RIWAYA: Ripoti kamili

RIWAYA: Ripoti kamili

Mzaramo tuletee ripoti kamili achana na hao wanafiki wenye roho mbaya wanaojifanya wanajua kila kitu
 
hivi hao wajuaji kinacho wauma hasa kitu gani? Kama kaileta hapa ww nn kinakukera kama si nye**e zinawasumbua. mijitu mingine inakera mpaka basi mione misikio imewasima kama side mirror
 
Umeona yy hajaendelea mpaka sasa kwan hajui kama si yake? Na anajua kabisa plagiarism adhabu yake ni nn? Angekuwa kua chuo tayar ashadisco huyu!!! Edit pale juu kama mwandishi ni flani na siyo kujiweka ww ndiyo mwandishi wakati hata ujanja huo wa kufikili hauna!!
umevurugwa wewe na hapa tunaendelea kama kawa
 
WATU hujiaminisha kuwa siku hizi hakuna mapenzi ya kweli na hata ukiwauliza mapenzi ya kweli yalikuwepo lini hawana jibu!! Zaidi watasema enzi za wazee wetu... kana kwamba waliishi enzi hizo na kushuhudia haya!!
Tafadhali usiwasikilize hawa, kwa sababu maneno yao ni yale maneno ya wakosaji... penzi la kweli chanzo chake ni wewe.. amua sasa kuzalisha penzi la kweli... usiishi kwa kufuata maneno ya watu.

NA HII NI SEHEMU YA KUMI NA SITA.

Looh! Macho yakanitoka gizani, licha ya mabadiliko yote makubwa katika mwili wa mtukanaji yule bado sura yake haikuweza kuyapotea macho yangu.
Alikuwa ni Tina!
Tina mke wangu, aliyepotea katika uso wangu miezi mingi sana iliyopita tena katika mazingira ya kutatanisha.......
Midomo ilijifumba kila nilipojaribu kuifunua, miguu iligoma kupiga hatua yoyote ile mbele.
Nilikuwa nimepagawa!!!

Nilidhani akifika na kunibaini sura yangu labda naye atapagawa na kuzizima kama mimi lakini ajabu aliniona na ni kama ambaye hakukumbuka lolote, hapo kweli nikakiri kuwa pombe si rafiki mzuri sana hasahasa kama utamuendekeza, Tina niliyekuwa namjua mimi ni yule Tina aliyenikanya juu ya matumizi ya vitu visivyokuwa vya msingi... akaniachisha sigara niliyoizoea, akaniweka katika mstari ulionyooka. Akaapa kuwa kamwe hatakuja kuwa na urafiki na pombe kwa sababu ilimsababishia umaskini mkubwa ulioambatana na fedheha baba yake!! Nami akanisihi nisije nikaingia katika mkumbo huo.
Leo hii namshuhudia Tina yuleyule akiwa amelewa chakari, afya yake imezorota sana.
“Tina!” nilijaribu kumuita.
“Nd’o jina langu unasemaje na wewe hanisi!!” alinibwatukia huku akikishika kiuno chake kana kwamba hapo awali tulikuwa tumegombana.
Alipomaliza kunibwatukia akamgeukia dada yake.
“sasa wewe nawe ushapewa huo ulemavu bado tu unataka wanaume.. hivi ungekuwa mzima si ungetembea na kila rika wewe..... dada uwe unaona aibu wakati mwingine”
Zawadi aliinama chini kwa aibu huku akitikisa kichwa, bila shaka aliamini kuwa Tina anazungumza jambo asilolijua hata kidogo.
Baada ya hapo akanyanyua kichwa.
“Kaka Mjuni, mzoee tu huyu mdogo wangu.... hajui alitendalo.” Alinieleza kwa sauti ya kinyonge kabisa.
Tina akaingilia kati akawa kama mbogo mwenye ghadhabu anatokwa na matusi makali ya nguoni ajabu hakuna aliyejali, bila shaka walikuwa wamemzoea tayari. Majirani walipita na kuendelea na shughuli zao bila kushangaa.
Nilimsogelea Tina huku nikishindwa kuamini eti kwa miezi hiyo michache alikuwa amenisahau... au ni mimi nilikuwa nimemfananisha!! Nilijiuliza huku nikizidi kumkaribia.
“Vipi kaka, unahamia kwangu ushamalizana na huyo mwenzako au? Naona unataka kula kuku na mayai yake!!” alinihoji.
“Tina mimi ni Mujuni... Mujuni Kalisti.....” nilijitambulisha huku nikimkazia macho yangu.
“Namfahamu Mjuni mmoja tu.... kuna Mjuni mmoja katika duniani nzima.. wewe labda fotokopi... ehee sawa Mjuni fotokopi nieleze unataka nini?” alinihoji kilevilevi.....
“Ni mimi huyo Mjuni unayemfahamu........” nilimsihi na sasa nilimfikia na kumshika mkono wake.
Nikautazama ule mkono huku akijaribu kuutoa kwa nguvu, hapo sasa akaanza kulalamika kuwa mimi ni polisi nimekuja kumpeleleza..... sikumuachia badala yake nilikifikia kile kidole ambacho nilimvisha pete siku ya harusi yetu ya kimila.
La!haula... ile pete ilikuwa palepale katika kidole kile. Ile kuigusa ile pete nikapatwa na mguso wa aina yake katika moyo wangu!!
“Ni mimi niliyekuvalisha pete hii... hakuna mwingine zaidi yangu...” nilimsihi... sasa Zawadi dadake alikuwa amepigwa na butwaa hakudhani hata kidogo kuwa tunaweza kuwa tunafahamiana.
“Niache wewe mwanaume, niache wewe ni mzimu.... mzimu jamanii mzimuuu nisaidieni..” alipiga mayowe huku akilazimisha nimuachie. Sasa majirani walianza kututazama kwa makini wakijongea eneo lile.
Hapo nikakumbuka jambo moja la mwisho ambalo nilihisi linaweza kusaidia kwa kiasi fulani. Niliukumbuka wimbo fulani wa kizazi kipya ulioimbwa na msanii aitwaye Dito unaoitwa Tushukuru kwa yote. Wimbo huu Tina aliyekuwa kama mimi tu ambao hatukuwa wapenzi wa nyimbo hizo lakini huu alikuwa akiupenda sana na ni yeye pia alinishawishi mimi kuupenda wimbo ule. Niliupenda sio tu kwa sababu Tina aliupenda bali niliupenda kwa sababu kila mstari ulikuwa na maana kubwa katika penzi letu... ni wimbo uliokuwa unatia moyo, unaimarisha penzi na pia kuamsha hisia thabiti......
Nilijikohoza kidogo na kisha nikayafumba macho yangu na kuhamia duniani yangu pekee dunia ambayo nilijiona ninaishi mimi na Tina tu hakuna aliyekuwa anatutazama. Na hapo nikaanza kuimba kama nilivyozoea kumuimbia.

“Kwa pamoja tutazame hapa tulipo
Anatuonyesha picha ya mbali huko tuendapo
Mengi utasikia yakisemwa usiweke moyoni
Kuteleza inatokea mambo ya ndani usiyalete hadharani
Kama ndege njoo turuke angani woote
Nikushike unishike ili tuwe woote!
Mvua ikinyesha iwe Baraka ya penzi letu
LOLOTE LIKITOKEA BASI TUANGUKE NA TUFE WOTE”


Nilimuimbia kipande hicho ambacho na yeye alikuwa akiniimbia mara kwa mara hasahasa nikiwa nimekwazika.....
Naam! Hakuna kitu kinaleta kumbukumbu na hisia kali kama nyimbo, msisimko uliompata Tina ulionekana dhahiri baada ya kuwa nimefumbua macho.
Tina sasa hakuwa na papara tena bali alilegea na kisha akaangukia magoti, na hapo alianza kuangua kilio kikubwa, sio kilio kwa sababu ya kuongozwa na pombe bali alikuwa akiumizwa na uwepo wangu pale. Alikuwa amekumbuka mbali Tina wangu!!
Alinisihi sana niondoke na akiamka pale aichukulie kama ndoto tu, alizungumza mengi sana ya kujutia hakika alisikitisha sana, hata kama una moyo mgumu lazima huruma ingechukua nafasi.
Nilibaki kimya nikimsikiliza tu.... huu ulikuwa usiku wa aina yake... sasa watu walianza kujaa na hakuona aibu yoyote ile kuendelea kuzungumza......
Alinieleza kuwa Mungu aliye hai anamuadhibu, sasa hana mbele wala nyuma yupoyupo tu... na alikiri kuwa anaamini kwa zaidi ya asilimia sabini atakuwa ameathirika.
“Ni heri nife kwa UKIMWI ili adhabu ikamilike, mimi si mwenye haki hata kidogo Mjuni, mimi ni wa kufa tu na ninastahili yote haya ninayopitia...” alizungumza Tina kwa uchungu mkubwa. Na hapo dada mtu hakuwa na swali, alikuwa ameanza kuupata mwanga.
Nilimsihi Tina asiendelee kuzungumza mbele ya watu na nikamuomba niondoke naye.
“Hapana Mjuni... hapana utaniua mjuni.....” alikataa. Nikamsihi kuwa mimi ni yuleyule na kamwe sijawahi kubadilika hivyo aniamini.
“Maneno yako yataniua mjuni..... yataniua.... niache tu nife kwa UKIMWI!!” alizidi kusihi.
Niliona nizungumze naye tena kidogo huenda atanielewa.
“Tina, hata mimi nimewahi kufanya makosa mengi sana na nikasamehewa.. hakuna mwanadamu ambaye hajawahi kufanya kosa... wewe ni nani hadi ujipe adhabu kubwa hivi....” nilimuhoji.
“Mjuni.... mimi ni mchafu, changudoa, mlevi, sina utu hata kidogo... yule Tina uliyemuoa akakuonyesha mapenzi si huyu wa sasa huyu ni shetani. Niache Mjuni na uende zako.... niliyokufanyia yanatosha....” alinijibu huku akilia......
Kilio cha Tina kiliniumiza sana kwa sababu alikuwa analia akimaanisha na ni kama alikuwa anayeombea nyakati zirejee nyuma. Na haikuwezekana......
Ndugu msikilizaji, ni kweli sikuwa na hisia za kimapenzi na Tina lakini kwa mwanamke niliyeanza naye maisha kuanzia chini, tukapanda hadi juu upendo ule wa kawaida tu usingeweza kufutika. Na hasahasa nilivyomtazama katika hali aliyokuwanayo basi ulikuwa wakati ambao alikuwa ananihitaji zaidi.
Nikaendelea kumsihi aongozane nami na hatimaye akakubali, nikachukua ruhusa kwa dada yake na kumuahidi kuwa siku inayofuata nitarejea nikiwa pamoja na Tina.
Wakati huo swali kuu lililokuwa linanisumbua ni juu ya Sonia... yupo wapi mtoto yule niliyempenda na swali jingine lilikuwa juu ya sarafina nilitaka kujua ni lini alimzaa mtoto yule na ni nani baba yake!!!

***Naam! Ndugu msikilizaji je? Ndo Ripoti inafikia ukingoni au ndo kwanza inanoga...ni nini hatma ya wawili hawa......

UKWELI HUMWEKA MTU HURU WAHENGA WALISEMA, lakini yapo mazingira ambayo ukiutanguliza ukweli basi unakuwa mwanzo wa kuwa mtumwa...... na ukiuficha huo ukweli unakuangamiza kabisa. Je kipi bora kuwa mtumwa ama kuangamia......
 
Nikaendelea kumsihi aongozane nami na hatimaye akakubali, nikachukua ruhusa kwa dada yake na kumuahidi kuwa siku inayofuata nitarejea nikiwa pamoja na Tina.
Wakati huo swali kuu lililokuwa linanisumbua ni juu ya Sonia... yupo wapi mtoto yule niliyempenda na swali jingine lilikuwa juu ya sarafina nilitaka kujua ni lini alimzaa mtoto yule na ni nani baba yake!!!
Sikuona kama ni jambo la busara sana kumpeleka Tina nyumbani kwangu, kwanza mchana ule sikuwa nimeenda makaburini kumsindikiza Freddy aliyekuwa ametutoka baada ya kujinyonga hivyo kuonekana na mwanamke pale ningeweza kuleta tafsiri nyingi sana mbayambaya machoni kwa wapangaji wenzake, na jambo la pili ambalo nililihofia lilikuwa juu ya kukosa uhuru sana. Kama marehemu Freddy na mkewe walipokuwa wanagombana kila mtu aliweza kusikia vipi kuhusu mimi kuzungumza na Tina. Sikutaka jambo hili liwe matangazo kwa kila mtu...
Nikaamua kumchukua Tina hadi katika nyumba ya kulala wageni yenye hadhi ya wastani.
Ndani ya kile chumba baada ya Tina kurejea katika hali yake ya kawaida alianza kuzungumza na kunisihi sana nisimuulize maswali na badala yake nimsikilize tu huenda mazungumzo yake yanaweza kutatua maswali yangu.
Na kweli Tina alianzia pale palipokuwa pananitatiza...
Akanikumbusha mara kadhaa alivyokuwa anaweweseka usiku enzi za raha katika ndo yetu, akanikumbusha pia jina alilokuwa akilitaja mara kwa mara hadi nikafikia hatua ya kumuuliza hilo jina ni la nani...
Aliposema hivi nikakumbuka kuwa alikuwa akiota sana jina la Sarafina!!
Hapa sasa nikaanza kuupata mwanga huku nikipata pia cha kuongeza katika Ripoti yangu.
Kumbe nilimuoa Tina akiwa tayari yu na mtoto mkubwa tu. Na kuhusu huyo mtoto ambaye ni Sarafina alijazwa mimba na mwanaume tapeli wa mapenzi aliyemdanganya kuwa akimzalia atamuoa. Ile kubeba mimba na mambo yakabadilika, mwanaume akawa haeleweki mara leo aseme hivi na kesho anabadilika kama kinyonge. Hadi unafika wakati wa kwenda hospitali kujifungua bado alikuwa hana msimamo, baada ya kujifungua maisha yakawa magumu sana na mwanaume akiwa haonekani mara kwa mara.
Tina akawahi sana kumwachisha titi sarafina ili aweze kuingia mtaani kupambana kumtafutia chakula, na hapo ndipo akaanza kumuacha mikononi mwa dada yake ambaye ni mlemavu.
Tina alifuta machozi kidogo kisha akaendelea kusema kuwa kutendwa vile na yule mzazi mwenzake haikuwa sababu kubwa sana ya kuwachukia wanaume na hata hapo anapozungumza hajawahi kuwa na chuki na wanaume wote kwa sababu anaamini wazi kuwa wapo wanaume wanao upendo wa dhati kabisa.
Maisha yalivyozidi kumpiga ndipo kama bahati akakutana na mwanaume wake wa kwanza kabisa aliyemtoa usichana wake. Alikuwa amechakaa vibaya sanaalipokutana na mwanaume huyu... na hapa akajikuta akiingia penzini angali mwanaye alikuwa mdogo sana.
Tina anakiri wazi kuwa alifahamu kuwa anafanya makosa lakini tatizo ni kwamba alikuwa muhitaji zaidi.
Hapo nikamuingilia kati na kumuuliza wazazi wake walilichukuliaje jambo hili na kwa nini hakuwaomba msaada.
Tina akatabasamu na kisha akaanza kujitukana yeye kisha akawatukana na wasichana wote wanaofanana na yeye katika jambo hilo la kudanganyika. Akaelezea kuwa aliibeba ile mimba nje ya matakwa ya wazazi wake ambao walimuapia kuwa iwapo atabeba mimba nje ya ndoa basi watampa laana, hivyo alipoibeba mimba hii alijidanganya kuwa wataoana upesi na yule mwanaume hivyo hata wazazi hawatajua kama alikuwa na mimba kabla ya ndoa. Na hata wakijua atakuwa ameolewa tayari haitakuwa na uzito...
Baada ya bwana yulekuikataa mimba ile basi ikabidi hata wazazi wasijue. Dada yake mlemavu wa miguu akamsaidia kuitunza siri....
Akashusha pumzi zake kishaakaendelea......
“Huyo mwanaume kweli alinifaa sana katika kipindi kile kigumu, na kwa sababu alikuwa mwanaume wangu wa kwanza sikuwa na mashaka naye na ninakiri kweli nilimpenda na nilitamani sana anioe.... hata yeye sikumueleza iwapo nibna mtoto tayari,nilikuwa najisikia vibaya sana kumkana Sarafina wangu kwa wanaume lakini nililazimika kufanya vile kwa sababu baadhi ya wanaume wakisikia una mtoto hata mpango waliopanga juu yako unaisha...” akasita Tina akanitazama na kuniita jina langu nikaitika.
“Bila shaka umemjua tayari baba yake Sarafina... nikikueleza kuwa mimi ni mchafu sana kwa maneno matupu hauwezi kunielewa lakini jaribu kufikiri mtoto wa kwanza haya huyo sawa utasema nilimpata kabla sijaolewa na wewe haya na huyu wa pili naye nikampata kwa ujinga ujinga tu.....” alisonya kisha akavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.
Tina aliendelea kusimulia hadi akafikia kwenye lile tukio ambalo nilikuwa nalihitaji sana, nilitaka kufahamu baada ya kutoroka nyumbani akiwa pamoja na Sonia ni wapi alielekea na ni wapi yupo Sonia.
“Niliyopitia ni mengi sana Mjuni nakusihi usiklize tu kwa sababu hata nisipoyasema ndo tayari yametokea na hayawezi kubadilishwa!!” alitoa kauli ile na kunifanya nibaki njia panda nikijiuliza ni kitu gani kilitokea huko nyuma. Wakati najiuliza haya nilikuwa pia najiuliza nitahimili vipi kupokea taarifa eti kuna namnanamna zilijitokeza Sonia akaaga dunia.
Nilikuwa nampenda sana mtoto yule.
“Sonia yupo wapi Tina?” uvumilivu ulinishinda nikajikuta nauliza....
Sonia badala ya kujibu alinitazama sana machoni moja kwa moja, kisha akainama na kuinuka tena......
“Mjuni Kalisti...” akaniita jina langu kikamilifu.....
Nikajikakamua na kuitika....
“Wewe ni mwanaume wa kipekee...” alisema huku akilazimisha kutabasamu.
“Tina tafadhali nieleze kuhusuSonia kwanza tafadhali nieleze.....” nilimsihi na hapo wasiwasi ukizidi kuchukua nafasi katika moyo wangu.....
“Nitaeleza kila kitu bila kuacha neno lolote Mjuni ninachoomba ni usikivu wako tu......”
Kauli hizi za Tina ziliendelea kunitafuta vibaya mno.........

**ehee! Ni kitu gani kilimtokea Tina na Sonia kuanzia alipotoroka hadi alipo hivi sasa?
Usiikose sehemu inayofuata... itakupa baadhi ya majibu......

MAISHA ni darasa lenye somo jipya kila siku. Wewe ni mwanafunzi katika darasa hili, ombea sana kila kukicha kuwa usije kuwa mfano kwa wanafunzi wenzako kujifunzia..... na inapotokea moja kati yenu anakuwa mfano jitahidi sana kuufanyia kazi mfano huo.
Kuna mengi sana huwatokea wanadamu wenzetu ambayo ni sawasawa na darasa la bure kabisa kwetu lakini wanadamu hufunga macho yao ili wasione na masikio yao ili wasisikie kisha kesho yake wanafanya kosa alilofanya fulani na kuambulia majuto....
 
Baada ya mimi kuamua kutulia na kumweleza Tina kuwa sitaingilia akizungumza ni hapo alianza kuelezea lile tukio la usiku ule mnene.
Haikuwa mpango wake lakini majuto yalimuongoza kufanya kile alichokifanya, kunyata usiku mnene wakati mimi nimelala hoi nikiwa nakoroma akamchukua mtoto wake nanguo chache za mtoto pamoja na zake, akaichukua pochi yake iliyokuwa na akiba kiasi ya pesa na hapo akanitazama nikiwa nimelala usingizi akanipungia mkono huku akinitupia busu la hewani kisha akaondoka zake dhamira ikiwa inamsuta kabisa kuwa halitakuwa jambo la heri hata kidogo kuendelea kuishi na kunitazama usoni wakati amenitendea mambo mengio mabaya,.
Safari yake hii haikumuhusisha mtu mwingine zaidi ya yeye kuwa mratibu wa kila kitu, alipoutoa mguu wake nje alijenga chuki rasmi dhidi ya wanaume wengi. Historia yake ilimuonyesha jinsi wanaume walivyosaidia kuyaharibu maisha yake, huku wawili kati yao wakimuachia kumbukumbu ya maisha yote. Walimzalisha watoto.....
Mtoto wa kwanza akitelekezwa huku huyu wa pili akiiharibu ndo kati yake na mtu aliyempenda yaani mimi Mjuni.
Tina akajiondokea kinyongea hadi kituo cha mabasi akapanda basi linaloelekea wilaya ya Kilindi huko Tanga.
Huko alikuwa anaishi rafiki yake wa kibiashara waliyefahamiana wakati ule anafanya biashara ya kuuza nguo.... ni huyu ambaye alimweleza kuwa anahitaji ampokee huko, japokuwa hakumueleza ni jambo gani linampeleka huko.
Ilikuwa safari ndefu sana iliyogubikwa na wimbi kubwa la mawazo kichwani mwa Tina, yote yaliyotokea alikuwa hajayasahau na yalikuwa yanamsulubu.
Alifika Kilindi na kupokelewa na huyo rafiki yake, hakumueleza kiundani sana yaliyojiri lakini alimueleza kuwa anaomba apumzike walau kwa siku kumi kisha atapata uelekeo mwingine.
Rafiki yule hakuwa na hiyana akamuhifadhi Tina, lakini siku mbili tu zilitosha kufahamu fika kuwa baridi kali kupitiliza katika wilaya ya Kilindi lilikuwa ni tatizo kwa mtoto Sonia.
Kifua kilianza kumbana mara ikawa kikohozi na akawa anashindwa kupumua vyema.
Wataalamu wa afya wakamshauri Tina amwondoa mtoto upesi katika wilaya hiyo kwani hali ile ya hewa ni hatari kabisa kwa usalama wake.
Wakati huo Tina hana pesa na rafiki yake yule alikuwa amesafiri kibiashara. Alijaribu kuwasiliana naye kwa njia ya simu na kumuo9mba msaada wa upesi lakini rafiki hakuwa akipatikana kwenye simu na pale nyumbani alikuwa amebaki na msichana wa kazi tu.
Tina angefanya nini angali alikuwa mgeni katika mji huo??
Alilazimika kuendelea kusubiri, lakini ukaja usiku ule ambao Sonia alizidiwa sana. Alikuwa anatetemeka sana na alionekana dhahiri kuwa hawezi kupumua vyema... haya yalitokea majira ya saa nne usiku.
Tina hana pesa, hana mtu amjuaye pale na rafiki hapatikani kwenye simu... msaidizi wa kazi hakuachiwa pesa ya kutosha zaidi ya shilingi elfu tano tu ya dharula kwa sababu ndani kila kitu cha kupika kilikuwepo.
Elfu tano ingesaidia kitu gani......
Hakiuweza kufaa kitu...
Mzazi hawezi kukubali kumtazama mtoto wake akiteseka atajaribu kufanya kila kitu ili kuweza kuitafuta nafuu ya mtoto....
Tuina akaona suluhu ni kuwasha jiko la mkaa ilimradi tu kulitafuta joto kiasi...
Unaweza ukawa umeishi mikoa na wilaya nyingi zenye kusifika kwa baridi... lakini kama haujaishi Kilindi.. huko kuna baridi haswa!!!
Kweli jiko likawashwa, na joto likapatikana walau. Na kitoto kikapunguza kutetemeka... sasa hata kutabasamu kilitabasamu...
Tina akapata tumaini jipya akaendelea kumbembeleza mtoto hadi akalala.
Tina akaingia katika dimbwi la mawazo, aliwaza siku za usoni za mtoto yule zitakuwaje na yeye pia akajiuliza baada ya siku kumi alizoomba ni wapi ataipeleka aibu yake??
Mawazo haya yakamtesa sana Tina hata akajikuta anasinzia bila kujua alisinzia saa ngapi......
Majira ya saa sita usiku alikuja kugutuka kutoka usingizini huku akipigania pumzi zake, alihema juu juu sana......na hakujua ni kitu gani kilisababisha hali hii.
Alipoipata nafuu akarejea kukinyanyua kitoto chake....
Naam! Hapa ikatokea taswira inayoumiza isiyofaa kusimuliwa mara kwa mara, Sonia alikuwa amekauka kau kama kipande cha mti mkavu.... alikuwa wa baridi kabisa....
Sonia hakuwa na uhai!!
Lile jiko waliloliacha linawaka liliendelea kuitumia hewa ya oksijeni ambayo Sonia na mama yake pia walikuwa wanaivuta usiku ule.
Tafadhali mpenzi msikilizaji wa mkasa huu, kamwe usije kuthubutu kulala na jiko la mkaa ndani na likiwa limewashwa... mkaa unatumia hewa ya oksijeni kuendelea kuwaka na wewe unatumia hewa ya oksijeni ili uendelee kuishi.....
Vita kati ya jiko la mkaa na mwili wa mwanadamu siku zote jiko la mkaa hushinda na mwanadamu huambulia mauti!!!



Asalaale! Tina akawa ameuchoma na kuupondaponda moyo wangu, kwani kati ya kila kitu nilichotaka kusikia kutoka kwake basi kimojawapo ni juu ya Sonia kupoteza uhai... sikuwa tayari kabisa kwa jambo hili hata kidogo. Lakini sasa Tina alikuwa amenieleza kuwa Sonia hakuwa anaishi tena alikuwa mfu!!!
Nilitaka kusema neno lakini ningesema neno gani la kubadili ukweli huu... sikuwa na neno lolote lile la kusema.
Nikabaki kulia kama mtoto mdogo, Tina akafika na kunikumbatia mabega yangu na kisha akaniomba sana msamaha...
“Kwa hiyo Sonia mlimzika wapi? “ nilimuuliza Tina kwa utulivu huku nikiyafuta machozi yangu.
Tinaakazishusha pumzi zake kwa nguvu na kisha akaendelea kunisimulia....

USIKU ule ulikuwa mrefu sana kwake aliomboleza sana kifo cha mtoto wake, msaidizi wa kazi aliamka na kusaidia kuomboleza na hatimaye majirani kadhaa walifika katika tukio hili lakini hawakuwa wakaaji sana walipita kutoa pole kisha wakamuacha Tina na maiti yake.
Hali hii ilimuonyesha Tina waziwazikuwa huu mzigo wote ulikuwa wake...
Alipoteza fahamu na kuja kustuka alfajiri akiwa bado yu na mwili wa mtoto wake alianza upya kumuita Sonia ili aamke na kumkumbatia lakini haikuwa kama alivyotaka iwe...
Majira ya saa nne rafiki yake alifika kutoka katika safari yake ya kibiashara.... alimweleza Tina kuwa akiwa safarini alipoteza simu hivyo hakuweza kufanya mawasiliano ya aina yoyote ile.
Akamtia sana moyo na kishaakashauri kuwa siku hiyohiyo Sonia apumzishwe kaburini!!
Tina alikataa kata kata na bila shaka alikataa kwa sababu aliamini labda Sonia ataamka baadaye.....
Katika purukushani za hapa na pale Tina alipoteza fahamu na zilipokuja kurejea Sonia alikuwa amezikwa tayari...
Kilio cha Tina kiliendelea kudumu zaidi na zaidi hadi siku alipomuomba rafiki yake nauli ili aende mbali na ardhi ya Kilindi kwa sababu kamwe hatakoma kulia....
Na hakutaka kuliona kaburi la mtoto wake kabisa, alipoulizwa sababu hakuwa na sababu alichoomba ni kuondoka tu!!!
Ikawa kama alivyohitaji... rafiki yule akamsaidia nauli na kumtakia mema popote atakapokuwa.

**Ni nini kilifuata baada ya kuingia jijini Dar es salaam??
Na nini hatma ya Ripoti hii kamili...
Usikose sehemu inayofuata


Mamlaka ya kuhukumu si yetu wanadamu... na kama yangekuwa yetu basi dunia isingekuwa sehemu salama ya kuishi. Hakuna mwanadamu mwenye utashi kiasi cha kufahamu huyu ni mwema na huyu si salama.
Wanadamu tunaongozwa na hulka, kama utamuhukumu mwenzako kwa hulka na mitazamo yako binafsi kumbuka na wewe wapo watakaokuhukumu hivyohivyo...
Ukihitaji kuhukumu hakikisha kwanza umeiandaa ripoti kamili.
Na je utajuaje kuwa ripoti yako ni kamili????
 
Tina alikataa kata kata na bila shaka alikataa kwa sababu aliamini labda Sonia ataamka baadaye.....
Katika purukushani za hapa na pale Tina alipoteza fahamu na zilipokuja kurejea Sonia alikuwa amezikwa tayari...
Kilio cha Tina kiliendelea kudumu zaidi na zaidi hadi siku alipomuomba rafiki yake nauli ili aende mbali na ardhi ya Kilindi kwa sababu kamwe hatakoma kulia....
Na hakutaka kuliona kaburi la mtoto wake kabisa, alipoulizwa sababu hakuwa na sababu alichoomba ni kuondoka tu!!!
Ikawa kama alivyohitaji... rafiki yule akamsaidia nauli na kumtakia mema popote atakapokuwa.

Tina aliondoka na kufanya safari hadi jijini Dar es salaam. Ilikuwa ni safari ambayo hakuelewa hata ina maana gani hasa na ilibaki kidogo tu wazo la kujiua limpitie kichwani mwake kwa sababu alijiona ni mtu asiyekuwa na thamani yoyote ile katika dunia.
Lakini wazo hili likaingiliwa na wazo jingine akamkumbuka sarafina mtoto wake. Akaona kuna namna fulani ya kutomtendea haki yule mtoto iwapo ataamua kumuacha duniani akiteseka pamoja na dada yake mlemavu.
Alipofikiria jinsi maisha yalivyo magumu na baba wa mtoto bado anaishi akajiapiza kuwa atafika jijini Dar Es salaam na kumshurutisha yule mwanaume aanze kumuhudumia mtoto wake. Tina akajikuta kwa mara ya kwanza akiwa na roho mbaya kabisa dhidi ya yule mwanaume.
“Mjuni.. nilikuwa nipo tayari hata kuua kama ingebidi... ni huyo aliyeanzisha njia mbaya katika maisha yangu na kisha kunitelekeza pasi na msaada madhubuti...” alizungumza Tina kwa hasira sana. Mimi nilikuwa mtulivu nikichukua neno kwa neno huku nikiendelea kuichambua ripoti yangu kichwani. Hasahasa vile vipande vya ripoti ambavyo nilikuwa sijamsomea Tina..... lakini sikutaka kumuingilia kwa sababu alikuwa yu katika morali nyingine kabisa.
Tina aliendelea kusimulia juu ya safari yake na hapa akafikia kuelezea jambo ambalo lilinifanya nimuonee huruma na kuyasahau kwa muda mengi aliyonikosea.
Tina alinieleza kuwa kweli alifika jijini Dar es salaam na kwa sababu hakuwa mgeni wa jiji hilo alifanikiwa kuwapata marafiki kadhaa wa mzazi mwenzake. Wakamuelekeza anapopatikana na kweli akafika kwa mwanaume huyo.
Mapenzi acha yaitwe mapenzi, hasahasa mtu ambaye mmechangia naye damu tayari na kuwa na kiunganishi cha mtoto, Tina alimkuta yule bwana akiwa anaishi na mwanamke mwingine. Hakutaka kuleta vurugu zozote zile kwa sababu hata yeye alikuwa ameolewa tayari, tatizo lilikuwa ile hali ya yule mwanaume kumkana Tina na kusema kamwe hajawahi kuzaa naye.
Hapo Tina akavumilia akaondoka, lakini ajabu yule mwanamke ambaye alikuwa ni halali kwa wakatio ule kwa yule mzazi mwenzake Tina akaropoka jambo la kidhalilishaji kwa Tina.
Tina aliyevurugwa na maisha tena aliyetoka kumpoteza mtoto wake mdogo akaona isiwe tabu ni heri amnyooshe kidogo yule dada. Na kweli akafanya vile akifanikiwa kumnasa vibao vitatu vikali kabla yule mwanaume hajaingilia kati kisha kumpeleka Tina hadi kituo cha polisi kuwa amekuja kumfanyia vurugu nyumbani kwake.
Tina akaingizwa rumande alipokaa kwa siku tatu kabla ya kuachiwa baada ya mashemeji zake wa zamani kufanya mpango hilo jambo likapita.
Kwa sababu hakuwa na pa kwenda akalazimika kwenda kuishi kwa siku hizo kwa hao waliomtoa rumande.
Walikuwa ni vijana waliokuwa wanaishi maisha ya kibachela al maarufu kama ‘maisha ya geto’. Angefanya nini Tina na hakuwa na pa kuelekea, ikawa siku ya kwanza ikawa ya pili na hatimaye siku saba zikapita akiwa anahudumiwa na mashemeji hao wawili ambao usiku walikuwa wanalala chumbani huku yeye Tina akilala sebuleni. Moyoni alitambua wazi kuwa ni hatari sana kwa sababu kuwa shemeji haibadilishi mihemko ya kiume.
Akili yake haikuwa imepata njia mbadala ya kufanya hadi usiku ule wa manane ambapo mashemeji wale waligeuka kuwa viumbe hatarishi kwake.
Walikuja wakiwa wamelewa na bila shaka walikunywa kwa ajili yake.....
“Mjuni mume wangu.... nilitetemeka sana na kuwasihi sana wasifanye wanachotaka kufanya lakini hawakuwa wakinielewa... japokuwa walikuwa wamelewa lakini walikuwa na nguvu sana. Na tatizo kubwa ni kwamba nilikuwa nimelala nikiwa na nguo nyepesi tu, kwa sababu nguo zangu nilikuwa nimezifua.
Nilijaribu kupiga kelele lakini haikusaidia kitu... mashemeji zangu zamu kwa zamu walisaidiana kunibaka... niliumia sana Mjuni niliumia moyo wangu.....” alishindwa kuendelea kusimulia Tina na kuanza kububujikwa na machozi huku akitokwa na kilio.
Nikaingia katika jukumu la kumbembeleza Tina aliyekuwa anaugulia katika hali inayogusa moyo sana.
Nilipomkumbatia Tina niligusana na mbavu zake, alikuwa amekonda sana... sio Tina yule niliyekuwa namkumbatia enzi zile!!
Tina baada ya kutulia aliendelea kunisimulia kuwa alipoteza fahamu na zilipokuja kurejea alijikuta yupo jalala asilolifahamu na watu wachache wakiwa wanamshangaa.
“Mjuni kama uliniombea mikosi naomba sana msamaha wako, nimelaaniwa Mjuni.... nimelaaniwa.....” alilalamika Tina huku akiendelea kulia.
Nilimueleza kuwa hakuna baya lolote nililowahi kumuombea.
Tina akatabasamu na kisha akaelezea kuwa kwa aliyoyapitia haiwezekani hata kidogo kuwa yametokea bila sababu.
Kuna jambo moja ambalo nilitamani sana Tina anielezee ili niweze kuufunga ukurasa wa Ripoti yangu lakini niliona hajanieleza. Nikamueleza kama ananiruhusu na mimi nizungumze, akasema nimwachie kwanza amalize yote kisha ataniachia nafasi.....
Na hapo akaelezea juu ya safari yake ya kutoka Dar kuelekea jijini Mwanza...... akaniambia kuwa anajisikia vibaya sana kunieleza alipata vipi nauli lakini nielewe tu kuwa alifika jijini Mwanza na kumkuta mtoto wake akiwa salama katika uangalizi wa mama yake mkubwa yaani Zawadi dada yake.
Chuki yake kwa yule mtoto ilikuwa inakuja pale alipokuwa akiiona sura ya baba yake katika uso wake... lakini anakiri kuwa hakuwahi kuacha kumpenda mtoto wake kamwe kwa sababu ilikuwa ni damu yake.
Lakini chuki dhidi ya wanaume ndiyo iliyomfanya awe kama nilivyomkuta.....
“Tina.. ni nini hasa kilikusibu ulipokuwa Mwanza hadi ukaanza kunywa pombe na yote haya mapya ninayoyaona kwako....” nilimuuliza kiutulivu.
Tina akaniuliza swali.
“Mjuni una moyo mgumu sana natambua lakini sidhani kama upo tayari kulisikia na hili nqa kulipokea!! alijibu huku akinitazama.
Nikamsihi sana kuwa nipo tayari kusikia jambo lolote lile... Tina akaniuliza mara mbilimbili kama nitaweza kuvumilia!!
Swali hili la kujirudiarudia lilinitia mashaka kidogo japokuwa nilijiaminisha kwake kuwa nipo tayari kusikia na kupokea lakini kiukweli nilikuwa naogopa.
 
wakuu tunaendelea na uondo kama kawa....Sorry weekend hii nilikuwa Ngomani kijiji kwetu Msanga Ngongele ndio maana tukashindwa kuonana humu kwa wakati....ila akijaharibika kitu tumefidia ili twende pamoja....

Na yoyote mwenye MALALAMIKO kuhusu hii story anashuriwa aende mahakamani kushtaki au sehemu yoyote ambayo anadhani hatapata haki...

Story itaendelea mpaka mwisho na baada ya hii zitakuja na nyingine nyingi kutoka kwa Mwandishi wako mahiri George Iron Mosenya..

Asanteni na tuzidi kuwa pamoja
 
Back
Top Bottom