Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

Dokta kashaambiwa kuwa anaeenda kutibiwa anatibiwa ili afe....sasa na yeye kajiongeza na nna uhakika hii taarifa atampelekea man Dizonga Mzee Wa mizoga afanye yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO. .

SEHEMU YA THELATHINI NA SABA.

_______________
ENDELEA........
________________
Kilio cha Dokta Smith, kilimfikia Dizonga aliyekuwepo nje, ilimbidi aingie ndani, akakutana na Ray Charles,

"unaenda wapi?" Ray Charles aliuliza huku akisimama,

"Dokta Smith analilia nini?" Dizonga aliuliza,

"Dizonga si nilishakuambia kazi yako iliishia getini, kinachoendelea ndani hakikuhusu tena" Ray Charles aliongea huku akimtazama Dizonga,

"sawa" Dizonga alijibu kinyonge na kuanza a kuondoka, ila alikuwa anataka sana kujua kinachomliza Dokta Smith, ila hakubahatika kujua, Dizonga alitoka nje na kukaa ndani ya uzio huku akiwa ameegemea gari yake, Ray Charles nae akaja,

"unaweza kuondoka tu, sioni sababu ya wewe kuendelea kuwa hapa, sasa hivi sitoongea tena na mdomo" Ray Charles alimwambia Dizonga, Dizonga akaona isiwe tabu, akaingia ndani ya gari na kuondoka zake.

Ray Charles akarudi mpaka katika chumba alichokuwepo Dokta Smith, na kumkuta akimgeuza geuza BQ,

"naweza kumchukua nikamuhifadhi sehemu nyingine?" Ray Charles alimuuliza Dokta Smith,

"wapi? hospital?" Dokta Smith aliuliza,

"hospital? Amekufa nimpeleke hospital akafanye nini?" Ray Charles aliuliza,

"ngoja nijaribu kumtibu tu" Dokta Smith aliongea,

"kumtibu? Kutibu mtu aliyekufa?, acha upuuzi mzee, tunapotezeana muda ujue" Ray Charles aliuliza kwa mshangao,

"ngoja nikueleweshe, niliposema amekufa ni kwa sababu Kuna dawa moja tu ya kumtibu huyu, na inatakiwa ipatikane ndani ya masaa sita kuanzia sasa, na hiyo dawa inaweza kupatikana China, marekani au Israel. Kwa maana hiyo ni ngumu kupatikana, kwa hiyo huyu masaa machache sana ya kuishi" Dokta Smith aliongea kwa huzuni,

"kumbe wewe mzee ni mwendawazimu, ulikuwa unalia nini wakati mtu bado hajafa? Subiri masaa sita yafike ndio ulie" Ray Charles aliongea na kumtazama BQ,

"sawa, mimi naomba uniachie huru niondoke, kwa maana hata nikitumia ujuzi gani, sitoweza kuokoa maisha ya huyu dada bila ya hiyo dawa" Dokta Smith aliongea,

"uondoke? Kuondoka huwezi mzee, mpaka tujue hatma ya huyu mwanamke" Ray Charles aliongea,

"bila hiyo dawa, hakuna hatma nyingine zaidi ya kifo, Nyie mlimuweka ndani siku zote bila hata ya kumpa chakula, mlikuwa mnategemea nini?" Dokta Smith aliongea kwa ukali na kufanya Ray Charles atabasamu,

"huyo dawa inaitwaje?" Ray Charles aliuliza,

"tremols" Dokta Smith alijibu,

"Sasa hivi ni saa ngapi? " Ray Charles aliuliza na kumfanya Dokta Smith atazame saa yake,

" saa moja kasoro robo" Dokta Smith alijibu,

"kwa maana hiyo mpaka Ikifika saa saba usiku, huyu mwanamke anatakiwa awe ameipata hiyo dawa?" Ray Charles aliuliza,

"ndio, lakini haipatikani, na ukisena uagize kutoka nje, haiwezi kufika ndani ya hayo masaa" Dokta Smith aliongea,

"ngoja nikajaribu kuzunguka hospitali, naweza kubahatisha" Ray Charles aliongea na kumfanya Dokta Smith amuangalie tu,

"hapa nchini hazipo" Dokta Smith aliongea,

"uwa sijafunzwa kukata tamaa, ngoja nikajaribu" Ray Charles aliongea huku akitoka nje, akaingia chumbani kwake na kuchukua funguo ya gari, kisha akarudi mpaka katika chumba alichokuwepo Dokta Smith na BQ, akakifunga kwa nje na kuondoka zake, aliamua kwenda kujaribu kutafuta dawa, ingawa aliambiwa hazipatikani.

**************

Tom alikuwa kama amechanganyikiwa, sasa alianza kuona mambo ni ya moto, alishaanza kuogopa baada ya kutekwa na kisha mtekaji kumuachia na kumwambia akimbie.

Tom alivyokuwa upande wa nyuma ya hospitali, ndipo alipohisi simu yake ikiita, alipoangalia jina la mpigaji, alikuta ni ile namba ya mkuu wa polisi, Tom hakupokea wala hakutaka simu, ila aliirudisha mfukoni ikiwa vile vile, kisha Tom akarudi taratibu mpaka maeneo ya wodi aliyolazwa, alikaa kwa mbali sana, ndipo aliposhuhudia vijana wawili wa makamo yake wenye makoti ya kofia wakiingia katika ile wodi, baada ya dakika akawaona wale vijana wakitoka huku wakiwa wamehamaki, wakaanza kuingia kila wodi, hapo ndipo akajua kweli alikuwa akitafutwa, Tom akaanza kuondoka , alihisi huenda mkuu wa polisi anahusika na huu mchezo wa yeye kutaka kukamatwa.

Tom alirudi mpaka upande wa nyuma wa hospital, na kupanda ukutani, kisha akarukia nje, akaanza kukimbia kuelekea nyumbani kwa mpenzi wake, alikimbia akachoka, maana kumbuka Tom ni lazy. Tom akasimamisha boda, akapanda na kumpa Dereva maelekezo ni wapi ampeleke.

Boda boda akaondoa pikipiki kwa kasi. Baada ya dakika tano pikipiki ilikuwa mlangoni katika chumba anaichoishi mpenzi wake Tom, bahati nzuri walimkuta na yeye amebeba kikapu kidogo, alikuwa anataka kutoka,

"wewe umeruhusiwa? Mimi ndio nilikuwa nakuletea chakula hivyo" Mpenzi wake Tom aliongea huku akimshangaa Tom,

"una buku jero hapo?" Tom alimuuliza mpenzi wake,

"nina elfu mbili" Mpenzi wake alijibu huku bado akimshangaa Tom,

"mpe hiyo hiyi" Tom aliongea na kisha mpenzi wake akafungua pochi yake, na kutoa noti ya elfu mbili, akampa Dereva bodaboda, dereva akaipokea nw kumrudishia mia tano, kisha Dereva akaondoka,

"vipi mwenzetu, mbona hima hima?" Mpenzi wake alimuuliza,

"tuingie ndani kwanza" Tom aliongea huku akitangulia kuingia ndani,

"wewe leo upo tofauti sana, au kile kipigo cha yule baba kimekutia wendawazimu?" Mpenzi wake aliuliza huku nae akimfuata Tom, akaingia mpaka ndani na kumkuta Tom akiwa amesimama,

"enhe, nambie" Mpenzi wake alianza kumuongelesha,

"tunatakiwa tuhame hapa, vinginevyo nitakufa, kuna watu wananiwinda, wanataka waniue" Tom aliongea huku akihema haraka haraka,
"haka mwenzangu, wewe hama tu, mimi siwezi kuondoka hapa" Mpenzi wake aliongea huku akimshangaa Tom,

"kwa hiyo lile balaa la usiku wa kuamkia leo unajifanya hukuliona? hujaona nilivyopigwa mpaka nikazimia? na mbaya zaidi Kuna watu wengine walikuja kunitafuta hospital na walitaka kuniua, hao watu ni tofauti na yule mtu aliyenivamia usiku" Tom aliongea na mpenzi wake akashtuka,

"lakini umewafanya nini wewe? Mbona unapenda kujiweka mashakani?" Mpenzi wake aliuliza,

"Mama, tuondoke, hayo maswali tutayajua mbele ya safari" Tom aliongea,

" tunaenda wapi sasa?" Mpenzi wake aliuliza,

"twende tukakae Lodge kwa muda, alafu tutatafuta chumba"" Tom aliongea,

"una pesa sasa?" Mpenzi wake aliuliza,

"ipo, mshahara wangu bado unaingia katika account yangu ya bank, nitautumia huo huo" Tom aliongea,

"sawa, kesho asubuhi tutaondoka" Mpenzi wa Tom aliongea,

"pumbavu kabisa, tuondoke sasa hivi tukalale uko, hiyo kesho tutarudi kuhamisha nguo tu" Tom aliongea kwa hasira,

"jamani!!!, na vyombo je?" Mpenzi wake aliuliza,

"bwana, kama unataka kufa, endelea kubaki hapa, mimi acha niondoke" Tom aliongea kwa hasira huku akiondoka,

"nisubiri sasa angalau nibebe nguo mbili tu" Mpenzi wake aliongea kwa kulalamika,

"wewe unaudhi, hujui tu" Tom aliongea huku akisimama mlangoni,

"jamani, yamekuwa hayo tena?" Mpenzi wake Tom aliongea huku akifungua kabati na kutoa nguo chache na kuziweka katika begi.

**************

Dizonga baada ya kuondoka nyumbani kwa Ray Charles, alirudi nyumbani kwake, alipofika alioga na kisha akaenda mezani na kupakua chakula.

"mgonjwa ulimpelekea chakula?" Dizonga aliuliza,

"ndio" Mke wake alijibu,

"sawa, ngoja nikakae nae, nina maongezi nae kidogo" Dizonga aliongea huku akibeba chakula chake, na kuelekea moja kwa moja katika chumba alichokuwepo Sajenti Minja,

"X soldier vipi?" Dizonga aliongea huku akikaa kitanda karibu na Sajenti Minja,

"poa ndugu" Sajenti Minja alijibu,

"umeuona yule Dokta, nimetoka kumtoa gerezani leo kwa oda ya Rais, kuna mgonjwa anatakiwa akamtibu" Dizonga aliongea,

"huyu Dokta si ndo yule Dokta Smith, alishikwa baada ya kupatikana na hatia ya kumtibu yule mwanamke muuaji?" Sajenti Minja aliuliza,

"ndio huyo huyo, kumbe upo makini?" Dizonga aliuliza,

"ni mgonjwa yupi anaenda kumtibu, kiasi kwamba akatolewa magereza bila kusomewa hukumu yake?" Sajenti Minja aliuliza,

"huyo mgonjwa hata mimi simjui" Dizonga alijibu, hakutaka kumuweka wazi Sajenti Minja,

"atakuwa ni ndugu wa Rais tu" Sajenti Minja aliongea,

"itakuwa hivyo. sasa X soldier, nimeongea na daktari mmoja ambaye ni rafiki yangu, amesema nikupeleke usiku ukafanyiwe vipimo vya X Ray, maana Dokta Smith leo amenisisitiza sana ufanyiwe vipimo ili kesho aanze kusimamia matibabu yako" Dizonga aliongea,

"vipi mazingira ya hiyo hospital unayotaka kunipeleka? hakuna unoko wowote?" Sajenti Minja aliuliza,

"sikutaka kumwambia kuwa mgonjwa ninayempeleka ni mtu anayetafutwa, maana ningemwambia hivyo inaweza kuwa sio salama kwetu, watu hawaaminiki siku hizi" Dizonga aliongea,

"ni kweli, ila hakushangaa uliposema mgonjwa wako utampeleka usiku?" Sajenti Minja aliuliza,

"alishangaa, ila nilimwambia nafanya hivyo kwa kuwa mgonjwa anatoka safarini, na anaingia usiku" Dizonga alijibu,

"sawa, tunaenda saa ngapi?" Sajenti Minja aliuliza,

"kwenye saa tano hivi, sasa hivi ni saa mbili kasoro" Dizonga aliongea huku akitazama saa katika simu yake,

"sawa ndugu yangu" Sajenti Minja aliongea,

"poa, acha nikaongee na wife, muda ukifika nitakuja" Dizonga aliongea huku akiinuka,

"sawa" Sajenti Minja aliongea huku akimtazama Dizonga aliyekuwa akitoka nje.

************

Mishale ya saa tano na dakika tatu, Dizonga alikuwa anaegesha gari ndani ya uzio wa hospital, kisha Dizonga akatelemka na kuzunguka upande wa pili, akamtoa Sajenti Minja na kumsaidia kutembea, waliingia mpaka ndani ya jengo la hospital na kuelekea moja kwa moja katika ofisi ya daktari aliyeongea na Dizonga,

"Karibu, umechelewa kama dakika tano hivi, usingekunikuta kwa maana nilidhani hutokuja tena, sema tu Kuna rafiki yangu amenipigia simu, amesema anakuja kuchukua dawa" Daktari aliongea,

"samahani kwa kuchelewa, si unajua gari zinazotoka mikoani uwa haziingii kwa muda?" Dizonga aliongea na kisha Sajenti Minja akamsapoti kwa kuchezesha kichwa chake kwa kukipandisha na kukishusha,

"mimi nadhani twendeni moja kwa moja katika vipimo, si ni x-ray tu?" Daktari aliuliza,

"ndio, ni x-ray tu" Dizonga alijibu, kisha daktari akavuta kiti cha matairi na kumtaka Sajenti Minja akae, Sajenti Minja alivyokaa, Dizonga akaanza kusukuma kiti cha matairi kumfuata daktari

Safari yao iliishia ndani ya chumba kikubwa ambacho kilikuwa na nafasi ndogo ya kupumzika mgonjwa baada ya vipimo, na pia kulikuwa na chumba kidogo chenye machine za kisasa za x-ray.

"muingize ndani ya chumba" Daktari aliongea huku akiingia katika kile chumba chenye machine za x-ray, Dizonga akaingia na Sajenti Minja,

"muweke juu ya hiki kitanda" Daktari aliongea na kisha Dizonga akambeba Sajenti Minja na kumuweka juu ya kitanda kile kilichozungukwa na vifaa vya kisasa kabisa,

"tutoke nje sasa" Daktari aliongea kisha Dizonga akatangulia kutoka, daktari akafuatia, chumba kile wakakifunga, kisha daktari akahamia katika computer,

"ni x-ray ya mwili mzima?" Daktari aliuliza,

"ndio" Dizonga alijibu,

"sawa " Daktari aliongea kisha akabonyeza bonyeza computer, kile chumba alichokuwepo Sajenti Minja kikatoa mwanga mwekundu kwa sekunde thelathini, kisha ule mwanga ukazima,

"ingia umtoe" Daktari aliongea na Dizonga akaingia katika kile chumba na kumtoa Sajenti Minja,

"funua mashuka na umuingize humo, kuna kitanda cha kupumzikia, kwa maana mwanga wa x-ray sio mzuri, anatakiwa apumzike kama dakika kumi hivi" Daktari aliongea, kisha Sajenti Minja akaingia katika kile chumba kilichofunikwa na mashuka, akakuta Kuna kitanda kidogo, akamlaza Sajenti Minja, Dizonga akarudi kwa daktari aliyekuwa bize na computer,

"alipata ajali huyu?" Daktari aliuliza,

"alipigwa na wenzake, sijui walizurumiana" Dizonga aliongea na kipindi hicho simu ya daktari ilikuwa ikiita, akatabasamu na kupokea,

"njoo kwenye chumba cha x-ray, acha uboya wakati maelekezo nilishakupa" Daktari aliongea na kukata simu, akaendelea kutabasamu,

"unasema alipigwa?" Daktari aliuliza huku akimuangalia Dizonga,

"ndio, wenzake walimchangia" Dizonga aliongea,

"khaaa, walikuwa wanampa kipigo cha aina gani? maana dah!!" Daktari aliongea huku akitazama computer na sura aliikunja aliikunja, na muda huo mlango wa mule ndani ulifunguliwa, akaingia Ray Charles, hapo Dizonga kidogo akimbie, maana hakutegemea kukutana na mtu huyo,

"dawa zikwapi wewe mwendawazimu?" Ray Charles aliuliza huku akimtazama daktari ambaye alikuwa akitabasamu tu,

"subiri basi, usiniendeshe mdogo wangu" Daktari aliongea Kwa utani na kumfanya Ray atabasamu,

"ujue nina mgonjwa anatakiwa apate hizo dawa haraka, yaani apate kabla ya saa saba, sasa hivi ni saa sita na dakika kumi" Ray Charles aliongea huku akiweka msisitizo,

"subiri nikakuletee, ningojee hapa hapa" Daktari aliongea huku akiinuka katika kiti na kutoka nje, akamuacha ndani Ray Charles na Dizonga ambaye alikuwa na wasiwasi muda wote,

"vipi sasa hivi upo huku, una mgonjwa?" Ray Charles alimuuliza Dizonga,

"ndio, ndio ninae. Vipi mgonjwa wenu anaendeleaje?" Dizonga aliamua kubadili mada,

"ndio hizi dawa nimemfuatia hapa, hali yake sio nzuri" Ray Charles alijibu na kipindi hicho yule Daktari alikuwa akirudi na mfuko mdogo uliojaa dawa.

"shika vizuri, zifiche kweli kweli, maana hizi dawa uwa hazitolewi kawaida" Daktari aliongea huku akimpatia Ray Charles ule mfuko wa dawa,

"sawa, wewe endelea na kazi, nitakuona kesho kama dawa zitafanya kazi" Ray Charles aliongea,

"sawa, mimi kuna mgonjwa namuangalia hapa, aisee kaumia umia mifupa mpaka inatisha" Daktari aliongea na kumfanya Ray Charles asogee katika computer na yeye akatazama, hapo Dizonga alikuwa na hofu kuu, moyoni alimlaumu Daktari kwa kulopoka,

"Yupo hai au amekufa?" Ray Charles aliuliza huku akitazama computer,

"Yupo hai, yupo katika chumba cha mashuka umo" Daktari aliongea na kufanya Dizonga sasa Jasho lianze kumtoka,

"Dizonga, ni ndugu yako?" Ray Charles alimuuliza Dizonga ambaye hata sura ilionesha wasiwasi,

"ndugu yake huyo, ndio kamleta hapa" Daktari alijibu na kumfanya Dizonga amtukanie tusi la nguoni, ila alimtukania moyoni,

"naweza kumuona?" Ray Charles alimuuliza Dizonga,

"muangalie tu" Daktari alijibu tena kabla hata Dizonga hajajibu,

"muache apumzike, utakuja kumuona kesho home " Dizonga alijibu,

"ndugu yako ni ndugu yetu, ngoja nimuone ili siku nyingine nisimpite barabarani" Ray Charles aliongea na kwenda kufungua mashuka ya kile chumba, akamkuta Sajenti Minja akiwa amelala kitandani.

Dizonga alitoka nje kabisa, alijua ndani kumeshaharibika.......

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO. .

SEHEMU YA THELATHINI NA SABA.

_______________
ENDELEA........
________________
Kilio cha Dokta Smith, kilimfikia Dizonga aliyekuwepo nje, ilimbidi aingie ndani, akakutana na Ray Charles,

"unaenda wapi?" Ray Charles aliuliza huku akisimama,

"Dokta Smith analilia nini?" Dizonga aliuliza,

"Dizonga si nilishakuambia kazi yako iliishia getini, kinachoendelea ndani hakikuhusu tena" Ray Charles aliongea huku akimtazama Dizonga,

"sawa" Dizonga alijibu kinyonge na kuanza a kuondoka, ila alikuwa anataka sana kujua kinachomliza Dokta Smith, ila hakubahatika kujua, Dizonga alitoka nje na kukaa ndani ya uzio huku akiwa ameegemea gari yake, Ray Charles nae akaja,

"unaweza kuondoka tu, sioni sababu ya wewe kuendelea kuwa hapa, sasa hivi sitoongea tena na mdomo" Ray Charles alimwambia Dizonga, Dizonga akaona isiwe tabu, akaingia ndani ya gari na kuondoka zake.

Ray Charles akarudi mpaka katika chumba alichokuwepo Dokta Smith, na kumkuta akimgeuza geuza BQ,

"naweza kumchukua nikamuhifadhi sehemu nyingine?" Ray Charles alimuuliza Dokta Smith,

"wapi? hospital?" Dokta Smith aliuliza,

"hospital? Amekufa nimpeleke hospital akafanye nini?" Ray Charles aliuliza,

"ngoja nijaribu kumtibu tu" Dokta Smith aliongea,

"kumtibu? Kutibu mtu aliyekufa?, acha upuuzi mzee, tunapotezeana muda ujue" Ray Charles aliuliza kwa mshangao,

"ngoja nikueleweshe, niliposema amekufa ni kwa sababu Kuna dawa moja tu ya kumtibu huyu, na inatakiwa ipatikane ndani ya masaa sita kuanzia sasa, na hiyo dawa inaweza kupatikana China, marekani au Israel. Kwa maana hiyo ni ngumu kupatikana, kwa hiyo huyu masaa machache sana ya kuishi" Dokta Smith aliongea kwa huzuni,

"kumbe wewe mzee ni mwendawazimu, ulikuwa unalia nini wakati mtu bado hajafa? Subiri masaa sita yafike ndio ulie" Ray Charles aliongea na kumtazama BQ,

"sawa, mimi naomba uniachie huru niondoke, kwa maana hata nikitumia ujuzi gani, sitoweza kuokoa maisha ya huyu dada bila ya hiyo dawa" Dokta Smith aliongea,

"uondoke? Kuondoka huwezi mzee, mpaka tujue hatma ya huyu mwanamke" Ray Charles aliongea,

"bila hiyo dawa, hakuna hatma nyingine zaidi ya kifo, Nyie mlimuweka ndani siku zote bila hata ya kumpa chakula, mlikuwa mnategemea nini?" Dokta Smith aliongea kwa ukali na kufanya Ray Charles atabasamu,

"huyo dawa inaitwaje?" Ray Charles aliuliza,

"tremols" Dokta Smith alijibu,

"Sasa hivi ni saa ngapi? " Ray Charles aliuliza na kumfanya Dokta Smith atazame saa yake,

" saa moja kasoro robo" Dokta Smith alijibu,

"kwa maana hiyo mpaka Ikifika saa saba usiku, huyu mwanamke anatakiwa awe ameipata hiyo dawa?" Ray Charles aliuliza,

"ndio, lakini haipatikani, na ukisena uagize kutoka nje, haiwezi kufika ndani ya hayo masaa" Dokta Smith aliongea,

"ngoja nikajaribu kuzunguka hospitali, naweza kubahatisha" Ray Charles aliongea na kumfanya Dokta Smith amuangalie tu,

"hapa nchini hazipo" Dokta Smith aliongea,

"uwa sijafunzwa kukata tamaa, ngoja nikajaribu" Ray Charles aliongea huku akitoka nje, akaingia chumbani kwake na kuchukua funguo ya gari, kisha akarudi mpaka katika chumba alichokuwepo Dokta Smith na BQ, akakifunga kwa nje na kuondoka zake, aliamua kwenda kujaribu kutafuta dawa, ingawa aliambiwa hazipatikani.

**************

Tom alikuwa kama amechanganyikiwa, sasa alianza kuona mambo ni ya moto, alishaanza kuogopa baada ya kutekwa na kisha mtekaji kumuachia na kumwambia akimbie.

Tom alivyokuwa upande wa nyuma ya hospitali, ndipo alipohisi simu yake ikiita, alipoangalia jina la mpigaji, alikuta ni ile namba ya mkuu wa polisi, Tom hakupokea wala hakutaka simu, ila aliirudisha mfukoni ikiwa vile vile, kisha Tom akarudi taratibu mpaka maeneo ya wodi aliyolazwa, alikaa kwa mbali sana, ndipo aliposhuhudia vijana wawili wa makamo yake wenye makoti ya kofia wakiingia katika ile wodi, baada ya dakika akawaona wale vijana wakitoka huku wakiwa wamehamaki, wakaanza kuingia kila wodi, hapo ndipo akajua kweli alikuwa akitafutwa, Tom akaanza kuondoka , alihisi huenda mkuu wa polisi anahusika na huu mchezo wa yeye kutaka kukamatwa.

Tom alirudi mpaka upande wa nyuma wa hospital, na kupanda ukutani, kisha akarukia nje, akaanza kukimbia kuelekea nyumbani kwa mpenzi wake, alikimbia akachoka, maana kumbuka Tom ni lazy. Tom akasimamisha boda, akapanda na kumpa Dereva maelekezo ni wapi ampeleke.

Boda boda akaondoa pikipiki kwa kasi. Baada ya dakika tano pikipiki ilikuwa mlangoni katika chumba anaichoishi mpenzi wake Tom, bahati nzuri walimkuta na yeye amebeba kikapu kidogo, alikuwa anataka kutoka,

"wewe umeruhusiwa? Mimi ndio nilikuwa nakuletea chakula hivyo" Mpenzi wake Tom aliongea huku akimshangaa Tom,

"una buku jero hapo?" Tom alimuuliza mpenzi wake,

"nina elfu mbili" Mpenzi wake alijibu huku bado akimshangaa Tom,

"mpe hiyo hiyi" Tom aliongea na kisha mpenzi wake akafungua pochi yake, na kutoa noti ya elfu mbili, akampa Dereva bodaboda, dereva akaipokea nw kumrudishia mia tano, kisha Dereva akaondoka,

"vipi mwenzetu, mbona hima hima?" Mpenzi wake alimuuliza,

"tuingie ndani kwanza" Tom aliongea huku akitangulia kuingia ndani,

"wewe leo upo tofauti sana, au kile kipigo cha yule baba kimekutia wendawazimu?" Mpenzi wake aliuliza huku nae akimfuata Tom, akaingia mpaka ndani na kumkuta Tom akiwa amesimama,

"enhe, nambie" Mpenzi wake alianza kumuongelesha,

"tunatakiwa tuhame hapa, vinginevyo nitakufa, kuna watu wananiwinda, wanataka waniue" Tom aliongea huku akihema haraka haraka,
"haka mwenzangu, wewe hama tu, mimi siwezi kuondoka hapa" Mpenzi wake aliongea huku akimshangaa Tom,

"kwa hiyo lile balaa la usiku wa kuamkia leo unajifanya hukuliona? hujaona nilivyopigwa mpaka nikazimia? na mbaya zaidi Kuna watu wengine walikuja kunitafuta hospital na walitaka kuniua, hao watu ni tofauti na yule mtu aliyenivamia usiku" Tom aliongea na mpenzi wake akashtuka,

"lakini umewafanya nini wewe? Mbona unapenda kujiweka mashakani?" Mpenzi wake aliuliza,

"Mama, tuondoke, hayo maswali tutayajua mbele ya safari" Tom aliongea,

" tunaenda wapi sasa?" Mpenzi wake aliuliza,

"twende tukakae Lodge kwa muda, alafu tutatafuta chumba"" Tom aliongea,

"una pesa sasa?" Mpenzi wake aliuliza,

"ipo, mshahara wangu bado unaingia katika account yangu ya bank, nitautumia huo huo" Tom aliongea,

"sawa, kesho asubuhi tutaondoka" Mpenzi wa Tom aliongea,

"pumbavu kabisa, tuondoke sasa hivi tukalale uko, hiyo kesho tutarudi kuhamisha nguo tu" Tom aliongea kwa hasira,

"jamani!!!, na vyombo je?" Mpenzi wake aliuliza,

"bwana, kama unataka kufa, endelea kubaki hapa, mimi acha niondoke" Tom aliongea kwa hasira huku akiondoka,

"nisubiri sasa angalau nibebe nguo mbili tu" Mpenzi wake aliongea kwa kulalamika,

"wewe unaudhi, hujui tu" Tom aliongea huku akisimama mlangoni,

"jamani, yamekuwa hayo tena?" Mpenzi wake Tom aliongea huku akifungua kabati na kutoa nguo chache na kuziweka katika begi.

**************

Dizonga baada ya kuondoka nyumbani kwa Ray Charles, alirudi nyumbani kwake, alipofika alioga na kisha akaenda mezani na kupakua chakula.

"mgonjwa ulimpelekea chakula?" Dizonga aliuliza,

"ndio" Mke wake alijibu,

"sawa, ngoja nikakae nae, nina maongezi nae kidogo" Dizonga aliongea huku akibeba chakula chake, na kuelekea moja kwa moja katika chumba alichokuwepo Sajenti Minja,

"X soldier vipi?" Dizonga aliongea huku akikaa kitanda karibu na Sajenti Minja,

"poa ndugu" Sajenti Minja alijibu,

"umeuona yule Dokta, nimetoka kumtoa gerezani leo kwa oda ya Rais, kuna mgonjwa anatakiwa akamtibu" Dizonga aliongea,

"huyu Dokta si ndo yule Dokta Smith, alishikwa baada ya kupatikana na hatia ya kumtibu yule mwanamke muuaji?" Sajenti Minja aliuliza,

"ndio huyo huyo, kumbe upo makini?" Dizonga aliuliza,

"ni mgonjwa yupi anaenda kumtibu, kiasi kwamba akatolewa magereza bila kusomewa hukumu yake?" Sajenti Minja aliuliza,

"huyo mgonjwa hata mimi simjui" Dizonga alijibu, hakutaka kumuweka wazi Sajenti Minja,

"atakuwa ni ndugu wa Rais tu" Sajenti Minja aliongea,

"itakuwa hivyo. sasa X soldier, nimeongea na daktari mmoja ambaye ni rafiki yangu, amesema nikupeleke usiku ukafanyiwe vipimo vya X Ray, maana Dokta Smith leo amenisisitiza sana ufanyiwe vipimo ili kesho aanze kusimamia matibabu yako" Dizonga aliongea,

"vipi mazingira ya hiyo hospital unayotaka kunipeleka? hakuna unoko wowote?" Sajenti Minja aliuliza,

"sikutaka kumwambia kuwa mgonjwa ninayempeleka ni mtu anayetafutwa, maana ningemwambia hivyo inaweza kuwa sio salama kwetu, watu hawaaminiki siku hizi" Dizonga aliongea,

"ni kweli, ila hakushangaa uliposema mgonjwa wako utampeleka usiku?" Sajenti Minja aliuliza,

"alishangaa, ila nilimwambia nafanya hivyo kwa kuwa mgonjwa anatoka safarini, na anaingia usiku" Dizonga alijibu,

"sawa, tunaenda saa ngapi?" Sajenti Minja aliuliza,

"kwenye saa tano hivi, sasa hivi ni saa mbili kasoro" Dizonga aliongea huku akitazama saa katika simu yake,

"sawa ndugu yangu" Sajenti Minja aliongea,

"poa, acha nikaongee na wife, muda ukifika nitakuja" Dizonga aliongea huku akiinuka,

"sawa" Sajenti Minja aliongea huku akimtazama Dizonga aliyekuwa akitoka nje.

************

Mishale ya saa tano na dakika tatu, Dizonga alikuwa anaegesha gari ndani ya uzio wa hospital, kisha Dizonga akatelemka na kuzunguka upande wa pili, akamtoa Sajenti Minja na kumsaidia kutembea, waliingia mpaka ndani ya jengo la hospital na kuelekea moja kwa moja katika ofisi ya daktari aliyeongea na Dizonga,

"Karibu, umechelewa kama dakika tano hivi, usingekunikuta kwa maana nilidhani hutokuja tena, sema tu Kuna rafiki yangu amenipigia simu, amesema anakuja kuchukua dawa" Daktari aliongea,

"samahani kwa kuchelewa, si unajua gari zinazotoka mikoani uwa haziingii kwa muda?" Dizonga aliongea na kisha Sajenti Minja akamsapoti kwa kuchezesha kichwa chake kwa kukipandisha na kukishusha,

"mimi nadhani twendeni moja kwa moja katika vipimo, si ni x-ray tu?" Daktari aliuliza,

"ndio, ni x-ray tu" Dizonga alijibu, kisha daktari akavuta kiti cha matairi na kumtaka Sajenti Minja akae, Sajenti Minja alivyokaa, Dizonga akaanza kusukuma kiti cha matairi kumfuata daktari

Safari yao iliishia ndani ya chumba kikubwa ambacho kilikuwa na nafasi ndogo ya kupumzika mgonjwa baada ya vipimo, na pia kulikuwa na chumba kidogo chenye machine za kisasa za x-ray.

"muingize ndani ya chumba" Daktari aliongea huku akiingia katika kile chumba chenye machine za x-ray, Dizonga akaingia na Sajenti Minja,

"muweke juu ya hiki kitanda" Daktari aliongea na kisha Dizonga akambeba Sajenti Minja na kumuweka juu ya kitanda kile kilichozungukwa na vifaa vya kisasa kabisa,

"tutoke nje sasa" Daktari aliongea kisha Dizonga akatangulia kutoka, daktari akafuatia, chumba kile wakakifunga, kisha daktari akahamia katika computer,

"ni x-ray ya mwili mzima?" Daktari aliuliza,

"ndio" Dizonga alijibu,

"sawa " Daktari aliongea kisha akabonyeza bonyeza computer, kile chumba alichokuwepo Sajenti Minja kikatoa mwanga mwekundu kwa sekunde thelathini, kisha ule mwanga ukazima,

"ingia umtoe" Daktari aliongea na Dizonga akaingia katika kile chumba na kumtoa Sajenti Minja,

"funua mashuka na umuingize humo, kuna kitanda cha kupumzikia, kwa maana mwanga wa x-ray sio mzuri, anatakiwa apumzike kama dakika kumi hivi" Daktari aliongea, kisha Sajenti Minja akaingia katika kile chumba kilichofunikwa na mashuka, akakuta Kuna kitanda kidogo, akamlaza Sajenti Minja, Dizonga akarudi kwa daktari aliyekuwa bize na computer,

"alipata ajali huyu?" Daktari aliuliza,

"alipigwa na wenzake, sijui walizurumiana" Dizonga aliongea na kipindi hicho simu ya daktari ilikuwa ikiita, akatabasamu na kupokea,

"njoo kwenye chumba cha x-ray, acha uboya wakati maelekezo nilishakupa" Daktari aliongea na kukata simu, akaendelea kutabasamu,

"unasema alipigwa?" Daktari aliuliza huku akimuangalia Dizonga,

"ndio, wenzake walimchangia" Dizonga aliongea,

"khaaa, walikuwa wanampa kipigo cha aina gani? maana dah!!" Daktari aliongea huku akitazama computer na sura aliikunja aliikunja, na muda huo mlango wa mule ndani ulifunguliwa, akaingia Ray Charles, hapo Dizonga kidogo akimbie, maana hakutegemea kukutana na mtu huyo,

"dawa zikwapi wewe mwendawazimu?" Ray Charles aliuliza huku akimtazama daktari ambaye alikuwa akitabasamu tu,

"subiri basi, usiniendeshe mdogo wangu" Daktari aliongea Kwa utani na kumfanya Ray atabasamu,

"ujue nina mgonjwa anatakiwa apate hizo dawa haraka, yaani apate kabla ya saa saba, sasa hivi ni saa sita na dakika kumi" Ray Charles aliongea huku akiweka msisitizo,

"subiri nikakuletee, ningojee hapa hapa" Daktari aliongea huku akiinuka katika kiti na kutoka nje, akamuacha ndani Ray Charles na Dizonga ambaye alikuwa na wasiwasi muda wote,

"vipi sasa hivi upo huku, una mgonjwa?" Ray Charles alimuuliza Dizonga,

"ndio, ndio ninae. Vipi mgonjwa wenu anaendeleaje?" Dizonga aliamua kubadili mada,

"ndio hizi dawa nimemfuatia hapa, hali yake sio nzuri" Ray Charles alijibu na kipindi hicho yule Daktari alikuwa akirudi na mfuko mdogo uliojaa dawa.

"shika vizuri, zifiche kweli kweli, maana hizi dawa uwa hazitolewi kawaida" Daktari aliongea huku akimpatia Ray Charles ule mfuko wa dawa,

"sawa, wewe endelea na kazi, nitakuona kesho kama dawa zitafanya kazi" Ray Charles aliongea,

"sawa, mimi kuna mgonjwa namuangalia hapa, aisee kaumia umia mifupa mpaka inatisha" Daktari aliongea na kumfanya Ray Charles asogee katika computer na yeye akatazama, hapo Dizonga alikuwa na hofu kuu, moyoni alimlaumu Daktari kwa kulopoka,

"Yupo hai au amekufa?" Ray Charles aliuliza huku akitazama computer,

"Yupo hai, yupo katika chumba cha mashuka umo" Daktari aliongea na kufanya Dizonga sasa Jasho lianze kumtoka,

"Dizonga, ni ndugu yako?" Ray Charles alimuuliza Dizonga ambaye hata sura ilionesha wasiwasi,

"ndugu yake huyo, ndio kamleta hapa" Daktari alijibu na kumfanya Dizonga amtukanie tusi la nguoni, ila alimtukania moyoni,

"naweza kumuona?" Ray Charles alimuuliza Dizonga,

"muangalie tu" Daktari alijibu tena kabla hata Dizonga hajajibu,

"muache apumzike, utakuja kumuona kesho home " Dizonga alijibu,

"ndugu yako ni ndugu yetu, ngoja nimuone ili siku nyingine nisimpite barabarani" Ray Charles aliongea na kwenda kufungua mashuka ya kile chumba, akamkuta Sajenti Minja akiwa amelala kitandani.

Dizonga alitoka nje kabisa, alijua ndani kumeshaharibika.......

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
Ooh C'mon kimenuka tayari....

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom