HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,399
- 6,077
I DIED TO SAVE MY PRESDANT
Mtunzi Patrick Ck
Simu 0764294499
Season 1
Sehemu 1
hughuli zote zilizopangwa
kufanyika katika kikao
cha bunge zilikamilika na
kabla ya kusitisha shughuli za
bunge kwa siku hiyo hadi siku
inayofuata,spika wa bunge
akamuita waziri anayeshughulika
na bunge mheshimiwa William
Kangoga ili aweze kutoa hoja ya
kutengua kanuni
“Meshimiwa Spika, naomba
kwa ruhusa yako sasa nitoe hoja
kwamba bunge lako tukufu
litengue kanuni ya bunge ili
kuwaruhusu vijana wetu
wanafunzi waliofanya vizuri katika
mithani yao ya kidato cha nne
waweze kuingia bungeni hapo
kesho.Mheshimiwa spika naomba
kutoa hoja”
Baada ya hoja ile kutolewa
wabunge wote wakasimama na
kuiunga mkono halafu spika
akawahoji na wote wakakubalianana hoja ile kwamba kanuni ya
bunge itenguliwe na kuwaruhusu
wanafunzi ishirini waliofanya
vizuri katika mitihani yao ya
kidato cha nne waweze kuingia
bungeni ili waweze kupongezwa na
bunge.
“Ahsanteni sana waheshimiwa
wabunge kwa kukubali watoto
wetu waje bungeni tuwapongeze
na kuwatia moyo ili waweze
kufanya vizuri zaidi huko mbele
waendako.” Akasema spika wa
bunge halafu akasitisha shughuli
za bunge hadi siku inayofuata saa
tatu za asubuhi
*********************
Ni saa tano za usiku sasa
lakini bado Patricia hakuwa na
usingizi.Yeye na mama yake
walikuwa katika chumba kilichoko
ghorofa ya nne ndani ya hoteli hii kubwa mjini Dodoma ijulikanayo
kama Dodoma view hotel.Ni moja
kati ya hoteli yenye hadhi ya juu
kabisa mjini Dodoma na ambayo
wabunge wengi wa bunge la
jamhuri ya muungano wa
Tanzania hupenda kufikia .
“Patricia mbona hulali?Si
unajua siku ya kesho itakakuwa
ndefu? Jitahidi ulale ili usije
ukasinzia katika ukumbi wa
Bunge” akasema Bi Doroth
Mwaukala mama mzazi wa Patricia
“Mama nashindwa kabisa
kupata usingizi siku ya leo.Usiku
nauona mrefu sana” akasema
Patricia binti aliyejaaliwa uzuri wa
kipekee mno
“Una wasi wasi?
“Ndiyo mama lakini si
sana.Nawaza kuhusu kesho sijui
itakuaje pale nitakaposhikana
mkono na mheshimiwa waziri
mkuu huku nikionekana katika
televisheni nchi nzima.Mama sikuwahi kuota siku kama ya
kesho itakuja kunitokea katika
maisha yangu.Bado siamini hadi
hapo nitakaposhikana mkono na
waziri mkuu ndipo nitaamini ni
kweli.Mama kesho ni siku yangu
kubwa mno” akasema
Patricia.Mama yake aliyekuwa
akimtazama mwanae
akatabasamu na kusema
“Usiwe na hofu Patricia.Hii si
ndoto bali ni kitu cha kweli
kinachokwenda kutokea hapo
kesho.Kama ingekuwa ni ndoto
tusingekuwa hapa Dodoma mida
hii katika hoteli kubwa na nzuri
kama hii.Patricia unapaswa
kujivunia mafanikio yako haya
makubwa uliyoyapata.Mwanangu
umenitoa kimaso maso mimi
mama yako kwani hakuna
aliyetegemea kama mwanafunzi
aliyeshika namba moja nchini
Tanzania atakuwa ni kutoka
katika familia masikini kama ya kwetu.Umeidhihirishia nchi na
dunia kwamba hata mtoto wa
masikini anaweza akafanya
mambo makubwa na ya
kushangaza.Umelipandisha
kileleleni jina la familia yetu na
kwa sasa sisi si watu wa
kudharaulika tena kama
ilivyokuwa hapo awali.Laiti baba
yako angekuwa hai kushuhudia
tukio hili sipati picha angekuwa
na furaha ya namna gani…”
akasema Bi Doroth.
“Mama sifa na shukurani
zimwendee mwenyezi Mungu kwa
neema na Baraka zake nyingi
kwangu lakini sifa na shukrani za
pekee pia ni kwako wewe
mama.Wewe ndiye kila kitu
kwangu na ndiye uliyefanikisha
haya yote yakawezekana.Umenipa
ushirikiano mkubwa.Maongozi na
maelekezo yako yameniweka
katika nafasi hii nilipo sasa.Mama
unastahili sifa za kipekee kwa kunijali na kuwa nami na
kunivumilia hata katika nyakati
zile ngumu kabisa.Umejinyima
mambo mengi ili mwanao niweze
kusoma na haya ndiyo matunda
yake” akasema Patricia halafu
akainuka na kuelekea dirishani
,akalifungua na kuutazama mji wa
Dodoma ulivyokuwa usiku hii.
“ Huu ni mwanzo wa safari
yangu ndefu ya maisha.Nina ndoto
nyingi sana za kutimiza maishani
na ndoto ya kwanza ni kuiondoa
familia yangu katika umasikni
huu mkubwa tulionao.Namuonea
huruma mama yangu namna
anavyohangaika
kunisomesha.Lazima nikiri
kwamba si kazi rahisi kwake lakini
amejitahidi kwa kila namna na
kuhakikisha kwamba hakuna siku
nimekosa shule.Huyu ni mama
anayestahili sifa za pekee kabisa.”
Akawaza Patricia halafu akalifunga dirisha na kurejea
kitandani
“ Patricia jitahidi ulale.Muda
umekwenda sana.Kesho
tunatakiwa tuamke asubuhi na
mapema” akasema Bi Doroth
“ Mhh ! mama sijui kama
nitaweza kupata usingizi.Sijazoea
kulala sehemu laini kama hii”
akasema Patricia na wote
wakacheka
“ Patricia unatakiwa uanze
kuzoea vitu kama hivi.Huu ni
mwanzo wako wa safari ndefu ya
maisha yako.Siku moja vitu kama
hivi utaviona vya kawaida.Jitahidi
ulale” akasema Mama yake halafu
akamfunika shuka vizuri akaenda
kuzima taa wakalala.
*********************
Ilikuwa ni mara ya kwanza
kwa Patricia kuingia katika
viwanja vya bunge.Aliustaajabia uzuri wa eneo hili.Hakukaukiwa
na tabasamu.Siku hii alikuwa
amependeza mno.Alivaa gauni
lenye rangi nyeupe chini na juu
likiwa na rangi nyeusi.Miguuni
alivaa viatu virefu vilivyoendana
na gauni alillolivaa.Mavazi haya ya
gharama alizawadiwa na Juliana
mwanamitindo maarufu hapa
nchini ambaye alifurahishwa mno
na matokeo ya Patricia.
Wanafunzi bora ishirini
walipokewa na katibu wa bunge
halafu wakakabidhiwa kwa
wafanyakazi wa bunge ambao
walianza kuwatembeza sehemu
mbali mbali za bunge .Patricia
alionekana kuwa na furaha
pengine kuliko wengine wote kwa
sababu hakujua kama siku moja
angeweza kufika mahala pale.Kati
ya wanafunzi ishirini waliofanya
vizuri mtihani wa kidato cha nne
wengi walionekana kutoka katika
familia bora zenye kujiweza kifedha.Ni Patricia pekee ambaye
alitoka katika familia iliyo masikini
zaidi lakini pamoja na umasikini
wa familia yake iliyokuwa ikiishi
katika chumba kimoja tu cha
kupanga ,aliweza kuwaongoza
wanafunzi wote nchini waliofanya
mtihani wa kidato cha nne na
kushika nafasi yakwanza.
Kwa siku ya leo ingekuwa
vigumu kuamini kwamba Patricia
anatoka katika familia duni
kwanamna alivyokuwa
amependeza kwa mavazi
aliyozawadiwa na mwanamitindo
Juliana.Wakati amekaa na
wenzake wakisubiri kuingia katika
ukumbi wa bunge mara akatokea
mama yake na kumuita pembeni
“ Mama kuna nini mbona
umefurahi namna hiyo?
“ Patricia huwezi
amini.Juliana amekuja .”
“ Juliana?! Patricia akastuka
“ Ndiyo “ Amekuja kufanya nini?
“ Amekuja kukusapoti katika
siku yako kubwa.”
“ Kweli mama ?!! akauliza
Patricia huku akiruka ruka kwa
furaha
“ Ndiyo Patricia.Anasema
kwamba hakutaka kukutaarifu
mapema kwamba atakuja alitaka
akushangaze”
“ mama yuko wapi dada
Juliana? Nipeleke nikaonanane
naye” akasema Patrcia na kwa
haraka wakatembea hadi katika
maegesho ya magari ambako
Juliana alikuwa garini na rafiki
yake aishiye mjini Dodoma.Mara
tu Patricia alipotokea,Juliana
akatoka garini na kumkumbatia
“Wow ! Dada Juliana sikujua
kama utakuja Dodoma”akasema
Patrcia.Juliana akatabasamu na
kusema
“Sikutaka kukutaarifu
mapema kama nitakuja Dodoma.I wanted to surprise you.Siwezi
kukosa katika siku yako kubwa na
muhimu kama hii ya leo.Patricia
najua una wasi wasi sana na
nimeona katika orodha ya watoto
ambao utaambatana nao leo
bungeni ,wote ni kutoka katika
familia zenye uwezo
mkubwa.Usiwe na wasi wasi you
have a huge support” akasema
Juliana na kumshika mkono
Patricia wakaingia
garini,akafungua mkebe mkubwa
wa poda na kuanza kumremba
halafu akavua heleni zake nzuri za
dhahabu
akamvisha.Akamuangalia na
kutabasamu.
“Now you look like a
princes.Go now.Tutaonana
baadae” akasema Juliana ,
Patricia akakimbia kwenda
kuungana na wenzake.Uso wake
ulikuwa na tabasamu zito.Baada
ya Patricia kuondoka,Juliana akaagana na Bi Doroth kwa ahadi
ya kuonana jioni ya siku hiyo
katika sherehe ya kuwapongeza
akina Patricia .
“Juliana nakushukuru sana
kwa msaada wako
mkubwa.Umeweza kunifuta aibu
kubwa siku ya leo. Bila wewe sijui
Patricia angeonekanaje leo.Lakini
kwa saabu yako leo Patricia
ameng’aa na kupendeza kuliko
wenzake wote” akasema Bi Doroth
“ Mama hupaswi
kunishukuru .Patricia ni kama
mdogo wangu.Mimi ni mmoja wa
watu walioguswa sana na matokeo
yake mazuriNinathamini sana
elimu hasa kwa mtoto wa kike na
ndiyo maana nimeamua kwa moyo
wangu kujitolea kumsaidia
Patricia ili aweze kutimiza malengo
yake.Bado ana safari ndefu sana
na ili afikie malengo yake
anahitaji sana sapoti yetu sisi
sote” akasema Juliana halafu akaagana na Bi Dprpth na
kuondoka kwa ahadi ya kukutana
jioni .
***************
Kipindi cha maswali na
majibu kilimalizika , Spika wa
bunge akasoma baadhi ya
matangazo ikiwa ni pamoja na
kuwatambulisha wageni waliofika
hapo bungeni kwa mafunzo halafu
akamuita katibu ili aweze kusema
ni kitu gani kilichokuwa
kinaendelea.Katibu akasimama na
kulitaarifu bunge kwamba ni
wakati wa kuwaruhusu wanafunzi
waliofanya vizuri waingie bungeni
wakabidhiwe vyeti na waziri
mkuu.Spika wa bunge akasimama
na kusema
“Waheshimiwa wabunge ,jana
tulitengua kanuni ya bunge ili
kuwaruhusu watu ambao si
wabunge kuingia ndani ya ukumbi wetu huu.Wageni tuliowaalika ni
wanafunzi ishirini bora katika
mtihani wa kidato cha nne
.Naombeni wakati vijana wetu
wakiingia humu
ukumbini,muwashangilie kwa
makofi kwani wamefanya kazi
kubwa sana” Akasema Spika na
kumuamuru askari wa bunge
awaongoze wanafunzi kungia
ukumbini .Lango kuu
likafunguliwa na wanafunzi
wakaingia wakiwa katika mistari
miwili,mmoja wa wanaume na
mwingine wa wanawake.Makofi
mengi ,vigere gere pamoja na meza
kugongwa vikasikika.Kilikuwa
kipindi cha furaha sana kwa
wabunge kuwashuhudia
wanafunzi wale ishirini bora.Spika
wa bunge akaomba utulivu halafu
akamkaribisha waziri mkuu ili
aweze kusema machache kabla ya
kuwakabidhi vyeti.Waziri mkuu
wa Tanzania mheshimiwa Thobias Kangeba kengaiza akasogea mbele
na kusema
“ Mheshimiwa spika naomba
nikushukuru sana kwa kunipa
nafasi hii niweze kusema
machache kuhusiana na tukio
hili.Napenda nikushukuru wewe
na bunge lako kwa kukubali
kutengua kanuni ili wanafunzi
hawa waweze kukaribishwa
bungeni na kupongezwa.Binafsi
ninafuraha kubwa sana kuwaona
wanafunzi hawa ingawa
ningefurahi zaidi kama
kungekuwa na uwiano sawa baina
ya wavulana na wasichana kwa
sababu naona kati ya wanafunzi
bora ishirini wasichana ni nane tu
na kumi na mbili ni
wavulana.Kuna haja ya kuendelea
kuwekeza zaidi katika elimu ya
mtoto wa kike ili kuwe na uwiano
sawa wa ufaulu.Pamoja na hayo
,kwa niaba ya serikali napenda
kutoa pongezi zangu nyingi kwenu wanafunzi kwa ufaulu huu
mzuri.Haikuwa kazi rahisi
.Yalikuwa ni mapambano na leo
hii mmeibuka
vinara..Nawapongeza pia walimu
na wazazi wenu kwa ushirikiano
wao wa kuwasaidia kuwafikisha
hapa mlipofika.”
“Mheshimiwa spika,mfumo
wetu wa elimu bado unakabiliwa
na changamoto nyingi kama vile
uhaba wa walimu,vitabu,vifaa vya
kufundishia na kujifunzia,lakini
serikali imekuwa ikjitahidi kutatua
changamoto hizi na leo hii
tunashuhudia mwanafunzi wa
kwanza Tanzania ametoka katika
shule ambazo zimejizolea
umaarufu kama shule za kata
ambazo zimekuwa na changamoto
nyingi.”
Makofi mengi yakapigwa
halafu waziri mkuu akaendelea
Mheshikiwa spika,ninaomba
niseme kwamba hata kama tukifanikiwa kutatua changamoto
zote zinazoikabiili sekta ya elimu
hapa nchini lakini bila juhudi
binafsi za wanafunzi wenyewe
kamwe hakutakuwa na ufaulu
mzuri.Kuna shule zenye walimu
wa kutosha na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia lakini
hazikufanya vizuri .Kwa hiyo basi
naomba niwaase wanafunzi
waongeze kasi ya kujisomea
.Mwalimu ana nafasi yake lakini
mwanafunzi pia ana nafasi yake.Ni
vyema kila mmoja akaitumia
vyema nafasi yake.”
“Mheshimiwa spika naomba
nimalizie kwa kutoa pongezi zangu
nyingi kwa niaba ya serikali na
kuwatakia kila la heri wanafunzi
hawa katika safari yao
ndefu.Someni kwa bidii na taifa
linawasuri mje
kulitumikia.Hongereni sana”
akamalizia nasaha zake
mheshimiwa waziri mkuu,wabunge wakamshangilia
kwa kugonga meza halafu spika
wa bunge akasimama
“Tunakushukuru sana
mheshimiwa waziri mkuu kwa
nasaha zako.Natumai wanafunzi
wote wamekusikia na
watayafanyia kazi yale uliyowaasa
Waheshimiwa wabunge
kinachofuata sasa ni mheshimiwa
waziri mkuu kuwakabidhi vyeti
vijana wote ishirini.” Akasema
Spika na zoezi la kutoa vyeti
likaanza.Wa kwanza kuitwa
kwenda kupokea cheti alikuwa
Patrcia.Ukumbi wote wa bunge
ukalipuka kwa makofi na
kushangilia wakimpongeza
msichana huyu kwa kushika
namba moja.Zoezi lilipomalizika
baadhi ya wabunge walipata nafasi
ya kusema machache na kuwaasa
wanafunzi kusoma kwa bidii.Kila
aliyesimama hakuacha
kumpongeza na kumtolea mfano
Mtunzi Patrick Ck
Simu 0764294499
Season 1
Sehemu 1
hughuli zote zilizopangwa
kufanyika katika kikao
cha bunge zilikamilika na
kabla ya kusitisha shughuli za
bunge kwa siku hiyo hadi siku
inayofuata,spika wa bunge
akamuita waziri anayeshughulika
na bunge mheshimiwa William
Kangoga ili aweze kutoa hoja ya
kutengua kanuni
“Meshimiwa Spika, naomba
kwa ruhusa yako sasa nitoe hoja
kwamba bunge lako tukufu
litengue kanuni ya bunge ili
kuwaruhusu vijana wetu
wanafunzi waliofanya vizuri katika
mithani yao ya kidato cha nne
waweze kuingia bungeni hapo
kesho.Mheshimiwa spika naomba
kutoa hoja”
Baada ya hoja ile kutolewa
wabunge wote wakasimama na
kuiunga mkono halafu spika
akawahoji na wote wakakubalianana hoja ile kwamba kanuni ya
bunge itenguliwe na kuwaruhusu
wanafunzi ishirini waliofanya
vizuri katika mitihani yao ya
kidato cha nne waweze kuingia
bungeni ili waweze kupongezwa na
bunge.
“Ahsanteni sana waheshimiwa
wabunge kwa kukubali watoto
wetu waje bungeni tuwapongeze
na kuwatia moyo ili waweze
kufanya vizuri zaidi huko mbele
waendako.” Akasema spika wa
bunge halafu akasitisha shughuli
za bunge hadi siku inayofuata saa
tatu za asubuhi
*********************
Ni saa tano za usiku sasa
lakini bado Patricia hakuwa na
usingizi.Yeye na mama yake
walikuwa katika chumba kilichoko
ghorofa ya nne ndani ya hoteli hii kubwa mjini Dodoma ijulikanayo
kama Dodoma view hotel.Ni moja
kati ya hoteli yenye hadhi ya juu
kabisa mjini Dodoma na ambayo
wabunge wengi wa bunge la
jamhuri ya muungano wa
Tanzania hupenda kufikia .
“Patricia mbona hulali?Si
unajua siku ya kesho itakakuwa
ndefu? Jitahidi ulale ili usije
ukasinzia katika ukumbi wa
Bunge” akasema Bi Doroth
Mwaukala mama mzazi wa Patricia
“Mama nashindwa kabisa
kupata usingizi siku ya leo.Usiku
nauona mrefu sana” akasema
Patricia binti aliyejaaliwa uzuri wa
kipekee mno
“Una wasi wasi?
“Ndiyo mama lakini si
sana.Nawaza kuhusu kesho sijui
itakuaje pale nitakaposhikana
mkono na mheshimiwa waziri
mkuu huku nikionekana katika
televisheni nchi nzima.Mama sikuwahi kuota siku kama ya
kesho itakuja kunitokea katika
maisha yangu.Bado siamini hadi
hapo nitakaposhikana mkono na
waziri mkuu ndipo nitaamini ni
kweli.Mama kesho ni siku yangu
kubwa mno” akasema
Patricia.Mama yake aliyekuwa
akimtazama mwanae
akatabasamu na kusema
“Usiwe na hofu Patricia.Hii si
ndoto bali ni kitu cha kweli
kinachokwenda kutokea hapo
kesho.Kama ingekuwa ni ndoto
tusingekuwa hapa Dodoma mida
hii katika hoteli kubwa na nzuri
kama hii.Patricia unapaswa
kujivunia mafanikio yako haya
makubwa uliyoyapata.Mwanangu
umenitoa kimaso maso mimi
mama yako kwani hakuna
aliyetegemea kama mwanafunzi
aliyeshika namba moja nchini
Tanzania atakuwa ni kutoka
katika familia masikini kama ya kwetu.Umeidhihirishia nchi na
dunia kwamba hata mtoto wa
masikini anaweza akafanya
mambo makubwa na ya
kushangaza.Umelipandisha
kileleleni jina la familia yetu na
kwa sasa sisi si watu wa
kudharaulika tena kama
ilivyokuwa hapo awali.Laiti baba
yako angekuwa hai kushuhudia
tukio hili sipati picha angekuwa
na furaha ya namna gani…”
akasema Bi Doroth.
“Mama sifa na shukurani
zimwendee mwenyezi Mungu kwa
neema na Baraka zake nyingi
kwangu lakini sifa na shukrani za
pekee pia ni kwako wewe
mama.Wewe ndiye kila kitu
kwangu na ndiye uliyefanikisha
haya yote yakawezekana.Umenipa
ushirikiano mkubwa.Maongozi na
maelekezo yako yameniweka
katika nafasi hii nilipo sasa.Mama
unastahili sifa za kipekee kwa kunijali na kuwa nami na
kunivumilia hata katika nyakati
zile ngumu kabisa.Umejinyima
mambo mengi ili mwanao niweze
kusoma na haya ndiyo matunda
yake” akasema Patricia halafu
akainuka na kuelekea dirishani
,akalifungua na kuutazama mji wa
Dodoma ulivyokuwa usiku hii.
“ Huu ni mwanzo wa safari
yangu ndefu ya maisha.Nina ndoto
nyingi sana za kutimiza maishani
na ndoto ya kwanza ni kuiondoa
familia yangu katika umasikni
huu mkubwa tulionao.Namuonea
huruma mama yangu namna
anavyohangaika
kunisomesha.Lazima nikiri
kwamba si kazi rahisi kwake lakini
amejitahidi kwa kila namna na
kuhakikisha kwamba hakuna siku
nimekosa shule.Huyu ni mama
anayestahili sifa za pekee kabisa.”
Akawaza Patricia halafu akalifunga dirisha na kurejea
kitandani
“ Patricia jitahidi ulale.Muda
umekwenda sana.Kesho
tunatakiwa tuamke asubuhi na
mapema” akasema Bi Doroth
“ Mhh ! mama sijui kama
nitaweza kupata usingizi.Sijazoea
kulala sehemu laini kama hii”
akasema Patricia na wote
wakacheka
“ Patricia unatakiwa uanze
kuzoea vitu kama hivi.Huu ni
mwanzo wako wa safari ndefu ya
maisha yako.Siku moja vitu kama
hivi utaviona vya kawaida.Jitahidi
ulale” akasema Mama yake halafu
akamfunika shuka vizuri akaenda
kuzima taa wakalala.
*********************
Ilikuwa ni mara ya kwanza
kwa Patricia kuingia katika
viwanja vya bunge.Aliustaajabia uzuri wa eneo hili.Hakukaukiwa
na tabasamu.Siku hii alikuwa
amependeza mno.Alivaa gauni
lenye rangi nyeupe chini na juu
likiwa na rangi nyeusi.Miguuni
alivaa viatu virefu vilivyoendana
na gauni alillolivaa.Mavazi haya ya
gharama alizawadiwa na Juliana
mwanamitindo maarufu hapa
nchini ambaye alifurahishwa mno
na matokeo ya Patricia.
Wanafunzi bora ishirini
walipokewa na katibu wa bunge
halafu wakakabidhiwa kwa
wafanyakazi wa bunge ambao
walianza kuwatembeza sehemu
mbali mbali za bunge .Patricia
alionekana kuwa na furaha
pengine kuliko wengine wote kwa
sababu hakujua kama siku moja
angeweza kufika mahala pale.Kati
ya wanafunzi ishirini waliofanya
vizuri mtihani wa kidato cha nne
wengi walionekana kutoka katika
familia bora zenye kujiweza kifedha.Ni Patricia pekee ambaye
alitoka katika familia iliyo masikini
zaidi lakini pamoja na umasikini
wa familia yake iliyokuwa ikiishi
katika chumba kimoja tu cha
kupanga ,aliweza kuwaongoza
wanafunzi wote nchini waliofanya
mtihani wa kidato cha nne na
kushika nafasi yakwanza.
Kwa siku ya leo ingekuwa
vigumu kuamini kwamba Patricia
anatoka katika familia duni
kwanamna alivyokuwa
amependeza kwa mavazi
aliyozawadiwa na mwanamitindo
Juliana.Wakati amekaa na
wenzake wakisubiri kuingia katika
ukumbi wa bunge mara akatokea
mama yake na kumuita pembeni
“ Mama kuna nini mbona
umefurahi namna hiyo?
“ Patricia huwezi
amini.Juliana amekuja .”
“ Juliana?! Patricia akastuka
“ Ndiyo “ Amekuja kufanya nini?
“ Amekuja kukusapoti katika
siku yako kubwa.”
“ Kweli mama ?!! akauliza
Patricia huku akiruka ruka kwa
furaha
“ Ndiyo Patricia.Anasema
kwamba hakutaka kukutaarifu
mapema kwamba atakuja alitaka
akushangaze”
“ mama yuko wapi dada
Juliana? Nipeleke nikaonanane
naye” akasema Patrcia na kwa
haraka wakatembea hadi katika
maegesho ya magari ambako
Juliana alikuwa garini na rafiki
yake aishiye mjini Dodoma.Mara
tu Patricia alipotokea,Juliana
akatoka garini na kumkumbatia
“Wow ! Dada Juliana sikujua
kama utakuja Dodoma”akasema
Patrcia.Juliana akatabasamu na
kusema
“Sikutaka kukutaarifu
mapema kama nitakuja Dodoma.I wanted to surprise you.Siwezi
kukosa katika siku yako kubwa na
muhimu kama hii ya leo.Patricia
najua una wasi wasi sana na
nimeona katika orodha ya watoto
ambao utaambatana nao leo
bungeni ,wote ni kutoka katika
familia zenye uwezo
mkubwa.Usiwe na wasi wasi you
have a huge support” akasema
Juliana na kumshika mkono
Patricia wakaingia
garini,akafungua mkebe mkubwa
wa poda na kuanza kumremba
halafu akavua heleni zake nzuri za
dhahabu
akamvisha.Akamuangalia na
kutabasamu.
“Now you look like a
princes.Go now.Tutaonana
baadae” akasema Juliana ,
Patricia akakimbia kwenda
kuungana na wenzake.Uso wake
ulikuwa na tabasamu zito.Baada
ya Patricia kuondoka,Juliana akaagana na Bi Doroth kwa ahadi
ya kuonana jioni ya siku hiyo
katika sherehe ya kuwapongeza
akina Patricia .
“Juliana nakushukuru sana
kwa msaada wako
mkubwa.Umeweza kunifuta aibu
kubwa siku ya leo. Bila wewe sijui
Patricia angeonekanaje leo.Lakini
kwa saabu yako leo Patricia
ameng’aa na kupendeza kuliko
wenzake wote” akasema Bi Doroth
“ Mama hupaswi
kunishukuru .Patricia ni kama
mdogo wangu.Mimi ni mmoja wa
watu walioguswa sana na matokeo
yake mazuriNinathamini sana
elimu hasa kwa mtoto wa kike na
ndiyo maana nimeamua kwa moyo
wangu kujitolea kumsaidia
Patricia ili aweze kutimiza malengo
yake.Bado ana safari ndefu sana
na ili afikie malengo yake
anahitaji sana sapoti yetu sisi
sote” akasema Juliana halafu akaagana na Bi Dprpth na
kuondoka kwa ahadi ya kukutana
jioni .
***************
Kipindi cha maswali na
majibu kilimalizika , Spika wa
bunge akasoma baadhi ya
matangazo ikiwa ni pamoja na
kuwatambulisha wageni waliofika
hapo bungeni kwa mafunzo halafu
akamuita katibu ili aweze kusema
ni kitu gani kilichokuwa
kinaendelea.Katibu akasimama na
kulitaarifu bunge kwamba ni
wakati wa kuwaruhusu wanafunzi
waliofanya vizuri waingie bungeni
wakabidhiwe vyeti na waziri
mkuu.Spika wa bunge akasimama
na kusema
“Waheshimiwa wabunge ,jana
tulitengua kanuni ya bunge ili
kuwaruhusu watu ambao si
wabunge kuingia ndani ya ukumbi wetu huu.Wageni tuliowaalika ni
wanafunzi ishirini bora katika
mtihani wa kidato cha nne
.Naombeni wakati vijana wetu
wakiingia humu
ukumbini,muwashangilie kwa
makofi kwani wamefanya kazi
kubwa sana” Akasema Spika na
kumuamuru askari wa bunge
awaongoze wanafunzi kungia
ukumbini .Lango kuu
likafunguliwa na wanafunzi
wakaingia wakiwa katika mistari
miwili,mmoja wa wanaume na
mwingine wa wanawake.Makofi
mengi ,vigere gere pamoja na meza
kugongwa vikasikika.Kilikuwa
kipindi cha furaha sana kwa
wabunge kuwashuhudia
wanafunzi wale ishirini bora.Spika
wa bunge akaomba utulivu halafu
akamkaribisha waziri mkuu ili
aweze kusema machache kabla ya
kuwakabidhi vyeti.Waziri mkuu
wa Tanzania mheshimiwa Thobias Kangeba kengaiza akasogea mbele
na kusema
“ Mheshimiwa spika naomba
nikushukuru sana kwa kunipa
nafasi hii niweze kusema
machache kuhusiana na tukio
hili.Napenda nikushukuru wewe
na bunge lako kwa kukubali
kutengua kanuni ili wanafunzi
hawa waweze kukaribishwa
bungeni na kupongezwa.Binafsi
ninafuraha kubwa sana kuwaona
wanafunzi hawa ingawa
ningefurahi zaidi kama
kungekuwa na uwiano sawa baina
ya wavulana na wasichana kwa
sababu naona kati ya wanafunzi
bora ishirini wasichana ni nane tu
na kumi na mbili ni
wavulana.Kuna haja ya kuendelea
kuwekeza zaidi katika elimu ya
mtoto wa kike ili kuwe na uwiano
sawa wa ufaulu.Pamoja na hayo
,kwa niaba ya serikali napenda
kutoa pongezi zangu nyingi kwenu wanafunzi kwa ufaulu huu
mzuri.Haikuwa kazi rahisi
.Yalikuwa ni mapambano na leo
hii mmeibuka
vinara..Nawapongeza pia walimu
na wazazi wenu kwa ushirikiano
wao wa kuwasaidia kuwafikisha
hapa mlipofika.”
“Mheshimiwa spika,mfumo
wetu wa elimu bado unakabiliwa
na changamoto nyingi kama vile
uhaba wa walimu,vitabu,vifaa vya
kufundishia na kujifunzia,lakini
serikali imekuwa ikjitahidi kutatua
changamoto hizi na leo hii
tunashuhudia mwanafunzi wa
kwanza Tanzania ametoka katika
shule ambazo zimejizolea
umaarufu kama shule za kata
ambazo zimekuwa na changamoto
nyingi.”
Makofi mengi yakapigwa
halafu waziri mkuu akaendelea
Mheshikiwa spika,ninaomba
niseme kwamba hata kama tukifanikiwa kutatua changamoto
zote zinazoikabiili sekta ya elimu
hapa nchini lakini bila juhudi
binafsi za wanafunzi wenyewe
kamwe hakutakuwa na ufaulu
mzuri.Kuna shule zenye walimu
wa kutosha na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia lakini
hazikufanya vizuri .Kwa hiyo basi
naomba niwaase wanafunzi
waongeze kasi ya kujisomea
.Mwalimu ana nafasi yake lakini
mwanafunzi pia ana nafasi yake.Ni
vyema kila mmoja akaitumia
vyema nafasi yake.”
“Mheshimiwa spika naomba
nimalizie kwa kutoa pongezi zangu
nyingi kwa niaba ya serikali na
kuwatakia kila la heri wanafunzi
hawa katika safari yao
ndefu.Someni kwa bidii na taifa
linawasuri mje
kulitumikia.Hongereni sana”
akamalizia nasaha zake
mheshimiwa waziri mkuu,wabunge wakamshangilia
kwa kugonga meza halafu spika
wa bunge akasimama
“Tunakushukuru sana
mheshimiwa waziri mkuu kwa
nasaha zako.Natumai wanafunzi
wote wamekusikia na
watayafanyia kazi yale uliyowaasa
Waheshimiwa wabunge
kinachofuata sasa ni mheshimiwa
waziri mkuu kuwakabidhi vyeti
vijana wote ishirini.” Akasema
Spika na zoezi la kutoa vyeti
likaanza.Wa kwanza kuitwa
kwenda kupokea cheti alikuwa
Patrcia.Ukumbi wote wa bunge
ukalipuka kwa makofi na
kushangilia wakimpongeza
msichana huyu kwa kushika
namba moja.Zoezi lilipomalizika
baadhi ya wabunge walipata nafasi
ya kusema machache na kuwaasa
wanafunzi kusoma kwa bidii.Kila
aliyesimama hakuacha
kumpongeza na kumtolea mfano