Riwaya: Konstebo Zungu

mzaramo

JF-Expert Member
Sep 4, 2006
6,371
5,174
RIWAYA: KONSTEBO NGUZU
NA: George Iron Mosenya

"Nimekosa magoli zaidi ya 9000 katika maisha yangu, nimepoteza mechi zaidi ya 300 katika maisha yangu, niliaminiwa mara 26 kuwa nitaipa timu yangu ushindi lakini nikashindwa. Nilishindwa tena na tena na tena katika maisha yangu NDIO MAANA NIKAFANIKIWA- Michael Jordan, mchezaji wa zamani wa mpira wa kikapu."

NA HII NI SEHEMU YA KWANZA

HALI haikuwa shwari katika kota za polisi maeneo ya Mabatini jijini Mwanza,shida ya maji ilisababisha baadhi ya maaskari kwenda kazini pasi na kuiloweka miili yao panapo maji. Umeme nao uliwalazimu wengi wao kuzipiga saluti huku nguo zao zikiwa hazijanyooshwa.
Hii haikuwa shida sana kwa kundi kubwa.
Majira ya saa tatu kasorobo gari la maji liliwasili, lilikuwa ni agizo la serikali baada ya vilio kuwa vingi kutoka kwa wafanyakazi hawa watiifu.
Akina mama wakatoka nje na kuikimbilia ile gari na kujikuta wameunda foleni ya kutisha huku kila mmoja akimuhimiza mwenzake asiruhusu mtu kuingia mbele yake kwani kila mmoja ana haraka na anayahitaji sana hayo maji.
Kama ilivyo ada, panapo shida ustaarabu husafiri kwenda mbali.
Akinamama watu wazima walikuwa wakipigana vikumbo haswa, huyu anamsukuma mwenzake aliyesukumwa naye anasukuma.
Ilikuwa ni vita ya kimyakimya.
Mwanamke mmoja mkimya alikuwa anatokwa jasho kutokana na kusimama muda mrefu katika ile foleni. Alikuwa akiitumia kanga yake kujipangusa lile jasho huku moyoni akilaumu sana kampuni inayohusika na usambazaji maji jijini humo kutokana na kushindwa kurekebisha tatioz hili lililoendelea kudumu hadi kwa siku kumi.
Wakati anapanga foleni mbele yake walimtangulia watu wasiopungua thelethini, lakini sasa walibaki takribani saba. Akapata ahueni na tumaini jipya likazaliwa katika moyo wake wa subira.
Macho yake yakiwa yanatazama mbele muda wote mara akagutushwa na mguso wa kusisitizwa katika bega lake. Akageuka...
"Naomba unijazie hizi ndoo mbili foleni yako ikifika." Sauti kavu ya kike ikamweleza, akashindwa kuelewa kuwa lilikuwa ombi ama amri.
"Mama, nenda ukapange foleni tafadhali." Akajibu kwa mkato kisha akapiga hatua mbele baada ya foleni kusogea.
"Kwani ukinijazia utapungukiwa nini, watu wengine wana roho mbaya kama nini... ndoo mbili tu!" Mama mtaka kutekewa maji akabwatuka.
"Kha! we shangazi vipi, we mwenzetu ushakoga unanukia pafyumu hapa, sie twanuka jasho halafu unataka urahisi tu. Ebwaneee kapange foleni huko..." Sasa mwanadada akajibu jeuri.
"Na nitachota kabla yako, malaya mgeni wewe..." Akabwatuka huku akiondoka zake kama aendaye kupanga foleni.
Yule binti akatamani kuendeleza shari lakini mmoja kati ya wanawake waliosikia mtafaruku huu akamwonya kuachana na ile shari.
Akatii!
Baada ya dakika mbili anamwona yule mama akiongoza njia kuelekea katika bomba.....
Macho yakamtoka pima asiamini kuwa ni kweli yule mama mnukia manukato anachota kabla yake, hasira zikajijenga katika moyo na kichwa chake.
Kweli akateka ndoo mbili. Akajitwika moja kichwani na nyingine ikaning'inia katika mkono wake wa kuume. Kisha kusudi kabisa akajipitisha mbele ya hasimu wake ambaye alikuwa akisota bado katika foleni.
"Kinyamkera utangoja mpaka miguu izame tumboni..." Neno chafu likamtoka yule mama.
Uvumilivu ukampiga chenga mwanadada akachomoka katika foleni akamvamia yule mama, ndoo ikamtoka kichwani na ile ya mkononi ikatua chini.
Ukafuata ugomvi mkubwa kati ya mama mtu mzima na mwanadada. Mwanadada alikuwa hodari akamrarua vyema yule mama mtu mzima huku akimpa zawadi ya kapu la matusi.
"Wewe Janeth wewe.... mke wa Inspekta huyo. Mungu wangu eeh! umefanya nini sasa... ungevumilia Janeth. Tumeshamzoea huyu hapa kota mbona sisi... ndo tabia zake."
Janeth akabaki kuduwaa, yaani kuwa mke wa inspekta ndo awe na tabia kama hizo. Janeth hakuwa akielewa sawa juu ya hivyo vyeo, kwake ikawa kama ndoto tu.
Baada ya saa moja kupita askari wawili wakafika kota za polisi mabatini wakamkamata Janeth ambaye alikuwa akiishi peke yake kwa wakati huo baada ya kaka yake ambaye ni askari kusafiri na mkewe kwenda kijijini.
Akawekwa rumande kwa siku nne!
Ilikuwa ni mara yake ya kwanza, hivyo aliteseka mwili na akili.
Alitoka akiwa amekonda mno.
Akapewa onyo kali juu ya kosa lake la kumshambulia mke wa Inspekta.
_____
KILA aliyekuwa nje alimwona Janeth alivyokuwa anapepesuka, kijana mmoja akawahi kumpokea tofauti na wengine waliobaki kusikitika bila kutoa msaada.
Akamfikisha hadi ndani, akatoka nje na kumletea maji ya kuoga, kisha akamkaribisha chai.
Baada ya huduma hizi Janeth akachangamka kidogo. Wakazungumza mawili matatu kisha kijana akajitambulisha wakati anataka kuaga.
"Naitwa Martin, Konstebo Martin Nguzu"
"Lipi jina lako, Konstebo ama Martin. Maana umeanza Martin ukasita kisha ukaanza na Konstebo...." Janeth akahoji.
Martin akatokwa na tabasamu hafifu kisha akamfafanulia Janeth kuwa Konstebo sio jina bali ni cheo katika jeshi la polisi.
Hakumweleza kuwa ni cheo cha chini kupindukia...
______
JIJINI Dar es salaam hali ya hewa ilikuwa tulivu lakini joto halikutoroka liliendelea kuweka kambi jijini humo.
Joto hili halikuyaathiri maji ya bahari ya hindi, hivyo watu walijazana katika fukwe mbalimbali kwa ajili ya kupambana na joto hili linalokera.
Katika ufukwe maarufu wa Koko mamia walikuwa wamejitosa katika maji wakijaribu kuzisahau shida zao kwa kuogelea.
Kijana mmoja alikuwa pembezoni akitazama watu wanavyoshindana kuyakata mkaji kwa mbwembwe. Alifurahia kutazama zaidi kuliko na yeye kujumuika katika maji yale.
Si kwamba alikuwa hajui kuogelea la! Maamuzi tu...
Na vile alikuwa mgeni jijini Dar hakutaka kuleta ujuaji aje aibiwe nguo zake aishie kudhalilika kwa kutembea nusu uchi na nguo za kuogelea barabarani.
Wakati anaendelea kutazama waogeleaji hakuacha kuangaza fahari nyingine ya macho.
Mabinti warembo wa Dar es salaam!
Alikiri kuwa hayakuwa maneno matupu, ni kweli ni warembo mno. Urembo ambao unaweza kusababisha mwanaume kukiuka viapo vyake....
Katika kutazama vivutio hivi likapita kundi la watu watatu. Mwanaume mmoja na wanawake wawili.....
Akaisikia sauti ambayo haikuwa ngeni sana katika masikio yake. Akasimama wima na kuanza kufuatilia kundi lile ili aweze kuona ni nani anayezungumza sauti ile.
Akaongeza mwendo na kulifikia lile kundi. Kishya akapiga moyo konde na kuwasemesha....
Wakasimama!
"Samahani.... kuna sauti naifananisha kati yenu." Akarusha kete yake.
Wakacheka!
"Ehee! sauti yako dada, si ngeni kabisa katika masikio yangu. Sijui kama tumewahi kuonana..."
"He! kaka, wenzako wanafananisha sura wewe unafananisha sauti, utajuaje labda uliisikia kwenye Televisheni ama huduma kwa wateja..." Akajibu kwa nyodo kiasi.
"Au ndo yaleyale anayoyasema mama yenu... mnafanana misauti hiyo hatari..."
"Eti kaka labda ulimsikia Zubeda ukadhani ndo mimi..." akajazia dada yule mrefu na aliyeumbika vyema hasa hasa miguu yake.
"Mimi naitwa Nguzu, Martin Nguzu. Sijui kama umewahi kulisikia jina hili." Akajaribu kujitambulisha huenda atakumbukwa.
"Samahani kaka, sijawahi kusikia hilo jina hakika." Alijibu kiupole.
"Labda umewahi kukaa Mwanza. Huku Shamaliwa, Igoma ama Nyegezi..." Alizidi kutafuta uthibitisho.
"Mh! kaka huyo mtu unamdai ama maana si kwa kulazimisha huko. Huu ni msako haswa..." Dada wa pembeni akachombeza.
"Hebu ngoja, kwanini tuandikie mate...." Dada aliyefananishwa akasema kisha akachukua simu yake akabofya na kuweka sikioni.
"Eh! Da Zuu kuna mtu kakufananisha huku...." Aliongea huku anacheka.
"Anaitwa Zungu sijui nani..."
"Naitwa Nguzu..." alirekebisha upesi Martin.
"Anaitwa Nguzu, hebu ongea naye bwana. Maana alivyotuganda looh!" Akampasia simu Martin Nguzu.
"Habari, naitwa Martin, Konstebo Martin Nguzu..." Akafanya utambulisho kama alivyowahi kufanya jijini Mwanza kwa mwanadada aitwaye Janeth lakini huyu wa sasa ni Zubeda.
Maongezi yalichukua takribani dakika moja kabla simu haijarejea mikononi mwa dada aliyefananishwa.
"Ndiye.." akashusha pumzi martin huku akitabasamu.
"Kumbe ni askari looh! ningeshangaa mlugaluga tu aje kuhangaika na watu asiowajua." Hatimaye yule mwanaume akazungumza. Mwanaume aliyekuwa pamoja na mabinti hao.
"Amesema nikupatie nambari yangu umtumie sasa hivi anipigie." tabasamu halikujipa likizo katika midomo yake pindi alipokuwa akiyatamka hayo.
Ikawa hivyo. namba ikatumwa lakini hakupigiwa simu...
Usiku wa saa nne simu yake ikaita...
Alikuwa ni Janeth ambaye kwa sasa anajulikana kwa jina la Zubeda.
Ni miaka mitatu ilikuwa imepita tangu waonane mara moja tu jijini Mwanza. Wamekutana tena jijini Dar es salaam!
Maisha ya Martin yalikuwa tulivu bila ubaya na mtu.
Huenda yangedumu katika utulivu huu kwa miaka mingine mingi, lakini kukutana na Janeth aitwaye Zubeda kwa sasa ikawa ni safari nyingine ya kutisha!
 

Attachments

  • 15871888_1251237634932841_8387503877891183478_n.jpg
    15871888_1251237634932841_8387503877891183478_n.jpg
    43.1 KB · Views: 307
"Nimejifunza katika maisha yangu kuwa walimwengu watasahau vyote ulivyosema, pia watasahau vyote ulivyofanya lakini kamwe hawatasahau ULIVYOWAFANYA WAJISIKIE aidha vibaya ama vizuri...."

HII NI SEHEMU YA PILI

Honi ya gari ilisikika mlinzi akafungua kizingiti kidogo kilichopo getini akaisoma nambari na kutambua kuwa ilikuwa nambari ya bosi wake. Upesi akalifungua geti vyema gari ikaingia ndani.
Tofauti na siku zote, siku hii gari lilipita hadi nyuma ya nyumba. Mlinzi hakufuatilia kwa sababu tayari alimuona bosi wake kupitia kioo cha mbele.
Gari lilizimwa kisha akashuka mwanadada ambaye hakuhitaji kukuonyesha mali zake nyingi ili uweze kumweka katika kundi la wanadada wapambanaji wa mjini ambao wamefanikiwa kuzikusanya noti na kuizoea harufu yake.
Alikuwa amevalia sketi fupi iliyoruhusu mapaja yake kuonekana japo kwa kuibiaibia, mkononi alishikilia simu mbili ambazo kwa bei ya harakaharaka unajenga nyumba kijijini kwenu kwa kutumia tofali za kuchoma na kuezeka kwa bati zenye hali nzuri na zinabaki senti kadhaa za kununulia jenereta dogo litakalofanya nyumba yako iwe kivutio kwa watoto mpaka wazazi wa hicho kijiji unachoishi nyakati za usiku.
Kwa mwendo wa madaha akaufungua mlango wa nyuma, akashuka kijana ambaye hawakuwa wakiendana hata kidogo. Huyu alikuwa mrefu wa haja mweusi na ambaye alionekana kuwa mwingi wa mazoezi kwa jinsi umbile la kifua chake lilivyogawanyika.
"Nguzu, hapa nd'o ninapojilaza walau siku ziende..." Alizungumza mwanadada ambaye Nguzu alipaswa kumtambua kama Zubeda na kusahau kabisa kama aliwahi kulijua jina la Janeth maishani mwake.
Nguzu alikuwa amejiandaa kisaikolojia kuanzia awali kuwa yule Janeth wa Mwanza aliyeswekwa rumande kwa sababu ya kumzongazonga mke wa inspekta atakuwa amebadilika mno. Lakini hakudhani kuwa angeweza kuwa anaishi katika nyumba nzuri kiasi kile, kuendesha gari zuri namna ile.
Umbo lake nalo lilikuwa limenoga, hakuwa yule kimbaumbau wa Mwanza mabatini.
Mate ya matamanio yakamruka Nguzu.
Akatamani gari, akatamani nyumba na maisha mazuri kwa ujumla.
Lakini angeyapata kwa wepesi gani ilihali alikuwa amegotea katika cheo cha ukonstebo katika jeshi la polisi na hapo alikuwa na majukumu lukuki yaliyojua kuutafuna vyema mshahara wake mdogo kila ulipokuwa unaingia.
Alipoingiza mguu wake sebuleni akazidi kughafirika, maisha ya Zubeda yalikuwa yanamkera si kwa sababu ni mabaya la! alikuwa na maisha mazuri kupindukia.
Akajaribu kuanza kujifananisha naye walau kidogo, Zubeda anamiliki luninga bapa yeye anamiliki ile modeli ya zamani yenye kisogo mfanowe mlima kilele cha mlima Kilimanjaro.
Nguzu akasonya na kupuuzia uwiano aliotaka kuuweka.
"Huenda ameolewa na kibopa hapa mjini! Acha matamanio Nguzu!" alijionya Nguzu na hapo akamuuliza Zubeda juu ya masuala ya mahusiano.
Upesi Zubeda akajibu kuwa hajaolewa na hatarajii kuolewa hivi karibuni.
Matamanio ya Nguzu yakarejea upya!.
"Njoo uione nyumba yangu Martin, Konstebo Martin Nguzu!" Zubeda akaiga namna Nguzu alivyokuwa akijitambulisha.
Nguzu akatokwa na cheko la haja!
Wakapita huku na kule hadi wakakifikia chumba cha Zubeda. Hapa ndipo Nguzu akahisi kuwa Zubeda ni mwongo tu hakuwa akiishi peke yake, na hii ni baada ya kuiona sare ya jeshi la polisi katika chumba kile.
"Hivi wanawake wataacha lini uongo wao jamani! kwani akiniambia kama ameolewa mimi nitapoteza fahamu ama?" Alijiuliza huku hamu ya kukisaili chumba ikimwisha.
"Zubeda una uhakika haujaolewa?" Kwa ghadhabu kiasi fulani akahoji.
"Eeh! sijaolewa vipi unataka kunitolea mahari." akajibu na kutupa utani juu yake.
"Na hizo sare.." Akahoji huku akikodoa macho ya kumsuta Zubeda.
"Ooh! sijakueleza kumbe, unapaswa kunipigia saluti Konstebo Martin Nguzu, mimi ni koplo Zubeda Msangi." alijibu kiuchangamfu sana.
Nguzu akabaki mdomo wazi, moyo ukaingiwa uchungu asiamini kuwa yule binti ambaye miaka kadhaa nyuma hakuwa akijua hata nini maana ya Konstebo leo hii ni Koplo. Cheo kimoja juu yake.
"Nadhani mwakani naweza kuwa ssajenti kama Mungu akipenda!" Alimalizia Zubeda.
Mungu akipenda?? akajiuliza Nguzu, ina maana Mungu haoni kuwa mimi ninahitaji zaidi kuliko huyu mwanamke au? akajiuliza katika nafsi yake na asipate majibu mjarabu.
Zubeda akatoa picha mbalimbali na kumwonyesha Nguzu, siku akiwa anaapa na picha kadhaa akiwa mafunzoni.
Nguzu akapwaya!
Kumbe kweli!! Akagutuka
Akapigia mstari kuwa hana hadhi yoyote mbele ya Zubeda.
Kikubwa alichomzidi ni kwamba yeye alikuwa mwanaume na Zubeda mwanamke, lakini hata akijitoa ufahamu kuhusu hilo bado Zubeda naye angejitapa kuwa yeye ni mwanamke na Nguzu hajawahi wala hatakuja kuwa mwanamke.
Nimepatikana leo! Alikiri Nguzu huku kijasho chembamba kikiulowanisha mgongo wake.
Bahati iliyoje kiyoyozi kilikuwa kinapepea, la sivyo kile kijasho cha usoni kile kinachoibuka ghafla mtu akiwa katika taharuki kingemuumbua Nguzu.

Zubeda alijitahidi kadri alivyoweza kumfanya Nguzu ajisikie yu huru lakini haikuwa heri katika moyo wa Nguzu.
Lakini jitihada za Zubeda kuujenga ukaribu baina yake na Nguzu hatimaye ile safari yao ambayo ilianzia jijini Mwanza ikafikia palipotarajiwa.
Ilikuwa ni siku nyingine ya kukutana kwao, walianza kwa kukumbushiana juu ya lile sakata la shida ya maji kota za polisi jijini Mwanza wakaunganisha na sekeseke la Zubeda kukabana na mke wa Inspekta. Wakafikia lile tukio la Nguzu kujitolea kumsaidia Zubeda kuanzia maji ya kuoga na baadaye chai.
Sasa Zubeda akamtaka Nguzu amtengenezee tena chai, Nguzu akafanya zaidi ya chai akampikia Zubeda ugali wa dona, nyama na mboga za majani.
Pishi likamnogea Zubeda akajikuta anataka tena na tena......
Mwishowe mapishi yakawa mapishi.
Uhusiano wa kimapenzi ukaibuka.
Lakini ulikuwa uhusiano wa kisasa uliotawaliwa na lugha za kisiasa.
Uliojaa masharti lukuki.
"Martin, sina la kukuficha safari yangu hadi hapa nilipo imetawaliwa na mikato mingi. Hadi sasa ninajihusisha kimapenzi na mume wa mtu, sio kwamba ninampenda kwa dhati ila nitakosa adabu nikisema kuwa simuheshimu. Ninamuheshimu sana moyo wangu unanishuhudia katika hili. Ujue niliwapuuzia vijana vijana hawa ama niwaite watoto, wao wanachoweza kukufanyia kwa ustadi mkubwa ni kukuburudisha mwili tu lakini kwenye masuala ya maisha wanakudumaza. Halafu wanabana sana yaani, ikitokea amekulipia kodi basi anataka kila siku aje kuifaidi kodi yake chumbani... looh!" Martin Nguzu akajikuta anatokwa na kicheko kwa jinsi Zubeda alivyokuwa analalamika.
Ni kweli lakini haikuwa masihara!
"N'do hivyo Martin yaani inafikia hatua unajuta, na vile damu inachemka anaweza akakuvunja mgongo. Nikaona hapana siwezi, nikajiweka kwa kile kibabu kina pesa na kuja hapa ni mara moja moja..... Jiulize Martin, kibabu kimenitafutia cheti cha fomfoo kwa jina hili la Zubeda, kimepambana nimeenda jeshini, kimepambana sijapitia msoto jeshini na hatimaye nimepata kazi. Kwanini nikidharau..... nakuapia kwa mizimu yote Martin, katu sijawahi kujihusisha na mapenzi na mwanaume mwingine tangu nianze kuwa na Inspekta. Wewe unakuwa wa kwanza tafadhali nakuomba sana usije ukaniharibia, usijekuwa kama vijana wenzako wanaopenda ngono kama walitangaziwa kuwa ukifanya sana unaongeza umri wa kuishi....." Akamalizia kwa utani kisha akampiga busu baridi kabisa Konstebo Nguzu katika papi za midomo yake.
Konstebo akajiona yu daraja moja na inspekta ama ikibidi hata mkuu wa majeshi.
Busu pekee!
Mahusiano yakaanza.
Hawakuliona giza lililokuwa linawanyemelea.
Wakapumbazwa na mwanga wa mwishomwisho wa mshumaa!.
Mbaya zaidi Nguzu hakutaka japo kulijua jina la inspekta ambaye anammiliki Zubeda.
Penzi likanoga Nguzu akambatiza Zubeda jina maridadi la kimahaba. Jina linalotamkika kwa sauti tulivu ya kiume na kuleta hamasa panapo faragha.
Akamuita Zuu!
_____
MUHARIRI wa gazeti la SIRI KALI alikuwa akiiendesha gari yake kwa mwendo wa kasi isiyohatarisha maisha yake ili awahi nyumbani. Kuna kitu alihitaji sana kupata uhakika kama kinaenda sawa na anavyodhania.
Ilikuwa kawaieda yake kutopenda kuwa mtu wa kuacha mambo juu juu kama ilivyokawaida ya wengine. Tangu akiwa shuleni alitambulika kwa waalimu wote kutokana na usumbufu wake, alikuwa hakubali kitu kimpite asikielewe kisha akae kimya tu.
Aliwasumbua sana waalimu kiasi kwamba ada yake ilikuwa inakwenda kihalali kabisa.
Tabia yake hii ikaendelea hata katika utu uzima wake akiwa kazini, aliifanya kazi yake kiustadi pasi na kubahatisha na pale alipohisi kuna utata aliwahi kutafuta uhakika kwa wanaojua zaidi yake.
Kutokana na gazeti alilokuwa anafanyia kazi kujihusisha sana na masuala ya siasa muhariri huyu alijiundia urafiki na na vitabu vya siasa ya afrika na dunia kwa ujumla lakini hakuwa mbali na masuala yahusuyo jeshi la polisi ambalo aligundua kuwa lipo jirani sana na siasa kuliko majeshi ya nchi za bara la ulaya ama Amerika.
Utendaji kazi wake wa kiwango cha juu ukamsababisha apewe jina ambalo hakuwahi kulisikia waziwazi zaidi ya tetesi pekee.
Wafanyakazi wenzake wakamuita Juma kimbelembele badala ya jina lake la kuzaliwa Juma Kiwele.
Hakujali maisha yakaendelea.
Alipofika nyumbani akabadili nguo zake na kisha bila kupumzika akamuaga mkewe akaondoa hadi mtaa wa tatu, akaimalizia safari yake kwa mzee wa kale ambaye alikuwa na rundo la magazeti ya miaka ya nyuma. Kuna kitu aliwahi kukiona akahitaji kukiona tena kiuhakika.
Mzee akamwachia ukumbi, akafukunyua kwa juhudi bila papara hatimaye akalipata gazeti la mwaka 1982. Kuna waraka ulikuwa umechapishwa.
"Kwa macho yangu nilitazama mwanangu wa kwanza akiuwawa mbele ya macho yangu, niheri angefyatuliwa risasi moja na kupoteza uhai. Alinyanyasika kabla ya kupoteza uhai, walimkata sikio lake ili akiri kuwa tumehifadhi bunduki ndani ya nyumba yetu, walimvunja magoti yake ili akiri kuwa sisi si raia wa Tanzania. Roho iliniuma sana haswa nilipokumbuka zile harakati za kugombea uhuru angali nikiwa kijana mbichi sana, nilipigana kufa na kupona kwa ajiri ya nchi yangu leo hii mwanangu anavunjwa miguu ili akiri kisichokuwa na ukweli. Sikuwa na la kufanya, akapoteza maisha wakatangaza kuwa alijaribu kutoroka akatandikwa risasi akapoteza damu nyingi kabla ya kugeuka maiti. Haikutosha hii, wakamwendea mke wangu kipenzi, bahati nzuri kwake hakupitia mateso bali alipoteza maisha baada ya kugundua kuwa mwanaye angali mfu!
Sikuwahi kuwa na bunduki lakini sasa ninayo, sikuwahi kuwa na roho mbaya lakini niliyonayo ninakaribiana na ibilisi, ninapoandika waraka huu bila kujalisha kuwa utachapishwa ama la nitakayoyafanya naomba nisilaumiwe na ninajua kuwa ipo siku nitakufa. Mkibahatika kuyaona maitiyangu na myape adhabu kwa kushindwa kuwa na moyo wa kusamehe!
Wakati mnayaadhibu maiti yangu mjiulize kila mmoja kwa nafsi yake.
Je? ungelikuwa wewe ungelistahimili uliyoyashuhudia??
Walidhani mimi ni mfu kwa mabaya waliyoutenda mwili wangu, lakini Mungu akawa upande wangu nikabaki hai...

Florian Ngengekuzenza Nguzu, 1982."

Waraka ule wa aina yake ukakomea pale, na baada ya hapo ukimya ukatanda mpaka miaka mitatu baadaye ambapo liliibuka kundi lililotikisa nchi, ujambazi ukakithiri utekaji na mambo yote ya kutishia amani.
Waraka ule ukiwa umesahaulika mmoja kati ya watekaji anakamatwa anabanwa na kusema kuwa kiongozi wake anaitwa Nguzu Ngengekuzenza lakini katu hajawahi kumtia machoni.
Msako unapita lakini hakuna walichoambulia. Hakuna aliyetambua ni wapi mzee yule alikuwa amejificha....
Mtindo wa matukio aliokuwa akiutumia Ngengekuzenza ambaye alisadikika kuwa mkuu wa oparesheni hiyo isiyokuwa na jina ulikuwa mtindo wa akili nyingi kuliko nguvu. Wakilinda huku analipua kule, wakiachia hapa anaingia mzima mzima.
Lakini hakuna aliyewahi kumtia machoni.
Mnamo mwaka 1988, Ngengekuzenza anakutwa amepoteza maisha mtaroni bila kuwa na jeraha wala ujumbe wowote.
Maswali mengi yakabaki bila majibu. Wengine wakisema hili hawa wanalipinga bila kuwa na hoja za msingi.
Muhariri akamaliza kupitia alichotaka kupitia kisha akapitia majina yote ya askari waliokuwa wamehamishiwa katika vituo mbalimbali jijini Dar es salaam.

Konstebo Martin Nguzu!

Jina hili likamkuna sana Juma, akawa anatamani sana kuonana na askari huyu amuulize mawili matatu iwapo ana uhusiano wowote na mzee yule wa miaka ya themanini aliyetikisa nchi na kisha kukutwa amepoteza maisha bila jeraha lolote.
"Nitamtafuta taratibu tu.." alijisemea wakati akiyaweka sawa magazeti yale mengi ili aweze kuaga na kuondoka.
"Kama ni yeye nitaandika makala ambayo itanipa Tunzo ya mwandishi bora. Kupata Tunzo na ujana huu mbona ni fahari sana. Nitawakomesha ofisini watanitungia jina jipya kwa soni itakayowakumba" Alijisemea huku akiwa wima na tabasamu pana usoni.
"Babu kuna gazeti moja ninatoka nalo."
"Ukumbuke tu kurudisha na kulitunza vyema mjukuu wangu Juma." Babu akamsihi.
Juma akaaga na kutoweka. Hakuelekea nyumbani badala yake alifuata uelekea tofauti ili ausogelee mwanga kuhusiana na martin Nguzu.
Alisahau kuwa mwanga haumwepushi mtu kupotea njia, mamia kwa mamia hupotea njia mchana kweupe na jua likuwa linaimulika dunia.
 
RIWAYA: KONSTEBO NGUZU
MAANDISHI YA: George Iron Mosenya

"Siku mbili za msingi katika maisha yako ni SIKU YAKO YA KUZALIWA na ile siku utakayogundua NI KWANINI UMEZALIWA...."

HII NI SEHEMU YA TATU

KUPENDWA RAHA, tena raha hii huja pale unapoyaona waziwazi mazingira ya penzi lenu kudumu sana.
Mapenzi mengi yanayohusisha watu wengi wasiokuwa na uwezo mzuri kifedha huvunjika mapema kwa sababu ya kutowajibika.
Sasa penzi la Konstebo Nguzu lingevunjikaje?
Zuu haombi kuongezewa salio kwenye simu, halalamiki kununuliwa simu mpya, ukiona anaomba kulipiwa kodi basi huo ujumbe ameutuma bahati mbaya huenda alikuwa anamaanisha ni yeye anataka kumlipia Nguzu kodi ya pango, haombi kununuliwa nguo badala yake analalamika kuwa kabati limejaa mno hana pa kuweka nguo nyingine.
Sasa penzi linavunjikaje hapo, labda wachokane tu!
Nguzu hakuwa na mpango wa kuchoka penzi hili.
Penzi lililomfanya anawiri na kujisahau kabisa kuwa yeye ni Konstebo, kuna kipindi aliwahi kujiona kuwa yungali Mkuu wa majeshi yote ya ardhi na anga nchini Tanzania.
Mapenzi bwana!
Ikiwa imepita miezi takribani minne tangu gundi ya huba iwaunganishe wawili hawa huku lile pepo la wizi wakilihalalisha na kuwa halali.
Konstebo Nguzu alikuwa eneo lake la kazi majira ya asubuhi.
Ilikuwa yapata saa mbili na dakika chache asubuhi katika kituo cha polisi Magomeni usalama, mgahawa ulikuwa umesheheni tayari wateja ambao asilimia kubwa walikuwa ni askari wa kituo kile. Nguzu akiwa mmoja kati yao
Si kwamba raia wema hawakuruhusiwa kutumia mgahawa ule lakini kama ilivyo ada ya Tanzania, raia wanawaogopa askari wao na askari wanapenda kuogopwa.
Watachangamanaje?
Mama muuza alikuwa amejikita katika kuwahudumiwa supu na chai askari waliokuwa wakiwania, kila mmoja akitaka kuhudumiwa wa kwanza ili aingie katika majukumu yanayomuhusu.
Vyeo hadi kwenye chakula cha kulipia? Nguzu alinung'unika katika nafsi yake baada ya kuambiwa ampishe askari mwenzake ahudumiwe kwanza kwa sababu tu alikuwa amemzidi cheo.
Akatii!
Kanuni muhimu kabisa katika jeshi, akawa ameifuata.
Kitendo cha kukatishwa zamu yake kikamfanya anune, kisha akaghairi kunywa supu akaagiza soda baridi akaketi na kuanza kunywa.
Hata kabla soda haijafika robo, akatakiwa kumpisha kiti mkubwa wake mwingine aketi.
Sasa ladha ya soda ikabadilika ghafla na kuwa chungu mithiri ya pombe inavyokuwa kwa mnywaji wa siku ya kwanza.
Akiwa ameegemea ukuta alijitazama begani hakuwa na nyota hata moja mwenzake alikuwa ameanza kuchafuka begani.
"Konstebo!" Sauti ikamtoa katika lindi la mawazo.
Akageuka huku na kule kutazama ikiwa ni yeye anaitwa ama kuna konstebo mwingine jirani na yeye.
Hakuwepo!
"Konstebo!" akaitwa tena kwa cheo chake, cheo cha chini kabisa katika jeshi la polisi. Akaitikia wito, akamwona yule bwana mwenye cheo cha Inspekta akimwonyeshea ishara kuwa kiti kipo wazi aketi.
Akaruka upesi akatua katika kiti.
Kitendo cha kupewa kiti na Inspekta kikarejesha ladha ya soda ile na ubaridi ukapenya vyema kooni.
Akiwa katika utulivu wa hali ya juu bila kuingilia mazungumzo aliyoyakuta alibaki kuinywa soda yake kwa hatua ndogo ndogo.
Lakini alikuwa anatetemeka, na hapa akagundua kuwa kuketi na watu wanaomzidi vyeo lilikuwa jambo lililomuathiri kupindukia.
Masiko yake yalikuwa wazi kusikiliza mazungumzo ya wawili aliowakuta pale.
Ilikuwa ni kuhusu kesi fulani iliyoonekana kuwasumbua vichwa, alitamani kuchangia hoja kidogo lakini akakumbuka kuwa wenzake walisahau ni lini mara ya mwisho kuwa katika cheo chake cha chini.
Akaufunga mdomo.
Lakini kichwani alikuwa anazungumza akijaribu kuwashauri wawili hawa ni kitu gani wanapaswa kufanya kuhusiana na kesi iliyokuwa mikononi mwao.
"Hawa watu nyota zao zote ni bure kabisa, sasa wao wanaona suluhisho ni kumkamata mke wa mshtakiwa. Je kama huyu bwana alimwoa huyu mwanamke ili kumfurahisha mama yake tu.. atajali nini? Mi binafsi sioni kama ni suluhuhisho...." akatokwa na tabasamu jepesi. Inspekta akaliona.
"Vipi Konstebo mbona unatabasamu, ni utamu wa haya mazungumzo ama..."
"Hapana afande, ni utamu wa hii soda, sijatumia siku nyingi sana..." Akajibu kwa utulivu wa hali ya juu.
"Unaitwa nani Konstebo..."
"Konstebo Nguzu, Martin Nguzu afande!"
"Unaitwa nani.." akauliza tena, Konstebo Nguzu akajitambulisha tena kwa ukakamavu.
"Sawa Konstebo Nguzu. Unaweza kutupisha kidogo sasa!" Inspekta alimwamuru, Konstebo Nguzu akajiondokea huku kichwani akiona ni jambo la fahari sana kujihusisha kimapenzi na Koplo Zubeda. Kwani kwa kufanya hivyo anayapooza maumivu yake yote ya kuamrishwa hovyo kila mara.
Amri alizoamini kuwa ni dharau!
Akiwa yu katika fukuto la ghadhabu, simu yake ya mkononi ikaitwa. Akalitazama jina na kupokea upesi.
Walau alikuwa amepigiwa na Koplo Zubeda, mwanamke aliyekuwa anamfariji na kumpa raha, hali iliyomfanya kuzisahau shida zake.
Wakazungumza kwa dakika kadhaa kujuliana hali kisha wakaagana huku wakipeana ahadai kedekede.
Kisha wakaingia kazinui, kila mmoja katika kituo chake.
Nguzu Magomeni na Koplo Zuu Chang'ombe polisi Temeke.
_______
SIMU YA JUMA (Kimbelembele) ilimweka, bado alikuwa kitandani maana hiyo ilikuwa ni siku yake ya mapumziko.
Koplo Mtani, jina lilisomeka. Akapokea upesi.
"Amakweli ukiwa unakitafuta kitu kwa dhati sana unaweza usikipate ila huwa kinajileta wakati umekata tamaa tayari." Alianzisha maongezi bila kusalimia.
"KUnani tena afande."
"Leo nimekutana na Nguzu wako. Tena tumeketi meza moja asubuhi kweupe pee! Kumbe ni ka konstebo, kapole halafu kakijana tu. " Alijibu kwa bashasha Koplo Mtani.
Juma akaketi kitako, na kuuliza maswali mfululizo. Koplo akayajibu yote kiufasaha na kumweleza kuwa siku inayofuata afike kituoni amwonyeshe mtu wake.
Damu ya muhariri wa gazeri la Siri Kali ikachemka, ubinafsi alioanza nao ukaendelea kumtawala hakumwambia mtu ni mpango gani anao dhidi ya Konstebo Martin Nguzu.
Kwanini amshirikishe mtu angali aliamini kuwa anenda kuandika makala pekee??
Amakweli maarifa mengi, mbele kiza!
Maarifa ya muhariri Juma Kihwele (Kimbelembele) hayakumfanya ang'amue kuwa si kila mtembezi hujua uelekeo.
Akatamani siku iliyotajwa ifike upesi.
Masaa akayaona hayasogei, hayawi hayawi mwezi ukaondoka zake baada ya kumaliza utawala wake wa muda, jua likatoka katika usingizi wake na kuisalimia dunia.
Akaianza siku na kauli dogoshi ya Koplo Mtani, 'Ni ka konstebo , kapole halafu kakijana tu'.
 
Hiiii nayo itaendeleaa mpaka mwisho au ndo Kama zileee kilaa siku tunatoa povu ziisheee hazielewekiii
 
Hii ni SEHEMU YA NNE

KIMBELEMBELE kilimfanya Juma Kihwele akose usingizi kabisa, alijigeuza huku mara ageuke kule. Alijisemesha kwa sauti ya chini na kucheka mwenyewe.
Mzigo wa kimbelembele kile ulikuwa mzito sana na dhahiri ulionekana kumwelemea. Akaamini kabisa bila kukigawa kidogo kile kimbelembele basi huenda pasingekucha.
Akamuita mkewe chumbani.
"Dear, nimeshindwa kulala mwenzako"
"Ushaanza! hapo unataka kuniambia matukio yenu ya kisiasa huko. Mi siyawezi." Alijibu mkewe huku akiketi.
"Bora ingekuwa habari za siasa, ya leo kubwa kuliko. Jamani mapenzi haya.." akasita akajikohoza kisha akaendelea.
"Unamfahamu Koplo Zubeda Msangi."
"Eeh! namfahamu si huyu mama wa hapo mtaa wa pili. Uliyeniambia wakati ule kuwa ni nyumba ndogo ya Inspekta nani vile."
"Eewala! Inspekta Kobo." Akahitimisha kwa madoido muhariri Juma Kihwele wa gazeti la SIRI KALI.
"Kafanya nini tena maana we nawe na kazi yako. Kuna habari kaandikwa ama..." Akahoji kwa utulivu akionekana kuwa bado hajavutiwa na simulizi hiyo ya mumewe.
"Bora angekuwa ameandikwa... Sikia ipo hivi, nilikuwa namfuatilia kijana mmoja hivi ni askari. Kuna vitu kadhaa nahitaji kujua kuhusu yeye. Huwezi amini katika kumfuatilia nikamwona anakuja hadi nyumbani kwa Koplo. Kama kawaida yangu nikitaka kujua jambo sichoki, nikaendelea kusubiri hadi walipotoka. Kwa kifupi Koplo Zubeda Msangi anajihusisha kimapenzi na hako kakijana kapole Konstebo Martin Nguzu ambaye nahitaji kufahamu mambo kadhaa kuhusu yeye." Akamaliza na kumtazama mkewe.
Bado hakuonekana kuvutika!
"Ubaya ni kwamba huyo sijui Konstebo sijui Inspekta wote siwajui vizuri. Nd'o nashindwa kuelewa unashindwa kulala kwa nini haswa. Kisa Zubeda anajihusisha na mtu mwingine amakiasa nini. Nifafanulie basi...."
"Mke wangu, katika kazi yetu ya uandishi kuna mambo mengi. Kuna baadhi ya fursa huja zenyewe machoni, hapa unabaki kupima mzani nani anakupa pesa nyingi. Je? ni bosi wako ofisini ama ni huyo muhusika wa hii habari..."
"Kwa hiyo unataka kuigeuza biashara hiyo habari? Na wewe ulipolala na yule dada wa mapokezi nani aligeuza biashara lile tukio lako ama wewe tu nd'o wayaona mabaya ya wenzako..... nilijua umeniitia mambo ya maana kweli mume wangu. Huo muda ningekuwa nimemfundisha Mariam kuhesabu moja hadi kumi na ameelewa kabisa. Yani we sijui upoje tu..." Akasimama na kutoka nje akiuacha mlango wazi.
Juma akabaki kimya kabisa, mkewe alikuwa amemgusa pabaya mno. Hakutaka kuikumbuka kabisa siku aliyofumaniwa na mkewe juu ya suala hilo la kujihusisha kimapenzi na msichana wa ofisini kwao. Ni kweli haikuandikwa popote, lakini hii haikuwa sababu nzito ya yeye kuachana na hili aliloligundua.
Ukimya huu haukumaanisha kuwa Juma aliamua kuachana na jambo hili. Akaona mtu sahihi wa kumshirikisha ni Koplo Mtani ambaye alimfahamu fika kuwa alikuwa ni mojawapo kati ya askari wasiokuwa waadilifu, rushwa ilikuwa rafiki yake wa karibu mno.
Kuisubiri asubuhi aliona ni kosa la jinai.
Akanyanyua simu na kumpigia kisha akamshirikisha hatua kwa hatua huku akiweka sharti la kutomtaja Inspekta anayejihusisha kimapenzi na Zubeda...
Licha ya kuwa mahiri sana katika kazi yake, lakini aliwapuuza wakongwe waliotangulia mbele ya haki waliponena kuwa hakuna siri ya watu wawili.
Juma Kimbelembele alikuwa ameisambaza na ipo kwa watu wawili naye akiwa wa tatu.
Kumshirikisha jambo lile Koplo Mtani kukampa ahueni, akajigeuza mara kadhaa akasinzia huku akiwaza kuigeuza habari hii mtaji. Aliamini fika kuwa hatakosa milioni kadhaa kibindoni ikiwa atazipanga karata zake vyema.
Wakati yeye anasinzia salama akiwa amejipunguzia uzito kiasi fulani katika mawazo yake. Upande mwingine nd'o kwanza palikuwa panakucha.
_____
MAPENZI RAHA, nilikuelezeni awali. Lakini huwa raha iso' kifani wakutanapo wawili wanaopendana kwa dhati. Halafu wasipishane sana umri na mitazamo katika uwanja huo wa mahusiano ya kimapenzi.
Muunganiko kati ya Konstebo Nguzu pamoja na Koplo Zuu ulikuwa wa aina yake, waswahili wanasema upele ulikuwa umepata wakunaji.
Siku hii hakuingia kazini mapema, aliwasiliana na mwenzake aliyekuwa na askari mwenzake aweze kumwakilisha katika majukumu yake hadi majira ya saa sita mchana.
Ikawa hivyo!
Nguzu akaamkia nyumbani kwa Zuu, wawili hawa walioshibana wakaanzia kupata kifungua kinywa kilichoandaliwa na Zuu mwenyewe.
Walikula kisha wakalishana huku wakisifiana mambo kadha wa kadha. Baada ya kula wakashushia maji ya matunda.
Kilichofuata ni Zuu kumshika mkono na kumkongoja chumbani Konstebo Nguzu, haikuwa mara yao ya kwanza kuingia katika chumba hiki. Awali Nguzu alikuwa akiogopa sana kufumaniwa lakini mazoea yakajenga kibanda cha kudumu katika mwili wake, kisha kwa sifa mazoea yakajibadili jina yakawa tabia.
Chumbani wakagida mvinyo wa bei ghali, kisha wakakubaliana waende kuogeshana bafuni.
Simu ya Nguzu ikaita ikawakatili uhondo wao.
"Jamali ananipigia, ngoja nimsikilize." Alimweleza Zuu kabla hajapokea ile simu.
Zuu akaelewa.
Baada ya kuongea kwa sekunde chache akakata simu, taharuki kiasi ikamvaa usoni.
"Nahitajika kituoni muda huu, mkuu wa kituo ananihitaji ni amri." alizungumza konstebo Nguzu huku akiwa amemkazia macho ya matamanio koplo Zubeda Msangi (Zuu).
Uzuri Zuu naye alikuwa ni askari alijua vyema maana ya amri. Kwa unyonge akakubali matokeo.
Akamuaga Nguzu kwa kumbusu katika papi za midomo yake. Machozi yakamtoka Zuu na asijue ni kwa nini yanamtoka wakati Nguzu akimuaga.
Wakakubaliana kuonana jioni ya siku hiyo wamalizie walichopanga kufanya asubuhi hiyo.
Wakabusiana tena kwa mara ya pili.
Nguzu akatoweka, uzuri alikuwa amebeba sare zake za kazi na alikuwa amezivaa tayari.
Akachukua usafiri wa pikipiki moja kwa moja kuelekea kituoni.

_____
UKIMWONA mtu mzima yu katika kilio pasi na sababu za msingi basi ana matatizo ya ziada katika akili zake, ama la ana tabia ya kulialia tangu utoto wake.
Lakini ukimwona mwanaume aliyekabiliana na majambazi kwa kutumia silaha, akawasambaratimba licha ya kupigwa risasi kadhaa zilizouvunja mguu wake. Ukimkuta huyu analia peke yake, kaa mbali kidogo kwanza uumize kichwa, si kilio cha kawaida asilani.
Inspekta Kobo alikuwa analia kama mtoto mdogo ofisini kwake.
Alikuwa na miaka arobaini na nane, heshima ya kuwa inspekta pekee haikutosha kuthamini mchango wake katika jeshi la polisi. Wakati wa ujana wake alitambulika kwa jina la Vandame kwa jinsi alivyokuwa akiyapenda mapambano, kwake tukio la ujambazi likitokea nd'o alikuwa anafurahi kwenda kukabiliana nao. Tena alipenda sana wakiwa na silaha.
Na hapo alikuwa na cheo cha chini bado, juhudi zake zikampandisha juu na hatimaye anazeeka akiwa Inspekta.
Haikutosha lakini walau.
Mlango wake uligongwa, akajifuta machozi upesi na kisha akamkaribisha aliyehitaji kuingia.
Mlango ukafunguliwa akausikia mshindo wa ukakamavu kisha ikafuata saluti.
Akaipokea kinyonge sana!
"Konstebo Martin, Martin Nguzu afande nimeitikia wito wako afande!" Kikakamavu mgeni akajitambulisha.
"Keti" akamsihi.
Nguzu akajitua katika kiti kilichokuwa jirani yake.
"Una umri gani konstebo?"
"Miaka ishirini na saba afande!"
"Ninaitwa Mathew Koboko, ama inspekta Kobo. Naamini hatujawahi kuonana, zaidi ya yote mimi sijawahi kukuona." akatulia akamtazama Nguzu. Nguzu akatikisa kichwa kukubali.
"Nina miaka arobaini na nane sasa, umri umenitupa mkono, siko imara sana nilivunjika mguu nikiwa nalitumikia jeshi, mkono wangu wa kuume pia unatetemeka mara kwa mara kwa sababu ya kutumia sana bunduki, mgongo wangu sio mzima sana nikiketisana naumia, nikitembea sana naumia. Akili yangu pekee nd'o ipo salama. Salama kwa asilimia zote" Akatulia na kumtazama Nguzu usoni. Kisha akamwomba radhi kabla hajapenga kamasi nyepesi zilizokuwa zikimwandama.
"Umeoa Nguzu?"
"Sijaona afande!"
"Mimi nimeoa mtoto wangu wa kwanza unamzidi miaka michache lakini ana mwili mkubwa zaidi yako." Akatulia na kulazimisha tabasamu kisha akaendelea tena.
"Nimekuita hapa ili nizungumze na wewe. Mimi kama Kobo na wewe kama Nguzu tena ni sawa na kijana wangu, lakini hapa tuzungumze kama wanaume wastaarabu walioketi baa kabla pombe hazijachanganya vichwa vyao. Najua wewe umekunywa pombe lakini sidhani kama umepitisha kiasi..."
"Nipo timamu afande!"
"Lakini umekunywa kidogo sivyo."
"Hapana afande!" Akakanusha Nguzu.
Inspekta Kobo akasimama taratibu, akayaendea maboksi kadhaa yaliyokuwa pale ofisini, akapekua boksi moja na kutoa chupa akaiweka mbele ya Nguzu.
"Nimekusamehe kwa kunidanganya kwa mara ya kwanza, usinidanganye tena kwa sababu hivi vyuma katika mguu wangu havinizuii kuurusha ukakufikia." akaiacha ile chupa na kurejea katika kiti chake.
"Haukuishia kunywa pombe pekee, Martin Nguzu umejipulizia marashi niliyoyanunua jijini Paris Ufaransa. Kwa kifupi umetoka nyumbani kwangu bwana mdogo. Nyumba inayonipa mimi faraja...." Akasita na kumwacha Nguzu apagawe kwanza.
Hakika alipagawa, hakuamini kuwa siku yaikeinaanza hivyo. Akatambua kuwa yupo ana kwa ana na mume mwenzake.
"Nilikwambia nimeoa Nguzu, lakini nipo salama zaidi nikiwa na Zubeda. Simtumii kwa sababu ya pote nilipomtoa, najua hajakwambia kiundani ni wapi nimemtoa... hawezi kukueleza kuwa nilimkutaanajiuza nikamnunua na hapo nikawa nimeyanunua maisha yake jumlajumla. Alikuwa amefyatuka akili zake na alikuwa amekata tamaa, nilitumia muda na uwekezaji mkubwa sana kumkomboa kutoka janga lile. Narudia tena ninaye mke ninayempenda hata kama yeye hanipendi, lakini kwa Zubeda ni sehemu ninayokuwa salama zaidi.
Siwezi kukulaumu eti umeniingilia katika anga zangu, kama ningekulaumu hata usingeiona sura yangu bali ni mimi ningeiona sura yako baada ya wewe kukatwa kichwa na vijana wangu. Nimeona niwe mstaarabu kidogo, maana na huu uzee nikiwa mkaidi haina maana ya kuwa mzee sasa.
Nguzu, imetosha kuingia nyumbani kwangu, niache basi nisije kufa na magonjwa ya moyo wakati risasi hazikuweza kuniua. Ujue nimelia sana leo hadi nimejishangaa, nimetambua wazi kuwa ninampenda sana Zubeda. Nawe ninakuomba uwe balozi wangu wa kweli, mtafute Zubeda mwambie mzee Kobo anampenda sana na sijawahi kumuwazia mabaya hata siku moja. Msihi haswa kuwa asinirudishe katikaujana wangu kwa namna yoyote ile. Unaweza kuondoka Konstebo Nguzu Martin Nguzu...." Alimaliza Inspekta Kobo kinyonge.
Nguzu akasimama akiwa anatetemeka sana, jasho likimtoka.
"Nenda nyumbani ukapumzike ukitoka humu ndani, nimekupatia mimi ruhusa hii Nguzu."
Nguzu akasimama huku akihema juu juu akapiga saluti na kutoweka pale ndani. Inspekta akamsindikiza kwa macho hadi alipotoweka.
______
Simu yake ilimgutusha kutoka katika dimbwi la mawazo. Ilikuwa ni namba ya Zubeda. Akatambua kuwa tayari mambo yamezidi kuharibika.
Akapokea huku akiwa anatetemeka sana, moyoni mwake akitamani hii iwe ndoto ya mchana.
"Laazizi! ukwapi?" Sauti tulivu kabisa ikahoji.
"Nyumbani vipi kwani?"
"Kuna tatizo Nguzu... tena linaweza kuwa tatizo kubwa sana tukilipuuzia."
"Ni kuhusu inspekta?" Nguzu akauliza.
"Si bora kingekuwa kile kibabu ninakiweza kile. Kuna mtu anaitwa Juma Kihwele sijui unamfahamu?"
"Hapana jina hilo ni geni kwangu Zuu. Kuna nini? na ni nani huyu?"
"Amenipigia simu anasema yeye ni muhariri na anahitaji tuonane kwa mazungumzo juu ya mimi kujihusisha kimapenzi na Inspekta halafu na sasa nipo na wewe. Sijui ameyatoa wapi haya maneno, Nguzu atatuharibia huyu wakati ambao sio muafaka hata kidogo. Nimekupigia maana hili linatuhusu mimi na wewe, nataka tumuwahi." Aakaweka kituo. Nguzu akapagawa, wakati anawaza kuwa ni jambo juu ya inspekta linakuja jingine khusu mwandishi.
"Nakusikiliza wewe, tunamuwahi vipi sasa?" akauliza kinyonge mno.
"Njoo nyumbani usiku tupange, kama saa tatu hivi."
"Hapana Zuu sitaweza kuja hapo usiku wa leo. Huoni kama tutazidi kulikuza tatizo... kwanini tusikutane sehemu ambayo sio hapo kwako?"
"Sawa panga wewe halafu utanifahamisha basi..." Akamaliza na kukata simu.
Nguzu akahisi kuugua, kama sio homa basi ni Malaria kali kupindukia.
Utamu utamu sasa ukageuka uchungu!
Hata kabla hajamweleza Zubeda yaliyojiri katika ofisi ya Inspekta Kobo yanatokea haya mengine ghafla!
Akapanga kukabiliana na hili jambo kabla halijakomaa, akasimama imara akapiga saluti na kujiapiza kuwa hatalala tena na kulialia kama mtoto badala yake atapambana kiume.
Hakujua kuwa wakati yeye akiamua kusimama,kuna ambao walikuwa wakikimbia mbio kali kwa nia ya kumzamisha katika shimo lenye kiza kinene.
 
Hii ni SEHEMU YA TANO

ALIJARIBU kujiaminisha kuwa huenda amesikia vibaya, akazidi kujikunja kitandani ili asinzie vizuri. Lakini mlango ulipiga kelele tena, kuna mtu alikuwa anaugonga.
Akiwa na mawenge ya usingizi aliufikia mlango na kuufungua bila kuuliza ni nani alikuwa anahitaji kuingia. Hakuwa katika fahamu zake taslimu.
"Nani?" aliuliza baada ya kuwa ameufungua mlango na kukutana na kiza kinene.
Badala ya kujibiwa akasukumwa ndani, kisha tochi kali ikayamulika macho yake akashindwa kutambua kunani mbele yake.
Akajaribu kutokwa na pigo la 'Karate' aliyojifunza akiwa kambini lakini akaishia kupiga ukuta na kutokwa na ukelele wa maumivu.
Mwanga ule ukapotea na kisha taa ya chumbani kwake ikawashwa. Akayapikicha macho yake na hatimaye aliweza kuona ni nani alikuwa mgeni wake asiyetoa taarifa.
Mkojo ukatoka mbio katika kibofu usiangalie kuwa pale si maliwatoni ama msalani. Ulipofika karibu na mlango wa kutokea ukamstahi.
Haukutoka!
"Nguzu, mbona unawahi sana kulala." Ilikuwa sauti tulivu kabisa ya Inspekta Kobo ndani ya nyumba anayoishi Konstebo Nguzu.
Konstebo Nguzu aliishiwa hamu zote, akabaki katika hali isiyoeleweka.
Inspekta Kobo akaketi. Nguzu akajilazimisha akapiga saluti.
"Nguzu, ni masaa mangapi yamepita tangu tuzungumze?" aliuliza kwa utulivu uleule. Kabla Nguzu hajajibu yeye aliendelea.
"Umenogewa na mali yangu ama? Yaani kweli nimekuita kwa upole na ustaarabu wa hali ya juu kiasi kile lakini kumbe usiku huu umepanga tena kukutanana Zubeda! Mbona unanifanyia hivyo konstebo...." Alizungumza kwa kulalamika Inspekta.
Nguzu kimya!
"Naomba unitazame machoni wakati unajibu swali hili." Akasita kisha akaendelea baada ya NGuzu kumtazama.
"Unampenda Zubeda kwa dhati ya moyo ama unampenda kwa sababu ni yule mwanamke ambaye hawezi kukulilia shida badala yake wewe nd'o waweza kumlilia shida?" Swali zito likamponyoka inspekta Kobo.
Nguzu akabaki kimya tena huku akionekana wazi kuzidiwa na uzito wa swali lile na pia alikuwa hajaizoea hali ya inspekta kuwa ndani ya nyumba yake.
"Martine Nguzu kwa kumbukumbu zako unafahamu inachukua muda gani kupanda kutoka cheo kimoja kwenda kingine katika jeshi la polisi?"
"Miaka mitatu.." Sasa alijibu huku amani ikiwa imetoweka.
"Unajua kuwa yaweza kukugharimu miaka walau kumi na nane kufikia cheo changu.... lakini mimi sikutumia miaka kumi na nane kuwa inspekta, nilifanya makubwa sana... nilikuwa nina roho mbaya mno na nilikuwa nikiikamata bunduki nakuwa shetani kamili." akaupitisha mkono wake na kuichomoa bastola yake kutoka mahali alipokuwa ameihifadhi.
Sasa Martin Nguzu aliweza kuzungumza hata ambayo hajaulizwa. Mara aseme Zubeda ndiye alimlaghai mara aseme hatarudia tena...
"Sina maana mbaya kuiweka bastola hii katika mkono wangu, ninajaribu kukueleza na unielewe vyema. Ningekuwa nimekuvamia hapa kwako kwa sababu unahusika na uuzaji wa madawa ya kulevya ama ujambazi, muda huu mguu wako mmoja ungekuwa unasubiri muda tu ukakatwe. Lakini sipo hapa kupambana na wewe Nguzu nipo hapa kukusihi tu, kama inawezekana naomba uniachie Zubeda wangu, nasisitiza ninajaribu kukusihi tu na wala sio kukulazimisha. Niachie huyu binti, amepitia mengi magumu nimejaribu kuitafuta furaha yake walau kidogo tu, nimewaumizawengi kwa kutumia bunduki sitaki kuumiza tena kwa kutumia moyo." akasita na kumwomba Martin maji ya kunywa, bahati nzuri hayakuwa mbali.
"Konstebo mfano mimi najitoa katika maisha ya Zubeda nakuachia wewe, je? utaweza kumjazia mafuta ya gari lake? utaweza kumnunulia nguo za gharama kiasi kile, utaweza kumbadilishia samani za ndani ya nyumba yake? utaweza kuwalipa wafanyakazi wake? Utaweza Nguzu?. Kama jibu ni hapana basi nikikuachia Zubeda kuna watu watakuja kukusaidia majukumu nawe utajikuta unaumia moyo huku ukilia kama mtoto.
Kwanini nikuache uyapitie hayo sasa.... kwanini nikuone upo katika njia mbovu nisikueleze ukweli. Nguzu kama Zubeda anakueleza ukweli, atakuwa amekueleza kuwa ninaenda kwake mara ngapi na ninashiriki naye tendo mara ngapi..... nadhani huwa anahisi mimi nimezeeka, ila sijazeeka Nguzu nipo imara mno tatizo ni moja tu, sio ngono iliyoniweka pale..... sio ngono Nguzu" Akashindwa kuendelea kuzungumza, chozi la mtu mzima likaiangukia sakafu ya Nguzu.
Huruma kali ikamshika Nguzu, akataka kusema neno lakini Inspekta akamzuia na hapo akaaga na kuondoka zake bila kuhitaji hitimisho.
Huu ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa Nguzu, akaitazama saa yake tayari ilikuwa saa nne kasoro dakika chache usiku.
_____
JUMA KIHWELE alikuwa nje akipunga upepo huku akingojea kwa hamu simu kutoka kwa Koplo Zubeda ili waweze kumaliza zoezi lao. Alikuwa nje kwa maksudi makubwa, hakutaka mkewe ajue kuwa ameendelea na ule mpango wa kuitumia ile habari ya Zuu kujihusisha na wanaume wawili kujiingizia kipato jambo ambalo mkewe hakuwa ameliunga mkono kabisa.
Kila mara alitazama simu yake kama kuna ujumbe wowote kutoka kwa Zuu, lakini hadi majira ya saa tatu usiku bado hali ilikuwa ya ukimya. Moyo wa subira ukaanza kuingiwa uchovu akafikiria kumpigia simu na kumchimba mkwara kuwa iwapo hatafanikisha kuonana kwao basi asimlaumu pakikucha.
Akiwa katika kusubiri kule akaliona gari likipaki eneo fulani jirani na upeowa macho yake kisha akashuka mtu ambaye anamfahamu vyema.
Kimbelembele kikachukua nafasi yake. Akataka kuhakikisha kuwa anamfahamu vipi mtu yule.
Inspekta! akastaajabu.
"Jamani si inspekta Kobo huyu." akajiseme huku akisubiri kuona anaenda uelekeo gani, alipopita naye akafuata nyuma. Moyoni alijua wazi kuwa Zuu atakuwa amemweleza kila kitu inspekta, ile mipango yake ya kuvuna chochote kitu akaiona inapoteza uelekeo.
Macho yake yaliyolizoea giza yakamwona inspekta akienda moja kwa moja nyumbani kwa Martin Nguzu.
"Wanaenda kukubaliana nini hawa viumbe eeh!" alijiuliza hukiu akitamani kujisogeza hadi jirani na ile nyumba aweze kuvuna mawili matatu. Lakini alihofia kufumaniwa kisha kudhalilishwa.
Akarejea ndani ya nyumba yake, alipofika nakuiona kamera yake akapata wazo jipya.
"Hawa wawili wanajihusisha na mwanamke mmoja, kwa namna yoyote ile kuna namna fulani ya kutoelewana itajitokeza. Na kama wakipigana basi nitanasa picha nyingine muhimu kwa ajiri ya gazetini." Wazo hili jipya likamfanya atoke nje na kamera yake akaenda hadi chini ya mti akaketi huku akiiona vyema nyumba ya Nguzu.
Kiupepo chenye ubaridi wa wastani kikaungana na mawazo tele ya Juma Kihwele na kuunda usingizi.
Jumaakajikutaamesinzia akiwa eneo lile.
Alikuja kushtuka baada ya kusikia makelele... akakurupuka akidhani kuna wizi umetokea mahali.
Macho yake yakakutana na moshi ukifuka katika nyumba ya Nguzu.
Nyumba ilikuwa inatetekea katika namna ya kutisha sana. Moshi mweusi tii uliichafua anga.
Mungu wangu! akahamaki Juma, kisha akaiweka sawa kamera yake na kwenda kupiga picha kadhaa jinsi tukio lilivyokuwa likiendelea.
Moyo wake ulikuwa unadunda sana. aliulaumu usingizi uliompitia chini ya mti na kusababisha asiweze kuona tukio lilitokea katika mazingira ya namna gani.
Akatimua mbio mpaka pale lilipokuwa limeegeshwa gari alilokuja nalo Inspekta. Hapakuwa na kitu.
"Inspekta amemchomea ndani Nguzu?" alijiuliza Juma huku akiwa na kimuhemuhe kipya kuliko kile cha awali cha kugundua kuwa wawili hawa wanajihusishakimapenzi na mwanamke mmoja.
Magari ya zimamoto hayakufika usiku ule... nyumba ikateketea yote na kusalia majivu.
Juma alirejea nyumbani kwake akiwa hayuko sawa kabisa, alimfikiria mkewe na kutaka kumshirikisha juu ya kitu kilichokuwa kimetokea lakini alikumbuka majibu yake wakati anataka kufuatilia mkasa ule yalivyokuwa. Akasita kumshirikisha, hili la sasa lilikuwa zito mno na lingeweza kumtia hatiani angefanya kuliropoka.
"Kwa hiyo kulikuwa na watu ndani?" Mkewe alimuuliza juu ya hiyo nyumba iliyoungua, kwani tayari alikuwa amesikia kwa majirani na alijua wazi mumewe hawezi kupitwa na habari ile.
"Yaani hapa sina moja wala mbili." alijibu kwa ufupi. Na hakutaka kuzungumzia tena jambo lile akaingia bafuni kuoga kisha akalala.
Kitu cha kwanza asubuhi ni kujua kama habari ile tayari imepata mwanga.
Naam! Ikatangazwa kuwa nyumba imeungua kwa chanzo ambacho bado hakijajulikana na inasadikika kuwa askari mmoja amepoteza maisha akiwa ndani ya nyumba hiyo.
Nambari ya askari yule ikatajwa na kisha jina likatambuliwa baadaye.
Konstebo Nguzu alikuwa katikati ya moto ule na alikuwa ameangamia.
_____
Taarifa hii ya habari ikasikilizwa na masikio ya Koplo Zubeda Msangi aliyekuwa anaendesha gari lake kuelekea nyumbani kwa Nguzu ambaye alikuwa hapatikani katika simu ilihali walipanga kuonana usiku ule.
Zubeda akiwa amevimba kwa hasira alikuwa anaenda kumlaumu waziwazi Nguzu kuwa si mtu anayejali hata chembe.
Kulisikia jina lake likitajwa kuwa hayupo duniani tena, Zubeda akajikuta akikanyaga pedeli ya kuongezea mwendo wa gari badala ya kupunguza mwendo na mara akajikuta akikwepa kitu asichokijua gari ikatumbukia mtaroni, Zubeda ambaye hakuufunga mkanda wake akajibamiza katika kioo na kupoteza fahamu palepale huku damu nyingi ikimtiririka.
Kwa sababu ilikuwa asubuhi, askari waliokuwa barabarani waliwahi sana kumtambua koplo Zubeda ambaye alikuwa ndani ya sare zake za kazi. Simu za upepo zikapigwa upesi kutoa taarifa ile.
 
HII NI SEHEMU YA SITA

KILIANZA kitanda kumsaliti, kila mtindo aliojaribu kukilalia ukagoma kumburudisha. Akastaajabu kitanda chake mwenyewe lakini amtii. Akasimama wima na kukitazama kwa sekunde kadhaa jinsi kilivyokosa nidhamu.
Akaondoka bila kukiaga na kuelekea sebuleni,huko akajibwaga katika kochi kubwa lililokuwa sebuleni, hili likampokea vyema na ule mbonyeo ukamfurahisha.
Heri yako bado unanitii! akajisemea, huku akiukunja mguu wake na kujaribu kuvuta taswira ya kitu kilichomfanya ashtuke usiku wa manane na kuanza kubabaika.
Moshi mnene! hiki nd'o kitu kilichokuwa kikitishia afya ya akili yake kwa wakati ule.
Akainyanyua simu yake na kujaribu kupiga katika nambari alizokuwa amepiga awali na hazikuwa zikipatikana.
"Ni kweli Sule anavuta bangi tena sana tu, lakini sidhani kama bangi yake inaweza kumfanya akafanya upuuzi mkubwa namna hii..." Akajisemea huku akiketi.
Alipoketi na kuwa kimya kwa muda kidogo akakumbwa na kitu ambacho kilimfanya ashindwe kuketi bali kusimama wima kabisa.
Kuna vitu viwili vilikivamia kichwa chake, ulikuwa ni mfano wa picha ambazo zilikuwa gizani na sasa akabaini kuwa aliziona lakini pasi na uhakika.
Picha ya kwanza ilikuwa ni mtu chini ya mti.
Ni nani yule? akajiuliza huku akijilazimisha kuing'arisha picha ile katika kumbukumbu zake.
Haikung'aa!
Picha ya pili ni ya mwanaume akizungumza, na haikuwa ngeni sauti ile katika masikio yake. Haikuwa sauti aliyokuwa akiishikia mara kwa mara kama ilivyo sauti ya mkewe ambaye ni daktari. Hii ilikuwa sauti ambayo aliwahi kuisikia asijue mwaka wala tarehe, hakukaribia kukumbuka hata mahali alipowahi kuisikia.
Ila aliwahi kuisikia.
Baada ya miaka mingi ya mapambano na kisha kuamua kutulia tuli baada ya kuvunjika mguu wake, akabaki katika mapambano ya kalamu na karatasi huku akiwa yu katika chumba tulivu chenye urafiki wa dhati na kiyoyozi.
Kwa jicho lake pevu kabisa Inspekta Kobo akajiona anaungiza mguu wake mbovu katika mapambano mapya.
Licha ya mkewe kuwa daktari inspekta alipendasana kumshirikisha masuala yake pindi yanapomwendea kombo.
Na hili lilikuwa limemnyima usingizi, akabofya simu yake na kumpigia mwenza wake, simu ikaita lakini haikupokelewa.
"Yupo chumba cha upasuaji huyu..." alijisea na hakujaribu tena kupiga.
Akafikiria kumpigia mpenzi wake wa siri, koplo Zubeda, akajiuliza mara mbilimbili kisha akaikumbuka ile kauli mbiu ya 'ukivuka mipaka basi siri mweleze mkeo unayempenda kwa dhati lakini kamwe usitapike siri zako mbele ya hawara. HAWARA hana dhamana...
Inspekta akakiri kuwa anampenda sana Zubeda lakini tahadhari lilikuwa jambo la muhimu sana.
Akarejea katika kochi akaketi.
"Nguzu atakuwa amekufa ama? na kama hajafa itakuwaje upande wangu..." alijiuliza Inspekta asipate wa kumjibu.
Watoto wake walikuwa wanaelea katika dimbwi la usingizi mzito.
Mawazo juu ya mawazo hatimaye usingizi ukamwonea imani, ukamsomba na kumuunganisha katika dimbwi walilokuwqa wakisafiri watoto wake kwa wakati ule.
Dimbwi la usingizi.....
Asubuhi akaamka akijisikia ahueni na akijaribu kujisahaulisha kuhusu kiza kilichojiri usiku uliopita.
Akiwa anafanya jitihada za kuyafuta haya akaipokea taarifa juu ya kuchomwa kwa nyumba aliyokuwa akiishi konstebo Nguzu, kilichosalimika ni nguo zake zilizokuwa zimeanikwa katika kamba iliyokuwa mbali kidogo na nyumba.
Si kichwa wala fuvu lake kilichosalia katika moto ule wa kutisha.
Inspekta akazishusha pumzi zake, akaanza kutembea huku na kule katika himaya ya nyumba yake. Akaunda mfano wa mzazi mdogo katika kichwa chake, akahisi uhai wa Nguzu ungeweza kuwa hatari sana kwake.
Hatari kwa sababu alikuwa na ubaya naye nafsi ya Kobo ikakiri kuwa ilikuwa imechefukwa haswa kutokana na uwepo wa Nguzu.
Kwa hatua hii ya kuzimika moja kwa moja akahisi kuwa itakuwa ni nafuu kubwa kama mtu aliyeingiliwa na mchanga jichoni akifanikiwa kuutoa na kisha jicho lake kubaki huru.
Lakini uhai huohuoungeweza kumweka matatani kwa sababu Nguzu angehojiwa juu ya nani amehusika katika moto ule, angwataja watu ambao ana ubaya nao, kwa nini asilitaje jina la inspekta Kobo kama jina la muhimu zaidi!!
Ni heri amezimika. Alihitimisha Inspekta Kobo.
Akahamia upande wa pili wa mzani, Nguzu amekufa vipi?
Je? ninahusika? akajiuliza, kisha akachukua simu na kupiga tena nambari aliyokuwa akihangaika nayo usiku uliopita.
Haikuwa inapatikana...
Hapo akarukia sehemu ya pili, ni nani alikuwa chini ya mti, na ni sauti ya nani aliisikia upande mwingine...
Haya yalikuwa maswali magumu zaidi. Maswali yaliyosababisha aamue kuwa upande wa yeyote yule ambaye amefurahia kifo cha Konstebo Nguzu.
Akaufunga ukurasa wa mawazo mazito juu ya ni nini atafanya ili Zubeda atulie na kuachana na Nguzu. Sasa aliwaza ni kitu gani amfanyie asije akazama kwa mwanaume mwingine kama ilivyokuwa kwa Nguzu.
Akaamua kumfanyia ugeni wa ghafla utakaotawaliwa na upya mkubwa sana kutoka kwake...
Akiwa mwenye kubwa tabasamu aliingia maliwatoni kujisafi mwili wake.
Kisha akalivamia jokofu na kutoa maji ya matunda. Akaigida kwa fujo glasi ya kwanza mpaka ikamalizika. Kisha glasi ya pili akainywa taratibu huku akiwa anaipanga ratiba yake kwa siku hiyo.
Simu yake ya mkononi ikatoa mlio kumaanisha kuwa kuna ujumbe mpya umeingia.
Akaifungua upesi kwa sababu simu ilikuwa kiganjani kwake.
"Bosi, shemeji kapata ajali yuko Temeke hospitali. Amekula mzinga na Suzuki yake"
Ujumbe ule wa maandishi ukawa kama ulioambatana na umeme mkali kuzidi kipimo, ukautekenya mkono wa inspekta glasi ikamtoka mkononi, kisha akaanguka chini kama mzigo baada ya miguu kuelemewa.
Mpasuko wa glasi na kishindo cha mwili mzito wa inspekta vikawashtua watoto waliokuwa wameamka tayari.
Balaa jingine likaibuka.
Walipiga mayowe huku wakiiitana kwa kusisitiza kuwa baba yao angali katika tatizo kubwa.
Inspekta Kobo alijaribu kusimama ili alete amani kwa watoto wake lakini akabaini kuwa hawezi kusimama, ule mguu wake ulioungwa kwa vyuma ulikuwa umeyumba.
Tusi pekee katika lugha ya kiitaliano alilolifahamu likamponyoka huku akiipigapiga sakafu.
Kelele zilivyozidi akatoa onyo, akawafokea watoto wake huku akijinadi zaidi ya mara mbili kuwa yeye ni mwanajeshi kamili wasihamanike.
Maneno ya shujaa huyu yakatuliza munkari, akafikishwa hospitali katika hali ya utulivu kabisa bila papara za kuwafanya majirani watambue kuwa inspekta Kobo amekumbwa na balaa.
_______
MAJIRA YA saa nne usiku kiwiliwili cha kiume kikiwa katika koti kubwa lililoungana na kofia yake kilikuwa kikikatiza katika wodi ya wanawake kwa mwendo wa haraka huku kichwa chake kila mara kikinyanyuka juu kutazama uelekeo wa mbele na kisha kuinama tena.
Safari ile iliyojaa umakini iliishia katika chumba kilichojitenga mbali na wodi za wanawake.
Watu wawili walimpokea kimyakimya na kumwingiza chumbani, akamwona mgonjwa wake.
"Nakupenda sana Zubeda." Lilikuwa neno la kwanza kumnong'oneza yule mgonjwa kisha akainama na kumbusu.
Zubeda akajaribu kutabasamu kidogo.
Inspekta Kobo alizungumza machache na Zubeda kisha akamweleza kuwa siku inayofuata atakuwa na muda mrefu zaidi wa kuzungumza mengi.
Akaaga na kuondoka!
Alitumia usafiri wa pikipiki, upesi akarejea nyumbani kwani kwa ratiba ya mkewe ilivyokuwa siku hiyo alipaswa kuwa nyumbani majira ya saa tano usiku.
Inspekta aliwasili baada ya dakika chache tangu saa tano ilipotimia. Hofu ilimtawala kidogo kwa sababu ya maswali ambayo angepokea kutoka kwa mkewe lakini pia angelaumiwa sana kwa kuanza mizunguko mapema kiasi hicho badala ya kupumzika.
Hakumkuta mkewe nyumbani, akaanza kujilaumu sana kwa kuhofia ujio wa mkewe, huenda angeweza kuendelea kuzungumza na Zubeda kwa muda mrefu zaidi.
Wakati akiwaza haya, Daktari Kobo ambaye ni mkewe alikuwa katika chumba cha mgonjwa akijaribu kuzungumza naye kwa lugha ya upole kabisa, ni kawaida ya madaktari kuitumia lugha inayoleta tumaini kwa mgonjwa.
Tofauti na ulivyokuwa utaratibu wa siku zote aliouzoea mgonjwa yule alistaajabu kuona mlango wa chumba kile alicholazwa unafungwa kwa ndani na yule daktari mwanamke.
Kisha mwanamama yule akakisogelea kitanda na kumjulia hali.
Mapigo ya moyo ya yule mgonjwa yakaanza kwenda mbio kupita kawaida.
"Bila shaka sina haja ya kujitambulisha.... na hakika sijaja kwa ubaya humu ndani. Unaitwa Zubeda na unajihusisha kimapenzi na mume wangu wa ndoa Inspekta Kobo." Akaweka kituo kisha akamwinamia mgonjwa yule.
"Nimekusudia kuzungumza na wewe kwanza kwa sababu wewe ni mwanamke mwenzangu, unafahamu nini kuhusu kifo cha Konstebo Nguzu?" Swali lile lilikuwa kama upinde wenye moto mkali mbele yake. Likamchoma haswa Zubeda.
"Sijui lolote." alijibu kwa ufupi mno.
"Zubeda, narudia tena, sipo hapa kwa sababu ya wivu wa kimapenzi, nina umri wa miaka thelathini na tisa sasa, nimeishi na inspekta kwa zaidi ya miaka kumi na nane. Nilikuwa ninao wivu zamani sio sasa.... ninawapenda sana watoto wangu sitaki wakose huduma zababa yao na huenda katika hili ni msaada pia kwako.Kuna taarifa ambayo haijazagaa kuwa wewe na inspekta mmeshirikiana kuichoma nyumba ya Nguzu huku yeye akiwa ndani na kusababisha mauti yake. Hili nd'o lililonileta hapa..... ungekuwa ni wivu wa mapenzi ningeagiza wakuchome sindano moja tu na siku inayofuata ungehamishiwa mochwari tayari kwa maziko, na mwili wako unmgeoza licha ya kupigwa na ubaridi wa mochwari. Sina nia mbaya... naomba unipe ushirikiano. Wewe na inspekta mpo matatani. Kumbuka kuwa IGP hapatani na inspekta Kobo sana, atawanyoosha katika hili. Niambie kama mmehusika ili tuweke kando masuala ya mapenzi kisha tuketi pamoja na kuitafuta suluhu kabla vithibitisho havijatapakaa."
Maneno ya dokta Kobo yalikuwa mazito mno, Zubeda hakuamini kile alichokisikia, hakuwahi kuzungumza na inspekta Kobo hata siku moja juu ya mpango huu wa kinyama kiasi hicho.
"Ukiachana na hiyo njama, sijawahi hata siku moja kuzungumza na inspekta juu ya konstebo Nguzu."
"Sema hayati..." Dokta alimrekebisha.
Marekebisho haya yakamuumiza Zubeda katika moyo wake, alikuwa amemzoea mno Martin Nguzu. Sasa anaambiwa amepoteza maisha.
"Inspekta Kobo nd'o mtu wa mwisho kuingia nyumbani kwa marehemu kabla moto haujaimeza nyumba ile. Hivi unadhani wakuijumlisha na tatizo la wewe kuwa na wapenzi wawili kwa waikati mmoja kuna mtu atahitaji ushahidi wa ziada. Zubeda utapotea vibaya mno, mimi sijui sana sheria lakini kama nikichaguliwa kutoa hukumu katika hili basi nikiwapeleka gerezani miaka michache kabisa ni thelathini thelathini. Wauaji wakubwa nyinyi.." Jazba ikataka kuchukua nafasi akatulia kwa muda kujizuia na hali ile.
"Shangazi, sijui lolote kuhusu huu mpango unaousema, sijawahi kuzungumza na Inspekta juu ya lolote kuhusu Nguzu. Hii ni kweli ya moyo wangu..."
"Sawa kama haujui. Mimi naondoka..." alizungumza doktahuku akiyanyanyua mabega yake juu. Akauendea mlango na kutoweka.....
_______
LILIANZA kuwa saa moja, kisha likafuata la pili yalipofika matatu subira ikafikia kikomo. Inspekta Kobo akachukua simu yake na kujaribu kumpigia mkewe amuulize nini kinajiri hadi hajafika nyumbani hadi muda huo.
Simu iliita kidogo kisha ikakatwa. Alipojaribu tena haikuwa ikipatikana. Akajaribu kupiga ofisini wakaelezea kuwa Dokta Kobo alitoka kazini tangu saa mbili usiku, wakastaajabu kupokea simu usiku wote huo wa kuuliziwa kwake.
Inspekta Kobo ambaye tayari alijiona ni mtu ambaye ameandamwa na majanga ya ghafla akaingiwa mchecheto, haikuwa kawaida kwa mkewe hata kidogo kuchelewa nyumbani.
Akafikiria kuwapigia rafiki zake wachache aliowafahamu lakini mshale wa saa ulimfanya aone haya.
Saa nane usiku kumuulizia mke!
Hapana.... Akaendelea kungoja huku pepo la wivu likianza kumchokonoa, akajiuliza ikiwa yeye ameweza kuwa na mwanamke nje inashindikana vipi kwa mkewe?
Swali hili likamghadhabisha na kujiona hatendewi haki hata kidogo ikiwa ni kweli mkewe amediriki kufanya hayo.
Usingizi ulimsomba majira ya saa kumi na moja kasoro dakika chache.
Akagutuka saa moja na nusu asubuhi na bado mkewe alikuwa hajarejea nyumbani wala simu yake ya mkononi haikuwa ikipatikana.
Hofu ikatanda maradufu.....
 
Hii ni sehemu ya Saba

LILIANZA kuwa saa moja, kisha likafuata la pili yalipofika matatu subira ikafikia kikomo. Inspekta Kobo akachukua simu yake na kujaribu kumpigia mkewe amuulize nini kinajiri hadi hajafika nyumbani hadi muda huo.
Simu iliita kidogo kisha ikakatwa. Alipojaribu tena haikuwa ikipatikana. Akajaribu kupiga ofisini wakaelezea kuwa Dokta Kobo alitoka kazini tangu saa mbili usiku, wakastaajabu kupokea simu usiku wote huo wa kuuliziwa kwake.
Inspekta Kobo ambaye tayari alijiona ni mtu ambaye ameandamwa na majanga ya ghafla akaingiwa mchecheto, haikuwa kawaida kwa mkewe hata kidogo kuchelewa nyumbani.
Akafikiria kuwapigia rafiki zake wachache aliowafahamu lakini mshale wa saa ulimfanya aone haya.
Saa nane usiku kumuulizia mke!
Hapana.... Akaendelea kungoja huku pepo la wivu likianza kumchokonoa, akajiuliza ikiwa yeye ameweza kuwa na mwanamke nje inashindikana vipi kwa mkewe?
Swali hili likamghadhabisha na kujiona hatendewi haki hata kidogo ikiwa ni kweli mkewe amediriki kufanya hayo.
Usingizi ulimsomba majira ya saa kumi na moja kasoro dakika chache.
Akagutuka saa moja na nusu asubuhi na bado mkewe alikuwa hajarejea nyumbani wala simu yake ya mkononi haikuwa ikipatikana.
Hofu ikatanda maradufu.....
Asubuhi akapokea ujumbe mfupi kutoka kwa mkewe.
"Nipo salama mume wangu, nipo kwa mama mdogo. Kuna jambo limenichanganya naomba uniache kidogo natafuta suluhisho. Watazame watoto..."
Inspekta akaufuta ujumbe ule. Alimjua vyema mkewe, haikuwa mara ya kwanza kuwa katika hali hiyo na kuamua kuwa mbali na mumewe.
"Nimemkwaza nini huyu?" alijiuliza lakini akipata ahueni kuwa mkewe yupo salama.
_____
Mwanaume mweusi sana mwingi wa misuli katika mikono yake alikuwa amejitwika mfano wa gunia katika bega lake, mwili wake ulitokwa jasho lililoufanya ung'are kana kwamba ametoka kuogelea katika dimbwi la mafuta ya kula.
Alijitutumua na gunia lile huku akitweta.
Lilionekana kumzidia, lakini hakuwa tayari kukubaliana na hali ile moja kwa moja.
Macho yake makali mithiri ya nyoka yalikuwa makini kutazama huku na kule ikiwa kuna kitu kibaya aweze kujihadhari.
Zaidi alililinda lile gunia kuliko alivyowaza kujilinda yeye mwenyewe.
Alipoufikia mlima aliliweka chini lile gunia akapumzika kidogo kisha akajitwika tena na kuendelea na safari ile ambayo mwisho wake haukuwa bayana ikiwa ni wa matumaini ama la.
Kilima kikamalizika akaanza kupita katika vichaka vya hapa na pale, mwisho akaufikia mto na kuanza kuogelea. Gunia likiwa juu kabisa, japo lililowana lakini haikuwa kwa kiasi kikubwa sana.
Mkondo wa maji ulikuwa una nguvu sana lakini bwana yule mwenye misuli mingi alifanikiwa kuwa imara zaidi akapenya na kutokea upande wa pili.
Huko akapokelewa gunia lile huku akipongezwa na wenzake wawili waliosaidiana lile gunia.
Hawa nao walikuwa imara sana mmoja akiwa mfupi na mwingine mrefu. Wote weusi miili yao, wakaendelea na safari ya gunia lile kuelekea pahali lilipohitajika kufikishwa.
"Hivi mali itakuwa salama kweli?" Mmoja akahoji wakati wa pumziko fupi la kubeba gunia lile.
Swali lile likazua ukimya wa muda, wakalitazama gunia kwa pamoja. Kisha wakaangaliana kana kwamba waliambiana sekunde za kulitazama na sekunde za kutazamana.
Ukafuata mguno kwa pamoja tena.
"Unahisi jamaa atakuwa amefanya madhara yoyote?" aliyeulizwa swali naye akauliza swali kabla hajajibu alichoulizwa.
"Au tufungue kidogo?" Swali tena kutoka kwa muulizwa.
Swali hili likawafanya tena walitazame lile gunia kwa muda, halafu bila kukubaliana wala kupingana wakalibeba lile gunia safari ikaendelea.
Hawakulifungua!
Ilikuwa safari ya masaa kadhaa hadi walipolitua gunia mahali lilipostahili. Wakatulia wakilitazama kwa takribani dakika moja kisha wakainama na kulifungua gunia lile.
Waliacha wazi kisha wakatoweka.
Zikapita dakika kadhaa akaingia bwana aliyebeba bakora mkononi mwake, akalifikia lile gunia bila kusema neno lolote akaanza kuishusha bakora yake mara kadhaa guniani.
Gunia lilikuwa limetulia tuli bado.
Akazidisha juhudi kuliadhibu gunia lile na chochote kilichokuwa ndani yake huku akizungumza maneno mengi ya kulifokea na mengine ya kusihi. Jasho lilikuwa limemlowesha mwili mzima na alikuwa anatetemeka sana.
Baada ya bakora ya kwanza kuonekana haitoi adhabu ipasavyo akabadilisha bakora, akachukua ndefu zaidi.
Akaizungusha kwa ghadhabu zote akaitua katika gunia.
Gunia likatikisika!
Mchapaji akatulia tuli asiamini kile alichokuwa anakiona, akaanza kupiga mayowe akiwaita wenzake kutokea katika giza.
Kelele zile zikawa tishio kwa mali iliyokuwa katika gunia lile.
Kilianza kidole kutikisika na kisha macho yakaanza kulazimisha kuiona nuru.
Akajaribu kugeuka lakini akahisi maumivu makali yanamwandama na kuna kitu kizito kilikuwa kimeuegemea mwili wake.
Akajaribu kuongea akahisi koo limekauka sana huku kiu kikuu kikimwandama.
"Nini hiki?" alijiuliza baada ya kugundua kuwa ile si ndoto bali ni kweli tupu.
Akatuliza akili na kujaribu kufikiri tena na tena lakini hakuna jibu alilopata.
Akatumia nguvu ili aweze kujigeuza tena ikashindikana. Alipovuta pumzi zake akagundua kuwa hapumui vizuri sana. Kuna kitu kingine kilikuwa kimebana katika kifua chake.
"Hakikisheni amekufa aisee! Ishu sio nyumba ishu ni yeye..." Masikio yake yakazisikia sauti zikihimizana.
"Kina nani hawa Mungu wangu!" alihamaki akiwa palepale katika wakati mgumu.
Akajikuta anaijiwa na fikra mbili za ajabu zilizooana, akajihisi kuwa muda si mrefu alisikia shangwe na maneno ya kuhimizana huku akiwa amefunikwa katika kitu asichokijua na sasa anasikia maneno mengine akiwa mahali tofauti kabisa.
Ni nani hawa watu? alijiuliza.
Na nipo wapi hapa sasa eeh!
Milango ya fahamu yote ilikuwa imefanya kazi yake kwa ukamilifu, macho yaliishia kuona giza, masikio yakisikia sauti za ajabu, ngozi ilikuwa imebanwa na kitu asichokijua, ulimi ulibaini kiu kikali kutokanana ukavuu wa mdomo na koo, pua yenyewe ilikuwa imelala huku ikisahau wajibu wake.
Ikakurupuka na upesi baada ya kugundua kuwa bosi wake ameamka.
Ikanusa na kumweleza bosi wake kuwa kuna harufu ya petroli na moshi.
Moto! Akili ikaungana na pua kutoa majibu.
Mungu wee! nilichomewa ndani mimi! akajisemea na ili kuhakikisha kama haoti akajaribu kujipapasa.
Alikuwa uchi wa mnyama.
Ndio, mara ya mwisho alivua nguo zake harakaharaka baada ya kugundua kuwa hawezi kuukwepa moto ule upesi lakini angeendelea kubaki na nguo moto ungemvamia upesi kulikoni alivyokuwa mtupu.
Inspekta amenichoma moto! alijaribu kutoa sauti.
Akaishia kunong'ona, zile sauti alizozisikia nje zikawa zimetoweka kwa wakati huo.
"Mzee Majenga ni nani kwani?" alijiuliza swali lile, ilikuwa mara ya kwanza kabisa jina lile kuja katika fikra zake lakini alihisi amelisikia sehemu wakati akihangaika katika moto ule.
"Zile shangwe ndani ya lile gunia ina maana ilikuwa ndoto?" alijiuliza huku sasa akiutumia uimara wake wa jeshini kukinyanyua kile kifusi kilichokuwa kimemgandamiza.
Akafanikiwa.
Hamadi! Nyumba yote ilikuwa imeteketea. Kuta zilizoanguka ndizo zilisalia pamoja na bati.
"Nimeponaje mimi" alijiuliza huku akijaribu kusimama wima.
Mguu wake ulikuwa una maumivu makali sana. Kutokana na lile giza hakuweza kuona kilichojiri katika ule mguu.
Akatembea uchi vilevile, akitafuta muafaka wowote usiku ule.
Akaelekea hadi lilipokuwa bomba la maji, akafungua na kunywa maji ya kutosha.
Karibu na bomba palikuwa na kamba ya kuanika nguo. Akachukua nguo ambayo haikuwa yake, kumbukumbu za kuanika nguo zilikuwepo lakini angeutoa wapi muda wa kuitafuta?
Nguo ile ikamvaa lakini hakujali.
Akatoweka eneo lile huku jina Majenga likigoma kukimbia katika kumbukumbu zake.
_______
"KONSTEBO ALIYECHOMEWA NDANI YA NYUMBA, Mengi yamejificha!"
"MAPENZI CHANZO CHA KONSTEBO KUUWAWA"
"KONSTEBO NGUZU. SI KIFO CHA KAWAIDA"
Vichwa vya habari vya magazeti matatu vilisomeka katika namna ya kutatanisha, ni nani ajihusihe na kifo cha konstebo iwe amekufa kifo cha kawaida ama ameuwawa?
Wachache sana, hata makonstebo wenzake wasingejihusisha.
Lakini vichwa hivi vya habari viliwashtua watu watatu kutoka pande tofauti lakini wawili kati yao walizungumza lugha moja huku muhusika wa tatu akiwa katika sintofahamu..
wawili wale walizungumza lugha ya biashara...
Wa kwanza kupagawa alikuwa ni Juma Kimbelembele muhariri wa gazeti la SIRI KALI, alichanganyikiwa kabisa kwa sababu ni yeye pekee aliyejiona ana umiliki wa habari kuhusu kifo cha Konstebo Nguzu kwa kuchomewa ndani huku akikihusisha na masuala ya mapenzi.
Penzi kati ya Konstebo na Inspekta Kobo.
Ajabu sasa anatazama gazeti linaizungumzia habari kwa kuhusisha yaleyale aliyoyaita siri.
Mbaya zaidi siri hii alikuwa ameiuza tayari na pesa ilikuwa ikitembea katika miradi yake mingine.
Upande wa pili, Dokta. Kobo mke wa Inspekta alikuwa anaelekea kurukwa na akili, kwa ajiri ya mume wake na familia kwa ujumla alikuwa ametokwa na pesa nyingi sana kwa ajili ya kumziba mdomo Juma ili asiandike habari zozote juu ya mume wake hasahasa skendo la kuwa kimapenzi na Koplo Zubeda.
Hata siku tatu hazijapita anaziona habari zile.
"Nimetapeliwa au?" alijiuliza akiwa katika chumba cha hoteli aliyojihifadhi mpaka pale ghadhabu zake juu ya mumewe zitakapomalizika. Alihofia kulala kitanda kimoja na mume wake ambaye amemsaliti, aliogopa sana shetani mpenda kifo asije kumwingia kichwani na kumsababisha amdunge mume wake sindano ya sumu.
Aliijua hasira yake hasahasa ambapo mumewe angejaribu kumwongopea zaidi.
Licha ya kujifaragua wakati yupo hospitali kwa Zubeda kuwa hana mapenzi ya dhati sana kwa mumewe, aliongopa na moyo wake ulilijua fika hilo.
Daktari huyu hakuwa na mahali pengine pa kuzilaza hisia zake zaidi ya kifuani kwa Inspekta Kobo.
Sasa angali anapambana mumewe asijafuliwe jina lake, tayari mambo yamekuwa kinyume.
Akanyanyua simu yake na kumpigia yule muhariri Juma aliyemfuata na kumshirikisha juu ya habari ile na kumtaka wafanye biashara.
Simu haikupokelewa.
Akatuma ujumbe mfupi ulioambatana na kitisho kikubwa.
Mmoja asiyekuwa na moja wala mbili alikuwa ni Inspekta Kobo.
Habari hii ilimfanya akayatafuta magazeti yale mara moja, akaziendea kurasa zilizoelezea kwa kina juu ya habari ile.
Akashusha pumzi kidogo baada ya kukuta jina lake halijawekwa wazi lakini mwandishi wa makala ile alionyesha kujua kila kitu ni vile hakuamua kutajha katika makala hii ili aje kuuza magazeti mengine wakati mwingine atakapoamua kulianika jina la muhusika waziwazi.
Inspekta akakumbuka kile kiwiliwili chini ya mti. Akaamini kuwa ni kiwiliwili kile kilimuona wakati anaingia na kutoka.
Yule mwandishi alijuaje nitaenda kwa Nguzu eeh! alijiuliza Inspekta huku ikimjia pia ile sauti aliyoisikia usiku ule.
Sauti ambayo si ngeni lakini alikuwa ameisahau tayari.
"Lakini sijamuua Nguzu mimi. Mungu wewe ni shahidi. Niliitafuta amani tu..... nilipanga kumuua lakini nilighairi wanishushudia mwenyezi Mungu." Alizungumza peke yake Inspekta huku moyo wake ukiona haya kwa sababu ni mwaka mzima na miezi ilipita bila kuingia katika nyumba za ibada.
Akarejea katika magazeti yale na kusoma majina ya waandishi wa habari zile.
Akabaini kuwa zile habari zilifichwa jina la mwandishi wakaishia kufanya mazoea yao ya kuandika kuwa imeandikwa na MWANDISHI WETU.
"Attaccati a sto cazzo" Akabwatuka lile tusi pekee la kiitaliano analolifahamu huku akiyatupa yale magazeti mezani.
"Who the hell is mwandishi wetu?! eeh! kwani sisi hatujui aliyeandika habari hiyo ni mwandishi wenu you bastard!" Alilalama peke yake huku sasa akiwa wima.
Akajaribu kuwafikiria wafanyakazi wa magazetini ambao ni wasumbufu. Ambao siku hazipiti hawajapiga simu jeshi la polisi kuuliza maswali kadha wa kadha.
Akainyanyua simu yake na kupiga katika kitengo cha mawasiliano jeshi la polisi.
"Komredi, umekuwepo kwenye shifti tangu jana?" akaulizia.
"Nimekaa siku ya tano leo, mwenzangu anaumwa. Vipi afande..."
"Naulizia kama kuna simu yoyote kutoka gazeti la SIRIKALI..."
"Lile gazeti la Juma Kihwele.." akauliza kimasihara. wakacheka kidogo kwa sababu walimjua vyema.
"Yule bwabna sijui atakuwa anaumwa. Leo siku ya sita au saba hakuna simu kutoka kwake."
Inspekta akashukuru na kukata simu.
"Huyu mjinga kuna kitu anajua, hawezi kukaa kimya siku zote hizi." alijisemea huku akichukua kalamu yake na karatasi kisha akaainisha mambo kadhaa.
MOJA, Juma Kihwele anaijua hii habari lakini ameogopa kuiandika kwa jina lake.....
PILI, haijui hii habari lakini alivyo na kimbelembele anaifuatilia kwa kina akiandika awalipue wahusika.
Yote mawili yalimaanisha kuwa Juma ni mtu muhimu sana katika hili jambo.
Inspekta akaingia chumbani kwake, akaitoa bastola yake mafichoni na kuitazama kwa muda kisha akasema nayo.
"Let's go to work boy! (Twend'zetu kazini)"
Simu yake ya mkononi ikaita wakati akiipachika bastola yake pahali alipozoea kuipachika.
Ilikuwa ni simu kutoka kwa mkewe.....
Mapigo ya moyo yakaenda mbio sana.
 
HII HAPA SEHEMU YA NANE

Inspekta akashukuru na kukata simu.
"Huyu mjinga kuna kitu anajua, hawezi kukaa kimya siku zote hizi." alijisemea huku akichukua kalamu yake na karatasi kisha akaainisha mambo kadhaa.
MOJA, Juma Kihwele anaijua hii habari lakini ameogopa kuiandika kwa jina lake.....
PILI, haijui hii habari lakini alivyo na kimbelembele anaifuatilia kwa kina akiandika awalipue wahusika.
Yote mawili yalimaanisha kuwa Juma ni mtu muhimu sana katika hili jambo.
Inspekta akaingia chumbani kwake, akaitoa bastola yake mafichoni na kuitazama kwa muda kisha akasema nayo.
"Let's go to work boy! (Twend'zetu kazini)"
Simu yake ya mkononi ikaita wakati akiipachika bastola yake pahali alipozoea kuipachika.
Ilikuwa ni simu kutoka kwa mkewe.....
Mapigo ya moyo yakaenda mbio sana.
Akaipokea ile simu huku akiwa anatetemeka mikono yake katika namna iliyomtishia amani.
Alipoiweka simu sikioni kimya kikatanda kutoka upande wa pili.
"Mama! Mama! Mke wangu... ongea basi mama." alizungumza kwa upole wa hali ya juu.
Badala ya kujibiwa akaanza kusikia pumzi zikipishana kwa kasi sana na hapo akaanza kukisikia kilio.
Dokta Kobo alikuwa analia.
Suala la mkewe kuangua kilio ikawa kama msumari wenye ncha kali unasukumwa katika paja lake angali ana fahamu zote.
Maumivu!
"Mama Melinda! una nini mke wangu nieleze... au niambie basi upo wapi nije sasa hivi." Alisihi Inspekta Kobo lakini simu ikakatwa bila kusikia neno lolote.
Akapagawa.
______
SHAMALIWA, Mwanza.
Umati wa watu haukuwa mkubwa sana. Walikuwa ni wanafamilia walioridhia ile taarifa ya kifo cha ndugu yao.
Mama mzazi wa Nguzu hakuisha kulia na kulalamika kuwa alimkanya mwanaye asijiunge na jeshi lakini hapohapo akikiri kuwa ugumu wa maisha ulikuwa chanzo cha yote hayo.
Waliojaribu kumbembeleza walikuwa wamefikia kikomo na sasa walimwacha alie kuzimia na kisha kuzinduka peke yake.
Kuzika majivu! Mama yake alikataa kata kata, alidai kuwa hakuyaaga majivu katika kituo cha basi bali alimuaga mwanaye tena kwa kumkumbatia, leo hii akubali kuyazika majivu asiyoyajua?
Hapana... akasimama kidete na wanafamilia wakamuunga mkono, hawakufanya maziko hayo.
Ambaye aliamini Martin Nguzu amefariki sawa, ambaye hakuamini sawa.
Mama Martin hakuwa katika upande wa walioamini.
Na kila alipojaribu kuamini, lilikuja wazo jingine kuwa yawezekana mwanaye amefanyiwa ubaya tu. Sio kifo cha kawaida.
Ndivyo walivyo akinamama.
Ule uchungu wa mwana unasababisha haya.
Siku ya tano ikiwa inayoyoma na jambo hililikiwa limepunguza makali mioyoni mwa wengine kasoro mama mtu.
Majira ya usiku ule uliingia ugeni ambao hakuna aliyeutilia maanani, maana kwa kipindi hicho watu walikuwa wanakaa nje, ndugu na jamaa wanacheza mchezo wa karata mpaka usiku wa manane na wengine kulala nje kabisa.
Huyu bwana alikuwa mkimya kabisa na koti lake kubwa la kuzuia baridi, alijitikisa kwa sababu za msingi tu na hakugeuka huku wala kule, alikuwa amejiinamia.
Kadri muda ulivyozidi kwenda na watu walizidi kupungua, wengi walienda kulala.
Huu nd'o muda ambao yule bwana alijitikisa tena kwa kiasi kikubwa.
Alisimama!
Akapiga hatua kadhaa bila mtu yeyote kumtilia mashaka, akasogea pembezoni akaichomoa pakti ya sigara na kutoa moja, akaiwasha na kuuvuta moshi wake ndani ya kifua chake na kwa umaridadi kabisa akaupuliza angani kisha akautazama unavyotokomea angani.
Akafanya vile takribani mara tatu, kisha akaizima. Akapiga hatua nyingine tena akaufikia mti kisha akaanza kuyatazama mazingira ya pale kwa uchache akahisi ni wakati muafaka wa kufanya kusudio lake na hakuona jambo lolote la kumzuia.
Akapiga hatua huku mkono wake ukiwa katika mifuko yake, akajipitisha jirani kabisa na kundi la akina mama wawili waliokuwa wamejilaza.
Akamwona muhusika wake.
"Ndiye!" akajisemea.
Kisha kwa kitendo cha upesi sana akainama, akamziba mdomo na kisha akaichomoa silaha yake na kwa lugha ya vitendo akazungumza naye.
"Ukileta vurugu nitakuchinja."
Huku akiwa amemdhibiti vyema kabisa akamnyanyua wakaondoka kutoka katika eneo lile.
Alipomfikisha pembeni kiasi akampiga teke kali miguuni, kisha akatua naye chini.
"Mzee Majenga anaishi wapi?" lilikuwa swali kavu kabisa kutoka katika sura ngumu.
Mama akabaki kuhangaika asijue ni nini hiki kinatokea angali ana kovu la msiba wa mwanaye wanatokea watu kumuuliza juu ya mzee Majenga.
"Alihamia Shinyanga." alijibu kwa ufupi.
"Nitakuua sina masihara. Alihamia lini na awali alikuwa ana anishi wapi? nani ndugu zake?" Alijaza maswali mazito.
"Kama mwanangu mmemchoma moto, ukinichinja hautakuwa umefanya dhambi mpya. Nipeleke kwa mwanangu, sina jibu jingine...." Alijibu kikaidi. Huku nafsi yake ikiwa radhi kabisa yule bwana amuue ili aondokane na huu uchungu wa kuishi bila mwanaye.
Mkono wenye nguvu ukashusha ngumi katika bega la yule mama kisha kiganja kikawahi kuziba mdomo.
Maumivu yakanyimwa kilio.
Yule mama akabaki kuhema juu juu huku akiwa ameyakodoa macho yake.
"Sasa utanijibu vizuri kabisa sivyo. Mzee Ma..." hakuweza kumalizia akahisi kuna mguso fulani kwa mbali katika bega lake.
Akageuka bila hofu yoyote, akakutana na giza likiwa ndani ya giza.
Lakini hili halikuwa giza ambalo linaweza kutembea.
Ngumi kali ikatokea katika lile giza la maajabu, ngumi moja ikatua katika koo la yule bwana.
Akajaribu kukohoa akawa ameikohoa roho yake. Umauti ukamfika.
"Mama!" giza lile likaita.
Mama aliyekuwa anahema juu juu huku akiwa anafanya dua maalumu kwa ajili ya kuiaga dunia akarejea katika fahamu zake.
Haikujalisha giza lile lilikuwa totoro kiasi gani, mama alitambua ubini wake ipasavyo.
"Martin!" akaita.
"Nipo hai mama." akajibiwa.
Mama akaamka akaketi kitako asiamini kuwa alikuwa anapokea miujiza katika uzee wake.
Ubaya wa wanawake siku zote ni pale akili zao zikitulia.
Mwanzo alikuwa ametulia tuli akizungumza na lile giza, lakini baada ya akili kukaa sawa akaanza kupiga mayowe.
Mkono ukawahi kumziba mdomo.
"Mama, huyu alikuwa anataka nini kwako."
"Simjui."
"Mama, sijauliza kama unamjua. Alikuwa anataka nini?"
"Muulize labda wewe atakueleza vizuri."
"Hakuna mzoga uliowahi kuzungumza katika dunai hii mama. Nieleze.."
"Amemuulizia mzee Majenga.... yule mzee alikuwa rafiki sana na babu yako. Wewe humjui..." alitoa maelezo yale.
Majenga!
Jina lile likapiga katika kichwa chake kwa kujirudiarudia, ni jina hili lilimjia punde tu baada ya kurejewa na fahamu asijue nani aliliingiza katika kichwa chake.
"Uliponaje mwanangu, nyumba iliteketea yote ile. Tuliona kwenye Televisheni.." mama alimuuliza.
"Mama usimwambie mtu yeyote kama umeonana na mimi, mimi nipo hai na ninaamini nina kazi kubwa ya kufanya kabla sijasimama hadharani na kuutangazia uma kuwa ninaishi." Alisihi Nguzu. Kisha akamkumbatia mama yake na kumbusu shavuni.
Upesi mama akaipapasa shingo ya nguzu katika giza lilelile.
Na hapo akatokwa na tabasamu pana lililosindikizwa na machozi ya furaha.
Aliyekuwa mbvele yake alikuwa yuleyule mtoto aliyetoka katika tumbo lake.
Martin Nguzu!
Ameponaje? hilo halikuwa swali lililomuhangaisha......
Bora uzima.
Walizungumza kwa dakika kadhaa kuhusu Majenga kisha wakaagana.
Akiwa anafanana na giza kwa jinsi alivyovaa alitembea kwa tahadhari kubwa huku akiamini wapo wengine wanaweza kuvaa kama yeye na kufanana na giza, akapiga hatua na kutoweka eneo lile.
Begani akiwa na mzoga wake...
_______
LILIANZA tumbo la kuhara, kila akiingia chooni linapoa anarejea chumbani. Linaanza tena anakimbilia chooni, linapoa.
Alikuwa amechanganyikiwa mno.
Hali hii ikamkumbusha kuwa angali akiwa mwanafunzi alikuwa anaugua haswa akisikia kuwa kuna bakora kwa ajiri ya wachelewaji ama ambao hawajafanya vyema kazi waliyoachiwa. Hivyo alikuwa mstari wa mbele kabisa kufanya kazi zote ipasavyo, kuheshimu sheria na kanuni za shule.
Na hata ilipotokea migomo hakutaka kushiriki, wenzake wakambeza na kumweka katika kundi la wanafunzi waitwao 'MBWA WAOGA' shuleni.
Alikuwa tayari kuitwa majina yale lakini alitambua kuwa anaitii sheria vyema.
Akaishi hivyo na akakua hivyo.
Akiwa katika utu uzima wake ana familia na yupo kazini, anajaribu kuisahau asili yake anaitaka pesa nyingi kwa njia zisizokuwa halali. Jaribio lake la kwanza linakuwa kuuza habari aliyoinasa mahali.
Kabla mchezo haujanoga anajikuta matatani.
Akatamani nyakati zirudi nyuma kidogo tu asijihusishe na hili jambo asilani. Lakini ni saa pekee inaweza kurudi nyuma na si wakati.
Juma Kihwele alikuwa amekamatika.
Akafikiria mtu wa karibu yake wa kuweza kumshirikisha hilo jambo, hasahasa ujumbe kutoka kwa Dokta. Kobo uliomfanya kupata tumbo la kuhara ghafla.
Mkewe, hapa asingethubutu kugusa hata kidogo kwa sababu tayari alikuwa amemwonya kuachana na masuala ya kufuatilia habari zisizomuhusu.
Akafikilia kukimbilia msikitini walau amweleze kiongozi wake wa dini. Huku napo akaona pagumu kuingilika, maana huku ni mambo kunyooshwa tu hakuna kona kona.
Kila sehemu aliyoiwaza akaona haiingiiliki.
Mwisho akajiwekea maamuzi ambayo aliyapa jina la 'NANI ATAMFUNGA PAKA KENGELE'
Katika maamuzi haya yeye alikuwa panya.
Akawavika vyeo vya U-paka Inspekta na mkewe.
Kisha akamchagua inspekta Kobo kwa kujipa imani kuwa yule ni mwanaume mwenzake hivyo watazungumza na yatamalizika tu.
Akaingia bafuni akausafisha mwili wake, akavalia nadhifu kisha akaamua kujihukumu. Akachukua simu yake na kuipekua nambari za Inspekta Kobo. Akajihisi kutetemeka wakati anapiga simu ile.
Kitetemeshi kikaisha alipogundua kuwa simu ile haipatikani. Akachukua maamuzi ya kumpigia Koplo Mtani yule aliyemsababisha akajiingiza katika mchezo huu asioujua. Lakini maamuzi yake yakayeyuka baada ya kujiona kuwa atakuwa anawaingiza watu wengi katika hili jambo aliloliita kuwa ni maongezi ya kiume dhidi ya Inspekta Kobo.
Kwa sababu alipajua ofisini kwake akaamua kwenda kimyakimya wakayamalize.
Akatoka na kuingia katika gari yake, akaitazama tasbihi iliyokuwa inaning'inia katika kioo cha ndani cha gari lake.
Kisha akawasha gari na kuondoka zake.
Baada ya dakika moja, gari jingine dogo likatoweka na kumfungia tela.
Hakujua kuwa wakati anawaza kumfunga paka kengele na wengine waliwaza hivyohivyo juu yake.
Kwa wakati mmoja Juma 'kimbelembele' alikuwa panya na hapohapo paka.
Kiumbe wa ajabu kupindukia!
Aliiendesha gari yake kwa utulivu huku kila mara akijilaumu nafsi yake kwa tamaa za ajabu ajabu.
"Tazama nimejenga nyumba nzuri kabisa, hata kama sijahamia bado lakini nina uhakika wa kuhamia siku yoyote, nina gari na nimekaribia kumnunulia mkewangu la kwake, nina amani ya nafsi, mtoto wangu anaishi vizuri kabisa, anasoma shule nzuri. Hiki nini kiliniingilia kichwani nikapatwa na tamaa mimi lakini, eeh! Ninaheshimika ofisini, bosi ananipandishia mshahara kila leo. Ni kipi nilitaka tena Juma mimi. Yaani shuleni waliponiita kimbelembele nilichukia na kuwaona hawanipendi, sasa najionea mwenyewe. Ona sasa naanza kuhangaika na kimbelembele changu, mtu mwenyewe Inspekta unakuta ana hasira zake huko anipige mabuti, mi kupigana sijui, jeshi lenyewe sijapitia..... Hivi Juma nilikuwaje mimi eeh!" alilalamika kwa sauti ya chini, malalamiko yaliyopelekea machozi kuanza kumbubujika.
Akashindwa kuona mbele vizuri, akaamua kuegesha gari lake kando.
Akajifuta machozi. Akaitazama simu yake na kugundua kuwa ilikuwa inaita pasi na kutoa mlio.
Akakumbuka aliiweka simu yake iwe katika hali ile. Akaishika kwa utulivu na kutazama. Ni mkewe alikuwa amempigia.
Akampigia kuuliza kulikoni.
"Mume wangu naomba urudi nyumbani muda huu, sasa hivi mume wangu... atawaua watoto huyu. Njoo mume wangu..." Alizungumza huku amepagawa mno mke wa Juma.
Simu ikakatwa bila kusubiri majibu kutoka upande wa pili.
Lile tumbo la kuhara lililosumbua kuanzia akiwa nyumbani likayasikia mazungumzo haya, kwa kirehere cha hali ya juu likatamani kusikia zaidi.
Likatoa wawakilishi palepale akiwa ameketi katika kiti chake cha gari....
Hali ya hewa ikachafuka....
 
HII SEHEMU YA 9

"Mume wangu naomba urudi nyumbani muda huu, sasa hivi mume wangu... atawaua watoto huyu. Njoo mume wangu..." Alizungumza huku amepagawa mno mke wa Juma.
Simu ikakatwa bila kusubiri majibu kutoka upande wa pili.
Lile tumbo la kuhara lililosumbua kuanzia akiwa nyumbani likayasikia mazungumzo haya, kwa kirehere cha hali ya juu likatamani kusikia zaidi.
Likatoa wawakilishi palepale akiwa ameketi katika kiti chake cha gari....
Hali ya hewa ikachafuka....

ALIBAKI katika mzubao kama mwanaume aliyemwona mwanadada mwenye mvuto akijongea kwenda upande wake akajilaghai katika kichwa chake kuwa amekutana na bahati ya mtende akajiandaa kumpokea, kisha mrembo yule anatokwa na neno la ghafla.
"Kaka umesahau kufunga zipu yako.."
Mzubao huo ulimkumba Juma Kihwele, alipotoka katika mzubao akahamia katika mlowano katika suruali yake.
Chozi likamtoka alipotambua kuwa haikuwa ndoto bali alikuwa kama anavyojiona.
Mbele na nyuma palikuwa pameshirikiana kumfedhehesha.
Ubahili akauweka kando, kabla harufu ile haijawafikia wasiohusika Juma Kihwele akapandisha vioo vya gari lake kisha akawasha kiyoyozi.
Alitambua wazi kuwa kiyoyozi hakitakuwa na msaada mkubwa lakini walau linatimia lile neno la 'Mchuma janga hula na wa kwao' kwanini yeye ale na wasiomuhusu?
Acha ale na kiyoyozi....
Akaigeuza gari kwa kasi akiwa ametaharuki.
Akawa amebadilisha uelekeo na kuelekea alipokuwa ametoka.
Jambo lile likawa na maana nyingine kwa waliomtazama...
____
KITENDO kile cha kubadilisha uelekeo kikawashtua wale waliokuwa katika gari iliyokuwa ikimfuatilia toka alivyoliacha geti la nyumbani kwake.
Dereva akabweka na kuwashtua wenzake, wote hawakuamini walipoiona gari ile ikiondoka kwa mwendo mkali. Kila mmoja akabaki kumlaumu mwenzake kwa kuukosa umakini.
Lawama zisingekuwa na msaada wowote dereva akapambana naye kutafuta njia ya kugeuza gari ili afukuzane na lindo lao walilolivizia kuanzia linatoka nyumbani
Sasa lindo limewatoroka ghafla. Wakabaki kujiuliza ni wapi ambapo waliteleza hadi yule bwana akawaona....
Swali hili likawafanya waanze kuamini kuwa bwana Juma ana watu wengi nyuma yake ambao wanamsaidia katika suala la ulinzi.

Hapa wakaongeza umakini na ile hali ya kumchukulia Juma kama mwandishi asiyekuwa na tahadhari katika maisha yake ikatoweka.
Hawakujua kuwa Juma Kihwele alikuwa amevurugwa vibaya mno, na hata ule mwendo kasi wa ghafla ulikuja ghafla kama ulivyoonekana na hakujua kama alikuwa anafuatiliwa.
JUMA aliwasili nyumbani, bila kujali kuwa alikuwa amechafua nguo yake alishuka upesi na kuingia ndani ya nyumba yake huku akiwa amenyoosha mikono yake juu kama namna ya kujisalimisha ili wavamizi wakijitokeza kwa nia ya kushambulia basi awe amejitetea tayari kuwa hana madhara yoyote kwao.
Huenda wataingiwa na huruma juu yake.
Hicho nd'o kitu pekee alichoweza kufanya kwa wakati ule.
Alilivuka geti lake huku akijilaumu kwa ubahili wake uliokithiri wa kushindwa kumlipa mlinzi ili awe analinda masaa ishirini na nne badala yake akaona usiku nd'o wakati pekee wenye hatari akaamua kulipia masaa kumi na mawili.
"Mlinzi mwenyewe analinda na rungu?" Alitoa kauli ya kupuuzia majuto yake.
Alitembea hatua kwa hatua hadi akaufikia mlango wa kuingilia ndani ya nyumba yake akabaini kuwa ulikuwa umefungwa kwa nje.
Bila shaka mvamizi yupo nje.
Huku akiwa anatetemeka akaufungua ule mlango, akaikuta familia yake yote ikiwa inatazama ukutani. Mama mwana pamoja na shemeji yake aliyekuwa pale kwa ajili ya likizo.
"Jamani.... kuna nini mke wangu?" Akamuuliza, mkewe akageuka huku akiwa anatetemeka na asiamini kuwa aliyesema naye alikuwa ni mumewe.

Akaanza kuangua kilio huku yote anayoyasema yasisikike vyema kiasi cha Juma kuanza kumkaripia kuwa anapaswa kuzungumza kwa utulivu ili wajue ni kitu gani kinaendelea.
"Ni nani alivamia hapa na kukueleza upige simu."
"Simjui, sijawahi kumwona hata siku moja."
"Anafananaje? na ni kitu gani anataka kwangu..."
Mkewe akamsogelea Juma na kumkumbatia, hakuwa na sababu nyingine ya kumkumbatia bali kumsihi waende chumbani.
"Hapana... tuzungumze hili jambo kwanza tuelewe muafaka!" alipinga vikali.
Mke akamsogelea tena na safari hii akamueleza ukweli kuwa alikuwa ananuka, anapaswa kwenda kusafisha mwili wake kwanza.
Akili ya Juma ikaingiwa na mchecheto, akatembea kinyonge kabisa kuelekea chumbani.
______
NJE ya nyumba ya Juma wale waliokuwa wakimfungia tela walikuwa wamewasili tayari na waliegesha gari lao mbali na nyumba yake. Walikuwa watatu na walitembea kama wasiofahamiana katika suala hili. Kila mmoja alijiweka katika shughuli zake, ilimradi iwe ngumu kujulikana kuwa kuna jambo wanafuatilia.
Umakini wa sasa ulikuwa umezidi wa awali ambapo walimchukulia Juma kirahisi sana. Sasa walikuwa makini kana kwamba wanapambana na adui mwenye hatari sana zaidi yao.
Silaha zao ziliwekwa tayari tayari.
Jicho moja pevu lilikuwa katika kona ngumu kufikika, lilikuwa limewapokea kuanzia walipowasili awali, wakamfungia tela Juma akiwashuhudia. Kisha akatengeneza vamizi la kumrejesha Juma nyumbani bila maafa yoyote, ili aendelee kuwasoma watu wanaomfuatilia Juma.
Akaivamia nyumba na kutoa kitisho kikali.
Zoezi likafanikiwa Juma amerejea na wao wamerejea.
Ni akina nani hawa? na wanataka nini kwa Juma? haya yalikuwa maswali ambayo yalihitaji kupatiwa majibu upesi sana kabla naye hajajua ni kitu gani anaweza kufanya katika mchakato huu.
Aliitoa taarifa hii ya mashaka yake juu ya watu anaowaona eneo hilo, taarifa ikapokelewa huku akisisitizwa kuwa makini zaidi.
Masaa yalizidi kwenda bila kuona juhudi za watu wale kuingia ndani ya nyumba ya Juma, walibaki kurandaranda huku na kule bila kujua kuwa wanafuatiliwa.

Kwa kuwatazama jinsi walivyokuwa wanatembea na kufanya mawasiliano alihisi yawezekana ni askari waliopo kazini, ama waliopoteza kazi zao, na kama si maaskari basi yawezekana waliwahi kupata mafunzo ya kijeshi kwa sababu maalumu.
Akajinyoosha kidogo mwili wake na kujipima ikiwa anaweza kukabiliana na vijana wale.
Wakati anajinyoosha akabaki kujicheka kuwa anauhangaisha mwili wake wa nini wakati ana kijana wake wa kazi ambaye kamwe hazeeki.
bastola kiunoni!
Majira ya saa tatu usiku akapiga hatua na kujichanganya barabarani, na hapohapo akageuka muigizaji, akazuga kuwa amelewa na anayumbayumba.
Lengo lake likiwa kumfikia mmoja kati ya wale vijana.
Akafanikiwa kupita jirani na kijana mmoja, akajikuta akicheka ndani ya moyo wake alipotambua kuwa hata kijana yule naye alikuwa katika fani ya maigizo na alikuwa yu katika kitengo cha kuigiza kuwa ni kijana anayetumia madawa ya kulevya na sasa ametulia tuli baada ya kujidunga.
Safi! akajisemea kisha akamchokoza.
Akamsema maneno yanayoudhi huku akiendelea kujiweka katika hali ileile ya ulevi.
Yule bwana hakujibu kitu badala yake aliendelea kuwa mtulivu.
Wakati wote huu alipokuwa anamfanyia bughudha katika sikio lake alikuwa na kifaa kidogo kilichokuwa kinatumika kwa ajiri ya mawasiliano.
Yule bwana aliyekuwa amejiweka kama mtumiaji wa madawa ya kulevya ahatimaye alinyanyua kichwa chake na kumtazama huyu mlevi kwa chati jinsi alivyokuwa anahangaika kumchokoza.
"Naomba uondoke hapa." alizungumza maneno machache kisha akainama.
Mlevi akaanza kucheka huku akidiriki kumzongazonga yule bwana, alifanya vile kwa sababu alijiamini kuwa yule bwana hana ubavu walau wa kuingiza hata ngumi moja katika mwili wake iwapo watakusudia kutupiana makonde na hata akifanikiwa kutupa konde halitamletea athari.
"Naomba uniache uondoke hapa wewe mlevi." alisisitiza. Lakini yule mlevi bado aliendelea kuwa pale. Mara atukane hivi mara aimbe vile.
Bwana aliyeketi akazidiwa na kero zile, akasimama wima na kumrushia ngumi kali yule mlevi, mlevi akaikwepa bila kujibu pigo.
Kukwepwa kule kukamfanya awe makini zaidi na yule mlevi. Macho yakamkagua haraharaka huku wakitazamana kama majogoo.

Akajaribu kurusha teke, mlevi akakwepa.
Wakati yule mlevi anakwepa teke lile, yule bwana aliyekuwa akikabiliana naye akaona kitu kilichomtisha.
Aliiona bastola.
Na hapohapo akazungumza maneno yaliyomchanganya yule bwana mlevi wa kuigiza.
"Angusha mbuyu kuna nyoka."
Maneno yale yakasafiri upesi katika akili ya yule mlevi wa kuigiza, akajaribu kuyafanyia kazi upesi lakini hakuweza kupata maamuzi sahihi.
Jicho likamtazama mlevi yule kutokea mbali kabisa katika kifaa maalumu, mlango wa chuma ukafunguliwa kisha mwanga ukatoka bila mlio wowote, mwanga ukasafiri kwa kasi kubwa na kisha ukaweka makazi ya muda katika kifua cha yule mlevi wa kuigiza.
Akatokwa na yowe kidogo kisha akaanza kujitupa huku na kule. Maneno aliyoongea hayakuwa nyoofu akaamua kunyamaza huku damu ikimtiririka.
Yule bwana aliyekuwa ameweka kambi chini ya mti ule akampekua na kutoa bunduki katika kiuno chake.
"Zahoro! huyu mjinga alikuwa na bunduki, huyu hakuwa mlevi aisee. Katumwa huyu hakutakiwa kuuwawa...... dah!" alizungumza kwa kutumia kifaa kilichokuwa sikioni.
Maneno yale aliyozungumza yakapita moja kwa moja kwenda mahali ambapo hawakutaka yafike. Na hawakujua kama yanavuka mipaka hiyo.
Yule bwana marehemu alikuwa akiwasiliana na mtu mwingine kabla hajauwawa. Hivyo alisikia yote hadi mwisho.
____
INSPEKTA KOBO akachanganyikiwa upya, hii ni baada ya kuyasikia maneno yaliyozungumzwa katika kifaa kilichokuwa sikioni mwa kijana wake aliyemtuma kufuatilia mienendo ya Juma Kihwele.
Alisikia sauti yake wakati akitapatapa na mwisho akaisikia ile sauti ya mtu aliyekuwanaye.
"Ni akina nani hawa?" alijiuliza huku aking'ata vidole vyake baada ya kukiri kuwa kuna watu hatari katika sakata hili ambalo kwa namna yoyote ile linaelekea kumwangukia na kumzika kabisa.
Kijana wake alikuwa ameuwawa!
"Angusha mbuyu kuna nyoka..." Hii sauti ikawa inajirudia katika kichwa chake. Ni kama aliwahi kusikia mahali...
"Yeees!" akarusha ngumi hewani, alikuwa amekumbuka kuwa sauti ile aliisikia usiku ule alipokwenda kwa Nguzu kwa ajili ya kumsihi aachane na Zubeda wake na alipoondoka nyumba ile ikachomwa moto na kuaminika kuwa imeondoka na uhai wa Nguzu.
"Huyu ni nani lakini? na kwanini wamchomee kijana wa watu ndani eeh!" akawaza na kuwazua kisha akaamua kutoka nje.
Akaingia katika gari yake na kunyoosha moja kwa moja hadi hospitali aliyokuwa amelazwa Zubeda. Akaingia moja kwa moja katika kile chumba kile ambacho alikuwa amekiwekea walinzi wa siri hasahasa baada ya mkewe kuingia mle ndani na kumuhoji Zubeda mambo mazito.
"Zubeda kila kitu kimeharibika na mambo yanazidi kuharibika, huu sio wakati wa kuzungumzia kilichotokea hapo katikati, huenda hicho kina unafuu. Naomba usikilize hii sauti kwa umakini na unieleze kama umewahi kuisikia... naomba usinifiche hata kama umeiskia katika mazingira ambayo haupendi mimi niyafahamu."
Akamwinamia na kumwekea kifaa sikioni kisha akakiwasha kile kifaa, Zubeda akaisikia sauti ya yule mwanaume ikizungumza yote iliyozungumza.
Koplo Zubeda akatikisa kichwa kuwa hakuna anachokielewa. Inspekta Kobo akashusha pumzi zake kwa juhudi zote, mambo yalikuwa yanazidi kuwa magumu.
"Vipi kuhusu Zahoro? unalifahamu hili jina?"
"Nawafahamu Zahoro kadhaa, ila sina ukaribu nao."
"Kuna mjinga anaitwa Nasoro nahisi amemuua kijana wangu." alizungumza kwa uchungu Inspekta huku akitazama juu.
Na alipoushusha uso wake alizungumza na Zubeda.
"Hautaendelea kulalia hiki kitanda, kuna watu wanaisaka roho yako wakati huu. Hakuna ninayemuamini kukulinda, nataka nikulinde mimi mwenyewe." Inspekta akanong'ona kwa hisia kali huku akiwa anamtazama Zubeda moja kwa moja machoni. Kabla Zubeda hajasema lolote Inspekta akaendelea, "Mke wangu ana hasira sana najua, lakini si sababu ya mimi kukuacha wewe katika hali isiyokuwa salama. Yameniumiza mengi katika hii dunia ya mapambano, nitajitonesha upya nikishuhudia maiti yako"
"Mlinde zaidi mkeo..." Zubeda akaingilia kati katika hilo.
"Yupo katika ulinzi wa hali ya juu." Alijibu Inspekta na hakutaka maongezi yaendelee, akatoweka kwa ajili ya kufanya hatua zote za kumwondoa Zubeda katika hospitali ile.
Zoezi likafanikiwa.
_____
KUKUTWA ametupwa mtaroni?
Tena akiwa hana jeraha bali alama moja tu katika shingo lake...
Pigo la aina gani hii?
Nani alitoa pigo hilo barabara!
Haya yalikuwa maswali mfululizo yaliyopita katika kichwa cha kiongozi wa oparesheni isiyokuwa na jina rasmi. Hii ni baada ya kupokea taarifa kutoka jijini Mwanza kuwa kijana wake anayemuamini kupindukia alikuwa ameuwawa kwa kupigwa pigo moja kali kabisa shingoni.
Tabasamu hafifu lilimdondoka wakati anajaribu kufikiria upya juu ya jambo hili.
Akanyanyua mkonga wa simu yake, akataka kupiga mahali akaghairi na kubaki akielea katika mzani wa maamuzi.
Akaushusha ule mkonga na kunyanyua simu yake ya mkononi. Akabofya nambari zilizokuwa zimetoka kumpatia taarifa kutoka jijini Mwanza.
"Kwa hiyo umesema hakuna sehemu nyingine aliyojeruhiwa? Je ujumbe wowote kwa ajili yetu?" akatulia na kusikilizia upande wa pili ukijibu. Baada ya majibu akazungumza kwa ukali kidogo.
"Ongea na Cheyo, aamrishe askari wake wazunguke kila kona hapo Shamaliwa wakamate vibaka wote wanaorandaranda kijinga jinga mitaani. Wawabane watasema kama waliona hilo tukio. Mwambie asiache mtu hata mmoja."
Waliendelea kuzungumza kwa sekunde kadhaa kisha simu ikakatwa.
Jijini Mwanza baada ya masaa mawili eneo la Shamaliwa nje kidogo ya jiji hapakuwa mahali salama hata kidogo, ukizurura unakamatwa, ukikaa unakamatwa ukicheka unakamatwa ukilia unakamatwa.
Hadi waliokutwa wanakata majani ya ng'ombe nao walikamatwa.
Katika kamata kamata ile ikazua jambo juu ya jambo
_____
KONSTEBO MARTIN NGUZU alikuwa anajaribu kuutafuta usingizi katika kitanda ambacho kilitawaliwa na kunguni waliokuwa na maksudi mabaya, taa ikiwashwa wanatoweka na ikizimwa wanaingia uwanjani kuinyonya damu ya Nguzu.
Mchezo huu wa kunguni wale ukawa kikwazo kikubwa kabisa kwake. Lakini hakuwa na yeyote wa kumlaumu kwa sababu alikusudia kujihifadhi katika nyumba ile ambayo lingetokea lolote lile angeweza kupiga ngumi moja pamoja na teke kisha dirisha likahama pahali pake na kuacha njia.
Bughudha hii ikamnyanyua mpaka nje, akazurura huku na kule pasi na uelekeo maalumu.
Katika kuzurura huku akaona haitakuwa jambo la heri kuzurura huku kichwa chake kingali wazi.
Akafanya tathmini ya muda mfupi huku akijishangaa namna ambavyo yu hai, lakini zaidi zilikuwa ni hisia mpya zinazokisumbua kichwa chake.
Majina mapya na mtazamo mpya katika fikra zake, jina Majenga lilikuwa la kwanza kabisa kujenga naye urafiki.
Sanjari na jina hili kuna ndoto ambazo zimekuwa zikimfuata bila kukoma, mara amuote mama yake mzazi na alipoifuata ndoto ile na kurejea jijini Mwanza anamkuta mama yake akiwa mikononi mwa mtu mbaya.
Anatokwa na pigo moja, pigo lililomwangusha yule bwana moja kwa moja.
Kuhusu lile pigo akajiuliza upya, ni lini amekuwa na uwezo wa kuangusha mtu kwa ngumi moja pekee?
Jibu lilikuwa rahisi sana kuwa hakuwahi kuwa na uwezo huo hapo kabla.
Utata mwingine uliomsumbua ni kuhusu magazeti yaliyoandika kuhusu kifo chake.
Kifo gani? Alijiuliza, lakini swali hili halikumshtua hata kidogo.
Kufa si jambo dogo ujue? alijisemea huku akiendelea kuzurura.
Hata tukio la kukuta pesa katika nguo aliyoianua katika kamba usiku ule baada ya kujinasua katika kifusi katika nyumba iliyokuwa imeanguka bado kilimtatanisha.
"Nani wa kusahau pesa katika nguo ndani ya jiji la Dar es salaam!!" alijisemea na kujikuta akitokwa na tabasamu kubwa sana kulikumbuka jiji lile na vituko vyake.
"Mzee Majenga kuna kitu anapaswa kunieleza, sidhani kama nipo kawaida." aliweka hitimisho lile.
Wakati anarejea katika chumba chake akaanza kumuwaza tena mama yake mzazi.
Nini kinatokea? alijiuliza huku hofu ikianza kumwingia.
Hakutaka kupuuzia hii hisia iliyomjia ghafla, akajiahidi kuwa siku inayofuata atalazimika kurejea jijini Mwanza.
Akarejea katika kile chumba chenye kunguni wapenda sifa. Akajilaza na kusinzia.
Alfajiri ilimkuta barabarani, akadandia gari na kurejea jijini Mwanza.
Ilikuwa kama hisia zake zilivyomuelekeza, alipoingia jijini Mwanza hata kabla hajajikita katika upelelezi wa chinichini akatambua juu ya kamakakamata ya wakazi wa Shamaliwa nje kidogo ya jiji la Mwanza.
Akajipeleka Shamaliwa kuhakikisha tu!
Mama yake alikuwa mojawapo kati ya watu waliokuwa mikononi mwa polisi.
Cheko la hasira likamponyoka, akatembea hadi katika kituo cha mabasi akajiweka katika basi ndogo iliyokuwa inafanya safari zake kuelekea Nyegezi. Akatulia katika nafasi iliyokuwa wazi. Mkononi akiwa na pesa kamili kwa malipo ya nauli ya kutoka Shamaliwa hadi Mabatini.
Alishuka mbali kidogo na kutembea kwa miguu taratibu hadi zilizopokuwa nyumba za polisi. Nyumba zilezile alizoishi pale miaka kadhaa nyuma.
Nyumba zile zikaikamata akili yake, akaukumbuka ule ugomvi kati ya Janeth ambaye baadaye alibadili jina na kuitwa Zubeda jinsi alivyokwidana na mke wa inspekta na mwisho kujikuta akitupwa rumande kwa siku kadhaa.
Kumbukumbu zaidi za kumwandalie binti yule kifungua kinywa zikamfanya ayakumbuke mapenzi yao motomoto baada ya kukutana jijini Dar es salaam huku Zubeda akiwa ni Koplo na yeye akisalia katika nafasi yake ya ukonstebo.
Tabasamu liliunda kibanda katika uso wa Martin, akatembea upesiupesi hadi katika nyumba mojawapo akaitazama kwa sekunde kadhaa, kisha akapita kwa kasi akaelekea nyumba nyingine, hii nayo akaitazama upesi upesi.
Akafanya vivyo hivyo katika nyumba nane. Baada ya kuridhika kuwa alikuwa makini kabisa kwa kila hatua aliyopita katika makazi yale pasi na mtu kumshtukia akaamua kuzua balaa alilopanga kulizua.
Lilikuwa balaa haswa!
 
Back
Top Bottom