kapesly
Senior Member
- Jan 1, 2017
- 163
- 108
Mtunzi:Mulabha
Msambazaji:Kapesly (Mimi)
Phn:0-655-777-272
Kama umevutiwa nayo unaweza nniambia, your reply my responseee
Mwanzo
Nimajira ya jioni ivi, gari aina ya benz nyeusi, inaonekana ikilandalanda maeneo jirani na Benki Kuu ya Taifa hapa nchini (BOT), ndani ya gari hio wanaoneka akna Jonathan, Kenn, Joven, Isack, Paul, Kizito na Mamba, wote wakiwa na karatasi zilizo na ramani ya benki hio. Mida ya saa moja ivi, Jonathan akachukua simu yake ya mkononi alfu akabonyeza namba kadha, kisha akaiweka simu Sikioni
"Jonathan, sasa mnaweza ingia ndani ila hakisheni kila mmoja wenu anavaa, kifaa chake cha mawasiliano" aliongea jama niliyempigia, nakunifanya nami nitoe amri hio haraka kwa wenzangu
"Jamani twenzetuni, kila mmoja ahakikishe amevaa mawasiliano yake" nilizungumza kwa sauti ya juu kidogo
"Johnathan, wamesema wameshaseti kila kitu tiyari" alizungumza Kenn, huku usu wake ukionyesha wasiwasi sana katika tukio tunalokwenda kulifanya muda mfupi ujao
"yaaah, kila kitu wameseti, thusway wamesema tuingie ndani, Sikieni tunadakika thelathini tu za kufanya kazi yetu" Niliongea, kisha kila mmoja akaanza kuvaa nguo za kujisitiri na mambo tuyoweza kukumbana nayo katika kazi yetu tunayoenda kuifanya
Wote tulivyo maliza kujipanga tiyari kwa kazi nzito tunayoelekea kuifanya Katika Benki yetu kubwa hapa nchini, tukashuka ndani ya Gari nakuanza kuelekea usawa na ilipo benki hii, tulivyoifikia ilipo kila mmoja akaelekea njia yake, Hatukutaka kupitia njia kuu ya benki hii kwa sababu ya majukumu tuliyokuja kuyatekeleza ndani humo, uzuri ni kwamba kila mmoja alikua amesoma ramani ya njia atakayo pita. Mimi binafsi nilipita njia iliyokua nyuma ya benki, katika milango ya dharula waitumiayo wahudumu pindi likitokea tatizo, japo ilikua imefungwa kwa lock maalumu lakini niliweza kupita salama salmini kwasababu mfumo wa mawasiliano wa benki ulikua umekwishwa kuharibiwa na Mkuu wetu wa mawasiliano ambaye ndiye aliyenipa ruhusa ya kua tuingie ndani, Mfumo wa mawasiliano wa benki hii uliharibiwa kwa dakika zipatazo arobaini na tano, muda huo wote hakuna mtu ambaye angeweza kutuona, kwakua hata Cctv Camera zilikua hazifanyi kazi kama inavyotakiwa. Kwakua hatukua na muda wa kupoteza nilitembea harakahara mpaka sehemu ya hazina kuu ya Benki hii ya taifa, Macho yangu yalinitoka kama Bundi mara baada ya kuona pesa nyingi mahala hapa, palikua na hela za mataifa tofautitofauti, hela kama dolla, yen, kwacha, uro, shilingi ya hapa nchini nazingine nyingine
"Tiyari nimeshafika ila wenzangu bado siwaoni?" nilizungumza kwa kutumia kifaa maalumu kinachotuunganisha na mkuu wetu wa mawasilano
"Okey, Jonathan hapo ndani ya Hazani mna lidude flani, kubwa hivi nenda hapo utaona kila kitu kisha fwata maelekezo watakuja tu, kwasababu milango waliyopita wao nimeshindwa kuharibu lock zake" alizungumza Mkuu wetu katika kitengo cha Mawasiliano, nami sikufanya makosa nikaliendea dude lilo kubwa humu ndani ya hazina, nakweli maana katika kifaa hicho nikaweza kuona jinsi benki yote ilivyokaa tena nikaona mpaka sehemu walizokwama wenzangu, kupitia kifaa hicho ambacho ni lidude likubwa nikafanikiwa kufungua milango walioyokwama wenzangu.
Kumbe hata hawakuwa mbali, maana nilivyofungua tu milango hio nao wakatokeza, kila mmoja wao akashikwa na bumbuwazi mara baada yakuona jinsi hazina ya nchi yetu ilivyopambwa na hela nyingi kiasi hicho
"Jamani tuanze kazi yetu, hatuna muda wa kupoteza hapa" nilizungumza mara baada ya kuona jinsi wenzangu walivyozuba mara baada ya kuona mpunga
"walisema tuchukue zipi? Sasa Mkurugenzi" Mamba aliniuliza swali hilo
"hapa hatuchagui kitu, ila dolla ndio ziwe nyingi" nilimjibu, kisha kila mmoja akachukua begi yake alikoificha, tukaanza kuchukua hela za nchi utafikiri tumeruhusiwa kuzichukua, kila mmoja alivyohakikisha amechukua kiasi cha kutosha akasimama ili kusikiliza utaratibu unaofwata
"nadhani kila mmoja anaikumbuka vizuri ramani ya njia yake, hivyo basi tutatoka kama tulivyoiingia humu ndani, tunadakika kumi na tano tu humu ndani" nilizungumuza huku nikawa nawaangazia macho yangu, kila mmoja wao alikua haamini kama ndo tunataka tutoke tena bila kutambulika ila mimi kwa uzoefu wangu niliona ni hali ya kawaida tu, ambayo inakwenda kukamika muda mfupi ujao.
Mmoja mmoja akaanza kutoka kuelekea mlango wake aliopitia wakati anaingia humu ndani, nami ndo nikawa wa mwisho nikipitia njia yangu, njia tulizopita wote zilikua ni njia za dharula, ambapo haikuwa rahisi kutambulika. Dakika chache wote tukawa tumetoka ndani ya Benki kuu ya Taifa hapa nchini, tukiwa tumelitia hasara kubwa Taifa letu, tukaelekea mahala ilipo gari yetu, tukaingizi begi zetu zilizojaa pesa, kila mmoja alivyomaliza kuweka tukaanza kupongezana.
"daaah! Yaani hata siamini, kazi njema sena hii jamani" kila mmoja alitamka maneno hayo kwa mwenzake wakati anamkumbutia, Tukiwa hapo nje kwenye gari letu, Tumejidai kwa kufanikiwa kutoka salama salimini ndani ya benki, Mara tukaona deffender tano za polisi zikija mkuku mkuku mahala tulipo, jambo lililotuogofywa sana
ITAENDELEA
Msambazaji:Kapesly (Mimi)
Phn:0-655-777-272
Kama umevutiwa nayo unaweza nniambia, your reply my responseee
Mwanzo
Nimajira ya jioni ivi, gari aina ya benz nyeusi, inaonekana ikilandalanda maeneo jirani na Benki Kuu ya Taifa hapa nchini (BOT), ndani ya gari hio wanaoneka akna Jonathan, Kenn, Joven, Isack, Paul, Kizito na Mamba, wote wakiwa na karatasi zilizo na ramani ya benki hio. Mida ya saa moja ivi, Jonathan akachukua simu yake ya mkononi alfu akabonyeza namba kadha, kisha akaiweka simu Sikioni
"Jonathan, sasa mnaweza ingia ndani ila hakisheni kila mmoja wenu anavaa, kifaa chake cha mawasiliano" aliongea jama niliyempigia, nakunifanya nami nitoe amri hio haraka kwa wenzangu
"Jamani twenzetuni, kila mmoja ahakikishe amevaa mawasiliano yake" nilizungumza kwa sauti ya juu kidogo
"Johnathan, wamesema wameshaseti kila kitu tiyari" alizungumza Kenn, huku usu wake ukionyesha wasiwasi sana katika tukio tunalokwenda kulifanya muda mfupi ujao
"yaaah, kila kitu wameseti, thusway wamesema tuingie ndani, Sikieni tunadakika thelathini tu za kufanya kazi yetu" Niliongea, kisha kila mmoja akaanza kuvaa nguo za kujisitiri na mambo tuyoweza kukumbana nayo katika kazi yetu tunayoenda kuifanya
Wote tulivyo maliza kujipanga tiyari kwa kazi nzito tunayoelekea kuifanya Katika Benki yetu kubwa hapa nchini, tukashuka ndani ya Gari nakuanza kuelekea usawa na ilipo benki hii, tulivyoifikia ilipo kila mmoja akaelekea njia yake, Hatukutaka kupitia njia kuu ya benki hii kwa sababu ya majukumu tuliyokuja kuyatekeleza ndani humo, uzuri ni kwamba kila mmoja alikua amesoma ramani ya njia atakayo pita. Mimi binafsi nilipita njia iliyokua nyuma ya benki, katika milango ya dharula waitumiayo wahudumu pindi likitokea tatizo, japo ilikua imefungwa kwa lock maalumu lakini niliweza kupita salama salmini kwasababu mfumo wa mawasiliano wa benki ulikua umekwishwa kuharibiwa na Mkuu wetu wa mawasiliano ambaye ndiye aliyenipa ruhusa ya kua tuingie ndani, Mfumo wa mawasiliano wa benki hii uliharibiwa kwa dakika zipatazo arobaini na tano, muda huo wote hakuna mtu ambaye angeweza kutuona, kwakua hata Cctv Camera zilikua hazifanyi kazi kama inavyotakiwa. Kwakua hatukua na muda wa kupoteza nilitembea harakahara mpaka sehemu ya hazina kuu ya Benki hii ya taifa, Macho yangu yalinitoka kama Bundi mara baada ya kuona pesa nyingi mahala hapa, palikua na hela za mataifa tofautitofauti, hela kama dolla, yen, kwacha, uro, shilingi ya hapa nchini nazingine nyingine
"Tiyari nimeshafika ila wenzangu bado siwaoni?" nilizungumza kwa kutumia kifaa maalumu kinachotuunganisha na mkuu wetu wa mawasilano
"Okey, Jonathan hapo ndani ya Hazani mna lidude flani, kubwa hivi nenda hapo utaona kila kitu kisha fwata maelekezo watakuja tu, kwasababu milango waliyopita wao nimeshindwa kuharibu lock zake" alizungumza Mkuu wetu katika kitengo cha Mawasiliano, nami sikufanya makosa nikaliendea dude lilo kubwa humu ndani ya hazina, nakweli maana katika kifaa hicho nikaweza kuona jinsi benki yote ilivyokaa tena nikaona mpaka sehemu walizokwama wenzangu, kupitia kifaa hicho ambacho ni lidude likubwa nikafanikiwa kufungua milango walioyokwama wenzangu.
Kumbe hata hawakuwa mbali, maana nilivyofungua tu milango hio nao wakatokeza, kila mmoja wao akashikwa na bumbuwazi mara baada yakuona jinsi hazina ya nchi yetu ilivyopambwa na hela nyingi kiasi hicho
"Jamani tuanze kazi yetu, hatuna muda wa kupoteza hapa" nilizungumza mara baada ya kuona jinsi wenzangu walivyozuba mara baada ya kuona mpunga
"walisema tuchukue zipi? Sasa Mkurugenzi" Mamba aliniuliza swali hilo
"hapa hatuchagui kitu, ila dolla ndio ziwe nyingi" nilimjibu, kisha kila mmoja akachukua begi yake alikoificha, tukaanza kuchukua hela za nchi utafikiri tumeruhusiwa kuzichukua, kila mmoja alivyohakikisha amechukua kiasi cha kutosha akasimama ili kusikiliza utaratibu unaofwata
"nadhani kila mmoja anaikumbuka vizuri ramani ya njia yake, hivyo basi tutatoka kama tulivyoiingia humu ndani, tunadakika kumi na tano tu humu ndani" nilizungumuza huku nikawa nawaangazia macho yangu, kila mmoja wao alikua haamini kama ndo tunataka tutoke tena bila kutambulika ila mimi kwa uzoefu wangu niliona ni hali ya kawaida tu, ambayo inakwenda kukamika muda mfupi ujao.
Mmoja mmoja akaanza kutoka kuelekea mlango wake aliopitia wakati anaingia humu ndani, nami ndo nikawa wa mwisho nikipitia njia yangu, njia tulizopita wote zilikua ni njia za dharula, ambapo haikuwa rahisi kutambulika. Dakika chache wote tukawa tumetoka ndani ya Benki kuu ya Taifa hapa nchini, tukiwa tumelitia hasara kubwa Taifa letu, tukaelekea mahala ilipo gari yetu, tukaingizi begi zetu zilizojaa pesa, kila mmoja alivyomaliza kuweka tukaanza kupongezana.
"daaah! Yaani hata siamini, kazi njema sena hii jamani" kila mmoja alitamka maneno hayo kwa mwenzake wakati anamkumbutia, Tukiwa hapo nje kwenye gari letu, Tumejidai kwa kufanikiwa kutoka salama salimini ndani ya benki, Mara tukaona deffender tano za polisi zikija mkuku mkuku mahala tulipo, jambo lililotuogofywa sana
ITAENDELEA