JIFUNZE kuwa mtu wa kusamehe, baba yetu wa mbinguni anatusamehe kila siku... kama yeye anatusamehe sisi kwa nini sisi kwa sisi tusipeane msamaha??
Na hii ni sehemu ya ishirini na mbili
Nilibaki katika butwaa kwa muda nilipoifungua pochi ile, nilikutana na picha ya Abduli.
Moyo wangu ulikufa ganzi, kijana muhangaikaji ambaye alikuwa mchapakazi kabisa alikuwa amefanya kitendo cha kizembe kabisa, kitendo cha kumnyewesha pombe Tibnaili ashiriki naye mapenzi.
Tina ambaye alikuwa ni muathirika........
Nilibaki katika utulivu uleule nikimtazama Abduli katika picha iliyokuwa katika pochi ile.
Nikatazama huku na kule kuwa huenda hata alitumia kinga.. sikuona dalili yoyote ya ganda lililotumika.
Ndugu msikilizaji, sikuumizwa bna kitendo alichomfanyia Tina kijana huyu, nilisikitishwa na ukungu ulotanda katika macho yake na hata asijue kile anachokifanya kuwa ni kosa kubwa ama la!
Niliichukua simu ya Tina kisha nikazitafuta namba za Abduli nilijua tu kuwa lazima waliwasiliana kabla Abduli hajaenda nyumbani kwake. Kweli ilikuwa hivyo.... lakini nilipotaka kupiga simu ile nilipata mashaka nitamueleza nini aweze kunielewa.
Kwa jinsi ninavyoyajua mapenzi, kwa lolote nitakalomweleza lazima atadhani ni wivu wa mapenzi unaonituma sema nisemalo.
Nikaachana na namba ile nikabaki kungoja Tina apatwe na fahamu.
Nilingoja hadi saa sita usiku ndipo Tina alizinduka kutoka kitandani.
Aliniitakwa jina la sabduli na kisha akaniuliza ni kwa nini nipo pale hadi giza lile.....
Baada ya kuona kimya akayapekecha macho yake na kutambua kuwa si Abduli bali ni Mjuni.
Tina akabigwa na butwaa akanbiuliza nilifika pale muda gani nikamueleza kuwa aliponitumia ujumbe niende kwake ndo muda niliokwenda.
Akatulia kwa muda akijiuliza kwa sauti ya chini ni ujumbe upi alikuwa amwenitumia.....
Na mara akakurupuka na kuketi kitako.... akaanza kuongea hovyohovyo kama mtu aliyepandisha mashetani.
Akaelezea kana kwamba tukio lile ndo kwanza linataka kutokea akasema kuwa Abduli alimchanganyia kilevi asichokijua katika juisi aliyomletea na anakumbuka alimuona akimpapasa kabla fahamu hazijamtoka.......
Wakati anamalizia kusema hayo nilimwona akijitazama katika maungo yake.
“Mjuni... Abduli ame... amenibaka jamani...” alisema Tina na kisha akaniangukia mapajani na kuanza kulia akiomboleza kwa hilo lililotokea. Nilimtia sana moyo na kumweleza kuwa yeye si chanzo cha jambo hilo hata kidogo hivyo asilie sana badal;a yake ni vyema tu ampe taarifa Abduli ili akapime afya yake.
“Noo! Mjuni sipo tayari mtu mwingine aijue afya yangu zaidi yako wewe....” alikataa Tina katakata. Na mimi nikamuunga mkono wazo lake hilo lakini huruma yangui ikiwa kwa Abduli kijana mchapakazi aliyeponzwa na tamaa zake za kimwili.”Nilikuahidi siku ya kwanza kabisa nitakuwa nawe kwa shida na raha... basi hata sasa sitakuwa upande wa mtu mwingine zaidi yako Tina..” nilimwambia huku nikimkumbatia kwa nguvu sana.
Ndugu msikilizaji wa mkasa huu wa mapenzi. Niliwahi kukuelezeni kuwa unaweza kulisubiri jambo fulani kwa muda mrefu na kamwe lisitokee na kukufanya ukate tamaa lakini kuna jambo linaweza kuja kwako kwa ghafla bila wewe kutarajia na kukufanya upigwe na bumbuwazi.
Ilikuwa hivi kwangu Mjuni mimi niliyepitia mengi huku nikitaraji kuwa na siku njema za usoni lakini majanga yakawa upande wangu kila kukicha.
Hatimaye ikafika siku ambayo walau nilipata kutasamu, siku hiyo Tina mwenye furaha aliomba kukutana na mimi. Akanieleza kuwa ameenda kwa madaktari bingwa na kisha kuomba ushauri juu ya jambo fulani na ameambiwa kuwa yawezekana kabisa japokuwa kuna gharama kiasi.
Nilimuuliza ni jambo gani akanieleza kuwa kuhusu gharama wala nisiwe na wasiwasi kwa sababu gharama zote zimelipwa tayari na kilichobaki ni kutelekeza tu jambo lenyewe.
Nilikuwa sijaelewa alikuwa ana maana gani Tina, nikabaki katika kusubiri atakalosema.
Kati ya siku ambazo Tina alizungumza mafumbo ya kunichanganya sana basi ni siku hii.. kila alichokuwa akisema kwangu ilikuwa ni msamiati mkubwa na mzito sana.
Na muda wote alikuwa ni mtu wa kutabasamu ama kucheka cheka bila mimi kuijua sababu bali yeye na nafsi yake!!!
Mwishowe akanieleza kuwa anahitaji kunizalia mtoto!
Nilishtushwa na kauli ya Tina na kuzidi kuvurugika zaidi... Tina ni muathirika na bado anasema anataka kunizalia mtoto hii inamaanisha nini hasa?
Nilijiuliza huku nikimtazama alivyokuwa akinisoma uso wangu!!!
Tina aliniambia nisimame kisha akaniambia nimsogelee, nikamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu sana.
“Mjuni Kalisti, umekuwa nguzo kuu katika maisha yangu kulikoni hata wazazi wangu ambaowalikata tamaa juu yangu... umekuwa nuru mpya katika njia yangu mbovu. Na zaidi umekuwa mwanaume kati ya wanaume ninaowajua.....” akasita na kunitazama usoni. Bado alikuwa anatabasamu.
Akaendelea kunimwagia sifa kemkem mimi nikawa najibu asante.
Baadaye akaiendea pochi yake na kutoka na karatasi kama nne.
“Hizi ni nini” nilimuuliza. Akacheka kisha akaniambia nizisome.....
Nilichokuwa naambulia ni kuona herufi tatu tu ‘H.I.V’ lakini mengine sikujua yana maana gani.
“hiyo ya bluu ni Bugando hiyo nyingine Angaza, na hiyo nyekundu ni Seketulee” akanijibu Tina akiwa bado mwenye furaha.
“Najua huwezi kuelewa upesi kwa nini basi nahitaji kukupa zawadi ya mtoto.....” akasita na kuelezea mlolongo wote wa maisha yake kama anielezavyo mara kwa mara.
kisha akanieleza jambo ambalo lilinifanya niupate ukurasa wa mwisho kabisa wa ripoti hii kamili.
Tina akanieleza kuwa hajawahi kuathirika na virusi vya Ukimwi bali alihitaji niwe mbali na maisha yake tu kwqa sababu alikuwa amejikatia tamaa, lakini kwa namna nilivyomjali na kumjali mtoto wake mwingine ambaye hata baba yake sikuwa namjua kwa sura, Tina alijikuta akinipenda upya na kujionayu mwanamke kati ya wanawake.
Hii ilikuwa taarifa ambayo niliiona kama ndoto ya mchana kweupe.
“Mjuni... nahitaji kukuzalia tu si mengineyo.....” alinisihi Tina.
Naam! Ili kuhakikisha tulienda kupima afya zetu upya, Tina alikuwa safi na mimi vilevile.
Kugundua kuwa Tuina yupo safi nikajikuta si tu kuhitaji mtoto na Tina bali kuyaendeleza mahusiano yale na kurejea kule tulipokuwa zamani.
Na hii ilikuwa rahisi kumshawishi Tina hasa baada ya kubeba mimba kweli......
Ule ukaribu ukazifanya zile pete zirejee katika matumizi yake, pete ambazo hakuna hata mmojawetu aliwahi kuivua.
Yule mtoto aliyekuja kuzaliwa miezi kadhaa baadaye akatuunganisha upya na kutufanya wamoja.
Yaliyopita yalipita sikujali nani atasema nini kuhusu mimi.....
Mtoto aliyezaliwa alikuwa wa kike, sikuwa na haja ya kuzunguka huku na kule kutafuta jina litakaloyafurahisha masikio yangu na Tina...... sote kwa pamoja tukakiita kitoto kile SONIA!! Hiyo ni Kwa heshima ya yule mtoto asiyekuwa damu yangu niliyekuwa nampenda kupita maelezo. Mtoto aliyepoteza maisha katika harakati za Tina kuikimbia aibu yake.
Nilijua kuwa wa kusema watasema mengi na wa kusengenya watasengenya sana, hata wewe unayeisomaripoti hii waweza kuwa mmoja wapo lakini amini kitu kimoja nilisema mwanzoni kabisa mwa ripoti hii kuwa.
Nimejifunza mengi katika maisha yangu, nimejifunza kuliweka wazi sikio langu kumsikiliza kila mtu iwe anazungumza upuuzi ama anajenga hoja chanya na madhubuti!!
Lakini yote juu ya yote, nafanya hivi lakini naweka maanani kitu kimoja tu. Ninakuruhusuni kunieleza lolote mnaloweza, ninakuruhusuni kunishauri lolote mnaloona linafaa kunishauri lakini aidha kuchukua ushauri wenu na kuufanyia kazi hii inabaki juu yangu mimi na akili zangu!!!
Sio kila mtakalosema nitalifanyia kazi...
Hakuna gharama yoyote katika kusikiliza ila kuna gharama katika kufanyia kazi hayo uliyoyasikiliza.
Naam!! niliufungua ukurasa wa ripoti hii nikiwa na Tina kama mke wangu ninayempenda sana na ninaufunga tena nikiwa na Tina lakini sasa akiwa mama Sonia na ndiye mwanamke ninayempenda zaidi...... sijui kuhusu hatma ya Anita yule mke wa marehemu Freddy na nijue ili iweje tena, nadhani wakati mwingine tunatakiwa kupuuzia yale yasiyotuhusu kiukaribu.
**Asanteni kwa kuufuatilia mkasa huu mwanzo hadi mwisho wake ikiwa kwa namna yoyote ile mkasa huu umeleta taswira hasi kwako natumia fursa hii kukutaka radhi......
MWISHO!!!