Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 009

Hakujua kuwa alikuwa njia moja na wanausalama. Hakujua kuwa vijana waliombele yake walikuwa wanausalama, tena wakimfuatilia yeye. Bado aliongoza akitembea kwa umakini, akichungulia na kuangalia kila sehemu kwa chati. Alikuwa tayari kumuua mwanaume anayempenda kwa sababu ya pesa. Licha ya kuwa tayari lakini hakuujua mwisho wa mambo yale utakuwa nini. Kingine kilichomtatiza ni mtu ambaye ameambiwa kuwa ameongezwa katika kazi ile ya kumfuta masimba katika uso huu wa dunia. Kilikuwa kitu kigumu mwanzo lakini kila alipokumbuka kifo cha Asteria na Rafiku yake, alijikuta akinong'ona mwenyewe. Muda nfupi baadae alikuwa akiingia ndani ya Bar moja maeneo yale ya tegeta. Baada ya kuingia, akaongoza mpaka moja kwa moja katika vyumba vya eneo lile. Akauendea mlango wa chumba ambacho huwa wanakutaniana. Akaugonga mlango katika namna ambayo ilitambulika ama kuzoeleka miongoni mwao. Mlango ukafunguliwa kisha akaruhusiwa kupita. Alipoingia mlango ukafungwa tena. Macho yake yakatembea usoni kwa kila mmoja, shauku yake ilikuwa ni kumuona mtu ambaye aliambiwa atakuwa nao katika sakata lile. Kila mmoja ndani ya chumba kile alikuwa kimya, ukimya ambao uliyaruhusu macho yao kutizamana. Sura ya mwanamke mrembo ndio sura pekee ngeni ambayo ilimpa majibu kuwa huyu alikuwa ndie mtu alieletewa ili kusaidiana naye. Akasogea macho yake yakilazimisha kutizamana na mwanamke huyu. Alikuwa akifanya hivyo kutaka kujua kama huyu mwanamke atakuwa mmoja kati ya watu wa aina yake. Ni kweli walitizamana, ni kweli waliangaliana na kuangaliana tena na tena. Lakini hakufanikiwa kukiona kile alichokuwa akikitafuta. Macho ya mwanamke huyu hayakumuonyesha kile alichokuwa anakitafuta. Hayakumjulisha kama yeye alikuwa nani. Bado yalikuwa macho ya kulegea, macho ya kusinzia na kibaya zaidi hayakumuonyesha chochote kile. Hilo likaonyesha kumpa mashaka. Akatafuta mahala puzuri na kukaa. Bado macho yake hayakuacha kuonyesha mashaka. Bado hakumuamini mwanamke yule. Ndio alikuwa mrembo, ndio alikuwa mzuri na alivutia katika kutizamwa na hata kuwekwa ndani na wanaume. Lakini licha ya uzuri huo bado hakukiona kile ambacho kingempa picha, picha kwamba anaweza kuzimudu kashkash zote za wanausalama. Akauvuta muda huku akimtizama Jimmy na wengine waliokuwepo pale ndani. Alitaka kusikia kutoka kwake, alitaka kusikia kwamba huyu ni nani, na ni vipi atamudu kupambana na masimba. Jimmy ni kama aliyasoma mawazo ya Jenipher. Akasimama kutoka pale alipokaa kisha kupiga hatua kusogea mpaka pale alipokaa Jenipher. Akamuangalia kwa muda kisha akanena.

"Nimekuletea Shetani yule akusaidie kumuondoa masimba katika uso wa dunia hii.." yalikuwa maneno yaliozunguka kichwani kwa teddy. Hakuuamini ushetani wa mwanadada yule. Alimuona ni kama wadada wa mjini na asingeweza chochote.

"Jimmy unadhani ataiweza hii kazi? Tambua tunachokifanya ni kazi ya kifo. Na hii kazi tunaifanya kwa siri sana. Pia tambua watu tunaopambana nao hawana masihara. Una uhakika yule mrembo ni shetani kweli?" Aliongea Jenipher akionyesha kuwa na mashaka.

Tabasamu likachanua usoni kwa Jimmy, kisha likafuatiwa na kicheko, kicheko ambacho kilitumika kama jibu kwa maswali ya Teddy. Wote wakasimama kwa pamoja kisha kushikana mikono. Mkataba ukaingiwa na makubaliano kufikiwa. Kilichobaki ilikuwa kazi ya kumuondoa Masimba, kisha wabia wenzao, harafu kugawana mzigo wao.

********

Wakati Vijana Wake wakiwa tegeta, masimba ndio kwanza alikuwa akiiisimamisha gari mtaa wa pili kutoka nyumba anayoishi Jimmy. Baada ya kushuka akaufunga mlango. Baada ya kuufunga mlango akaangaza huku na huko, aliporidhika akatembea bila wasiwasi kuelekea ilipo nyumba ya Jimmy. Hakuwa na wasiwasi juu ya kuingia katika jumba hilo kwani vijana wake walikuwa wakimpa taarifa za kile kilichokuwa kikiendelea kule tegeta. Alijua ndani ya muda huo alikuwa na uwezo wa kuingia na kutoka pasipo wasiwasi wowote. Alitembea kama mwananchi wa kawaida akiangalia hiki na kangalia kile. Mtaa wote ulikuwa kimya, hapakuwa na watu ambao wangemsumbua ama kumtilia mashaka. Mzigo umekamatwa na kutangazwa katika vyombo vya habari. Lakini cha ajabu mzigo huu unaonyesha kutokukamatwa, unaonyesha kuna mchezo nyuma ya sakata hilo. Nani yupo nyuma ya jambo hili? Ndio kitu peke ambacho alijiuliza masimba pasipo kupata majibu. Akaendelea kutembea huku mazingira yakimpa uhuru wa kufanya kitu. Sasa alikuwa akiangaliana na jumba la Jimmy Lambert. Lilikuwa jumba la kifahari, likiwa limezungushiwa Uzio, uzio ambao ulikuwa mrefu kiasi chake. Ukiondoa hilo pia jumba hilo lilizungushiwa nyaya maalum za umeme ambazo zilisaisia kuongeza usalama wa jumba lile. Pia licha ya hivyo vitu, lakini pia hapakuwa na walinzi. Mlinzi alikuwa mmoja ambaye alikaa kwenye geti la mbele. Baada ya kuliangalia vyakutosha sasa aliamua kuingia ndani. Huyu aliamulia kuingia katika Geti la mbele. Akasogea akitembea kawaida sana. Mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa mlangoni mkononi akiwa ameshikilia bunduki aina ya gobole. Masimba akasogea zaidi na zaidi mpaka karibu kabisa na mlinzi yule. Kabla hajazungumza naye chochote, Masimba akachomoa simu kisha kumpa mlinzi yule. Mlinzi akasita kwanza kuipokea. Akamwangalia mtu huyo usoni, mtu ambaye alikuwa akimpa simu pasipokuongea naye chochote. Macho yake yakakutana na tabasamu, tabasamu ambalo liliitoa hofu ya mlinzi yule.

"Ongea Na Jimmy Lambert ana maagizo anataka kukupa." Akaingea Masimba pasipo masihara. Mlinzi yule akalifanya kosa la kupiga hatua kumsogelea Masimba. Hakufanikiwa kusogea tena kwani pigo moja la karate likatua Shingoni. Mlinzi akatambarajika chini. Akamvuta na kumuweka kando ya maua ya jumba lile. Alipohakikisha hawezi kuonwa na watu, alilisukuma geti na kujitoma ndani. Alitembea kwa tahadhari kubwa mpaka uani mwa jumba lile. Akasimama hapo akiangalia zilipo camera za usalama za jumba la Jimmy. Baada ya kuhakikisha hamna chochote kile, akachomoa funguo zake malaya kisha kuichomeka sehemu, punde mlango ulikuwa ukifunguka na kumruhusu Masimba Kuingia. Baada ya kuhakikisha ameingia, masimba akaichomoa bastola yake na kuanza kuingia kila sehemu akipekua. Kwa kuwa alikuwa akipewa taarifa na vijana wake juu ya uwepo wa jimmy na washirika wake, hakuwa na wasiwasi katika kupekua. Alifungua vyuma karibia vyote kwa kutumia funguo malaya na kuvipekua. Hakuweza kupata kitu chochote. Wakati anaingia kwenye chumba anacholala jimmy, ndipo hapo alipouona mlango mdogo, mlango ambao alizani labda ni wachoo ama bafu.. lakini alipoutingisha ulikuwa mgumu na haukuwa unafunguka kwa Funguo Malaya.

MASIMBA AKATULIA
 
Kitu kimoja ambacho nadhani hamkijui wasomaji wa riwaya hii ni kwamba.. hii riwaya inaandikwa moja kwa moja hapa hapa.. siikopi na kupaste so ni kazi ambayo waandishi wengi inawasumbua na hawawezi kama ninavyofanya mimi. Ni uvumilivu wenu
tumekuelewa acha tuwe wapole
 
Kitu kimoja ambacho nadhani hamkijui wasomaji wa riwaya hii ni kwamba.. hii riwaya inaandikwa moja kwa moja hapa hapa.. siikopi na kupaste so ni kazi ambayo waandishi wengi inawasumbua na hawawezi kama ninavyofanya mimi. Ni uvumilivu wenu
Shaka ondoa ibra waungwana tumekuelewa
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 010

Mlango ulikuwa mgumu na haukuweza kufunguka hata kwa funguo malaya. Hilo likamfanya masimba atulie kwanza. Alitulia akiwaza ni kipi cha kufanya ili kuufungua mlango. Akawaza na kuwazua huku akijaribu mara kwa mara kuufungua mlango. Lakini bado mlango ulikuwa mgumu kufunguka. Akaachana na kimlango hicho kisha kuiendea droo ya kitanda. Hapo pia akatumia funguo malaya kufungua, safari hii alifanikiwa. Baada ya kuifungua droo ile, akayatupa macho yake kwa chati ndani yake. Cha kwanza kukiona zilikuwa funguo kama tano, funguo ambazo mara moja alitambua kuwa ni zile ambazo huwenda zinatumika kuufungua mlango ule. Akazitwaa kisha kurudi pale mlangoni. Zoezi la kufungua likaanza tena. Safari hii haikumchukua muda, kimlango kile kikafunguka.. macho yake yakapokewa na mabegi matano, mabegi ambayo aliyatambua kuwa ndio ule mzigo ambao ulitangazwa kukamatwa uwanja wa ndege. Kichwa chake kikachemka kwa haraka sana, alitakiwa kuondoka na mabegi yale katika muda ule. Alitaka kuliacha hili suala katika kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe. Lakini kuna kitu kimoja kilikuwa kikimtatiza.. mzigo huu usingeweza kutoka pale airport kwa nguvu ya Jimmy pekee. Jimmy hakuwa na uwezo wa kuishawishi Idara ya Usalama pasipo kuwepo kwa msaada wa mtu mwingine hapa. Mtu huyo ni nani? Lilikuwa swali pekee lililosumbua kichwani mwake. Alitambua lazima kuna uwepo wa mtu tena mkubwa sana katika sakata lile. Kwa mara ya kwanza majukumu yakaendelea kuongezeka. Sasa alikuwa akimuhitaji huyu mtu wa tatu. Lakini pia alitambua ahadi ya kupigiwa simu na mwanamke yule mrembo. Baada ya kufikiria kwa muda mrefu pasipokupata majibu sahihi, akaona huu ulikuwa wakati wa kuondoka pale ndani, lakini akajiapiza kwamba ni lazima atoke pale akiwa na mzigo ule. Akavuta begi la kwanza kisha la pili, alipotaka kuvuta begi la tatu, masikio yake yakainasa michakato ya miguu ya mtu, ikionyesha kusogea pale mlangoni. Masimba akainuka haraka na kujisogeza pembeni kidogo ya mlango. Punde akauona mlango ukifunguliwa kisha mdomo wa bastola ukatangulia Mbele, bado akaendelea kutulia, hata mtu yule alipoingia bado hakujitoa pale. Alitaka kumfahamu huyu alikuwa nani.akamsubiri mtu yule aurudishie mlango ndipo amkabili. Hilo likafanyika, muda mfupi mtu yule alikuwa akitizamana na mdomo wa bastola huku macho yasio na mzaha yakimtizama. Mtu yule hakulitegemea hilo, akajikuta akiupoteza umakini, sasa alikuwa akitetemeka. Hakuonekana kama ni mjuzi katika misukosuko, bali huyu alionekana kuwa mgeni katika medani hii ya mapambano. Masimba akaendelea kumtizama huku bastola yake ikiwa imelengwa kwenye paji la uso la mwanaume yule. Mara tukio la ajabu likatokea, tukio ambalo lilimfanya masimba aamini kuwa huyu mtu alikuwa mbwa koko. Mkojo ulikuwa ukimtoka na kulowanisha mavazi yake. Hilo lilimfanya masimba apange kumtumia katika kuyaondoa mabegi katika chumba kile. Punde alikuwa akiishusha bastola na kuanza kumtizama mateka wake. Hakuongea naye chochote zaidi ya kumpa Ishara ya kufanya kile ambacho alitaka kukifanya. Muda mfupi walikuwa wakitoka nje huku wameongozana, mateka yule akiwa na mabegi mawili makubwa, hata masimba naye ilikuwa hivyo. Bastola ilikuwa mkononi akimuongoza mtu yule njia za kupita. Wakafanikiwa kutoka getini pasipo na ugumu wowote kwani bado mlinzi yule hakuwa amerudiwa na fahamu. Alimuongoza mateka wake mpaka mahali alipoiacha gari yake. Wakapakia mabegi yao na muda mfupi walikuwa wakiondoka hapo kwa pamoja huku bado bastola ikizigusa mbavu zake.

******

Ilikuwa yapata majira ya saa nne usiku wakati Teddy akiwa njiani kuelekea kimara nyumbani kwa dada wa Asteria tayari kwa kwenda kuifanyakazi. Wakati anayavuka mataa ya ubungo, simu yake ya kiganjani ikawa inaita. Akasonya huku akiitoa simu yake kutoka mfukoni. Jina la Jimmy likasomeka kwenye kioo cha simu yake. Haraka akapokea na kuipeleka simu sikioni.

"Rudi mikocheni Haraka." Baada ya maneno hayo simu ikakatwa, rudi mikocheni haraka kisha simu kukatwa ni kitu ambacho kilimchanganya akili yake. Atumwe akawaue ndugu wa Asteria, wakati bado hajakamilisha hilo aambiwe arudi mikocheni tena! Ulikuwa ujumbe ulioonyesha hapakuwa na usalama. Akaavunja sheria za barabarani kwa kugeuza gari sehemu ambayo haikuruhusiwa. Watu waliokuwa pembeni mwa barabara sambamba na askari wa usalama barabarani walikishuhudia kitendo kile kwa karibu sana. Hata walipomsogelea kutaka kumsimamisha, Teddy akawapelekea gari kwa kasi sana, askari wakaruka na kuangukia pembeni. Teddy akakanyaga mafuta gari ikawa inatembea kwa mwendo wa hatari. Kila mmoja alikuwa akiiangalia gari kwa mshangao. Wengine waliahangilia na hata kupiga miluzi, lakini wachache walilaani huku wakitukana matusi mazito. Teddy hakusikia ndio kwanza alikuwa akiipita Changanyikeni na sasa alikuwa akiitafuta mwenge. Kila mmoja aliekuwa akiitizama gari ile ilivyokuwa ikiendeshwa, alifumba macho akiogopa kutizama. Wakati anafika maeneo ya Mwenge mataa, mbele yake akakiona kile ambacho kilimfanya aupunguze mwendo. Mbele yake kurukuwa na diffender tano za palisi na Askari wasiopungua Ishirini, kila mmoja akiwa na Sub Machine Gun akiwa ameilekeza kule lilipo gari la TEddy. Amri ikatolewa akitakiwa kushuka akiwa amenyoosha mikono juuu.. Teddy akatii huku bastola akiiacha ndani ya gari. Aliposhuka chini tu huku akiwa amenyoosha mikono askari wengi walimtambua kuwa alikuwa ni mwenzao, lakini licha ya kumtambua huko hawakuacha kumuuliza hili na lile. Baada ya kama dakika tano walimuachia na kumtaka kuwa muangalifu.

********

Alisimamisha gari nje ya jumba la Jimmy, akashuka na kuingia ndani. Hapo akapokelewa na mwili ambao haukuonekana kama una Uhai. Mbele yake alisimama Jimmy sambamba na washirika wao kila mmoja akionekana kuchanganyikiwa. Tedy bado hakuwa amekielewa kile kilichokuwa kikiendelea humo ndani. Hata pale alipoambiwa aingie chumbani hakuwa bado anatambua kile ambacho kimetokea. Alipoingia chumbani kisha kutupa macho yake pale kwenye hazina yao, Teddy akaporomoka chini akiwa ameishiwa nguvu. Mzigo wao wao wa Mamilioni ya Shilingi ulikuwa umetoweka. Mzigo uliomfanya awe tayari kumuua Mpenzi wake haukuwepo tena. Mzigo uliomfanya amuue Asteria haukuwepo tena. Umeenda wapi? Nani amewazunguka? Masimba? Hapana!! Juma Kitumbe? Inawezekana!!! Yalikuwa mawazo yaliopishana kichwani mwake. Alipoinua kichwa kuwatizama Wenzake, alijikuta Akitizamana na Midomo Miwili Ya Bastola.

NGOMA NDIO KWANZA NI MBICHI
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 011

Alikuwa akitizamana na midomo miwili ya bastola. Washikaji wakiwa katika umakini wa hali ya juu. Teddy hakuamini kile alichokuwa akikitizama. Akataka kujaribu kumuuliza Jimmy kinachoendelea, lakini sauti haikutoka, akabaki akiitizama midomo ya bastola ambayo ilikuwa umbali mfupi kutoka usawa wa paji la uso wake. Akili yake ikaganda, ikashindwa kufanya kazi kwa wakati, mzigo umepotea, harafu tena anashikiwa bastola! Hilo likamchanganya kama sio kumshangaza. Akakitamani kitendo kile kiwe ndoto, lakini bado haikuwa hivyo. Mzigo haukuwepo na kibaya zaidi alikuwa akitizamana na midomo ya bastola. Akainamisha kichwa chini akijaribu kukiamini kile kinachoendea pale. Kwa mara nyingine akainua kichwa kutizama tena, lakini safari hii hakukiona kile ambacho alikiona mwanzo. Hakuwa akitizamana tena na midomo ya bastola, hapakuwepo na watu wawili waliokuwa wameshika bastola. Walipotea na kutokuonekana kabisa. Mbele ya macho yake alisimama Jimmy pekee. Hata Jimmy hakuwa yule wa tabasamu. Huyu alionekana kuchanganyikiwa na hata kukata tamaa. Uso ulikunjamana kwa hasira, sasa alikuwa akimtizama Teddy kwa macho yake makali. Uso wake ulikuwa ukiongea kifo, macho yake yalikuwa yakiitangaza shali. Kila alipokuwa akimuangalia Teddy mishipa ya hasira ilikuwa ikizidi kuharibu taswira yake. Alikuwa akihitaji kuongea na Teddy. Alitambua teddy hakuwa mhusika wa kilichotokea, alimjua tena na pia aliufahamu uaminifu na hata msimamo wake. Asingeweza kukifanya kile. Hilo likampa ugumu kuongea, kitendo cha watu wao kumnyooshea Bastola kilimpa wakati mgumu sana. Alimjua fika katika medani ya mapambano, alimjua fika katika medani ya mapigano, huyu alikuwa ni zaidi ya Jean Claude Van Damme na hata zaidi ya Don Yen na Hata Jet lee. Kitendo cha kumnyooshea bastola ni kumkosea sana. Hilo likamfanya Jimmy awe mnyenyekevu mbele ya mwanadada huyu. Lakini kile alichokitegemea hakikuwa hivyo.uso wa teddy haukuwa katika masihara tena, alimuangalia Jimmy kwa macho yenye maswali lukuki. Akatamani kuongea neno moja lakini hakuipata nafasi hiyo. Teddy alisimama na kupiga hatua bila hata kumuangalia Jimmy. Alitembea akitoka katika jumba lile akiwa ni mwenye hasira sana. Aliuhisi mchezo mzima kuchezwa na watu wake hao ili kumzunguka. Hilo hakuwa tayari kuliona likitokea. Alikuwa tayari kumuua yoyote katika hilo. Alishakubali kumuua masimba sababu ya mzigo ule, sasa kwa nini hawa wanataka kunizunguka?
Lilikuwa swali ambalo lilikivuruga na kukichanganya kichwa cha teddy. Bado Jimmy hakuweza kuongea kitu. Bado jmmy alikuwa akimkodolea macho. Teddy akakiinua kichwa chake kwa mara ya pili kisha kumuangalia tena jimmy. Macho yake yalikuwa yakiongea kitu kingine kabisa. Hakuwa teddy yule mrembo na mwenye tabasamu, huyu alikuwa teddy tofauti kabisa. Bado hakuyaondoa macho yake usoni kwa Jimmy. "Huu ndio Wema wangu? Haya ndio malipo ya kuwasaidia mzigo wenu? Umenisahau mimi ni nani? Umesahau kuwa ninauwezo wa kuwaua kwa muda mfupi tu? Sasa naomba uniambie ukweli, nataka kuujua mzigo uko wapi na nani ameuondoa hapa. Usipokuwa mkweli maiti yako itakutwa humu ndani. Aliongea teddy akimuangalia jimmy pasipo kupepesa macho bastola ikiwa mkononi. Jimmy alijikuta midomo ikimkauka, akajikuta mate yakishindwa kupita kooni. Alimtizama teddy machoni kwa muda mrefu akitamani kuongea kitu. Hakupata neno la kuongea, alijikuta akianza kutetemeka. Jimmy leo alikuwa akimuogopa teddy.

Akaona kukaa kimya kutasababisha makubwa. Kwa sauti ya uoga akaanza kuelezea kila kitu tokea waliporudi na kuikuta maiti ya mlinzi, akaeleza walivyoingia ndani wakishuhudia mzigo wao ukiwa haupo. Hakuficha chochote kile. Baada ya Jimmy kumaliza kuongea teddy hakuongea kitu. Alipiga hatua mpaka nje pale ulipolazwa mwili wa mlinzi yule. Akaufunua na kuuangalia kwa makini. Cha kwanza kukiona ni jeraha shingoni kwa marehemu yule.

"Masimba!" Lilikuwa neno pekee kutoka kwa teddy. Hili likamfanya jimmy aliekuwa amesimama nyuma kidogo ya teddy asogee na kuonyesha kushangazwa. "Masimba aliingia hapa na ndiye aliefanya hiki kitu. Na kama kweli ni yeye alieuchukua mzigo, itabidi uwasiliane na mwamvita muda huu, ili watakapo kutana ajue anatakiwa kufanya nini." Aliongea teddy akitoka pale akionyesha ni mwenye mawazo.

*********
Ulikuwa usiku wa saa mbili na nusu pale simu ya Masimba ilipotoa sauti kuonyesha kulikuwa na ujumbe mfupi wa maneno. "Upo wapi Masimba? Uliuliza ujumbe ule. Masimba akatulia kwanza kujipa muda wa kufikiria.

"Nipo nyumbani!" Alijibu nakutulia tena.

'Bila shaka utakuwa upo tayari kwa sasa kukutana na mimi?" Ujumbe mwingine ukaonyesha kuuliza.

"Yeah! Naomba tukutane Ngamia Pub kigamboni, nadhani panafaa kwa aina ya maongezi yetu.". Alituma ujumbe huo ambao ulipokewa kwa ukimya wa muda mrefu. Kwa mtu aina ya Masimba aliutambua ukimya ule. Aliutambua kwa maana moja. Mwanamke yule alikuwa akifanya mawasiliano na watu wengine, watu ambao alitambua lazima watakuwa wameshaanza kuelekea sehemu ya mkutano wao. Hakuwa na shaka kwa kuwa Charty John alikuwepo sehemu ya tukio akimuangalia kila aingiaye na kutoka. Hakuwa na shaka kuhusu hilo.

Muda mfupi alikuwa akiingia maliwatoni, akajimwagia maji, kisha kutoka na kuyaendea mavazi yake. Baada ya kuvaa na kujiangalia akachukua bastola zake mbili revolver colt na dernng up automatically na kuziweka sehemu yake. Baada ya kumaliza hapo akaweka vitu vyake sawa pale ndani. Muda mfupi alikuwa akiliacha jumba lake akielekea sehemu ya tukio akiwa katika tabasamu la aina yake. Siku zote alipenda kucheza na watu wa aina yake, alipenda kucheza na watu walioupenda mchezo ule. Alitaka kumalizana na hawa kisha kurudi kwa teddy. Alitaka kumfanya kuwa wa mwisho.

*****

Sehemu kubwa ya eneo hili la mjimwema lilikuwa limechangamka watu wakionyesha kuifurahia siku hii. Muziki ilikuwa ukisikika, muziki ambao ulikuwa ukiwa burudisha vijana kwa wazee. Sehemu yote ilikuwa katika hali ya kupendeza na hata kuvutia. Charty alikuwa pembeni kabisa macho yake yakiwa busy kutizama kila tukio linaloendelea hapo. Muda mfupi akaiona gari aina ya Toyata ikisimama eneo la maegesho. Macho yake yakavutiwa na watu walioshuka kwenye gari ile. Hayakuvutiwa kwa uzuri wa mavazi yao ama sura zao, bali alivutiwa kwa kuwa ndio wale aliowaona mchana wakimfuatilia masimba. Hilo likamuweka kwenye utayari. Muda mfupi akamuona mwanamke yule akiingia pale, alikuwa katika mavazi ya aina yake. Sketi fupi ilioishia juu ya magoti kwa juu kabisa. Sketi ya kubana na kusababisha mistari ya chupi aliovaa kuonekana kwa uwazi zaidi. Wateja wote wakageuka kutizama kule alipokuwa akitokea mwanamke yule. Miluzi ikasikika na shangwe kutamalaki. Wakati mwanamke yule akiendelea kuwahenyesha wanaume na kuzivunja shingo zao, masimba ndio kwanza alikuwa akiwasili eneo la tukio, bastola mbili zikiwa kiunoni, akitembea kuelekea pale pale.

Kesho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom