wako unauweka rehani ili
kulilinda.Siku zote football ni
salama pengine kuliko hata rais”
akasema kanali Sebastian
“Baba ahsante ngoja niende
nikajiandae kwa hiyo safari ya
kesho” akasema Theresa
“Theresa kesho vaa mavazi ya
kawaida na usibebe mzigo mkubwa kwani ni safari ya siku
moja tu.Chukua vitu vichache
utakavyovihitaji kwa masaa
machache” akasema kanali
Sebastian.
**************
Mkutano wa wakuu wa nchi
zinazopitiwa na mto Nile
ulimalizika jijini Cairo Misri na saa
kumi na mbili za jioni rais wa
Tanzania akaagana na mwenyeji
wake ambaye ni rais wa Misri
akaondoka kurejea
Tanzania.Ilikuwa ni safari nzuri
sana kwa Theresa ambaye alipata
nafasi ya kutembelea sehemu mbali mbali za kihistoria
zinazopatikana jijini Cairo
Katika safari ya kurejea
Tanzania walikuwepo pia
waandishi nane wa habari
wanaotoka nchini Marekani
wakielekea nchini Tanzania lakini
kwa bahati mbaya walichelewa
ndege yao hivyo ikawalazimu
kuomba lifti katika ndege ya rais
ili wawahi ratiba yao ya kuandika
habari kuhusiana na mbuga za
wanyama zinazopatikana nchini
Tanzania.Rais alifurahishwa sana
na namna waandishi wale
walivyojitolea kutaka
kuifahamisha dunia juu ya vivutio
mbali mbali vya utalii
vinavyopatikana nchini Tanzania.Ndani ya ndege rais
alifanya mazungumzo na
waandishi wale na walijadiliana
mambo mbali mbali kuhusu
ukuzaji wa utalii nchini na namna
ya kutangaza vivutio vilivyopo
nchini Tanzania.Baada ya
maongezi ya takribani saa moja na
nusu waandishi wale wakamuacha
rais apumzike nao wakaenda
kuchukua nafasi zao.Ni safari ya
takribani masaa matano hivyo
hakukuwa na maongezi mengi mle
ndegeni na kila mmoja alikuwa
amejipumzisha baada ya uchovu
wa kutwa nzima.Hakuna
aliyetegemea kama kulikuwa na
hatari yoyote mbele yao Safari iliendelea hadi jijini
Nairobi ambako ndege ya rais
ililazimika kutua kwa dharura
baada ya marubani kubaini
kwamba ndege imepungukiwa
mafuta na walikuwa na wasi wasi
mafuta yaliyopo yasingetosha
kuwafikisha Dar es
salaam.Yaliibuka mabishano
makali kati ya walinzi wa rais na
marubani wakihoji kwa nini ndege
ya rais ipungukiwe mafuta?
Ilimlazimu rais kuingilia kati
mabishano yale na mafuta
yakawekwa kisha safari
ikaendelea
Muda mfupi baada ya kuingia
katika anga la Tanzania,ghafla
kukatokea jambo lililowastua walinzi wa rais.Sehemu ya jikoni
kulianza kufuka moshi.Iliwalazimu
walinzi wawili wa rais kwenda
haraka sana eneo la jikoni kwenda
kuangalia chanzo cha moto ule na
mara ikasikika milio ya risasi na
kuibuka kizaazaa kikubwa mle
ndegeni.Wale jamaa walioingia
ndegeni kama waandishi wa
habari wakainuka na kukimbilia
eneo la jikoni na baada ya muda
kila mmoja wao akawa na silaha
kali.Wote walionekana ni watu
wenye mafunzo makubwa sana ya
kupambana kwa kutumia
silaha.Walianza kushambuliana na
walinzi wa rais na kuua watu
hovyo mle ndegeni.Mara tu risasi
za kwanza ziliposikika na kuzua taharuki,Kanali Sebastian
alichukuliwa haraka sana pamoja
na football na kukimbizwa katika
chumba cha rais ambacho
kinaaminika ni salama
sana.Hakumuacha nyuma Theresa
“Nini kimetokea huko nje?
Rais akauliza kwa wasi wasi huku
jasho likimtiririka
“Tumevamiwa” akasema
mmoja wa walinzi wa rais huku
akimvisha rais fulana ya kuzuia
risasi
“Tumevamiwa na ani?
Akauliza rais kwa woga
“Mzee tunatakiwa tukuondoe
haraka sana humu ndegeni kwani
hawa jamaa…...” Hakumaliza
sentensi yake kwani ikaanzakusikika milio ya risasi karibu na
chumba cha rais.Watu wote mle
ndani ya chumba cha rais walivaa
fulana za kuwakinga na risasi
pamoja na miavuli mgongoni
tayari kabisa kwa kuondoka mle
ndegeni.
“Mheshimiwa rais
tuondoke,tayari hawa jamaa
wamekaribia.Tunakushusha chini
kwa mwavuli”
“Hapana.Kitu cha kwanza
tuhakikishe football iko
salama.Kabla ya kunitoa mimi
lazima kwanza tuhakikishe
Sebastian na football ametoka
humu ndegeni” akasema rais
“Mheshimiwa rais jukumu letu
kubwa ni kuhakikisha unakuwa salama.Wewe kwanza halafu
wengine watafuata” akasema
mmoja wa walinzi wake akiwa
amemshika mkono rais
“Hapana kwanza footb…….”
Kabla hajamaliza sentensi yake
ukatokea mlipuko wa baruti na
kuusambaratisha mlango wa
kuingilia mle chumbani mwa rais
na risasi zikaanza
kumiminwa.Walinzi wa rais nao
wakajibu mapigo kwa kumimina
risasi wakimkinga rais
asishambuliwe.
‘Seba run..!!! akapiga kelele
rais na kwa kasi ya aina yake
Sebastian akamshika mkono
Theresa akamvuta wakaingia
jikoni huku mlinzi wake mmoja akiwa nyuma yao.Sebastian
alifahamu vyema ndege hii ya rais
na mfumo wake wote wa
usalama.Pale jikoni kulikuwa na
mlango unaoingia chumba cha
stoo.Wakaingia na kulifunua zuria
katikati ya stoo kulikuwa na
mlango mdogo unaofunguliwa kwa
namba.Akabonyeza namba kadhaa
haraka haraka na mlango
ukafunguka.Kulikuwa na ngazi ya
kushuka chini.Akaingia na
kumshika mkono Theresa
wakaingia ndani na kushuka ngazi
kuelekea chini.Ghafla milio ya
risasi ikasikika mle stoo.
“The football !!!!..akapiga
kelele mmoja wa wale jamaa
aliyeingia stoo na kukuta mlango umefunguliwa na kuna ngazi za
kushuka chini.Wenzake watatu
wakaja na kuungana naye kisha
kwa haraka wakaanza kushuka
chini kuifuata ile ngazi
waliyotumia akina Sebastian
kushukia chini
Sebastian na mwanae Theresa
na mlinzi mmoja walifika katika
sehemu ya kufungulia mlango wa
dharura wa ndege ambao ni
maalum kwa ajili ya kumuokoa
rais.Wakiwa wanajadiliana ghafla
wakatokea wale jamaa na kuanza
kuwarushia risasi.Umahiri wa
Kanali Sebastian na mlinzi wake
katika silaha ulisaidia kiasi cha
kuwafanya wale jamaa wajifiche
na Sebastian akautumia mwanya huo kubonyeza sehemu ya
kufungulia mlango wa dharura
ukafunguka.Mara ghafla wale
jamaa wakaibuka wote watatu kwa
pamoja toka mahala walipokuwa
wamejificha na kuanza kumimina
risasi.Kanali Sebastian akamshika
mkono mwanae Theresa na
kuruka nje.Sebastian hakumuachia
Theresa katika upepo ule mkali na
giza nene,walishuka kwa kasi
kubwa na mara mwavuli aliokuwa
ameuvaa kanali Sebastian
mgongoni ukafunguka na
wakaanza kushuka chini taratibu.
Kumbukumbu ile ikamfanya
Theresa ahisi baridi ghafla na
woga mkubwa.Akatoka mle katika
ofisi akaenda kuzunguka zunguka ndegeni kuhakiki kwamba hakuna
mtu yeyote wa kumtilia shaka mle
ndani ya ndege.Kumbu kumbu ya
tukio lile lililotokea kwa miaka
kumi iliyopita ilimstua
mno.Alibadilishana mawazo na
walinzi wa rais halafu akaenda
kuketi kitini.Alihisi hali yake
kuanza kubadilika
“Miaka zaidi ya kumi imepita
sasa lakini bado naona kama tukio
lile limetokea jana.Bado ninakuwa
na woga mkubwa kila ninaposafiri
na rais.Mimi na baba ndiyo pekee
tulitoka salama katika ile ndege
kwani ilianguka karibu na wanja
wa ndege wa kimataifa wa
Kilimanjaro na wote waliokuwemo
ndani walifariki dunia.Kwa sasa ni mimi pekee niliyebaki hai ambaye
ninafahamu nini kilitokea usiku
ule.Ni tukio la kutisha sana ambalo
halitaweza kamwe kunitoka
kichwani mwangu.Siwezi
kulisahau giza lile nene kama vile
tuko jehanamu. Namshukuru sana
baba kwani alipambana kwa kila
alivyoweza hadi akafanikiwa
kuniokoa vinginevyo na mimi
ningekufa kwani hakuna yeyote
aliyekuwa ananijali zaidi yake”
akaendelea kuwaza
“Watu wale waliofanya lile
shambulio walikuwa na lengo la
kuipata football lakini baba kwa
umahiri alifanya kila awezalo na
kuhakikisha hawafanikiwi lengo
lao na football ikawa salama.Hii inaonyesha ni namna gani begi lile
lilivyokuwa na thamani kubwa
sana.Limebeba mambo mazito
.Hata rais mwenyewe alipotakiwa
awe wa kwanza kutoka mle
ndegeni alisema hawezi kutoka
yeye kabla football haijatoka
ndegeni.Wote waliipa football
uzito mkubwa sana.Kuna siri gani
ndani ya hiyo football?Liko wapi
lile begi?Nakumbuka tulipofika
chini tulitua katika msitu mmoja
uliokuwa karibu na makazi ya
watu.Sikumbuki ilikuwa saa ngapi
ila tulitembea hadi tulipoikuta
barabara kuu.Baba akaniambia
kwamba pale tulipo palikuwa ni
usa river.Tulilala pale na asubuhi
siku iliyofuata tulipanda basi hadi Dar es salaam.Baba alikuwa na lile
begi na baada ya hapo sikuwahi
kuliona tena.Sifahamu amelificha
wapi ila aliniachia mkufu huu
wenye msalaba wa dhahabu na
kunitaka niutunze na niuvae kwa
siku zote za maisha
yangu.Alinielekeza nimpatie
mkufu huu rais atakayekuwepo
madarakani baada ya miaka kumi
kupita toka ajali ile kutokea.Rais
aliyepo madarakani baada ya hiyo
miaka kumi kupita ni mwanae
Vivian.Alihisi kwamba mwanae
anaweza kuwa rais kwa kipindi
hiki? Hata hivyo nimeogopa
kumpatia dada Vivian huu mkufu
kwa kuhofia maisha yake.Naamini
mkufu huu una jambo kubwa na ndiyo maana akaniomba niutunze
na nije kumpa rais wa
sasa.Nimekuwa najiuliza maswali
mengi sana kuhusiana na mkufu
huu,je una muunganiko wowote na
football?Begi lile la football baba
alilificha wapi? Au alilirejesha
ikulu?Kila mara maswali haya
yamekuwa yanakifanya kichwa
changu kigonge kwani sijawahi
pata majibu yake.Baba ameniachia
mzigo mzito sana na sijui nitautua
vipi au nani nimtwishe? Akawaza
Theresa na kumbu kumbu
nyingine ikamjia NOVEMBER 2007 – DAR ES
SALAAM
Imekwisha pita miezi minne
toka ilipotokea ajali ya ndege ya
rais na kuua watu wote
waliokuwemo ndani yake
isipokuwa kanali Sebastian na
Theresa pekee.Kanali Sebastian
alipata wakati mgumu sana kwani
vyombo vya uchunguzi ambavyo
vilimuhoji sana kuhusiana na
kilichotoka katika ajali ile na
namna alivyoweza
kusalimika.Pamoja na kuhojiwa
sana lakini Kanali Sebastian
hakuwahi kuweka wazi kwamba
alinusurika yeye na Theresa.Mara
zote alisimama katika msimamo
wake mmoja kwamba aliyenusurika katika ajali ile
alikuwa ni yeye peke yake na
hakutaka kumuhusisha kabisa na
Theresa.Kama mtu pekee
aliyekuwa amelibeba begi la siri
maarfu kama football alihojiwa
mahala liliko begi hilo na
hakuwahi kueleza
ukweli.Alichokieleza na ambacho
hakikuwa kweli ni kwamba walinzi
wawili wa rais waliasi na kutaka
kumuua rais na kikatokea kizaa
zaa ndegeni na alipotaka kutoroka
na mkoba ule wa football ulipigwa
risasi na ili kuokoa maisha yake
akaamua kuachia na kuruka nje .
“Mpaka leo sielewi ni kwa nini
baba hakutaka kuweka wazi
kuhusiana na kile kilichotokea ndegeni na kuhusu ile
football.Hajawahi mweleza mtu
yeyote mahala alikoificha.Kwa nini
aliamua kuificha badala ya
kuirejesha serikalini wakati akijua
kabisa kwamba kuna siri za
serikali mle ndani? Kwa nini afiche
siri za nchi? akajiuliza Theresa
“Ninajiuliza maswali haya
lakini siwezi kuyapatia majibu.Mtu
pekee ambaye angeweza kuwa na
majibu sahihi ni baba lakini
hayupo.Hapo ndipo huwa
ninachoka na kuamua kuliacha
suala hili kama lilivyo na
kuendelea kuibeba siri hii hadi
siku nitakapoingia kaburini japo
naamini baba alikuwa na makusudi yake kufanya vile
alivyofanya” akawaza
“Lakini ni kweli niko tayari
kuendelea kuibeba siri hii hadi
kaburini? Nimekuwa najiuliza
swali hili mara kadhaa lakini kila
ninapomuangalia dada najikuta
sina namna ya kufanya zaidi ya
kuendelea kuibeba japo baba
alinitaka nimpatie rais wa sasa
mkufu huu.Sina hakika kama alijua
mwanae ndiye atakayekuwa rais
wa Tanzania baada ya kipindi cha
miaka kumi.Hapana sintamueleza
Vivian kwani kufanya hivyo ni
kumuweka hatarini.Baba alitolewa
uhai wake kwa sababu ya jambo
hili na hata mimi nilinusurika
kuuawa kwa sababu kwanza nilikuwa mwanafunzi na pili baba
hakuwahi kuweka wazi kwamba
nilikuwemo katika ndege ile ya
rais.Kama ningejulikana lazima
ningeuawa pia” akaendelea
kuwaza Theresa na machozi
yakamtoka akawahi kuyafuta ili
mtu yeyote asigundue kwamba
alikuwa katika mawazo mazito
“Masikini familia yangu
waliuawa kikatili mno na
nilishuhudia kila kitu.Mpaka leo
bado picha za mauaji yale zinanijia
usingizini.Bado namuona baba
akianguka na kufa huku
akimiminiwa risasi kama
mnyama”
Theresa akashindwa kuyazuia
machozi yasimtoke.Kumbu kumbu ya namna walivyouawa wazazi
wake ilipomjia.
April Hudson Mubara mjane
wa rais Anorld Mubara alirejea
nchini akitokea Marekani
alikoenda mapumzikoni baada ya
kifo cha mume wake.Moja kwa
moja alienda kuishi katika shamba
lao lililokuwepo katika kijiji cha
mchangawima Chalinze.Alitaka
apumzike sehemu yenye utulivu
mkubwa.Baada ya kufahamu
kwamba amerejea nchini Kanali
Sebastian alimpigia simu na
kumtaarifu kwamba atakwenda
kuonana naye kumpa pole kwani
toka yalipofanyika mazishi ya rais
Anorld hawakuwahi kuonana
tena.Bi April alikubali kuonana na Kanali Sebastian kwani alikuwa
mtu wa karibu sana na mumewe
na wakapanga siku ya
kuonana.Siku ilipofika Kanali
Sebastian akaichukua familia yake
yote ili kwenda kumpa pole Bi
April kwa kifo cha mume wake.
Wakiwa wameikamata
barabara inayoelekea katika
shamba la rais Anorld,mara kwa
mbele wakakuta kizuizi cha askari
na magari mawili ya askari
yameegeshwa pembeni.Ni eneo
lililokuwa kimya sana na
hakukuwa na watu eneo hili na
mahala polisi walipoweka kizuizi
chao kulikuwa na vichaka vichaka.
“Hawa askari wanafanya nini
huku? Mbona wameweka kizuizi kwani kuna magari yanakuja huku
zaidi ya machache yanayokwenda
katika shamba la rais Anorld?
Akauliza mke wa kanali
Sebastian.Alionyesha wasiwasi
“Barabara hii inakwenda
katika shamba la rais.Inawezekena
wanaimarisha ulinzi ili kuzuia
watu wasiotambulika kwenda
katika nyumba ya rais wakati huu
ambao bi April yupo huku kwa
mapumziko” akasema kanali
Sebastian
“Hata kama ni ulinzi kwa nini
wasilinde askari wachache?Mbona
hawa wako zaidi ya kumi?
Akauliza mke wa Sebastian na
askari mmoja akasimama kati kati
ya barabara akanyoosha mkono akamtaka kanali Sebastian
asimamishe gari.Taratibu
akapunguza mwendo na
kusimamisha gari pembeni ya
barabara kama
alivyotakiwa.Akafungua mlango na
kushuka ili ajitambulishe kwa
askari wale na wamruhusu apite
lakini alipopiga hatua kama tatu
kuwaendea,ghafla ikasikika milio
ya risasi.Kanali Sebastian
akaanguka chini.Ndani ya gari mke
wake, ,mwanae Kelvin na Theresa
walipatwa na mshangao mkubwa
sana kwa kitendo kile.Haraka
haraka Kelvin akashuka garini ili
kumkimbilia baba yake
aliyeanguka pale chini lakini
alipotaka kumuinamia baba yake naye akachezea mvua ya risasi na
kuanguka karibu na baba yake
“Theresa hawa si
polisi.Tafadhali fanya
nitakavyokuelekeza.Jifiche chini ya
kiti na usiinue kichwa hadi
nitakapokuelekeza.Ninataka
kulirudisha nyuma gari hili ili
tujaribu kujiokoa vinginevyo
watatuua” Akasema mke wa kanali
Matope na kukaa sehemu ya
dereva akaukamata usukani na
kuweka gia ya kurudi nyuma kisha
akakanyaga pedeli ya mafuta na
kwa kasi ya aina yake gari likaanza
kurudi nyuma.Askari kama
watano wakaanza kulikimbiza lile
gari huku wakirusha risasi lakini
kwa ujasiri mkubwa Getruda Matope mke wa kanali Sebastian
matope akafanikiwa kulirudisha
gari nyuma na kupata sehemu ya
kugeuza na kisha akaliondoa kwa
kazi kubwa.Theresa aliyekuwa
amejificha chini ya kiti cha nyuma
akainua kichwa baada ya kusikia
mama yake anakoroma.
“Mama” akaita Theresa na
kugundua kwamba mama yake
alikuwa anatokwa na damu
mdomoni.Alikuwa amepigwa risasi
tumboni.Ghafla akakanyaga breki
kwa nguvu na gari likaserereka
hadi katika shamba la
mpunga.Getruda alikuwa anavuta
pumzi kwa taabu sana na damu
ikimtoka mdomoni mama !! akaita Theresa huku
akilia
“Theresa…r..un..ruuuuun..!!
“Hapana mama.Siwezi
kukuacha hapa peke yako !!
akasema Theresa
“Run..Thr..ru…rr…runnnnn!!
akasema Getruda kwa taabu na
kuvuta pumzi ndefu akaangukia
usukani.Theresa akaliona vumbi
kubwa nyuma yao linakuja kwa
kasi akajua ni zile gari mbili za
askari akafungua mlango na
kushuka akaanza kukimbia
akikatisha katika shamba la
mpunga.Alihisi miguu yake haina
nguvu lakini akajitahidi kwa kadiri
alivyoweza hadi alipolipita shamba la mpunga na kuingia katika
shamba la michungwa.
Akaweka mikono masikioni
mwake na kuhisi kutetemeka
mwili
“Bado nasikia milio ie ya risasi
masikioni mwangu hadi leo
hii.Kwa mara ya pili nilinusurika
kuuawa.Bila ujasiri wa mama na
mimi hivi sasa ningekuwa mfu”
akawaza na kufuta machozi
“Nahisi baba alitabiri kifo
chake kwani wiki moja tu kabla ya
kifo chake ndipo aliponipa huu
mkufu wenye msalaba.Aliamini
hataweza kufika wakati huu na
ndiyo maana akanibebesha mimi
siri kubwa iliyo katika msalaba
huu na laiti kama ningejulikana basi ningekwisha
uawa.Nitaendelea kuubeba huu
msalaba hadi siku naingia
kaburini.Nitakapofungua tu
mdomo wangu na kuropoka
chochote ndio utakua mwisho
wangu,sintabaki salama”
akaendelea kuwaza Theresa na
kuinuka akaelekea bafuni akalia
machozi mengi sana halafu
akanawa uso na kujipaka poda
upya usoni ili asitambulike kama
alikuwa analia.Akavaa miwani
myeusi kuficha macho yake na
kurejea kukaa akaendelea na kazi
zake huku dege likiendelea
kuchana anga kuelekea New york
Marekani.
 
Mchakamchaka umeanza potii kulubule kishapuliza bigula tuamke tukimbie nae.Imeanza na moto ngoja tukimbize kwanza
 
Walah naharibu kaz huku, tangu i died to save .... Mpaka now kweny football ofcn wanadai nimekuwa mkimya na cm yangu tu.... Salute mkuu
 
Back
Top Bottom