the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,112
- Thread starter
- #561
Usiwaze mkuufinally nimewafikia""" mkuu ukiadd ingine usisahau kunitag legendary
Sent from my SM-G532F using Tapatalk
the Legend☆
Usiwaze mkuufinally nimewafikia""" mkuu ukiadd ingine usisahau kunitag legendary
Sent from my SM-G532F using Tapatalk
Asubuhi Sana tayari ishapita mkuu!!Asubuhi sana itaendelea dear, usiwaze
the Legend☆
Saasa ndio kusema.?RIWAYA : SALA YA SARAH
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA SITINI.
ENDELEA..................
Sajenti Minja bado alikuwa anachanganywa na matukio ya kutisha yanayotokea mfululizo, baada ya kutoka hospitali kufuatilia uchunguzi wa kifo cha Harry, Sajenti Minja alipokea simu nyingine iliyomtaka afike hospitali binafsi ambapo kulikuwa na tukio la daktari kupigwa risasi.
Sajenti aliendesha gari lake mpaka eneo la tukio na kutelemka, akaelekea moja kwa moja mpaka ndani ya jengo la hospitali na kukaribishwa na wafanyakazi, akawasalimia,
"nani alikuwepo kipindi tukio linatokea?" Sajenti Minja aliuliza,
"hakuna mtu anayejua ni muda gani tukio limetokea, ila kuna wadada wapo hapa walimuona mtu wa mwisho kuingia kwenye chumba cha Dokta" Daktari mmoja alimjibu Sajenti Minja,
"wapo wapi hao wadada?" Sajenti Minja akauliza,
"ni hao hapo waliokaa mapokezi" Daktari alijibu na kumfanya Sajenti Minja awasogelee, kisha akawasalimia wale wadada wawili warembo, anita na lydia.
"nasikia nyie ndio mmemuona mtu wa mwisho kuingia kwenye hicho chumba?" Sajenti Minja aliuliza,
"ndio, sisi tupo hapa muda wote, kwa hiyo mtu yoyote anayeingia kwenye chumba hicho cha daktari tunamuona" Lydia alijibu,
"huyo mtu yupoje?" Sajenti Minja aliuliza,
"sura yake hatujaikariri vizuri, ila ni mwanaume mweupe, amenyoa upara na ana michoro mwilini" Lydia alijibu huku Anita akitikisa kichwa kuashiria kuwa maneno ya mwenzake yapo sawa. Kwa maelezo hayo tu, kichwa cha Sajenti Minja kikafananisha huyo mtu aliyeelezewa hapo na akayakumbuka maneno ya mlinzi wa Harry kuhusu mtu kama huyo kuonekana nyumbani kwa Harry kabla ya kifo cha familia ya Harry.
"Trigger" Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameangalia chini na kufanya wale mabinti wasielewe kitu chochote.
"mzee hii hospitali haina camera za kunakiri matukio?" Sajenti Minja alimuuliza daktari,
"kwa bahati mbaya hatuna afande" Daktari alijibu,
"Daktari aliyekutwa na hilo tukio amefanyiwa uchunguzi?" Sajenti Minja aliuliza,
"yupo, ametolewa chumba cha upasuaji nusu saa tu iliyopita, hali yake sio mbaya sana, anaweza kuongea" Daktari alitoa jibu lililofanya Sajenti Minja ashtuke,
"kumbe hajafa?" Sajenti Minja aliuliza kwa mshangao,
"yupo hai, zile risasi zilimpiga mkononi na kifuani upande wa kulia" Daktari alijibu,
"naweza kuongea nae?" Sajenti Minja aliuliza,
"inawezekana tu, twende ukaongee nae" Daktari alijibu huku akianza kutembea na kisha Sajenti Minja akamfuata.
Walielekea mpaka kwenye wodi moja na kuingia, akamkuta yule Dokta aliyepigwa risasi akiwa amelala, ila mwili tu, macho yalikuwa wazi,
"askari huyu, amekuja kukujulia hali" Daktari aliyeongozana na Sajenti Minja aliongea kumfahamisha mwenzake,
"karibu bwana" Dokta aliyepigwa risasi aliongea huku akilazimisha tabasamu, kisha wakasalimiana na Sajenti Minja,
"unaweza kunieleza mlolongo ulivyokuwa mpaka ukawa kwenye hali hiyo?" Sajenti Minja alimuuliza yule Dokta aliyepigwa risasi,
"kuna bwana alikuja, akawa anataka majibu ya vipimo ambavyo sio vyake, nikamkatalia, akatoka nje yule bwana, ila kwa utaalam wangu wa saikolojia, nikamsoma yule bwana na kugundua kuwa ni lazima arudi tena baadae, tena alionekana atarudi kwa shari kwa sababu hata muonekano wake ni wa kihuni, amejichora chora michoro mingi mwilini. Basi baada ya yule kijana kuondoka, nilichofanya ni kuchukua karatasi nyingine na kujaza vitu vya uongo, kisha juu nikaandika jina la mtu ambaye anadai amemtuma, uzuri ni kwamba huyo kijana ambaye alikuja kuchukua vipimo nilikuwa nimemkariri kwa kutokana na aina ya vipimo alivyochukua. Basi wakati nikiwa nimemaliza kuweka majibu ya uongo, nikachukua karatasi na kuiweka kwenye bahasha, kisha nikaandika jina la muhusika juu ya bahasha, ndipo mlango ulipofunguliwa na kisha huyo kijana akaingia, akanitolea bastola na kunitaka nimpe majibu, nikampa yale ya uongo ili niokoe uhai wangu" Dokta aliyepigwa risasi aliongea,
"na kwanini umpe ya uongo?" Sajenti Minja aliuliza,
"huwezi jua yale majibu alikuwa anayataka kwa sababu ipi, na pia majibu ya vipimo ni siri inayobaki kati ya muhusika na dokta, kwa hiyo sikuona sababu ya kumpatia majibu ya ukweli" Dokta alijibu,
"tokea tukio limetokea, muhusika mwenye majibu hayo amekuja?" Sajenti Minja aliuliza,
"nimesikia amekuja na kuuliza, alivyoambiwa hali iliyotokea, ameondoka amesema atakuja baadae au kesho" Daktari ambaye aliongozana na Sajenti Minja alijibu,
"ni vipimo ambavyo vinahusu nini?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia yule Dokta aliyejeruhiwa,
"DNA TEST, alileta damu na pia yeye akatoa damu kwa ajili ya kuangalia kama wana uhusiano wa kindugu" Dokta aliyejeruhiwa alijibu,
"majina ya huyo mtu unayakumbuka?" Sajenti Minja aliuliza,
"ni Vin Dennis nafikiri, na alikuwa anataka kulinganisha damu yake na Sarah Isack" Dokta aliyejeruhiwa alijibu na kufanya moyo wa Sajenti Minja upate mshtuko,
"sawa, basi endapo huyo mtu mwenye majibu atakuja tena, naombeni mchukue namba yake, nikija tena mtanipatia" Sajenti Minja aliongea huku akiinuka,
"sawa, sijui tukutambue kwa jina gani afisa?" Daktari aliyeongozana na Sajenti Minja aliuliza,.
"Joel Minja" Sajenti Minja alijibu huku akiondoka na yule Daktari mwingine alimsindikiza.
**************
Sarah siku ya leo hakuwa na ratiba maalum, alichoamua ni kuchukua simu yake kisha akaitafuta namba ya simu ya Vin kupitia mtandaoni, kisha akajaribu kupiga ile namba, ikawa inaita,
"habari" Sarah aliongea baada ya upande wa pili kupokea simu,
"nzuri" Vin alijibu kifupi,
"upo wapi muda huu?" Sarah aliuliza,
"naongea na nani?" Vin aliuliza,
"Sarah naongea" Sarah alijibu,
"nipo hotelini, Vin hotel" Vin alijibu,
"ninaweza kukuona?" Sarah aliuliza,
"njoo Vin hotel, ila hakikisha hakuna mtu atakayekujua" Vin aliongea kwa msisitizo,
"sawa, ndani ya nusu saa nitakuwa nimefika" Sarah aliongea na kukata simu, kisha akaingia bafuni kuoga, baada ya hapo akachukua baibui refu na kuvaa, kichwa akakivika mtandio mkubwa na zaidi alijifunga huo mtandio kama mama mtu mzima,
"vipi shoga, leo unaenda kuonana na sheikh nini? Maana sio kwa mtandio huo" Dokta Pendo alimuuliza Sarah,
"naelekea Vin hotel, kuna mtu naenda kumuona mara moja" Sarah alijibu huku akitabasamu,
"kwa wema au vurugu zako tu?" Dokta Pendo aliuliza,
"kwa wema shoga, huoni hata mavazi nimevaa ya kistaharabu?" Sarah alijibu kwa mtindo wa kuuliza,
"sawa shoga" Dokta Pendo aliongea,
"huyu mzee yupo wapi?" Sarah alimuulizia babu yake,
"alikuwa ametandika mkeka kule nyuma ya nyumba, nadhani alikuwa anataka Kulala" Dokta Pendo alijibu,
"poa basi, akiniulizia mwambie nimeenda kununua mahitaji ya nyumbani, usimwambie kuwa nimeenda Vin hotel" Sarah Alimwambia Dokta Pendo,
"usijali shoga, usisahau kuniletea castle za kopo" Dokta Pendo aliongea huku akitabasamu,
"tokea umepona umekuwa mnywaji kweli, nitakuletea shoga, na huyo mlevi mwenzio nitamletea na za kwake pia" Sarah aliongea huku akicheka,
"haya bwana" Dokta Pendo aliongea huku akifurahi na kipindi hicho Sarah alikuwa akielekea nje, akaingia ndani ya gari lake na kuondoka na kumuacha Dokta Pendo akifunga geti kubwa la nyumba.
Sarah aliendesha gari kwa mwendo wa haraka kidogo ili asitoke nje ya muda ambao amemuahidi Vin, na alikuwa anakwenda kwa Vin kwa lengo la kutaka kujua kuhusu kama Vin alifuatilia vipimo vya damu au alimpuuza?
Sarah alifika Vin hotel na kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha Vin, akagonga mlango, baada ya sekunde chache mlango ulifunguliwa na Vin mwenyewe, akamkaribisha Sarah, Sarah akaingia na kukaa kwenye kochi,
"mbona ulivyofika hukunipigia simu?" Vin alimuuliza Sarah,
"sikuwa na sababu ya kufanya hivyo wakati chumba nakijua vizuri" Sarah alijibu huku akitabasamu,
"umejuaje nakaa katika chumba hiki?" Vin aliuliza,
"muda tu najua, na kama ningeamua kukudhuru, ningekudhuru mapema tu" Sarah aliongea kwa kujiamini,
"isingekuwa rahisi kunidhuru" Vin nae alijibu kwa kujiamini,
"angalia pale" Sarah alimuonesha Vin pembeni ya dirisha, kulikuwa na kitu kama cha kuwekea ua,
"si ni urembo wa kuwekea ua?" Vin aliuliza,
"kaangalie kwa karibu zaidi" Sarah aliongea na kumfanya Vin ainuke aende kuangalia, haukuwa ni urembo wa kuwekea maua, aligundua hilo bomu, akashtuka,
"rudi ukae dogo, sina nia mbaya" Sarah aliongea na kufanya Vin ageuke na kumtazama,
"sasa kama huna nia mbaya si ulitoe?" Vin aliuliza huku akijiuliza hilo bomu liliwekwa lini,
"njoo tuongee, nitalitoa tu" Sarah aliongea huku akicheka na kumfanya Vin aende kukaa huku akiwa hajiamini kabisa,
"nambie umefikia wapi? Ulienda kupima damu?" Sarah alimuuliza Vin,
"yeah, nilienda kupima, ila majibu yameonesha hatuna undugu" Vin aliongea huku akipekua chini ya meza na kuitoa ile bahasha yenye majibu ya vipimo, Sarah akaichukua na kuifungua kisha akasoma kwa Muda,
"umepima hospitali moja tu?" Sarah aliuliza huku sura yake ikiwa haina nuru aliyokuja nayo,
"kama majibu yameonesha hivyo, hata uende hospitali kumi bado itakuwa hivyo hivyo" Vin aliongea huku akitabasamu,
"umeyaamini?" Sarah aliuliza,
"ningependa kuyachukua mimi ningeyaamini, ila alienda Trigger, na ubaya zaidi aliyachukua kwa nguvu, amemuua mpaka daktari" Vin aliongea,
"sasa bado hujapata jibu ni kwanini afanye hivyo, huoni kuna kitu wanakuficha?" Sarah aliuliza,
"ni kweli, na kuna maelezo haya nilitumia mtu anisaidie kuyapata" Vin aliongea huku akiwasha lap top yake na kumsikilizisha Sarah maongezi yaliyokuwa yanafanyika baina ya Trigger na Strategic.
Sarah akasikiliza tangu mwanzo mpaka mwisho wa yale maongezi, muda wote machozi yalikuwa yakimtoka tu kutokana na maneno ya Trigger,
"baada ya kusikiliza hayo maneno umeamua kufanya nini?" Sarah alimuuliza Vin huku akifuta machozi,
"nimeamua niruds marekani tu, maana bado mnanivuruga" Vin aliongea huku akirudia kuiweka sauti ya Trigger,
"kabla hujaondoka, unatakiwa uende ukamtafute daktari aliyetajwa na Trigger hapo, anaweza kukupa mwanga, uzuri na hospitali ambayo wanadai walitumia kukufutia kumbukumbu wameitaja" Sarah aliongea,
"na kama amekufa?" Vin aliuliza na kumfanya Sarah atabasamu,
"usipende kujikatisha tamaa, mtoto wa kiume inabidi upambane ili ujue ukweli wa maisha yako" Sarah aliongea huku akitabasamu na muda alisimama, alikuwa anataka kuondoka,
"sawa, nitafanya hivyo" Vin alijibu kivivu,
"kafanye leo, muda bado upo, mimi naondoka, nitakupiga simu usiku" Sarah aliongea huku akiwa bado amesimama, ila ghafla mlango ulifunguliwa na akaingia Trigger, mkononi akiwa na bastola, Vin akamuangalia Sarah na kisha akatabasamu.
Sarah akabaki ameduwaa huku akiishangaa hiyo hali na wakati huo asijue atapambana vipi angali hana silaha yoyote hata kisu tu au kiwembe..................?
********ITAENDELEA**********
the Legend☆

Hahahaa, Trigger ndo huyo kashaingia na bastola yake ambayo akiinua haishushi mpaka risasi itoke
Hahahaa, Trigger ndo huyo kashaingia na bastola yake ambayo akiinua haishushi mpaka risasi itoke
the Legend☆
Hahahaa, tuhamie kwa BQ naenda kuweka episode mpya
Hapo umenenaaa,Hahahaa, tuhamie kwa BQ naenda kuweka episode mpya
the Legend☆
Hahahaa, cha 3 kipo njiani kinakuja
Hahhaaha tater bwanaKingine kipi bibie..!?
Hivi ni mm sielewi kuna episode imepitwa au mm ndio nimeiruka hiyo episodeRIWAYA : SALA YA SARAH
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA HAMSINI NA TISA.
ENDELEA..................
Trigger na Taita wakapatwa na mshtuko, ila Vin hakuonekana kujali,
"kulikuwa na sababu gani ya kumuua Dokta na kuchukua majibu haya kwa nguvu?" Vin aliuliza huku akitoa macho kwenye ile karatasi na kumuangalia Trigger,
"Mimi ndiye niliyemtuma" Taita alijibu,
"kwanini umtume? Unadhani ni sahihi wewe kuingilia mambo yangu?" Vin aliuliza kwa hasira,
"nilifanya hivyo baada ya kusikia Sarah anataka kwenda kufanya shambulio hospitali, ilinibidi nimtume Trigger ili upate majibu yako yakiwa salama" Taita alijibu,
"ni upuuzi unaongea, ila endeleeni kufanya vitu kama hamna akili timamu" Vin aliongea kwa hasira,
"leo umeamua kunikosea hadabu kwa ajili ya majibu ya hospitali?" Taita aliuliza kwa ukali,
"nyie ndio mmenikosea adabu" Vin alijibu kwa hasira,
"jamani msigombane kwa vitu visivyokuwa na maana" Trigger aliongea,
"na wewe ni mnafki sana, kama mwanamke" Vin aliongea kwa hasira huku akimtazama Trigger,
"kwanini boss?" Trigger aliuliza,
"sijui" Vin alijibu huku akiinuka na ile karatasi yake ya majibu na kuondoka nayo na kuwaacha Taita na Trigger wakiangaliana.
"hili ni tatizo" Trigger aliongea kwa sauti ndogo,
"mpuuze, achana nae" Taita aliongea,
"kwa hali ilivyo, hatokuwa sawa kumpuuza" Trigger aliongea,
"kwa hiyo unataka kufanyaje?" Taita aliuliza huku akimtazama Trigger,
"inabidi tumwambie Strategic amfuatilie Vin kwa kila hatua anayoifanya, isije baadae akaujua ukweli, naona muda huu anatafuta sana ukweli" Trigger aliongea,
"hilo ni jambo jema, muagize Strategic afanye hivyo" Taita aliongea,
"sawa, baadae basi" Trigger aliongea,
"sawa" Taita alijibu kisha Trigger akaondoka zake.
***********************
Vin aliondoka pale huku akiwa na maswali mengi sana kichwani mwake, kifupi Vin alichanganyikiwa kutokana na majibu aliyoyaona kwenye cheti, majibu yalikataa kuwa Vin na Sarah sio ndugu, sasa kilichomchanganya ni kitendo cha Trigger kwenda kuiba yale majibu, alihisi huenda kuna namna imefanyika, alihisi huenda Trigger alimshurutisha daktari aandike majibu ya uongo, au Taita na Trigger hawakuwa na uhakika na aina ya majibu yatakayotoka.
Vin alifika Vin hotel na kuingia moja kwa moja kwenye chumba chake, alipofika ndani akatoa simu na kupiga namba anayoijua yeye,
"upo wapi?" Vin aliuliza,
"nipo maeneo ya Vin hotel" Strategic alijibu,
"njoo chumbani kwangu" Vin aliongea kisha akakata simu, baada ya dakika tano Strategic alikuwa chumbani kwa Vin,
"vipi?" Strategic aliuliza baada ya kuingia,
"bado nahitaji msaada wako" Vin aliongea huku akivua shati,
"ongea tu boss" Strategic aliongea,
"majibu ya vipimo nimeyapata, ila hayaoneshi kama sarah ni ndugu yangu" Vin aliongea,
"sasa tatizo lipo wapi?" Strategic aliuliza,
"tatizo hayo majibu sijayapata moja kwa moja, ingekuwa nimeyapokea mimi kutoka mikononi kwa Dokta ni sawa, ila nimeyakuta tu juu ya meza pale nyumbani, sasa sijui kama yamebadilishwa au yapo sawa" Vin alijibu,
"unahitaji msaada gani?" Strategic aliuliza,
"nahitaji utafute ukweli kupitia kwa Trigger" Vin aliongea,
"sawa, nitafanya hivyo, ila endapo tutapata mtaalam wa kuweka vitega sauti ili nikiwa naongea nae uwe unapata taarifa moja kwa moja" Strategic aliongea,
"hiyo kazi ndogo, nitaifanya mimi hapa" Vin aliongea,
"sawa, nadhani uifanye sasa hivi" Strategic aliongea kisha Vin akaenda kwenye begi lake na kulifungua, kisha akavitoa viwaya waya vingi na kuviweka juu ya meza,
"sasa itabidi niziweke ndani ya shati mbele usawa wa kifungo cha juu" Vin aliongea,
"waya zote hizo unaniwekea?" Strategic aliuliza,
"we nakuwekea mic (maiki), hizi nyaya zinabaki hapa" Vin aliongea huku akicheka, na kipindi hicho simu ya Strategic ilikuwa ikiita,
"Trigger" Strategic aliongea huku akimtazama Vin,
"pokea, ila usimwambie kama tupo wote na wala usimwambie kama tumeonana leo" Vin alimtahadharisha Strategic na Strategic akaitikia kwa kichwa kuonesha amekubaliana na maneno ya Vin,
"mkuu" Strategic aliongea baada ya kupokea simu,
.
"upo wapi bwana mipango?" Trigger aliuliza,
"nipo town" Strategic alijibu,
"na mimi nipo town, njoo tuonane" Trigger aliongea,
"sawa mkuu, nipe dakika kumi" Strategic alijibu,
"fresh" Trigger alijibu na kukata simu.
"sijui ananiitia nini?" Strategic aliongea baada ya kukata simu,
"nenda kumsikiliza, chukua na hii mic ipachike kwa ndani" Vin aliongea huku akimpatia mic na Strategic akapokea na kuipachika ndani ya shati lake.
"usiniangushe mista, wewe ndio tegemeo langu kwa sasa" Vin aliongea huku akiziunga nyaya zake kwenye lap top.
"tupo pamoja kaka" Strategic alijibu huku akiondoka kwa mwendo wa haraka.
Strategic alienda mpaka kwenye gari yake na kuingia, kisha akaiondoa kwa mwendo wa kasi. Alipofika maeneo ya mjini alitoa simu yake na kumpigia Trigger na kumuuliza ni wapi alipo? Trigger akamuelekeza kisha Strategic akaelekea uko moja kwa moja.
Strategic aliegesha gari nje ya hotel moja na kupitiliza moja kwa moja mpaka eneo la ndani ambalo lilikuwa na uwazi ambao ulitokana na bwawa la kuogelea lililokuwepo hapo ndani. Strategic akatupa macho kushoto na kulia, akaweza kumuona Trigger aliyekuwepo amekaa pembeni ya bwawa ambapo kulikuwa na kijitanda kidogo na meza ambayo Trigger alitumia kuweka pombe kali.
Strategic alitembea mpaka sehemu alipo Trigger, akakaa,
"kachukue glass tuendelee" Trigger alimwambia Strategic,
"hapana, pombe situmii" Strategic aliongea huku akitabasamu,
"kaagize utakacho basi" Trigger aliongea,
"ngoja, Muhudumu akipita hapa nitamuagiza" Strategic aliongea,
"sasa bwana kuna jambo nimekuitia, ni kuhusu vin" Trigger aliongea,
"amefanya nini?" Strategic aliuliza,
"aisee Vin anatakiwa afuatiliwe kwa ukaribu sana, kwa maana kwa sasa Sarah anamzuzua, anadai ni ndugu yake" Trigger aliongea,
"hiyo habari nimeisikia muda mrefu sana, kwani ukweli ni upi kuhusu undugu wao?" Strategic alianza kumchimba Trigger huku akijua fika Vin anasikia kila kitu,
"wale ni ndugu, ila juzi Vin alienda kupima damu hospitali, ila vipimo vimeonesha hawana undugu, hapo ndio tulishangaa" Trigger aliongea kwa mshangao,
"kwa hiyo majibu ya vipimo Vin ameyapata?" Strategic aliuliza,
"ametukuta nayo mimi na Taita, amekasirika sana na ndio maana nataka umfuatilie" Trigger aliongea,
"kwani wazazi Vin wapo wapi?" Strategic aliuliza,
"ni habari ndefu, ila kifupi ni kuwa wameuawa wote, tena waliteketea kwa moto" Trigger alijibu,
"sasa ikawaje Vin akapona, au hakuwepo ndani?" Strategic aliuliza,
"Vin nilimtoa mimi kabla nyumba haijaungua, niliwatoa yeye na Sarah baada ya Harry kumshauri Taita, ila baadae Harry huyo huyo akasema ni bora Vin abaki ila Sarah arudishwe ndani kwenye moto, nikamuingiza Sarah ndani, ila kosa ambalo nalijutia mpaka leo ni kutokumfunga Sarah, hiyo ilisababisha Sarah afanikiwe kutoka salama, ila sijajua alitumia mbinu zipi?" Trigger aliongea,
"kwa hiyo baba yake Sarah ndiyo baba yake Vin?" Strategic aliendelea kuchunguza,
"ndio, ila majibu ya hospitali yanaonesha hawana undugu" Trigger alijibu,
"sasa kwanini Taita aliwaua wazazi wa Vin alafu akachukua Vin, si bora angemuua na Vin?" Strategic aliuliza,
"bwana we, kwanza Taita na mama yao Vin na Sarah walikuwa ndugu, yaani mtoto wa mkubwa na mdogo, tena walizaliwa wao tu, baada ya baba zao kufa tatizo likaja kwenye mirathi, hapo ndipo ugomvi ulipoanzia" Trigger alijibu,
"ila nadhani njia bora ilikuwa ni kuwaua wote, yaani Vin na Sarah, sasa mlivyowaacha hai ndio matokeo yake hayo kila siku vurugu na Sarah" Strategic aliongea,
"huyu Vin tulimuacha hai na tukamfuta kumbukumbu zake zote, huyu alitakiwa awe mrithi wa Taita kwa maana Taita hana uwezo wa kuzalisha" Trigger aliongea na kumfanya Strategic ashangae,
"kumbukumbu zinafutwa? Zinafutwaje?" Strategic aliuliza kwa mshangao,
"zinafutwa hospitali, ila uwa zinarudi baada ya muda fulani, ila kwa Vin inakuwa ngumu kumbukumbu kumrudia kwa maana tulimfuta wakati akiwa mdogo sana, alikuwa na miaka minne" Trigger aliendelea kuongea bila kujua maongezi yao yote Vin anayasikia,
"ni hospitali gani hiyo mliyoitumia, maana na mimi ni bora nifute za kwangu kwa maana stress zitaniua" Vin aliuliza kwa utani huku akicheka,
"tulifanyia hospitali kuu ya mkoa, na dokta aliyetufanyia alikuwa ni baba mmoja alikuwa akiitwa Innocent Malle, sijui hata kama yupo hai, maana kipindi kile alikuwa na muonekano wa kuwa na umri wa miaka arobaini au hamsini, si unajua siku hizi watu hatuishi sana?'" Trigger aliongea na kugida ile chupa yenye pombe nyeupe mfano wa maji,
"kipindi hicho mkuu ulikuwa na umri gani?" Strategic aliuliza huku akicheka,
"nilikuwa chalii sana, nilikuwa na miaka ishirini na mbili, sasa hivi ni miaka ishirini imepita tangu tukio lile lifanyike" Trigger aliongea na kumfanya Strategic ashangae,
"ni muda sana, sasa acha mimi niondoke" Strategic aliongea,
"fanya hiyo kazi niliyokuagiza, hakikisha Vin hajui chochote, maana wewe unaweza kumwambia haya yote tuliyoongea hapa" Trigger aliongea huku akimtazama Strategic,
"nitamwambia muda gani wakati huyo Vin mi siendi naye sawa, ananata sana" Strategic aliongea huku akicheka,
"mmarekani yule, lazima awanatie" Trigger aliongea huku akicheka na kipindi hicho Strategic alikuwa akitoka zake.
*****************
Vin alikuwa bize akifuatilia maongezi kati ya Trigger na Strategic, sasa alianza kupata mwanga kidogo, ila kilichomchanganya ni matokeo ya vipimo kuonesha hana undugu na Sarah, na kipindi hicho amemsikia Trigger akidai Sarah na Vin ni ndugu,
"sihitaji kumuamini yoyote, kati ya Sarah wala Taita, bora nirudi marekani nikaendelee na maisha yangu" Vin aliongea peke yake huku akiwa na hasira, kisha akaizima lap top yake na kuingia bafuni..............
***********ITAENDELEA************
the Legend☆
Mh, labda jana kuna episodes hujazisoma dearHivi ni mm sielewi kuna episode imepitwa au mm ndio nimeiruka hiyo episode
Nakumbuka mara ya mwisho nimesoma trigger katoka hospt kuchukua vipimo imekuwaje tena
Trigger ni wakumwagia tindikali akili imkae sawaHahahaa, Trigger ndo huyo kashaingia na bastola yake ambayo akiinua haishushi mpaka risasi itoke
the Legend☆
Mh nimetoka uko bwana ebu endelea kidogo tu
Mbona jana nilisoma mwisho niliishia trigger alivyoenda hospital kuchukua majibuMh, labda jana kuna episodes hujazisoma dear
the Legend☆