Riwaya: Huba la miss Tanzania

Riwaya: Huba la miss Tanzania

HUBA LA MISS TANZANIA-PART 17
Shebby akiwa yupo kamili gado kwa kupiga matukio mengine ya kutikisa jiji alikuwa anaegesha gari yake kwenye uwanja wa Biafra-Kinondoni mbele ya Chuo Kikuu Huria 'Open University of Tanzania (OUT)'. Akashuka nje ya gari lake, akaangalia saa yake ya mkononi akatabasamu ilikuwa ni saa tatu kasorobo ya usiku. Alichofanya Shebby kwanza ni kutafuta lilipo duka la kuuzia dawa za binadamu 'Pharmacy' iliyopo jirani na hapo eneo la Biafra usiku huo.


"Habari za usiku dada yangu, pole sana na kazi!" alisalimia Shebby baada ya kufungua mlango wa duka hilo la madawa na kuingia ndani. "Ahsante sana, usinipe pole nipe hongera, Tanzania ya sasa kauli mbiu ni 'Hapa kazi tu' mpaka kieleweke " akajibu mhudumu yule kwa bashasha wakaangua kicheko wote kwa pamoja. "Sijui nikusaidie nini kaka yangu, nipo tayari kukuhudumia" alivunja furaha ile ya kicheko mhudumu yule ambaye dalili zote zilionyesha anakaribia kufunga duka lake. "Dada yangu mie nina aleji ya macho, yanakuwa mekunduu sasa naomba unisaidie dawa ya macho 'Altazine' nikaminyie jichoni nipate kulala vizuri maana yanawasha kwelikweli" alijieleza Shebby kwa ufasaha. "Hiyo dawa ipo pole sana thamani yake ni shilingi elfu nne tu za Kitanzania" alijibu yule dada huku akiitafuta dawa hiyo kutoka kwenye shelfu za kutunzia dawa na kumkabidhi dawa hiyo Shebby.

"Mhhhh...mbona sio hii, naona wameandika 'Visine Eye drops' wakati mie nahitaji Altazine, nyie wauza madawa bwana wakati mwingine wababaishajiii...." alizungumza Shebby kwa hasira kidogo baada ya kuona jina ni tofauti na dawa aliyoiagiza. "Baba yangu usikasirike dawa ni hiyo hiyo tofauti ni majina ya kibiashara tu 'brand name' hiyo dawa uliyoitaka ya Altazine ina majina kochokocho. Altazine inajulikana pia kama Geneye Extra, Geneyes, Opti-Clear, Optigene 3, Redness Relief, Redness Relief Original, Visine, Visine Maximum Redness Relief, Vision Clear hayo yote ni majina yake" alifafanua kiufasaha kuonyesha hajakaa pale dukani bure bure bali amekaa kwa sababu amesomea elimu ya famasia. "Samahani sana kwa kutoheshimu taaluma yako lakini nyie wenyewe ndio mnatuchanganya majina yote hayo ya kazi gani sasa" aliomba msamaha Shebby huku akijitetea kwa mkoroganyiko huo uliotokea.


"Unachotakiwa wewe kuzingatia ni viambata vyake vya kwenye 'Generic Name' ambayo ni tetrahydrozoline ophthalmic ambayo kazi yake ni kupunguza kipenyo cha mishipa ya damu inayoelekea kwenye jicho ili kupunguza jicho kuwa na rangi nyekundu" Alifafanua kwa weledi mkubwa, ufafanuzi ambao ulimshibisha vilivyo Shebby. Hakuwa na muda wa kupoteza, akailipia dawa yake ya macho na kutimka zake haraka haraka kuelekea Break Point.


Profesa Kaganda alikuwa tayari kashawasili kwenye mkahawa wa 'Break Point Restaurant' uliopo maeneo ya Kinondoni. Shebby baada ya kuzisoma nyendo za Profesa Kaganda kwa zaidi ya wiki moja, akagundua ratiba yake akitoka chuoni IFM kufundisha, aghalabu anapitia Break Point ya Kinondoni anapata mlo wake wa usiku, kisha anaendeleza moja moto, moja baridi kabla ya kurejea nyumbani kwake Salasala. Shebby na yeye alishajifanya kijiwe chake ni Break Point cha kupatia mlo wake ili mradi azisome vizuri nyendo za mlengwa wake. Shebby akapita vichochoro vya ndani kwa ndani mpaka akaja kuibukia Break Point ndani ya mwendo wa takribani dakika 10 tu. Alipoangalia kwenye maegesho ya magari Shebby akatabasamu, baada ya kuliona gari la Profesa limeegeshwa nje ya mkahawa.


Shebby akiwa amevaa kofia yake ya pama ya rangi ya kahawia na miwani yake nyeusi, huku juu akiwa amevalia jaketi la baridi la kisasa rangi nyeusi lenye michirizi ya rangi ya uzurungi lililotengenezwa kwa ngozi ndani yake akiwa na fulana ya Polo ya rangi ya kijani bila kusahau sarawili yake ya dangirizi nyeusi yenye mifuko mifuko mingi na safari buti zake. Kwa ufupi alikuwa anaonekana ni mtanashati na maridadi kwa mavazi, lakini moyo wake ndani ulikuwa mweusi ti ti ti kwa kiu ya kulipiza kisasi kwa wote waliomaharibia huba lake kwa Miss Tanzania. Mkahawa siku hiyo ya Ijumaa ulikuwa umeshona watu vilivyo utasema kuna chakula na vinywaji vya bure kumbe wanalipia pesa zao. Watu wa mataifa mbalimbali kuanzia wazungu, wahindi, waarabu na Waafrika ambao wana maisha bora, sio mahohe hae, pangu pakavu tia mchuzi. Walikuwa wanakula na kunywa huku wanazungumza kwa furaha kubwa.


Kama kawaida yake Profesa Kaganda alikuwa ni mtu mpekepeke asiyependa kujichanganya na watu akiwa kwenye starehe zake, alikuwa amejitenga kwenye meza ya kukaa watu wanne, wakiwa wapo wawili tu. Shebby moja kwa moja akaenda kuungana nao sasa wakawa watu watatu. "Good evening waungwana...!" alisalimia Shebby na kukaa kiti mkabala na mbaya wake. Wakaitikia salamu ile huku wanamkaribisha kwa bashasha kama ujuavyo ukarimu wa Watanzania wakikutana utasema ni ndugu wa familia moja kwa namna wanavyochangamkiana. Mhudumu akamfuata Shebby kwa ajili ya kumsikiliza mahitaji yake. "Niletee Wali kwa nyama ya nyati iliyopikwa chukuchuku tu kwa nyanya, kwa upande wa kinywaji niletee juisi yoyote ya matunda unayoipenda wewe ninywe! " aliagiza Shebby kwa mhudumu yule. Ambaye alitii maagizo ya mteja wake na kwenda kupeleka oda yake jikoni.

Break Point ni mkahawa ambao ulikuwa unasifika jijini Dar es Salaam kwa mapishi ya nyama za porini, kuanzia nyati, swala na nyinginezo. Hilo ndio jambo ambalo lilikuwa pia linamvutia Profesa Kaganda kula milo yake hapo. Alikuwa ni msomi ambaye hana mke nyumbani kwake anaishi kinembanemba tu. Alishawahi kuwa na mke wa Kijerumani aliyewahi kuzaa nae watoto wawili wa kiume akiwa masomoni nchini Ujerumani. Kilichotokea baina yao mpaka ndoa hiyo kuvunjika ni siri yao na Manani, lakini kwa muda mrefu watu wanaomjua hawajahi kumuona mkewe wala watoto wake. Alikuwa ni mtu wa kula bata kwa kwenda mbele hana majukumu yoyote ya kifamilia zaidi ya kujihudumia yeye mwenyewe tu.


Alipoletewa chakula chake akawa Shebby anakishambulia kwa pupa chakula kile kitamu hasa ukichukulia alikuwa na njaa kali. Kipindi chote wapo watatu kwenye meza walikuwa wanabadilishana mazungumzo mbalimbali ya mambo yanayoendelea nchini Tanzania kuanzia siasa mpaka kwenye burudani. Huku Shebby akitafuta nafasi ya kumfanyia tukio alilolikusudia Profesa Kaganda. Fursa adhimu aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ikawadia, yule mwenzao kwenye ile meza akawaaga, akanyanyuka zake kuondoka. Mezani wakabaki wawili tu, Profesa Kaganda na Shebby, mahasimu wawili wasiopikika chungu kimoja, utamu zaidi ukichagizwa kwa mmoja kumtambua mwenzake wakati mwingine hamjui mwenzake.

Laiti Profesa Kaganda angefahamu kuwa mbele yupo wakala wa Ziraeli malaika mtoa roho za waja, Wallahi angetimua mbio zile za Kibanga ampiga mkoloni. Lakini ajuaye ya ghaibu ni Rabana, mlango wa funguo za siri anazo yeye tu hajamuwakilisha yoyote.


"Waitress...Weeeeh...Waitressssss.....kuja hapa ongeza bia moja ya mwisho hapa kisha ulete bili yangu, nikalale zangu mieee...." alimuita mhudumu Profesa Kaganda huku akiwa ndio amemaliza msitu wa bia zilizotapakaa mezani pale. Alipoagiza tu kabla hajaletewa akanyanyuka kuelekea msalani kujisaidia. Hapo hapo Shebby kachomoa kutoka kwenye mfuko wake wa dangirizi dawa yake ya macho na kuiminyia matone kama manne tu kwenye glasi ile aliyokuwa anaitumia kunywea pombe zake Profesa Kaganda.


"Usifungue kwanza hiyo bia yake msubiri kwanza arudi, maana kaka yangu huyu akilewa ana matata sana yaani" alizungumza Shebby baada ya mhudumu Kuja kwa ghafla na bia aliyoagizwa na kutaka kuifungua. Hali iliyopelekea Shebby aidondoshe ile dawa yake chini kwa uoga kwa malengo ya kuwa ataiokota mhudumu akiondoka zake. Akamdanganya pia mhudumu kama yule Profesa ni kaka yake wa damu ili kuwafanya wahudumu wa pale waamini kuwa ni wamoja. "Yaani....kumbe hata nyie wanandugu mnamjua vizuri eeeh huyu Profesa akiwa hajautwika mtindi ni mtu mzuri sana, hariri hanaga shida na mtu lakini shida yake akilewa tu mhhhhhh...fujo tupu mtindo mmoja mara anapapasa papasa wahudumu miili yao kimahaba utasema kaingia balehe juzi juzi" aliongea mhudumu yule akionyesha kuchoshwa na tabia chafu za Profesa Kaganda.


Huo ndio unyanyasaji wa kijinsia mashuhuri sana kwa wahudumu wa baa na mikahawani wanaofanyiwa na wateja wao pindi wakilewa lakini hamna wa kuwapazia sauti kutokana na unyanyasaji huo wa mashambulio ya aibu. Kwanza wakipaza sauti zao watafukuzwa kazi mara moja na wamiliki wa maeneo wanayofanyia kazi kwa kisingizio cha kuwa mteja ni mfalme hivyo umridhishe chochote akitakacho. Tegemeo lao pekee la kutetea haki zao lilibakia kwa ' CHODAWU' Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Mahotelini, Majumbani na Huduma za Jamii, lakini wapi chama hicho kilikuwa kwenye usingizi mzito wa pono, si hayati si mamati wapo wapo siku zinasonga.


"Safi sana kwa kunisubiria, mteja ni mfalme maana usalama siku hizi ni mdogo wewe binti lazima nishuhudie unavyofungua" alizungumza Profesa Kaganda baada ya kutua pale mezani na kumuona mhudumu amesimama na bia yake anamsubiria yeye. "Kweli Bwana broo...siku hizi dunia inakaribia machweo kabisa kila aina za uhalifu unaovuma zama hizi" alijifaragua Shebby huku moyoni akijua tayari kashamuingia mkenge Profesa Kaganda. Akafunguliwa bia ile Profesa kisha kwa heshima na taadhima dada yule akaimimina bia ile kwenye glasi iliyofanyiwa mambo mambo na Shebby. Bila kuchelewa ilipojazwa tu kinywaji kile, Profesa akainyanyua juu kwa juu huku anaanza kuigiza kwa mtindo wa tarumbeta bila kupumzika, kisha alipoitua chini ilikuwa ipo tupu.


Alipoishika bia yake ili ajimiminie tena kwa mara ingine akawa kama mtu mwenye kizunguzungu anasitasita. "Profesa nini tena..?" Shebby alijishebedua kumuuuliza wakati anajua tayari Altazine imeshafanya vitu vyake mwilini. "Naa...ji... si..ki... a dizz....ne...ssss, ni...pe.....leke...... kwe...nye ga...riiii..." alizungumza kwa shida sana akiwa analalamika kuhisi kizunguzungu.


Shebby ndio fursa aliyokuwa anaitaka hiyo akaanza kumnyanyua kwa kutumia mabega yake anamburuta anamtoa nje ya mkahawa ule. Hamna aliyejali sana tukio hilo walijua tu ni mlevi aliyezidiwa na kileo anasaidiwa kupelekwa nyumbani kwake na ndugu yake au msamaria mwema. Ikawa ndio mwisho wa Profesa Kaganda kuonekana kwenye uso wa dunia hii.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 17
Shebby akiwa yupo kamili gado kwa kupiga matukio mengine ya kutikisa jiji alikuwa anaegesha gari yake kwenye uwanja wa Biafra-Kinondoni mbele ya Chuo Kikuu Huria 'Open University of Tanzania (OUT)'. Akashuka nje ya gari lake, akaangalia saa yake ya mkononi akatabasamu ilikuwa ni saa tatu kasorobo ya usiku. Alichofanya Shebby kwanza ni kutafuta lilipo duka la kuuzia dawa za binadamu 'Pharmacy' iliyopo jirani na hapo eneo la Biafra usiku huo.


"Habari za usiku dada yangu, pole sana na kazi!" alisalimia Shebby baada ya kufungua mlango wa duka hilo la madawa na kuingia ndani. "Ahsante sana, usinipe pole nipe hongera, Tanzania ya sasa kauli mbiu ni 'Hapa kazi tu' mpaka kieleweke " akajibu mhudumu yule kwa bashasha wakaangua kicheko wote kwa pamoja. "Sijui nikusaidie nini kaka yangu, nipo tayari kukuhudumia" alivunja furaha ile ya kicheko mhudumu yule ambaye dalili zote zilionyesha anakaribia kufunga duka lake. "Dada yangu mie nina aleji ya macho, yanakuwa mekunduu sasa naomba unisaidie dawa ya macho 'Altazine' nikaminyie jichoni nipate kulala vizuri maana yanawasha kwelikweli" alijieleza Shebby kwa ufasaha. "Hiyo dawa ipo pole sana thamani yake ni shilingi elfu nne tu za Kitanzania" alijibu yule dada huku akiitafuta dawa hiyo kutoka kwenye shelfu za kutunzia dawa na kumkabidhi dawa hiyo Shebby.

"Mhhhh...mbona sio hii, naona wameandika 'Visine Eye drops' wakati mie nahitaji Altazine, nyie wauza madawa bwana wakati mwingine wababaishajiii...." alizungumza Shebby kwa hasira kidogo baada ya kuona jina ni tofauti na dawa aliyoiagiza. "Baba yangu usikasirike dawa ni hiyo hiyo tofauti ni majina ya kibiashara tu 'brand name' hiyo dawa uliyoitaka ya Altazine ina majina kochokocho. Altazine inajulikana pia kama Geneye Extra, Geneyes, Opti-Clear, Optigene 3, Redness Relief, Redness Relief Original, Visine, Visine Maximum Redness Relief, Vision Clear hayo yote ni majina yake" alifafanua kiufasaha kuonyesha hajakaa pale dukani bure bure bali amekaa kwa sababu amesomea elimu ya famasia. "Samahani sana kwa kutoheshimu taaluma yako lakini nyie wenyewe ndio mnatuchanganya majina yote hayo ya kazi gani sasa" aliomba msamaha Shebby huku akijitetea kwa mkoroganyiko huo uliotokea.


"Unachotakiwa wewe kuzingatia ni viambata vyake vya kwenye 'Generic Name' ambayo ni tetrahydrozoline ophthalmic ambayo kazi yake ni kupunguza kipenyo cha mishipa ya damu inayoelekea kwenye jicho ili kupunguza jicho kuwa na rangi nyekundu" Alifafanua kwa weledi mkubwa, ufafanuzi ambao ulimshibisha vilivyo Shebby. Hakuwa na muda wa kupoteza, akailipia dawa yake ya macho na kutimka zake haraka haraka kuelekea Break Point.


Profesa Kaganda alikuwa tayari kashawasili kwenye mkahawa wa 'Break Point Restaurant' uliopo maeneo ya Kinondoni. Shebby baada ya kuzisoma nyendo za Profesa Kaganda kwa zaidi ya wiki moja, akagundua ratiba yake akitoka chuoni IFM kufundisha, aghalabu anapitia Break Point ya Kinondoni anapata mlo wake wa usiku, kisha anaendeleza moja moto, moja baridi kabla ya kurejea nyumbani kwake Salasala. Shebby na yeye alishajifanya kijiwe chake ni Break Point cha kupatia mlo wake ili mradi azisome vizuri nyendo za mlengwa wake. Shebby akapita vichochoro vya ndani kwa ndani mpaka akaja kuibukia Break Point ndani ya mwendo wa takribani dakika 10 tu. Alipoangalia kwenye maegesho ya magari Shebby akatabasamu, baada ya kuliona gari la Profesa limeegeshwa nje ya mkahawa.


Shebby akiwa amevaa kofia yake ya pama ya rangi ya kahawia na miwani yake nyeusi, huku juu akiwa amevalia jaketi la baridi la kisasa rangi nyeusi lenye michirizi ya rangi ya uzurungi lililotengenezwa kwa ngozi ndani yake akiwa na fulana ya Polo ya rangi ya kijani bila kusahau sarawili yake ya dangirizi nyeusi yenye mifuko mifuko mingi na safari buti zake. Kwa ufupi alikuwa anaonekana ni mtanashati na maridadi kwa mavazi, lakini moyo wake ndani ulikuwa mweusi ti ti ti kwa kiu ya kulipiza kisasi kwa wote waliomaharibia huba lake kwa Miss Tanzania. Mkahawa siku hiyo ya Ijumaa ulikuwa umeshona watu vilivyo utasema kuna chakula na vinywaji vya bure kumbe wanalipia pesa zao. Watu wa mataifa mbalimbali kuanzia wazungu, wahindi, waarabu na Waafrika ambao wana maisha bora, sio mahohe hae, pangu pakavu tia mchuzi. Walikuwa wanakula na kunywa huku wanazungumza kwa furaha kubwa.


Kama kawaida yake Profesa Kaganda alikuwa ni mtu mpekepeke asiyependa kujichanganya na watu akiwa kwenye starehe zake, alikuwa amejitenga kwenye meza ya kukaa watu wanne, wakiwa wapo wawili tu. Shebby moja kwa moja akaenda kuungana nao sasa wakawa watu watatu. "Good evening waungwana...!" alisalimia Shebby na kukaa kiti mkabala na mbaya wake. Wakaitikia salamu ile huku wanamkaribisha kwa bashasha kama ujuavyo ukarimu wa Watanzania wakikutana utasema ni ndugu wa familia moja kwa namna wanavyochangamkiana. Mhudumu akamfuata Shebby kwa ajili ya kumsikiliza mahitaji yake. "Niletee Wali kwa nyama ya nyati iliyopikwa chukuchuku tu kwa nyanya, kwa upande wa kinywaji niletee juisi yoyote ya matunda unayoipenda wewe ninywe! " aliagiza Shebby kwa mhudumu yule. Ambaye alitii maagizo ya mteja wake na kwenda kupeleka oda yake jikoni.

Break Point ni mkahawa ambao ulikuwa unasifika jijini Dar es Salaam kwa mapishi ya nyama za porini, kuanzia nyati, swala na nyinginezo. Hilo ndio jambo ambalo lilikuwa pia linamvutia Profesa Kaganda kula milo yake hapo. Alikuwa ni msomi ambaye hana mke nyumbani kwake anaishi kinembanemba tu. Alishawahi kuwa na mke wa Kijerumani aliyewahi kuzaa nae watoto wawili wa kiume akiwa masomoni nchini Ujerumani. Kilichotokea baina yao mpaka ndoa hiyo kuvunjika ni siri yao na Manani, lakini kwa muda mrefu watu wanaomjua hawajahi kumuona mkewe wala watoto wake. Alikuwa ni mtu wa kula bata kwa kwenda mbele hana majukumu yoyote ya kifamilia zaidi ya kujihudumia yeye mwenyewe tu.


Alipoletewa chakula chake akawa Shebby anakishambulia kwa pupa chakula kile kitamu hasa ukichukulia alikuwa na njaa kali. Kipindi chote wapo watatu kwenye meza walikuwa wanabadilishana mazungumzo mbalimbali ya mambo yanayoendelea nchini Tanzania kuanzia siasa mpaka kwenye burudani. Huku Shebby akitafuta nafasi ya kumfanyia tukio alilolikusudia Profesa Kaganda. Fursa adhimu aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ikawadia, yule mwenzao kwenye ile meza akawaaga, akanyanyuka zake kuondoka. Mezani wakabaki wawili tu, Profesa Kaganda na Shebby, mahasimu wawili wasiopikika chungu kimoja, utamu zaidi ukichagizwa kwa mmoja kumtambua mwenzake wakati mwingine hamjui mwenzake.

Laiti Profesa Kaganda angefahamu kuwa mbele yupo wakala wa Ziraeli malaika mtoa roho za waja, Wallahi angetimua mbio zile za Kibanga ampiga mkoloni. Lakini ajuaye ya ghaibu ni Rabana, mlango wa funguo za siri anazo yeye tu hajamuwakilisha yoyote.


"Waitress...Weeeeh...Waitressssss.....kuja hapa ongeza bia moja ya mwisho hapa kisha ulete bili yangu, nikalale zangu mieee...." alimuita mhudumu Profesa Kaganda huku akiwa ndio amemaliza msitu wa bia zilizotapakaa mezani pale. Alipoagiza tu kabla hajaletewa akanyanyuka kuelekea msalani kujisaidia. Hapo hapo Shebby kachomoa kutoka kwenye mfuko wake wa dangirizi dawa yake ya macho na kuiminyia matone kama manne tu kwenye glasi ile aliyokuwa anaitumia kunywea pombe zake Profesa Kaganda.


"Usifungue kwanza hiyo bia yake msubiri kwanza arudi, maana kaka yangu huyu akilewa ana matata sana yaani" alizungumza Shebby baada ya mhudumu Kuja kwa ghafla na bia aliyoagizwa na kutaka kuifungua. Hali iliyopelekea Shebby aidondoshe ile dawa yake chini kwa uoga kwa malengo ya kuwa ataiokota mhudumu akiondoka zake. Akamdanganya pia mhudumu kama yule Profesa ni kaka yake wa damu ili kuwafanya wahudumu wa pale waamini kuwa ni wamoja. "Yaani....kumbe hata nyie wanandugu mnamjua vizuri eeeh huyu Profesa akiwa hajautwika mtindi ni mtu mzuri sana, hariri hanaga shida na mtu lakini shida yake akilewa tu mhhhhhh...fujo tupu mtindo mmoja mara anapapasa papasa wahudumu miili yao kimahaba utasema kaingia balehe juzi juzi" aliongea mhudumu yule akionyesha kuchoshwa na tabia chafu za Profesa Kaganda.


Huo ndio unyanyasaji wa kijinsia mashuhuri sana kwa wahudumu wa baa na mikahawani wanaofanyiwa na wateja wao pindi wakilewa lakini hamna wa kuwapazia sauti kutokana na unyanyasaji huo wa mashambulio ya aibu. Kwanza wakipaza sauti zao watafukuzwa kazi mara moja na wamiliki wa maeneo wanayofanyia kazi kwa kisingizio cha kuwa mteja ni mfalme hivyo umridhishe chochote akitakacho. Tegemeo lao pekee la kutetea haki zao lilibakia kwa ' CHODAWU' Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Mahotelini, Majumbani na Huduma za Jamii, lakini wapi chama hicho kilikuwa kwenye usingizi mzito wa pono, si hayati si mamati wapo wapo siku zinasonga.


"Safi sana kwa kunisubiria, mteja ni mfalme maana usalama siku hizi ni mdogo wewe binti lazima nishuhudie unavyofungua" alizungumza Profesa Kaganda baada ya kutua pale mezani na kumuona mhudumu amesimama na bia yake anamsubiria yeye. "Kweli Bwana broo...siku hizi dunia inakaribia machweo kabisa kila aina za uhalifu unaovuma zama hizi" alijifaragua Shebby huku moyoni akijua tayari kashamuingia mkenge Profesa Kaganda. Akafunguliwa bia ile Profesa kisha kwa heshima na taadhima dada yule akaimimina bia ile kwenye glasi iliyofanyiwa mambo mambo na Shebby. Bila kuchelewa ilipojazwa tu kinywaji kile, Profesa akainyanyua juu kwa juu huku anaanza kuigiza kwa mtindo wa tarumbeta bila kupumzika, kisha alipoitua chini ilikuwa ipo tupu.


Alipoishika bia yake ili ajimiminie tena kwa mara ingine akawa kama mtu mwenye kizunguzungu anasitasita. "Profesa nini tena..?" Shebby alijishebedua kumuuuliza wakati anajua tayari Altazine imeshafanya vitu vyake mwilini. "Naa...ji... si..ki... a dizz....ne...ssss, ni...pe.....leke...... kwe...nye ga...riiii..." alizungumza kwa shida sana akiwa analalamika kuhisi kizunguzungu.


Shebby ndio fursa aliyokuwa anaitaka hiyo akaanza kumnyanyua kwa kutumia mabega yake anamburuta anamtoa nje ya mkahawa ule. Hamna aliyejali sana tukio hilo walijua tu ni mlevi aliyezidiwa na kileo anasaidiwa kupelekwa nyumbani kwake na ndugu yake au msamaria mwema. Ikawa ndio mwisho wa Profesa Kaganda kuonekana kwenye uso wa dunia hii.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Asantee,me nakupenda burew
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 18
️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ofisi za Bwana Mathew Kilanga, Mkuu wa kitengo cha siri cha usalama wa nchi, zilikuwa zipo katika jengo la "Benjamin William Mkapa Pension Tower" roshani ya tano katika mtaa wa Azikwe. Zamani jengo hili lilikuwa linajulikana kama "Mafuta house". Ilikuwa ni ofisi ya wastani isiyo na mbwembwe nyingi, huku akisaidiwa na katibu muhtasi wake mwanamke makini na mwerevu "Kokunawa Rweikiza" mhaya mzaliwa wa Bukoba vijijini.

Alikuwa mwanamke kidosho haswa lakini anayejitambua vilivyo, hivyo hakupata tabu kufanya kazi na Bosi Mathew Kilanga. Tofauti na makatibu muhtasi hawa wa kizazi kipya utakuta anamhudumia mteja huku anapaka rangi ya mdomo, mara anachati na simu yake kwenye mitandao ya kijamii huku wateja wanamsubiria, ili mradi tafrani tupu. Waliowahi kufanya nae kazi kigogo huyu wa ushushu wengi walishindwa kuendana na kasi yake katika utendaji wake wa kazi. Lakini Koku yeye akawa anamjulia haswa bwana Mathew, mpaka sasa akawa amedumu nae kwa muda wa miaka isiyopungua kumi mfululizo bila kuharibu kazi yoyote anayoagizwa kutekeleza, wala kupewa barua ya onyo kazini la kuharibu kazi.


Kokunawa wiki yote iliyopita tokea alipouliwa mfanyabiashara Pateli kinyama alikuwa akiingia ofisini asubuhi saa 1:30 muda wa kurudi nyumbani haujulikani, siku akiwa sana saa 4:00 usiku, lakini kutoka saa 6:00 usiku ilikuwa ndio kawaida. Alikuwa na kazi ya kupokea barua pepe za taaarifa za kiintelijinsia kutoka ofisi ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam kisha kuzipeleka kwa mkuu wake wa kazi kwa utekelezaji. Taarifa hizo za kiintelijinsia alikuwa anazidurufu na kuzipeleka kwa Bosi wake Bwana Mathew Kilanga azipitie na kama kuna zinazohitajika kujibiwa zijibiwe kwa haraka ili mradi suala la Bwana Pateli kuuliwa na watu wasiojulikana ilikuwa ni dosari kubwa kwa vyombo vya usalama. Kwa ufupi ni kwamba Koku alikuwa anakesha mfano wa nesi wa zamu anavyokesha na wagonjwa wake.


Mida ya saa saa 4:30 usiku Kachero Manu Yosepu alikuwa ndio kwanza anapanda ngazi kuelekea sakafu ya tano ofisini kwa bosi wake. Kachero Manu Yosepu alikuwa hapendi kutumia "Lift" anapopanda ngazi za jengo la ghorofa. Huo ulikuwa ni utamaduni wake na huwezi kumbadilisha. Ilikuwa ni moja ya mazoezi yake ya kuimarisha misuli ya miguu katika upandaji wa ngazi. Bwana Mathew Kilanga alishaanza kuulizia kwa sekretari wake kama Kachero Manu kasharipoti kazini usiku huo au bado. Uzuri wake kutoka anapoishi Kachero Manu na ofisini kwao ni mwendo wa robo saa tu kwa kutembea. Ilipofika saa 4:36 usiku Kachero Manu akagonga mlango wa ofisi kwao kuelekea kwa mkuu wake wa kazi kisha akanyonga kitasa bila kusubiri kukaribishwa akapokewa na tabasamu mwanana la sekretari wa bosi, Kokunawa. Habari za usiku dada "Koku", Mkesha wa watu wasiojulikana unaendeleaje? alitania kachero Manu kumtania Kokunawa kawa kawaida yao. "Habari za usiku ni mbaya , hongera zako unaetoka usingizini, mimi na bosi wako tuko kazini toka asubuhi saa 1:30, ila kupenda kwako usingizi kutakuotesha kitambi shauri yako ushindwe kazi zote mbili za nyumbani kwa wifi na za ofisini zinazokupa mkate wako wa siku, ooh wewe haya tu" wakacheka wote kwa pamoja kicheko cha nguvu kwa mapigo ya utani wa Koku.

Ghafla simu ya mezani ya sekretari Kokunawa ikaita tena, ilikuwa inapigwa toka kwa bosi akiulizia kama kachero Manu kasharipoti ofisini, akajibiwa ndio ameingia hivi sasa. Alivyokata simu tu, Kokunawa akamwambia Kachero Manu "fanya haraka bosi anasema hana muda wa kupoteza, amekuwa mkali kama pilipili na sauti yake inaonyesha kashaanza kukasirika, si unamjua bosi wako kama kazaliwa na kazi vile utasema Tanzania ya baba yake mzazi". "Sawa ngoja nimuone haraka, tutaonana nikitoka nataka nikupeleke kula mlo wa usiku kwenye hoteli kubwa kubwa binti mrembo upumzike kula senene kila siku" akajibu Kachero Manu huku akitokomea kwenye veranda ya kuelekea kwenye mlango wa ofisi ya bosi wake, akimuacha sekretari Kokunawa yupo hoi kwa kicheko hana mbavu.


Alivyofika akagonga hodi na kufungua mlango moja kwa moja kisha akasalimia "Shikamoo Kiongozi, habari za usiku huu". Bosi wake alimkuta bado amesimama hajakaa kwenye kiti chake, akajibu salamu hiyo. "Habari za usiku ni mbaya sana, karibu kiti ukae" huku akimuashiria kwa mkono kiti cha kukaa. Ahsante sana akajibu kachero Manu, kisha akavuta kiti akakaa na akatoa kompyuta mpakato yake kutoka kwenye begi lake akaiwasha, kisha akaitafuta pragramu ya uandishi ya "mikrosofti wordi" tayari kwa kuandika vitu vya msingi kwenye majukumu ya kazi atakayopewa. Kikapita kimya cha kama dakika moja, bosi akakohoa kikohozi kikavu, kisha nae akaja kuvuta kiti chake akakaa. Akachukua chupa yake ya kahawa akamimina kikombe kimoja kikubwa akaifunga, kisha akapiga mafunda matatu mfululuzo huku amefumba macho yake mithili ya mnywaji pombe haramu ya "Gongo", kuonyesha uchungu wa kahawa hiyo.


Halafu akaisogeza chupa pale alipoketi kachero Manu kumpa ishara kuwa anaruhusiwa kunywa kahawa akipenda, kisha akaanza kuongea huku anamkazia macho Kachero Manu. "Mtu asiyejulikana amefanya tukio baya tena, muda mfupi uliopita kamuua Profesa Kaganda mhadhiri nguli wa Chuo cha usimamizi wa fedha 'IFM'". akaweka kituo cha mazungumzo yake kisha akamimina tena kahawa kwenye kikombe akaendelea na mazungumzo yake. "Sasa agizo toka kwa wakubwa juu wamependekeza wewe ndio uhakikishe unakomesha mauaji haya ya hovyo hovyo yanayochafua taswira ya Tanzania kimataifa, nchi ambayo tunajulikana kama kisiwa cha amani.


Tunafahamu kuwa wewe ni Kachero maalumu wa matukio makubwa ya kimataifa, huwa hatukusumbui kwenye matukio ya kihalifu madogo madogo, lakini kwa hili tunaomba sana utusaidie. Maana wananchi wa zama hizi ni waelewa sio wajinga huwezi kuwadanganya kuwa tunafuatilia tu, lazima tuonyeshe juhudi za kweli kukabiliana na mauaji haya hobelahobela yasiyojulikana chanzo. Maana Tatizo la Watanzania kila tukio la hovyo kama hili watalinasibisha na siasa hata kama chanzo kikiwa ni kingine. Tunatambua kazi yako ya kutukuka kule Cabo-delgado, Msumbiji (Soma Riwaya CABO-DELGADO) ulivyowatia adabu vibaraka wa makaburu, pia kule Kigali ulipomshikisha adabu kahaba aliyetishia maisha ya viongozi wa serikali na wafanyabiashara (Soma Riwaya DILI LA COVID 19), na kazi zako lukuki za kuwaadabisha wahujumu wa amani na usalama wa nchi.

Sasa hauna muda wa kupoteza, ndani ya wiki moja tu mtuhumiwa awe amekufa nataka nione maiti yake au awe yupo hai namtaka nimuone anapandishwa kwenye karandinga la magereza Kuelekea Mahakamani ili haki itendeke. Ripoti kamili walipofikia polisi kwenye upelelezi wao wa tukio hili ipitie kwa katibu muhtasi dada yako Koku ameshakuandalia. Kwa kuanzia sasa hivi kwanza uelekee eneo la tukio kwenye mkahawa wa Break Point, Kinondoni upate penyenye zinazoweza kukusaidia katika upelelezi wako. Jeshi la polisi limenyoosha mikono juu, zigo umetwishwa wewe, kachape kazi" alimalizia maongezi yake mafupi Bwana Mathew Kilanga.

Wakaagana nae haraka haraka Kachero Manu akafanya hima kwenda kwa katibu muhtasi wao kuchukua nyaraka ili awahi eneo la tukio kabla ushahidi haujaharibika. Mbona mnuno kama wote, kama vile umenyweshwa uji wa shubiri kulikoni mwenzetu" katibu muhtasi Koku kama kawaida yake alimpiga kijembe Kachero Manu wakati alikuwa anajua fika kila kitu kilichosababisha aitwe ofsini Kachero Manu usiku huo.

" Acha utani Bibi kimeshanuka tayari huko, Babu yako kashanitibulia mapumziko yangu usijifanye hujui kitu, kasema nikabidhi kila kitu tena kwa haraka asije kunikuta hapa bado nipo ninasogoa kikazuka kisanga kipya" aliongea kiunyonge Kachero Manu kiunyonge mkubwa kuonyesha hajapendezwa na majukumu aliyopewa ila ndio kazi aliyoajiriwa nayo hana budi kutimiza wajibu wake.

Ilibaki kidogo tu apinge yeye kukabidhiwa jukumu hilo wakati wapo vijana wengi idarani wachanga ambao wangeweza kupewa jukumu hilo. Kwake yeye alijifananisha na nyundo inayotaka kuondosha uhai wa inzi, wakati kofi moja tu kungetosha. Ila aliposikia yeye kusimamia upelelezi huo ni agizo toka mamlaka za juu, akanywea akawa hana ujanja tena bali ni utekelezaji tu.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Mbio za sakafuni huishia ukingoni, hivyo janja janja yote ya Profesa Kaganda ya kuwanyanyasa kingono watoto wa walalahoi waliopata bahati ya mtende ya kusoma elimu ya chuo kikuu ikageuka kuwa ni historia. Alisahau kabisa msemo wa wahenga, yakuwa tamaa mbele mauti nyuma. Mabinti ambao walikuwa wanategemewa na familia zao zenye kipato cha kijungu meko, waje kuwakomboa kutoka kwenye lindi la umaskini, yeye Profesa badala ya kuwa daraja la kuwavusha kwenye mto wa ufukara, na kuwapeleka katika nchi ya maziwa na asali yeye akajigeuza kuwa mamba wa kuwatafuna vidosho hao mtoni bila huruma.

Majuto ni mjukuu, akawa sasa yupo ndani ya friza mochwari huko Muhimbili tayari kuandaliwa kupelekwa kuzikwa huko kwao Bukoba kwenye mashamba ya ndizi. Kachero Manu alitinga ndani ya muda muafaka huku akikuta bado maiti haijaondoshwa eneo la tukio. Maiti ya Profesa Kaganda ilikutwa imekatwa sehemu zake za siri, huku ikiwa imepigwa risasi eneo la moyo ipo ndani ya gari imelazwa. Aliyegundua maiti hiyo alikuwa ni mlinzi wa eneo hilo baada ya kuona wameingia watu wawili kwenye gari kisha akatoka mmoja tu tena kwa haraka na kutokomea zake kisha gari haiondoki. Alipokwenda kufanya taftishi kulikoni kwa kuchungulia kwenye kioo cha gari, ndio akakutana na kimbwanga hicho cha kushtusha.


Kwa kutumia vifaa vyake vya kazi Kachero Manu akiwa amevaa vikinga mikono yake, akachunguza anachokitaka kisha akapiga picha kadhaa anazotaka na kutoa maagizo kadhaa kwa wana usalama waliokuwa wanafuata muongozo wake kuhusiana na kwenda kuhifadhi mwili wa Profesa gwiji wa mambo ya takwimu. Mhudumu aliyewahudumia Profesa na Shebby kwenye meza yao akaitwa na kuhojiwa ili atoe maelezo nyoofu yanayoweza kusaidia upelelezi huo.


Kachero Manu: "Habari yako na pole na matatizo, ehee... unaitwa nani, na una umri gani? "
Mhudumu: " Nimeshapoa tayari, naitwa Angela Chama, mwezi Desemba mwaka huu natimiza miaka 26"(Alijibu huku anajifuta machozi kwa hanchifu yake nyeupe)
Kachero Manu: "Ehee..unafahamu nini kuhusu marehemu Profesa Kaganda maana wewe ndio mshukiwa namba moja, maana umemuhudumia mwanzo mwisho mpaka akazidiwa na kileo"
Mhudumu: " Mama weeeeh...kaka polisi muogope Mungu wako, mie ninahusikaje hapo jamani ?"(Alilala mhudumu Angela huku anaanza kububujikwa na machozi ya nguvu)
Kachero Manu: "Tuliza mzuka, nieleze sasa unachokijua kama kweli wewe sio mhusika! "(Kachero Manu alikuwa anatabasamu lengo lake limeshatimia la kumpanikisha Angela ili atapike kila kitu anachokijua)
Mhudumu: "Sawa!.Profesa alikuja hapa mkahawani kwetu kama kawaida yake majira ya kama moja usiku. Bahati nikawa mimi sina mteja wa kumhudumia nikamkaribisha kwenye meza iliyo tupu akakaa hapo nikaanza kumhudumia.


Baadae waliongezeka wateja wengine wawili wakakaa nae pamoja. Baadaye mmoja wao alijitambulisha kwangu kama ni ndugu yake na Profesa baada ya kutaka kufungua bia ya Profesa alipoenda msalani akanizuia. Baadae waliondoka pamoja akiwa anamkokota, Profesa akionekana amezidiwa na kileo. Hivyo ndivyo kwa ufupi ninavyofahamu tukio hilo"


Kachero Manu: " Je huyo aliyejitambulisha kama ndugu, umeshawahi kumuona hapa mkahawani katika siku za nyuma? "
Mhudumu: "Hapana kwakweli na alikuwa haonekani vizuri kwa sababu alivaa kofia kubwa ya pama na miwani usoni"
Kachero Manu: "Uliwahi kumtilia mashaka kama ni mtu muovu? "
Mhudumu: "Hata chembe sikumshuku,maana kipindi nataka kufungua kinywaji cha mwisho cha Profesa wakati hayupo mezani Profesa alinikataza kata kata kuwa nimsubirie kwanza Profesa arudi msalani ndio nifungue kwa kuhofia masuala ya kiusalama. Pia kwa jinsi walivyokuwa wanaongea wawili hao kwa bashasha ni kama vile wanafahamiana sana"
Kachero Manu: "Je imeshawahi kutokea siku za nyuma Profesa kuzidiwa na kinywaji mpaka kubebwa?"
Mhudumu :" Sijawahi kushuhudia nikiwepo zamu kumuona amezidiwa labda kwa siku ambazo sipo kazini! "
Kachero Manu: "Sasa kwanini hukutilia mashaka kuwa kama kuna jambo baya limemkumba?".
Mhudumu: "Aaaah..mmhhhh..(Kijasho chembamba kikawa kinamvuja mhudumu yule hana cha kujibu)
Kachero Manu: "Au hujaelewa swali, nirudie tena kuuliza? "(Alitilia msisitizo huku akimkazia machoni kuonyesha yupo kazini hatanii)
Mhudumu: "Nimeelewa swali, siwezi kumjibia marehemu kwa sababu siku hazifanani, huenda alianza kupata moja moto moja baridi viwanja vingine hapa akaja kusuuzia tu. Hiyo inatokeaga tu mara nyingi kwa walevi hata wale nguli"( Alijibu kiumakini yule dada mhudumu).
Kachero Manu: "Ahsante kwa ushirikiano wako, sitosita kukutafuta tena kwa mahojiano zaidi ikibidi kufanya hivyo. Ila kanionyeshe meza waliyokuwa wamekaa na nadhani mlipewa maagizo msiondoshe kitu chochote mezani hapo! "
Mhudumu: "Tulipokea maagizo hayo na tumeyafanyia kazi, hakuna kilichoondolewa eneo la tukio" alijibu mhudumu yule kwa kujiamini akiwa sasa uoga wote umemuisha, huku akinyanyuka kuelekea kwenye meza waliyokuwa wameketi Profesa Kaganda na Shebby.


Walipofika hapo kwenye meza, Kachero Manu akakagua vilivyo meza hiyo na mabaki yaliyobaki ya pombe ya Profesa Kaganda yale ya kwenye chupa na kwenye glasi. Akaamrisha iende kupimwa kwenye ofisi ya mkemia mkuu. Kabla hajaondoka pale mezani akaona dawa ya kutibu ugonjwa wa macho chini ya meza, ambayo iliyofunguliwa kuonyesha kuwa imetumika tayari ikiwa imetelekezwa eneo la tukio. Kwa Kachero makini kila kitu chochote eneo la tukio ni msaada mkubwa kukufikisha kwenye uchunguzi sahihi. Kachero Manu akatabasamu kisha akavaa vikinga mikono yake na kuiokota dawa hiyo na kuifadhi kwenye vyombo vyake maalumu. Baada ya hapo akawa ameshamaliza taftishi yake aliyoikusudia, huku muda ukiwa umeyoyoma, saa ikisoma saa 7:15 usiku.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
Hii nayo mwanzo ,mwisho.Hakuna arosto?
Itaisha Inshallah sipo kibiashara nipo kiburudani zaidi, hizi ngoma kwenye kabati zinafika hata 30 hata nikiamua kuchapa vitabu sina uwezo huo saa kuchapa zote,hivyo kuwa na amani tu
[emoji41][emoji41][emoji41]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 20
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Nilipozinduka nilisimuliwa na manesi wanaonihudumia kuwa niliokolewa na polisi wa doria mtaani waliopigiwa simu na wasamaria wema. Polisi hao walifanya juhudi kubwa ya kunichomoa kutoka kwenye mikono ya wananchi wenye hasira kali kwa kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya raia hao. Polisi wale wakanibeba mzobemzobe kwenye gari lao mpaka hospitali ya taifa ya Muhimbili. Nilizindukia hospitalini Muhimbili nikiwa nimetundukiwa dripu za damu. Niliambiwa nilizimia kwa zaidi ya masaa 7, na nilipoteza damu nyingi sana. Shukrani za pekee kwa madaktari wa hospitali ya taifa Muhimbili, kwa juhudi zao za kuokoa uhai wangu vinginevyo ningekuwa marehemu tayari. Mkono mmoja wa kushoto nilikuwa nimefungwa pingu iliyounganishwa na kitanda cha chuma, kuashiria nje ya wodi kuna askari maalumu anayechunga usalama wangu. Kila nilipokuwa nafikiria tukio zima, nikilikumbuka machozi yalikuwa yananibubujika kama maji bila kikomo. Nikakubali matokeo kuwa mkubwa ni jaa, hivyo sina budi kupokea misukosuko toka kwa Maulana kwa moyo mkunjufu, huku nikiamini Mungu pekee ndio atakayenitakatisha kutoka kwenye tuhuma hizo chafu walizonibambikizia, zisizo na kichwa wala miguu. Mwili wangu ulikuwa umepambwa na mishono ya nyuzi za madaktari katika harakati zao za kudhibiti upotevu wa damu mwilini mwangu. Sindano ya ganzi ilipoisha nguvu yake, maumivu ya mwilini mwangu yalikuwa makali hayaeleweki utasema kuna mtu amechukua kisu kikali cha buchani ananicharanga nacho mwilini. Njaa ilikuwa kali lakini hamna wa kuniandalia chakula zaidi ya uji wa hospitalini niliyoletewa na nesi wangu muuguzi. Hakuna ndugu wala jamaa aliyejitokeza pale hospitalini labda kutokana na ukosefu wa taarifa za tukio baya lililonikumba. Baadhi ya manesi na madaktari walianza kuninyanyapaa na kuniangalia kwa sura ya mabezo baada ya kupata taarifa kuwa nimechezea kipigo kutokana na jaribio la ubakaji kwa mwanafunzi. Nikamshukuru Mungu wamechelewa kujua mpaka wamenipa huduma zote stahiki vinginevyo wangenitelekeza mapokezi mpaka ningefariki. Wananchi walikuwa tayari wameshanihukumu kwenye mahakama zao za mtaani kuwa mimi ni mbakaji nimestahiki malipo ya uovu wangu. Maneno ya ahlan wa sahalan ya binti yule mwanafunzi kuwa nimembaka tayari yalishaniletea ngondo na wanajamii. Wanajamii ambao walionekana wamechoshwa haswa na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto wadogo vinavyofanywa na watu wazima, bila kuchukuliwa adhabu stahiki na vyombo vya dola. Kila raia mwema aliyepata taarifa ya kutaka kubaka, waliniona mimi ni mlanisi wa chusu, kifo kilikuwa halali yangu. Tayari wana habari wa mtaani walishasambaza habari zangu kwenye mitandao ya kijamii yote kuwa Mchumba wa Miss Tanzania, Zabibu ameshushiwa kipigo kwa kutaka Kubaka mwanafunzi maeneo ya Makongo. Lengo la Naibu Waziri Mkuu Dr.Sanko la kunichafua heshima na hadhi yangu katika jamii kulitumia, ili tu kumfanya mpenzi wangu Zabibu akasirike kisha animwage na yeye apate upenyo wa kumtwaa jumla jumla Zabibu. Kwenye mitandao ya kijamii huko watu walikuwa wananiona mkia wa mbuzi tu, sina thamani hata chembe. Kisanga changu kilipomfikia Zabibu huko ughaibuni kwenye mashindano, moyo wake ulimpasuka haswa. Dunia ya sasa ni kama kijiji kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, hivyo ndani ya muda mfupi taarifa zikamfikia kupitia mtandao wa kijamii wa 'Instagram' na makundi ya 'Whatsapp'. Taarifa ambazo zlimfedhehesha na kumhuzunisha vilivyo huku akiwa haamini kama kweli Shebby anayemjua yeye anaweza kufanya tukio kama hilo la aibu. Taarifa ambayo ilisababisha maandalizi ya Zeddy kwa ajili ya mashindano hayo yadorole vilivyo, na siku ya fainali hizo za Miss World alifanya vibaya sana kwa kushika mkia kwa warembo wa dunia nzima. Aliporejea tu nchini Tanzania akanikuta tayari nipo rumande gerezani nimeshapandishwa kizimbani zaidi ya mara mbili. Akafanya hima hima pa mtima pamoyo kuja kunitembelea gerezani, huku nikimuapia haki tena kuwa sina hatia, waja wananipakazia. Familia yangu walishapata taarifa za kisanga changu wakawa wananjitahidi kuniletea chakula asubuhi, mchana na usiku kule gerezani huku mama yangu mzazi akiwa hajiwezi kwa kilio kila nilipokuwa ananiona siku nikipandishwa mahakamani. Namshukuru Zeddy kwa kuamua kuweka ushabiki wa mashoga zake na mihemko pembeni akawa ananiunga mkono, yupo na mimi bega kwa bega bila kujali wala habali. Huku kwa gharama zake mwenyewe akaniwekea wakili nguli kwenye hii kesi yangu ili mradi haki iweze kutendeka kwa upande wangu. Nilipopandishwa mahakamani mara ya tatu huku upande wa mashitaka wakiwa ndio wanajiandaa kuanza kutoa ushahidi wao huku yule binti mwanafunzi niliyesingiziwa kumbaka akiwa ameambatana na mama yake mzazi na baadhi ya wanafamilia wake wakiwa wameshatinga mahakamani tayari kwa kuanza kutoa ushahidi, kwa bahati hakimu mkazi aliyepangiwa kesi yangu siku hiyo alikuwa na dharura hivyo kesi yangu ikapangiwa siku nyingine. Wakati nimeshapandishwa karandinga la magereza narudishwa rumande ndipo Zabibu akakutana pale katika uwanja wa mahakama na Shangazi yake toka nitoke na baba yake mzazi akiwepo pale mahakamani. "Khaaaaaa...Shangazi Mwanabure Shikamoo, umekuja lini toka Tanga na mbona upo hapa mahakamani kulikoni? " lilikuwa ni swali la Zeddy kwa shangazi yake baada ya kustaajabishwa na uwepo wake pale mahakamani bila kutegemea. Walikuwa hawajaonana kitambo kirefu sana. "Aaah..Marahaba siamini mpwangu Zabibu upo! hata salamu tu kweli nyie mkija mjini mnatutupa, chambilecho asiyekuwepo machoni na moyoni hayupo, hivi hata binamu yako Zawadi unajua kama yupo hapa Jijini lakini? alijibu salamu yule shangazi mtu huku anatoa lawama kedekede kwa Zabibu kwa kuacha kuwasalimia ndugu zake wa damu tokea ahamie jijini Dar es Salaam. "Nisamehe Shangazi, muungwana akivuliwa nguo huchutama, nitajirekebisha. Masomo yalinizidia ila sasa nimemaliza chuo sina tena kisingizio nitawatafuta ndugu zangu wote niwafahamu vilivyo" alijitetea Zabibu kwa kujifaragua huku moyoni akijua kabisa ni kosa kubwa amefanya la kutotaka kuwatafuta nduguze wa kutoka kijijini kwao Mzundu huko Handeni, Tanga. "Nimekuja mpwangu mambo ya aibu tupu, huyu binamu yako huyu mwanangu Zawadi kashakuwa gubegube na tapeli huku mjini, hana kazi wala bazi yupo yupo tu. Kasingizia kijana wa watu kuwa mwanawe kabakwa na mwanawe ni mwanafunzi wakati hasomi hata darasa moja, hapiki hapakui shule ilimshinda yule mjukuu wangu toka akiwa darasa la nne kule kijijini. Sasa anafuata nyayo za mama yake mzazi dhahiri shahiri bila mficho. Leo wana bahati hakimu hajafika mahakamani nilipanga kuwaumbua hadharani maana hawanisikilizi ninachowaambia, wanajitafutia laana zisizo na sababu zozote sijui kawakosea nini kijana wa watu masikini" Shangazi Mwanabure, shangazi yake Zawadi ambaye alikuwa anasifika kwa UchajiMungu wake alikuwa analalamika kwa huzuni kutokana na usanii wa binti na mjukuu wake. Taarifa hiyo ya shangazi mtu ilifufua matumaini mapya katika moyo wa Zabibu na kuanza kupata mwangaza wa kulimaliza suala hilo la mchumba wake Shebby nje ya mahakama. "Huyo wanayemsingizia ubakaji ndio mchumba wangu niliyeahidi kwa baba kuwa ataleta barua ndio maana na mimi nipo hapa mahakamani" alijiongelesha Zabibu kwa shangazi yake huku akisubiria mapokeo yake. "Mtume Muhammadi weeeeeeeh....unaona ngondo hii sasa wanaotaka kuisababisha hawa mabaradhuli, wananifanya nionekane sikuwatolea adhana masikio mwao walipozaliwa, hivi leo kaka yangu, baba yako mzazi Bwana Shamsi na matata yake yale asikie mwanangu Zawadi ndio kakufanyia vitimbi hivyo mie nitakuwa mgeni wa nani mimi!. Atavunja kabisa na udugu wenyewe mpaka kifo hatonisemeza" aliloloma Shangazi yake Zabibu kwa huzuni huku akionyesha kabisa hatokubali tena kesi hii ya uzushi kuendelea mahakamani ili kulinda udugu baina yao. Wakaagana Shangazi mtu na Zabibu wakipeana ahadi za kutembeleana ili kuyamaliza kiukoo, huku mtoto aliyesingizia kubakwa na mama yake wakiwa wameshaondoka viwanja vya mahakamani kitambo kirefu. Tokea siku hiyo mtoto huyo alijisingizia kubakwa na mama yake mzazi hawakukanyaga tena mahakamani, kesi ikawa inatajwa kwa muda wa miezi sita bila mashahidi upande wa washtaki kung'aza pua zao mahakamani. Ndipo hakimu akafanya maamuzi sahihi ya kuniachia huru, huku nikiwa nimeteseka gerezani miezi sita bila hatia. Shebby alikuwa amezama kwenda lindi la bahari ya fikra akikumbukia taabu na mateso aliyoyapata yaliyosababishwa na Naibu Waziri Mkuu Dr. Sonko, ambaye ndio alitengeneza tuhuma hizo feki ili mradi tu nipotelee gerezani kimoja aweze kumfaidi Zabibu bila ushindani. "Naapa kiapo cha Yasin Mkubwa! Dr.Sonko nitakuua hata kama unalindwa na mkururu wa walinzi ambao ni makomandoo kuanzia nyumbani kwako mpaka mitaani unapotembea, kifo kwako ni lazima nitakuua hayawani mkubwa wewe" Shebby alikuwa yupo nyumbani peke usiku huo anajiwekea nadhiri ya kuitekeleza kwa Dr.Sonko kwa sauti ya juu. Mara kengele maalumu aliyoiweka kwa kuitegesha, ya kumkumbusha muda sahihi bila kupitiliza wa kunywa dawa zake za UKIMWI, ARV ikawa inalia. Akanyanyuka haraka kwenye sofa na kwenda kwenye kabati lake la kuhifadhia dawa akachukua tembe zake anazohitaji kisha akamimina maji kwenye glasi na kuzibugia kisha akazima taa ya sebuleni na kuelekea chumbani kwake kulala tayari ilishakuwa usiku wa saa 4:00.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 21
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Kachero Manu kichwa kilikuwa kinambangua hajui namna ya kumtia mbaroni Shebby na siku alizopewa na Bosi wake, zilikuwa zinayoyoma bila matumaini yoyote ya kumtia mkononi. Alishaanza kuona dalili za maji kuzidi unga katika jukumu zima la kumkata muuaji huyo. Maagizo ya Bosi wake Bwana Mathew Kilanga yalikuwa wazi, yakuwa anampa juma moja tu amlete mhalifu anayesakwa akiwa hai au mfu. Alikuwa anamjua fika Bwana Kilanga asipopata suluhu ndani ya wiki moja aliyoitoa, hana simile lazima ataomba msaada wa makachero wa Ughaibuni ili kutetea kitumbua chake kisitiwe mchanga na wakubwa zake.

Katika kitu alikuwa anaona aibu na fedheha Kachero Manu, ni kitendo cha kuitwa makachero wa nje ya nchi kama "Federal Bureau of Investigation" (FBI) ya Marekani kuja kufanya uchunguzi Tanzania. Makachero ambao baadhi yao wamesoma vyuo vinavyofanana wakati wa mafunzo yao ya ujasusi na Kachero Manu, tofauti ni nchi tu wanazozitumikia na matumizi ya teknolojia. Jukumu alilopewa alilichukulia poa sana kumbe lilikuwa ni zito kiaina yake.

Majibu toka ofisi ya Mkemia mkuu wa serikali aliyokuwa akiyasubiria kwa hamu kubwa yalithibitisha pasina kuacha mashaka kama alivyohisi mwanzoni kuwa kinywaji cha Profesa Kaganda kilinyunyiziwa dawa ya kutibu macho yenye kiambata hatari cha 'nafazoline'. Hivyo mshukiwa namba moja wa mauaji ya Profesa Kaganda ni mtu aliyekaa nae jirani pale Mkahawani, Break Point. Mtuhumiwa ambaye kwa simulizi za mashuhuda waliomuona ni mtu mrefu, mwenye jumbile la kimazoezi, amevalia kofia ya aina ya pama na miwani ya giza.

Kachero Manu akawa anapimisha katika idadi ya Watanzania zaidi ya milioni 55 kumtafuta mtu mmoja tu usiyemfahamu kimahesabu kumpata kwake bahati nasibu.Ni sawa na kuutafuta mguu wa sisimizi uliokorogewa ndani ya sufuria ya madikodiko. Mbaya zaidi licha ya kazi hii ya kumsaka Shebby, muuaji asiyejulikana lakini bado aliendelea na majukumu yake ya msingi ya kila siku ya kuhakikisha ulinzi na usalama wa viongozi wakuu wote wa nchi, kuanzia Rais, Mawaziri mpaka Wabunge kuwa wapo salama. Majukumu ambayo daima yalimfanya awe mtu wa kutaratamba huku na kule kama jibwa koko lisilo na makazi maalumu. Tena kipindi cha sintofahamu ya mauaji ya shaghalabagala ya watu mahashumu katika jamii, umakini ndio ulikuwa unahitajika zaidi katika kuimarisha ulinzi wa viongozi wa kitaifa.

Uzembe wowote katika ulinzi wa viongozi ungepelekea Kachero Manu kuwajibishwa na viongozi wake. Hivyo kila siku asubuhi alikuwa na jukumu la kupokea taarifa za vijana wake za kufahamu kiongozi gani wa kitaifa yupo eneo gani na nani yupo eneo hilo kuchunga usalama wa kiongozi huyo. Siku hiyo ya Jumamosi akapokea taarifa kuwa viongozi wengi wa kitaifa wapo majumbani wametulizana kasoro Naibu Katibu Mkuu pekee Dr.Sonko ndio alikuwa anatakiwa kuwepo ukumbi wa 'Nkurumah Hall', Chuo Kikuu cha Dar es Salam kufungua kongamano la wiki moja la wanachuo wajasiriamali.


Ulinzi wa Naibu Waziri Mkuu Dr.Sonko wenyewe watu wa usalama walijua ulikuwa ni mgumu sana hasa kutokana na kujichanganya sana na jamii kutokana na kuendekeza mambo ya vijana. Cheo chake kilikuwa ni kipya katika muundo wa vyeo serikalini, hivyo alikuwa anataka kuionyesha jamii kuwa cheo chake ni muhimu sana ndio maana kimeanzisha. Kachero Manu akaona tu moyo wake unamtuma aende tu huko 'Nkurumah Hall' kuongeza nguvu ya ulinzi ww kiongozi huyo pia kuhudhuria mkutano wowote wa Nkrumah ilikuwa ni burudani. Hasa akikumbukia mijadala ya 'Nkurumah Hall' huwa inakuwa ya hoja za kisomi zaidi ukienda lazima kichwani urudi na chakula ya kunawirisha ubongo. Wanasiasa wengi wale wa maneno ya lolololo wasioweza kujenga hoja na kuzitetea, Nkrumah hall walikuwa wanapaogopa kama kituo cha polisi.

Kumbe moyo wake ulikuwa unampelekea kwenda kuonana na muuaji wake anayemsaka kwa udi na uvumba, Shebby. Shebby alikuwa anazo ratiba zote za mizunguko ya adui yake pekee aliyebakia kumuadabisha Dr.Sonko. Penyenye za misafara yake alikuwa anapewa na waandishi wa habari wanaozunguka kwenye misafara yake Dr.Sonko.

Mipango ya Shebby ilikuwa ni kumfanyia tukio mbaya wake siku ya tarehe 5/07 ambapo Dr.Sonko amepangiwa kufanya ziara katika maadhimisho ya sherehe za Sabasaba Jijini Dar es Salaam. Hiyo ndio alipanga iwe siku ya kufanya tukio huku wakigawana majengo ya serikali na Dr.Sonko, yeye akielekea gerezani huku Dr Sonko akielekea mochwari akiwa maiti.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Kadamnasi ya vijana wa Vyuo vikuu mbalimbali nchini Tanzania walikuwa wamejazana katika ukumbi mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unaoitwa Nkrumah Hall. Ukumbi huo pia serikali ya Tanzania ilikuwa imeutangaza kama moja ya urithi wa taifa tokea mwaka 2015. Ukumbi huo ulipewa jina hiyo kwa heshima ya rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah. Ghana ilikuwa nchi ya kwanza ya watu weusi kupata Uhuru wake barani Afrika. Ilijipata Uhuru mwaka 1957 kutoka mikononi mwa wakoloni wa Uingereza.

Miongoni mwa mambo ya kukumbuka kutoka kwa Kwe Nkrumah ilikuwa ni ndoto yake ya kuliona bara Afrika linakuwa taifa kimoja kiutawala 'UNITED STATES OF AFRICA', kama ilivyo Marekani. Ndoto ambayo mpaka leo hii bado haijafanikiwa kutimizwa.

Wanachuo walikuwa wanapokuja kwenye mijadala inayofanyikia kwenye ukumbi huo, wanajiandaa kwelikweli kwa hoja zenye mashiko. Kijana mmoja mrefu, mweusi, mtanashati aliyevalia kaunda suti ya rangi ya kahawia na pama lake la rangi ya kijivu na miwani nyeusi ya giza alikuwa ni miongoni, na viatu vyake vyeusi alikuwa ni mmoja wa waliohudhuria.

Huyu hakuwa mwingine bali ni Shabani Zomboko au ukipenda muite Shebby alikuja kuonana na mbaya wake Naibu Waziri Mkuu, Dr.Sonko. Kachero Manu nae alikuwepo ukumbini hapo kusimamia vijana wake wanaolinda viongozi wa kitaifa kama wanayapeleka mambo ya kiulinzi kwa kuzingatia itifaki sahihi. Punde si punde Dr.Sonko akiambatana na maofisa wake muhimu wakawasili ukumbini pale tayari kwa kuanza kwa harakati za ufunguzi wa kongamano lile. Kachero Manu alikuwa kule mbele ya jukwaa anawaangalia wale waliohudhuria kongamano lile. Macho yake yakavutika tu bila kupenda na muonekano wa Shebby. Akakumbukia maelezo ya mhudumu na mlinzi wa mkahawa wa Break Point kuwa mhalifu wanayemhisi alivalia pama na miwani nyeusi.

Kachero Manu akajikuta anavutiwa kuanza kumchora Shebby kama anacheza tu vile. Akatoa penseli yake ya karatasi kwenye mkoba wake mdogo na kuanza kumtazama Shebby kisha anamchora umbile lake. Kazi ambayo ilimchukua dakika 10 tu kukamilisha uchoraji ule. Laiti ungefanikiwa kuiona picha hiyo ya kuchora ya Shebby ungesema sio ya kuchora bali ni ya kupiga kwa jinsi ilivyochorwa kwa umahiri mkubwa na Kachero Manu. Aliweza kumchora vizuri zaidi kutokana na Shebby kukaa mbele mbele kutoka pale zilizo mbele ya meza za wageni rasmi. Kilichomzidi kumtia mashaka zaidi Kachero Manu ni muonekano wa Shebby ulionyesha kabisa hayupo pale mkutanoni.

Alionekana ni mtu mwenye mawazo mengi sana kichwani mwake, jambo ambalo Kachero Manu lilizidi kumpa mashaka. Ukafika wakati wa mgeni rasmi, Mheshimiwa Dr.Sonko kufungua kongamano hilo.
Waheshimiwa Mawaziri, Wabunge na Viongozi wote wa kitaifa, Mabibi na Mabwana mliohudhuria itifaki imezingatiwa. Nakukaribisheni kwenye kongamano hili la kubuni na kujadili mikakati ya kuwawezesha vijana wetu wa Vyuo Vikuu kuanzisha shughuli za kijasiriamali.

Pamoja na kwamba tatizo la ukosefu wa ajira linawalenga watu wote katika nyanja mbalimbali lakini Kipindi hiki tunawalenga zaidi vijana. Takwimu zinaonyesha kuwa wao ni zaidi ya asilimia 60% ya idadi ya watu wote nchini Tanzania. Tatizo la ajira bado ni kama bomu linalosubiriwa kulipuka wakati wowote, hivyo hapa leo tujadili fursa zilizopo nchini Tanzania zinazoweza kutumika kuondosha tatizo la ajira kwa vijana. Natoa ofa kwa wajasiriamali wanawake wa chuo kikuu chochote watakaojiunga kwenye kikundi wakaja na mawazo ya kibunifu ya kijasiriamali kila kikundi nitawapa milioni 20" alipomalizia hivyo shangwe na vigeregere vikalipuka ukumbini mule kufurahia ahadi ile ya Dr. Sonko.

Ahadi ile ya Dr.Sonko ilikuwa ni geresha tu, ulimbo wa kunasa vimwana wa Vyuo vikuu, sio kwamba kweli ana uchungu kwa vijana wasio na ajira. Wanaomfahamu wanajua alishapandisha bilisi wa ngono kwa kutaka kuwatega visura wa vyuo. Alijua watakapopewa ahadi ya milioni 20 lazima watachakarika kuhakikisha wanaunda vikundi vyao, hapo ndio atakapowanasa. Wakati mjadala katika kongamano lile unaendelea bambam, Shebby akawa amepotea katika mazingira ya kutatanisha katika upeo wa Kachero Manu.

Kachero Manu alimuona wakati ananyanyuka kitini pake, akajua anaelekea msalani atakuwa ni mwenye kurejea punde tu. Lakini dakika zilikuwa zinaenda harijojo haonekani kurejea ndani ya Nkrumah hall. Chapuchapu Kachero Manu kwa kuwatumia vijana wake akaomba apatiwe nyaraka za usajili wa wote waliohudhuria kwenye ukumbi ule. Ambapo usajili makini ulikuwa unafanyika kwa kutumia kitambulisho cha taifa. Kila aliyesajiliwa alielekezwa sehemu yake ya kukaa, hakukuwa na ruhusa ya kukaa borongoborongo kwa kadri unavyopenda wewe bila utaratibu.

Hivyo ilikuwa ni rahisi tu kujua pale alipokaa Shebby ni nani jina lake na anasoma kitivo na kozi gani. "Anaitwa Shabani Zomboko, kazaliwa 5/06/1989...ina maana ana miaka 30 lakini kaandikisha anasoma digrii ya utawala wa biashara 'Business Administration', yupo mwaka wa pili wa masomo katika Chuo kikuu cha Dodoma, kwa umri wake kusoma digrii ya kwanza kuna walakini labda ametokea kazini huenda..." alikuwa ni Kachero Manu anamtafakari na kumfanyia taftishi Shebby. Akaamua kwa njia za kidukuzi anazozijua yeye bila kutumia nywira ya chuo hicho aingie kwenye mtandao wa chuo hicho cha Dodoma ili ajithibitishie kama kweli mwanachuo mwenye jina la Shabani Zomboko amesajiliwa na chuo hiko." Khaaaah..!huyu ananipa mashaka aisee..hamna mwanachuo mwenye jina hilo aliyesajiliwa!" alijikuta anaropoka taratibu akiwa ukumbini mule wakati kongamano linaendelea mpaka akajishtukia huenda ametoa sauti kubwa iliyosikika na wengine.

Haraka haraka akakabidhi majukumu yake kwa mtu wa chini yake kicheo na kutoka nje ya ukumbi. Akawa anaangaza angaza huenda akaambulia kumuona Shebby nje ya ukumbi ule ili amkabili uso kwa uso, lakini alama za uwepo wake zilikuwa hazionekani, alikuwa tayari kashamuachia vumbi tupu. Kachero Manu akaelekea eneo la maegesho ya magari na kuwasha gari lake huku akiliondoa eneo lile kwa mchepuko wa kasi utasema kuna mtu anamfukuzia akitokomea eneo lile la Nkrumah Hall.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 22
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Leo ni Jumamosi, zimebaki siku tatu kabla ya maonyesho hayo ya Sabasaba, siwaelewi unajua..na pesa zote mlizohitaji nimelipia" alikuwa Shebby anafoka, amekasirika kama mbogo anaenda pumzi njia mbilimbili, anagongagonga meza mbele ya afisa biashara wa kampuni ya 'MZIZIMA CLEARING AND FORWARDING CO LTD' iliyopo mtaa wa Mkwepu maeneo ya Posta. Kampuni ambayo ilikuwa inajishughulisha na utoaji wa mizigo bandarini inayoagizwa na wateja wao toka ughaibuni. "Samahani sana kwa kukucheleweshwa mzigo wako hata sisi tunatumia, lakini ni tatizo lililo nje ya uwezo wetu, zama hizi sio kama zamani enzi hizo mizigo bandarini ilikuwa inatolewa borongoborongo, segemnege bila kufuata utaratibu lakini sasa ukaguzi ni mkali sana wanapitia vibali vyote kwa umakini kuhakikisha kodi zote za serikali zimelipwa kwa usahihi, ndipo mzigo unaruhusiwa kutoka bandarini. Hivyo nakuhakikishia mteja wangu mtukufu kesho Jumapili majira ya adhuhuri mzigo wako tutakuwa tunakukabidhi, ondoa mashaka kabisa, tuna uzoefu na hizi kazi kwa zaidi ya muongo mmoja" alijibu kwa heshima na taadhima afisa huyo anayefahamu nini maana ya huduma kwa mteja hivyo akawa anamtuliza mteja wake. "Lakini kesho ni Jumapili, kweli wanafanya kazi hizo mamlaka za uhakiki?" huku akiwa anaiweka vizuri kofia yake ya pama kichwani iliyokuwa inataka kuanguka, aliuliza mteja huyo aliyekuwa amejawa na tashwishi moyoni mwake huku akianza kupoa sasa hasa baada ya kuhakikishiwa kuwa kesho mzigo wake unaotoka China ulikuwa unawasili. "Nakuhakikishia mamlaka zote kuanzia TFDA, TBS na TRA zote zipo kazini masaa 24 pale bandarini hivyo ondoa shaka kila kitu kitakuwa vizuri kama nilivyokuahidi" alijibiwa mteja yule na afisa yule. "Sawa, sina tatizo Mungu akipenda tutaonana kesho Inshallah!' alizungumza mteja yule kisha akasimama na kupeana mikono na afisa yule akiashiria wanaagana. Kisha akafungua mlango wa ofisi hiyo iliyopo roshani ya pili katika jengo hilo la roshani tisa na kuanza kushuka chini ya jengo kwa mwendo mashi mashi huku uso wake ukiwa umevaa tabasamu la ushindi. Mzigo wake maalumu unatakaotumika na wahandisi wasichana wajasiriamali wa chuo kikuu kuonyesha ubunifu wao kwenye maonyesho ya biashara ya Sabasaba kuanzia tarehe 01/07 mpaka tarehe 10/07. Tayari walishapata kibanda cha kuonyesha bidhaa zao katika viwanja vya Sabasaba. Alipanga mzigo wake ufike mapema ili apange mipango yake bila papara. Hakutaka kosa lolote lifanyike ambalo litapelekea kuharibu mipango yake yote aliyoipanga kisayansi, ndio maana alikasirishwa sana na taahira ya mzigo iliyofanywa na kampuni hiyo ya usafirishaji mizigo. Huku akitembea kwa madahiro anatikisa funguo wa gari lake kwenye kidole akawa ameshafika kwenye eneo la maegesho ya magari. Akaingia kwenye gari yake na kuanza kuiondoa maeneo yale ya mtaa wa Mkwepu ili akatafuta mkahawa ambao atautumia kupata mlo wake wa mchana, hasa ukichukulia hakupata staftahi mshindio kama alivyozoea kila siku hivyo njaa ilikuwa inamtafuna vilivyo. Baada ya kuiendesha gari takribani muda wa kama wa dakika zisizozidi 10 tu hivi, simu yake ya mkononi ikaanza kuita. Akapunguza sauti ya muziki kwenye redio ya kwenye gari yake ili aipokee simu hiyo, kisha akaitoa simu hiyo kwenye upindo wa mkanda wake wa suruali kisha akaangalia mtu anayepiga simu yake. Akakunja matuta kwenye paji la uso wake, "Aaaaah...kumbe Sada anataka nini tena...!" aliwaza Shebby akiwa hataki usumbufu wowote kipindi hicho muhimu kwake kupangilia mambo yake bila kufanya makosa yoyote. Aliujua usumbufu wa Sada kwa muda mrefu kwake usio na kikomo bila kukata tamaa, ambaye alikuwa haoni wala hasikii kwa Shebby. Akawa anajishauri apokee au ampotezee lakini mwishoni akaamua aipokee simu hiyo, kisha akabonyeza kitufe cha kupokea simu yake. "Eheee.....Sada niambie bestito wangu, una mpya gani tena za kunijuza kipenzi changu" alianza kuzungumza Shebby kumuongelesha aliyempigia simu huku anajilazimisha ucheshi. "Mhhhh.....unanitenga tu bestitooo, au shemeji kakupa marufuku usitupigie simu vidoezi?? " alirudisha utani Sada kwa Shebby, mfanyakazi wa mapokezi wa 'RAJA SAFARI TOURS' ambaye walizoeana sana na Shebby tokea akiwa muajiriwa wa RAJA. "Aaah...wapi ni harakati tu za kusaka fulusi ndio zinatutenga, ila tupo pamoja sana" alijitetea Shebby hakutaka kuonekana anafanya taadi. "Tuyaache kwanza, wewe umefanya nini, nimeanza kuogopa tunaweza kuonana kwa haraka ndani ya nusu kutoka sasa?" Sada alimueleza lengo la kumpigia simu Shebby. Shebby akashusha pumzi kwa nguvu, huku anajiuliza kaharibu kitu gani tena mpaka Sada anamtafuta kwa udi na uvumba. "Hamna nilichoharibu, sasa njoo Slipway Hoteli fasta tuyajenge maana umenitisha..." alizungumza Shebby huku tayari akiwa ameshaegesha gari pembeni ya barabara akiogopea kusababisha ajali kwa kupokea simu ya taharuki huku anaendesha gari. "Sawa, siku hizi umekuwa matawi ya juu mambo yako ni Slipway tu haya, ngoja nije haraka maana simu hizi sio salama sana kwa kitu ninachotaka kukueleza, ni mambo nyeti " alikubali mualiko wa Shebby wa kukutana nae Hoteli ya Slipway iliyopo maeneo ya Msasani. Sada akaagana na Shebby akakata simu yake huku akifanya harakati za kuomba ruhusa ili akaonane na Shebby chapuchapu. Ulikuwa ni umbali wa takribani kama kilomita 7 kutoka ofisini kwa Sada kwenye maghorofa ya RAJA SAFARI TOURS mpaka kufika Hoteli ya Slipway ambapo Shebby alikuwa anakaribia kufika kwa ajili ya kupata mlo wake wa mchana. Shebby sasa alishasahau ladha ya vyakula vya kwa mama nitilie, usicheze na pesa wewe, milioni 200 aliyoingiziwa kwenye akaunti yake na tajiri Bwana Nadeem ilikuwa inaongea. Alikuwa anatembelea gari kiwango na tumbo lake linapata maakuli ya viwango.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 23
️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Ooh my God.....looh salaleee...! picha yangu kabisaaa au mtu anayefanana na mimi?" aliuliza kwa mshtuko Shebby baada ya kusimuliwa na Sada juu ya ujio wa mtu wanayemhisi ni afisa usalama, ambaye alikuwa hana asili wala fasili mtu huyo machoni mwao. Mtu huyo alikuwa si mwingine bali ni Kachero Manu alikuwa amefika kazini kwao RAJA SAFARI TOURS kufanya taftishi na baadhi ya watumishi wa hapo. Kilichomleta hapo kwenye kampuni hiyo ni kujaribu kufanya taftishi kama muuaji wa Profesa Kaganda ndio huyo huyo muuaji wa Bwana Pateli! Taftishi ambayo ilizaa matunda asiyoyategemea kwa Kachero Manu. "Ni sura yako wewe nakufahamu vizuri sibahatishi na sijaja hapa kuleta maneno ya mkahawani au kwenye vijiwe vya kahawa" Sada alikazia maneno kwa ukali akionyesha kutopendezewa na ubishi wa Shebby. "Nisamehe bestito sijakusudia kukubishia, haya tuyaache kwanza, ehee...! Akasemaje sasa huyo jamaa kuwa nimefanya tukio gani? " aliomba msamaha Shebby huku akiendelea kumdodosa Sada. "Kapita kuhoji kila mtu pale kazini huku anamuonyesha picha yako, sasa Mzee Sheni yule mpishi wako uliyekuwa unaenda nae mbugani karopoka maneno ya sumu hata yasiyohusu, sijui oooh...! Ulikufukuzwa kazi kwa sababu mkichangia bibi na Bosi wetu marehemu Pateli, hapo ndio huyo mgeni akavutika na udaku wa Mzee Sheni kaondoka nae ofisini katokomea kusipojulikana... kila mtu anasikitika juu yake yule Mzee sijui ataacha lini taarifa za lolololo, zitakuja kumponza siku za usoni" alizidi kupasua maneno Sada bila mficho kwa Shebby bila kuelewa kuwa amemfaa vilivyo. "Naanza kuogopa sasa mie nimefanya kosa gani mpaka nasakwa kwa udi na uvumba! " alijisemesha kwa huzuni Shebby hali ya kuwa anajua kila kitu kinachoendelea. "Dalili zinaonyesha ni usalama wa taifa huyo mtu, maana kaja na gari zao nyeusi zile" alizidi kuweka tashididi ya mazungumzo yake. Shebby sasa taharuki ilimkamata vilivyo, alitambua sasa polisi wameshafika mbali kwenye uchunguzi wao wa mauaji ya mfululizo kuanzia kwa Bosi Pateli na Profesa Kaganda. Hivyo akizubaa kidogo tu itakula kwake atashindwa kutekeleza kisasi chake kwa Dr.Sonko. "Inabidi bestito Sada unipe hifadhi nyumbani kwako la sivyo nitaumbuka! " alivunja ukimya Shebby kwa Sada akiomba auni ya ulinzi. Sada alivuta pumzi ndefu baada ya kusikia maneno yake ya Shebby. "Unanipa mtihani mzito sana Shebby, maana hujaniambia umefanya nini mpaka unatafuta, lakini pia hata mie unanipa mashaka unaonekana mambo yako kiuchumi sasa yapo bambam unasukuma ndinga la gharama huenda kuna tukio zito umefanya unatafutwa!" Sada alitikisa kiberiti kwa Shebby huku akionyesha kama hatokubali kirahisi. Lakini uhalisia wa mambo Sada alikuwa anampenda kwa dhati Shebby alikuwa hawezi kupindua kwa chochote atakachomwambia. Kwa zaidi ya miaka 6 tokea wamefahamiana, Sada alikuwa moyoni anaungua kwa joto la mapenzi kwa Shebby, na ndio maana alipoona kuna mtu anamsaka Shebby alishindwa kujizuia kutokumpa taarifa. Miaka yote alikuwa anajipa moyo ipo siku tu, huenda Shebby atamtakia kuwa anampenda. Aliposikia Shebby amenasa kwenye huba la Miss Tanzania na kishatangaza ndoa, aliugua karibia mwezi mzima, yu mahamumu hoi bin taabani hajiwezi kitandani. Alipopata nafuu na kurudi kazini alianza kuzoea kuwa Shebby ndio kapuruchuka sio wake tena, lakini walipoonana siku Shebby amekuja kuchukua barua yake toka kuzimu pale ofisini, ugonjwa wake wa huba kwa Shebby ukaibuka upya. Meseji cha chombezo zile za umeamkaje, umeshindaje na za usiku mwema zilikuwa hazikauki katika simu ya Shebby toka kwa Sada. "Hata wewe Sada, mwandani wangu huniamini unaniona kama mimi ni mjuba nishakua mtu wa ovyo sasa nani ataniamini tena?" alijifaragua kujilalamisha mbele ya Sada huku akijivika usoni mwake huzuni kubwa na kujitia kuinama chini. "Baby.....usinidhanie vibaya, sikuwa na nia mbaya nikihofia tu nikataka unitoe wasiwasi mimi nakuaminia zaidi ya asilimia 100% huwezi kuniingiza matatizoni" alijibu Sada huku moyoni akiwa na mlipuko wa furaha wa kuitwa mwandani na Shebby kwa mara ya kwanza kwa muda wa miaka 6. Shebby akawa anachekea tumboni kwa namna alivyomnasa kiulaini Sada kwenye mtego wake wa kumpa hifadhi mpaka anaitwa 'baby'. Maana alifahamu fika sasa msako dhidi yake wakimkosa nyumbani kwake, utahamia kwenye mahoteli na nyumba za kulala wageni hivyo hatokuwa salama kabisa. Kimbilio pekee ambapo ni salama palibaki nyumbani kwa Sada na ingekuwa ngumu kwa vyombo vya usalama kuleta hisia kuwa Shebby yupo nyumbani kwa Sada." Nilikuwa nataka kushangaa sana kama na wewe Sada ni rafiki mnafiki yule mkia wa fisi, ambaye wakati wa shida anakuepa kama mkoma vile" alizungumza Shebby kwa kujiamini huku anamalizia 'Ice-cream' yake kushushia mlo wake kabambe. Wakaendelea kusogoa hadithi moja mbili tatu huku wakijiandaa kuondoka kuelekea nyumbani kwa Sada huku furaha ya Sada ikiwa ni sheshe kama kumsukuma mlevi akijua fika Shebby akifika kwake vibwanga na vitimbi atakavyomfanyia hawezi kupindua kwake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ulikuwa ni usiku mbichi wa saa 2:30 usiku katika maeneo ya 'Mbezi Juu-Kwa Pembe' siku hiyo ya Jumamosi,Kachero Manu alikuwa ndio kwanza anaegesha kwenye eneo la maegesho la 'LIBRA SOCIAL HALL' gari yake aina ya 'Toyota Crown Royal Saloon' rangi ya maziwa. Aliegesha eneo ambalo hatapata usumbufu pindi atakapohitaji kuliondoa gari lake kwa haraka hasa ukichukulia siku hiyo ni ya mwishoni mwa juma, kadamnasi ya watu walikuwa wamefurika kuja kustarehe mpaka che. Ilikuwa dalili zinaonyesha ndani ya ukumbi ule kulikuwa kuna tafrija ya harusi inafanyika. Wahudhuriaji walikuwa wanazidi kumiminika huku wakiwa wamevalia mavazi yao nadhifu huku wakionekana wana furaha kubwa. Ghafla wakati Kachero Manu anajiandaa kuvuka upande aingie kwenye moja ya mashine za kutolea fedha zilizopo hapo hapo 'LIBRA SOCIAL HALL' usafiri wa Bwana na Bibi harusi ulikuwa unaingia. Fahari ya macho ikabidi Kachero Manu akodoe macho kuwaangalia wapendanao hao waliokuwa ndio wanashuka kwenye gari yao ya kifahari huku Bibi harusi akionekana kupendeza mpendezo wa Shamsi Matlai. Wakawa wanatembea masi masi kwa mwendo wa pole kuingia ukumbini mule,huku nyimbo mbalimbali za muziki zkipigwa kuchagiza uingiaji wao ndani ya ukumbi. Kachero Manu akapuuzia kuendelea kufuatilia yasiyomhusu akavuka ng'ambo ya pili na kuingia kwenye moja ya mashine ya kutolea fedha ya katikati inayomilikiwa na benki ya NBC, huku yasari kwake kulikuwa na mashine ya benki ya NMB na yamini kwake kuna mashine ya benki ya CRDB, na zote zilikuwa na watu wanachukua fulusi zao wakafanye mapochozi ya usiku huo kwenye starehe zao za mwishoni mwa juma. Akachukua kiasi cha pesa anachohitaji kisha akatoka na kuifuata barabara ya giza ya upande wa kulia kama alivyoelekezwa nyumbani kwa Shebby. Alitembelea kwa mwendo wa mashi mashi kwa takribani robo saa, mpaka akakutana na kibanda umiza kimejaza watu kibao wanashuhudia mchuano wa mechi za ligi kuu ya uingereza kabumbu uwanjani wachezaji wanamenyana katika runinga. Akapita na hamsini zake na hamna hata mmoja hata aliyegeuka kumtazama yeye. Alivyoenda mbele zaidi akaanza kuteremka bonde kushuka chini kwa mbali akawa ameziona nyumba nga'mbo ya pili zimejitenga. Akaenda mubashara kwenye baiti mojawapo ya kati kati ambayo ni duka la kuuza bidhaa ndogondogo. Alipofika dukani, alikuta wateja wanahudumia bidhaa mbalimbali za mahitaji yao ya siku, akazuga nae pia ni kama mhitaji wa bidhaa huku macho yake yote yanakodoa nyumba ya pili yake ambayo ndio nyumba haswa anayoishi Shebby. Alimuona mama mmoja yupo nje ya kibaraza anachoma maandazi. Akafanya maamuzi ya kumvaa yule kumuulizia kama Shebby yupo kwenye baiti. "Mama shikamoo...mimi ni mgeni wa mpangaji mwenzenu Shabani Zomboko sijui nimemkuta? " aliuliza Kachero Manu kwa yule mama. "Marhaba mwanangu, wala sifahamu maana huyo Shebby kutoka kwake na kurejea kwake anajuaga mwenyewe, labda umpigie simu au pita moja kwa moja na veranda hiyo chumba chake kimejitenga peke yake utakiona tu! " alijibu yule bila kumtazama usoni Kachero Manu huku akiweka maandazi mapya ya kuchoma kwenye karai linalochemka mafuta ikiwa ni ishara hana haja ya maswali zaidi yupo kikazi zaidi. Kachero Manu akajiongeza akaanza kutembea na veranda huku akigusa kiunoni kuhakikisha mguu wa kuku wake upo salama tayari kwa kutumika kama ikibidi. Kwa bahati baiti yote ilikuwa kimya kasoro chumba kimojawapo kulikuwa na muziki unapigwa kwa sauti ya chini. Akafika kwenye kile chumba kilichoungana na sebule alichopanga Shebby akakuta taa zimezimwa ishara ya kwamba hamna mtu ndani. Akaanza kubisha hodi kujiridhisha kama kweli hamna mtu. Aligonga kama mara tatu ukimya ukawa umetamalaki. Akaangalia muda kwenye saa yake ya mkononi, saa ikasoma ni saa 3:15 usiku juu ya alama. Himahima akachomoa mkungu wa funguo zake malaya mfukoni akaanza kukorokochoa kwa funguo hizo kwenye kitasa hicho cha mlango. Funguo wa tatu kujaribisha ukakubali kukifungua kitasa kile sasa mlango ukawa umefunguka. Haraka haraka akaingia ndani na kuurudishia mlango ule bila kufunga tena na ufunguo, alijua hatopoteza wakati mrefu. Akawasha kurunzi yake ndogo ya kumuwezesha kupata nuru ya kutosha kumuongoza chumbani mule huku mkono mwingine ukiwa umebeba bastola tayari kwa kushughulika ikibidi. Alipotupa macho kwenye sebule ile kwa haraka haraka hakuona chochote kitakachokuwa msaada kwake akaamua aelekee chumbani kwa Shebby. Kwa bahati alipokanyaga tu zulia la kujifutia miguu akahisi kama kuna kitu kigumu chini yake. Akanyanyua zulia lile akaona funguo mbili moja kubwa na nyingine zimeunganishwa kwa silsila nyembamba. Akatabasamu kwa jinsi mambo yanavyokwenda bambam. Akafungua mlango wa chumba kile akaingia bila hata kuubugaza mlango kwa pupa yake aliyokuwa nayo. Alipomulika kurunzi kitandani akakuta picha zimezagaa pale kitandani akasogelea na kuokota picha mojawapo. Ilikuwa ni picha ya Profesa Kaganda ikiwa imewekwa alama ya vema kuonyesha tayari ameshashughulikiwa. "Shabaaashi...! Huyu ndio muuaji asiyejulikana maluhuni mkubwa Shebby utanitambua mimi ni nani! " alijikuta anaropoka kwa sauti ya taratibu. "Tupa silaha yako chini na nyoosha mikono juu" ilikuwa ni sauti ya kama muungurumo wa radi katika masikio ya Kachero Manu huku mtutu baridi wa bastola ukiwa umegusa sikio lake la kushoto. Alishtukizwa kwa namna asiyoitarajia hata kidogo mpaka akajilaumu kwa kutochukua tahadhari ya kutosha. Bila ubishi wowote akatupa chini bastola yake na kunyoosha mikono yake, likawa ni kosa la kujutia la pili kwa Kachero Manu. Mtu yule aliyemuweka chini ya ulinzi akamnukiza puani kwa kitambaa, hanchifu kilicholowa kemikali. Pale pale Kachero Manu akajikuta anaishiwa nguvu na kuanguka chini puuuh kwa kupigiza kichwa kwenye tendegu la mguu wa kitanda kama papai lililoiva sana. Akapoteza fahamu chumbani mule mwa Shebby.
[emoji811][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 23
️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Ooh my God.....looh salaleee...! picha yangu kabisaaa au mtu anayefanana na mimi?" aliuliza kwa mshtuko Shebby baada ya kusimuliwa na Sada juu ya ujio wa mtu wanayemhisi ni afisa usalama, ambaye alikuwa hana asili wala fasili mtu huyo machoni mwao. Mtu huyo alikuwa si mwingine bali ni Kachero Manu alikuwa amefika kazini kwao RAJA SAFARI TOURS kufanya taftishi na baadhi ya watumishi wa hapo. Kilichomleta hapo kwenye kampuni hiyo ni kujaribu kufanya taftishi kama muuaji wa Profesa Kaganda ndio huyo huyo muuaji wa Bwana Pateli! Taftishi ambayo ilizaa matunda asiyoyategemea kwa Kachero Manu. "Ni sura yako wewe nakufahamu vizuri sibahatishi na sijaja hapa kuleta maneno ya mkahawani au kwenye vijiwe vya kahawa" Sada alikazia maneno kwa ukali akionyesha kutopendezewa na ubishi wa Shebby. "Nisamehe bestito sijakusudia kukubishia, haya tuyaache kwanza, ehee...! Akasemaje sasa huyo jamaa kuwa nimefanya tukio gani? " aliomba msamaha Shebby huku akiendelea kumdodosa Sada. "Kapita kuhoji kila mtu pale kazini huku anamuonyesha picha yako, sasa Mzee Sheni yule mpishi wako uliyekuwa unaenda nae mbugani karopoka maneno ya sumu hata yasiyohusu, sijui oooh...! Ulikufukuzwa kazi kwa sababu mkichangia bibi na Bosi wetu marehemu Pateli, hapo ndio huyo mgeni akavutika na udaku wa Mzee Sheni kaondoka nae ofisini katokomea kusipojulikana... kila mtu anasikitika juu yake yule Mzee sijui ataacha lini taarifa za lolololo, zitakuja kumponza siku za usoni" alizidi kupasua maneno Sada bila mficho kwa Shebby bila kuelewa kuwa amemfaa vilivyo. "Naanza kuogopa sasa mie nimefanya kosa gani mpaka nasakwa kwa udi na uvumba! " alijisemesha kwa huzuni Shebby hali ya kuwa anajua kila kitu kinachoendelea. "Dalili zinaonyesha ni usalama wa taifa huyo mtu, maana kaja na gari zao nyeusi zile" alizidi kuweka tashididi ya mazungumzo yake. Shebby sasa taharuki ilimkamata vilivyo, alitambua sasa polisi wameshafika mbali kwenye uchunguzi wao wa mauaji ya mfululizo kuanzia kwa Bosi Pateli na Profesa Kaganda. Hivyo akizubaa kidogo tu itakula kwake atashindwa kutekeleza kisasi chake kwa Dr.Sonko. "Inabidi bestito Sada unipe hifadhi nyumbani kwako la sivyo nitaumbuka! " alivunja ukimya Shebby kwa Sada akiomba auni ya ulinzi. Sada alivuta pumzi ndefu baada ya kusikia maneno yake ya Shebby. "Unanipa mtihani mzito sana Shebby, maana hujaniambia umefanya nini mpaka unatafuta, lakini pia hata mie unanipa mashaka unaonekana mambo yako kiuchumi sasa yapo bambam unasukuma ndinga la gharama huenda kuna tukio zito umefanya unatafutwa!" Sada alitikisa kiberiti kwa Shebby huku akionyesha kama hatokubali kirahisi. Lakini uhalisia wa mambo Sada alikuwa anampenda kwa dhati Shebby alikuwa hawezi kupindua kwa chochote atakachomwambia. Kwa zaidi ya miaka 6 tokea wamefahamiana, Sada alikuwa moyoni anaungua kwa joto la mapenzi kwa Shebby, na ndio maana alipoona kuna mtu anamsaka Shebby alishindwa kujizuia kutokumpa taarifa. Miaka yote alikuwa anajipa moyo ipo siku tu, huenda Shebby atamtakia kuwa anampenda. Aliposikia Shebby amenasa kwenye huba la Miss Tanzania na kishatangaza ndoa, aliugua karibia mwezi mzima, yu mahamumu hoi bin taabani hajiwezi kitandani. Alipopata nafuu na kurudi kazini alianza kuzoea kuwa Shebby ndio kapuruchuka sio wake tena, lakini walipoonana siku Shebby amekuja kuchukua barua yake toka kuzimu pale ofisini, ugonjwa wake wa huba kwa Shebby ukaibuka upya. Meseji cha chombezo zile za umeamkaje, umeshindaje na za usiku mwema zilikuwa hazikauki katika simu ya Shebby toka kwa Sada. "Hata wewe Sada, mwandani wangu huniamini unaniona kama mimi ni mjuba nishakua mtu wa ovyo sasa nani ataniamini tena?" alijifaragua kujilalamisha mbele ya Sada huku akijivika usoni mwake huzuni kubwa na kujitia kuinama chini. "Baby.....usinidhanie vibaya, sikuwa na nia mbaya nikihofia tu nikataka unitoe wasiwasi mimi nakuaminia zaidi ya asilimia 100% huwezi kuniingiza matatizoni" alijibu Sada huku moyoni akiwa na mlipuko wa furaha wa kuitwa mwandani na Shebby kwa mara ya kwanza kwa muda wa miaka 6. Shebby akawa anachekea tumboni kwa namna alivyomnasa kiulaini Sada kwenye mtego wake wa kumpa hifadhi mpaka anaitwa 'baby'. Maana alifahamu fika sasa msako dhidi yake wakimkosa nyumbani kwake, utahamia kwenye mahoteli na nyumba za kulala wageni hivyo hatokuwa salama kabisa. Kimbilio pekee ambapo ni salama palibaki nyumbani kwa Sada na ingekuwa ngumu kwa vyombo vya usalama kuleta hisia kuwa Shebby yupo nyumbani kwa Sada." Nilikuwa nataka kushangaa sana kama na wewe Sada ni rafiki mnafiki yule mkia wa fisi, ambaye wakati wa shida anakuepa kama mkoma vile" alizungumza Shebby kwa kujiamini huku anamalizia 'Ice-cream' yake kushushia mlo wake kabambe. Wakaendelea kusogoa hadithi moja mbili tatu huku wakijiandaa kuondoka kuelekea nyumbani kwa Sada huku furaha ya Sada ikiwa ni sheshe kama kumsukuma mlevi akijua fika Shebby akifika kwake vibwanga na vitimbi atakavyomfanyia hawezi kupindua kwake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ulikuwa ni usiku mbichi wa saa 2:30 usiku katika maeneo ya 'Mbezi Juu-Kwa Pembe' siku hiyo ya Jumamosi,Kachero Manu alikuwa ndio kwanza anaegesha kwenye eneo la maegesho la 'LIBRA SOCIAL HALL' gari yake aina ya 'Toyota Crown Royal Saloon' rangi ya maziwa. Aliegesha eneo ambalo hatapata usumbufu pindi atakapohitaji kuliondoa gari lake kwa haraka hasa ukichukulia siku hiyo ni ya mwishoni mwa juma, kadamnasi ya watu walikuwa wamefurika kuja kustarehe mpaka che. Ilikuwa dalili zinaonyesha ndani ya ukumbi ule kulikuwa kuna tafrija ya harusi inafanyika. Wahudhuriaji walikuwa wanazidi kumiminika huku wakiwa wamevalia mavazi yao nadhifu huku wakionekana wana furaha kubwa. Ghafla wakati Kachero Manu anajiandaa kuvuka upande aingie kwenye moja ya mashine za kutolea fedha zilizopo hapo hapo 'LIBRA SOCIAL HALL' usafiri wa Bwana na Bibi harusi ulikuwa unaingia. Fahari ya macho ikabidi Kachero Manu akodoe macho kuwaangalia wapendanao hao waliokuwa ndio wanashuka kwenye gari yao ya kifahari huku Bibi harusi akionekana kupendeza mpendezo wa Shamsi Matlai. Wakawa wanatembea masi masi kwa mwendo wa pole kuingia ukumbini mule,huku nyimbo mbalimbali za muziki zkipigwa kuchagiza uingiaji wao ndani ya ukumbi. Kachero Manu akapuuzia kuendelea kufuatilia yasiyomhusu akavuka ng'ambo ya pili na kuingia kwenye moja ya mashine ya kutolea fedha ya katikati inayomilikiwa na benki ya NBC, huku yasari kwake kulikuwa na mashine ya benki ya NMB na yamini kwake kuna mashine ya benki ya CRDB, na zote zilikuwa na watu wanachukua fulusi zao wakafanye mapochozi ya usiku huo kwenye starehe zao za mwishoni mwa juma. Akachukua kiasi cha pesa anachohitaji kisha akatoka na kuifuata barabara ya giza ya upande wa kulia kama alivyoelekezwa nyumbani kwa Shebby. Alitembelea kwa mwendo wa mashi mashi kwa takribani robo saa, mpaka akakutana na kibanda umiza kimejaza watu kibao wanashuhudia mchuano wa mechi za ligi kuu ya uingereza kabumbu uwanjani wachezaji wanamenyana katika runinga. Akapita na hamsini zake na hamna hata mmoja hata aliyegeuka kumtazama yeye. Alivyoenda mbele zaidi akaanza kuteremka bonde kushuka chini kwa mbali akawa ameziona nyumba nga'mbo ya pili zimejitenga. Akaenda mubashara kwenye baiti mojawapo ya kati kati ambayo ni duka la kuuza bidhaa ndogondogo. Alipofika dukani, alikuta wateja wanahudumia bidhaa mbalimbali za mahitaji yao ya siku, akazuga nae pia ni kama mhitaji wa bidhaa huku macho yake yote yanakodoa nyumba ya pili yake ambayo ndio nyumba haswa anayoishi Shebby. Alimuona mama mmoja yupo nje ya kibaraza anachoma maandazi. Akafanya maamuzi ya kumvaa yule kumuulizia kama Shebby yupo kwenye baiti. "Mama shikamoo...mimi ni mgeni wa mpangaji mwenzenu Shabani Zomboko sijui nimemkuta? " aliuliza Kachero Manu kwa yule mama. "Marhaba mwanangu, wala sifahamu maana huyo Shebby kutoka kwake na kurejea kwake anajuaga mwenyewe, labda umpigie simu au pita moja kwa moja na veranda hiyo chumba chake kimejitenga peke yake utakiona tu! " alijibu yule bila kumtazama usoni Kachero Manu huku akiweka maandazi mapya ya kuchoma kwenye karai linalochemka mafuta ikiwa ni ishara hana haja ya maswali zaidi yupo kikazi zaidi. Kachero Manu akajiongeza akaanza kutembea na veranda huku akigusa kiunoni kuhakikisha mguu wa kuku wake upo salama tayari kwa kutumika kama ikibidi. Kwa bahati baiti yote ilikuwa kimya kasoro chumba kimojawapo kulikuwa na muziki unapigwa kwa sauti ya chini. Akafika kwenye kile chumba kilichoungana na sebule alichopanga Shebby akakuta taa zimezimwa ishara ya kwamba hamna mtu ndani. Akaanza kubisha hodi kujiridhisha kama kweli hamna mtu. Aligonga kama mara tatu ukimya ukawa umetamalaki. Akaangalia muda kwenye saa yake ya mkononi, saa ikasoma ni saa 3:15 usiku juu ya alama. Himahima akachomoa mkungu wa funguo zake malaya mfukoni akaanza kukorokochoa kwa funguo hizo kwenye kitasa hicho cha mlango. Funguo wa tatu kujaribisha ukakubali kukifungua kitasa kile sasa mlango ukawa umefunguka. Haraka haraka akaingia ndani na kuurudishia mlango ule bila kufunga tena na ufunguo, alijua hatopoteza wakati mrefu. Akawasha kurunzi yake ndogo ya kumuwezesha kupata nuru ya kutosha kumuongoza chumbani mule huku mkono mwingine ukiwa umebeba bastola tayari kwa kushughulika ikibidi. Alipotupa macho kwenye sebule ile kwa haraka haraka hakuona chochote kitakachokuwa msaada kwake akaamua aelekee chumbani kwa Shebby. Kwa bahati alipokanyaga tu zulia la kujifutia miguu akahisi kama kuna kitu kigumu chini yake. Akanyanyua zulia lile akaona funguo mbili moja kubwa na nyingine zimeunganishwa kwa silsila nyembamba. Akatabasamu kwa jinsi mambo yanavyokwenda bambam. Akafungua mlango wa chumba kile akaingia bila hata kuubugaza mlango kwa pupa yake aliyokuwa nayo. Alipomulika kurunzi kitandani akakuta picha zimezagaa pale kitandani akasogelea na kuokota picha mojawapo. Ilikuwa ni picha ya Profesa Kaganda ikiwa imewekwa alama ya vema kuonyesha tayari ameshashughulikiwa. "Shabaaashi...! Huyu ndio muuaji asiyejulikana maluhuni mkubwa Shebby utanitambua mimi ni nani! " alijikuta anaropoka kwa sauti ya taratibu. "Tupa silaha yako chini na nyoosha mikono juu" ilikuwa ni sauti ya kama muungurumo wa radi katika masikio ya Kachero Manu huku mtutu baridi wa bastola ukiwa umegusa sikio lake la kushoto. Alishtukizwa kwa namna asiyoitarajia hata kidogo mpaka akajilaumu kwa kutochukua tahadhari ya kutosha. Bila ubishi wowote akatupa chini bastola yake na kunyoosha mikono yake, likawa ni kosa la kujutia la pili kwa Kachero Manu. Mtu yule aliyemuweka chini ya ulinzi akamnukiza puani kwa kitambaa, hanchifu kilicholowa kemikali. Pale pale Kachero Manu akajikuta anaishiwa nguvu na kuanguka chini puuuh kwa kupigiza kichwa kwenye tendegu la mguu wa kitanda kama papai lililoiva sana. Akapoteza fahamu chumbani mule mwa Shebby.
[emoji811][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ahsante sana mkuu
 
Back
Top Bottom