RIWAYA: Kesho iliyoondoka (Gone Tomorrow)

Chachasteven

JF-Expert Member
Jul 4, 2014
1,878
1,849
Angalizo: Kabla ya kuanza nitoe angalizo na maoni kidogo. Ila pia nianze kwa kuomba samahani kukatisha riwaya iliyopita kwa wale ambao mlikuwa mnaifuatilia uwanja wa mauaji.

Sababu ni nyingi na siwezi kuzitaja zote!! Ieleweka tu, Uwanja wa mauaji haitaweza kuendelea na ndiyo maana ili kulipa na kuonesha ninajali nimeamua, kwa moyo mmoja, kuwaletea hii nyingine.

Sehemu ya kwanza itakuwa hewani usiku ambapo nitafuta haya maelezo. Halafu kuanzia kesho asubuhi nitaweka sehemu mbili mbili.

Yaani moja asububi na nyingine jioni. Ahsanteni kwa kunielewa.

SEHEMU YA KWANZA (Post ya nne) : RIWAYA: Kesho iliyoondoka (Gone Tomorrow)
 
SEHEMU YA KWANZA

Kumgundua mtu anayetaka kufanya shambulio kwa kujilipua ni rahisi sana. Huwa wanaonesha dalili zote ambazo kwazo unaweza kuelewa nia yao. Lakini zaidi ni kwa sababu ya uoga unaojichora juu ya nyuso zao. Kwa tafsiri nyepesi, huwa wanakuwa kwenye taharuki.

Shirika la ujasusi la Israel liliandika kitabu cha kuwagundua na kujilinda dhidi yao. Walituambia nini cha kuangalia. Walitumia kanuni ya uchunguzi wa vitendo na kuelewa saikolojia, ndiyo wakaunda orodha ya viashiria vya tabia za washambuliaji wa kujilipua. Nilijifunza orodha hio kutoka kwa kapteni wa jeshi la Israel miaka kumi iliyopita. Alikuwa anaiamini. Hivyo na mimi nilikuwa naiamini. Na kwa sababu wakati huo nilikuwa kwenye majukumu si mbali na yeye, niliona pointi za kwenye hio orodha zikifanya kazi Israeli penyewe haswa Jerusalem, na ukanda wa Magharibi kuanzia Lebanon huko, Wakati mwingine Syria au hata Jordan kwenye mabasi, ndani ya maduka na mabarabarani palipokuwa na mikusanyiko wa watu wengi. Wakati huo macho yangu yalikuwa yakitembea na akili yangu ikikimbia kuona kama nitathibitisha orodha ya hizo pointi kwa mtu yeyote.

Miaka kumi imepita tokea kipindi hicho, lakini bado naijua vyema orodha ya viashiria hivyo vya tabia za mtu anayetaka kujitoa mhanga. Macho yangu pia bado yanatembea. Tabia ambayo tokea nilipojifunza siwezi kuiacha. Lakini pia nilijifunza kanuni muhimu sana kutoka kwa jamaa fulani wakati wa utumishi wangu jeshini: Ona. Usiishie kuangalia. Elewa. Usiishie kusikiliza tu. Kadri unavyoitumia hii kanuni, ndivyo unavyozidi kuendelea kubaki hai kwenye uso wa dunia.

Orodha yenyewe ina pointi kumi na mbili kama mtu unaemshuku ni mwanaume. Pointi kumi na moja, kama unaemshuku ni mwanamke. Tofauti kwenye hizi pointi ni kuwa wanaume huwa wananyoa ndevu zao. Hii inawasaidia kutotiliwa mashaka au kutozua tashwishi mbele ya watu. Matokeo yake nusu ya ngozi ya uso wa chini hubadilika rangi na kuwa hafifu kidogo, kwa sababu unakuta hawajajianika kwenye jua kwa muda mrefu tokea siku ya kunyoa.

Lakini leo sikuwa na haja na mtu aliyetoka kukata ndevu zake siku sio nyingi au muda mrefu.

Nilikuwa nafanyia kazi orodha ya pointi kumi na moja. Mtu niliyekuwa namshuku alikuwa ni mwanamke!

Nilikuwa nimepanda kwenye gari moshi za chini ya ardhi za jiji la New York nikielekea ukanda wa juu. Ilikuwa ni saa nane za usiku! Nilipanda gari hilo kuanzia mtaa wa Bleeker ambapo lilikuwa wazi isipokuwa watu watano tu ndiyo walikuwa ndani yake. Gari moshi huwa zinakuwa ndogo sana zikiwa zimejaa. Zikiwa hazijajaa zinakuwa kubwa, pweke na tupu sana. Taa zake pia huwa zina joto kali na zinaumiza macho ukiziangalia nyakati za usiku ingawa ni zile zile ambazo zinatumika na mchana.

Nilipoingia ndani nilijivuta hadi kwenye siti ya pili kutoka mwisho upande wa dirisha la gari kwa nyuma. Abiria wengine wote walikuwa mbele yangu hivyo niliweza kuwaona vizuri. Watatu walikuwa wamekaa mkono wangu wa kushoto na wawili mkono wa kulia.

Namba za gari nililokuwa nimepanda ilikuwa ni 7622. Modeli yake ilikuwa ni R142A. Ilikuwa ni tolea la zamani ila mpya kwenye sistimu ya New York. Ilitengenezwa Kawasaki huko Kobe, Japan. Halafu ikasafirishwa na meli hadi mtaa wa 207 ambapo ilifungwa na kuingia barabarani. Nilijua pia inao uwezo wa kutembea maili zaidi ya mia mbili bila tatizo lolote. Pia nilikuwa najua kuhusu mfumo wake wa automatiki kwenye matangazo, ambapo ilitoa maagizo kwa sauti ya mwanaume na maelekezo kwa sauti ya mwanamke. Hii ilitokana na imani ya wamiliki kuwa kwa kufanya hivyo wanaondoa dhana ya unyanyasaji wa kijinsia kisaikolojia. Lakini pia nilijua kuwa gari za aina hiyo zilikuwa zimetengenezwa na uwezo wa kubeba abiria wasiozidi arobaini wakiwa wamekaa na abiria 148 waliosimama. Pia kwenye gari moshi hiyo kulikuwa na matangazo mengi ya jeshi la polisi, lakini lililokamata akili yangu zaidi ni lile lililosema: Ukiona Jambo ambalo siyo la kawaida, toa taarifa.

Abiria aliyekuwa amekaa karibu na mimi alionekana kuwa mhispania. Alikuwa ni mwanamke, aliyekaa mkono wa kushoto, mbele karibu na mlango. Alikuwa mdogo, umri kati ya miaka 30 hadi hamsini, na kimuonekanao alikuwa na uchovu mwingi uliokuwa umemvaa. Alikuwa kaning’iniza mkoba kwenye mkono wake na sidhani kama macho yake yalikuwa yanaona kitu. Alikuwa kasinzia.

Mbele yake kidogo alikuwa kakaa jamaa fulani. Yeye pia alikuwa kakaa peke yake kwenye siti ya watu nane. Nilimkadiria labda ametokea Balkanas kwa sababu ya nywele zake nyeusi tii na ngozi iliyochoka, pengine kutokana na kazi ngumu ambazo anafanya. Alikuwa hajalala ila muonekano wake ulionesha anataka kulala. Alikuwa anayumba na kushtuka kwa usingizi. Umri wake niliukadiria kuwa kati ya miaka hamsini japokuwa alikuwa amevalia nguo ambazo sio za rika lake. Jinsi aina ya “baggy” na tisheti ya NBA iliyokuwa imeandikwa jina la mchezaji ambalo sikuweza kulifahamu kutokana na kukingwa na viti.

Mtu wa tatu alikuwa ni mwanamke pia. Kwa mtazamo alionekana kuwa ni mtu wa Afrika Magharibi. Alikuwa amekaa upande wa kushoto, kusini kati kati mwa mlango. Ngozi yake ilikuwa imepauka kwa vumbi na uchovu. Alikuwa amevaa gauni zuri la batiki ambalo rangi zake zilikuwa za kumeremeta na ziliendana na zile za mtandio aliokuwa amefunga kichwani. Alikuwa amefumba macho yake pia.

Labda nikuambie kitu, Mimi ninaijua New York vyema sana. Naijua kuliko hata wazawa wake. Huwa ninajiita mwananchi wa dunia na bila shaka New York ndio mji mkuu wa dunia, hivyo ninao ujuzi na uelewa mpana sana kuhusu New York kama ambavyo mtanzania alivyo na ujuzi na uelewa mpana kuhusu Dodoma. Au mfaransa alivyo na uelewa kuhusu Paris. Nazifahamu vyema tabia za wakazi wa New York japo sishiriki katika tabia hizo. Na ndiyo maana ilikuwa rahisi kwangu mimi kujua hawa watu watatu waliokuwa wamekaa upande wa kushoto wa gari moshi hili walikuwa ni wafanyakazi, au wasafisha ofisi ambao walikuwa wametoka kwenye zamu zao za usiku wakielekea nyumbani kwaajili ya kupumzisha miili na akili zao kwa masaa machache tu kabla ya kuikabili siku ndefu nyingine iliyokuwa mbele yao.

Abiria wa nne na wa tano walikuwa tofauti.

Abiria wa tano alikuwa ni mwanaume. Umri wake ulikuwa kama wa kwangu, miaka kati ya 45 hadi 46. Alikuwa amekaa kwenye siti ya watu wawili mkono wa kulia kwangu. Alikuwa amevalia kawaida, lakini nguo zake zilikuwa sio za bei ndogo. Suruali aina ya chinos na shati ya golf. Alikuwa macho pia. Macho yake muda wote yalikuwa yameelekezewa sehemu moja muda wote. Alikuwa akiangalia mbele kwa umakini na utulivu mkubwa kama aliyekuwa akiwaza na kupiga hesabu kali za jambo f’lani.

Lakini pamoja na hayo, Abiria namba nne ndiye niliyekuwa nina mashaka naye.
Ukiona jambo ambalo siyo la kawaida, toa taarifa.

Kwanza, alikuwa amekaa upande wa kulia peke yake kwenye siti ambayo ilikuwa maalumu kwaajili ya watu nane. Alikuwa ni mzungu na umri wake niliukadiria kuwa kati ya miaka arobaini hadi arobaini na tisa. Nywele zake zilikuwa zimenyolewa vizuri sana. Alikuwa kavaa nguo nyeusi kuanzia juu hadi chini. Kutokana na sehemu alipokuwa amekaa, nilikuwa namuona vizuri bila kizuizi isipokuwa machuma ambayo yalikuwa mbele yangu ndiyo yalikuwa yananipa ugumu kidogo. Licha ya machuma hayo kutia kizuizi, bado kengele za hatari kwenye kichwa changu ziligonga kwa kasi.

Kwa mujibu wa Shirika la ujasusi la Israeli, nilikuwa namuangalia mshambuliaji wa kujilipua. Mtu ambaye alikuwa anaenda kujitoa muhanga kwa kujilipua bomu!

SEHEMU YA PILI: BOFYA HAPA
 
SEHEMU YA PILI
Ghafla, wazo la kuhisi yule mwanamke wa kizungu alikuwa na lengo la kujitoa muhanga kwa kujilipua lilinitoka. Sio kwa sababu ya ubaguzi wa rangi au imani, hapana. Wanawake wa kizungu wanaweza kupandwa na ukichaa wakati wowote ule kama mtu yeyote yule. Sababu kuu iliyonifanya niondoe wazo langu juu yake ni udhaifu uliokuwepo katika mkakati wake. Ule muda haukuwa sahihi kwaajili ya kufanya shambulizi la kujilipua. Japo ni kweli njia ya chini ya ardhi ya New York ilikuwa ni shabaha nzuri sana kwa mauaji ya aina hio ukihusanisha na gari moshi tulilokuwa tumepanda pia lilikuwa ni shabaha nzuri kwa namna yoyote ile, kwa sababu linasimama likiwa na watu arobaini waliokaa na watu mia na arobaini na nane waliosimama. Hivyo, angesubiri hadi milango ikafunguka, halafu akabonyeza kitufe kuruhusu bomu lilipuke.. Mamia wangekufa na kujeruhiwa. Wengine wangeachwa kwenye mshtuko na taharuki kubwa, au bomu lingeweza kuanzisha moto mkubwa na kupelekea uharibifu wa miundo mbinu na kufungiwa kwa kituo kikubwa cha usafiri kwa sababu za kiusalama. Ni hasara kubwa sana, lakini kwa watu ambao huwa sielewi vichwa vyao vinafanya vipi kazi, hayo wanaona ni mafanikio kwao!

Haina ubishi kuwa shabaha na maeneo aliyokuwa amechagua yalikuwa sahihi. Tatizo ni kwamba muda haukuwa sahihi.

Asingeweza kujilipua kwenye gari moshi ambalo limebeba watu sita tu. Isingekuwa rahisi kwa sababu lengo lake ni kuua wengi. Asingeweza kubonyeza kitufe ili alipue makaratasi na walala hoi na omba omba ambao lazima wangekuwa wamejilaza kwenye kituo kikuu cha stesheni ambapo ndipo ilikuwa mwisho wa safari.

Gari moshi lilisimama kituo cha Astor. Milango ilifunguka. Hakuna aliyeshuka. Hakuna aliyepanda. Milango ilijifunga tena na injini zilianza kuunguruma. Safari ikaendelea.

Kengele za hatari zilianza tena kulia tena masikioni kwangu. Kichwani kwangu ile orodha ya pointi kumi na moja ya viashiria na tabia za mshambuliaji wa kujilipua ilianza kupita kwa kasi.

Ya kwanza ilikuwa wazi na bayana kwa mwanamke yule. Haina mjadala. Ni mavazi yasiyokuwa ya kawaida. Unajua mikanda ya kufungia mabomu inatengenezwa kikawaida sana. Hata wewe unaweza ukatengeneza ukiwa nyumbani. Chukua karatasi ngumu za canvas futi mbili kwa tatu. Ikunje kunje hadi upate umbo la mfuko wenye tobo la futi moja kwenda ndani. Ufunge huo mfuko wa karatasi za canvas tumboni kwa mtu anayeenda kujilipua na ushone nyuma kwenye mgongo ili uungane usianguke. Kwenye uwazi au mdomo wa mfuko dumbukiza njiti za dynamite, halafu ziunge kwa waya. Baada ya hapo jaza mashimo ya dynamite kwa misumari. Ukimaliza shona mdomo wa mfuko na uongeze mikanda ya kushikilia bomu kwenye mabega ya mshambuluaji ili alibebe vizuri. Ni thabiti na rahisi sana. Hata hivyo, namna pekee ya kufanya watu wasitambue kuwa umebeba kitu kama hicho inakulazimu uvae koti kubwa la baridi. Jambo ambalo linazua mashaka hasa nchi za mashariki ya kati na kwa New York msimu wa kuvaa makoti ya baridi unatokea angalau mara tatu kati ya miezi kumi na mbili.

Leo haikuwa moja wapo ya hizo mara tatu za kuvaa nguo za baridi. Ilikuwa ni mwezi septemba na kulikuwa na joto kubwa sana, achilia mbali kuwa chini ya ardhi kwa hatua tuliyokuwepo na taa zile za gari moshi, joto lilikuwa limeongezeka kwa zaidi ya nyuzi sentigredi 10 kuliko kawaida. Binafsi nilikuwa nimevaa tisheti nyepesi sana. Abiria namba nne alikuwa amevaa mkoti mkubwa mweusi wenye zipu iliyofungwa hadi kugusana na kidevu chake.

Ukiona jambo ambalo siyo la kawaida, toa taarifa.

Akili yangu ilihama kwenda pointi namba mbili. Hii ilikuwa ngumu kuthibitisha kwa wakati huo. Pointi ya pili ni muondoko wa kiroboti. Hii mara nyingi huwa inatazamwa kwenye mkusanyiko wa watu wengi wanaotembea. Sehemu kama vile mijini au nje ya makanisa na misikiti au hata sokoni. Hivyo ni ngumu kuithibisha kwa mtu ambaye alikuwa amekaa kwenye gari muda wote.

Hawa watu wanaojitoa muhanga huwa wanatembea miondoko ya kiroboti sio kwa sababu wanaigiza, hapana. Ni kwa sababu wanakuwa wamebeba kilo nyingi sana kwenye miili yao, ambazo zinayashusha chini mabega yao kutokana na mikanda inayoshika begi na bega la mshambuliaji. Wanaojilipua pia huwa wanatafuna kitu kama jojo kati kati ya fizi na mashavu yao ili kupunguza ukali wa mlipuko wa bomu. Ninalifahamu hilo kwa sababu bomu la dynamite huwa linalipuka kwa pressure kubwa sana na linatenganisha kiwili wili na kichwa cha mshambuliaji kwa muda wa nusu sekunde tu. Kwanini?? Kwa sababu kichwa cha binadamu hakijachomelewa au kufungwa bolt za kukiunganisha na shingo. Ni kwa nguvu ya mvutano wa gravity na misuli tu ndiyo inafanya kichwa kitulie hapo kwenye shingo. Hata hivyo, viunganishi hivi viwili nguvu yake ni ndogo sana kupingana na pressure inayotoka kwenye bomu la Dynamite. Mwalimu wangu mmoja wa ki-Israel aliwahi kiniambia, njia rahisi ya kufahamu kama mlipuko ni matokeo ya shambulizi la mtu kujilipua au bomu la kutegwa ni kutafuta kichwa cha mtu eneo lenye umbali wa radii 9 au 8 kutokea mlipuko mkubwa ulipo. Mara zote huwa hakiharibiwi na mlipuko.

Gari moshi lilisimama Union Square. Hakuna mtu aliyeshuka. Hakuna mtu aliyepanda. Joto la nje lilijaribu kuingia ndani ya gari moshi kupambana na A/C lakini kabla haliaanja mashambulizi milango ilifungwa na safari iliendelea.

Pointi namba tatu hadi namba sita zinazunguka kwenye hali aliyonayo mshambuliaji. Kutoka jasho, Kukosa utulivu na uoga kujichora kwenye uso wake. Ingawa kwa mtazamo wangu, suala la kutoka jasho ni matokeo ya mapokeo ya mtu kwa vichokoo na mazingira, ila kwa mujibu wa shirika la ujasusi la Israeli, kutoka jasho ni matokeo ya mavazi yasiyo ya kawaida na njiti za dynamite.
Kisayansi, dynamite inatengenezewa mbao, na mbao ni kichochea joto kizuri sana! Pia uoga na kukosa utulivu ni viashiria za tabia za mshambuliaji wa kujilipua. Kwanini? Kwa sababu huwa wanaelekea kwenye dakika zao za mwisho za uhai wao. Kwa ufupi huwa hawajielewi. Akili zinakuwa zinawaambia waamini na wasiamini kuna paradiso na mito inayotiririsha maziwa na asali na wanawake bikira wanawasubiria huko wanakokwenda baada ya kumaliza kujiua na kuua watu wasio na hatia. Ukweli ni kwamba, maongezi na mipango ni jambo moja. Kutekeleza hicho ulichokipanga na kukiongelea ni jambo jingine. Ndiyo maana wanakuwa na uoga na kutotulia kabla ya kubofya kitufe.

Abiria namba nne alikuwa na sifa zote za kuitwa mshambuliaji wa kujilipua. Alionekana kama mtu anaeelekea mwisho wa barabara la uhai wake pale ambapo treni ingefika mwisho wa safari – stesheni kuu.

Pointi namba saba: Upumuaji.

Namna alivyokuwa anapumua ilikuwa ni kwa hesabu. Hewa ndani, hewa nje. Hewa ndani, hewa nje. Ni kama wanavyofanya wamama wanojifungua ili kupunguza maumivu ya kuzaa.

Hewa ndani, hewa nje. Ndani, nje.

Pointi namba nane: Washambuliaji wa kujilipua huwa wanaangalia mbele muda wote. Hakuna anayejua kwanini, ila rekodi za video na maelezo ya shuhuda walioponea chupu chupu wamekuwa na msimamo kwenye kauli hiyo. Wanaojitoa muhanga huwa wanaangalia mbele tu. Labda ni kwa sababu wanakuwa kama mbwa au watoto: wanakuwa wanahisi kama hawaoni mtu yeyote basi na wao wanakuwa hawaonekani. Au ni aibu wanayokuwa nayo kuwaangalia watu ambao wanaenda kuwaua. Hakuna anayejua sababu ya hili, ila haina ubishi kuwa huwa wanaangalia mbele tu.

Abiria namba nne alikuwa anaangalia mbele muda wote. Hilo halikuwa na ubishi. Alikuwa anaangalia mbele hadi nikahisi kioo kitavunjika kwa ukali wa jicho lake na muda aliotumia kukiangalia.

Kuanzia pointi namba moja hadi namba nane ndizo tabia alizozionesha abiria namba nne. Nilirudi nikaegemea kiti changu. Nilitulia kwa sekunde kadhaa ili kutafakari. Bado akili yangu ilikuwa inaniambia pamoja na hayo yote kuwa sahihi, mpango wake wa kulipua bomu ulikuwa na kosa kubwa sana kiufundi. Muda ambao alipanga kufanya shambulizi haukuwa sahihi wala rafiki kwake.

Nilikaa kidogo. Akili ikaanza kukimbia. Macho yalianza kutembea. Pointi namba tisa, kumi na kumi na moja pia zilionekana kwa abiria namba nne. Hakuna ubishi juu ya hilo. Mbaya zaidi zote zilikuwa nzito kuliko hata pointi namba moja hadi pointi namba nane. Hakuna ubishi juu ya jilo pia!

SEHEMU YA TATU: BOFYA HAPA.
 
Hii hadithi inaonekana ni nzuri hivyo sitaisoma.. ikifika page ya 10 ndio nitarudi
 
SEHEMU YA TATU.
Pointi namba tisa. Midomo inayocheza. Hadi leo, mashambulizi mengi ya milipuko ya mabomu ya muhanga ni matokeo ya ushawishi wa dini, na dini inayohusishwa sana na mashambulizi ya aina hiyo ni uislamu.

Mashahidi ambao wameponea chupu chupu kwenye mashambulio hayo wamenukuliwa wakisema kabla ya bomu kulipuka, midomo ya mshambuliaji huwa inacheza cheza muda wote... Abiria namba nne alikuwa anachezesha midomo yake kila baada ya kupumzika kwa sekunde ishirini au zaidi kidogo. Kwa kuwa alikuwa hasikiki nilihisi labda alikuwa anajitambuliaha huko ambako alikuwa anategemea kwenda.

Treni ilisimama mtaa wa 23. Milango ilifunguka. Hakuna aliyeshuka. Hakuna aliyepanda. Nilibaki nimekaa kwenye kiti changu. Milango ilifungwa na treni iliendelea na safari.

Pointi namba 10: Begi kubwa.
Dynamite ni bomu imara sana. Halilipuki kwa bahati mbaya hivyo huwa linahitaji kuamuliwa na blasting caps imara. Hizi huwa zinafungwa kwenye Dynamite na chanzo cha umeme kama betri na swichi. Unahitaji betri kwaajili ya Volti na Ampu. Hivyo seli ndogo za AA hazifai kwaajili ya mlipuko mkubwa kama wa Dynamite. Betri lenye volti hadi tisa au zaidi ndiyo bora zaidi, na ili upate mlipuko mzuri zaidi utahitaji betri kubwa kidogo. Kubwa sana kiasi cha kushindwa kukaa kwenye mfuko wa nguo, na ndiyo maana linahitajika begi. Betri linawekwa chini ya begi, ambapo waya zinatokea humo hadi kwenye swichi.

Abiria namba nne alikuwa amevalia begi kubwa jeusi alilokuwa amelikumbatia kwenye mapaja yake. Kwa namna nilivyokuwa nimekaa, basi lilionekana tupu isipokuwa ni kama lilikuwa limebeba kitu kimoja kikubwa sana. Akili zangu ziliniambia ni betri la bomu tu!

Hatimaye treni lilisimama mtaa wa 28. Nilikuwa natakiwa nishukie hapa, lakini nilitulia tu milango ilipofunguka. Hakuna abiria aliyepanda. Hakuna abiria aliyeshuka. Milango ilifungwa na safari iliendelea.

Pointi namba 11: Mikono ndani ya begi.
Miaka ishirini iliyopita ndiyo pointi namba kumi na moja iliongezwa kwenye orodha. Kabla ya hapo kulikuwa na pointi kumi tu kwa wanawake. Lakini dunia inabadilika kwa kasi sana. Yaani tendo halafu mwitikio... Jamii ya waisraeli na watu makini waliiongeza hii kanuni. Kwanini? Kwa sababu mshukiwa wako angefanya maamuzi ya kujilipua usingeweza kukimbia. Hakuna haja kwa sababu hakuna mtu anaweza kukimbia kulishida bomu. Ulichotakiwa kukifanya ni kukimbia na kumkumbatia huyo unayemdhania. Ndiyo! Ulitakiwa kumkimbilia na kumkubatia mtu anayetaka kujilipua halafu kuishikilia mikono yake kwa nguvu ili asibonyeze kitufe. Mashambulio kadhaa yalifanikiwa kuzuiliwa kwa hiyo njia na watu wengi wakaokolewa, lakini haikuchukua muda wataalamu wa mabomu nao wakaja na mbinu yao. Waliwafundisha wanaojilipua kuweka vidole vyao muda wote kwenye kitufe, hivyo walifanya lile kumbatio kuwa butu. Na kwa kuwa kitufe kinakuwa kwenye begi, ndiyo maana inapaswa anayejilipua aweke mikono kwenye begi muda wote.

Abiria namba nne alikuwa ameweka mikono yake kwenye begi alilokuwa amelibeba. Hakuna ubishi juu ya hilo. Vidole vyake vilikuwa juu ya swichi ya bomu hivyo ni kitendo cha kunyanyua juu kidole na bomu lilipuke. Hakuna ubishi juu ya hilo pia.

Gari moshi lilisimama mtaa wa 33. Milango ilifunguka. Hakuna mtu aliyeshuka, ila wakati huu kuna abiria alipanda kwenye behewa letu. Alikuja hadi nyuma ya siti niliyokuwa nimekaa. Niligeuka nikamuangalia. Akili iliniambia nimpe ishara ya kumtaka ashuke ili aendelee kuishi. Lakini sikufanya hivyo. Kwanza, hakuwa ananiangalia na hakuwa hata anajali kama kuna mtu anamuangalia. Pili, ninaijua vyema New York. Kutoa ishara zisizoeleweka kwa mtu ambaye hamfahamiani haswa nyakati za usiku kama huu hakuna umuhimu sana. Hivyo nilitulia tu.

Milango ya treni ilikaa wazi kwa muda mrefu kidogo safari hii. Kwa sekunde kadhaa niliwaza kuwaambia abiria waliokuwemo mule watoke. Lakini sikufanya hivyo! Ingekuwa ni kichekesho. Moja, kulikuwa na vizuizi vingi ikiwemo lugha. Sikuwa najua neno lolote la kihispania, achilia mbali bomu kwa kihispania. Bomba, labda?? Hapana! Bomba ni balbu. Hivyo ningeonekana chizi mbele ya yule mwanamke wa kihispania aliyekuwa amekaa mbele yangu.

Akili yangu ilianza kubishana juu ya neno lipi la kihispania ni sahihi kulitafsiri bomu.
"Bombala." niliwaza. Labda nilikuwa sahihi? Sijui.

Pia sikuwa najua lugha nyingine yeyote ya Albania. Au lugha yeyote ya Magharibi mwa Afrika. Hata hivyo, nilihisi labda yule mwanamke mwenye asili ya Afrika alikuwa anajua kuongea Kifaransa. Na mimi pia naongea kifaransa.
"une bombe. La femme la-bas a une bombe sous son manteau." "Yule mwanamke pale ana bomu amevaa ndani ya mkoti wake." Ajabu nilipomuangalia yule mwanamke wa KiAfrika alikuwa amelala, ingekuwa namsumbua tu. Mwisho wa siku niliendelea kukaa kwenye kiti changu. Milango ilifungwa. Safari iliendelea.

Nilibaki namshangaa abiria namba nne. Akili yangu ilianza kuona picha ya mkono uliokuwa ndani ya begi alilokuwa amebeba. Nilianza kuona mkusanyiko wa nyaya nyingi zilizozunguka ndani ya hilo begi. Nilianza kuwaza nguvu ya bomu la Dynamite.

Kikawaida, umeme unasafiri kwa kasi sana karibu sawa na kasi ya mwanga. Kwa nguvu ya bomu kama la Dynamite ukihusanisha na mazingira ya gari moshi tulilokuwemo wote tungelipukutika tukawa vumbi ndani ya sekunde tu. Hakuna masalia ambayo yangebaki. Sana sana mifupa midogo zaidi kwenye mwili wa binadamu iliyopo kwenye masikio (anvil na stirrup) ndiyo ambayo pengine ingeponea chupu chupu.

Nilibaki kumuangalia yule mwanamke. Hakukuwa na namna ya kumfikia. Kwanza, alikuwa umbali wa takribani hatua thelathini kutoka nilipokuwa nimekaa. Kidole gumba chake, bila shaka, kilikuwa juu ya swichi kwa nchi chache tu. Nafasi zake za kuumaliza mchezo zilikuwa kubwa kuliko nafasi nilizokuwa nazo kuutuliza. Alikuwa tayari. Mimi sikuwa tayari.

Gari moshi iliendelea kuchana mawimbi. Mlio wake wa injini uliobishana na upepo ulianza kusikika masikioni mwangu.

Nilianza kujiuliza maswali mengi. Mpango wa yule mwanamke ulikuwa nini?? Kama lengo ni watu, huko tulipokuwa tunaelekea hakukuwa na mkusanyiko wa watu wengi kwa masaa yale. Ukizingatia night club nyingi tulikuwa tumekwishazipita.

Nilibaki namtazama tu kwa macho ya mkazo. Mkazo mwingi hadi alihisi kitu.

Aligeuza kichwa chake taratibu kuniangalia kama aliyekuwa akiendeshwa na rimoti.

Macho yetu yaligongana. Uso wake ulibadilika... Alikuwa amejua kuwa nimemgundua!

SEHEMU YA NNE: BOFYA HAPA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom