Riwaya: Niacheni nikufuru

Riwaya: Niacheni nikufuru

RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com


SEHEMU YA NANE

Johnson aingia matatani.

NASIMULIA

Nakumbuka siku hii, majira ya saa mbili kasoro usiku. Mke wangu Jackline alirudi nyumbani na kunikuta sebuleni nikiwa niko bize na tanakilishi yangu. Nilikuwa na jukumu la kuifanya upya kazi iliyopotea ili niiwasilishe kwa Bosi siku tatu zijazo.

Jackline aliufungua mlango wa sebuleni na kunikuta nimekaa kochini.

..........."Ooh J wangu, waooooo" alisema kwa sauti punde tulipokutanisha macho yetu na kunisogelea ili anikumbatie.
Ila mimi wala sikumjali, nilikuwa na hasira zisizo kifani moyoni mwangu. Haiwezekani mtu tangu narudi kazini mida ya saa kumi, sijamkuta nyumbani, ndo anarudi sahizi tena hata taarifa ya kunijulisha mahali alipotaka kwenda hakunipa.

............"Jamani Baby, mbona unanifanyia hivyo?. Mi nataka nikuwawo ila wewe hata hunipi ushirikiano". Jackline aliongea kwa kulalamika huku akiwa amenisogelea karibu.

Hapo ndipo tatizo jingine lilipotokea. Jackline ananukia rosheni ile ile aliyoipaka siku ile aliyonidanganya kuwa alimsindikiza Roida kwa shangazi yake. Hapo moyo ukapiga 'paa'. Moyo ulianza kwenda kasi baada ya kugundua kuwa Jackline ameipaka tena rosheni ya Idris ila ameipata wapi?, au alienda tena kwa kina Roida?, mbona Idris aliniambia kuwa Roida amesafiri, ataendaje huko bila Roida kuwepo?. Hakika nilikuwa na maswali mengi yaliyopita kichwani mwangu. Na wa kunijibu haya maswali hakuwa mwingine bali mke wangu Jackline. "Jackline anachepuka kwa Idris", niliwaza moyoni.

Nikiwa bado nimekaa pale kwenye sofa nikamuuliza Jack "Umetoka wapi?"

..........."Jamani laazizi wangu, kwahiyo hicho ndo kimefanya unune?, si nilikuwa na Roida kwao". Jackline alinidanganya.

..........."Una uhakika ulikuwa na Roida?. Nilimuuliza.

.........."Sasa hayo ndo maswali gani J, mimi nitakaa na nani zaidi ya Roida?" Alijitetea.
Sikuwa na papara, nikatoa simu yangu mfukoni na kuanza kuitafuta namba ya Roida, nikampigia na kuweka Loud speaker.

..........."Hello, Roida, habari yako?" Nilisema baada ya simu kupokelewa.

........."Nzuri shem za kwako huko" alijibu.

........."Huku kwema kabisa. Nasikia umesafiri, umeenda kwenu. Ni kweli?" Nilimuuliza.

........."Ndio shem wangu, nimekuja kuwatembelea wazazi wangu mara moja. Tangu juzi niko Iringa" Roida alijibu. Hapo nikamtazama Jackline usoni. Alikuwa ameduwaa tu.

........."Sawa shem wangu, mi nakupa hai tu.Wasalimie sana Baba na mama. Kwaheri" nilimjibu.

........."Poa, nitawasalimia. Nawe kwaheri" Roida alijibu, nikakata simu na kuiweka mezani.

..........."Haya, bila shaka umesikia vizuri kabisa maongezi yangu na Roida. Leo haukuwa na Roida, sasa niambie ulikuwa wapi?" Nilianza kuongea huku nikiinuka pale kwenye sofa na kumsogela Jackline. Jack hakujibu kitu, alikuwa kama amemwagiwa maji ya baridi.

.............."Jack, huwezi kunidanganya kitu. Siku ile ulipochelewa kurudi hadi ukaletwa na Roida ulinidanganya kuwa umetoka kwa shangazi yake Roida" nikaongea kisha nikatulia kidogo ili aweke mazingatio katika yale ninayoyasema.

.........."Siku ile sikukudanganya, ni kweli tulikuwa kwa shangazi yake" Jack alijitutumua kujibu.

..........."Usinifanye mtoto Jack, najua umeanza kutembea na rafiki yangu Idris, hata sahizi umetoka huko kwa Idris" Niliongea huku hasira zimenipanda. Sio siri hakuna swala linalouma kama kuibiwa mke/ mume. Tena ni heri akachepuke na watu wa mbali, kuliko kuchepuka na mtu wako wa karibu, mtu ambae tatizo lako ni lake, na tatizo lake ni lako.INAUMA

............"Hiyo rosheni uliyoipaka ni ya Idris, naijua vizuri na inauzwa bei ghali, inaitwa " Crème de la Mer", Idris aliagiza kutoka Afrika kusini. Kwahiyo baada ya kufanya ufuska wako, ukaamua kuoga na kuipaka" Niliongea kwa uchungu huku nikiwa nimemsogelea ili nimshushie kipigo cha paka mwizi.

............"Kabla sijaanza kukuchakaza hapa naomba unijibu hili swali, umeanza lini kulala na huyo mjinga mwenzako" nilimuuliza huku ningali nimemshika mikono.
Hakujibu kitu bali alikuwa ananiangalia tu

........"Kwahiyo umegoma kujibu" nilimuuliza.

........."Hata nikikujibu haina maana. Nishakutana na rijali anayejua kunikuna" Jack alinijibu kwa dharau.

Hili jibu lake liliniumiza sana, sijui hata ilikuwaje ila ninachokumbuka ni kwamba nilimpiga mtama akaanguka chini, nikamuinua tena na kuanza kumpiga vibao. Nikaona haitoshi nikavua mkanda wa suruali yangu na kuanza kumcharaza huku nikimuuliza "Kwanini hukuniambia mapema kama huna malengo ya kimaisha na mimi?, kwa nini ulikubali hadi tufunge ndoa ndipo unioneshe haya madudu yako?, kwanini umenipotezea muda wangu wewe shetani?' Niliongea sana huku nikimpiga.


USHAURI

Ukimfumania mkeo/ mumeo au ukibaini kuwa amekusaliti, huna haja ya kumpiga, kumjeruhi wala kumdhuru kwa namna yoyote ile. Kuachana nae kwa amani au kupotezea juu ya hilo tukio ni jambo la hekima sana kuliko kujifanya una hasira za karibu. Wengi wapo Jela, wanajilaumu kwa maamuzi ya kuua/kujeruhi wake zao, kuua/kujeruhi waume zao, kuua/kujeruhi michepuko ya wake/waume zao. Usipoteze uhuru wako kwa hasira za kijinga. Ndio ni hasira za kijinga, kumuua/kumjeruhi ni ujinga kwa kiwango cha 'Standadi geji (Standard gauge)'. JOHNSON NAJUTIA KUMPIGA JACKLINE.

Nakumbuka nilimpiga sana Jackline kwa muda mrefu hadi mlinzi wetu wa getini akaja kuamulia. Nikiwa bado nina hasira nilichukua gari langu,nikaliwasha na kuelekea kwa Idris. Njiani niliendesha kama kichaa, spidi niliyokuwa naitumia haikuwa nzuri kwa afya, niliona gari halikimbii kabisa wakati mimi nina hamu ya kumuwahi huyu mjinga anayevamia wake za watu. Ila baada ya dakika kumi nilikuwa nimefika nyumbani kwa Idris.

Mlinzi wa getini alinifungulia geti, maana alikuwa akinifahamu vizuri. Niliingia hadi ndani, nikapark gari langu sehemu ya parking na kuelekea mlango mkuu wa kuingilia ndani sebuleni. Mlango ulikuwa umefungwa. Nikapiga hodi zaidi ya mara kumi ila haukufunguliwa. Nikajaribu kumpigia simu Idris nayo haikupokelewa. Nikaelekea kwa mlinzi na kumuuliza kama Bosi wake yupo, alinijibu kuwa ndio yuko ndani. Nikarudi tena pale mlangoni na kuanza kupiga hodi upya, ila hakuna jibu lolote nililolipata. Kumbe kipindi ninatoka nyumbani, Jackline alimpigia Idris simu na kumueleza kuwa niko njiani naelekea kwake, kwahiyo ajiandae. Kwahiyo Idris aliujua kabisa ujio wangu pale kwake hata kabla sijaikaribia nyumba yake. Nilipoona mlango umefungwa kwa ndani, nikaamua kutumia nguvu kuufungua ili hata kama ikishindikana basi niuvunje kabisa.

Kitendo cha mke wangu, tena wa ndoa kutembea na rafiki yangu Idris kiliniuma sana. Nilitaka nimuoneshe adabu Idris ikiwezekana nimpe hata ukilema ili mradi ajutie kwa ujinga alioufanya na mke wangu. Wakati nikiwa naendelea kuhangaika na ule mlango, ghafla askari polisi wanne waliingia pale getini na kunifuata huku wameshika mitutu ya bunduki. Akili yangu iliganda ghafla mara baada ya kuwaona. Walinisogelea na kuniamuru nipige magoti. Nikatii amri yao. Askari mmoja kati ya wale wanne alinisogelea na kunipiga kitako cha bunduki maeneo ya kichwani. Ghafla nikapoteza fahamu. Sikujua kilichoendelea tena kwenye huu uso wa dunia.

TUKUTANE TENA SEHEMU INAYOFUATA
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com



SEHEMU YA TISA

MKONZE-NJE YA MJI WA DODOMA

Ni majira ya saa mbili usiku, sauti kali za kubishana zinasikika kwenye nyumba moja kuukuu. Mwanaume akimlaumu mwanamke wake kwa kuvunja makubaliano na mwanamke nae akimlaumu mwanaume wake kwa kutaka mambo ya haraka haraka.

............"We mwanaume gani, umejawa na gubu kama mtoto wa kike, nimeshakwambia haya yote nayafanya kwa manufaa yetu. Bado unalaumu tu, ntakuacha mimi". Ilikuwa ni sauti ya mwanamke.

........"Haaaa, unadhani mi naogopa kuachwa, we niache, wala sitoumia. Ila sitoweza kuvumilia tena huu ujinga wako. Nilikuruhusu ulale na yule boya wako kwa ajili ya faida yetu sote, ila wewe naona badala ya kufanya kilichokupeleka kule, umeamua ukapotee mazima" Mwanaume nae aliwaka kwa hasira.

..........."Kwahiyo ulitaka nitembee nae leo alafu kesho niwe nimekamilisha mipango. Mambo hayaendi hivyo. We nipe mwezi mmoja zaidi" Mwanamke aliongea.

.........."Hujielewi wewe mwanamke, kwahiyo miezi mitatu niliyokupatia umeona haitoshi, unataka nikuongezee tena mwezi mmoja. Hivi unajua Roida ni kiasi gani mimi naumia?". .mwanaume alizidi kulaumu.

............"Sikia Devi, mimi nakupenda sana mpenzi wangu. Ila kama kweli unataka tufanikishe hili jambo basi nipe tena japo mwezi mmoja tu. Baada ya hapo tutaishi kama zamani. Kuwa muelewa my hubby to be". Roida alishusha sauti yake na kuanza kum'bembeleza mpenzi wake huyo aitwae David.

........."Basi hakikisha huo mwezi mmoja tu ukiisha uwe umekamilisha kila kitu, haya maisha ya kimasikini siyataki tena. Pia kuwa mbali na wewe ni mateso kwangu. Naomba ulielewe hilo". David nae alishusha hasira zake.

........."Usijali laazizi wangu, mimi na wewe dam dam. Ngoja tulikamilishe hili tuanze kutengeneza familia yetu. Tabasamu basi, au bado umenuna". Roida aliendelea kumtuliza wa ubani wake.

Hakika wapendanao wakigombana, shika jembe ukalime. Katika hali ya kawaida ilikuwa ni ngumu sana kuamini kwamba wapenzi hawa wangefikia muafaka, ila ndo hivyo sahizi ndo kwanza wamekumbatiana pale kitandani huku wakipeana mahaba mazito, ugomvi wote umeisha. Mapenzi bwana.


KIJIJINI SENG'WA-MASWA MKOANI SIMIYU

......."Luhende, ntulilege simu unyanda oko umwile nagusadaga gete (Luhende, mpigie simu mdogo wako, mwambie naumwa sana)". Ilikuwa ni sauti ya Mama Singu au ukipenda muite Mama Johnson akimuelekeza mwanae wa kwanza kwa jina la Luhende. Sauti hii ilisikika ndani ya nyumba moja pale kijijini iliyojengwa kwa tofali za kuchomwa na kuezekwa bati. Ni nyumba chache sana pale kijijini zenye muonekano kama wa nyumba ya Mama Singu.




Nyumba ya Mama Singu ni miongoni mwa nyumba chache pale kijijini zilizojengwa kwa tofali za kuchoma na kuezekwa bati.

......."Ila mama nekege duhu usingu aendelee na kaji dudidumwinha presha ule, ila ulu uzidiwa dugumwila ize (Ila mama, tumuache Singu aendelee na kazi, tutampa presha bure. Ila ukizidiwa tutamtaarifu aje)". Luhende alimjibu mama ake ambae alikuwa amedhoofu kitandani. Wajukuu zake wapatao kumi nao walikuwa wamemzunguka pale kitandani.

............"Sawa mwanone, nisebhejege ubugota bhone namwe (Sawa mwanangu, nichemshie dawa yangu ninywe)" Mama Singu aliitikia nakumpa maelekezo mwanae huku akijitahidi kugeukia ubavu wa pili.

Luhende ni baba wa watoto watano. Yeye pamoja na mkewe Bhoke, walikuwa wakiishi kijiji cha jirani. Ila baada ya mama kuzidiwa na uzee pamoja na homa za hapa na pale ilim'bidi kurudi tena kwa mama yeye na familia yake yote ili kumuhudumia. Pia Luhende ana wadogo zake wawili Ngasa (Mtoto wa pili kuzaliwa) na Singu "Johnson" ambae ni mtoto wa tatu na wa mwisho katika familia ya mzee Mabula. Ngasa yeye alihamaga pale kijijini miaka mingi sana iliyopita yeye na mkewe na kuelekea Mkoani tabora ambapo alikuwa akijishughulisha na ufugaji. Singu nae yupo Dodoma kikazi. Kama ilivyo kwa Singu (Johnson), Sanga nae kila akipata muda alikuwa akija kumtembelea mama yao.

Shughuli za kilimo na ufugaji ndizo zilizokuwa zikitoa uhai kwa familia hii na wanakijiji wengine pale kijijini.

Luhende alimuagiza mtoto mmoja akachemshe dawa ya mitishamba, baada ya kuchemshwa dawa ililetwa na Mama Luhende aliipokea na kuinywa.


........."Haya, humu ndani wote ondokeni. Muacheni bibi apumzike". Luhende au ukipenda muite 'Baba milembe' aliongea na kuwataka watoto wote mule ndani wanyanyuke na kwenda kucheza.
Watoto nao wakatii amri, wakanyanyuka na kuondoka. Wakamuacha Baba yao pamoja na Bibi..

............" Mama naomba uniambie ulichotaka kuzungumza muda ule. Ni kweli mimi si mtoto wa baba yangu Mzee Mabula?" Luhende aliuliza.

..........."Ni kweli, Mzee Mabula sio baba yako Mzazi. Ila unayemuita Baba mdogo ndie huyo sasa Baba yako mzazi" Mama aliongea kwa tabu huku akivuta pumzi kwa nguvu.

..........."Mama, kwanini hukuniambia tangu zamani?. Mimi nilichokuwa nakifahamu ni kwamba mtoto ambae sio wa Mzee Mabula ni Singu peke yake, sikujua kama na mimi si mtoto wa Mzee Mabula, kwanini ulifanya hivi mama?". Luhende aliuliza.

.........."Ni stori ndefu mwanangu, ila nikwambie tu ukweli, mimi nililazimishwa tu kuolewa na huyu Baba yenu, kwahiyo sikumpenda kabisa. Na sikuwa tayari kumzalia mtoto hata mmoja". Mama Luhende alieleza.

............"Kwahiyo hata Ngasa si mtoto wa Mzee Mabula?". Luhende aliuliza.

.........."Ni Ngasa pekee ndie mtoto wa mze Mabula, ila nyie wawili muliobaki si watoto wake". Mama Luhende alijibu kwa kifupi huku akikohoa.

.........."Ila baba kabla hajafa alikuwa akijua kama mimi si mtoto wake?".Luhende aliuliza tena.

........."Alikuja kujua mwishoni kabisa kabla hajafariki, nilimueleza kila kitu" . Mama Luhende alitoa ufafanuzi.

............" Na pia ulisema utanieleza kuhusu ugonjwa wa baba" Luhende alikumbushia.

............"Bila shaka unakumbuka kipindi kile Baba yako alipovamiwa kule shambani na kupigwa na watu wasiojulikana hadi kuzimia na hatimae mwisho wa siku akapata kiharusi". Mama Luhende alikumbushia tukio la kujeruhiwa mzee mabula.

............"Ndio nakumbuka, kipindi kile alipovamiwaga na majambazi wakampiga hadi akazimia. Mzee Nyanda ndie aliyemkuta kule shambani akiwa hajitambui, akaja kuita watu hapa kijijini wakaelekea kum'beba" Luhende alijibu.

..........."Ni tamaa tu ya mali. Ni mimi na Baba yako mdogo (ambae ndie baba yako mzazi) tulishirikiana kumdhuru Mzee Mabula kwa kuwakodi watu kutoka kijiji cha Itilima, ambao walimpiga hadi kuzimia. Alipigwa sana maeneo ya kichwani. Alilazwa hospitalini miezi saba. Alipotoka akawa amepalalaizi baadhi ya viungo vyake" Mama Luhende alieleza huku akitokwa na machozi.

.............."Mama, yani wewe na Bamdogo ndo mlishirikiana kumdhuru baba?, kwa kosa gani alilowatendea hadi mukafikia kuchukua hatua hiyo?". Luhende aliuliza huku nae mifereji ya machozi ikianza kutengenezwa usoni mwake.

..........."Munisamehe sana wanangu, ndio maana nataka umuite Singu na Ngasa waje hapa niwaombe msamaha wanangu" Mama Luhende alizidi kulia huku akijutia kosa lake.

Mazungumzo yaliishia pale baada ya Luhende kutoka nje kwa hasira huku machozi yakimtiririka mashavuni.

USHAURI

Mwanaume/mwanamke, epuka kulazimisha mapenzi, epuka kulazimisha kupendwa. Ukiona hupendwi ondoka, usilazimishe. Wengi wamepata ukilema, wengi wamefirisika na wengi wamekufa kwa kulazimisha kupendwa. Usilazimishe kujenga nyumba kwenye mkondo wa mto.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com


SEHEMU YA KUMI

Kituo kikuu cha polisi-Dodoma

..........."Mungu wangu, kazi ya Bosi. Haaaa kazi ya Bosi, mamaaa kazi ya Bosi sijaifanya. Aah aah aah, nitajieleza nini mimi?", hakika nilipagawa haswa, sikujali kama mahabusu wenzangu walikuwa wakiniangalia ama la, nilizidi kujiongelesha peke yangu ndani ya chumba cha selo na kukaa kitako. Nilikumbuka kuwa nilipewa majukumu na Bosi wangu ya kuimaliza kazi ya kuandaa nyaraka mbalimbali katika kompyuta. Ni kazi niliyotakiwa kuifanya ndani ya siku tatu tu kisha niikabidhi kwake. Ila leo ni siku ya tatu tangu niondoke pale nyumbani. BALAA



.........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliita mara ya kwanza kwenye selo ya mahabusu wanaume.

..........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliiita mara ya pili.

..........."Nipo Afande", nilikurupuka ghafla kutoka kwenye lindi la mawazo. Nliitika kwa nguvu baada ya kusikia jina langu likiitwa. Ni takribani siku mbili zilipita tangu nilipopoteza fahamu kule kwa yule mjinga aliyeniibia mke, ila ni siku tatu zimepita tangu niondoke nyumbani kwangu. Kama ulikimbia hesabu basi hautojua ni siku ipi nilizinduka.

............"Hebu kuja huku nje upesi", yule afande aliongezea.
Nilikurupuka mahali nilipokaa na kuelekea kwenye geti la mahabusu, afande alilifungua geti na mimi nikapita. Tulielekea moja kwa moja kwenye chumba fulani ambapo niliwakuta maafande watatu na rafiki yangu Godfrey. Godfrey alikuja kuniwekea dhamana.

............"Yani lijitu linajiita 'Nzagamba' (Ng'ombe dume) ila halina hata hadhi ya kuwa 'Mbogoma' (Ng'ombe jike)", afande mmoja kati ya wale watatu aliongea kwa ukali huku akiniangalia punde nilipoingia.

........."Unatutunishia misuli eeh, afande anaongea huku wewe umesimama. Adabu ya wapi hii" Afande mwingine alidakia huku akinisukuma ili nichuchumae. Nilitii amri, nikachuchumaa huku wao wangali wamesimama.

.........."Unamfahamu huyu aliyeko mbele yako?" Afande mwenye cheo kikubwa kushinda wote kati ya wale watatu ambae alikuwa kimya tangu niingie pale aliniuliza.

........."Ndio namfahamu. Ni mfanyakazi mwenzangu. Anaitwa Godfrey Haule" nilimjibu kwa kirefu. Kabla hata sijakaa vizuri, nilipigwa kofi la mgongoni na afande mwingine mwenye cheo cha "Koplo"

............"Jibu swali uliloulizwa, acha kiherehere cha kujifanya unajua kujieleza", aliongezea.

Yule afande mwenye cheo kikubwa hata hakuonesha kujali tukio la mimi kupigwa kibao cha mgongoni, bali aliendelea kuzungumza.
........"Amekuja kukudhamini, na taratibu zote amekamilisha. Tunakuachia urudi mtaani ila kwa shariti moja, acha vurugu. Ukiletwa tena hapa utajuta"

.........."Ndio afande nimekuelewa" nilimjibu. Baada ya mazungumzo hayo mafupi tulitoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo kulikuwa na vitu vyangu vilivyohifadhiwa pale siku nilipoletwa. Niliacha simu janja(Smartphone), saa, na waleti yangu. Kila kitu kilikuwa kimehifadhiwa vizuri na hakuna kilichopotea. Nilichukua vitu vyangu na kuruhusiwa kutoka nje ya kituo kile. Na kwa majira ilikuwa ni saa saba na ushee mchana.

.........."Pole sana kaka kwa matatizo yaliyokukuta, changamoto ni sehemu ya maisha" Godfrey alianzisha mazungumzo punde tulipoingia kwenye gari lake.

..........."Ahsante ndugu yangu, nimeshapoa. Ulijuaje kama niko kituoni", nilimjibu na kumuuliza swali.

.........."Leo asubuhi Idris amenipa habari zako, amesema ulimpiga mkeo. Mkeo ndo akaamua kuja kukufungulia mashtaka ya kumjeruhi" Godfrey alinijibu huku gari likiwa limeanza kutoka pale kituo cha polisi.

Sikujibu kitu ingawa nilishtuka sana baada ya kusikia kwamba eti mke wangu ndo amenipeleka 'lock-up'. Idris aliamua kumuongopea Godfrey kwa manufaa yapi?. Wakati nakumbuka nilikamatwa na polisi nikiwa nyumbani kwa Idris na yeye bila shaka ndie aliepiga simu polisi. Ila ajabu ni kwamba anasema eti mke wangu 'Jackline' ndie aliyenifungulia mashtaka.

Safari iliendelea tukiwa kimya kabisa ndani ya gari bila kuongeleshana. Safari iliishia kwenye mgahawa mmoja uitwao 'Free Point'. Tulishuka garini na kuelekea ndani ya mgahawa. Tukachagua sehem ya kukaa na hatimae muhudumu alikuja kutuhudumia. Mimi niliagiza wali Sangara na sharubati ya baridi. Godfrey aliagiza chipsi kuku na soda ya Coke.

Mazungumzo yakaanza upya tukiwa tunakula.

..........."Ilikuwaje tena rafiki yangu hadi waifu akaamua kukutupa selo", God aliniuliza.

Nikanyamaza kidogo kisha nikazungumza. "Ni stori ndefu kaka, ila ukweli ni kwamba aliyenitupa selo ni Idris, sio waifu"

.........."Haaaa, mbona munanichanganya sasa. Idris alikutupaje?", God aliuliza.

Ilinibidi nianze kumueleza Godfrey tukio zima tangu siku ya kwanza Roida aliponiomba waondoke na mke wangu ili akapajue kwao hadi siku ya tukio la mimi kumpiga mke wangu.

............."Duuuh, kumbe ndivyo ilivyokuwa?. Sasa Idris na yeye kwa nini aliamua kukufanyia huo unyama wa kutembea na mke wako" Godfrey aliongea kwa masikiti

.........."Daah, ndo hivyo kaka, ila sahizi nikirudi tu hom sitaki tena kumuona huyu mwanamke. Namuacha aendelee na maisha yake. Nimeumia God, inauma sana kugundua kuwa mke wako anatembea na mwanaume mwingine, tena mwanaume mwenyewe ni rafiki yako wa karibu", niliongea huku nikiwa na huzuni.

.........."Vumilia Broo, subiri tufike home alafu tutajua nini cha kufanya", Godfrey aliongea kisha tukaendelea kula. Tulipomaliza kula, Godfrey alilipa bili kisha tukaondoka kuelekea nyumbani kwangu.


NYUMBANI KWA IDRIS

Jackline amelala kwenye sofa na kanga moja tu, ndani hajavaa chochote, huku uso wake akiwa ameuegemeza mapajani mwa Idris. Idris nae anaonekana akimkanda kanda Jackline kwa maji ya moto maeneo ya usoni ambayo yaliumizwa kwa kipigo alichokipata kutoka kwa Johnson.

........"Baby, yule shetani mi simtaki tena. Ona ameniharibu usoni" Jackline aliongea kwa kudeka huku akikaza uso kutokana na maumivu ya kukandwa.

........."Usijali, tumeshampa adhabu yake. Atakaa mahabusu kwa siku tatu ndipo ataachiwa. Nishaongea na rafiki yangu ambae anafahamiana na mkuu wa kituo wa pale" Idris alimfariji Jackline huku akiwa amemaliza zoezi lake la kumkanda.

........"Ila honey, sio siri nahisi furaha sana kuwa na wewe kuliko kukaa na yule mjinga asiyejua mapenzi. Naomba uwe wangu Idris, nakupenda sana", Jack aliendelea kuzungumza huku akimkumbatia Idris.

.........."Usijali, mimi ni wako. Nakupenda pia", Idris alijibu.

.........."Vipi kuhusu Roida, naomba umuache ili uwe na mimi. Sitaki uendelee nae", Jackline aliongea.

.........."Usijali, Roida ntamuacha 'soon'. Nipe mwezi mmoja tu nitakuwa nimemuacha", Idris alijibu.

........."Poa honey, nakupenda sana", Jack alijibu huku akisimama na kupeleka mdomo wake kwenye papi(lips) za Iddy, nae Iddy akausogeza mdomo wake na kukutanisha na papi(lips) za Jack na kuanza kubadilishana mate.

Zoezi halikukomea hapo, Idris akaanza kuupeleka mkono wake taratibu maeneo ya ikulu ya Jackline ambapo palikuwa hakuna kufuli na kuanza kumsugua sugua kwa vidole vyake. Mkono mwingine nao ulikuwa na jukumu la kuminya minya matiti malaini ya mlimbwende huyu.
Jack nae hakuwa nyuma kwenye kujibu mapigo, palepale sofani, akajipinda kama nyoka na kuanza kufungua zipu ya suruali ya Idris, akamtoa babu wa Idris na kuanza kumchezea chezea huku akimsifia Idris kwa kubalikiwa kuwa na Dudu kubwa, mara tatu zaidi ya kibamia cha mume wake 'Johnson'

Baada ya dakika kumi zoezi likabadilika na maangamizi yakaanza rasmi. Jack alishusha mguu mmoja chini ya sofa, na mwingine aliupandisha juu ya sofa, kanga ikaanguka na kusababisha kabibi kake kalikonyolewa vizuri kuonekana. Hakika Jack ameumbika, titi zake ndogo zilizosimama vizuri, pamoja na ta***k lake kubwa vilimfanya avutie zaidi. Idris alivua suruali na boksa na kujilaza chali huku akipitisha mguu mmoja katikati ya miguu ya jackline na mwingine ukiwa pembeni kidogo. Sasa wakawa wanaangaliana. Jack yuko juu na Idris yuko chini. Jack alimchukua babu wa idris na kumuingiza ndani ya bibi wake. Hakika alikuwa amelowa haswa. Ni kelele tu na staili mbali mbali ndizo zilikuwa zikishuhudiwa ndani ya ile sebule.
(SIJUI KILICHOENDELEA)




OFISINI

............"Zainabu, naomba unichapishie hii barua, alafu udurufu nakala kadhaa, uziwasilishe kwa kila mkuu wa Idara ukiwaeleza kuwa JOHNSON ALFREDY NZAGAMBA sio msimamizi tena wa Idara zote hapa ofisini na wala si mfanyakazi tena wa ofisi hii. Kanitia aibu sana huyu kijana. Mimi nitaenda kuieleza nini leo Bodi ya wakurugenzi. Shenzi kabisa huyu. Na sitaki kumuona akikanyaga hapa", Bosi alifoka kwa hasira huku akimkabidhi katibu muhtasi wake karatasi aliyoiandika kwa mkono ili aichape kwa mashine na kudurufu nakala kazaa.

..........."Sawa Bosi nimekuelewa. Naichapa sahizi", Zainabu alitii amri ya Bosi wake na kuipokea ile karatasi.

Bosi alirudi ndani ya ofisi yake huku akimuacha Zainabu akiandaa nakala. Bosi alifura kwa hasira. Hakujua ataenda kuwaeleza nini wajumbe wenzake katika mkutano wa bodi ambao ulitakiwa kufanyika siku hii ya Alhamis. Kazi aliyompati Johnson ndio kazi iliyokuwa ikisubiriwa kujadiliwa na wajumbe wengine katika kikao cha bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma Mtambuka serikali (WVHM) tawi la Dodoma Jiji.


Ofisi anayofanyia kazi Johnson inahusika na Uzabuni wa kutoa huduma za ununuzi wa vifaa na huduma mtambuka serikalini (VHM) ambayo inafanya kazi chini ya "Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA). Kwahiyo ofisi yao inajukumu la kutafuta tenda mbalimbali zinazotolewa na serikali kwenye miradi mbalimbali kuanzia ukandarasi wa barabara, madaraja, majengo na huduma za Taasisi nyingine za umma na pia kununua vifaa na nyezo hitajika katika miradi husika.


KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI (WVHM)

Mwenyekiti wa bodi ya chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma mtambuka serikalini (WVHM) Jiji la Dodoma, Mr Abbas Jamal alifungua kikao kwa kutoa salamu na kuelezea majukumu ya chama chao, mafanikio, changamoto, malengo na matarajio ya chama. Hatimae akamkaribisha karani wa chama ambae alieleza shughuli zote zilizofanywa na chama yakiwamo mapato na matumizi ya chama. Baada ya maelezo hayo mafupi alikaribishwa katibu wa chama, Mr Hassan Msangi (Bosi wake Johnson). Kwanza alianza kusifia maendeleo ya chama chao na kusisitiza mshikamo wa wajumbe ndani ya chama katika kutatua changamoto mbalimbali.

Baada ya maelezo yake ya utangulizi, akaingia sasa katika lengo kuu la kikao kile ambalo ni kujadili nyaraka zinazohusu tathmini ya manunuzi na mahitaji ya rasilimali vitu na watu katika mradi mkubwa wa nyumba za Serikali Dodoma.

........."Kwanza kabisa ningependa kuchukua nafasi hii kuwaomba msamaha kwa mara ya pili wajumbe wenzangu. Niliwaahidi kuwa hadi kufikia leo zile nyaraka za makadilio na tathmini za ununuzi wa vifaa na rasilimali watu za nyumba za serikali hapa Dodoma ningeziwasilisha leo", Mr Hassan Msangi alitoa ufafanuzi kisha akanyamaza kidogo kuwapa nafasi ya kutafakari wajumbe wenzake, kisha akaendelea.

.........."Kwa bahati mbaya ni kwamba, yule kijana mchapakazi tuliyemtarajia akamilishe zile nyaraka amepatwa na matatizo tena. Kuna changamoto za kifamilia zilipelekea kuwekwa mahabusu hadi muda huu ninapoongea hapa. Nami ndo nimepata taarifa za yeye kuwa mahabusu leo hii asubuhi", Mr Hassan alimalizia kwa kuomba tena msamaha.

......."Haiwezekani, hii ni mara ya pili unatuletea hapa ngonjera zako, unajua ni bilioni ngapi tunaenda kupoteza kwa uhuu upuuzi wako, lete nyaraka hapa" mjumbe mmoja alifoka kwa hasira baada ya kusikia Mr. Hassan Msangi hajaleta nyaraka za tathmini.

..........."Hapa Mr. Hassan lazima uvuliwe nyadhifa zako zote ndani ya chama, wewe unatuletea ujinga. Watu tumekopa mamilioni ya fedha kwa ajili ya huu mradi alafu wewe unaleta habari gani hizi", mjumbe mwingine alidakia.
Hakika kikao kilitibuka baada ya Mr. Hassan(Bosi wa Johnson) kutoleta nyaraka za tathmini. Baada ya vurugu na matusi kupamba moto, mwenyekiti alisimama na kuomba watu watulie. Hatimae wakapiga kura ya kutokuwa na imani na katibu wao, Mr. Hassan Msangi.

Mr. Hassan Msangi akavuliwa rasmi ukatibu wa chama na kupigwa marufuku ya kutohudhuria wala kushiriki shughuli zozote za chama kwa takribani miezi mitatu. Majukumu ya kuandaa nyaraka alipatiwa mtu mwingine na kikao kikafungwa rasmi.


*****************************************************

.........."Johnson, the son of Bitch, I must kill you, naapia lazima nikufyekelee mbali. Lazima ulipe kwa hii dharau niliyofanyiwa na wajumbe wenzangu. Nitakuuaaaaaaaaa", yalikuwa ni maneno ya Mr. Hassan aliyoyatamka kwa hasira punde alipoingia garini kutoka kwenye kikao.


*Johnson ameachishwa kazi

*Johnson anasakwa auawe kwa hasara aliyomsababishia Bosi wake Mr. Hassan

*Jackline anataka Idris amuache Roida

*Idris anakihitaji cheo cha Johnson kwa udi na uvumba.



JE, NINI KITAENDELEA.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA.
 
Mara ya kwanza nilidharau kusoma lkn kumbe hii nayo ni simulizi na elimu tosha na haya ndo maisha tunayoyaishi ktk dunia ya sasa asante sana ndg ulieleta hii elimu yenye uchungu ndani yake
 
Mara ya kwanza nilidharau kusoma lkn kumbe hii nayo ni simulizi na elimu tosha na haya ndo maisha tunayoyaishi ktk dunia ya sasa asante sana ndg ulieleta hii elimu yenye uchungu ndani yake
Tuko pamoja. Endelea kuelimika
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com


SEHEMU YA KUMI

Kituo kikuu cha polisi-Dodoma

..........."Mungu wangu, kazi ya Bosi. Haaaa kazi ya Bosi, mamaaa kazi ya Bosi sijaifanya. Aah aah aah, nitajieleza nini mimi?", hakika nilipagawa haswa, sikujali kama mahabusu wenzangu walikuwa wakiniangalia ama la, nilizidi kujiongelesha peke yangu ndani ya chumba cha selo na kukaa kitako. Nilikumbuka kuwa nilipewa majukumu na Bosi wangu ya kuimaliza kazi ya kuandaa nyaraka mbalimbali katika kompyuta. Ni kazi niliyotakiwa kuifanya ndani ya siku tatu tu kisha niikabidhi kwake. Ila leo ni siku ya tatu tangu niondoke pale nyumbani. BALAA



.........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliita mara ya kwanza kwenye selo ya mahabusu wanaume.

..........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliiita mara ya pili.

..........."Nipo Afande", nilikurupuka ghafla kutoka kwenye lindi la mawazo. Nliitika kwa nguvu baada ya kusikia jina langu likiitwa. Ni takribani siku mbili zilipita tangu nilipopoteza fahamu kule kwa yule mjinga aliyeniibia mke, ila ni siku tatu zimepita tangu niondoke nyumbani kwangu. Kama ulikimbia hesabu basi hautojua ni siku ipi nilizinduka.

............"Hebu kuja huku nje upesi", yule afande aliongezea.
Nilikurupuka mahali nilipokaa na kuelekea kwenye geti la mahabusu, afande alilifungua geti na mimi nikapita. Tulielekea moja kwa moja kwenye chumba fulani ambapo niliwakuta maafande watatu na rafiki yangu Godfrey. Godfrey alikuja kuniwekea dhamana.

............"Yani lijitu linajiita 'Nzagamba' (Ng'ombe dume) ila halina hata hadhi ya kuwa 'Mbogoma' (Ng'ombe jike)", afande mmoja kati ya wale watatu aliongea kwa ukali huku akiniangalia punde nilipoingia.

........."Unatutunishia misuli eeh, afande anaongea huku wewe umesimama. Adabu ya wapi hii" Afande mwingine alidakia huku akinisukuma ili nichuchumae. Nilitii amri, nikachuchumaa huku wao wangali wamesimama.

.........."Unamfahamu huyu aliyeko mbele yako?" Afande mwenye cheo kikubwa kushinda wote kati ya wale watatu ambae alikuwa kimya tangu niingie pale aliniuliza.

........."Ndio namfahamu. Ni mfanyakazi mwenzangu. Anaitwa Godfrey Haule" nilimjibu kwa kirefu. Kabla hata sijakaa vizuri, nilipigwa kofi la mgongoni na afande mwingine mwenye cheo cha "Koplo"

............"Jibu swali uliloulizwa, acha kiherehere cha kujifanya unajua kujieleza", aliongezea.

Yule afande mwenye cheo kikubwa hata hakuonesha kujali tukio la mimi kupigwa kibao cha mgongoni, bali aliendelea kuzungumza.
........"Amekuja kukudhamini, na taratibu zote amekamilisha. Tunakuachia urudi mtaani ila kwa shariti moja, acha vurugu. Ukiletwa tena hapa utajuta"

.........."Ndio afande nimekuelewa" nilimjibu. Baada ya mazungumzo hayo mafupi tulitoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo kulikuwa na vitu vyangu vilivyohifadhiwa pale siku nilipoletwa. Niliacha simu janja(Smartphone), saa, na waleti yangu. Kila kitu kilikuwa kimehifadhiwa vizuri na hakuna kilichopotea. Nilichukua vitu vyangu na kuruhusiwa kutoka nje ya kituo kile. Na kwa majira ilikuwa ni saa saba na ushee mchana.

.........."Pole sana kaka kwa matatizo yaliyokukuta, changamoto ni sehemu ya maisha" Godfrey alianzisha mazungumzo punde tulipoingia kwenye gari lake.

..........."Ahsante ndugu yangu, nimeshapoa. Ulijuaje kama niko kituoni", nilimjibu na kumuuliza swali.

.........."Leo asubuhi Idris amenipa habari zako, amesema ulimpiga mkeo. Mkeo ndo akaamua kuja kukufungulia mashtaka ya kumjeruhi" Godfrey alinijibu huku gari likiwa limeanza kutoka pale kituo cha polisi.

Sikujibu kitu ingawa nilishtuka sana baada ya kusikia kwamba eti mke wangu ndo amenipeleka 'lock-up'. Idris aliamua kumuongopea Godfrey kwa manufaa yapi?. Wakati nakumbuka nilikamatwa na polisi nikiwa nyumbani kwa Idris na yeye bila shaka ndie aliepiga simu polisi. Ila ajabu ni kwamba anasema eti mke wangu 'Jackline' ndie aliyenifungulia mashtaka.

Safari iliendelea tukiwa kimya kabisa ndani ya gari bila kuongeleshana. Safari iliishia kwenye mgahawa mmoja uitwao 'Free Point'. Tulishuka garini na kuelekea ndani ya mgahawa. Tukachagua sehem ya kukaa na hatimae muhudumu alikuja kutuhudumia. Mimi niliagiza wali Sangara na sharubati ya baridi. Godfrey aliagiza chipsi kuku na soda ya Coke.

Mazungumzo yakaanza upya tukiwa tunakula.

..........."Ilikuwaje tena rafiki yangu hadi waifu akaamua kukutupa selo", God aliniuliza.

Nikanyamaza kidogo kisha nikazungumza. "Ni stori ndefu kaka, ila ukweli ni kwamba aliyenitupa selo ni Idris, sio waifu"

.........."Haaaa, mbona munanichanganya sasa. Idris alikutupaje?", God aliuliza.

Ilinibidi nianze kumueleza Godfrey tukio zima tangu siku ya kwanza Roida aliponiomba waondoke na mke wangu ili akapajue kwao hadi siku ya tukio la mimi kumpiga mke wangu.

............."Duuuh, kumbe ndivyo ilivyokuwa?. Sasa Idris na yeye kwa nini aliamua kukufanyia huo unyama wa kutembea na mke wako" Godfrey aliongea kwa masikiti

.........."Daah, ndo hivyo kaka, ila sahizi nikirudi tu hom sitaki tena kumuona huyu mwanamke. Namuacha aendelee na maisha yake. Nimeumia God, inauma sana kugundua kuwa mke wako anatembea na mwanaume mwingine, tena mwanaume mwenyewe ni rafiki yako wa karibu", niliongea huku nikiwa na huzuni.

.........."Vumilia Broo, subiri tufike home alafu tutajua nini cha kufanya", Godfrey aliongea kisha tukaendelea kula. Tulipomaliza kula, Godfrey alilipa bili kisha tukaondoka kuelekea nyumbani kwangu.


NYUMBANI KWA IDRIS

Jackline amelala kwenye sofa na kanga moja tu, ndani hajavaa chochote, huku uso wake akiwa ameuegemeza mapajani mwa Idris. Idris nae anaonekana akimkanda kanda Jackline kwa maji ya moto maeneo ya usoni ambayo yaliumizwa kwa kipigo alichokipata kutoka kwa Johnson.

........"Baby, yule shetani mi simtaki tena. Ona ameniharibu usoni" Jackline aliongea kwa kudeka huku akikaza uso kutokana na maumivu ya kukandwa.

........."Usijali, tumeshampa adhabu yake. Atakaa mahabusu kwa siku tatu ndipo ataachiwa. Nishaongea na rafiki yangu ambae anafahamiana na mkuu wa kituo wa pale" Idris alimfariji Jackline huku akiwa amemaliza zoezi lake la kumkanda.

........"Ila honey, sio siri nahisi furaha sana kuwa na wewe kuliko kukaa na yule mjinga asiyejua mapenzi. Naomba uwe wangu Idris, nakupenda sana", Jack aliendelea kuzungumza huku akimkumbatia Idris.

.........."Usijali, mimi ni wako. Nakupenda pia", Idris alijibu.

.........."Vipi kuhusu Roida, naomba umuache ili uwe na mimi. Sitaki uendelee nae", Jackline aliongea.

.........."Usijali, Roida ntamuacha 'soon'. Nipe mwezi mmoja tu nitakuwa nimemuacha", Idris alijibu.

........."Poa honey, nakupenda sana", Jack alijibu huku akisimama na kupeleka mdomo wake kwenye papi(lips) za Iddy, nae Iddy akausogeza mdomo wake na kukutanisha na papi(lips) za Jack na kuanza kubadilishana mate.

Zoezi halikukomea hapo, Idris akaanza kuupeleka mkono wake taratibu maeneo ya ikulu ya Jackline ambapo palikuwa hakuna kufuli na kuanza kumsugua sugua kwa vidole vyake. Mkono mwingine nao ulikuwa na jukumu la kuminya minya matiti malaini ya mlimbwende huyu.
Jack nae hakuwa nyuma kwenye kujibu mapigo, palepale sofani, akajipinda kama nyoka na kuanza kufungua zipu ya suruali ya Idris, akamtoa babu wa Idris na kuanza kumchezea chezea huku akimsifia Idris kwa kubalikiwa kuwa na Dudu kubwa, mara tatu zaidi ya kibamia cha mume wake 'Johnson'

Baada ya dakika kumi zoezi likabadilika na maangamizi yakaanza rasmi. Jack alishusha mguu mmoja chini ya sofa, na mwingine aliupandisha juu ya sofa, kanga ikaanguka na kusababisha kabibi kake kalikonyolewa vizuri kuonekana. Hakika Jack ameumbika, titi zake ndogo zilizosimama vizuri, pamoja na ta***k lake kubwa vilimfanya avutie zaidi. Idris alivua suruali na boksa na kujilaza chali huku akipitisha mguu mmoja katikati ya miguu ya jackline na mwingine ukiwa pembeni kidogo. Sasa wakawa wanaangaliana. Jack yuko juu na Idris yuko chini. Jack alimchukua babu wa idris na kumuingiza ndani ya bibi wake. Hakika alikuwa amelowa haswa. Ni kelele tu na staili mbali mbali ndizo zilikuwa zikishuhudiwa ndani ya ile sebule.
(SIJUI KILICHOENDELEA)




OFISINI

............"Zainabu, naomba unichapishie hii barua, alafu udurufu nakala kadhaa, uziwasilishe kwa kila mkuu wa Idara ukiwaeleza kuwa JOHNSON ALFREDY NZAGAMBA sio msimamizi tena wa Idara zote hapa ofisini na wala si mfanyakazi tena wa ofisi hii. Kanitia aibu sana huyu kijana. Mimi nitaenda kuieleza nini leo Bodi ya wakurugenzi. Shenzi kabisa huyu. Na sitaki kumuona akikanyaga hapa", Bosi alifoka kwa hasira huku akimkabidhi katibu muhtasi wake karatasi aliyoiandika kwa mkono ili aichape kwa mashine na kudurufu nakala kazaa.

..........."Sawa Bosi nimekuelewa. Naichapa sahizi", Zainabu alitii amri ya Bosi wake na kuipokea ile karatasi.

Bosi alirudi ndani ya ofisi yake huku akimuacha Zainabu akiandaa nakala. Bosi alifura kwa hasira. Hakujua ataenda kuwaeleza nini wajumbe wenzake katika mkutano wa bodi ambao ulitakiwa kufanyika siku hii ya Alhamis. Kazi aliyompati Johnson ndio kazi iliyokuwa ikisubiriwa kujadiliwa na wajumbe wengine katika kikao cha bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma Mtambuka serikali (WVHM) tawi la Dodoma Jiji.


Ofisi anayofanyia kazi Johnson inahusika na Uzabuni wa kutoa huduma za ununuzi wa vifaa na huduma mtambuka serikalini (VHM) ambayo inafanya kazi chini ya "Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA). Kwahiyo ofisi yao inajukumu la kutafuta tenda mbalimbali zinazotolewa na serikali kwenye miradi mbalimbali kuanzia ukandarasi wa barabara, madaraja, majengo na huduma za Taasisi nyingine za umma na pia kununua vifaa na nyezo hitajika katika miradi husika.


KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI (WVHM)

Mwenyekiti wa bodi ya chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma mtambuka serikalini (WVHM) Jiji la Dodoma, Mr Abbas Jamal alifungua kikao kwa kutoa salamu na kuelezea majukumu ya chama chao, mafanikio, changamoto, malengo na matarajio ya chama. Hatimae akamkaribisha karani wa chama ambae alieleza shughuli zote zilizofanywa na chama yakiwamo mapato na matumizi ya chama. Baada ya maelezo hayo mafupi alikaribishwa katibu wa chama, Mr Hassan Msangi (Bosi wake Johnson). Kwanza alianza kusifia maendeleo ya chama chao na kusisitiza mshikamo wa wajumbe ndani ya chama katika kutatua changamoto mbalimbali.

Baada ya maelezo yake ya utangulizi, akaingia sasa katika lengo kuu la kikao kile ambalo ni kujadili nyaraka zinazohusu tathmini ya manunuzi na mahitaji ya rasilimali vitu na watu katika mradi mkubwa wa nyumba za Serikali Dodoma.

........."Kwanza kabisa ningependa kuchukua nafasi hii kuwaomba msamaha kwa mara ya pili wajumbe wenzangu. Niliwaahidi kuwa hadi kufikia leo zile nyaraka za makadilio na tathmini za ununuzi wa vifaa na rasilimali watu za nyumba za serikali hapa Dodoma ningeziwasilisha leo", Mr Hassan Msangi alitoa ufafanuzi kisha akanyamaza kidogo kuwapa nafasi ya kutafakari wajumbe wenzake, kisha akaendelea.

.........."Kwa bahati mbaya ni kwamba, yule kijana mchapakazi tuliyemtarajia akamilishe zile nyaraka amepatwa na matatizo tena. Kuna changamoto za kifamilia zilipelekea kuwekwa mahabusu hadi muda huu ninapoongea hapa. Nami ndo nimepata taarifa za yeye kuwa mahabusu leo hii asubuhi", Mr Hassan alimalizia kwa kuomba tena msamaha.

......."Haiwezekani, hii ni mara ya pili unatuletea hapa ngonjera zako, unajua ni bilioni ngapi tunaenda kupoteza kwa uhuu upuuzi wako, lete nyaraka hapa" mjumbe mmoja alifoka kwa hasira baada ya kusikia Mr. Hassan Msangi hajaleta nyaraka za tathmini.

..........."Hapa Mr. Hassan lazima uvuliwe nyadhifa zako zote ndani ya chama, wewe unatuletea ujinga. Watu tumekopa mamilioni ya fedha kwa ajili ya huu mradi alafu wewe unaleta habari gani hizi", mjumbe mwingine alidakia.
Hakika kikao kilitibuka baada ya Mr. Hassan(Bosi wa Johnson) kutoleta nyaraka za tathmini. Baada ya vurugu na matusi kupamba moto, mwenyekiti alisimama na kuomba watu watulie. Hatimae wakapiga kura ya kutokuwa na imani na katibu wao, Mr. Hassan Msangi.

Mr. Hassan Msangi akavuliwa rasmi ukatibu wa chama na kupigwa marufuku ya kutohudhuria wala kushiriki shughuli zozote za chama kwa takribani miezi mitatu. Majukumu ya kuandaa nyaraka alipatiwa mtu mwingine na kikao kikafungwa rasmi.


*****************************************************

.........."Johnson, the son of Bitch, I must kill you, naapia lazima nikufyekelee mbali. Lazima ulipe kwa hii dharau niliyofanyiwa na wajumbe wenzangu. Nitakuuaaaaaaaaa", yalikuwa ni maneno ya Mr. Hassan aliyoyatamka kwa hasira punde alipoingia garini kutoka kwenye kikao.


*Johnson ameachishwa kazi

*Johnson anasakwa auawe kwa hasara aliyomsababishia Bosi wake Mr. Hassan

*Jackline anataka Idris amuache Roida

*Idris anakihitaji cheo cha Johnson kwa udi na uvumba.



JE, NINI KITAENDELEA.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA.
Mkuu hii kitu inazidi kuwa tamu asee daaah bonge la story
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com


SEHEMU YA KUMI

Kituo kikuu cha polisi-Dodoma

..........."Mungu wangu, kazi ya Bosi. Haaaa kazi ya Bosi, mamaaa kazi ya Bosi sijaifanya. Aah aah aah, nitajieleza nini mimi?", hakika nilipagawa haswa, sikujali kama mahabusu wenzangu walikuwa wakiniangalia ama la, nilizidi kujiongelesha peke yangu ndani ya chumba cha selo na kukaa kitako. Nilikumbuka kuwa nilipewa majukumu na Bosi wangu ya kuimaliza kazi ya kuandaa nyaraka mbalimbali katika kompyuta. Ni kazi niliyotakiwa kuifanya ndani ya siku tatu tu kisha niikabidhi kwake. Ila leo ni siku ya tatu tangu niondoke pale nyumbani. BALAA



.........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliita mara ya kwanza kwenye selo ya mahabusu wanaume.

..........."Johnson Alfredy Nzagamba", sauti iliiita mara ya pili.

..........."Nipo Afande", nilikurupuka ghafla kutoka kwenye lindi la mawazo. Nliitika kwa nguvu baada ya kusikia jina langu likiitwa. Ni takribani siku mbili zilipita tangu nilipopoteza fahamu kule kwa yule mjinga aliyeniibia mke, ila ni siku tatu zimepita tangu niondoke nyumbani kwangu. Kama ulikimbia hesabu basi hautojua ni siku ipi nilizinduka.

............"Hebu kuja huku nje upesi", yule afande aliongezea.
Nilikurupuka mahali nilipokaa na kuelekea kwenye geti la mahabusu, afande alilifungua geti na mimi nikapita. Tulielekea moja kwa moja kwenye chumba fulani ambapo niliwakuta maafande watatu na rafiki yangu Godfrey. Godfrey alikuja kuniwekea dhamana.

............"Yani lijitu linajiita 'Nzagamba' (Ng'ombe dume) ila halina hata hadhi ya kuwa 'Mbogoma' (Ng'ombe jike)", afande mmoja kati ya wale watatu aliongea kwa ukali huku akiniangalia punde nilipoingia.

........."Unatutunishia misuli eeh, afande anaongea huku wewe umesimama. Adabu ya wapi hii" Afande mwingine alidakia huku akinisukuma ili nichuchumae. Nilitii amri, nikachuchumaa huku wao wangali wamesimama.

.........."Unamfahamu huyu aliyeko mbele yako?" Afande mwenye cheo kikubwa kushinda wote kati ya wale watatu ambae alikuwa kimya tangu niingie pale aliniuliza.

........."Ndio namfahamu. Ni mfanyakazi mwenzangu. Anaitwa Godfrey Haule" nilimjibu kwa kirefu. Kabla hata sijakaa vizuri, nilipigwa kofi la mgongoni na afande mwingine mwenye cheo cha "Koplo"

............"Jibu swali uliloulizwa, acha kiherehere cha kujifanya unajua kujieleza", aliongezea.

Yule afande mwenye cheo kikubwa hata hakuonesha kujali tukio la mimi kupigwa kibao cha mgongoni, bali aliendelea kuzungumza.
........"Amekuja kukudhamini, na taratibu zote amekamilisha. Tunakuachia urudi mtaani ila kwa shariti moja, acha vurugu. Ukiletwa tena hapa utajuta"

.........."Ndio afande nimekuelewa" nilimjibu. Baada ya mazungumzo hayo mafupi tulitoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo kulikuwa na vitu vyangu vilivyohifadhiwa pale siku nilipoletwa. Niliacha simu janja(Smartphone), saa, na waleti yangu. Kila kitu kilikuwa kimehifadhiwa vizuri na hakuna kilichopotea. Nilichukua vitu vyangu na kuruhusiwa kutoka nje ya kituo kile. Na kwa majira ilikuwa ni saa saba na ushee mchana.

.........."Pole sana kaka kwa matatizo yaliyokukuta, changamoto ni sehemu ya maisha" Godfrey alianzisha mazungumzo punde tulipoingia kwenye gari lake.

..........."Ahsante ndugu yangu, nimeshapoa. Ulijuaje kama niko kituoni", nilimjibu na kumuuliza swali.

.........."Leo asubuhi Idris amenipa habari zako, amesema ulimpiga mkeo. Mkeo ndo akaamua kuja kukufungulia mashtaka ya kumjeruhi" Godfrey alinijibu huku gari likiwa limeanza kutoka pale kituo cha polisi.

Sikujibu kitu ingawa nilishtuka sana baada ya kusikia kwamba eti mke wangu ndo amenipeleka 'lock-up'. Idris aliamua kumuongopea Godfrey kwa manufaa yapi?. Wakati nakumbuka nilikamatwa na polisi nikiwa nyumbani kwa Idris na yeye bila shaka ndie aliepiga simu polisi. Ila ajabu ni kwamba anasema eti mke wangu 'Jackline' ndie aliyenifungulia mashtaka.

Safari iliendelea tukiwa kimya kabisa ndani ya gari bila kuongeleshana. Safari iliishia kwenye mgahawa mmoja uitwao 'Free Point'. Tulishuka garini na kuelekea ndani ya mgahawa. Tukachagua sehem ya kukaa na hatimae muhudumu alikuja kutuhudumia. Mimi niliagiza wali Sangara na sharubati ya baridi. Godfrey aliagiza chipsi kuku na soda ya Coke.

Mazungumzo yakaanza upya tukiwa tunakula.

..........."Ilikuwaje tena rafiki yangu hadi waifu akaamua kukutupa selo", God aliniuliza.

Nikanyamaza kidogo kisha nikazungumza. "Ni stori ndefu kaka, ila ukweli ni kwamba aliyenitupa selo ni Idris, sio waifu"

.........."Haaaa, mbona munanichanganya sasa. Idris alikutupaje?", God aliuliza.

Ilinibidi nianze kumueleza Godfrey tukio zima tangu siku ya kwanza Roida aliponiomba waondoke na mke wangu ili akapajue kwao hadi siku ya tukio la mimi kumpiga mke wangu.

............."Duuuh, kumbe ndivyo ilivyokuwa?. Sasa Idris na yeye kwa nini aliamua kukufanyia huo unyama wa kutembea na mke wako" Godfrey aliongea kwa masikiti

.........."Daah, ndo hivyo kaka, ila sahizi nikirudi tu hom sitaki tena kumuona huyu mwanamke. Namuacha aendelee na maisha yake. Nimeumia God, inauma sana kugundua kuwa mke wako anatembea na mwanaume mwingine, tena mwanaume mwenyewe ni rafiki yako wa karibu", niliongea huku nikiwa na huzuni.

.........."Vumilia Broo, subiri tufike home alafu tutajua nini cha kufanya", Godfrey aliongea kisha tukaendelea kula. Tulipomaliza kula, Godfrey alilipa bili kisha tukaondoka kuelekea nyumbani kwangu.


NYUMBANI KWA IDRIS

Jackline amelala kwenye sofa na kanga moja tu, ndani hajavaa chochote, huku uso wake akiwa ameuegemeza mapajani mwa Idris. Idris nae anaonekana akimkanda kanda Jackline kwa maji ya moto maeneo ya usoni ambayo yaliumizwa kwa kipigo alichokipata kutoka kwa Johnson.

........"Baby, yule shetani mi simtaki tena. Ona ameniharibu usoni" Jackline aliongea kwa kudeka huku akikaza uso kutokana na maumivu ya kukandwa.

........."Usijali, tumeshampa adhabu yake. Atakaa mahabusu kwa siku tatu ndipo ataachiwa. Nishaongea na rafiki yangu ambae anafahamiana na mkuu wa kituo wa pale" Idris alimfariji Jackline huku akiwa amemaliza zoezi lake la kumkanda.

........"Ila honey, sio siri nahisi furaha sana kuwa na wewe kuliko kukaa na yule mjinga asiyejua mapenzi. Naomba uwe wangu Idris, nakupenda sana", Jack aliendelea kuzungumza huku akimkumbatia Idris.

.........."Usijali, mimi ni wako. Nakupenda pia", Idris alijibu.

.........."Vipi kuhusu Roida, naomba umuache ili uwe na mimi. Sitaki uendelee nae", Jackline aliongea.

.........."Usijali, Roida ntamuacha 'soon'. Nipe mwezi mmoja tu nitakuwa nimemuacha", Idris alijibu.

........."Poa honey, nakupenda sana", Jack alijibu huku akisimama na kupeleka mdomo wake kwenye papi(lips) za Iddy, nae Iddy akausogeza mdomo wake na kukutanisha na papi(lips) za Jack na kuanza kubadilishana mate.

Zoezi halikukomea hapo, Idris akaanza kuupeleka mkono wake taratibu maeneo ya ikulu ya Jackline ambapo palikuwa hakuna kufuli na kuanza kumsugua sugua kwa vidole vyake. Mkono mwingine nao ulikuwa na jukumu la kuminya minya matiti malaini ya mlimbwende huyu.
Jack nae hakuwa nyuma kwenye kujibu mapigo, palepale sofani, akajipinda kama nyoka na kuanza kufungua zipu ya suruali ya Idris, akamtoa babu wa Idris na kuanza kumchezea chezea huku akimsifia Idris kwa kubalikiwa kuwa na Dudu kubwa, mara tatu zaidi ya kibamia cha mume wake 'Johnson'

Baada ya dakika kumi zoezi likabadilika na maangamizi yakaanza rasmi. Jack alishusha mguu mmoja chini ya sofa, na mwingine aliupandisha juu ya sofa, kanga ikaanguka na kusababisha kabibi kake kalikonyolewa vizuri kuonekana. Hakika Jack ameumbika, titi zake ndogo zilizosimama vizuri, pamoja na ta***k lake kubwa vilimfanya avutie zaidi. Idris alivua suruali na boksa na kujilaza chali huku akipitisha mguu mmoja katikati ya miguu ya jackline na mwingine ukiwa pembeni kidogo. Sasa wakawa wanaangaliana. Jack yuko juu na Idris yuko chini. Jack alimchukua babu wa idris na kumuingiza ndani ya bibi wake. Hakika alikuwa amelowa haswa. Ni kelele tu na staili mbali mbali ndizo zilikuwa zikishuhudiwa ndani ya ile sebule.
(SIJUI KILICHOENDELEA)




OFISINI

............"Zainabu, naomba unichapishie hii barua, alafu udurufu nakala kadhaa, uziwasilishe kwa kila mkuu wa Idara ukiwaeleza kuwa JOHNSON ALFREDY NZAGAMBA sio msimamizi tena wa Idara zote hapa ofisini na wala si mfanyakazi tena wa ofisi hii. Kanitia aibu sana huyu kijana. Mimi nitaenda kuieleza nini leo Bodi ya wakurugenzi. Shenzi kabisa huyu. Na sitaki kumuona akikanyaga hapa", Bosi alifoka kwa hasira huku akimkabidhi katibu muhtasi wake karatasi aliyoiandika kwa mkono ili aichape kwa mashine na kudurufu nakala kazaa.

..........."Sawa Bosi nimekuelewa. Naichapa sahizi", Zainabu alitii amri ya Bosi wake na kuipokea ile karatasi.

Bosi alirudi ndani ya ofisi yake huku akimuacha Zainabu akiandaa nakala. Bosi alifura kwa hasira. Hakujua ataenda kuwaeleza nini wajumbe wenzake katika mkutano wa bodi ambao ulitakiwa kufanyika siku hii ya Alhamis. Kazi aliyompati Johnson ndio kazi iliyokuwa ikisubiriwa kujadiliwa na wajumbe wengine katika kikao cha bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma Mtambuka serikali (WVHM) tawi la Dodoma Jiji.


Ofisi anayofanyia kazi Johnson inahusika na Uzabuni wa kutoa huduma za ununuzi wa vifaa na huduma mtambuka serikalini (VHM) ambayo inafanya kazi chini ya "Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA). Kwahiyo ofisi yao inajukumu la kutafuta tenda mbalimbali zinazotolewa na serikali kwenye miradi mbalimbali kuanzia ukandarasi wa barabara, madaraja, majengo na huduma za Taasisi nyingine za umma na pia kununua vifaa na nyezo hitajika katika miradi husika.


KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI (WVHM)

Mwenyekiti wa bodi ya chama cha Wazabuni wa Ununuzi wa Vifaa na Huduma mtambuka serikalini (WVHM) Jiji la Dodoma, Mr Abbas Jamal alifungua kikao kwa kutoa salamu na kuelezea majukumu ya chama chao, mafanikio, changamoto, malengo na matarajio ya chama. Hatimae akamkaribisha karani wa chama ambae alieleza shughuli zote zilizofanywa na chama yakiwamo mapato na matumizi ya chama. Baada ya maelezo hayo mafupi alikaribishwa katibu wa chama, Mr Hassan Msangi (Bosi wake Johnson). Kwanza alianza kusifia maendeleo ya chama chao na kusisitiza mshikamo wa wajumbe ndani ya chama katika kutatua changamoto mbalimbali.

Baada ya maelezo yake ya utangulizi, akaingia sasa katika lengo kuu la kikao kile ambalo ni kujadili nyaraka zinazohusu tathmini ya manunuzi na mahitaji ya rasilimali vitu na watu katika mradi mkubwa wa nyumba za Serikali Dodoma.

........."Kwanza kabisa ningependa kuchukua nafasi hii kuwaomba msamaha kwa mara ya pili wajumbe wenzangu. Niliwaahidi kuwa hadi kufikia leo zile nyaraka za makadilio na tathmini za ununuzi wa vifaa na rasilimali watu za nyumba za serikali hapa Dodoma ningeziwasilisha leo", Mr Hassan Msangi alitoa ufafanuzi kisha akanyamaza kidogo kuwapa nafasi ya kutafakari wajumbe wenzake, kisha akaendelea.

.........."Kwa bahati mbaya ni kwamba, yule kijana mchapakazi tuliyemtarajia akamilishe zile nyaraka amepatwa na matatizo tena. Kuna changamoto za kifamilia zilipelekea kuwekwa mahabusu hadi muda huu ninapoongea hapa. Nami ndo nimepata taarifa za yeye kuwa mahabusu leo hii asubuhi", Mr Hassan alimalizia kwa kuomba tena msamaha.

......."Haiwezekani, hii ni mara ya pili unatuletea hapa ngonjera zako, unajua ni bilioni ngapi tunaenda kupoteza kwa uhuu upuuzi wako, lete nyaraka hapa" mjumbe mmoja alifoka kwa hasira baada ya kusikia Mr. Hassan Msangi hajaleta nyaraka za tathmini.

..........."Hapa Mr. Hassan lazima uvuliwe nyadhifa zako zote ndani ya chama, wewe unatuletea ujinga. Watu tumekopa mamilioni ya fedha kwa ajili ya huu mradi alafu wewe unaleta habari gani hizi", mjumbe mwingine alidakia.
Hakika kikao kilitibuka baada ya Mr. Hassan(Bosi wa Johnson) kutoleta nyaraka za tathmini. Baada ya vurugu na matusi kupamba moto, mwenyekiti alisimama na kuomba watu watulie. Hatimae wakapiga kura ya kutokuwa na imani na katibu wao, Mr. Hassan Msangi.

Mr. Hassan Msangi akavuliwa rasmi ukatibu wa chama na kupigwa marufuku ya kutohudhuria wala kushiriki shughuli zozote za chama kwa takribani miezi mitatu. Majukumu ya kuandaa nyaraka alipatiwa mtu mwingine na kikao kikafungwa rasmi.


*****************************************************

.........."Johnson, the son of Bitch, I must kill you, naapia lazima nikufyekelee mbali. Lazima ulipe kwa hii dharau niliyofanyiwa na wajumbe wenzangu. Nitakuuaaaaaaaaa", yalikuwa ni maneno ya Mr. Hassan aliyoyatamka kwa hasira punde alipoingia garini kutoka kwenye kikao.


*Johnson ameachishwa kazi

*Johnson anasakwa auawe kwa hasara aliyomsababishia Bosi wake Mr. Hassan

*Jackline anataka Idris amuache Roida

*Idris anakihitaji cheo cha Johnson kwa udi na uvumba.



JE, NINI KITAENDELEA.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA.
Shukran mkuu.
Kazi nzuri sana.
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com



SEHEMU YA KUMI NA MOJA

Gari nililopanda mimi na Godfrey lilipiga honi karibu na geti la kuingilia nyumbani kwangu. Mlinzi alilifungua geti na gari likaingia moja kwa moja na kuelekea sehemu ya parking.

........"Vipi Jongo, habari za hapa", nilimsalimia mlinzi punde niliposhuka tu garini.

........"Hapa kwema kabisa. Pole kwa matatizo yaliyokupata Bosi wangu", mlinzi aliitikia salamu yangu na kunipa pole.

.........."Nishapoa. Vipi Dada yako yumo ndani?", nilimuuliza.

........"Hapana Bosi, tangu ile siku ya ugomvi wenu, hajaonekana tena hapa. Broo Idris alikuja hapa kumchukua na gari siku ileile", mlinzi alitoa ufafanuzi.

Moyo wangu ulipata ganzi upya. Taarifa ya mke wangu kutokuonekana tena pale nyumbani tangu siku ile tulipokorofishana ilikuwa ni kama shoti ya umeme mwilini mwangu. Tena kibaya zaidi ni kwamba amekuja kuchukuliwa na Idris. "Ina maana Idris ameamua kunitangazia vita hadharani?, kumsaidia kwangu kote kule hadi akafanikiwa kupata kazi ofisini kwetu ndo ameamua kunilipa haya?", niliumia sana moyoni mwangu, ila nikaukumbuka usemi wa waswahili unaosema "TENDA WEMA NENDA ZAKO". Ngoja nami niende zangu.

Nilishapania kuvunja ndoa na Jackline, ila pia niliweka nadhiri moyoni mwangu ya kumsababishia ukilema wa maisha Idris kwa namna yoyote ile. Yes Idris lazima alipie ubaya kwa aliyonitendea. Siwezi kumuacha hivihivi.

Mimi ni mkatoliki mzuri sana, nimepata ubatizo, komunyo na kipeimara, na sheria nyingine nyingi za dini nimetimiza ila hii kauli ya kusema "Akupigae shavu la kushoto, mgeuzie na la kulia" sitaki kuisikia. Sheria yangu mimi ni hii "Akupigae shavu la kushoto, mpige ngumi ya pua. Akumwagiae maji machafu, muogeshe kwa tindikali", yes hiyo ni sheria yangu. Idris lazima aogelee bwawa la tindikali.

Basi baada ya kusikia maelezo kutoka kwa mlinzi, niliongozana na rafiki yangu Godfrey tukaingia sebuleni. Nilimuacha yeye akiangalia luninga, mi nikapitiliza hadi chumbani kwangu ambapo nilivua zile nguo nilizotoka nazo mahabusu, nikaelekea bafuni kuoga. Nilipomaliza nikapaka mafuta na kuvaa nguo nyingine. Nilipohakikisha sasa nipo fiti nikarejea tena sebuleni kupiga stori na Godfrey.

........"Sasa ndugu yangu, naomba nikukumbushe kitu kimoja, uanaume haupimwi kwa kutumia nguvu, wala hasira. Bali uanaume unapimwa kwa kuangalia busara, hekima na uvumilivu wakati wa kutatua changamoto mbalimbali", Godfrey alizungumza kidogo kisha akanyamaza ili kunipa muda wa kuyatafakari maneno yake.

............"Kwanini umeamua kusema hivyo?", nilimuuliza.

.........."Nilifurahishwa sana na uamuzi uliouchukua pale getini mlinzi alipokujibu kuwa waifu wako aliondoka na Idris tangu siku ile mlipogombana. Nilidhani utapanick na kuamua kwenda huko kwa Idris, ila ajabu ni kwamba wala hujapanick. Huo sasa ndo uanaume wenyewe ninaouzungumzia mimi. Hongera sana broo", Godfrey alizungumza huku akinipa mkono wa pongezi.

........"Unajua kaka, muda mwingine inatupasa kupuuzia ujinga wa watu wajinga, ndio maana sikupanick nilipoelezwa mahali waifu wangu alipo. Kama ameamua kuishi na huyo mjinga mwenzake sawa, mi sina tatizo. Ninachohitaji hapa ni kufuata taratibu zote zinazohitajika katika kuvunja ndoa, bas", nilimpa ufafanuzi Godfrey.

Laiti kama Godfrey angejua nililokuwa naliwaza moyoni, sidhani kama anganisifia kwa uamuzi wangu wa kupotezea hili swala. Mimi si kondoo, huwezi kuingia kwenye anga zangu alafu nikuache tu, lazima nikuumize. Idris nilimuweka kiporo tu, ili kusubiri muda wa njaa kuuma nianze kumtafuna.

Wakati tukiwa bado tunapiga stori pale sebuleni, ghafla simu ya Godfrey ikaanza kuita. Aliipokea na kuanza kuzungumza na mpigaji. Walitumia kama dakika mbili hivi kuzungumza. Ila mimi sikujua walichokuwa wakizungumza. Baada ya kukata simu ndipo alipoanza kuniambia:

.........."Johnson, kwanza kabisa naomba nikupe pole kwa hili ninalotaka kukuambia, ila naamini hili nalo litapita, maisha yataendelea" Godfrey alizungumza na kunyamaza kidogo kama mtu anayetafakari jambo.

.........."Kwani vipi, kuna tatizo gani limetokea?, na huyo aliyekupigia ni nani?", nilimuuliza Godfrey huku mapigo yangu ya moyo yakiwa juu.

.........."Bosi amesambaza barua Idara zote pale ofisini, barua hizo zinaeleza kuwa wewe si mtumishi tena. Pia amemteua Idris kukaimu nafasi yako", Godfrey alinieleza kile alichokuwa anaongea kwenye simu.
Hakika nilijihisi kama naishiwa nguvu pale kwenye sofa, pumzi nazo nikaona kama zimeanza kunisaliti. Mungu wangu, ni balaa gani tena hili linanitokea mimi?, nilijikuta nikidondosha chozi pale sebuleni mbele ya Godfrey. Yani mshahara wangu wa zaidi ya shilingi milioni nne kwa mwezi naenda kuukosa, yale marupurupu ya vikao na padiem nayo yanapotea. Nitakuwa mgeni wa nani mimi?. Hakika niliumia sana.

Tena kilichoniumiza zaidi ni kwamba, mtu aliyenisababishia haya matatizo ndie ameteuliwa na bosi kuchukua cheo changu. Hili siwezi kumuachia mungu anilipie, nitajilipia mwenyewe. Idris lazima akutane na joto la jiwe, hii ndio nadhiri niliyojiwekea.


MKONZE-NJE YA MJIJI DODOMA

........."Sasa kipenzi changu, mi naomba ubaki salama. Naamini hizi siku saba nilizokaa na wewe umenifaidi vya kutosha, niache mimi nikamalizie hiki kimkia kilichobaki. Ila badala ya kwenda kukaa mwezi mmoja, nakuahidi nitakaa wiki moja tu kisha ntarudi tena kwako. Kila kitu nitakuwa nimekamilisha ndani ya wiki moja. Idris ameniamini sana siku hizi, kwahiyo kupata "Access" ya akaunti zake ni rahisi", Roida alikuwa akiongea huku amemkumbatia mpenzi wake 'David'.
Ni maneno ya kumuaga mpenzi wake huyo ili arudi tena Dodoma mjini kwa Idris.

........."Poa love, mi nakuaminia sana. Naomba mungu akuongoze ukafanikiwe", David alijibu.

Roida alisindikizwa na mwandani wake huyo hadi stendi ya daladala za Mkonze - Sabasaba. Alipanda gari na safari ya kurejea mjini ikaanza.


NYUMBANI KWA IDRIS

......."Hello honey, unarudi saa ngapi nyumbani?, mi nishakumis huku. Fanya uje kunipa dozi, nipone mwenzako", ni sauti ya kudeka ya Jackline (mke wa Johnson) akiongea na Idris kwenye simu.

........."Nimekumis pia malkia wangu, ndo nataka nirudi sahizi. Vipi nikubebee zawadi gani?", Idris aliuliza.

........."Ooh, waaooo, nibebee tunda la apple (Tufaha). Tena beba mawili kama ishara ya kuchipua kwa penzi letu na kusahau mateso niliyokuwa nayapata kwa yule shetani Johnson asiyejua hata kupetipeti na kumridhisha mwanamke" Jackline alijibu huku akitupa lawama zake kwa mumewe 'Johnson'.

........"Usijali, tena na sahizi nimepandishwa cheo hivi, utakula bata hadi uchoke mwenyewe, mwanamke mrembo kama wewe ni dhambi kuteseka. Sipo tayari kuliona chozi lako likidondoka Jackline, nitapigania furaha yako hadi kufa kwangu.
Yule boya usimkumbuke tena. Bas poa, badae", Idris nae alijitapa.

........"Ahsante kwa maneno matamu, 'bye too' mwaaaaaa", Jackline alijibu na kumalizia na busu. Kisha akakata simu.

****************************************************

Hongereni sana wanawake mnaojitambua, mungu azidi kuwapigania.

Ila hawa wengine "Manungaembe" mola awasamehe tu. Yani Jackline ameshasahau alipotolewa na mumewe kule kijijini. Leo amepata sharobaro mwenye tango(usemi wa vijana) ameamua kumsahau kabisa mumewe, eti ana kibamia (Usemi wa vijana). Anadai eti hamkuni vizuri na hajui kupetipeti. ASTAQFIRULLAH

*****************************************************



Ni takribani siku tano sasa zimepita tangu Jackline aondoke nyumbani kwa mumewe 'Johnson', hata msamiati wa kurudi kwa mumewe haukuwepo kichwani mwake.

.........."Niambie mume wangu, kwahiyo lile swala la Roida nililokuambia ushalifikiria?", Jackline alimuuliza Idris punde aliporudi nyumbani kutoka kazini. Walikuwa wamejilaza chumbani huku Jack akiwa kavalia gauni jepesi la kulalia.

Maungo yake ya ndani yalikuwa yakionekana vizuri jinsi alivyonona. Hakika Jackline aliumbika mno. Na sura yake nzuri ya kuvutia ndo kabisaaaa. Kuna watu waliumbwa, asikwambie mtu, na miongoni mwa hao walioumbwa ni Jackline. Ila kuna wengine walitengenezwa, japo siwajui ni kina nani hao. SIJAKUTAJA WEWE MSOMAJI.

..........."Kama nilivyokwambia Jackline, nipo tayari kuachana na Roida ili niwe na wewe, nakupenda sana", Idris alijibu.

..........."Utamuacha lini?, mi sipendi kumuona hapa", Jack aliuliza tena huku akionekana kununua.Hakutaka tena kuwa na mshindani katika penzi lake hili jipya.

.........."Usinune kipotabo wangu, naomba utabasamu. Leo Roida anakuja. Kwahiyo akiingia tu hapa usiku huu namwambia tuachane", Idris alim'bembeleza jack huku akimchezea mashavuni.

........."Waaooo, hapo nimefurahi. Akija tu naomba umwambie kuwa asikanyage tena hapa. Nisije nikatapika bure nikimuona hapa", Jack aliongea huku akionesha dalili ya kufurahi baada ya kuahidiwa na Idris kuwa atamuacha Roida.

........"Mbona hujanikumbusha kuhusu appple lako, au ulitaki tena", Idris alibadili mada.

........"Oooh, nilisahau mwenzako, ila naomba unikune kwanza, mwili wangu una hamu balaa. Alafu ndo unipatie zawadi yangu", Jackline aliongea kwa sauti ya kudeka na kuanza kufungua vifungo vya dshati vya Idris. Akaliweka pembeni shati la Idris.

Akahamia kwenye suruali, ila hakuivua bali alimfungua tu zipu na kumtoa nyoka wa Idris. Idris alilala chali pale kitandani. Jackline akamlalia Idris kwa juu huku kichwa chake kikiangalia miguuni mwa Idris, na miguu yake ikawa kichwani mwa Idris.

Idris nae alipoona Jackline kalala kifudi fudi huku miguu yake ikiwa karibu na kichwa chake, ikam'bidi amvue Jackline gauni na kuanza kunyonya u**k wa Jackline.

Jack yuko bize kumlamba nyoka wa Iddy, na Iddy nae yuko bize kumlamba bibi wa Jackline.
Huu mchezo ulidumu kwa takribani dakika saba kisha shughuli rasmi ya kunjunjana ikaanza.


NYUMBANI KWA Mr. HASSAN MSANGI (BOSI WA JOHNSON)

.........."Sasa vijana naombeni munisikilize kwa umakini", Mr Hassan aliongea huku akiwaangalia vijana wake wanne wenye miili mikubwa, vifua vipana, na misuli iliyotapakaa mikononi mwao. Walikuwa katika chumba cha siri cha nyumba hii ya Bwana Hassan

.........."Huyu mpuuzi munaemuona kwenye picha anatakiwa auawe haraka sana. Kanisababishia hasara zaidi ya milioni mia saba kwa ujinga alioufanya", aliongea kisha akanyamaza kidogo ili kuwapa mazingatio vijana wake.

........."Kuna dili limeharibika kisa ujinga wake huyu mpuuzi. Mtafuteni kisha mumuue ndani ya masaa 24 kuanzia sasa", aliongea na kuwapa picha wale vijana. Kila mmoja aliitazama ile picha kwa umakini wa hali ya juu kisha wakairudisha ile picha kwa Bosi wao bila ya kuzungumza chochote.

..........."Anaitwa Johnson Alfredy Nzagamba, anaishi Area "A" kwa mkorea, nyumba namba 109. Nimeshatanguliza 'Advance' kwa mkuu wenu, malizieni kazi muje kumalizia kilichobaki", Aliwapa maelekezo wale vijana wake.
Kikao kiliishia pale na kila mtu akatawanyika.



USIKU WA MANANE, NYUMBANI KWA JOHNSON

Johson, yupo kitandani kwake amelala fofofo, hajui kinachoendelea huko nje. Ghafla anasikia kitasa cha mlango wake wa chumbani kikiminywa na kuachiwa. Anashtuka na kukaa kitako pale kitandani. Anachukua simu yake na kumpigia mlinzi wake wa getini.

.........."We Jongo, kuna nini huko nje, mbona nasikia kama watu wanafungua milango ya ndani", Johnson aliuliza kwa papara punde simu ilipopokelewa.

..........."Pole sana, mlinzi wako ametangulia kuzimu, bado wewe tu, hebu fungua mlango haraka kabla hatujavunja", Sauti kali ya bezi ilisikika simuni.

Johnson alipanick, alishajua sasa mwisho wake umefika, amevamiwa na majambazi. Kabla hata hajakata simu, ghafla mlango wa chumbani kwake unavunjwa na wanaume watatu waliovalia mask wanaingia ndani.

......"Paaa, paaa,paaa, paaa,paaaa", sauti za risasi zinasikika ghafla mule chumbani na wale majambazi watatu wanaanguka chini hata kabla hawajapata muda wa kujitetea. Johnson anashangaa imekuwaje tena wale majambazi wamepigwa risasi, nani amewaua?.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom