RIWAYA; Mkanda wa Siri

RIWAYA; Mkanda wa Siri

RIWAYA: MKANDA WA SIRI
imeandikwa na Halfani Sudy
SIMU: 0674 395733

Sehemu ya Kumi na Saba

Saa 6: 01 A:M

Usiku uleule kwa kutumia mashine waliyokuwa nayo 'waliiprint' ile picha toka katika simu ya Peter. Sasa kila mmoja alikuwa na picha ya mvuvi mwenye mkanda wa siri mkononi mwake.
Wakiisubiri kesho kwa shauku kubwa sana.

*****

Asubuhi na mapema..... Malolo, Malkia na Peter walikuwa safarini kuelekea katika kisiwa cha Pemba...kumsaka yule jamaa ambaye walikuwa na picha yake mkononi tayari. Walijiridhisha kwa kuangalia tena taarifa ya habari alfajiri na kupata jina la mahali alipokuwa anaishi yule mvuvi, kwa bahati mbaya kabisa taarifa ya habari haikutaja jina la mvuvi, zaidi ya kutaja cheo chake, kwa mujibu wa taarifa ya habari toka katika Televisheni ya Taifa, Jamaa alikuwa ni mwenyekiti wa B.M.U ( Beach Management Unit) katika kisiwa cha Pemba.
Waliondoka huku pale Kisarawe alibaki Chifu, Binunu na Dokta wa familia.
Hawakujua....hawakujua!
Yaani laiti wangejua? Bora hata wasingeenda..

Ukiondoa kina Malkia ambao walikuwa wameenda Pemba kwa waliobaki, Binunu ndiye alikuwa wa kwanza kuamka. Aliamka dakika thelathini baada ya wakina Malkia kuelekea Pemba. Alitoka chumbani kwake na moja kwa moja alienda sebuleni, na kukaa mahali palepale alipokaa jana, sehemu anayokaa siku zote tangu wahamie Kisarawe. Alikuwa anapepesa macho huku akiangalia hapa na pale. Alikuwa anaongea peke yake maneno ambayo bila shaka hata yeye mwenyewe alikuwa hayaelewi maana yake, lakini cha ajabu yeye mwenyewe ndiye alikuwa anacheka kutokana na maneno yake. Kwa hakika Binunu alikuwa kichaa dhahiri.

Dakika thelathini baadae Chifu nae aliamka. Moja kwa moja alielekea sebuleni. Akiwa amejifunga taulo tu kiunoni huku juu akiwa amevaa 'vest' nyeupe aina ya spider. Chifu alikuwa anapiga mluzi akiufatiza wimbo wa kihindi wa All is Well, wimbo mzuri uliopamba tamthilia ya kihindi ya 3 Idiots.
Chifu sasa alikuwa na amani, amani iliyotokana na uhakika, alikuwa na uhakika kwa kikosi kilichoelekea Pemba iwe isiwe lazima kitarejea na Mkanda. Wale ni watu makini aliowatumia miaka kadhaa sasa, na walikuwa wameshafanya operesheni ngumu na za hatari tena zaidi ya hii. Ikiwemo Operesheni Pambana na Simba, Operesheni iliyoanza kama biashara lakini baadae ikageuka na kuwa vita! Chifu alimkumbuka kiongozi wa operesheni hii ya sasa, Malkia. Mwanamke wa kipemba aliyetoka kuwa mfanyakazi wake wa ndani lakini kwasasa aligeuka kuwa mpenzi wake. Mwanamke aliyemfundisha mwenyewe ukatili, ambaye kwa sasa amekuwa katili zaidi yake. Mwanamke mwenye kutumia akili za kuzaliwa kuwahi kutokea hapa duniani.

Chifu alimkumbuka Malolo, mwanaume wa shoka, mwanaume mahiri katika mapambano ya ana kwa ana. Alitingisha kichwa kukili uwezo wa Malolo. Malolo alikuwa ni mtu sahihi kabisa kuwemo katika operesheni hii.

Mwisho alimkumbuka Peter, alivyomkumbuka Peter aliguna tu mwenyewe kwa sauti kubwa, na kuacha kupiga mluzi, hakuwa na maneno mazuri zaidi ya kumuelezea Peter.....

Chifu alipiga hatua mpaka sofani, alienda kukaa katika sofa lilelile alilokaa jana yake, tofauti ni kwamba jana alikaa na mkewe lakini leo alikaa peke yake. Alitulia tuli huku akiangalia runinga.

Runinga ilikuwa inaonesha kipindi cha magazetini.

"Wataalamu wamesahau kuzima hata runinga? Kweli wanapenda kazi"
Chifu alisema huku akichukua kikopo kidogo kilichokuwepo pale mezani. Alikifungua na kumimina unga mweupe katika kiganja chake cha mkono wa kulia. Alivyouona tu ule unga madenda yalimtoka. Ni miaka arobaini na tatu sasa tangu aanze kuutumia unga ule, unga ulioitwa haramu na Serikali lakini kwake ulikuwa halali, tena halali tamu lakini hadi leo alikuwa hajauzoea bado, akiuona tu lazima madenda yamtoke. Unga wa ajabu sana ambao humpa hisia za ajabu siku zote. Kiganja chake cha mkono wa kulia chenye ule unga laini mweupe alikipeleka usawa wa pua yake.
Alianza kuunusa taratibu.

Mara Dokta wa familia alienda sebuleni, walisalimiana na Chifu, baada ya maongezi ya kama dakika mbili Dokta alimuaga Chifu kuwa anaenda kufuata dawa za Binunu.
Akaondoka.

Sasa Chifu alikuwa yeye na Binunu. Chifu akiwa makini juu ya ule unga mweupe kiganjani mwake huku mara chache akiangalia runinga ili kufahamu habari kuu za siku ile kama zilivyoandikwa na magazeti.
Dakika zipatazo tano aliangalia katika runinga, dakika ya sita ilipotimu alihamishia macho yake kwa Binunu. Alimwangalia kwa sekunde zipatazo thelathini, kisha akarudisha macho yake katika runinga, macho ya Chifu hayakudumu sana katika runinga, yalirudi katika kiganja chake, alitabasamu na kuuvuta kwa pupa ule unga wote uliobaki pale kiganjani, alitoa mguno wa raha.
Baada ya kuuvuta ule unga, kwa kasi macho yake yalirudi tena kwa Binunu.
Binunu alikuwa hana hili wala lile, alikuwa hajui yuko mahali gani, hajui yuko na watu aina gani, yeye alikuwa anaongea tu kila neno lililomjia katika akili yake dumavu iliyochanganyikiwa.
Safari hii macho ya Chifu yalidumu kwa Binunu kwa takribani dakika moja, kisha yalirudi tena katika runinga. Alimkuta msomaji wa magazeti akisoma habari za michezo, yeye na habari za michezo wapi na wapi, aliachana na runinga. Sekunde tatu tu macho yake yalirudi kule yalikokuwa dakika moja iliyopita, kwa Binunu. Safari hii macho ya Chifu yalikutana na kitu cha ajabu, akili ya Chifu ilipumbazwa kwa nusu dakika. Alimwangalia kwa jicho tofauti mwanamke yule aliyechanganyikiwa. Sehemu za kati za mapaja yake zilivimba kidogo. Hisia zake zilimwambia kitu kingine kabisa.
Bila kutumia akili wala kuwaza mara mbili Chifu, alikuwa tayari amelevywa na ule unga haramu aliouvuta hivi punde, alinyanyuka taratibu kwenye sofa na kuanza kumfata Binunu pale chini.....

Chifu kaona nini huyu, anataka kufanya nini sasa ? Inaitwa Mkanda wa siri...
 
RIWAYA: MKANDA WA SIRI
imeandikwa na Halfani Sudy
SIMU: 0674 395733

Sehemu ya Kumi na Nane

Chifu Abdullah alimfikia Binunu pale chini. Kwa mara ya kwanza tangu aanze kuishi na Binunu ndio aliuona uzuri halisi wa Binunu. Na uzuri ule ulibariki moja kwa moja nia haramu ya Chifu ambayo kwa kiasi kikubwa ilichochewa na ule unga haramu aliouvuta. Unga ambao siku zote akiuvuta kitendo kinachofuata ni kufanya ngono, kama alivyofunzwa na mwalimu wake wa mapenzi na unga miaka arobaini na tatu iliyopita.

Chifu alifika hadi mahali pale alipokuwa amekaa Binunu, alisimama huku akimwangalia Binunu kwa chini, tena akimwangalia kwa jicho lenye kuonesha maana halisi ya matamanio, denda la matamanio lilimdondoka tena, na kuishia kusambaa kifuani kwake, ingawa safari hii denda lile lilimdondoka kwa dhamira tofauti na ile ya awali.

Mwanzoni madenda yalimdondoka kwa hamu ya unga haramu, unga alioanza kuuvuta akiwa na miaka kumi na saba tu na sasa akiwa na miaka sitini lakini bado aliganda katika matumizi ya unga ule. Ukimuuliza Chifu kiumbe gani ambaye hawezi kumsahau hapa duniani, asingetumia hata sekunde tatu kufikiria, harakaharaka angekujibu ni mwanamke aitwaye Wema Shayo. Mwanamke mzuri wa kichaga aliyemuingiza Chifu katika matumizi mabaya ya madawa ya kulevya.

*****

Alikuwa na umri wa miaka kumi na saba tu Chifu alipotokea kumpenda sana Wema Shayo, alimpenda kwa maana sahihi ya kuitwa upendo wa dhati. Lakini yule mwanamke hakuwa tayari kabisa kumkubalia Chifu ombi lake, sio kwamba hakumpenda Chifu la hasha alimpenda sana ila kulikuwa kuna kizuizi ambacho kilimfanya amkatae. Upande wa Chifu hakukata tamaa. Siku zote alimuelezea Wema kiasi gani alikuwa anampenda sana, na alishaandika barua mara kadhaa za mapenzi kuuelezea upendo wake wa dhati kwa Wema, lakini yule mwanamke alishikilia msimamo wake, alikataa katakata.

Siku moja usiku Chifu na Wema walikutana kama bahati mbaya katika uwanja wa Mbagala Zakheim kulikuwa na maonesho ya sinema. Chifu aliitumia vizuri siku ile kumuelezea Wema jinsi anavyompenda.

"Mimi siyo kwamba sikupendi Abdullah, ila kuna KIZUIZI, sipendi kabisa uingie katika mtego huo, hutotoka, wewe ni mwema sana kwangu, kwanini nikutese... !" Wema alisema baada ya kuyatafakari kwa kina maneno ya ushawishi toka kwa Chifu.
"Kizuizi gani hiko kinachoweza kutokutuunganisha mimi na wewe Wema, amini nakupenda kwa dhati na niko tayari kufanya chochote kile ili kukiondoa hiko kizuizi, naapa Wema " Chifu aliongea kwa kumaanisha.
"Una hakika Abdullah?" Wema aliuza kwa sauti yake ya upole. Sauti iliyopenya moja kwa moja hadi katika moyo wa Chifu.
"Sijawahi kukudanganya Wema na sitothubutu hata siku moja kukudanganya, kwanza kukudanganya wewe ni sawa na kuudanganya moyo wangu"

Wema alimwangalia Chifu kwa sura yake ya upole na kuanza kulia, Chifu alimsogeza Wema na kumuweka katikati ya kifua chake, alianza kumpangusa machozi kwa mkono wake wa kulia mwanamke yule wa ndoto zake.

"Unanipenda kweli Abdullah?" Wema aliuliza kwa sauti ya kwikwi.
"Nakupenda zaidi ya neno lenyewe nakupenda linavyomaanisha, nakupenda zaidi ya unavyofikiria, kumbuka ni miezi saba sasa imepita tangu nilivyokutamkia kwamba nakupenda, pamoja na majibu yako ya kukatisha tamaa lakini bado nimeonesha kama nakupenda, amini nakupenda kwa dhati Wema na sio kwamba nakutamani kama wafanyavyo wanaume wengine, nakupenda toka katika uvungu wa moyo wangu, wewe ni kila kitu kwangu....." Chifu aliongea kwa kumaanisha.
"Abdullah na mimi nakupenda sana, ila......" Wema hakumalizia kusema, Chifu alimkatisha.
"Wema, Wema, Wema.. ila nini sasa, nitamkie na wewe kama unanipenda kama nikupendavyo, nami nipate faraja ndani ya moyo wangu..."
"Mi..mi ..ni te..ja..." Wema alitamka maneno hayo kwa sauti ya kitetemezi.
"Eti!" Chifu alishangaa huku macho kayatoa pima.
"Na siwezi kushiriki tendo la ndoa mpaka nivute unga..." Wema aliendelea kuongea kana kwamba hakuona mshangao wa Chifu.
"......na na huyo ninayeshiriki nae vilevile awe ametumia pia..hapo ndipo hujisikia raha!" Wema alipigilia msumari wa mwisho katika jeneza la Chifu.

Kwa haraka Chifu alimuacha Wema na kusogea nyuma hatua kama mbili, alikuwa anahema juujuu. Huku akimwangalia mwanamke yule toka utosini mpaka miguuni.
Hakuamini.
Hakuamini.
Hakuamini.
Maneno yale alitamani yawe ameyasikia ndotoni.

"Au naota?" Alijiuliza mwenyewe kimoyomoyo.
Chifu aliuma kwa nguvu mdomo wake wa chini kwa meno kama ni ndoto basi aamke. Ingawa aliumia lakini hakuamka, hakuamka kwa kuwa ile haikuwa ndoto. Ilikuwa ni kweli... Wema mwanamke ampendae alikuwa mbele yake. Na kama kweli neno ampendae bado lilikuwa na maana kwake mpaka sasa, ilimpasa atumie madawa ya kulevya.

Mtihani mkubwa!

"Nimekuelewa Wema, kwa kuwa kesho sinema itakuwepo tena tukutane hapahapa uwanjani tuone tumefikia wapi, yanipasa nikafikirie kwanza"
"Sawa lakini nakuomba usimwambie mtu Abdullah, hakuna anayeijua siri hii zaidi yako, na yule aliyefanikiwa kunivutisha madawa kwa mara ya kwanza..ambaye nitakwambia siku nyingine kuhusu yeye" Wema aliongea sauti yenye kuonesha kujuta.
Abdullah aliitikia kwa kichwa.

Usiku wa siku ile Abdullah hakulala, alikuwa anawaza na kuwazua. Ukweli ni kwamba alikuwa anampenda sana Wema, sana tena sana, lakini alikuwa anachukia sana matumizi madawa ya kulevya. Je ni halali kufanya haramu ili upate ukipendacho?
Hadi asubuhi aliamka na swali hilo.
Aliamka na hakuwa na jibu.

Mchana wa siku ile aliona saa zinaenda kwa kasi sana, na hatimaye saa mbili usiku ilifika, muda wa sinema.
Usiku wa kufanya maamuzi magumu!

Siku hiyo Wema alienda mapema sana katika viwanja vya Mbagala Zakheim, huku akimsubiri Abdullah kwa hamu kubwa sana, ukweli ni kwamba nae alikuwa anampenda sana.

Abdullah alikuwa amejiinamia chumbani kwake akiwaza aende ama asiende. Kwenda kwenye sinema ilimaanisha kwenda kumuona mwanamke wa ndoto yake, kwenda kwenye sinema kulimaanisha kwenda kufungua ukurasa mzuri wa mapenzi na mwanamke ampendae, kwenda sinema pia ilimaanisha kuanza rasmi kutumia madawa ya kulevya. Alikuwa anampenda sana Wema, lakini alikuwa hayapendi hata kidogo madawa ya kulevya.

"Nitatumia mara moja tu, kisha nitamshawishi Wema tuache. Nampenda sana Wema, kwanini nisiuoneshe upendo wangu kwake kwa hili? Nisipoenda ataamini kuwa nilikuwa simpendi. Baadae ya kuwa mpenzi wangu nitamshawishi kwa kumwambia madhara ya madawa ya kulevya naamini atanielewa na tutaacha tu..." Baada ya kuwaza maneno hayo alinyanyuka taratibu kitandani na kuelekea katika uwanja wa sinema.

Ilikuwa ni saa tano usiku, Wema alikuwa ameshakata tamaa, akiamini ametoswa na Abdullah. Alikuwa amesimama huku akiangalia sinema lakini alikuwa haelewi kitu, ndipo alipostuka baada ya kuhisi akishikwa bega na mtu, aligeuka nyuma akiwa na ghadhabu, ghadhabu ya kutoswa.
Alipigwa na butwaa!
Alikuwa anatazamana na Chifu. Walikumbatiana kwa nguvu, kila mmoja akilia.

Wiki moja baadae Chifu alianza rasmi kutumia madawa ya kulevya.

*****

Pale ukumbini Chifu aliinama na kumshika mikono yote miwili Binunu aliinuka taratibu, huku akiendelea kuongea maneno yake yasiyoeleweka, na bila kujua sababu ya kunyanyuliwa. Sasa wote walikuwa wamesimama wima, wanatazamana!
Chifu alimsukuma Binunu katika lile sofa ambalo alikaa Peter jana yake. Binunu alidondoka mzimamzima.
Na Chifu alimsogelea.

Katika kichwa chenye akili iliyochanganyikiwa ya Binunu kuna mambo yalikuwa yanapita mithili ya sinema. Ule msukumo mbaya toka kwa Chifu ulimfanya Binunu akumbuke miaka kumi na saba iliyopita. Alikumbuka jinsi mtu mmoja alivyomsukuma mama yake mzazi kwa namna ileile na kuangukia sofani vile vile kama alivyoanguka yeye leo. Alikuwa na miaka tisa tu kipindi hiko, lakini mambo yaliyotokea siku hiyo yalijirudia kichwani mwake mithili ya sinema leo, tena akiwa amechanganyikiwa.

Chifu alimsogelea Binunu na kulinyanyua kwa juu gauni la pinki alilolivaa Binunu.

Jinsi gauni lile lilivyonyanyuliwa Binunu alikumbuka jinsi gauni la mama yake mzazi lilivyonyanyuliwa kwa namna ileile miaka kumi na saba iliyopita huko Kilwa Masoko. Sinema iliyopo kichwani mwake ilimuonesha kuwa gauni la mama yake lilivyofunuliwa vile aliona jinsi baba yake mzazi alivyotoa ukelele mkali wa ghadhabu kuashiria kukerwa na kitendo kile alichokuwa anafanyiwa mkewe kipenzi. Laiti Chifu angejua vitu alivyokuwa anaviona Binunu akilini mwake, ni bora angemwachia tu.....

Sasa Chifu aliishika nguo ya ndani ya Binunu na kuanza kuivua kwa mtindo wa kuivuta kwa nguvu....

Je Chifu atafanikiwa kumbaka Binunu?
Hata mimi nataka kujua....
 
RIWAYA; MKANDA WA SIRI
imeandikwa na Halfani Sudy
SIMU: 0674 395733

Sehemu ya Kumi na Tisa

Kina Malolo walifika katika kisiwa cha Pemba. Kila mmoja akiwa na ile picha ya mvuvi mkononi mwake.
Wale walikuwa ni watu makini, na walijua sehemu sahihi ya kwenda kumsaka yule mvuvi, walienda katika fukwe ya bahari. Na kutokana na umaarufu wa mtu waliyekuwa wanamtafuta hawakupata shida kabisa kumpata mvuvi aliyekuwepo katika picha ile. Mtu wa watatu tu kumuuliza aliwaambia kila kitu kuhusu mvuvi huyo, tena na kuwasindikiza hadi katika kibanda cha yule mvuvi. Ndani ya mioyo ya kina Malkia ilikuwa ni furaha isiyo na kifani, kazi yao ilitokea kuwa rahisi sana...walikuwa wanaamini ndani ya robo saa mkanda utakuwa tena mikononi mwao, iwe kistaharabu ama kwa nguvu. Wakichoamini wao huyo jamaa alipewa mkanda na yule msichana baada ya kutokea ile ajari mbaya ya meli ya MV Donors, kumbe wala haikuwa hivyo...

Ayoub Mbembati alikuwa ni mvuvi aliyejipatia umaarufu muda mfupi sana katika kisiwa cha Pemba. Hii ilitokana na hekima, busara, upole, uwajibikaji na uchapakazi. Uvuvi ilikuwa ni kazi yake kuu tangu alivyohamia katika kisiwa cha Pemba miaka kadhaa iliyopita...uvuvi ilikuwa ni kazi aliyoirithi toka kwa baba yake mzazi, mzee Mbembati. Na kutokana na makuu aliyoyapitia Ayoub ndomana alitokea kuwa na sifa hizo.

Ayoub alikuwa mvuvi, lakini mvuvi duni akiyetumia zana duni. Na bado maisha yake yaliendelea kuwa duni. Baba yake mzazi alifariki akiwa duni pia, tena alifariki kifo kibaya sana mbele ya Ayoub, ni Ayoub pekee ndiye aliyeijua sababu ya kifo cha baba yake. Kifo kilichoacha vitendawili kadhaa mpaka leo. Na sababu ya kifo hiko ambayo ilikuwa ndani ya kifua chake ndiyo iliyomfanya ahame kimyakimya katika mji wa Kilwa Masoko na kuibukia katika kisiwa cha Pemba, mzee Mbembati alifariki kifo kibaya sana akimfata mkewe mwezi mmoja tu baada ya kufariki kwa ugonjwa wa malaria.

Ayoub Mbembati, kitu pekee alichorithi toka kwa baba yake mzazi ni mkanda, mkanda ambao ulisababisha kifo cha kikatili cha baba yake, mkanda ambao ndio uliomfanya ahame bila kupenda katika mji aupendao na kwenda kuishi ugenini, lakini cha kusikitisha mkanda haukudumu sana mikononi mwake.....yaliyotokea hadi leo bado yalikuwa bado katika kichwa chake.

Shirika la W.W.F lilipeleka mradi wa kutunza mazingira ya bahari na maliasili za bahari Pemba, na mikoa mingi yenye bahari na maziwa katika nchi ya Tanzania. Mradi ulioleta matumaini kwa wakazi wa jamii za kivuvi, ikiwemo wakazi wa kisiwa cha Pemba. Wananchi walitakiwa kutunza na kulinda mali za bahari, hapo ndipo vilipoanzishwa vikundi vilivyojulikana kama Beach Management Unit ( BMU) kwa ajili ya kufanya doria baharini na nchikavu kwa lengo la kupiga vita uvuvi haramu, kulinda bahari na mali zake, na Ayoub Mbembati ndipo alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa BMU...Na cheo hiko ndicho kilichomfanya aonekane kwenye taarifa ya habari ya TBC akielezea umuhimu wa kuhifadhi bahari, na kuonwa na Binunu Issa.

*****

Kule Kisarawe hali ilikuwa mbaya sana kwa Binunu. Chifu shetani alikuwa kamkalia kohoni. Alikuwa anataka kumbaka Binunu. Sasa nguo ya ndani ya Binunu ilikuwa katikati ya mapaja yake.
Kichwani sinema ya ajabu ya Binunu iliendelea, alikumbuka jinsi siku ambayo mama yake alikuwa anafanyiwa kitendo kama kile. Sinema ilimuonesha kwamba nguo ya ndani ya mama yake mzazi ilipofika maeneo yale baba yake alikurupuka kwa hasira. Lakini hakufika akikotaka kwenda. Alipigwa kwa nguvu na kiwiko cha bunduki katika paji la uso wake.
Baba yake damu zilimbubujika!

Damu za kwenye sinema zilimkumbusha kitu kipya kabisa leo...
Naam...Binunu sasa alikumbuka !
Sasa haikuwa sinema, ilikuwa dhahiri shahri, Binunu alikumbuka mtu aliyekuwa anamfanyia vile mama yake alivuta vitu fulani kabla hajamfanyia kile kitendo kibaya mama yake mzazi, alivuta kama alivyovuta huyu wa leo. Tena aina ya vikopo walivyotoa hivyo vitu alivyokuwa anavuta huyu aliye mbele yake leo, na aliyembaka mama yake miaka kadhaa iliyopita vilikuwa vinafanana. Vikopo vyeusi vyenye rangi nyeupe, vikopo vilivyotengeneza taswira ya mnyama Pundamilia.
Na taulo la Chifu lilianza kufunguka...

Chifu alikuwa anaendeshwa na hisia zilizotokana na madawa ya kulevya zaidi badala ya akili zake za asili. Madawa ambayo siku zote humshauri kama yanamvyomshauri leo, baada ya kuvuta ni ngono. Kama ukipata nafasi ya kumuuliza Chifu faida ya unga ule angekwambia moja tu, unga ulimfanya ampate Wema Shayo, mwanamke aliyempenda zaidi hapa Duniani, baada ya hapo unga ulimsukumia Chifu katika engo mbaya sana, ulimtoa kwa kasi sana toka kuwa binadamu wa kawaida hadi kuwa mnyama. Na yote hayo yalisababishwa na pesa, ilimpasa apate pesa ili aweze kununua unga, ambao sasa ulikuwa umeweka kambi ya kudumu katika mishipa ya damu yake. Hapo ndipo alipoanza kuwa mwizi, tabia mbaya ambayo hakuwa nayo kabisa hapo kabla, alianza kuiba vitu vidogovidogo vya nyumbani kwao, aliporidhika alihamia vitu vikubwa, aliiba runinga, deki na friji, na kwenda kuuza kwa bei rahisi ili apate pesa ya kwenda kununulia unga. Maneno ya wazazi wake hayakusaidia kitu, ilikuwa ni kama wanampigia mbuzi gitaa. Alivyomaliza vitu nyumbani kwao alihamia katika nyumba za jirani, na hatimaye aliiba popote pale alipoona cha kuiba. Nguvu za madawa ya kulevya zilimpeleka vibaya, na hapo ndipo alipopanda ngazi rasmi, toka mwizi wa kawaida mpaka jambazi, kumbuka alikuwa na miaka kumi na nane tu hapo. Baada ya kupanda ngazi ndipo alipopata wazo jipya, wazo ambalo lilibarikiwa na mpenzi wake, Wema Shayo. Alizamia meli na kwenda Afrika ya kusini...eti kutafuta maisha. Huko ndiko Chifu alikobadilika hasa.
Kwa mara ya kwanza huko ndiko aliua mtu, Mzulu aliyemfanyisha kazi kwa ujira wa kupewa madawa ya kulevya. Baada ya Chifu kumaliza ile kazi, Mzulu alijifanya mjuaji kwa kudhani anaweza kumdhulumu mtoto yule...kumbe Chifu alikuwa mdogo kwa umri lakini mkubwa kwa matendo, hasa matendo ya kikatili. Kilichofuatia hapo Mungu pekee ndio anajua, lakini kwa alichomfanyia yule Mzulu kilimpeleka kaburini na yeye kuhukumiwa kifungo cha maisha jela akiwa mtoto mdogo sana. Jela ikamfundisha shurba Chifu, ukatili, umajinuni na ubabe, pamoja na umri wake mdogo lakini yeye nd'o alikuwa mwamba katika gereza lililokuwepo katika mji wa Soweto.
Na huko ndipo lilipoibuka jina la Chifu, Chifu sasa akawa Chifu wa Gereza la Soweto, na jina lake la awali la Abdullah kufutika kabisa masikioni mwake.
Na baada ya miaka miwili ya jela ndipo mfumo wa kubadilishana wafungwa kati ya Tanzania na Afrika Kusini ulianzishwa, na Chifu alikuwa mmoja wa wafungwa wa mwanzoni waliofaidika na mfumo huo hasa kutokana na umri wake kuwa mdogo, alirudishwa jijini Dar es salaam, alifikia katika gereza la Ukonga.
Hapo Chifu alikuwa na miaka ishirini....

Na sasa Chifu alikuwa yu tayari kumuingilia Binunu. Alimtanua miguu yake kwa nguvu pale chini na kuingia kwa kati.....
Sinema ya kutisha iliyopo kichwani mwa Binunu ilimkumbusha kitu, siku mama yake alivyofanyiwa kitendo kama kile. Siku mama yake alivyoingiliwa kwa kati namna ile alifanya kitu. Naye alifanya kitu hichohicho ambacho alichofanya mama yake miaka kumi na saba iliyopita. Naye aliamua kufanya kitendo hikohiko. Kitendo kama kilichofanywa na mama yake mzazi miaka kumi na saba iliyopita. Binunu alikumbuka vizuri sana kuwa mama yake alimng'ata shingoni upande wa kulia yule jamaa aliyekuwa amemuingilia kati kwa lengo la kumbaka. Naye alidhamiria kufanya hivyohivyo, kama alivyokuwa anaoneshwa katika sinema yake kichwani. Alimwangalia yule jamaa upande wa kulia shingoni kwa lengo la kumng'ata. Upande uleule wa shingo aliong'ata mama yake miaka kumi na saba iliyopita, jamaa alikuwa na kovu!
E bwana wee!
Binunu akili zake zote zilirudi.

"Wewe ndiye uliyembaka mama yangu" Binunu alisema kwa sauti nzito yenye kukwaruza. Chifu aliduwaa...ilikuwa kama ameona mdudu wa kutisha sana, na yeye hakuwa na uwezo wa kujitetea wala kujiokoa....ilikuwa kama mgonjwa ambaye amepigwa sindano ya ganzi lakini akishuhudia jinsi kidonda chake kibichi kikivyoshonwa huku yeye akiwa hasikii maumivu..Chifu hakuamini kabisa kama maneno yale yalikuwa yametoka kinywani mwa Binunu.
"Kwanini mlimuua baba yangu mzazi?" Binunu alibadilisha aina ya sentensi na maana ya sentensi, mwanzo ilikuwa kauli taarifa, sasa ilikuwa katika muundo wa swali. Mwanzoni alimuulizia mama yake, na sasa alimuulizia baba yake. Sasa Chifu alisimama wima, akiwa uchi wa mnyama. Akimwangalia Binunu kwa woga na mashaka. Raha iliyokuwa ikiletwa na madawa ya kulevya ilikata ghafla. Raha ambayo aliyoanza kuipata mara tu pale alipoanzisha uhusiano na Wema Shayo na hadi leo alikuwa anaipata kila avutapo unga. Raha ambayo alihakikisha inamfikia hadi katika gereza la Ukonga kwa njia yoyote ile. Na baada ya kuaminika na mtu aliyekuwa anaingiza kwa siri raha ile gerezani yeye ndiye aliyepata bahati ya kuwa msambazaji, kazi aliyoifanya kwa ufanisi mkubwa sana. Hadi wauzaji wa madawa wakubwa walipotamani kumtoa gerezani ili atoe huduma ya usambazaji nje ya gereza. Haikuwa kazi ngumu kutoka gerezani kama unavyoweza kufikiria. MONEY TALKS! na Chifu alirejea tena uraiani baada ya kukaa gerezani kwa muda wa miaka mitano.
Na hapo alikuwa na miaka ishirini na mitano tu.

Alivyotoka nje ya gereza alikuta kila kitu kimebadilika, wazazi wake wapendwa walikuwa wamehama walipokuwa wanakaa na nyumba ilikuwa imeuzwa. Wema Shayo, mwanamke aliyekuwa anampenda sana, alikuwa ameshafariki miaka mitatu iliyopita baada kupigwa na raia wenye hasira kali baada ya kukamatwa alipoenda kuiba katika duka la Mhindi mmoja Kariakoo. Hapo ndipo Chifu alipopata wazazi wapya, wazazi wake wapya walikuwa madawa ya kulevya, na Chifu alipata mpenzi mpya, mpenzi wake mpya alikuwa madawa ya kulevya. Hakujishughulisha kuwatafuta wazazi wake kama asivyojishughulisha kutafuta mpenzi mpya. Aliendelea na kazi yake mpya aipendayo ya kusambaza madawa ya kulevya katika mikoa yote ya Tanzania. Huku Chifu akiwa hamjui hata 'Boss' wa biashara hiyo. Lakini aliifanya kwa moyo wake wote na ufanisi mkubwa kama ilivyo ada yake. Na hapo ndipo Chifu alianza kuwa Chifu kweli.

"Ulimbaka mama yangu mbele yangu, mbele ya baba yangu, Mlimuuwa baba yangu mbele ya macho yangu, mbele ya macho ya mama....mlimpiga risasi kikatili sana, mama nimpendae mlimbaka kisha mlimuuwa kwa kumkaba shingoni, tena ni wewe ndiye ulimkaba..na kumuuwa mama yangu mpendwa bila huruma yoyote, niambie ni kosa gani kubwa walilowafanyia wazazi wangu? Hadi mkawafanyia vitendo vya kikatili namna ile? Baba alikuwa mwalimu mwema kwa wanafunzi wake na wananchi wote, alikuwa mshauri mwema kwa kila mtu, alikuwa tumaini jema, mtu asiye na ugomvi na mtu yeyote yule, mama alikuwa mama mwema asiyejua kabisa kugombana na watu, alikuwa mithili ya baba, labda ndomana walipendana na kuoana, walikuwa wanafanana tabia, na wahenga waliwahi sema " ndege wanaofanana huruka pamoja', kwanini sasa mliwafanyia vile ndege wale wazuri wafananao kwa tabia njema???" Binunu alikuwa anauliza maswali huku akinyanyuka sofani kumfuata Chifu.

"Hiyo tabia uiitayo njema ndiyo ilimponza marehemu baba yako..." Chifu aliongea kizembe bila kujitambua.

"Amma!" Unasemaje bwege wewe?" Binunu alimaka kwa hasira huku akiendelea kumsogelea Chifu akiwa kafura kwa hasira. Ama kwa lugha nyepesi tunaweza sema hatari ilikuwa inamsogelea Chifu. Tena hatari kubwa sana!
Binunu alikuwa anacheka kwa dharau huku akimsogelea Chifu. Chifu aliendelea kurudi nyuma taratibu. Huku moyo ukimdunda kwa kasi kubwa sana!

"Yaani mlimuuwa baba yangu kikatili namna ile, yaani ulimbaka mama yangu kisha ukamuua kinyama sana, eti leo unaniambia kizembe tu....ni tabia njema yake ndio sababu ya kumuua baba, nd'o sababu ya kumuua na kumbaka mama, ulisikia wapi tabia njema ikaleta matokeo mabaya tena ya kusikitisha namna ile, ngoja nikwambie kitu mzee.....tabia njema siku zote huleta matokeo mema, na tabia mbaya ndio huleta matokeo mabaya, iko hivyo.... matokeo mabaya kama yatakayokukuta wewe leo hii na hii yote ni kutokana na tabia yako mbaya ya kuuwa watu wenye tabia njema.." Binunu alisema kwa jazba sasa, wakiwa wamekaribiana kabisa na Chifu.

Sebuleni sasa palikuwa hapatoshi, Binunu alikuwa amerudiwa na akili zake zote zilizokuwa zimeenda kusikojulikana, tena na akili za ziada zilikuwa zimerudi. Amerejewa na kumbukumbu zake zilizopotea tangu siku ile ilipotokea ajari ya kupangwa ya MV donors. Kitu ambacho Chifu labda alikuwa hajui. Binunu sasa hakuwa Binunu yule aliyekuwa anamfahamu kabla...

Je nini kitatokea? Sehemu ijayo ni sehemu ya mwisho kwa season 1 ya Riwaya hii. Season 2 ipo tayari na inapatikana WhatsApp kwa Sh 1500 tu, ni 0674 395733.
 
HALFANI SUDY katika MKANDA WA SIRI

Sehemu ya Ishirini

Sebuleni sasa palikuwa hapatoshi, Binunu alikuwa amerudiwa na akili zake zote zilizokuwa zimeenda kusikojulikana, tena na akili za ziada zilikuwa zimerudi. Amerejewa na kumbukumbu zake zilizopotea tangu siku ile ilipotokea ajari ya kupangwa ya MV donors. Kitu ambacho Chifu labda alikuwa hajui. Binunu sasa hakuwa Binunu yule aliyekuwa anamfahamu kabla. Kipindi kile akiwa mtoto dhaifu aliyekuwa haelewi chochote wakati wazazi wake wanauliwa. Kwa sasa Binunu alikuwa amepitia mengi sana tangu siku ile ya mauaji ya wazazi wake, miaka kumi na saba iliyopita. Vitu vilivyomjenga na kuwa mwanamke hatari sana. Kuuwa kwake ilikuwa ni mchezo rahisi sana kuliko mchezo wowote rahisi unaofahamu wewe. Binunu alikulia mtaani akiwa na miaka kumi na moja tu. Baada ya miaka miwili ya mateso toka kwa ndugu wa wazazi wake. Alipoingia mtaani, mtaa ulimpokea na kumfunza mambo mengi sana. Mtaa ukamfundisha njia moja tu kama bado anataka kuendelea kuishi, kutumia nguvu ili kupata kila kitu. Naye alilielewa vizuri sana somo hilo, alitumia nguvu ili ale, alitumia nguvu ili avae, alitumia nguvu ili alale, alitumia nguvu ili kujitetea kwa lolote lile baya kwake, kubakwa na kadhalika...

Mtaa ukamtoa kwa kasi toka kuwa kiumbe dhaifu wa kike na kumpeleka kuwa kiumbe mkorofi sana. Asiyeogopa mtu yeyote yule duniani. Kumbuka alikuwa na umri wa miaka kumi na moja tu, na hapo ndipo alipobatizwa jina baya la Chokoraa. Kutokana na ubabe wake uliokubuhu Binunu aliogopwa na kila mtu kuanzia Tandika sokoni na hatimaye akawa homa ya jiji Dar es salaam nzima, dunia ya wababe ilitambua kwamba kuna mbabe mmoja wa kike aitwaye Binunu. Wabeba mzigo, wahuni, mateja walitambua Binunu ni nani, mwanamke mwenye umbo dogo lakini mwenye nguvu ya mapambano, huku mwalimu wake wa medani hiyo ukiwa ni mtaa.

Baada ya miaka saba kupita....Binunu alihama katika ubabe wa mtaani na wizi mdogomdogo na kuingia kwenye ujambazi. Akawa jambazi, Binunu alikuwa jambazi kweli. Akaanza kutumika katika matukio mbalimbali makubwa ya kijambazi, kuvamia benki na kupora pesa, kuvamia vituo vya mafuta na supermarket mote kutafuta pesa. Na mara zote alifanikiwa, alifanikiwa kuiba na kuua! Fani yake mpya ya ujambazi ikamfundisha kitu kipya katika medani, kutumia akili, sasa Binunu akawa anatumia nguvu alizozipata mtaani na akili alizozipata katika ujambazi. Kwa kifupi Binunu alikuwa ni muuaji wa kukodiwa aliyekamilika, anauwa kwa nguvu, anaiba kwa akili na kisha baadae kulipwa pesa. Aliishi hivyo toka alipo timu miaka kumi na nane mpaka miezi mitatu iliyopita alipofatwa na Martin kwa ajili ya operesheni aliyoahidiwa pesa nyingi sana, Operesheni Mkanda wa Siri. Bila kujua operesheni hii sio ilikuwa ya kukodiwa tu na kuvuna pesa kama zilivyo operesheni zingine. Bila kujua ‘OMS’ Ilikuwa inamhusu yeye kwa asilimia miamoja. Mkanda wa siri ukiotafutwa ndio ulikuwa sababu ya kuondoa maisha ya wazazi wake hapa duniani..... Bila kujua Martin Hisia alimuingiza Binunu katika Operesheni iliyompelekea Binunu maamuzi kuwa ni yake kulipa kisasi cha vifo vya wazazi wake ama kujua sababu za vifo vya wazazi wake pamoja na wauaji, na kwasasa chaguo lilikuwa ni lake, maana mbele yake alikuwa na mmoja wa watu waliowauwa wazazi wake. Na ushahidi ulionesha hivyo, na kwa bahati nzuri mwenyewe kakili kwa mdomo wake. Binunu aliingia kwenye operesheni inayomhusu lakini bila kujua, aliingia kwa miguu yake yote miwili.

Alitoka Dar es salaam mwezi mmija na wiki moja iliyopita na kwenda katika visiwa vya Zanzibar, ili kuungana na Richard katika ‘OMS;. Binunu hakuwa amesomea ujasusi darasani kama ilivyo kwa Brown, lakini maisha magumu aliyopitia mtaani yalimfanya kuwa zaidi ya jasusi. Na kufikia kiwango cha kukodiwa katika ‘OMS’. Maisha yote magumu ya mtaani unayoyajua wewe Binunu alikuwa ameshayapitia, na kufuzu kwa kiwango cha juu, mitihani yote wanayopitia watoto wa kike wa mitaani Binunu aliyapitia na yote alifuzu kwa kiwango cha juu. Mtaa ndio uliomfundisha kuuwa ili kutetea haki yake, mtaa ulimfundisha kuuwa ili kutetea heshima yake. Katika maisha yake ya mtaani aliua mtu kwa mara ya kwanza akiwa na miaka kumi na sita tu. Alimuua jamaa akiyeitwa Dula Mbabe.

Ilikuwa usiku wa manane akiwa amelala mbele ya duka moja pale Tandika. Alihisi kupapaswa na mtu mapajani, mwanzoni alidhani ni ndoto, lakini baada ya kuhisi akizidi kupapaswa ghafla alifumbua macho, ndipo alipokutana na vitu viwili kwa mpigo. Alikutana na Kisu kirefu pamoja na sura ya kutisha ya Dula Mbabe. Mbabe wa Tandika. Jamaa alikuwa anataka kumbaka Binunu, Binunu sio kwamba hakuwa tayari kubakwa tu, pia hakuwa amewahi hata kufanya mapenzi kwa hiyari yake. Sasa ataingiaje katika ulimwengu wa mapenzi kwa mtindo wa kubakwa? Kilichofuatia baada ya pale kilitikisa jiji zima la Dar es salaam. Kichwa cha Dula Mbabe kiliokotwa Temeke Sudani, kiwiliwili kisicho na miguu cha mtu asiyejulikana kiliokotwa mbele ya Temeke hospitali huku miguu ikiokotwa katika dampo la Yombo. Polisi hawakupata shida kujua kwamba viungo vile ilikuwa ya mtu mmoja, Dula Mbabe. Jambazi waliyekuwa wanamsaka kwa muda mrefu bila mafanikio. Hawakujishughulisha kumsaka muuaji, walijua itakuwa ni kisasi toka kwa majambazi wenzie baada ya kudhulumiana mali za wizi.
Huo ndo ulikuwa mwanzo wa Binunu kuuwa...
Sababu kuu ya kuwa mkatili kiasi kile ni kwamba, Binunu alianza kuwa mtoto wa mtaani akiwa na umri mdogo sana, na kwa kiasi kikubwa mtaa ndio uliobadiri akili na vitendo vya Binunu. Hata mpango wa kwenda kuvamia kasri ya Abdullah ili kuupora mkanda ni yeye ndiye alikuwa ameupanga. Mpango wa kutumia spray za ocer na foner, huku yeye akiziita kwa ujumla spray zile kama OcaFona. Richard alishangaa sana uwezo wa akili wa Binunu katika kupanga. Alikuwa ameshafanya operesheni kadhaa na watu tofautitofauti, watu mahiri katika medani, lakini hii waliifanya kwa ufanisi mkubwa zaidi, walipata walichokitaka bila kutumia nguvu, na mipango ya Binunu ikienda sawa kwa asilimia mia. Alimkubali sana mwanamke yule na kufikia hatua ya kumwamini na kumpa mkanda wa siri kwenda nao Dar akamkabidhi Martin. Lakini kwa bahati mbaya kabisa meli ya MV Donors ikiwa na Binunu pamoja na mkanda ilizamishwa kwa hila za Malolo katikati ya bahari Hindi. Ajari ilikuwa mbaya sana, kuliko ajari yoyote ya meli iliyowahi kutokea katika kisiwa cha Zanzibar. Ajari ilikuwa na madhara kwa Binunu pia, alijigonga vibaya katika kisogo na kupoteza kumbukumbu pamoja na kuchanganyikiwa. Pamoja na ujasusi wake wote lakini Binunu akili ilimpaa. Kama alikuwa na akili angalau za kuweza kujuta basi labda angejuta kiuwendawazimu kwa kitendo chake cha kujiingiza katika operesheni ile. Ni kudra za Mwenyezi Mungu tu ndizo zilizomuokoa Binunu. Alisukumwa na maji ya bahari yaliyompeleka hadi ufukweni. Na nusu saa baadae aliokotwa na wavuvi wawili, na baada ya muda mrefu wa kushauriana wavuvi wale waliamua kumpeleka katika uwanja wa Maisala. Huku wakilichukuwa wao begi dogo likiloning'inia mgongoni mwa Binunu. Begi lenye mkanda wa siri lilichukuliwa na wavuvi huku Binunu akicheka kiuwendawazimu. Na kutokea yote yaliyotokea...

SASA leo Binunu aliyebadilishwa na mtaa alikuwa ana kwa ana na Chifu, mtu aliyeamini kuwa ndiye aliyewaua wazazi wake wapendwa miaka kumi na saba iliyopita. Na taswira mbaya ya wazazi wake ilimjia tena kichwani mwake. Aliwaona wakiwa hawana uhai wamelaliana chini. Huku damu za baba yake mzazi zikuwa zimemtampakaa mama yake mzazi, ilikuwa ni taswira mbaya sana ya kusikitisha ambayo Binunu aliishuhudia akiwa na umri mdogo. Kumbuka mama yake alikuwa ametoka kubakwa kabla hajauwawa. Taswira ambayo haikuthubutu kutoka katika ubongo wake kwa muda wa miaka kumi na sababu. Na taswira ile mbaya ya wazazi wake ilimpandisha hasira maradufu. Kwa haraka alinyoosha mikono yake yote miwili na kumkaba shingoni kwa nguvu. Huku kidole gumba cha mkono wa kulia akikikandamiza katika koromeo la Chifu. Chifu macho yalimtoka pima!
Mkono wa kulia wa Chifu ukaushika mkono wa kushoto wa Binunu, na mkono wa kushoto wa Chifu ukaushika mkono wa kulia wa Binunu. Akijaribu kuitoa mikono ya Binunu shingoni mwake, lakini hakuweza!
Mikono ya Binunu ilikuwa imara, haikusogea hata chembe. Na kilitokea kitendo cha ghafla. Binunu alimpiga Chifu kichwa takatifu katikati ya utosi wake!
Chifu hakukitegemea kabisa kitendo kile, Binunu alimstukiza sana, wakati yeye akihangaika kuitoa ile roba pale shingoni, Binunu alifanya kitu kingine.
Chifu alichanganyikiwa.
Na muda uleule, Utosi wa Chifu ulivimba kitu kinachoitwa nundu. Chifu naye hakukubali. Hakuwa tayari kudhalilishwa kiasi kile, tena na mwanamke. Aliacha kuushika ule mkono wa kushoto wa Binunu na kuutumia kurusha ngumi ya nguvu kuelekea katika shavu la kushoto la Binunu. Yule mwanamke aliyekulia mtaani aliikwepa ngumi ile kwa ustadi mkubwa sana, huku akiutoa mkono wa kulia katika shingo ya Chifu na kuutumia kurusha ngumi yake ya nguvu, ngumi iliyompata Chifu bara'bara katika mbavu upande wa kushoto. Jamaa alitoa mguno mdogo wa maumivu. Binunu alitanua mikono yake yote miwili mithili ya mtu anayetaka kupaa angani na kuibamiza kwa nguvu zake zote katika kichwa cha Chifu. Mkono wa kulia ulitua katika sikio la kushoto la Chifu na mkono wa kushoto ulitua katika sikio la kulia la Chifu. Masikio yote mawili ya Chifu yalipatwa na pigo lile. Alisikia mivumo mibaya masikioni mwake kutokana na pigo lile liitwalo Malaika.

"Ni sababu gani iliyokufanya uwaue wazazi wangu?" Binunu aliuliza kwa sauti kubwa yenye ghadhabu.
Chifu alikaa kimya.
Alikuwa anamtazama tu yule mwanamke. Siyo kama alikaa kimya kwa jeuri ama kiburi, la hasha alikuwa hajasikia chochote alichoulizwa. Bado masikioni mwake kulikuwa na mivumo kutokana na pigo baya la Malaika alilopigwa. Binunu alihisi jamaa hataki kujibu swali lake. Hasira zilizidi kumpanda. Alirudia tena kupiga pigo lilelile la Malaika. Ni mivumo ya vuuuu vuuuu iliendelea maradufu katika masikio yote ya Chifu. Chifu alibaki mdomo wazi, chozi la uchungu la kiume lilimdondoka sakafuni.

Je nini kitatokea? Leo nataka tuimalize season 1, so likes zikifika 200 inaendelea hapohapo..
 
RIWAYA; MKANDA WA SIRI
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0674 395733

Sehemu Ya Ishirini na Moja

Saa 9: 04 A.M
Katika kisiwa cha Pemba bado wakina Malkia walikuwa wanamsubiri Ayoub. Hawakutaka kutoka pale mpaka waonane nae na kuongea nae. Bado walikuwa na imani kwamba pale ndipo kwenye jibu la mkanda wa siri.

Baada ya masaa mawili, Ayoub alikuwa anarejea katika kibanda chake. Akiwa amebeba mfuko wa rambo uliosheheni samaki wabichi. Akiwa umbali kama wa mita miamoja aliwaona watu wanne wakiwa wamekaa mbele ya kibanda chake. Kati ya watu wale alimfahamu mtu mmoja tu.

"Wale wengine ni kina nani?" Ayoub alijiuliza kimoyomoyo.

Hakuwa na miadi na wageni kwa siku ile. Ayoub aliendelea kwenda katika kibanda chake bila kujua kwamba alikuwa anaisogelea hatari. Kwa mwendo wa taratibu Ayoub aliendelea kuelekea katika kibanda chake dhaifu. Kibanda alichokitengeneza kwa dharura tu baada ya kuhama kwa lazima katika nyumba aliyokuwa amepanga awali. Alitembea huku akiwa na mashaka mengi sana ndani ya moyo wake. Moyo ulikuwa unamdunda pasi na kawaida. Ni mara ya tatu sasa katika maisha yake moyo kumdunda namna ile....Hakuwahi kudundwa na moyo kiasi kile tangu siku ile alivyouwawa baba yake na siku aliyovamiwa chumbani kwake na watu wasiojulikana. Matukio mawili ambayo yamebaki kuwa kitendawili kwake hadi leo. Hakujua vyanzo vyake, hakujua sababu zake. Matukio ya kutisha ambayo yalimtoa Ayoub katika hali aliyokuwa nayo akiwa mtoto, hali ya ucheshi, na matukio hayo yalimtengeneza Ayoub katika hali aliyonayo sasa, hali ya ukimya na upole.
Na hapo ndipo wakina Malkia nao walimuona....

Wakina Malkia walivyoona mtu anaelekea pale wote walisimama wima. Wakijua mtu wa kulifumbua fumbo lao lililodumu mwezi mzima alikuwa amewasili. Mtu muhimu kwa mustakabali wa mkanda uliowapotea kimaajabu. Na sasa walikutana.

"Wageni wako hawa Mwenyekiti" Yule mvuvi aliyewapeleka pale alisema baada ya salamu.

"Ahaaa, nashukuru sana kaka" Ayoub alisema huku akiziangalia kwa zamu sura za wageni zilizopo mbele yake. Alijaribu kuziuliza kumbukumbu zake lakini zilimjibu kwamba hakuwahi kukutana na sura kama zile tangu azaliwe.

"Karibuni sana wageni wangu" Ayoub alisema kwa sauti ya upole yenye kuonesha ukarimu ndani yake.

"Naitwa Angel Michael, huyu anaitwa Maziku Donge na huyu anaitwa Jackson Fued..." Malkia aliwatambulisha wenzake na yeye mwenyewe kwa majina ya uwongo huku akiwaonesha kwa vidole wenziwe wakati wa utambulisho.
Huku wote wakimwangalia yule jamaa kwa pamoja.

"Nashukuru sana kuwafahamu... Mimi kwa majina ninaitwa Ayoub...Ayoub Mbembati, ni mwenyekiti wa BMU ya hapa...karibuni sana" Ayoub alisema kwa sauti yake ya upole.

"Ayoub Mbembatiii!" Wote walisema kwa pamoja kwa taharuki, kasoro yule mvuvi aliyewasindikiza. Mstuko dhahiri ulionekana kwa wageni wale watatu. Walianza kuangaliana kwa muda.
Hawakuyaamini masikio yao.
Mstuko na taharuki ile ilipokewa kwa namna tofauti na yule mvuvi msindikizaji pamoja na Ayoub mwenyewe. Kwanini wageni washangae namna ile kwa kusikia tu jina la Ayoub. Kuna tatizo...tatizo gani sasa?

Mdundo wa hofu wa moyo wake ulioanza pindi tu alipowaona kwa mbali wageni wale ulimthibitishia Ayoub kwamba ulikuwa sahihi, na wale wageni hawakuwa watu wema. Hawakuwa wema kwa vipi, hakujua, alichojua ni kutafuta namna ya kujiokoa. Ilimfunukia kwamba pale hapakuwa mahali salama.

"Ayoub Mbembati..." Malkia alitamka kwa sauti ndogo ya kuchoka. Lilikuwa jina ambalo hakutaka kulisikia kabisa kwa wakati ule. Jina lile lilikuwa na thamani, tena thamani kubwa sana miezi miwili iliyopita, lakini siyo sasa. Sasa halikuwa na thamani kabisa.

*****

Kule Kisarawe hali ilikuwa ngumu sana kwa Chifu Abdullah. Binunu alikuwa amechachamaa kwa jazba na hasira. Ulikuwa ni wakati mgumu sana kwa Chifu. Pengine ingekuwa enzi zake asingeweza kunyanyaswa kiasi kile na yule mwanamke, lakini sasa umri ulikuwa umemtupa mkono. Binunu alitumia vizuri udhaifu huo wa Chifu. Alikuwa ameshampiga mabao ya masikio mara tano sasa. Chifu alikuwa hawezi kabisa kujitetea. Kichwa chote kilikuwa kinamuuma vibaya sana. Na Binunu hakuwa na dalili kabisa ya kuacha kumpiga kwa namna ileile, sehemu ileile, kwa nguvu ileile. Na Chifu aliona asipojitahidi kujibu anachoulizwa atakufa kifo kibaya. Atakufa akiwa kiziwi. Pamoja na maumivu makali na mivumo isiyoisha masikioni mwake lakini sasa alijitahidi kumsikiliza ili amjibu.

"Kwanini uliwauwa wazazi wangu?" Binunu aliuliza kwa ukali huku akitambua kuwa Chifu alikuwa hasikii. Na kweli Chifu hakusikia, lakini alijibu. Chifu aliona mdomo wa Binunu jinsi ulivyokuwa unacheza.
Alimuelewa.

"M..ka...nda!" Chifu alisema kwa sauti ya kukatakata. Binunu alisikia vizuri sana jibu la Chifu. Na muda uleule alikumbuka sauti ya kukwamakwama ya baba yake siku ile wakati anakata roho. Jinsi ikivyokwamakwama na kumwambia kuwa mkanda anao Ayoub.

"Inamaana mkanda tulioenda kuuiba kwenye kasri juzi ndio mkanda alioniambia baba miaka kumi na saba iliyopita kuwa upo kwa Ayoub?" Binunu alijiuliza kimoyomoyo...huku akikumbuka tukio lile na kudhani limetokea juzi tu, kumbe ulikuwa mwezi sasa umepita.
Na kumbukumbu hiyo ilimzidisha hasira maradufu.
Binunu alipandwa na hasira maradufu huku akiwa hailewi kabisa mambo yale yalivyokuwa yanatokea. Sasa alipata kitendawili kipya kabisa kichwani mwake...Hakuelewa kwanini sasa kina Martin walikuwa wanauhitaji ule mkanda. Mkanda wa siri uliosababisha kifo cha wazazi wake wapendwa. Mikono ya Chifu ilikuwa imeziba masikio yake yote mawili, ikizuia mapigo yale ya hatari sana kutoka kwa Binunu. Binunu sasa aligairi, hakufanya kama alivyofanya awali. Alibadili kitendo...
Alimshika Chifu shingoni kama alivyomshika awali, kwa kasi Chifu nae aliacha kuziba masikio na kuipeleka mikono yake juu ya mikono ya Binunu.

"Na hii ni kwa niaba ya baba!" Binunu alitamka maneno hayo huku akimpiga Chifu kichwa takatifu, kichwa cha nguvu mara mbili ya kile alichompiga awali.
Chifu alijaribu kukwepesha kichwa chake, lakini kasi ya Binunu kupeleka kichwa kile ilikuwa ni zaidi ya kasi ya Chifu aliyoitumia kukwepa.
Kilimpata!
"Na hiyo kwa niaba ya mama..khabithi wewe!" Binunu alisema huku akipiga ngumi ya nguvu kwa mkono wake wa kulia, ngumi iliyotua katikati ya uso wa Chifu. Chifu aliinama chini huku akiwa ameshika uso wake kwa viganja vyake vyote viwili. Binunu alikuwa amempiga palepale kilipotua kichwa.
"Na hiyo kwa niaba ya mzee Mbembati...baradhuli mkubwa wewe!" Teke kali toka kwa Binunu lilimpata bara'bara katikati ya miguu yake. Kumbuka Chifu alikuwa uchi wa mnyama. Teke lile lilimrusha juu Chifu na kumpelekea kwenda kujigonga vibaya sana ukutani. Chifu alilala chali akiwa hoi bin taaban. Pumzi zake zilikuwa zinatoka kwa mbali sana. Alikuwa anapigania hewa ili aweze kuishi. Bila wasiwasi wowote Binunu alimsogelea taratibu Chifu, mguu wake wa kulia alimuwekea Chifu kifuani na kuanza kumkandamiza kwa nguvu. Madonge makubwa ya damu yalitoka mdomoni mwa Chifu. Alikuwa anatapika huku sura yake ikiwa imechakaa vibaya sana. Sura ikiwa haina matumaini ya kuishi. Binunu alinyanyua juu ule mguu wake wa kulia na kuurejesha chini kwa kasi sana na nguvu kubwa, mguu ulitua palepale ulipotua awali, katika kifua cha Chifu. Chifu alitapika madonge ya damu huku akiunguruma mithili ya Simba mzee. Binunu hakuwa na huruma hata kidogo, hakumhurumia Chifu, sasa alinyanyua juu mguu wake wa kushoto na kupiga katika sehemu za siri za Chifu, kumbuka Chifu alikuwa uchi wa mnyama.
Na pigo lile lilitua vizuri sana.
Chifu alitoa ukelele mkali, na kuanza kulia mithili ya mtoto mdogo. Binunu aliinama pale chini na kumshika Chifu shingoni. Alilishika koromeo la Chifu kwa vidole vyake viwili, kidole gumba na kidole cha shahada. Na kuanza kulivuta. Macho yalimtoka pima Chifu mithili ya kijusi aliyebanwa na mlango. Maumivu akiyoyapata Chifu yalikuwa hayana mfano, na kwa bahati mbaya kwake alishindwa kabisa kujitetea, msaada pekee kwake ulikuwa ni kupiga makelele, alikuwa anapiga tu makelele yasiyo na maana yoyote kwa Binunu. Binunu alilibinya lile koromeo la Chifu, kitendo kilichofanya amlize Chifu apendavyo. Yule mwanamke akalivuta bwana koromeo. Alilivuta kwa nguvu nia yake ni kulitoa nje!. Roho ya Chifu haikutaka kukaa tena katika mwili ule uliokuwa unapitia katika mateso makali sana. Roho haikuweza kuvumilia maumivu yale. Roho ya Chifu iliruka juu na kwenda kuzimu. Chifu alikata roho akiwa anapitia maumivu makali sana, maumivu ambayo hakuwahi kuyafikiria hata siku moja, maumivu makali ilikuwa kama anachunwa ngozi akiwa hai.

Binunu aliingia ndani, alilivua lile gauni. Alijifuta damu za Chifu zilizomtapakaa mwilini kwa kutumia lilelile gauni, sasa alivaa suruali ya jeans nyeusi na tshirt ya bluu, chini alivaa raba nyeusi zilizomkaa vema bila hata kujua nguo zile za nani. Alitoka nje ya nyumba ile na kutokomea kusikojulikana.

*****

"Wewe kumbe ndo Ayoub Mbembati..?" Malkia aliuliza kwa sauti yake ya uchovu. Sauti isiyokuwa na matumaini yoyote. Walikuwa wamecheza mchezo uitwao pata...potea.

"Ndio mimi Angel, mimi ndiye Ayoub...kwani kuna tatizo gani?" Ayoub alijibu kwa sauti yenye mashaka na kumalizia kwa kuuliza swali. Hakuna aliyenyanyua mdomo wake kumjibu Ayoub. Wote walitazamana tena, kisha wakatikisa vichwa vyao kwa masikitiko. Hali iliyozidi kumchanganya Ayoub pamoja na yule mvuvi msindikizaji. Wakina Malkia hawakuwa na la ziada pale, haikuwa na maana yoyote kujibu swali la Ayoub. Kumbukumbu mbaya zilipita vichwani mwao.

Ni kumbukumbu gani, tuwe wote katika sehemu ijayo na ya mwisho kwa season 1.
 
Back
Top Bottom