Riwaya: 'J u l y 7'

Riwaya: 'J u l y 7'

asante sana kudikudi nilikuwa naifuatilia kwa umakini, vipi kuhusu ile ya isabel mbona mmeiachia kati
 
CHAPISHO LA 14
Tajan akaingia ndani ya chumba hicho akiwa na
dvcam moja iliyofungwa juu ya miguu maalumu
ya chuma, akaiweka mbele yake na kuigeuzia
kule aliko Amata na ShaSha, Shailan akajifunga
kitambaa cheusi usoni mwake na kusimama
mbele ya camera ile kisha akaanza kuongea,
kutoa ujumbe wakati chombo kile kikinasa picha
ile. Nusu saa baadaye walikuwa wamekamilisha
zoezi lao, waliamua wawachinje watu hao watatu
siku iliyofuata huku wakipiga picha zingine
ambazo zingekuwa ni salamu ya mwisho kwa
serikali kama wasingekubali kumfungulia ndugu
yao, kaka yao, mpigania uhuru mwenzao.
6
ASUBUHI ya siku iliyofuata ilimkuta Madam S
katika ofisi yake akiendelea na majukumu yake
kama kawaida, ndani ya ofisi yake kubwa na
nzuri iliyobeba heshima zote za kuitwa ofisi. Kila
mara aliangalia saa yake kana kwamba kuna mtu
au kitu anachokisubiri ambacho mi na wewe
hatukukijua isipokuwa yeye peke yake. Ilipita
nusu saa ikawa saa, Madam S aliinua simu yake
ya mezani na kubofya namba kadhaa kisha
kutega chombo cha kusikilizia sikioni mwake
lakini baadae alikishusha na kukiweka palepale
alipokitoa.
Kwngele ya mlangoni kwake ililia, nae kwa
kutummia chombo maalum aliweza kumuona
Yule anayegonga kengele hiyo, Madam S
akabonyeza tarakimu kadhaa zilizotengenezwa
maalum juu ya meza yake na mlango ukajiondoa
kitasa chake na kuruhusu mtu huyo kuingia
ndani.
DHL, ni kijilebo kidogo kilichoning’inizwa katika
box kubwa lililowekwa katika meza ya kando
kidogo ofisini mwa Madam S, mlinzi wa getini
alilileta ndani humo. Madam S alilisogele na
huku akiwa ameshika saa yake akichezea
kidubwasha Fulani, alipolikaribia akasimama na
kuliangalia vyema, kabla hajalifungua alipiga
simu getini na kumuita Yule mlinzi kumuuliza ni
nani aliyeleta kasha lile, akajibiwa kuwa ni
mfanyakazi wa DHL ambaye alikuwa na pikipiki.
Kwa uzoefu wa kazi za kipelelezi kwa maiaka
mingi, madam S aligundua wazi kuwa lile kasha
halikutoka DHL kwani ufungwaji wake ulikuwa
tofauti na ule aliouzoea, alilichunguza tena na
tena na kugundua mambo mengi ambayo ni
tofauti na utaratibu wa DHL, akalichukua na
kuingiza kwenye kikabati maalumu chenye
mitambo ya x-ray ili kuweza kuona ndani kuna
nini kabla ya kulifungua. Mtambo ule baada ya
kuwashwa ulionesha ndani ya kasha lile mlikuwa
na kitu mfano wa dvd, akalitoa ndani na
kulifungua, hakukosea, ilikuwa ni dvd moja ikiwa
katika kasha lake, akaitoa na kuigeuzageuza,
kisha akaifuata luninga yake kubwa iliyopo hapo
ofisisni na kuitumbukiza dvd ile, akasubiri kuona
kitu kitakachofuata. Mtu aliyevalia vazi jeusi
lililomfunika mpaka usoni, alionekana ametulia
tuli, kisha akaanza kuongea kufikisha ujumbe ule
alioukusudia. Madam S alisikiliza kwa makini
ujumbe huo wenye vitisho vingi vya mauaji ya
kutisha kutoka kwa magaidi waliokuwa wakidai
kufunguliwa kwa mwenzao Jegan aliyefungwa na
serikali ya Tanzania. Mwisho wa dvd hiyo
aliziona picha za mateka waliowakamata
akiwemo Kamanda Amata, Gina na mwingine
asiyemjua. Kijasho kilimtoka Madam S, moyo
ulimuenda mbio, akanyanyua simu iliyopo mezani
na kubonya namba Fulani Fulani,
“Yes, nakuja sasa hivi, kuna ujumbe mzito
umetufikia asubuhi hii,” Madam S akakata simu
baada ya kuongea maneno hayo, alionekana
wazi kuchanganyikiwa kwa hilo, akanyanyuka na
kuondoka zake.
Breki ya kwanza ilikuwa katika jengo la wizara
ya ulinzi, kwa kasi alishuka katika ngari yake na
kuuendea mlango ambao aliufungua bila kubisha
hodi, moja kwa moja alikutana na mheshimiwa
waziri aliyekuwa akimsubiri kwa hamu.
“Ndio madam,” alimkaribisha huku akiipokea ile
dvd na kuelekea kwenye luninga yake,
akatumbukiza kwenye chombo maalum cha
kusoma dvd hiyo na kutazama,
“…tumesema tumechoka, nah ii sasa ni mara ya
mwisho, hatutarudia tena, tunaomba mumuachie
huru ndugu yetu, mpigania uhuru mwenzetu
mliyemfunga katika gereza lenu la Ukonga, Jegan
Grashan. Tuliwapa siku saba lakini sasa
tumeona wazi kuwa hamna nia ya kutekeleza
ombi letu. Basi kama ilivyo ada kwa kuwa
imebaki siku moja na masaa machache, matukio
mabaya ya kutisha yatakayoondoa roho za walio
wengi yatatukia mara tu mmalizapo kutazama
dvd hii, watanzania makumi, mamia kwa maelfu
watateketea kutokana na ugumu wa mioyo yenu,
muachieni huru kaka yetu nasi tuwaachie nchi
yenu, la, damu itamwagika na kamwe matukio
haya hayatasahaulika katika historia ya taifa
lenu, kizazi hata kizazi. Kama mlikuwa mnajidai
na mpelelezi wenu kutuharibioa mipango yetu,
sasa ni huyu hapa tunae, hata mumtafute vipi
kamwe hamtompata, muachieni Jegan
tumuachie Kamanda Amata, siku yetu Julai Saba
imefika, nchi itatetemeka kwa hofu na kilio kikuu,
lakini utangulizi wa yote mtaupata sasa, kaeni
chonjo…”
Ujumbe ule uliishia hapo na mheshimiwa waziri
aliona picha ile ya kwa uzuri kabisa, kamanda
Amata aliyekuwa hoi bin taaban chini sakafuni,
mheshimiwa waziri alionekana wazi akitetemeka.
“Madam, hapa hatuna ujanja, twende Ikulu
haraka,” Mheshimiwa waziri aliyasema hayo
huku tayari alikuwa ameitoa ile dvd na kushika
njia kuelekea nje, gari yake ikaja jirani mara
moja, wote wawili wakaingia na kuondoka.

KIVUKONI – DAR ES SALAAM
Honi ya pantoni ilisikika watu walikimbilia na
kuingia ndani ya chombo hicho ili wapate kuvuka
kutoka Kigamboni kuelekea upande wa pili
uliojulikana maarufu kama Ferry. Watu wengi
walijaa, wakubwa kwa watoto, wanafunzi,
wafanyakazi na wafanyabiashara, wote wakiwa
kwenye michakato ya kuwahi shughuli zao za
kila siku, nahodha wa chombo hicho alipoona
kimejaa na tayari kuondoka aling’oa nanga na
pantoni ikaanza kusogea majini taratibu, kwa
mwendo wa madaha.
Katika banda la kupumzikia abiria upande wa
Kigamboni, palibaki watu wachache ambao
walifika pale dakika kadhaa baada ya kile
chombo kuondoka, hivyo iliwapasa kusubiri
kitakaporudi.
“Wewe ni msafiri au? Maana naona umekaa
hapa karibu dakika ishirini sasa, wengine
wakiondoka na wengine wakifika, we upo
hapahapa, hapa si kijiwe cha wavuta bangi kaka,
kama huvuki basi uondoke hapa,” Mgambo
mmoja alikuwa akimsemesha kijana aliyekuwa
ameketi katika moja ya vibench vilivyopo hapo,
Yule kijana aliomba samahani na kuondoka eneo
hilo, mkononi mwake alikuwa na redio ndogo
iliyokuwa ikikoroma kana kwamba haipati
mawimbi ya sauti, nay eye alikuwa akijaribu
kuirekebisha mara kwa mara, akatoka na
kuielekea tax iliyokuwa imeegeshwa jirani kabisa
na kituo cha polisi, akaingia na kuketi kiti cha
nyuma, akageuza shingo yake na kutazama
nyuma kule baharini.
Muziki wa Bob Marley, ‘So Much Trouble in In
the World’ ulikuwa ukisikika kutoka katika spika
zilizofungwa juu ya chombo hicho, kilendelea
kukata maji kuelekea Ferry, na sasa kilikuwa
katikati ya upande wa Kigamboni na Ferry, watu
walikuwa wakitazama mandhari safi ya jiji
kongwe la Dar es salaam, wakibadilishana
mawazo, hili na lile, wanafunzi wakifikiria kufika
mashuleni haraka huku wakiwaza jinsi gani
watapata usafiri kutokana na manyanyaso ya
kondakta dhidi ya wanafunzi, tabia iliyokithiri
katika jiji la Dar es salaam, tabia inayopelekea
wanafunzi wa kike kupata mimba ovyo kwa
sababu ya urahisi wa usafiri hawana budi
kujirahisisha ama kwa madereva tax au
makondakta wa daladala, serikali inashindwa
kuwatetea katika hilo, ikawahi kuanzisha mradi
wa mabasi ya wanafunzi uliokuwa ukiendeshwa
na vijana wa chama lakini pesa zote zikaliwa na
mradi ulikopotelea si mimi wala wewe tunajua.
Wakiwa katikati ya maji, kitu kisichotegemewa
kikatokea, huku walio Ferry wakiitazama pantoni
ile ikiwa inakuja taratibu na wale wa Kigamboni
wakiiangalia ikiwa inaenda taratibu, sasa
zilikuwa zikipishana inayotoka Ferry na
inayotoka Kigamboni. Mtu mmoja aliyekuwa
akisubiri katika banda la kusubiria usafiri huo
upande wa Ferry aliinua mkono wake na
kuitazama saa yake iliyomwambia ni saa tatu na
nusu asubuhi, aliishikashika saa yake na
alipoiachia alishtushwa na mtikisiko mkubwa
mkubwa, mlipuko mzito ulioacha kitu kama
tetemeko la ardhi la sekunde kadhaa, watu
walionekana kutawanyika huku na kule wakiwa
hawajui hata wapi wanakimbilia au nini
kinawakaimbiza, mji wa Dar es salaam ulizizima
kwa kishindo hicho. Moshi mzito, mweusi,
uliobebwa na moto mwekundu sana vilionekana
katikati ya bahari eneo la kuvukia vyombo hivyo
vya usafiri, vilio vilitawala, hakuna aliyejua nini
kimetokea.
“Zimegongana! Zimegongana!” wengi walisikika
wakisema hivo, “Hapana zimelipuka!” wengine
walisikika namna hiyo, kizaazaa. Mamia ya
wasafiri walikuwa wakiteketea kwa moto, nani
wa kuwaokoa, vyombo vyetu vya zimamoto
havikuwa na uwezo wa kufika pale, hakukuna na
hata meli ya kusogea kufanya uokozi zote
ziliogopa mlipuko kwani nazo zinatumia mafuta.
Moto mkubwa ulikuwa ukiendelea kuwaka,
pantoni zilikuwa zikiendelea kuteketea na abiria
wengi walioko ndani, wenye uwezo walijirusha
majini, wengine waliojua kuogelea wakafanya
hivyo, wenzangu na mimi walibaki wakihangaika
kunusuru pumzi zao za mwisho.
≈≈≈
“Hawa jamaa hatuna njia ya kuwadhibiti
sasa, kama Amata aliyekuwa akiongoza
operesheni hii nae wamemteka, tutafanya
nini?” Makamu wa Rais alikuwa akiongea na
wadau wa usalama ofisini kwake katika
Ikulu ya Tanzania, aliwatazama mmoja mmoja
kwa zamu, hakuna aliyeonekana kama ana
jipya katika hilo, Madam S, waziri wa mambo
ya ndani, waziri wa ulinzi na jeshi la
kujenga Taifa, IGP, Mkuu wa majeshi na
kamishna mkuu wa Magereza, kimya
kiliwakumba, giza likawatawala.
“Mheshimiwa hayupo, lakini sina budi
kufanya maamuzi ya haraka, nitampigia simu
na jibu tutatoka nalo sasa hivi kabla hali
haijawa mbaya,” makamu wa Rais
alipomaliza kusema hayo, aliitazama saa yake
ya mkononi na alipoishusha alisikia mtetemo
kama kishindo kizito cha kudondoka kitu,
picha kubwa zilizokuwako ukutani zianguka
na kuvunjika vipande vipande, kisha utulivu
ukarejea tena. Jopo lote lililokuwa katika
kikao hicho cha dharula lilihamanika kwa
kishindo hicho, “Nini?” aliuliza makamu wa
Rais, “Bila shaka ni mlipuko mzito umetokea,
kwa kishindo hiki, itakuwa ni maili mbili au
zaidi,” Mkuu wa majeshi alikuwa akisema
hayo huku akinyanyuka kitini, mara simu ya
IGP ikapata uhai, akainyakua kutoka
mfukoni mwake ili kuizima asiharibu
mkutano, lakini alipotazama kioo cha simu
hiyo ilijiandika ‘Detective’, akaona ilikuwa ni
habari nzito, “Inspector General of police,”
IGP aliitikia kwa kujitambulisha cheo chake
moja kwa moja, hii ilitokana na uzito wa
simu iliyopigwa, simu ambayo inaweza
kukaa hata miezi mitatu isipigwe, simu
iliyoandikwa ‘detective’, simu nyeti, kwa
mambo nyeti.
“Mlipuko mkubwa umetokea maeneo ya
Ferry, pantoni zote mbili zimewaka moto
kwa mara moja wakati zikipishana,” ilikuwa
sauti ya upande pili, “Umesomeka chukua
hatua, nafika sasa hivi,” IGP alijibu na
kukata simu. Sura yake iliyojikunja
ilionekana wzi mbele yaw engine, akawapa
ujumbe na wote wakaonekana wazi
kuchanganyikiwa, makamu wa Rais akatoa
amri ya kufuatailia swala hilo nay eye
akisubiri taarifa hiyo.
“Ugaidi,” Madam S alisikika akiongea kwa
sauti ya chini, akipigisha viganja vya mikono
yake kuashiria ameshindwa afanye nini.
Iliwachukua dakika tano tu kufika eneo hilo,
hali waliyoikuta ilikuwa tete, wapiga mbizi
kutoka jeshi la polisi la wanamaji lenye kituo
chake jirani kabisa na Ferry wakishirikiana
na kikosi cha jeshi la wanamaji kutoka
Kigamboni ‘Navy’ walikuwa wakishirikiana
katika uokoaji huku gari za zima moto zikiwa
zimefika lakini haziwezi kusogea eneo la
tukio.
Vilio vya wenye ndugu vilisikika kila kona,
wakati gari za wagonjwa zilipokuwa zikitoka
na kuingia kukusanya majeruhi ambao
wameopolewa kutoka majini. Siku ilikuwa
nzito kwa viongozi wa serikali, hawakuwa na
la kufanya zaidi ya kukutana tena na tena
kujadili swala hilo, msiba wa kitaifa.
Madam S alisimama kwenye njia panda ya
kuingia Ferry na ile inayokuja Posta ya
zamani akiangalia kila kinachoendelea huku
akiwa hajui hata wenzake aliokuja naoi
wamepotelea wapi, midomo ilimchezacheza
kwa hasira, machozi yalimtiririka kwa
uchungu, alitamani amuone huyo
anayesababisha haya yote ili amfundishe
adabu, lakini hakumjua, alimkumbuka sana
Kamanda Amata katika sakata kama hili
tayari angekuwa amekwishajua fununu za
mhusika, maana wakati mwingine alipenda
kumuita ‘The black dog’ kutokana na tabia
yake ya kugundua vitu haraka, Madam S
aliifananisha na kunusa. Hakuwa na uamuzi,
ahata alipokuja kushikwa mkono na Chiba
kuondolewa eneo lile yeye bado alikuwa
hajielewi.
“Chiba, Kamanda ametekwa!” Madam S
alimwambia Chiba wakiwa ndani ya gari.
“Unasema?” Chiba aliuliza kwa mshtuko, Madam
S akamueleza kwa kirefu sana juu ya ile dvd.
Chiba alibaki kusikitika, akachukua kompyuta
yake ndogo na kuifungua kisha akaanza
kubonyezabonyeza namba Fulani Fulani na
kufuatilia aina ya mchoro uliokua unajionesha
ukijichora kitu kisichojulikana.
“Unafanya nini Chiba?” Madam S aliuliza.
“Natafuta uelekeo wa micro chip ya Amata labda
itaniambia yuko wapi, ili tujue tunafanya nini,”
Chiba alimjibu Madam. Baada ya muda mfupi wa
Chiba kuchokorachora kompyuta yake,
alimgeukia Madam S, “Madam” Chiba aliita,
akamtazama Madam ambaye alikuwa amejiinua
kutoka katika siti aliyokuwa amekaa katika
mtindo wa kujilaza, “Signal, inanionesha
Kamanda yupo maeneo ya Bunju,”
“Bunju?!” Madam aliuliza.
“Ndiyo ni Bunju,” Chiba alijibu.
“Ok, fanya unaloweza ujue alipo na ikiweza
upange rescue haraka, hawa jamaa inaonekana
wameshatuweza kwa kumteka Kamanda”
Madam alimwambia Chiba, mara Simu yake
Madam S ikapata uhai kwa mara nyingine,
akaichukua haraka kutoka katika mfuko wa koti
lake na kutazama, private namba, akaifyatua
kitufe cha kusikilizia na kuweka sikioni, ilikuwa ni
simu inayomhitaji mkutanoni haraka.
“Chiba nipeleke ofisi kuu,” aliamuru Madam S na
Chiba alitii amri ya boss wake, akawasha gari na
kuingia barabarani, muda mfupi baadae alikuwa
tayari mbele ya jingo hilo chakavu la kizamani,
jingo la mkoloni, city hall.
“Fanya nililokwambia, kasha nipe mrejesho wa
siri,” madam alimwambia Chiba, akashuka na
kuingia ndani ya jingo hilo.
KUNA NINI OFISI KUU?
 
EPISODE 15

“Mimi nilishasema, hawa jamaa watafanya kitu
mbaya, tumuachie huyo mtu wao tuishi kwa
amnai, sasa tazama jinsi watu wasio na hatia
wanavyotekea, tutafakari mara mbili ndugu
zangu, sio tunasikiliza ubishi wa mtu mmoja
tena asiye na maamuzi kati jopo hili. Yuko wapi
sasa? Si hawa wameshamteka!” alilalama Waziri
wa ulinzi mheshiimiwa Maige. Wajumbe wa
mkutano huo wote walikuwa kimya hakuna
aliyethubutu hata kunyanyua mdomo wake, kila
mtu alikuwa akimlaumu mwingine ndani ya
moyo wake. Mara mlango ukafunguliwa na
katibu wa ofisi hiyo, Miranda, na baada yake
akaingia bi mkubwa Madam S, akavuta kiti
kilichokuwa wazi na kuketi.
“Mi nafikiri, sasa turejee uamuzi wetu, kwa kuwa
leo ni tarehe sita mapema hii, kesho tarehe saba
wanayomtaka mtu wao, hatujui mi na wewe nini
wamepanga kufanya hiyo kesho, ina maana
ulinzi uliowekwa haukuwa sawa?” mkuu wa
majeshi akauliza, IGP akamtazama kwa jicho
baya sana.
“Lazima tujue tunapambana na watu wanaojua
medani za vita, wameangalia wapi tumelegeza
wametumia nafasi, hatutakiwi kulaumiana ila
tunatakiwa tuamue la kufanya kwa kuwa muda
ndiyo huo unakwenda na Julai 7 imekaribia.” IGP
nae alitoa hoja yake. Mara mlango ukafunguliwa
tena akaingia Miranda na karatasi mkononi na
kumkabidhi Waziri wa ulinzi, akaitupia macho na
kasha akaiweka mezani. “Ripoti ya awali ya ajali
hii hapa,” Waziri aliwaeleza wajumbe na kila
mmoja aliipitia na kuirudisha mezani.
“Vijana wetu wa Jeshi la wananchi
wameng’amua kuwa mlipuko ule ni wa bomu, na
bado wanachunguza ni bomu la aina gani, maiti
zilizoopolewa ni kama sabini hivi na majeruhi
wengi sana wamekimbizwa hospitali,” waziri
maige aliangusha machozi alipokuwa akisema
hayo. Wote katika mkutano ule walibaki kimya
kwa muda. Mara ngumi nzito ya nguvu ikatua
mezani mpaka kufanya glass za maji kuanguka
na maji kuwalowesha wajumbe, “Nasema hivi
Jegan aachiwe mara moja na watu wake
waondoke nchini ndani ya masaa kumi na
mawili,” Waziri wa ulinzi alitamka kwa hasira,
karatasi ikaletwa na akamkabidhi waziri wa
mambo ya ndani aandike hati hiyo ya kuachiwa
huru kwa gaidi huyo. Madam S aliinyakuwa ile
karatasi na kuikunjakunja kasha akaitia katika
chombo cha takataka, kila mmoja akamatazama
mwanamke huyu aliyeonekena kuvimba kwa
hasira mpaka mishipa ya uso ilidinda.
“Tusiamue mambo kama watoto, kwa kutumia
hasira, tumuachie!? Na damu za Watanzania
hawa zilipwe na nani, na Kamanda Amata yuko
wapi? Siafiki, siafiki, lazima tuingie kwenye
mapambano ya nkono kwa mkono, kama
mnaogopa kikosi changu na mimi mwenyewe
tutaingia kazini kuanzia sasa,” Madam S alifoka,
baadae kila mmoja akaona usahihi wa maneno
hayo. Ulikuwa mvutano uleule ambao ulitokea
siku tatu nyuma, kutokuelewana kukaendelea
katika hilo. Mwisho wa yote, ikaundwa kamati
ya watu watatu ili wakakutane na makamu wa
Rais, kutoka kwao watapata lile wanaloona
linafaa kuamuriwa.
≈≈≈≈
Sherehe iliendelea katika ukumbi mdogo ndani ya
yadi ile ya Bunju, freedom fighters walikuwa
wakijipongeza kwa kazi waliyoifanikisha siku
hiyo, huku ikiwa tayari kazi ya julai 7
imwkamilika bado kufyatua tu.
“Sasa vijana, tumefikia tamati ya maafikiano
yetu na serikali hii isiyo na masikio, leo
tumewapa onyo lakini kesho wataiona kazi
yenyewe watakapookota maiti zilizokuwa jivu
mia kwa mamia, lazima dunia itikisike. Sasa
Shakrum, weka kamera yako tayari twende
kuchinja wale mbuzi,” Shailan aliwaambia
swhaiba zake, kasha wote wakashuka kwenye
kila chumba cha chini, chumba walichomfunga
Amata na Yule Mkorea, walipofungua
hawakuamini macho yao, hakuna mtu ndani.
Shailan na wenzake wote wakajikuta wamepigwa
na butwaa hawajui watu wale wametokaje mle
ndani, kila mtu alimtazama mwenzie, wote
wakatoka tena nje na kuufunga mlango ule.
Wakatawanyika na kuwauliza walinzi ambao
waliwaeleza wazi kuwa hakuna mtu aliyetoka
nje, lazima watakuwa ndani umohumo, msako
mkali ukaanza kila pembe ya jengo na kila
chumba kilichopo ndani humo.
Kamanda Amata na Shasha walikuwa
wamejificha katika katika bomba kubwa la maji
machafu lililopita chini tu ya chumba hicho
walimofungiwa. Amata aligundua hilo baada ya
kusikia kitu kama maji yanayotembea wakati
alipokuwa amelala pale chini, baada ya kutoka
wale jamaa, alijivuta mpaka kwa Yule binti wa
Kikorea na kumchomoa pini iliyobana nywele
zake, maana alijua wazi kutokana na ile shepu
ya pini angeweza kufungua pingu walizofungwa,
alipoichomoa kwa meno akaibana hivo na
kujaribu kuingiza katika tundu la ufunguo la
pingu aliyofungwa ShaSha na kufanikiwa
kuifungua, kasha ShaSha akamalizia kufungua
zilizobaki pamoja na zile za Amata, katika
kutazama huku na huko waligundua kuwa kuna
mlango uliozibwa kwa mbao laini, wakautoa
uzibo huo kwa umakini sana na kujikuta kwenye
choo kingine, wakang’oa sinki lake na kupata
tundu la kutosha ambalo chini yake kulikuwa na
lile bomba kubwa la maji machafu ambalo
lilikuwa limekusanya maji ya mtaa huo.
Ijapokuwa ilikuwa ni tabu kupita kwa kutambaa
na kupambana na harufu mbaya na chafu lakini
hawakuwa na budi kujiokoa kwa njia hiyo.
Waliendelea kutambaa humo bombani kwenye
hewa nzito sana ambayo kama hauna mazoezi
ya kutumia pumzi lazima ufie njiani.
Mwendo kama wa lisaa limoja walianza kuona
mwanga wa jua mbele yao uking’aa kupitia yale
maji, hapo wakapata moyo kuwa sasa wamefika
nchi kavu, wakaongeza nguvu zilizokuwa
zikipungua muda baada ya muda, walitambaa na
kujikuta wanatokea baharini, ShaSha na
Kamanda Amata walijikuta baharini, hiyo kwao
ilikuwa ni faraja sana waliogelea kidogo kuondoa
harufu na uchafu uliyowaganda mwilini,
wakaogelea kuondoka eneo lile mpaka mbali
penye maji safi, wakatoka nchi kavu na kujitupa
kwenye mchanga. Kamanda Amata alimgeukia
ShaSha, “Wewe ni nani?” alimuuliza,
“ShaSha, kutoka India” akajibu
“Unafanya nini hapa? Huoni unahatarisha
maisha yako?” Kamanda aliuliza
“Nipo kazini,” akajibu kwa kifupi huku
akijinyanyua kwenye ule mchanga akasimama
wima lakini bila kutegemea alijikuta akipigwa
ngwala kali na kudondoka, kabla hajafika chini
Amata alaijivingiriha na kumdaka kwa ustadi,
akamkumbatia.
“Kuwa muangalifu ShaSha,” akamwambia kasha
akamtupia pembeni.
“Tuko wapi?” ShaSha akauliza
Amata aliangalia mazingira yale lakini hakuyajua
kutokana na mikoko mingi iliyojaa eneo hilo,
akampa ishara ya kuondoka, ShaSha
akanyanyuka na wote wakafuatana wakitembea
juu ya mchanga huo mweupe wakiwa hawajui
wapi wanaelekea. Baada ya mwendo mrefu
waliona madau ya wavuvi yakiwa yameegeshwa,
wakaendelea kusogea mpaka eneo lile,
“Bagamoyo,” Amata alimwambia ShaSha. Kisha
akaendelea kutembea mpaka nchi kavu na
kuyapita yale madau mpaka kwenye barabara
kubwa. ShaSha akajiangalia na kujaribu kujinusa
hapa na pale, akaona bado ananuka uchafu,
akamnusa na Amata vivyo hivyo. Kamanda
Amata alaimshika mkono ShaSha na kutembea
taratibu wakapita mitaa kadhaa na kutokea
katika hoteli kubwa ya Paradise, wakaingia
mpaka kaunta, kila mtu aliyewaona akajishika
pua kutokana na hali hiyo, mlinzi wa hoteli
alaikwenda kuwazuia lakini meneja akampa
ishara ya kuwaacha wafike kaunta.
“Habari Kamanda Amata,” Yule meneja mwenye
asili ya kipemba alimsabahi Kamanda
“Si salama, naomba chumba change cha
kawaida tafadhali,” Kamanda alitoa oda, na mara
moja wakaongozwa mpaka ghorofa ya pili na
kukabidhiwa funguo ya chumba hicho. Kabla ya
yote kila mtu alijikuta akiuendea mlango wa
bafuni wakakutana mlangoni mikono yao miwili
ikiwa imekamata kitasa cha mlango huo.
Wakatazamana, macho yakakutana, ShaSha
akaona aibu akainama chini, Kamanda Amata
akiwa bado kashika kitasa juu ya mkono wa
ShaSha akakinyonga na mlango ukafunguka,
bafu kubwa la kisasa likawakaribisha, wakaingia
na kila mmoja akajitupa ndani ya beseni kubwa
linaloweza kuwabeba wote wawili, michezo ya
kuogeshana ikaanza na kumwagiana maji, kila
mmoja akimmwagia mwenzake mwisho
Kamanda Amata alimdaka ShaSha na kumvutia
kwake, akamtazama usoni kwa tuo, ShaSha
akaelewa lugha inayozungumzwa na macho ya
Kamanda, vinywa vyao vikakutana, ndimi zao
zikacheza pamoja, miili yao ikakutana, viungo
vyao vikabadilishana mawazo, wote wawili
wakazama katika bahari ya mapenzi.
KAMANDA AMATA AMEKUTANA NA SHASHA NA
WAMEWEZA KUTOROKA,,,,
KIKAO CHA WADOSI KITALIFIKISHA API JAHAZI
HILI?
USIKOSE EPISODE 16......
 
EPISODE 16
7
KAMANDA AMATA ALITOKA ndani ya bafu hilo la
kisasa katika hoteli ya Paradise pale Bagamoyo,
akiwa na taulo kiunoni mwake alipita kabisa na
luninga, akili yake ikamtuma kwanza kuwasha
luninga hiyo kujua nini kimejiri huko duniani
muda ambao yeye hakuwepo huko. Luninga ile
ilimkaribisha kwa moshi mzito uliokuwa
ukionekana kwenye kioo chake, akatamani kujua
kilichotokea akaketi kwenye kitanda na kukodoa
macho akiizama ‘breaking news hiyo’, baada ya
dakika tatu za kuangalia habari hiyo alikurupuka
kama kichaa, ShaSha alikuwa bado akijivuta
kama kawaida ya wananawake wengi,
kujivutavuta dio mpango mzima kwao.
Kamanda Amata tayari alikuwa ndani ya suti
nyeusi safi iliyomtoa kweli kweli. ShaSha
alipofika chumbani alimkuta Kamanda
amekwishajiandaa, “Vipi, mi nilijuwa tunakula
fungate, mbona mwenzangu hivyo?” ShaSha
aliuliza kwa kiingereza chake kilichochanganywa
na lafudhi ya kihindi. “Hapana mama hapa ni
kazi,” Amata alijibu huku akimuonesha ile
luninga pale.
“Tayari, ugaidi umeshafanyika bila kificho na
kesho ni Julai saba, lazima niwahi kuokoa
jahazi,” kamanda Amata alimalizia kuongea huku
akifunga kiatu cha mwisho, akamwangalia
ShaSha pale aliposimama, “Twende au utakuja
baadae?” akamuuliza.
“Hapana tunaondoka wote, habaki mtu hapa,”
ShaSha alijibu huku akinyakuwa moja ya gauni
zuri la kibuluu lililokuwa limening’inizwa katika
vining’inizio kadhaa vilivyowekwa hapo, wakati
yeye anavaa, Kamanda Amata alikuwa
akishushia glass iliyojaa pombe aina yaVodka ili
akili yake ichangamke vizuri.
Dakika kumi baadae wawili hao walikuwa tayari
nje ya hotel hiyo wamekwishakukamilisha itifaki
zote. Waliingia ndani ya tax moja ilikuwa imeleta
mgeni hotelini hapo, “Bunju tafadhali, karibu na
Baobab,” Amata alimwambia Yule dereva, naye
akatii bila hata kuuliza. Kutokana na ustadi
aliouonesha dereva Yule kwa kuendesha gari,
haikuwachukua muda wakafika eneo hilo,
ShaSha aliiona gari yake ikiwa imepaki palepale
katika ile pub aliyoingia jana yake. Dereva
akaegesha gari kwa mbele kidogo, Amata na
ShaSha wakashuka, Amata akampa noti za elfu
kumi tatu, ambazo alipewa pale kaunta katika
hotel ile.
“Ile pale gari yangu,” ShaSha alimwambia
Amata, wakatazamana. “Subiri hapa,” Amata
alimwambia ShaSha, akachomoa miwani yake na
kuipaika usoni kisha akainedea gari ile mpaka
pale, akashika saa yake na kuizungusha katika
mtindo Fulani, ile saa ikatoa mlio Fulani hafifu,
akarudi kwa ShaSha na kumwamru wasonge
mbele kidogo.
“Vipi mbona umeiacha?” ShaSha aliuliza
“Imetegwa bomu, haiku salama,” wakatembea
mwendo mfupi wakafika kwa jamaa wanaouza
na kufyatua matofali, “Subiri hapa,”
akamwambia, Kamanda Amata akawasalimu
wale vijana na kupita mpaka eneo ambalo wao
huwa wanatumia kuteka maji au pi kujipumzisha,
pana kijito kilichopita kuelekea baharini lakini
kimezungukwa na machaka mengi utafikiri
hakuna mtu anayefanya shughuli eneo hilo. Wale
vijana wakawa wakimshangaa hawakujua ni
wapi anaelekea, “Mheshimiwa choo hiki huku!”
mmoja wao alipaza sauti kumwambia Kamanda
akijua kuwa kaenda kujisaidia, akapotelea
vichakani bila kumjibu yeyote. Aliikuta pikipiki
yake ipo salama, akaitazama tena kwa jinsi ileile,
akaikuta ko salama kabisa.
Kutoka ndani ya kichaka, wale vijana
walishuhudia bonge la pikipiki la Kirusia likiibuka
kama kifaru cha jeshi ‘Cagiva’ , “Twende zetu”
alimwambia ShaSha aliyekuwa kabaki mdomo
wazi, kwa wepesi wake alijirusha na kutua katika
kiti cha mashine hiyo huku mikono yake
akimutana mbele ya tumbo la Amata. Haikuwa
mwendo wa kitoto, dakika chache walikuwa
wakiipita Boko na kuitafuta Tegeta ambako
hawakujali fole za kuja Mbezi mpaka Mwenge
wao walipita pembeni pembeni na kujikuta
wakifika katika mataa ya Mwenge mapema
kuliko walivyotegemea. Muda wote ShaSha
alikuwa kimya ametulia katika mgongo wa
Kamanda Amata akisikiliza mlio mzuri wa
pikipiki hilo.
≈≈≈≈
Shailan bado hakuamini kile ambacho
alikishuhudia, Kamanda Amata amewezaje
kutoroka kwa jinsi walivyomdhibiti kwa
minyororo na kumuweka katika chumba
ambacho kwao kilikuwa ni chumba pekee chenye
usalama wa asilimia mia moja. Alikuwa
amesimama akiangali nje ya nyumba hiyo
kupitia dirisha kubwa lililomruhusu kufanya
hivyo. Shakrum alikuwa ameketi katika kiti
kingine ndani ya sebule hiyo ndogo. “Tunahitaji
kikao cha haraka,” Shailan alimwambia Shakrum,
Shakrum ahakuhitaji kuhoji aliiendea meza ya
mbele yake na kutuma ujumbe kwa wote
wanaohusika kukutana hapo mara moja, na
haikuchukua muda ndani ya nusu saa wajumbe
wote walikuwa wamekwishafika, na kukusanyika
katika meza kubwa ya duara, simu zao zote
zilikusanywa na kuzimwa maana hakukutakiwa
kuwe na mawasiliano yoyote kutoka nje.
“Nimekuiteni, ndugu zangu, sina mengi, leo
tumefanya kazi nzuri na tumejipongeza lakini
kilele cha pongezi zetu kimeingia shubiri, mateka
wetu wametoroka,” Shailan aliwaambia wajumbe.
Scolleti alikuwa wa kwanza kushtuka
akamtazama Shailan kwa jicho kali, “Na Yule
msichana wa Kihindi je?” akauliza.
“Nimesema mateka wetu wote isipokuwa Yule
tuliyemhifadhi kule Mabibo,” Shailan aliwaeleza,
ukimya ukachukua nafasi yake.
“Sasa hatujui kama hiyo kesho wanatupatia mtu
wetu au la, maana hapa nimeanza kupata
wasiwasi.” Shailan aliendelea kuongea kwa
huzuni.
“Shailan, kama tulivyopanga, kesho kila kitu kipo
tayari, tumefanya uchunguzi wetu tumeshajua
kuwa tukio tunalolitaka litakuwa ni saa nane
kamili, na sisi tumeomba watupatie mtu wetu
saa saba kamili, wakichelewa tu tunafanya yetu
halafu kuanzia hapo ni mashambulizi mfululizo,”
Shakrum alizungumza huku akipigapiga meza
kwa ngumi yake.
“Mimi nipo tayari kwa msaada wowote
mtakaouhitaji kwa hizo shughuli zote, ila
naomba Yule msichana wa Kihindi kihwa chake
mniletee,” Scolleti aliongezea.
“Msiwe na shaka, Amata atakuja tu, maana
atakuta ujumbe wake kuwa malaya wake yupo
huku,” Tajan aliongeza kuwatia moyo wenzake.
Basi kikao kikavunjika, na siku hiyo wote
waligawana maeneo ya kufanya kazi zao za
kuchunguza mambo mbalimbali.
≈≈≈≈
Gina alirudiwa na fahamu zake baada ya kutoka
katika usingizi mzito usiopimika, akajigeuza na
kujikuta kwenye sakafu baridi, akiwa amelazwa
na minyororo mikononi mwake, alijishangaa,
alikuwa kwenye nguo ya kulalia tu, hakuelewa
kinachoendelea hapo, aljaribu kutazama na
kuchunguza chumba kile, kilikuwa kitupu kabisa
hakina samani yoyote, wala hakikuwa na picha
wala dirisha la kuwezesha kuona nje. ‘Niko
wapi?’ alijiuliza, ‘Nimekujaje?’akazidi kuzama
katika maswali yasiyo na majibu. Akatulia chini
kwenye sakafu baridi na chumba hicho
kilionekana wazi kuwa kilikuwa ni ‘cold room’
chumba cha kuhifadhia nyama na vitukama
hivyo. Baridi ya chumba hicho ilimuingia mwilini
bila huruma, alihisi kuganda lakini hakuwa na la
kufanya. Mara akaona kitasa cha mlango ule
mzito wa chuma kikifunguliwa kwa jinsi
kilivyokuwa kikiinamia upande wa chini, moyo
wake ulianza kwenda mbio kwani hakujua
anayeingia ni adui au rafiki, akajituliza palepale,
mara kijana mmoja mwenye asili ya kiarabu au
kihindi lakini alikuwa na ngozi nyeusi iliyokata
tama aliingia kwa mwendo wa kunyata kama
anayewinda kitu, alimwogopa nani ilhali alikuwa
pekee ndani humo.
Alisimama na kumtazama Gina aliyekuwa
kajikunyata pale katika kona ya chumba hicho,
uso wake ukiwa umekutanishwa na magoti yake,
gauni lake la kulali alilovaa lilimwagika china na
kururhisi mapaja yake manene kubaki wazi,
alijuwa fika kuwa huo ni mtego tosha kwa kijana
huyo, Yule jamaa alimfikia Gina na kuanza
kumpapasa kimahaba, Gina aliinua uso wake na
kumtazama jamaa huyo alienokana kujawa na
mate kinywaji kwa uchu wa penzi haraka haraka,
alianza kumshikashika Gina kwa fujo, mara
mapajani mara sijui wapi, huku bastola yake
akiwa kaiweka pembeni kabisa, Gina alijifanya
kujilegeza na kutoa sauti ya kukataa jambo hilo,
Yule jamaa alimbembeleza na kumuahidi
kumletea chakula mchana huo kwani yeye ndiye
alikuwa kwenye lindo, Gina alimtazama tena na
tena jinsi suruali yake ilivyotuna. “Sasa
tutafanyaje mapenzi huku nina minyororo?”
alimuuliza Yule kijana, badala ya kujibu akawa
anachekacheka tu alipoanza kuyaona matiti ya
Gina sasa yakiwa nje ya kigauni hicho, Yule
jamaa alijipapasa mifukoni na kutoa funguo,
akaifungua ile minyororo, hakika penzi kitovu cha
uzembe. Alipokuwa akiiweka pembeni ile
minyororo ndipo alipokutana na kabali maridadi
kutoka kwa Gina iliyopigwa kwa miguu yake
miwili, Yule jamaa alikukuruka lakini wapi,
alikutana na miguu ya Gina yenye nguvu ya
ajabu, baada ya dakika mbili alilegea na kutulia,
Gina alimuachia taratibu, akamvua fulana yake
na kuivaa yeye kwa haraka kisha akamtoa na
suruali, akamuacha humo ndani, akaokota ile
bastola na kuuelekea mlango kwa hadhari
kubwa. Aliufungua taratibu kwa kuuvuta ndani
kisha akachungulia akiwa na bastola yake
mkononi, akajitokeza na kujibanza pembeni mwa
ukuta huo, akaangalia kwa makini ili agundue ni
wapi alipo lakini ilikuwa ngumu maana macho
yake yalipambana na ngaxi nyingi hata yeye
mwenyewe hakujua ni wapi aweze kupita, pale
ambapo moyo ulimtuma ndipo alipoikwea ngazi
ya mbele yake kwa haraka mpaka korido ya juu,
akaambaa na ukuta na kuipita milango kadhaa,
mlango mmoja uliokuwa mbele yake alipotaka
kuupita alisikia sauti za watu wakiongea,
akasimama na kutulia kusikiliza ni nini hasa
walikuwa wakiongea. Gina alitulia pale kama
dakika tano hivi alivutiwa na mazungumzo ya
humo ndani hata akajisahau kama yupo eneo la
hatari.
Kutoka chumba cha usalama katika jengo hilo
mtu aliyekuwa akicheza na camera za usalama
alikuwa anamuona Gina kila alichokuwa akifanya
tangu alipotoka katika chumba cha siri mpaka
alipofika hapo, akainua simu yake ya upepo,
“Gadi namba sita tafadhali, mateka wetu
ametoroka ulinzi, yupo ngazi namba sita katika
mlango namba 7 hakikisha hafanyi madhara
yoyote, ova” Yule bwana alibonya kitufe
kimojawapo katika ile redio yake, “Nimekusoma,
linafanyiwa kazi,” Yule mlinzi aliyepigiwa alijibu.
Gina bado aliganda palepale akisikiliza kile
kilichokuwa kikizungumzwa mle ndani,
akajisahau kabisa, mara alihisi akiguswa begani,
Gina akatulia kisha akageuka kwa kasi na
kuachia konde moja ambalo lilimpepesua Yule
mlinzi akajibamiza kwenye mlango wa chumba
kingine, kabala Gina hajamfikia Yule mlinzi
akanyanyuka kutoka pale alipoangukia na
kusimama wima lakini bunduki yake ilikuwa iko
mbali kidogo, kabla hajaichuku Gina aliruka juu
na kutua kifuani mwake kwa miguu miwili, wote
wawili wakaanguka chini na kishindo kile
kikawashtua wale walio katika ule mkutano,
wakatoka na kukuta pigano lile, wote kwa
pamoja wakamvamia Gina. Ilikuwa ni ngumu
kujitutumua, wakamkamata na kumfunga kamba.
Tajan aliyekuwa katika mkutano huo alimtazama
Gina kwa jicho la gadhabu sana, akihema kama
mbwa aliyekosa windo lake, alirusha teke likatua
shavuni mwa Gina na kumtupa upande wa pili,
akamfuta na kumkanyaga kichwani kwa nguvu
kisha kuutuliza pale mguu wake. Gina alihisi
maumivu makali sana, damu zilimtoka mdomoni,
hakuweza kufanya chochote kutokana na zile
kamba za mikononi walizomfunga kwa nyuma.
Wakamchukua na kuondoka naye.
≈≈≈
Kamanda Amata aliwasili eneo la Kivukoni pale
Magogoni mchana ambapo pilikapilika za uokoaji
zilikuwa zimekwishapungua ila bado watu
walikuwa ni wengi na polisi nao wengi. Aliegesha
pikipiki yake na kuteremka akifuatiwa na ShaSha,
akavuta hatua kuelekea geti la kuingilia abiria.
Ijapokuwa ilikua ni shida kidogo lakini alijitahidi
kupenya na hadi kufika ndani ambako miili
mingi ya watu waliopoteza maisha ilihifadhiwa,
alisimama na kutazama hali ile isiyovumilika,
moyo wake ulipata uchungu uliochanganyika na
hasira mbaya.
“Kamanda!” sauti moja iliita kutoka nyuma yake,
akageuka na kumuona kijana mmoja aliyevalia
sare za kijeshi za kikosi cha wanamaji,
wakasalimiana kisha akamvuta pembeni, “Okoa
jahazi Kamanda, Watanzania wanakufa kama
hivi,” aliongea huku akitoa machozi, Kamanda
Amata aligundua kuwa Yule kijana ni daktari wa
jeshi baada ya kumuona akiwa na Stetoscope
(BP Machine) shingoni mwake.
“Usijali dokta, ndio nimefika, tutalifanyia kazi,”
Kamanda Amata alijibu, akabaki hana la kusema
zaidi ya kusikiloiza vilio na kuangalia miili ile
iliyolala bila roho kwa dhambi na ukatili wa watu
wachache, ‘Jegan Grashan!’ alijisemea huku
akiuma meno alipoinua uso wake macho yake
yakautana na ule mnara mkubwa wa kuongozea
meli uliojengwa kwa mtindo wa meli pale
pembezoni mwa soko dogo la samaki,
aliutazama na kuutazama, akili yake
ikamwambia kitu, akatoka haraka na kuelekea
kwenye ule mnara. Alipigana vikumbo na watu ili
apate njia, huku akikimbia na huku akitembea,
akafika pale mnarani na kuingia katika ofisi za
kwanza pale chini kisha akaiendea lifti na
kupanda kwenda juu kabisa, alipofika mlangoni
akakuta mlango umefungwa, akajaribu kubofya
kengele mara ukafunguliwa na akaingia ndani.
Katika kile chumba kulikuwa na vijana wawili na
msichana mmoja walikuwa kwenye viti
wakifanya kazi zao katika mitambo maalum
iliyofungwa ndani humo.
“Karibu, tukusaidie nini?” Yule msichana aliuliza
“Umeiona ile Pantoni iliyolipuka leo?” kamanda
akauliza. “Sidhani kama kuna mtu aliye eneo hili
ambaye hakuiona,” Yule mwanadada akaejibu.
“Sawa, nahitaji kuona kamera zenu za usalama
kabla ya tukio na mpaka dakika kumi baadae,
tafadhali,” Kamanda Amata alitoa amri. “Mkuu,
utaratibu hauendagi hivyo mkuu, hizi ni ofisi za
watu,” kijana mwingine akasema lakini kabla
hajamaliza alikatishwa na Kamanda Amata,
“Sikia we kijana, hicho kiti unachokalia utakiacha
sawa, haya ni amri tekeleza ninalotaka haraka,”
wale vijana hawakuwa na jinsi, “Shida
mheshimiwa funguo hatukai nazo sisi za hicho
chumba chenye hizo tv,” Yule mwanadada
akaongezea. Kamanda akaupigab teke ule
mlango unaoingia kwenye hicho chumba nao
ukaachia, akaingia ndani na kuketi kati kiti
akazitazama zile tv zilikuwa kama ishirini hivi
zikionesha pande tofauti. Akaangali ile inayopiga
picha za Kigamboni, Kivukoni akaipata,
akarudisha lile tukio nyuma mpaka dakika mbili
kabla na kutazama kwa makini. Aliweza kuona
jinsi zile Pantoni zilipokuwa zikitoka mpaka
zilipolipuka, haikumpa maana sana, akairudia
tena na tena, kitu kimoja kikamjia kichwani,
aliona wakati watu wote wakiwa wameingia
katika Pantoni upande wa Kigamboni kulikuwa
na mtu mmoja aliyebaki, ijapokuwa hakuona
vizuri lakini alihisi hivyo, ‘sasa hiki kina maana
gani?’ alijiuliza, akaona hakuna chochote cha
kumsaidia, alipotaka kuondoka, akasita, akakaa
tena, kurudisha ile picha lisaa limoja nyuma, na
kutazama safari zingine kama tatu hivi za
pantoni ile. Sasa aliona Yule aliyedhania kuwa ni
mtu bado akiwa ameketi pale tangu safari tatu
nyuma, wasiwasi ukamuingia, ‘Kama si msafiri
alikuwa akifanya nini pale,’ akawaza hakupata
jibu. Akatoka na kuteremka chini bila kuongea na
mtu yeyo mle ndani, safari ya miguu ikamfikisha
palepale kivukoni, kichwani akiwa na mambo
mawili tu lakini kabla ya kuyatekeleza. Akafika
kwenye geti la kuingilia pale wanaposubiria
abiria, akapenya na kuifikia ofisi ya mkuu wa
kitengo, lakini hakuwa ofisini, akauliza baadhi ya
watu aliowaona kuwa ni wafanyakazi
wakamuitia. Wakiwa wawili tu ofisini
mazungumzo yakaanza.
“Unaweza kuniambia mlipuko huu ni wa nini?”
Kamanda aliuliza. “Kwa kweli sijui, yaani mi
nilikuwa ofisini nikasikia tu kishindo, hata wewe
mwenyewe tazama vioo vya madirisha jinsi
vilivyovunjika,” akajibu Yule mzee alieonekana
tangu machoni kuwa hajui lolote lakini pia
mwenye hofu kuu na moyo wa kuchanganyikiwa.
“Sasa sikia, huu ni mlipuko wa bomu, na ni
bomu ambalo lilitegwa kwenye Pantoni moja
wapo kati ya zile mbili, sasa basi nahitaji orodha
ya wafanyakazi wako waliokuwa zamu siku ya
jana na leo,” Amata aliongea kwa ukali. Yule
mzee akasukuti, akamtazama Kamanda, “Sikia
kijana hapa sisi hatuna zamu, tunafika wote na
kutoka wote,” akamjibu. “Sawa sasa naomba
uniitie wafanyakazi wote hapa ili tuone
tunafanya nini kwa pamoja sawa”, zoezi hilo
likafanyika mara moja, wafanyakazi
walikusanywa wote eneo Fulani, “Wote mpo?”
Kamanda akauliza, “Hapana si wote, ukiacha
wale waliofariki kwenye ajali ambao ni kama sita
hivi hapa sijajua ni nani na nani” alijibu Yule
mzee huku akiwa anatokwa na machozi.
Kamanda Amata alisogea pembeni na kuonge na
OCD wa kituo cha polisi cha kati, akimwambia
wale wafanyakazi wopte wapelekwe polisi
kuhojiwa haraka iwezekanavyo. Dakika mbili tu
gari za polisi zilifika na kuwasomba wote
wakaondoka nao. Kamanda Amata sasa alikuwa
akifanya jambo la pili, alikiendea kituo cha pilisi
cha wanamaji kilichopo hatua chache kutoka
Magogoni na kuwaomba wamvushe kwa boti yao
ya akiba wakafanya hivyo.
KAMANDA AMATA ATAFANYA NINI?
 
CHAPISHO LA 17

≈≈≈≈
MADAM S alitoka katika kikao na kutokea geti
kuu akiwa hajielewi sawasawa baada ya
maamuzi yaliyopitishwa katika kikao hicho,
waliombwa kukutana tena jioni ya siku hiyo ili
kujua nini cha kufanya, wakati huo pia
akisubiriwa mkuu wa nchi kufika kwani alikuwa
nje kwa ziara ya kikazi.
Chiba alikuwa tayari amefika katika katika eneo
hilo na gari yake, akamchukua Madam S, kisha
kwa mwendo wa taratibu akaingia barabarani
kama anaelekea stesheni ya treni, kisha akakata
kulia na kuzunguka mnara wa saa na kurudi
barabar ya Samora kuja picha ya askari, “Yes
madam,” Chiba alimchokoza. “Nipe habari za
Kamanda,” Madam alirudisha mazungumzo kwa
mtindo huu. “Kamanda yupo kazini, kama masaa
mawili sasa,” Chiba alijibu, “What? Don’t tell
me!!!” (Nini? Usiniambie!!!) , Madam S
alichanganyikiwa kwa jibu hilo, haraka sana
akamuamuru Chiba kuelekea Magogoni,
walipofika pale hawakumkuta Kamanda,
wakaenda kwa mmoja wa vijana wao, akaweleza
Kamanda Amata amevuka ng’ambo mara moja.
“Tangu amefika ameshafanya nini?” Madam
akauliza. “Kiukweli amefika hapa nilimuona
anaongea sana na mtawala wa eneo hili mara
baadae kakusanya wafanyakazi wote kapeleka
polisi, mwenyewe anajua kwa nini, lakini pia
nilimuona akielekea kule kwenye mnara wa
kuongozea meli.” Yule kijana alijibu. “Ok asante,”
Madam akamalizana na huyo kijana kisha
akatoka na Chiba na kurudi garini. “Sasa nina
amani, kama kamanda amerudi, lakini nampa
pole kwa kuwa Gina ametoweka,” Madam S
alizungumza wakati alipokuwa akikaa vyema
kitini. “Unasemaje Madam? Gina ametoweka?”
Chiba akauliza kwa mshangao, “Ndiyo,
nimemtafuta sana lakini sijampata na si kawaida
yake msichana huyu,” Madam S alimaliza huku
akitafuna jojo yake.
Saa moja baadae, Kamanda Amata alirudi
upande wa Magogoni, na mara moja aliigundua
gari ya Chiba iliyoegeshwa pembezoni kabisa
mwa kituo cha daladala akaisogelea na kumuona
akiwa na Madam S, akaufungua mlango wa
nyuma na kuketi. Madam S aligeuka ghafla na
kukutana na Amata, furaha yake ndani ya
tabasamu pana haikuweza kujificha. “Pole sana
Kamanda,” Madam alimpoza. “Asante Madam,
ndio kazi zetu, unapotea kisha unapatikana lakini
inapobidi, unapotea kabisa. Madam tuna kazi
ngumu sana na hawa jamaa inabidi tujipange
vya kutosha, hiyo kesho sijui itakuwaje, mimi
usiku huu lazima nifanye kazi ya ziada kuvuruga
mipango yao yote, cha msingi ni kwamba
nimeshajua kambi zao zilivyo haitanisumbua, leo
ni usiku wa kazi Madam, sehemu zote nyeti
ziwekewe ulinzi madhubuti,” Amata aliongea kwa
jazba. “Sikia Kamanda, we kapumzike kidogo,
kisha jioni saa kumi na mbili tunakutana pfisi
kuu, uje tafadhali halafu kutoka pale tutapanga
kikosi kazi.” Madam S alimueleza Kamanda,
Chiba akavuta droo ya dashboard na kutoa
kimkebe kidogo, akampatia Kamanda,
wakaagana na kila mtu akashika hamsini zake.
§§§§§
“Hatukuwa na jinsi kwa maana watu wetu
wanakufa tu, kwa nini tung’ang’anie kukaa na
mtu mmoja gerezani wakati mamia yaw a kwetu
yanateketea?” Makamu wa Rais alikuwa
akiongea Mheshimiwa Rais alipokuwa amerudi
ghafla kutoka nje ya nchi kwenye mkutano wa
kimataifa wa nchi zinazoendelea.
“Ok, kama mmeona kwa pamoja na watu wa
vyombo vya usalama mi sina neno, mtoeni huyo
mtu na hao watu wake waondoke nchini ndani
ya masaa machache,” Mheshimiwa Rais alitoa
amri.
Hakukuwa na lingine zaidi ya kutekeleza
lililokuwepo, hati ya kuachiliwa Jegan Grashan
iliandaliwa na wanaohusika na kazi hiyo.
Madam S bado alikuwa akiumiza kichwa katika
hilo, kwa kuwa ni yeye peke yake ambaye
alipinga kuachiwa kwa gaidi huyo hivyo hakuwa
na budi kwa sababu Waswahili wanasema wengi
wape. Kama alitegemea amri au uamuzi tofauti
kutoka kwa mheshimiwa Rais basi haikuwa
hivyo kwani uamuzi wake ulipita mlemle
ambamo wengine waliamua. Maneno ya
Kamanda Amata yalimrudia mara kwa mara
akilini mwake, ‘Mkimuachia mi namuua’ lilikuwa
likikifanya kichwa chake kutotulia.
§§§§§
Kamanda Amata alichanganyikiwa kutomkuta
Gina nyumbani, alipompigia simu hakumpata,
akaingia ndani ya chumba ambacho Gina mara
nyingi huwa akilala kila ajapo kumtembelea.
Kitanda kilikuwa kama kilivyo, kwa jinsi shuka
ilivyobakia, Kamanda Amata alijuwa wazi kuwa
Gina hakuamka mwenyewe bali alibebwa na kitu
au mtu, akatoka na kuingia kwenye kichumba
chake cha siri ambacho humuonesha mambo
yote yaliyotukia nyuma, akijifungia kwa ndani na
kuwasha viscreen vyake na kutazama matukio
yaliyopita hasa kwenye chumba cha Gina, ndipo
alipoona nyendo za mtu anayenyata, hila zote
alizofanya na kumbeba Gina kisha kuondoka
naye. Akajaribu kumsogeza uso wake mtu huyo
lakini kutokana na giza hakuweza kumuona
sawia ila alijua wazi kuwa watakuwa ni wale
wale wabaya wake, alipiga ngumi mezani ya
hasira, ‘ama zao ama zangu’ akanyanyuka na
kuingia chumbani kwake ambako alichukua
silaha zake muhimu kwa kazi za usiku, akilini
mwake akiiwaza ile Julai saba 7 ambayo jamaa
hao wanajivunia, hakujua kwa uwazi ni nini
wanataka kufanya. Mara simu yake ya mezani
ikaita, akaiendea na kuinyakuwa mara moja,
akaiweka sikioni, hakuongea lolote bali alimtegea
mtu wa upande wa pili aseme lolote, alisikia
sauti ya mtu anayepigwa na kelele za kilio cha
kike, aliitambua sauti hiyo kuwa ni Gina, uchungu
ukaushika moyo wake, akauma meno kwa
hasira.
“Tunajua kuwa umetutoroka, usalama wa huyu
Malaya wako ni wewe kujisalimisha kwetu,”
kisha ile simu ikatulia, “Nakuja kujisalimisha
kaeni tayari kunipokea,” kisha akakat simu ile.
Kama kuna kitu ambacho Kamanda Amata
alikichukia ni dharau kama hizo, aliitazama saa
yake, tayari ilitimu saa 11 jioni, akaendeloea
kujiweka sawa. Jambo linguine lilimchanganya ni
kuwa wapi Gina atakuwa amefichwa, Bunju au
kwenye yadi ndogo Mabibo, hakujua, alihisi wazi
kuwa anahitaji msaada, msaada wa mtu
mwenye akili kama yake, akamkumbuka ShaSha,
yuko wapi, hajui. Alikumbuka tu kuwa mara ya
mwisho walikuwa wote pale Kivukoni lakini sasa
hajui alipokwenda, ‘atakuwa wapi?’alijiuliza bila
kupata jibu.
§§§§§
SHASHA baada ya kuona kamanda Amata
amegubikwa na mambo mengi pale Kivukoni,
akaamua kumtoroka, alitafuta tax na kupata
kisha akamuamuru dereva kumpeleka Manyanya
hotel, Kinondoni.
Alipofika jambo la kwanza alifungua laptop yake
na kuweka flash yake ili ajue kati ya vile
alivyovichukua kwenye kompyuta ya Scolleti
kama vina tija. Kompyuta yake ikawaka na
kuanza kuonesha mafaili mbalimbali,
makabrasha na nyaraka anuai za Scolleti. Kati
ya makabrasha hayo, moja lilimvutia zaidi
lilionesha habari nyingi za Scolleti kote
alikokuwa akipita na kufanya mambo yake, siri
ya utajiri wake na mipango anayoipanga, kitu
kilichomshtua zaidi ni ufadhili wa pesa nyingi
anaoufanya kwa vikundi vya wakorofi sehemu
mbalimbali za dunia, kuwapa nguvu kufanya
mapinduzi ili yeye afaidi mkataba mnono na wao
wakishaipindua serikali au wakisha miliki
maeneo Fulani. Alianzia huko Thailand mara tu
baada ya kutoka India na kuwa mfanyabiashara
maarufu. Pale India katika mji wa Bombay
alikuwa akimiliki mahoteli kadhaa aliyoachiwa na
wazazi wake na kwa kuwa yeye alisomeshwa
maswala ya biashara, ndipo alipoweza
kuyaendesha mahoteli hayo na pia kujenga
mengine makubwa zaidi ya hayo katika miji
mbalimbali ya India kama Delhi, Mumbai,
Bangalore na mingine mingi. Kama haitoshi
aliamua kuongeza mabishara sasa akaingia
kwenye maswala ya uingizaji mafuta ndani ya
India kutokea Mashariki ya kati, katika sakasaka
zake za biashara hizo ndipo siku moja
alipokutana na mtu mmoja aliejulikana kwa jina
la Muntazil da Silva, mtu huyo alikuwa ni chotara
wa Kihindi upande wa mama na Kibrazil upande
wa baba, lakini yeye alikuwa akiishi India na
kufanya shughuli zake huko Brazil na Chile.

SCOLLETI

MIAKA 25 NYUMA- BOMBAY, INDIA
ILIKUWA asubuhi ya saa 4:30, katibu wa Scolleti
alipompigia simu bosi wake akimwambia kuwa
kuna mgeni anayetaka kuonana naye, japokuwa
siku hiyo ilikuwa ni siku ambayo Scolleti
hakupenda kuonana na wageni lakini ilibidi
amkaribishe mgeni huyo baada ya kuwa jina
alilotajiwa alilifahamu fika.
“Karibu sana bwana Muntazil,” alimkaribisha
huku akiwa amesimama wakipeana mikono.
“Kwanza samahani bwana Scolleti, nimekuja bila
miadi lakini nilikuwa na jambo muhimu la
kukueleza, kesho mimi ninasafiri kwenda Saudi
Arabia kwenye mambo yangu ya kibiashara,
lakini nimeona nikualike tufuatane ili nawe
ukaone nini tunafanya labda utavutiwa kuwekeza
katika nyanja kama zangu,” Bwana Muntazil
alimueleza kwa tuo bwana Scolleti. Akiwa kimya
huku akiandikaandika katika kitabu chake cha
kumbukumbu, aliinua uso wake na kumtazama
mgeni wake huyo, “Nakusikiliza, bwana
Muntazil,” Scolleti alimwambia mgeni wake.
“Sasa ujio wangu hapa ukiachilia mbali kuwa
nimeonana na wewe, lakini nilitaka kukuomba
kufuatana name, kwani mwenzio nilianza hivihivi
kwa mahoteli, mashule, maduka, lakini nikaja
kuingia kwenye mgogoro na serikali ya Delhi
wakataifisha vitu vyote, ndipo nilipoondoka nchi
hii na kwenda kwa mama zangu huko Brazil
ambako mjomba wangu alinipa mtaji mdogo tu
lakini leo hii nimewekeza kwenye Nyanja nyingi
huko America ya kusini, Africa na mashariki ya
kati, sasa siku moja na wewe utaangukia kwenye
mikono hii hii ya dola, unafikiri utajikwamua vipi,
twende huku halafu utaamua,” Muntazil
alimshawishi Scolleti kwa kina mpaka Scolleti
akakubaliana naye na siku hiyo wakapanga
safari.
Siku ilofuata wawili hao pamoja na whudumu
wachache walikuwa hewani kwenye ndege
binafsi inayomilikiwa na bwana Muntazil
wakielekea Saudi Arabia ambako wangekaa siku
mbili kisha kuelekea Brazil na Chile kabla ya
kurudi India.
Wakiwa Saudi Arabia, Scolleti alijifunza mengi
sana huko mashariki ya kati, biashara ya
kusafirisha mafuta na kumiliki visima vya mafuta
ambayo bwana Muntazil alikuwa akiifanya na
ilikuwa ikimuingizia pesa nyingi sana. Scolleti
aliitamani sana biashara hiyo ambayo ilimtoa
udenda kwa jinsi ilivyoingiza pesa nyingi kwa
muda mfupi. “Bwana Muntazil, biashara hii
nimeipenda sana, je waweza kunisaidia nami
nipate kama si kumiliki basi kusafirisha,” Scolleti
alimwambia Muntazil. “Usijali swahiba,
hatujamaliza bado, inawezekana ukakutana na
biashara nzuri kuliko hii, subiri tumalize ziara
yetu kisha utachagua,” Muntazil akmwambia
Scolleti. Baada ya siku hizo mbili waliondoka
kwa ndege ileile na kutua Chile, ambako walifikia
kwenye nyumba ya kifahari yenye kila kitu ndani
yake, wahudumu wa kumwaga wakikuhudumua
kila utakalo. Scolleti aliushangaa sana utajiri wa
bwana huyo, wakati kule India alikuwa akimiliki
shule moja tu lakini ilikuwa yakisasa kuliko shule
nyingine yoyote katika nchi hiyo. “Muntazil, hili
jumba ni la kwako au umekodi?” Scolleti
alimuuliza Muntazil. “Bwana Scolleti,
nilishakwambia kuwa mimi nimewekeza nje
zaidi, hii ni nyumba yangu mwenyewe, na hawa
wote ni wafanyakazi wangu wa kike kwa wa
kiume nawalipa vizuri kuliko wanavyolipwa
serikalini, ndani ya jumba hili nina wafanyakazi
mia moja,” Muntazil alimwambia Scoleeti
alieonekana kushtuka kwa maneno hayo.
“Mbona hawa hata ishirini hawafiki? Au
wanaingia kwa zamu?” Scolleti aliuliza.
“Hapana bwana Scolleti, wote wanaingia muda
sawa na wanakaa humu humu hawatoki, asilimia
90 kati yao ni yatima, nimewakusanya na
kuwaweka hapa wakifanya kazi na kulipwa ujira
mzuri sana,” Muntazil alimwambia Scolleti
wakiwa mezani kwa chakula cha jioni. Scoletti
alijiona mwenye bahati sana kujifunza hayo yote
kwa rafiki yake huyo. Naye alitamani kuwa kama
yeye, tamaa ya kujiwekea mali nyingi ikamfika,
“Sasa bwana Muntazil, hapa Chile umewekeza
katika nini?” akauliza Scolleti. “Hapa
nimewekeza kwenye kilimo, nina heka za
kutosha za mashamba makubwa ya mimea
ambayo kwayo naingiza hela nyingi sana, usiku
huu tutakwenda huko, tusubiri helkopta inakuja
kutuchukua,” Muntazil alijibu.
Majira ya saa tano usiku, helcopta kubwa ya
kisasa ilitua katika uwanja wa jumba lile,
Muntazil na mgeni wake waliondoka na kuingia
katika helkopta hiyo na kuondoka zao. Safari
ilikuwa ni kwenda katika mashamba ya Muntazil
yaliyopo kusini mwa nchi ya Chile, katika jimbo
la Temuco. Walifika usiku huohuo na kuingia
mashambani, mataa makubwa ya umeme
yaliangaza kiasi kwamba uliweza kuona kila kitu
vizuri kabisa, mahindi manenen yaliyojaza vyema
yalilijaza shamba zima. “Muntzail. Mahindi yiote
haya unamuuzia nani au unatoa msaada?”
Scolleti aliuliza.
“Hapana, kaka, mahindi haya ni jalada tu kitabu
chenyewe kipo ndani, twende kwa maana usiku
huu huu inabidi turudi Santiago,” Muntazil
alimwambia Scolleti kisha wote wakapanda
ndani ya kigari maalumu na kuingia nshambani
usiku huo wakiifuata njia ndogo inayopita
katikati ya mahindi hayo.
Uwanda mkubwa ulikuwa katikati ya shamba lile
la mahidi, mimea iliyokuwa na rangi ya kijani
iliyokolea ilionekana wazi kuwa katika udongo
wenye rutuba nyingi, “Hii ni chai?” Scolleti
aliuliza, “Hapana hii ni cocaine,” Muntazil alijibu
huku akihamia upande wa pili wa eneo hilo
walilosimama. “What? Umesema nini? Au
sijasikia vyema?” Scolleti akuliza tena, “Hiyo ni
cocaine, nikivuna hapa robo heka tu, nina uwezo
wa kujenga mahoteli kama yako yote na zaidi, je
unaonaje hii siyo biashara ya kujipatia kipato
nawe uwe wa tisa kati ya wale G8?” Muntazil
alimwambia Scolleti. Baada ya hapo alimpitisha
sehemu mbalimbali na kumuaonesha jinsi
wanavyovuna na kuifunga vizuri kabla ya kwenda
kiwandani kwa usindikaji na usafirishaji katika
maeneo mbalimbali. Walipomaliza ziara yao huko
Temuco, usiku huohuo walirudi kwa helcopta
mpaka Santiago kwenye jumba lilelile la
Muntazil. “Vipi Scolleti mbona upo kimya sana?”
Muntazil akamuuliza, “Nafikiria juu yah ii
biashara ya kule Temuco, inakuwaje kama
serikali ikigundua unachokifanya?” Scolleti
akauliza. “Sikia Scolleti, serikali zote duniani
zinaongozwa na mwanadamu, na huyo
mwanadamu anaongozwa na pesa, na hiyo pesa
tunayo sisi, unafikiri nini kinakuja hapa? Mkuu
wan chi hii anajua kila ninachokifanya, wana
usalama alikadhalika, hakuna lolote, mi nVuna
nasindika, nauza kwa wafanyabiashara wengine
kisha wao ndiyo wanasafirisha nje, mimi
sisafirshi nje nauzia humuhumu ndani na baadhi
ya wanunuzi wangu ndio haohao uliowataja,
serikali,” Muntazil aliongea kwa kujiamini.
Scolleti aliangalia saa yake ilikuwa ni saa
10:45 alfajiri, alijihisi uchovu sana, lakini
ziara yao ilikuwa inakaribia mwisho,
wakatoka tena na Muntazil ndani ya jumba
hilohilo wakaingia milango kama mitano
tofauti kisha wakatokea mahali ambapo
wanafungia farasi, Muntazil akaingia na
kumuamuru Scolleti kufanya hivyo, kisha
akafunga ule mlango. Ndani ya banda hilo
kulikuwa na farasi wawili weupe, “Usiku
huu farasi wa nini Muntazil?” Scolleti
aliuliza.
USIKU HUU FARASI WA NINI?
ITAENDELEA.... USIONDOKE....
 
CHAPISHO LA 18
“Hapana hatuchukui farasi, simama hapa,”
Muntazil alimwambia Scolleti nae akasimama
karibu kabisa na ukuta wa nyuma juu ya nyasi
kavu, Muntazil akatoa mfukoni kitu kama rimoti
na kubonyeza vitufe kadhaa mara lile eneo
likaanza kushuka chini na kuacha wale farasi
wakiwa kulekule juu. Mara wakasimama na
kutoka kwenye kile kipande kilichowashusha
chini na chenyewe kikarudi juu. Muntazil na
Scolleti walitembea kwa mwendo wa wastani
katika jumba lenye vyumba vingi sana humo
ndani. “Scolleti, hapa ndio eneo la usindikaji,
wanafanya kazi wanawake tu, kwa hiyo uwe
mvumilivu ila kama utamtamani mmoja wao
niambie nitampa taarifa atkuhudumia kabla
hatujaondoka kisha mimi nitamlipa, usijali, upo
tayari?” Muntazil akauliza. Moyo wa Scolleti
ulianza kudunda maana hakujua nini maana ya
kauli ya swahiba wake. Mlango ukafunguka,
wakaingia na kukaribishwa na mwanadada
mmoja mrembo sana mwenye kiuno
kilichojigawanya sawia, kwa rijali yoyote hapo
lazima apige goti na mwenyekiti wa kijiji hana
budi kusimama. Scolleti alipigwa bumbuwazi
baada ya kuona wasichana wengi sana takribani
thelathini wakiwa wametingwa na kazi katika
mashine zao, hakuna aliyeonekana kuongea na
mwenzake, nyuso zao zilifichwa kwa barakoa
maalum iliyofunika mdomo na pua na kuruhusu
macho tu, zaidi ya hapo hawakuwa na vazi
linguine, matiti yao yaliyopishana kwa umbo na
ukubwa yalibaki nje, viuno vyao ambavyo kila
mmoja alikuwa na shepu yake vilionekana wazi,
cha namba nane, tano hata namba moja
kilikuwepo. Kwa ujumla wasichana wale
walikuwa wakifanya kazi bila nguo, uchi wa
nyama na walikuwa wanawake tupu. Muntazil
alimgeukia Scolleti na kumuona akiwa kachoka
ghafla, eneo la chini ya kitovu lilikuwa limetuna
kama mtu aliweka kipande cha muhindi.
“Scolleti, pole sana, usijali, mmoja atakupoza
munkali wako, hapa ndipo tunasindika madawa,
hawa wadada hawavai nguo ili kuepusha wizi,
maana akitoka na kete moja au tatu tayari
anatengeneza pesa ndefu,” akamwambia. Baada
ya hapo walitoka na kwenda upande wa
wanaume nako ni hivohivo, walipomaliza
wakapanda lifti sehemu nyingine na kuja juu
katika lile jumba la bwana Muntazil. “Sasa, huyu
mhudumua atakupeleka katika chumba,
utapumzika na saa tano asubuhi tutaondoka
kwenda Amazonia, Brazil ambapo tutakuwa na
kikao cha dakika kumi na tano tu kisha tunarudi
India.
Scolleti akaondoka na Yule mhudumu mpaka
chumba cha ghorofa ya juu, akakaribishwa na
kuingia ndani kisha akajifungia mlango kwa
ndani, alipogeuka nyuma kukielekea kitanda, lo,
alibaki hana la kufanya kwa kile alichokiona
kitandani. Msichana mmoja kati ya wale
aliowakuta kule katika kitengo cha kusindika
dawa za kulevya, Scolleti alikumbuka jinsi
alivyokuwa akimtolea macho kwa umbo lake zuri
la kuvutia, walitazamana, Scoletti hakuelewa la
kufanya lakini alijikuta hali yake imekuwa mbaya
huko chini, mapozi aliyokuwa akiweka Yule
msichana pale kitandani yalimmaliza Scoletti,
akiwa katika kutafakari hayo, yul;e binti
alinyanyuka na kumfuata pale aliposimama huku
kidole kimoja kikiwa kinywani kikibanwa kwa
meno ya mbele ya taya la juu na la chini, Yule
msichana akamkumbatia Scoletti huku mkono
mmoja akianza kuchezea sehemu nyeti za
bwanyenye huyo. Hali ikawa mbaya
wakakokotana mpaka kitandani na kubwagana.
Scoletti alitolewa nguo zote na kubaki kama
alivyo kisha akapewa michezo ya ajabu
iliyomtoa jasho na mara nyingine alijikuta akilia
kama mtoto.
§§§§§
RIO DE JENEIRO
UPEPO MKALI ulikuwa ukipiga kutoka baharini na
kuishia kwenye kuta za nyuma zilizojengwa
katika ufukwe huo. Kwa wengine ilikuwa ni
burudani lakini kwa wageni ambao hawakuizoea
hali hiyo ilikuwa ni kero kubwa, kila mara
walionekana kugeuza sura zao kule ambako
upepo huo ulikuwa ukielekea.
Katika moja ya nyumba zilizopo katika ufukwe
huo, kulikuwa na kikao cha watu kumi na mbili
kikiendelea katika ulinzi mkali, ulinzi wa siri
ambao duru za usalama hazikuujua kama upo
hapo.
Muntazil na mgeni wake Scoletti walikuwa
wamekutana na watu wengine kumi katika moja
ya vyumba vya jengo hilo ambalo ukiliona kwa
nje ni bovu kupita maelezo lakini kwa ndani
lilikuwa linalingana na hoteli ya nyota tano.
Meza kubwa yenye umbo la ovali iliwaunganisha
wadau hao, kila mmoja akiwa na chombo
maalum cha kuongelea na pia cha kusikilizia,
hakuna mtu wa pembeni aliyeweza kusikia
mazungumzo hayo isipokuwa tu Yule mwenye
vyombo hivyo. Scoletti alitambulishwa kwa watu
hao, nae akajua kuwa kumbe mbele yake
amekutana na viongozi wa makundi hatari sana
kama Tamil Tiger kikundi cha waasi cha
Thailand, Hamas wa Palestina, Gorilla wa Peru
na vikundi vingine asivyovijua. Scolleti alikuwa
akifuatilia kila linalozungumzwa akagundua
biashara haramu ya Muntazil ya kuwafadhili
wapiganaji hao kwa pesa na silaha kali za kivita
ili waendeleze mapigano katika nchi zao,
wadhibiti sehemu nyeti kama zenye madini,
mafuta na utajiri mwingine, wakati majeshi ya
serikali yakipambana na vikundi hivyo wao
upande mwingine wakivuna utajiri ule uliopo
katika maeneo hayo. Scoletti alifuataili na
kusikiliza, hakuongea lolote wala kushauri,
alikuwa akisikiliza taarifa zinazowasilishwa na
watu hao huku akisikiliza maelekezo na
utekelezaji wa kikauli kutoka kwa Muntazil lakini
hakuona hata wakati mmoja Muntazil
akimkabidhi mmoja wao bastola au jiwe,
alichosikia tu ‘nitawaongezea mabomu ya mkono
tani moja,’ wengine akawaambi, ‘Nitawaletea
jeep za kivita kumi na tano,’ engine wakaahidiwa
kupewa RPG za kutosha na kupewa mafunzo
maalumu ya kikombandoo ili kuutingisha
utawala wan chi yao. Mara baada ya kujibu
matakwa yao hayo sasa ikawa zamu ya wale
watu kusema wanachotoa kwa msaada huo,
wengine walisema ‘kilo kadhaa za dhahabu,’
wengine ‘makasha ya almasi,’ wengine
wakamwambia ‘tutateka sehemu nyingine yenye
mafuta ili uendelee kugema na hapo,’. Scolleti
aligundua mzunguko mzima wa ulimwengu na
matukio yake, akashusha pumzi nzito na
kuzifiikiria roho za watu wanaopoteza maisha
katika masakata hayo yasiyo na macho.
Kilichomshangaza ni kuwa hakusikia hata
sehemu moja wakisema ‘tutajenga shule’ au
‘hospitali,’ haikuwapo hiyo. Baada ya dakika
kumi na tano tu kikao hiko kiliisha, na kila mtu
akaondoka bila kumuaga mwenzio, hakuna
kupeana mikono wala nini.
“Muntazil, hii ni biashara gani?” Scoletti
akamuuliza swahiba wake.
“Hivi ndivyo dunia inavyoendeshwa, wewe
ukijenga shule wenzio wanakuja kubomoa,”
Muntazil alijibu, akakohoa kidogo na kuendelea,
“mimi nikifadhili hawa kwa dola milioni thelethini,
kwangu zinarudi na kuwa dola milioni sitini na
ushehe, ni biashara nzuri sana naipenda sana,
nina uwezo wa kuinunua ikulu ya Marekani na
kuihamishia Afrika ya Mashariki bila kuivunja,”
maneno hayo ya jeuri yalimtoka Muntazil na
kumwendea Scoletti. Muntazil akamtazama
Scolleti ambaye bado alikuwa ameketi kitini
kama aliyepigwa shoti ya umeme, “Swahiba,
dunia haina mwenyewe, kila mtu ataiacha,
unafikiri matajiri wakubwa wanaojenga
mahospitali, au mashule , au vyuo, pesa wanatoa
wapi? Changamka kaka, mi nitakuongezea mtaji
wa dola milioni kumi, kisha upate kikundi kimoja
tu cha waasi ambacho utakifadhili kwa silaha na
kila kitu chenyewe kitakupa mzigo wa maana,
upo tayari?” Muntazil alimshawishi Scoletti,
kimya kikatawala kati ya hao wawili, wakabaki
wakitazamana. Scoletti alitamani kiloa kitu lakini
alitakiwa aanze na kimoja. Baada ya mapatano,
Scoletti aliamua kuanza na waasi. Kikundi chake
cha kwanza kukifadhili kilikuwa ni kikundi cha
waasi cha huko Mali, kilichofanya mauaji ya
kutaka kuipindua serikalim akiwapa silaha na
yeye kupata madini ya aina mbalimbali, pesa
ikamnogea, akapata kikundi kingine cha huko
Mexico cha kuuza na kusambaza madawa ya
kulevya, akajitengenezea hela chafu. Baada ya
hapo akajikita katika nchi mbalimbali, kila
alipokuwa anajulikana hila zake alitimuliwa kwa
masaa ishirini na nne, serikali ya India
ikishutumiwa kwa ajili ya huyo raia wake, lakini
walifumba macho. Baada ya malalamiko mengio
yaliyotishia kuvunjika kwa uhusiano wa
kidiplomasia ndipo walipoamua kumfungia kazi
mtu huyo. Scoletti alijikuta Africa, Africa ya
Mashariki na kubwa lililomleta ni ufadhili wa
Freedom Fighter wanaotokea huko Mashariki ya
kati wakija kutekeleza lile wanaloliita vita ya
ukombozi, akawafadhili kwan kila kitu
wakafanikiwa kulipua balozi za Marekani katika
nchi ya Tanzania na Kenya. Bahati mbaya au
nzuri wana usalama wa Tanzania walifanya kazi
kubwa chini ya idara nyeti, idara ya juu
inayoongozwa na mwanamama mahiri kwa kazi
za kijasusi, Madam S, na kufanikiwa kumtia
mbaroni mlipuaji huyo, Jegan Grashan ambaye
amesumbua mataifa mengi na walishindwa
kumpata. Kilichokuja kutokea ni kuwa vita ile ya
ukombozi ikaamishiwa katika ardhi ya Tanzania,
kumkomboa ndugu yao mwanamapinduzi
mwenzao. Serikali ya India ikamtuma
mwanadada ShaSha kufanya uchunguzi na
kumjua kwa undani mtu huyo, kutokana na
kuchoka na lawama, ShaSha alipewa kibali cha
kuua, “Mkamate akibisha mlipue!” maneno
aliyoambiwa na bosi wake wa idara nyeti ya
usalama wa Taifa huko India.
§§§§§
SHASHA aliridhika na alichokisoma kwenye
makabrasha hayo, akayatuma katika idara ya
usalama wa Taifa huko India. Sasa kwake kazi
ilikuwa ni moja tu, kumsaka popote alipo ili
ikibidi ammalize, ShaSha hakuona haja ya
kubishana na kiumbe huyo majinuni.
Akanyanyuka na kuliendea kabati la chumba
hicho na kutazama vifaa vyake kama vyote vipo
katika hali nzuri, alipofungua kabati tu, pande la
mtu likatoka ndanii ya kabati hilo na kisu
kikubwa mkononi mwake, ShaSha akamuepa
kisha akampiga karate hatari nyuma ya shingo
yake, Yule mtu alikuwa imara, ijapokuwa
aliyumba kidogo lakini alisimama na kurusha
ngumi moja nzito ambayo ilikuta ShaSha bado
yupo eneo lilelile ikatua shavuni na kumpeleka
chini. Yule bwana akjirusha mzimamzima
akitanguliza jisu lake lenye hasira ili kumchoma
ShaSha lakini alibugi, ShaSha alijiviringa pembeni
na kujiinua kwa ustadi kisha kumfumua teke
moja kali lililopiga tumboni mpaka Yule bwana
akatema damu na kujibwaga chini kama mzigo.
ShaSha akasimama pembeni akiwa tayari kwa
mashambulizi mengine lakini alichelewa, kutoka
nyuma yake kitu kizito kilipiga kisogoni,
akayumba na kupoteza fahamu, akaanguka chini
juu ya lile jitu la mwanzoni. ShaSha akajaribu
kupambana na giza lililokuwa likimfunika macho
lakini ilikuwa ngumu, akajikuta akifunikwa na
giza hilo kisha kuishiwa nguvu, kimya kikuu
kikakijaza kichwa chake, akalala usingizi mzito,
usingizi usio na ndoto.
Kelele ya mapangaboi ya helkopta yalikuwa
ykisikika katika masikio ya ShaSha, “Vipi
ameamka?” alisiki kwa mbali watu wakiulizana,
“Bado, lakini si muda mrefu atakuwa ameamka,”
sauti nyingine ilijibu, “Akiamka tu, umpeleke kwa
boss mambo yote yataishi huko,” ile sauti ya
kwanza ilikuwa inaelekeza. ShaSha alihisi
maumivu makali sana sehemu ya nyuma ya
kichwa chake, alikumbuka kuwa hapo ndipo
alipopigwa na kitu kile ambacho hakuwahi
kukifahamu mara moja. Aliendelea kujifanya
hajapata fahamu ili ajue kinachoendelea ndani
hapo, alijaribu kufumbua macho kwa mbali,
akagundua kuwa alichokuwa akifikira ni
mapanga ya helkopta kumbe ni feni la juu
lilikuwa likizunguka huku likipiga kelele kwa
ubovu wake.
8
HASIRA zilikuwa zimekitawala kichwa cha
Kamanda Amata, aliamua kufanya maangamizi
ambayo hayatasahaulika katika historia ya nchi
hii, kwanza kwa kitendo cha kuuwa raia wale
kwenye pantone bila sababu maalumu, pili kwa
kumteka Gina, kipenzi chake. Kamanda Amata
aliapa lazima kisasi kifanyike na baya zaidi
lilikuwa ni lile la kuachiwa huru Jegan Grashan,
ilhali yeye alifanya kazi ngumu sana kumkamata
mtu huyo aliyeshindikana kila kona ya dunia.
‘Lolote liwalo wacha liwe!’ alijiwazia mwenyewe
huku akiendelea kutega saa za mabomu yake
kadhaa aliyeokuwa nayo katika yadi ndogo ya
freedom fighter pale Mabibo, mabomu kama
matano aliyoyatega kiustadi kabisa akikumbuka
alichofundishwa kule Cuba. Alipohakikisha yote
kayaweka sehemu sahihi ambayo alijuwa hata
yakilipuka hayatawadhuru raia wa pembezoni ila
uharibifu utakaotokea katika jengo hilo
utasababisha moto mkubwa, hilo alilifanya
akihakikisha ndani ya jengo hilo hakuna Gina
baada ya kusaka kila chumba na kuhakikisha
hayupo, ‘Kesho saa nne’ alijisemea mwenyewe
huku akisonya, kisha akatafuta njia ya kutoka
katika yadi hiyo, ndipo aliposikia mtu akikohoa
nyuma yake, aligeuka kwa haraka na kukutana
na dhoruba kali ya mateke ya usoni, japokuwa
alijitahidi kuyapangua lakini mawili ya kwanza
yalimfikia. Kamanda Amata akarudi nyuma hatua
kadhaa na kuepa teke moja kisha kupiga ngumi
mbili maridadi zilizotua kwenye korodani za mtu
huyo, nae bila kipingamizi alitua chini kama
mzigo, Kamanda Amata akakanyaga shingo kwa
nguvu zote na kusikia wazi mifupa iliyoshika
shingo hiyo ikivunjika, akapiga goti kutaka
kumuuliza kitu akakuta tayari mtu huyo hana
uhai, akamvuta na kumuhifadhi kwenye jaba
kubwa lilillokuwa tupu akalifunika juu yake.
Akatembea kwa hadhari na kufanikiwa
kutoka nje ya jengo hilo huku akiwaacha
walinzi hawana habari yoyote juu ya
lililoendelea ndani. Akatoka na kuiendea
pikipiki yake aliyoiegesha kwenye moja ya
club za usiku hapo mabibo, alipoitazama saa
yake ilikuwa imetimu saa nane za usiku,
akaliswasha pikipiki hilo na kuifuata
Barabara ya Mandela kuelekea Ubungo, pale
akanyoosha na kupita barabara ya Sam
Nujoma mpaka Mwenge akapinga kushoto na
kupiga gia kuelekea Bunju ambako kuna
yadi kubwa kabisa ya jamaa hao, kichwani
mwake alijua kwa vyovyote watu hao
wamehifadhiwa katika moja ya yadi hizo ili
watekeleze mauaji yao. Huku akiwa na
mawazo mengi juu ya Gina, akiwa hajui ni
wapi atakuwa amefichwa na mashetani hao.
Mara saa yake ikaanza kumfinya usiku huo,
huku akiwa mwendo wa kasi katika pikipiki
lake hilo aliinua mkono na kuiruhusu saa
hiyo kutoa ujumbe kwa kuibonyeza kitufe
Fulani, saa ile ikaanza kutema mkanda wa
maneno, ‘uelekeo wapi?’ ujumbe ulikuwa ni
kutoka kwa Madam S, hakuufuatilia kujibu
aliendelea kusonga na pikipiki lake, mpaka
alipofika eneo husika na kuficha pikipiki
lake sehemu kisha kurudi kwa mguu mpaka
jengo hilo lililozungukwa na ukuta mkubwa
sana. Akafanya analoweza na kuukwea ukuta
ule ambao siku hiyo haikuwa mara ya
kwanza kwake kuukwea, ilikuwa ni mara ya
pili, lakini leo ni kwa shari kidogo. Alitua
chini taratibu bila kushtua hata mbu,
akatulia katika hali hiyo kwa sekunde
kadhaa, kisha akaanza kutembea na
kuuelekea mlango ule aliutumia siku ya
kwanza, lo, haukuwa mlango tena bali
ulizibwa wote kwa matofali na kupigwa
plasta kabisa na rangi nyeupe juu. Sasa
hakuwa na budi kutumia mlango wa mbele
kuingia ambao ni mlango wa hatari zaidi
kwani ulinzi wote uko huko, kwa kuwa
alikwishajua kuwa jengo hilo lina camera za
usalama kila kona alikuwa tayari amejiandaa
kwa hilo.
Akaendelea kuvuta hatua ndogo ndogo huku
akiwa ndani ya mavazi meusi yaliyomficha
kila kitu isipokuwa macho tu ambayo
yalifunikwa kwa miwani maalumu yenye
uwezo wa kuona gizani. Alitazama na
kuwaona walinzi waliokuwa wakitembea
huku na huku wakiwa katika doria ya ndani
humo. Akiwa kama paka anayetaka
kumkamata panya, Kamanda Amata alinyata
taratibu sana kuuendea mlango uliokuwa
jirani yake. Lakini kichwani aliona wazi
kuwa hatoweza kufikia lengo lake bila ya
kuonekana na walinzi hao ambao walikuwa
wakiranda huku na huku. Akajibana kwenye
tenka moja la mafuta na kumsubiri mlinzi
aliyekuwa anakuja upande huo, alipofika tu,
alimvuta na kumpatia kabali ya maana, Yule
mlinzi hakutoa hata sauti, alilegea na
kuwekwa chini kwa upole, kamanda
akampigapiga kichwani kumpa salamu ya
pumziko la milele, akajivuta tena kwa kupita
chini ya tenka lile ambalo lilikuwa
limewekwa juu ya vyuma virefu na kuweza
kupita bila kuuinama. Mlango ulikuwa
umbali wa mita kama mia moja hamsini hivi,
lakini katikati ya eneo hilo hakukuwa na
kitu hata kimoja, hivyo ingekuwa rahisi
kwake kuonekana, hakuna ujanja, alichomoa
bastola yake iliyofungwa kiwambo cha sauti
na kasha akajaribu kupita kwa kasi katika
eneo hilo, lakini kabla hajaufikia mlango,
risasi kutoka upande wa walinzi zilisikika,
Kamanda Amata alijitupa chini na kusota
kwa mgongo huku bastola yake ikianza kazi,
shabaha zisizokosa ziliwa maliza walinzi
wale wane, ‘Sikutaka kuwaua lakini imebidi’
alijisemea moyoni, kisha Kamanda
akanyanyuka na kujificha karibu kabisa na
ua kubwa pembeni mwa mlango. Akasikia
nyayo za watu wanaokimbia, akatulia na
kiliskiliza nyayo hizo, kwa harakaharaka
alishajua kuwa wapo watatu.
NINI KITAENDELEA.....?
 
duh walivyokamatwa sijajua kabisa. naona hapo mtunzi alijisahau
 
CHAPISHO LA 19

Mara utulivu ukarejea, hakusikia tena zile
nyanyo, nay eye akaendelea kutulia palepale ili
kuona kitakacho endelea, akiwasubiri hao
waliokuwa wakija upande huo. Kivuli cha mtu
aliyekuwa akija kwa mwendo wa kunyata
kilionekana kwenye mwanga wa taa kikiibuka
kutoka nyuma ya ukuta, Kamanda Amata
aliendelea kutulia palepale, akakitazama kivuli
kile na kugundua mtu huyo alikuwa na bunduki
mikononi mwake, akamsubiri ili ajitokeze
waziwazi.
Amakweli, subira huvuta heri, Yule mlinzi
aliyekuwa akinyata akajitokeza, bado akiwa
katika hali ya kujihami alitazama huku na kule
bunduki ikiwa mkononi, Amata nae akajipanga
kwa shambulizi la ghafla wakati huo akijua kuwa
wengine watakuwa maeneo hayohayo, akaona
ngoja asubiri kinachoendelea labda na wengine
watajitokeza ili aone ni vipi ataanzisha
shambulio lake. Yule mlinzi wa kwanza alipoona
utulivu na hajkujua adui yake yuko wapi, akatoa
ishara ya mkono kuwaita wengine, mara wale
waliobaki wakajitokeza waziwazi tena
wakitembea bila woga kuzielekea zile maiti mbili
nza walinzi wenzao. “Wamekufa!” mmoja
akawaambia wenzake, “Wamekufa?!” mwingine
akauliza kwa sauti ya tashwishwi, baada ya
hapo wote wakalundikana katika zile maiti
wakijaribu kuangalia hiki na kile, “Wamepigwa
risasi, unaona majeraha haya?” Yule wa kwanza
aliwaambia wenzake. “Sasa mbona hatukusikia
mjibishano wa risasi? Mi nimesikia risasi mbili tu
za wao,” mwingine alionesa shaka.
“Tumevamiwa,” Yule aliyesimama karibu na
Amata, aliyekuwa wa kwanza kujitokeza
aliewaeleza wenzake, kisha wakatawanyika
kumsaka muuaji, “Hakikisheni mnampata, yumo
humuhumu!” akawasisitiza kisha nay eye
akachukua nafasi nyingine nzuri ya kumtafuta
adui.
Kamanda Amata akawa akicheka moyoni
akiwasikiliza kwa kila walilokuwa wakiongea,
akwasubiri watawanyike ili aanze kufanya vitu
vyake. Alipohakikisha kuwa eneo lile kabaki Yule
mlinzi wa kwanza tu, na wakati huo alikuwa
ametoa simu akijiandaa kupiga mahali, Amata
akaona kuwa hapo hapo ndio nafasi ya kufanya
mambo yake, alichomoka kutoka pale alipojificha
kwa kasi na kuruka hewani amako miguu yake
ilitua mgongoni mwa Yule mtu, simu
ikamponyoka nay eye mwenyewe kujikuta
akisukumiwa mbele kwa kasi na kujibamiza
kwenye gari ya mafuta iliyokuwa imeegeshwa
eneo hilo. Kabla hajajiweka sawa Kamanda
Amata alikuwa tayari amefika na kumsindikizia
kichapo kikali kilichomzimisha jamaa huyo.
Alipohakikisha ametulia, alimsogeza na
kumuweka jirani na kichwa cha lori hilo,
akamuinua na kumuegemeza kasha akamuashia
sigara na kumpachika kinywani mwake kiasi
kwamba ukija haraka haraka utasema mtu huyo
amepumzika akivuta sigara. Kamanda Amata
akauendea mlango na kuuchezea kwa namna ya
ajabu, ilikuwa sekunde kadhaa tu alipojikuta
ndani ya ujia mrefu, akarudisha mlango nyuma
yake na kutulia akiangalia kama kuna kamera ya
usalama eneo hilo, alitazama darini hakukuwa
nayo wala pembezoni hakukuwa na kitu kama
hicho, taa ya mwanga hafifu sana ilikuwa
ikiwaka kumulika kijia hicho, ‘Usalama kwanza,’
akachomoa bastola yake na kufumua ile taa,
giza likatawala katika ule ujia, Kamanda Amata
akaona kijitaa chekundu kikiwakawaka palepale
alipoipiga ile taa, akatikisa kichwa kuashiria
kuwa ameng’amua kitu. Akasogea taratibu
mpaka eneo lile, kwa akaichika ile kamera
iliyokuwa ikining’inia, akakta nyaya zake kasha
akaungania ule mweusi na mwekundu pamoja,
akafasha shoti sakiti. Fuse inayolinda kamera
hizo katika ‘distribution box’ ikaungua kwa
kitendo kile na kufanya kamera zote kushindwa
kufanya kazi.
Kamanda Amata akaendelea mbele huku
akisoma milango iliyoandikwa majina na vyeo
vya wahusika, alipofungua chumba kimoja baada
ya kingine hakupata anachokitafuta. Katika
chumba cha mwisho amako ndani yake kulikuwa
na makorokoro mengi, pampu za mafuta na
mambo kibao, ndipo alipopata hisia ya kuwepo
kwa Gina eneo hilo. Baada ya kupekua na
kukagua kila kilichomo, kwa kutumia kurunzi
ndogo kama kalamu, aliweza kuiona heleni moja
ikiwa chini, akaiokota na kuigeuzageuza, “Gina,”
alijisemea kwa sauti ya chini. Akaichukua na
kuitazama tena kwa makini, akatabasamu,
ilikuwa ni heleni ya Gina, heleni ambayo mara
kadhaa alimwambia akijikuta kwenye matatizo
kama hayo aidondoshe chini kama ikibidi
kuondolewa eneo hilo. Kamanda Amata
akaichuku na kuibana sikioni mwake huku kitufe
chake cha urembo akiwa amekipachika katika
sikio lake kwa ndani, haikuwa heleni ya kawaida,
bali mtu alipoivaa ni heleni ila kwenye kazi kama
hizo unatakiwa kukifungua kitufe ca urembo na
kukipachika kwenye tundu la sikio hapo utaweza
kusikizana na Yule mwenye heleni ilobakia na
mkfanya mawasiliano bila shida.
§§§§§
SCOLLETI alikuwa katika hatua za mwisho za
mazungumzo na watu wake, Shailan, Shakran,
Tajan na wengine wawili wakiweka mambo
sawa.
“Jamani tayari julai saba imefika, tumejipanga
vya kutosha?” Scolleti aliuliza.
“Hapa tuko tayari, kila kitu kimepangwa kwa
sababu kuna mambo makubwa mawili, kesho
watamfungulia Jegan saa nne kamili asubuhi,
hivyo sisi tutakuwa kule kwenye point yetu kama
kawaida wakati wa tukio hilo, hawa jamaa nina
wasiwasi nao sana, tukijitokeza pale kumchukua
Jegan usishangae wote tukakamatika.” Shakran
aliwaeleza wajumbe.
“Sikilizeni, mpango upo hivi, Jegan atachukuliwa
na watu wa ubalozi wa nchi yake kesho muda
huo, sisi kama alivyosema Shakran tutakuwa
tayari kwenye point husika kwa ajili ya kuwapa
shukrani Watanzania, kikosi cha ukombozi
kitakuwa tayari katika bahari ya hindi kwa
kutumia boti iendayo kasi ambayo itatufikisha
Mombasa kesho jioni,” Shailan alieleza.
Kwa ufadhili alioutoa bwana Scolleti, boti ya kasi
kutoka Ugiriki ilikuwa tayari katika pwani ya
Pemba ikisubiri utekelezaji wa amri itakayofuata,
ili iweze kusogea karibu na Bagamoyo kwa zoezi
la kuwatorosha freedom fighters.
Scolleti akatingisha kichwa kuonesha kuwa
ameridhika na matumizi ya fedha nyingi
alizokuwa amewekeza kwa jamaa hao kwa
makubaliano ya yeye kupata mafuta kutoka
visima vinavyomilikiwa nao huko Mashariki ya
kati kwa muda wa miaka mitano zaidi.
Aliendelea kukenua huku akiwatazama mmoja
mmoja, “Kwa hiyo leo kuanzia saa nne asubuhi
televisheni za Tanzania zitapendeza kwa maua
mazuri mtakayorusha kumpokea Jegan uraiani?”
Scolleti akawauliza.
“Kabisa yaani kama ulikuwepo,” Shailan akajibu.
“Na vipi kuhusu huyu mwanamke wao?” Scolleti
aliuliza akimaanisha Gina.
“Huyo nia yetu tumtumie kama chambo cha
kumnasa Kamanda Amata, lakini sijajua mpaka
sasa kinaendelea nini, hakuna taarifa katika yadi
zote mbili,” Shailan akajibu. Shakrum akainua
redio call yake na kuita.
“Yadi moja, yadi moja, ova”.
“Yadi moja tunakupata, ova,” akajibiwa.
“Usalama tafadhali, nipe ripoti, ova”
“Kila kitu salama, hakuna tatizo, ova” akajibiwa
kwa kupewa taarifa hiyo ambayo kwa walinzi
hao ilikuwa sawa, baada ya hapo aliita yadi ya
pili ili kujua nako nini kinaendelea, majibu
hayakuwa tofauti, lakini kumbe hakujua kama
aliyejibu kutoka yadi mbili alikuwa kawekewa
mtutu wa bastola kichwani akishinikizwa kujibu
hivyo, shinikizo la Kamanda Amata. “Ok sasa
twende kwenye point yetu na tusubiri muda
ufike, Tajan utabaki yadi mbili kusubiri kama
kutakuwa na lolote, ikiwa hakuna basi saa nne
umuue Yule mwanamke kisha uje kwenye point
yetu,” Shailan alikuwa akipanga kikosi,
akamgeukia Yule mwingine, “Tashrini, wewe
utakuwa gereza la Ukonga pale kutujulisha kila
kinachoendelea, ukishahakikisha Jegan
ameondolewa eneo lile ufuate msafara na
uhakikishe amefika ubalozini bila kugundulika,
baada ya hapo uje kwenye point, saa tano kamili
tutaondoka wote kwenye point kuelekea
Mombasa tukiwa na Jegan Grashan, Scolleti
kama ulivyopewa maelekezo, ila kwa sasa
tunakushukuru kwa msaada wako, asante,”
Shailan alimaliza na kila mtu akawa katika hali
ya kwenda kwenye kitengo alichopewa.
§§§§§
GINA akiwa amechoka sana, mwilini mwake
akiwa na nguo ya kulalia tu, alikuwa chini ya
ulinzi mkali, walinzi wanne walikuwa nje ya
kibanda alichofungiwa wakizungukazunguka na
bunduki zao zilizosheheni risasi zikiwa mikononi
mwao huku vidole vyao vikiwa vimepachikwa
katika kifyatulio tayari kwa amri yoyote
itakayotolewa. Mara sikio la Gina likaanza
kupata ukelele wa kitu kama mluzi, kwataabu
kidogo akanyanyua mkono na kukifyatua kile
kitufe cha heleni na kukipachika sikioni mwake.
“Heyyy!!” akanong’ona, kisha akajibiwa vivyo
hivyo.
“Uko wapi Gina,?” Kamanda Amata aliuliza kwa
kunong’ona maana huwezi kuongea kwa sauti
eneo kama hilo.
“Wamenifunga chini ya ardhi, tafuta mlango
uliondikwa ‘Kisima’ ” Gina alitoa maelekezo.
Mara Yule askari wa jirani yake akasikia
mnong’ono ule.
Akamuendea Gina mpaka pale alipo,
akamtazama usoni akiwa kamuinamia.
“We mwanamke, unaongea na nani au umepata
kichaa?” Yule askari akamuuliza huku akiwa
kamshika kichwani na bunduki yakeikiwa
imeshikwa kwa mkono mmoja.
“Naongea na shetani, unataka kumuona?” Gina
akamuuliza Yule askari.
“Unaleta upumbavu sio! Akarusha mkono ili
amtandike kofi Gina, Gina akaepa lile kofi na
kumpiga kichwa askari huyo, akaangukia upande
wa pili, Ginaakajinyanyua na kumuwahi koromeo,
alimkaba kwa nguvu zake zote,Yule askari
alijitahidi kujikukurusha kutoka katikamikonoya
Gina ambayoilisukumwa na nguvu za hasira.
Yule askari akainua miguuyake na kuidaka
shingo ya Gina kisha akamvuta nyuma kwa
miguu yake. Gina aliiachia shingo ya askari huyo
na kutaka kujinusuruna ile kabali ya miguu
toka kwa askari Yule, alipoona
kuwa njia hiyo anayotumia ni ya kizamani
alijifayatua na kukubali uole mvutonwa ile
miguu, akajirusha nyuma na kuchomoka bilatabu
katika miguu hiyo, kwa haraka akasimama
wima. Kelele za askari wengine wakiitana nakuja
upande huo kutoa msaada zilimfikia Gina sawia
kabisa, Yule askari pale chini alipotakakujiinua
alizimishwa kwatekekali la usoni,akarudi chini na
ile bunduki ikamtoka mikononi, Gina akaiwahi na
kuimiliki mikononi mwake, akaiweka sawa na
risasiya kwanza ikamteremsha askari aliyekuwa
juu ya ngazi akiteremka kuja chini, akajibwaga
kama mzigo. Gina alianzakufanya kazi ya
kujinasua kutoka huko kisimani, akayapita
mapipa kadhaa ya mafuta nakutoke upande
mwingine.
“Kamanda Amata!” aliita.
“Nakusoma, Gina niko njiani kuelekea huko,”
aliongeakwa kunong’ona kama awali.
“Nimedhibiti kisima, usiwe na shaka,” Gina
alimpa taarifa Kamanda Amata ambaye alikuwa
mbioni kwenda kumuokoa.
Majibizano ya risasi za Gina na wale askari
yalisikika wazi kabisa. Gina alijikuta anaingia
katika pambano la hatari na askari hao huku
akitafuta njia ya kutokea ndani humo.
“Tulia hivyo hivyo mwanamke hayawanimkubwa
wewe!” sauti ilitokea kwa nyuma, Gina akageuka
wakati akiamuriwa kuweka silaha yake chini na
kunyoosha mikono yake hewani.
“Unajifanya komandoo wa kike sio?” Yule askari
aliongea huku akimfuata Gina na shotgun yake
ikiwa tayari kwa lolote lakini kabla hajamfikia,
alipaishwa juu na kujibwaga chini kama gunia
jirani kabisa na miguu ya Gina, Gina akainua
shingo uso kutazama kule risasi hiyo ya
ukombozi ilikotokea maana alijua wazi kama
Yule askari angemfikia basi ilikuwa ni kipigo cha
mbwa mwizi, akamuona Kamanda Amata kama
kawaida yake akirusha karanga moja moja
kinywani mwake.
“Kamandaaa!” akaita kwa furaha huku
akimkimbilia.
“Ginaaaa!” Naye alijibu wakakumbatiana kwa
furaha, kisha wakaanza harakati za kutoka nje,
Kamanda alitangulia mbele na Gina alifuata
nyuma. Njia ilikuwa nyeupe ya kutokea nje kwani
Kamanda alikuwa tayari kafanya kazi kubwa ya
kuwateremsha wote waliokuwa hai ndani ya
jengo hilo.
Walitoka nje ya jengo hilo na kuuendea ukuta
upande wa nyuma, akaikutanisha mikono yake
kwa nyuma kwa kuifunganisha viganja.
“Gina kanayaga hapo uruke nje!” akamwambia
Gina. Baada ya Gina kuruka na kutua nje ya
ukuta huo naye akapanda kiufundi zaidi kisha
wote wawili wakatokomea na kuacha maafa
katika yadi hiyo, akaenda alipoficha pikipiki yake
na kuitoa, akakaa nyuma ya usukani na Gina
akatulia nyuma yake.
“Kamanda kabla hujaondoka sikiliza, kuna
mpango mbaya sana hawa jamaa wameupanga
dhidi ya Watanzania leo saa nne asubuhi, lakini
sijajua ni wapi wanataka kutekeleza unyama
huo,” Gina aliongea haraka harakakiasi kwamba
ilikuwa ni ngumu kwa Kamanda kuipata vizuri
sentensi hiyo. Gina akarudia alilolisema
akisisistiza kuwa amewasikia wao wenyewe
wakiongea katika kikao chao usiku huo.
Kamandaa akaitazama saa yake, akaona jinsi
ilivyopanga vishale vyake, kile kifupi kwenye
namba nne juu kidogo na kile kishale kirefu
kilikaribia namba sita, yaani saa kumi na dakika
ishirini na kadhaa, akaishusha na kuwasha
pikipiki lake kisha akaondoka kwa kasi.
§§§§§
Baada ya kikao cha Scolleti na watu wake
kukamilika, Scolleti alibaki peke yake katika
ofisi hizo za FK Security Group,
alipohakikisha kila kitu kipo sawa na hakuna
mtu mwingine mle ndani, akabonya kitufe
Fulani kilichofichwa ukutani nyuma ya
kalenda, mara mlango mkubwa ukafunguka
kwa chini na ngazi ndefu zikaonekana
zikishuka, akateremka taratibu na ule
mlango ukajifunga nyuma yake. Akalegeza
tai yake na kuvuta suitcase yake iliyokuwa
kitandani, akapekuwa ndani na kukuta kila
anachokihitaji kipo sawa, akapekua hapa na
pale na kuweka sawa hati mbalimbali
ikiwemo ya kusafiria, tiketi ya ndege
iliyokuwa iondoke saa mbili asubuhi ya julai
saba kuelekea Nairobi kwa kikao kingine na
hao watu wake wa Freedom Fighters.
Akafunga mkoba huo na kuingia maliwato,
 
CHAPISHO LA 20

......akajiswafi na kutoka nusu saa baadae.
Alipohakikisha yuko kamili akaburuza hiulo
sanduku lake na kutoka njea kwa mlango
mwingine. Kelele za majogoo zilikuwa tayari
zikipasua anga kuashiria kuwa kumekucha.
Saa kumi na moja alfajiri, Scolleti alishika kitasa
cha mlangowa gari yake aina ya Land Cruiser
VX, akapakia sanduku lake na kisha yeye
mwenyewe kuingia mlango wa dereva. Akaketi
tayari kwa kuondoka, mara akahisi kitu baridi
kikimgusa nyuma ya shingo yake.
“Tulia, fuata maelekezo ninayokwambia, washa
gari na utoke nje ya eneo hili,” ilikuwa sauti nya
kike iliyopenya masikio ya Scolleti, haikuwa sauti
ngeni. Akawasha gari na kutoka getini
akifunguliwa na walinzi kisha akafuata barabara
hiyo mpaka katika barabara kubwa ya Bagamoyo
karibu kabisa na mataa ya Morocco. Yule
mwanamke akamuamuru kufuata barabara ya
kwenda Mwenge naye akafanya hivyo, alipoingia
tu barabara kubwa kuelekea Mwenge na muda
huohuo Kamanda Amata alikuwa akiwasili eneo
hilo, akapiga kona kali na pikipiki lake na kuanza
kuifuata ile VX kwa maana alikuwa anaifahamu
sana. Aliifuata taratibu mpaka maeneo ya Tangi
bovu ile VX ikasimama pembeni. Akateremka
akiwa mikono yake iko kichwani.
ShaSha nae akateremka chini akiwa kamnyoshea
bastola Scolleti.
“Kila kona watu wanalalamika juu yako,
nimetumwa kwa jambo moja tu, serikali yako ya
India imekuchoka, imechoka kulalamikiwa na
nchi rafiki hata kupelekea kuharibu uhusiano wa
kidiplomasia kwa ajili yako haya yote,” ShaSha
aliongea kwa lugha ya Kihindi, Kamanda Amata
na Gina walisimama kwa tahadhari nyuma
kidogo ya nguzo kubwa ya chuma iliyobeba
tangazo kubwa la Safari Lagera, alikuwa akisikia
wanachokiongea alikuwa akielewa kidogo lugha
hiyo.
“Siko tayari kurudi India,” Scolleti alijibu.
“Swala sio kurudi India, kwanza hakuna
anayekutaka kule, hata mimi nimetumwa
kuchukua nafasi ya Israel ambaye anachelewa
kuja kwako kutimiza kazi yake, nimetumwa
kukuua,” ShaSha aliongea kwa uchungu. Scolleti
aliposikia swala la kuuawa akashusha mikono
yake na kugeuka mzima mzima na kutazamana
na domo la bunduki ya mwanamke huyo.
“We msichana, wenzako hawakuwa wajinga
kukutuma, ni kwa sababu ya kimbelekimbele
chako tu, nani hapa duniani mwenye uwezo wa
kupambana au kumkamata au kumuua Scolleti?
Kwa taarifa yako ni Mungu tu, na hata huyo
Mungu mpaka leo anajishauri anianzie wapi,”
Scolleti aliongea kwa kujiamini huku mikono yake
kajishika kiunoni.
“Unajiamini sio?” ShaSha akauliza.
“Sio najiamini, ila nataka nikwambie kitu
ambacho wewe hukijui, sikiliza, wewe na serikali
ya Tanzania nani mwenye uwezo wa
kunikamata? Kama wao wamenipokea na kila
mwezi nawapa pesa nzuri iliyotakata viongozi
nao wananihifadhi ujue wazi utafia hapa. Kila
mtu atakushangaa kusikia umeniua, Watanzania
watakushangaa sana na kukupiga mawe,”
akasonya, “Toa kibunduki chako hapa,” akaipiga
kwa kofi ile bunduki ya ShaSha nayo ikatoka
mkononi na kuanguka chini, alipotaka kuiokota
tu Scolleti akawa tayari na bastola mkononi.
“No no no no, usijaribu hilo kabisa,” Scoleti
alimwambia ShaSha huku akimuelekezea bastola
kubwa lenye nguvu, revolver, kichwani mwake,
“Kama unataka utajiri we sema, nitakupa pesa
na si kunifatafata mimi, mi sifuatwifuatwi namna
hii, unanidhalilisha, sasa kwa taarifa yako mimi
sikamatiki, na kila anayeifuata harufu yangu
lazima nimmalize kama nitakavyokufanya wewe,
polisi wengi na wapelelezi wan chi hii na
nyinginezo wametajirikakwa pesa zangu, mimi
ndio Scolleti Shang’harandha, nakuua halafu
ukawaambie kuzimu kuwa chini yaofisi yangu
kuna ghala kubwa la silaha za kisasa, sawa?”
Scolleti alipomaliza kusema hayo. Aliondoa
usalama wa bastola yake, kidole kwenye
kifyatulio akakikunja huku akibana meno, ShaSha
akajishika kichwani kwa mikono yote miwili
akijua kuwa sasa nay eye siku yake imekwisha.
“Aaaaaaaiiiiggghhhh!!!!” Scolleti alitoa ukelele wa
uchungu huku ile bunduki yake ikimtoka
mkononi, na mkono wa kushoto akijishika
kiganja cha ule mkono ulioshika bunduki, damu
zikitiririka. ShaSha aliiwahi ile bunduki yake pale
chini na kuiweka tayari kutekeleza lile
alilotumwa.
“Nani alikwambia kuwa serikali hii inakuogopa?”
Ilikuwa ni sauti ya Kamanda Amata akisogea
taratibu pale aliposimama Scolleti, “Unajifanya
unatoa misaada ya kibinadamu kumbe nyuma
yake unafanya maovu makubwa ya
kumuangamiza binadamu huyohuyo, sasa leo
ndiyo mwisho wa yote haya.”
Kabla Amata hajamalizia kauli yake, ShaSha
aliyekuwa sasa hataki kupoteza nukta, alifumua
kifua cha Scolleti kwa risasi tatu, bwanyenye
huyo akajibwaga chini kwenye vumbi.
“Go Bastard !” ( nenda mwanaharamu ), ShaSha
aliishusha bunduki yake huku akihema kwa
hasira, kisha akageuka na kumtazama Kamanda
Amata.
“Sorry Kamanda, najua, labda ulimtaka akiwa
hai, lakini nimetimiza nililotumwa, na wakuu
wangu wa kazi watapenda kuona picha za mwili
huu leo hii ukiwa hauna uhai, lakini asante sana
kwa kuniokoa”. ShaSha alimwambia Kamanda
huku akimwendea na kumkumbatia kwa nguvu,
akampa busu la ulimi. Gina kutoka pale alipo
alisonya na kuita “Kamanda!”. ShaSha na
Kamanda wakageuka, na kuachana.
“Gina, huyu ni ShaSha, detective kutoka India,”
kisha akamgeukia Gina na kumtambulisha kwa
ShaSha.
Baada ya kupiga picha kadhaa kwa kamera yake
ndogo wakasaidiana na kuupakia ule mwili
katika buti la ile VX kisha Kamanda Amata
akapiga namba ya dharula, 112, na kuwataarifu
polisi juu ya mauaji hayo akijitambulisha kama
raia mwema.
Juu ya pikipiki moja wote watatu walitosha na
kuondoka eneo hilo. Tayari muda huo watu
walianza kutoka majumbani mwao na kuanza
shughuli mbalimbali, saa kumi na mbili asubuhi.
§§§§§
9
Pambazuko la
Julai 7


MADAM S alitulia kando ya dirisha lake la
ofisini, ilikuwa ni saa moja imepita tangu
aingie ofisini asubuhi hiyo, hakujisikia
kufanya lolote siku hiyo, mawazo na akili
yake yote vilisimama, kwa ujumla alikuwa ni
mtu wa mawazo mengi sana. Aliitazama saa
yake na kuona bado dakika tisini Yule gaidi
aachiwe huru kutoka gerezani. Akainua simu
yake na kumpigia kijana wake.
“Chiba, naomba uwe unanipa taarifa yoyote
ya kinachoendelea hapo Ukonga mi sijisikii
kuja huko kisha tuonane hapa mchana wa
leo,” akakata simu. Akabonya namba
nyingine na kuweka sikioni.
“Kamanda Amata, saa nne kamili Jegan
Grashan anaachiwa huru..” kabla hajamaliza
kusema sauti ya Amata iliikata ile ya Madam
S.
“Sikiliza Madam! Kwanini tunakuwa waoga
hivi, kazi ya kukimaliza kikundi chao
inawezekana kabla ya hiyo saa nne, kwa nini
mnamuachia mtu ambaye amedhulumu
maisha ya binadamu wengi duniani,
sikubaliani na ninyi, mkimuachia najua
nitachofanya lakini Grasha hawezi kuiacha
hii ardhi ya Tanzania akiwa hai,” Kamanda
akakata simu.
Madam S alishusha pumzi ndefu na kurudi
katika kiti chake akajitupa na kuchukua
kitambaa cha kufutia jasho akajifuta uso
wake.
Kwa ujumla Madam S alikuwa
amechanganyikiwa, hajuila kufanya, mara
simuyake ikaita tena, ilikuwa nisimu ya
Kamanda Amata, akaitazama na kisha
akaipokea mara moja.
“Madam, hao jamaa mnaotaka kumuachia
ndugu yao, wametega bomu kama si mabomu
katika uwanja wa maonesho wa Mwalimu
Nyerere pale Sabasaba, taarifa hiyo
nimeipata kutoka katika tafutishizangu
zausiku wa leo. Naomba kwa amri yako
ulishughulikie hilo haraka sana kabla
Watanzania wengine hawajapoteza maisha,”
kamanda Amata alimwambia Madam S kisha
akakata simu na kuizima kabisa.
Madam S, alikiona kiti cha moto, kila
alipopiga simu kwa Kamanda Amata
haikupatikana, mara alijishika kichwa mara
akaijisjika kiuno, aliliendea dirisha kubwa
lililo katika ofisi yake linaloangalia barabara
kubwa, akatfakari, na kuitaza kalenda yake
ya ukutani, Julai 7 iliipamba kurasa ya
mbele, siku hiyo ambayo ni mapumziko ya
kitaifa Tanzania ilikuwa ni siku ya ufunguzi
rasmi wa maonesho ya saba saba, maonesho
ya kimataifa ya biashara ambayo hujumuisha
makampuni makubwa kutoka mataifa
mbalimbali, aliwasha luninga yake na kukuta
matangazo ya moja kwa moja kutoka katika
uwanja huo wa Mwl Nyerere. Mamia kama si
maelfu ya Watanzania walikuwa wakizidi
kumiminika ndani ya uwanja huo.
Madam S akakurupuka kutoka katika
mawazo ambayo yalimchelewesha kutoa
maamuzi, akainua simu na kupiga moja kwa
moja kambi ya jeshi la Mgulani na kuwapa
hiyo taarifa na kuwaomba wasiipuze....
KUMEKUCHA ..... USIKOSE SEHEMU IJAYO....
 
CHAPISHO LA 21
UWANJA WA MAONESHO SABASABA


Saa 2:57 asubuhi

MUDA HUO kila aliye nyumbani alikuwa akitoka
kama sin a familia yake basin a marafiki kwenda
kujionea bidhaa mbalimbali zinazooneshwa huko
katika viwanja vya sabasaba. Tarehe saba
mwezi wa saba daima ni siku ya mapumziko
kwa wafanyakazi wa kila aina hapa nchini
isipokuwa tu wale wenye idara nyeti.
Mambo mengi sana yalikuwa huko kama
vinywaji, vitafunwa, bendi mbalimbali za muziki
zikitumbuiza katika mabanda mbalimbali ya
biashara, michezo ya watoto kama mabembea,
treni ndogo ambayo inakuzungusha kuona
mandhari ya uwanja huo na kadhalika. Mistari
mirefu ya Watanzania ilikuwa ikisubiri kuingia
ndani ya uwanja huo asubuhi hiyo, kila mtu
alitaka kuwahi kuingia ili akaitumie pesa yake
vizuri, ilikuwa ni kawaida kwa kila mwaka
kuwapo na tukio hilo. Polisi wenye farasi na
mbwa walizagaa tayari kwa lolote maana penye
wengi pana mengi.
Siku hii ikuwa mheshimiwa waziri mkuu wan chi
aje kutembelea maonesho hayo, hivyo ulinzi
uliimarishwa kila kona.
Katika moja ya mabanda yaliyomo humo ndani
hili lilionekana kuvutia wengi sana, watu
walikuwa wakijazana kuangalia umahiri wa
vijana aliokuwa wakionesha katika kukabiliana
na majanga ya moto na mambo ya uokoaji.
Wakiwa wamevaa maguo yao ya kiung’aa
ambayo hayashiki moto, kila mtu alipenda
kwenda hapo kujifunza juu ya kujikinga na
kuukabili moto, moto na athari zake, aina za
moto na jinsi gani ya kumsaidia mtu aliyepatwa
ajali ya moto. Kutokana na hilo kila mtu
alisogelea banda hilo hilo kuangalia na kujifunza.
§§§§§
Ngrrrrrrrrrrrrrrrr ngrrrrrrrrrrrrrrr, simu iliita kwa
fujo katika moja ya ofisi za jeshi Mgulani. Huyu
bwana aliyekuwa katika chumba cha
mawasiliano alikuwa amesinzia hata hakusikia
kelele zote hizo za simu hiyo ya kizamani
ambayo ikiunguruma lazima uzibe masikio kwa
kelel zake. Akakurupuka kama aliyetoka
kufumaniwa, akainyakuwa na kuiweka sikioni.
“Hallo, hapa ni kikosi cha jeshi Mgulani,
nikusaidie nini?” aliongea askari Yule.
“Unaongea na idara ya usalama wa taifa,
naweza kuongea na mkuu wa kambi?” sauti ya
madam S iliunguruma katika chombo hicho. Yule
askari akatulia kwa pozi na taharuki, kisha
akajibu, “Subiri na usikate simu tafadhali,” alijibu.
Baada ya sekunde chache Madam S
aliunganishwa na mkuu wa kambi hiyo, kambi ya
Generali Twalipo, taarifa ya tetesi za bomu
ilimfikia mkuu huyo, Meja Jenerali Kisanga, naye
akapeleka taarifa panapohusika, muda huohuo
wakapewa taarifa wataalamu wa milipuko wa
jeshi, wakajiandaa na kila kitu kinachohitajika
wakaingia kwenye jeep takribani tatu za kijeshi,
safari fupi ya kufika eneo hilo ikawadia.
Kila mtu alishangaa katika ule uwanja wa
maonesho, wanajeshi kama thelethini wakiwa na
vifaa vya ajabu waliteremka na kusimamaisha
zoezi la watu kuingia ndani ya uwanja huo, kisha
kutoa taarifa kwa wanausalama waliopo humo
ndani kuanza kutoa watu wote waliomo ndani ili
uwanja huo ubaki mweupe yaani bila watu.
Kiongozi wa oparesheni hiyo alitoa amri mara
moja watu wote kutolewa nje, msafara wa waziri
mkuu ukasitishwa kutoka nyumbani kwake
kwenda katika viwanja hivyo, hali ikawa tete,
milango ya kuingilia uwanja huo haikuwa
ikitosha kutokea, kila mtu alifikiri kuokoa maisha
yake.
Wanajeshi waliokuwa na vifaa mikononi vya
kuweza kutambua milipuko waliingia ndani ya
uwanja huo na kutembea kila mahali kutafuta
uwezekano wa kuwepo aina yoyite ya mlipuko.
Counter-IED kifaa maalumu kwa kazi hiyo
kinachofanya kazi peke yake bila kushikwa na
mtu kilitumwa kuingia katioka uwanja huo,
kilikuwa kikitembea barabarani taratibu
kikisimama hapa na pale, huku wanajeshi
wengine wakitapakaa sehemu mbalimbali. Bado
watu walikuwa wakiendelea kutoka katika
uwanja huo, ilikuwa ni patashika kweliweli.

GEREZA LA UKONGA

Saa 09:00 asubuhi
GARI za ofisi ya ubalozi wa nchi ya Jegan
Grashan ziliingia katika geti la Magereza lililoko
upande wa kaskazini nmwa ngome hiyo,
zikajivuta taratibu kuelekea lango kuu la gereza
mpaka kwenye maegesho. Waandishi wa habari
kama kawaida walikuwa hapo wakitaka
kushuhudia na kupiga picha za gaidi huyo
ambaye siku hiyo alikuwa akiachiwa huru. Askari
wa KM wa Magereza walikuwepo kulinda
usalama kama kuna hatari yoyote itakayotokea.
Kamishna wa magereza, mkuu wa magereza
mkoa wa Dar es salaam na wahusika wengine
walikutana kwenye chumba maalumu kwa ajili
ya kukabidhiana mfungwa huyo. Maofisa wa
ubalozi walikuwa pale tayari kumchukua raia
wao. Ilikuwa utata mtupu. Jegan Grashan
aliletwa ndani ya chumba hicho akiwa na pingu
pamoja na minyororo miguuni mwake
akasimamishwa sehemu ndani ya chumba hicho hicho.

Saa 09:15 asubuhi
Kamanda Amata, alikuwa juu ya pikipiki lake
akielekea Ukonga kushuhudia zoezi hilo, Madam
S alikuwa akifunga ofisi na hajui aende wapi,
ama sabasaba au Ukonga, alikuwa akijishika
kichwa kila mara kujiuliza la kufanya, hali ilikuwa
sio nzuri kichwani mwake, mama huyu alijiona
kwa siku hiyo moja kazeeka ghafla.
Wakati huohuo, freedom fighters walikuwa tayari
kwenye sehemu waliopangiana kukutana, lakini
walishangaa wawili kati yao walikuwa bado
kufika, wakajaribu kupigiana simu ili kujua
kulikoni majibu waliyoyapata yalikuwa tata.
Maafa, maafa ni hali iliyowakata matumaini ya
kumpata mwenzao, mara kidogo wakapata
taarifa ya kuuawa kwa Scolleti hapo
wakachanganyikiwa, hawakujua wafanye nini.
Shailan aliamu kuwapanga vijana wake upya,
akawaita hao wote walio katika yadi zile waende
haraka katika point ya kukutani ambapo wenzao
wote tayari walikuwa kwenye boti maalumu
wakisubiri kufuinguliwa kwa ndugu yao,
waondoke naye.

Saa 09:30 asubuhi
Madam S anazinduka, anawasha gari kuelekea
Ukonga, ilikuwa ni mapumziko hivyo hakukuwa
na foleni barabarani, aliendesha kwa kasi gari
yake aina ya BMW, ili awahi tukio hilo, alipuuzia
simu zote zilizokuwa zikiita, wakati huo. Akili na
mawazo yote yalikuwa kuwahi Ukonga.
Kamanda Amata alikuwa tayari kawasili eneo la
tukio, akaegesha pikipiki lake nje ya wigo na
kutulia usawa kabisa wa lango kuu,
akitenganishwa na barabara ya Pugu na
seng’enge iliyolinda gereza hilo, alimuona
Madam Salipokuwa akiingia getini na gari yake,
Kamanda akatikisa kichwa kuashiria, ‘kazi
imeamka’.
Kichwani mwake Kamanda alikuwa na mambo
mengi lakini alishindwa afanye nini, Sabasaba
aliamini kabisa kuwa JW watakamilisha hiyo
kazi ya kuutafuta huo mlipuko, lakini magaidi
wengine walikuwa wametoroka na mpaka hapo
hakujua wamekwenda wapi, alikuwa akisubiri
milipuko aliypitengeneza katika yadi zile ifanye
kazi, lakini zaidi alikuwa akitaka kumuona huyo
Jegan Grashan akiachiwa huru, akabaki juu ya
pikipiki lake huku akili ikiwa imesawajika, haijui
jema wala baya.
§§§§§
SHAILAN aliinua mkono wake kutaza saa yake
aina ya casio , tayari muda ulikuwa ukiyoyoma,
alikuwa akisubiri taarifa ya kutoka kwa Tashrini
aliyekuwa pale gerezani, ili awaambie tu kuwa
ndugu yao kaachiwa nao waanze sherehe kwa
kufungua champagne .
Yote yalikuwa sambamba, vijana wa JW wakati
huo kijasho kikiwatoka kusaka huo mlipuko
walioambiwa lakini bado walikuwa
hawajang’amua chochote, walianza kukata tama,
wakisema hakuna mlipuko wowote kwani kila
mahali ni salama kabisa, walitoa taarifa hiyo
kwa vyombo vya usalama. Na wao kujipanga
kuondoka kurudi kambini.
Chiba na Gina walikuwa wakielekea uwanja wa
maonesho ya sabasaba kushuhudia hali ilivyo,
wakapata taarifa hiyo ya kuwa kila kitu kiko
salama.
“Hapana Chiba, kuna mlipuko kule umewekwa,
naamini kabisa, kwa maana walipokuwa
wanautengeneza nilisiki amazungumzo yao!”
Gina aliongea kwa jazba huku akipigapiga
dashboard ya gari ya Chiba.
“Basi mama utavunja gari yangu wakati hata
mkopo benki sijamaliza,” Chaba akajibu kwa
utani.
Mara Chiba akaitoa gari yake baranbarani na
kuiweka pembeni alipokuwa maeneo ya polisi
ufundi.
“Vipi?” Gina aliuliza.
“Kuna mawimbi ya kielektroniki ya kigeni kabisa
yamepita kwenya kompyuta yangu,” akafungua
dashboard ya gari kwa kubonyeza mahali Fulani,
kulikuwa na kijikompyuta kidogo, akaingiza
nywila zake nayo ikaanza kufanya kazi,
akabonya hapa na pale, akaanza kusikia
mawimbi mbalimbali ya sauti, huku yakiwa
yanajichora kwa mistari ya kuyumbayumba lakini
pia yalikuwa yakifanya sauti Fulani. Chiba
alijaribu kuiweka sawa sauti hiyo ili aweze
kupata tafsiri ya mionzi hiyo, akajaribu na
kujaribu lakini ilikuwa ngumu kuigundua kirahisi,
akapima umbali inapotoka na inapokwenda kwa
kutumia namba maalumu anazojua mwenyewe.
“Gina, kuna hapa kuna kitu hakiendi sawa,
nikizungusha antenna yangu, inaniambia kuna
mawimbi mapya na mageni yanatokea mashariki
kuelekea, range yake sio mbali sana,” Chiba
alikuwa akituamia chombo maalumu
kilichofungwa katika gari yake, chombo
kinachojulikana kwa jina ‘MiniGRAIL’
kinachoweza kunasa mawimbi yoyote ya
kielektroniki yanayopita hewani. Chiba akachuku
laptop yake yenye nguvu, akapachika vifaa
maalumu vya kusikilizia, kisha akamwambia Gina
aendeshe gari kuelekea uwanja wa sabasaba.
Saa 09:45 asubuhi
“Jegan Grashan, uliyefungwa kwa tuhuma za
ugaidi katika ofisi za balozi ya Marekani,
unaachiwa huru na serikali ya Tanzania kwa
tamko la Rais wan chi, kuanzia saa nne kamili
leo hii utakuwa raia huru. Pamoja nahayo,
serikali inakutaka kuondoka nchini ndani ya
masaa 12 kwa njia yoyote, na hutakiwi
kukanyaga tena ardhi ya Tanzania, iwe wewe,
mkeo au watoto wako, imesainiwa jana tarehe 6
Julai na kugongwa mhuri wa Ikulu.” Hati hiyo
‘removal’ ilisomwa na kamishna wa
MagerezaTanzania huku akitetemeka,
alipomaliza, alimtaka Jegan kusaini mahali
Fulani, akafanya hivyo kisha nay eye akasaini
pale panapomstahili, wakapeana mikono na
zoezi hilo likakamilika, Jegana akatakiwa kuketi
chini kusubiri saa nne kamili ili atoke nje ya
gereza.
Madam S aliyefika kwa kuchelewa kidogo, alikuta
ndiyo wakisoma hiyo hati kutoka Ikulu, akatulia
na kushuhudia huyo jamaa akimwaga wino wa
kuondoka kama raia huru. Ijapokuwa ilimuuma
lakini hakuwa na jinsi, ikishaandikwa na Rais
basi haiwezi kubadilika labda abadili yeye
mwenyewe.
Japokuwa siku hiyo ilikuwa ni mapumziko lakini
pia ilikuwa siku ya maombolezo ya watu
waliopoteza maisha kwenye pantone eneo la
Kivukoni siku iliyotangulia.
§§§§§
Gina aliegesha gari nje ya uwanja wa maonesho
ya biashara ‘sabasaba’ Chiba akashuka na
kompyuta yake akawa akieelekea ndani ya
uwanja huo. Moja kwa moja akiongozana na
Gina walifika kwenye banda kubwa la maonesho,
banda la zimamoto, liliandikwa kwa nakshi nzuri,
FK SECURITY and FIRE BRIGADE, banda hilo
lilijawa na watu kama mwanzo wakiangalia hayo
maonesho ya uokoaji. Chiba alipofika eneo hilo,
akaingia ndani ya ofisi kubwa iliwekwa vitu
mbalimbali, sasa akagundua kuwa yale mawimbi
aliyoyanasa yanaishia hapo kati banda hilo.
Akavua makorokoro yake na kuyaweka mezani
akachukua simu yake na kubofya namba flani.
“Chiba anaongea,” alizungumza mara tu baada
ya simu ile kupokelewa na Madam S,
“Ndio Chiba niambie,” Madam S alimwambia.
“Kuna mawimbi ya kielektroniki nimeyagundua
katika mtambo wangu, na nimeyafuatilia sasa
nipo hapa uwanja wa sabasaba, nina wasiwasi
na banda hili la FK Security maana signal
zinaonesha kuwa hapa niliposimama ndio point
ziro, nipe mamlaka nifanye kazi inaonekana kuna
hatari kubwa sana eneo hili,” Chiba alimaliza.
Kila mtu aliyekuwa ndani ya banda hilo
alimshangaa Chiba, hakumuelewa ni nini alikuwa
akisema.
Madam S, alijikuta akidondokwa na simu
mikononi, akiwa kapigwa na bumbuwazi, akili
ikamchanganyika, akamtazama Jegan pale
kwenye kiti, kisha akaiokota simu yake.
“Fanya lolote kuzuia hali hiyo,” Madam S alijibu,
kisha akapiga namba ya Kamanda Amata na
kumpa taarifa hiyo, akatoa tena taarifa Jeshini
kwa mara nyingine.
NI HALI YA HATARI, JE NINI KITATOKEA?
 
SEHEMU YA MWISHO...

Shailan, Shakrum wakiwa ndani ya boti
wakimsubiri Jegan, muda wao ulikuwa umefika
wa kile wanachokiita ‘kutoa shukrani kwa
Watanzania’ , Shakrum alifungua briefcase yake
kubwa na kuanza kubofya hapa na pale akipanga
renji na kila kitu, kisha akawasha kuitafuta sakiti
aliyoitengeneza ndani ya tanki la mafuta lakini
lililojazwa gesi aina ya methane upande mmoja
na mwingine liquefied petroleum gas (LPG),
vyote vilikuwa vimeshindiliwa kwa mkandamizo
mkubwa sana kiasi kwamba zikidaka moto basi
ilo tanki lote lazima ligeuke kombora baya kuliko
kombora lenyewe.
Shakrum alipofanikiwa kupata uelekeo wa sakiti
hiyo na kuanza kuhesabu muda wa kuiwasha ili
itengeneze moto ndani ya tanki hilo, tayari Chiba
alikuwa ameyanasa mawimbi hayo, hivyo
alichokifanya hapo sasa ilikuwa ni jinsi gani ya
kuyakata, ili kusiwe na mawasiliano kati ya vitu
hivyo viwili. Chiba akaendele kucheza na
kompyuta yake, ilikuwa ngumu kuelewa ni nini
anakifanya kwa ni ni namba tu zilizokuwa
zikonekana kupishana na katika kioo cheusi cha
kompyuta. Kwa kutumia program maalum kwa
kazi hiyo ambayo Chiba aliipata wakati akiwa
katika mafunzo huko NASA alifanikiwa
kuyakamata mawimbi yale na kuyafanya
yasitende lililokusudiwa, kisha akaanza kufanya
ukaguzi sehemu mbalimbali za jengo lile.
“Oooh shiiit!” Shakrum alionekana wazi
kuchanganyikiwa kwa hilo, aligundua kuwa kuna
muingiliano wa mawimbi umetokea, kila
alipojaribu bado alijikuta anakwama, nywele
zikamsimama.
“Washenzi wameyaingilia mawimbi yangu,”
akamwambia Shailan.
“Inawezekanaje?” Shailan akauliza.
“Itakuwa kuna mtaalam wa mambo haya ndiye
kafanya hili” Shakrum akajibu.
“Sasa tutafanyaje?” Shailana akauliza.
“Hatuna jinsi kama inawezekana hapa ni kufika
eneo husika na kutumia mbinu nyingine, mbinu
mbadala ya kulipua lile tank bila ya sisi
kudhurika,” Shakrum alieleza huku akiisogeza
kompyuta byake pembeni, akakizungusha kiti na
kugeuka walipo wenzake. Mara simu ya Shailana
ikaita, alipoitazama ilikuwa namba ya Tashrini,
akajua mambo yameiva, kwa vyovyote vile.
“Ndiyo Tashirini, nipe taarifa,” Shailan
alizungumza kwenye simu.
“Jegan yuko huru na sasa anatoka gerezani,
nasikia kelele nyingi za wafungwa wengine,
zikimsindikiza nje,” Tashrin akajibu.
“Mungu mkubwa, kamwe hamtupi mja wake, hii
ndiyo njia pekee ya kuwashinikiza hawa
wanaojipendekeza kwa mataifa ya Maghalibi,”
Shailan alijibu huku wengine wote wakishangilia.
Saa 04:00 asubuhi – Gereza la Ukonga
JEGAN Grashan aliachiwa huru, hakuwa na pingu
za mikono wala za miguuni. Alitembea kwa
hatua zake mwenyewe ijapokuwa alikuwa na
uchovu kidogo. Madam S na wakuu wengine
waliokuwa pale, walimshuhudia gaidi huyo
akiondoka taratibu katika gereza hilo, akipita
katika mlango mkubwa na kuelekea katika gari la
ubalozi lililoandaliwa huku akisindikizwa na
maofisa usalama wa ubalozi wa nchi yake,
akaingia na kufunga mkanda sawia, akashusha
kioo na kumuonesha Madam S alama hya mkono
akiashiria kuwa amemtukana tusi baya kabisa,
ile gari ikaondoka. Msafara wa gari nne zenye
namba za njano kwenye kibao cha kijani
zililiacha geti la gereza na kushika barabara ya
Nyerere kuelekea mjini.
Kamanda Amata akawasha pikipiki lake na
kuvaa kofia yake ya usalama iliyomficha uso
wake, moyo wake ulijawa na gadhabu ya
kuachiwa huru Jegan, hakupenda hata kidogo.
‘Liwalo na liwe,’ akajisemea na kuaca kati yake
na wao magari kama sita hivi kisha akaingia
barabara ni na kuondoka.
Uwanja wa maonesho sabasaba
Gina alisikia mlio wa beep kutoka eneo Fulani
lililokuwa na matanki makubwa kwa ajili ya
maonesho ya kampuni hiyo.
“Chibaaaa!” akamwita kwa ukelele, Chiba
akaacha kompyuta yake na kukimbilia kwa Gina,
akausikia mlio wa beep hiyo, haraka sana
akapanda juu ya tanki moja na kulifungua kwa
shida mfuniko wake, ule mlio ulikuwa
ukiongezeka. Wakati hayo yakitukia, polisi
waliokuwemo uwanjani wakisaidiana na vijana
wa skauti kutoa watu nje ya uwanja, na
kuwaweka mbali na eneo hilo, vijana wa jeshi
walirudishwa tena kuhakikisha usalama huo.
Chiba alikuwa akifungua ule mfuniko kwa tabu
maana aulifungwa kwa kifungo maalum,
haikuwezekana kukata kwa gesi maana unaweza
ukasababisha mlipuko usio wa lazima.
§§§§§
Kamanda Amata akiwa tayari kwenye pikipiki
yake aliingia barabara ni, nyuma ya msafara wa
gari zilizombeba Jegan, kichwa chake
kilishatawaliwa na gadhabu mbaya juu ya mtu
huyo, hakuamini kabisa kuwa anakuwa huru na
kuacha uovu wake, hapana, bali aliamini wazi
kuwa bado maadamu yupo hai basi ataendelea
kufanya yale anayokusudia kwa raia wengine
wasio na hasira, alivuta mafuta na kutafuta
sehemu nzuri ambayo angeweza kufanya yake,
kufanya lile alilokusudia. Kama unavyojua kasi
ya gari za ubalozi haikuwa ya kawaida, yakiwa
yamewasha vimulivimuli na kupishwa yalikuwa
yakienda kasi kwelikweli. Mara saa ya Kamanda
ikaanza kutoa kamlio hafifu, akauinua mkono na
kuisikiliza inasemaje.
“Kamanda Amata, Chiba hapa,” alikuwa ni Chiba
aliyekuwa akimpigia Kamanda wakati huo.
“Nimekusoma chiba endelea,” kamanda aliirusu
simu hiyo.
“Nipo, uwanja wa maonesho wa sabasaba hapa
Mtoni Mtongani,” akaendelea kusema.
“Endelea,” Kamanda akamruhusu aendelee
kuzungumza.
“Kuna aina ya mlipuko ambayo imetegwa hapa,
sasa najaribu kutafuta chanzo lakini naona
kidogo utaalam unaniishia, pamepekuliwa kwa
mitambo ya kisasa lakini hakujaonekana bomu
wala kitu kinachofanana na hicho, nipe aidia
mpya tafadhali,” Chiba alieleza lile linalomsibu.
“Ok, jaribu kutazama mitungi ya gesi kama ipo
maana nayo inaweza kufanya milipuko mibaya
kuliko bomu lenyewe, hakikisha kwa amri yako
umeclear eneo lote ili kama itabidi kufa basi ufe
peke yhako kama kiapo chetu kinavyosema, niko
njiani kuja huko huko, Jegan Grashan
amekwishaachiwa huru,” Kamanda Amata
alimjibu na kukata simu ile kisha akarudisha
mkono kwenye usukani wa pikipiki na kuongeza
kasi zaidi na zaidi, alikuwa akipita gari kwa
overtake za hatari mpaka madereva wa magari
walikuwa wakitukana kila mtu kwa lugha yake.
Dakika mbili baadae aliziona zile gari za ubalozi
zikiwa kasi katika eneo la Karakana karibu na
Tazara, sekunde chacahe akawa ameufikia
msafara huo.
‘Mtu wenu anaachiwa ninyi bado mnataka
mtulipue, sasa leo ama zangui ama zenu,’
Kamanda alijisemea huku akiupita ule msafara
kwa kasi na kuwa mbele yake. Kisha kama mtu
aliyepagawa alikunja kona kali na kuwa mbele
yao, zile gari nazo zikafunga breki kali mbele ya
pikipiki hiyo zikisota na kufanya ukelele mkali
kwa msuguano wa tairi za barabara, gari mbili
za nyuma ziligongana zenyewe kwa zenyewe na
ile ya mbele almanusura imgonge Kamanda
ambaye tayari alikuwa na bastola mkononi,
alikwishaiondoa usalama na alikuwa akiitafuta
shabaha yake anayoitaka. Kidole cha shahada
kikaitekenya ile bastola, risasi tatu zilipasua kioo
na kufumua kifua cha Jegana Grashan.
Muda na saa hiyohiyo
Milipuko mikubwa ilitokea katika maeneo mawili
tofauti, mmoja katika yadi ya Bunju ya
kuhifadhia mafuta iliyokuwa ikimilikiwa na
Scolleti nay a pili yadi ya Mabibo, kwa nukta na
sekunde ileile mabomu yaliyotegwa na Kamanda
Amata yalifanya mambo yaliyokusudiwa.
Mji wa Dar es salaama ulipatwa na hekaheka
siku hiyo kwani barabara ya Ally Hassan Mwinyi
ilifunikwa na gari za zima moto na ile ya
Mandela nayo vivyo hivyo. Moshi mkubwa
ulitanda anga ya Dar es salaam.
‘Kama walijifan ya wao magaidi basi hawakujua
kama na mimi ni gaidi zaidi yao,’ Kamanda
alijisemea huku akipita vitongojo vya katikati vya
wilaya ya Temeke, akafika mahali kulikuwa na
nyumba nyingi zilizobanana, Kamanda Amata
alipinda kona na kuingia katika ua wa nyumba
hiyo, moja kwa moja akaiegesha pikipiki yake
kwenye stoo ndogo ya mkaa, akaizima, akina
mama waliokuwa wakifua na kuosha vyombo
walipiga kelele na kuwanyakua watoto wao.
Kamanda Amata akashuka na kuvua ile kofia
ngumu akaipachika juu ya kioo cha kutazamia
nyuma, akavua yale mavazi ya kuendeshea
pikipiki na kuyaweka pale juu, akabaki na suti
safi nyeusi iliyopambwa na tai ya buluu,
hakuongea na mtu alitoka haraka na alipofika nje
alipanda tax aliyoikuta barabarani.
“Sabasaba tafadhali,” alimwamuru dereva.
§§§§§
Watu wa usalama wa ubalozi walijitahidi
kumsaidia Jegan Grashan lakini walichelewa,
ilikuwa ni mvurugano eneo lote, wamachinga
walikimbia huku na huku , wakiijaribu kunusuru
maisha yao.
Wanausalama wa ubalozi hawakuwahi
kumkamata Kamanda Amata kwani tayari
Alishakwisha waacha mbali. Wakabaki
wakitizamana hawana la kufanya.
Muda si mrefu, Land Cruiser moja nyeusi
ilipunguza mwendo katika eneo hilo la ajali
ambapo polisi wa usalama barabarani alikuwa
tyari yuko kazini na wale maofisa wa ubalozi
wakiwa wamezagaa nje na bastola zao
mikononi. Kioo cha gari ile kikateremka taratibu,
Madam S, akatzama lile tukio, akatikisa kichwa
chake na kupandisha kioo kisha gari ikaongeza
mwendo na kupotelea mjini.
§§§§§
Habari mbaya zilimfikia Shailan na Shakrum
waliokuwa katika boti wakisubiri wenzi wao ili
watoroke na kuwaachia Watanzania vilio vikuu
ndani ya siku wanayoipenda, siku ya Julai saba.
Shailana alihisi kuchanganyikiwa, kwanza kwa
habari ya kifo cha Scolleti, pili milipuko ya yadi
zote mbili, haikumuuma sana kwani si mali yao,
ila hili la kifo cha Jegan Grashan, Shailan na
Shakrum walilia machozi huku wakiwa
wamekumbatiana, na walikuwa hawajui hatima
ya wenzao waliokuwa katika yadi hizo ambao
walikuwa wakiwasubiri pamoja na Tashirni
aliyeleta taarifa hiyo. Shakrum akaiendea
televisheni na kuiwasha, hakukosea, kioo
kilikuwa kimepamba kwa maua ya moshi mzito
na wakati mwingine kwa tukio la Kalakana pale
Tazara, hasira akazima Tv na kurudi kwenye
kompyuta yake, akaketi lakini alipojaribu
kuichezea akakuta imefungwa kwa codes
maalum ambazo hakujua ni nani aliyefunga,
“Shiiiiiittttt!” akapiga ukelele nan kuipiga ngumi
ile kompyuta.
Shakrum na Shailan hawakuwa na la kufanya,
walitamani waondoke peke yao lakini hawakuona
vema, akaendelea kusubiri wenzao mpaka muda
waliopanga.

Saa 4:30 asubuhi

Simu ya Kamanda Amata ikaita tena wakatyi
akiwa maeneo ya Tandika kuelekea sabasaba,
akaitazama, Madam S, akatabasamu, ‘Lazima
kapata salamu zangu pale barabarani’
akajiwazia.
“Kamanda, upo wapi?” akauliza kwa ukali.
“Nipo Sabasaba Madam vipi?” Kamanda akajibu.
“Hivi we una akili kweli?” Madam akafoka
kwenye simu.
“Kwanini Madam? Nina akili timamu kabisa,”
Kamanda akajibu.
“Unajua unachokifanya wewe? Sasa
umeshaharibu na we mwenyewe unalijua hilo,”
Madam akaendelea kufoka kwenye simu.
“Madam tutaongea ofisini mi nipo kazini kwa
sasa,” Kamanda akajibu na kukata simu.
Madam S alikasirishwa sana na kitendo
alichokifanya Kamanda Amata, alipopita katika
eneo lile la tukio na kuona hali halisi alijua wazi
ni Amata kwa sababu alikwishasema mbele yake
na alishakula yamini juu ya hilo. Alijua nini
kinakuja kumkuta Amata, Madam alilia machozi
kwa hilo, alisikitika na kuumia sana, lakini
lilikuwa limekwishatokea, hakukuwa na jinsi.
Aliendesha gari yake taratibu kuelekea uwanja
wa maonesho ya sabasaba.
§§§§§
Chiba alifanikiwa kuufungua mfuniko wa tanki
kubwa la gesi, kosa moja alilolifanya ni kuwa
hakujiandaa kwa hali hiyo, ijapokuwa aliipata
sakiti iliyofungwa chini tu ya mfuniko huo lakini
yeye mwenyewe aliathirika sana na ile gesi
mbaya. Gina alimshuhudia Chiba akianguka
kutoka katika lile tanki kwa msukumo mkubwa
sana, akajishika mdomo kwa kiganja cha mkono
wake, akili ikaja haraka, akageuka huku na kule,
na kuona kabati lenye gas mask, akalivunja na
kuchukua, akaivaa haraka kisha akakimbilia kule
aliko Chiba akiwa na mask nyingine iliyojazwa
hewa ya oksijeni na kumvika Chiba.
“Msaada!” alipiga kelele ndipo vijana wa jeshi
walipoona jambo lile, nao haraka wakawahi
mask na kwenda kufungaa mfuniko wa tanki lile
kwa tabu sana kwani mkandamizo wa gesi
ulikuwa ni mkubwa hivyo mvujo wake nao
ulikuwa wa nguvu sana. Bkutokana na ujasiri na
ukakamavu wa vijana hao walifanikiwa kuufunga
na kupunguza athari ya gesi hiyo.
Hali ya Chiba ilikuwa mbaya, Gina akamkokota
na kutoka nae katika eneo leneye hewa, kwa
bahati nzurti katika banda hilo kulikuwa na gari
ya wagonjwa iliyowekwa kwa ajili ya maonesho,
kmpakia Chiaba nay eye akaketi katika usukani,
na kuitoa gari hiyo kwa kasi eneo lile huku akiwa
amewasha ving’ora vyote. Akainua simu na
kumpigia dokta Jasmine. Dr Jasmine
akamwelekeza moja kwa moja ampeleke
hospitali ya taifa Muhimbili, Gina alitoka katika
geti la uwanja huo kwa kasi na kuingia barabara
ya Kilwa kurudi mjini.
Kamanda Amata alipishana na ile gari ya
wagonjwa lakini hakujua kuna nini ijapokuwa
dereva wa gari ile aliweza kumfananisha.
Alikimbia haraka mpaka kwenye banda husika na
kukuta vijana wa jeshi wakihaha huku na huku
kujarib u kudhibiti hali iliyokuwepo hapo.
Kamanda Amata alipofika alizuiwa kupita eneo
hilo lakini kwa kitambulisho chake alairuhusiwa
huku akipewa mask na kuivaa, akaingia ndani ya
banda hilo na kukuta baadhi ya wanajeshi
wakijaribu kutoa huduma ya kwanza kwa
wafanyakazi ambao walikuwamo ndani ya banda
hilo lakini gesi ile iliwaathiri. Kamanda Amata
akaiwahi kompyuta ya Chiba iliyokuwa juu ya
meza Fulani, ilikuwa inaendeleaa na kazi ambayo
Chiba alikuwa anaifanya. Akatazama kwenye
kioo cha kompyuta hiyo, akaelewa kilichokuwa
kinafanyika mara ya mwisho. Chiba kabla
hajaenda kutafuta sehemu ya mlipuko alikuwa
akijaribu kutafuta uelekeo wa wapi mawimbi yale
ya kielektroniki yalikuwa yakitokea, mpaka yeye
anaiacha kompyuta hiyo bado ilikuwa ikiendelea,
Kamanda Amata akasoma nyuzi (degrees)
zilizojiandika, akaelewa, kilikuwa kipimo cha
ardhi katika longitude na latitude, na eneo husika
lililolengwa kadiri ya nyuzi hizo aligundua ni
maeneo ya Kigamboni, akaendelea kuperuzi na
kwa chini kidogo, akasoma kwa makini sana
namba zile zilizokuwa zikibadsilishana hapa na
pale ili kupata uelekeo sahihi.
“Kigamboni Kaskazini,” akajisemea na kisha
akiinua ile kompyuta na kutoka nayo mpaka nje,
akatzama huku na kule na kuiona gari ya chiba
akaiendea, akaingi na kujifungi ndani yake, kama
anavyofanya Chiba, akaunganisha ile kompyuta
na kijimtambo maalum kilichofungwa ndani ya
gari hiyo, sasa akaweza kusoma eneo halisi kwa
kutumia screen ndogo iliyopo ndani ya gari hiyo,
akaiwasha na kutoka katika uwanja huo,
akachukua simu ya upepo iliyo ndani ya gari
hiyo na kubofya kitufe Fulani.
“Madam S, Madam S,” akaita kwa mtindo huo.
“Nakupata Chiba,” madam S akajibu.
“Hapana sio Chiba, hapa ni Kamanda Amata,”
akamrekebisha.
“Nimekusoma nipe ripoti,” akaendelea Madam.
“Natoka uwanja wa maonesho wa sabasaba, hali
sio mbaya sana lakini Chiba inaonekana ana hali
mbaya ameondolewa na Gina kuelekea
hospitalini, la pili inaonekana kuna jambo
maeneo ya Kigamboni kadiri ya tafutishi
nilizozikuta katika kioo cha Chiba, niko mbioni
kuelekea huko, haraka iwezekanavyo.” Kamanda
akabofya kitufe kingine katika redio hiyo.
“Umesomeka Kamanda, mama anabadili uelekeo,
tukutane Kigamboni,” madam S akamaliza na
kukata ile simu.
§§§§§
Simanzi na majonzi viliwajaa Shakrum, Shailan
na wengine waliokuwa ndani ya boti, ukimya
ulitawala wakati injini ya boti hiyo ikiwa
inaunguruma kwani muda ulikuwa tayari
umewadia wa kung’oa nanga. Kutoka mbali
Shailani aliona kitu kama boti ndogo inayokuja
kwa kasi, akachukua darubini na kutazama
hakuamini macho yake kwa kile anachokiona,
Tashrini na wengine wawili walikuwa katika boti
hiyo wakija kwa ajili ya safari. Ingawa wao
walisalimika lakini maumivu makaubwa yalibaki
kwa ndugu yao Jegan Grashan. Dakika tatu tu
ile boti ilifika ukingoni kabisa mwa ile boti kubwa
ya akini Shakrum, wakashuka na kuhamia katika
boti hiyo kisha milango ikafungwa tayari kwa
kuondoka.
“Maafa yaliyotokea ni makubwa sana,” Tajan
alimweleza Shailan.
“Nini?” aliuliza Shakrum.
“Akiba yote ya mafuta kamanda Amata kalipua
yadi zote mbili hivi tunavyoongea zinateketea
kwa moto. Scolleti amekwishauawa na Yule
mwanamke wa Kihindi, Jegan nae kapigwa risasi
na mtu asiyejulikana,” Tajan alitoa ripoti.
Shakrum alikuwa amesimama akimsikiliza, mara
hiyo akajiegemeza katika moja ya nguzo zilizo
katikati ya boti hiyo akiwatazama wenzake hao.
“Na mlipuko wetu umetenguliwa kule sabasaba,
wametuweza, kiukweli sikufikiri kama hawa
jamaa watakubali Jegan aondoke hivihivi,”
Shakrum alieleza.
“Jamani, hapa tumeshacheza pata potea, washa
mashine tuondoke, si ajabu na sisi
wakatukamata hapahapa au wakatushushia
kombola moja tu tukapotea wote,” Shaiilan
aliwaeleza wenzake, injini ikawashwa, milango
ikafungwa, kiyoyozi kikaanza kuyoyoza, taratibu
chombo kikaanza kuondoka eneo hilo
kikichanganya polepole na kugeuka kuelekea
upande mwingine, kila mmoja ndani ya chombo
hicho alikuwa tayari ameketi mahala pake
aliyekuwa anafungua kinywaji sawa, aliyesoma
gazeti sawa, tayari walikuwa wamekwishaamua
kuondoka.
§§§§§

OFISI ZA UBALOZI WA KHAZAKISTAN

Gari za ubalozi ziliingia katika kiwanja cha ofisi
hizo, maofisa wa usalama wakashuka na
kuiendea gari iliyokuwa haina kioo, ndani yake
alikuwamoi Jegan Grashan.
“Nilijua hawawezi kukuacha hivihivi,” alisema
mmoja wa maofisa hao alipokuwa anamvua
bullet proof Jegan.
“Dah! Mungu mkubwa, nashukuru mlijiandaa
Yule jamaa alikuwa ananimaliza kabisa,” Jegan
alijibu huku akimkabizi Yule mwanausalama lile
koti. Jegan Grashan akateremka garini na
kukanyaga ardhi ya uraiani, kwa hatua za
polepole huku akiwa ameshikwa mkono na
mmoja wa wanausalama ambaye mkononi
mwake alikuwa amekamata short gun
alisindikizwa kuingia ndani ya jengo hilo.
“Ni saa nne sasa karibu na dakika arobaini na
tano, boti itakuwa inang’oa nanga, kwa vyovyote
vile wao wanajua wewe umekwishakufa,” ofisa
mwingine wa ubalozi alimweleza Jegan.
“Haina shaka, naweza ungana nao sasa na
kuondoka, asanteni sana,” Jegan aliwashukuru
na kuwakumbatia mmoja mmoja, kisha
akakiendea chombo cha mawasiliano na
kuwasiliana na ndugu zake hao walioko ndani ya
boti.
Jegan aliingizwa kwenye chombo maalum na
kufungiwa ndani yake kisha ikabonyezwa swichi
Fulani na chombo kile kikawasha injini zake
ndani ya chumba maalumu kilichojazwa maji
ambacho moja kwa moja kinatokea kwenye
mkondo wa bahari. Dakika moja baadaye kile
chombo kikasukumwa kwa nguvu na kutoka
ndani ya jengo kwa kupitia kidirisha Fulani,
kikapaa na kujibwaga baharini kisha kwa
mwendo wa kasi kikapotelea baharini.
Ndani ya boti saa 4:45 asubuhi
Furaha na shangwe ziliijaza boti hiyo baada ya
kusikia sauti ya mpendwa wao Jegan
ikawahakikishia kuwa yuko hai, hajafa. Furaha
ilikuwa mara mbili ya ile ya kwanza pale
walipokipokea chombo maalumu kilichomhifadhi
Jegan, na walipofungua ndani walimtoa ndugu
yao huyo na sherehe ikawa sherehe, shampein,
risasi za hewani vyote vililindima katika boti
hiyo, nyimbo zikaimbwa na kuchezwa, kati yao
wote hakuna aliyepotea, wote walikutana tena
kama ndoto yao ilivyokuwa.
“Nimeachiwa huru, asanteni sana kwa juhudi
zenu za kuishinikiza serikali ya Tanzania,
mmefanya lililo jema hata sasa niko nanyi.
Lakini huu sio mwisho wa mapambano, huu ni
mwanzo, lazima tuikomboe nchi takatifu kutoka
katika mikono ya watu wa Maghalibi na vibaraka
vyao. Nisingeelewa kanchi kama haka ka Afrika
mashariki kajifanye kana sauti ya kupambana na
sisi, dunia yenyewe inapiga magoti mbele yetu,
wao ni nani? Hawakujiuliza kuwa kwa nini
Amerika na washirika wake kama Uingereza,
Ufaransa na wengineo wako kimya? Wote hao
wanajua kuwa freedom fighters tunajua
tunachokifanya wanajua hilo ndo maana walibaki
kimya,” Jegan Grashan alitoa hotuba ya nyodo
katika boti na kufuatiwa na nderemo za wafuasi
wake. Hakukuwa na linguine zaidi ya kuondoka,
safari ikaanza taratibu, boti ile ilikuwa ikiambaa
na maji ya bahari ya Indi ikichana mawimbi
kuelekea Mombasa ambako wenzi wao walikuwa
wakiwasubiri.
§§§§§
Kamanda Amata alijirusha majini na kupiga
mbizi, akipita chini kwa chini kuielekea ile boti
ambayo ilionekana kwa mitambo maalumu ya
kijeshi pale kigamboni. Msoma rada alieleza wazi
kuwa walikuwa wakiichunguza boti hiyo karibu
masaa kumi tangu imefika eneo hilo, hawakuitilia
nashaka kwa kuwa ilikuwa ikipepeza bendera ya
ya Tanzania. Siku hii ndipo walipogundua kuwa
haikuwa boti ya kawaida bali imeingia hapo kwa
shughuli maalumu.
Madam S alimtazama Amata akipotelea majini,
nay eye alirudi upande mwingine ambako
kulikuwa na wanajeshi wanamaji waliojiandaa
tayari kwa lolote lile. Kamanda Amata alipewa
maagizo ya kuhakikisha kuwa waliopo
wanakamatika wakiwa hai na uhai wao. Aliifikia
ile boti kwa muda mfupi tu, bahati nzuri
alipoifikia na chombo kilichombeba Jegan
Grashan kilikuwa kikiwasili, aliona pale
kilipoingilia ma yeye akajipenyeza hapohapo.
Wakiwa ndani ya boti wanashangilia ushindi huo,
ndipo Kamanda Amata alipomshuhudia Jegan
Grashan ambaye alijua wazi kuwa amemuua kule
Tazara akiwa hai mbele ya macho ya wengine.
Jambo hili lilimtia hasira na uchungu, akabadili
mpango wake haraka na kujitokeza mzima
mzima. Wakati wao wanapiga shampeini na
risasi za hewani kushangilia ushindi, Kamanda
Amata alikuwa kazimama mbela yao kama
mzuka.
“Jegan Grashan, nani aliyekwambia kuwa
utaondoka ndani ya nchi hii ukiwa na pumzi
yako? Kama ulijuwa kuwa umepona sasa ndio
mwisho wa maisha yako, nafikiri hukutaka kufa
peke yako ulikuwa na akili sana na sasa mtakufa
wote pamoja kwa mkono wangu huu, wasalimie
kuzimu, mwanaharamu, mwanadamu ambaye
hukustahili hata kuzaliwa,” Kamanda Amata
alishikwa na hasira kali, akisema maneno hayo
hakuna aliyeamini kama mbele yao yupo kiumbe
huyo anayeogopwa kila kona ya sayari yetu,
kabla hawajajiweka sawa wakiwa bado kwenye
butwaa, kichwa cha Jegan Grashan kilifumuliwa
kwa risasi mbili kutoka katika bastola ya Amata,
mara hii alihakikisha anakufa.
Kamanda Amata alijirusha upande wa pili na
risasi yab tatu ikamfumua Yule aliyeshika
shotgun aliyekuwa akimlenga Kamnda, hola!
Alifanikiwa kupiga viti na vyupa vya pombe
wakati Kamanda akijiviringa kuelekea upande
mwingine. Ilikuwa ni hali ya taharuki kwa
freedom fighters.
“Muueni shetani mweusi!” Shakrum alipiga kelele
huku akitafuta pa kujificha. Tayari watu watatu
walikuwa chini bila uhai.
“Jegannnnnn!!!!!!” Ilikuwa sauti ya Shailan
aliyekuwa akilia kwa uchungu aliposhuhudia
mwana mapinduzi wao akifumuka kichwa.
Dakika moja baadae wote walikuwa chali
sakafuni, Shakrum alibaki hai kwa kuwa aliwahi
kujificha. Kamanda Amata akatazamana na
Shailan.
Jicho la hasira la Kamanda Amata lilikuwa
likimwangalia Shailan aliyekuwa amemshika
Jegan mfu akilia kwa uchungu.
“Kama kuna aliyewaambia kuwa mtaondoka nchi
hii mkiwa hai amewadanganya kabisa,
hamkustahili kuishi wala kuzaliwa,” Kamanda
Amata aliongea hayo na kufyatua risasi moja
iliyopiga kifua cha Shailan na kumtupa nyuma.
Alipotaka kufyatua risasi ya pili akajikuta
ameishiwa risasi. Mara akajikuta akidakwa kwa
nyuma, kabla hajakaa sawa, alikabwa shingo.
Amata akafikiri la kufanya kwa haraka, akainama
na kumyanyua huyo mtu na kumbwaga mbele,
Shakrum. Hasira za Amata zikawaka maradufu,
Shakrum akanyanyuka na kumkabili Kamanda
Amata.
“Nilikuwa nakutamani sana wewe kiumbe! Na
sasa umeingia mkononi mwangu, sitakupa hata
nukta ya kuomba sala ya mwisho,” Shakrum
alimwambia Kamanda Amata, alipomaliza
sentensi yake alimvamia Kamanda kwa jinsi ya
ajabu, akampiga ngwara moja maridadi,
Kamanda alijirusha hewani akaichanua miguu
yake na kuipata shingo ya Shakrum, alimpiga
teke kwa mguu wake wa kulia nyuma ya shingo,
Shakrum aliyumba na kujipigiza ukutani. Akaruka
sarakasi na kusimama wima, akaweka mikono
katika mtindo wa kuvutia wa mapigo ya karate,
Kamnda Amata naye akajipanga kivingine.
Shakrum alitoa mapigo ya kasi mfululizo
kumuelekea Kamnda Amata lakini hakuna hata
pigo moja lililomfikia Amata, mapigo yote
yalipanguliwa kiufundi sana, mwisho wa yote
Kamanda Amata akajirusha sarakasi na kumpa
Shakrum nafasi ya mita kama tano kutoka
kwake. Kwa sekunde chache alizozipata Amata
alijipanga na kupeleka mapigo ya kazi ambayo
yote yalimuioshia Shakrum na kumtupa chini
akiwa hoi.
“Mi nilifikiri unajua kupigana kumbe ni
mwanafunzi namna hiyo!” Amata alimwambia
shakrum aliyekuwa akitambaa chini huku yeye
akimfuata kwa nyuma.
“Ulipigania Jegan kuachiwa huru, sasa wewe
utakaa jela badala yake,” Amata alimwambia
Shakrum na kumkamata ukosi wa fulana yake na
kumvuta kwa nguvu mpaka kijana huyo
akakohoa, akamuinua kwa nguvu na kumbamiza
ukutani. Shakrum hakuwa na la kufanya,
Kamanda Amata akatoa pingu tayari kumfunga
Shakrum lakini lo, bomu aina ya grunet
lililoondolewa pini ya usalama likaanguka kutoka
mkononi mwa Shakrum na kutua chini
liokadunda mara ya kwanza na likaelekea
kugoinga sakafu mara ya pili.
Shakrum alimshika kamanda kwa nguvu zake
zote.
“Hatoki mtu hapa, kama wewe umeua ndugu
zangu, lazima nawe ufe na sisi,” Shakrum
alimwambia Amata.
“Kamwe haiwezekani!” Kamanda Amata akajibu
na kumpiga kichwa cha nguvu kilichomfanya
Shakruma amwachie. Kamanda Amata
hakupoteza sekunde, alikimbia kwa kasi yake
yote, hakukuwa na mlango ila dirisha kubwa la
kioo mbele yake, alichumpa na kutanguliza
kichwa akakipiga kioo nay eye mwenyewe kutoka
nje kupitia hapo. Nyuma yake ulitokea mlipuko
mkubwa, ile boti yote ikateketea kwa moto.
§§§§§
Madam S alijishika kichwa baada ya
kuushuhudia mlipuko ule kupitian chomb o
maalumu katka kambi ya jeshi la wanamaji
Kigamboni.
“Oooh! My son! ( Oooh Kijana wangu! )” alipiga
kelele.
Moyo ulimwenda mbio hakujua afanye nini.
Akikumbuka Chiba kaumizwa na gesi, sasa
Kamanda ndani ya mlipuko, Madam S alijikuta
anabaki peke yake, machozi ya uzee
yalimdondoka huku mikono yake ikifunika kinywa
chake kwa uchungu.
Chumba kizima walichokuwa maofisa wa Jeshi
pamoja na Madam S wakishuhudia tukio lile
kilikuwa kimya, hakuna hata aliyekohoa. Madam
S alihisi akishikwa bega. Akageuka na
kumtazama aliyemshika, alikuwa waziri wa ulinzi
aliyefika muda huo katika kambi hiyo ya
wanamaji.
“Pole Madam, lakini vijana wetu wamekufa
kishujaa!” alimwambia Madam S.
“Nani aliyekwambia vijana wangu wamekufa?”
madam S alijikuta akipiga kelele kupingana na
kauli hiyo. Mara kelele zikaibuka katika chumba
kile, Madam alipogeuka alimuona Kamanda
Amata akiogelea majini baada ya kuibuka.
“Mpe msaada haraka!” ilikuwa ni sauti ya waziri
wa ulinzi, na mara hiyo hiyo boti iendayo kazi
ikaanza safari yake na kumfuata Kamanda
Amata.
Madam S alijikuta akifurahi kwa tukio hilo,
hakuamini kabisa anachokiona mbela yake.
“Mungu mkubwa!” alishukuru.
 
10
MADAM S aliinua simu yake baada ya kushusha
pumzi ndefu, katika sakata hilo ni yeye tu
aliyekuwa upande wa peke yake tangu mwanzoni
baada ya kusikiliza kile ambacho Kamanda
Amata alimwambia tangu mwanzo kuwa
hakubaliani na kuachiwa huru Jegan. Ijapokuwa
Madam S aliwasikiliza wajumbe wengine katika
jopo lile la baraza la usalama la taifa chini ya
waziri wa ulinzi, aligeuka baadae kwa kuungana
na kijana wake, TSA 1 lakini swala moja
walikuwa wakitofautiana. Kamanda Amata aliapa
wazi kuwa laiti Jegan akiachiwa huru yeye
atamrudisha kwa risasi, uamuzi huu ungekuwa
kinyume na maadili ya kazi kama kungetolewa
hati ya jambo hilo. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa,
Kamanda Amata alimpiga risasi Jegan Grashan
katika msafara wa gari za ubalozi. Ijapokuwa
Jegan alikuwa amevikwa nguo zisizoingia risasi
na kusalimika katika tukio hilo. Aligadhibika sana
alipomuona Jegan akiwa hai ndani ya boti ile,
akipongezana na wenzake na kutoa maneno ya
kashfa, Kamanda Amata hakushindwa kutumia
bastola ile ile iliyofanya kazi katika tukio la
kwanza, na sasa alifumua kichwa kabisa maana
labda angekuwa na nguo nyingine isiyopitisha
risasi. Alijua alilolifanya.
‘Liwalo na liwe!’ alijisemea moyoni huku
akiitazama boti ile iliyokuwa ikiteketea kwa
moto, hakuna hata mtu aliyetoka, hakikusalia
hata chuma juu ya chuma kingine. Kazi ilikuwa
imekwisha namna hiyo. Akajigeuza na kuendelea
kuogelea kuelekea pwani ambako palikuwa na
umbali kidogo lakini alipoanza kuogelea tu,
aliona helkopta kubwa ya jeshi ikija eneo lile,
akaipungia mkono na chombo kile kikasogea
hadi pale alipo na kumteremshia kamba
iliyofuingwa kwa mafundo mafundo, akaikamata
na dude lile likaondoka nae kutoka pale kwenda
nae nchi kavu.
KIGAMBONI – KAMBI YA JESHI LA WANAMAJI

saa 7:14 mchana
MADAM S alisimama kwenye uwanja wa
kushukia helkopta, pembeni yake kulikuwa na
waziri wa ulinzi, walikuwa wakimwangalia
Kamanda Amata alipokuwa akija upande wao
akiwa chapachapa, ametota maji.
Madam S alimkumbatia Kamanda Amata kwa
nguvu zote bila kujali kama kalowa maji,
alimbusu mashavuni.
“Kazi nzuri kijana wangu, nimefurahi sana kwa
ulilofanya, nina uhakika hakuna aliyetoka mle
ndani,” Madam S alimwambia Amata.
“Hakuna anyeweza kutoka kwenye mikono ya
Kamanda aamuapo jambo, si Jegan, si Shailan
wala Shakrum, wote leo nyama zao zinaliwa na
watoto wa samaki, lazima ulimwengu ujue kuwa
kuna wana usalama makini katika kazi, Mungu
ibariki Tanzania, nahitaji kumuona kaka yangu
Chiba,” Kamanda alimwambia Madam S,
akamtazama waziri wa ulinzi kisha akapita b ila
kumsalimia na kuingia kwenye gari ya usalama,
akaketi katika siti ya nyuma na Madam akaingia
siti ya mbele nyuma ya usukani wakaiacha
kambi hiyo na kuelekea mjini.

MUHIMBILI

saa 7:54
CHIBA alitolewa kwenye chumba cha daktari na
kupelekwa sehemu maalumu ambayo ni yeye
peke yake alikuwa amehifadhiwa humo, chumba
maalum chenye mitambo tiba ya kila aina
ambayo ina uwezo wa kukushikia roho yako
wakati wewe ukifanya mambo mengine. Alilazwa
kitandani na kuwekewa hewa ya oksijeni ili
imsaidie kupumua huku mitambo mbalimbali
ikishirikiana kuonesha mwenendo mzima wa
maisha ya mtaalamu huyo. Ijapokuwa ni yeye
alikuwa mtaalamu wa kompyuta lakini mara hii
kompyuta zilikuwa zikimuongoza yeye. Hakuweza
kufungua macho ndani ya ubongo wake alikuwa
akipitiwa na mapito mengi mabaya nay a
kutisha, aliota Kamanda Amata anakufa kifo cha
moto, na mara akaota Kamanda Amata
anafukuzwa kazi. Ndoto mbaya zaidi ilikuja
baada ya muda mfupi, alipoota wapelelezi wawili
maarufu sana wa Tanzania wakiuawa vibaya
katika sehemu moja ya Afrika wakiwa
wanataimiza majukumu yao ya kiserikali. Mara
vile vyombo vikaanza kupiga kelele na kuonesha
kuwa mapigo yake ya moyo yanashuka kwa
kasi. Muuguzi aliyekuwa hapo akamwita dakatari
haraka. Dr Jasmin, alikuwa akitokwa na jasho akijaribu kuokoa maisha ya Chiba, Chiba alikuwa akipigania maisha yake ya mwisho, ulikuwa mpambano mkali na shetani. Katia maono yake
alikuwa akipambana na joka kubwa lenye vichwa
saba, haukuwa mpambano wa kitoto, lakini
Chiba alijitahidi kutumia nguvu na ujuzi wake
wote ili kulishinda joka hilo, lakini haikuwa hivyo.
Joka lilimdhibiti Chiba likamkaba mwilia wake na
kumnyonga.
Mitambo tiba iliyokuwa ikipima mwenendo wa
moyo wa Chiba ilionesha mstari ulionyooka
kuashiria kuwa Chiba hana uhai tena. Dr
Jasmine alishindwa kuvumilia hali hiyo alijikuta
akilia kama mtoto. Nukta hiyohiyo Madam S na
Kamanda Amata waliingia ndani ya wodi hiyo
wakiwa haihai walipofika pale walikuta vurugu
ya madaktari wakisaidiana na wauguzi, wakati
huo Gina alikuwa hana hali kwa kilioo cha
vikwifuvikwifu.
“Nini Gina?” Kamanda aliuliza.
“Man down Kamanda,” Gina alimwambia huku
akilia. Kamanda Amata alielewa haraka maana
ya neno hilo likimaanisha Chiba amekufa,
Kamanda Amata hakusubiri linguine, haraka
alikimbilia walipo madaktari ambapo tayari
Madam S alikuwa amekumbatiana na Dr
Jasmine wakilia kwa uchungu.
“Noooooooooo!!!!!!!” kamnda Amata alipiga kelele
na kuwatawanya madaktari waliokuwa pale,
wengine wakaanguka na wengine wakayumba na
kusimama wima. Kamanda Amata alimtazama
Chiba ambaye alikuwa ametulia kimya macho
yake yakiwa meupe, mboni zake hazikuonekana,
“No my brother, don’t leave me!!!!!!” (Hapana
ndugu yangu, usiniache peke yangu,) Kamanda
Amata kama kawaida yake huwa hakubali
kushindwa jambo, wakati madaktari wakimshika
amuache Chiba hakukubaliana nao, alitazama
huku na huku, akaona waya wa umeme wa
6.0mm uliokuwa ukipitisha umeme kuelekea
kwenye mitambo ya oksijen, Kamanda kutoka
aliposimama alikanyaga kimeza cha dawa za
mgonnjwa na kuukamata ule waya akaning’inia
nao mpaka ule waya ukachomoka katika joint
box, akashika jirani na miisho yake ambayo
ilikuwa ni nyaya mbili, nyekundu na nyeusi, bila
huruma wala kuchelewa akampiga shoti Chiba
akiwa kitandani, akarudia mara ya pili. Jambo
lisiloaminika likajitokeza, mashine iliyokuwa
ikipima mapigo ya moyo ikaanza kusoma
mapigo ya juu sana na baada ya sekunde kumi
ikatulia na kuonesha mapigo yaliyo sawa. Chiba
akafumbua macho, akamtazama Kamanda,
Madam S, Madaktari na wauguzi waliopo katika
wodi ile. Chiba akaondoa mwenyewe kwa
mikono yake ile barakoa ya oksijeni, akainuka na
kuketi kitandani.
“Kamanda Amata, umepona?” akauliza Chiba.
“Nimepona kaka,” Kamanda akajibu.
“Jegan najua amekufa na wenzake je?” Chiba
akauliza tena.
“Wote wamekufa, hakuna aliyesalia,” Kamanda
akajibu, Chiba akampa ishara Kamanda Amata
ya kuwa asogee jirani, akamkumbatia kwa
nguvu. Kamanda akautupa ule waya chini, na
wakati huo fundi umeme alikuwa keshafika
baada ya kuitwa haraka.
“Asante Kamanda Amata,” Chiba akashukuru.
“Asante na wewe kwa kuokoa maisha ya
Watanzania wengi,” Kamanda akamshukuru
Chiba. Wale madaktari wakamchomoa vifaa
vyote vilivyokuwa mwilini mwake. Chiba akatoka
kitandani na kuongozana na Madam S, Kamanda
Amata, Gina na Dr Jasmine wakatoka na kuingia
kwenye gari kisha wakaliacha eneo la Muhimbili
na kutokomea zao.
§§§§§
 
BAADA YA SIKU MBILI-OFISI NYETI

KAMANDA Amata akiwa amesimama mbele ya
meza kubwa, safi ambayo unaweza kujiona
mwenyewe, alikuwa akitazamana na Madam S
ambaye naye alikuwa amesimama wima, wote
wakiwa katika vazi la kufanana, suti nyeusi, shati
jeupe na tai ndefu nyeusi kasoro Madam S.
Chiba alikuwa pembeni na watui wengine wawili
akiwamo Dr Jasmine.
“Tukisimama hivi unaelkewa kabisa kuwa
tunahitaji nkuongea kiofisi zaidi,” Madam S
alimwambia Kamanda Amata ambaye alikuwa
kimya bila kujibu lolote, akatoa kitambaa chake
cheupe na kufuta machozi yaliyokuwa
yanayajaza macho yake angavu, kisha
akaendelea, “Baada ya kikao cha jopo lilelile
lililokuwa likikaa tangu mwanzo wa sakata hili
mpaka jana limekaa tena. Na agenda kubwa
ilikuwa ni juu yako Kamanda wangu, kwanza
unapongezwa sana kwa kazi nzuri uliyoifanya
kwa kushirikiana na wenzako wote,
mmeudhihirishia ulimwengu kuwa usalama wan
chi hii upo mikononi mwetu wenyewe, lakini
pamoja na pongezi hizo Kamanda, kuna habari
mbaya nay a kusikitisha juu yako na juu ya ofisi
yetu pia,” akakohoa kidogo na kuendelea tena,
“Siku zote kwenye kitambaa cheupe
kinachoonekana ni doa jeusi tu, watu
hawaangalii wema ila mabaya yako na
kukupatiliza kwayo, ndani ya kazi yako nzuri
ambayo sisi kama wanausalama tumeiweka
kwene kablasha linalojulikana kama JULAI 7,
Kamanda umeonekana kufanya kazi kijeuri bila
utii kwa maamuzi yako mwenyewe na kupinga
maagizo ya jopo la usalama na kwa sababu hiyo
baraza la usalama limekupa barua ya
kusimamisha kazi katika kitengo cha ujasusi cha
TSA, utakivua cheo chako cha TSA1 na
kukabidhiwa mtu mwingine kuanzia nimalizapo
kusema haya, haijatolewa kama ombi bali ni amri
na itekelezwe mara moja, imesainiwa na waziri
wa Ulinzi kwa niaba ya baraza zima la usalama
wa taifa.” Madam S alimaliza na kufuta machozi.
Kamanda Amata alitulia kama dakika moja,
kimya kilitawala, hakuna aliyeongea isipokuwa
kufuta machozi na makamasi yaliyokuwa
yakiwatoka waliopo kwa uchungu. Aliyekuwa
ngangari ni katibu wa wizara ya ulinzi tu,
akasogea na bahasha ya khaki, akatoa karatasi
tatu nyeupe zilizochapwa kwa mashine ya
kisasa, upande mmoja ilisainiwa na waziri wa
ulinzi na upande wa pili zilibaki saini mbili moja
ya Kamanda na nyingine ya Madam S kama
mkuu wa kitengi maalumu, kitengo cha kijasusi
kisicho na mipaka. Akaipokea ile barua na
kusaini kisha akampa Madam S nae akazisaini
kisha, wakagawana moja kwa ofisi ya baraza la
usalama wa Taifa, nyingine kwa ofisi ya TSS nay
a mwisho akapewa Kamanda Amata, naye
akamkabidhi Gina.
Baada ya hapo, Kamanda Amata akavua beji
maalumu ya usalama wa taifa na kumkabidhi
Madam S, beji ya dhahabu, kimkoba kidogo cha
bastola ambacho ndani yake kilikuwa na vifaa
kadhaa vya kijasusi ambavyo alikabidhiwa pindi
alipopewa kazi hiyo maalumu. Mwisho akapeana
mikono na wote waliopo ndani ya ofisi hiyo
nyeti.
Ilikuwa ngumu kuzuia machozi ya kila mmoja
lakini hali halisi ilikuwa hiyo.
“Nakuhitaji nyumbani Kamanda ndani ya masaa
matatu, wewe na wenzi wako kwa chakula,”
Madam S alimpa ujumbe Amata.

NYUMBANI KWA MADAM S

“Sikuweza kukutetea tana Kamanda, ijapokuwa
wapo nwaliojaribu lakini wengine walikazia
ufukuzwe kazi” Madam S alimwambia Kamanda
Amata walipokuwa wameketi katika bustani
kubwa ya nyumba hiyo, Gina, Chiba na Dr
Jasmine walikuwa ndani wakiendele kupata
vinywaji.
“Usijali Madam, yote maisha, mimi nimetoka TSS
atakuja mwingine naye kutimiza wajibu wake,”
Kamanda alimwambia Madam S.
“Najua, lakini kwa sasa kumpata mtu shupavu,
mwelevu, mwepesi, mwenye mbinu na ujuzi wa
mipango ya kumsaka adui au kummaliza, mbabe
kama wewe itachukua miaka mingi sana, usijali
Kamanda naamini kuwa muda mfupi tu mataifa
makubwa yatakuchukua, mi nakutakia maisha
mema sana Kamanda, kwa lolote tuwasiliane
mimi ni mama yako na wewe ni mwanangu,”
Madam S akamaliza, wakakumbatiana kwa
nguvu kila mmoja akimwaga machozi ya
uchungu kisha wakaachana na kurudi ndani.
§§§§§
Gina na Kamanda Amata waliondoka kwa
Madam S na kupitia vijiwe kadhaa kabla
hawajafika nyumbani.
“Nikupeleke kwako au?” Kamanda akauliza.
“Sitaki, leo nataka kulala kwako,” Gina
akamwambia Kamanda Amata kisha
wakaendelea na safari mpaka nyumbani kwa
Kamanda Amata. Walikuwa wamelewa, Gina
alifika na kuingia chumbani akifuatiwa na
Kamanda.
“Kamanda Amata, uliyekuwa TSA1 wenye roho
mbaya wamekufukuza kazi, usijali mimi leo
nataka nikupe kazi njione kama kweli we
mwanaume,” Gina aliongea kwa sauti ya
kilevilevi.
“Gina ulale sasa,” Kamanda alisititiza na kutoka
kwenda sebuleni. Gina akachukua nafasi hiyo
kwenda maliwato, akaoga na kurudi kisha
akaingia ndani ya kitanda kikubwa na kujifunika
kwa shuka safi yenye maua ya kuvutia, akazima
taa kali na kuwasha ile ya buluu.
Dakika chache baadae Amata aliingia chumbani,
naye vivyo hivyo, akaenda kuoga na kurudi, Gina
kwa hila zake akajifunua shuka na kulitupa
pembeni akabaki kama alivyozaliwa.
“Njoo Kamanda, najua una mambo mengi leo,
njoo nikufariji,” Gina alimwambia Kamnda huku
akiwa anjipindapinda pale kitandani.
Kamanda Amata akamtazama mrembo huyu
ambaye siku zote walikuwa wakiheshimiana sana
lakini leo hii heshima ilikuwa inataka kubadili
uelekeo.
Gina alikuwa akimtazama Kamanda, Kamanda
alikuwa akimtazama Gina aliyekuwa kajilaza pale
kitandani, mwanga wa taa buluu ulifanya umbo
la Gina lionekane kama madini ya Tanzanite,
lilimvtia Kamanda, akapatwa na wakati mgumu,
kabla hajaamua la kufanya. Gina aliinuka na
kumtoa taulo Kamanda kisha akaizungusha
mikono yake na kuiokutanisha nyuma ya shingo
ya Kamanda Amata.
“Nakupenda sana Kamanda Amata”.
æ MWISHO æ
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom