Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA NNE.

_______________
ENDELEA........
________________

Baada ya Ray Charles kuvua gloves, akamtazama BQ kwa dakika,

"mikataba ipo wapi?" Ray Charles alimuuliza BQ, ila bahati mbaya BQ hakuwa na fahamu, alikuwa amelala tu, Damu zilikuwa zikimtoka katika jeraha lake baada ya kutupwa chini na Ray Charles hapo hawali.

"ngoja kwanza" Ray Charles aliongea na kutoka nje, hapo akamkuta Rais akiwa na Dizonga na vijana wengine wakiongea mambo mawili matatu,

"kazi imeisha?" Rais alimuuliza Ray Charles,

"bado" Ray Charles alijibu kwa upole,

"Kwanini Ray, au unampenda huyu mwanamke?" Rais aliuliza,

"Kuna wazo nimepata, tunaweza kujadiliana kidogo?" Ray Charles aliuliza,

"tujadiliane hapa au ndani?" Rais aliuliza,

"tuingie ndani" Ray Charles na kutangulia kuingia ndani, Rais alikuja kwa nyuma na kumtupia jicho BQ,

"Ray bwana, kumbe ulishaanza kumuadhibu, kwanini umeacha sasa?" Rais aliongea huku akicheka kwa dhiaka,

"Kuna kitu nimefikiria mkuu, mimi bado sijataka tumuue huyu, endapo tunamuua na mikataba haijapatikana, inaweza kufanya usiwe na amani katika utawala wako, tena amani itapotea zaidi endapo mikataba itakuwa mikononi kwa wapinzani, wanaweza kuleta kashfa itakayokufanya uachie madaraka" Ray Charles aliongea na kuangalia chini,

"hiyo haiwezekani, wananchi waandamane niachie madaraka? haiwezekani, nitawamaliza vibaya mno" Rais aliongea kwa jazba,

"pia hata jeshi linaweza kukuondoa madarakani endapo utakiuka haki za wanadamu" Ray Charles aliendelea kuongea,

"Ray hiyo ndio point uliyoniitia baada ya kushindwa kumuua huyu mwanamke?" Rais aliuliza kwa ukali,

"hapana, point niliyokuitia ni kwamba hatupaswi kumuua huyu mwanamke mpaka aamke na tupate mikataba" Ray Charles aliongea,

"anaamka vipi sasa na tumeshindwa kupata suluhisho la kumuamsha?" Rais aliendelea kuuliza kwa jazba,

"mimi suluhisho nadhani nimelipata, ingawa linaweza kusaidia au kutosaidia, ila ni vyema tujaribu" Ray Charles aliongea na kumkazia jicho Rais,

"sema sasa, haya mambo ya kuongea nusunusu ni kupoteza muda Ray" Rais aliongea huku jazba bado zikiwa zimemtawala,

"Kuna yule Dokta wa kizungu ambaye yupo gerezani anakabiliwa na kesi ya kumsaidia mtuhumiwa, yule Dokta ni bora tumfanyie mpango tu atolewe, alafu tumchukue ili aje kumtibu huyu mwanamke" Ray Charles aliongea na kumuangalia Rais.

Rais akafikiria kwa muda, alihisi hilo ni wazo zuri sana,

"ni wazo zuri Ray, hapo ndio umeongea point, sio mwanzo ulikuwa unabwabwaja tu utumbo" Rais aliongea huku akimpiga piga bega Ray Charles,

"Sasa naomba hiyo kazi ya kwenda kumtorosha unipe mimi" Ray Charles aliongea,

"hapana Ray, nipe muda wa kufikiri kwanza ili nipate njia sahihi ya kumtwaa yule Dokta, tusije kufanya makosa kama tuliyoyafanya hospitali kipindi unaenda kumchukua huyu mwanamke" Rais aliongea kwa sauti tulivu,

"sitofanya makosa, nipe hiyo nafasi" Ray Charles alisihi,

"hapana Ray, nipe muda wa kufikiri kwanza, hilo wazo lako ni zuri sana" Rais aliongea,

"Mkuu huyu mwanamke endapo siku ya leo itaisha na ataendelea kuwa hivi na chakula hapati, anaweza kufa" Rais Charles aliongea,

"Ray acha ubishani, nimekwambia nipe muda. Unataka niongeeje ili nieleweke?" Rais aliuliza,

"sawa" Ray Charles alijibu,

"funga mlango na tutoke nje" Rais aliongea na kisha Ray Charles akatoka nje huku Rais akiwa nyuma yake. Walipotoka nje, Ray Charles alifunga mlango kisha akafuata uelekeo alioendea Rais.

***************

Mkuu wa polisi bado kichwa kilikuwa kinamuuma, yaani lile tukio la hospital, hasa hasa kumuona tena Ray Charles, yaani ni tukio ambalo hakuwa analiamini kabisa,

"kumbe Minja alikuwa hatua moja mbele yangu. Nakumbuka aliwahi kunambia kuwa kipindi kile yule mwanamke muuaji alivyopigwa risasi, alipigwa na Ray Charles, ila nikamuona Minja mpumbavu, nilihisi anakurupuka tu" Mkuu wa polisi alikuwa akiwaza mwenyewe,

"Sasa Kuna nini kati ya huyu mwanamke na Ray Charles??" Mkuu wa polisi alijiuliza,

"nimekumbuka, kulikuwa na kesi hapa ya kijana mmoja kudai kutekwa na Ray Charles, nayo niliipuuza, ngoja niangalie sasa" Mkuu wa polisi aliwaza na kuchukua simu yake, kisha akapiga namba ya kaunta, simu iliita kidogo tu na kupokelewa,

"naam mkuu" Polisi aliyepo kaunta aliitika baada ya kupokea simu,

"nitafutie kabrasha moja la kesi ya utekaji, jina la mtuhumiwa ni Ray Charles, alafu niletee ofisini kwangu" Mkuu wa polisi aliongea,

"sawa mkuu" Askari aliyepo kaunta alijibu kisha mkuu wa polisi akakata simu, akawa anangojea hilo file la kesi.

Baada ya nusu saa mlango wa ofisi ya mkuu wa polisi uligongwa,

"ingia" Mkuu wa polisi aliongea kisha mlango ukafunguliwa na akaingia Askari mmoja aliyekuwa na makabrasha mkononi, yule Askari baada ya kuingia akapiga saluti, kisha akamkabidhi mkuu wa polisi yake makabrasha aliyoyashika mkononi, kisha yule Askari akageuka kikakamavu na kuondoka ndani ya ofisi ya mkuu wa polisi.

Mkuu wa polisi akasoma jalada la juu ya lile kabrasha, kisha akafungua ndani na kuanza kusoma maelezo yalioyoandikwa, aliyarudia kusoma mara mbili, kisha akakutana na jina la mtoa tuhuma, alikuwa ni Thomas Anthony ambaye anadai alitekwa na Ray Charles, kisha akasababishiwa maumivu ya mwili kwa kupigwa.

Na uzuri ni kuwa namba ya simu ya Tom aliiacha katika lile kabrasha, huo ukawa msaada mwingine kwa mkuu wa polisi, yaani ilimrahisishia kazi mkuu wa polisi, ilikuwa rahisi zaidi kumpata Tom.

***********

Tom alizinduka saa moja jioni na kujikuta yupo hospital amezungushiwa bandeji kichwani, pembeni alikuwa mpenzi wake,

"ha!!! Tom umeamka?" Mpenzi wake aliuliza kwa mshangao, na muda huo Tom alikuwa akiangaza macho yake kushoto na kulia, akijaribu kuyasoma mazingira ya mule ndani,

"ngoja nikamuite daktari" Mpenzi wake aliongea huku akiinuka kitandani,

"ngoja, nani kanileta hapa?" Tom aliuliza huku akijitahidi kukaa,

"majirani tu, toka saa kumi alfajili mpaka sasa hivi ulikuwa umezimia, ulikuwa unakufa Tom" Mpenzi waliongea na kumfanya Tom aanze kuvuta kumbukumbu, hapo ndipo alikumbuka kilichomtokea,

"wewe hujaumia?" Tom alimuuliza mpenzi wake,

"hapana, nipo poa tu" Mpenzi wake alijibu,

"ilikuwa hatari sana" Tom aliongea na kusikitika,

"kwani yule kaka aliyetuvamia ulimfanya nini? Mbona alionekana kama Kuna kitu anakuonya?" Mpenzi wake aliuliza,

"Yule ndiye yule aliyenitekaga kipindi kile nikaja kuokolewa na Sajenti Minja" Tom aliongea,

"ila wewe Tom usikute ulianza kumchokonoa wewe, haiwezekani mtu aje tu atuvamie usiku" mpenzi wake aliongea,

"umeshaanza, yaani wewe imani yako siku zote ni kwamba kila tukio linalonikuta, basi mimi ndio uwa mchokozi" Tom aliongea kwa hasira,

"mimi nakujua wewe, sio mgeni wa matukio yako" Mpenzi wake Tom aliongea na wakati huo simu ya Tom ilikuwa ikiita,

"allow" Mpenzi wake alipokea, kwa maana simu ilikuwa mikononi kwake,

"hujambo?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"sijambo, shikamoo" Mpenzi wa Tom aliamkia baada ya kugundua anaongea na mtu aliyemzidi umri,

"marahaba, hii ni namba yako au umepokea tu" Sauti ya upande wa pili iliuliza, ikabidi mpenzi wa Tom ampe simu Tom,

"nani? " Tom alimuuliza mpenzi wake,

"sijui, ongea nae" Mpenzi wake alijibu.

"naam" Tom aliongea,

"wewe ndio Thomas Anthony?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"ndio" Tom alijibu,

"unaweza kufika kituo cha polisi leo?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"Kuna nini?" Tom aliuliza,

"wewe si umeshawahi kuleta kesi ya kutekwa na kuteswa hapa kituoni?" Sauti ilihoji na kumfanya Tom afikirie kidogo,

"ndio, ni mimi" Tom alijibu,

"uje sasa kituoni, kuna maswali machache nataka nikuulize" Sauti iliongea,

"mimi nipo hospital, nimelazwa, usiku wa kuamkia leo Ray Charles alinivamia na kutaka kuniua" Tom aliongea kwa jazba,

"tena? sawa nakuja hapo, hospital gani" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"siwezi kukutajia hospital niliyopo, kwa sababu sikuamini" Tom aliongea,

"mimi ni mkuu wa polisi wa mkoa, niamini tu" Sauti ya upande wa pili ilijibu na kufanya Tom kufikiria kwa muda kidogo,

"sawa, nipo hospital ya mkoa" Tom alijibu

"sawa, nakuja" Mkuu wa polisi aliongea na kukata simu,

"afadhali nimempata huyu kijana, hii itakuwa ni kazi rahisi sana kupata angalau mwanga kuhusu Ray Charles, na leo tena alimvamia eti!!" Mkuu wa polisi aliongea na kuvua miwani yake, akasikia simu yake ikiita, alipotupia macho katika kioo cha simu yake, akakuta anaepiga ni Rais, akapokea haraka,.

"ndio mkuu" Mkuu wa polisi aliongea kwa sauti tulivu,

"nasikia yule mwanamke muuaji alitoroshwa hospitali?" Rais aliuliza,

"ndio mkuu, ila aliyemtorosha nimeshamtambua" Mkuu wa polisi alijikuta anaongea kwa uoga ili aonekane ni mchapa kazi,

"ni nani huyo?" Rais aliuliza huku akipata hofu,

"Kuna mtu mmoja namuhisi, anaitwa Ray Charles" Mkuu wa polisi aliongea na kufanya moyo wa Rais upige kwa kasi zaidi,

"unamuhisi? kwa hiyo unafanya kazi kwa kuhisi bila kuwa na uhakika?" Rais aliuliza kwa sauti Kali,

"Kuna video niliichukua hospitali inayoonesha hilo tukio, pia Kuna kesi mbili tatu zipo hapa kituoni zinazomuhusu huyo mtu, ya kwanza ni ile inayofanana na hii, kwamba aliwahi kumpiga risasi yule mwanamke muuaji, na ya pili ni kuwa Kuna kijana alishawahi kumteka na kumjeruhi, na usiku wa kuamkia leo alimvamia nyumbani kwake na kumpiga, huyo kijana yupo hospital ya mkoa amelazwa, nataka niende baadae nikamuhoji" Mkuu wa polisi aliongea na kushangaa simu ikikikatwa,

"sijui hajapenda maongezi yangu" Mkuu wa polisi aliongea na kuiweka simu mezani.

Kwa upande wa Rais alionekana ana gadhabu sana kusikia zile habari kutoka kwa mkuu wa polisi. Rais akapiga simu kwa vijana wake wanne, haraka sana wakawa wamefika katika ofisi ya Rais,

"Ray kawa mpumbavu sana, nilijua amemuua Tom kumbe hajamuua!!, sasa basi, Nyie wanne, nataka mpange mpango wa dakika kumi wa kuingia katika hospital ya mkoa na mkammalize Tom, kwa maana ameshakuwa kikwazo sasa, endapo mkuu wa polisi ataenda kumuhoji, basi Ray atakuwa muarifu anayetafutwa" Rais aliongea kwa jazba,

"picha yake ipo?" Dizonga aliuliza,

"ninayo " Kijana mwingine alijibu,

"sawa, twendeni, tukifika, mimi nitakaa upande wa ndani wa geti, jirani na mlinzi, alafu Oppy utakuwa nje katika gari, Ally na Tod mtaingia ndani, msimuue ndani ya hospital, maana kuna camera, isije ikawa umeme kama aliofanya Ray" Dizonga aliwapanga wenzake,

"kwa hiyo mtafanyaje?" Rais aliuliza,

"huyu tutafanya kama tunamtorosha, alafu tutakuja nae huku, kummaliza" Dizonga aliongea,

"wazo zuri D, fanyeni hivyo" Rais aliongea,

"na pale hospital itabidi tutoke nae kirafiki, au tuvae kinyago usoni ili camera zisinase nyuso zetu" Dizonga aliongea,

"sio lazima vinyago, hata makoti yenye kofia yanaweza kuwa msaada" Kijana mwingine aliongea,

"tutatumia makoti tu" Mwingine aliunga mkono,

"sawa, nendeni sasa" Rais aliongea na kisha vijana wakajiandaa na kuingia katika gari, safari ya kwenda hospitali ikaanza.

Walitumia muda mfupi kufika hospital, Dizonga akashuka na kuongea na simu kwa muda mfupi, kisha akarudi ndani ya gari na kukuta wenzake wakimaliza kuchora ramani ya mipango yao,

"wewe Dizonga utakaa hapa getini kwa ndani, Oppy utakuwa katika gari nje, hakikisha gari imewaka muda wote, alafu mimi na ally tunaingia wodi hadi wodi kumtafuta huyo maiti mtarajiwa" Kijana mmoja aliongea na kisha wakapeana tano wote kama ishara ya kukubaliana kwa kile wanachofanya. Wakatelemka na kufanya kama walivyopanga.

**********

Tom alikuwa amekaa kitandani akimsubiri mkuu wa polisi muda huo, alikuwa akichezea simu yake, ghafla mlango ukafunguliwa, akaingia Dizonga akiwa na koti lenye kofia kubwa, Tom alishtuka kwa maana sura ya Dizonga ilionesha imekuja kishari tu, Tom akataka kumuuliza yeye ni nani, lakini hakupata muda huo, kwani Dizonga aliruka na kutua juu ya kitanda, kisha akamkaba Tom mpaka akapoteza fahamu, kisha akatoka nae huku akiwa anamsukuma na toroli ya wagonjwa, koridoni alipishana na mkuu wa polisi akielekea katika wanapotoka wao, Dizonga akatabasamu baada ya kupishana na mkuu wa polisi,

"kwisha kazi" Dizonga aliongea wakati akimtoa Tom nje, Tom ambaye hakuwa anajitambua wakati huo......

********ITAENDELEA********

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA NNE.

_______________
ENDELEA........
________________

Baada ya Ray Charles kuvua gloves, akamtazama BQ kwa dakika,

"mikataba ipo wapi?" Ray Charles alimuuliza BQ, ila bahati mbaya BQ hakuwa na fahamu, alikuwa amelala tu, Damu zilikuwa zikimtoka katika jeraha lake baada ya kutupwa chini na Ray Charles hapo hawali.

"ngoja kwanza" Ray Charles aliongea na kutoka nje, hapo akamkuta Rais akiwa na Dizonga na vijana wengine wakiongea mambo mawili matatu,

"kazi imeisha?" Rais alimuuliza Ray Charles,

"bado" Ray Charles alijibu kwa upole,

"Kwanini Ray, au unampenda huyu mwanamke?" Rais aliuliza,

"Kuna wazo nimepata, tunaweza kujadiliana kidogo?" Ray Charles aliuliza,

"tujadiliane hapa au ndani?" Rais aliuliza,

"tuingie ndani" Ray Charles na kutangulia kuingia ndani, Rais alikuja kwa nyuma na kumtupia jicho BQ,

"Ray bwana, kumbe ulishaanza kumuadhibu, kwanini umeacha sasa?" Rais aliongea huku akicheka kwa dhiaka,

"Kuna kitu nimefikiria mkuu, mimi bado sijataka tumuue huyu, endapo tunamuua na mikataba haijapatikana, inaweza kufanya usiwe na amani katika utawala wako, tena amani itapotea zaidi endapo mikataba itakuwa mikononi kwa wapinzani, wanaweza kuleta kashfa itakayokufanya uachie madaraka" Ray Charles aliongea na kuangalia chini,

"hiyo haiwezekani, wananchi waandamane niachie madaraka? haiwezekani, nitawamaliza vibaya mno" Rais aliongea kwa jazba,

"pia hata jeshi linaweza kukuondoa madarakani endapo utakiuka haki za wanadamu" Ray Charles aliendelea kuongea,

"Ray hiyo ndio point uliyoniitia baada ya kushindwa kumuua huyu mwanamke?" Rais aliuliza kwa ukali,

"hapana, point niliyokuitia ni kwamba hatupaswi kumuua huyu mwanamke mpaka aamke na tupate mikataba" Ray Charles aliongea,

"anaamka vipi sasa na tumeshindwa kupata suluhisho la kumuamsha?" Rais aliendelea kuuliza kwa jazba,

"mimi suluhisho nadhani nimelipata, ingawa linaweza kusaidia au kutosaidia, ila ni vyema tujaribu" Ray Charles aliongea na kumkazia jicho Rais,

"sema sasa, haya mambo ya kuongea nusunusu ni kupoteza muda Ray" Rais aliongea huku jazba bado zikiwa zimemtawala,

"Kuna yule Dokta wa kizungu ambaye yupo gerezani anakabiliwa na kesi ya kumsaidia mtuhumiwa, yule Dokta ni bora tumfanyie mpango tu atolewe, alafu tumchukue ili aje kumtibu huyu mwanamke" Ray Charles aliongea na kumuangalia Rais.

Rais akafikiria kwa muda, alihisi hilo ni wazo zuri sana,

"ni wazo zuri Ray, hapo ndio umeongea point, sio mwanzo ulikuwa unabwabwaja tu utumbo" Rais aliongea huku akimpiga piga bega Ray Charles,

"Sasa naomba hiyo kazi ya kwenda kumtorosha unipe mimi" Ray Charles aliongea,

"hapana Ray, nipe muda wa kufikiri kwanza ili nipate njia sahihi ya kumtwaa yule Dokta, tusije kufanya makosa kama tuliyoyafanya hospitali kipindi unaenda kumchukua huyu mwanamke" Rais aliongea kwa sauti tulivu,

"sitofanya makosa, nipe hiyo nafasi" Ray Charles alisihi,

"hapana Ray, nipe muda wa kufikiri kwanza, hilo wazo lako ni zuri sana" Rais aliongea,

"Mkuu huyu mwanamke endapo siku ya leo itaisha na ataendelea kuwa hivi na chakula hapati, anaweza kufa" Rais Charles aliongea,

"Ray acha ubishani, nimekwambia nipe muda. Unataka niongeeje ili nieleweke?" Rais aliuliza,

"sawa" Ray Charles alijibu,

"funga mlango na tutoke nje" Rais aliongea na kisha Ray Charles akatoka nje huku Rais akiwa nyuma yake. Walipotoka nje, Ray Charles alifunga mlango kisha akafuata uelekeo alioendea Rais.

***************

Mkuu wa polisi bado kichwa kilikuwa kinamuuma, yaani lile tukio la hospital, hasa hasa kumuona tena Ray Charles, yaani ni tukio ambalo hakuwa analiamini kabisa,

"kumbe Minja alikuwa hatua moja mbele yangu. Nakumbuka aliwahi kunambia kuwa kipindi kile yule mwanamke muuaji alivyopigwa risasi, alipigwa na Ray Charles, ila nikamuona Minja mpumbavu, nilihisi anakurupuka tu" Mkuu wa polisi alikuwa akiwaza mwenyewe,

"Sasa Kuna nini kati ya huyu mwanamke na Ray Charles??" Mkuu wa polisi alijiuliza,

"nimekumbuka, kulikuwa na kesi hapa ya kijana mmoja kudai kutekwa na Ray Charles, nayo niliipuuza, ngoja niangalie sasa" Mkuu wa polisi aliwaza na kuchukua simu yake, kisha akapiga namba ya kaunta, simu iliita kidogo tu na kupokelewa,

"naam mkuu" Polisi aliyepo kaunta aliitika baada ya kupokea simu,

"nitafutie kabrasha moja la kesi ya utekaji, jina la mtuhumiwa ni Ray Charles, alafu niletee ofisini kwangu" Mkuu wa polisi aliongea,

"sawa mkuu" Askari aliyepo kaunta alijibu kisha mkuu wa polisi akakata simu, akawa anangojea hilo file la kesi.

Baada ya nusu saa mlango wa ofisi ya mkuu wa polisi uligongwa,

"ingia" Mkuu wa polisi aliongea kisha mlango ukafunguliwa na akaingia Askari mmoja aliyekuwa na makabrasha mkononi, yule Askari baada ya kuingia akapiga saluti, kisha akamkabidhi mkuu wa polisi yake makabrasha aliyoyashika mkononi, kisha yule Askari akageuka kikakamavu na kuondoka ndani ya ofisi ya mkuu wa polisi.

Mkuu wa polisi akasoma jalada la juu ya lile kabrasha, kisha akafungua ndani na kuanza kusoma maelezo yalioyoandikwa, aliyarudia kusoma mara mbili, kisha akakutana na jina la mtoa tuhuma, alikuwa ni Thomas Anthony ambaye anadai alitekwa na Ray Charles, kisha akasababishiwa maumivu ya mwili kwa kupigwa.

Na uzuri ni kuwa namba ya simu ya Tom aliiacha katika lile kabrasha, huo ukawa msaada mwingine kwa mkuu wa polisi, yaani ilimrahisishia kazi mkuu wa polisi, ilikuwa rahisi zaidi kumpata Tom.

***********

Tom alizinduka saa moja jioni na kujikuta yupo hospital amezungushiwa bandeji kichwani, pembeni alikuwa mpenzi wake,

"ha!!! Tom umeamka?" Mpenzi wake aliuliza kwa mshangao, na muda huo Tom alikuwa akiangaza macho yake kushoto na kulia, akijaribu kuyasoma mazingira ya mule ndani,

"ngoja nikamuite daktari" Mpenzi wake aliongea huku akiinuka kitandani,

"ngoja, nani kanileta hapa?" Tom aliuliza huku akijitahidi kukaa,

"majirani tu, toka saa kumi alfajili mpaka sasa hivi ulikuwa umezimia, ulikuwa unakufa Tom" Mpenzi waliongea na kumfanya Tom aanze kuvuta kumbukumbu, hapo ndipo alikumbuka kilichomtokea,

"wewe hujaumia?" Tom alimuuliza mpenzi wake,

"hapana, nipo poa tu" Mpenzi wake alijibu,

"ilikuwa hatari sana" Tom aliongea na kusikitika,

"kwani yule kaka aliyetuvamia ulimfanya nini? Mbona alionekana kama Kuna kitu anakuonya?" Mpenzi wake aliuliza,

"Yule ndiye yule aliyenitekaga kipindi kile nikaja kuokolewa na Sajenti Minja" Tom aliongea,

"ila wewe Tom usikute ulianza kumchokonoa wewe, haiwezekani mtu aje tu atuvamie usiku" mpenzi wake aliongea,

"umeshaanza, yaani wewe imani yako siku zote ni kwamba kila tukio linalonikuta, basi mimi ndio uwa mchokozi" Tom aliongea kwa hasira,

"mimi nakujua wewe, sio mgeni wa matukio yako" Mpenzi wake Tom aliongea na wakati huo simu ya Tom ilikuwa ikiita,

"allow" Mpenzi wake alipokea, kwa maana simu ilikuwa mikononi kwake,

"hujambo?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"sijambo, shikamoo" Mpenzi wa Tom aliamkia baada ya kugundua anaongea na mtu aliyemzidi umri,

"marahaba, hii ni namba yako au umepokea tu" Sauti ya upande wa pili iliuliza, ikabidi mpenzi wa Tom ampe simu Tom,

"nani? " Tom alimuuliza mpenzi wake,

"sijui, ongea nae" Mpenzi wake alijibu.

"naam" Tom aliongea,

"wewe ndio Thomas Anthony?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"ndio" Tom alijibu,

"unaweza kufika kituo cha polisi leo?" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"Kuna nini?" Tom aliuliza,

"wewe si umeshawahi kuleta kesi ya kutekwa na kuteswa hapa kituoni?" Sauti ilihoji na kumfanya Tom afikirie kidogo,

"ndio, ni mimi" Tom alijibu,

"uje sasa kituoni, kuna maswali machache nataka nikuulize" Sauti iliongea,

"mimi nipo hospital, nimelazwa, usiku wa kuamkia leo Ray Charles alinivamia na kutaka kuniua" Tom aliongea kwa jazba,

"tena? sawa nakuja hapo, hospital gani" Sauti ya upande wa pili iliuliza,

"siwezi kukutajia hospital niliyopo, kwa sababu sikuamini" Tom aliongea,

"mimi ni mkuu wa polisi wa mkoa, niamini tu" Sauti ya upande wa pili ilijibu na kufanya Tom kufikiria kwa muda kidogo,

"sawa, nipo hospital ya mkoa" Tom alijibu

"sawa, nakuja" Mkuu wa polisi aliongea na kukata simu,

"afadhali nimempata huyu kijana, hii itakuwa ni kazi rahisi sana kupata angalau mwanga kuhusu Ray Charles, na leo tena alimvamia eti!!" Mkuu wa polisi aliongea na kuvua miwani yake, akasikia simu yake ikiita, alipotupia macho katika kioo cha simu yake, akakuta anaepiga ni Rais, akapokea haraka,.

"ndio mkuu" Mkuu wa polisi aliongea kwa sauti tulivu,

"nasikia yule mwanamke muuaji alitoroshwa hospitali?" Rais aliuliza,

"ndio mkuu, ila aliyemtorosha nimeshamtambua" Mkuu wa polisi alijikuta anaongea kwa uoga ili aonekane ni mchapa kazi,

"ni nani huyo?" Rais aliuliza huku akipata hofu,

"Kuna mtu mmoja namuhisi, anaitwa Ray Charles" Mkuu wa polisi aliongea na kufanya moyo wa Rais upige kwa kasi zaidi,

"unamuhisi? kwa hiyo unafanya kazi kwa kuhisi bila kuwa na uhakika?" Rais aliuliza kwa sauti Kali,

"Kuna video niliichukua hospitali inayoonesha hilo tukio, pia Kuna kesi mbili tatu zipo hapa kituoni zinazomuhusu huyo mtu, ya kwanza ni ile inayofanana na hii, kwamba aliwahi kumpiga risasi yule mwanamke muuaji, na ya pili ni kuwa Kuna kijana alishawahi kumteka na kumjeruhi, na usiku wa kuamkia leo alimvamia nyumbani kwake na kumpiga, huyo kijana yupo hospital ya mkoa amelazwa, nataka niende baadae nikamuhoji" Mkuu wa polisi aliongea na kushangaa simu ikikikatwa,

"sijui hajapenda maongezi yangu" Mkuu wa polisi aliongea na kuiweka simu mezani.

Kwa upande wa Rais alionekana ana gadhabu sana kusikia zile habari kutoka kwa mkuu wa polisi. Rais akapiga simu kwa vijana wake wanne, haraka sana wakawa wamefika katika ofisi ya Rais,

"Ray kawa mpumbavu sana, nilijua amemuua Tom kumbe hajamuua!!, sasa basi, Nyie wanne, nataka mpange mpango wa dakika kumi wa kuingia katika hospital ya mkoa na mkammalize Tom, kwa maana ameshakuwa kikwazo sasa, endapo mkuu wa polisi ataenda kumuhoji, basi Ray atakuwa muarifu anayetafutwa" Rais aliongea kwa jazba,

"picha yake ipo?" Dizonga aliuliza,

"ninayo " Kijana mwingine alijibu,

"sawa, twendeni, tukifika, mimi nitakaa upande wa ndani wa geti, jirani na mlinzi, alafu Oppy utakuwa nje katika gari, Ally na Tod mtaingia ndani, msimuue ndani ya hospital, maana kuna camera, isije ikawa umeme kama aliofanya Ray" Dizonga aliwapanga wenzake,

"kwa hiyo mtafanyaje?" Rais aliuliza,

"huyu tutafanya kama tunamtorosha, alafu tutakuja nae huku, kummaliza" Dizonga aliongea,

"wazo zuri D, fanyeni hivyo" Rais aliongea,

"na pale hospital itabidi tutoke nae kirafiki, au tuvae kinyago usoni ili camera zisinase nyuso zetu" Dizonga aliongea,

"sio lazima vinyago, hata makoti yenye kofia yanaweza kuwa msaada" Kijana mwingine aliongea,

"tutatumia makoti tu" Mwingine aliunga mkono,

"sawa, nendeni sasa" Rais aliongea na kisha vijana wakajiandaa na kuingia katika gari, safari ya kwenda hospitali ikaanza.

Walitumia muda mfupi kufika hospital, Dizonga akashuka na kuongea na simu kwa muda mfupi, kisha akarudi ndani ya gari na kukuta wenzake wakimaliza kuchora ramani ya mipango yao,

"wewe Dizonga utakaa hapa getini kwa ndani, Oppy utakuwa katika gari nje, hakikisha gari imewaka muda wote, alafu mimi na ally tunaingia wodi hadi wodi kumtafuta huyo maiti mtarajiwa" Kijana mmoja aliongea na kisha wakapeana tano wote kama ishara ya kukubaliana kwa kile wanachofanya. Wakatelemka na kufanya kama walivyopanga.

**********

Tom alikuwa amekaa kitandani akimsubiri mkuu wa polisi muda huo, alikuwa akichezea simu yake, ghafla mlango ukafunguliwa, akaingia Dizonga akiwa na koti lenye kofia kubwa, Tom alishtuka kwa maana sura ya Dizonga ilionesha imekuja kishari tu, Tom akataka kumuuliza yeye ni nani, lakini hakupata muda huo, kwani Dizonga aliruka na kutua juu ya kitanda, kisha akamkaba Tom mpaka akapoteza fahamu, kisha akatoka nae huku akiwa anamsukuma na toroli ya wagonjwa, koridoni alipishana na mkuu wa polisi akielekea katika wanapotoka wao, Dizonga akatabasamu baada ya kupishana na mkuu wa polisi,

"kwisha kazi" Dizonga aliongea wakati akimtoa Tom nje, Tom ambaye hakuwa anajitambua wakati huo......

********ITAENDELEA********

the Legend☆
Usilolijua ni sawa na usk wa giza.
Mkuu wa kituo ukijakushtuka baba utakua umechelewa sana dah.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom