Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA SITINI NA MOJA.

ENDELEA..................

"ooh samahani, kumbe upo na shemeji" Trigger aliongea huku akirudi nyuma na kutoka nje, uzuri ni kuwa hakuweza kumtambua Sarah kwa kuwa Sarah alimpa mgongo na pia mavazi aliyokuwa ameyavaa Sarah yalikuwa ni mapana na ya kiutu uzima, ikawa shida kwa Trigger kumtambua.

"subiri, Kaa hapo usitoke, ni Trigger huyo" Vin aliongea huku nae akitoka nje kumfuata, Sarah akakaa ila kwa tahadhari, aliamini chochote kinaweza kutokea.

Vin alitoka na kumkuta Trigger akiwa amesimama nje ya mlango,

"vipi kuna chochote?" Vin alimuuliza Trigger,

"mzee anakuita, ameniagiza nikufuate" Trigger aliongea,

"sasa hivi nina mgeni, nitakuja huko muda wowote, kwanini hamkunipigia simu?" Vin aliuliza,

"kwa kuwa niliamini nitakukuta tu" Trigger alijibu huku akitabasamu,

"poa, mwambie nakuja" Vin aliongea na kisha Trigger akaondoka zake.

Vin akarudi ndani,

"kuna usalama?" Sarah alimuuliza Vin,

"upo, mzee ananiita mara moja" Vin aliongea,

"nenda kwanza kamtafute daktari niliyokuambia, mzee wako utaenda kumuona baadae" Sarah aliongea,

"hilo suala nalifuatilia muda huu" Vin alijibu,

"sawa, ni naenda" Sarah aliongea huku akisimama,

"Kaa hapo kwanza, subiri" Vin aliongea huku akitoa simu yake, kisha akabonyeza namba ya Strategic,

"upo hapo nje?" Vin aliuliza kwenye simu,

"ndio mkuu" Strategic alijibu,

"umemuona Trigger akiondoka?" Vin aliuliza,

"ndio, ameondoka muda sio mrefu" Strategic alijibu,

"poa" Vin alijibu na kukata simu, akamgeukia Sarah,

"unaweza kuondoka sasa" Vin alimwambia Sarah,

"ina maana umeweka ulinzi nje?" Sarah aliuliza huku Akitabasamu,

"ulinzi muhimu" Vin alijibu na kumfanya Sarah aondoke huku akitabasamu.

Vin akakaa kwenye kochi na mawazo juu ya Sarah yakamuanza tena, kuna upande ulikuwa unakubali Sarah ni ndugu yake, ila kuna upande ulipinga kabisa hilo suala.

"ngoja nifuatilie ukweli kuhusu mimi kwanza, suala la undugu litafuata baadae" Vin aliongea na kunyanyuka, kisha akaelekea kwenye kabati na kuchagua suti, kisha akavaa na kutoka nje.

Alitoka mpaka nje na kuingia kwenye gari lake, kisha akatoa simu na kumpigia Strategic,

"umeniona?" Vin aliuliza baada ya simu kupokelewa,

"vizuri sana" Strategic alijibu huku akicheka,

"njoo kwenye gari yangu, kuna sehemu nataka twende" Vin aliongea kisha akakata simu.

Baada ya muda mchache Strategic aligonga kioo cha na kumfanya Vin afungue mlango,

"wewe ni mwenyeji mji huu?" Vin alimuuliza Strategic,

"ndio, vipi kwani?" Strategic aliuliza,

"nataka niyafuatilie maongezi ya Trigger mliokuwa mkiongea naye, kwa hiyo muda huu nipeleke hospitali kuu ya mkoa" Vin aliongea,

"sawa, na Trigger alivyokuja alikuwa na habari gani?" Strategic aliuliza huku akiwasha gari,

"alikuja kuleta taharifa kuwa mzee ananiita" Vin alijibu,

"ooh, sawa" Strategic aliongea huku akiondoa gari.

Safari yao iliishia katika hospitali kuu ya mkoa, Vin akatelemka na kumuacha Strategic ndani ya gari.

Vin akaingia moja kwa moja mpaka eneo la mapokezi na kumkuta mwanamke mtu mzima akiwa amekaa, Vin akamsalimia,

"namuulizia Dokta mmoja anaitwa innocent Malle" Vin aliongea huku akimtazama huyo mama,

"mhmm...anafanya kazi hapa? Mbona simjui? Au ni hawa vijana wanaofanya field?". Mama yule aliuliza maswali mfululizo na kumfanya Vin atabasamu,

"hapana, alishawahi kunitibu miaka ishirini iliyopita, alikuwa mfanyakazi wa hapa, nilikuwa nje ya nchi sasa nimrudie, na nataka nionane nae na sikuwa na sehemu nyingine ya kumuulizia zaidi ya hapa" Vin aliongea na kumfanya mama ashangae,

"miaka ishirini ni mingi mwanangu, ebu nenda chumba kile unaweza kupata msaada" Mama yule aliongea huku akimuelekeza Vin kwa kutumia kidole chake cha shahada.

Vin akaelekea moja kwa moja mpaka kwenye hicho chumba, akagonga hodi na kuruhusiwa kuingia, akamkuta kijana mmoja akiwa amekaa,

"karibu" Kijana alimkaribisha Vin,

"asante" Vin aliitikia huku akiwa hajui aanzie wapi kueleza shida yake,

"nakusikilza boss" Kijana aliongea huku akimtazama Vin,

"namuulizia Dokta Innocent Malle" Vin aliongea,

"yupo, unashida gani?" kijana alijibu na kumshangaza Vin,

"umemjuaje wakati wewe ni kijana na kwa makadirio huyo Dokta atakuwa amestaafu miaka mingi nyuma?" Vin aliuliza huku akitabasamu,

"Mimi ndio mtu ambaye nashughulika na wafanyakazi wastaafu wa hii hospitali, ndio maana nimemtambua kwa urahisi huyo mzee" kijana alijibu huku akitabasamu,

"nitampata wapi kwa sasa?" Vin aliuliza,

"una shida naye ipi?" kijana aliuliza na kumfanya Vin acheke,

"alikuwa ni daktari wa familia yetu kipindi nikiwa mdogo, nilisafiri kwa muda mrefu sana, sasa nimerudi na nimeona ni vyema nimtafute" Vin aliongea,

"ok, yupo, ngoja nikupitie namba yake ya simu" Yule kijana aliongea huku akibonyeza vitufe vya kompyuta yake.

"si atakuwa amezeeka sana?" Vin aliuliza huku akijifanya anamjua,

"umri umeenda, ila bado ana nguvu" Kijana alijibu huku akimpatia Vin karatasi yenye namba za simu za Dokta Innocent Malle

"asante sana" Vin alipokea kile kikaratasi na kushukuru, kisha akaanza kuondoka huku zile namba akiziingiza kwenye simu yake, alitoka mpaka nje kwenye gari na kupiga namba ya simu ya Dokta Innocent Malle, simu iliita kisha ikapokelewa na Dokta mwenyewe, Vin akaomba aonane nae, ingawa ilikuwa ngumu kukubaliwa kwa haraka, ila baada ya kuomba sana, Dokta Innocent Malle alikubali kuonana na Vin, akamuelekeza nyumbani kwake.

Vin akamgeukia Strategic na kumwambia pa kumpeleka, strategic akawasha gari na kuiondoa kwa mwendo wa wastani.

Iliwachukua nusu saa tu Strategic kufika nje ya nyumba ambayo walielekezwa, waliitambua kutokana na namba ya mtaa na namba ya nyumba pia. Strategic akaegesha gari na kisha wakatelemka, wakabonyeza kitufe cha getini ambacho kilikuwa ni kengele, baada ya dakika moja geti lilifunguliwa na Kijana mmoja ambaye alilingana umri na Vin,

"karibuni" Kijana aliongea,

"asante" Vin aliitikia huku akiingia ndani, walipoingia ndani walikutana na mandhari nzuri, nyumba ilikuwa na uwanja mkubwa ambao ulipandwa miti mingi ya matunda iliyosababisha kivuli kipatikane kwa asilimia kubwa. Vin na Strategic waliendelea kuitazama ile nyumba huku wakionekana kuvutiwa na mazingira ya pale.

"karibuni" Kijana aliyewakaribisha aliongea huku akiwaelekeza kakibanda kadogo kalichoezekwa kwa nyasi, ambapo ndani ya kakibanda hako kulikuwa na meza kubwa iliyozungukwa na makochi ya sofa ambayo yalikuwa makuu kuu ila yalipendeza kukaa sehemu ile.

"karibuni" Kijana aliongea tena baada ya Vin na Strategic kufika ndani ya kibanda kile,

"shukran sana" Vin alijibu huku akikaa kwenye kochi,

"nyie ndio mliopiga simu mnataka kuongea na mzee?" Kijana aliuliza huku akiwaangalia,

"ndio, ni sisi" Vin alijibu,

"msubirini kidogo" Kijana aliongea na kuelekea ndani, baada ya dakika mbili kijana alirejea huku mkononi akiwa na chupa mbili za chai na ndoo yenye vikombe vidogo vya udongo, akaweka mezani.

"chupa hii ina kahawa na hii ina chai ya kawaida, mtajihudumia mtakacho" Kijana aliongea na kurudi zake ndani na kuwaacha Vin na Strategic wakitazamana.



********************

Sarah alivyotoka Vin hotel kuongea na Vin, aliamua kupitia super market kwa ajili ya kununua vitu vya nyumbani. Aliingia super market na kuchukua mahitaji yake, alipomaliza alienda kwa mpokea pesa ambaye alivihakiki vitu vya Sarah na kisha akamtajia malipo, Sarah akalipa na kutoka na vitu vyake mpaka nje, akaviingiza ndani ya gari na kisha akaingia kwenye gari na kuanza kuondoka.

Wakati Sarah akiwa anaondoka eneo hilo, ndio muda ambao Sajenti Minja alikuwa anaingia hapo, wakati wakapishana, Sajenti Minja alitupia jicho kwenye gari alilopo Sarah, akamtambua.

Alichofanya Sajenti Minja ni kupishana na gari ya Sarah kisha akageuza gari yake na kuanza kumfuatilia Sarah, alitaka kujua ni wapi anapokaa. Sajenti Minja kwa kutumia akili zake zote za kipelelezi aliendelea kuifuatilia gari ya Sarah huku akiwa makini kutumia mbinu tofauti ili Sarah asimgundue kwa maana alijua Sarah ni mtu hatari kwa hiyo kwa vyovyote vile ni lazima na yeye atakuwa makini kila wakati.

Gari ya Sarah ilizidi kwenda mpaka kwenye mtaa mmoja uliokuwa mgeni machoni kwa Sajenti Minja, kisha Sarah akasimamisha gari lake mbele ya nyumba moja ambayo ilikuwa ngeni pia kwa Sajenti Minja. Sajenti Minja nae akasimamisha gari lake mbele ya nyumba ambayo hakuijua, aliamua afanye hivyo ili hata Sarah akishuka kwenye gari yake asiweze kutilia mashaka

Umbali wa eneo aliposimama Sarah na eneo ambalo Sajenti Minja aliegesha gari yake, ulikuwa ni umbali mrefu sana, kilichomsaidia Sajenti Minja ni barabara kuwa nyoofu, kwa hiyo aliweza kumuona Sarah vizuri sana kwa kila hatua aliyokuwa anaifanya.

Sajenti Minja alimshuhudia Sarah akishuka kwenye gari yake na kisha akaenda kufungua geti, akamshuhudia tena Sarah akirudi ndani ya gari na kuiingiza gari ndani ya geti, baada ya sekunde chache aliweza kuona geti likirudishiwa.

Sajenti Minja akatoa simu yake mfukoni, kisha akatoa kichwa ndani ya gari na kumsimamisha kijana mmoja aliyekuwa akipita, akamsalimu,

"dogo huu mtaa unaitwaje?" Sajenti Minja aliuliza,

.

"tambeleya" Dogo alijibu na kisha Sajenti Minja akashukuru na dogo akaendelea na safari. Sajenti Minja akapiga simu, baada ya muda mtu wa upande wa pili akapokea simu,

"upo ofisini?" Sajenti Minja aliuliza baada ya simu kupokelewa,

"ndio mkuu" Mtu wa upande wa pili alijibu,

"chukua gari mbili zikiwa na askari wenye silaha, alafu nitakuelekeza unifuate" Sajenti Minja aliongea na kukata simu, aliamua kuchukua askari wengi kwa maana alihufahamu utata wa Sarah kwenye mapambano.

Baada ya dakika kumi simu ya Sajenti Minja iliita, ilikuwa namba ya yule askari aliyempigia muda mchache uliopita, Sajenti Minja akapokea na kisha akamuelekeza ni wapi alipo, akakata simu.

Baada ya dakika ishirini gari mbili za polisi zikiwa na askari wakutosha na wote wenye silaha walisimamisha gari pembeni ya gari ya Sajenti Minja, Sajenti Minja akashuka na kuingia kwenye gari la mbele la polisi,

"twende" Sajenti Minja alimwambia dereva ambaye alifuata maelekezo mpaka mbele ya nyumba aliyoingia Sarah, Sajenti Minja akashuka kwenye gari na kisha akawataka askari wote watelemke, waliposhuka wakamzunguka Sajenti Minja,

"mnachotakiwa ni kuivamia hii nyumba, mtu yoyote mtayemkuta humu mkamateni, haya vamieni" Sajenti Minja aliongea kwa amri kisha askari wakavamia kwa fujo ile nyumba huku Sajenti Minja akija kwa nyuma yao.

Askari walivamia nyumba na kuizunguka yote, ila mlango wa kuingilia ndani ya nyumba ulikuwa umefungwa kwa ndani, na taa ya ndani ya nyumba ilikuwa imewashwa,

"mliopo ndani jisalimisheni" Sajenti Minja aliongea kwa sauti kubwa, ila hakuna mtu aliyetoka, badala yake wakashuhudia taa za ndani zikizimwa zote,

"lete bunduki" Sajenti Minja alimwambia askari aliyepo jirani yake, askari akampatia Sajenti Minja bunduki, Sajenti Minja akarudi nyuma kisha akafyatulia risasi kadhaa eneo la kitasa, baada ya hapo akaupiga mlango take, mlango ukafunguka,

"twendeni ndani" Sajenti Minja aliamrisha na askari kama kumi aliongozana nao kuingia ndani na wengine walibaki nje wakiimarisha ulinzi...................

***********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
Minja nae ana kaki here here,,ndio maana Ray kamuua upande wa pili
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA SITINI NA MOJA.

ENDELEA..................

"ooh samahani, kumbe upo na shemeji" Trigger aliongea huku akirudi nyuma na kutoka nje, uzuri ni kuwa hakuweza kumtambua Sarah kwa kuwa Sarah alimpa mgongo na pia mavazi aliyokuwa ameyavaa Sarah yalikuwa ni mapana na ya kiutu uzima, ikawa shida kwa Trigger kumtambua.

"subiri, Kaa hapo usitoke, ni Trigger huyo" Vin aliongea huku nae akitoka nje kumfuata, Sarah akakaa ila kwa tahadhari, aliamini chochote kinaweza kutokea.

Vin alitoka na kumkuta Trigger akiwa amesimama nje ya mlango,

"vipi kuna chochote?" Vin alimuuliza Trigger,

"mzee anakuita, ameniagiza nikufuate" Trigger aliongea,

"sasa hivi nina mgeni, nitakuja huko muda wowote, kwanini hamkunipigia simu?" Vin aliuliza,

"kwa kuwa niliamini nitakukuta tu" Trigger alijibu huku akitabasamu,

"poa, mwambie nakuja" Vin aliongea na kisha Trigger akaondoka zake.

Vin akarudi ndani,

"kuna usalama?" Sarah alimuuliza Vin,

"upo, mzee ananiita mara moja" Vin aliongea,

"nenda kwanza kamtafute daktari niliyokuambia, mzee wako utaenda kumuona baadae" Sarah aliongea,

"hilo suala nalifuatilia muda huu" Vin alijibu,

"sawa, ni naenda" Sarah aliongea huku akisimama,

"Kaa hapo kwanza, subiri" Vin aliongea huku akitoa simu yake, kisha akabonyeza namba ya Strategic,

"upo hapo nje?" Vin aliuliza kwenye simu,

"ndio mkuu" Strategic alijibu,

"umemuona Trigger akiondoka?" Vin aliuliza,

"ndio, ameondoka muda sio mrefu" Strategic alijibu,

"poa" Vin alijibu na kukata simu, akamgeukia Sarah,

"unaweza kuondoka sasa" Vin alimwambia Sarah,

"ina maana umeweka ulinzi nje?" Sarah aliuliza huku Akitabasamu,

"ulinzi muhimu" Vin alijibu na kumfanya Sarah aondoke huku akitabasamu.

Vin akakaa kwenye kochi na mawazo juu ya Sarah yakamuanza tena, kuna upande ulikuwa unakubali Sarah ni ndugu yake, ila kuna upande ulipinga kabisa hilo suala.

"ngoja nifuatilie ukweli kuhusu mimi kwanza, suala la undugu litafuata baadae" Vin aliongea na kunyanyuka, kisha akaelekea kwenye kabati na kuchagua suti, kisha akavaa na kutoka nje.

Alitoka mpaka nje na kuingia kwenye gari lake, kisha akatoa simu na kumpigia Strategic,

"umeniona?" Vin aliuliza baada ya simu kupokelewa,

"vizuri sana" Strategic alijibu huku akicheka,

"njoo kwenye gari yangu, kuna sehemu nataka twende" Vin aliongea kisha akakata simu.

Baada ya muda mchache Strategic aligonga kioo cha na kumfanya Vin afungue mlango,

"wewe ni mwenyeji mji huu?" Vin alimuuliza Strategic,

"ndio, vipi kwani?" Strategic aliuliza,

"nataka niyafuatilie maongezi ya Trigger mliokuwa mkiongea naye, kwa hiyo muda huu nipeleke hospitali kuu ya mkoa" Vin aliongea,

"sawa, na Trigger alivyokuja alikuwa na habari gani?" Strategic aliuliza huku akiwasha gari,

"alikuja kuleta taharifa kuwa mzee ananiita" Vin alijibu,

"ooh, sawa" Strategic aliongea huku akiondoa gari.

Safari yao iliishia katika hospitali kuu ya mkoa, Vin akatelemka na kumuacha Strategic ndani ya gari.

Vin akaingia moja kwa moja mpaka eneo la mapokezi na kumkuta mwanamke mtu mzima akiwa amekaa, Vin akamsalimia,

"namuulizia Dokta mmoja anaitwa innocent Malle" Vin aliongea huku akimtazama huyo mama,

"mhmm...anafanya kazi hapa? Mbona simjui? Au ni hawa vijana wanaofanya field?". Mama yule aliuliza maswali mfululizo na kumfanya Vin atabasamu,

"hapana, alishawahi kunitibu miaka ishirini iliyopita, alikuwa mfanyakazi wa hapa, nilikuwa nje ya nchi sasa nimrudie, na nataka nionane nae na sikuwa na sehemu nyingine ya kumuulizia zaidi ya hapa" Vin aliongea na kumfanya mama ashangae,

"miaka ishirini ni mingi mwanangu, ebu nenda chumba kile unaweza kupata msaada" Mama yule aliongea huku akimuelekeza Vin kwa kutumia kidole chake cha shahada.

Vin akaelekea moja kwa moja mpaka kwenye hicho chumba, akagonga hodi na kuruhusiwa kuingia, akamkuta kijana mmoja akiwa amekaa,

"karibu" Kijana alimkaribisha Vin,

"asante" Vin aliitikia huku akiwa hajui aanzie wapi kueleza shida yake,

"nakusikilza boss" Kijana aliongea huku akimtazama Vin,

"namuulizia Dokta Innocent Malle" Vin aliongea,

"yupo, unashida gani?" kijana alijibu na kumshangaza Vin,

"umemjuaje wakati wewe ni kijana na kwa makadirio huyo Dokta atakuwa amestaafu miaka mingi nyuma?" Vin aliuliza huku akitabasamu,

"Mimi ndio mtu ambaye nashughulika na wafanyakazi wastaafu wa hii hospitali, ndio maana nimemtambua kwa urahisi huyo mzee" kijana alijibu huku akitabasamu,

"nitampata wapi kwa sasa?" Vin aliuliza,

"una shida naye ipi?" kijana aliuliza na kumfanya Vin acheke,

"alikuwa ni daktari wa familia yetu kipindi nikiwa mdogo, nilisafiri kwa muda mrefu sana, sasa nimerudi na nimeona ni vyema nimtafute" Vin aliongea,

"ok, yupo, ngoja nikupitie namba yake ya simu" Yule kijana aliongea huku akibonyeza vitufe vya kompyuta yake.

"si atakuwa amezeeka sana?" Vin aliuliza huku akijifanya anamjua,

"umri umeenda, ila bado ana nguvu" Kijana alijibu huku akimpatia Vin karatasi yenye namba za simu za Dokta Innocent Malle

"asante sana" Vin alipokea kile kikaratasi na kushukuru, kisha akaanza kuondoka huku zile namba akiziingiza kwenye simu yake, alitoka mpaka nje kwenye gari na kupiga namba ya simu ya Dokta Innocent Malle, simu iliita kisha ikapokelewa na Dokta mwenyewe, Vin akaomba aonane nae, ingawa ilikuwa ngumu kukubaliwa kwa haraka, ila baada ya kuomba sana, Dokta Innocent Malle alikubali kuonana na Vin, akamuelekeza nyumbani kwake.

Vin akamgeukia Strategic na kumwambia pa kumpeleka, strategic akawasha gari na kuiondoa kwa mwendo wa wastani.

Iliwachukua nusu saa tu Strategic kufika nje ya nyumba ambayo walielekezwa, waliitambua kutokana na namba ya mtaa na namba ya nyumba pia. Strategic akaegesha gari na kisha wakatelemka, wakabonyeza kitufe cha getini ambacho kilikuwa ni kengele, baada ya dakika moja geti lilifunguliwa na Kijana mmoja ambaye alilingana umri na Vin,

"karibuni" Kijana aliongea,

"asante" Vin aliitikia huku akiingia ndani, walipoingia ndani walikutana na mandhari nzuri, nyumba ilikuwa na uwanja mkubwa ambao ulipandwa miti mingi ya matunda iliyosababisha kivuli kipatikane kwa asilimia kubwa. Vin na Strategic waliendelea kuitazama ile nyumba huku wakionekana kuvutiwa na mazingira ya pale.

"karibuni" Kijana aliyewakaribisha aliongea huku akiwaelekeza kakibanda kadogo kalichoezekwa kwa nyasi, ambapo ndani ya kakibanda hako kulikuwa na meza kubwa iliyozungukwa na makochi ya sofa ambayo yalikuwa makuu kuu ila yalipendeza kukaa sehemu ile.

"karibuni" Kijana aliongea tena baada ya Vin na Strategic kufika ndani ya kibanda kile,

"shukran sana" Vin alijibu huku akikaa kwenye kochi,

"nyie ndio mliopiga simu mnataka kuongea na mzee?" Kijana aliuliza huku akiwaangalia,

"ndio, ni sisi" Vin alijibu,

"msubirini kidogo" Kijana aliongea na kuelekea ndani, baada ya dakika mbili kijana alirejea huku mkononi akiwa na chupa mbili za chai na ndoo yenye vikombe vidogo vya udongo, akaweka mezani.

"chupa hii ina kahawa na hii ina chai ya kawaida, mtajihudumia mtakacho" Kijana aliongea na kurudi zake ndani na kuwaacha Vin na Strategic wakitazamana.



********************

Sarah alivyotoka Vin hotel kuongea na Vin, aliamua kupitia super market kwa ajili ya kununua vitu vya nyumbani. Aliingia super market na kuchukua mahitaji yake, alipomaliza alienda kwa mpokea pesa ambaye alivihakiki vitu vya Sarah na kisha akamtajia malipo, Sarah akalipa na kutoka na vitu vyake mpaka nje, akaviingiza ndani ya gari na kisha akaingia kwenye gari na kuanza kuondoka.

Wakati Sarah akiwa anaondoka eneo hilo, ndio muda ambao Sajenti Minja alikuwa anaingia hapo, wakati wakapishana, Sajenti Minja alitupia jicho kwenye gari alilopo Sarah, akamtambua.

Alichofanya Sajenti Minja ni kupishana na gari ya Sarah kisha akageuza gari yake na kuanza kumfuatilia Sarah, alitaka kujua ni wapi anapokaa. Sajenti Minja kwa kutumia akili zake zote za kipelelezi aliendelea kuifuatilia gari ya Sarah huku akiwa makini kutumia mbinu tofauti ili Sarah asimgundue kwa maana alijua Sarah ni mtu hatari kwa hiyo kwa vyovyote vile ni lazima na yeye atakuwa makini kila wakati.

Gari ya Sarah ilizidi kwenda mpaka kwenye mtaa mmoja uliokuwa mgeni machoni kwa Sajenti Minja, kisha Sarah akasimamisha gari lake mbele ya nyumba moja ambayo ilikuwa ngeni pia kwa Sajenti Minja. Sajenti Minja nae akasimamisha gari lake mbele ya nyumba ambayo hakuijua, aliamua afanye hivyo ili hata Sarah akishuka kwenye gari yake asiweze kutilia mashaka

Umbali wa eneo aliposimama Sarah na eneo ambalo Sajenti Minja aliegesha gari yake, ulikuwa ni umbali mrefu sana, kilichomsaidia Sajenti Minja ni barabara kuwa nyoofu, kwa hiyo aliweza kumuona Sarah vizuri sana kwa kila hatua aliyokuwa anaifanya.

Sajenti Minja alimshuhudia Sarah akishuka kwenye gari yake na kisha akaenda kufungua geti, akamshuhudia tena Sarah akirudi ndani ya gari na kuiingiza gari ndani ya geti, baada ya sekunde chache aliweza kuona geti likirudishiwa.

Sajenti Minja akatoa simu yake mfukoni, kisha akatoa kichwa ndani ya gari na kumsimamisha kijana mmoja aliyekuwa akipita, akamsalimu,

"dogo huu mtaa unaitwaje?" Sajenti Minja aliuliza,

.

"tambeleya" Dogo alijibu na kisha Sajenti Minja akashukuru na dogo akaendelea na safari. Sajenti Minja akapiga simu, baada ya muda mtu wa upande wa pili akapokea simu,

"upo ofisini?" Sajenti Minja aliuliza baada ya simu kupokelewa,

"ndio mkuu" Mtu wa upande wa pili alijibu,

"chukua gari mbili zikiwa na askari wenye silaha, alafu nitakuelekeza unifuate" Sajenti Minja aliongea na kukata simu, aliamua kuchukua askari wengi kwa maana alihufahamu utata wa Sarah kwenye mapambano.

Baada ya dakika kumi simu ya Sajenti Minja iliita, ilikuwa namba ya yule askari aliyempigia muda mchache uliopita, Sajenti Minja akapokea na kisha akamuelekeza ni wapi alipo, akakata simu.

Baada ya dakika ishirini gari mbili za polisi zikiwa na askari wakutosha na wote wenye silaha walisimamisha gari pembeni ya gari ya Sajenti Minja, Sajenti Minja akashuka na kuingia kwenye gari la mbele la polisi,

"twende" Sajenti Minja alimwambia dereva ambaye alifuata maelekezo mpaka mbele ya nyumba aliyoingia Sarah, Sajenti Minja akashuka kwenye gari na kisha akawataka askari wote watelemke, waliposhuka wakamzunguka Sajenti Minja,

"mnachotakiwa ni kuivamia hii nyumba, mtu yoyote mtayemkuta humu mkamateni, haya vamieni" Sajenti Minja aliongea kwa amri kisha askari wakavamia kwa fujo ile nyumba huku Sajenti Minja akija kwa nyuma yao.

Askari walivamia nyumba na kuizunguka yote, ila mlango wa kuingilia ndani ya nyumba ulikuwa umefungwa kwa ndani, na taa ya ndani ya nyumba ilikuwa imewashwa,

"mliopo ndani jisalimisheni" Sajenti Minja aliongea kwa sauti kubwa, ila hakuna mtu aliyetoka, badala yake wakashuhudia taa za ndani zikizimwa zote,

"lete bunduki" Sajenti Minja alimwambia askari aliyepo jirani yake, askari akampatia Sajenti Minja bunduki, Sajenti Minja akarudi nyuma kisha akafyatulia risasi kadhaa eneo la kitasa, baada ya hapo akaupiga mlango take, mlango ukafunguka,

"twendeni ndani" Sajenti Minja aliamrisha na askari kama kumi aliongozana nao kuingia ndani na wengine walibaki nje wakiimarisha ulinzi...................

***********ITAENDELEA************

the Legend☆

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom