Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA.

___________________
ENDELEA.........
______________________

Kile kitendo cha Ray Charles kumuweka kichwa kwenye chuma, kilisababisha BQ ajiulize ni huduma gani hiyo mpya anataka kupewa, pia hata mikono iliyobeba kichwa chake ilikuwa migumu, haikuwa mikono ya kawaida.

Kwa hiyo sasa wakati kichwa cha BQ kikiwa juu ya ile chuma, Ray Charles akajiandaa na kuachia ngumi kali kuelekea katika kichwa cha BQ, BQ ghafla akafungua macho, ndipo akashtuka kuona ngumi ikija usoni, BQ akakwepesha kichwa, Ile ngumi ya Ray Charles ilipiga chuma ya kitanda mpaka ikakatika. BQ akajivuta na kujiinua, maana tayari pingu ya mguuni ilikuwa imeshakatwa na Ray Charles, ilibaki ya mkononi tu.

Ray Charles yeye alishangaa baada ya BQ kuikwepa ngumi ile, maana alijua BQ hana fahamu, ila bado Ray Charles alikuwa na nafasi nyingine ya kummaliza BQ, kwa BQ alikuwa na pingu mkononi. Ray Charles akamfuata BQ, BQ akaona Kuna haja ya kujitetea, BQ akachomoa drip, kisha ile chuma ya drip akamrushia Ray Charles, Ray Charles akaidaka, bado akawa anamsogelea BQ, BQ akaruka upande wa pili wa kitanda na kisha akainama, alipoinuka akaamka mzima mzima na kitanda, akamvaa Ray Charles, Ray Charles akajikuta anasukumwa kurudi nyuma, Ray Charles akakimata kitanda, kisha akakiinua juu kikiwa na BQ, alafu akakipigiza chini, BQ akadondoka, akauona mkasi, akachukua na kwa utaalam wa hali ya juu akafungua pingu ya mkononi kwa kutumia miguu na mkasi, akawa huru sasa, BQ akasimama na kutabasamu, akakisogeza kitanda pembeni na kusogea karibu kabisa na Ray Charles,

"Leo umepotea njia, sio kama ulivyoniotea mwanzo na risasi" BQ aliongea na kukunja vizuri gauni la hospitali.

Ray Charles alibaki kimya akimuangalia tu, BQ akakunja ngumi ya mkono mmoja,

"Sasa sogea" BQ aliongea na kujitayarisha kwa pambano, Ray Charles akaanza kumsogelea taratibu, BQ akamtisha, ila Ray uwa hatishiki. BQ kuona hivyo, akapiga hatua moja nyuma BQ kisha akarusha teke kali lililotua katika kichwa cha Ray Charles, Ray Charles akayumba, akakasirika kwa kupigwa lile teke,

"we mwepesi tu, ila uwa unanikutaga sipo vizuri kiafya" BQ aliongea huku akicheka na kuzidi kumuongezea hasira Ray Charles, Ray Charles akaing'uka mikono kama anatoa uchafu, kisha akakunja ngumi sasa, BQ akajiandaa na mkono wake mmoja.

Ray Charles alirusha ngumi za haraka haraka kama ishirini hivi, BQ alijikuta anarudi nyuma mpaka akaenda kugota kwenye kioo, maana hakuwa na uwezo wa kupangua zile ngumi, endapo angezuia ngumi hata moja tu, angevunjika mkono.

BQ akawa anahema kwa haraka haraka, yaani pale ndio ilikuwa mwisho, hana pa kukimbilia tena,

"one two, one two" Ray Charles aliongea huku akiruka ruka na akirusha rusha ngumi kama mpiga masumbwi, BQ alipata uoga wa ghafla,

"Tuendelee sasa" Ray Charles aliongea na kumfuata BQ kwa kasi, kisha Ray Charles akapiga ngumi mbili za haraka kulenga kichwa cha BQ, BQ akainama, zile ngumi zikapasua kioo dirishani, Ray Charles hakujali hilo, yeye alitaka kuua tu. Ray Charles akasogea tena na kuachia ngumi nyingine kali zaidi, BQ akainama kisha akakamata miguu ya Ray Charles na kujaribu kumbeba, alishindwa. Akaamua amsukume tu,

"ngoja kwanza" BQ aliongea huku akihema,

"ebu nipe hayo maji" BQ aliongea huku akimnyooshea kidole nyuma ya Ray Charles, Ray Charles akafanya makosa kugeuka, BQ akavuta fire extinguisher iloyopo ukutani na kumpiga nayo kichwani, Ray Charles akapepesuka, BQ akapiga tena, kisha akampulizia usoni, Ray akawa haoni mbele kutokana na ile gesi ya fire extinguisher. Ray Charles akajifuta macho na kuweza kuona vyema tena, ila cha ajabu hakukuta mtu, akachungulia dirishani, akamuona BQ akikimbia kwa nje, tayari BQ alishatokea dirishani muda mrefu tu.

"shit" Ray Charles aliongea kwa hasira na kisha akajitupa dirishani kwenye lile jengo la ghorofa moja. Ray Charles akatua juu ya gari ndogo, mpaka ile gari ikabonyea kutokana na uzito wa Ray Charles.

Ray Charles akarukia chini na kuanza kukimbia kuelekea mahali BQ alipokimbilia. Ray Charles alikimbia kwa muda kidogo ila hakufanikiwa kumpata BQ, Ray Charles akapiga ngumi mti kwa hasira, kisha akawa anaondoka pole pole mara baada ya kashindwa tena kumuua BQ.

Aliumia sana kumkosa BQ, maana aliambiwa endapo atashindwa kumuua BQ, basi mtoto wake atakuwa matatizoni. Ray Charles alikosa raha, maana aliijua vyema roho ya Rais.

Ray Charles akaondoka zake, kitu ambacho hakujua ni kuwa ile njia anayoondoka nayo, ndio hiyo hiyo aliyoondoka nayo BQ.

**************

Tom alikuwa na siku kadhaa hajamuona Sajenti Minja, hata alipopiga simu, simu ya Sajenti Minja ilikuwa haipatikani.

Tom alikuwa yupo kwenye jumba moja la kubeti, alikuwa akiangalia michezo ya mbio za mbwa na farasi. Baada ya nusu saa Tom aliinuka na kuanza kuondoka, alitoka nje na kupiga hatua mbili tatu, akasimama ili asubiri gari ipite ili avuke barabara, ila gari aliyokuwa akiisubiri ipite ilisimama mbele yake jirani kabisa na yeye, kisha Dereva wa ile gari akashusha kioo,

"Habari yako kaka?" Dereva wa ile gari alimsalimia Tom,

"aaagh nzuri tu, vipi?" Tom alijibu kwa kigugumizi huku akimtazama yule Dereva ambaye alikuwa ni mama mtu mzima kidogo,

"safi, naomba uninulie gazeti hapo, maana nguo niliyovaa nashindwa hata kutelemka katika gari" Yule mama aliongea huku akimpatia noti elfu moja Tom,

"gazeti gani?" Tom aliuliza huku akiipokea ile pesa,

"leta udaku spesho" Mama alijibu huku akitabasamu. Tom akasogea mpaka sehemu iliyo na gazeti na kununua hilo gazeti, ila aliona gazeti moja la siasa likiwa na picha ya Sajenti Minja,

"SAJENTI WA POLISI ALIVYOTOROSHWA NA WAARIFU WENZAKE" hicho ndio kichwa cha habari kilichoandikwa juu ya gazeti lile,

"nipe na hili" Tom aliongea huku akitoa pesa yake mfukoni na kupewa lile gazeti la siasa, Tom akaweka mfukoni gazeti lake, kisha akampelekea yule mama wa kwenye gari gazeti lake la udaku.

Tom baada ya kumpa yule mwanamke gazeti, Tom alivuka barabara na kuanza kuelekea nyumbani, njia nzima alitamani asome gazeti, aliona kama anachelewa kufika, ila nafsi ilimzuia, Tom akaona ni bora akalisomee nyumbani tu huku akiwa ametulia.

Tom alikaza mwendo mpaka nyumbani, akamkuta mpenzi wake akikatakata spinach, Tom akavua shati na kukaa kitandani, akatoa gazeti mfukoni na kuanza kupitia ile habari inayomuhusu Sajenti Minja, aliipitia yote huku jasho jembamba likimchuruzika asomapo kila aya,

"mwenzetu leo vipi?" Mpenzi wake alimuuliza baada ya kuwa kumtazama Tom muda mrefu,

"kwani vipi?" Tom nae aliuliza huku akimkata jicho mpenzi wake,

"umekuja tu wangu wangu hata huongei, unaanza kusoma mgazeti, jasho linakutoka, kwanza sijawahi ona ukinunua gazeti, sijui leo imekuaje?" Mpenzi wake aliuliza huku akiinuka katika kochi,

"Sajenti Minja kafukuzwa kazi, pia alitoroka kituoni baada ya kukamatwa kwa kushirikiana na yule dada muuaji ambaye yeye ndio aliyefanya mpaka leo sina kazi" Tom alimwambia Mpenzi wake,

"huyo Sajenti Minja ndio nani?" Mpenzi wa Tom alihoji,

"we nawe kichwa chako kama cha bata, hakitunzagi kumbukumbu, humjui Sajenti Minja? si yule rafiki yangu polisi" Tom alijibu,

"khaaa, kumbe ndio yule? Sasa ni kweli uwa anashirikiana na huyo mwanamke muuaji?" Mpenzi wake aliuliza,

"hapana kwa kweli, hii haiwezekani kabisa, hapo walimuonea " Tom aliongea kwa masikitiko,

"Sasa nani aliyemtorosha polisi kama hana uhusiano na waarifu?" Mpenzi wake aliuliza,

"inawezekana ametoroshwa kweli, ila sio na waarifu, itakuwa mipango yake tu, kwa maana yule ni komando, kama ni waarifu wamemtorosha Sajenti Minja, kwanini hao waarifu hawajaenda kumtorosha hospital yule dada muuaji?, maana ni mwenzao" Tom aliuliza,..

"Sasa unanihoji mimi kwani mimi najua kitu? Ngoja niende gengeni kuchukua nyanya, maana nikikaa hapa nitahojiwa weee, kama mimi ndio tageti Minja, sijui sadent Minja!" Mpenzi wake aliongea huku akielekea nje na kumuacha Tom akiwa anairudia kuisoma ile habari.

"kwanini atoroshwe Sajenti Minja, tena ndani ya kituo kikuu cha polisi wenye silaha za kutosha? Kwanini hasitoroshwe yule dada muuaji ambaye yupo tu hospital na ulinzi wa kule hospital ni wa kawaida tu" Tom alijiuliza huku akijikuna kidevu,

"huu mchezo huu" Tom aliongea mwenyewe na kujilaza kitandani.

**************

Ray Charles alikuwa bado anatembea huku akiwaza namna ya kumdanganya Rais kuhusu BQ. Ray Charles alitembea na giza lile huku akiwa amevurugwa akili kabisa, hakujua ni kipi atakutana nacho endapo atafika kwa Rais.

Ray Charles aliendelea na mwendo mpaka akatokea sehemu moja iliyochangamka kidogo, ila aliona Kuna sehemu watu wamezunguka na kutengeneza duara, yaani kama kulikuwa na tukio wanalishuhudia, Ray Charles akapuuza, sio mtu ambaye anapenda sana kujuchanganya na watu,

"Yule atakuwa ametoroka hospital, si huoni hata zile nguo ni za hospital kabisa?"

"atakuwa mwendawazimu yule, haiwezekani mtu mwenye akili timamu atoroke hospital, alafu mwanamke?" Haya ni maongezi ya wazee wawili waliokuwa wakipishana na Ray Charles, hawa wazee walikuwa wakitoka katika lile eneo ambalo kulikuwa na kundi lake watu wakiangalia kitu.

Yale maneno yalimshawishi Ray Charles aende kuona katika lile kundi Kuna nini? maana hata yeye ametoka kumkimbiza mwanamke aliyevaa nguo za hospitali, Ray Charles akajikuta ameshawishika kuingia katika lile kundi la watu ili kuona ni kipi kinajili hapo.

Ray Charles alijinyepenyeza na hatimae akatokea mbele kabisa ya watu, hapo ndipo alipoweza kumuona BQ akiwa amelala chini, alipoteza fahamu tena, Ray Charles akatabasamu, akataka kutoa bastola yake, ila akaona anaweza kuleta tafrani katika eneo hilo watu wengi.

Ray Charles akafikiri kwa muda na kisha akamsogelea karibu kabisa BQ, akamshika shavuni kama anampima homa, kisha Ray Charles akambeba BQ juu juu,

"unamjua huyo?" Kijana mmoja alimuuliza Ray Charles, lakini Ray Charles hakutaka kujibu, alipenya mpaka akatoka katika lile kundi la watu, akasimamisha Baja na kuingia na BQ,

"nipeleke maeneo ya ikulu" Ray Charles alimwambia Dereva bajaj kisha Dereva akaondoa bajaj, Ray Charles akamlaza BQ mapajani mwake, Ray Charles akatabasamu.

Bajaj ilitembea mpaka maeneo ya ikulu,

"simamisha hapa" Ray Charles alimuamrisha dereva Bajaj ambaye alitii, kisha Ray Charles akatelemka na kumlipa Dereva Bajaj, kisha Ray Charles akambeba BQ na kutembea nae kwa mwendo mfupi, kisha akaingia nae Ikulu.

Ray Charles alipitiliza moja kwa moja mpaka katika kile chumba chao alichomuulia Sajenti Minja.

Alifika na kumtupa BQ chini, kisha akampigia simu Rais na kumpa taarifa. Baada ya dakika kumi Rais aliingia mule, kwanza alivyomuona BQ, Rais alijikuta akitoa tabasamu la ushindi,

"kwisha habari yake" Rais aliongea na kutabasamu, kisha akachomoa bastola kiunoni kwa Ray Charles, akamuelekezea BQ kichwani......

********ITAENDELEA**********

the Legend☆
.
1087067905558387774.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom