Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI.

___________________
ENDELEA.........
______________________
Wale vijana baada ya kuitupa miili ya Sajenti Minja na yule pandikizi la mtu, wale vijana walikuwa wakijirudisha huku kila mtu akiwa kimya, hakuna aliyeongea. Gari yao ilienda mpaka ikakaribia ikulu, kijana mmoja akaguna,

"nini wewe" Mwenzake aliyekaa nae siti ya nyuma akauliza,

"aisee sikioni kitambulisho changu, nna wasiwasi kitakuwa katika gunia la ile maiti ya pili, maana nakumbuka wakati naiweka ile maiti katika gunia, kitambulisho kilikuwa katika mfuko wa shati" Yule kijana aliongea,

"Bob huu uzembe, twendeni tu ndani, labda kitakuwa ndani tu" Dereva wa ile gari aliongea, alionekana kuchoka,

"Sasa tukishaingia ndani alafu ikaonekana kitambulisho sina? unataka niuawe ndani kwa sababu ya uzembe?" Yule jamaa aliuliza,

"kweli, sio poa mwenzetu akiuawa, bora turudi tukaangalie katika yale magunia ya maiti" Kijana mwingine alimuunga mkono,

"Sasa tufike tena kule, tuanze kuingia kwenye maji tulowane, tufungue gunia,..dah" Dereva wa ile gari aliongea kwa kulalamika,

"nyie twendeni tu, tukifika uko mimi mwenyewe nitaingia na kufungua gunia" Yule kijana aliongea,

"poa bwana, ila Dizonga huu ni usumbufu mshkaji wangu" Dereva aliongea na kutaja jina la yule mwenzake aliyesahau kitambulisho,

"kusahau si kupo tu, kwani Kuna mtu hajawahi kusahau hapa?" Mwingine nae aliongea baada ya kuona kama Dizonga analaumiwa.

Dereva akageuza gari na kuanza karudi huku akionekana kukasirika.

" ebu simama nikachukue dawa, mtoto wangu anasumbuliwa na mafua" Dizonga aliongea baada ya kuona duka la dawa,

"Dizonga unazingua mshkaji wangu, tunazidi tu kuchelewa" Dereva alilalamika huku akisimamisha gari,

"tusamehane" Dizonga aliongea huku akitelemka katika gari, akakimbia kuelekea kwenye duka la madawa na kuwaacha wenzake wakimtazama tu,

"Dizonga anazingua sana" Yule jamaa aliyekaa nyuma aliongea,

"wewe si ulikuwa unamtetea?" Dereva aliongea kwa jazba,

"lazima nimtetee, sisi ni timu, wewe unafikiri Rais angejua kuwa Dizonga kapoteza kitambulisho, unadhani angemuacha hai?" Yule jamaa wa nyuma aliuliza,

"aaagh, kazingua tu" Dereva aliongea na kipindi hicho Dizonga alikuwa akiingia katika gari.

'"samahanini nimechelewa kidogo" Dizonga aliongea Ila hakuna aliyemjibu, Dereva akaondoa gari.

Walifika baharini na kuegesha gari yao, kisha wakashuka na kuelekea eneo ambalo waliipeleka ile miili.

Walifika lile eneo, kisha Dizonga akavua viatu,

"nyie nisubirini hapa, ngoja niingie mwenyewe" Dizonga aliongea huku akiingia katika maji,

"Sasa mbona umeingia na nguo?" Mwenzake mmoja aliuliza,

"nikisema nivue nitachekelewa, miili yenyewe inaonekana kwa mbali" Dizonga alijibu huku akitembea katika yale maji yanayomfikia kiunoni. Alitembea mpaka alipofika katika maji ya shingo, akajitupa na kuanza kuogelea kuelekea miili ilipo, aliwaacha wenzake wakimuangalia tu.

Wenzake waliendelea kukaa ufukweni pale, baada ya dakika ishirini, Dizonga alionekana akirudi huku akivuta gunia lenye mwili wa Sajenti Minja. Alisogea mpaka ufukweni, kisha akachana lile gunia na kuutoa mwili wa Sajenti Minja, alafu akalichana lile gunia na kutafuta kitambulisho chake, akafanikiwa kukipata, akatabasamu kisha akausukumia majini mwili wa Sajenti Minja.

"tuondokeni sasa" Dereva aliongea,

"hakuna cha kusubiri" Dizonga alijibu huku akizivua nguo zake zilizokuwa zimelowana, akazitia katika mfuko wa nylon kisha ule mfuko akauingiza katika begi lake la mgongoni, kisha yeye akaingia katika gari akiwa mtupu,

"tembeza moto bab" Dizonga aliongea kisha Dereva akaondoa gari kwa fujo.

****************

Ndani ya chumba cha hospitali, BQ fahamu zilimrejea, uwa hakurupuki fahamu zinapomrejea, uwa anaendelea kufunga macho huku masikio na pua vikifanya kazi ya kutambua eneo husika. BQ alivuta harufu ya dawa, akakumbuka mara ya Mwisho alikuwa duka la madawa, lakini masikio yake bado hayajasikia chochote, kulikuwa na hali ya utulivu sana.

BQ taratibu akafungua macho, akajikuta yupo amelala kwenye kitanda kilichokuwa na mashuka meupe, na pembeni akaona Kuna chuma la drip, hapo akahisi mkono wake ndio umeunganishwa na ile drip iliyokuwa inang'inia katika lile chuma. BQ akageuza shingo ili kuhakikisha, ila alitangulia kuiona pingu, akashtuka, tayari aligundua yupo chini ya ulinzi.

BQ akataka kujivuta ili akae, akahisi miguu mizito, akanyanyua shingo na kuona miguu yote imefungwa pingu, akachoka kabisa, yaani walimuweza haswa.

akajaribu kuivuta miguu kwa nguvu, lakini hakufanikiwa kufungua, ni kelele tu zilisikika baada ya chuma ya pingu kusuguana na chuma ya kitanda, BQ akatoa tusi la nguoni, na muda huo alisikia hatua za mtu akisogea mlangoni mwa chumba alichopo, BQ akajilaza haraka na kufunga macho tena, akajifanya amezimia.

Zile hatua zilizidi kusogea na kisha mlango ukafunguliwa, akaingia Askari, akatupa macho kila pembe ya kila chumba, kisha akasogea mpaka dirishani na kufungua, akatoa kichwa na kutazama nje, akaingiza kichwa ndani na kufunga dirisha,

"vipi, mbona unakagua hivyo?" Askari mwingine aliingia na kumuuliza yule Askari anayekagua katika ile wodi aliyolazwa BQ,

"nimesikia kama mtu anagonga vyuma humu ndani" Askari wa hawali aliongea na kumfanya mwenzake acheke,

"wee jamaa wewe, itakuwa usingizi unakusumbua, maana nasikia leo umekesha hospital hapa" Askari mwingine aliongea huku akiendelea kucheka,

"sidhani kama ni usingizi, nimesikia kabisa kwa macho yangu" Yule Askari aliongea,

"si unaona sasa, umesikia kwa macho yako? Sio masikio" Askari mwenzake aliuliza na kucheka,

"aya bwana, ndio umekuja kunipokea?" Askari wa hawali aliuliza,

"ndio, nenda kapumzike bwana, maana Kuna muda mtu akiwa na usingizi mwingi hata akili inapungua" Mwenzake aliongea na kuendelea kucheka,

"sawa kaka, acha mimi niende" Askari wa hawali aliongea huku akitoka nje, mwenzake akamfuata na wakafunga mlango na kutoka nje, BQ akafungua macho, akaangaza macho wodi yote,

"mtihani huu" BQ aliongea peke yake na kutikisa kichwa kwa masikitiko.

Akatupia macho kwenye chupa ya drip, akaona ndio kwanza ipo nusu, pia alihisi kiu ya maji na hukutaka kuomba msaada wa kuyapata hayo maji. Wakati akiwa bado hajui cha kufanya, alisikia hatua za mtu zaidi ya mmoja zikisogelea mlango wa wodi aliyokuwepo, BQ akafunga macho na kujikausha, kisha mlango ukafunguliwa, alikuwa mkuu wa polisi na watu wengine akiwepo daktari, wakaingia na kukizunguka kitanda,

"vipi maendeleo yake lakini?" Mkuu wa polisi alimuuliza daktari,

"bado sioni unafuu, nilitegemea atapata fahamu leo, ila naona imeshindikana" Daktari alijibu,

"ni nini umegundua kinamsumbua mpaka kapoteza fahamu muda mrefu hivi?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"ni jeraha la kichwani, bado bichi sana, yaani hilo jeraha hajapona kabisa, sasa linapoanza kumuuma humletea maumivu ya kichwa na kusababisha kupoteza fahamu" Daktari aliongea huku akisoma katika kijitabu chake,

"kwa hiyo dawa yake ni nini?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"kwa sasa hakuna dawa ya moja kwa moja, ila ninachofanya ni kumchoma sindano za kukausha kidonda hicho, na kingine kipo upande wake wa kushoto, na vyote ni vidonda vya risasi" Daktari aliongea na kumuangalia mkuu wa polisi,

"ataamka tu, safari hii lazima afungwe" Mkuu wa polisi aliongea huku akielekea nje, na wengine wakamfuata. Walipotoka tu, BQ akazidi kujiona yupo hatarini, uwa na roho ngumu, ila siku hiyo machozi yalimtoka, hakuwa na msaada kutoka kwa mtu yoyote.

**********

Siku ya leo Rais alikuwa kufuatilia habari, alijaza magazeti mengi katika meza yake, na kila gazeti alikuwa ameshalipitia, ila Kuna habari mbili tu zilionesha kumfurahisha, habari ya kwanza ni ile ya kukamatwa BQ, na habari ya pili ni ile iliyoonesha Sajenti Minja ametoroshwa kituo cha polisi.

Aliifurahi sana kwa maana aliona kazi yake dhidi ya watu wanaomsumbua inaisha kirahisi sana, kwa maana BQ tayari yupo mikononi mwa polisi, kwa hiyo suala la kumuua ni mipango midogo midogo tu.

Kitu kingine alichokipenda ni kuona kuwa amewaaminisha watu kuwa Sajenti Minja ametoroshwa na watu wakaamini, ila ukweli aliujua yeye na watu wake, kuwa Sajenti Minja tayari ameshakufa.

"Ray" Rais aliita na kwa haraka mlango wa kuingilia ofisini ukafunguliwa, akaingia Ray Charles aliyekuwa amevaa shati nyeusi na suruali ya kitambaa,

" nimepata wazo, nataka tushirikiane. Nataka ukamuue yule dada kule hospitali, usifanye makosa tena, endapo utashindwa tena kumuua, mwanao nitamuua" Rais aliongea huku akitabasamu,

"hakuna shida, ila uwa nakosa raha kwenye mambo kama haya unaishirikisha familia yangu" Ray Charles aliongea kwa utulivu,

"Ray, inabidi sasa familia yako niingize, kwa maana naona ufanisi wako umepungua Ray" Rais aliongea huku akiinuka na kumpiga piga mgongo Ray Charles, ambaye alikaa kimya,

"na kama nitakuta polisi, niue wote?" Ray Charles aliuliza,

"kweli umeuliza swali zuri, nitaongea na mkuu wa polisi" Rais aliongea,

"sawa, na nitaenda muda gani kutekeleza hilo agizo?" Ray Charles aliuliza,

"kesho kabla jua halijaonekana, nataka roho ya BQ iwe haipo" Rais aliongea,

"sawa mkuu" Ray Charles alijibu,

"nisubiri nje hapo" Rais aliongea na kisha Ray Charles akatoka nje. Rais akachukua simu yake na kumpigia mkuu wa polisi,

"naam mkuu" Mkuu wa polisi aliongea baada ya kupokea simu,

"naona sasa mmekuwa wepesi mpaka waarifu wanakuja kutorosha watu wao kituoni?" Rais aliuliza,

"hapana mkuu" Mkuu wa polisi alijibu,

"ni nini sasa kinaendelea kiasi kwamba mmedharaulika kiasi hicho? muarifu kuja kumtorosha mtu kituoni" Rais aliongea,

"hata mimi sielewi, nadhani kutakuwa na polisi wanashirikiana na waarifu" Mkuu wa polisi aliongea,

"huyo Minja aliyetoroshwa wewe ndiye ulimpendekeza aisimamie na kumtafuta yule mwanamke muuaji. Unataka kuniambia ulikuwa hujui uhusiano uliopo kati ya Sajenti Minja na yule mwanamke muuaji?" Rais aliuliza,

"sikuwa nafahamu kitu mkuu" Mkuu wa polisi alijibu,

"kifupi sina imani na nyinyi tena, kwa hiyo sasa, naomba uondoe polisi wako wote katoka ile hospital ambayo yupo yule mwanamke muuaji, maana mnaweza kumtorosha tena na kudanganya ametoroka mwenyewe" Rais aliongea kwa mamlaka,

"kwa hiyo mkuu kama kutakuwa hakuna polisi hata mmoja, si itakuwa hatari zaidi na kuwa rahisi kwa mtuhumiwa kutoroka?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"unaniuliza sasa?, wewe kama nani?" Rais aliuliza,

"sawa sawa mkuu, nitafanya kama ulivyoagiza" Mkuu wa polisi aliongea kwa upole,

"kuanzia sasa hivi, ondoa Askari wote, nitapeleka watu makini zaidi kumlinda yule mwanamke, kwanza nilikuambiaga umuue kabisa, ila wewe unaendelea kumlea" Rais aliongea kwa hasira,

"ni kweli mkuu, ila nilikuwa nasubiri nafasi ya kufanya hivyo" Mkuu wa polisi alijitetea,

"pumbavu, unazidi kunikera tu, wewe nitakushusha cheo na sitokuamisha mkoa" Rais aliongea na kukata simu, akamuacha mkuu wa polisi akiangalia simu yake tu,

"dah" Mkuu wa polisi alishusha pumzi na kusikitika, kisha akapiga simu hospitali na kuwataka Askari wote waondoke eneo hilo, Askari waliishangaa hiyo amri, ila hakuna aliyehoji, hawakufundishwa kuhoji amri za wakubwa, walifundishwa kutii tu.

************

Mida ya saa tatu usiku, Ray Charles alikuwa kwenye korido za hospital akielekea katika wodi aliyolazwa BQ, haikuwa tabu sana usiku ule mtu kuonekana katika korido, kwa sababu ni wodi maalum kwa hiyo mpaka mtu aingie mule, ujue amekaguliwa vya kutosha.

Ray Charles alitembea kwa mwendo wa taratibu, alionekana hana haraka. Alitembea mpaka ilipo wodi ya BQ. Wakati huo BQ alikuwa bado anajaribu kufanya jaribio la kufungua pingu, ila hakufanikiwa. BQ alisikia hatua za mtu akisogea mlangoni, BQ akafunga macho na kuendelea kujifanya amepoteza fahamu.

Ray Charles akaingia na kumkuta BQ akiwa amefunga macho, Ray Charles akafunga mlango kwa ndani, kisha akasogea dirishani na kufunga madirisha, kisha akashusha pazia. Akarudi mpaka kitandani na kumuangalia BQ aliyekuwa amelala, Ray Charles akainua mkono wake na akauangalia, kisha akavua gloves na kubaki uhalisia wake, yaani mkono wake wa chuma ulibaki wazi. Ray Charles akanyanyua mguu wa BQ wenye pingu na kuutizama, kisha akapiga ngumi ile pingu, pingu ikaachia, BQ akawa haelewi kinachoendelea, alijiuliza huyo aliyeingia ni polisi au daktari? Lakini hakuwa na jibu, na wala hakuwa na mpango wa kufungua macho.

Ray Charles akasogea mpaka kilipo kichwa cha BQ kisha akachomoa drip na mipira mingine iliyokuwa inamsaidia BQ kupumua. Kisha Ray Charles akakinyanyua kichwa cha BQ na kukilaza juu ya chuma ya kitanda, alichotaka kufanya ni kupiga ngumi kichwa cha BQ na kumpasua kabisa.

Ray Charles akakiweka vizuri kichwa cha BQ juu ya chuma ya kitanda, kisha akavuta ngumi kali sana kuishusha juu ya kichwa cha BQ......

********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom