Riwaya: Kikosi cha Kisasi

Riwaya: Kikosi cha Kisasi

Arusha vitabu kama hiv hupatikana wapi?
Kuna bookshop ilikuwa ktkt ya mji barabara ya Goliondoi ilipo bank M..ila cjui walihamia wapi ndio nilikuwa naona hivyo vitabu..mi ninacho cha njama ila baadhi ya kurasa hazipo.
 
MAUAJI YA KISHENZI

VI

Ilikuwa saa tatu na dakika kumi Willy alipowasili nyumbani kwa Robert. Alipoingia ndani alikuta wenzake wote wako tayari na wanamsubiri kwa hamu. Kule kuingia tu wenzake walijua jambo kubwa lilikuwa limetokea kwani sura yake ilikuwa imebadilika kabisa na kwenye bega shati lake lilikuwa na damu. Aliondoka akiwa amevaa suti lakini sasa alikuwa hakuvaa koti na wala tai hii yote ilidhihirisha kuwa huko alikokuwa mambo yalikuwa yamechafuka. Wote walikaa kimya huku wanamwangalia. Willy alienda akaketi kwenye kochi na Robert akamletea glasi ya whisky. Willy alianza kuwasilimulia kwa kinaganaga mambo yote yaliyokuwa yametokea toka alipoondoka mpaka wakati huo alipokuwa amerudi.

"Hii ina maana kuwa kuna chama au kikundi kinachoitwa White Power. Tukigundua kikundi hiki ni kikundi gani na kina madhumuni gani, na kwa nini kinaua ndugu zetu wapigania uhuru basi kazi yetu itakuwa imekamilika," Willy aliwaambia. Wenzake waliokuwa wanamsikiliza kwa makini, walionyesha sura ya masikitiko sana.

"Ingawa nilikuwa sijamwona Mwadi, nimehudhunishwa sana na tukio hili," alisema Kofi. Ozu na Robert nao walitingisha vichwa kuonyesha kuwa na wao walisikitishwa sana na mauaji haya ya kishenzi.

"Kama nilivyofikiria toka mwanzo baada ya kufanya upelelezi wangu kuwa kampuni yoyote iliyokuwa inawakilisha maslahi ya makaburu kiuchumi lazima itakuwa inashughulikia na maslahi mengine ya kisiasa kwa makaburu, sasa naanza kuona mwanga kabisa kwa haya magereji na hii kampuni ya wakala ya Sozidime ni ofisi za kijasusi za makaburu wanazozitumia huku wakidanganya watu kuwa zinashughulikia biashara. Kama Kofi alivyoeleza, nakubaliana naye kuwa watu wenye magereji haya na kampuni hiyo ni majasusi. Hii ndiyo sababu wameweza kufanya uhalifu mkubwa bila kujulikana kwa sababu wote hawa ni majasusi wa ujuzi wa hali ya juu kiasi cha kwamba idara ya polisi au ya upelelezi ya nchi ya Kiafrika ni vigumu kuwagundua. Hivyo hii habari ya watu hawa kuwa na gereji ni geresha tu ya kuficha shughuli zao hasa," alisema Robert kwa kirefu.

"Nafikiri ingekuwa rahisi kwetu kukikabili kikundi hiki cha 'WP' kama serikali ya Zaire ingekuwa inajua tuko hapa kwa sababu ya shughuli hiyo. Maana najua kuanzia sasa lazima tuwe macho maana tunaweza tukajikuta mikononi mwa polisi kabla hatujatekeleza shughuli yenyewe," alisema Ozu.

"Maneno yako ni sawa, lakini tatizo tulilonalo ni kwamba msimamo wa serikali ya Zaire juu ya jambo kama hili haujulikani bado. Nafikiri hii ndiyo sababu tumetumwa hapa kisiri kwa sababu ofisi inayoshughulikia jambo hili nayo haijawa na uhakika na msimamo wa serikali ya Zaire. Lakini hata hivyo inabidi itabidi Robert amwambie Chifu juu ya matatizo tunayoweza kuyakabili kama serikali ya Zaire haitakuwa na habari yoyote kuhusu sisi. Uamzi atakatoa ndiyo huo tutaufuata, kwa sasa hivi sisi tuendelee na shughuli hizi kisiri kama tulivyoagizwa," alifafanua Willy.

"Sisi tuko tayari kwenda huko "GAD GARAGE' kama tulivyokuwa tumepanga nafikiri kazi uliyoifanya kwa leo imetosha, wewe baki sisi twende," Ozu alimshauri Willy.

"Hata kidogo, kazi tunayoenda kuifanya ni ngumu, hivi lazima twende wote ila Robert itambidi abaki", Willy alieleza.

"Hapana, na mimi lazima niende, lazima na mimi nipewe nafasi ya kupambana na watu hawa." Robert alilalamika.

"Si hivyo, shughuli hii ni kubwa hivi hatuwezi kwenda wote kwa pamoja, tutakuwa tunafanya mchezo. Kwanza wewe ni mtu ambaye huwezi kukisiwa kwa jambo lolote ovu na mtu yeyote hivyo lazima ubaki kama akiba yetu kwa wakati mbaya zaidi. Vile vile itabidi ubaki ili uweze kuzungumza na ofisi yetu ya Lusaka, kusudi uweze kuwaeleza yote yaliyotokea vile vile wakueleze kama wana habari zozote," Willy alimweleza.

"Sawa kabisa, lazima Robert abaki," Ozu alikubaliana na Willy.

"Na mimi nakubaliana na nyinyi kabisa, lazima Robert abaki kwa usalama wetu baadaye," Kofi alimuunga mkono.

"Haya wengi wape", alijibu Robert kwa masikitiko.

"Wewe ni balozi bwana tuachie sisi huu unyama", Ozu alimtania.

"Nimeishiwa risasi, Robert nisaidie," Willy aliomba.

Robert aliingia chumbani na kurudi na pakiti mbili za risasi. Willy alijaza bastola yake halafu akawauliza kama wenziwe walikuwa wanahitaji nao.

"Sisi tuko tayari kabisa", Ozu alijibu. Kofi alionyesha bastola zake mbili alizokuwa ameisha zijaza risasi tayari. Willy aliwagawia wenzake risasi za akiba. Roberti alimletea Willy shati la kubadilisha. baada ya hapo wakaondoka kuelekea 'GARAGE GAD' inaendelea
 
MAUAJI YA KISHENZI

VII

Saa hizi saa tatu za usiku, Pierre alikuwa nyumbani kwake akingojea kwa hamu kupata maelezo kamili, juu ya msako uliokuwa ukiendelea. Alikuwa ameishapata ripoti kutoka kwa Muteba, kuhusu maelezo waliyokuwa wameyapata toka kwa Tete juu ya Willy. Vile vile alimweleza kuwa Kabaya alipokwenda kumwona Mwadi alihisi kuwa Mwadi alikuwa anajua mengi juu ya Willy lakini hakutaka kueleza hivi Kabeya akamuua.

"Ni dhahiri kuwa huyu Willy ni mpelelezi, mmoja wa wale wengine, kwa hivi katika msako wetu na yeye yumo," Muteba alikuwa amemweleza. Akiwa anangojea ripoti wa Pierre alikuwa na wasiwasi sana juu ya wapelelezi hawa. Mara simu ililia akainua haraka haraka.

"Hallo," aliita.

"Patron, Muteba hapa, kumetokea mauaji mengine kwa upande wetu. Kabeya, Charles na Ngoma wameuawa. Bila shaka wameuawa na huyu Willy." KWa sauti ya utaratibu Pierre aliuliza.

"Unazungumzia wapi?|

"Nipo nyumbani kwa Kabeya".

"Wape habari Jean na Papa kuwa wote njooni tuonane hapa," Pierre aliamru na kukata simu.

ITAENDELEA
 
SURA YA TISA

USIKU WA KAZI

Wakati wanaelekea gereji G.A.D. Willy aliwaeleza wenziwe mpango aliokuwa nao juu ya mashambulizi ya usiku huu. Baada ya mabishano kwenye mambo fulani fulani walikubaliana mpango huo. "Kwa hiyo jamani usiku huu utakuwa ni usiku wa kazi kubwa," Willy alimalizia.

"Tumwombe Mungu." OZu alisema.

"Mungu atatusaidia, maana sisi tunachopigania ni haki za ndugu zetu huko Kusini mwa Afrika na wala hatumuonei mtu," Kofi aliongezea.

Gereji G.A.D. ilikuwa sehemu za Gombe barabara ya T.S.F karibu na stesheni ya Televisheni lakini kwa upande mwingine. Willy alikuwa ameitafuta gereji hii wakati wa mchana na alikuwa ameiangalia kwa uangalifu sana. Basi akiwa anaendesha kwenye hi barabara ya 30 Juin alikata kona na kuingia barabara ya T.S.F. Akiwa anaendesha kwa mwendo wa kawaida alipita mbele ya gereji.

Ozu aliangalia saa yake ilikuwa ni saa nne kasoro. "Bado mapema sana, tungoje mpaka watakapofunga stesheni hapo saa tano," Ozu alishauri.

"Hata mimi naona hivyo maana hata mitaa ya huku bado ina watu, waweza kutuletea kisanga," Willy alisema, Kofi ambaye macho yake na mawazo yake yalikuwa kwenye hilo jengo la G.A.D. aliangalia ingawaje kwa upesi na kuona kuwa kulikuwa na walinzi upande ule wa mbele wa jengo hili.

"Kutakuwa na ulinzi mkali kwenye jengo hilo baada ya tukio la jana," aliwaeleza wenziwe.

"Lazima tutegemee hivyo," alijibu Ozu. Willy alienda mbele kidogo akageuza gari na kurudi huku wakipita kwa kasi sana mbele ya jengo hilo.

"Naona twende Cafe de la Paix tukapoteze muda pale, nadhani ni mahali penye usalama wa kutosha", Willy alishauri.

"Pale ni pazuri sana, tunaweza tukauwa hii saa moja pale bila shida," alijibu Kofi. Cafe de la Pix iko barabara ya 30 Juin. Willy aliendesha gari hadi pale, akaliegesha wakatelemka.

"Tukae kwenye viti vye nje", alisema Willy. Walikaa hapo nje na wakaagiza vinywaji. Kila mmoja wao aliagiza Whiski. Wakati wakiendelea na kinywaji chao Willy alimwita mfanyakazi mmoja aliyepita pale karibu.

"Samahani ndugu naomba kukuuliza", Willy alimwambia.

"Bila samahani", alijibu.

"Unaijua gereji Baninga?"

"Ndiyo".

"Iko wapi?"

"Iko huko sehemu za Kintambo, barabara ya Bangala iko karibu na shule."

"Asante sana nimeelewa", Willy alijibu na yule mtu aliondoka.

Mahali penyewe nimepafahamu sasa nimeishafika pale. Mbele ya ile shule kuna kiwanja cha mpira na gereji hii inatazamana na goli la mwisho kama ukiwa unatokea Kasavubu", alieleza Kofi.

"Basi hamna taabu," alijibu Ozu. Ilipotimia saa tano, waliondoka na kuingia ndani ya gari lao na kuelekea gereji G.A.D. Walipoingia barabara ya T.S.F. waliegesha gari lao karibu na majengo ya stesheni ya Televisheni na wote wakatelemka. Wakati wafanyakazi wa stesheni ya Televisheni walikuwa wamemaliza zamu yao ya saa tano walikuwa wanaishiaishia kuondoka. Kwa hivi kuegesha gari lao wakati ule ilikuwa vigumu kutambulika.

"Mimi na Kofi tutatangulia kuingia ndani. Ozu atatufuata mara tu ukisikia mlio wa bunduki", Willy alieleza.

"Vizuri," alijibu Ozu.

"G.A.D. Gaereji" ilikuwa imejengwa kwa mtindo sawa na 'Garage Papadimtriuo' Willy na Kofi waliamua kuingilia gereji hii kwa kupitia nyuma. Waliingia kwenye uchochoro uliokuwa kati ya nyumba ya pili na ya tatu toka kwenye gereji na kuelekea nyuma ya nyumba hizi na nyumba ya barabara ya pili.

Walitembea kwa tahadhari kubwa, lakini walipofika nyuma ya ngome ya gereji hawakukuta ulinzi wowote.

"Nitatangulia mimi", Kofi alimnong'oneza Willy. Kofi alipanda juu ya mabega ya Willy akashika juu kabisa ya ngome. Aliangaza chini akakuta yuko nyuma ya ofisi kama vile alivyoona kule 'Gereji Papadimitriuos'. Hakukuwa na mlinzi yeyote kitu kilichomshangaza sana. kwani baada ya tukio la jana alitegemea kukuta ulinzi mkali kwenye magereji ya hawa watu. Alipanda juu akajitandaza juu ya ukuta wa ngome kisha akampa Willy mkono wake na kumvuta ili kumsaidia kupanda. Walipokuwa wamepanda wote ukuta walitelemka taratibu na kuangukia ndani ya ngome.

"Kama nyumba hii imejengwa kama ile ya Papadimitriuo, kuna dirisha kubwa kuzidi hili la nyuma kwa upande wa kushoto. Dirisha hili liko kwenye chumba cha mkutano, Tukiweza kupita humo tutakuwa tumeingia ndani ya chumba cha mkutano," Kofi alimnong'oneza Willy.

"Tutajaribu kupitia huko", Willy alijibu.

Walipoenda kwenye pembe ya upande wa kushoto Willy aliona kuna mlango upande ule, na wakati akichungulia mlango huo ulifunguliwa. Alimfanyia ishara Kofi na kumtahadharisha. Watu wapatao sita wakiwa na bunduki kubwa kubwa, walitokea kwenye mlango huu. Willy alishukuru bahati yao nzuri kwani alitambua kuwa walikuwa wamewawahi wakati watu hawa aidha akijitayarisha au wakihutubiwa. Ilionekana watu hawa hawakutegemea shambulio lolote kabla ya saa sita, watu wanne kati ya hawa sita walielekea upande wa mbele wa nyumba na wawili walielekea upande huu wa nyuma ambako Willy na Kofi walikuwa.

"Watu wawili wanakuja huku", Willy alimnong'oneza Kofi. Walijibanza sawa na ukuta kusubiri. Watu hawa bila kujua kuna nini walikuja wanazungumza pole pole. Walipofika kwenye pembe hii ya kwenda nyuma wakasimama wakaweka silaha zao tayari. Kwa sababu hapakuwa na mwanga wa kutosha hawakuweza kuwaona upesi akina Willy kwa namna walivyokuwa wamejibanza kwenye ukuta. Willy alimwacha yule wa mbele akampita kidogo, yule wa pili aliyekuwa anafuata wenzake karibu karibu huku wanaangalia kwenye ngome alimgusa Willy maana alipita karibu sana na ukuta. Kugutuka tu Kofi na Willy waliwashambulia kabla akili zao hazijajua ni nini kinatokea. Kofi alimshambulia yule wa mbele na Willy yule wa nyuma. Watu hawa walipigwa na kuwaua kwa mikoni bila hata kupiga kelele. Pala karibu kulikuwa na gari bovu wakalifungua wakarundika maiti za watu hawa humo ndani zikafichika. Walipoangalia zile bunduki wakakuta ni 'machine gun' ambazo zilikuwa zimeishapakiwa risasi tayari kwa kutumika.

"Loo tumepata silaha, sheria yake", alisema Kofi huku anaipima pima bunduki aliyochukua kutoka kwa yule mtu aliyemuua. Willy naye alichukua ile ya mtu mwingine.

"Nia yangu ni kutaka kuingia ndani, hivyo tutaingilia kwenye mlango huo waliotokea hawa watu", Willy alimnong'oneza Kofi.

"Sawa". KOfi alijibu. Wakiwa sasa wamebeba hizi 'machine gun' tayari tayari walielekea kwenye mlango. Walipofika kwenye ule mlango Wili aliweka sikio kwenye tundu la kuwekea ufunguo wa kufungulia, lakini hakusikia kitu. Alijaribu mlango akakuta umefungwa. Alitoa funguo zake malaya, akafungua kufuli taratibu bila kelele. Wakati huo Kofi alikuwa tayari tayari kwa lolote ambalo lingeweza kutokea. Walifungua mlango, na kuingia ndani na kufunga tena na funguo. Walijikuta wamo kwenye chumba kikubwa ambacho hakikukwa na kitu chochote ndani.

"Nafikiri wanachukulia mazoezi humu." Kofi alisema.

"Nafikiri", Willy alijibu kwa mkato. Walienda na kujaribu mlango mwingine wa kutokea ndani, wakakuta haukufungwa. Willy aliufungua taratibu akachungulia, hakukuwa na mtu ukumbini, akamfanyia Kofi ishara, wakajitokea ukumbini. Chumba kilikuwa kinatazamana na chumba walichokuwa wametoka kilikuwa kimewekwa kibao kilichoandikwa 'MKURUGENZI' Willy alimuonyesha Kofi ishara kuwa alikuwa anataka waingie mle. Willy alijaribu ule mlango akakuta umefungwa, alitoa funguo zake malaya akajaribu tena zikafungua, wakaingia ndani na kujifungia. Kofi alitoa kurunzi ndogo mfukoni akaangaza kwenye meza kubwa iliyokuwemo, mbele ya meza kulikuwa na kibao kilichoandikwa "Jean Vergence" Hiki kibao kiliwafahamisha kuwa hii ofisi ilikuwa ni ya mwenye gereji. Willy alichukua kurunzi kutoka kwa Kofi akaanza kuangaza kwenye ukuta. Nyuma ya kiti kwenye meza hii kulikuwa na kabati la chuma. Willy alifikiria kuwa humo ndani ya hili kabati ndimo kungekuwa na makaratasi ya maana ambayo yangeweza kuwasaidia katika shughuli zao. Alisogelea kabati akaanza kulichunguza kama angeweza kulifungua. Kofi naye alisogea na kuliangalia. Willy alitoa fungu la funguo malaya zikiwemo funguo kadhaa malaya za kufungulia makabati kama haya. Funguo hizi alikuwa amezichukua kwani alitegemea matatizo kama haya. Alijaribu ufunguo wa kwanza lakini haukufungua, alijaribu wa pili nao ulikataa, alipojaribu wa tatu ukafungua. Ndani ya kabati hili la chuma mlikuwa na sanduku dogo la fedha. Willy hakuwa anatafuta hicho hivyo alimulika mle ndani vizuri akaona mlikuwa na saraka ndani. Alivuta akakuta imefungwa alitoa funguo zake malaya tena akaanza kujaribu kufuli la saraka hii, kwa bahati alipojaribu tu mara moja ikafunguka. Alipovuta akakuta mna bahasha moja kubwa akaitoa na kuifungua. Mara akasimama na bahasha yake mkononi.

"Hawa watu wamekwenda wapi?" walisikia mtu anauliza ukumbini.

"Hatujui maana sisi tulikuwa wanne tulioelekea mbele na wenyewe wakaelekea nyuma ya ofisi kama walivyotupanga, sasa hatuelewi imekuwaje..." sauti nyingine ilijibu. Walisikia mlango wa kile chumba walichoingilia unafunguliwa na sauti ikapotea.

"Wanawatafuta, watawaona sasa hivi." Kofi alinong'ona.

"Tuondoke humu", Willy alijibu.

Willy aliweka bahasha aliyokuwa ameichukua vizuri ndani ya shati, akafunga mkanda wake wa suruali sawa sawa, akafungua mlango akiwa 'machine gun' yake ameiweka begani na bastola mkononi tayari kukabiri hatari yoyote. Kofi naye alitoka nyuma ya Willy na kurudisha mlango. Ghafla mlango wa mbele wa nyumba ulifunguliwa na mlango wa kile chumba kikubwa nao ukafunguliwa. Kwa sababu taa ilikuwa inawaka ukumbini wale watu waliofungua milango hii walionana ana kwa ana na Kofi na Willy. Wale watu walizubaa kidogo maana wao hawakutegemea kukutana na mtu yeyote ukumbini. Yule wa mbele alitaka kurudisha mlango lakini Willy aliwahi kumpiga risasi kabla yeye hajaweza kufanya hivyo. Alipoanguka chini bastola yake ilifyatuka na kufanya kelele nyingi. Bastola za akina Willy zilikuwa hazikufanya kelele kwani walikuwa wakitumia sailensa.

Baada ya mlio huu wa bastola, walisikia watu wanakimbia kwa nje. Kusikia hivi wakajua mambo yameiva. Waliweka bastola mifukoni, na kushikilia 'machine gun' vizuri. Kisha wakaruka ndani ya chumba kikubwa, wakasubiri kwani walisikia nyayo zikija, kwa upande wa mlango wa kutokea nje wa chumba hiki. Mara mlango ukafunguliwa kwa teke na risasi zikamiminika ndani ya chumba hiki, wao wakabana kabisa kwenye ukuta. Yule mtu aliyekuwa anamimina risasi alipohakikisha kwamba hakuna mtu, aliingia ndani na hapo ndipo alishambuliwa na Kofi aliyemwauza kwa risasi. Walipokwisha kufanya hivi walitoka nje kwa kutokea mlango walioingilia pembeni mwa nyumba hii. Kofi aliekea nyuma na Willy akaelekea mbele ya nyumba hii. Wakaanza mashambulizi thabiti.

Ozu aliyekuwa amejificha kwenye uchochoro mmoja karibu na gereji hii, aliposikia mlio tu wa bunduki alijua kuwa kazi imeanza. Alikimbia mpaka kwenye lango la mbele, na kama alivyofikiria alikuta walinzi waliokuwa pale mlangoni wanakimbilia ndani kufuata mlio wa bunduki ulikotokea. Hivi hakupata upinzani wa aina yoyote pale langoni, kwa bahati alikuta lango limerudishwa tu bila kufungwa. Alisukuma lile lango na kuingia ndani, huku akiwa amejikinga mwenye magari mabovu akielekea kule kwenye ofisi ambako ndiko kulikuwa kunatokea milio ya bunduki.

Masamba ambaye ndiye alikuwa ameachiwa jukumu la kulinda gereji hii wakati Jean ameondoka alijikuta katika wakati mgumu sana. Alikuwa ameachiwa walinzi sita wakiwemo wapiganaji bunduki sita hodari sana. Yeye mwenyewe alikuwa muuaji hodari wa 'WP'. Na kazi hii alikuwa ameitekeleza vizuri kabisa kila alipokuwa ameamriwa kufanya. Akiwa katika ofisi yake, na huku akisikia mapigano yanaendelea huko nje, aliinua 'machine gun' yake na akachukua bastola mbili akaondoka tayari kwa kusaidia walinzi wake kwenye uwanja wa mapambano. Willy na Kofi walikuwa wamewazingira walinzi wa gereji hii. Ilikuwa rahisi kwao kuwazingira kwani walinzi hawa walikuwa wamekimbilia kule mlio wa bunduki ulikuwa bila kwunza kuangalia mambo yanakwendaje. Walitupiana risasi na Kofi kwa upande ule wa nyuma ya ofisi. Willy ambaye aliwaingilia kwa kutokea mbele hawakumuona, wao walifikiria wako kule risasi zilikokuwa zinatokea tu.

Willy alitambaa juu huku akiwa amezuiwa na magari haya mavovu. Kofi aliendelea kijibishana risasi na hawa watu ili kumpta nafasi Willy kuwashambulia kwa nyuma bila wao kutambua. Willy alipofika karibu kabisa nao, aliweza kuona jinsi walivyokuwa wamejipanga. Alitoa bastola yake na kuwapiga walinzi wawili risasi waliokuwa karibu naye. Kwa sababu bastola yake ilikuwa na sailensa wale walinzi wengine hawakutambua maana kulikuwa na giza. Akasogea tena mpaka akawakaribia wengine wawili nao akawapiga risasi, mmoja wao haikumpata vizuri hivi akageunza na kuanza kupiga risasi upande ule wa Willy alikokuwa lakini Willy alimuwahi na kummaliza. Tukio hili ndilo liliwafahamisha walinzi waliokuwa wamebaki kuwa walikuwa wameishaingiliwa kwa nyuma. Kwa hofu walianza kupiga risasi hovyo hii ikampa nafasi Kofi kutoka kwenye kona aliyokuwa amejibanza na kushambulia watu hawa kwa 'machine gun'. Wawili kati ya walinzi hawa waliuawa, na mmoja alitupa silaha yake akakimbilia mwenyewe magari kuelekea mlangoni.

Willy walikutana na Kofi na kujibanza kwenye gari moja.

"Naona tumewamaliza", alidai Kofi.

"Sina uhakika", alijibu Willy.

Ozu aiyekuwa anatafuta mlio wa bunduki taratibu na kwa tahadhari kubwa alijigonga kwenye kitu. Alipoangalia amejigonga kwenye nini, akakuta ni mdomo wa tanki la petroli, linalopeleka petrol ndani ya gereji. Mara mawazo yake yakashituliwa kwani aliona mlango wa mbele unafunguliwa. Aliona mtu anachungulia kwa uangalifu sana halafu akatokeza akiwa ameshikilia bunduki yake tayari. Ozu aliona huyo si Kofi wala Willy, hivi akamwendea. Alichukua jiwe akalitupa nyuma ya huyu mtu. Mtu huyu aligeuka kama umeme huku akimimina risasi. Ozu alichukua nafasi hii akampiga risasi ambayo ilimpata huyu mtu kwenye bega, akatupa bunduki yake na kuruka wakati huo huo nyuma ya gari mojawapo, Masamba alijua huu ndiyo mwisho wa maisha yake. Hakujua mtu aliyekuwa amempiga risasi alikuwa amepiga kutokea sehemu gani. Alifikiria kukimbia lakini akaona hakuna njia ya kutoka sehemu hii, hivi aliamua apigane na watu hawa mpaka mwisho wake.

"Lazima Ozu ameingia unasikia mlio huo," Kofi alimnong'oneza Willy.

"Kumbe bado kuna walinzi, wewe zunguka ulikotokea, mimi nitarudi nilikotokea. Ukifika kwenye pembe ya nyuma na ya upande wa kushoto piga risasi, hii itanipa mimi nafasi ya kuwaingia watu hawa kumsaidia Ozu," Willy alieleza. Ozu alijua amempiga yule mtu risasi, lakini haikuwa imemuingia sana kwa kutokana na yule mtu alivyoruka baada ya kupigwa risasi. Ilimdhihirishia Ozu kuwa mtu huyu alikuwa ni hodari, hivi alikata shauri amwendee kwa pupa. Mara alisikia risasi zinalia upande aliokuwa ameangukia huyu mtu. Hii ikampa nafasi Ozu na Willy kujua mtu huyu alikuwa wapi. Ozu alipiga risasi mahali pale ambako Masamba alikuwa . Masamba alijiviringisha kutoka mahali pale lakini Willy akamuona na kumwachia risasi chungu nzima, na kumuua pale pale. Baada ya hapo kila mmoja wao alijibanza kukawa kimya. Ozu alipiga mluzi ambao ulikuwa ni wa kujijulisha. Willy alijibu halafu Ozu akabibu walisubiri tena kidogo kuhakikisha kuwa hakuna mtu mwingine ndipo wakapigiana mluzi wa kuondoka. Wakati wanakutanika mbele ya ofisi hii ndipo waliona yule mlinzi mmoja aliyekuwa ametupa bunduki yake na kukimbia akipitia kwenye lango na kukimbia nje.

"Huyo mmoja amewahi kutoroka", Ozu aliwaonyesha.

"Tuondoke hapa, maana polisi au kundi la watu hawa linaweza kufika wakati wowote", Willy alishauri.

"Pale mbele nimeona mahali ambapo tanki ya petrol lilipochimbuliwa, mnaonaje tukilipua gereji isionekane tena kabisa?" Alieleza Ozu.

"Wazo zuri sana, hakika tukilipua gereji hii tutakuwa tumebomoa kambi moja ya hawa wadhalimu na kubakiwa na makambi mawili ambayo vile vile itabidi tuyalipue,"alijibu Willy. Ozu alichukua machine gun iliyokuwa imetupwa na Masamba, na haraka haraka wakakimbilia pale kwenye mdomo wa tanki. Mfuniko wa mdomo wa tanki ulikuwa umefungwa na kufuli. Ozu alipiga kufuli kwa risasi likasambaa na akafungua mfuniko wa tanki hili. Tanki lilikuwa limejaa petroli.

"Tangulieni," Ozu aliwashauri. Willy na Kofi walikimbia kwenye uficho na kumwacha Ozu akishughulika. Ozu alichukua kitambaa chake, akakilowanisha ndani ya petroli akachukua kiberiti toka mfukoni kwake, akaenda mbele hatua chache halafu, akakiweka kile kitambaa moto, akakitupa pale kwenye mdomo wa tanki akaondoka mbio. Kufika mlangoni akakuta akina Willy wameshafika ndani ya gari, akarukia na wakaondoka kasi. Walipofika kwenye kona ya T.S.F. na 30 Juin walisimama kidogo kungojea kama mlipuko utatokea au vipi! Lakini waliona gari la polisi linakuja ikabidi waondoke.

"Tunaelekea 'Garage Baninga'... kabla hata Willy hajamaliza kusema, kulitokea mlipuko mkubwa ambao uliitingisha sehemu nzima ya Gombe.

ITAENDELEA
 
Sijawahi kukisoma HUJUMA ingawa nasikia kilizuiwa kusambazwa.Naamini marufuku yake ilishsaisha hasa ukiangalia wakati huu wa kidigital tulionao.Mwenye muswada huo basi anaweza akajipanga akatushushia hapa.Asante.
Hujuma imo humu mbona,itafute utaipata
 
SURA TA TISA

USIKU WA KAZI

II

Yule mlinzi aliyetoroka kutoka ndani ya ile gereji, alikimbia mpaka kwenye kibanda cha simu kilichokuwa karibu. Alipiga simu kwenye nambari ya simu waliyokuwa wamepewa kupiga kama jambo lolote litatokea.

"Hallo," aliita.

"Hallo unasemaje?" Sauti ilijibu.

"G.A.D." alijibu.

"WP", alijibiwa.

"Aha, G.A.D imeshambuliwa tafadhali tumeni msaada upesi sana kama kikosi kizima kinatushambulia," alieleza huku akitetemeka.

"Sawa," alijibiwa na simu ikakatwa. Pierre na wenzake walikuwa wamemaliza mkutano wao uliokuwa umeitishwa usiku ule wakati simu wakati simu ilipolia. Pierre aliinua simu, "Hallo", aliita.

"Patron?" aliulizwa.

"Ndito", alijibu. 'G.A.D. inashambuliwa sasa hivi. Mapambano bado yanaendelea, nimetuma watu wengine kwenda kusaidia kutoka Papadimitriou," alielezwa.

"Vizuri tunakuja," alijibu na kukata simu. "G.A.D. inashambuliwa twendeni", aliwaeleza wenzake kwa kifupi.

"Hapana Patron, wewe baki sisi tutaenda kule hatuwezi kwenda wote", Jean alishauri.

"Ndiyo sisi tutakwenda wewe baki", Papa alikubaliana na Jean

"Mkiwakuta watu hawa tafadhali wauweni kabisa, sina haja ya kuwahoji, wameishafanya ubaya mwingi kiasi cha kuonana nao. Mimi nitawapa muda wa kutangulia halafu nitampigia afisa mmoja wa polisi rafiki yangu kuwa wezi wanashambulia gereji 'G.A.D.", alieleza Pierre. Kisha aliingia ndani ya stoo akatoa bunduki na mabomu ya mikono akawapa hawa wenzake na wakaondoka wakiwa tayari kwa mapambano huko G.A.D.

Ni wakati walipokuwa wanaingia barabara ya Bokasa waliposikia mlipuko mkubwa uliotingisha sehemu nzima ya Gombe. Waliongeza mwendo na walipofika kwenye kona ya barabara ya 30 Juin na T.S.F. ndipo walipotambua kilichokuwa kimetokea kwani, watu wote waliokuwa wanakaa sehemu hiyo walikuwa wanakimbia ovyo kwa hofu. Walipofika sehemu ya 'Gereji G.A.D' ilipokuwa imesimama hawakukuta kitu. Tokea majengo, magari na kila kitu kilichokuwemo ndani ya sehemu ile kiliteketezwa. Nyumba zilizokuwa jirani nazo ziliharibika ingawaje si sana, maana ngome ya gereji ilizisaidia kustahimili mlipuko huu, kwani ngome yote nayo ilianguka.

"Hakika hawa watu ni wanaharamu sana," alisema Jean kwa chuki. Mara wakasikia milio ya magari ya polisi na zimamoto unaelekea sehemu hii.

Walinzi waliokuwa wametokea Gereji Papadimitriou walifika nao wamechelewa.

"Rudini sehemu zenu", Papa alimwelezea kiongozi wa watu hawa. Papa, Muteba na Jean waliingia ndani ya gari lao na kuelekea gereji ya Papadimitriou katika uchunguzi mwingine.
 
SURA YA TISA

USIKU WA KAZI

III

Wakati Willy na wenzake wakielekea gereji Baninga. Kofi aliwaeleza namna gereji ile ilivyokaa maana aliwahi kufika kwenye gereji hii alipokuwa ameharibikiwa na gari, safari moja alipokuwa hapa mjini Kinshasa. "Gereji yenyewe imezungukwa kwa ua wa seng'enge na uwanja wake ni mkubwa kuliko G.A.D. Kuna stesheni ya petroli nje tu ya gereji, na stesheni hii ni mali ya gereji hii. Hivi nina imani kuwa tanki la petroli la stesheni hii litakuwa ndani ya ua wa gereji kwa usalama. Kuna majengo mawili makubwa mojawapo likiwa ni ofisi na moja linatengeneza kivuli cha magari. Kitu kingine cha kufikiria ni kwamba katika sehemu hii ya Kintambo kuna kambi ya jeshi ambayo iko karibu nusu maili kutoka kwenye gereji hii. Nafikiri maelezo haya yatawapa mwanga jinsi gani tutakavyoiingilia gereji hii", alimaliza Kofi.

"Kama ni hivyo, mimi naona ya kwamba uzi uwe ule ule. Tukifika pale mashambulizi yetu yawe ya moja kwa moja. Ozu kazi yake itakuwa kutafuta mdomo wa tanki uko wapi wakati sisi tukipambana na walinzi watakaokuwepo. Ozu akishapata mdomo huu, atapiga risasi hewani kutupa ishara, halafu atafanya kama alivyofanya kule na kuondoka. Shambulizi hili itabidi tulifanye kwa muda mfupi sana ili tusiwape nafasi wanajeshi kutuwahi. Kwani ikiwa watasikia mlio wa bunduki lazima watakuja. Nataka wafike wakati sisi tumeishaondoka," alishauri Willy.

"Hamna taabu silaha tulizonazo zinatosha kabisa kuzuia jeshi zima", alisema Ozu ambaye alikuwa anafurahishwa sana na matukio ya usiku huu. Yeye kama wenzake alipenda sana kashikashi za namna hii. Walipofika barabara ya Bangala walisimamisha gari karibu na shule halafu walichukua silaha zao na kuanza kukiimbilia gereji Baninga. Kila mtu alichukua sehemu yake. Ozu ndiye alikuwa aingie kwa mbele. Kofi kwa nyuma na Willy kwa pembeni. Wote walipokuwa wameshika nafasi zao walingojea Kofi aanze mashambulizi kama walivyokuwa wamepanga.

Kofi aliruka ua wa seng'enge na kutumbukia ndani ya gereji na pale pale akaanza kusambaza risasi. Wale walinzi waliokuwa pale wengine walianza kusinzia. Mara waliposikia mlio wa bunduki walishika bunduki zao na kuanza kukimbia bila mpango. Willy aliruka seng'enge kwa upande wa pembeni na kuanza kushambulia vile vile. Ozu naye aliruka upande wa mbele na kuanza kushambulia vile vile. Walinzi wa hapa waliingiwa na kiwewe maana walisikia mashambulizi yanatoka kila sehemu. Hii iliwafanya waende ovyo na hivi ikawa rahisi kwa Willy na wenzake kuwashambulia. Ozu aliangalia stesheni ya petroli ilipokuwa na akahisi sehemu gani tanki lingeweza kuwa. Huku akiwa anashambulia alienda sehemu ile na kuanza kutafuta. Willy na Kofi walikuwa wanashambulia vizuri sana na walikuwa wameua walinzi wengi. Walinzi waliobaki waliendelea kujihami kwa kupiga risasi mfululizo bila kukoma, ili kuzuia mashambulizi yaliyokuwa yanakuja. Kwa ajili ya kiwewe hawakujua kuwa kwa kufanya hivi wangeweza kumaliza risasi, mkasa ambao walijikuta wamo baada ya muda mfupi. Hivi walianza kukimbia ovyo.

Ozu aliona mdomo wa tanki akapiga risasi hewani. Kisha akaanza kulishambulia kufuli, na baada ya kulisambaza kwa risasi akafungua mdomo wa tanki. Willy na Kofi walisikia ishara hii waliruka na kutoka nje ya ua. Wakati Willy anaruka alimuona mlinzi mmoja naye anaruka ua karibu na yeye, Willy alimfuata na kumkamata. Mara Kofi naye alifika wakamvuta yule mtu na kukimbia naye. Tanki la petroli lilikuwa karibu na seng'enge, hivi Ozu alitafuta tambara akalipata, akalichovya ndani ya petroli, na halafu karuka ua wa seng'enge. Alipofika nje ya seng'enge aliwasha lile tambara moto, akalitupa kwenye mdomo wa tanki lilipokuwa limefunikwa na akaanza kukimbia kule walikoacha gari.

"Tayari", aliwaeleza wenzake ambao walikuwa na mateka wao. Aliingia ndani ya gari wakaondoka. Kazi hii ilikuwa imefanywa kwa dakika nne. "Je huyu mnampeleka wapi?", Ozu aliuliza.

"Atatusaidia kazi moja sasa hivi," Willy alijibu.

"Mbele kidogo kwenye barabara ya Kasavubu baada ya kona ya Kasavubu na barabara ya Bangala kama unaelekea mjini walikuta kibanda cha simu. Willy alisimamisha gari na kumuamuru yule mtu ateremke. Willy, Ozu na yule mtu waliteremka na kumuacha Kofi akiwa ameliwasha gari tayari tayari kwa kuondoka wakati wowote. Walipofika kwenye kibanda cha simu Willy alimweleza mtu huyu, "Kama unataka kuishi nipe nambari za simu ya gereji Papadimitriou. Nikipiga nikiwapata, nitakupa simu uzungumze nao. Waeleze maneno haya. Gereji Baninga imeshambuliwa lakini hawa watu walioshambulia tumepambana nao wakakimbilia hapa shuleni, sasa tumewazingira tunarushiana risasi tunaomba msaada, umeelewa?" Willy alimuuliza.

"Ndiyo", yule mtu alijibu kwa woga. Mtu yule alitoa nambari za simu ya Papadimitriou bila kusita. Willy alipiga na ikapokelewa mara moja akampa yule mtu. Yule mtu alizungumza nao, na baada ya kujitambulisha aliwaeleza maneno aliyokuwa ameelezwa kusema na Willy, na baada ya kuzungumza tu Willy akakata simu. Halafu akamkata huyu mtu mkono na shingo akaanguka chini akiwa amezirai.

"Twenze zetu sasa gereji Papadimitriou," aliwaeleza wenzake huku wakiingia ndani ya gari.

"Ahaa, nimekuelewa sasa kwanini umefanya hivyo. plani nzuri sana," alisema Ozu. Mara wakasikia mlipuko mkubwa mno uliotetemesha sehemu yote hii ya Kintambo.

ITAENDELEA
 
SURA YA TISA

USIKU WA KAZI

IV

Jean, Muteba na Papa walikuwa wanaingia ofisini kwa Papa, ili wafanye mipango ya kuwazuia watu hawa, wakati Lemba mmoja wa wasaidizi wao wakubwa aliyekuwa amebaki baada ya Kabeya, Charles na Masambba, alipowajia. "Tumepata simu kutoka Baninga kwa Mavungu. Anasema Baninga nayo imeshambuliwa lakini wameweza kupambana na watu hawa, na hivi sasa wamewazingira pale shuleni wanaomba msaada kwani mapigano makali yanaendelea".

"Kazi nzuri, twende huko sisi wenyewe, Lemba acha watu wanne tu hapa wengine wote twende mchana hapo sasa ndio mahali pa kufa na kupona", Papa aliamrisha. Wote wakiwa wamebeba silaha zao tayari, waliingia ndani ya magari matatu na kuelekea Kintambo. Bila kujua wakapishana na gari la akina Willy ambalo lilikuwa linaelekea gereji Papadimitriou. Plani ya Willy ilikuwa imefanya kazi.
 
SURA YA TISA

USIKU WA KAZI

V

Magari ya akina Papa yalipopishana na gari la akina Willy, nara moja akina Willy waliyatambua.

"Hao wanakwenda plani yangu imefanya kazi," Willy aliwaeleza wenzake.

"Lo, tuna bahati sana usiku huu", alinena Ozu.

"Hii gereji Papadimitriou iko vipi?" Aliuliza Willy.

"Imejengwa sawa sawa na gereji G.A.D. haina tofauti hata kidogo. Jinsi ulivyoona ndani ya G.A.D ndivyo ilivyo hivyo na Papadimitriou", alieleza Kofi.

"Inabidi tutumie uzi ule ule wa kuyalipua makambi haya. Je kuna petroli stesheni mle ndani?" Aliuliza Willy tena.

"Kama nilivyokwambia petroli stesheni ya Papadimitriou iko ndani kama ile ya G.A.D. na imekaa vile vile. Nafikiri hata mahali tanki lilipochimbiwa litakuwa katika sehemu kama ya kule G.A.D.," Kofi alisisitiza.

"Bila shaka", alizidi kusisitiza Ozu.

"Kama ni hivyo operesheni yetu ni kama kawaida. Hapa napo lazima tufanye haraka kama tulivyofanya kule Baninga, maana watu hawa wakikuta wamedanganywa watarudi kama risasi," alieleza Willy wakati anasimamisha gari lake kwenye kona ya barabara ya Assossa na Kabambare. Kila mtu akiwa amechukua silaha yake kamili kamili walikimbia huku wakiwa wanajificha ndani ya vivuli vya nyumba za jirani.

Wote waliamua kushambulia kutoka kwa nyuma, na kwa vile walikuwa wamepandwa na mori sasa walikuwa wakifurahia shughuli yote hii. Walipandishana ukutani haraka haraka na kutumbukia ndani. Walinzi wote wanne waliokuwa wamebaki hapa walikuwa wako mbele ya ofisi wakielezana walivyokuwa na bahati ya kuachwa kwenda kwenye mapambano na watu hawa watatu.

"Nasikia watu hawa wana ujuzi kweli, kuonana nao ni kutafuta kifo tu, ni watu wasiowezekana," mmoja wao alieleza.

"Mimi leo ndiyo mwisho wangu kwa kazi hii, kesho natoroka moja kwa moja sitarudi," wa pili alieleza. Wote wakacheka bila kujua kuwa wameingiliwa.


"Utaacha pesa zote hizi! mimi niko tayari nipambane na hao watu ili nipate hizi pesa ikiwa nitamaliza mkataba huu hai", mwingine alisema.

Willy na wenzake waligawanyika. Willy alipita upane wa kulia na Kofi na Ozu wakapita upande wa kushoto na kunyatia wakielekea mbele. Walipofika karibu na mbele wote walisikia maneno waliyokuwa hawa walinzi wanazungumza.

Walipokuwa wamefika kabisa kwenye pembe ya kutokea mbele. Willy alijitokeza na kusambaza risasi na Kofi na Ozu wakafanya hivyo vile vile. Walinzi wote wanne waliuawa pale pale.

Bila kupoteza muda walitafuta mahali tanki lilipokuwa limechimbiwa wakapata bila taabu. Ozu alifanya shughuli yake kama kawaida baada ya kufungua mdomo wa tanki, akachovyo kitambaa alichopewa na Kofi ndani ya petroli wakaondoka hatua chache . Ozu akawasha kitambaa akakitupa pale kwenye mdomo wa tanki, na wote wakakimbia na kuondoka pale. Walienda moja kwa moja mpaka kwenye gari lao wakaingia wakawasha moto huku wakingojea mlipuko.

"Haya matanki ya petroli yameturahisishia kazi. Usiku wa leo sintakaa niusahau", alisema Ozu. Mara wakasikia magari yanakuja.

"Hao wanarudi", Willy aliwatahadharisha wenzake. na wakati huo huo mlipuko ukatokea uliotetemesha sehemu nzima ya Lingwala. "Kwa leo kazi hii imetosha twendeni tukapumzike", Willy alishauri.

ITAENDELEA.
Usikuni mwema jamani.samahani kwa iddy kukuingilia majukumu yako ila naomba tuwe pamoja kwa hii story
 
Back
Top Bottom