Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI.

____________
ENDELEA..
_____________
"ujanja mfukoni, haya ebu niue sasa" Rais aliongea huku akimshikisha bastola BQ, lakini ndio hivyo tena, BQ hakuwa na fahamu.

"Ray kwanini umemleta, si ungemuua uko uko hospital?" Rais aliuliza huku akimuangalia Ray, hakujua kuwa Ray alishashindwa kumuua BQ, na alitorokwa ndani ya jengo la hospital, ila alimpata tena BQ kwa bahati tu.

"ni bora tungeipata mikataba kwanza ndipo tumuue, vinginevyo kama Ile mikataba itakuwa amempa mwanasheria au kaiweka sehemu, inaweza ikaja kutusumbua baadae hata kama huyu mwanamke atakuwa amekufa" Ray Charles alijibu,

"eti eee? Kwa Ray hiyo tunafanyaje sasa?" Rais aliuliza,
"huyu ni kumtafutia chumba na kumuacha mpaka fahamu zimrejee, alafu tutambana atuoneshe mikataba ilipo, tukiipata ndio tunamuua" Ray Charles aliongea,

"safi kabisa, je hospital hukukuta upinzani wowote?" Rais aliuliza,

"hapana" Ray Charles alijibu,

"sawa, huyu mpeleke katika vyumba vya nyumba ya nyuma, uko utamfungia katika chumba kimoja, nadhani utarudi kumuona tena kesho ili tujue hali yake" Rais aliongea huku akiondoka na kumuacha Ray Charles akiwa amesimama pembeni ya mwili wa BQ.

Rais alivyotoka tu, Ray Charles akambeba BQ na kutoka nae katika kile chumba cha kifo, na kumpeleka katika nyumba nyingine iliyokuwa upande wa nyuma katika eneo lile la ikulu. Alivyomfikisha alimtupa chini, BQ akadondokea katika lile jeraha lake la kichwani na kufanya damu zianze kutoka, Ray Charles hakujali, akatoka nje na kufunga mlango, kisha akaondoka zake.

******************

Edward Sambo alikuwa sebuleni kwake akipitia habari tofauti tofauti katika magazeti, alisikia mtu akigonga mlango,

"nani?" Edward Sambo aliuliza kwa uoga, alikuwa hajiamini kabisa tangu BQ amvamie mara mbili,

"mimi mlinzi" Mgonga hodi alijibu,

"unataka nini?" Edward Sambo aliuliza,.

"Kuna mgeni wako" Mlinzi alijibu,

"anaitwa nani?" Edward Sambo aliuliza kwa wasiwasi,

"Tom, Thomas Anthony" Mlinzi alijibu na kufanya Edward Sambo ashangae, maana ni muda sana hajawahi kukutana na Tom, na pia hawakuwa na mazoea sana, sasa alijiuliza Tom amefuata nini hapo?

"mruhusu aingie, ila mkagueni sana" Edward Sambo aliongea kisha yule mlinzi akarudi getini.

Baada ya muda Tom aliingia sebuleni kwa Edward Sambo, akamkuta Edward Sambo akisoma gazeti. Tom akaelekea moja kwa moja kukaa kwenye kochi,

"shikamoo mzee" Tom alimsalimia Edward Sambo,

"marahaba kijana, za siku?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"nzuri kwa kweli, ingawa kuna mitihani ya hapa na pale, Ila tunapambana" Tom alijibu huku akitabasamu,

"kweli kabisa, karibu sana, nikuketee kinywaji gani?" Edward Sambo aliuliza huku akisimama,

"hapana, nashukuru mzee" Tom aliongea na kumfanya Edward Sambo arudi kukaa katika kochi,

"umekujaje kujaje leo, umekuja kuchimba mambo yako au umekuja kuniona tu?" Edward Sambo aliuliza na kumfanya Tom atabasamu,

"nimekuja kujua ukweli kuhusu Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa, maana habari zinadai alikuwa hapa mara ya Mwisho kabla hajaondoka na mtuhumiwa" Tom aliongea na kumuangalia Edward Sambo,

"Kijana yaliyokukuta katika ufuatiliaji wako wa lile sakata la memory card bado umeyasahau? au unapenda tu kujitaftia matatizo mengine?" Edward Sambo aliongea huku akivua miwani,

"mimi sijaja kufuatilia habari yoyote, nafanya uchunguzi wangu kuhusu Sajenti Minja. Sajenti Minja amekuwa kama ndugu kwangu, na wewe ni mtu wake wa karibu siku nyingi sana" Tom aliongea na kutabasamu,

"Sasa unataka kuchunguza nini? Umeambiwa Minja ametoroshwa na wenzake, wenzake wakina nani? polisi? wanajeshi? Jibu litakuwa hapana, polisi wala mwanajeshi hawezi kumtorosha Minja, ila ni waarifu. Je kwanini waarifu wamtoroshe Minja? Kwa sababu ni mwenzao. Jibu ni rahisi tu" Edward Sambo aliongea,

"ni ngumu kuaminika kuwa Sajenti Minja ni muarifu, hainiingii akilini" Tom aliongea,

"endapo ungeona yale mazingira aliyoondoka nayo Minja huku akiwa na muarifu, na namna alivyokataa kuongozana na Askari wengine, basi usingekataa hiki nilichokueleza" Edward Sambo aliongea,

"sawa, huenda ni kweli, ila sijawahi kuhisi Waka kuona dalili kuwa Kuna uhusiano wowote kati ya Sajenti Minja na yule mwanamke muuaji" Tom aliongea,

"hivi unamjua yule mwanamke?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"nimeshawahi kuonana nae sana tu kabla hajaanza kufanya mauaji hapa mjini, maana alianzia katika wilaya niliyokuwa nafanyia kazi hapo awali" Tom alijibu,

"unamjua vizuri? Jibu ndio au hapana, hayo maelezo mengine ya nini sasa" Edward Sambo aliongea kwa ukali

"hapana, simjui" Tom alijibu,

"wewe si ulifuatilia kwa karibu sakata la memory card, kwanini unasema humjui yule mwanamke?" Edward Sambo aliuliza,

"inawezekana nimemsahau" Tom alijibu na kumfanya Edward Sambo acheke,
"ukija siku nyingine, nitakukumbusha" Edward Sambo aliongea,

"kwa hiyo huyu mwanamke ni zao la memory card?" Tom aliuliza huku akijaribu kuvuta kumbukumbu, ila kila kumbukumbu anayoivuta kuhusu mwanamke wa katika lile sakata, picha iliyokuwa ikimjia ni ya BQ, ila sasa anachojua yeye ni kuwa BQ alishakufa siku nyingi tu, huyu hawezi kuwa BQ kwa maana hata sura ni tofauti, huyu mwanamke wa sasa hivi havutii, ana majeraha usoni na isitoshe hana mkono mmoja.

"ndio, huyu mwanamke ni zao la memory card, kwa hiyo hapa kinachoendelea ni mambo yale yale ya memory card, huyu mwanamke and mikataba ambayo alisaini na Tammy Semmy, mikataba ya umiliki majengo, ila sasa serikali inamtambua Tammy Semmy ni muarifu, kwa hiyo mikataba yote aliyoingia na watu au nchi yoyote, hiyo mikataba ni batili, ila kwa sheria za kimataifa, hiyo ni Mikataba halali kabisa" Edward Sambo aliongea,

"kwa hiyo yule mwanamke ana haki?" Tom aliuliza,

"ndio, ila hatakiwi kuishi, kizazi chote kilichoisumbua nchi katika sakata la memory card, ni lazima kipotee, ibaki historia tu" Edward Sambo aliongea,

"duh, sawa mzee" Tom aliongea,

"ila si unajua hata yule mwanamke muuaji nae alikamatwa?" Edward Sambo aliuliza,

"ndio, ila nimesikia pia jana usiku alitoroshwa" Tom aliongea,

"ndio hivyo, sasa umeshajiuliza mtu aliyekuwa amezimia ametoshwaje?, polisi hawakuwepo, je walikuwa wapi? kama habari zinasema hakukuwa na Askari hata mmoja eneo lile la wodi, je nani aliwaondoa Askari pale? Kijana Kuna mambo mengi sana nyuma ya pazia" Edward Sambo aliongea na kutikisa kichwa,

"kweli, hayo maswali nilijiuliza sana, ila sikupata jibu, ila pia nikahisi huenda hospital watakuwa na camera zilizoshika hayo matukio" Tom aliongea,

"una akili sana, ila sasa kwanini hospital wapo kimya Mpaka muda huu?" Edward Sambo aliuliza,

"hapo ndio sijajua sasa" Tom alijibu,

"mimi ni mmoja wa watu wachache sana waliobahatika kuona video za lile tukio, kuna rafiki yangu yupo mule ndani, ni daktari, alinirushia kwa ufupi ile video. Ila hata polisi hawajaiona, na kwa maelezo ya ndani kabisa ya hospital, yanadai wamezuiwa wasiongee chochote, wajifanye hawajui chochote" Edward Sambo aliongea,

"ni nini kilitokea sasa?" Tom aliuliza,

"Kuna mtu aliingia ndani ya hospital usiku, akaingia na kuanza kupambana na yule dada, alafu kumbe yule mwanamke muuaji hakuwa amezimia, alikuwa amezinduka muda tu, madaktari wenyewe waligundua hilo baada ya kurudia rudia kutazama zile video. Basi yule mtu alipambana na yule mwanamke, ila yule mwanamke alipata upenyo, akatorokea dirishani, mpaka sasa hivi haijulikani alipokimbilia" Edward Sambo aliongea,

"Sasa kwanini serikali inaficha hii kitu?" Tom aliuliza,

"mimi nadhani Kuna mawili, la kwanza kulinda heshima ya polisi, kwa maana haiwezekani polisi wasiwepo eneo la tukio la kumlinda yule mwanamke muuaji. Pili, inawezekana hili tukio la huyu mwanamke kutoroka lilipangwa na viongozi wa serikali, au kwa kuongeza, inawezekana pia huyu mwanamke alitakiwa auawe bila kufikishwa kwenye vyombo vya sheria" Edward Sambo aliongea,

"hiyo video unayo hapo, video ya huyo mtu aliyekuwa akipambana na yule mwanamke muuaji?" Tom aliuliza,

"ndio, ninayo. Unataka kuiona?" Edward Sambo alimuuliza Tom,

"ipo, nitakurushia, ila hutakiwi kumuonesha mtu, endapo utamuonesha mtu na ikasambaa, ujue hakuna atayesalimika kati yetu" Edward Sambo aliongea,

"kuhusu hilo, usijali" Tom aliongea na kisha Edward Sambo akamrushia ile video. Wakaongea na mengine kwa masaa kadhaa, baadae Tom akaaga na kuondoka, huku akiwa na shauku ya kuiona ile video aliyorushiwa na Edward Sambo.

Tom aliondoka na kufika nyumbani kwake, alipofika cha kwanza alifungua ile video na kuanza kuangalia, alishtuka alipogundua kuwa yule mtu ni Ray Charles,

"ni nani huyu, na kwanini anafanya hivi?" Tom alijiuliza huku akishangaa namna BQ anavyokwepa zile ngumi za Ray Charles.

"nataka kumuona tena huyu mtu" Tom aliongea, huku akiingia Facebook, kisha akaipost ile video ya Ray Charles akipambana na BQ, hakuandika neno lolote, alitaka wahusika wenyewe wamtafute, ila aliamini ni ngumu sana watu kujua anapoishi, maana ni uswahilini, tena ndani ndani.

Muda ulizidi kwenda huku ile video ikizidi kusambaa mtandaoni, ingawa Tom hakuandika neno lolote, ila tayari ilishajulikana ile video ni ya mwanamke muuaji jinsi alivyotoroka hospital, ila yule mtu wa pili ambaye ni Ray Charles, hakuna aliyemjua.

Masaa yalizidi kusogea tu, mara Tom akaona simu yake ikiita, alipoangalia jina la mpigaji, alikuwa ni Edward Sambo, Tom hukupokea ile simu, alijua Edward Sambo hana la kumuuliza zaidi ya kuuliza kwa nini amepost ile video? Tom akaitupa simu pembeni na kulala, muda ulikuwa umeenda sana, ilikuwa saa tano usiku.

Tom akapitiwa usingizi na kulala.

Usiku mnene Tom alishtuka, alisikia kama mtu anajaribu kuvunja mlango wa chumba, Tom akawasha taa na kumuangalia mpenzi wake ambaye muda huo hakuwa na habari, alikuwa anakoroma tu kutokana na usingizi.

Tom akazidi kupata hofu, akataka kupiga kelele, ila akaona hapana, akaona inawezekana ni kibaka tu, Tom akazima taa na kubeba chuma moja nw kusimama nalo mlangoni, alichotaka kufanya ni kumpiga huyo mwizi endapo ataingia ndani.

Mlango uliendelea kuchokonolewa kitasa bila mafanikio yoyote, mwisho alisikia kama mtu ametupa kitu kama kisu au bisibisi chini, Tom akaamini kuwa huenda huyo mwizi ameshindwa kufungua kitasa.

Wakati Tom akiwa na imani hiyo, alisikia kishindo kikubwa kikifuatia na mlango kufunguka, mtu akasimama mlangoni, Tom hakuweza kumjua kutokana na giza, alichofanya Tom ni kunyanyua chuma chake na kukishusha kwa nguvu katika kifua cha yule mtu, ukatoka ukelele mkali wa chuma kugongana na chuma, Tom akashtuka na kuwasha taa, hakuamini macho yake kwa alichokiona, alikuwa ni Ray Charles akiwa amesimama mlangoni huku macho yake yakiwa yameiva kwa wekundu, hasira zilikuwa zimemtawala...

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KWANZA.

Ni nyakati za saa mbili na nusu asubuhi, anaonekana mwanamke mmoja ambaye ukimtazama mara moja tu, hutosita kugundua kuwa mwanamke huyu ni kichaa, chizi, mwendawazimu au ni mtu mwenye matatizo mengi ya akili.

Alikuwa na nywele ndefu zilizokaa kwenye mpangilio mbovu kabisa, yaani zilikuwa shaghalabaghala huku baadhi ya upande wa kichwani kukiwa na uchafu uliokamatana na nywele zake zile ndefu ambazo kila mwanamke alitamani kuwa nazo kutokana na afya na urefu wa nywele ile, zilionekana hazijakuna na mafuta na shampoo kwa kipindi kirefu sana.

Katika uso wa mwanadada huyu, hakukuwa na tatizo, alionekana ana mvuto kidogo ingawa upande mmoja kulikuwa na makovu yalioonekana yameachwa kutokana na vidonda vilivyotokana na moto, makovu yale yalipanda mpaka upande mmoja kichwani na kufanya upande huo mmoja wa juu mbele, nywele kushindwa kuota, kwa hiyo alitumia mbinu za kuzilaza baadhi ya nywele zake upande ule wenye kovu na kufunika kwa kiasi kikubwa lile kovu lake la kichwani.

Endapo hutojali na kuamua kutumia muda wako mrefu kumuangalia huyo dada, utagundua kuwa huyo ni dada hata ngozi ya mwili wake ni nzuri, tena zile ngozi zilizozoea mafuta ya bei ghali ila alijitahidi kuificha ile ngozi na kuonekana kama mtu aliyetoka kufukuliwa kwenye shimo la mkaa.

Na kitu kingine ni kuwa huyu mwanamke hakuwa na mkono, mkono mmoja wa kulia ulikuwa umekatika, umekatikia juu ya kiwiko na kufanya kuwa na kipande cha mkono, ule mkono mwingine wa kushoto ulikuwa hauna kasoro na alikuwa ameshika mfuko wa nylon wenye rangi ya ubuluu, mifuko ile yenye mchoro wa muigizaji maarufu wa kimarekani mwenye hasili ya uitaliano na umarekani ajulikanaye kama Silvester Stallone, almaarufu kama RAMBO. Mifuko hiyo huku uswahilini tunaiita mifuko ya Rambo.

Dada yule alitembea mwendo wa polepole na gauni lake fupi la kulalia lilioishia juu ya magoti na lilikuwa na rangi halisi ya maziwa, ila kutokana na kufubaa, lilibadilika rangi na kuwa na rangi kama tatu mchanganyiko ambazo ni ugoro, weusi na maziwa.

Dada yule hakuonekana kujali namna watu wanavyomkwepa na wanavyomuangalia, aliendelea kutembea na mkono wake mmoja uliokuwa na mfuko wa Rambo ambao ndani yake kulikuwa na karatasi zisizojulikana.

Safari ya dada huyu iliishia kwenye ofisi kubwa ya serikali, ofisi ya mkuu wa wilaya. Dada akapita getini

"wewe unaenda wapi?" Mgambo aliyekuwa getini alimuuliza huku akimfuata kwa lengo la kumtoa nje, aliamini huyu mwanamke ni kichaa,

"leo si ni jumatatu? Mheshimiwa si kila jumatatu anasikiliza malalamiko ya wananchi wa eneo lake?" Dada yule aliuliza kwa sauti ya upole huku akimuangalia yule Mgambo,

"ndio, na wewe una malalamiko?" Mgambo aliuliza huku akiwa anaona kama anaongea na mwendawazimu,

"ndio, nahitaji kuonana nae"" Dada aliendelea kuongea kwa utulivu na kumfanya yule mgambo atoe cheko la dhihaka na kufanya mapengo yake yaonekane vyema,

"ebu nieleze hayo matatizo yako, nitayashughulikia" Mgambo aliongea na kumfanya yule dada atabasamu, meno yake meupe yakaonekana,

"anatakiwa ayasikie mkuu wa wilaya na wala sio mlinzi wa getini" Dada aliongea na kupiga hatua akielekea ndani, ila yule Mgambo alihisi amedharauliwa sana kwa ile kauli, kauli kutoka kwa mwendawazimu, Mgambo akakimbia na kusimama mbele ya yule mwanamke,

"hujaruhusiwa kuingia ndani, humu wanaingia watu wenye akili timamu tu" Mgambo aliongea kwa jazba,

"kwa hiyo mimi sina akili timamu? mimi na wewe nani chizi?" Dada aliongea huku akimuangalia Mgambo kwa dharau, Mgambo akaamua atumie nguvu sasa, akaanza kumsukuma yule mwanamke, mwanamke alitaka kujaribu kushindana ila alishindwa kwa kuwa hakuwa na nguvu na pia alikuwa akitumia mkono mmoja ingali mwenzie alitumia mikono miwili.

Katika kusukumana, yule dada akaangusha mfuko wake wa Rambo chini na yeye pia akaanguka chini. Alipofika chini alimkata jicho la hasira yule Mgambo ambaye bado pia nae alionekana pia ana hasira na yule mwanamke.

Yule mwanamke akainuka kwa hasira sasa ili kukabiliana na huyo Mgambo,

"kuna nini hapa?" Sauti ya ukali ilisikika ikiuliza na kumfanya yule mgambo ahache kukabiliana na yule mwanamke,

"si huyu mwendawazimu analazimisha kuingia ndani akaonane na mkuu wa wilaya" Mgambo alijibu huku akihema haraka haraka,

"eti ni kweli?" Kijana aliyejibiwa na Mgambo aliuliza huku akimuangalia yule mwanamke,

"sijalazimisha, ila kama utaratibu unavyokuwaga siku kama ya leo ni rasmi mkuu wa wilaya aliitenga kwa ajili ya kuongea na sisi wananchi wake, ndio nimekuja nashangaa napita getini huyu mlinzi ananizuia" Yule mwanamke alijibu kwa utulivu huku akimuangalia yule kijana aliyevaa mavazi nadhifu,

"yaani una maongezi na mkuu wa wilaya, si ndio?" Kijana aliuliza huku akiwa bado anamshangaa yule mwanamke ambaye alionekana ni mwehu ila aliongea vuzuri tu,

"ndio, nina malalamiko kidogo" Dada alijibu,

"ingia hapo, utakuta kuna foleni watu wamekaa kwenye benchi nao wanahitaji kuonana na mheshimiwa kama wewe unavyohitaji, kwa hiyo ukifika Kaa kwenye benchi subiri zamu yako" Kijana aliongea na kisha yule mwanamke akainama na kuokota mfuko wake wa Rambo, kisha akaelekea kwenye mlango alioelekezwa,

"ila mheshimiwa huoni umemruhusu mwendawazimu akaonane na mkuu wa wilaya?" Mgambo aliuliza,

"huwezi jua, huenda kuna malalamiko ya maana anayo, pia yule ni mwanadamu, ana haki ya kusikilizwa" Kijana aliongea kisha nae akaelekea pale pale alipoingia yule mwanamke, ila alimkuta yule dada amesimama kwenye mstari ila mbali kidogo na wa mbele yake.

"sogea karibu na mwenzako, mnatakiwa kuwa karibu karibu" Kijana alimwambia yule dada,

"kuna watu watatu waliokuwepo mbele yangu ila wametoka na wamekaa pembeni" Dada aliongea huku akitabasamu na kumfanya yule kijana ageuze shingo na kuwaona wanawake watatu wakiwa wamekaa pembeni,

"usijali, sogea mbele umsogelee wa mbele yako" Kijana aliongea huku akiwa amemshika bega yule dada. Yule dada akasogea mbele, cha ajabu mtu wa mbele yake nae akachomoka na kwenda kukaa pembeni,

"ndivyo wote wamefanya hivi, nadhani ni kutokana na muonekano wangu" Dada aliongea, hakutaka kuliacha tabasamu lake limtoke mdomoni,

"usijali, sogea tena mbele" Kijana aliongea,

"hapana, endapo nitamsogelea kila mtu atatoka kwenye mstari, nitakuwa nimeharibu utaratibu, ni bora mimi nikae pembeni na wao warudi mstarini, nitamkariri mtu wa mbele yangu" Dada aliongea huku akitoka kwenye mstari na kumfanya yule kijana aondoke na kuingia kwenye ofisi moja, kisha akatoka na kiti cha plastic,

"njoo ukae hapa" Kijana aliongea na kisha yule dada akaelekea kilipo kiti na kukalia, cha ajabu baada ya yeye kutoka tu kwenye foleni, baadhi ya watu waliotoka kwenye mstari kwa sababu yake, walirudi kwenye foleni na kukaimu nafasi zao, dada yule baada ya kugundua hilo, aliachia tabasamu hafifu huku akiwaangalia.

Baada ya nusu saa, zamu ya yule dada ilifika, akainuka taratibu na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye mlango mweupe uliokuwa na maandishi yaliyoandikwa (DC) na kubandikwa juu ya mlango. Aliendelea kupiga hatua huku nyuma kuna baadhi ya watu walikuwa wakimsema chini chini.

Alipoufikia mlango alisukuma na kuingia, ndani akakuta watu wawili, Mwanaume mmoja ambaye ndiye alimtambua kama mkuu wilaya ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti nyuma ya meza kubwa ya kifahari na pia huyo mkuu wa wilaya alikuwa nae alikuwa amemtolea macho huyo dada mwenye muonekano kama kichaa.

Pembeni ya mkuu wa wilaya alikuwa amekaa msichana ambaye alikuwa ameshika kalamu na daktari ndogo, alikuwa anaandika maelezo ya kila mtu aliyekuwa anaingia hapo ndani, pia huyo msichana alikuwa amemtolea macho huyo dada aliyeingia hapo.

Dada mwenye muonekano kama kichaa akaachia tabasamu ili awatoe wasiwasi, ila watu hao wala hawakucheka, walikuwa wamemkodolea macho tu,

"nani amekuruhusu kuingia?" Msichana alimuuliza yule dada,

"Japan!!!!!!! kwani kuingia humu kuna utaratibu gani zaidi ya kupanga foleni nje?" Dada alijibu huku akishangaa,

"toka nje" Msichana aliongea huku akimuangalia yule dada mwenye muonekano wa kichaa,

"sasa mbona unanifukuza hata kabla sijamueleza mheshimiwa shida yangu?" Dada aliuliza huku akitabasamu na muda huo mkuu wa wilaya alisimama na kutoa noti ya elfu kumi na kumpatia yule dada kichaa,

"chukua hii, itakusaidia" Mkuu wa wilaya aliongea huku akimpatia pesa yule dada kichaa,

"siko hapa kwa ajili ya kuomba pesa, nina shida tofauti kabisa" Dada kichaa aliongea huku akitabasamu,

"una shida gani wewe, kama hutaki hela toka bwana" Msichana aliongea huku akiinuka ili amtoe nje yule dada,

"muache, Ebu niambie una shida gani?" Mkuu wa wilaya alimuuliza yule dada na kufanya yule dada auweke mfuko wake juu ya meza na kutaka kuufungua kwa kutumia ule mkono wake mmoja,

"hapana, usitoe karatasi, wewe sema tu nitakusikia" Mkuu wa wilaya aliongea na kufanya dada kichaa asitishe zoezi lake,

"nina mikataba hapa, ila imekiukwa na watu niliowekeana nao" Dada kichaa aliongea huku akiwa amesimama, maana hakukaribishwa hata kiti,

"mikataba hiyo inahusu nini?" Mkuu wa wilaya aliuliza,

"ni kuhusu majengo mawili ya mjini, yaani jengo la wizara ya fedha lile la ghorofa kumi na mbili, na jengo la jirani lile la benki kuu" Dada kichaa aliongea huku akimuangalia mkuu wa wilaya,

"yamefanyaje hayo majengo?" Mkuu wa wilaya aliuliza,

"kulingana na mikataba, yale majengo ni mali yangu" Dada kichaa aliongea na kufanya mkuu wa wilaya na yule msichana anayemsaidia wakatazamana na kucheka chini chini, sasa waliamini kabisa huyo dada ni kichaa kabisa,

"hiyo mikataba ulifanya na nani?" Mkuu wa wilaya aliuliza huku akitabasamu,

"rais aliyepita, Tammy Semmy, nilifanya naye hiyo mikataba kipindi akiwa makamo wa rais" Dada kichaa aliongea na kufanya mkuu wa wilaya acheke tena, tena safari hii alicheka wazi wazi kabisa bila kujificha,

"sasa hapo umejidhihirisha ukichaa wako, yaani wewe ulivyo hivyo ni rais yupi anaweza kukaa na wewe, achana na suala la kusainishana mikataba, yaani kukaa tu na wewe haiwezekani" Mkuu wa wilaya aliongea huku akiinuka kwenye kiti,

"lakini mheshimiwa nina hii hapa kwenye mfuko" Dada kichaa aliongea huku akiuonesha mfuko wake,

"yaani yaani mikataba mikubwa ya kumiliki majengo makubwa unaiweka kwenye rambo?" Msichana msaidizi wa mkuu wa wilaya aliongea na kucheka kwa dharau na kipindi hicho mkuu wa wilaya alikuwa akifungua mlango,

"nani amemruhusu huyu mwendawazimu aingie humu ofisini kwangu?" Mkuu wa wilaya aliongea kwa sauti kubwa huku akiwa amesimama mlangoni na kufanya watu wote wamuangalie,

"mimi hapa mheshimiwa" Kijana aliyempokea yule dada kichaa kwa ukarimu alijibu,

"njoo umtoe humu, sio kila mtu anayefika hapa basi anastahili kuongea na mimi" Mkuu wa wilaya aliongea kwa ukali,

"Ila ungenisililiza kwanza" Dada kichaa aliongea huku akiwa amesimama pembeni ya mkuu wa wilaya,

"toka nje, siwezi kusikiliza zaidi ya ulichonieleza, namaanisha siwezi kusikiliza upumbavu tena" Mkuu wa wilaya aliongea kwa ukali na kumshika yule dada na kumsukumia nje, akadondoka chini yeye na mfuko na wake, kisha akaokota mfuko wake na kusimama, akamgeukia mkuu wa wilaya na kutaka kuongea kitu, ila akasita kisha akitabasamu, alafu akageuka na kuanza kuondoka huku watu wakimuangalia,

"huyu hakutakiwa kuruhusiwa kufika hapa, hastahili kuingia ofisini kwangu, huyu hastahili kuwa hapa labda mirembe" Mkuu wa wilaya aliendelea kubwata huku yule dada akiendelea kupiga hatua, hakuonekana kujali maneno ya mkuu wa wilaya ila aliyasikiliza.

Yule dada alitembea mpaka alipofika usawa wa yule Kijana aliyemkarimu mwanzo, Dada akasimama ila hakutaka kumtazama yule Kijana usoni, ila dada alitabasamu huku akiamini fika yule Kijana anamtazama,

"sikustahili kuwa hapa, nilistahili kuwa mirembe, ila nadhani kesho asubuhi kila mtu atakutwa anapostahili" Dada kichaa aliongea kisha akaanza kuondoka na kumuacha yule Kijana akiyashangaa yale maneno ya yule dada kichaa huku hasijue maana yake.

Baada ya yule dada kuondoka kila mtu eneo lile alicheka huku kila mmoja akiongea neno lake, isipokuwa yule Kijana tu, alikuwa bado anahisi kabisa yule dada kichaa hakutendewa haki.

*****************************

Siku iliyofuata, mishale ya saa moja asubuhi, yule kijana mkarimu alikuwa amevaa kitanashati, alikuwa akiwahi kazini, ila alishangaa kuona kundi kubwa la watu likikimbia kuelekea ilipo shule ya msingi, akapuuza, alihisi ni mwizi tu anakimbizwa.

Akaendelea kusogea mbele kwa hatua za haraka haraka, akapishana na kundi jingine la watu wakielekea upande ule ule, tena safari hii hakutaka kupuuza,

"kuna nini uko?" Kijana alimuuliza Msichana mmoja aliyekuwa nae anakimbilia uko,

"kuna mtu amekufa, amepigiliwa misumari juu ya mti" Msichana alijibu huku akikimbia.

Kijana akaona ni bora na yeye akashuhudie, haikuwa tukio lililozoeleka eneo hilo, hilo lilikuwa tukio jipya kabisa.

Kijana akaanza kupiga hatua kuelekea eneo la shule, alipofika aliweza kuona kundi la watu likiwa limeuzunguka mti, Kijana akaanza kupangua watu na mwisho anajikuta yupo mbele ya mti, juu ya mti kuna mwili wa mwanaume ukiwa umetundikwa, yaani mikono yake imegongelewa na misumari kwenye shina la mti na mwili wake ulikuwa ukining'inia, na mwili haukuwa na nguo, ulikuwa mwili wa mwanaume.

Yule kijana akauangalia ila hakumgundua yule maiti, kijana kwenye kutupa macho kuwaangalia baadhi ya watu waliopo pale, aliweza kumuona yule dada kichaa nae akiwa miongoni mwa mashuhuda wa tukio lile, hakutaka kumfuatilia sana.

"mshusheni sasa, mnangoja nini?" Ilikuwa sauti ya polisi mmoja akiwaambia wananchi.

Vijana kadhaa wakatoka na kwenda kutafuta ngazi, baada ya muda wakarudi, wakapanda na kuutelemsha ule mwili, sasa hapo ndipo watu walishtuka, ulikuwa ni mwili wa Mkuu wa wilaya, kundi zima likakazima kwa mshtuko, mpaka polisi wenyewe wakashikwa na mshangao.

Yule kijana ndio akachanganyikiwa zaidi, maana ndio boss wake,

"kuna karatasi kwenye pua" Kijana aliongea baada ya kuona kuna kikaratasi kidogo kilichojitikeza kwenye pua ya mkuu wa wilaya, watu wote wakaiangalia pua ya mkuu wa wilaya, kweli kulikuwa na karatasi. Polisi mmoja akaichomoa ile karatasi na kuisoma kimya kimya,

"kuna ujumbe gani?" Polisi mwingine akauliza,

"imeandikwa "kesho kila mtu atakuwa anapostahili" Polisi yule aliusoma ule ujumbe na kumfanya yule kijana afikirie Yale maneno amewahi kuyasikia wapi? akumbuka kuwa yale maneno yaliongewa siku iliyopita na yule dada kichaa, yule kijana akamtupia jicho yule dada kichaa na akakuta pia yule dada anamtizama, yule dada akatabasamu.

Yule kijana akamsogelea polisi na kuongea nae,

"yule dada nahisi anajua kitu kuhusu hili tukio" Kijana aliongea huku akiwa ameinamisha kichwa chini ili dada kichaa hasijue kinachoendelea,

"Dada yupi?" Polisi aliuliza,

"humuoni huyo dada kichaa mbele yetu?" Kijana aliuliza huku akiinua kichwa, cha ajabu hakumuona tena yule dada kichaa, kijana akashangaa, akapanda juu ya ngazi iliyotumiwa kuutungua mwili wa mkuu wa wilaya.

Kijana akapanda na kuanza kuzungusha macho kuona kama ataweza kufanikiwa kumuona yule dada, ila hakumuona, yaani alipotea ghafla tu.

Kijana akashuka na kutaka kutoka katikati ya lile kundi ili akamtafute yule dada,

"wewe utakuwa mshukiwa wa kwanza wa hili tukio, kuna unakijua wewe" Polisi aliongea na kumshika mkono yule kijana na kwenda kumuingiza kwenye gari huku yule kijana akilalamika bila polisi yoyote kujali malalamiko yake.......

**********ITAENDELEA*********

the Legend☆
Acha hao wenye dhararu wafe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA NANE.

______________
ENDELEA.....
_______________

"mfunge pingu" Askari mmoja aliyekuwa na cheo alimuamrisha mwenzake,

"wee, asithubutu mtu kunisogelea, msidhani nilivyoinua mkono juu kujisalimisha basi ndio mnifunge pingu" Dada kichaa aliongea huku akitabasamu,

"ebu mkamateni bwana, anatupotezea tu Muda hapa" Askari aliongea kwa hasira.

*************

Wakati ndani ya ofisi ya naibu waziri kukiwa na kashkash hiyo, upande wa chini Askari wengine walikuwa wakipanda kuelekea juu kwenye Ile Ile ofisi ya naibu waziri.

Askari hao wapatao watano walikuwa mbio mbio huku wakijua kabisa Kuna wenzao kadhaa wameshatangulia kwenye ofisi ya naibu waziri, Ila wao walitaka kwenda tu ilimradi waonekane mbele ya naibu waziri.

Walipofika kwenye mlango wa naibu waziri, wakasukuma kwa kujiamini kwa maana walijua wenzao wapo ndani, ni kweli waliwakuta wapo ndani, lakini hawakumkuta hata mtu mmoja akiwa mzima ndani ya chumba hicho cha ofisi,

"eeh!!!nini kimetokea???" Askari aliyekuwa wa kwanza kuingia aliuliza huku akirudi nyuma kwa uoga, lakini hukuna aliyemjibu, Askari wote sura zao zilionekana zimejaa mshangao ulioambatana na hofu kuu. Hukuna aliyejua kitu kilichoendelea kwenye ofisi Ile,

"madam nae amekufa?" Askari yule aliyeuliza swali la kwanza na hakujibiwa na wenzake, alijikuta akiuliza swali jingine mara baada ya kumuona naibu waziri akiwa amekaa na kichwa chake kikiwa kimelalia kiti na pia mkono wake aliupeleka shingoni ambako kulikuwa na kalamu iliyomuingia barabara katika sehemu ya koromeo.

Hapo Askari wote wakachanganyikiwa, wakachanganyikiwa kwa mawili, la kwanza ni kukuta wenzao wote wakiwa wamekufa, tena kwa Muda mfupi tu,, kwa maana tangu kengele ya hatari ilie mpaka Muda huo zilikuwa zimepita dakika kumi tu.

La pili lililowachanganya ni kukuta pia naibu waziri akiwa amekufa, wakaona wataonekana wazembe sana na huenda wanaweza kufukuzwa kazi,

"inawezekana mtu aliyefanya tukio hili ametokea dirishani" Askari mwingine aliongea baada ya kugundua dirisha la Ile ofisi lipo wazi. Askari yule akasogea mpaka dirishani na kuchungulia kwa nje, hakuona kitu, Askari akatoa simu ya upepo na kutoa taharifa makao makuu juu ya tukio hili la mauaji ya kutisha.

*********

Tom aliamka mapema ili kufuatulia nyendo za yule Dada kichaa, alitoka na kumuacha mpenzi wake akiandaa chai. Tom alienda moja kwa mpaka kwenye kibanda cha mama lishe kilicho nje ya Guest aliyofikia yule Dada kichaa, kisha akaagiza chapati, bahati nzuri alikuta chapati za foleni, akashukuru kukuta hivyo kwa maana alitaka kukaa hapo Muda mrefu.

Ilikuwa saa moja na nusu asubuhi, akakaa mpaka saa mbili na nusu, akapatiwa chapati zake na kulipia, akaondoka hapo kwenye chapati na kuhamia kwenye duka dogo lililokuwa maeneo hayo, lengo lake lilikuwa ni kumuona tu yule Dada kichaa,

"nipatie sukari kilo moja na iriki za mia tano" Tom aliongea huku akimpa pesa mwenye duka, Ila muda wote alijitahid kugeuza geuza shingo ili aangalie watu wanaotoka na kuingia ndani ya ile guest.

"kaka bidhaa hizi hapa" Muuza duka aliongea na kumfanya Tom amgeuzie shingo, na Wakati huo simu ya Tom ilikuwa ikiita, akaitoa mfukoni na kuangalia jina la mpigaji, akajikuta akitabasamu, akapokea,

"vipi" Tom aliongea baada ya kupokea simu,

"hizo chapati umeenda kununua au umeamua ukae kabisa upike wewe?" ilikuwa sauti ya mpenzi wake akiongea kwa ukali,

"mama kulikuwa na foleni, lakini nakuja muda si mrefu, nipo njiani" Tom alijibu kwa upole,

"kama ulikuta foleni si ungeacha oda,. Mbona upo lazy lazy hivyo?" Mpenzi wake aliendelea kung'aka,

"sawa, nakuja" Tom alijibu Ila aligundua simu imeshakatwa, Tom akatabasamu, akamgeukia muuzaji,

"samahani kaka, hivi leo hujaona Dada yoyote akitoka pale guest?" Tom alimuuliza Muuza duka,

"Mbona swali lako gumu broo? Maana ni wadada wengi sana wanaoingia na kutoka pale guest" Muuza duka alijibu,

"sawa, ni Dada mmoja hivi ana mkono mmoja" Tom aliongea,

"yah, nilimuona asubuhi sana akitoka" Muuza duka alijibu,

"hujamuona akirudi?" Tom aliuliza,

"sijamuona aisee, huenda Muda mwingine nilikuwa bize sana na wateja akapita bila mimi kumuona" Muuza Duka alijibu,

"asante kaka" Tom aliongea na kuondoka huku akimuacha muuza duka akiwa na maswali kumuhusu yeye, akahisi huenda Tom ni askari mpelelezi au huenda Tom ana mahusiano yoyote na yule mwanadada.

********

Ilikuwa ni saa la pili tu tangu naibu waziri afe, habari zilienea kwa kasi sana juu ya kifo chake, watu wengi walijiuliza iliwezekana vipi mtu kuingia kwenye ofisi ya naibu waziri na kumuua, hakukuwa na ulinzi eneo hilo au?

Wananchi wengine walienda mbali zaidi kimawazo na kuhisi huenda serikali imehusika na kifo hicho, kwa maana kwa maelezo ya hawali ya polisi walidai kuwa inaonekana camera zilitolewa mule katika ofisi kabla ya tukio. Sasa Wananchi walihoji inawezekana vipi mtu wa kawaida akaweza kuingia kwenye lile jengo na kutoa camera katika ofisi ya naibu waziri na wakati kuna ulinzi wa kutosha, tena wa masaa ishirini na manne?

Wakati Wananchi wakijitwisha mzigo huo wa maswali, ndani ya ofisi kuu ya polisi kulikuwa na mtu mmoja wa makamo aliyekalia kiti kilicho nyuma ya meza kubwa, na mbele ya meza kulikuwa na viti vingine vipatavyo nane, navyo vilikaliwa na askari walioonekana wana vyeo, na sura zao hazikuwa na furaha hata kidogo.

"huu ni muendelezo, tayari matukio kama haya yameshatokea kwenye wilaya moja ya mkoa wetu, aliuawa mkuu wa wilaya na msichana mmoja aliyekuwa akimsaidia, siku chache akauawa mkuu wa mkoa, na sasa ameuawa naibu waziri. Angalieni hii chain, wameanza viongozi wa wilaya, wakafuata wa mkoa, sasa vifo vimehamia kwenye uongozi wa serikali, ameanza naibu waziri, kwa chain inavyoonekana inaelekea anaweza kufuata waziri yoyote yule, haswa haswa ninavyoona atafuata waziri wa katiba na sheria. Sasa basi, hili suala sio la kukalia kimya wala halifichiki tena, tayari habari za kifo cha naibu waziri zimesambaa nchini kote, na bahati mbaya zaidi mtuhumiwa hajulikani, camera za ofisi ya naibu waziri zinaonesha zilitolewa kabla ya tukio, pia camera za jengo zimeonesha hazijanakiri tukio lolote, kwa maana hiyo ni kwamba vifaa vya kuhifadhi kumbukumbu za camera, inaelekea vilitolewa pia. Ila watu wa mapokezi wanadai kuwa mtu wa mwisho kuingia kwenye ofisi ya naibu waziri ni mwanamke ambaye alikuwa mlemavu, yaani hakuwa na mkono mmoja, na mwanamke huyo huyo ndio aliweza kuhusishwa na matukio mengine ya mauaji niliyoyaelezea hapo hapo hawali" Mkuu wa polisi wa nchi alieleza huku wale askari wengine wakimtazama, wengine walikuwa na karatasi wakiandika yale maelezo.

"kwa maana hiyo basi, mkitoka hapa hakikisheni mnasambaza askari maeneo yote kwa ajili ya kumtafuta huyo mtuhumiwa na kuimarisha ulinzi, na mtu yoyote ambaye atahisiwa anatakiwa akamatwe mara moja, pia hakikisheni upelelezi huu unaenda chini chini na kwa siri kubwa sana, raia wa kawaida hawatakiwi kujua. Na kutokana na hili tukio la mauaji ya kutisha ya naibu waziri, imembidi waziri wa katiba na sheria asitishe ziara zake za mikoani, na jioni ya leo atakuwa hapa mkoani na ulinzi wake umeimarishwa zaidi.

Nimemaliza, je Kuna mtu ana wazo lolote?" Mkuu wa polisi aliuliza, lakini hakuna mtu aliyejibu, akavua miwani yake,

"nadhani hakuna la ziada, sasa mnachotakiwa kufanya ni kutawanyika na kwenda kutekeleza maagizo niliyoyaelezea. Nimemaliza" Mkuu wa polisi aliongea kisha watu wakatawanyika na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa amebaki mwenyewe kwenye kile chumba cha mkutano.

Alikaa akitafakari kwa Muda mrefu, kisha akainuka na kuondoka kwenye chumba kile, akaelekea ofisini kwake, na kujibwaga kwenye kiti, kisha akavua miwani yake na kuiweka juu ya meza.

********

Wakati taarifa za kifo cha naibu waziri zikienea kwa kasi nchini kote, muuaji alikuwa amekaa mbele ya runinga iliyopo kwenye chumba alichopanga guest, alikuwa akipaka rangi kucha za vidole vyake vya miguuni, huku masikio yakiwa makini kusikiliza habari zinazorushwa.

Ila habari zote kuhusu kifo cha naibu waziri hazikuwa habari kwake, habari iliyokuwa habari kwake ni ile ya waziri wa katiba na sheria kuahirisha ziara na anarejea siku hii ya leo.

Hiyo habari ilimfanya Dada kichaa ahache kupaka kucha zake rangi na kutolea macho runinga, akajikuta akitabasamu peke yake,

"bora angeendelea tu na ziara, kuahirisha kwake ni sawa na kunifuata mimi rafiki wa Israel mtoa roho" Dada kichaa aliongea peke yake na kisha akaendelea kupaka rangi vidole vyake vya miguuni, kisha alipomaliza aliinuka na kujitupa kitandani, akatoa simu na kuitega kengele ya kumuasha kulingana na Muda anaotaka yeye.

"nitaenda kumuona Waziri, baadae usiku" Dada kichaa aliongea huku akiweka simu yake mezani, Kisha akalala usingizi mzito Bila wasiwasi wowote, yaani kama mtu ambaye hatufutwi na wala hajafanya uharifu wowote.

************

Nyakati za jioni, giza likiwa linashamiri kwa kasi sana, Tom alikuwa maeneo ya nje ya Ile guest, alikuwa akiendelea kufanya upelelezi wake, na kitu kilichochochea zaidi Tom kuamua kumuwinda kabisa yule Dada kichaa ni zile habari za kifo cha naibu waziri, yeye Tom aliamini kabisa muuaji atakuwa huyu Dada, ingawa serikali ilikuwa bado haijasema muuaji alionekanaje wala hawakusema ni nani wanayemuhisi.

Saa zilizidi kwenda, Tom alikuwa amekaa kwenye kibanda cha kuoneshea mpira, alikuwa amekaa kwa nje. Baridi likamzidia, Tom akainuka ili aende nyumbani akavae koti. Alipoinuka na kupiga hatua mbili Tatu, aliweza kumuona mwanamke akitoka ndani ya Guest, akamuangalia kwa umakini zaidi, alikuwa ni yule Dada kichaa akiwa amebeba begi dogo mgongoni, na hapo ilikuwa yapata saa nne usiku.

Tom akaamua hasiende tena kuvaa koti, akaamua amfuatilie yule Dada kichaa.

Dada kichaa alitembea mpaka barabarani, kisha akasimama kwa muda, ikapita bajaj, akaisimamisha, akaingia na kuelekeza anapotaka kwenda, dereva bajaj akageuza bajaj na kuiondoa.

Tom alibaki Amesimama, maana hakukuwa na usafiri mwingine, akabaki amesimama huku akiitazama namna Ile bajaj ikipotea machoni mwake.

Akiwa amekata tamaa kabisa, aliiona bodaboda ikija mbele yake, akaisimamisha,

"Kuna bajaj imeelekea njia ile, naomba unisaidie kuifuatilia" Tom aliongea huku akirukia kwenye bodaboda, dereva nae hakutaka kuhoji zaidi, akaiondoa bodaboda kwa kasi kama mteja wake anavyotaka.

Walitembea kwa mwendo wa dakika tano, wakaweza kuiona ile bajaj,

"Ile, sasa tuifuatilie kwa umbali huu, usiisogelee karibu'" Tom alimwambia dereva ambaye alitii.

Waliendelea kuifuatilia kwa dakika kumi, kisha bajaj ikasimama,

"na mimi nisimame?" Dereva bodaboda aliuliza,

"nyoosha tu, uipite" Tom aliongea kwa maana alihisi wakisimama wanaweza kushtukiwa.

Bodaboda ikaipita bajaj na kwenda umbali zaidi, kisha Tom akamtaka dereva asimame, akashuka na kumlipa pesa yake, bodaboda ikaondoka.

Tom akatupia macho kwenye bajaj akaona yule Dada kichaa akashuka, Tom akatembea na kuingia kwenye kichochoro, akawa anamchungulia yule Dada kichaa.

Dada kichaa alitembea kuelekea upande ule ule wa Tom alipo, Ila alipofika ule usawa wa Tom yeye hakuingia kichochoroni, aliendelelea kufuata barabara. Tom akawa anamtazama tu.

Yule Dada kichaa akaenda moja kwa moja kugonga geti la nyumba moja ya kifahari, Kisha akawa anaongea na mlinzi baada ya geti kufunguliwa, Tom hakuweza kusikia yale maongezi kwa maana alikuwa mbali na geti.

Tom akiwa anachungulia, alimshuhudia mlinzi akilegea na kudondoka chini, akashangaa. Akiwa bado anashangaa, aliweza kumuona yule Dada kichaa akiingia ndani ya lile geti, Tom akaendelea kushangaa.

Baada ya dakika kumi za Dada kichaa kuzama ndani ya geti, Tom akaona bora nae asogee jirani na geti, akapiga hatua za haraka haraka mpaka getini, akasukuma geti kidogo na kuchungulia, akapigwa na mshangao mara baada ya kuwaona Askari wapatao kumi wakiwa wamelala chini na wengine damu zilikuwa zikiwavuja, hakuna hata mmoja aliyeonekana yupo hai.

Akaingia kwa mwendo wa hatua za taratibu zisizokuwa na vishindo vikubwa, akatembea mpaka mlangoni na kusikia sauti za watu zikiongea, akapenyeza jicho kwenye uwazi mdogo uliokuwepo hapo mlangoni, akashtuka baada ya kumuona waziri wa katiba na sheria akiwa amekaa na mbele yake alikuwepo yule Dada kichaa,

"mimi sio mkorofi, endapo mtafuata sheria na kunipa mali yangu, sitowapa tabu tena" Dada kichaa aliongea kwa kujiamini,

"hiyo mikataba unayo hapo?" Waziri aliuliza huku akionekana akitetemeka, na pembeni kulikuwa na familia yake ambayo ilikuwa imefungwa kamba,

"hapana, kwa kuwa ni mambo ya kiofisi, nitakuletea kesho mapema ofisini kwako. Kumbuka kuwa sitaki kukuta kikwazo chochote, yaani nikija, polisi wakae mbali na mimi, na chombo chochote cha usalama kisinisogelee" Dada kichaa alizungumza kwa msisitizo,

"sawa, wewe utaileta mikataba nitaiangalia. una mwanasheria?" Waziri aliuliza,

"mwanasheria wa nini wakati mikataba imeweka wazi kila kitu" Dada kichaa aliongea,

"sawa" Waziri aliongea, kisha yule Dada kichaa akasimama, akaenda mpaka eneo jirani na mlango ambalo kulikuwa na kitufe ambacho ukikibofya tu, polisi wanajua Kuna hatari, Dada kichaa akabonyeza kile kitufe,

"polisi watakuja Muda wowote, acha niondoke" Dada kichaa akaongea na kuanza kuelekea nje.

Tom alipoona yule Dada anakuja mlangoni, akachomoka kwa kasi na kujificha nyuma ya nyumba, yule Dada kichaa akatoka na kufunga kwa nje mlango wa nyumba ya waziri, kisha akakanyaga maiti kadhaa za Askari na kutoka nje ya geti.

Baada ya dakika mbili, Tom nae akaamua atoke nje, akatembea kwa tahadhari mpaka getini, akafungua geti, akakuta ndio gari ya polisi inasimama, akapata kiwewe, akarudi ndani kwa kasi,

"wewe simama" Askari waliongea kwa amri huku wakiruka kwenye gari na kumfuata Tom ndani.

Tom alivyorudi ndani ya geti, akiwa na kasi na kiwewe, alijikwaa kwenye maiti na kudondokea kichwa, akaanguka chini na macho yakawa yanakosa nguvu,

"huyu ndio kawaua awa Askari, kwanza usiku huu amefuata nini kwenye nyumba ya waziri?" Askari mmoja aliongea huku akiwa amesimama mbele ya Tom na bunduki ikiwa mkononi, Tom alitaka kujitahidi aongee ili kujinasua kwa Askari, Ila hakuwa na nguvu tena, macho yalikosa uvumilivu, yakajifunga, Tom hakuona kitu tena, aliona giza na mwili ukashindwa kufanya kazi, Tom akapoteza fahamu..........

************ITAENDELEA*************

the Legend☆
Mfyuu Tom kiherehere kimekuponza, ukichokitafuta umekipata

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom