mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,007
- Thread starter
- #21
HUBA LA MISS TANZANIA-PART 17
Shebby akiwa yupo kamili gado kwa kupiga matukio mengine ya kutikisa jiji alikuwa anaegesha gari yake kwenye uwanja wa Biafra-Kinondoni mbele ya Chuo Kikuu Huria 'Open University of Tanzania (OUT)'. Akashuka nje ya gari lake, akaangalia saa yake ya mkononi akatabasamu ilikuwa ni saa tatu kasorobo ya usiku. Alichofanya Shebby kwanza ni kutafuta lilipo duka la kuuzia dawa za binadamu 'Pharmacy' iliyopo jirani na hapo eneo la Biafra usiku huo.
"Habari za usiku dada yangu, pole sana na kazi!" alisalimia Shebby baada ya kufungua mlango wa duka hilo la madawa na kuingia ndani. "Ahsante sana, usinipe pole nipe hongera, Tanzania ya sasa kauli mbiu ni 'Hapa kazi tu' mpaka kieleweke " akajibu mhudumu yule kwa bashasha wakaangua kicheko wote kwa pamoja. "Sijui nikusaidie nini kaka yangu, nipo tayari kukuhudumia" alivunja furaha ile ya kicheko mhudumu yule ambaye dalili zote zilionyesha anakaribia kufunga duka lake. "Dada yangu mie nina aleji ya macho, yanakuwa mekunduu sasa naomba unisaidie dawa ya macho 'Altazine' nikaminyie jichoni nipate kulala vizuri maana yanawasha kwelikweli" alijieleza Shebby kwa ufasaha. "Hiyo dawa ipo pole sana thamani yake ni shilingi elfu nne tu za Kitanzania" alijibu yule dada huku akiitafuta dawa hiyo kutoka kwenye shelfu za kutunzia dawa na kumkabidhi dawa hiyo Shebby.
"Mhhhh...mbona sio hii, naona wameandika 'Visine Eye drops' wakati mie nahitaji Altazine, nyie wauza madawa bwana wakati mwingine wababaishajiii...." alizungumza Shebby kwa hasira kidogo baada ya kuona jina ni tofauti na dawa aliyoiagiza. "Baba yangu usikasirike dawa ni hiyo hiyo tofauti ni majina ya kibiashara tu 'brand name' hiyo dawa uliyoitaka ya Altazine ina majina kochokocho. Altazine inajulikana pia kama Geneye Extra, Geneyes, Opti-Clear, Optigene 3, Redness Relief, Redness Relief Original, Visine, Visine Maximum Redness Relief, Vision Clear hayo yote ni majina yake" alifafanua kiufasaha kuonyesha hajakaa pale dukani bure bure bali amekaa kwa sababu amesomea elimu ya famasia. "Samahani sana kwa kutoheshimu taaluma yako lakini nyie wenyewe ndio mnatuchanganya majina yote hayo ya kazi gani sasa" aliomba msamaha Shebby huku akijitetea kwa mkoroganyiko huo uliotokea.
"Unachotakiwa wewe kuzingatia ni viambata vyake vya kwenye 'Generic Name' ambayo ni tetrahydrozoline ophthalmic ambayo kazi yake ni kupunguza kipenyo cha mishipa ya damu inayoelekea kwenye jicho ili kupunguza jicho kuwa na rangi nyekundu" Alifafanua kwa weledi mkubwa, ufafanuzi ambao ulimshibisha vilivyo Shebby. Hakuwa na muda wa kupoteza, akailipia dawa yake ya macho na kutimka zake haraka haraka kuelekea Break Point.
Profesa Kaganda alikuwa tayari kashawasili kwenye mkahawa wa 'Break Point Restaurant' uliopo maeneo ya Kinondoni. Shebby baada ya kuzisoma nyendo za Profesa Kaganda kwa zaidi ya wiki moja, akagundua ratiba yake akitoka chuoni IFM kufundisha, aghalabu anapitia Break Point ya Kinondoni anapata mlo wake wa usiku, kisha anaendeleza moja moto, moja baridi kabla ya kurejea nyumbani kwake Salasala. Shebby na yeye alishajifanya kijiwe chake ni Break Point cha kupatia mlo wake ili mradi azisome vizuri nyendo za mlengwa wake. Shebby akapita vichochoro vya ndani kwa ndani mpaka akaja kuibukia Break Point ndani ya mwendo wa takribani dakika 10 tu. Alipoangalia kwenye maegesho ya magari Shebby akatabasamu, baada ya kuliona gari la Profesa limeegeshwa nje ya mkahawa.
Shebby akiwa amevaa kofia yake ya pama ya rangi ya kahawia na miwani yake nyeusi, huku juu akiwa amevalia jaketi la baridi la kisasa rangi nyeusi lenye michirizi ya rangi ya uzurungi lililotengenezwa kwa ngozi ndani yake akiwa na fulana ya Polo ya rangi ya kijani bila kusahau sarawili yake ya dangirizi nyeusi yenye mifuko mifuko mingi na safari buti zake. Kwa ufupi alikuwa anaonekana ni mtanashati na maridadi kwa mavazi, lakini moyo wake ndani ulikuwa mweusi ti ti ti kwa kiu ya kulipiza kisasi kwa wote waliomaharibia huba lake kwa Miss Tanzania. Mkahawa siku hiyo ya Ijumaa ulikuwa umeshona watu vilivyo utasema kuna chakula na vinywaji vya bure kumbe wanalipia pesa zao. Watu wa mataifa mbalimbali kuanzia wazungu, wahindi, waarabu na Waafrika ambao wana maisha bora, sio mahohe hae, pangu pakavu tia mchuzi. Walikuwa wanakula na kunywa huku wanazungumza kwa furaha kubwa.
Kama kawaida yake Profesa Kaganda alikuwa ni mtu mpekepeke asiyependa kujichanganya na watu akiwa kwenye starehe zake, alikuwa amejitenga kwenye meza ya kukaa watu wanne, wakiwa wapo wawili tu. Shebby moja kwa moja akaenda kuungana nao sasa wakawa watu watatu. "Good evening waungwana...!" alisalimia Shebby na kukaa kiti mkabala na mbaya wake. Wakaitikia salamu ile huku wanamkaribisha kwa bashasha kama ujuavyo ukarimu wa Watanzania wakikutana utasema ni ndugu wa familia moja kwa namna wanavyochangamkiana. Mhudumu akamfuata Shebby kwa ajili ya kumsikiliza mahitaji yake. "Niletee Wali kwa nyama ya nyati iliyopikwa chukuchuku tu kwa nyanya, kwa upande wa kinywaji niletee juisi yoyote ya matunda unayoipenda wewe ninywe! " aliagiza Shebby kwa mhudumu yule. Ambaye alitii maagizo ya mteja wake na kwenda kupeleka oda yake jikoni.
Break Point ni mkahawa ambao ulikuwa unasifika jijini Dar es Salaam kwa mapishi ya nyama za porini, kuanzia nyati, swala na nyinginezo. Hilo ndio jambo ambalo lilikuwa pia linamvutia Profesa Kaganda kula milo yake hapo. Alikuwa ni msomi ambaye hana mke nyumbani kwake anaishi kinembanemba tu. Alishawahi kuwa na mke wa Kijerumani aliyewahi kuzaa nae watoto wawili wa kiume akiwa masomoni nchini Ujerumani. Kilichotokea baina yao mpaka ndoa hiyo kuvunjika ni siri yao na Manani, lakini kwa muda mrefu watu wanaomjua hawajahi kumuona mkewe wala watoto wake. Alikuwa ni mtu wa kula bata kwa kwenda mbele hana majukumu yoyote ya kifamilia zaidi ya kujihudumia yeye mwenyewe tu.
Alipoletewa chakula chake akawa Shebby anakishambulia kwa pupa chakula kile kitamu hasa ukichukulia alikuwa na njaa kali. Kipindi chote wapo watatu kwenye meza walikuwa wanabadilishana mazungumzo mbalimbali ya mambo yanayoendelea nchini Tanzania kuanzia siasa mpaka kwenye burudani. Huku Shebby akitafuta nafasi ya kumfanyia tukio alilolikusudia Profesa Kaganda. Fursa adhimu aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ikawadia, yule mwenzao kwenye ile meza akawaaga, akanyanyuka zake kuondoka. Mezani wakabaki wawili tu, Profesa Kaganda na Shebby, mahasimu wawili wasiopikika chungu kimoja, utamu zaidi ukichagizwa kwa mmoja kumtambua mwenzake wakati mwingine hamjui mwenzake.
Laiti Profesa Kaganda angefahamu kuwa mbele yupo wakala wa Ziraeli malaika mtoa roho za waja, Wallahi angetimua mbio zile za Kibanga ampiga mkoloni. Lakini ajuaye ya ghaibu ni Rabana, mlango wa funguo za siri anazo yeye tu hajamuwakilisha yoyote.
"Waitress...Weeeeh...Waitressssss.....kuja hapa ongeza bia moja ya mwisho hapa kisha ulete bili yangu, nikalale zangu mieee...." alimuita mhudumu Profesa Kaganda huku akiwa ndio amemaliza msitu wa bia zilizotapakaa mezani pale. Alipoagiza tu kabla hajaletewa akanyanyuka kuelekea msalani kujisaidia. Hapo hapo Shebby kachomoa kutoka kwenye mfuko wake wa dangirizi dawa yake ya macho na kuiminyia matone kama manne tu kwenye glasi ile aliyokuwa anaitumia kunywea pombe zake Profesa Kaganda.
"Usifungue kwanza hiyo bia yake msubiri kwanza arudi, maana kaka yangu huyu akilewa ana matata sana yaani" alizungumza Shebby baada ya mhudumu Kuja kwa ghafla na bia aliyoagizwa na kutaka kuifungua. Hali iliyopelekea Shebby aidondoshe ile dawa yake chini kwa uoga kwa malengo ya kuwa ataiokota mhudumu akiondoka zake. Akamdanganya pia mhudumu kama yule Profesa ni kaka yake wa damu ili kuwafanya wahudumu wa pale waamini kuwa ni wamoja. "Yaani....kumbe hata nyie wanandugu mnamjua vizuri eeeh huyu Profesa akiwa hajautwika mtindi ni mtu mzuri sana, hariri hanaga shida na mtu lakini shida yake akilewa tu mhhhhhh...fujo tupu mtindo mmoja mara anapapasa papasa wahudumu miili yao kimahaba utasema kaingia balehe juzi juzi" aliongea mhudumu yule akionyesha kuchoshwa na tabia chafu za Profesa Kaganda.
Huo ndio unyanyasaji wa kijinsia mashuhuri sana kwa wahudumu wa baa na mikahawani wanaofanyiwa na wateja wao pindi wakilewa lakini hamna wa kuwapazia sauti kutokana na unyanyasaji huo wa mashambulio ya aibu. Kwanza wakipaza sauti zao watafukuzwa kazi mara moja na wamiliki wa maeneo wanayofanyia kazi kwa kisingizio cha kuwa mteja ni mfalme hivyo umridhishe chochote akitakacho. Tegemeo lao pekee la kutetea haki zao lilibakia kwa ' CHODAWU' Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Mahotelini, Majumbani na Huduma za Jamii, lakini wapi chama hicho kilikuwa kwenye usingizi mzito wa pono, si hayati si mamati wapo wapo siku zinasonga.
"Safi sana kwa kunisubiria, mteja ni mfalme maana usalama siku hizi ni mdogo wewe binti lazima nishuhudie unavyofungua" alizungumza Profesa Kaganda baada ya kutua pale mezani na kumuona mhudumu amesimama na bia yake anamsubiria yeye. "Kweli Bwana broo...siku hizi dunia inakaribia machweo kabisa kila aina za uhalifu unaovuma zama hizi" alijifaragua Shebby huku moyoni akijua tayari kashamuingia mkenge Profesa Kaganda. Akafunguliwa bia ile Profesa kisha kwa heshima na taadhima dada yule akaimimina bia ile kwenye glasi iliyofanyiwa mambo mambo na Shebby. Bila kuchelewa ilipojazwa tu kinywaji kile, Profesa akainyanyua juu kwa juu huku anaanza kuigiza kwa mtindo wa tarumbeta bila kupumzika, kisha alipoitua chini ilikuwa ipo tupu.
Alipoishika bia yake ili ajimiminie tena kwa mara ingine akawa kama mtu mwenye kizunguzungu anasitasita. "Profesa nini tena..?" Shebby alijishebedua kumuuuliza wakati anajua tayari Altazine imeshafanya vitu vyake mwilini. "Naa...ji... si..ki... a dizz....ne...ssss, ni...pe.....leke...... kwe...nye ga...riiii..." alizungumza kwa shida sana akiwa analalamika kuhisi kizunguzungu.
Shebby ndio fursa aliyokuwa anaitaka hiyo akaanza kumnyanyua kwa kutumia mabega yake anamburuta anamtoa nje ya mkahawa ule. Hamna aliyejali sana tukio hilo walijua tu ni mlevi aliyezidiwa na kileo anasaidiwa kupelekwa nyumbani kwake na ndugu yake au msamaria mwema. Ikawa ndio mwisho wa Profesa Kaganda kuonekana kwenye uso wa dunia hii.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Shebby akiwa yupo kamili gado kwa kupiga matukio mengine ya kutikisa jiji alikuwa anaegesha gari yake kwenye uwanja wa Biafra-Kinondoni mbele ya Chuo Kikuu Huria 'Open University of Tanzania (OUT)'. Akashuka nje ya gari lake, akaangalia saa yake ya mkononi akatabasamu ilikuwa ni saa tatu kasorobo ya usiku. Alichofanya Shebby kwanza ni kutafuta lilipo duka la kuuzia dawa za binadamu 'Pharmacy' iliyopo jirani na hapo eneo la Biafra usiku huo.
"Habari za usiku dada yangu, pole sana na kazi!" alisalimia Shebby baada ya kufungua mlango wa duka hilo la madawa na kuingia ndani. "Ahsante sana, usinipe pole nipe hongera, Tanzania ya sasa kauli mbiu ni 'Hapa kazi tu' mpaka kieleweke " akajibu mhudumu yule kwa bashasha wakaangua kicheko wote kwa pamoja. "Sijui nikusaidie nini kaka yangu, nipo tayari kukuhudumia" alivunja furaha ile ya kicheko mhudumu yule ambaye dalili zote zilionyesha anakaribia kufunga duka lake. "Dada yangu mie nina aleji ya macho, yanakuwa mekunduu sasa naomba unisaidie dawa ya macho 'Altazine' nikaminyie jichoni nipate kulala vizuri maana yanawasha kwelikweli" alijieleza Shebby kwa ufasaha. "Hiyo dawa ipo pole sana thamani yake ni shilingi elfu nne tu za Kitanzania" alijibu yule dada huku akiitafuta dawa hiyo kutoka kwenye shelfu za kutunzia dawa na kumkabidhi dawa hiyo Shebby.
"Mhhhh...mbona sio hii, naona wameandika 'Visine Eye drops' wakati mie nahitaji Altazine, nyie wauza madawa bwana wakati mwingine wababaishajiii...." alizungumza Shebby kwa hasira kidogo baada ya kuona jina ni tofauti na dawa aliyoiagiza. "Baba yangu usikasirike dawa ni hiyo hiyo tofauti ni majina ya kibiashara tu 'brand name' hiyo dawa uliyoitaka ya Altazine ina majina kochokocho. Altazine inajulikana pia kama Geneye Extra, Geneyes, Opti-Clear, Optigene 3, Redness Relief, Redness Relief Original, Visine, Visine Maximum Redness Relief, Vision Clear hayo yote ni majina yake" alifafanua kiufasaha kuonyesha hajakaa pale dukani bure bure bali amekaa kwa sababu amesomea elimu ya famasia. "Samahani sana kwa kutoheshimu taaluma yako lakini nyie wenyewe ndio mnatuchanganya majina yote hayo ya kazi gani sasa" aliomba msamaha Shebby huku akijitetea kwa mkoroganyiko huo uliotokea.
"Unachotakiwa wewe kuzingatia ni viambata vyake vya kwenye 'Generic Name' ambayo ni tetrahydrozoline ophthalmic ambayo kazi yake ni kupunguza kipenyo cha mishipa ya damu inayoelekea kwenye jicho ili kupunguza jicho kuwa na rangi nyekundu" Alifafanua kwa weledi mkubwa, ufafanuzi ambao ulimshibisha vilivyo Shebby. Hakuwa na muda wa kupoteza, akailipia dawa yake ya macho na kutimka zake haraka haraka kuelekea Break Point.
Profesa Kaganda alikuwa tayari kashawasili kwenye mkahawa wa 'Break Point Restaurant' uliopo maeneo ya Kinondoni. Shebby baada ya kuzisoma nyendo za Profesa Kaganda kwa zaidi ya wiki moja, akagundua ratiba yake akitoka chuoni IFM kufundisha, aghalabu anapitia Break Point ya Kinondoni anapata mlo wake wa usiku, kisha anaendeleza moja moto, moja baridi kabla ya kurejea nyumbani kwake Salasala. Shebby na yeye alishajifanya kijiwe chake ni Break Point cha kupatia mlo wake ili mradi azisome vizuri nyendo za mlengwa wake. Shebby akapita vichochoro vya ndani kwa ndani mpaka akaja kuibukia Break Point ndani ya mwendo wa takribani dakika 10 tu. Alipoangalia kwenye maegesho ya magari Shebby akatabasamu, baada ya kuliona gari la Profesa limeegeshwa nje ya mkahawa.
Shebby akiwa amevaa kofia yake ya pama ya rangi ya kahawia na miwani yake nyeusi, huku juu akiwa amevalia jaketi la baridi la kisasa rangi nyeusi lenye michirizi ya rangi ya uzurungi lililotengenezwa kwa ngozi ndani yake akiwa na fulana ya Polo ya rangi ya kijani bila kusahau sarawili yake ya dangirizi nyeusi yenye mifuko mifuko mingi na safari buti zake. Kwa ufupi alikuwa anaonekana ni mtanashati na maridadi kwa mavazi, lakini moyo wake ndani ulikuwa mweusi ti ti ti kwa kiu ya kulipiza kisasi kwa wote waliomaharibia huba lake kwa Miss Tanzania. Mkahawa siku hiyo ya Ijumaa ulikuwa umeshona watu vilivyo utasema kuna chakula na vinywaji vya bure kumbe wanalipia pesa zao. Watu wa mataifa mbalimbali kuanzia wazungu, wahindi, waarabu na Waafrika ambao wana maisha bora, sio mahohe hae, pangu pakavu tia mchuzi. Walikuwa wanakula na kunywa huku wanazungumza kwa furaha kubwa.
Kama kawaida yake Profesa Kaganda alikuwa ni mtu mpekepeke asiyependa kujichanganya na watu akiwa kwenye starehe zake, alikuwa amejitenga kwenye meza ya kukaa watu wanne, wakiwa wapo wawili tu. Shebby moja kwa moja akaenda kuungana nao sasa wakawa watu watatu. "Good evening waungwana...!" alisalimia Shebby na kukaa kiti mkabala na mbaya wake. Wakaitikia salamu ile huku wanamkaribisha kwa bashasha kama ujuavyo ukarimu wa Watanzania wakikutana utasema ni ndugu wa familia moja kwa namna wanavyochangamkiana. Mhudumu akamfuata Shebby kwa ajili ya kumsikiliza mahitaji yake. "Niletee Wali kwa nyama ya nyati iliyopikwa chukuchuku tu kwa nyanya, kwa upande wa kinywaji niletee juisi yoyote ya matunda unayoipenda wewe ninywe! " aliagiza Shebby kwa mhudumu yule. Ambaye alitii maagizo ya mteja wake na kwenda kupeleka oda yake jikoni.
Break Point ni mkahawa ambao ulikuwa unasifika jijini Dar es Salaam kwa mapishi ya nyama za porini, kuanzia nyati, swala na nyinginezo. Hilo ndio jambo ambalo lilikuwa pia linamvutia Profesa Kaganda kula milo yake hapo. Alikuwa ni msomi ambaye hana mke nyumbani kwake anaishi kinembanemba tu. Alishawahi kuwa na mke wa Kijerumani aliyewahi kuzaa nae watoto wawili wa kiume akiwa masomoni nchini Ujerumani. Kilichotokea baina yao mpaka ndoa hiyo kuvunjika ni siri yao na Manani, lakini kwa muda mrefu watu wanaomjua hawajahi kumuona mkewe wala watoto wake. Alikuwa ni mtu wa kula bata kwa kwenda mbele hana majukumu yoyote ya kifamilia zaidi ya kujihudumia yeye mwenyewe tu.
Alipoletewa chakula chake akawa Shebby anakishambulia kwa pupa chakula kile kitamu hasa ukichukulia alikuwa na njaa kali. Kipindi chote wapo watatu kwenye meza walikuwa wanabadilishana mazungumzo mbalimbali ya mambo yanayoendelea nchini Tanzania kuanzia siasa mpaka kwenye burudani. Huku Shebby akitafuta nafasi ya kumfanyia tukio alilolikusudia Profesa Kaganda. Fursa adhimu aliyokuwa anaisubiria kwa hamu ikawadia, yule mwenzao kwenye ile meza akawaaga, akanyanyuka zake kuondoka. Mezani wakabaki wawili tu, Profesa Kaganda na Shebby, mahasimu wawili wasiopikika chungu kimoja, utamu zaidi ukichagizwa kwa mmoja kumtambua mwenzake wakati mwingine hamjui mwenzake.
Laiti Profesa Kaganda angefahamu kuwa mbele yupo wakala wa Ziraeli malaika mtoa roho za waja, Wallahi angetimua mbio zile za Kibanga ampiga mkoloni. Lakini ajuaye ya ghaibu ni Rabana, mlango wa funguo za siri anazo yeye tu hajamuwakilisha yoyote.
"Waitress...Weeeeh...Waitressssss.....kuja hapa ongeza bia moja ya mwisho hapa kisha ulete bili yangu, nikalale zangu mieee...." alimuita mhudumu Profesa Kaganda huku akiwa ndio amemaliza msitu wa bia zilizotapakaa mezani pale. Alipoagiza tu kabla hajaletewa akanyanyuka kuelekea msalani kujisaidia. Hapo hapo Shebby kachomoa kutoka kwenye mfuko wake wa dangirizi dawa yake ya macho na kuiminyia matone kama manne tu kwenye glasi ile aliyokuwa anaitumia kunywea pombe zake Profesa Kaganda.
"Usifungue kwanza hiyo bia yake msubiri kwanza arudi, maana kaka yangu huyu akilewa ana matata sana yaani" alizungumza Shebby baada ya mhudumu Kuja kwa ghafla na bia aliyoagizwa na kutaka kuifungua. Hali iliyopelekea Shebby aidondoshe ile dawa yake chini kwa uoga kwa malengo ya kuwa ataiokota mhudumu akiondoka zake. Akamdanganya pia mhudumu kama yule Profesa ni kaka yake wa damu ili kuwafanya wahudumu wa pale waamini kuwa ni wamoja. "Yaani....kumbe hata nyie wanandugu mnamjua vizuri eeeh huyu Profesa akiwa hajautwika mtindi ni mtu mzuri sana, hariri hanaga shida na mtu lakini shida yake akilewa tu mhhhhhh...fujo tupu mtindo mmoja mara anapapasa papasa wahudumu miili yao kimahaba utasema kaingia balehe juzi juzi" aliongea mhudumu yule akionyesha kuchoshwa na tabia chafu za Profesa Kaganda.
Huo ndio unyanyasaji wa kijinsia mashuhuri sana kwa wahudumu wa baa na mikahawani wanaofanyiwa na wateja wao pindi wakilewa lakini hamna wa kuwapazia sauti kutokana na unyanyasaji huo wa mashambulio ya aibu. Kwanza wakipaza sauti zao watafukuzwa kazi mara moja na wamiliki wa maeneo wanayofanyia kazi kwa kisingizio cha kuwa mteja ni mfalme hivyo umridhishe chochote akitakacho. Tegemeo lao pekee la kutetea haki zao lilibakia kwa ' CHODAWU' Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Mahotelini, Majumbani na Huduma za Jamii, lakini wapi chama hicho kilikuwa kwenye usingizi mzito wa pono, si hayati si mamati wapo wapo siku zinasonga.
"Safi sana kwa kunisubiria, mteja ni mfalme maana usalama siku hizi ni mdogo wewe binti lazima nishuhudie unavyofungua" alizungumza Profesa Kaganda baada ya kutua pale mezani na kumuona mhudumu amesimama na bia yake anamsubiria yeye. "Kweli Bwana broo...siku hizi dunia inakaribia machweo kabisa kila aina za uhalifu unaovuma zama hizi" alijifaragua Shebby huku moyoni akijua tayari kashamuingia mkenge Profesa Kaganda. Akafunguliwa bia ile Profesa kisha kwa heshima na taadhima dada yule akaimimina bia ile kwenye glasi iliyofanyiwa mambo mambo na Shebby. Bila kuchelewa ilipojazwa tu kinywaji kile, Profesa akainyanyua juu kwa juu huku anaanza kuigiza kwa mtindo wa tarumbeta bila kupumzika, kisha alipoitua chini ilikuwa ipo tupu.
Alipoishika bia yake ili ajimiminie tena kwa mara ingine akawa kama mtu mwenye kizunguzungu anasitasita. "Profesa nini tena..?" Shebby alijishebedua kumuuuliza wakati anajua tayari Altazine imeshafanya vitu vyake mwilini. "Naa...ji... si..ki... a dizz....ne...ssss, ni...pe.....leke...... kwe...nye ga...riiii..." alizungumza kwa shida sana akiwa analalamika kuhisi kizunguzungu.
Shebby ndio fursa aliyokuwa anaitaka hiyo akaanza kumnyanyua kwa kutumia mabega yake anamburuta anamtoa nje ya mkahawa ule. Hamna aliyejali sana tukio hilo walijua tu ni mlevi aliyezidiwa na kileo anasaidiwa kupelekwa nyumbani kwake na ndugu yake au msamaria mwema. Ikawa ndio mwisho wa Profesa Kaganda kuonekana kwenye uso wa dunia hii.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]