Willy Gamba 1
JF-Expert Member
- Jan 5, 2015
- 352
- 377
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA KUMI NA SITA
Siku kama hiyo ya jumamosi chuoni hapo kuna
kuwa na disko ndani ya ukumbi wa chuo na
baadhi
ya wanafunzi huwa wanachaguliwa kucheza
nyimbo za aina mbalimbali ilikuonesha uwezo
wao
na vipaji vyao,
Rafiki zake na victoria waliweza kugundua kuwa
victoria ameanza kumpenda david hivyo walianda
mpango na kuongea na wanachumba wenzie na
david kuwa itakapofika muda wa kucheza basi
david acheze na victoria na wengine waliobaki
watacheza na wao,
Swala hilo lilionekana jema sana kwa washikaji
zake na david maana waliona sheshe kaingia
kwenye kichaka cha simba hivyo hakuna jinsi
zaidi
ya kumlarua tu na kumla nyama, mpango huo
ulikubalika,
Mida ya saa mojamoja hivi usiku wanafunzi
walionekana kujiandaa vyema, wenye kuazima
nguo waliazima, na wenye kugongea marashi
waligongea ilimradi kila mtu aonekane maridadi
siku hiyo mbele ya wavulana na mbele ya
wasichana ndani ya ukumbi huo,
Mipango yote hiyo wakati ikiendelea david
hakuwa
na taarifa yoyote ile, yeye alijiandaa kawaida
maana hakuwa mpenzi sana wa mziki na
mipango
yake ilikuwa ni kwenda kuangalia kwa muda tu na
kumuona mtoto victoria kisha arudi zake bwenini,
sauti ile ya mziki uliokuwa unasikika ukumbini
ulianza kuwa kusanya watu eneo lile.wengi
walipendeza na nguo zao za anasa,wengine
walionesha mizuka yao kwa kucheza nje hata
kabla
ya kuingia ndani acha wale waliokuwa
wamekumbatiana kwenye giza wakiendelea na
mambo yao ya ajabu ambayo haya stahiri
kuonwa
na watoto,
yote hayo david aliyaona na kubaki kusikitika tu
na
kuendelea kuzunguka kumtafuta victoria, wakati
akiwa anashangaa ghafla alikuja msichana
mmoja
kwa nyuma ,hakika alikuwa mrembo sana,
akamshika kiuno david hali iliyomfanya ageuke
kwa
haraka sana, kitendo kile cha kugeuka haraka na
yule dada alikuwa anataka kumkumbatia basi
wakajikuta wanadondoka chini na yule dada
akiwa
juu ya david,,
watu waliwazunguka na kuanza kuwa pigia
makofi
hata wale waliokuwa mbali walitamani kutaka
kujua kuna nini eneo lile hivyo nao hawakusita
kusogelea,
umati huo uliokuwa unasogea alikuwepo na
victoria pia, ndani ya dakika chache kila mtu
aliweza kushuhudia kitendo kile na yule dada
alifurahi sana kwa tukio lile maana alikuwa
kajipatia umaarufu mkubwa kumkumbatia
mwanaume asiye kuwa na mpango na wanawake
halafu anapendwa na wengi,
david alijitahidi kumsukuma yule dada pale chini
na akafanikiwa, alinyanyuka kwa hasira na
kuanza
kuwasukuma watu wampishe ili apite andoke
zake,
alipo wamaliza ghafla mbele yake akamuona
victoria aliyekuwa anataka kuanza kulia,
kwakuwa kila mmoja alikuwa anampenda
mwenzie
hivyo nyuso zao ziliteseka kwa aibu na victoria
kuanza kukimbia eneo lile na david kumfuata kwa
nyuma, watu hawakuelewa kinachoendelea zaidi
walizidi kushangilia tu kwa kujionea filamua ya
mapenzi ya bure,
Victoria alikimbia mpaka akapotezana na david,
hivyo david akawa anazidi kumtafuta maeneo
yote
yale ya chuo lakini hakumuona kwa muda huo
Hasira za victoria zilimpeleka mpaka kwenye stoo
ya chuo ambayo ilikuwa na kiza na kuanza kulia,
alijilaumua sana kwa kuchelewa kumwambia hisia
zake mwanaume aliye mpenda kwa muda mfupi
na
akiwa ndani ya maumivu alilia sana huku
akiendelea kufikiria na maneno ya upweke
yakamtoka,,,,
âânani ambaye atauokoa moyo wangu kwenye
mafuriko haya ya machozi eeh jaman nimechoka
kuwa mtumwa wa kumtumikia bwana maumivu,
nani aje kuwa mkombozi wangu na kunifariji kwa
kipindi hiki kigumu eeh?
Victoria alijuta kuwa na moyo wa upendo kwa
kuwa ulikosa mtu wa kuutunza, machozi hayo
alimkumbuka mtu aliye kuwa na ahadi naye ya
kukutana, na aliya kumbuka maneno matamu
aliyokuwa anatumiwa hivyo alihisi moyo wake
unaweza kupata faraja kupitia mtu huyo bila ya
kujua mtu mwenyewe ni david aliyempenda bila
kumwambia pia ndiye aliye mfanya yeye kuwa
mahali hapo ambapo si salama kwa usiku huo,
Victoria hakuwa na budi kuanza kulitafuta jina la
mtu huyo kwa jinsi alivyo liweka yeye ili ampigie
waonane, wakati anaendelea kulitafuta kumbe
david alikuwa amekaribia maeneo hayo ya stoo
na
alishtushwa na mwanga wa simu uliokuwa
unaonekana kule stoo na hisia zikaja huenda
atakuwa victoria hivyo ikabidi aufuate ili awe na
uhakika kama kweli ni victoria,
David hakuchukua muda mpaka kufika kwenye
mlango wa stoo na alianza kuchungulia mle ndani
na kugundua kuwa yule ni victoria kwa kusaidiwa
na ule mwanga wa simu uliokuwa unammulika
mrembo huyo ambaye david mwanzo alimuita
Qeen
tz,
kabla victoria hajalipata jina la mtu anayetaka
kuonana nae ghafla rafiki yake akamtumia ujumbe
ulikuwa unamuuliza,
âuko wapiâ?
victoria alisonya na kuendelea kutafuta jina la
mtu
wake bila kujibu ujumbe huo ndipo rafiki yake
huyo
akaamua kumpigia na wimbo uliokuwa unaita ni
huu,,,,,,,
âIâm so lonely broken angelâ
âIâm so lonely,listen to my heartâ
âone and only broken angelâ
âcome and save me, before I fall apartâ
Victoria pia hakuweza kupokea hata hiyo simu
mpaka nyimbo hiyo iliyoendana na upweke
alionao
ma iliyomuongezea machozi ilipo kata yenyewe,
David aliusikia wimbo huo pale nje na kilio cha
mtoto mzuri victoria ndipo alipojitokeza na
maneno
matamu ya mahaba yalitoka kwa sauti inayo
sisitiza upendo,,,,,
âniko hapa kukutoa upweke ulionaoâ
Sauti hiyo iliushtua sana moyo wa Victoria
alitamani kumjua huyo mtu aliye ingia humo
ndani
japo alihiisi kama sauti anaifahamu vile, ndipo
alipommulika usoni kwa kutumia mwanga wa
simu
na kugundua kuwa ni david,
Mdomo wenye ulimi mzuri ndani yake na
uliojaaliwa kutamka maneno mazuri ya upendo
ulitaka kusema kitu lakini ulipingwa na sauti iliyo
shiba ya shababi david kwa kauli yenye kusisitiza
mahaba,,,,,,
âVictoria moyo wako unaweza kutoka kwenye
mafuriko ya machozi kama utaruhusu kuliachia
tabasamu ulilolificha kwa muda mrefu kwa mtu
unaye mpenda na kuhisi kuwa anaweza kuwa
baharia wako atakaye kufikisha nchi ya furaha
yenye upepo na kijua cha mapendo ya dhati na
kuepukana na visamaki pamoja na vichura
vidogovidogo vilivyokuja na tamaa ya maji
ambavyo kiangazi ikifika havionekaniâ
âWengi watakuhitaji kwa muda mfupi lakini ni
kwasababu ya kutaka kutimiza kiu yao ya uzinzi
tu
ila mimi david niko hapa kwa ajili ya kutaka
kulinda uzuri wako usipotee na kuharibiwa na
watu
wasio jua thaman yako fikiria leo nafuta chozi
lako
kwa maneno ya dhati toka moyoni mwangu
ambayo sijawahi kumueleza mwanamke yoyote
yule katika ulimwengu huu lakini kwako
yameweza
kutoka tena bila hata ya kujali ile namba ya siri
ambayo kwa mwanaume mwenye kujielewa ni
lazima ndio aifanye kuwa funguo ya moyo si
nyingine ni tabia pekee,, hilo kwangu sikujali
tafadhali naomba upokee maombi haya ambayo
tayari yamesha pitigwa saini ya upendoâ
Victoria alizidi kuweweseka manaa hakuamini
kama angeweza kukutana na mwanaume aliye
mpenda kwa dhati katika mazingira hayo, kicheko
cha furaha kilicho changanyika na aibu kiliendelea
kumtesa moyoni mwake, miguu yake ikawa na
kazi
ya kuchimbachimba chini huku vidole vyake vya
mkono wa kulia akivinyonya kama mtoto mdogo
aliye kuwa na hamu ya ziwa la mama yake,
aliinua
uso wake uliokuwa unangâa hata kama kulikuwa
na
kiza na kumrembulia jicho david, jecho lenye kope
za asili na majimaji ndani yake ambayo yalizidi
kumfanya david kujipa asilimia 99% za kumpata
Victoria,
Miguu yao ilionekana kupiga hatua ndogo ndogo
wakisogeleana kwa hisia mpaka ku kawa na
umbali wenye mita sifuri(zero distance) na
kilichoendelea hakisimuliki,
Ndani ya muda wa kama saa moja na nusu hivi
walionekana wakitoka kwenye chumba hicho
kilichokuwa na kiza huku nyuso zao zikiwa na
furaha,
Victoria kila walipo kuwa wana tembea umbali wa
hatua tano lazima aegemee kifua cha david huku
akiachia kicheko ambacho kilimfanya david
atabasamu na kumuachia busu la msisimko
shavuni mwake,
Kutembea kwao pamoja walivutia wengi ambao
walikodoa mi macho kuwa tizama na kutaka
kuhakikisha kama yule ni david au siye, wakawa
na
kazi ya kutaniana tu na kukimbizana kwenye
viunga vya maua chuoni hapo hata habari ya
disko
wakawa wamesahau kabisa,
Moyo wa david ukawa umeingiwa na furaha ya
ajabu ambayo hakuwahi kuipata kwenye maisha
yake lakini Victoria mwanamke wa kwanza
ameweza kuibadilisha akili ya david na
kumuingiza
sehemu ambayo wengi wana lia,
Rafiki zake na Victoria waliokuwa wana mtafuta
walibaki midomo wazi walipo wakuta pamoja
wamekumbatiana huku wakiwa wameegemea mti,
kila mmoja wao alionekana kufurahia mahusiano
yao kwa kuwa waliendana sana.
Siku nyingi zilikatika na habari zili sambaa chuoni
hapo juu ya watu hao wawili kuwa katika
mahusiano ya kimapenzi, waliokuwa
wanampenda
Victoria waliumia kwa kumkosa hata yule
Emmanuely regan aliye mtenda alianza kuona
wivu
jinsi watu walivyo kuwa wana wasifia kwa
kuendana kwako,
Wasichana wengi nao walijitahidi kutaka kutoa
kasoro za Victoria kwa kuwa walikuwa
wanampenda david lakini jitihada zao ziligonga
mwamba kwa wawili hao kushikamana kupita
kiasi,
****************************************
Miaka minne ya david kukaa chuoni ikawa
imewadia ni baada ya kumaliza mtihani wao wa
mwisho na kila mmoja kuwa ndani ya mavazi
yalio
fanana kama sale ya siku hiyo maalumu ya
kuhitimu ambayo yaliandaliwa mahafali makubwa
chuoni hapo watu wengi walihuzulia wakiwemo
wazazi wa wanafunzi lakini wengi wao walikuwaa
ni wakutoka pale pale Rwanda,,
Victoria na david walikuwa miongoni mwa
wanafunzi ambao hawakuwa na watu wa
kuwasindikiza katika mahafali hayo, japo huzuni
ilimtawala sana kwa kuona wazazi wa wenzie
lakini Victoria alijua wajibu wake kwa david hivyo
alimliwaza kwa maneno matamu na kumwambia
kuwa yeye ndio mama yake, hivyo awe na mana
ndani ya moyo wake,
David alizidi kuonesha upendo kwa Victoria
maana
alipata faraja aliyoikosa kwa muda mrefu na kwa
wakati muafaka ambao alikuwa kwenye mawazo
mazito,
Watu walikusanyika eneo maalumu ambapo viti
vya wahitimu vilitengwa karibu na wazazi na vile
vya wanafunzi wengine viliwekwa kando kidogo
Meza kubwa iliyokuwa mbele aliweza kuwepo
mgeni rasmi ambaye ni rais wa nchi hiyo
muheshimiwa paul kagame akiwa ameambatana
na
familia yake ambao walikuwa wame kaa pembeni
kidogo,
Muongozaji shuhuri aliweza kusoma ratiba
itakayo
waongoza ili kukamilisha mahafalli hayo, taratibu
zote zilifuatwa na kabla ya mgeni rasmi
muheshimiwa paul kagame kusimamishwa
alitakiwa kusimama mwanafunzi mmoja kwa ajili
ya kuwa kilisha wengine kwa kusema kitu
ambacho kitaweza kuwasaidia huko mtaani
wanako kwenda na wale watakao baki chuoni
hapoa ili mgeni rasmi naye aweze kutoa mchango
wake katika chuo hiko kwa kuendeleza na kukuza
maendeleo ya elimu nchini Rwanda,,
Mkuu wa chuo alipelekewa majina matano ya
wanafunzi ili achague atakaye wakilisha
wanafunzi
wote chuoni hapo,kula ya mkuu wa chuo
ilidondokea kwa mtoto wa alfredi kazinge ambaye
ni david na jina hilo kutangazwa mbele ya
wanafunzi wote na muhusika alitakiwa kwenda
mbele ya hadhara ile ya watu wengi kwenda
kuzungumza mambo ya msingi,,,,,,
Waliokuwa wanasikia tu habari za david bila
kumjua muhusika walifurahi sana maana ndio
ilikuwa nafasi pekee ya wao kumuona, sauti za
makofi zilisikika kwa wingi kumkaribisha kijana
huyo mtanashati aliye pata bahati ya
kuzungumza
ili kumkaribisha rais wa nchi hiyo mheshimiwa
paul kagame,
Jambo hilo lilimfanya david kupata uwoga maana
hakujiamani kama ni yeye ndiye anaye hitajika
kwenda pale mbele ya hadhara ile kubwa japo
alikiri jina lililo tajwa ni la kwake, Victoria aliye
kuwa karibu alimshika began a kumuomba ajikaze
na kujiamani kama mwanaume aende,
Wengi walitamani wangeitwa wao lakini aliye
chaguliwa ni kijana aliyeonekana mnyonge sana
chuoni, vidole vingi vilikwenda kwa david na
minonâgono mingi kusikika,
makofi yalizidi david alipo nyanyuka na kuanza
kuelekea kule ilipo maiki ya kuongelea
ITAENDELEA
Siku kama hiyo ya jumamosi chuoni hapo kuna
kuwa na disko ndani ya ukumbi wa chuo na
baadhi
ya wanafunzi huwa wanachaguliwa kucheza
nyimbo za aina mbalimbali ilikuonesha uwezo
wao
na vipaji vyao,
Rafiki zake na victoria waliweza kugundua kuwa
victoria ameanza kumpenda david hivyo walianda
mpango na kuongea na wanachumba wenzie na
david kuwa itakapofika muda wa kucheza basi
david acheze na victoria na wengine waliobaki
watacheza na wao,
Swala hilo lilionekana jema sana kwa washikaji
zake na david maana waliona sheshe kaingia
kwenye kichaka cha simba hivyo hakuna jinsi
zaidi
ya kumlarua tu na kumla nyama, mpango huo
ulikubalika,
Mida ya saa mojamoja hivi usiku wanafunzi
walionekana kujiandaa vyema, wenye kuazima
nguo waliazima, na wenye kugongea marashi
waligongea ilimradi kila mtu aonekane maridadi
siku hiyo mbele ya wavulana na mbele ya
wasichana ndani ya ukumbi huo,
Mipango yote hiyo wakati ikiendelea david
hakuwa
na taarifa yoyote ile, yeye alijiandaa kawaida
maana hakuwa mpenzi sana wa mziki na
mipango
yake ilikuwa ni kwenda kuangalia kwa muda tu na
kumuona mtoto victoria kisha arudi zake bwenini,
sauti ile ya mziki uliokuwa unasikika ukumbini
ulianza kuwa kusanya watu eneo lile.wengi
walipendeza na nguo zao za anasa,wengine
walionesha mizuka yao kwa kucheza nje hata
kabla
ya kuingia ndani acha wale waliokuwa
wamekumbatiana kwenye giza wakiendelea na
mambo yao ya ajabu ambayo haya stahiri
kuonwa
na watoto,
yote hayo david aliyaona na kubaki kusikitika tu
na
kuendelea kuzunguka kumtafuta victoria, wakati
akiwa anashangaa ghafla alikuja msichana
mmoja
kwa nyuma ,hakika alikuwa mrembo sana,
akamshika kiuno david hali iliyomfanya ageuke
kwa
haraka sana, kitendo kile cha kugeuka haraka na
yule dada alikuwa anataka kumkumbatia basi
wakajikuta wanadondoka chini na yule dada
akiwa
juu ya david,,
watu waliwazunguka na kuanza kuwa pigia
makofi
hata wale waliokuwa mbali walitamani kutaka
kujua kuna nini eneo lile hivyo nao hawakusita
kusogelea,
umati huo uliokuwa unasogea alikuwepo na
victoria pia, ndani ya dakika chache kila mtu
aliweza kushuhudia kitendo kile na yule dada
alifurahi sana kwa tukio lile maana alikuwa
kajipatia umaarufu mkubwa kumkumbatia
mwanaume asiye kuwa na mpango na wanawake
halafu anapendwa na wengi,
david alijitahidi kumsukuma yule dada pale chini
na akafanikiwa, alinyanyuka kwa hasira na
kuanza
kuwasukuma watu wampishe ili apite andoke
zake,
alipo wamaliza ghafla mbele yake akamuona
victoria aliyekuwa anataka kuanza kulia,
kwakuwa kila mmoja alikuwa anampenda
mwenzie
hivyo nyuso zao ziliteseka kwa aibu na victoria
kuanza kukimbia eneo lile na david kumfuata kwa
nyuma, watu hawakuelewa kinachoendelea zaidi
walizidi kushangilia tu kwa kujionea filamua ya
mapenzi ya bure,
Victoria alikimbia mpaka akapotezana na david,
hivyo david akawa anazidi kumtafuta maeneo
yote
yale ya chuo lakini hakumuona kwa muda huo
Hasira za victoria zilimpeleka mpaka kwenye stoo
ya chuo ambayo ilikuwa na kiza na kuanza kulia,
alijilaumua sana kwa kuchelewa kumwambia hisia
zake mwanaume aliye mpenda kwa muda mfupi
na
akiwa ndani ya maumivu alilia sana huku
akiendelea kufikiria na maneno ya upweke
yakamtoka,,,,
âânani ambaye atauokoa moyo wangu kwenye
mafuriko haya ya machozi eeh jaman nimechoka
kuwa mtumwa wa kumtumikia bwana maumivu,
nani aje kuwa mkombozi wangu na kunifariji kwa
kipindi hiki kigumu eeh?
Victoria alijuta kuwa na moyo wa upendo kwa
kuwa ulikosa mtu wa kuutunza, machozi hayo
alimkumbuka mtu aliye kuwa na ahadi naye ya
kukutana, na aliya kumbuka maneno matamu
aliyokuwa anatumiwa hivyo alihisi moyo wake
unaweza kupata faraja kupitia mtu huyo bila ya
kujua mtu mwenyewe ni david aliyempenda bila
kumwambia pia ndiye aliye mfanya yeye kuwa
mahali hapo ambapo si salama kwa usiku huo,
Victoria hakuwa na budi kuanza kulitafuta jina la
mtu huyo kwa jinsi alivyo liweka yeye ili ampigie
waonane, wakati anaendelea kulitafuta kumbe
david alikuwa amekaribia maeneo hayo ya stoo
na
alishtushwa na mwanga wa simu uliokuwa
unaonekana kule stoo na hisia zikaja huenda
atakuwa victoria hivyo ikabidi aufuate ili awe na
uhakika kama kweli ni victoria,
David hakuchukua muda mpaka kufika kwenye
mlango wa stoo na alianza kuchungulia mle ndani
na kugundua kuwa yule ni victoria kwa kusaidiwa
na ule mwanga wa simu uliokuwa unammulika
mrembo huyo ambaye david mwanzo alimuita
Qeen
tz,
kabla victoria hajalipata jina la mtu anayetaka
kuonana nae ghafla rafiki yake akamtumia ujumbe
ulikuwa unamuuliza,
âuko wapiâ?
victoria alisonya na kuendelea kutafuta jina la
mtu
wake bila kujibu ujumbe huo ndipo rafiki yake
huyo
akaamua kumpigia na wimbo uliokuwa unaita ni
huu,,,,,,,
âIâm so lonely broken angelâ
âIâm so lonely,listen to my heartâ
âone and only broken angelâ
âcome and save me, before I fall apartâ
Victoria pia hakuweza kupokea hata hiyo simu
mpaka nyimbo hiyo iliyoendana na upweke
alionao
ma iliyomuongezea machozi ilipo kata yenyewe,
David aliusikia wimbo huo pale nje na kilio cha
mtoto mzuri victoria ndipo alipojitokeza na
maneno
matamu ya mahaba yalitoka kwa sauti inayo
sisitiza upendo,,,,,
âniko hapa kukutoa upweke ulionaoâ
Sauti hiyo iliushtua sana moyo wa Victoria
alitamani kumjua huyo mtu aliye ingia humo
ndani
japo alihiisi kama sauti anaifahamu vile, ndipo
alipommulika usoni kwa kutumia mwanga wa
simu
na kugundua kuwa ni david,
Mdomo wenye ulimi mzuri ndani yake na
uliojaaliwa kutamka maneno mazuri ya upendo
ulitaka kusema kitu lakini ulipingwa na sauti iliyo
shiba ya shababi david kwa kauli yenye kusisitiza
mahaba,,,,,,
âVictoria moyo wako unaweza kutoka kwenye
mafuriko ya machozi kama utaruhusu kuliachia
tabasamu ulilolificha kwa muda mrefu kwa mtu
unaye mpenda na kuhisi kuwa anaweza kuwa
baharia wako atakaye kufikisha nchi ya furaha
yenye upepo na kijua cha mapendo ya dhati na
kuepukana na visamaki pamoja na vichura
vidogovidogo vilivyokuja na tamaa ya maji
ambavyo kiangazi ikifika havionekaniâ
âWengi watakuhitaji kwa muda mfupi lakini ni
kwasababu ya kutaka kutimiza kiu yao ya uzinzi
tu
ila mimi david niko hapa kwa ajili ya kutaka
kulinda uzuri wako usipotee na kuharibiwa na
watu
wasio jua thaman yako fikiria leo nafuta chozi
lako
kwa maneno ya dhati toka moyoni mwangu
ambayo sijawahi kumueleza mwanamke yoyote
yule katika ulimwengu huu lakini kwako
yameweza
kutoka tena bila hata ya kujali ile namba ya siri
ambayo kwa mwanaume mwenye kujielewa ni
lazima ndio aifanye kuwa funguo ya moyo si
nyingine ni tabia pekee,, hilo kwangu sikujali
tafadhali naomba upokee maombi haya ambayo
tayari yamesha pitigwa saini ya upendoâ
Victoria alizidi kuweweseka manaa hakuamini
kama angeweza kukutana na mwanaume aliye
mpenda kwa dhati katika mazingira hayo, kicheko
cha furaha kilicho changanyika na aibu kiliendelea
kumtesa moyoni mwake, miguu yake ikawa na
kazi
ya kuchimbachimba chini huku vidole vyake vya
mkono wa kulia akivinyonya kama mtoto mdogo
aliye kuwa na hamu ya ziwa la mama yake,
aliinua
uso wake uliokuwa unangâa hata kama kulikuwa
na
kiza na kumrembulia jicho david, jecho lenye kope
za asili na majimaji ndani yake ambayo yalizidi
kumfanya david kujipa asilimia 99% za kumpata
Victoria,
Miguu yao ilionekana kupiga hatua ndogo ndogo
wakisogeleana kwa hisia mpaka ku kawa na
umbali wenye mita sifuri(zero distance) na
kilichoendelea hakisimuliki,
Ndani ya muda wa kama saa moja na nusu hivi
walionekana wakitoka kwenye chumba hicho
kilichokuwa na kiza huku nyuso zao zikiwa na
furaha,
Victoria kila walipo kuwa wana tembea umbali wa
hatua tano lazima aegemee kifua cha david huku
akiachia kicheko ambacho kilimfanya david
atabasamu na kumuachia busu la msisimko
shavuni mwake,
Kutembea kwao pamoja walivutia wengi ambao
walikodoa mi macho kuwa tizama na kutaka
kuhakikisha kama yule ni david au siye, wakawa
na
kazi ya kutaniana tu na kukimbizana kwenye
viunga vya maua chuoni hapo hata habari ya
disko
wakawa wamesahau kabisa,
Moyo wa david ukawa umeingiwa na furaha ya
ajabu ambayo hakuwahi kuipata kwenye maisha
yake lakini Victoria mwanamke wa kwanza
ameweza kuibadilisha akili ya david na
kumuingiza
sehemu ambayo wengi wana lia,
Rafiki zake na Victoria waliokuwa wana mtafuta
walibaki midomo wazi walipo wakuta pamoja
wamekumbatiana huku wakiwa wameegemea mti,
kila mmoja wao alionekana kufurahia mahusiano
yao kwa kuwa waliendana sana.
Siku nyingi zilikatika na habari zili sambaa chuoni
hapo juu ya watu hao wawili kuwa katika
mahusiano ya kimapenzi, waliokuwa
wanampenda
Victoria waliumia kwa kumkosa hata yule
Emmanuely regan aliye mtenda alianza kuona
wivu
jinsi watu walivyo kuwa wana wasifia kwa
kuendana kwako,
Wasichana wengi nao walijitahidi kutaka kutoa
kasoro za Victoria kwa kuwa walikuwa
wanampenda david lakini jitihada zao ziligonga
mwamba kwa wawili hao kushikamana kupita
kiasi,
****************************************
Miaka minne ya david kukaa chuoni ikawa
imewadia ni baada ya kumaliza mtihani wao wa
mwisho na kila mmoja kuwa ndani ya mavazi
yalio
fanana kama sale ya siku hiyo maalumu ya
kuhitimu ambayo yaliandaliwa mahafali makubwa
chuoni hapo watu wengi walihuzulia wakiwemo
wazazi wa wanafunzi lakini wengi wao walikuwaa
ni wakutoka pale pale Rwanda,,
Victoria na david walikuwa miongoni mwa
wanafunzi ambao hawakuwa na watu wa
kuwasindikiza katika mahafali hayo, japo huzuni
ilimtawala sana kwa kuona wazazi wa wenzie
lakini Victoria alijua wajibu wake kwa david hivyo
alimliwaza kwa maneno matamu na kumwambia
kuwa yeye ndio mama yake, hivyo awe na mana
ndani ya moyo wake,
David alizidi kuonesha upendo kwa Victoria
maana
alipata faraja aliyoikosa kwa muda mrefu na kwa
wakati muafaka ambao alikuwa kwenye mawazo
mazito,
Watu walikusanyika eneo maalumu ambapo viti
vya wahitimu vilitengwa karibu na wazazi na vile
vya wanafunzi wengine viliwekwa kando kidogo
Meza kubwa iliyokuwa mbele aliweza kuwepo
mgeni rasmi ambaye ni rais wa nchi hiyo
muheshimiwa paul kagame akiwa ameambatana
na
familia yake ambao walikuwa wame kaa pembeni
kidogo,
Muongozaji shuhuri aliweza kusoma ratiba
itakayo
waongoza ili kukamilisha mahafalli hayo, taratibu
zote zilifuatwa na kabla ya mgeni rasmi
muheshimiwa paul kagame kusimamishwa
alitakiwa kusimama mwanafunzi mmoja kwa ajili
ya kuwa kilisha wengine kwa kusema kitu
ambacho kitaweza kuwasaidia huko mtaani
wanako kwenda na wale watakao baki chuoni
hapoa ili mgeni rasmi naye aweze kutoa mchango
wake katika chuo hiko kwa kuendeleza na kukuza
maendeleo ya elimu nchini Rwanda,,
Mkuu wa chuo alipelekewa majina matano ya
wanafunzi ili achague atakaye wakilisha
wanafunzi
wote chuoni hapo,kula ya mkuu wa chuo
ilidondokea kwa mtoto wa alfredi kazinge ambaye
ni david na jina hilo kutangazwa mbele ya
wanafunzi wote na muhusika alitakiwa kwenda
mbele ya hadhara ile ya watu wengi kwenda
kuzungumza mambo ya msingi,,,,,,
Waliokuwa wanasikia tu habari za david bila
kumjua muhusika walifurahi sana maana ndio
ilikuwa nafasi pekee ya wao kumuona, sauti za
makofi zilisikika kwa wingi kumkaribisha kijana
huyo mtanashati aliye pata bahati ya
kuzungumza
ili kumkaribisha rais wa nchi hiyo mheshimiwa
paul kagame,
Jambo hilo lilimfanya david kupata uwoga maana
hakujiamani kama ni yeye ndiye anaye hitajika
kwenda pale mbele ya hadhara ile kubwa japo
alikiri jina lililo tajwa ni la kwake, Victoria aliye
kuwa karibu alimshika began a kumuomba ajikaze
na kujiamani kama mwanaume aende,
Wengi walitamani wangeitwa wao lakini aliye
chaguliwa ni kijana aliyeonekana mnyonge sana
chuoni, vidole vingi vilikwenda kwa david na
minonâgono mingi kusikika,
makofi yalizidi david alipo nyanyuka na kuanza
kuelekea kule ilipo maiki ya kuongelea
ITAENDELEA