Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI.

____________
ENDELEA..
_____________
"ujanja mfukoni, haya ebu niue sasa" Rais aliongea huku akimshikisha bastola BQ, lakini ndio hivyo tena, BQ hakuwa na fahamu.

"Ray kwanini umemleta, si ungemuua uko uko hospital?" Rais aliuliza huku akimuangalia Ray, hakujua kuwa Ray alishashindwa kumuua BQ, na alitorokwa ndani ya jengo la hospital, ila alimpata tena BQ kwa bahati tu.

"ni bora tungeipata mikataba kwanza ndipo tumuue, vinginevyo kama Ile mikataba itakuwa amempa mwanasheria au kaiweka sehemu, inaweza ikaja kutusumbua baadae hata kama huyu mwanamke atakuwa amekufa" Ray Charles alijibu,

"eti eee? Kwa Ray hiyo tunafanyaje sasa?" Rais aliuliza,
"huyu ni kumtafutia chumba na kumuacha mpaka fahamu zimrejee, alafu tutambana atuoneshe mikataba ilipo, tukiipata ndio tunamuua" Ray Charles aliongea,

"safi kabisa, je hospital hukukuta upinzani wowote?" Rais aliuliza,

"hapana" Ray Charles alijibu,

"sawa, huyu mpeleke katika vyumba vya nyumba ya nyuma, uko utamfungia katika chumba kimoja, nadhani utarudi kumuona tena kesho ili tujue hali yake" Rais aliongea huku akiondoka na kumuacha Ray Charles akiwa amesimama pembeni ya mwili wa BQ.

Rais alivyotoka tu, Ray Charles akambeba BQ na kutoka nae katika kile chumba cha kifo, na kumpeleka katika nyumba nyingine iliyokuwa upande wa nyuma katika eneo lile la ikulu. Alivyomfikisha alimtupa chini, BQ akadondokea katika lile jeraha lake la kichwani na kufanya damu zianze kutoka, Ray Charles hakujali, akatoka nje na kufunga mlango, kisha akaondoka zake.

******************

Edward Sambo alikuwa sebuleni kwake akipitia habari tofauti tofauti katika magazeti, alisikia mtu akigonga mlango,

"nani?" Edward Sambo aliuliza kwa uoga, alikuwa hajiamini kabisa tangu BQ amvamie mara mbili,

"mimi mlinzi" Mgonga hodi alijibu,

"unataka nini?" Edward Sambo aliuliza,.

"Kuna mgeni wako" Mlinzi alijibu,

"anaitwa nani?" Edward Sambo aliuliza kwa wasiwasi,

"Tom, Thomas Anthony" Mlinzi alijibu na kufanya Edward Sambo ashangae, maana ni muda sana hajawahi kukutana na Tom, na pia hawakuwa na mazoea sana, sasa alijiuliza Tom amefuata nini hapo?

"mruhusu aingie, ila mkagueni sana" Edward Sambo aliongea kisha yule mlinzi akarudi getini.

Baada ya muda Tom aliingia sebuleni kwa Edward Sambo, akamkuta Edward Sambo akisoma gazeti. Tom akaelekea moja kwa moja kukaa kwenye kochi,

"shikamoo mzee" Tom alimsalimia Edward Sambo,

"marahaba kijana, za siku?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"nzuri kwa kweli, ingawa kuna mitihani ya hapa na pale, Ila tunapambana" Tom alijibu huku akitabasamu,

"kweli kabisa, karibu sana, nikuketee kinywaji gani?" Edward Sambo aliuliza huku akisimama,

"hapana, nashukuru mzee" Tom aliongea na kumfanya Edward Sambo arudi kukaa katika kochi,

"umekujaje kujaje leo, umekuja kuchimba mambo yako au umekuja kuniona tu?" Edward Sambo aliuliza na kumfanya Tom atabasamu,

"nimekuja kujua ukweli kuhusu Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa, maana habari zinadai alikuwa hapa mara ya Mwisho kabla hajaondoka na mtuhumiwa" Tom aliongea na kumuangalia Edward Sambo,

"Kijana yaliyokukuta katika ufuatiliaji wako wa lile sakata la memory card bado umeyasahau? au unapenda tu kujitaftia matatizo mengine?" Edward Sambo aliongea huku akivua miwani,

"mimi sijaja kufuatilia habari yoyote, nafanya uchunguzi wangu kuhusu Sajenti Minja. Sajenti Minja amekuwa kama ndugu kwangu, na wewe ni mtu wake wa karibu siku nyingi sana" Tom aliongea na kutabasamu,

"Sasa unataka kuchunguza nini? Umeambiwa Minja ametoroshwa na wenzake, wenzake wakina nani? polisi? wanajeshi? Jibu litakuwa hapana, polisi wala mwanajeshi hawezi kumtorosha Minja, ila ni waarifu. Je kwanini waarifu wamtoroshe Minja? Kwa sababu ni mwenzao. Jibu ni rahisi tu" Edward Sambo aliongea,

"ni ngumu kuaminika kuwa Sajenti Minja ni muarifu, hainiingii akilini" Tom aliongea,

"endapo ungeona yale mazingira aliyoondoka nayo Minja huku akiwa na muarifu, na namna alivyokataa kuongozana na Askari wengine, basi usingekataa hiki nilichokueleza" Edward Sambo aliongea,

"sawa, huenda ni kweli, ila sijawahi kuhisi Waka kuona dalili kuwa Kuna uhusiano wowote kati ya Sajenti Minja na yule mwanamke muuaji" Tom aliongea,

"hivi unamjua yule mwanamke?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"nimeshawahi kuonana nae sana tu kabla hajaanza kufanya mauaji hapa mjini, maana alianzia katika wilaya niliyokuwa nafanyia kazi hapo awali" Tom alijibu,

"unamjua vizuri? Jibu ndio au hapana, hayo maelezo mengine ya nini sasa" Edward Sambo aliongea kwa ukali

"hapana, simjui" Tom alijibu,

"wewe si ulifuatilia kwa karibu sakata la memory card, kwanini unasema humjui yule mwanamke?" Edward Sambo aliuliza,

"inawezekana nimemsahau" Tom alijibu na kumfanya Edward Sambo acheke,
"ukija siku nyingine, nitakukumbusha" Edward Sambo aliongea,

"kwa hiyo huyu mwanamke ni zao la memory card?" Tom aliuliza huku akijaribu kuvuta kumbukumbu, ila kila kumbukumbu anayoivuta kuhusu mwanamke wa katika lile sakata, picha iliyokuwa ikimjia ni ya BQ, ila sasa anachojua yeye ni kuwa BQ alishakufa siku nyingi tu, huyu hawezi kuwa BQ kwa maana hata sura ni tofauti, huyu mwanamke wa sasa hivi havutii, ana majeraha usoni na isitoshe hana mkono mmoja.

"ndio, huyu mwanamke ni zao la memory card, kwa hiyo hapa kinachoendelea ni mambo yale yale ya memory card, huyu mwanamke and mikataba ambayo alisaini na Tammy Semmy, mikataba ya umiliki majengo, ila sasa serikali inamtambua Tammy Semmy ni muarifu, kwa hiyo mikataba yote aliyoingia na watu au nchi yoyote, hiyo mikataba ni batili, ila kwa sheria za kimataifa, hiyo ni Mikataba halali kabisa" Edward Sambo aliongea,

"kwa hiyo yule mwanamke ana haki?" Tom aliuliza,

"ndio, ila hatakiwi kuishi, kizazi chote kilichoisumbua nchi katika sakata la memory card, ni lazima kipotee, ibaki historia tu" Edward Sambo aliongea,

"duh, sawa mzee" Tom aliongea,

"ila si unajua hata yule mwanamke muuaji nae alikamatwa?" Edward Sambo aliuliza,

"ndio, ila nimesikia pia jana usiku alitoroshwa" Tom aliongea,

"ndio hivyo, sasa umeshajiuliza mtu aliyekuwa amezimia ametoshwaje?, polisi hawakuwepo, je walikuwa wapi? kama habari zinasema hakukuwa na Askari hata mmoja eneo lile la wodi, je nani aliwaondoa Askari pale? Kijana Kuna mambo mengi sana nyuma ya pazia" Edward Sambo aliongea na kutikisa kichwa,

"kweli, hayo maswali nilijiuliza sana, ila sikupata jibu, ila pia nikahisi huenda hospital watakuwa na camera zilizoshika hayo matukio" Tom aliongea,

"una akili sana, ila sasa kwanini hospital wapo kimya Mpaka muda huu?" Edward Sambo aliuliza,

"hapo ndio sijajua sasa" Tom alijibu,

"mimi ni mmoja wa watu wachache sana waliobahatika kuona video za lile tukio, kuna rafiki yangu yupo mule ndani, ni daktari, alinirushia kwa ufupi ile video. Ila hata polisi hawajaiona, na kwa maelezo ya ndani kabisa ya hospital, yanadai wamezuiwa wasiongee chochote, wajifanye hawajui chochote" Edward Sambo aliongea,

"ni nini kilitokea sasa?" Tom aliuliza,

"Kuna mtu aliingia ndani ya hospital usiku, akaingia na kuanza kupambana na yule dada, alafu kumbe yule mwanamke muuaji hakuwa amezimia, alikuwa amezinduka muda tu, madaktari wenyewe waligundua hilo baada ya kurudia rudia kutazama zile video. Basi yule mtu alipambana na yule mwanamke, ila yule mwanamke alipata upenyo, akatorokea dirishani, mpaka sasa hivi haijulikani alipokimbilia" Edward Sambo aliongea,

"Sasa kwanini serikali inaficha hii kitu?" Tom aliuliza,

"mimi nadhani Kuna mawili, la kwanza kulinda heshima ya polisi, kwa maana haiwezekani polisi wasiwepo eneo la tukio la kumlinda yule mwanamke muuaji. Pili, inawezekana hili tukio la huyu mwanamke kutoroka lilipangwa na viongozi wa serikali, au kwa kuongeza, inawezekana pia huyu mwanamke alitakiwa auawe bila kufikishwa kwenye vyombo vya sheria" Edward Sambo aliongea,

"hiyo video unayo hapo, video ya huyo mtu aliyekuwa akipambana na yule mwanamke muuaji?" Tom aliuliza,

"ndio, ninayo. Unataka kuiona?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"ipo, nitakurushia, ila hutakiwi kumuonesha mtu, endapo utamuonesha mtu na ikasambaa, ujue hakuna atayesalimika kati yetu" Edward Sambo aliongea,

"kuhusu hilo, usijali" Tom aliongea na kisha Edward Sambo akamrushia ile video. Wakaongea na mengine kwa masaa kadhaa, baadae Tom akaaga na kuondoka, huku akiwa na shauku ya kuiona ile video aliyorushiwa na Edward Sambo.

Tom aliondoka na kufika nyumbani kwake, alipofika cha kwanza alifungua ile video na kuanza kuangalia, alishtuka alipogundua kuwa yule mtu ni Ray Charles,

"ni nani huyu, na kwanini anafanya hivi?" Tom alijiuliza huku akishangaa namna BQ anavyokwepa zile ngumi za Ray Charles.

"nataka kumuona tena huyu mtu" Tom aliongea, huku akiingia Facebook, kisha akaipost ile video ya Ray Charles akipambana na BQ, hakuandika neno lolote, alitaka wahusika wenyewe wamtafute, ila aliamini ni ngumu sana watu kujua anapoishi, maana ni uswahilini, tena ndani ndani.

Muda ulizidi kwenda huku ile video ikizidi kusambaa mtandaoni, ingawa Tom hakuandika neno lolote, ila tayari ilishajulikana ile video ni ya mwanamke muuaji jinsi alivyotoroka hospital, ila yule mtu wa pili ambaye ni Ray Charles, hakuna aliyemjua.

Masaa yalizidi kusogea tu, mara Tom akaona simu yake ikiita, alipoangalia jina la mpigaji, alikuwa ni Edward Sambo, Tom hukupokea ile simu, alijua Edward Sambo hana la kumuuliza zaidi ya kuuliza kwa nini amepost ile video? Tom akaitupa simu pembeni na kulala, muda ulikuwa umeenda sana, ilikuwa saa tano usiku.

Tom akapitiwa usingizi na kulala.

Usiku mnene Tom alishtuka, alisikia kama mtu anajaribu kuvunja mlango wa chumba, Tom akawasha taa na kumuangalia mpenzi wake ambaye muda huo hakuwa na habari, alikuwa anakoroma tu kutokana na usingizi.

Tom akazidi kupata hofu, akataka kupiga kelele, ila akaona hapana, akaona inawezekana ni kibaka tu, Tom akazima taa na kubeba chuma moja nw kusimama nalo mlangoni, alichotaka kufanya ni kumpiga huyo mwizi endapo ataingia ndani.

Mlango uliendelea kuchokonolewa kitasa bila mafanikio yoyote, mwisho alisikia kama mtu ametupa kitu kama kisu au bisibisi chini, Tom akaamini kuwa huenda huyo mwizi ameshindwa kufungua kitasa.

Wakati Tom akiwa na imani hiyo, alisikia kishindo kikubwa kikifuatia na mlango kufunguka, mtu akasimama mlangoni, Tom hakuweza kumjua kutokana na giza, alichofanya Tom ni kunyanyua chuma chake na kukishusha kwa nguvu katika kifua cha yule mtu, ukatoka ukelele mkali wa chuma kugongana na chuma, Tom akashtuka na kuwasha taa, hakuamini macho yake kwa alichokiona, alikuwa ni Ray Charles akiwa amesimama mlangoni huku macho yake yakiwa yameiva kwa wekundu, hasira zilikuwa zimemtawala...

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆
Tom ss umekipata ulichokitafuta manina wwcheza sebene hilo kwa raha zako

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom