Riwaya: Niacheni nikufuru

Riwaya: Niacheni nikufuru

RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa5@gmail.com


SEHEMU YA SITA

Nyumbani kwa Idris
Jumatatu Asubuhi

............."Roida, najua haufahamu nini lengo langu la kumtaka kimapenzi Jackline. Sijamtaka kisa ana shepu ya kuvutia, wala sijamtaka kisa ana sura nzuri yenye kuvutia, Bali ninamuhitaji Jackline kwa lengo moja tu" Idris alizungumza kidogo kisha akapumzika kidogo kumpa Roida muda wa kuyatafakari maneno yake kisha akaendelea

............"Johnson ni rafiki yangu mkubwa, ila kwenye maslahi sina budi kumsaliti, Namtumia Jackline ili amuangamize mumewe" Idris aliongea huku akimuangalia Roida ambae muda wote huo alikuwa amejilaza kitandani angali yu uchi wa mnyama.

............"Bado sijakuelewa, nieleweshe vizuri. Johnson ana kitu gani hadi unahitaji kumuangamiza?" Roida aliuliza kwa tahamaki huku akiinuka pale kitandani na kukaa kitako.

..............."Nahitaji cheo chake pale ofisini" Idris alijibu kwa kifupi

............"Ila elimu si amekuzidi, sasa utakichukua vipi cheo chake" Roida aliuliza.

.............."Kielimu tupo sawa, ufanisi wa kazi ni sawa. Hakuna nilichozidiwa na Johnson ila Bosi akaamua kumpa cheo cha 'Msimamizi mkuu wa Idara zote pale ofisini'" Idris aliongea huku akivuta pumzi ndefu

............"Kwahiyo Jackline anahusika vipi na huo mkakati wako" Roida aliuliza

.............."Ondoa shaka, utakuja kufahamu umuhimu wa Jackline baadae. Sahizi endelea kuwa mtazamaji" Idris alijibu huku akisimama na kuelekea katika kabati lake na kuchukua suruali na shati la mikono mirefu. Akazivaa tayari kwa kwenda kazini.


NASIMULIA

Hakuna siku ambayo sitakuja kuisahau katika shughuli zangu za kiofisi kama siku hii ya jumatatu. Nakumbuka ilikuwa ni siku ya Jumatatu asubuhi. Siku hii niliwahi sana kufika ofisini kutokana na majukumu niliyokuwa nikiyafanya wikend. Kuna taarifa mbalimbali nilizotakiwa kuwasilisha kwa Bosi. Ninachokumbuka ni kwamba nilichukua tanakilishi (kompyuta) yangu mpakato na kuingia nayo ofisini kwangu kabla sijapeleka taarifa kwa bosi.

Jukumu langu kama mkuu wa Idara zote hapa ofisini ni kuhakikisha uwajibikaji wa wafanyakzi wote, kutatua kero mbalimbali zinazohusu idara zote hapa ofisini na mwisho kabisa kuhakikisha naweka mahusiano yaliyo bora kati ya wafanyakazi na Bosi mkuu, na pia kati ya ofisi na wateja.

Kila ninapokuja kazini, kitu cha kwanza ni kuhakikisha idara zote wafanyakazi wamehudhuria kazini na kupokea taarifa mbalimbali za kila idara. Kwahiyo nikatoka ofisini kwangu na kuelekea kwa katibu muhtasi

.............."Hello Zainabu, za asubuhi" nilimsalimia katibu muhtasi pale ofisini

............."Salama, sijui za huko kwako" aliniitikia

............"Nitokako ni wazima, vipi Godfrey ameshaingia ofisini kwake" nilimuuliza

............."Hapana bado hajaripoti hapa, hata daftari la mahudhurio hajasaini" alinijibu

............."Na Idris nae" nikamuuliza tena

............"Hata yeye bado hajafika" aliongezea

Aliponijibu hivyo sikusubiri sana nikaamua kuelekea idara mbalimbali kisha nikarudi ofisini kwangu na kusubiri niitwe na bosi mkuu ili niwasilishe nyaraka mbalimbali nilizozifanyia kazi wikendi.
Dakika ishirini baadae simu yangu iliita. niliipokea na kuiweka sikioni.

..........."Naomba uje ofisini kwangu haraka" Sauti kwenye simu ilisikika. Kabla sijajibu sim ikakatwa. Nilichukua diski mweko(Flash disk) ili niweze kunyonya nyaraka zinazohitajika ili nizipeleke ofisini kwa bosi.

Hapo ndipo kizaazaa kilipoanza. Nyaraka zote nilizozifanyia kazi wikendi na kuziweka katika tanakilishi yangu hazikuwepo. Na ni nyaraka muhimu zinazohusiana na mikataba ya miradi mbalimbali. Nakumbuka nilizihifadhi(sevu) kwa jina la "Urban projects" na nilizinakili sehemu mbali mbali katika tanakilishi yangu, ila kote huko sikuziona.

............"Mbona sizioni hizi nyaraka?, nakumbuka nilizisevu kwenye folda hili na hili, lakini kote hazipo, kwanini" nilijiongelesha mwenyewe kama kichaa huku nikijitahidi kutafuta sehem zote kwenye tanakilishi yangu ambapo zinaweza zikawepo hizi nyaraka. Ghafla simu iliita tena

............"Johnson, si nimekwambia uje haraka ofisinu kwangu?", Bosi aliniuliza kwa ukali punde nilipopokea ile simu.

............"Na na na nakuja Bosi" nilimjibu kwa kigugumizi.

............"Nakupa sekunde ishirini uwe hapa" alimalizia na kukata simu.

Hakika nilichanganyikiwa sana. Hizi nyaraka nimehangaika nazo kwa takribani wiki mbili, na wikendi ndio nilikuwa namalizia kazi, ila leo kazi yote niliyoifanya imepotea. Sikuwa na namna zaidi ya kuripoti kwa bosi pasi na nyaraka.

........."Hodi hodi" niligonga mlango wa ofisi ya bosi mara tatu na kusubiri jibu

........."Ingia" Bosi alinijibu. Nikaingia na kukaa kwenye kiti mbele ya meza ya bosi.

..........."Shi shi shikamoo Bosi" nilimuamkia kwa kitetemeshi. Kiumri alinipita zaidi ya miaka ishirini

..........."Marhaba Johnson, vipi mbona una wasiwasi What's wrong?" Bosi aliniuliza.

............"Samahani muheshimiwa, nilijitahidi sana kuifanya kazi uliyonipa kwa takribani wiki mbili na niliimaliza yote. Ila..." nilijieleza kwa bosi kisha nikanyamaza ghafla bila ya kumalizia sentensi yangu

............."Ila nini Johnson" Bosi aliniuliza kwa hamaki

............"Ma..ma..mafaili siyaoni" nilijibu kwa mkato

............"Hebu nieleweshe vizuri kijana wangu, naona unazunguka zunguka tu, huyaoni kivip?" Bosi aliongea kwa ukali.

.........."Mafaili yenye nyaraka zote niliyahifadhi kwenye tanakilishi(Kompyuta yangu) ila leo asubuhi nilipokuwa nataka kuyahamishia kwenye flashi nashangaa sijayaona kabisa. Sijui imekuwaje" nilimueleza bosi kwa unyenyekevu wa hali ya juu.

............."Be serious guy, don't mess with me, nazihitaji hizo nyaraka hapa. Inuka kaniletee hizo nyaraka haraka sana" Bosi alifoka kama mbogo.

............"Muheshimiwa, sijawahi kukuangusha katika kazi zako zote ulizowahi kunipa nikufanyie, hii leo sijui ni kipi kimetokea. Naomba unisamehe mkuu" niliongea huku nikipiga magoti mbele ya bosi.

............"Hivi unajua kwamba hii kandarasi imesimama ili kupisha tathmini zetu?, hivi unajua kwamba leo ndio siku ninayotakiwa kuonana na bodi ya wakurugenzi ili kuwasilisha makadirio yetu?. Unataka mimi niende nikawajibu nini?" Bosi aliniuliza maswali mfululizo.

Nilishindwa nimjibu nini Bosi wangu. Nikawa kimya kama bubu. Ni mchawi gani aliyeingia kwenye tanakilishi yangu na kufuta nyaraka zangu za muhimu?. Nilijiuliza bila kupata jibu. Nywira (Passwords) za hii tanakilishi yangu hakuna anayezijua zaidi ya mimi, Idris na mke wangu Jackline.
Bosi alinifokea sana. Hakuna siku niliyosemwa na kukejeliwa na bosi wangu kama siku hii. Ila nashukuru mungu hakuchukua hatua ya kunifukuza kazi wala kunisimamisha. Alipochoka kunifokea akaniruhusu niondoke.

USHAURI /PENDEKEZO

Ndugu msomaji wa kisa hiki. Katika maisha nimejifunza jambo moja. Akupepeae kwa upepo mwanana, ndie akuleteae joto kali sana. CHUNGA SANA MIENENDO YA WATU UNAOWAAMINI". Akumulikae mchana, usiku akuchoma.

tuendelee.............

Nakumbuka nilipotoka ofisini kwa Bosi, moja kwa moja nilielekea ofisini kwangu. Niliwakuta rafiki zangu Godfrey na Idris karibu na mlango wa kuingilia ofisini kwangu.

..........."Oooh papaa J J mutu muzito, nakuona umetoka kuongea na mkubwa mwenzako, sisi watoto tupo tu tunang'aza sharubu" Idris alinilaki kwa bashasha punde nilipowafikia.

............."Aaah wapi kaka, hakuna cha mkubwa wala mdogo, wote sawa tu" nilimjibu kiunyonge

.............."Vipi Broo, mbona umenyong'onyea sana leo?, sio kawaida yako kuwa mpole, nayajua makeke yako" Godfrey aliniuliza kwa hamaki mara baada ya kuniona sijachangamka kama siku nyingine.

............"Ni majanga ndugu zangu, nimetoka kutukanwa na Bosi hapa sina hamu" nilimjibu Godfrey huku nikifungua mlango ili niingie ndani. Nao walinifata kwa nyuma na mzungumzo yakaendelea.

.........."Usitupanikishe kaka, imekuwaje tena" Idris aliniuliza kwa bashasha.
Ikabidi niwaeleze ukweli wote wa kilichotokea tangu nilipokabidhiwa kazi na Bosi wiki mbili zilizopita hadi siku ya leo nilipotaka kwenda kuiwasilisha.

............"Kumbuka vizuri kaka, inawezekana umejichangaya mwenyewe ulipoweka hayo mafaili yako" Godfrey alitoa ushauri wake

............."Niko makini sana God, huwa nafanya mambo yangu kwa umakini mkubwa mno. Nakumbuka kabisa haya mafaili niliyahifadhi kwa jina la 'Urban Projects' na mara kwa mara nilikuwa nayapitia, ila leo asubuhi ndo yamepotea" nilimjibu kwa mfadhaiko

............." Au inawezekana kuna mtu aliingia ofisini mwako asubuhi na kufuta?" Idris alihoji.

............"Hapo ndo sijajua, maana funguo ya ofisi yangu ninayo mimi na katibu muhtasi tu. Sasa sijui ni kitu gani kilichotokea" niliwapa ufafanuzi.

..........."Peleleza kwanza kwa Zainabu, inawezekana aliingia ofisini kwako akachezea kompyuta yako. Ni ngumu mafaili kujifuta bila sababu. Kama ingekuwa ni virusi basi hata mafaili mengine yasingekuwa salama" Godfrey akatoa mawazo yake.
Nikaona ni kweli, ni muhimu kwenda kumuuliza katibu muhtasi kama aliingia ofisini mida ya asubuhi kipindi nimeenda kufatilia mahudhurio ya wafanyakazi katika Idara mbali mbali.

Tulitoka wote watatu na kuelekea kwa katibu muhtasi.

............"Zai nimekuja tena kwako, nina swali nahitaji unijibu" niliongea punde nilipofika mezani.

............"Uliza Bosi usijali" aliitikia

............."Ni nani aliyeingia ofisini kwangu leo kipindi nimetoka ile asubuhi" nilimuuliza

............"Aaaa..aaa asubuhi i...i....le Idris alikuja ku..." Zainabu aliongea kwa kigugumizi kisha akaka kimya.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com


SEHEMU YA SABA

Nilishindwa kuelewa sababu ya Zainabu kunyamaza ghafla.

.........." Vipi Zai, mbona umenyamaza ghafla" nilimuuliza

..........."Eeeh hamna tatizo, nilitumwa na Idris kuchukua muhuri ofisini kwako alipowasili tu ile asubuhi. Wewe ulikuwa umeelekea idarani" Zainabu alinieleza kwa kirefu. Ni kweli, swala la mihuri pale ofisini huwa tunashea.

............."Kwahiyo ulipoingia kuchukua muhuri ukaamua kushika na kompyuta yangu?" nilimuuliza kwa hasira. Geofrey na Idris walikuwa kimya muda wote huo.

..........."Hapana Bosi, nilichukua tu muhuri na kutoka nje" alijibu

Nilibaki njia panda. Sikujua kama Zainabu anahusika kunihujumu ama la. Ila kwanini aongee kwa kubabaika nilipomuuliza kama aliingia ofisini kwangu?. 'Any way', nikaamua kupotezea.

Majira ya saa saba mchana ningali nimejipumzisha ofisini kutokana na msongo wa mawazo, simu yangu ya mezani iliita. Ilikuwa ni simu kutoka kwa Bosi akinihitaji nifike ofisini kwake haraka. Nilipatwa na hofu, ila nikapiga moyo konde. Nikaweka vifaa vyangu vizuri na kutoka nje ya ofisi. Nilifunga ofisi yangu kwa funguo na kuelekea moja kwa moja ofisini kwa bosi.

............"Johnson, leo umeniangusha sana kijana wangu. Mda huu natakiwa niwahi kikaoni ila sijui naenda kuwaeleza nini. Vipi hujafanikiwa kupata ulipoyahifadhi hayo mafaili?" Bosi aliniuliza kwa sauti ya upole punde nilipoingia ofisini kwake

........"Najua nimekukosea sana Bosi wangu, najutia kwa uzembe nilioufanya, nisamehe sana mkuu. Sijajua ni nani aliyefuta haya mafaili kwenye tanakilishi yangu" nilimueleza Bosi wangu kwa unyenyekevu.

............"Vipi labda hujaangalia kwenye 'Recycle bin', inawezekana ulifuta kwa bahati mbaya" Bosi aliongea kwa utulivu.

............"Nimekagua kote, sijaiona. Ingekuwa hayajafutwa ningeona tu, ila haya yamefutwa mefutwa kabisa" niliongea.

............."Sasa unahisi nani atakuwa amefuta, na kwa malengo yapi?" Bosi aliniuliza ila sikuwa na jibu la kumpa zaidi ya kukaa kimya.

.........."Johnson, leo nimekusamehe, ila naomba usirudie tena kufanya huu uzembe. Sasa nakupa siku tatu tu uwe umeifanya upya hii kazi. Leo nitajua mwenyewe naenda kuwaongopea nini wajumbe wenzangu ndani ya bodi" Bosi aliongea huku akichukua disk mweko(Flash disk) yake iliyo na kazi husika na kunipatia. Nilimshukuru kwa kunisamehe na kumuahidi kutorudia tena kosa kama hilo.

Nilimaliza kuzungumza nae, na kutoka nje ya ofisi huku nikitabasamu.


NYUMBANI KWA JOHNSON

........"Idris, umenitoa kwenye ulimwengu wa giza. Umenifanya niijue thamani ya mapenzi. Kwanini nilichelewa kufahamiana na wewe?. Hakika wewe ni mwanaume rijali, siwezi kupitisha hii siku ya leo kabla sijatoroka hapa nyumbani kuja kwako kupokea tiba" Jackline alituma ujumbe mfupi wa maneno kwenda kwa Idris. Alikuwa chumbani kwake yu uchi wa mnyama akichezea nyeti zake.

..........."Jack, najua umenimis ila naomba uvumilie hadi wikendi ndipo tuonane. Sipendi Johnson agundue chochote kuhusu hiki tunachokifanya" Idris alijibu.

............."Hapana Iddy, nimefikia kiwango cha mwisho cha uvumilivu. Pliz, ukitoka kazini naomba uniruhusu nije. Nakuhitaji Iddy" Jackline aliendelea kubembeleza.

............."Ila mumeo akitoka kazini si umuombe tu mfanye, au atakukatalia?" Idris aliujibu tena ujumbe wa Jack.

............"John hana uwezo wa kufanya kama wewe, huwa ananipaka shombo tu na kuniacha na hamu zangu, naomba nije utulize kiu yangu, ukinikatalia nitajifia mwenzako nakuhitaji daktari wangu" Jackline alizidi kubembeleza.

..........."Duuh, poa sahizi ndo nataka nirudi home. Kwahiyo jipange uje" Iddy alijibu

.........."Ok, nashukuru kwa kulipokea ombi langu. Nakupenda Idris" Jackline alishukuru sana

.........."Nakupenda pia" Idris alijibu.


Kuna usemi usemao kuwa 'Mwanaume fukara ni muaminifu kwa ndoa yake' ila 'Mwanaume mwenye hela ni muharibifu wa ndoa yake'. Kwangu mimi Johnson Nzagamba, ilikuwa ni tofauti . Kwa mshahara na malupulupu mengine niliyokuwa nalipwa ofisini, nilikuwa na uwezo wa kuwa na mwanamke yeyote nimtakae, mabinti wengi walitamani kuwa na mimi kutokana na muonekano wangu jumlisha pesa zangu. Wake za watu nao hawakuwa nyuma katika kunishawishi ili niingie mtegoni, ila mimi Johnson nilikuwa na misimamo thabiti. Sikutaka kabisa kufikiri wala kuthubutu kumsaliti mke wangu Jackline. Wengi waliniona mshamba nisiyeendana na wakati, eti raha ya pesa ni kujua kuzitumia. Yaani kutumia pesa kwa mashangigi na wake za watu ndio usasa huo?, hapana niacheni na ushamba wangu. Nilikuwa nikimpenda sana Jackline. Sikujua kwamba "KIVULI HAKIKUMBATIWI

Nakumbuka siku hii ya Jumatatu nilirudi nyumbani majira ya saa kumi alasiri. Sikumkuta mke wangu, bali mlinzi wa getini tu. Nilipomuuliza mlinzi akanijibu kwamba hakuambiwa mahari alipoelekea Jackline.

Nikachukua simu na kuanza kumtafuta mke wangu, ila kwa bahati mbaya hakupatikana hewani.

.........."Huyu Jackline hii michezo ya kuondoka bila kuniaga wala kunipa taarifa ameianza lini, na simu ameizima makusudi au?" nilijiuliza huku nikielekea chumbani. Nilivua nguo zangu za ofisi na kuelekea sebuleni na kuanza kuifanya kazi niliyopatiwa na Bosi. Sikutaka kujisumbua sana kumfikiria mke wangu. Hata hamu ya kula sikuwa nayo.


NYUMBANI KWA IDRIS

Chumbani

..........."Mbona nyumba iko kimya sana, Roida umemficha wapi?" Jackline aliuliza akiwa amelala kitandani huku kichwa amekiegemeza kifuani mwa Idris.

............"Amesafiri leo asubuhi, ameelekea kwao kusalimia" Idris alijibu.

............"Poa, nipatie basi kilichonileta hapa we mwanaume. Nataka niwahi kurudi nyumbani mume mwenzako asishtuke bureee" Jackline aliongea kwa sauti ya kudeka huku akiinuka pale kitandani na kuanza kumvua Idris suruali.

............"Usiseme mume mwenzangu, sema shemeji yangu. Wewe ushaolewa na Johnson," Idris alijibu huku nae akianza kumvua Jackline sketi yake.

........."Hakuna mwanaume pale, lile ni pambo tu la kiume limevishwa nguo. Mwanaume gani yule ana kadudu kadogo hata kidole changu cha mwisho ni kikubwa" Jackline alijibu huku akiwa tayari keshamvua nguo zote za chini Idris na kuanza kumchezea chezea babu wa Idris.

............"Hahahaha, usinichekeshe Jack, ina maana sahizi ndo umejua kuwa mumeo ana kidole?" Idris alijibu huku nae akiwa anayachezea chezea matiti ya Jackline

............"Sio siri, tangu ile siku unikune ipasavyo, najikuta hata kupiga stori na Johnson sipendi. Namuona tu kama mke mwenzangu tu, hana analolijua yule kwenye mapenzi. Yani sikuhizi nitakuwa namtoroka hadi aseme tuachane. Unajua sana kubembeleza Iddy tofauti na yule mwenzako, una maneno mengi ya kimahaba, na kazi unaiweza haswa. Naomba niwe Sexy toy wako". Jackline aliongea kwa kubembeleza huku akiwa tayari kashawekwa kibra kwa ajili ya kuchinjwa.

Mzunguko wa kwanza ulipoisha, Iddy alitoka na kuelekea Sebuleni kwenye friji na kuchukua glasi mbili, moja ya maji baridi na nyingine ni ya juisi ya matunda na kurudi nazo chumbani. Glasi ya Juis alimpatia Jack na ile ya maji alibaki nayo.

............"Mmmh wewe, unaniletea tena juisi ili nizidiwe kama siku ile, najua tu kuna vitu muliniwekea" Jackline aliongea kwa sauti nyembamba na laini ya kitoto huku akipokea ile glasi.

............"Leo nimetia dawa kidogo tu, huwezi kuzidiwa, hebu kunywa tuendelee na kazi yetu" Idris alijibu huku akimsaidia Jack kuinyanyua ile glasi ya juisi na kumnywesha.

........."Hiyo dawa uliyotia humu inaitwaje, maana ni nzuri sana. Siku ile ya kwanza nilipokunywa nili-enjoy sana.

.........."Inaitwa SEP (Sex Enhancement Pills), ni kama chumvi kwenye mboga, inaongeza radha ya chakula" Idris alijibu huku akiendelea kumshika shika Jack maeneo nyeti ya mwili.

Ndani ya dakika tano Jack akawa yuko hoi kwa hamu alizokuwa nazo. Filimbi ikapulizwa, watu wakaingia tena uwanjani.

Ilichukua takribani masaa mawili kwa wote kuridhika. Wakaelekea bafuni kuoga, Walipomaliza kujiandaa, hatimae Jackline akamuaga Idris na kurudi kwake, kwa mume wake wa ndoa Johnson mida ya Saa mbili kasoro usiku.

AHSANTENI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom