RIWAYA: Mume Gaidi

SEHEMU YA 100 ............ MWISHO


kitu nilichofanya ndio kilichofanya niwe kama nilivyokuwa.
Ila niliomba ushauri kwanza, kipindi hiko nilikuwa na mpenzi wa kuitwa Maria.
Nadhani Maria hakuwa mshauri mzuri kwangu kwani yeye alitakiwa kunikataza kitu hiki cha hatari ila yeye aliniruhusu na kunielekeza njia ya kufanya.
Siku hiyo nilikuwa na Maria nikamweleza kila kitu kuhusu familia yangu na kumwambia kuwa nataka kummaliza bamdogo yani kumuua kwani nilijua kwa kufanya hivyo kutampa nafasi mama ya kurudi tena kwa baba, Maria akaniambia kuwa kama nimeamua hivyo basi ni sawa na nikamuuliza nifanyeje akaniambia nitumie sumu, nimuwekee yule baba kwenye chakula anachopenda sana.
Sikuwa mtaalamu sana na maswala ya simu ila Maria alizijua sumu porini.
Sikutaka kumshirikisha mama kwa hili kwani angeniona mtoto wake ni muuaji. Wala sikutaka kumshirikisha mdogo wangu mzuri wa kike aliyezaliwa na mama kwa kupitia bamdogo, mdogo wangu mzuri Chaurembo aliyekuwa mrembo kweli kama jina lake.
Nilipokuwa tayari kwa zoezi hilo, Maria akanipeleka porini na kunichumia majani hayo ya sumu.
Akaenda kuyaponda kisha kuyachanganya na maji na kuyachuja halafu akaweka kwenye kichupa na kunikabidhi, aliniambia kuwa ile ni sumu inayoua mara moja na kweli kwa hilo hakuongopa kabisa.
Siku hiyo nikaenda kwa bamdogo kwa lengo moja la kummaliza tu.
Nilipofika nikakuta mama ameandaa chakula mezani, nikamwambia mama kuwa nina njaa ila mama akaniambia nisile kile chakula ni cha baba. Ningoje ataniandalia changu, kwakweli niliposikia hivyo nilifurahi sana, nikavizia mama ametoka nje nami nikafunua kichupa changu cha dawa na kutia kwenye bakuli la mboga ambayo ilikuwa ni nyama ya kuku iliyoungwa vizuri sana.
Baada ya kutia ile dawa, mama akaniita nje akaniambia nimuendee kwa fundi nguo kumchukulia nguo yake halafu nikirudi nitakuta chakula changu kiukweli nilichukia kwani nilitaka kumshuhudia yule baba akila kile chakula nikamuuliza kuwa kwanini asingewatuma wakina Neema na Chaurembo? Mama akaniambia kuwa nao wametoka kidogo, wamepeleka maziwa kwa wateja wao ikabidi nisibishe sana. Niliamua kwenda aliponituma mama huku nikiamini kuwa nitakaporudi lazima nitapata habari ya msiba tu.
Nilipotoka kwa fundi na nguo ya mama kwenye mfuko, nilimkuta Neema akiwa nje amekaa huku akisononeka nikajua lazima mambo yameharibika tayari nikamuuliza mbona yupo nje akaniambia kuwa njaa inamuuma, nikamshangaa wakati chakula kipo ndani nikajiuliza labda anangoja baba yake ale kwanza.
Nikamuuliza kwanini asile, alinijibu
"Mama kaniambia nisile hadi niende kuchukua mahindi kule bondeni wakati baba amekataa kula kile chakula alichoandaliwa nae amesema ameshiba, baada ya kuniachia mimi na Chaurembo tule kile chakula eti yeye ndio kaamua kula na Chaurembo sijui kwavile mimi sio mwanae wa......"
Kabla hajamalizia ile sentensi nilihisi kama moyo wangu umeripuka, niliangusha ule mfuko pale pale na kukimbilia ndani.
Nilimkuta mama akiwa chini huku akitapatapa, mdogo wangu Chaurembo ndio hakutamanika kabisa pale chini. Nilimuita Neema kwa nguvu na kumwambia alete maziwa ili tujaribu kuwanusuru ila ilisemekana kuwa maziwa yote yaliuzwa na yaliyobaki mama aliyaficha, hali ilikuwa mbaya sana ila Neema alienda kuomba maziwa kwa majirani huku tukijaribu kutafuta uwezekano wa kuwawahisha hospitali. Kwakweli ilikuwa kazi ngumu kwani hata maziwa aliyoleta Neema nayo hayakusaidia na kufika nao hospitali walikuwa tayari marehemu.
Hili lilikuwa ni pigo kubwa sana kwangu hata pale msiba ulipoisha bado nilikuwa na pigo kubwa sana.
Nilijikuta nikimchukia Maria kupita maelezo kamavile yeye ndiye aliyeshauri kuwa niue.
Ila sikuachana nae kwavile bado nilikuwa nampenda.
Ila moyoni nilikuwa namuwazia mawazo mabaya sana Maria bila ya yeye kujua laiti kama angejua basi angejiepusha na mimi mapema sana.
Nilikuwa mtu wa mawazo tu na kumuona kwangu bamdogo nikaona kama akinizidishia maumivu tu ya kuendelea kumkumbuka mama yangu.
Nikafanya mpango wa kummaliza bamdogo ila bado ilishindikana.
Kipindi hicho nyumbani kulikuwa na mgogoro wa dada yangu Rehema na mwanaume ambaye amezaa nae, wakati tukirumbana hadi kufikia kugawana wala watoto na yule mwanaume kufukuzwa pale kijijini kumbe Maria nae alikuwa amejifungua mtoto wangu ila alikaa kimya bila hata ya kuniambia.
Bado nilikuwa na uchungu juu ya bamdogo na kipindi hicho baba na bamdogo walianza kupatana patana tena, na mimi nikaitumia nafasi hiyo kummaliza bamdogo.
Nikaweka mtego shambani kwa bamdogo kwa bahati mbaya baba na bamdogo walienda pamoja kwenye lile shamba na ule mtego ukamvaa baba yangu na kummaliza papo hapo.
Ukoo mzima ukamchukia bamdogo na kumwambia kuwa ndio chanzo, bamdogo akafukuzwa pale kijijini na akaondoka na binti yake Neema kwenda kuanza maisha mengine kabisa.
Roho iliniuma kwa kusababisha kifo cha baba na mama na mdogo wangu ila yote ni katika harakati za kummaliza bamdogo.
Nikawa kama vile mtu aliyechanganyikiwa, nikapotea nyumbani na kuzamia Mombasa, nilikaa huko kwa miaka mitano huku nikipanga namna ya kummaliza bamdogo.
Niliporudi bado sikuwa na amani ya moyo, nilimkuta dada ameolewa ila akiwa mjamzito tena na katoto kake ka kwanza kakiwa kamekua kua vya kutosha.
Nikapata wazo la kumtembelea Maria, nikamkuta nae akiwa na mtoto halafu ni mjamzito.
Nilichukia sana, nilipomuuliza alidai kuwa yule mtoto ni wangu ila hakuniambia kwavile nilipotea ila ule ujauzito kuna mwanaume amempata, kuja kufatilia nikagundua kuwa huyo mwanaume ndio yule aliyezaa na dada yangu mtoto wa kwanza, roho ikaniuma sana kuona yule mwanaume kaona haitoshi kuniharibia dada yangu na sasa amehamia kwa mchumba wangu.
Nikaapa kuwa lazima nije kulipa kisasi.
Ila labla ya kuanza mapinduzi ya kisasi niliamua kwanza kuondoka na wale watoto wa kiume ili nikawafunze kazi huko Mombasa.
Dada nikamdanganya kuwa natoka na mwanae mara moja, kisha nikaenda nae hadi kijiji cha kina Maria na kumchukua mwanangu huku nikidai kuwa naenda kutembea nae tu.
Kwakweli watoto hawa wawili niliweza kuwatofautisha kwa majina tu ukizingatia sijaishi nao.
Niliondoka na watoto wale hadi Mombasa, nikakaa huko kwa siku chache kisha nikawakabidhi kwa rafiki yangu na mimi kurudi tena kijijini, lengo lilikuwa ni kumshawishi dada yangu ili niende nae Mombasa ila ile kurudi tu kijijini dada yangu akaanza kunishambulia kwa maneno na kunidai mtoto wake ila alikuwa ameshajifungua na ana mtoto mchanga, nikaachana nae pale na kuelekea kwa Maria kwani nilijua kuwa na yeye lazima atakuwa amejifungua, moyoni nikajisemea kuwa lazima nikammalize huyo mwanaume.
Nilipofika kwa Maria naye alianza kunidai mtoto wake na yule mwanaume sikumuona, nikaona Maria ananiletea longolongo tu hivyo hata sikumchelewesha, nilichukua kisu na kumchoma nacho tumboni yani sikuwa na huruma kabisa kisha nikaondoka.
Kurudi tena kwa dada naye akawa anadai mtoto wake namwambia yuko Mombasa hataki kunielewa anamtaka mwanae halafu akaniitia polisi.
Nilikuwa kama mtu niliyechanganyikiwa, nilijikuta nikimnyanyua yule mtoto mchanga wa dada na kumuinua juu kisha kumbamiza chini kama mzigo, na alilia mlio mmoja tu kisha ikawa kimya.
Wale mapolisi wakaona wanikamate kinguvu ili kuepusha majanga mengine.
Nikapelekwa jela ila mambo ambayo nilikuwa nafanya humo ikaonekana kama vile sina akili nzuri, hivyo wakanipeleka jela ya vichaa na kwakweli nilikuwa kichaa kwa kipindi hiko kwani nilifanya mambo ya ajabu hadi ya kujishtukia.
Nilikaa jela kwa miaka mitano kasoro, badae nikaanza kutafuta namna ya kutoroka pale gerezani.
Nilipopata nafasi sikuangalia nyuma nilitoroka moja kwa moja na kukimbilia kwa bamdogo kule ambako alikuwa amehamia tangia kifo cha baba, ni mimi tu niliyepajua kwa bamdogo kwakuwa ndugu zake na ukoo mzima walimtenga nami nikaona kuwa kule nitakuwa salama zaidi.
Nilimkuta Neema akiwa na mabinti wawili kwa kuwakadilia miaka huyu mkubwa alikuwa na miaka nane na mdogo miaka minne.
Pale kwa bamdogo hapakuwa na tatizo kwani Neema alinihudumia vizuri sana tatizo lilikuwa kwa huyu binti yake mkubwa huyu wa kuitwa Fausta alikuwa na nyodo sana halafu alikuwa ananidharau sana mara nikiwekewa chakula aseme kuwa mimi nakula sana, nikimtuma kitu anakataa kwakweli huyu binti alikuwa ananikera sana na kama ingekuwa amri yangu basi ningekimaliza muda mrefu sana.
Roho iliniuma kwa kusodolewa na binti mdogo kama Fausta ila nikawa navumilia tu, kitu kibaya ni kuwa Neema hakuweza kumgombeza mtoto wake huyo ingawa alikuwa anaona mambo ya ajabu aliyokuwa ananifanyia, ukimwambia anajibu ni utoto tu huo msamehe bure dah huyu mtoto nilimchukia sana.
Nilikaa kwa bamdogo miaka miwili kasoro hadi pale Fausta ambaye anatetewa na mama yake kuwa ni utoto alipokwenda kunishtaki polisi kuwa mimi ni muharifu, nilishangaa mapolisi kuja na kunikamata.
Nilichukia sana na kuapa kuwa laziama nimmalize yule mtoto nikitoka jela.
Safari hii nilikaa tena jela kwa miaka mitatu hadi pale nilipopata nafasi ya kutoroka ila niliwapa mapolisi wawili sumu na nilipotoka jela safari yangu ilikuwa ni kwa bamdogo kwa lengo la kummaliza Fausta.
Kufika pale nilimkuta mama yao ndani, nilipomuuliza alikataa kunitajia Fausta alipo hata nilipojaribu kumtishia bado hakutaja, nikaona ananiwekea usiku tu nikachukua kisu na kumchoma nacho habari yake ikaisha.
Wakati natoka nikakutana na bamdogo mlangoni.
Bila kuchelewesha muda nilimchoma na kisu ili kupoteza ushahidi kisha nikaingia chumbani na kusomba pesa zote milizozikuta na kuondoka nazo, zikaniwezesha kusafiri na kwenda tena Mombasa.
Kufika kule niliwakuta watoto wamekua kweli ila bado waliwataka mama zao nikawaambia kuwa mama zao wamekufa ila hawakutaka kukubali, Maiko alipoona nimebadilika akatulia ila Juma alijifanya mbishi na kuendelea kunisumbua sana, sikutaka kero hivyobasi nikamfyekelea mbali huku nikijua nimemfyeka mtoto wa dada yangu kumbe nimemfyeka mwanangu na kumuacha mtoto wa dada yangu dah Maiko ni mshenzi sana.
Nikawa nafanya biashara za magendo na watu wa kule ila kila leo biashara za magendo zinatanuka hadi kufikia kuuza viungo vya watu, nikasafiri nchi nyingi kupeleka viungo hivyo na nikawa na pesa nyingi pia ni hapo nilipoamua kulipa kisasi kwa yeyote niliyejisikia kummaliza, hata oda ya kummaliza mzee Ayubu niliitoa mimi kwani alitembea na mpenzi wangu.
Katika kisasi changu nimesumbuliwa na kiumbe mmoja tu huyu wa kuitwa Fausta. Mungu akupe maisha marefu ila ukweli ni kwamba nakuchukia sana na ningekumaliza siku nyingi sana wewe.
Najua mpo mtakaoumizwa na hii barua ila ndio hivyo yalishatokea ya kutokea.
Na katika watu walioniharibia mpango wangu wa kuwa bilionea kwasasa ni huyu wa kuitwa Patrick, nakuchukia sana wewe kijana. Umeharibu maisha yangu sana.
Ila samahanini kwa yote niliyowakosea, ni mimi MASHAKA"
Kila mmoja alijikuta akipumua kwa nguvu baada ya ile barua.
Kila mmoja alikuwa kimya kabisa, Deborah akauvunja ukimya ule.
DEBORAH: Jamani kila mmoja nadhani amesikia maelezo ya hiyo barua.
REHEMA: Yani nimeumizwa sana kuona mdogo wangu alifanya vitendo vya makusudi kiasi hiko. Ameharibu ukoo mzima.
DEBORAH: Ni kweli ila kinachotakiwa ni kuvunja hiyo laana kwenye ukoo wenu.
REHEMA: Kitu kingine ni ndoa ya Pamela na Adamu, nyie wawili mlikosea sana kuoana ndugu sasa watoto wenu mtawaweka wapi?
Amina alikuwa ameinama na kutoa machozi ukizingatia kifo cha mtoto wake Tulo halafu na barua iliyosomwa ilimuumiza sana, naye akaamua kusema.
AMINA: Jamani huyo Maria ndio mama yangu mzazi ambaye nilipewa habari kuwa aliuliwa kikatili kumbe aliyemuua ni huyu jamaa!!
Amina alisikitika sana na wakaamua kumbembeleza.
DEBORAH: Mmh!! Na huyo mzee Ayubu nae ilikuwaje kuzaa na huyu na huyu na huyu?
REHEMA: Ngoja nimtetee kwa hilo, kwanza kabisa alizaa na mimi ila kwetu wakamkataa na tukagawana watoto, pili akazaa na Neema nadhani bamdogo pia alimkataa kwakuwa bado anasheria za kule, tatu akaenda kuzaa na huyo Maria ambaye aliuliwa na Mashaka kwakweli hakuwa na la kufanya hapo jamani. Ila ninachomlaumu ni kuwa alipoona kijiji hakimtaki angehama kabisa na asingethubutu kuzaa na mwanamke mwingine yeyote wa karibu ila nadhani kifo cha Maria ndio kilichomkimbiza Morogoro, pole sana mzee Ayubu.
Ikabidi wajadili hatma ya Tusa na Patrick, safari hii Patrick bila kinyongo akaamua kuachana na Tusa kwa amani tu ili kuepusha mabalaa mengine katika ukoo.
PATRICK: Kwa hiyari yangu na kwa amani kabisa naamua kuachana na Tusa ila Deborah ataendelea kuwa mama yangu siku zote za maisha yangu.
Kauli ile ilimfurahisha sana Deborah kwani aliona swala la Patrick kuachana na Tusa ni swala zuri sana na pia ilikuwa furaha kwa Sele aliyempenda Tusa kupitiliza hata Tusa nae alifurahi ila kilichomuuma ni kuwa kwanini Patrick atokee kuwa kaka yake.
Adamu na Pamela waliumia kitu kimoja kikubwa nacho ni kukataliwa na Patrick.
Marium bado alikuwa na swali kwa mwanae kuwa kwanini hawezi kuachana na Tusa.
MARIUM: Hivi mwanangu Sele huyu mwanamke alikupa nini hadi hutaki kumuacha?
SELE: Mama, mimi na Tusa tulikula kiapo cha milele najua Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote ila mimi. Nampenda sana naye ananipenda sana.
PATRICK: Ni kweli kabisa asemavyo Sele, Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote yule. Kwa jinsi ambavyo nimeishi na Tusa na mambo mengi niliyomfanyia ni wazi kuwa Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote zaidi ya huyo Sele.
DEBORAH: Kama ndio hivyo tuwaache waoane tu maana wanapendana, ingekuwa mwanaume mwingine angemuacha Tusa kitambo kwa mapito aliyopitia ila kwakuwa Sele ana mapenzi ya dhati basi na amuoe Tusa.
PATRICK: Sele anapaswa kuigwa kwenye jamii, na nitasimamia harusi yao yote.
Tusa alimshangaa sana Patrick kwani hakuwazia kuwa ipo siku Patrick atakuwa ni mwanaume wa kutamka maneno mazuri kiasi kile.
Mwita nae aliungana na ndugu zake na kuamua kuvunja laana zote ambazo zimeikumba hiyo familia.
Harusi ikapangwa kisha Sele na Tusa wakafunga ndoa.
Kila mmoja aliwatakia maisha marefu Sele na Tusa, kisha Deborah akamwambia Sele.
DEBORAH: Natumaini utakuwa mume mwema, nawatakia maisha marefu na usithubutu kuwa kama MUME GAIDI, pesa tafuta kwa njia halali na Mungu atakuwezesha.
Waliyafurahia yale mahusia na kupiga makofi.
Baada ya hapo kikafanyika kikao cha mwisho cha familia na hapo ndipo Yuda nae akatangaza kumuoa Tina na hukuna aliyepinga.
Deborah aliamua kuwaaga na ndugu zake kuwa wanataka kurudi kwao Mwanza ila kabla ya kuondoka Patrick aliweka sherehe ya kuagana na familia ya kina Tusa.
Katika sherehe hiyo alimsimamisha Deborah na kuongea maneno haya,
"Huyu mwanamke mnayemuona mbele yenu, ndiye mama yangu, chakula changu, furaha yangu, amani yangu na kila kitu katika maisha yangu. Nampenda sana huyu mama, sitamtupa wala kumtenga hadi naingia kaburini"
Kisha akamuangalia kwa karibu Deborah na kumwambia,
"Nakupenda sana mama"
Akamkumbatia kwa furaha na kesho yake wakasafiri kurudi Mwanza wakiwa na furaha iliyopitiliza.
Pamela aliumia sana na kujiona kuwa na mkosi mkubwa sana maishani mwake. Kitendo cha kumtupa mtoto kilimuumiza sana.
Walipokuwa Mwanza, siku hiyo Patrick alilala usiku na kutokewa na mzimu wa mzee Ayubu kisha ukampungia mkono kama ishara ya kumuaga tena huku akitabasamu.
shukran mkuu nimemaliza
 
Nachompendea huyu mtaalam,hadithi zake zinaisha kabisa,sio wale wa sijui whatsap sijui nini. Shukrani mkuu.
 
SEHEMU YA 100 ............ MWISHO


kitu nilichofanya ndio kilichofanya niwe kama nilivyokuwa.
Ila niliomba ushauri kwanza, kipindi hiko nilikuwa na mpenzi wa kuitwa Maria.
Nadhani Maria hakuwa mshauri mzuri kwangu kwani yeye alitakiwa kunikataza kitu hiki cha hatari ila yeye aliniruhusu na kunielekeza njia ya kufanya.
Siku hiyo nilikuwa na Maria nikamweleza kila kitu kuhusu familia yangu na kumwambia kuwa nataka kummaliza bamdogo yani kumuua kwani nilijua kwa kufanya hivyo kutampa nafasi mama ya kurudi tena kwa baba, Maria akaniambia kuwa kama nimeamua hivyo basi ni sawa na nikamuuliza nifanyeje akaniambia nitumie sumu, nimuwekee yule baba kwenye chakula anachopenda sana.
Sikuwa mtaalamu sana na maswala ya simu ila Maria alizijua sumu porini.
Sikutaka kumshirikisha mama kwa hili kwani angeniona mtoto wake ni muuaji. Wala sikutaka kumshirikisha mdogo wangu mzuri wa kike aliyezaliwa na mama kwa kupitia bamdogo, mdogo wangu mzuri Chaurembo aliyekuwa mrembo kweli kama jina lake.
Nilipokuwa tayari kwa zoezi hilo, Maria akanipeleka porini na kunichumia majani hayo ya sumu.
Akaenda kuyaponda kisha kuyachanganya na maji na kuyachuja halafu akaweka kwenye kichupa na kunikabidhi, aliniambia kuwa ile ni sumu inayoua mara moja na kweli kwa hilo hakuongopa kabisa.
Siku hiyo nikaenda kwa bamdogo kwa lengo moja la kummaliza tu.
Nilipofika nikakuta mama ameandaa chakula mezani, nikamwambia mama kuwa nina njaa ila mama akaniambia nisile kile chakula ni cha baba. Ningoje ataniandalia changu, kwakweli niliposikia hivyo nilifurahi sana, nikavizia mama ametoka nje nami nikafunua kichupa changu cha dawa na kutia kwenye bakuli la mboga ambayo ilikuwa ni nyama ya kuku iliyoungwa vizuri sana.
Baada ya kutia ile dawa, mama akaniita nje akaniambia nimuendee kwa fundi nguo kumchukulia nguo yake halafu nikirudi nitakuta chakula changu kiukweli nilichukia kwani nilitaka kumshuhudia yule baba akila kile chakula nikamuuliza kuwa kwanini asingewatuma wakina Neema na Chaurembo? Mama akaniambia kuwa nao wametoka kidogo, wamepeleka maziwa kwa wateja wao ikabidi nisibishe sana. Niliamua kwenda aliponituma mama huku nikiamini kuwa nitakaporudi lazima nitapata habari ya msiba tu.
Nilipotoka kwa fundi na nguo ya mama kwenye mfuko, nilimkuta Neema akiwa nje amekaa huku akisononeka nikajua lazima mambo yameharibika tayari nikamuuliza mbona yupo nje akaniambia kuwa njaa inamuuma, nikamshangaa wakati chakula kipo ndani nikajiuliza labda anangoja baba yake ale kwanza.
Nikamuuliza kwanini asile, alinijibu
"Mama kaniambia nisile hadi niende kuchukua mahindi kule bondeni wakati baba amekataa kula kile chakula alichoandaliwa nae amesema ameshiba, baada ya kuniachia mimi na Chaurembo tule kile chakula eti yeye ndio kaamua kula na Chaurembo sijui kwavile mimi sio mwanae wa......"
Kabla hajamalizia ile sentensi nilihisi kama moyo wangu umeripuka, niliangusha ule mfuko pale pale na kukimbilia ndani.
Nilimkuta mama akiwa chini huku akitapatapa, mdogo wangu Chaurembo ndio hakutamanika kabisa pale chini. Nilimuita Neema kwa nguvu na kumwambia alete maziwa ili tujaribu kuwanusuru ila ilisemekana kuwa maziwa yote yaliuzwa na yaliyobaki mama aliyaficha, hali ilikuwa mbaya sana ila Neema alienda kuomba maziwa kwa majirani huku tukijaribu kutafuta uwezekano wa kuwawahisha hospitali. Kwakweli ilikuwa kazi ngumu kwani hata maziwa aliyoleta Neema nayo hayakusaidia na kufika nao hospitali walikuwa tayari marehemu.
Hili lilikuwa ni pigo kubwa sana kwangu hata pale msiba ulipoisha bado nilikuwa na pigo kubwa sana.
Nilijikuta nikimchukia Maria kupita maelezo kamavile yeye ndiye aliyeshauri kuwa niue.
Ila sikuachana nae kwavile bado nilikuwa nampenda.
Ila moyoni nilikuwa namuwazia mawazo mabaya sana Maria bila ya yeye kujua laiti kama angejua basi angejiepusha na mimi mapema sana.
Nilikuwa mtu wa mawazo tu na kumuona kwangu bamdogo nikaona kama akinizidishia maumivu tu ya kuendelea kumkumbuka mama yangu.
Nikafanya mpango wa kummaliza bamdogo ila bado ilishindikana.
Kipindi hicho nyumbani kulikuwa na mgogoro wa dada yangu Rehema na mwanaume ambaye amezaa nae, wakati tukirumbana hadi kufikia kugawana wala watoto na yule mwanaume kufukuzwa pale kijijini kumbe Maria nae alikuwa amejifungua mtoto wangu ila alikaa kimya bila hata ya kuniambia.
Bado nilikuwa na uchungu juu ya bamdogo na kipindi hicho baba na bamdogo walianza kupatana patana tena, na mimi nikaitumia nafasi hiyo kummaliza bamdogo.
Nikaweka mtego shambani kwa bamdogo kwa bahati mbaya baba na bamdogo walienda pamoja kwenye lile shamba na ule mtego ukamvaa baba yangu na kummaliza papo hapo.
Ukoo mzima ukamchukia bamdogo na kumwambia kuwa ndio chanzo, bamdogo akafukuzwa pale kijijini na akaondoka na binti yake Neema kwenda kuanza maisha mengine kabisa.
Roho iliniuma kwa kusababisha kifo cha baba na mama na mdogo wangu ila yote ni katika harakati za kummaliza bamdogo.
Nikawa kama vile mtu aliyechanganyikiwa, nikapotea nyumbani na kuzamia Mombasa, nilikaa huko kwa miaka mitano huku nikipanga namna ya kummaliza bamdogo.
Niliporudi bado sikuwa na amani ya moyo, nilimkuta dada ameolewa ila akiwa mjamzito tena na katoto kake ka kwanza kakiwa kamekua kua vya kutosha.
Nikapata wazo la kumtembelea Maria, nikamkuta nae akiwa na mtoto halafu ni mjamzito.
Nilichukia sana, nilipomuuliza alidai kuwa yule mtoto ni wangu ila hakuniambia kwavile nilipotea ila ule ujauzito kuna mwanaume amempata, kuja kufatilia nikagundua kuwa huyo mwanaume ndio yule aliyezaa na dada yangu mtoto wa kwanza, roho ikaniuma sana kuona yule mwanaume kaona haitoshi kuniharibia dada yangu na sasa amehamia kwa mchumba wangu.
Nikaapa kuwa lazima nije kulipa kisasi.
Ila labla ya kuanza mapinduzi ya kisasi niliamua kwanza kuondoka na wale watoto wa kiume ili nikawafunze kazi huko Mombasa.
Dada nikamdanganya kuwa natoka na mwanae mara moja, kisha nikaenda nae hadi kijiji cha kina Maria na kumchukua mwanangu huku nikidai kuwa naenda kutembea nae tu.
Kwakweli watoto hawa wawili niliweza kuwatofautisha kwa majina tu ukizingatia sijaishi nao.
Niliondoka na watoto wale hadi Mombasa, nikakaa huko kwa siku chache kisha nikawakabidhi kwa rafiki yangu na mimi kurudi tena kijijini, lengo lilikuwa ni kumshawishi dada yangu ili niende nae Mombasa ila ile kurudi tu kijijini dada yangu akaanza kunishambulia kwa maneno na kunidai mtoto wake ila alikuwa ameshajifungua na ana mtoto mchanga, nikaachana nae pale na kuelekea kwa Maria kwani nilijua kuwa na yeye lazima atakuwa amejifungua, moyoni nikajisemea kuwa lazima nikammalize huyo mwanaume.
Nilipofika kwa Maria naye alianza kunidai mtoto wake na yule mwanaume sikumuona, nikaona Maria ananiletea longolongo tu hivyo hata sikumchelewesha, nilichukua kisu na kumchoma nacho tumboni yani sikuwa na huruma kabisa kisha nikaondoka.
Kurudi tena kwa dada naye akawa anadai mtoto wake namwambia yuko Mombasa hataki kunielewa anamtaka mwanae halafu akaniitia polisi.
Nilikuwa kama mtu niliyechanganyikiwa, nilijikuta nikimnyanyua yule mtoto mchanga wa dada na kumuinua juu kisha kumbamiza chini kama mzigo, na alilia mlio mmoja tu kisha ikawa kimya.
Wale mapolisi wakaona wanikamate kinguvu ili kuepusha majanga mengine.
Nikapelekwa jela ila mambo ambayo nilikuwa nafanya humo ikaonekana kama vile sina akili nzuri, hivyo wakanipeleka jela ya vichaa na kwakweli nilikuwa kichaa kwa kipindi hiko kwani nilifanya mambo ya ajabu hadi ya kujishtukia.
Nilikaa jela kwa miaka mitano kasoro, badae nikaanza kutafuta namna ya kutoroka pale gerezani.
Nilipopata nafasi sikuangalia nyuma nilitoroka moja kwa moja na kukimbilia kwa bamdogo kule ambako alikuwa amehamia tangia kifo cha baba, ni mimi tu niliyepajua kwa bamdogo kwakuwa ndugu zake na ukoo mzima walimtenga nami nikaona kuwa kule nitakuwa salama zaidi.
Nilimkuta Neema akiwa na mabinti wawili kwa kuwakadilia miaka huyu mkubwa alikuwa na miaka nane na mdogo miaka minne.
Pale kwa bamdogo hapakuwa na tatizo kwani Neema alinihudumia vizuri sana tatizo lilikuwa kwa huyu binti yake mkubwa huyu wa kuitwa Fausta alikuwa na nyodo sana halafu alikuwa ananidharau sana mara nikiwekewa chakula aseme kuwa mimi nakula sana, nikimtuma kitu anakataa kwakweli huyu binti alikuwa ananikera sana na kama ingekuwa amri yangu basi ningekimaliza muda mrefu sana.
Roho iliniuma kwa kusodolewa na binti mdogo kama Fausta ila nikawa navumilia tu, kitu kibaya ni kuwa Neema hakuweza kumgombeza mtoto wake huyo ingawa alikuwa anaona mambo ya ajabu aliyokuwa ananifanyia, ukimwambia anajibu ni utoto tu huo msamehe bure dah huyu mtoto nilimchukia sana.
Nilikaa kwa bamdogo miaka miwili kasoro hadi pale Fausta ambaye anatetewa na mama yake kuwa ni utoto alipokwenda kunishtaki polisi kuwa mimi ni muharifu, nilishangaa mapolisi kuja na kunikamata.
Nilichukia sana na kuapa kuwa laziama nimmalize yule mtoto nikitoka jela.
Safari hii nilikaa tena jela kwa miaka mitatu hadi pale nilipopata nafasi ya kutoroka ila niliwapa mapolisi wawili sumu na nilipotoka jela safari yangu ilikuwa ni kwa bamdogo kwa lengo la kummaliza Fausta.
Kufika pale nilimkuta mama yao ndani, nilipomuuliza alikataa kunitajia Fausta alipo hata nilipojaribu kumtishia bado hakutaja, nikaona ananiwekea usiku tu nikachukua kisu na kumchoma nacho habari yake ikaisha.
Wakati natoka nikakutana na bamdogo mlangoni.
Bila kuchelewesha muda nilimchoma na kisu ili kupoteza ushahidi kisha nikaingia chumbani na kusomba pesa zote milizozikuta na kuondoka nazo, zikaniwezesha kusafiri na kwenda tena Mombasa.
Kufika kule niliwakuta watoto wamekua kweli ila bado waliwataka mama zao nikawaambia kuwa mama zao wamekufa ila hawakutaka kukubali, Maiko alipoona nimebadilika akatulia ila Juma alijifanya mbishi na kuendelea kunisumbua sana, sikutaka kero hivyobasi nikamfyekelea mbali huku nikijua nimemfyeka mtoto wa dada yangu kumbe nimemfyeka mwanangu na kumuacha mtoto wa dada yangu dah Maiko ni mshenzi sana.
Nikawa nafanya biashara za magendo na watu wa kule ila kila leo biashara za magendo zinatanuka hadi kufikia kuuza viungo vya watu, nikasafiri nchi nyingi kupeleka viungo hivyo na nikawa na pesa nyingi pia ni hapo nilipoamua kulipa kisasi kwa yeyote niliyejisikia kummaliza, hata oda ya kummaliza mzee Ayubu niliitoa mimi kwani alitembea na mpenzi wangu.
Katika kisasi changu nimesumbuliwa na kiumbe mmoja tu huyu wa kuitwa Fausta. Mungu akupe maisha marefu ila ukweli ni kwamba nakuchukia sana na ningekumaliza siku nyingi sana wewe.
Najua mpo mtakaoumizwa na hii barua ila ndio hivyo yalishatokea ya kutokea.
Na katika watu walioniharibia mpango wangu wa kuwa bilionea kwasasa ni huyu wa kuitwa Patrick, nakuchukia sana wewe kijana. Umeharibu maisha yangu sana.
Ila samahanini kwa yote niliyowakosea, ni mimi MASHAKA"
Kila mmoja alijikuta akipumua kwa nguvu baada ya ile barua.
Kila mmoja alikuwa kimya kabisa, Deborah akauvunja ukimya ule.
DEBORAH: Jamani kila mmoja nadhani amesikia maelezo ya hiyo barua.
REHEMA: Yani nimeumizwa sana kuona mdogo wangu alifanya vitendo vya makusudi kiasi hiko. Ameharibu ukoo mzima.
DEBORAH: Ni kweli ila kinachotakiwa ni kuvunja hiyo laana kwenye ukoo wenu.
REHEMA: Kitu kingine ni ndoa ya Pamela na Adamu, nyie wawili mlikosea sana kuoana ndugu sasa watoto wenu mtawaweka wapi?
Amina alikuwa ameinama na kutoa machozi ukizingatia kifo cha mtoto wake Tulo halafu na barua iliyosomwa ilimuumiza sana, naye akaamua kusema.
AMINA: Jamani huyo Maria ndio mama yangu mzazi ambaye nilipewa habari kuwa aliuliwa kikatili kumbe aliyemuua ni huyu jamaa!!
Amina alisikitika sana na wakaamua kumbembeleza.
DEBORAH: Mmh!! Na huyo mzee Ayubu nae ilikuwaje kuzaa na huyu na huyu na huyu?
REHEMA: Ngoja nimtetee kwa hilo, kwanza kabisa alizaa na mimi ila kwetu wakamkataa na tukagawana watoto, pili akazaa na Neema nadhani bamdogo pia alimkataa kwakuwa bado anasheria za kule, tatu akaenda kuzaa na huyo Maria ambaye aliuliwa na Mashaka kwakweli hakuwa na la kufanya hapo jamani. Ila ninachomlaumu ni kuwa alipoona kijiji hakimtaki angehama kabisa na asingethubutu kuzaa na mwanamke mwingine yeyote wa karibu ila nadhani kifo cha Maria ndio kilichomkimbiza Morogoro, pole sana mzee Ayubu.
Ikabidi wajadili hatma ya Tusa na Patrick, safari hii Patrick bila kinyongo akaamua kuachana na Tusa kwa amani tu ili kuepusha mabalaa mengine katika ukoo.
PATRICK: Kwa hiyari yangu na kwa amani kabisa naamua kuachana na Tusa ila Deborah ataendelea kuwa mama yangu siku zote za maisha yangu.
Kauli ile ilimfurahisha sana Deborah kwani aliona swala la Patrick kuachana na Tusa ni swala zuri sana na pia ilikuwa furaha kwa Sele aliyempenda Tusa kupitiliza hata Tusa nae alifurahi ila kilichomuuma ni kuwa kwanini Patrick atokee kuwa kaka yake.
Adamu na Pamela waliumia kitu kimoja kikubwa nacho ni kukataliwa na Patrick.
Marium bado alikuwa na swali kwa mwanae kuwa kwanini hawezi kuachana na Tusa.
MARIUM: Hivi mwanangu Sele huyu mwanamke alikupa nini hadi hutaki kumuacha?
SELE: Mama, mimi na Tusa tulikula kiapo cha milele najua Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote ila mimi. Nampenda sana naye ananipenda sana.
PATRICK: Ni kweli kabisa asemavyo Sele, Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote yule. Kwa jinsi ambavyo nimeishi na Tusa na mambo mengi niliyomfanyia ni wazi kuwa Tusa hawezi kuishi na mwanaume yeyote zaidi ya huyo Sele.
DEBORAH: Kama ndio hivyo tuwaache waoane tu maana wanapendana, ingekuwa mwanaume mwingine angemuacha Tusa kitambo kwa mapito aliyopitia ila kwakuwa Sele ana mapenzi ya dhati basi na amuoe Tusa.
PATRICK: Sele anapaswa kuigwa kwenye jamii, na nitasimamia harusi yao yote.
Tusa alimshangaa sana Patrick kwani hakuwazia kuwa ipo siku Patrick atakuwa ni mwanaume wa kutamka maneno mazuri kiasi kile.
Mwita nae aliungana na ndugu zake na kuamua kuvunja laana zote ambazo zimeikumba hiyo familia.
Harusi ikapangwa kisha Sele na Tusa wakafunga ndoa.
Kila mmoja aliwatakia maisha marefu Sele na Tusa, kisha Deborah akamwambia Sele.
DEBORAH: Natumaini utakuwa mume mwema, nawatakia maisha marefu na usithubutu kuwa kama MUME GAIDI, pesa tafuta kwa njia halali na Mungu atakuwezesha.
Waliyafurahia yale mahusia na kupiga makofi.
Baada ya hapo kikafanyika kikao cha mwisho cha familia na hapo ndipo Yuda nae akatangaza kumuoa Tina na hukuna aliyepinga.
Deborah aliamua kuwaaga na ndugu zake kuwa wanataka kurudi kwao Mwanza ila kabla ya kuondoka Patrick aliweka sherehe ya kuagana na familia ya kina Tusa.
Katika sherehe hiyo alimsimamisha Deborah na kuongea maneno haya,
"Huyu mwanamke mnayemuona mbele yenu, ndiye mama yangu, chakula changu, furaha yangu, amani yangu na kila kitu katika maisha yangu. Nampenda sana huyu mama, sitamtupa wala kumtenga hadi naingia kaburini"
Kisha akamuangalia kwa karibu Deborah na kumwambia,
"Nakupenda sana mama"
Akamkumbatia kwa furaha na kesho yake wakasafiri kurudi Mwanza wakiwa na furaha iliyopitiliza.
Pamela aliumia sana na kujiona kuwa na mkosi mkubwa sana maishani mwake. Kitendo cha kumtupa mtoto kilimuumiza sana.
Walipokuwa Mwanza, siku hiyo Patrick alilala usiku na kutokewa na mzimu wa mzee Ayubu kisha ukampungia mkono kama ishara ya kumuaga tena huku akitabasamu.

Bonge la story... Safi sana...

Chapter Closed...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom