Riwaya: Chokoraa

Riwaya: Chokoraa

Casuist

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2014
Posts
1,189
Reaction score
2,971
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George IronMosenya


SEHEMU YA KWANZA

Moshimweusi uliokuwa unatoka katika jalala lililokuwa linachomwa ulifanyamfano wa ukungu usiopendeza machoni.
Wapita njia waliongezamwendokasi walivyokaribia eneo lile. Wengine waliziba pua zao kwakutumia viganja vya mikono yao kuepukana na hewa hiyo chafu.
Baadhiyao walijiziba na magazeti, wengine kwa bahasha zao. Ilikuwa ni jionina kila mmoja alikuwa anarejea kutoka katika mizunguko yake.

Kwajinsi watu walivyokuwa wametingwa na mambo vichwani mwao hawakuwezakulishuhudia kundi la viumbe hai ambalo halikubabaishwa na moshi huomzito. Na hata kama wangeona wasingekuwa na la kusaidia zaidi yakupata la kuongea na kujisahaulisha suluba ya siku nzima hukowalipotoka.

Ardhi iliyobeba uchafu wa kila aina iliyopewa jina lajalala ilikuwa katika mahangahiko ikifukuliwa kwa fujo na watotowanne wa rika moja huku mkubwa akikadiriwa kuwa na miaka kumi namitano
Macho yao yalikuwa mekundu, matambala ambayo zamaniyaliitwa nguo yalifunika miili yao.
Wengine walikuwa wameinamawengine wakiwa wamepiga magoti, mikono yao ikiwa 'bize' kuchimbaardhi na kutoka na vyuma chakavu.

Matambala waliyovaa yaliwafanyawote wafanane, na ilikuwa ngumu kutambua iwapo wana jinsiatofauti.
Hakuna aliyezungumza na mwenzake, nyuso zaozilizotiririka jasho zilitangaza njaa kali na chuki.

Mtoto mmojaalivyojiridhisha kuwa eneo lile vyuma vilikuwa vimekwisha alinyanyukana mfuko wake wa chumvichumvi, akachukua mkono wake mchafuakajipangusa jasho. Tambala alilokuwa amevaa lilisomeka kwa shidamaandishi 'I LOVE TANZANIA', lilikuwa kubwa kumpita na lilikuwalimetatuka na kuruhusu matiti yake yaliyokuwa yameanza kujifunzakusimama yachungulie nje. Huyu pekee alikuwa mkubwa kupitawenzake.

Alijikongoja na fuko lake hadi akalifikia jalala jingine.Hapo pia alipapasa bila kupata chochote. Akasimama wima akiwa amekatatamaa. Alipopiga hatua nne kuliacha jalala macho yake yalivutiwa nakifurushi cha uchafu wa siku nyingi, akatua tena fuko lake akachukuakimti kigumu akaliendea lile furushi na kuanza kupekenyua.

Lahaula!Tabasamu pana likachanua usöni mwake, akayapongeza macho yake kwakuvutiwa na furushi lile. Akavuta kwa nguvu, akatoka na jembechakavu.
Biashara nzuri kwa siku hiyo!

Wakati anasimamakuliendea fuko lake, akasita kabla ya kupiga hatua. Hakuwa pekeyake!
"Siso yangu hiyo!" sauti ya kiume ilikoroma. Bintiakamtazama yule chokoraa mwenye nywele zinazotaka kufanana namwarabu, ngozi nyeusi yenye ukurutu unaotiririka jasho.

"Sisoyangu hiyo uliyoshika" sauti ya mvulana haikuwa na mzaha.Alimaanisha!
Yule binti akashtuka na kulitazama lile jembemkononi kana kwamba hakutambua kama amelishikilia.

Kisha akapuuziaakapiga hatua kadhaa kuliendea fuko lake, yule kijana akamfanyiashambulizi la kushtukiza, akamnyakua lile jembe. Alipotaka kukimbiayule binti akawa mwepesi akakamata shati chakavu la yule kijana. Kamavile wembe mkali unavyokutana na karatasi laini ndivyo lilivyoachanatambala lile.
"Mamaa! Umenichania shati we malaya!"

"Nanimalaya? Malaya mama yako aliyekuzaa akakutupa jalalani mwanahizayamkubwa nipatie jembe langu!" binti naye alijibu mapigo kwa sautikali.

Pasipokutegemea alivamiwa na kuchabangwa teke tumboni kwanguvu, akajipindua na kuanza kuugulia maumivu. Tambala lililokuwalinamuhifadhi likakosa umakini, chupi yake ambayo zamani ilikuwanyeupe lakini sasa ikiwa kama ina kutu ilichungulia nje. Mbavu zakezilizohesabika kutokana na wembamba zilitokeza nje.

Yule mhanga wakuchaniwa shati akiwa hajaridhika na pigo lile alimrukia tenaakamchabanga teke kali katika zile mbavu zilizokuwa nje kimakosa,sasa binti akanyoosha mikono kuomba msamaha huku maumivu yakiukunjauso wake.
Hakuupata msamaha bali kukaribisha kipigo kingine.Tumboni tena!
"Mariaa! Mariaa!" sauti ilisikika kutokeakatika ule moshi mzito.

Maria aliyekuwa amekumbatia uchafu wajalalani alisikia lakini hakuweza kugeuka. Mbavu zilikuwa zinamuumana alipumua kwa shida sana.

Vishindo vya miguu vikafika karibuyake.
"Kwanini unampiga?
"Kwanini unampiga?"sauti ya kitoto ililalamika kwa uchungu.
"Kwani na wewe dogounasemaje?" alijibu kwa ubabe na jeuri yule mhanga wa kuchaniwashati.
Maria alisikia kila kitu lakini hakuweza kuongea. Alitamaniyule mtoto angekuwa mtu mzima huenda angemsaidia.
Yule kijanaambaye alikuwa kama amepandwa na mori ya kimasai, alijitazama tenashati lake lililoachana, hasira ikapanda upya!

Akampuuzia yulemtoto. Akamrukia Maria. Sasa aliamua kutumia mikono.
"Utalipashati langu utalipa we malaya." maneno hayo hayakutoka bure,yalisindikizwa na mdundo wa mapigo ya ngumi na vibao katika uso waMaria, ambaye naye tambala lake lilikuwa limeuacha mwili. Matitimawili madogo yakitazamana na mbingu za bluu.

Hapa likatokea tukiolisirotarajiwa na wote mpiga na mpigwa.
Yule mtoto mwenye umri wamiaka tisa aliyekulia katika kundi maarufu na hatari jijini Mwanza la'watoto wa wakoma' alichomoka mbiombio akamfikia mpigaji.

Kitendocha sekunde tatu hali ikabadilika. Maria akabaki huru, yule mpigajiakatua chini akiwa anagalagala, damu ikiruka kwa fujo mgongoni mwake.Mtoto wa wakoma alikuwa anatoweka kuelekea mashariki.
Wembe wenyemakali ulikuwa umepenya katikati ya mgongo wa yulempigaji.
****
Chumvi chumvi ilipenya katika koo lakealivyojaribu kumeza mate. Akatambua kuwa midomo ilikuwa imepasuka.Mbavu zilikuwa zinauma sana lakini hakuwa na budi kusimama.Akaunganisha tambala lake, kidogo likamstiri. Yule mpigaji hakuwepotena eneo lile. Zilisalia damu nzito pale ardhini.

Maria alibakikatika sintofahamu, hakujua ni kwa namna gani yule mtoto alimuokoa.Sasa alikuwa amesimama wima, mwili wote ukiwa unauma na giza lilikuwalimeanza kutanda.

Upepo uliokuwa unavuma kutokea jalalani, jaamaarufu la 'mchafu kuoga' jijini Mwanza. Uliileta harufu mbaya katikapua zake.
Kwa mara ya kwanza katika maisha yake akajuta kuzaliwa.Akaupata ukiwa maradufu, ukiwa wa kutengwa na dunia
Taswira yamama yake mzazi ikakimeza kichwa chake, japo alilelewa naye kwakipindi kifupi lakini anakumbuka amani aliyokuwanayo kwa kuyapatamalezi yale bora.

Akiwa na miaka tisa pekee, mama yake (MamaMaria) baada ya kutoka masomoni katika chuo cha Kigurunyembe Morogoroanapatwa na maswaibu ya kuchekesha, baada ya kuyakwepa magari mjiniMorogoro na jijini Dar es salaam alipokwenda katika mafunzo yavitendo. Anakuja kugongwa na baiskeli mjini Singida. Aliyemgonga nimwanamke. Badala ya kukasirika mama Maria alicheka.
Alicheka maanahakuumia!

Hata alivyomsimulia mumewe na mtoto wao wa pekee Maria.Wote walimcheka na kumtania!!
Siku iliyofuata hakuwezakuamka!

Mguu ulikuwa umevimba! Mguu ule uliogongwa nabaiskeli.
Baba Maria alishangaa. Maria alikuwa shuleni wakatihuo!
Kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo mguu ulizidikuvimba!
Huduma za hospitali zikahitajika.
Akakimbizwaupesi.

Ile tamthilia ya kuchekesha iliyoanzia kwa kugongwa nabaiskeli, ikamalizikia kwa huzuni kuu. Mama Maria akaaga dunia hatakabla hajafika hospitali.

Maria alimngojea mama yake aendekumchukua shuleni lakini hakutokea! Siku hiyo akajiunga na rafikizake wakarejea nyumbani ambapo alikuta kundi la watu
Wengi wakiwawameizunguka nyumba yao. Ulikuwa msiba!
Maria akiwa na miaka kumina tatu akabakiwa na malezi ya baba pekee baada ya kuwa amerushaudongo kumfukia mama yake kaburini.

Mzee Paul alivyorejea katikabiashara zake. Yule mama aliyemgonga marehemu Mama Maria na hatimayekupoteza uhai kimaajabu akawa haishi kufika pale nyumbani. Wakatimwingine alikuwa akimpeleka Maria shuleni, anampikia chakula.
Baadaya miezi sita, Maria akatambulishwa rasmi kuwa yule ni mama yakempya.
Muuaji wa mama yake sasa anakuwa mama yake!
Angefanyanini angali ni mdogo!
Akakubali!

Mambo yakabadilika, yulemwanamke akaanza manyanyaso kwa Maria. Akamfanyisha kazi nzitokumzidi.
Cha ajabu mzee Paul hakujali.

Baada ya kuyazoea yalemanyanyaso. Miaka miwili baadaye alikuja mgeni ambaye Mariaalitmbulishwa kama kaka yake.
Hili nalo hakupinga walahakuuliza!

Ule ukaka ukawa na utata ndani yake.
Mara leoanamtekenya, mara amkumbatie.
Maria hakuwa na pa kulalamika.

Sikumoja walipobaki wawili nyumbani yule kaka akambaka! Kishaakatoweka.
Siku aliyomweleza mama yake wa kambo ndiyo sikualiyofukuzwa nyumbani.
Maajabu! Baba akabariki uamuzi huo!

Mariaakiwa na miaka kumi na tano anapokelewa na mtaa wenye ndugu wachachewasiojali.
Mapokeo hayo mabovu kutoka kwa ndugu anaowafahamuyanamfadhaisha!
Baadaye akiwa kwa shangazi yake anagundulika kuwani mjamzito. Hakuna aliyetaka kumsikiliza, akalazimishwa kurudinyumbani kwa baba yake.

Akarejea kwa shingo upande. Siku hiyoaliyofika hakukuta mtu lakini funguo ulikuwa juu ya mlango. Mariaakafungua na kuzama ndani!

Akapokelewa na fungu la pesa katikameza ya kulia chakula. Akili ikakimbia maili mia mbele. Akawaza juuya kutoa mimba, alihitaji pesa, kama vile kunguru anyakuapo vifarangandiyo naye alivyonyakua zile pesa zilizokuwa zimeigandamiza karatasi,yenye maandishi.

Laiti kama angefikiria walau kuisoma ile barua,angegundua kuwa baba yake amejirudi anamtafta yeye (Maria) kwa udi nauvumba na barua ile ilikuwa ya kumfukuza yule mwanamke mwenye rohombaya!
Na zile zilikuwa pesa kwa ajili yake.
Mariahakuisoma

Laiti angeisoma asingefikia pale ambapoalifikia!!


***

Doreen alilipokea tatizo la Mariakama la kwake. Ni msichana huyu pekee ambaye Maria alikuwa anamuaminikati ya rafiki zake. Kwa kuwa pesa likuwepo kila kitukingewezekana.
Vyuma vikapenya katikati ya miguu ya Maria, matusiya nguoni mfululizo kutoka kwa daktari mwenye kipara ambaye tayarialikuwa amepokea shilingi elfu hamsini kwa ajili ya kufanya dhambihii ya utoaji mimba. Hatimaye mabonge mabonge ya damu yaliyoanzakujikusanya katika mji wa uzazi wa Maria yakaharibiwa maksudi, mimbaikawa imetolewa kwa uchungu mkubwa.

Ni Doreen aliyemshawishiMaria kukimbilia jiji la Mwanza kutafuta maisha. Maria hakufikirimara mbili akakubali.
Huku akapokelewa na mtaa, mtaa ukamsulubu nasasa amepigwa vibaya na chokoraa wa kiarabu, amevimbausoni.
Anamkumbuka mama yake mzazi.
Anamkumbuka mamaMaria.
Nani kama mama???

***MARIA ametengwa na dunia sasaameangukia mtaani…mtaa unamsulubu!!! Nini hatma yake??
***Je!!Nini kitaendelea katika RIWAYA hii ya CHOKORAA!!!


culbby mlyn Analyse princetx slim5 MUSSOLIN ram Angelicious showtie Ngoami amina mabata Moderator binti kiziwi Nicas Mtei korino Sukula aniceth mzahula Khantwe kelcie Meljons
 
SEHEMU YA PILI


RIWAYA: CHOKORAA

MTUNZI: George IronMosenya


SEHEMU YA PILI
Vyuma vikapenya katikati ya miguu ya Maria, matusi ya nguoni mfululizo kutoka kwa daktari mwenye kipara ambaye tayari alikuwa amepokea shilingi elfu hamsini kwa ajili ya kufanya dhambi hii ya utoaji mimba. Hatimaye mabonge mabonge ya damu yaliyoanza kujikusanya katika mji wa uzazi wa Maria yakaharibiwa maksudi, mimba ikawa imetolewa kwauchungu mkubwa.

Ni Doreen aliyemshawishi Maria kukimbilia jijila Mwanza kutafuta maisha. Maria hakufikiri mara mbili akakubali.
Huku akapokelewa na mtaa, mtaa ukamsulubu na sasaamepigwa vibaya na chokoraa wa kiarabu, amevimba usoni.
Anamkumbukamama yake mzazi.
Anamkumbuka mama Maria.
Nani kamamama???

*******
Baridi kali iliyoambatana na upepo mkali ilimuhangaisha sana binti ambaye alikuwa akishangaa huku na kule kuthibitisha kuwa ni mgeni katika jiji hil ambalo lna baridi kali likiambatana na jiji la Arusha.
Mama aliyekuwa anamuongozaalikuwa amejikita katika mazungumzo na mwanamke mwenzake, waliongeakinyakyusa huku wakigongesha mikono yao kuonesha kuwa ni marafiki wasiku nyingi.
"Maria!" aliita kwa sauti ya juu kidogo yulemama.
"He! Kumbe anaitwa Maria!! Jina la mama yangu hilo."
Mariaakiwa anasulubiwa na baridi alijongea huku akiwa anatetemeka.
"Shkamoo mama." Alisalimia kwa nidhamu lakinihakujibiwa.
"Maria! Huyu ndiye bosi wako sawa. Nimekutoa Dar kwaajili ya kufanya kazi sawa!! Usilete mchezo kabisa." Mwenyeji waMaria alimpa mawaidha mbele ya yule mama wa kinyakyusa aliyefahamikakwa jina la mama Atuganile na ofisi yake iliitwa ‘mama Atumgahawa'.
Maria kwa mara ya kwanza akawa pekee tena katika jijila Mbeya. Maeneo ya Sai.
Alimshukuru yule mama aliyempeleka Mbeyabaada ya kumpa hifadhi ya muda jijini Dar es salaam baada ya mkasa wakupigwa na mtoto chokoraa wa kiarabu.
Maria alimchukulia yule mamakama Mungu wake wa hapa duniani!!
Hakujua siri iliyoposirini!!

Siku hiyo alionyeshwa mahala pake pa kulala.
Alistaajabu lakini hakusema.
Ilikuwa ni lazima angoje mpakashughuli za mgahawa zimalizike ndipo apangue mabenchi yaliyopo palendani ndipo aweze kulala. Alistaajabu kidogo kwa kuwa aliwahi kulalanje mara kwa mara jijini Mwanza akiwa chokoraa. Alinyeshewa mvua nakuumwa mbu.
Kilichomstaajabisha kwa huko Mbeya ni ile hali ya hewaya ubaridi kisha anakabidhiwa upande wa kanga kwa ajili yakujifunika.
Laiti mama yangu angekuwa hai…!!! Aliwaza Maria.Maisha yakaendelea.
Shughuli za mgahawani zilikuwa na sulubalakini haikuwa tatizo kwa Maria maana mwili wake uliyazoea maishayale.

Ilikuwa siku ya jumapili usiku wa saa mbili! Kwa kawaidasiku kama hii mama Atuganile huwa na kawaida ya kutofungua mgahawa.Kwani ni siku yake ya kuabudu. Siku ya jumapili hutumika kwa ajili yamaandalizi.
"Unapafahamu Uyole?" mama Atu alimuuliza Maria.Akapata jawabu kuwa Maria hapafahamu.
Mama Atu akamuelekeza Mariamagari ya kupanda na wapi ashuke ili aweze kufikisha mzigo atakaompa.Maria alitaka kupingana na mama yule kisa ni usiku lakini akakumbukakuwa pale hayupo kwa mama yake mzazi. Akatii!!
Akapewa maelekezopamoja na bahasha!! Akatoweka.
Ndani ya dakika ishirini tayarikipanya kilikuwa kimezima injini maeneo ya Uyole.
Kamaalivyoelekezwa akiwa na bahasha yake mkononi alivuka barabara nakulifikia duka. Hapo akapokelewa na mtoto wa kiume. Huyu ndiyealiyempeleka huko panapotakiwa.
Akaingia mlangoukafungwa!!!
Mwanaume mwenye umri wa miaka zaidi ya thelathiniakaachia tabasamu hafifu. Maria akashangaa na kumsalimia.Hakujibiwa!
Akampatia ile bahasha, ikapokelewa.
Hata haikusomwasana. Ikawekwa chini.
"Karibu!." Sauti ikamtoka yule bwana,sauti nyembamba tofauti na umbo lake.
"Mama amenituma nikuleteehiyo." Alijibu kwa hofu huku machale yakianza kumcheza.
Yulebwana badala ya kujibu. Akachukua simu yake akabonyeza namba kadhaakisha akasikiliza.
"Nipo naye tayari amefika. Umemueleza kilakitu?"
Akatulia upande wa pili ukajibu kwa kirefu. Kisha akakatasimu na kuirejesha mezani.
Kwa hatua za kunyemelea akaanzakumsogelea Maria. Maria akaanza kurudi nyuma lakini chumba kilikuwakidogo. Akaufikia ukuta. Akagota hapo. Akanyoosha mikono kama anatakakumzuia.
Lishe haikuwa nzuri na Maria alikuwa amedhoofu. Hivyoalijikuta katika mikono imara ya dude nene lenye sautinyembamba.
Maria akabakwa kwa mara ya pili!!
Tena siku hii hadiasubuhi!!
Kilio kikawa ndugu yake Maria. Akatamani asirudi kwamama Atu lakini ni huyo pekee aliyekuwa ndugu yake. Maria binti mdogokabisa akafunika kombe ili mwanaharamu apite. Akarejea kwa mamaAtu.
Yule bwana alimpatia shilingi elfu tano kama ujiraalioupunguza makali nakumwambia Maria ile ilikuwa nauli. Piaalimnunulia nguo mpya. Wakati anamuaga alimuita ‘mpenzi.
Mariaakajisikia kupasuka!!
Miaka kumi na mitano, suluba zaidi yamaelezo!!

Aliporejea kwa yule mama hakusema neno. Akaingiakazini moja kwa moja. Akili ikiwa haijui ni maamuzi gani sahihiyanahitajika.
Kabla akili fupi na change ya Maria haijajua ninicha kufanya. Lile tukio lilijirudia. Safari hii alinunuliwaviatu.
Bwana alikuwa yuleyule. Siku hii wakiwa wanakunywa supualimtamkia kuwa alikuwa anataka kumuoa.
Kero nyingine!! Mariaakachukizwa na unyanyasaji huo.
Katika jiji geni masikioni mwake.Maria akatamani kurejea maisha ya uchokoraa kupambana na watotowenzake katika soko la kuuza vyuma chakavu kuliko kudhalilika namnahii.
Wazo lake likawa limekuja wakati muafaka. Yule mama mbayaaliyemuuza kwa bwana mnene mwenye sauti ya kike alijisahau siku hiiakaacha kiboksi chake cha kutunzia pesa akawapelekea chakula mafundiwaliokuwa wanajenga kanisa maeneo ya Ilomba jirani na Sai jijiniMbeya.
Akili ya Maria ikamkumbusha lile fungu alilolitwaa nyumbanikwa baba yake. Akafanya kama alivyofanya mjini Singida.
Akaibukana pesa zote zilizokuwa katika kisanduku kile.
Siku iliyofuataakiwa ndani ya gari ndipo aihesabu na kugundua alikuwa ameondoka nashilingi elfu tisini za mama mbaya.
MamaAtuganile!!

*****

Aliupita mji uliomlea wa Singida kamavile hauoni. Hakutaka hata kushuka wala kula chochote kinachouzwapale. Alikuwa ameuchukia mji huo.
Aliendelea kuwa mtulivu hadijiji lilipompokea tena. Jiji la Mwanza.
Siku aliyofika alilalanymba za kulala wageni. Kwa mara ya kwanza pia.
Asubuhi aliamkaakijisikia amani sana. Akamkumbuka Douglasi ambaye walizoea kumuitadogolasi. Huyu ni yule mtoto ambaye alimsaidia kwa kumchana na wembeyule chokoraa wa kiarabu ambaye alikuwa anampiga pasipokuwa namakosa.
Alijua wapi pa kumpata na hakika alimpata.
Baridi laMbeya na makombo ya chakula cha mama Atu kiasi yalikuwa yamembadiliMaria na kumng'arisha lakini bado alibakia kuwa chokoraa.
Dogolasialikuwa dhaifu sana, ni kama hakuwa amepata chakula kwa siku mbili autatu. Midomo yake ilikuwa imepauka na mwili ukiwa umelegea. Mariaalimnyemelea akamfumba macho.
Dogolasi alitamani kuongea lakinikoo lilikuwa limekauka.
Maria akamwachia dogolasi akageuka.
Mariaakamkumbatia kwa nguvu dogolasi. Wakajikuta wote wanalia.
"DaMaria sijala tangu juzi….halafu walinipiga wenzangu…da Mariaa…."Dogolasi alishindwa kuendelea kuongea donge la uchungu likamkabakooni. Akalia kwa uchungu. Maria naye akalia. Kilio cha Dogolasikilimkumbusha siku ile ananyanyaswa na yule mwarabu, Dogolasi aliliakwa sauti kama anayoisikia hapa. Ilimuuma!!
Laiti mama yanguangekuwepo ningemwambia amchukue huyu awe mdogo wangu!! AlijiwaziaMaria. Akamchukulia Dogolasi kama mdogo wake!!
Baada ya wotekumaliza kuyafuta machozi yao. Maria alimshika mkono Dogolasiwakaenda gengeni kupata chakula. Walau sasa yule mtoto mdogo ambayehajulikani kama alitupwa na mamaye ama alizaliwa na mtaa aliwezakutabasamu.

Kile kilio alicholia Douglas kilikuwa na mengindani yake. Haikuwa njaa tu bali yalikuwemo na mengine.
Japokuwaulikuwa umepita mwezi tangu amchane yule mwarabu koko na wembe. Kunajambo lilikuwa linaendelea.
Yule mwarabu alimsaka na kumkamatayule mtoto wa wakoma. Safari hii hakupata nafasi ya kutumia wembewake tena. Adhabu yake ikawa adhabu asiyostahili kuibeba mwanadamu wakawaida aliyezaliwa na mwanamke anayeshika uchungu.
Adhabu ambayoilitendwa na wengine na sasa wanatumikia kifungo cha maishajela.
Ulawiti!!
Yule mwarabu na kundi lake walifanya kisasi chanamna hii kwa yule mtoto aliyemchana na wembe ili kumuokoaMaria.
"Mpaka umlete yule Malaya ndipo tunaacha!!" alitoakaripio hilo yule mwarabu baada ya kumaliza kumtesa yulemtoto.
Adhabu ile ilichangia kumuathiri Douglas.
Walimfanyievile mara kwa mara. Angeshtaki wapi wakati mtaa ndiyo mzazi wake namzazi huyu haongei!!
Angefanya nini chokoraa huyu!!!

Sasa amekutana na Maria. Douglass aanachukua maamuzi magumu. Akiwa na miaka tisa anaamua kuitetea nafsi yake.
Anakusudia kumtoa muhangaMaria ili waache kumlawiti!!
Anaamua kufanya usaliti huuusiku!!
Majira ya saa nne Douglass moyo ukimuuma kabisa anawasili katika kijiwe cha akina mwarabu koko. Anajisikia mdomo mzito kusema lakini anajikaza. Anajaribu tena machozi yanamtoka. Picha ya Mariaakinyanyaswa na wahuni hao inajijenga usoni pake!!

***Je?Dogolasi (Douglas) atamuuza Maria!! Ama ataendelea kutumikia adhabu!!
***Nini hatma ya CHOKORAA HAWA….

culbby mlyn Analyse princetx slim5 MUSSOLIN ram Angelicious showtie Ngoami amina mabata binti kiziwi Nicas Mtei korino Sukula aniceth mzahula Khantwe kelcie Meljons Washawasha
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA TATU

MTUNZI: George IronMosenya


SEHEMU YA TATU
Yule mwarabu na kundi lake walifanya kisasi cha namna hii kwa yule mtoto aliyemchana na wembe ili kumuokoa Maria.
"Mpaka umlete yule Malaya ndipo tunaacha!!" alitoa karipio hilo yule mwarabu baada yakumaliza kumtesa yule mtoto.
Adhabu ile ilichangia kumuathiriDouglas.
Walimfanyie vile mara kwa mara. Angeshtaki wapi wakatimtaa ndiyo mzazi wake na mzazi huyu haongei!!
Angefanya ninichokoraa huyu!!!
Sasa amekutana na Maria. Douglass aanachukuamaamuzi magumu. Akiwa na miaka tisa anaamua kuitetea nafsiyake.
Anakusudia kumtoa muhanga Maria ili waache kumlawiti!!
Anaamua kufanya usaliti huu usiku!!
Majira ya saa nne Douglass moyo ukimuuma kabisa anawasili katika kijiwe cha akina mwarabu koko. Anajisikia mdomo mzito kusema lakini anajikaza. Anajaribu tena machozi yanamtoka. Picha ya Maria akinyanyaswa na wahuni hao inajijenga usoni pake!!

Dogolasi hatimaye aliweza kutamka. Akawaeleza juu ya uwepo wa Maria.
"Ole wako uweunatudanganya!"
"Siwadanganyi yupo amelala pale nyuma."
Wanaume watatu wakasimama wakiongozana na Douglasi.
"Nipale hivi sitaki anione mimi." Alitoa maelekezo huku HATIAikimshambulia kwa hatua ya kumuuza Maria. Alikuwa anbatetemeka nakujihisi msaliti.
Akayakumbuka mafundisho aliyokuwa anayapatakanisani wakati akiutafuta ubatizo wake. Akamkumbuka Yuda Iskaliotiyule aliyemsaliti Yesu. Douglasi akajiinamia na kuanza kulia baada yakumsikia Maria akipiga mayowe ya kuomba msaada na baada ya muda akawakimya.
Wanamuua!! Aliwaza Douglasi na ghafla akajikuta akipandwana maruhani ya maajabu. Akajisikia ana nguvu sana. Akazamisha mkonowake katika pindo la nguo yake. Akachomoka na kisu ambacho ni maalumukwa ajili ya tohara ya wanaume. Akazama katika kaputula yake akaibukana wembe mpya.
Akatimua mbio, akiruka mashimo mawili matatu.Akalifikia eneo la tukio.
Akakuta tukio likiwa linaendelea. Mariaalikuwa mikononi mwa wanaume watatu. Wawili wamemshika kikamilifu nakumziba mdomo. Mwingine mmoja alikuwa anambaka. Na wale wenginewalikuwa watupu katika maandalizi ya kumbaka tena na tenaMaria.
Hakujali kama yeye ni mdogo. Akaruka akatua kwa yulealiyekuwa juu ya Maria. Kisu cha kutahiria kikakwangua sikio lakeakaruka maili kadhaa mbele akabiringita mbali na mwili waMaria.
Mmoja aliyekuwa anashangaa bila kujua nini kinaendeleaaligutushwa na na ubaridi usoni pake. Halafu yakafuata maumivumakali. Akapiga yowe. Alikuwa amechanwa na wembe mkaliusoni.
Mwanaume wa tatu akawa mwepesi akajirusha pembeni. Kishaakamvaa Douglasi akampiga teke. Katoto haka kadogo kakaanguka mbalihuku kanalia.
Yule aliyechanwa sikio akamalizia filamu hii yamapigano. Wanaume watatu waliobalehe dhidi ya mtoto mdogo kabisaanayehitaji malezi ya baba na mama na jamii kwa ujumla.

Maria alirejewa na fahamu majira ya saa kumi na moja alfajiri akiwa namaumivu makali sana katika mwili mzima. Alikumbuka kuwa alibakwa nawanaume wengi hakumbuki walijirudia mara ngapi ngapi. Akauma menoyake kwa hasira! Akasimama akashangaa watu wale hawakuchukua pesayake . Maajabu!!
Akajikongoja baada ya kujifuta damu kidogoiliyokuwa inatiririka.
Douglass!! Jina hilo lilishambulia kichwachake kama vile lilingoja asimame!!
Maria akajiuliza huyu mtotomdogo yupo wapi. Na alikuwa wapi wakati anatendewa unyama ule.Hakupata jawabu hilo hadi asubuhi inavyosambaa taarifa ya chokoraaaliyekutwa amekufa katika jalala.
Maria aliyaunganisha meno yakealipomtambua Douglas akiwa ni maiti. Huku akiwa amejeruhiwa sana.Zaidi ya kipigo alichopokea alikuwa amelawitiwa pia.
Machoziyakamtoka!!
Douglas akaiaga dunia akiwa chokoraa, alikufaakijaribu kumuokoa Maria. Anakufa bila kuwa na ndugu.
Halmashauriya wilaya ya Ilemela ikachukua jukumu la kuuzika mwili katika namnaya kuufukia na kuusahau.
Hakuna hatua zozote za upelelezizilizochukuliwa. Douglas akasahaulika rasmi katika mlolongo wamachokoraa, Douglas akafuta katika simulizi yetu.

Mnyongemnyongeni lakini haki yake mpeni!
Msemo huu ulichukua nafasikatika nafsi ya Mariam. Punde tu baada ya mwili wa Douglas kupatikanaakiwa mfu. Mnyonge huyu hakuwa amepewa haki yake hata kidogo.
Hatamimi sitatendewa haki yangu! Hata mimi naonewa na nitakufa nitazikwakama mzoga wa mbwa!
Hasira zikamkaba Maria. Akaamua kuwa kamaatazikwa kama mbwa basi lazima aishi kama mbwa. Tena mbwa mwenyeukichaa.

Baada ya wiki moja. Maria mwenye hasira na chuki.Aliyeamua kuwa mbwa.
Anakutana na chokoraa wanaojaribu kuishi kamawafalme katika ngome ya uchokoraa. Waliomchukulia yeye kuwa swalaambaye huonewa na wanyama pori wote.
Ilikuwa saa nane usiku.Akasikia ubaridi ukipenya katika mapaja yake. Kisha akazibwamdomo.
Maria aliyekuwa amejifika umbwa kichaa. Akaijiwa na fahamu.Akafumbua macho. Akakuta nguo yake inamaliza kutolewa.
Akapandishakichaa chake cha kupinga unyanyasaji.
Hatimaye ile siku ya kufanyaumbwa kichaa kwa vitendo ikawa imewadia.
Akapapasa bila kuletavurugu. Akakikamata kisu kikali ambacho tangu kinolewe hakikuwahikufanya kazi.
Sura iliyokuwa gizani ikamsogelea. Akasikiaanapapaswa zaidi. Walikuwa watatu!!!
"Tulia hivyo hivyo ukiletafujo tunakufanya kama mdogo wako." Sauti ilimuamrisha.
AkamkumbukaDouglas. Kumbe aliuwawa na watu hawa! Basi ni hawa walinibaka!Aliwaza Maria. Hasira zikamchemka kichwani.
Hasira zikampandazikiambatana na kichaa cha mbwa alichojipandikiza makusudi.
Yulealiyemtishia kisu alikuwa wima, mbali na yeye.
Hivyo hakumtisha.Yule mwarabu koko alipoanza kumbaka. Alijikuta akipiga kelele kuu.
Kelele ya kutisha. Jisu kubwa kali. Lilipennya katika kitovuchake. Kisha likachomoka kama vile halikuwa limetenda jambo lolote.Ile rangi ya kung'aa haikuwepo lilikuwa jekundu.
Mbwa huyumwenye kichaa bila uoga akamrukia yule bwana mwenye kisu kidogo. Jisulililokuwa na damu likapenya sehemu zake za siri barabara. Akapigakelele moja kuu akaanguka chini.
Mmoja akafanikiwa kukimbia lakinimbwa mwenye kichaa anayeitwa Maria alikuwa nyuma yake. Alipojikwaa tu. Mbwa akawa juu yake. Mbwa akaanza kushambulia kwa kisu. Picha ya Douglas akiwa mfu jalalani ikamjia Maria akazidi kuchoma nakuchomoa.
Ilikuwa afadhali kwa wale wawili wa awali huendawalipoteza uhai katika namna ya maumivu ya mara moja.
Huyu wamwisho roho yake huenda hata haikuweza kuzifikia mbingu salama.
Jisulilizama na kuchomoka, likazama tena na kuchomoka.
Hadi wotewawili walipotulia.

Maiti tatu asubuhi na muhusika mwingine aliyedhaniwa amekufa anazinduka akiwa na pingu, hospitali.
Huyualikuwa ni mbwa mwenye kichaa cha chuki. Chokoraa wa kike,Maria!!
Alilala akiwa na chuki na kisasi na sasa anaamka akikabiliwa na kesi ya mauaji. Mauaji ya watu wanne.Akashangaa!!
Watatu kwa usiku mmoja na akarushiwa kesi ya kumuuaDouglas.
Vipi kuhusu kumlawiti sasa? Au na ulawiti alifanyaMaria!!! Kichekesho lakini serikali ikajifanya haijui kujibu maswali.Ikasema sheria itachukua mkondo wake.

Hawakuwepo wazazi walandugu wa marehemu hawa wanne kusikiliza kesi. Hivyo Maria akawaameshtakiwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Bila kuwa namtetezi.
"Bi. Maria Paul. Mwenye umri wa miaka ishirini na moja anahukumiwa …….." kimya kikali kikatawala kisha yule jaji bilakumtazama Maria usoni alivunja KALAMU NYEKUNDU.
Hii ikimaanisha kuwa amehukumiwa hukumu ya kunyongwa ama maisha yake yote kumalizikia gerezani. Labda utokee msamaha wa raisi. Lakini msamaha wa raisihauendi kwa yatima kama yeye. Na wenyewe pia mpaka kujuana.
Alitamani kujitetea kuwa alikuwa na miaka kumi na tano lakini vifungu vyasheria asivyovijua vikambana. Akawa kimya. Hadi mahakama ilipohairishwa na yeye kutupwa gerezani.
Mnyonge mnyongeni lakinihaki yake mpeni!! Alisikia kauli hizi kutoka kwa baadhi ya watuwaliohudhuria mahakamani. Akainama chini akadondosha chozi.

***MARIA licha ya kuteseka mtaani bado mtaa unamuhukumu..sasa anaenda kutumikia kifungo cha maisha/kunyongwa. Je ndiyo mwisho wa CHOKORAAHUYU.



culbby mlyn Analyse princetx slim5 MUSSOLIN ram Angelicious showtie Ngoami amina mabata binti kiziwi Nicas Mtei korino Sukula aniceth mzahula Khantwe kelcie Meljons Washawasha
 
SEHEMU YA NNE
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya


SEHEMU YA NNE


Hawakuwepo wazazi wala ndugu wa marehemu hawa wanne kusikiliza kesi. Hivyo Maria akawa ameshtakiwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Bila kuwa na mtetezi.
"Bi. Maria Paul. Mwenye umri wa miaka ishirini na moja anahukumiwa …….." kimya kikali kikatawala kisha yule jaji bila kumtazama Maria usoni alivunja KALAMU NYEKUNDU.
Hii ikimaanisha kuwa amehukumiwa hukumu ya kunyongwa ama maisha yake yote kumalizikia gerezani. Labda utokee msamaha wa raisi. Lakini msamaha wa raisi hauendi kwa yatima kama yeye. Na wenyewe pia mpaka kujuana.
Alitamani kujitetea kuwa alikuwa na miaka kumi na tano lakini vifungu vya sheria asivyovijua vikambana. Akawa kimya. Hadi mahakama ilipohairishwa na yeye kutupwa gerezani.
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni!! Alisikia kauli hizi kutoka kwa baadhi ya watu waliohudhuria mahakamani. Akainama chini akadondosha chozi.


******


Katika uzio huu wanawake wenye nguo tofauti kabisa na wengine walikuwa wamejikita katika kumzongazonga mwenzao ambaye zile nguo zilikuwa zimempwaya, alivutwa mithili ya mwivi anayekaribia kuadhibiwa. Baadaye alitokeza mwanamke mmoj mnene aliyekuwa anatembea kifua mbele kama mwanaume anayefanya mazoezi ya kunyanyua vyuma. Taratibu lile kundi likamuachia yule msichana.
Mama mnene akafika akamchukua. Haya yote yalikuwa yanatokea gerezani na Maria kwa mara ya kwanza alikuwa ameupoteza uhuru wake.
Gereza la Keko jijini Dar es salaam liliukwapua uhuru wake.
Wafungwa wanaohukumiwa kifungo cha kunyongwa wawapo gerezani huishi peke yao kwa kutengwa, hwajichanganyi na wafungwa wengine. Wafungwa hawa ambao wanangojea kitanzi hawafanyishwi kazi ngumu. Kazi kubwa wanazofanya ni kusafisha mahali pao pa kulala. Kwa upande wa wanaume waliona bila kujali lolote maana walikuwa wafu watarajiwa na walijua kuwa ni lazima watakufa.
Kila mahali kuna mtemi gerezani. Na upande huu wa wanawake wanaongoja kitanzi alikuwepo Mamamia, huyu ndiye alikuwa anatetemesha selo nzima ya wanawake wanaongojea kitanzi. Ni huyu ambaye bila kusema neno alipotokea tu kila mtu akakaa mbali na Maria.
Waliufahamu undava wa mwanamama huyo. Na pia walijua kuwa kila mgeni anayepokelewa pale gerezani alikuwa haki ya Mamamia kumfanya mke.
Ilikuwa hivyo pia kwa Maria. Mamamia aliondoka naye hadi katika chumba kizuri. Akakaribishwa.
Maisha yakaanzia hapo!! Kule kubakwa mtaani kukahamia huku gerezani. Lakini huku alifanywa mke wa mwanamke mwenzake.
Hapo sasa hakuwa na ujanja japo alikuwa anaumizwa sana na hali ile lakini wakati mwingine alijipa moyo kuwa muda wowote ule atakufa hivyo hakuna harakati zaidi anaweza kufanya kujitoa katika janga hilo.
Baada ya mwezi mzima afya yake ikabadilika. Mume wake wa gerezani alikuwa wa kwanza kugundua.
Mamamia alikuwa mtulivu sana siku hii, alimuita Maria baada ya kuwa wamepata chakula. Maria akadhani kuna mahali amefanya makosa, maana Mamamia alikuwa ana wivu sana kwa wafungwa wenzake.
"Una miaka mingapi Maria."
"Kumi na tano mama nakaribia kumi na sita." Alijibu kwa upole.
"Ulikuwaje ukafika huku mbona u mdogo sana."
Maria akaweka kimya kirefu kisha akajieleza kwa urefu huku akiwa ameinama. Machozi yakiwa yanamtoka na kilio cha kwikwi kikiyaingilia maongezi yake.
Alipomaliza na kuunyanyua uso wake. Alimkuta yule mama analia kwa uchungu. Wakakumbatiana!! Bila kusema lolote kisha wakaachiana.
"Maria ulipobakwa mara ya pili wamekupa mimba tena." Mamamia alimwambia Maria. Maria akakodoa macho yake kumtazama Mamamia. Hakuamini alichokisikia, lakini Mamamia alimaanisha alichokiongea.
Mama huyu mnene alisimama tena akamsogelea Maria akamgongagonga mgongoni. Akamtia moyo.
Kuanzia siku hiyo Mamamia akaacha rasmi suala la kujifanya mume wa Maria na badala yake akauvaa umama Maria.
Akaanza kumpa huduma zote Maria anazoweza kumpatia.
Zilizoshindikana akawa anamshirikisha mkuu wa gereza ambaye alikuwa anawatembelea mara kwa mara.
Miezi mitano ikakatika. Maria akiendelea kuitunza mimba yake kwa uangalizi wa Mamamia.
Asubuhi moja Maria alipokea ujumbe kutoka kwa mwanamke mmoja kati ya ishirini waliokuwa wanangoja kitanzi. Mamamia alikuwa anamuhitaji. Ujumbe ule ulimshangaza. Ni kwanini Mamamia anaagiza mtu amuite wakati anajua kuwa anaumwa tumbo? Hakuleta ubishi alisimama na kuelekea eneo husika.
Nondo zikawatenganisha. Mamamia alikuwa anatokwa jasho jingi na alikuwa anatetemeka.
"Maria mwanangu! Naenda kanisani." Alianza kujieleza Mamamia. Maria hakuelewa, kanisa liliwezaje kumtoa jasho na kumfanya atetemeke.
Mamamia alipoona Maria haelewi aliendelea. "Naenda kujikabidhi kwa Mungu aliyetuumba mimi, wewe na wao, akawapa madaraka wanadamu watutawale. Kisha akawaweka na wengine watuonee, halafu wengine wakayachukua mamlaka ya kujiweka kuwa miungu watu, wakajipa mamlaka ya kuzitwaa roho. Naenda kuungama dhambi zangu niingie katika kitanzi. Nilitamani kuwa nawe hadi nimuone mjukuu wangu lakini wakati umefika." Alizungumza kwa sauti yenye kitetemeshi cha uoga. Maria akatetemeka sana kusikia kitanzi. Tumbo likazidi kumuuma. Akatolewa pale. Akageuka akamwona Mamamia akijilazimisha kutabasamu, kisha akafanya ishara ya msalaba.
Huo ukawa mwisho wa Maria kumtia machoni Mamamia. Mama aliyempokea vibaya kwa kumfanya mke lakini baadaye akageuka kuwa mama mzuri mwenye upendo. Huu ukawa mwanzo wa kuishi maisha ya hofu tena!


Miezi iliyobakia pale gerezani ikamfanya awe kama mpira wa kona. Anawaniwa na kila mmoja. Leo huyu kesho yule. Wote wanamminyaminya hovyo. Hawakuijali mimba yake.
Hata kabla mwezi wa tisa haujatimia vizuri aliushika uchungu.
Wafungwa wakapiga kelele! Msaada ukaletwa!
Maria akaingia kwa mara ya kwanza katika chumba cha wazazi kwa ajili ya kujifungua.
Akiwa na miaka kumi na sita anageuka kuwa mzazi.
Ilikuwa siku ya ijumaa. Akamuita mtoto wake Friday akiamini kuwa ni wa kiume. Akili ilipotulia kapunguza herufi moja.
Mtoto yule wa kike akapewa jina la Frida. Cheti cha kuzaliwa hakikuwa na jina la baba!!
Maria aliishi kwa muda wa siku kumi akimlea Frida.
Kisha akarejea rasmi gerezani. Huko akaendelea kuolewa mara kwa mara na wenzake waliojifanya wababe.
Maria aliruhusiwa kumnyonyesha mwanaye, ambaye sasa alikuwa chumba cha jirani. Wakati mwingine Frida alikuwa analia sana lakini Maria hakuruhusiwa kumuona.


Maisha haya yalienda kwa miaka miwili. Frida akahamishiwa gerezani. Chumba maalumu akawa anaishi na mama yake.
Frida asiyekuwa na kosa lolote akatumikia kifungo na mama yake!!
Alikula alichokula mama yake, alishuhudia jinsi mama yake alivyokuwa akinyanyaswa. Hakuwa na la kufanya mtoto huyu.
Neno lake la kwanza kutamka lilikuwa ‘baba'. Maria alilia sana siku hiyo maana hata hakuwahi kumjua baba mzazi wa mtoto wake. Lakini ule mchanganyiko wa rangi aliokuwanao Frida ulimfanya amuhisi yule mwarabu koko kuwa anahusika!! Lakini haikusaidia kitu kwani alikuwa marehemu tayari.
Wakati akiwa na miaka miwili na nusu Frida. Mama yake aliugua ugonjwa wa ajabu ulimshambulia sehemu za siri. Gereza halikujali.
Aliendelea kuugua huku akiishia kupewa dawa za kutuliza maumivu tu!! Hali ikazidi kuwa mbaya ndipo akapelekwa hospitali.
Kama Mamamia alivyomuita na kumuaga wakati anaelekea kunyongwa ndivyo naye alivyoomba Frida apelekwe hospitali aliyokuwa naugulia.
"Frida hata wewe utakuwa chokoraa kama mama yako." Maria alimwambia mwanaye ambaye hakuwa anaelewa nini kinaendelea.
Siku iliyofuata mapazia yenye rangi za kijani yalizungushwa katika kitanda cha mtoto huyu mwenye mtoto. Hatimaye roho ya Maria ikapumzishwa!!!
Baada ya msoto wa miaka kadhaa na tabu za mtaani kisha mateso ya gerezani hatimaye Maria akafa kishujaa akiwa ameuachia mtaa damu yake!!!
Frida!! Mtoto wa gerezani asiyekuwa na hatia!!


Baada ya mwili wa Frida kufukiwa, hatimaye Frida akachukuliwa na familia ya mkuu wa gereza. Huku akaanzishwa shule ya awali.


Frida hakuwa na marafiki wa karibu. Alikuwa ni mkimya sana. Hakuifurahia shule. Na hakuwa na amani nyumbani alipokuwa anaishi.
Watoto wenzake walimuonea sana. Licha ya kuonewa lakini bado aliadhibiwa kila mara.
Hii ilitokana na yule mkuu wa gereza ambaye walau alikuwa ana huruma kwake kuhamishwa gereza. Sasa alikuwa anakuja nyumbani mara chache. Hakutaka uhamisho wa mapema wa familia yake hivyo waliendelea kuishi palepale.
Mke wa mkuu wa gereza na watoto wake wawili walifanana kimatendo hivyo Frida hakuwa na wa kumtetea.
Akanyanyasika huku anasoma.
Mkuu wa gereza aliporudishwa katika gereza lile tena walau Frida akaanza kuipata amani.
Miaka ikapita. Frida akasoma shule ya jirani katika elimu ya msingi. Frida hakuwa na baba na walizoea kumtania Frida gereza. Hakujali.
Alipomaliza darasa la saba. Tayari alikuwa na miaka kumi na sita.
Mkuu wa gereza mara kwa mara alikuwa anakaa na Frida na kumueleza juu ya maisha ya mama yake ambayo aliyafahamu kwa kumsikiliza mara kwa mara. Alimsisitiza juu ya kusoma kuwa huo ndio ukombozi wake pekee.
Frida aliyasikiliza kwa umakini maneno yale mazito kutoka kwa mkuu wa gereza. Akajikuna kichwa chake na kuyaruhusu yamkae vyema.
Unyanyapaa aliofanyiwa na watoto wa familia ile ya mkuu wa gereza, wanafunzi shuleni. Ilimfanya ajihisi anafanana na marehemu mama yake. Akajiweka makini asije kufa kama mama yake.
Hivyo licha ya kujitambua kuwa kifua chake chenye chuchu ndogo kilikuwa kinawatamanisha wanaume wengi. Hakujiweka karibu nao na hakutaka kuwasikiliza walipojaribu kumtaka kimapenzi.
Wakatio Frida anajilinda na mambo haya. Nyumbani kikazuka kizaazaa.
Mkuu wa gereza alikuwa amesafiri lilipojitokeza jambo hili.
Mtoto wake wa pili na wa mwisho alikuwa amegundulika kuwa ana ujauzito. Ilikuwa ni aibu kubwa kwa mama yule aliyewadekeza watoto wake.
Sasa yalikuwa yamemrudi!!
Frida alizidi kujifunza kupitia tukio hili. Lakini hakujifunza sana kabla kesi haijamgeukia. Mama mwenye nyumb alijua ni jinsi gani mume wake alikuwa mkali sana, alihofia kesi hii inaweza kuhatarisha ndoa ama maisha yake. Akatafuta wa kumuuzia kesi hii akaumiza kichwa. Kisha akajikuta katika orodha likijitokeza jina moja tu. Frida Gereza.
Mama alimuita kwa sauti ya juu. Alipofika akapokelewa na kibao kizito akayumba lakini akawahi kupata muhimili kwa kushika ukuta.
"Nani amempa mimba Jesca?" aliulizwa. Akashangazwa na swali hilo. Akashangaa. Akapokea tena ngumi nzito ya mgongo akapiga kelele.
Hapo sasa akawa amebariki kipigo. Akaanza kushughulikiwa. Kisha akafukuzwa nyumbani pale majira ya saa mbili usiku akiwa anafua nguo zake za shule. Alipewa shilingi elfu mbili aende anapojua.
Frida angeweza vipi kung'ang'ania makazi yasiyokuwa ya kwake? Akaondoka binti huyu ambaye ana kumbukumbu nzuri ya kuambiwa kuwa yeye ni chokoraa na marehemu mama yake.
Sasa akayaamini maneno ya marehemu!! Akaingia katika mtaa ambao hajauzoea na wala hakuwahi kuingia kabla.
Tofauti na mama yake. Frida aliingia akiwa na chuki iliyopitiliza!!
Kisasi kikiwa kimemkaba koo!!
Machozi yakamtoka Frida akalia kwa uchungu sana na kutengeneza picha inayopamba ukurasa wa mbele kabisa wa kitabu cha CHOKORAA.


culbby showtie sam II Washawasha
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha sana maisha wanayoishi watoto hawa wasio na hatia ambao ni matunda ya ME na KE. Imeniumiza.
 
dah! ni shdaa lakn yote ni mapito ya dunia inauma hasa kwa watoto km hawa.
 
SEHEMU YA TANO


RIWAYA: CHOKORAA


MTUNZI: George Iron mosenya


SEHEMU YA TANO

Mama alimuita kwa sauti ya juu. Alipofika akapokelewa na kibao kizito akayumba lakini akawahi kupata muhimili kwa kushika ukuta.
"Nani amempa mimba Jesca?" aliulizwa. Akashangazwa na swali hilo. Akashangaa. Akapokea tena ngumi nzito ya mgongo akapiga kelele.
Hapo sasa akawa amebariki kipigo. Akaanza kushughulikiwa. Kisha akafukuzwa nyumbani pale majira ya saa mbili usiku akiwa anafua nguo zake za shule. Alipewa shilingi elfu mbili aende anapojua.
Frida angeweza vipi kung'ang'ania makazi yasiyokuwa ya kwake? Akaondoka binti huyu ambaye ana kumbukumbu nzuri ya kuambiwa kuwa yeye ni chokoraa na marehemu mama yake.
Sasa akayaamini maneno ya marehemu!! Akaingia katika mtaa ambao hajauzoea na wala hakuwahi kuingia kabla.
Tofauti na mama yake. Frida aliingia akiwa na chuki iliyopitiliza!!
Kisasi kikiwa kimemkaba koo!!
Machozi yakamtoka Frida akalia kwa uchungu sana na kutengeneza picha inayopamba ukurasa wa mbele kabisa wa kitabu cha CHOKORAA.


******


Alipita njia za uchochoro akiwa haoni mbele vizuri. Machozi mazito yalikuwa yameuziba uso wake, alikuwa kama kipofu asiyekuwa na mkongojo wa kumuelekeza vikwazo vilivyopo katika njia.
Alitokea kituo cha mabasi. Hakuwa na uhakika ni wapi anatakiwa kwenda. Mkononi alikuwa na shilingi elfu mbili alizopewa na mama, huku mfukoni akiwa na shilingi mia tano na hamsini iliyosalia kama chenji baada ya kuwa ameagizwa dukani muda mfupi kabla ya kutimuliwa.
Daladala ikapita akajikuta yu ndani tayari.
"Frida Gereza." Alisikia sauti ya kike ikimuita.
Alipogeuka alikutanisha macho na msichana aliyekuwa anatabasamu. Lakini ghafla akakoma kutabasamu baada ya kuyaona macho ya Frida. Mekundu na michirizi ya machozi mashavuni.
Wote walikuwa wamesimama baada ya kukosa nafasi ya kukaa katika basi hili liendalo Mwenge.
"Frida ni nini kibaya." Aliuliza kwa upole. Frida hakumjibu dada huyu ambaye alikuwa ni kiongozi pale shuleni akifahamika zaidi kama ‘dada mkuu'.
Frida hakuweza kujibu. Badala yake machozi yakamtoka maradufu.
"Usilie Frida…haya sikia nikwambie, unashukia wapi mamii"
"Siju…sijuii" alijibu huku analia.
Dada mkuu akatumia busara ambazo zilimuwezesha kuchaguliwa kushika kitengo hicho katika shule hiyo ya msingi. Akachukua kitambaa akamfuta Frida machozi kisha akamnong'oneza jambo. Frida akatulia tuli na hapakuwa na maongezi tena.
Walikuwepo wazazi wa kiume na wa kike katika daladala ile lakini hakuna hata mmoja aliyerjikita katika kulifuatilia tukio hili. Kwa jiji la Dar es salaam hii ni kawaida kabisa, wao wanasema ‘mtoto mtoto wako, mtoto wa mwenzio si wako.' Hivyo Frida Gereza hakuwa akiwahusu hata kidogo.
"Tuache Mwananyamala hospitali." Dda mkuu alimkumbusha kondakta. Kisha akatoa nauli, "kata wawili. Wote wa kusoma." Alipepeta mdomo upesi akatoa nauli na kulipa. Akarejeshewa baki yake.
Gari iliposimama dada mkuu akamvuta mkono Frida aliyekuwa amesinzia huku amesimama. Wakashuka!!
Dada mkuu akatazama pochi yake . kisha akamwongoza Frida katika banda la mama ntilie wa Mwananyamala A karibu na kituo cha polisi.
Akaagiza chakula, wakachangia sahani moja. Pesa yao iliwaruhusu kula hivyo.
Wakagida na maji yasiyochemshwa kisha wakatembea na kupata nafasi ya kukaa katika uwanja ule.
"Haya niambie umekuwaje Gereza?" alianzisha maongezi dada mkuu.
Frida mtoto wa Gereza akavuta pumzi akatazama juu mbinguni kama anayesubiri kushukiwa na roho mtakatifu.
Umbo lake kubwa tofauti na umri wake mdogo lilikuwa limehifadhiwa katika kanga zilizowekwa katika mfumo wa kutanda. Kama mwanamke akiwa msibani.
Kwa sauti ya kunong'oneza akaanza kujieleza. Moja baada ya jingine. Mwanadada jasiri kabisa aliyepewa jina la Mwanaidi alipozaliwa na sasa ni dada mkuu katika shule ya msingi akawa anamsikiliza.
Hatimaye akamaliza!! Mwanaidi akajikuta anatokwa na jasho! Hakujua kama Frida ni yatima tena aliyezaliwa gerezani akizaliwa na mama anayesubiri kunyongwa. Na hatimaye mama huyo akaaga dunia kabla ya kuhukumiwa!!
"Kwa hiyo haujui unapokwenda."
Frida akatikisa kichwa kuashiria anakubali!
"Sasa Frida…kuhusu kulala…..aah! hebu ngoja." Dada mkuu akagundua akili ya Frida bado ilikuwa fupi. Akaamua kumsaidia kufikiri.
"Ubaki hapahapa…nakuja."


Mwanaidi akatoweka. Frida akabaki mpweke na shilingi elfu mbili yake. Alikuwa hana analofikiri zaidi ya kujutia kuzaliwa.
Kwanini mama aliua watu wengi hivyo!! Halafu wanaume!! Frida alijiuliza baada ya kujikuta akimuwazia marehemu Maria. Hakupata majibu mpaka alipoguswa begani.
Mwanaidi alikuwa amerejea.
Akamwongoza hadi katika nyumba ya kiwango cha kawaida. Bati lenye kutu likionekana kwa kumulikwa na taa za nyumba ya jirani. Pale hapakuwa na umeme.
"Utaweza kupanda hapa dirishani!!" alimuuliza Frida kwa sauti ya kunong'oneza.
Frida akakubali kwa kichwa. Mwanaidi akamtazama kwa huruma akidhani Frida ni mtoto wa mama. Kufumba na kufumbua Frida alikuwa amenata katika nondo akingojea maelekezo.
"Ingia taratibu kabisa!!" alinong'ona tena dada mkuu.
Frida akatua ndani kama paka. Hakuna aliyesikia.
Mwanaidi naye akafanya kama Frida. Wakajikuta ndani.
"Frida mdogo wangu leo ulale hapa, kesho tutajua cha kufanya nitakupeleka shuleni sawa." Mwanaidi akawa anabembeleza.
"Mwanaidiii!! Sauti kali iliita.
"Shhhh!! Mama huyo." Mwanaidi alimwambia Frida lakini akiwa anaogopa.
"Frida ingia uvunguni!!"
Frida akazama uvunguni na kukumbana na vumbi kali. Akajikaza.
Mara ghafla mlango wa chumba cha Mwanaidi ukafunguliwa.
"Tangu nikutume ni saa ngapi." Sauti iliuliza kwa shari sana.
"Mama usafiri ulikuwa tatizo!!" alijibu Mwanaidi.
"Malaya wewe….usafiri ulikuwa tatizo.." aliongea kwa kubana pua mwanamke huyo.
Ghafla akamvamia na kuanza kumnasa vibao.
"Joooohn!! Niletee huo mkanda…" alitoa amri kwa sauti kuu.
"Mama nisamehe!!"
Mkanda ukafikishwa na mtoto mdogo. Kichapo kitakatifu kikaanza kushuka. Frida akawa anayasikilizia maumivu huku akiwa uvunguni.
Kosa alilofanya Mwanaidi ni kujaribu kujificha kwa kurukia kitandani. Yule mama mweupe aliyeiharibu ngozi yake kwa mikorogo akamrukia akiwa na nia ya kumkwangua na makucha yake marefu yasiyopendeza.
Kitanda kilichotengenezwa na fundi asiyekuwa makini na kazi yake ama aliyeletewa mbao za kiwango cha chini, kikaitika ‘kaaa!!!' chaga mbili zenye uzito wa ziada zikatua juu ya mwili wa Frida. Hakika aliweza kulivumilia vumbi lakini uzito huu hata ungekuwa wewe msomaji!!
Yowe likatoka!! Yowe kubwa sana. Mwanaidi akaukunja uso wake kuonyesha kuwa amekata tamaa tayari mpango umekuwa batili!! Yule mama wa mikorogo akadhania ni jini ndani ya chumba akatimua mbio, lile giza hakujua anapoelekea akakutana na ukuta. Puu! Akajibamiza akatowa yowe.
Mwanaidi akacheza akili ya upesi akanyanyua chaga Frida aweze kutoka. Akafanikiwa. Lakini aliyeharibu filamu hii na kuirudisha katika majonzi ya awali ni yule mtoto mdogo aliyeagizwa mkanda wa kumuadhibia Mwanaidi.
Aliingia pale chumbani na tochi. Akamulika bila kutarajia. Mama wa mikorogo akaona kitu. Akamuona Frida pale chumbani.
Kanga yake ilikuwa imemtoka na ndani akasalia na kinguo kifupi alichoondoka nacho nyumbani.
Yowe jingine likamtoka!! Sasa baba mwenye nyumba akafika eneo la tukio. Akathibitishiwa kuwa Mwanaidi ni Malaya na siku hiyo alikuwa ammleta Malaya mwenzake ndani.


Baada ya dakika thelathini, Mwanaidi alikuwa akizurura usiku bila kujua wapi yeye na Frida watalala. Alikuwa amefukuzwa.
Upole wake kumsaidia maskini mwenzake umemponza yatima huyu aliyekuwa anafanya kazi za ndani wakati huo huo akisoma shule ya msingi na kupewa wadhifa wa dada mkuu!!
Mwanaidi na Frida matatani!!
Usiku mrefu kwa watoto hawa!!


Lile eneo walilokaa kusimuliana juu ya mkasa wa Frida ndipo hapo walikaa kujadili pia upande wa pili wa Mwanaidi.
Mwisho wa maongezi wakajikuta wote ni wamoja.
"Huwa ananipiga sana..anasema mimi nina mahusiano na mume wake..wakati mwingine anadai mimi nawaroga watotowake..Frida mimi hata sijui uchawi ni nini leo hii naambiwa mimi nawaroga watoto wake. Kila kitu ninachofanya kwake kibaya. Ananifanyisha kazi ngumu. Sijawahi kulalamika. Pesa yangu silipwi. Mume wake akijaribu kunitetea kesho yake napigwa eti nafanya naye mapenzi mumewe. Si ulisikia na leo alipojaribu kunitetea. Mume wake ni mtu mzuri lakini yule mwanamke ni shetani. Tazama sasa amechoma hadi nguo zangu" alishindwa kuendelea kuzungumza ikawa zamu ya Frida kubembeleza.
Ilikuwa simanzi kwa yeyote yule mwenye moyo wa nyama. Hakika iliumiza.
Wawili hawa wakalala palepale.
Siku iliyofuata. Wakafunga safari kuelekea kituo cha kulea watoto yatima. Kigogo jijini Dar es salaam, kinachojulikana kama ‘Dogodogo Center'. Ni huku Mwanaidi alilelewa baada ya kutelekezwa na mama yake.
Sasa anarudi akiwa na mtoto mwingine yatima. Frida!!!


**FRIDA anajikuta anamtegemea MWANAIDI lakini kama vile mikosi imeumbwa kwa ajili yao…mpango unaharibika.
***Wawili hawa wanaenda katika kituo cha kulea yatima. Je! Maisha yataenda sawa???


amina mabata hamful mbalu culbby Washawasha showtie
 
Ama kweli Yatima hadeki. Asante Casuist
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA SITA
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya
MAWASILIANO: 0655 727325


SEHEMU YA SITA


Mwisho wa maongezi wakajikuta wote ni wamoja.
"Huwa ananipiga sana..anasema mimi nina mahusiano na mume wake..wakati mwingine anadai mimi nawaroga watotowake..Frida mimi hata sijui uchawi ni nini leo hii naambiwa mimi nawaroga watoto wake. Kila kitu ninachofanya kwake kibaya. Ananifanyisha kazi ngumu. Sijawahi kulalamika. Pesa yangu silipwi. Mume wake akijaribu kunitetea kesho yake napigwa eti nafanya naye mapenzi mumewe. Si ulisikia na leo alipojaribu kunitetea. Mume wake ni mtu mzuri lakini yule mwanamke ni shetani. Tazama sasa amechoma hadi nguo zangu" alishindwa kuendelea kuzungumza ikawa zamu ya Frida kubembeleza.
Ilikuwa simanzi kwa yeyote yule mwenye moyo wa nyama. Hakika iliumiza.
Wawili hawa wakalala palepale.
Siku iliyofuata. Wakafunga safari kuelekea kituo cha kulea watoto yatima. Kigogo jijini Dar es salaam, kinachojulikana kama ‘Dogodogo Center'. Ni huku Mwanaidi alilelewa baada ya kutelekezwa na mama yake.
Sasa anarudi akiwa na mtoto mwingine yatima. Frida!!!


*****


Miaka ilikuwa imepita utaratibu nao ukawa umebadilika. Kituo cha ‘Dogodogo center' alichokulia Mwanaidi sasa kilikuwa na utaratibu mpya kabisa. Kilikuwa maalumu kwa ajili ya watoto wa kiume pekee.
Wingu zito la mimba za yatima kwa yatima lilikuwa limetawala hivyo wakawekwa mbalimbali ili kupunguza kidogo hali hiyo. Dogodo center ikawa kwa ajili ya wavulana pekee.
Mwanaidi na Frida wakapewa maelekezoi juu ya kituo cha kulea yatima kilichopo maeneo ya Kipati nje kidogo ya jiji la Mbagala.
Ilikuwa bahati kuwa walikuta watoto wengine wa kike wakiwa katika taratibu za kupelekwa kule Mbagala Kipati. Wakapata kuondoka nao.


Wakasajiliwa baada ya kuulizwa maswali mawili matatu!!
Wawili hawa wakaungana na watoto wengine pale kituoni!!


Maisha ya kulelewa yakaanza rasmi.
Shule waliyokuwa wanasoma ilikuwa mbali na kituo cha kulelea yatima hivyo neno la mwisho waliloambiwa ni kwamba taratibu za kutafuta uhamisho zinafanyika.
Walidumu na kauli hiyo vichwani kwa muda mfupi tu ikasahaulika.


Maisha ya pale kituoni hayakuwa mabaya, waliishi vizuri tu. Wakipata mahitaji yao ya msingi. Wababe walikuwepo kama ilivyo ada! Mwanaidi na Frida walikuwa wanyonge. Lakini hawakunyanyasika sana!!


*****


Kiubaridi cha siku hiyo kiliwafanya watoto wengi wajikute wakiwa na masweta ya misaada kutoka taasisi isiyokuwa ya kiserikali. Kila mmoja alikuwa amejikita katika linalomuhusu. Wengine walikuwa na marafiki zao wakicheza. Wengine walikuwa wanasukana nywele na baadhi walikuwa vitandani tayari.
Frida na Mwanaidi walikuwa chini ya mti wakiwa katika mazungumzo. Muongeaji mkuu alikuwa ni Mwanaidi. Frida alikuwa anasikiliza tu.
Kabla ya wawili hawa kukaa na kuzungumza. Siku hii Mwanaidi alikuwa mjini kwa siku nzima baada ya kupata ruhusa kutoka kituoni. Kuna jambo zito alitoka nalo huko mjini.
"Frida!!"
"Bee!"
"Unajua kuwa kuna umri wa mwisho kukaa hapa kituoni."
"Hapana sijui."
"Ndio ujue na ninadhani tumebakiza miezi michache tutaambiwa tuondoke." Alizungumza huku akiangalia anga. Frida akakumbwa na taharuki!!!
"Tunarejea mtaani tena. Una chochote cha kufanya mtaani..jibu ni hauna na mimi sina."
Mwanaidi aliendelea kuzungumza mengi hatimaye akalifikisha jambo gumu kwa Frida. Mkuu wa kituo alikuwa akimuhitaji Frida kimapenzi ili aweze kuwaongezea miaka ya kuishi pale kituoni.
Miaka waliyoandikiwa katika fomu walizojaza siku ya kuingia ni miaka kumi na saba na miezi mitatu kwa Frida na miaka kumi na saba na miezi tisa kwa Mwanaidi jambo ambalo halikuwa kweli hata kidogo.
Na sheria na kanuni ziliwataka wakifikisha miaka kumi na nane kuingia mtaani kama watu wazima.
Wakuu hawa wa vituo walifanya hivi ili kuepuka gharama za kuwatunza watoto wengi. Wadhamini wao walijitoa kwa moyo lakini wanadamu hawa wenye roho mbaya waliweka ujanja ujanja na kuwagandamiza watoto hawa.
Kibaya zaidi waliofanya haya wote walikuwa wanazungumza Kiswahili na waliowanyanyasa pia walizungumza Kiswahili. Yule muwezeshaji mwenye huruma alikuwa anazungumza kiingereza safi huku akijua maneno mawili tu ya Kiswahili ‘NAWAPENDA SANA'
Mwezeshaji alikuwa ni mzungu mwenye upendo huku akiwaacha waswahili wakinyanyasana wao wao. Pesa za muwezeshaji wanazipigia mahesabu ya kuezeka na kupaua nyumba zao. Mawazo batili ya muafrika!!!


Kwanza Frida hakumuelewa Mwanaidi alitaka kumaanisha nini kwa kauli yake ile ya kumtaka Frida awe na uhusiano wa usiku mmoja na msimamizi wa kituo ili waweze kudumu pale.
Lakini baada ya maelezo marefu Frida alielewa na kupinga vikali. Hakuwa tayari kwa wazo la Mwanaidi.
Jeuri yake ilikatika baada ya Mwanaidi kumweleza kuwa mahali hapo walipo lile sio ombi bali lazima!! Hapo sasa Frida akashusha pumzi kwa nguvu. Akakosa la kusema.
Mwanaidi akambembeleza sana rafiki yake huyu, akatumia kila aina ya ushawishi hatimaye Frida akakubali japo kwa shingo upande.
Angeshtaki wapi unyanyaswaji huu iwapo aliyemnyanyasa ni mkuu wa kituo.
Usiku wa makubaliano ukafika. Mwanaidi akamtwaa Frida hadi nyumba ya kulala wageni maeneo ya Mbagala Kizuiani. Frida alikuwa anatetemeka wakiwa wanaingia chumbani. Hakuwa amewahi kufanya mapenzi hapo kabla. Maisha ya kuishi gerezani na kisha katika nyumba za magereza yalimbana sana na kamwe hakuwahi kushiriki mchezo huu mchafu. Sasa anatakiwa kufanya kwa lazima.
Sayansi aliyosoma darasa la tano ilimkumbusha jambo moja tu. Mimba!! Na ikamdokezea kuhusu matumizi ya kinga kuizuia isiingie katika mji wa uzazi.
Saa nne usiku mlango ukagongwa. Likafanyika tendo moja tu!! Mwanaidi nje, mnyanyasaji anayesimamia kituo ndani!!
Hapakuwa na maongezi sana!! Frida akabakwa kwa hiari yake mwenyewe. Kwa ajili ya kujipigania aweze kuendelea kuishi kituoni.
Saa kumi na moja alfajiri Mwanaidi akaingia na kuondoka na Frida kama walivyoingia awali!


*****


Muonja asali haonji mara moja!
Mnyanyasaji akataka tena!! Tofauti na makubaliano ya awali kuwa angefanya mara moja na kuwaongezea miaka ya kuishi pale kituoni.
Frida kiroho upande akaingia tena katika adhabu hii aliyorithishwa na mama yake mzazi aliyefia gerezani. Mnyanyasaji akaendelea kunogewa zaidi na zaidi!!
Mbaya kupindukia hakuwahi kutumia kinga!!!
Frida alilazimika kuvumilia japo hakupenda!!
Idadi ya mialiko ya kwenda nyumba za kulala wageni ilipozidi. Frida akakumbuka jambo!! Akamkumbuka mama yake mzazi. Akamkumbuka marehemu Maria Paul.
Akakumbuka kuwa alihukumiwa kunyongwa baada ya kuua wanaume watatu.
Au walimfanya kama wanavyonifanya!! Mbona aliua wanaume peke yao? Frida alijiuliza sana. Kifo cha mama yake kikamshtua akili yake. Akajiona ni mjinga ambaye hajijui kama ni mjinga.
Mawio na machweo yakapita. Ikafika siku ya kutembelewa na muwezeshaji kutoka nchi za mbali. Huyu alikuwa ni yule mzungu mwenye upendo wa dhati kwa watoto wasiokuwa wa nchi yake.
Frida hakuwa anajua kiingereza. Alitamani sana kumweleza yule mzungu juu ya unyanyasaji anaofanyiwa na msimamizi mkuu wa kituo chao. Siku moja kabla hajafika yule msimamizi aliufanya tena mwaliko. Kama kawaida akamadhibu bila makosa na kumfanya mtumwa wa ngono.
Asubuhi ya mwezeshaji kufika kituo kilipendeza sana baada ya usafi yakinifu!!
Mwezeshaji alifika na zawadi nyingi. Watoto wenyeji walimchangamkia sana na nyuso zao zilionyesha matumaini.hakika alikuwa ana upendo unaoonekana machoni waziwazi.
Alikuwa analia na watoto akiona wapo katika majonzi. ‘NAKUPENDA SANA' ndilo neno aliloweza kusema.


Majira ya mchana watoto wote waliitwa katika holi la kulia chakula. Mbele yao walikuwepo wanaume wawili na wanawake watatu. Walitambulishwa mbele yao kama madaktari na washauri.
Walizungumza nao mengi na kuwaeleza kuwa walikuwa wamefika pale kwa ajili ya kutazama kama watoto hao wanaweza kuwa wameathirika na ugonjwa wa Malaria.
Zoezi la uchukuaji damu lilichukua muda mfupi. Kisha watoto wakaruhusiwa kuendelea na shughuli zao wakati wataalamu hao wakiendelea na utafiti.
Ni wachache sana walioelewa nini kinaendelea. Wazoefu walijua kuwa wanapimwa mimba!! Mwanaidi akiwa mmoja kati ya waliokuwa wanafahamu. Akamtonya Frida juu ya jambo hilo. Frida hakushtuka hata kidogo. Alikumbuka kuwa shuleni alifundishwa kuwa dalili za mimba ni kichefuchefu!! Naye hakuwahi kukipata hapo kabla.


****


Majibu yalimuumiza sana kichwa mzungu!! Alizunguka huku na huko. Alimkaripia sana mkuu wa kituo. Chumba kilikuwa na kiyoyozi lakini mzungu alikuwa anatokwa jasho. Hakutaka kuamini kabisa inawezekana vipi kituo kilicho na ulinzi imara kama ule mtoto anabeba mimba. Mkuu wa kituo alijaribu kujitetea lakini mzungu hakumuelewa.
Maneno mengi hayavunji mfupa. Mzungu akatoa kauli. Kwa nini mate yatumike kuandika angali kuna wino?
"Her name is Fridah! I need her right now!" (Anaitwa Frida, namuhitaji hapa sasa hivi!) alikoroma mzungu!
Mkuu wa kituo akatoka nje akiwa anatetemeka!!
Ndio. Lazima atetemeke maana kwa namna yoyote Frida lazima atamtaja kuwa yeye ndiye muhusika wa mimba ile!! Kibarua kitaota majani!!
Hofu ikatanda sana!! Hadi anafika nje hakujua afanye nini!!!


Wakati mnyanyasaji huyu akiwa katika hofu kuu. Frida alikuwa katika mawazo ya ataweza vipi kuzungumza na yule mzungu mwenye upendo wa hakli ya juu. Alihitaji kutoa shtaka lake dhidi ya mkuu wa kituo. Uamuzi huu hakumshirikisha Mwanaidi. Aliuhifadhi moyoni.
Mara akiwa katika mawazo hayo mazito. Akasikia akiitwa jina lake kwa mbali. Akageuka!! Alikuwa mkuu wa kituo!!
Moyo ukamwenda mbio Frida. Na ilikuwa kawaida kila alipomuona mwanaume huyu alimchukulia kama mnyama mkali.


***FRIDA hajui kama ana mimba!!! Mzungu ameligundua hili…muhusika wa hii mimba ni MKUU WA KITUO je nini kitatokea?? Mzungu anahitaji kuzungumza na Frida ambaye naye alikuwa anahitaji hiyo nafasi!!!
 
Back
Top Bottom