kidi kudi
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 2,630
- 2,298
JULAI 7
story by richard MWAMBE
Dunia inakumbwa na wimbi la ugaidi,
matukio ya kutisha yanayopoteza maisha
ya walio wengi katika pande mbalimbali
za dunia ikiwemo Afrika hususan
Tanzania. Nchi zinazoendelea
zinajumuishwa kuwa na mahusiano na
mataifa beberu ya Maghalibi.
Idara za usalama za Tanzania
znafanikiwa kumtia mkononi Jegan
Grashan akihusishishwa na mlipuko wa
ubalozi wa USA, Dar es salaam. Swahiba
zake wanaishinikiza serikali imuache huru
kwa kutekeleza milipuko kadhaa, wanaipa
siku saba iwe imekamilisha hilo. Je
litawezekana?
Tiririka na mkasa huu mwingine
unaomhusisha Kamanda Amata.
1
MVUA KUBWA ilikuwa ikinyesha katika jiji la Dar
es salaam, jiji linalosifika kwa joto kali
linalowafanya watu wake kujutia kila siku kwa
nini wanaishi hapo, lakini bado kuhama
hawataki. Radi za hapa na pale ziliendelea
kumulikan ardhi yote ya eneo la Tazara katika
makutano ya barabara zenye majina ya viongozi
wakubwa Africa, barabara ya Nyerere na ile ya
Mandela, umeme ulikuwa umekatika na giza
lilitawala kila mahali jioni hiyo, haikuwa usiku
sana kwani ndiyo kwanza kipindi cha majira
kutoka RTD kilikuwa kikianza, hakuna aliyeweza
kuvuka katika makutano hayo, magari yalijaa kila
upande mpaka kule kwenye service road, kelele
za honi zilitawala na matusi ya hapa na pale,
wengine wakijifanya ndiyo askari kuongoza
magari lakini bado hali ilikuwa tete, si wakwenda
Buguruni, wala Ukonga wote walitua pale, mvua
iliendelea kunyesha kwa fujo na ngurumo
zikitawala.
Katikati ya makutano yale kulikuwa na gari aina
ya Peugeot imesimama hali inaunguruma, dereva
wake alishuka na kupiga kelele za hapa na pale
akiwaomba wengine wampishe lakini hakuwapo
wa kumpisha, kwa hasira yule bwana aliubamiza
mlango wa gari na kujichanganya na vijana
waliojaa eneo lile, haikupita dakika mbili mlipuko
mkubwa ulitokea katika gari ile, anga lote
lilifunikwa na rangi nyekundu iliyochanganyika na
moshi mweusi, watu walitawanyika huku na kule
wengine wakitokea katika madirisha ya daladala,
ilimradi tu kujiokoa. Vilio vilisikika huku na kule
watu waliumia sana na wengine kupoteza
maisha, gari zaidi ya ishirini zilidaka moto eneo
lile.
Gari za zimamoto kutoka kampuni binafsi na lile
la jiji yalifika huku polisi wa kutuliza ghasia
wakiwa tayari kusaidia majeruhi kuwakimbiza
hospitali ya Dar Group, Temeke na wengine
Muhimbili moja kwa moja, kazi ilikuwa ngumu
kwa kila mtu aliyekuwa pale, wananchi wote
walisogezwa mbali na eneo la tukio ili kupisha
shughuli za uokoaji. Baada ya takribani dakika
arobaini na tano gari ya jeshi ilisimama karibu
kabisa na jengo la S.S Bakhresa, wakashuka na
vifaa vyao kuelekea pale palipotokea mlipuko
walilizungushia gari lile utepe maalum na
kukusanya kila kilichoonekana na uhusiano na
mlipuko ule kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Hali
iliendelea kuwa tete eneo lile kila mtu alilia
kivyake.
* * *
Ingia kaka, umemaliza kazi bwana mmoja
alisema huku akiufungua mlango wa Toyota
prado na kumruhusu huyo aliyemwita kaka
kuingia kwenye gari hiyo, kasha ikageuza na
kuchukua barabara ya Mandela kuelekea
Buguruni.
Bado, kazi ndiyo kwa nza inaanza yule bwana
aliwaeleza wenzake huku gari ile ikitokomea kwa
kasi maeneo ya Sukita kuielekea Ubungo.
Hii ni vita ya tatu ya dunia, na tunaiendelezea
hapa Tanzania, kwa kuwa ulinzi wan chi hii
hauko makini aliongea bwana mmoja
aliyeonekana kama ndiyo kiongozi wao.
* * *
Mlio mkali wa simu ulimshtua madam S
usingizini, alisonya na kuiinua simu ile huku
akiwa bado kitandani mapema namna hiyo.
Hey, nani? aliuliza kwa hasira.
Madam S, washa runinga yako TBC kasha
nitakupia baadaye kidogo sauti ya upande wa
pili ilitoa ombi, madam S bila kuchelewa
aliichukua rimoti na kuiamuru runinga ile kufanya
kazi. Alipigwa na butwaa na moyo ukaanza
kumuenda mbio, ukizingatia na umri nao ulikuwa
umekwenda, aliifutailia habari ile, na kwa mbali
macho yake yalianza kujaa machozi. Oh my
God alijisemea moyoni, Nini tena hii? alijiuliza
mwenyewe wakati akimfuatilia Grace Kingalame
akitoa maelezo ya moja kwa moja kutoka eneo
la tukio. Madam S alinyanyuka kitandani na
kuutafuta mlango wa bafu, baada ya kujiweka
sawa alivalia suruali yake nadhifu na fulana yake
nyeupe iliyoandikwa Naipenda Tanzania , na juu
yake alijitupi kijikoti cheusi, bastola yake
aliipachika sawia katika mkanda wa suruali
aliyovaa na kutoka moja kwa moja aliiendea gari
yake aina ya Toyota Spacio na kuondoka
akiiacha nyumba yake ikibaki na mlinzi tu. Njia
nzima madam S alikuwa akilaani kilichotokea
hapo Tazara, kama kawaida yake alitamani huyo
mtu amkamate mara moja ili amuoneshe
shughuli nene kwa kufanya jambo kama hilo.
Alifika eneo la tukio na kukuta shughuli
zikiendelea hasa zile za uchunguzi, pale
alikutana na wakuu wa polisi na vyombo vingine
vya usalama kila mmoja akiwa hana la kusema
juu ya tukio hilo, laana za kumlaani aliyetenda
hilo na vizazi vyake vyote ndizo zilikuwa
midomoni mwao.
Atakamatika tu Madam S alimwambia IGP
walipokuwa katika mazungumzo huku
wakiangalia shughuli ile ikikaribia kufika
ukingoni.
Madam S aliinua simu yake na kuitazama,
ilikuwa yapata saa tano usiku, aliwaaga wenzake
na kuondoka eneo lile mara moja huku akiwa na
mawazo lukuki kichwani mwake.
Siku iliyofuata
Miranda! sauti nzito iliita kutoka mlango wa
pili, ilikuwa ni sauti ya waziri wa ulinzi ambaye
ndiyo kwanza alikuwa akiingia ofisini kwake
asubuhi hiyo. Miranda alitii wito huo mara moja
alikiacha kiti chake na kuufuata mkango mkubwa
wa kioo uliokuwa kushoto kwake na kuufungua.
Nimefika mzee! aliitikia. Bwana Sixtus Maige,
waziri mwenye dhamana ya ulinzi katika serikali
ya Tanzania aliinua sura yake iliyoonekana
usawajika kwa mawazo na kujawa mikunjo ya
hasira na uchungu.
Naomba uniitie Madam S, kitengo maalum
usalama wa Taifa tafadhali, fanya hilo sasa hivi
aliamuru na Miranda mara moja alitii agizo
alilopewa. Ndani ya ofisi yake aliandika fax ya
haraka na kuituma kunakohusika, kisha akatulia
akiendelea na majukumu yake mengine.
Dakika kumi na tano zilikuwa nyingi, mlango wa
katibu muhtasi wa waziri wa ulinzi miss Miranda
ulifunguliwa na mwanamama wa makamo
aliingia ndani na kumtazama binti yule aliyekuwa
anajitazama kwenye kioo huku akipaka rangi ya
mdomo. Miranda alistuka aliposikia mlango
ukifunguliwa na kugeuka haraka.
Nimepata ujumbe msichana, mzee yupo?
madam S aliuliza na Miranda bila kujibu
alimuonesha ishara ya kuingia katika ofisi ya
mheshimiwa.
Karibu sana madam S, nilikuwa nakusubiri kwa
hamu kubwa, kwa kukuona tu nahisi kazi
imekwisha waziri wa ulinzi mheshimiwa Maige
alimkaribisha mgeni wake na kumuonesha kiti
cha kukaa naye bila kusita akafanya hivyo,
kasha mheshimiwa akaendelea, Madam S najua
wazi kuwa unafahamu lile nililokuitia, sina haja
ya kulieleza maana jana sote tulikuwa kule
Tazara kwenye lile tukio. Wito wangu hapa ni
kutaka kuona pamoja nawe jinsi ya kulimaliza
hili swala na kuwakamata wahusika,
mheshimiwa Rais amesema lifanyike mara moja,
na mi nikaona kuwa wewe ndiye unaejua jinsi ya
kuifanya kazi hii kwa utaalam
Ooh mheshimiwa, nimekusikia, nimetafakari
sana juu ya hili swala tangu jana, lakini akili
yangu haisomi
Kwa nini?
Sasa hivi sina watu, TSA 1 tumetuma huko
China kwa ajili ya ile issue ya madawa ya
kulevya, TSA 2 naye yupo kule Malawi kwa ajili
ya kuweka mazingira tayari kwa ile kazi yetu,
tufanyeje mheshimiwa, serikalai itakalosema sisi
tutatii madam S aliongea kwa msisitizo
mkubwa.
Ok! Nimekuelewa vizuri, sasa naomba TSA 1,
kamanda Amata arudi mara moja kwa ajili ya
kazi hii waziri maige alitoa oda.
Sawa mheshimiwa, litatekelezwa mara moja
madam S alijibu kwa heshima.
Akifika nchini naomba moja kwamoja uje nae
hapa mheshimiwa aliongeza. Madam S aliinua
mkono wake na kuitazama saa yake kasha
akabonyeza kitufe Fulani na kuendelea
kubonyeza vijitufe vingine juu ya saa hiyo aina
ya casio, kasha akatulia na uendelea na
mazungumzo na waziri Maige wakijadili hali
halisi ya tukio zima lililotukia usiku wa jana.
Hong Kong China
Cheung Sha beach, Lantau
Kamanda Amata alikuwa juu ya kitanda safi
kilichotengenezwa kwa plastick huku akiwa
amejilaza kifua chake alikiruhusu kipigwe na
upepo wa pwani, akiitazama bahari tulivu
iliyokuwa na mawimbi kiasi, pembeni yake
mwanadada mrembo alikuwa amejilaza pamoja
nae wakiongea mawili matatu.
Baada ya mazungumzo yao yaliyokuwa marefu
kiasi na kujawa na vicheko vya mahaba,
walinyanyuka kutoka kwenye vitanda hivyo na
kuelekea hotelini alikofikia kamanda Amata kwa
ajili ya kuendeleza mazungumzo yao kwa
vitendo. Akiwa anakaribia katika ngazi za
kuingilia mapokezi ya hotel hiyo alipishana na
mtu mmoja aliyekuwa akimtazama sana, Amata
hakumtilia maanani mtu huyo, mkono wake wa
kuume ukiwa kiunoni mwa mwanadada akili yake
isingeweza kuwa makini tena katika jambo
lingine. Walipanda ngazi kadhaa na kuufikia
mlango wa chumba chake, Amata alikitazama
kitasa cha mlango ule na kumrudisha kwa
nyuma yule mwanadada kisha akatumbukiza
ufunguo wake na kuufungua ule mlango, kwa
hatua za hadhari aliingia ndani ya chumba ile,
aliangaza huku na huku lakini hakuona dalili ya
mtu ndani mle, lakini kila alipopiga hatua kwenda
ndani alihisi damu ikikimbia na nywele
kumsimama, alisogea kwa ndani ili kwenda
kuichukua bastola yake aliyoificha chini yam to,
hamad! Teke la nguvu lilitua tumboni mwake,
kwa wepesi wa hali ya juu, Amata aliudaka ule
mguu upande wa kanyagio na kuuzungusha kwa
nguvu mpaka akauvunja, yowe la uchungu
lilimtoka yule mtu, Amata alimsukuma na
kumbamizia ukutani, akageuka nyuma haraka
kumtazama yule mwanadada ndipo alipokutana
na bastola iliyokwishatolewa usalama ikiwa
mikononi mwa yule mwanadada ikimlenga yeye,
Amata alijirusha kwa haraka na risasi iliyotoka
ilichimba ukuta, kwa haraka aliuzungusha mguu
wake na kumpiga ngawala safi yule mwanadada
ambaye alipaa juu na kutua katika meza kubwa
ya kioo huku bastola ikimtoka mkononi, iliokotwa
na kamanda Amata na kushikwa barabara
mikononi mwake. Sina muda wa kupoteza,
alijiwazia na kuifyatua ile bastola, risasi moja
alifumua kichwa cha yule jamaa na nyingine
ilizama moyoni mwa yule mwanadada,
Wanaharamu, mara akasikia kamlio kadogo
kama ka mashine ya typewriter kakilia kutoka
katika kitu kama kitabu juu ya droo ya kitanda,
alikawahi na kutoa kijikaratasi kirefu kilichokuwa
na maandishi machache.
Hali siyo nzuri, rudi haraka mgonjwa anahitaji
msaada wako, Tena Sana Aisee alikirudisha kile
kikaratasi katika ile notebook bandia kumbe
ilikuwa ni fax mashine akaifungua tena ile fax
machine yake na kurudia kusoma kile kikaratasi,
akabaki akishangaa Nini kimetokea? alijiuliza
kwa kuwa kazi aliyotumwa huko ilikuwa ndiyo
kwanza imepamba moto, alinyanyauka na
kufungua kabati la nguo kasha akapaki kila kitu
begini, alipokamilisha akaitazama ile miili ya
wale viumbe wawili waliotaka kuiondoa roho
yake, akatoka taratibu katika chumba hicho na
kujipanga kwenda uwanja wa ndege tayari kwa
safari.
Dar es salaam
Kamanda Amata alikaribishwa na vichwa vya
habari vya kutisha katika magazeti siku hiyo,
Mlipuko mkubwa waitikisa Dar es salaam na
lingine likaandika, Ugaidi waigubika Dar , na
mengine mengi yaliandika kila moja kwa jinsi
zake.
Kamanda Amata aliinua uso wake na kumtazama
waziri wa ulinzi kasha akamtazama madam S na
kushusha pumzi ndefu.
Yes, Kamanda, hiyo ndiyo hali halisi iliyoukumba
mji wetu, taifa lipo kwenye maombolezo ya siku
tatu, bendera nusu mlingoti. Serikali inaiomba
ofisi yenu wewe pamoja na madam S
kuikamilisha kazi hii kwa haraka na ufanisi
mkubwa, tuko tayari kuto msaada wowote pale
utakapoitajika, nawatakia mafanikio mema katika
hili na Mungu awatangulie waziri wa ulinzi mh
Maige alimaliza rai yake
Amin! kamanda Amata alijibu na kumtazama
madam S. akiwa ndani ya suti yake nyeusi
Amata alinyanyuka kitini na kuongozana na
madam S kutoka katika ofisi hiyo, walipita pale
alipo Miranda na kugana nae, jicho la kamanda
Amata lilimtazama kwa tuo mwanadaa huyo
ambaye daima utamkuta akitengeneza kama
siyo nywele basi rangi ya midomo kupitia kijikioo
kidogo alichokihifadhi katika motto wa meza.
Hata usipojiremba, we bado ni mrembo tu
Amata alianza uchokozi wa maneno kwa
mwanadada Yule.
Mmmmm kamanda, kuna warembo nitakuwa
mimi? alimjibu huku akiyarembua yale macho
yake makubwa, Nitoe lunch leo, alitupa ombi
huku akiendelea kujitazama kiooni.
Usijali, mrembo kama wewe hakuna mwanaume
atakayekunyima lunch, hata dinner kabisa
Amata alijibu huku akiwa ameushika mlango
tayari kutoka.
Piipiiii, honi za gari ya madam S zilimshtua
kamanda kwenye maongezi yale.
Unaitwa na mama yako huko uende, Miranda
alimwambia Amata
Ok Beibi, nitakucheki mida alijibu na kutoka
nje.
Aliingia garini na kuketi, kasha akajifunga
mkanda wa usalama.
Hivi hii tabia yako utaiacha lini? Wengine wake
za watu hao! madam S alimueleza Amata.
Aaa bibi, hata mimi mtu jamani alijibu kwa
utani.
Shauri yako hivi vingine vitakugharimu sana
Shaka ondoa
* * *
Hili bomu lilikuwa ni bomu la masaa, bomu
ambalo hutegwa makusudi kwa malengo
maalum, kwa hiyo siyo mlipuko wa kawaida ni
wa kukusudiwa kapteni Savana alikuwa akimpa
ripoti ya kwanza ya uchunguzi kamanda Amata
walipokutana pale makao makuu ya jeshi
Upanga.
Kwa hiyo unataka kuniambia mlipuaji alitega
kwa malengo maalum?
Ndiyo
Kamanda Amata alitazama lile faili lililo mbele
yake na kuligeuzageuza. Baada ya mazungumzo
ya kina waliagana na Amata akaenda mahali
pengine kwa uchunguzi. Breki ilikuwa katika
kituo cha polisi cha Tazara kuitazama gari ile
iliyotumika kwa mlipuko ule. Mezani mbele yake
alikutana na ASP Majegero.
Kuna lolote mmepata kuhusu hii gari iliyobeba
mlipuko? lilikuwa ni swali la Amata kwa ASP
majegero.
Aaa hapana ila bado tunaendelea na uchunguzi
ukizingatia gari yenyewe imeungua vibaya
inakuwa ni ngumu kutekeleza hilo kwa wakati
Ok, hebu nilione. Wote wawili walitoka na
kuzunguka uani kuiona gari ile, Amata aliitazama
jinsi ilivyochakaa, aliizunguka na mara
akakutana na kile alichokuwa akikitafuta .
Plate namba ya gari hiyo iliyoungua vibaya kwa
moto, Amata aliingoa na kuitazama kisha bahati
nzuri namba zake zilikuwa za kugongwa siyo zile
za kupuliza, Amata alisoma namba zile kiurahisi
na kuziandika kwenye kijitabu chake kidogo
kasha akaagana na Yule askari polisi na
kuondoka zake. Breki ya kwanza ilikuwa katika
jingo la TRA pale Samora evenue, alishuka na
kufika mapokezi ambapo aliomba kuonana na
ya kuperuzi katika mtandao wao.
Kadiri ya namba hii hiyo ni gari inayomilikiwa
na mama mmoja anaitwa Miss Jesca Mdachi
Yule dada alimjibu Amata.
Ok, maelezo yake mengine tafadhali Kamanda
Amata aliomba
Yule mwanadada aligeuka kwenye kompyuta na
kuprint karatasi Fulani akarudi na kumpatia
Amata.
Kila kitu kimeandikwa hapa alimwambia Amata
Ok asante sana mrembo Amata alishukuru.
Kuna linguine tafadhali? Yule dada alihoji kama
kuna lingine anahitaji msaada nalo. Amata
alimtazama Yule dada kwa uchu alivutiwa na
kifua chake kilichobeba matiti yaliyojaa vizuri.
Hapana kingine zaidi ya namba yako ya simu,
kama upo radhi Amata alitoa ombi lingine la
binafsi, Yule mwanadada alimtabasamia Amata
kisha akauvuta mkoba wake na kutoa business
card na kumpatia, kisha Amata akaondoka zake.
USIPITWE NA RIWAYA HII SEHEMU YA PILI......
story by richard MWAMBE
Dunia inakumbwa na wimbi la ugaidi,
matukio ya kutisha yanayopoteza maisha
ya walio wengi katika pande mbalimbali
za dunia ikiwemo Afrika hususan
Tanzania. Nchi zinazoendelea
zinajumuishwa kuwa na mahusiano na
mataifa beberu ya Maghalibi.
Idara za usalama za Tanzania
znafanikiwa kumtia mkononi Jegan
Grashan akihusishishwa na mlipuko wa
ubalozi wa USA, Dar es salaam. Swahiba
zake wanaishinikiza serikali imuache huru
kwa kutekeleza milipuko kadhaa, wanaipa
siku saba iwe imekamilisha hilo. Je
litawezekana?
Tiririka na mkasa huu mwingine
unaomhusisha Kamanda Amata.
1
MVUA KUBWA ilikuwa ikinyesha katika jiji la Dar
es salaam, jiji linalosifika kwa joto kali
linalowafanya watu wake kujutia kila siku kwa
nini wanaishi hapo, lakini bado kuhama
hawataki. Radi za hapa na pale ziliendelea
kumulikan ardhi yote ya eneo la Tazara katika
makutano ya barabara zenye majina ya viongozi
wakubwa Africa, barabara ya Nyerere na ile ya
Mandela, umeme ulikuwa umekatika na giza
lilitawala kila mahali jioni hiyo, haikuwa usiku
sana kwani ndiyo kwanza kipindi cha majira
kutoka RTD kilikuwa kikianza, hakuna aliyeweza
kuvuka katika makutano hayo, magari yalijaa kila
upande mpaka kule kwenye service road, kelele
za honi zilitawala na matusi ya hapa na pale,
wengine wakijifanya ndiyo askari kuongoza
magari lakini bado hali ilikuwa tete, si wakwenda
Buguruni, wala Ukonga wote walitua pale, mvua
iliendelea kunyesha kwa fujo na ngurumo
zikitawala.
Katikati ya makutano yale kulikuwa na gari aina
ya Peugeot imesimama hali inaunguruma, dereva
wake alishuka na kupiga kelele za hapa na pale
akiwaomba wengine wampishe lakini hakuwapo
wa kumpisha, kwa hasira yule bwana aliubamiza
mlango wa gari na kujichanganya na vijana
waliojaa eneo lile, haikupita dakika mbili mlipuko
mkubwa ulitokea katika gari ile, anga lote
lilifunikwa na rangi nyekundu iliyochanganyika na
moshi mweusi, watu walitawanyika huku na kule
wengine wakitokea katika madirisha ya daladala,
ilimradi tu kujiokoa. Vilio vilisikika huku na kule
watu waliumia sana na wengine kupoteza
maisha, gari zaidi ya ishirini zilidaka moto eneo
lile.
Gari za zimamoto kutoka kampuni binafsi na lile
la jiji yalifika huku polisi wa kutuliza ghasia
wakiwa tayari kusaidia majeruhi kuwakimbiza
hospitali ya Dar Group, Temeke na wengine
Muhimbili moja kwa moja, kazi ilikuwa ngumu
kwa kila mtu aliyekuwa pale, wananchi wote
walisogezwa mbali na eneo la tukio ili kupisha
shughuli za uokoaji. Baada ya takribani dakika
arobaini na tano gari ya jeshi ilisimama karibu
kabisa na jengo la S.S Bakhresa, wakashuka na
vifaa vyao kuelekea pale palipotokea mlipuko
walilizungushia gari lile utepe maalum na
kukusanya kila kilichoonekana na uhusiano na
mlipuko ule kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Hali
iliendelea kuwa tete eneo lile kila mtu alilia
kivyake.
* * *
Ingia kaka, umemaliza kazi bwana mmoja
alisema huku akiufungua mlango wa Toyota
prado na kumruhusu huyo aliyemwita kaka
kuingia kwenye gari hiyo, kasha ikageuza na
kuchukua barabara ya Mandela kuelekea
Buguruni.
Bado, kazi ndiyo kwa nza inaanza yule bwana
aliwaeleza wenzake huku gari ile ikitokomea kwa
kasi maeneo ya Sukita kuielekea Ubungo.
Hii ni vita ya tatu ya dunia, na tunaiendelezea
hapa Tanzania, kwa kuwa ulinzi wan chi hii
hauko makini aliongea bwana mmoja
aliyeonekana kama ndiyo kiongozi wao.
* * *
Mlio mkali wa simu ulimshtua madam S
usingizini, alisonya na kuiinua simu ile huku
akiwa bado kitandani mapema namna hiyo.
Hey, nani? aliuliza kwa hasira.
Madam S, washa runinga yako TBC kasha
nitakupia baadaye kidogo sauti ya upande wa
pili ilitoa ombi, madam S bila kuchelewa
aliichukua rimoti na kuiamuru runinga ile kufanya
kazi. Alipigwa na butwaa na moyo ukaanza
kumuenda mbio, ukizingatia na umri nao ulikuwa
umekwenda, aliifutailia habari ile, na kwa mbali
macho yake yalianza kujaa machozi. Oh my
God alijisemea moyoni, Nini tena hii? alijiuliza
mwenyewe wakati akimfuatilia Grace Kingalame
akitoa maelezo ya moja kwa moja kutoka eneo
la tukio. Madam S alinyanyuka kitandani na
kuutafuta mlango wa bafu, baada ya kujiweka
sawa alivalia suruali yake nadhifu na fulana yake
nyeupe iliyoandikwa Naipenda Tanzania , na juu
yake alijitupi kijikoti cheusi, bastola yake
aliipachika sawia katika mkanda wa suruali
aliyovaa na kutoka moja kwa moja aliiendea gari
yake aina ya Toyota Spacio na kuondoka
akiiacha nyumba yake ikibaki na mlinzi tu. Njia
nzima madam S alikuwa akilaani kilichotokea
hapo Tazara, kama kawaida yake alitamani huyo
mtu amkamate mara moja ili amuoneshe
shughuli nene kwa kufanya jambo kama hilo.
Alifika eneo la tukio na kukuta shughuli
zikiendelea hasa zile za uchunguzi, pale
alikutana na wakuu wa polisi na vyombo vingine
vya usalama kila mmoja akiwa hana la kusema
juu ya tukio hilo, laana za kumlaani aliyetenda
hilo na vizazi vyake vyote ndizo zilikuwa
midomoni mwao.
Atakamatika tu Madam S alimwambia IGP
walipokuwa katika mazungumzo huku
wakiangalia shughuli ile ikikaribia kufika
ukingoni.
Madam S aliinua simu yake na kuitazama,
ilikuwa yapata saa tano usiku, aliwaaga wenzake
na kuondoka eneo lile mara moja huku akiwa na
mawazo lukuki kichwani mwake.
Siku iliyofuata
Miranda! sauti nzito iliita kutoka mlango wa
pili, ilikuwa ni sauti ya waziri wa ulinzi ambaye
ndiyo kwanza alikuwa akiingia ofisini kwake
asubuhi hiyo. Miranda alitii wito huo mara moja
alikiacha kiti chake na kuufuata mkango mkubwa
wa kioo uliokuwa kushoto kwake na kuufungua.
Nimefika mzee! aliitikia. Bwana Sixtus Maige,
waziri mwenye dhamana ya ulinzi katika serikali
ya Tanzania aliinua sura yake iliyoonekana
usawajika kwa mawazo na kujawa mikunjo ya
hasira na uchungu.
Naomba uniitie Madam S, kitengo maalum
usalama wa Taifa tafadhali, fanya hilo sasa hivi
aliamuru na Miranda mara moja alitii agizo
alilopewa. Ndani ya ofisi yake aliandika fax ya
haraka na kuituma kunakohusika, kisha akatulia
akiendelea na majukumu yake mengine.
Dakika kumi na tano zilikuwa nyingi, mlango wa
katibu muhtasi wa waziri wa ulinzi miss Miranda
ulifunguliwa na mwanamama wa makamo
aliingia ndani na kumtazama binti yule aliyekuwa
anajitazama kwenye kioo huku akipaka rangi ya
mdomo. Miranda alistuka aliposikia mlango
ukifunguliwa na kugeuka haraka.
Nimepata ujumbe msichana, mzee yupo?
madam S aliuliza na Miranda bila kujibu
alimuonesha ishara ya kuingia katika ofisi ya
mheshimiwa.
Karibu sana madam S, nilikuwa nakusubiri kwa
hamu kubwa, kwa kukuona tu nahisi kazi
imekwisha waziri wa ulinzi mheshimiwa Maige
alimkaribisha mgeni wake na kumuonesha kiti
cha kukaa naye bila kusita akafanya hivyo,
kasha mheshimiwa akaendelea, Madam S najua
wazi kuwa unafahamu lile nililokuitia, sina haja
ya kulieleza maana jana sote tulikuwa kule
Tazara kwenye lile tukio. Wito wangu hapa ni
kutaka kuona pamoja nawe jinsi ya kulimaliza
hili swala na kuwakamata wahusika,
mheshimiwa Rais amesema lifanyike mara moja,
na mi nikaona kuwa wewe ndiye unaejua jinsi ya
kuifanya kazi hii kwa utaalam
Ooh mheshimiwa, nimekusikia, nimetafakari
sana juu ya hili swala tangu jana, lakini akili
yangu haisomi
Kwa nini?
Sasa hivi sina watu, TSA 1 tumetuma huko
China kwa ajili ya ile issue ya madawa ya
kulevya, TSA 2 naye yupo kule Malawi kwa ajili
ya kuweka mazingira tayari kwa ile kazi yetu,
tufanyeje mheshimiwa, serikalai itakalosema sisi
tutatii madam S aliongea kwa msisitizo
mkubwa.
Ok! Nimekuelewa vizuri, sasa naomba TSA 1,
kamanda Amata arudi mara moja kwa ajili ya
kazi hii waziri maige alitoa oda.
Sawa mheshimiwa, litatekelezwa mara moja
madam S alijibu kwa heshima.
Akifika nchini naomba moja kwamoja uje nae
hapa mheshimiwa aliongeza. Madam S aliinua
mkono wake na kuitazama saa yake kasha
akabonyeza kitufe Fulani na kuendelea
kubonyeza vijitufe vingine juu ya saa hiyo aina
ya casio, kasha akatulia na uendelea na
mazungumzo na waziri Maige wakijadili hali
halisi ya tukio zima lililotukia usiku wa jana.
Hong Kong China
Cheung Sha beach, Lantau
Kamanda Amata alikuwa juu ya kitanda safi
kilichotengenezwa kwa plastick huku akiwa
amejilaza kifua chake alikiruhusu kipigwe na
upepo wa pwani, akiitazama bahari tulivu
iliyokuwa na mawimbi kiasi, pembeni yake
mwanadada mrembo alikuwa amejilaza pamoja
nae wakiongea mawili matatu.
Baada ya mazungumzo yao yaliyokuwa marefu
kiasi na kujawa na vicheko vya mahaba,
walinyanyuka kutoka kwenye vitanda hivyo na
kuelekea hotelini alikofikia kamanda Amata kwa
ajili ya kuendeleza mazungumzo yao kwa
vitendo. Akiwa anakaribia katika ngazi za
kuingilia mapokezi ya hotel hiyo alipishana na
mtu mmoja aliyekuwa akimtazama sana, Amata
hakumtilia maanani mtu huyo, mkono wake wa
kuume ukiwa kiunoni mwa mwanadada akili yake
isingeweza kuwa makini tena katika jambo
lingine. Walipanda ngazi kadhaa na kuufikia
mlango wa chumba chake, Amata alikitazama
kitasa cha mlango ule na kumrudisha kwa
nyuma yule mwanadada kisha akatumbukiza
ufunguo wake na kuufungua ule mlango, kwa
hatua za hadhari aliingia ndani ya chumba ile,
aliangaza huku na huku lakini hakuona dalili ya
mtu ndani mle, lakini kila alipopiga hatua kwenda
ndani alihisi damu ikikimbia na nywele
kumsimama, alisogea kwa ndani ili kwenda
kuichukua bastola yake aliyoificha chini yam to,
hamad! Teke la nguvu lilitua tumboni mwake,
kwa wepesi wa hali ya juu, Amata aliudaka ule
mguu upande wa kanyagio na kuuzungusha kwa
nguvu mpaka akauvunja, yowe la uchungu
lilimtoka yule mtu, Amata alimsukuma na
kumbamizia ukutani, akageuka nyuma haraka
kumtazama yule mwanadada ndipo alipokutana
na bastola iliyokwishatolewa usalama ikiwa
mikononi mwa yule mwanadada ikimlenga yeye,
Amata alijirusha kwa haraka na risasi iliyotoka
ilichimba ukuta, kwa haraka aliuzungusha mguu
wake na kumpiga ngawala safi yule mwanadada
ambaye alipaa juu na kutua katika meza kubwa
ya kioo huku bastola ikimtoka mkononi, iliokotwa
na kamanda Amata na kushikwa barabara
mikononi mwake. Sina muda wa kupoteza,
alijiwazia na kuifyatua ile bastola, risasi moja
alifumua kichwa cha yule jamaa na nyingine
ilizama moyoni mwa yule mwanadada,
Wanaharamu, mara akasikia kamlio kadogo
kama ka mashine ya typewriter kakilia kutoka
katika kitu kama kitabu juu ya droo ya kitanda,
alikawahi na kutoa kijikaratasi kirefu kilichokuwa
na maandishi machache.
Hali siyo nzuri, rudi haraka mgonjwa anahitaji
msaada wako, Tena Sana Aisee alikirudisha kile
kikaratasi katika ile notebook bandia kumbe
ilikuwa ni fax mashine akaifungua tena ile fax
machine yake na kurudia kusoma kile kikaratasi,
akabaki akishangaa Nini kimetokea? alijiuliza
kwa kuwa kazi aliyotumwa huko ilikuwa ndiyo
kwanza imepamba moto, alinyanyauka na
kufungua kabati la nguo kasha akapaki kila kitu
begini, alipokamilisha akaitazama ile miili ya
wale viumbe wawili waliotaka kuiondoa roho
yake, akatoka taratibu katika chumba hicho na
kujipanga kwenda uwanja wa ndege tayari kwa
safari.
Dar es salaam
Kamanda Amata alikaribishwa na vichwa vya
habari vya kutisha katika magazeti siku hiyo,
Mlipuko mkubwa waitikisa Dar es salaam na
lingine likaandika, Ugaidi waigubika Dar , na
mengine mengi yaliandika kila moja kwa jinsi
zake.
Kamanda Amata aliinua uso wake na kumtazama
waziri wa ulinzi kasha akamtazama madam S na
kushusha pumzi ndefu.
Yes, Kamanda, hiyo ndiyo hali halisi iliyoukumba
mji wetu, taifa lipo kwenye maombolezo ya siku
tatu, bendera nusu mlingoti. Serikali inaiomba
ofisi yenu wewe pamoja na madam S
kuikamilisha kazi hii kwa haraka na ufanisi
mkubwa, tuko tayari kuto msaada wowote pale
utakapoitajika, nawatakia mafanikio mema katika
hili na Mungu awatangulie waziri wa ulinzi mh
Maige alimaliza rai yake
Amin! kamanda Amata alijibu na kumtazama
madam S. akiwa ndani ya suti yake nyeusi
Amata alinyanyuka kitini na kuongozana na
madam S kutoka katika ofisi hiyo, walipita pale
alipo Miranda na kugana nae, jicho la kamanda
Amata lilimtazama kwa tuo mwanadaa huyo
ambaye daima utamkuta akitengeneza kama
siyo nywele basi rangi ya midomo kupitia kijikioo
kidogo alichokihifadhi katika motto wa meza.
Hata usipojiremba, we bado ni mrembo tu
Amata alianza uchokozi wa maneno kwa
mwanadada Yule.
Mmmmm kamanda, kuna warembo nitakuwa
mimi? alimjibu huku akiyarembua yale macho
yake makubwa, Nitoe lunch leo, alitupa ombi
huku akiendelea kujitazama kiooni.
Usijali, mrembo kama wewe hakuna mwanaume
atakayekunyima lunch, hata dinner kabisa
Amata alijibu huku akiwa ameushika mlango
tayari kutoka.
Piipiiii, honi za gari ya madam S zilimshtua
kamanda kwenye maongezi yale.
Unaitwa na mama yako huko uende, Miranda
alimwambia Amata
Ok Beibi, nitakucheki mida alijibu na kutoka
nje.
Aliingia garini na kuketi, kasha akajifunga
mkanda wa usalama.
Hivi hii tabia yako utaiacha lini? Wengine wake
za watu hao! madam S alimueleza Amata.
Aaa bibi, hata mimi mtu jamani alijibu kwa
utani.
Shauri yako hivi vingine vitakugharimu sana
Shaka ondoa
* * *
Hili bomu lilikuwa ni bomu la masaa, bomu
ambalo hutegwa makusudi kwa malengo
maalum, kwa hiyo siyo mlipuko wa kawaida ni
wa kukusudiwa kapteni Savana alikuwa akimpa
ripoti ya kwanza ya uchunguzi kamanda Amata
walipokutana pale makao makuu ya jeshi
Upanga.
Kwa hiyo unataka kuniambia mlipuaji alitega
kwa malengo maalum?
Ndiyo
Kamanda Amata alitazama lile faili lililo mbele
yake na kuligeuzageuza. Baada ya mazungumzo
ya kina waliagana na Amata akaenda mahali
pengine kwa uchunguzi. Breki ilikuwa katika
kituo cha polisi cha Tazara kuitazama gari ile
iliyotumika kwa mlipuko ule. Mezani mbele yake
alikutana na ASP Majegero.
Kuna lolote mmepata kuhusu hii gari iliyobeba
mlipuko? lilikuwa ni swali la Amata kwa ASP
majegero.
Aaa hapana ila bado tunaendelea na uchunguzi
ukizingatia gari yenyewe imeungua vibaya
inakuwa ni ngumu kutekeleza hilo kwa wakati
Ok, hebu nilione. Wote wawili walitoka na
kuzunguka uani kuiona gari ile, Amata aliitazama
jinsi ilivyochakaa, aliizunguka na mara
akakutana na kile alichokuwa akikitafuta .
Plate namba ya gari hiyo iliyoungua vibaya kwa
moto, Amata aliingoa na kuitazama kisha bahati
nzuri namba zake zilikuwa za kugongwa siyo zile
za kupuliza, Amata alisoma namba zile kiurahisi
na kuziandika kwenye kijitabu chake kidogo
kasha akaagana na Yule askari polisi na
kuondoka zake. Breki ya kwanza ilikuwa katika
jingo la TRA pale Samora evenue, alishuka na
kufika mapokezi ambapo aliomba kuonana na
ya kuperuzi katika mtandao wao.
Kadiri ya namba hii hiyo ni gari inayomilikiwa
na mama mmoja anaitwa Miss Jesca Mdachi
Yule dada alimjibu Amata.
Ok, maelezo yake mengine tafadhali Kamanda
Amata aliomba
Yule mwanadada aligeuka kwenye kompyuta na
kuprint karatasi Fulani akarudi na kumpatia
Amata.
Kila kitu kimeandikwa hapa alimwambia Amata
Ok asante sana mrembo Amata alishukuru.
Kuna linguine tafadhali? Yule dada alihoji kama
kuna lingine anahitaji msaada nalo. Amata
alimtazama Yule dada kwa uchu alivutiwa na
kifua chake kilichobeba matiti yaliyojaa vizuri.
Hapana kingine zaidi ya namba yako ya simu,
kama upo radhi Amata alitoa ombi lingine la
binafsi, Yule mwanadada alimtabasamia Amata
kisha akauvuta mkoba wake na kutoa business
card na kumpatia, kisha Amata akaondoka zake.
USIPITWE NA RIWAYA HII SEHEMU YA PILI......