Mapengo junior
vip mbona simulizi yako imeanzia sehemu ya 3,nataka mtiriliko ili nianze kuisoma ndugu.
SIMULIZI.........PENZI CHUNGU -
SIMULIZI.........PENZI CHUNGU
MWANDISHI... HALFANI SUDY
SEHEMU YA 1
Suto Sutani, alikuwa ni msichana mwenye umri wa miaka 22. Alikuwa msichana mrefu wastani, Suto alikuwa na umbo zuri sana, alikuwa na ngozi nyeupe yenye kupendeza. Katika umri wake wa miaka 22, Suto hakuwa na mpenzi. Hakuwahi kufanya mapenzi, Hakuwahi kupata upendo toka kwa mwanaume yeyote yule duniani. Suto hakupata upendo hata wa baba yake mzazi. Mzee Sutani alimkataa Suto siku ileile aliyozaliwa. Sababu ya kumkataa ilibaki kuwa siri yake.
Bruno Michael, alikuwa kijana mtanashati sana. Alikuwa kijana aliyezaliwa katika familia yenye uwezo kiasi. Alikuwa kijana mwenye uzuri wa umbo na sura, uwepo wa pesa kiasi katika familia yao, vilifanya wanawake wengi sana wamhusudu sana Bruno pale mtaani kwao, Tabata dampo.
Bruno na Suto, walikuwa wanakaa mtaa mmoja, mtaa wa Tabata dampo. Wakati Suto na mama yake walikuwa wamepanga katika nyumba ya mzee Danigo, nyumba yenye vyumba sita na wapangaji sita ndani yake, nyumba ya kiswahili iliyojengwa Kiswahili.
Bruno alikuwa anakaa katika nyumba nzuri ya wazazi wake, nyumba yenye vyumba vitatu, yenye kila kitu ndani, nyumba ya kisasa iliyojengwa kisasa.
Ilikuwa siku ya jumamosi asubuhi, Bruno alikuwa hajaenda chuo siku hiyo. Wazazi wake walikuwa wameenda sokoni kununua mahitaji mbalimbali ya nyumbani kwa gari yao ndogo aina ya Suzuki.
Bruno alikuwa amekaa sebuleni akisoma kitabu cha Riwaya ya Ulaaniwe, riwaya iliyotungwa na Gwiji wa riwaya Tanzania, George Iron Mosenya.
Akili ya Bruno ilikuwa imezama hasa katika riwaya ile yenye kusikitisha sana, huku muziki mwanana wa mwanamziki Ben Pol ukisikika katika spika za redio yake.
Ghafla mlango wa sebuleni uligongwa.
"Karibu" Bruno alisema huku akikiweka juu ya sofa kitabu chake cha riwaya.
"Ahsante " Sauti ya kike ilijibu nje ya mlango ule.
"Sukuma, upo wazi "
Mlango ukafunguliwa.
Aliingia Suto, akiwa amevaa suruali nzuri aina ya jeans na blauzi fupi nyeupe. Mkononi alikuwa ameshika mkanda wa video.
"Kaka Bruno, nimeazima mkanda huu kwa kina Alex, naomba uniwekee niuangalie kidogo" Suto aliomba kwa sauti yake nzuri.
"Sawa, usijari" Bruno aliitikia.
Bruno alikuwa havutiwi kabisa na wasichana, alijiona mzuri, alijiona mtanashati, alikuwa ananata sana pale mtaani. Hakuwapenda wasichana, hakutaka hata kuwa na ukaribu nao. Lakini leo alipatikana, hakuwa na jinsi, walikuwa sebule moja na Suto Sutani.
Bruno aliuchukua ule mkanda mikononi mwa Suto na kwenda kuuweka kwenye deki, na kuzima redio iliyokuwa inaimba. Ulikuwa mkanda wa taarabu . Bruno alirudi sofani na kuendelea kusoma riwaya yake.
Suto akiwa na furaha isiyo na kifani kumuona Mzee Yusuph akiimba kideoni, huku madada wakicheza kwa umahiri mkubwa.
Kidogo kidogo taarabu ikaanza kumuingia kichwani Suto. Mziki wa taarabu ukapenya katika mishipa ya damu yake. Mwili ukamsisimka, Suto alikuwa mpenzi mkubwa sana wa taarabu. Taratibu alianza kutingisha kichwa pale sofani. Bruno alikuwa kazama riwayani, hakumuona Suto alivyokuwa anatingisha kichwa chake.
Taarabu ikachanganya, Suto alijikuta anasimama , akaanza kutingishika mwili wote taratibu. Bruno sasa aliweka kidole kurasa aliyoishia kuisoma, ili isipotee, macho yake yote mawili yapo kwa Suto Sutani.
Suto alikuwa hana habari kabisa. Sasa alikuwa anatingisha nyonga yake barabara. Bruno alibaki kahemewa.
Macho ya Bruno yalipanda kwa wizi, sasa yalitua katika kiuno cha Suto, kilikuwa kiuno kizuri sana. Chenye mviringo unaoeleweka. Bruno alikuwa makini, kiuno kizuri kilikuwa kinafata vizuri ule mdundo wa taarabu. Bruno sasa alikuwa anaangalia dhahiri, sio kiwizi tena.
Kiuno kizuri cha Suto kilikuwa mahiri sana.
Suto alikuwa bize na taarabu, akiwa kasahau kabisa uwepo wa Bruno kwa muda. Bruno alikuwa bize na kiuno cha Suto, akiwa kakisahau kitabu cha riwaya kwa muda.
Bruno naye alisimama taratibu, akawa anamsogelea Suto. Kitabu akikiacha palepale kwenye sofa. Suto alizidi kukatika, na Bruno alizidi kumsogelea. Walikaribiana sana sasa.
Suto kwa mbali alihisi kiuno chake kikishikwa ,
ITAENDELEA