RIWAYA: Kesho iliyoondoka (Gone Tomorrow)

RIWAYA: Kesho iliyoondoka (Gone Tomorrow)

Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
KUNA YEYOTE ANAYE ENDELEA KUSUBIRIA KAZI HII PEDWA?

KAMA YUPO KILIO CHAKE NA KIU YAKE INAKWENDA KUFUTWA MAANA KUNA FUNUNU KUHUSU KESHO ILIYO ONDOKA.
NI KUPATIKANA IKIWA KATIKA KITABU CHA JARADA GUMU.

HEBU FANYA HIVI
WEKA MAONI YAKO KWANZA ILI TUFAHAMU WALIO TAYARI KUENDELEA KUISOMA RIWAYA HII.
 
2987766_Kesho_iliyo_ondoka_4.jpg
2987766_Kesho_iliyo_ondoka_4.jpg
 
Bila shaka fasihi imeshiba humo,

Ngeli
Tashtiti
Tamathali za semi
ki-ya masharti
vielezi

Mzigo unapatikana wapi tuburudishe akili?
Hakika kazi inao ujazo wa kurasa za kutosha,Maana imesukwa na wasusi wa riwaya za kijasusi .Ni ladha mjarabu mno.Kitabu kinatoka kwa oda maalum lakini wasomaji wa JF hawataachwa na alosto pia wataburudika na harakati hizi hapa hapa jamvini kama kawaida.Maana hapa ni nyumbani na mcheza kwao Utuzwa. AMKENI SASA KESHO ILIYO ONDOKA INARUDI TENA..
 
Hakika kazi inao ujazo wa kurasa za kutosha,Maana imesukwa na wasusi wa riwaya za kijasusi .Ni ladha mjarabu mno.Kitabu kinatoka kwa oda maalum lakini wasomaji wa JF hawataachwa na alosto pia wataburudika na harakati hizi hapa hapa jamvini kama kawaida.Maana hapa ni nyumbani na mcheza kwao Utuzwa. AMKENI SASA KESHO ILIYO ONDOKA INARUDI TENA..
ha ha haa

Mwamba umesuka Aya ikasukika

Swali narejesha kwako, mzigo naupataje?

Ama PM inahusika?
 
ha ha haa

Mwamba umesuka Aya ikasukika

Swali narejesha kwako, mzigo naupataje?

Ama PM inahusika?
Mzigoo utapatikana kwa mfumo wa hardcopy Utaupata kwa oda kwa gharama ya tsh15000.


Unaweza kuweka oda kupitia namba zifuatazo 0763170858.Chiamaro Mokiri

NA 0656353765 Nelson Ntimba.


kumbuka oda ni kwa ajiri ya kitabu cha Hardcopy na utapata kitabu chako baada ya kulipia.

Utaratibu mwingine utatolewa hapa hapa jukwaani. Wale watakao toa oda zao mapema watakutana na nakala yao mapema zaidi .
 
SEHEMU YA SABA



Muda ulikuwa umesonga kwa kasi sana askari yule niliyepaswa kumsubilia kwa mahojiano ili aweze kuwasili.

Muda huo uliwadia kama utani,Maana muda kazi yake siku zote huwa za uhakika.Hata ungojee kidogo ama kwa kitambo kirefu muda ufika kwa usahii.Mbele yangu alikuwa amesimaa mwanaume wa kizungu mwenye nywele za brown akiwa na mikono ya kikakamavu.Muonekano wake ulionyesha ni mtu wa kazi haswa kwa vile alikuwa amejazia mikononi mwake.Sura yake nyekundu iliyo ivia kwa ndani ilionyesha ni mwanaume anaye chomwa na jua haswaa.Mavazi yake ya kiraia hayakuficha uaskari wake maana nimekutana na watu wa namna yake mara nyingi.Maana kazi yangu ilikuwa inanifanya niwe matatani tena nikiwa nahojiwa mara nyingi na watu wenye muonekano kama wa huyu mwanaume.

"Michael Kichaka hili ndilo jina lako la asili ama nakufananisha " Mwanaume huyu wa kizungu ambaye alikuwa ameingia kwenye chumba cha mahojiano alianza maswali yake yasiyo na maana wala uhusiano na tukio lililo tukia muda mfupi ulio kuwa umepita.Lakini sikumjibu wala sikujari kauli hiyo maana askari wa upelelezi dunia nzima wanafanana tabia yao.Maana lengo lake lilikuwa ni kunitia hasira ili nisiwe na ujanja wa kukwepa maswali yake atakayo kuwa ananiuliza.Lakini alikuwa amejidanganya maana hilo wala lisinge nitisha kwa chochote maana nilikuwa ni mtu tofauti kwa wakati huu ambaye alipaswa kuongea naye.



Jambo baya hata zaidi sikuwa mtuhumiwa bali nilikuwa shahidi wa tukio la kutisha ambalo askari huyu alipaswa anisikilize ili apate kufahamu."Mbona unatabasam tangu naanza kuongea bwana Kichaka nimejikojolea nini?”

Huku akijiangalia kwenye zipu yake lakini hii ilikuwa ni aina yake ya kuyarudisha mazungumzo aliyo kuwa ameyapoteza kwa ukali wake wa kiaskari.



Nami niliamua nisiendelee kumfanya mjinga wacha nijishushe ili twende sawa katika mambo anayo hitaji kunihoji.Maana ratiba yangu kufikia hapo ilikuwa imesha nishika mashati.Hivyo kukaa kwangu kimya kungeniharibia ratiba za kazi muhimu iliyo kuwa imenileta katika jiji hili la New York.

“Naitwa Nickson ni afisa wa kitengo maalum cha kupambana na magaidi.Natumaini unaweza kunielezea kinaga ubaga mambo ambayo umeyaona kwa abiria mwenzako ambaye amejilipua na bunduki.Maana tumepata mambo ya ziada katika mwili wake baada ya kuufanyia uchunguzi wa daktari.Ndiyo maana tumekuchelewesha katika ratiba zako lakini hizi ni taratibu zetu za kiusalam.”



Je naonekana kama nina uhusiano na huyu mwanamke kwa muonekana afande maana mimi pekee ndiye mliye nishikilia?Kama kuna jambo la ziada nahitaji kufahamishwa mapema maana kukaa mikononi mwenu huwa si vizuri ingawa nyie mnapenda kujihita wana usalama lakini kwetu huwa ni mwiko kukaa na polisi maana huwa hawaaminiki.Hivyo mitaa yetu inawachukia hata kama polisi hajawafanyia jambo baya.



“Je na wewe unamaanisha unawachukia askari kama majirani zako wanavyo wachukia?



Aliniuliza swali lake huku akiwa amenitumbulia macho yanayo onyesha kuna kitu kama nimekigusa moyoni mwake.Nilikuwa nimempatia katika lengo langu ambalo nilipaswa sasa kulitumia kufahamu mengi zaidi.



Nimesema mitaa inawachukia polisi siyo askari maana kila raia ana undugu na askari .Wakati mwingine afande nielewe maana unaweza kunihukum kwa kosa la lugha tata ili hali nipo sahii katika lugha nyingine.Lakini tuachane na hayo ya mitaa na polisi.





Nilikaa vyema kwenye kiti na kujikohoza kidogo ili koo langu likae sawa.Lakini wakati huu huyu Mzungu mwenye nywele za rangi ya Brown akaanza kumakini kufuatilia nyendo zangu.Jambo hili kamwe sikulipenda maana lilikuwa linanisogeza karibuzaidi na hatari ya kuwa na uhusiano na mwanamke huyu aliye jilipua kwa bunduki.Sikuhitaji jambo hilo liwe katika moyo wangu.



Lakini nilipata udadisi kidogo juu ya mambo aliyo kuwa ameyasema kwa makusudi kumhusu mwanamke huyo.Udadisi ni kati ya tabia zangu mbaya ambazo nilikuwa nazo tangu udogo wangu.Hivyo sikuwa na tabia ya kuchukulia mambo madogo kwa udogo kama wengine.Maana kila neno ambalo lingesemwa hapo lingekuwa faida ama hasara kwangu kama ningelikuwa napuuzia mambo.Nilijikuta napata hamu ya kufahamu nini wamekipata kwa mwanamke huyo kijana aliye yaacha maisha kwa kujilazimisha.



Kengele ya hatari ilianza kulia kichwani mwangu baada ya kukutanisha macho yangu na huyu askari mwenye nywele za brown.Lakini sikuonyesha mshituko wangu nje maana ningelimpatia nafasi kubwa ya kunitega na maswali ama kizibiti kidogo.

Nilifahamu ananichunguza kama nina uzoefu na mahojiona lakini kama alikuwa na makusudio hayo wakati huu pia alikuwa ameenda mbali zaidi maana somo ambalo nilikuwa nimelifaulu katika ujasusi ni kuficha silika yangu nyuma ya upole na utalatibu.Hivyo nilimuonea huruma kwa mitego yake ya kijinga kujaribu kitumia kwa mjuvi wa mambo ya usalama.Lakini sikujifanya mjuaji ili mazungumzo yaishe haraka kama nilivyo hitaji."Je unahitaji maji ama kahawa maana naona umekauka koo lako?" Aliniuliza huku akipiga hatua hadi kwenye kikabati kidogo na tuanza kuweka kahawa iliyo sindikwa yenye nembo ya bendera ya nchi ya Marekani.Matendo yake yalikuwa ya haraka sana kama mhudumu wa hoteli mwenye uzoefu maana hakusubilia nichague mji wala kahawa bali alikadilia mazingira peke yake.Nilikinyanya kikombe cha kahawa aliyo kuwa ameileta na kuisogeza puani na kuanza kuruhusu harufu yake nzuri ipenye kwenye mianzi ya pua yangu.Hakika kahawa hii ilikuwa ni nzuri kwa kiwango cha kimataifa lakini ilikuwa na zaidi maana niliweza kuisikia ladha ya vanila pia kwa mbali.Ingawa sukari haikuwepo lakini niliupenda uasilia wake wa kimataifa.

Kiasilia mimi ni mpenzi wa kahawa iliyo kaangwa na kusindikwa katika mifuko ya nailoni.Lakini huwa napenda kahawa iliyo chemshwa angalau kwa kiwango cha juu.Kahawa hiyo naiona ya kipekee maana huwa inaleta zaidi ya ladha na hapo ndipo huniburudisha nafsi yangu.



“Unaweza kunijibu maswali yangu sasa maana nitakayo kuuliza bila kukwepesha maana wewe ndiye shahidi wa kwanza wa tukio hili.Kumbuka kama ukijaribu kuficha jambo lolote lile utahusishwa na tukio hili moja kwa moja maana ni tukio lenye utata sana kwa wakati kama huu.”



Maneno yake yalikuwa kama yana kitu ndani yake maana wakati huu msisitizo wake ulikuwa wazi.Niliona sina sababu yeyote ya kumficha ili hali yupo kwa ajiri ya usalama wa nchi na wananchi.***************************************************************************************



“Hivyo unataka kunambia ni hayo tu unayo niambia kuhusu tukio hili, Je unaweza kunieleza ulifamuje kama huyu mwanamke alikuwa na siraha hatari maana ni wewe tu uliye mtambua.Wenzako wote wamesema wewe pekee ndiye uliye kuwa unaongea naye na ndiye alikunyoshea bunduki.Je uliona nini ndani ya begi hilo ambalo unahisi siyo la kawaida?”



Maswali yake mengi yalinifanya nishushe pumzi ndani kwa ndani maana ni kama alikuwa ananisanifu ingawa sikulipa nafasi.



Wewe unasema lakini nilicho kiona nimekwambia naona hiyo inatosha sasa sitosema zaidi maana.Waulize ambao wameona tukio hili kwa umakini zaidi yangu maana wote tulikuwa ni wasafiri.



“Nimemaliza na wewe lakini kama tukikuhitaji tutakutafuta uweze kuisaidia serikari.Kumbuka kuacha anwani zako na namba ya simu hapa kabla ya kuondoka.”



Sina simu wala anwani kwa sasa hivyo naomba niondoke maana hilo ndilo pekee nimebakiwa nalo kati ya maombi yako uliyo niomba niyafanye.



“Kwa nini huna simu kwa sasa wala anwani unajaribu kuficha nini?

Maana kuishi bila simu inaonyesha wewe ni mtu asiye na mahusino na wengine ama wewe ni gaidi unajaribu kujificha.”



Alionyesha mshituko kwa kuona sina simu wala anwani yeyote ile.Lakini mimi sikujari zaidi nilichukua vifaa vyangu na begi langu dogo ambalo nilikuwa nimelikabidhi wakati naingia kwenye kituo hiki kwa ajiri ya mahojiano.Wakati namalizia kukusanya vifaa vyangu nilimuona akichukua simu yake ya kisasa ambayo kwa haraka sikufahamu inatengenezwa na kampuni gani.Lakini ni kati ya simu maalum kwa watu maaluum hasa wanao fanya kazi za siri katika serikali ndiyo huwa nazo.



Simu ya satilate ndiyo ilikuwa imebebwa na mwanaume huyu na alionyesha alikuwa ananipiga picha lakini alijifanya hana mpango na mimi.



Mawazo mabaya ya kuuzwa yalianza kukitawala kichwa changu maana siyo kawaida kumuona askari wa kawaida na simu ya Satilaiti.Hapa kutakuwa na la ziada siyo bure maana hii siyo kawaida.Lakini sikutaka kuyapa nafasi mawazo hayo maana yangeliniharibia siku.



Tayari nilikuwa huru hivyo sikuona sababu ya kuendelea kubaki mahali ambapo wengi upaona salama lakini kwangu hapo ndipo mahali.
 
Mpelelezi aliyekuja alikuwa ni mwanamke na alikuja akiwa peke yake. Alikuwa amevaa shati la kijivu la mikono mifupi na suruali. Alikuwa hajachomekea na nilihisi ni kwasababu sehemu ya shati iliyoning’inia ilikuwa ni kwaajii ya kuficha bunduki, pingu au chochote kile alichokuwa amebeba. Alikuwa na uso wa mviringo uliojaa nywele. Hakuwa amevaa urembo wowote. Hata pete tu hakuwa nayo. Nilikadiria umri wake kuwa kwenye miaka ya thelathini na tano kupanda juu. Labda arobaini mwisho. Alikuwa ni mwanamke wa kuvutia. Nilivutiwa naye mara tu nilipomuona. Alinionesha kitambulisho chake. Kilikuwa kina namba za ofisini kwake na namba yake ya simu. Kilikuwa pia kina barua pepe yake. Alilitamka jina lililokuwa kwenye kadi yake hiyo. Jina lenyewe lilikuwa ni Theresa Lee. Alikuwa na asili ya Asia. Nilihisi kutokana na jina lake la Lee.

Alianza kuongea, “Unaweza kuniambia ni nini haswa kilichotokea?”

Aliongea kwa sauti ya upole, huku akiwa kaziinua kope zake. Unaweza kuniambia? Unaweza? Kama vile, unaweza kustahimili kuniambia? Nilitabasamu, kidogo. Katikati ya New york ni sehemu ambayo mauaji yapo kwa asilimia chache sana. Na hata kama Theresa alikuwa ameshuhudia kesi za mauaji tangu siku ya kwanza alipoingia ofisini, bado nilikuwa namzidi kuona maiti kwa wingi. Tena kwa idadi kubwa tu. Na kusema kweli yule mwanamke kwenye treni sio kwamba maiti yake ilikuwa imeharibika sana, hapana. Nilikuwa nimeona maiti zenye kutisha kuliko ile.

Kwahivyo nilimwambia kila kilichotokea, kuanzia kule mtaa wa Bleecker, kuja zile pointi kumi na moja, namna nilivyojaribu kuokoa jahazi, yale maongezi, bunduki na hatiame kujiua kwa yule mwanamke.

Theresa Lee akataka tuiongelee orodha ya zile pointi kumi na moja.

“Tunayo hiyo orodha,” Alianza kusema. “Ninadhani inapaswa kuwa siri.”

“Imekuwa wazi takribani miaka ishirini sasa,” Nilimwambia. “Kila mtu anaijua. Sio siri tena.”

“Wewe uliionea wapi?”

“Israeli,” Nilijibu na kuongeza. “Kipindi ambacho imemalizwa tu kuandikawa.”

“Inawezekana vipi”

Kwahivyo nikaanza kumtajia historia yangu. Kwa ufupi. Jeshi la marekani, miaka kumi na tatu ya polisi wa wanajeshi, kuwa kwenye kitengo cha uchunguzi, huduma niliyofanya karibu ulimwengu mzima, jumlisha vikazi vya hapa na pale hadi pale nilipopunguzwa na jeshi.

“Ulikuwa afisa tu au cheo gani?”

“Cheo kikubwa cha Meja.” Niijibu.

“Na sasa hivi unafanya nini?”

“Nimestaafu.”

“Mbona umri wako bado sana.”

“Niliamua nile maisha nikiwa bado kijana.”

“Na unahisi unakula maisha kweli?”

“Sio sana.”

“Na jana usiku ulikuwa unafanya nini? Huko Bleecker?”

“Nilienda kusikiliza muziki.”

“Na ulipopanda treni ulikuwa unaelekea wapi?”

“Nilikuwa naenda kutafuta chumba mahali popote au labda ningeenda kuchukua basi.”

“Uende wapi?”

“Popote.”

“Kama utalii au?”

“Ndiyo.”

“Kwani unaishi wapi?”

“Siishi popote. Mimi naenda popote nitakapotaka.”

“Begi lako liko wapi?”

“Sina begi.”

Watu wengi wakifika hapo huwa wananiuliza maswali yasiyo na msingi, Lakini Theresa hakuniuliza. Baadala yake macho yake yalibadilika na akabadilisha mada, “Ninashangaa kuona orodha ilikuwa haipo sahihi. Nilidhani ilitakiwa kuwa asilimia miamoja sahihi.”

Aliongea kwa kuniaminia. Kama vile ambavyo askari mmoja angeongea na askari mwenzie.

“Ilikuwa haiko sawa kwa sehemu ndogo tu, lakini kwenye kujiua ilikuwa ipo sawa.” Nilijibu.

“Ni kweli, lakini ilikuwa ukweli nusu tu.”

“Ni bora ukweli nusu kuliko uongo mtupu.” Nilijibu halafu nikaongeza swali. “Mmekwishafahamu chochote kuhusu huyo mwanamke?”

“Bado. Lakini tutapata chochote muda sio mrefu. Wananiambia kwenye tukio wamepata funguo na waleti. Naamini vitatoa mwanga. Lakini kuna kitu bado sielewi kwanini alivaa koti.”

Nilisema, “Mimi pia sijui.”

Theresa alikaa kimya, kama aliyekwazika. Nilianza kuongea, “Haya mambo kila siku yanatakiwa kufanyiwa mamboresho. Binafsi nahisi tuongeze pointi ya kumi na mbili kwa wanawake.”

“Wazo zuri.”

“Na kuna kitabu nilisoma kinasema kuwa ile sehemu kuhusu kukuta bikra mbinguni ni tafsiri iliyokosewa. Inamaanisha ni kitu chenye sukari. Maziwa na asali.”

“Unataka kuniambia wanajilipua kwa sababu ya maziwa na asali?”

“Sina hakika.”

“Wewe ni mtaalamu wa lugha?”

“Hapana! Ila naongea Kiingereza,” Nilisema. “Na kifaransa. Halafu kwanini mwanamke anayejilipua atakake bikra? Unajua maandiko mengi matakatifu yametafsiriwa vibaya. Haswahaswa sehemu ambazo mabikra wamehusishwa. Hata ukiangalia Agano jipya kwa mfano. Kuna watu wanasema Mariam alikuwa ni mama kwa mara ya kwanza, sio bikra. Ninaamini waandishi wakifufuka watacheka sana kuona kilichoandikwa sasa hivi.”

Theresa Lee hakutoa oni lolote. Baadala yake aliuliza, “ Upo sawa?”

Nilichukulia swali lake kama anauliza pengine nilikuwa nahitaji ushauri wa daktari kutokana na nilichokishuhudia. Labda pengine kuongea sana kwangu kulimfanya ahisi nimechanganyikiwa. Lakini nilikuwa nimekosea.

“Nipo sawa,” Nilimwambia.

“Mimi ningekuwa wewe ningekuwa ninajuta sasa hivi kwa kumfuata yule mwanamke. Pengine wewe ndiye ulisababisha kifo chake. Labda ungemuacha angebadilisha maamuzi yake.”

Tulikaa kimya kwa muda baada ya hiyo kauli halafu akatokea askari mwingine aliyetingisha kichwa kumuita Theresa. Waliongea kwa sauti ya chini ambayo sikuweza kung’amua maneno. Theresa alikuja tena na kuniomba niongozane naye kwenye chumba cha mahojiano.

“Kwanini?” Niliuliza.

“Ndiyo utaratibu.” Alinijibu. “Ili tuchukue maelezo yako yachapwe jarada lifungwe.”

“Sina uhuru wa kukubali au kukataa?”

“Usianze ubishi,” Theresa aliniambia. “Kumbuka kuna ile orodha ya pointi kumi na moja na wewe ni shahidi. Tunaweza kuamua kukuweka tu ndani hadi uote mvi na ufe. Kwahivyo usijaribu kuleta usumbufu usio na sababu.”

Niliinua mabega juu na kumfuata hadi kwenye gari yake. Ilikuwa ni Ford Victoria, na uwezo wake lazima nikiri ulikuwa mzuri. Ilitupeleka mpaka kituoni kulipokuwa na hiyo ofisi ya mahojiano. Tuliingia na kupanda ngazi za juu. Tulipokifikia chumba alikifungua na kunipisha niingie ndani kwanza. Alipohakikisha nimeingia aliufunga mlango kwa nje na kuniacha ndani peke yangu. Nilikaa humo peke yangu kwa dakika ishirini hadi Theresa alipoufungua tena mlango.

Awamu hii hakuwa peke yake. Alikuwa amembatana na bwana mmoja hivi aliyekuwa amebeba faili. Aliliweka faili mezani na kumtambuisha yule bwana kama askari mwenzake. Aliniambia jina lake lilikuwa ni Dochery. Aliniambia yule Dochery alikuwa na maswali kadhaa ya kunihoji.

“Maswali yapi?” Niliuliza.

Kwanza akaanza kwa kunipatia kahawa na nitumie bafu kuoga. Nilikubali vyote. Dochery alinisindikiza hadi sehemu ambayo nilitumia kuoga, niliporudi kulikuwa na vikombe vitatu vya kahawa mezani. Nilichukua kikombe kimoja cha kahawa na kukionja. Kahawa ilikuwa ipo poa sana. Theresa na yule Dochery walichukua vikombe viwili vilivyokuwa vimebaki.

“Embu anza tena kusimulia mkasa mzima ulivyokuwa,” Theresa alisema.

Kwahivyo nilianza upya. Ndani ya dakika tano tulianza kulijadili suala zima tena. Kama watu watatu wanaofanya kazi pamoja. Halafu ghafla hali ikabadilika.

Dochery aliuliza, “Ulijisikia vipi?”

Niliuliza, “Nilijisikia vipi kuhusu nini?”

“Kipindi anajiua?”

“Nilifarijika angalau alikuwa haniui mimi.”

Dochery alianza kusema, “Sisi ni kitengo cha mauaji. Lazima tuchunguze chanzo cha kesi yeyote kujua kama kuna utata wowote. Nadhani unaelewa.”

“Utata kama upi?” Niliuliza.

“Tunahakikisha kama hakuna zaidi ya kinachoonekana kwa macho tu.”

“Hakuna zaidi. Alijipiga risasi mwenyewe.”

“Hayo umesema wewe.”

“Hakuna aliyekuwa kwenye ile treni atakuambia tofauti na ninachokuambia.”

Dochery alisema, “Huwa kuna mambomambo hapo katikati.”

“Unanihisi vinginevyo?” Nilisema.

“Ndiyo. Labda wewe ndiye uliyempiga risasi.”

Theresa Lee aliniangalia kwa jicho la huruma. Nikasema, “Sikumuua mimi.”

“Basi labda ilikuwa ni bunduki yako.”

“Haikuwa bunduki yangu. Ile bunduki ni mzigo mkubwa sana na sina begi la kuibebea.”

“Wewe una umbo kubwa la mwili. Suruali yako inaweza ikawa na mifuko mikubwa.”

Theresa Lee akanitazama tena kwa jicho la huruma. Kama anayeniambia, pole unapitia haya yote.

“Hiki ni nini? Unajifanya askari mwerevu, au unaonyesha ulivyo askari mjinga?”

“Unasema mimi ni mjinga?”

“Umethibitisha hilo wewe mwenyewe. Kama nilimpiga mimi sasa hivi ningekuwa nimefungwa pingu. Ningekuwa nimechukuliwa alama za vidole na usingenipeleka bafuni kuoga halafu ukabaki nje. Lazima ungekuwa na mimi kila sehemu.”

“Siwezi kufanya hivyo mpaka nithibitishe uliua kweli.”

“Kwani watu wa hospitali wanasemaje?”

“Bado hatujapata taarifa kutoka kwao.”

“Lakini mashahidi wengine walikuwepo.”

Theresa alitikisa kichwa kukataa, “Hawana msaada wowote. Hawakuona kilichotokea.”

“Lazima waliona.” Nilisema.

“Mgongo wako ulikuwa umewakinga. Halafu, walikuwa hata hawaangalii kinachoendelea. Halafu wengi wao walikuwa wamesinzia na hawajui hata Kiingereza. Kwahivyo maelezo yao yalikuwa hayana msaada wowote.”

“Na yule jamaa fulani aliyekuwa mbele yangu. Mbona alikuwa macho. Na alionekana kama raia wa Marekani na anajua Kiingereza?”

“Jamaa yupi?”

“Alikuwa abiria namba tano. Alikuwa kavaa chinos na tisheti ya golfu.”

Theresa alilifungua faili lake. Alipopitisha mach akatikisa kichwa kidogo. “Hakuna abiria wa tano. Treni ilikuwa na abiria wanne tu, ukiweka na huyo mwanamke.!”
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom